Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Jipatie ofa ya kitabu cha PRESIDENT WIFE....Ni Riwaya Kali ya Kusisimua

$
0
0
OFA KWA JUMAPILI YA LEO 13 August 2017
Jipatie ofa ya kitabu cha PRESIDENT WIFE(Shadow of D.F.E) kwa sh 5000 kupitia mitandao ya Whatsapp 06570725588 na Email eddazaria G.Msulwa.
 
Pia unaweza kusoma kitabu cha SORRY MADAM season one pamoja na SHE IS MY WIFE kila kimoja utakipata pia kwa sh 5000.
HIZI NI BAADHI YA STORY NILIZO ZIANDIKA NA ZINAPATIKANA
1. AIISSII U KILL ME
2. AM NOT A DOCTOR
3. MY LIFE
4.HARD DAY
5. SEX DEALERS
NA NYINGINE NYNGI. KARIBUNI SANA NA NINAOMBA MUZIDI KUENDELEA KUNIUNGA MKONO KATIKA KIPAJI CHANGU HICHI CHA UANDISHI.
WASILIANA NAMI 0657072588 AU 0768516188
KARIBUNI SANA TENA SANA

Sumaye Atingishwa Tena.....Rais Magufuli Afuta Shamba lake la ekari 326

$
0
0
Waziri Mkuu wa mstaafu, Frederick Sumaye ameingia matatani tena baada ya Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero kumpokonya shamba lake lenye ukubwa wa ekari 326 kwa madai ya kutoendelezwa huku ikisema Rais John Magufuli ameridhia hatua hiyo.

Hili ni shamba la pili Sumaye kunyang’anywa baada ya ekari 33 zilizopo eneo la Mabwepande kuchukuliwa Novemba mwaka jana huku Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi akisema Serikali ilifikia uamuzi huo baada ya kiongozi huyo mstaafu kushindwa kuliendeleza kama notisi ya siku 90 ilivyoeleza.

“Oktoba 28, mwaka huu, Rais John Magufuli alibatilisha hati ya kumiliki ardhi ya shamba namba 3,074 lililopo Mabwepande. Shamba hilo lilikuwa na hati namba 53086. Jina la mmiliki lililoandikwa katika hati ni Frankline Sumaye,” alisema Hapi.

Jana, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mvomero, Frolent Kyombo alisema Rais Magufuli amekubali kufutwa kwa umiliki wa shamba hilo kupitia ilani ya ubatilisho ya Mei mwaka huu.

Kabla ya kupokonywa shamba hilo, Kyombo alisema Sumaye alipewa notisi ya siku 30 iliyomtaka kueleza sababu za kutoendeleza matumizi ya shamba hilo kwa shughuli za kilimo kama lilivyosajiliwa lakini hakutoa sababu zilizoweza kushawishi kutofanyika kwa mabadiliko hayo.

“Hatua ya pili, tukatoa ilani ya ubatilisho wa shamba hilo, kuna maelezo alitoa lakini tuliona hayakuwa na uzito, tukayatupilia mbali, shamba hilo alikuwa anaendesha shughuli za kilimo pamoja na ufugaji. Alikuwa anatumia asilimia 15 hadi 20 tu ya shamba lote,” alisema Kyombo.

Alisema mbali na kutumia sehemu ndogo huku nyingine ikiwa haitumiki, Mwenyekiti huyo wa Chadema Kanda ya Pwani alikuwa amekiuka Sheria ya Mipango Miji, namba 8 ya mwaka 2007 pamoja na Sheria ya Ardhi namba 4 ya 1999.

“(Sumaye) alitakiwa kutumia shamba hilo kwa ajili ya kilimo tu na siyo kwa shughuli nyingine za ufugaji, hilo ni kosa kwa mujibu wa sheria hizo. Kwa hiyo mchakato umeashaanza wa kuligawa shamba hilo kwa wananchi na tunategemea miezi minne ijayo tutakuwa tumemaliza taratibu zote,” alisema.

Desemba 15, 2015, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi alitangaza kiama kwa watu wanaomiliki mashamba bila kuyaendeleza huku wakiyatumia kama dhamana ya kukopea fedha benki.

Akizungumza kwa mara ya kwanza baada ya kuteuliwa na Rais Magufuli, alisema kuna watu wamehodhi mashamba makubwa lakini hawayaendelezi, hawayalipii kodi na mbaya zaidi, wanayatumia kukopa fedha benki.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya August 14

Raila Odinga awataka wafuasi wake wagome kwenda kazini

$
0
0
Kiongozi wa Muungano wa Vyama vya Siasa Nchini Kenya (NASA), Raila Odinga amewashauri wafuasi wake kutoingia ofisini kuanzia leo jumatatu ili kuonyesha shinikizo la kutokubaliana na matokeo ya uchaguzi mkuu uliofanyika hivi karibuni.

