Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya August 15
↧
↧
Waziri Mkuu Ataka Bodi Ijayo Ya Tumbaku Ijipange......Aitaka isimamie zao hilo na kutafuta masoko, iache kutoa vibali vya ununuzi
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema tumbaku ni siasa na tumbaku ni uchumi na ameitaka Bodi ya Tumbaku itakayoundwa ijipange kumlinda mkulima.
Waziri Mkuu alitoa agizo hilo Jumapili, Agosti 13, 2017 wakati akizungumza na watumishi wa idara za kilimo na ushirika na viongozi wa wilaya za mkoa huo kwenye kikao alichokiitisha ili awape maagizo maalum. Kikao hicho kilihudhuriwa pia na Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia kilimo, Eng. Mathew Mtigumwe na baadhi ya wakurugenzi kutoka wizara hiyo.
Alisema wajumbe wa bodi hiyo walishatajwa lakini kwa sasa hivi wanasubiri uteuzi wa Mwenyekiti wa bodi hiyo. Hata hivyo, Waziri alimwelekeza Katibu Mkuu wa Kilimo awaite wajumbe wa bodi hiyo wakutane na kumchagua Makamu Mwenyekiti wa muda ili waanze kazi ya kukutana na WETCU zao.
“Kwa sababu bodi ni ya nchi nzima, ni vema wakakutana na WETCU zao na AMCOS zao ili waanze kukusanya taarifa ya tumbaku kutoka Chunya, Namtumbo, Serengeti na mahali mengine ili wapeleke message hii ya msimu ujao,” alisema Waziri Mkuu.
Alisema ili kuongeza ufanisi kwenye zao hilo, itabidi baadhi ya majukumu ya bodi yapunguzwe ikiwemo kazi ya utoaji vibali vya kusafirisha na kununua tumbaku. “Hivi kama kibali cha kuuza tumbaku ya Namtumbo kinatolewa na Bodi ambayo makao makuu yake yako Tabora, sasa utawezaje kufuatilia kutoka Tabora? Ka nini kazi hiyo isifanywe na chama kikuu cha ushirika kilichopo huo?” alihoji Waziri Mkuu.
Alionya kwamba endapo bodi itaachiwa iingie kila mahali, haitaweza kulaumiwa pindi jambo likiharibika. “Ninyi kazi yenu kubwa iwe ni usimamizi kuanzia kwenye WETCU na AMCOS zake. Simamieni masoko, hakikisheni wanaokuja kununua wako tayari kufuata mfumo uliowekwa na Serikali,” alisema.
Waziri Mkuu alisema bodi ijayo inalo jukumu pia la kushirikiana na vyuo vya utafiti ili kuhakikisha kuwa tafiti zinafanyika na kupata mbegu bora zenye kustahimili magonjwa na hali ya hewa.
Akizungumzia kuhusu upangaji wa madaraja kwenye zao la tumbaku, Waziri Mkuu alisema kuna hatua imefanyika kwani hivi sasa madaraha yamepunguzwa kutoka zaidi ya 100 yaliyokuwepo na kufikia 39. Hata hivyo, alisema wingi wa madaraja bado ni changamoto kwenye upangaji wa bei.
“Bodi na wizara lazima mzungumze na makampuni ya ununuzi na mkubaliane mfumo gani utatumika kuhusu madaraja ya tumbaku. Kazi yetu kubwa na kumlinda mkulima.”
“Wenzenu wa korosho walikuwa na madaraja mengi lakini sasa yamebakia mawili, grade 1 na grade 2 na bei ya kila daraja inajulikana kwa hiyo rahisi kumuibia mkulima,” alisisitiza.
Naye Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tabora, Mzee Hassan Wakasuvi akitoa shukrani kwa Waziri Mkuu kwa ziara yake alisema wameyapokea maelekezo hayo na hawatasita kuwasukuma watendaji wanaochelewa kutimiza wajibu wao.
“Miaka miwili iliyopita, tumbaku ilikuwa ni zao linaloongoza kwa kuingiza fedha za kigeni hapa nchini. Lakini hivi tumeshuka, na tumeiacha korosho ndiyo inaongoza, tumedhamiria kurudi kwenye nafasi yetu, na hatutasita kuwaweka pembeni watendaji wa Serikali wataotuchelewesha kufikia azma yetu hiyo,” alisema.
Waziri Mkuu amemaliza ziara yake ya siku nne na ameahidi kurudi kumalizia wilaya za Nzega, Igunga na Tabora Manispaa ambazo hakuzitembelea.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMATATU, AGOSTI 14, 2017.
↧
Waziri Mkuu Awabana Maafisa Ushirika, Kilimo........Ataka wasimamie zao la tumbaku kwa umakini ili kumkoboa mkulima
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka maafisa kilimo na maafisa ushirika wa mkoa wa Tabora wasimamie kwa umakini ukuzaji wa zao la tumbaku kuanzia msimu ujao.
“Mkakati wetu wa kuinua zao hili unaanza msimu ujao, ninaondoka Tabora lakini nataka kila mmoja wenu atumie nafasi yake kuelezea suala hili kwa kina kwa wakulima wa zao la tumbaku ili tubadilishe mfumo na tuweze kuwakomboa,” alisema.
Waziri Mkuu alitoa agizo hilo Jumapili, Agosti 13, 2017wakati akizungumza na watumishi wa idara za kilimo na ushirika na viongozi wa wilaya za mkoa huo kwenye kikao alichokiitisha ili awape maagizo maalum. Kikao hicho kilihudhuriwa pia na Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia kilimo, Eng. Mathew Mtigumwe na baadhi ya watendaji kutoka wizara hiyo.
Aliwataka watendaji hao watumie vyombo vya habari vya ndani ya mkoa na vya kitaifa kuelezea mkakati mpya ambao serikali inao wa kuinua zao la tumbaku. “Tumieni vyombo vya habari kila mmoja apange ratiba kuelezea atafanya nini, toeni elimu kwa sababu vyombo hivi vinasikika hadi kwenye mikoa ya jirani,” alisisitiza.
“Afisa kilimo wa wilaya lazima ujue una wakulima wangapi, je wakulima wako kila mmoja analima ekari ngapi? Na katika ekari hizo, ana mahitaji ya pembejeo kiasi gani?” alisema.
“Afisa ushirika wa wilaya nawe hakikisha unasajili idadi ya vyama vya msingi (AMCOS) vilivyoko kwenye eneo lako, lazima ujue AMCOS ziko ngapi na zina wanachama wangapi. Afisa kilimo na afisa ushirika muanze kazi hiyo mara moja,” alisisitiza.
“Ulizeni mahitaji yao ni yapi, kwa kila mwanachama na kila AMCOS, kisha muziwasilishe kwa Mkuu wa Mkoa ili naye azifikishw kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo. Pale wizarani, tunataka Mkurugenzi wa Pembejeo ajue mahitaji ya kila mkoa ili pembejeo ziweze kuwasilishwa kwa wakulima miezi miwili kabla msimu wa kilimo haujaanza, kama ambavyo tumeagiza,” alisema.
Akifafanua kuhusu uagizaji wa mbolea, Waziri Mkuu alisema Serikali imeanzisha mfumo wa pamoja wa mbolea (bulk procurement) na akawataka wataalamu wa wizara ya kilimo wamalize mgogoro wa siku nyingi uliokuwepo baina yao na kiwanda cha mbolea cha Minjingu.
“Kumekuwa na maneno maneno kuhusu mbole ya NPK, lakini wakati sisi tunaidharau, wenzetu wa nchi jirani wanaongoza kwa kuagiza mbolea nyingi kutoka Minjingu. Acheni kuagiza mbolea hiyo kutoka nje ya nchi, tukachukue pale Minjingu,” alisisitiza.
