Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Korea Kaskazini: CIA wamepanga kumuua Kim Jong-un

$
0
0
Serikali ya Korea Kaskazini imesema kuwa imepata taarifa kutoka wizara ya ya mambo ya ndani yaKorea Kusini kuwa mawakala wa kundi la kigaidi linaloungwa mkono na Shirika la Ujasusi la Marekani (CIA) na shirika la ujasusi la Korea Kusini wameingia nchini humo kwa lengo la kumuua rais wa nchi hiyo.

Korea Kaskazini imesema kuwa kabla ya kutekelezwa kwa azmio hilo itahakikisha inawasaka mawakala hao na kuwaangamiza bila huruma

Imeyasema hayo wakati wasiwasi ukiongezeka kati ya Marekani na Korea Kaskazini dhidi ya tuhuma za matumizi ya silaha za nyuklia.

Aidha, shirika la habari la Korea Kaskazini limesema kuwa njama hiyo inahusisha kutumiwa kwa silaha kali ya bio-kemikali pamoja na kemikali yenye miale ya sumu.

Hata hivyo, mwishoni mwa wiki, Rais Marekani Donald Trump alisema anatamani kukutana na kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong-un, ili waweze kufanya mazungumzo.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Mbowe Afunguka Mazito Sakata la Madiwani wa CHADEMA Kuhamia CCM

$
0
0
Mwenyekiti wa (CHADEMA) na Mbunge wa Hai Freeman Mbowe amefunguka na kusema ni upambavu mkubwa kutumia zaidi ya milioni mia saba kwa ajili ya kufanya marudio ya uchaguzi wa udiwani wa kata tatu baada ya madiwani wa CHADEMA kudaiwa kununuliwa na CCM.

Mbowe amesema hayo juzi alipokuwa akiongea na wakazi wa Machame Uroki akiwa kwenye ziara yake jimboni Hai na kusema fedha ambazo zinakwenda kwa ajili ya uchaguzi wa marudio zingeweza kufanya mambo mengine ya msingi.

"Gharama ya kurudia uchaguzi wa diwani mmoja ni shilingi milioni mia mbili hamsini, madiwani watatu waliopewa fedha wakaikimbia CHADEMA wakawaacha wananchi huo ni usaliti gharama ya kurudia uchaguzi kwenye kata tatu ni milioni mia saba na hamsini. 

"Hizi ni pesa zenu, hizi ni pesa za Watanzania pesa hizi zingetumia kujenga shule ya msingi kwa Kasagile, hizi ni pesa zingetumika kujenga barabara, tunaacha kujenga hospitali tunakwenda kuzitumia fedha hizi kwenye uchaguzi milioni mia saba na hamsini ni upumbavu mkubwa" alisema Mbowe
Hata hivyo Mbowe amesema kuwa licha ya madiwani hao kununuliwa hata uchaguzi ukifanyika kesho anaamini kuwa chama chake kitaibuka na ushindi kwa kata zote tatu

"Niwaambie tu CCM haki ya Mungu hizo Kata tatu haiondoki hata moja labda watu wa Uroki mniambie mko tayari tuwaachie hizo Kata, tutakesha usiku tutakesha mchana haipotei Kata hata moja waite uchaguzi hata kesho, kuna watu wanafika bei tuachane nao tuna mambo ya kupigana katika maisha yetu" alisisitiza Mbowe

Madiwani wa tatu wa jimbo la Hai walijiuzulu nafasi zao na kusema wanamuunga mkono Rais Magufuli na serikali ya awamu ya tano kutokana na utendaji wake madiwani hao ni pamoja na Diwani wa Kata ya Machame Magharibi, Goodluck Kimaro, Diwani wa Kata ya Weruweru, na  Diwani wa Kata ya Mnadani, Everist Peter Kimati ambao wote wamejiunga na CCM.