Ameyasema hayo jana wakati akihutubia wafuasi wake jijini Nairobi kwa mara ya kwanza tangu kutangazwa kwa matokeo, ambapo Rais Uhuru Kenyatta alitangazwa mshindi kitu ambacho kilipingwa vikali na Odinga.

Aidha Odinga alisema kuwa siku ya Jumanne, muungano wa vyama hivyo utatoa msimamo wake kuhusu mwelekeo watakaouchukua kulingana na kutokubaliana na matokeo hayo kwa madai kuwa yamechakachuliwa.

Rais Uhuru Kenyatta alitangzwa mashindi kwa kura 8,203,290 huku Raia Odinga akipata kura 6,762,224 kitu ambacho muungano huo wa vyama vya siasa unapinga matokeo hayo kwa kusema yamebadilishwa.

Hata hivyo, Katibu mkuu wa zamani wa Umoja wa Mataifa, Kofi Annan, ambaye alikuwa mpatanishi mkuu baada ya mzozo wa kisiasa nchini Kenya miaka kumi iliyopita, amemshauri Odinga kutumia hatua za  kisheria kutafuta haki kuhusu matokeo ya uchaguzi wa urais kama anaona kaonewa.

TAKUKURU Kuwachunguza Vigogo wa Escrow kama Wameficha Pesa Nje ya Nchi

$
0
0
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) imesema kuwa imeamua kushirikisha taasisi zingine za kimataifa ili kuwachunguza baadhi ya watuhumiwa wa Escrow kama wamehifadhi fedha nje ya nchi.

Hayo yamesemwa na Afisa Habari na Uhusiano wa taasisi hiyo, Mussa Misalaba alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam, ambapo amesema kuwa watuhumiwa wote wa Escrow bado wanaendelea kuchunguzwa.

Amesema kuwa Takukuru inaendelea kuwachunguza watuhmiwa wote huku ikishirikiana na baadhi ya taasisi za nje na kwamba uchunguzi huo unafanyika kwa umakini zaidi ili haki itendeke.

“Hili jambo linafanyika kwa umakini mkubwa, usione kimya kuna jambo linafanyika, kwa sasa ni mapema sana kusema chochote kuhusu jambo hili kwakuwa linahitautlivu mkubwa kulishughulikia,”amesema Misalaba

Aidha, hivi karibuni TAKUKURU iliwafikisha mahakamani baadhi ya watuhumiwa wa ufisadi na uhujumu uchumi ili kujibu mashtaka yanayowakabili.

Waliofikishwa mahakamani kujibu tuhuma ni pamoja na Theofilo Bwakea, Mkurugenzi wa Kampuni ya VIP Engineering and Markerting, na aliyekuwa Mkurugenzi wa Kampuni ya IPTL, James Rugemalila wote wakikabiliwa kesi ya uhujumu uchumi

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

MCT Yatangaza Ripoti ya Uchunguzi wa Uvamizi wa Studio za Clouds TV

$
0
0
Baraza  la Habari Tanzania (MCT) limezindua Ripoti ya Hali ya Vyombo vya Habari hapa nchini kwa mwaka 2016 (State of the Media Report) ambapo ripoti hiyo hutolewa kila mwaka ili kuushirikisha umma

Pia Baraza hilo linatoa ripoti kuhusu kuvamiwa kwa Studio za Clouds Media na kubaini jinsi tukio hilo lilivyoathiri uhuru wa vyombo vya habari na uhuru wa uhariri.

Akizungumza na wanahabari leo jijini Dar es Salaam, Katibu wa Baraza hilo amesema ripoti hiyo haina lengo baya, bali ni kuweka bayana hali ya tasnia ya habari na kwamba hambo hilo si mara ya kwanza kwani baraza hilo limekuwa likitoa ripoti kama hizo kila mwaka.

“Hatujafanya uchunguzi huu kwa kuwa tuna mapenzi na Clouds Media wala kwa sababu tuna mahusiano na Mkuu wa Mkoa, badala yake tumetoa ripoti hii kwa mujibu wa katiba ya MCT,” alisema katibu.