Alisema mwenye kiwanda ameahidi kwamba akipewa oda ya mbolea, yeye atazisafirisha hadi kiwandani. “Hakuna haja ya kuwaumiza wakulima na mbolea za bei mbaya wakati tunayo hapa nyumbani na tena ya bei nafuu. Wenye makampuni ya kununua tumbaku wanauza mfuko mmoja kwa dola 70 sawa na sh.150,000 hii ya Minjingu yenye ubora uleule inauzwa sh. 60,000 kwa mfuko mmoja, tena zikiwa zimefikishwa wilayani.”
“Ninawasihi viongozi wa ushirika na wa wilaya tusaidiane kumuondoa mkulima kwenye utegemezi wa mikopo ya benki na badala yake tuwaelimishe wajiwekee akiba ya kumudu pembejeo za msimu unaofuata,” alisisitiza.
Alisema kama kutakuwa na ulazima wa kuingia kwenye mikopo, viongozi hao hawana budi kuhakikisha kuwa wanaisimamia kwa kikamilifu. “Kama mtaingia kwenye mikopo, lazima mjipange kuisimamia mikopo hiyo ili isije ikawarudisha nyuma wakulima wetu kwenye mfumo ambao ulikuwa unawaumiza,” aliongeza.
Akifafanua kuhusu ununuzi wa tumbaku, Waziri Mkuu alisema AMCOS ndizo zenye tumbaku na kwa maana hiyo ndiyo zitahusika na uuzaji. Katika kila wilaya, wekeni mfumo wa usimamizi kupitia Kamati ya Ulinzi na Usalama. Malori yakikamatwa na marobota yaliyouzwa nje ya mfumo, ni lazima hatua kali zichukuliwe,” alisisitiza.
“Ninasema hakuna mazungumzo tena nje ya AMCOS, ni kwa kampuni ya ununuzi au kwa mtu binafsi. Na kuanzia sasa, Associations za tumbaku zimefutwa. Mkuu wa Mkoa na wakuu wa wilaya hakikisheni hakuna associations kwenye zao la tumbaku, tunataka kila mmoja akanunue kwenye AMCOS na kila mkulima asajiliwe kwenye AMCOS,” alisisitiza.
Alisema Serikali ilivunja Chama Kikuu cha Ushirika Kanda ya Magharibi (WETCU) kutokana na ubadhirifu uliokuwa ukifanywa na viongozi wa chama hicho na kwamba hivi sasa kutakuwa na WETCU mbili ambapo ya kwanza (WETCU I) itahusika na wilaya za Kaliua na Urambo na ile ya pili (WETCU II) itahudumia wilaya za Sikonge, Uyui, Nzega na sehemu ndogo ya Tabora Manispaa.
Alisema hatua hiyo imechukuliwa ili kuwe na vyama vikuu viwili vyenye AMCOS chache lakini zenye uwezo wa kuwafikia wakulima, kusikiliza mahitaji yao na kutatua matatizo yao. WETCU ya zamani ilikuwa na AMCOS 214 na haikuweza kuwafikia wakulima wote.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMATATU, AGOSTI 14, 2017.
↧
Makamba: Serikali haina nia ya kurudisha viroba
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), January Makamba amesema Serikali haina nia ya kurudisha sokoni pombe zilizotengenezwa katika mifuko ya plastiki 'viroba' na kuwataka Watanzania kupuuza uzushi unaoenezwa kwamba pombe hizo zitarudi.
Makamba alitoa kauli hiyo jana, Jumatatu Agosti 14 alipotembelea eneo la Kimara Temboni lilipo ghala la kuhifadhi pombe mbalimbali ikiwamo viroba linalomilikiwa na Kampuni Thema.
Makamba alisisitiza kwamba Serikali uamuzi wake wa kuzuia pombe hizo upo palepale na haujabadilika hivyo watu waache kupotosha wenzao.
"Baada ya kupiga marufuku kuna kampuni zilikuja ofisini kuomba kuongezewa muda, lakini tuliwakatalia na kuwaambia waheshimu uamuzi uliotolewa sasa hizi tetesi ya kwamba vinarudi sokoni sijui zinatoka wapi," alisema Makamba.
Makamba ambaye pia ni Mbunge wa Bumbuli amesema njia ya pekee kwa wafanyabiashara hao wa viroba wanaotakiwa kuifanya ili kupunguza hasara ni kubadilisha pombe hizo na kuziweka katika chupa zenye ujazo unaotakiwa.
Amesema kamwe Serikali haiwezi kurudi nyuma na kwamba mafanikio yameanza kuonekana kutokana na hatua hiyo.
↧
Kutana Na Mwanamke Aliye Jitolea Kumtibu Mume Wake Tatizo La Nguvu Za Kiume Lililosababishwa na Kujichua
Tina anasema aligundua tofauti kwa mumewe mara baada ya mumewe kurejea nchini akitokea masomoni nchini Malaysia ambako alikaa kwa muda wa mwaka mmoja na miezi minane.
“Kila nilipo kuwa nikikutana faragha na mume wangu, niligundua tofauti kubwa sana, kwani uwezo wa mume wangu katika tendo la ndoa ulikuwa umepungua kwa kiasi kikubwa sana na wakati mwingine hakuwa kabisa na uwezo wa kufanya tendo la ndoa “.
Baada ya kugundua tofauti hii, niliamua kumueleza mume wangu wazi wazi na kumtaka tutafute tiba kwa ajili ya tatizo lake .
Niliamua kufanya hivi kwa sababu ninampenda sana mume wangu na sikutaka kutoka nje ya ndoa yangu kwa sababu eti mume wangu ana udhaifu katika tendo la ndoa.
Akielezea kuhusu chanzo cha yeye kuwa na udhaifu mkubwa katika tendo la ndoa , mume wa Tina alisema :
“ Kwa muda wote wa mwaka mmoja na nusu nilio kuwa nasoma nje ya nchi nilikuwa nafanya masturbation ili kukudhi haja zangu. Alisema .
Mume wa Tina aliongeza kuwa “ Niliporudi nyumbani Tanzania, mchezo huu ulikuwa tayari umeniathiri kisaikolojia na kimaumbile pia.
JINSI KUJICHUA KULIVYO MUATHIRI MUME WA TINA
Mume wa Tina anasema , mchezo wa kujichua ulimuathiri kwa kiwango kikubwa sana. Akielezea baadhi ya madhara ambayo ameyapata kutokana na kujichua, mume wa Tina anasema :
1. Kwanza maumbile yangu ya kiume yamelegea na kusinyaa sana.
2. Ngozi ya kwenye uume wangu imekufa ganzi. Huwa sihisi chochote kabisa. Hata ninapomuingilia mke wangu huwa nakuwa kama sijamuingilia. Yani sihisi chochote kabisa.
3. Kama hiyo haitoshi, hata ninapokuwa nafanya masturbation, nikifika kileleni huwa nakuwa sisikii chochote yani nakuwa kama nimekojoa tu mkojo wa kawaida… Ili kusikia hali ya kawaida, inanibidi nikae labda kwa siku tatu au nne halafu nifanye tena masturbation, hapo ndio ninaweza kusikia kawaida.
4. Ikitokea nimefanikiwa kufanya tendo la ndoa, hufanya katika hali ya ulegelege na huwa ninamaliza ndani ya sekunde chache sana, nikijitaidi sana naweza chukua dakika moja tu.
5. Ninapo maliza kufanya tendo la ndoa, misuli ya uume huwa inauma sana na huwa sina uwezo wa kurudia tena tendo mpaka kesho au baada ya siku mbili.
6. Uume wangu hauwezi kusimama wenyewe mpaka niupapase mimi mwenyewe tena kwa muda mrefu sana.
7. Na mara nyingi huwa ninakosa kabisa hamu ya tendo la ndoa hata ninapokuwa na mke wangu kitandani.
Mwanaume huyu anaeleza kuwa suala la kujichua kwa muda mrefu limemuathiri kisaikokojia kiasi kwamba, wakati mwingine inambidi kutumia dawa kali za kizungu za kuongeza nguvu ili aweze kufanya masturbation.
