Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Pata Tiba ya Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FUUl POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM .HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

"Sitaki haya mambo nikae narudia rudia"... Sikiliza jinsi Rais Magufuli alivyomchimba mkwara mzito waziri wa viwanda Charles Mwijage

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli jana alielezea kutoridhishwa kwake na hatua zinazochuliwa na Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji dhidi ya watu waliouziwa viwanda na kisha kuvitelekeza.


"........kwenye hilo ndiyo unanikwaza. Viwanda ambavyo havifanyi kazi vipo tu kwa nini havifutwi ?, Waziri Mwijage unamuogopa nani wakati mimi ndiye niliyekuteua. 

"Nimekuelezea tukiwa ofisini tukiwa kwenye 'cabinet' na hadharani kote hujanisikia, unataka nikuelekeze nikiwa kaburini ?", alisema Rais Magufuli.
 
==>Msikilize hapo chini alivyomchimba mkwara mzito waziri wa viwanda Charles Mwijage

Halima Mdee Awasilisha Pingamizki Mahakamani .......Kesi Yaahirishwa Hadi Septemba 12

$
0
0
Mbunge wa Kawe, Halima Mdee kupitia kwa Mawakili wake amewasilisha pingamizi la awali katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kuwa Mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi yake ya kumtolea lugha chafu Rais Magufuli.

Mawakili watano wa Halima Mdee, wakiongozwa na Hekima Mwesigwa wamewasilisha pingamizi hilo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Godfrey Mwambapa baada ya Wakili wa Serikali Leonard Chalo kudai shauri hilo limekuja kwa ajili ya kitajwa.

Mwesigwa amedai kuwa wana mapingamizi mawili, kwanza hati ya mashtaka ina mapungufu, pia Mahakama hiyo haina mamlaka akisema kuwa Mahakama hiyo haina mamlaka kwa sababu, Mkuu wa Wilaya aliyetoa amri ya kukamatwa kwa Mdee ameshindwa kufuata matakwa ya kisheria.

Baada ya kueleza hayo kesi hiyo imeahirishwa hadi September 12, 2017.

Kauli ya Chadema kuhusu kuzuiwa kufanya Kongamano Geita

$
0
0
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), wametoa tamko lao baada ya jeshi la polisi kuzuia kongamano lililotakiwa kufanyika kumuenzi aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama hicho, Alphonce Mawazo mkoani Geita.

Mmoja wa wanachama wa Chadema, Dr. Mussa Mdede ambaye pia katika kongamano hilo alikuwa mmoja kati ya watoa mada, amesema kitendo hiko cha polisi kuzuia Kongamano ni kitendo kinyume na sheria Namba 5 ya Vyama vya Siasa ya Mwaka 1995.

”Jeshi la polisi linahitajika kuimarisha ulinzi na usalama kwenye mikutano ya hadhara ndivyo sheria inavyosema”. amesema Mdede.

” Kongamano ambalo limezuiwa ni shughuli ya ndani ambayo kimsingi sheria ya vyama vya siasa inatulinda. Kimsingi ni kongamano ambalo lilikuwa halali na tunapofanya kongamano  la ndani hatuhitaji ulinzii wa jeshi la polisi” amesema Mussa Mdede.

Hivyo Mdede amemuomba mkuu wa jeshi la polisi nchini, IGP Simon Sirro kutumia nafasi yake kuwakumbusha polisi majukumu yao kwani kwa sasa anaona wanafanya kazi kwa mwamko wa kisiasa.

"Chadema tunasema, kwanza tunamwambia IGP Simon Sirro kwamba awakumbushe Askari wake kufanya kazi kwa weledi wasifanye kazi kwa kisiasa. Katika awamu hii ya tano jeshi la polisi limekuwa likifanya siasa waziwazi.” Mussa Mdede.

Picha 4: Rais wa Simba SC, Evans Aveva na Makamu wake, Geofrey Nyange Wakiwa Mahakamani

$
0
0
Leo August 7, 2017 Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeahirisha kwa mara nyingine kesi ya kutakatisha fedha na kughushi inayowakabili Rais wa Simba SC, Evans Aveva na Makamu wake, Geofrey Nyange maarufu Kaburu hadi Agosti 16, 2017 baada ya upelelezi kutokamilika.