==>Tazama hapo chini

Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota........Anatoa Mvuto wa Biashara, Kupandishwa Cheo, Kurudishiwa Mali Uliyoibiwa na Mengne

$
0
0
Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota........Anatoa Mvuto wa Biashara, Kupandishwa Cheo, Kurudishiwa Mali Uliyoibiwa na Mengne
 
Kutana Maajabu ya Mtabibu MAALIM MOHAMEDI MASUDI Mganga wa Waganga Sasa Yupo Mikoa Yote Tanzania
Pia anatoa Tiba kwa Njia ya Simu ukiwa popote Pale Tanzania au Nje ya Tanzania..
MAALIM MOHAMEDI MASUDI ni Mtabibu na Mtafiti wa Dawa za Asili ya Africa, na Duniani Katika utoaji wa Tiba za Asili..
 
Je unasumbulia na Mapenzi..?
(Umeachwa na Umpendae awe Mume/ Mke au mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine na Bado Unampenda?) Umejaribu sehemu Nyingi bila Mafanikio?Wasiliana na MAALIM MOHAMEDI MASUDI Akusaidie Kumshika Umpendae Asikusaliti(LIMBWATA) Kumtawala Mpenzi wako kwa sababu Maalum..Anauwezo wa Kusambalatisha Mahusiano yao ndani ya siku Moja tu.
Je Unasumbuliwa na Madeni?
Biashara yako Haina wateja?
Unatatizo la kutokushika Mimba na umehangaika sehemu nyingi bila mafanikio?
Wasiliana na MAALIM MOHAMEDI MASUDI Kwa Majibu ya Maswali yako..

Anasafisha NYOTA na Kutoa PETE za BAHATI kuendana na NYOTA yako. UTAJIRI USIO NA MASHARTI.(Magic Wallet_Pochi ya Maajabu Isio Isha Hela)
KUWA MAARUFU na KUJULIKANA
Kupandishwa CHEO na HESHIMA Mahala pa KAZI.
Utapewa Nguvu ya Kujilinda na MALI ZAKO zako na Mwili wako.. Huzuia Chuma Ulete katika Biashara.. Hurudisha MALI zilizo Potea au KUDHULUMIWA.

Mvuto wa Biashara na Mwili wako.
Hutibu kabisa Nguvu za Kiume na Kurefusha Uume kwa saizi Unayotaka.
Magonjwa Sugu(Miguu Kufa Ganzi, kisukari, Presha, Pumu nk.
Wasiliana nae kwa namba
0655516982
0688856265
0621898709(Whatsapp)

Waziri Lukuvi Azindua Mji Wa Kisasa Arusha........Aviagiza Halmashauri Na Majiji Kuharakisha Kutoa Vibali Vya Ujenzi

$
0
0
Na Nahmoud Ahmad Arusha
Waziri wa ardhi , nyumba na maendeleo ya makazi William Lukuvi amewaagiza viongozi wa halmashauri na majiji nchini kuharakisha utoaji wa vibali vya ujenzi na kuachana na urasimu unaosababisha kuwepo kwa ujenzi holela .

Lukuvi aliyasema hayo jana alipokuwa akizungumza katika uzinduzi wa nyumba  kumi za  mfano za mradi wa mji wa kisasa wa  Safari City  zilizopo Mateves sambamba  na kutoa hati miliki kwa wanunuzi 100 wa kwanza wa viwanja zinazotekelezwa na shirika la nyumba la taifa (NHC) .

Alisema kuwa kumekuwepo na ucheleweshaji mkubwa wa vibali vya ujenzi unaosababishwa na wahusika wenyewe na hivyo kupelekea wananchi hao kujenga kiholela kutokana na wananchi hao kuchoka kusubiri.

Aidha kufuatia hali hiyo alimwagiza mkuu wa mkoa wa arusha Mrisho Gambo kufanya ukaguzi wa mafaili ya vibali vya ujenzi na kuweza kugundua idadi ya watu ambao hawajapatiwa vibali vyao mpaka sasa hivi.

“Unajua idadi kubwa ya wananchi wanaojenga kiholela sio kwamba wamevunja sheria bali wanafanya hivyo kwa ajili ya ucheleweshaji wa vibali kwa hiyo hatua hiyo inasababisha pia kuchelewa kutoana na kusubiri kwa muda mrefu bila kupata jibu lolote”aliongeza Lukuvi.

Awali mkurugenzi mkuu wa shirika la nyumba la taifa Nehemia Mchechu alisema kuwa mradi huo wa kitovu cha mji wa kisasa wa safari city jijini hapa una ukubwa wa hekari 559.4 na ni sehemu ya miji iliyopangiliwa kitaalamu na kwa kuzingatia sheria za mipango miji.

“Mradi huu ulibuniwa na shirika la nyumba kwa lengo la kupunguza uhaba wa makazi kwenye jiji hili ambapo tumetenga maeneo kwa ajili ya waendelezaji kujenga sehemu za biashara,burudani ,utalii,hospitali, elimu,huduma za kijamii kama vile polisi,na zimamoto lakini pia yapo maeneo ya wazi kwa ajili ya michezo na mapumziko”alisema Msechu.