“ Wakati mwingine, nakuwa nahitaji kufanya masturbation, lakini nakuwa sina nguvu ya kufanya hivyo, hivyo inanibidi niende kununua na kutumia madawa makali ya kizungu kwa ajili ya kupata uwezo wa kufanya masturbation. “ Anasema .
Tina anasema mara baada ya kugundua hali hii, alimshawishi mume wake waanze kutafuta suluhisho sahihi la tatizo linalo mkabili, na mwisho wa siku wakafanikiwa kupata taarifa kuhusu tiba asilia iitwayo Jiko , na kufanikiwa kupata tiba hiyo pamoja na maelekezo yake ya namna ya kuitumia pamoja na lishe yake.
Jumapili ya tarehe 13 AGOSTI 2017 , Neema Herbalist , ilienda kuitembelea familia ya Tina ili kuwajulia maendeleo yao na kuona jinsi wanavyo endelea na tiba na maendeleo ya tiba yapo vipi.
Tulifurahi kuona kuwa, mwanadada Tina amesimamia zoezi zima ka kuhakikisha mume wake anatumia tiba ya Jiko kwa usahihi kabisa na hatimaye tatizo lake liweze kupona kabisa .
Tina anasimamia zoezi hili kwa kumuandalia na kumtayarishia mumewe dawa ya Jiko pamoja na kumuandalia na kumtayarishia lishe na vyakula mbalimbali ambavyo ni muhimu kwa mwanaume anae tumia tiba ya kumaliza tatizo la ukosefu na/ama upungufu wa nguvu za kiume.
Kuhusu maendeleo ya mumewe, Tina anasema anashukuru Mungu sasa hivi mumewe ameonyesha maendeleo makubwa sana na ana amini baada ya mwezi mmoja wa kutumia tiba hii, mume wake atakuwa amepona kabisa tatizo la ukosefu na upungufu wa nguvu za kiume.
KUHUSU SWALA LA MUMEWE KUWA ADDICTED NA KUJICHUA
Kuhusu suala la mumewe kuwa addicted na tabia ya kujichua Tina anasema, anatumia dawa maalumu aliyo ipata katika duka la NEEMA HERBALIST .
Dawa hii ya asili ( KAMA INAVYO ONEKA HAPO CHINI, YENYE RANGI YA BLUE ), haimfanyi mtu kuacha kujichua moja kwa moja, ila inasaidia kumuondolea mtu uwezo wa kufanya masturbation.
Dawa hii huchanganywa na mafuta maalumu ya asili halafu mhusika, anajipaka kwenye mikono, akijipaka kwenye mikono… Akijipaka kwenye mikono hawezi kujishika kwenye sehemu yoyote ile laini ikiwemo sehemu za kiume, kwani akifanya hivyo, itamuwasha na kuchoma sana sehemu laini ya mwili aliyo igusa. Hivyo automatically mhusika hawezi kabisa kujaribu kufanya masturbation, kwani akijaribu kufanya hiovyo itamuwasha sana.
DAWA HII PIA, NI KIBOKO YA KUTIBU NA KUPONYESHA KABISA MAJERAHA YASIYO PONA ( VIDONDA NDUGU )
Tina anasema; kila inapo fika asubuhi huwa nahakikisha mume wangu anajipaka dawa hii kwenye mikono yake, ili niwe na uhakika kwamba hatoweza kufanya masturbation nitakapo kuwa mbali nae.
Tunatoa pongezi kubwa sana kwa mwanadada Tina, kwani ni wanawake wachache sana wanao weza kuwa na moyo kama wa Tina.
Kama wanawake wote walio katika ndoa, wangekuwa na moyo kama wa Tina, basi tatizo la ukosefu na upungufu wa nguvu za kiume, lingeweza kudhibitiwa na hatimaye kutokomezwa kabisa, kwa sababu uzoefu wetu unaonyesha kuwa, asilimia kubwa ya wanaume walio katika ndoa , huwa hawataki kuwashirikisha wake zao, pindi wanapo jigundua kuwa wana tatizo la ukosefu na ama upungufu wa nguvu za kiume na hivyo kuendelea kulifanya tatizo kuwa kubwa zaidi, kwani wanaume hawa huwa wanashindwa kutumia kwa uwazi tiba ya kutibu tatizo lao kwa kuhofia wake zao kujua.
KUHUSU NAMNA TABIA YA KUJICHUA INAVYO SABABISHA TATIZO LA UKOSEFU NA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME, BONYEZA LINK HII HAPA :
NA JINSI YA KUPATA DAWA YA JIKO. FIKA KATIKA DUKA LA NEEMA HERBALIST LILILOPO UBUNGO JIJINI DAR ES SALAAM, JIRANI NA SHULE YA MSINGI UBUNGO NATIONAL HOUSING, NYUMA YA JENGO LA UBUNGO PLAZA.
↧
↧
Mambo 10 Ambayo Tanzania na Misri Zimekubaliana Kushirikiana baada Ya Rais Wao Kutua Nchini Jana
Tanzania na Misri zimekubaliana kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi na kijamii katika maeneo makuu 10, ikiwemo kuimarisha uhusiano, ulinzi na kujenga kiwanda kikubwa cha nyama pamoja na kiwanda cha dawa nchini.
Pamoja na makubaliano hayo ya kiuchumi na kijamii, suala la matumizi ya maji ya Mto Nile halijapatiwa muafaka na mazungumzo yanaendelea kuwezesha kukamilisha matumizi yenye faida ya mto huo kwa nchi zote zinazohusika.
Aidha, Misri imempongeza Rais John Magufuli kwa utawala mzuri kwa namna anavyopambana na rushwa na ufisadi na kufafanua kuwa nchi hiyo (Misri) inaendelea kushirikiana na Tanzania katika mapambano hayo.
Makubaliano hayo takriban 10 yalielezwa jana Ikulu, Dar es Salaam na marais hao wawili wa Tanzania, Dk Magufuli na wa Misri, Abdel Fattah Al Sisi wakati wakizungumza na waandishi wa habari.
Rais Magufuli alisema wamekuwa na mazungumzo marefu mara baada ya Rais Al Sisi kuwasili jana mchana na ziara hiyo ikifanyiwa kazi kwa yale waliokubaliana, italeta manufaa makubwa kwa nchi hizo mbili.
“Tumezungumza mengi leo, nchi ya Misri ina historia kubwa katika dunia ya sasa, ustaarabu wa maisha ya binadamu ukiachia mbali binadamu wa kwanza inaelezwa aliishi Tanzania (Olduvai Gorge), wasanifu majengo wa kwanza waliishi Misri, ushahidi upo hata leo pyramids leo bado hakuna anayeweza kuzijenga.
“Vitabu vitakatifu vinaandika kuhusu Misri, Mtume Yesu alikimbilia Misri alipotaka kuuawa, ni eneo la kukimbilia wenye shida na sisi tutakimbiza shida zetu kwao ili atusaidie kuzitatua,” alisema Dk Magufuli.
Alisema pamoja na kwamba hatujapakana kimipaka na Misri, lakini maji ya Mto Nile yameziunganisha nchi hizo mbili kwani chanzo cha maji kwenda Mto Nile ni pamoja na Mto Kagera na maji ya Ziwa Victoria ambalo asilimia 51 lipo Tanzania, 44 Uganda na tano Kenya.
Makubaliano
Akielezea kuhusu maeneo ya makubaliano, Rais Magufuli alisema kwanza kutokana na historia ya mahusiano mema na ya muda mrefu baina ya Baba wa Taifa wa nchi hizo mbili; Mwalimu Julius Nyerere na Gamal Abdel Nasser, wamekubaliana kuimarisha mahusiano hayo kwa mustakabali wa nchi hizo mbili.