Lowassa, Mbowe Wampongeza Uhuru Kenyatta kwa Ushindi

$
0
0
Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kupitia kwa Mwenyekiti wake Freeman Mbowe na Mjumbe wa Kamati Kuu Edward Lowassa wametoa pongezi kwa Rais Mteule wa Kenya Uhuru Kenyatta kwa kuchaguliwa tena kuongoza nchi ya Kenya kwa awamu ya pili.

Mbowe amewapongeza wananchi wa Kenya kwa kuweza kufanya uchaguzi wa uwazi na haki

"Kwa niaba ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), na wapenda Demokrasia wa Tanzania, natoa pongezi kwa chama cha Jubilee na Uhuru Kenyatta kwa kuchaguliwa tena kuiongoza nchi ya Kenya.Lakini pia nawapongeza zaidi wananchi wa Kenya kwa uchaguzi wa uwazi na haki, Mungu ibariki Jumuiya ya Afrika Mashariki" alisema Mbowe

Aidha Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA Mhe, Edward Lowassa pia amempa neno Rais Mteule wa Kenya na kusema kuwa ushindi huo wa pili wa Uhuru Kenyatta ni kwamba wananchi wa Kenya wamezungumza kupitia kura kuwa wana imani na uongozi wake na maono yake katika nchi hiyo.

Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kilikuwa kinamuunga mkono Rais Uhuru Kenyatta katika kampeni mbalimbali na kiliweka wazi uhusiano huo kwa kile kilichodai kuwa Uhuru Kenyatta ni mtu ambaye anasimamia Demokrasia.

Rais Magufuli Ampongeza Uhuru Kenyatta kwa Ushindi Kenya

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 12 Agosti, 2017 amempongeza Rais Mteule wa Kenya Mhe. Uhuru Kenyatta baada ya jana kutangazwa mshindi wa nafasi ya Urais na Tume Huru Ya Uchaguzi Kenya ( IEBC).

Tume Huru ya Uchaguzi Kenya ilitangaza Kenyatta kuwa mshindi kwa kupata kura 8,203,290 (54.27%) dhidi ya mpinzani wake Raila Odinga 6,762,224 (44.74%), kufuatia matokeo hayo Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli ametoa pongezi kwa Uhuru Kenyatta kwa kuchaguliwa kwa mara nyingine tena.

"Nakupongeza Ndg.Uhuru Kenyatta kwa kuchaguliwa kuwa Rais wa Kenya kwa kipindi kingine. Nakutakia mafanikio mema" alisema Rais Magufuli kupitia mtandao wake wa Twitter

Kwa mujibu wa Tume Huru ya Uchaguzi Kenya (IEBC) ilisema kuwa uchaguzi huo ulikuwa wa huru na haki na kudai kuwa umekuwa ni uchaguzi wa kipekee kwa Kenya kwani watu waliojitokeza kujiandikisha na kupiga kura ni wengi zaidi ukilinganisha na chaguzi zilizofanyika kipindi cha nyuma.

Mahakama yaruhusu mkutano mkuu wa club ya simba kufanyika Agosti 13

$
0
0
 Mahakama ya hakimu mkazi Kisutu imetupilia mbali ombi la bodi ya wadhamini wa klabu ya Simba la kutaka kuzuia mkutano Mkuu wa klabu hiyo uliopangwa kufanyika August 13 mwaka huu.

Hakimu Mkazi amesema haitokua busara kuzuia mkutano huo kwani Agenda za mkutano  hazionyeshi kama kuna agenda ya mabadiliko ya mfumo kama ambavyo wadhamini wanadai.

Pia Mahakama imesema sio busara kuzuia Mkutano kwani tayari baadhi ya wanachama wa Simba wanaoishi mikoani wameshawasili hivyo kuzuia mkutano huo ni kuwatia hasara, lakini pia uongozi wa klabu umeshafanya maandalizi.

Na mwisho kabisa mahakama imesema kwa kuwa mlalamikaji ambae ni Mzee Kilomoni ana haki ya kuhudhuria Mkutano Mkuu ni vema akaenda kwenye mkutano huo akaeleza maoni yake.