Aidha Mchechu aliziomba taasisi kuunga mkono maagizo aliyoyatoa raisi kwa halmashauri na taasisi zinazohusika kuhakikisha kuwa zinaweka miundombinu  yote muhimu katika maeneo yanayohitajika kuendelezwa na NHC ili kuweza kupunguza gharama za nyumba zinazojengwa

Waziri Mpango awasimamisha kazi watumishi wanne wa TRA

$
0
0
Na Benny Mwaipaja, Songwe/Mbeya 
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, amewasimamisha kazi watumishi wanne wa Idara ya Forodha, katika Mpaka wa Tanzania na Zambia, Mjini Tunduma, ili kupisha uchunguzi wa kudaiwa kuhusika na upotevu wa lakiri 10 zinazotumika kufunga kwenye shehena ya mizigo inayopita mpakati hapo kutoka nje ya nchi.

Mpango amewataja watumishi hao kuwa ni pamoja na Harrison Mwampashi, John Makorere, Stephene Josia na Frank Kessy na kuviagiza vyombo vyote vya Ulinzi na Usalama mpakani hapo viwahoji huku wakiwa wamesimamishwa kazi.

Watumishi hao wanadaiwa kuiba lakiri hizo kumi kutoka ofisi za TRA-Tunduma wanakofanyiakazi, ambapo 4 kati ya hizo lakiri zilikutwa zimefungwa kwenye mizigo ya malori yanayoshikiliwa katika mpaka huo baada ya uchunguzi kufanyika huku malori mengine 5 yakizuiwa baada ya kuonekana lakiri zao zimechezewa.

Taarifa zinasema kuwa baada ya uchunguzi, mawakala ama wamiliki wa malori hayo wamedai walipewa lakiri hizo na watuhumiwa na kwamba uchunguzi zaidi umebaini kuwa kiwango cha mizigo kilichomo kwenye makontena yaliyobeba mizigo ya magogo na kufungwa lakiri hizo za wizi hakilingani na idadi ya
mizigo iliyoko kwenye nyaraka jambo linaloashiria kuwa wanazitumia lakiri hizo kudanganya idadi na uzito wa mizigo yao ili kukwepa ushuru na kodi mbalimbali za Serikali.

“Hakuna kitu muhimu kama uadilifu kwa mtumishi wa Mamlaka ya Mapato na hatutasita wala hatutamwonei aibu mtu yeyote, tutachukua hatua kwa mujibu wa sheria ili kulinda fedha za umma,” alionya Dkt. Mpango.

Alisema kuwa Serikali imebaini baadhi ya watumishi wa Mamlaka ya Mapato na Idara za Forodha mipakani wanashirikiana na wafanyabishara wasio waaminifu kuingilia mifumo ya kukusanyia mapato, kitendo ambacho kinaweza kurudisha nyuma juhudi za serikali kuwahudumia wananchi wake.

Dkt. Mpango amewaonya wafanyakazi wote wa forodha na Mamlaka ya Mapato nchini, kuwa wazalendo na waaminifu katika kukusanya mapato ya Serikali na kuacha kujihusisha na vitendo vinavyokwaza ufanisi wa Mamlaka hayo.

Rais wa Misri Awasili Tanzania kwa Ziara ya Kikazi

$
0
0
Rais wa Misri, Abdel Fattah El-Sisi amewasili nchini Tanzania na kupokelewa na mwenyeji wake, Rais John Pombe Magufuli kwa ziara ya kikazi ya siku mbili. 

Amewasili kwa ndege maalum ya serikali ya Misri na kupokelewa kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.

Shuhudia LIVE Rais Magufuli Alivyompokea Rais wa Misri na Jinsi Mizinga Ilivyopigwa

$
0
0
Tazama hapa moja kwa moja kutoka uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Rais wa Misri, Abdel Fattah El Sisi alivyowasili Tanzania kwa ziara ya kikazi ya siku mbili ambapo mwenyeji wake Rais Dkt, John Pombe Magufuli pamoja na viongozi mbalimbali wamempokea  uwanjani hapo .

==>Tazama hapo chini

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Ikulu yagoma kulipa mabilioni ya zabuni licha ya Mahakama Kuiamuru Ilipe

$
0
0
Hatimaye Ikulu imesema hailitambui deni la Sh1.6 bilioni ambalo Serikali inadaiwa na kampuni ya GBL and Associates Ltd ya jijini Dar es Salaam baada ya kuinyang’anya zabuni ya kununua na kuuza meno ya tembo iliyoshinda miaka 29 iliyopita.