Dk Magufuli alisema wamekubaliana kuunda upya Kamisheni za Kudumu za Kiuchumi za Pamoja baina ya Tanzania na Misri ,ambazo ziliundwa awali na waasisi hao (Nyerere na Abdel Nasser) wa nchi hizo mbili. “Tumekubaliana hizi kamati (kamisheni) za kudumu ziundwe upya, wakutane mawaziri wan chi hizi mapema,” alisema Magufuli.
Eneo jingine ni kukuza biashara kati ya nchi hizo ambapo alisema kwa kuwa Misri inahitaji nyama na Tanzania ni nchi ya pili kwa mifugo mingi, nchi hiyo (Misri) itajenga kiwanda kikubwa cha nyama nchini ili wasafirishe nyama yenye viwango bora kwenda Misri.
Kiwanda hicho kikikujengwa, ajira kwa Watanzania zitapatikana, mapato na wafugaji watapata kipato zaidi kwa kuuza nyama moja kwa moja katika kiwanda hicho. Katika eneo la biashara, kwa sasa kiwango cha biashara baina ya Misri na Tanzania ni Dola za Marekani milioni 78.02.
Kiwango ambacho jana Rais Magufuli alisema ni kidogo na kinahitajika kuongezeka. Rais pia alieleza kuwa, Misri imekubali kuleta nchini teknolojia ya kilimo cha umwagiliaji nchini ili kukuza sekta ya kilimo.
Asilimia 95 ya nchi ya Misri ni jangwa na asilimia tano pekee huitumia kwa kilimo hasa cha umwagiliaji.
Alielezea eneo jingine kuwa ni sekta ya afya, ambapo amesema wamekubaliana na Rais Al Sisi kuendelea kuleta wataalamu na vifaa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili na Hospitali za Zanzibar na wamepanua wigo kwa kuongeza fedha kuwezesha operesheni za figo kufanyika kabla ya mwaka 2020.
Hata hivyo, hakueleza ni kiasi gani cha fedha walichoongeza. Katika sekta ya afya, pia wamekubali kujenga kiwanda cha kutengeneza dawa nchini hasa ikizingatiwa kuwa Misri ni moja kati ya nchi zenye viwango vikubwa vya ubora wa dawa duniani na hivyo ujenzi huo utaongeza ajira, afya, mapato na kukuza uchumi zaidi.
Kwa mujibu wa Rais Magufuli, uwekezaji wa kampuni za Misri nchini ni wa Dola za Marekani milioni 887.07 na umewezesha ajira nyingi.
Kuhusu utalii, Magufuli alisema wamekubaliana kuendesha sekta hiyo kwa kushirikiana na Shirika la Ndege la Misri na Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL).
Kwa sasa Misri inapokea zaidi ya watalii milioni 10 kwa mwaka na Tanzania ni wastani wa watalii milioni mbili kwa mwaka.
Ulinzi ni eneo jingine ambalo marais hao wawili wamekubaliana ili kuhakikisha amani kwa mataifa hayo inaimarika na Rais Al Sisi aliipongeza Tanzania inavyoshiriki kurejesha amani katika nchi za maziwa makuu na Rais Mtaafu Benjamini Mkapa kwa namna anavyosimamia amani Burundi.
Aidha, Tanzania pia itanufaika katika sekta ya elimu, ambapo marais hao wawili wamekubaliana kubadilishana walimu kwa lugha (Kiswahili, Kiarabu na dini) pamoja na IT.
Hata hivyo, pamoja na makubaliano hayo, Dk Magufuli alisema eneo la Mto Nile bado mazungumzo yanaendelea ili kuhakikisha kuwa maji ya Mto huo yanazinufaisha nchi zote zinazoguswa nao.
“Tunatambua maji ya Mto Nile ndio uhai wa Misri, tunatendelea katika mazungumzo ili mto huo umnufaishe kila nchi husika,” alisema Dk Magufuli.
Alieleza pia kuwa Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein alipata nafasi ya kuongeza na Rais Al Sisi na kueleza changamoto kadhaa za Zanzibar na amekubali kuja tena nchini ili kufanya ziara Zanzibar ambako aliwahi kufika kibinafsi miaka 10 iliyopita.
Eneo jingine marais hao wamesaini makubaliano ya kupambana na rushwa na katika eneo hilo, Rais Magufuli alisema rushwa ni saratani inayohitaji nguvu ya pamoja kuimaliza huku Rais Al Sisi akiisifu Tanzania na Magufuli kwa namna wanavyopambana na rushwa na ufisadi na kueleza ataendeleza ushirikiano katika mapambano hayo.
Rais Al Sisi pia alieleza kuhusu makubaliano hayo na kusisitiza kuwa, Misri itaendelea kushirikiana na Tanzania katika miradi mikubwa ya maji kwa kujenga visima na kilimo cha umwagiliaji pamoja na maeneo ya afya.
“Namshukuru kaka yangu Rais Magufuli kwa makaribisho mazuri, ili ushirikiano uendelee namkaribisha Misri ili kuendelea kujadiliana namna ya kukuza maendeleo ya nchi zetu,” alisema Field Marshal Al Sisi.
Rais Magufuli alieleza kukubali kuitembelea Misri kwa wakati muafaka.
.
Pamoja na makubaliano hayo ya kiuchumi na kijamii, suala la matumizi ya maji ya Mto Nile halijapatiwa muafaka na mazungumzo yanaendelea kuwezesha kukamilisha matumizi yenye faida ya mto huo kwa nchi zote zinazohusika.
Aidha, Misri imempongeza Rais John Magufuli kwa utawala mzuri kwa namna anavyopambana na rushwa na ufisadi na kufafanua kuwa nchi hiyo (Misri) inaendelea kushirikiana na Tanzania katika mapambano hayo.
Makubaliano hayo takriban 10 yalielezwa jana Ikulu, Dar es Salaam na marais hao wawili wa Tanzania, Dk Magufuli na wa Misri, Abdel Fattah Al Sisi wakati wakizungumza na waandishi wa habari.
Rais Magufuli alisema wamekuwa na mazungumzo marefu mara baada ya Rais Al Sisi kuwasili jana mchana na ziara hiyo ikifanyiwa kazi kwa yale waliokubaliana, italeta manufaa makubwa kwa nchi hizo mbili.
“Tumezungumza mengi leo, nchi ya Misri ina historia kubwa katika dunia ya sasa, ustaarabu wa maisha ya binadamu ukiachia mbali binadamu wa kwanza inaelezwa aliishi Tanzania (Olduvai Gorge), wasanifu majengo wa kwanza waliishi Misri, ushahidi upo hata leo pyramids leo bado hakuna anayeweza kuzijenga.
“Vitabu vitakatifu vinaandika kuhusu Misri, Mtume Yesu alikimbilia Misri alipotaka kuuawa, ni eneo la kukimbilia wenye shida na sisi tutakimbiza shida zetu kwao ili atusaidie kuzitatua,” alisema Dk Magufuli.
Alisema pamoja na kwamba hatujapakana kimipaka na Misri, lakini maji ya Mto Nile yameziunganisha nchi hizo mbili kwani chanzo cha maji kwenda Mto Nile ni pamoja na Mto Kagera na maji ya Ziwa Victoria ambalo asilimia 51 lipo Tanzania, 44 Uganda na tano Kenya.
Makubaliano
Akielezea kuhusu maeneo ya makubaliano, Rais Magufuli alisema kwanza kutokana na historia ya mahusiano mema na ya muda mrefu baina ya Baba wa Taifa wa nchi hizo mbili; Mwalimu Julius Nyerere na Gamal Abdel Nasser, wamekubaliana kuimarisha mahusiano hayo kwa mustakabali wa nchi hizo mbili.
Dk Magufuli alisema wamekubaliana kuunda upya Kamisheni za Kudumu za Kiuchumi za Pamoja baina ya Tanzania na Misri ,ambazo ziliundwa awali na waasisi hao (Nyerere na Abdel Nasser) wa nchi hizo mbili. “Tumekubaliana hizi kamati (kamisheni) za kudumu ziundwe upya, wakutane mawaziri wan chi hizi mapema,” alisema Magufuli.