Rais Magufuli Amteua Bernard Hezron Konga Kuwa Mkurugenzi Mkuu Wa NHIF

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya August 13


Wallace Karia aukwaa urais wa TFF

$
0
0
Mwenyekiti wa Kamati ya uchaguzi mkuu wa TFF Revocatus Kuuli amemtangaza Wallace Karia kuwa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kufuatia uchaguzi wa shirikisho hilo uliofanyika jana Makao Makuu ya Tanzania Dodoma.

Wallace Karia aliibuka mshindi wa nafasi ya Urais wa shirikisho hilo huku nafasi ya Makamu ya Rais ikichukuliwa na Michael Wambura,.

Kwa matokeo hayo Wallice Karia anakuwa mrithi wa aliyekuwa Rais wa shirikisho la Mpira wa Miguu nchini Jamal Malinzi

Baada ya kutangazwa washindi viongozi hao waliweza kula kiapo mbele ya wajumbe wa Kamati ya Uchaguzi, na baada ya hapo Rais mpya wa shirikisho la mpira wa miguu (TFF) Wallace Karia aliwashukuru wajumbe na watanzania kIujumla na kusema kuwa furaha aliyonayo iende kuwa furaha ya kazi kwa kufanya kazi kwa ajili ya maendeleo ya soka la Tanzania.

Hata hivyo Wallace alisema katika uongozi wake uwazi na uwajibikaji ndiyo nguzo kuu na kusema hivi sasa ubabaishaji katika mpira wa miguu sasa umekwisha, ubabaishaji wa soka sasa ni mwisho.

China Yamuonya Trump Kuhusu Matamshi Yake Dhidi ya Korea Kaskazini

$
0
0
Rais wa China Xijinping amemtaka rais Donald Trump kuchunga mtamshi na vitendo vinavyozidisha hali ya kuzua wasiwasi ,chombo cha habari cha kiserikali kimeripoti.

Rais Trump na Korea Kaskazini wamekuwa wakirushiana cheche za maneno huku rais huyo wa Marekani akionya kuikabili kivita vikali Korea Kaskazini.

Lakini China ambaye ni mshirika mkuu wa Korea Kaskazini ametaka pande zote mbili kuwa na uvumilivu.
 
Taarifa ya ikulu ya Whitehouse imesema kuwa Marekani na China zilikubaliana kwamba Korea Kaskazini inatakiwa kusitisha uchokozi
Hofu kubwa inayoendelea kutanda kuhusu mpango wa kinyuklia wa Korea Kaskazini ilizidi baada ya taifa hilo kufanyia majaribio makombora yake ya masafa marefu mnamo mwezi Julai na kisha kutishia kukishambulia kisiwa kimoja cha Marekani

Unasumbuliwa na Kiharusi,Ngiri au Kifafa?......Unatatizo la Nguvu za Kiume, Kuachika au Tatizo la Uzazi? . Kutana na Mtalaamu Huyu Akusaidie

$
0
0
SASA YUPO DAR; Anauwezo wa kutabiri nyota yako na kukuletea mafanikio makubwa katia biashara yako, kazini na malengo yako ya maisha.Pia anatoa pete ya bahati yenye uwezo wa kukuletea mafanikio makubwa na kutimiza ndoto zako.

Je, Umedhurumiwa? unamdai na hakulipi?...Njoo upatiwe dawa ulipwe haraka. Anadawa ya kumvuta mpenzi wako popote alipo kwa masaa 6 tu na kumtuliza asitoke kwako

Je, unaugomvi usioisha na mpenzi wako na unaachwa mara kwa mara? Njoo upate dawa ufurahie penzi tulivu la umpendae.

Anadawa za nguvu za kiume, kuimarisha mishipa iliyolegea, kuongeza homoni na kukufanya udumu katika tendo hadi dakika 45 na unaweza kurudia tendo hata mara 4 bila kuchoka.

Anatibu Busha bila kupasua,uzazi, mshipa wa ngiri,kiharusi,kifafa,kuondoa majini machafu nakadhalika.