Uamuzi huo umetolewa licha ya kuwapo hukumu ya Mahakama Kuu inayoeleza wazi kwamba Serikali ilikosea kuifutia kampuni hiyo zabuni iliyoshinda bila sababu za msingi.

Nyaraka zinaonyesha kuwa madai ya GBL yaliwahi kufika mezani kwa marais wastaafu Ali Hassan Mwinyi na Jakaya Kikwete ambao waliagiza wasaidizi wao kutafuta ukweli juu ya suala hilo. Tawala hizo zilizopita zilikwishatoa maagizo kampuni hiyo ilipwe.

Mgogoro kati ya Serikali na GBL ulianza mwaka 1988 baada kuinyang’anya zabuni ya kununua tani 16 za meno ya tembo licha kutangazwa mshindi wa mchakato huo na Wizara ya Ardhi, Maliasili na Utalii.

Kwa mujibu wa tangazo la zabuni lilitolewa katika gazeti la Serikali la Daily News la Februari 29, 1988 kupitia Bodi ya Taifa ya Zabuni, mshindi wa zabuni hiyo alitakiwa kufanya malipo yote na kukusanya meno hayo ndani ya siku 30 tangu siku ya kukabidhiwa barua ya ushindi.

Hata hivyo, kabla siku hizo 30 hazijatimia, aliyekuwa kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Wanyapori anayetajwa kwa jina la A. Malemaro alimwandikia mmiliki wa kampuni hiyo marehemu Gabriel Lugendo kumjulisha uamuzi wa Serikali kuifutia kampuni yake zabuni kwa kushindwa kulipa fedha ndani ya siku saba, jambo lililozua madai ya muda mrefu.

GBL iliomba zabuni hiyo ikishirikiana na Taathing Ivory Wares ya Hong Kong ambayo ilikwishakopa benki kukamilisha biashara hiyo. Baadaye Serikali ililazimika kurudisha fedha ambazo kampuni hiyo ililipa.

Jaji wa Mahakama Kuu, Yahaya Rubama aliwahi mwaka 1989 kuamua kuwa uamuzi wa kuifutia zabuni hiyo GBL haukuwa wa haki na uvunjwaji wa mkataba.

Awali, kampuni hiyo ilidai Sh507 milioni ambazo ziliongezeka na kufikia Sh4 bilioni pamoja na riba. Hata hivyo, deni hilo lilipunguzwa hadi Sh1.6 bilioni baada ya makubaliano kati ya Serikali na GBL.

Aprili mwaka huu, Katibu Mkuu Kiongozi John Kijazi aliiandikia GBL akiijulisha kuwa Ikulu imepitia malalamiko yake ikiwamo viambatanisho vyake na hitoria ya suala hilo na kuridhika kwamba madai hayo hayana msingi wa sheria.

Balozi Kijazi anasema Ikulu imeridhika kuwa kampuni hiyo ilifutiwa zabuni ya mauzo ya meno ya tembo kwa kushindwa kulipa ndani ya wakati yaani ndani ya siku saba baada ya kupokea barua ya kuarifiwa ushindi wa zabuni.

Kwa mujibu wa barua ya Kijazi ya Aprili 20, kampuni hiyo haikuwa mnunuzi halisi wa meno hayo ila kampuni ya Ms Tathing Ivory Factory ya Hong Kong ambayo hatimaye ililipia meno hayo na fedha hizo baadaye kurejeshwa kwa kampuni hiyo baada ya GBL kufutiwa zabuni.

Anasema ilibainika pia kuwa kwa mujibu wa Mkataba wa Kimataifa wa Biashara ya Wanyama na Mimea iliyo Hatarini Kutoweka (Cites), kampuni ya Ms Tathing Ivory Factory haikuwa na sifa ya kufanya biashara ya meno ya tembo na nchi zilizosaini mkataba huo, ikiwamo Tanzania.

Hata hivyo, Mkurugenzi Mtendaji wa GBL Thomas Lugendo alisema katika barua yake ya Mei 24 kuwa, Ikulu haijafuata sheria, kanuni na taratibu za nchi kwa kuwataka kulipa fedha ndani ya siku saba wakati tangazo la zabuni lilitoa siku 30.

“Ikulu inasema tumeshindwa kulipa ndani ya siku saba lakini tangazo la zabuni lilitoa siku 30. Kutuambia tulipe ndani ya siku saba ni kinyume na tangazo la zabuni. Hatukuafiki na hata Rais wa Awamu ya Pili Ali Hassan Mwinyi hakuafiki,” anasema Thomas Lugendo.