Eneo jingine ni kukuza biashara kati ya nchi hizo ambapo alisema kwa kuwa Misri inahitaji nyama na Tanzania ni nchi ya pili kwa mifugo mingi, nchi hiyo (Misri) itajenga kiwanda kikubwa cha nyama nchini ili wasafirishe nyama yenye viwango bora kwenda Misri.
Kiwanda hicho kikikujengwa, ajira kwa Watanzania zitapatikana, mapato na wafugaji watapata kipato zaidi kwa kuuza nyama moja kwa moja katika kiwanda hicho. Katika eneo la biashara, kwa sasa kiwango cha biashara baina ya Misri na Tanzania ni Dola za Marekani milioni 78.02.
Kiwango ambacho jana Rais Magufuli alisema ni kidogo na kinahitajika kuongezeka. Rais pia alieleza kuwa, Misri imekubali kuleta nchini teknolojia ya kilimo cha umwagiliaji nchini ili kukuza sekta ya kilimo.
Asilimia 95 ya nchi ya Misri ni jangwa na asilimia tano pekee huitumia kwa kilimo hasa cha umwagiliaji.
Alielezea eneo jingine kuwa ni sekta ya afya, ambapo amesema wamekubaliana na Rais Al Sisi kuendelea kuleta wataalamu na vifaa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili na Hospitali za Zanzibar na wamepanua wigo kwa kuongeza fedha kuwezesha operesheni za figo kufanyika kabla ya mwaka 2020.
Hata hivyo, hakueleza ni kiasi gani cha fedha walichoongeza. Katika sekta ya afya, pia wamekubali kujenga kiwanda cha kutengeneza dawa nchini hasa ikizingatiwa kuwa Misri ni moja kati ya nchi zenye viwango vikubwa vya ubora wa dawa duniani na hivyo ujenzi huo utaongeza ajira, afya, mapato na kukuza uchumi zaidi.
Kwa mujibu wa Rais Magufuli, uwekezaji wa kampuni za Misri nchini ni wa Dola za Marekani milioni 887.07 na umewezesha ajira nyingi.
Kuhusu utalii, Magufuli alisema wamekubaliana kuendesha sekta hiyo kwa kushirikiana na Shirika la Ndege la Misri na Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL).
Kwa sasa Misri inapokea zaidi ya watalii milioni 10 kwa mwaka na Tanzania ni wastani wa watalii milioni mbili kwa mwaka.
Ulinzi ni eneo jingine ambalo marais hao wawili wamekubaliana ili kuhakikisha amani kwa mataifa hayo inaimarika na Rais Al Sisi aliipongeza Tanzania inavyoshiriki kurejesha amani katika nchi za maziwa makuu na Rais Mtaafu Benjamini Mkapa kwa namna anavyosimamia amani Burundi.
Aidha, Tanzania pia itanufaika katika sekta ya elimu, ambapo marais hao wawili wamekubaliana kubadilishana walimu kwa lugha (Kiswahili, Kiarabu na dini) pamoja na IT.
Hata hivyo, pamoja na makubaliano hayo, Dk Magufuli alisema eneo la Mto Nile bado mazungumzo yanaendelea ili kuhakikisha kuwa maji ya Mto huo yanazinufaisha nchi zote zinazoguswa nao.
“Tunatambua maji ya Mto Nile ndio uhai wa Misri, tunatendelea katika mazungumzo ili mto huo umnufaishe kila nchi husika,” alisema Dk Magufuli.
Alieleza pia kuwa Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein alipata nafasi ya kuongeza na Rais Al Sisi na kueleza changamoto kadhaa za Zanzibar na amekubali kuja tena nchini ili kufanya ziara Zanzibar ambako aliwahi kufika kibinafsi miaka 10 iliyopita.
Eneo jingine marais hao wamesaini makubaliano ya kupambana na rushwa na katika eneo hilo, Rais Magufuli alisema rushwa ni saratani inayohitaji nguvu ya pamoja kuimaliza huku Rais Al Sisi akiisifu Tanzania na Magufuli kwa namna wanavyopambana na rushwa na ufisadi na kueleza ataendeleza ushirikiano katika mapambano hayo.
Rais Al Sisi pia alieleza kuhusu makubaliano hayo na kusisitiza kuwa, Misri itaendelea kushirikiana na Tanzania katika miradi mikubwa ya maji kwa kujenga visima na kilimo cha umwagiliaji pamoja na maeneo ya afya.
“Namshukuru kaka yangu Rais Magufuli kwa makaribisho mazuri, ili ushirikiano uendelee namkaribisha Misri ili kuendelea kujadiliana namna ya kukuza maendeleo ya nchi zetu,” alisema Field Marshal Al Sisi.
Rais Magufuli alieleza kukubali kuitembelea Misri kwa wakati muafaka.
.
↧
Pata Mvuto wa Biashara, Kupandishwa Cheo, Kurudishiwa Mali Uliyoibiwa, Magonjwa Sugu na Mengne Mengi
Kutana Maajabu ya Mtabibu CHIEF SULTAN(MAKATA WA MAKATANI) Mganga wa Waganga Sasa Yupo Mikoa Yote Tanzania
Pia anatoa Tiba kwa Njia ya Simu ukiwa popote Pale Tanzania au Nje ya Tanzania..
CHIEF SULTAN ni Mtabibu na Mtafiti wa Dawa za Asili ya Africa, na Duniani Katika utoaji wa Tiba za Asili..
Je unasumbulia na Mapenzi..?
(Umeachwa na Umpendae awe Mume/ Mke au mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine na Bado Unampenda?) Umejaribu sehemu Nyingi bila Mafanikio?Wasiliana na CHIEF SULTAN Akusaidie Kumshika Umpendae Asikusaliti(LIMBWATA) Kumtawala Mpenzi wako kwa sababu Maalum..Anauwezo wa Kusambalatisha Mahusiano yao ndani ya siku Moja tu.
Je Unasumbuliwa na Madeni?
Biashara yako Haina wateja?
Unatatizo la kutokushika Mimba na umehangaika sehemu nyingi bila mafanikio?
Wasiliana na CHIEF SULTAN Kwa Majibu ya Maswali yako..
Anasafisha NYOTA na Kutoa PETE za BAHATI kuendana na NYOTA yako. UTAJIRI USIO NA MASHARTI.(Magic Wallet_Pochi ya Maajabu Isio Isha Hela)
KUWA MAARUFU na KUJULIKANA
Kupandishwa CHEO na HESHIMA Mahala pa KAZI.
Utapewa Nguvu ya Kujilinda na MALI ZAKO zako na Mwili wako.. Huzuia Chuma Ulete katika Biashara.. Hurudisha MALI zilizo Potea au KUDHULUMIWA..
Mvuto wa Biashara na Mwili wako.
Hutibu kabisa Nguvu za Kiume na Kurefusha Uume kwa saizi Unayotaka.
Magonjwa Sugu(Miguu Kufa Ganzi, kisukari, Presha, Pumu nk.)Humaliza Kesi za Muda mrefu ndani ya siku 14 tu.
Anatoa NDAGU Zisizokuwa na Masharti.. Kwa maelezo Zaidi wasilina nae kwa
whatsapp +255 0658 316 976
Call +255 755 911 233
↧
Rais Magufuli Ahamisha Uwanja wa Michezo Dodoma
Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA) Dodoma ilitenga Ekari 143 zilizopo Nara Barabara ya Singida nje kidogo ya mji wa Dodoma kwa ajili ya ujenzi wa uwanja na kituo cha michezo kitakachojengwa kwa msaada wa serikali ya Morocco.