Mpigie kwa simu: 0755505099

Japan Yapeleka mtambo wa kutibua makombora ya Korea Kaskazini Yatakayorushwa katika Kisiwa cha Marekani

$
0
0
Japan imepeleka mtambo wa kutibua makombora magharibi mwa taifa hilo kufuatia tishio la Korea Kaskazini kwamba itarusha kombora la masafa marefu katika kisiwa cha Guam nchini Marekani.

Mtambo huo kwa Jina PAC3 (Patriot Advanced Capability-3) umepelekwa katika eneo la shimane, Hiroshima na Kochi ambapo Pyongyang( Korea Kaskazini )  inasema kombora lake litapaa kabla ya kuanguka katika maji ya Guam.
 
Jeshi la kulinda baharini la Japan limeripotiwa kutuma mtambo wa kutibua makombora katika bahari ya Japan likiwa na mfumo wa kufuatilia makombora ya masafa marefu.

Waziri Mkuu: Serikali Italipa Madeni Yote Ya Watumishi

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali italipa madeni yote ya watumishi ambayo yamehakikiwa na kukutwa kuwa ni halali.

“Mheshimiwa Rais, Dk. John Pombe Magufuli alisitisha malipo sababu ya zoezi la kubaini watumishi hewa, sasa kazi hiyo imeshakamilika, yale yaliyobainika kuwa ni halali yatalipwa. Tunataka watumishi mfanye kazi ya kuwahudumia wananchi kwa bidii,” alisema.

Ametoa kauli hiyo jana (Jumamosi, Agosti 12, 2017) wakati akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Uyui kwenye mkutano uliofanyika kata ya Goweko, wilayani Uyui mkoani Tabora.

Akiwa katika wilaya za Sikonge, Urambo, Kaliua na Uyui, Waziri Mkuu alielezwa na baadhi ya wabunge wa mkoa huo kwamba kuna watumishi ambao walihamishwa kutoka manispaa kwenda wilaya za jirani lakini hawajalipwa fedha zao kwa zaidi ya miaka mitano sasa.

Kwa nyakati tofauti, Waziri Mkuu ambaye ameweka utaratibu wa kukutana na watumishi wa umma kila anapofanya ziara za kikazi mikoani, aliwaeleza watumishi wa wilaya hizo kwamba Serikali imeanzisha mfumo wa kielektroniki wa malipo ya mishahara kwa watumishi wa umma ambao unalenga kuondoa tatizo la madai ya malimbikizo ya stahili zao.

“Hivi sasa tunadhibiti uzalishaji wa madeni mapya ya watumishi, hakuna madeni ya matibabu, ya likizo au ya masomo. Kila mtumishi anaruhusiwa kujiendeleza, lakini ni lazima kwanza aandike barua kwa Mkurugenzi wa Halmashauri kuelezea nia yake na akikubaliwa, ndipo aanze kutuma maombi kwenye vyuo. Mtumishi akiamua kuomba chuoni moja kwa moja ndipo alete madai yale, hatapewa chochote kwa sababu ni nje ya utaratibu,” alisema.

Akifafanua utendaji kazi wa mfumo huo, Waziri Mkuu alisema mfumo huo ujulikanao kama LAWSON, unatumika kwenye ajira za watumishi wote nchini, wa Serikali Kuu na wale wa Serikali za Mitaa  na kwamba unasaidia kutunza, kutuma na kuhuisha  taarifa za watumishi kwa wakati na kwa ufanisi tangu mtu anapoajiriwa hadi inapofikia wakati wa kupandishwa madaraja ama kustaafu.

Akifafanua kuhusu upandishaji madaraja ya watumishi, Waziri Mkuu alisema Serikali imeondoa utaratibu wa mtumishi kulazimika kuandika barua ya kukiri kupandishwa daraja/cheo ndipo aanze kupata stahili zake mpya.