Kuhusu madai kuwa kampuni hiyo haikuwa mnunuzi halisi wa meno hayo isipokiwa kampuni ya Taathing Ivory Wares Factory, Lugendo anasema: “Hili ni jambo ambalo isingekuwa vyema kulijibu kwa heshima ya Serikali,” anasema Thomas huku akirejea maneno ya Jaji Rubama.

Jaji Rubama alisema katika hukumu yake: “Katika mwenendo wa biashara za kimataifa, zinazotembea ni karatasi za mikataba. Mimi nimeshinda tenda, nauza kwa mtu mwingine, yule wa mwisho ndiye anabeba mzigo wa fedha ambaye kwa hapa ni kampuni ya Taathing.”

Kuhusu kampuni ya Taathing Ivory Factory kutokuwa katika nchi ambayo ni mwanachama wa Cites, Lugendo alimtaka Balozi Kijazi kurejea tangazo la zabuni lililosema waomba zabuni kutoka nchi wanachama na siyo kampuni zinazonunua.

“Sisi ni Watanzania, maombi yetu yametoka Tanzania kule tutakouzia Serikali haihusiki, hata kama tungechukua meno ya tembo tukayahifadhi kama mapambo yetu. Serikali ilishauza inahusika nini baada ya kuyauza?” alihoji Lugendo.

Rais Magufuli, Dangote, Obama kuhudhuria sherehe za kuapishwa kwa Kenyatta

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Dkt John Magufuli na Rais mstaafu wa Marekani, Barack Obama ni miongoni mwa viongozi wanaotarajiwa kuhudhuria katika sherehe za uapisho wa Rais mteule wa Kenya, Uhuru Kenyatta.

Kamati ya maandalizi ya sherehe hizo inayoongozwa na Katibu Kiongozi, Joseph Kinyua imebainisha kuwa imeandaa orodha ya majina ya viongozi wa kimataifa kwa ajili ya kushuhudia tukio hilo la kihistoria la uapisho wa Kenyatta endapo ushindi wa Kenyatta hautopingwa mahakamani.

Kwa mujibu wa Katiba ya nchi hiyo, sherehe za uapisho hufanyika siku 14, baada ya mshindi wa uchaguzi kutangazwa ili kutoa fursa kwa chama chochote kinachotaka kupinga matokeo kufanya hivyo.

Viongozi wengine wanaotarajiwa kualikwa katika sherehe hizo wakiwemo wakuu wa nchi ni pamoja na Rais wa Rwanda Paul Kagame, Rais wa Uganda Yoweri Museveni, Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma na Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari. Wengine ni Kansela wa Ujerumani Angela Merkel na Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May.

Aidha, katika orodha hiyo pia yupo Rais wa Liberia, Ellen Johnson Sirleaf, mfanyabiashara tajiri namba moja Afrika Aliko Dangote, Kiongozi wa Jumuiya ya Ismailia, Aga Khan, Waziri Mkuu mstaafu wa Italia, Matteo Renzi na Rais Xi Jinping wa China.

“Tupo kwenye maandalizi ya sherehe za uapisho wa Rais wakati tukisubiria hatua za kikatiba kukamilika. Orodha hii ni ya marafiki wa Kenyatta, viongozi wa Afrika na viongozi wengine wa kimataifa, tunaotarajia kuwaalika”, amesema mmoja wa wanakamati hiyo ya maandalizi.

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Mipaka na Uchaguzi Kenya, Wafula Chebukati mwishoni mwa wiki alimtangaza rasmi Rais Kenyatta na Naibu wake, William Ruto kuwa washindi katika uchaguzi uliofanyika wiki iliyopita nchini humo.

Tundu Lissu Awapongeza Wakenya kwa Kumchagua Kenyatta......Adai Wangemchagua Odinga Wangekoma!

$
0
0
Rais wa TLS na Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA, Tundu Lissu amefunguka na kusema wao kama CHADEMA waliwaambia watu wa Kenya kuwa kama watarogwa na kumchagua Raila Odinga kuwa Rais wa nchi hiyo wangekoma kwani aliweka wazi ataongoza kama Rais wa Tanzania.

Tundu Lissu anasema kuwa katika uchaguzi uliofanyika nchini Kenya tarehe 8 Agosti 2017 unatoa mafunzo mengi kwa Tanzania kwani Kenya wameweza kupiga hatua kubwa na kutoa haki ya msingi ya kupiga kura kwa wafungwa na Raia wake waliopo nje ya Kenya jambo ambalo Tanzania ni kitu kisichowezekana.