Waziri wa Habari, Mwakyembe amesema kuwa Rais Magufuli alitoa oda ya uwanja huo kuhamishwa na kupelekwa maeneo yaliyo karibu na mji wa Dodoma ili kutoka fursa kwa vijana na watoto kutumia uwanja huo pindi utakapokamilika kwani sehemu ambayo ilitengwa awali ni mbali sana kutoka mjini Dodoma.
"Tunamshukuru sana Rais wetu wa Tanzania Magufuli kwa kuikumbuka sekta ya michezo kwa kuomba Morrocco watujengee eneo changamani, walio wengi wanafikiri ni kiwanja cha mpira wa miguu lakini hapana hili ni eneo changamani litakuwa na michezo ya aina yote.
"Mwanzoni kama mnakumbuka tulipata eneo Nara eneo kubwa tu tuliomba ekari 150 tulipewa lakini Mhe. Rais Magufuli aliona kuna umbali kutoka Dodoma mjini mpaka Nara zaidi ya kilomita 70 akaona siyo rafiki, yeye angependa kuona vijana wake wa shule ya msingi na sekondari wakitoka shule wanakimbia uwanjani na umbali usiwe kikwazo" alisema Mwakyembe
"Mwanzoni kama mnakumbuka tulipata eneo Nara eneo kubwa tu tuliomba ekari 150 tulipewa lakini Mhe. Rais Magufuli aliona kuna umbali kutoka Dodoma mjini mpaka Nara zaidi ya kilomita 70 akaona siyo rafiki, yeye angependa kuona vijana wake wa shule ya msingi na sekondari wakitoka shule wanakimbia uwanjani na umbali usiwe kikwazo" alisema Mwakyembe
Aidha Mwakyembe anadai kuwa Rais Magufuli aliagiza litafutwe eneo lingine
"Rais Magufuli aliagiza litafutwe eneo karibu na Dodoma mjini tujenge hiyo 'stadium' na kwa bahati nzuri sana agizo la Rais lilitekelezwa, tunamshukuru sana Mkuu wa Mkoa wa Dodoma kuhakikisha tunapata eneo zuri kuelekea Dar es Salaam karibu na Nane Nane linaitwa Zuguni ambapo sasa tumepata ekari 300 na hizo zote tunazihitaji kwa sababu tunataka eneo hili changamani liwe la mfano katika ujenzi wa viwanja Tanzania kwa sababu tunataka baadaye kuwa na hoteli, kuwe na hosteli kwa vijana, tuwe na majumba makubwa ya michezo" alisisitiza Mwakyembe
Wahandisi, wabunifu na wataalam wa udongo kutoka nchini Morocco wameingia nchini Tanzania kufanya ziara na tathmini juu ya ujenzi wa eneo hilo changamani Dodoma
↧
Uhuru Kenyata Aruhusu Maandamano ya Wakenya Wanaompinga na Amewataka Polisi Wawape Ulinzi
Rais Uhuru Kenyatta huenda akaingia katika vitabu vya kumbukumbu na historia kwa marais wa Afrika kwa kuamua kuruhusu maandamano ya amani kupinga ushindi wake alioupata katika Uchaguzi Mkuu wa Agosti 8.
Kenyatta amewataka polisi kujizuia kutumia nguvu kubwa na badala yake wawape ulinzi wakati wa maandamano hayo ya amani na yanayoruhusiwa kisheria kwa watu ambao hawafurahii matokeo ya uchaguzi uliopita.
Rais Kenyatta alisema hayo jana alipokuwa akitoa ujumbe kwa wagombea walioshindwa katika uchaguzi huo uliofanyika Jumanne iliyopita.
Kenyatta alisema hayo akiwa Jengo la Harambee alikokwenda kukutana na Kamati ya Maandalizi ya Hafla ya kuapishwa kwake.
Katika ujumbe huo uliomlenga zaidi Raila Odinga aliyekuwa mgombea urais kupitia muungano wa Nasa, Kenyatta aliwataka wagombea wote ambao hawakuridhishwa na matokeo ya uchaguzi wachukue hatua zilizobainishwa na Katiba ili kupata wanachotaka.
“Marafiki zetu ambao hawataki kukubaliana na matokeo ... tumenyosha mkono wetu wa udugu kwao ... watumie njia zozote zilizobainishwa katika katiba kuelezea kutoridhishwa kwao,” alisema.
“Wale wanaotaka kushawishi wengi wagome wanaweza kufanya hivyo, lakini kwa kuzingatia vifungu vya sheria. Mwishoni mwa siku sisi sote ni Wakenya. Hakuna haja ya kudhuriana. Hakuna haja ya kuharibiana mali...tunawashukuru polisi kwa kazi nzuri lakini waendelee kujizuia.”
“Polisi wako tayari kuwalinda wakati mnafanya maandamano na wale waliochukia waelewe kwamba hawahitaji kibali changu wala cha Jubilee kufanya maandamano ya amani.”
Hata hivyo, alitoa onyo kali kwamba serikali haitavumilia maandamano yatakayosababisha vifo na uharibifu wa mali za watu kutokana na vurugu.
Vilevile alitoa onyo dhidi ya waporaji na waharibifu wa mali katika baadhi ya maeneo ya nchi, ambako yameripotiwa maandamano baada ya uchaguzi.
“Wakenya wengi wamesema uchaguzi umepita na wamerejea kazini. Hawataki maandamano ya ghasia. Msivuruge maisha ya watu wengine. Kama serikali hatutaruhusu uharibifu wa mali wala upotevu wa maisha na uporaji.”
Rais Uhuru alitoa kauli hiyo baada ya viongozi wa muungano wa Nasa kuhamasisha wafuasi wao kukataa matokeo yaliyompa ushindi Uhuru na makamu wake, William Ruto.
Baada ya kazi ya kuhesabu kura kukamilika, Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) ilimtangaza Kenyatta kuwa mshindi kwa kura 8,203,290 sawa na asilimia 54.27.
IEBC ilisema mgombea urais kwa muungano wa Nasa, Raila Odinga alipata kura 6,762,224 sawa na asilimia 44.74 matokeo ambayo wanayapinga.
Wakiitikia wito wa viongozi wao kati ya Jumatano na Jumamosi maeneo, ambayo ni ngome ya upinzani ya Kisumu, Kibera, Homabay na Migori yalikumbwa na vurugu na soko la Garissa lilichomwa moto.
Nasa walidai kwamba, kwa mujibu wa vyanzo vyao kutoka ndani ya IEBC Raila alishinda kwa kura milioni nane akifuatiwa na Uhuru. Walidai wizi huo ulifanikishwa kwa kudukua kompyuta iliyokuwa inahifadhi matokeo na kumbukumbu nyingine.
Juzi, akizungumza na wafuasi wake waliojitokeza kwa wingi katika eneo la Kibera, Raila aliwataka wafuasi wake wote kususia kazi jana ili kuomboleza vifo vya waliouawa katika makabiliano na polisi.Pia, alisema atatoa msimamo leo wa nini cha kufanya.
Katika kile kinachoonekana kuwa ni kutii wito wa serikali, watu walionekana kupuuza wito wa Raila wa kususia kazi kuomboleza watu waliouawa katika makabiliano kati ya polisi na waandamanaji waliokuwa wanapinga matokeo ya uchaguzi wa urais.
Wengi walionekana barabarani wakirejea kwenye shughuli zao jana na kuendelea na maisha ya kawaida.
↧
↧
Usikubali Kuaibika.......Pata Tiba ya Nguvu za Kiume Utunze Heshima Yako
Tatizo la kukosa hamu ya tendo la ndoa au upungufu wa nguvu za kiume limekuwa kubwa sana, sio Tanzania tu bali duniani kote.
UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME HUSABABISHA MAMBO KAMA:-
☆Kukosa hamu ya tendo la ndoa
☆Uume kusimama kwa ulegevu
☆Kuwahi kufika kileleni
☆Kushindwa kurudia tendo kwa wakati
☆Kuchoka sana baada ya round ya kwanza na hata kukinai kabisa.