“Hii imeondoa ucheleweshaji wa kufanyika marekebisho ya mshahara na pili imeondoa tofauti za mishahara kwa watumishi wenye ngazi moja (sifa sawa za kitaaluma, tarehe moja ya kuajiriwa) ambao walikuwa wakilipwa tofauti kwa sababu mmoja aliwahi kuandika barua ya kukiri na mwingine alichelewa kuandika barua kama hiyo hiyo,” alisema.

“Mimi nimekuwa kwenye utumishi wa umma kwa muda mrefu, sijawahi kuona mtu anaandikiwa barua ya kupandishwa daraja halafu anakataa. Kikubwa ni kwa maafisa utumishi kuona kama kuna watumishi wanastahili kupandishwa madaraja, watume taarifa zao mapema (kabla ya tarehe 10 ya kila mwezi ili waingizwe kwenye mfumo huu, kisha wawaandikie barua za kuwajulisha wahusika. Hata barua ikichelewa kumfikia mtumishi, mshahara wake hautachelewa na kwa njia hii tutaepuka kuweka madeni yasiyo na tija,” alisema.

Waziri Mkuu alitumia fursa hiyo kuwakumbusha watumishi hao wajibu wao wa kuwahudumia Watanzania bila kujali hali zao na akasisitiza kuwa Serikali haitamuonea mtumishi yeyote ambaye anatimiza wajibu wake.

“Napenda kusisitiza kuwa malengo ya Serikali ni kuimarisha utendaji wa watumishi lakini pia Serikali hii haitamvumilia mtu mdanganyifu, mzembe, asiye mwadilifu na mla rushwa. Tukikukamata hatuundi tume kwa sababu tume nazo zinamaliza fedha tu. Tukiwa na ushahidi wa kutosha, tunamalizana hapohapo,”aliongeza.

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

TFF Kuanza Kuchapisha Taarifa Ya Mapato Na Matumizi Ya Fedha Kwenye Magazeti

$
0
0
Na: Genofeva Matemu – WHUSM
Uongozi mpya wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) umetakiwa kufikia Januari mwakani kuwajibika kama mashirika mengine ya mpira wa miguu duniani yanavyowajibika kuchapisha taarifa ya mapato na matumizi kwenye magazeti ili wananchi wapate fursa ya kufahamu namna fedha zinavyopatikana na jinsi zinavyotumika katika kuboresha  na kuendeleza usimamizi bora wa soka nchini.

Rai hiyo imetolewa na Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo  Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe wakati wa kufunga Mkutano Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) jana  katika ukumbi wa St. Gasper Mkoani Dodoma

Aidha Mhe. Mwakyembe aliwapongeza viongozi wapya waliochaguliwa kuiongoza TFF kwa muda wa miaka minne kwa kuwataka kufanya kazi kwa ushirikiano na kwa pamoja katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku huku akiwapongeza washiriki wote waliothubutu kuwania uongozi katika nafasi mbalimbali wakati wa uchaguzi Mkuu wa TFF wa mwaka huu.

Kwa upande wake Rais mpya wa TFF Bw. Wallace Karia amewaahidi wapiga kuwa wake kufanya kazi kwa weledi wa hali ya juu kwani nafasi aliyopewa na wajumbe hao kwa kumuamini ni deni ambalo atalilipa kwa kuleta mafanikio makubwa katika mchezo wa soka.

Bw. Karia alisema kuwa furaha waliyonayo viongozi wote waliochaguliwa kuiongoza TFF kwa muda wa miaka minne iende kuwa furaha ya kazi kwa kufanya yale watanzania wanatarajia kutoka kwao.

Waziri Mkuu Aagiza Kukamwata Kwa Wazazi Wanaowaozesha Mabinti Wao Wakiwa Wadogo

$
0
0
Na Tiganya Vincent-Tabora
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa ameagiza kukamatwa kwa wazazi wenye tamaa ya fedha ambao wamekuwa wakiwakatisha masomo mabinti zao kwa ajili ya kuwaozesha.