"Kenya inatufundisha umuhimu wa kuwa na Katiba mpya, Katiba ya Kidemokrasia, Katiba inayoweka uhuru kwa wale wanaoshiriki uchaguzi kwa kuweka utaratibu wa kuhakiki taratibu za uchaguzi katika kila hatua na hilo ni jambo muhimu sana, lakini Kenya inatufundisha umuhimu wa kuwa na Demokrasia tumeona wafungwa wakipiga kura, tumeona waandishi wa habari wakiruhusiwa kuiingia gerezani kueleza umma jinsi zoezi la upigaji kura linavyoendelea hata kwa watu ambao wamepata adhabu kwa mujibu wa sheria za Kenya lakini kwetu sisi hicho kitu hakipo kabisa, tumeona raia wanaokaa nje ya Kenya wameshiriki uchaguzi sisi hilo haliwezekani" alisema Tundu Lissu

Aidha Tundu Lissu amesema kwa mambo yote ambayo yameendelea Kenya katika uchaguzi yanatoa funzo kuwa na mfumo wa Demokrasia lakini pia amegusia chama cha CHADEMA kuwa rafiki na Chama Cha Jubilee na kusema siyo dhambi.

"Sisi kuwa na chama rafiki Kenya wala siyo kitu cha ajabu sana, tuna chama rafiki Ghana tunavyama rafiki kila mahali na wakati wa uchaguzi marafiki wanaungana mkono, wakati wa uchaguzi ANC wanaunga mkono CCM, Museven na NRM yake wanaunga mkono CCM na sisi kwenye uchaguzi huo wa Kenya tumeunga mkono Jubilee, na kwenye uchaguzi huu wa juzi Raila Odinga aliwaambia waKenya kuwa wakimchagua ataongoza nchi kama Rais wa Tanzania ilibidi tuwaambie Wakenya kuwa mtakoma" alisisitiza Tundu Lissu

Katika Uchaguzi uliofanyika tarehe 8 Agosti 2017 nchini Kenya tume ya uchaguzi nchini humo ilimtangaza Uhuru Kenyatta kuwa mshindi wa nafasi ya Urais kwa kupata kura zaidi ya milioni nane huku mpinzani wake Raila Odinga na Muungano wa NASA wakishika nafasi ya pili kwa kupata kura milioni sita.

Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) laonywa jinsi lilivyomaliza mgogoro wa Makonda na Clouds.

$
0
0
Kufuatia maoni ya baadhii ya watu mbalimbali na waandishi wa habari kutoridhika na maamuzi ya Jukwaa la Wahariri (TEF), viongozi wamepewa onyo la kutorudia makosa baada ya kukiri.

Katika mkutano mkuu uliofanyika Agosti 13, viongozi hao walikiri kuitisha mkutano na waandishi wa habari Agosti 9 bila ya kupata idhini.

Hatua hiyo ilisababisha kujengeka kwa taswira mbaya kiuwajibikaji, kanuni na utaratibu.

Katika taarifa ya Mwenyekiti Maalum wa TEF, Walace Mauggo imeeleza kuwa jukwaa kwa kauli moja limetoa onyo kwa viongozi wake kutorudia yale ambayo yamejitokeza.

“Baada ya kutafakari na kutathmini mwenendo wa mkutano huo, jukwaa lilobaini kuwepo kwa kasoro kubwa wakati wa kurejesha mahusiano wa kikazi na kiongozi ambaye habari zake zilizuiwa kuripotiwa kwa takribani miezi mitano,” imeeleza taarifa hiyo.

Pia wametakiwa kuhakikisha kunapotokea masuala makubwa kama hayo ambayo yashafanyiwa maamuzi na mkutano mkuu na taasisi nyingine za habari yanarudiswa maamuzi kwa wanachama kabla ya hatua za  mwisho.

Mauggo ameeleza kuwa TEF haitasita kuchukua hatua kwa kiongozi au mtu yoyote atakayeonekana kutishia usalama wa wanahabari, uhuru wa uhariri na vyombo vya habari.

Matokeo Ya Uuzwaji Wa Hisa 560,000,100 Za Vodacom Tanzania Katika Soko La Awali

$
0
0
Toleo la hisa za Kawaida za Kampuni ya Vodacom Tanzania Public Limited Company (“Vodacom Tanzania” au “VODA”) kwa bei ya  TZS 850/= kila hisa lilizinduliwa Alhamisi tarehe  9 Machi, 2017 na kuhitimishwa Ijumaa tarehe 28 Julai, 2017. Toleo lilenga kukusanya jumla ya TZS 476,000,085,000 kutokana na mauzo ya hisa 560,000,100. 
 
Matokeo ya toleo hilo yanaonyesha kuwa kiasi cha TZS 476,000,085,000 kilikusanywa kama ilivyopangwa. Kati ya  mauzo hayo, 60% imeotokana na  mauzo kwa wawekezaji wa hapa Nchini na 40% imetokana na mauzo kutoka kwa waekezaji wa Kimataifa.
 