@natural beauty pro. Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo hata kwa wenye kisukari kwa:-
1.HANDSOME UP ORIGINAL ni kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @220,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 7.5 @140,000/=
3.Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @150,000/=
4.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni na kurudia tendo hata mara 3 bila kuchoka @130,000/=
5.DISCREET.Ni dawa ya kuondoa mvi milele na zisiludi tena @130,000/=
KWA BIDHAA HIZI NA NYINGINE NYINGI TEMBELEA UKURASA WETU WA INSTAGRAM :-
@natural2162
@natural2162
@natural2162
Wasiliana nasi Popote ulipo duniani kwa no (+255)
0759029968 na 0659618585
NB:Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa NATURAL BEAUTY pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.
Bidhaa zetu zimetengenezwa kwa mimea na matunda na hazina kemikali wala madhara kwa mtumiaji. Zimethibitishwa kiafya.
< WELCOME ALL>
↧
Fid Q Ampinga Waziri Mwakyembe
Msanii Fareed Kubanda ambaye wengi humuita 'Fid Q', amejibu kauli ya Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Harrison Mwakyembe aliyosema wasanii wasiimbe siasa, na kusema kuwa siyo rahisi kwa wasanii kuacha kitu kitu hicho.
Fid Q amesema Waziri hakuwa sahihi kusema hivyo, kwani siasa ipo kwenye maisha yetu ya kila siku, ambayo wasanii ndiyo kitu ambacho hutazama ili kuweza kufanya kazi zao.
"Nafikiri suala la Waziri wa Habari kusema wasanii wasiimbe siasa halikuwa sahihi, nafikiri labda alitaka kusema wasanii wasiwaimbe wanasiasa, kwa sababu siasa ni sehemu ya maisha yetu, na tunaguswa nayo kwa namna moja au nyingine, tunataka au hatutaki, na sanaa ni kitu ambacho hakina mipaka ili mradi hujavuka mstari, na kazi ya msanii ni kuelimisha jamii si tu kuburudisha", alisema Fid Q.
Fid Q aliendelea kusema kuwa hata mafanikio ambayo Mh. Waziri aliyazungumzia, anatakiwa atambue kuwa msanii kufanikiwa sio kuwa na mali tu, hata kubadilisha jamii kupitia sanaa yake ni mafanikio makubwa.
"Bob Marley aliimba siasa mpaka leo tunatambua legacy yake inaendelea kuishi, Fela Kuti pia, alafu mafanikio ya msanii siyo lazima masuala ya pesa, magari sijui majumba, mafanikio kwa msanii ni namna sanaa yake inaweza kubadilisha jamii, na kuamini kwamba pesa, magari na nyumba za kifahari ndiyo vitu vya mafanikio, si nadharia nzuri na yenye busara kwenye jamii", alisema Fid Q.
↧
Sumaye: Sipo Tayari Kurudi CCM Kwa Mateso, Bora Waninyang'anye Kila Kitu
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA ambaye pia ni Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye amefunguka na kusema licha ya mambo anayofanyiwa na serikali ikiwa pamoja na kunyang'anywa mashamba yake lakini hawezi kurudi CCM.
Sumaye amedai kuwa toka alipohama chama hicho na kuingia upinzani wapo viongozi walitamka wazi kuwa dawa yake ni kupokonywa mali zake mpaka awe masikini na kudai hayo mambo ndiyo yameanza lakini hayawezi kumfanya kurudi tena katioka chama hicho.
"Hata lile lililotokea Mwabepande nililitegemea kama mtakumbuka kipindi nilichohama kutoka CCM na kuja upinzani mwaka 2015 katika kipindi cha kampeni wapo viongozi walitamka wazi kuwa huyu dawa yake kunyang'anywa mali zake mpaka awe masikini, nilipoanza kuandikiwa barua mara sijafanya hiki sijui sijafanya hiki nikajua wazi kuwa hakuna sababu nyingine zaidi ya sababu za kisiasa na nina adhibiwa kwa kuwa nimekwenda upinzani" alisema Sumaye
Aidha Sumaye amekiri kuwa mashamba hayo aliyapata kwa njia halali na siku zote amekuwa akiyalipia kwa muda wote huo na kusema mashamba yake yeye amekuwa akiyaendeleza tofauti na inavyoelezwa kuwa mashamba hayo hayaendelezwi.
"Mimi nitaiachia mahakama iendelee mpaka hapo itakaposema ama imeshindwa ama nifanye nini kama wanafikiria mimi nitarudi CCM kwa kuteswa, nasema sirudi CCM eti kwa sababu nateseka" alisisitiza Sumaye
Serikali imetangaza kuchukua mashamba mbalimbali ya wananchi ambayo hayajaendelezwa kwa muda mrefu na wamiliki wa waeneo hayo, jambo ambalo limemkuta na Mhe. Sumaye kwa mashamba yake mawili kudaiwa kuchukuliwa na serikali kwa kigezo hicho hicho kuwa hayajaendelezwa kwa muda mrefu.
↧
Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.
NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.
MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA.
MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.
NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,
Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605
DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.
↧
↧
Shilole Apangua Madai Ya Kuiba Mume Wa Mtu
Msanii Zuwena Mohamed 'Shilole' amekanusha zile tetesi zilizokuwa zinamuandama za kuiba mume wa mtu na kudai jambo hilo halina ukweli ila watu wamezoea kumuongelea vibaya kwa kuwa yeye ni mtu maarufu.
Shilole amefunguka hayo baada ya kuandamwa takribani majuma mawili hivi sasa kuwa amevunja ndoa ya mwanamke mwenzake na hatimaye kumchukua mwanaume huyo jumla jumla na kukaa naye nyumbani kwake jambo ambalo lilipelekea watu wengi kumtolea maneno kwenye mitandao ya kijamii.
"Siyo kweli, sijawahi kuiba mume wa mtu mimi. Ila huyo mwanaume ni kweli alikuwa na mke lakini walisha achana siku nyingi hivyo kuwa naye siyo sababu ya kuivunja ndoa yao", alisema Shilole.
Pamoja na hayo, Shilole ameendelea kwa kusema kuwa anatarajia kuolewa siku si nyingi kutokea sasa japo hakutegemea jambo hilo kutokea kwake tena.
"Panapo majaliwa nategemea kuolewa mwezi wa 10 au 11 mwaka huu haupinduki lazima ntakuwa nimeolewa. Kiukweli sikutamani kabisa kuolewa kwa sababu nilishaufunga ule ukurasa lakini imetokana tu ushawishi wa mwanaume niliyekutana naye. Wakwe zangu wamenipokea vizuri siku nilivyotambulishwa na wamenipenda kiukweli kwa kuwa mimi nipo vizuri kila sehemu", alisema Shilole.
Katika hatua nyingine, Shilole amewataka watu watambue kuwa yeye siyo chanzo cha migogoro ya kuvunjika kwa ndoa ya mpenzi wake wa zamani Nuh Mziwanda kama watu wanavyodhani.
"Mimi kiukweli siyo chachu ya ndoa ya Nuh Mziwanda na Nawal kuvunjika hata kidogo kila mmoja ana mambo yake anafanya lakini nashangaa kwanini nahusishwa mimi kwenye mambo yao yakitokea, maana hata wakigombana chumbani wanasema mimi ndiyo chanzo. Siyo sawa kiukweli maana yameshapita ile kitu lakini nashangaa bado kuendelea kuwepo kwenye midomo ya watu", alisisitiza Shilole.
Kwa upande mwingine, Shishi amedai hata akiolewa hatoweza kubadilika kwa kuwa kazi yake haiwezi kuingiliana na ndoa yake hata siku moja
↧
Eneo la Maonyesho ya nanenane Dodoma sasa kujengwa viwanda
Eneo la maonyesho ya nanenane lililopo Nzuguni nje kidogo ya mjini wa Dodoma litamegwa kwa ajili ya kuanzisha viwanda.