Mhe. Majaliwa alitoa kauli hiyo jana Wilayani Uyui katika mkutano wa hadhara

Alisema kuwa kuanzia sasa Watendaji wanatakiwa kuwakamata na kuwafikisha katika vyombo vya dola bila woga wazazi wa binti na wale wa kijana wanaokatisha masomo ya watoto wa kike kwa lengo la kuwaozesha.

Waziri Mkuu alisema kuwa Serikali haitawavulia wazazi na watu wanaochangia kurudisha maendeleo ya wasichana kwa  kisingizio cha kuwafungisha ndoa wakati bado ni wanafunzi.

“Nawaagiza Watendaji wote kuwakamata wazazi wa binti na wale kijana ambao mtawakuta wakiwa wanawaozesha mabinti wao ambao kimsingi walipaswa kuwa shule……msimuogope mtu wakamateni wote wawe wazazi wa binti hata wa yule anayetarajia kuoa ili hatua kali za kisheria dhidi yao ziweze kuchukuliwa” alisisitiza Mhe. Majaliwa.

Aliwaonya pia vijana ambao wanamiliki na kuendesha  pikipiki maarufu kama boda boda ambao wamekuwa wakiwapakia wanafunzi kwa lengo la kuwarubuni ili wajihusishe na vitendo vya ngono kuacha mara moja.

Waziri Mkuu alisema mtu atakayekamatwa Serikali itamfikisha Mahakamani ili aweze kupata adhabu kali.

Alisisitiza kuwa ni vema wakaacha wanafunzi hao wakasoma na sio kuwarubuni.

Mkoa wa Tabora ni miongoni mwa mikoa mitatu hapa nchini inayoongoza kwa mimba na ndoa za utotoni.

Waziri Mkuu Akataa Ombi la Wabunge wa Mkoa wa Tabora

$
0
0
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amekataa ombi la wabunge wa Ulyankulu na Kaliua ya mkoani Tabora ya kuigawa Wilaya ya Kaliua ili kusogeza huduma kwa wananchi waishio kwenye kata na tarafa zilizo mbali.

Hii si mara ya kwanza kwa kiongozi wa juu wa Serikali kutamka hadharani kwamba hawatagawa maeneo mapya utawala.

 Julai mwaka jana akiwa katika ziara ya kikazi katika mkoa huo, Rais John Magufuli pia alikataa ombi la kuugawa Mkoa wa Tabora akisema haoni umuhimu wa kufanya hivyo na badala yake fedha hizo zielekezwe katika kuboresha miundombinu ya barabara, maji na huduma za afya.

“Nataka huduma kwanza mkoa baadaye, huwezi ukaigeuza kila wilaya ikiwa mkoa. Kila unapotengeza mkoa Serikali inaingia gharama. Ninataka niseme ukweli ni nafuu tutekeleze ahadi kwanza,” alisema Rais Magufuli katika ziara hiyo.

Awali, Februari mwaka huu, Rais Magufuli aliridhia kuanzishwa kwa wilaya mpya za Songwe, (Mkoa wa Songwe), Kibiti (Pwani), Kigamboni na Ubungo (Dar es Salaam), Malinyi (Morogoro) na Tanganyika (Katavi).

Kabla ya kutangaza wilaya hizo, mwaka 2015, Serikali iligawanya baadhi ya majimbo mbalimbali kutokana na ukubwa na kupata majimbo mapya 26.

Miongoni mwa majimbo hayo ni Kibamba, Kigamboni, Makambako, Butiama, Tarime Mjini, Bunda Mjini, Tunduma, Newala Mjini, Mbagala, Vwawa, Mafinga Mjini, Nanyamba, Handeni Mjini, Ushetu, Nzega Mjini, Ndanda na Madaba.

Jana, akiwa katika mikutano ya hadhara iliyofanyika Ulyankulu na Kaliua ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya kikazi katika Mkoa wa Tabora, Majaliwa aliwaambia wananchi na wabunge hao kwamba Serikali imesitisha mchakato kutoa maeneo mapya ya utawala hadi itakapotangazwa vinginevyo.