Taarifa hii inazingiatia idhini ya Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA) kuhusu Toleo hili la Hisa, na Wawekezaji ambao maombi yao yamekubaliwa wataingiziwa hisa zao katika  akaunti zao zinazihifadhiwa na Soko la Hisa la Dar  es Salaam (DSE Central Securities Depository). Stakabadhi za Umilki wa Hisa zinaweza kupatikana kutoka kwa mawakala ambako Hisa husika  zilinunuliwa. 
 
Toleo la Hisa za Vodacom Tanzania limekuwa toleo kubwa zaidi na la kihistoria kufanyika nchini, na kuhusisha Watanzania zaidi ya 40,000 wengi wao wakiwa wanashiriki kwa mara ya kwanza katika masoko ya mitaji hapa nchini.  Kwa hiyo, Toleo hili limewezesha kupanuka kwa ushiriki wa Wananchi katika soko la mitaji na dhamana, na pia katika uchumi wa Taifa.
 
Kwa kuzingatia ratiba iliyoidhinishwa, tarehe 7 Agosti 2017, ndiyo tarehe ya kutangaza matokeo ya toleo. Baada ya kuingizwa kwa hisa katika akaunti za CSD za Wanahisa, hisa zitaorodheshwa katika Soko la Hisa la Dar es Saalam  na mauzo yake kuanza saa 4 asubuhi, tarehe 15 Agosti, 2017. Wanahisa wanahimizwa kupata Stakabadhi za Hisa zao zilizohifadhiwa katika Hifadhi ya Dhamana (CSD) kutoka kwa Mawakala ambako walinunua hisa hizo. 
 
Vodacom Tanzania inafurahi na kujivunia ukweli kwamba Watanzania wengi wamejitokeza kununua hisa zake. Aidha, Vodacom Tanzania inawashukuru wanahisa wote wa ndani na kutoka nje ya nchi kwa imani waliyoionyesha kwake na kuamua kuwa sehemu ya jamii pana inayounganishwa na maono ya kugusa maisha na kuipeleka Tanzania katika ulimwengu wa kidigitali.

Pata Tiba ya Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FUUl POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM .HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Raia Wa Afrika Kusini Kizimbani Kwa Makosa Manne, Ikiwemo Kutumia Visa Ya Kughushi

$
0
0
RAIA wa AfriKa Kusini, Menolaos Tsampos, (61), amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo kujibu mashtaka ya kutishia kwa mtandao, kuishi nchini kwa muda wa miaka minne bila kibali na kutumia paspoti yenye visa ya kugushi.

Mshtakiwa huyo ambaye kabla ya kuanza kusomewa mashitaka yake alitishia kuwapiga waandishi waliokuwa wakimpiga picha kwa kujaribu kurusha mateke na ngumi.

 Amesomewa mashtaka yake hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Cyprian Mkeha ambapo amekana mashtaka yote na amerudishwa rumande hadi hapo upande wa mashtaka utakapothibitisha uhalali wa Visa yake na makazi yake ya kudumu.

Akisoma hati ya Mashtaka wakili wa serikali, Nassoro Katuga amedai, Juni 22, mwaka huu ndani ya jiji la Dar es Salaam, mshtakiwa kwa kutumia mfumo wa kompyuta, alimuandikia barua pepe Costa Gianna Koulos, yenye maneno ya vitisho kwa nia ya kumsababishia Koulos hisia za uoga.

Pia imedaiwa kuwa, Julai 20 Mshtakiwa Tsampos, alimuandikia barua pepe nyingine Koulos yenye maneno hayo ya vitisho na kumpa masaa 48 kumtaka wakae na kumaliza tofauti zao kinyume na hapo atamfanyia kitu kibaya. 

Wakili Katuga ameendelea kudai kuwa mshtakiwa huyo mwenye pasi ya kusafiria namba 246184272,  raia wa Afrika Kusini, Julai 6, mwaka huu alikamatwa akiishi nchini bila ya kuwa na kibali maalumu.

Aidha Agosti 7, mwaka huu katika kituo cha polisi cha Kati, Tsampos, alikutwa akiwa na pasi ya kusafiria yenye namba M00101612 ikiwa na Visa ya kughushi.

Mshtakiwa amekanusha kutenda makosa hayo na amerudishwa rumande baada ya mahakama kuutaka upande wa utetezi kufanya uchunguzi na kuhakikisha kama kweli mshtakiwa anaishi mbezi kama ana visa yake. Kesi hiyo imeahirishwa hadi Agosti 16, mwaka huu.

  
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images