Uamuzi huo umetangazwa leo Jumanne na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Jodarn Rugimbana wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mjini hapa.
"Tutagawa eneo hilo lenye ukubwa wa ekari 400 kwa ajili ya viwanda na litakalobakia litatengenezwa uwe uwanja wa kimataifa,"amesema.
Amesema katika maonyesho yaliyomalizika wiki iliyopita ambayo yamesimamiwa na mkoa baada ya kuondolewa kwenye usimamizi wa Chama cha wakulima (Taso) wamefanikiwa kukusanya Sh 226 milioni.
↧
Q Chief: TID ana matatizo ya akili........ Naomba Aniache, Apambanane na Hali Yake!
Msanii Q Chief amemchana swahiba wake wa kipindi kirefu Khaleed Mohamed 'TID' kuwa ana matatizo ya akili na ndiyo maana anazungumza vitu visivyomuhusu kwa jamii.
Q Chillah amebainisha hayo baada ya kuwepo na ugomvi miongoni mwao hivi karibuni ambapo TID alihojiwa na EATV kuhusu suala hilo akadai yeye hamfahamu msanii anayeitwa Q chief na wala hana urafiki naye.
“Mimi naona kama watu wazima kila mtu angeangalia na kupambana na hali yake na kuangalia jinsi gani anaweza kurudi kwenye nafasi yake ya muziki.
" Kwa nini kila siku anizungumzie mimi nahisi kuna kitu special amekiona kwangu na hataki kuniambia hivyo atakuwa ana matatizo.
"TID ana matatizo ya kisaikolojia hivyo anatakiwa ajitathmini kiundani, kama mpaka waheshimiwa wameamua kumsaidia lazima aonyeshe muelekeo ili waendelee kuwa na imani na yeye", alisema Q Chillah.
Kwa upande mwingine, Q Chillah amesema hatopenda mambo ambayo ameimba kwenye tungo zake mbalimbali yaje kuwakuta watoto wake
Kwa sasa Q Chief anafanya vyema na wimbo wake mpya 'Naogopa' ambao ameuachia siku za karibuni.
↧
Pata Tiba ya Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za:
FUUl POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri
TUPO TZ DAR ES SALAAM .HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE
TUPO TZ DAR ES SALAAM .HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE
↧
↧
Jackline Wolper Hajaipenda Hii Katuni......Tazama Hapa Alivyomchana Madee
Muigizaji wa filamu Bongo, Jacqueline Wolper hajapenda kitendo cha msanii mwenzake kumtengezea katuni aliyoitumia katika video yake bila makubaliano na hivyo kamvaa na kumpa ONYO Kali.
Kupitia amtandao wa Instagram Wolper ameandika maneno yanayoashiria kukerwa na kitendo hicho cha msanii wa muziki, Madee a.k.a Rais wa Manzese na kumtaka msanii huyo awasiliana naye endapo atahitaji kufanya biashara hiyo.
"Embu ona jamani macho natia huruma kama na upwiro kilo 200 …hii mikaka yetu yakibongo kuna mida inaboa kuna mida inakuwa powa ..sasa Madee Rais wamnzese nikuulize swali…ulishindwa nini kunyanyua ka cm kako nakunipgia ata kinafk nakunambia unanivdio queen katuni sjui sanam unajua wewe…." Ameandika Wolper na kuongeza;
"Acha dharau wewe pumbavu piga cm omba kwanza….ata kma umlipi m2 sisi tunasaidiana wote wasanii leo kwangu kesho kwako,🙄👉. nakunishika kimahaba umenishika una dhambi wewe kaka na suit umenivalia kma unaenda kutoa posa kwa masawe🙄..sasa onyooo siku nyingne ombaga utapewa acha kuparamia kama vile unaomba round kwa kimada wako kwanza unitafute utoe ata faini ya kuniweka macho kama nimevuta ugoro…ila nyimbo kali nisiwe mchoyo nanimependa idea ila mwambie alinichonga nakunipa hyo shepu nitampasua 🙄"
Madee alitumia sura ya Wolper katika video yake mpya ‘Sikila’ ambayo amemshirikisha Tekno kutoka nchini Nigeria.
↧
Wapiga Debe Waanza Kuondolewa Rasmi Dar es Salaam
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limeanza kutekeleza operesheni iliyoitangaza wiki iliyopita kwa kuwaondoa wapigadebe kwenye vituo vya daladala kutokana na kuwa chanzo cha wizi.
Kaimu Kamanda wa Kanda Maalum Dar es Salaam, Lucas Mkondya, jana alisema kuwa, operesheni hiyo imeanza jijini baada ya kukithiri kwa kesi zitokanazo na wizi kwenye vituo hivyo.
Alisema kwa siku kunaripotiwa matukio 20 hadi 50 ya wizi kwenye vituo vya daladala jijini huku wapigadebe wakidaiwa kuwa kichaka cha wizi huo.
Alisema operesheni hiyo, itakayoendeshwa kwa wiki nzima imelenga kuvifanya vituo hivyo kuwa maeneo salama.
“Vituoni kunakuwa na wizi na wezi wanafahamika, sasa ni mkakati wa kuwaondoa na kama wiki ikimalizika wizi haujaisha, tutawaondoa wote ambao hawana shughuli maalum vituoni hata kama hawapigi debe,” alisema.
Agizo la Kamanda Mkondya si jipya hata hivyo kwa wapiga debe baada ya maazimio kama hayo, kadhaa kushindwa katika miaka ya nyuma.
Akizungumza Machi 16, mwaka jana jijini, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), George Simbachawane alimtaka Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kuhakikisha anawaondoa wapiga debe wote kwenye vituo vya mabasi kwa sababu hizo hizo.
Waziri Simbachawene alitoa agizo hilo, wakati wa semina kwa wakuu wa mikoa wote nchini ambao walikuwa wameapishwa na Rais John Magufuli, Ikulu katika siku iliyotangulia.
Waziri huyo, alisema kazi ya kupiga debe sio rasmi na isiyo na kipato kitachoweza kumkwamua kijana husika kuondokana na umaskini.
“Namuomba Mkuu wa Mkoa ahakikishe anawaondoa hawa wapiga debe kwenye vituo vya mabasi kwa kuwa wamekuwa wakichangia kutokea kwa uhalifu," alisema Simbachawene.
"Kipato cha mpiga debe kwa siku hakiwezi kumkwamua kimaisha, sana sana wanatumia nafasi hiyo, kufanya uhalifu.
Wanatakiwa kuondolewa haraka waende kwenye kazi hata za kilimo.”
↧
Mrema Amshukuru Rais Magufuli kwa Kumsaidia Kupona Kansa
Mwenyekiti wa Bodi ya Msamaha kwa Wafungwa (Parole), Augustine Mrema ametoa shukrani zake kwa Rais John Magufuli kwa kumsaidia kupata matibabu nchini India na kufanikiwa kupona ugonjwa wa kansa.
Mrema alisema kwa sasa utendaji wake wa kazi utaimarika kwa kuwa ameshapona ugonjwa uliokuwa ukimsumbua na kushindwa kutumikia wananchi na Taifa.
Akizungumza mbele ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Bikira Maria Mama Mwokozi jijini Dar es Salaam, alisema kuanzia sasa atamsaidia vizuri Rais katika nafasi yake ya kuwatetea wafungwa kupitia msamaha wa Bodi ya Parole.
Alisema amefikia hatua ya kutoa shukrani kwa sababu ya muujiza aliopata kutoka kwa viongozi wa Serikali na dini waliomuombea.
Paroko Kiongozi wa kanisa hilo, Cathbert Magaga aliwataka waumini wengine kuiga mfano wa Mrema wa kutoa shukrani na siyo kunyamaza kwa kuwa Mungu atawasaidia.
↧
More Pages to Explore .....