Akijibu maombi ya wabunge hao Magdalena Sakaya (Kaliua) na John Kadutu (Ulyankulu), ambao walisema kuna haja ya kuigawa Wilaya ya Kaliua ili kusogeza huduma kwa wananchi waishio kwenye kata zilizo mbali na tarafa Majaliwa alisema, “Tumesitisha kutoa maeneo mapya ya utawala ili tuimarishe kwanza yale ya awali. Tunaimarisha kwanza miundombinu ya majengo ya ofisi, nyumba za watumishi kwenye wilaya na halmashauri mpya, zikitengamaa tutafanya uamuzi upya.”

Kuhusu migogoro baina ya wanavijiji na maeneo ya hifadhi, Majaliwa alisema Serikali bado inafanya uhakiki wa mipaka katika maeneo ya hifadhi na ikikamilisha mchakato huo na itatoa taarifa.

Ili kuharakisha mchaktato huo, Majaliwa aliwataka wananchi wanaoishi pembezoni mwa vijiji vinavyopakana na maeneo ya hifadhi wasifanye upanuzi wowote hadi uhakiki wa mipaka utakapokamilika.

“Tumeamua kuweka beacons katika maeneo yote ya hifadhi ili kubaini mipaka imepita wapi. Wananchi mkiwaona watu wa hifadhi wanapita huko msigombane nao. Ni hatua ya awali ya kubaini maeneo ya mipaka,” alisema.

Awali Mbunge wa Kaliua (CUF), Magdalena Sakaya alimweleza Majaliwa kwamba wananchi wanashindwa kujenga makazi ya kudumu katika maeneo waliyopo kwa sababu wanatishiwa kwamba wapo hifadhini.

Hata hivyo, Majaliwa alisema Serikali inafanya mapitio na ikilazimu, itabidi ifanye marekebisho ya sheria inayohusu Misitu ya Hifadhi pamoja na sheria inayohusu masula ya wakimbizi.

Pata Tiba ya Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FUUl POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM .HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Kigwangalla Awapa Makavu Vijana kwa Kuwa na Tamaa ya Maisha Mazuri Bila Kufanya Kazi

$
0
0
Naibu waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Khamis Kigwangala, ameweka wazi sababu ya vijana wengi kufeli kwenye maisha na kusema kuwa wanapenda kuishi maisha yasiyo na uhalisia.

Kwenye ukurasa wake wa twitter ambapo alikuwa akijibizana na baadhi ya watanzania wanaotumia mtandao huo kuhusu tabia ya vijana kutopenda kujishughulisha na kuchagua kazi, Dkt. Kigwangala amesema vijana wa sasa hivi wengi wanapenda kuishi maisha ya kwenye mitandao, na kuacha yale yenye uhalisia na kuweza kujishughulisha kujikwamua kiuchumi, huku akiweka wazi malipo pekee sio sababu ya vijana wengi kuchagua kazi.

"Siyo malipo pekee, pia matarjio na matumizi ya vijana, wengi wanataka kuishi maisha ya 'Instagram' na 'Facebook'...badala ya uhalisia, tamaa ya maisha mazuri bila kupiga kazi nalo ni tatizo jingine, kubwa tu!", aliandika Dkt. Kigwangala.

Naibu Waziri Kigwangala aliendelea na mazungumzo hayo na kusema kuwa kwa jinsi hali ilivyo, kuna haja ya kuweka nguvu yenye ukali ili kuweza kutatua hali hiyo, na kushawishi vijana wajitambue kuishi maisha yenye uhalisia.

"Kama mapambano ni makali zaidi sasa tunapaswa tuandae nguvu na mbinu kali za kiwango cha ukali uliopo, siyo kukata tamaa, Na huo ndiyo mwanzo wa tofauti ya waliofanikiwa na wasofanikiwa, kusimama kwenye uhalisia ama kuleta ubishoo kwenye kazi", aliandika Dkt. Kigwangala.

==>Soma tweet zake hapo chini

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images