Kesi hiyo imeahirishwa mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Mwambapa baada ya Wakili wa TAKUKURU, Kishenyi Mutalemwa kueleza kuwa upelelezi haujakamilika na kuomba iahirishwe hadi tarehe nyingine.

Unasumbuliwa na Kiharusi,Ngiri au Kifafa?......Unatatizo la Nguvu za Kiume, Kuachika au Tatizo la Uzazi? . Kutana na Mtalaamu Huyu Akusaidie

$
0
0
SASA YUPO DAR; Anauwezo wa kutabiri nyota yako na kukuletea mafanikio makubwa katia biashara yako, kazini na malengo yako ya maisha.Pia anatoa pete ya bahati yenye uwezo wa kukuletea mafanikio makubwa na kutimiza ndoto zako.

Je, Umedhurumiwa? unamdai na hakulipi?...Njoo upatiwe dawa ulipwe haraka. Anadawa ya kumvuta mpenzi wako popote alipo kwa masaa 6 tu na kumtuliza asitoke kwako

Je, unaugomvi usioisha na mpenzi wako na unaachwa mara kwa mara? Njoo upate dawa ufurahie penzi tulivu la umpendae.

Anadawa za nguvu za kiume, kuimarisha mishipa iliyolegea, kuongeza homoni na kukufanya udumu katika tendo hadi dakika 45 na unaweza kurudia tendo hata mara 4 bila kuchoka.

Anatibu Busha bila kupasua,uzazi, mshipa wa ngiri,kiharusi,kifafa,kuondoa majini machafu nakadhalika.

Mpigie kwa simu: 0755505099

VIDEO: Rais wa Simba Evans Aveva na Makamu wake Geofrey Nyange Kaburu wakati wanaingia Mahakamani leo.

$
0
0
 Leo August 7, 2017 Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeahirisha kwa mara nyingine kesi ya kutakatisha fedha na kughushi inayowakabili Rais wa Simba SC, Evans Aveva na Makamu wake, Geofrey Nyange maarufu Kaburu hadi Agosti 16, 2017 baada ya upelelezi kutokamilika.
 
==>Makosa 5 yanayowakabili
1. Kughushi
Aveva alighushi nyaraka ili kujilipa deni ambalo inadaiwa aliikopesha Simba USD 300,000.

2. Nyaraka za uongo
Walitumia nyaraka za uongo ili kulipa deni kutoka benki ya CRDB.

3. Kutakatisha fedha
Tarehe tofauti Aveva na Kaburu walikula njama za kutakatisha fedha UDS 300000.

4. Kutakatisha fedha
Aveva alijipatia fedha kutoka Barclays bank tawi la Mikocheni.

5. Kutakatisha fedha Kaburu
Kaburu alimsaidia Aveva kupata pesa USD 300,000 kutoka Barclays Bank tawi la Mikocheni. 


==>Watazame hapo chini Rais wa Simba Evans Aveva na Makamu wake Geofrey Nyange Kaburu wakati wanaingia Mahakamani leo.

Mbunge Stephen Ngonyani (Prof. Maji Marefu) Ataka Rais Magufuli aongezewe muda wa kukaa madarakani

$
0
0
Mbunge wa Korogwe Vijijini Steven Hillary Ngonyani alimaarufu kama Profesa 'Maji Marefu' amefunguka na kutaka Rais Magufuli aongezewe miaka mingine 10 ya kuongoza ili atawale nchi hii kwa miaka 20.

Majimarefu  amesema hayo leo wakati wa uzinduzi wa standi mpya ya mabasi iliyopo katika halmashauri ya mji wa Korogwe ambapo amedai kuwa Rais Magufuli anafanya kazi ambayo Watanzania wanaipenda na inaonekana hivyo itakuwa ni jambo jema kama ataongezewa muda zaidi ya kuongoza.

"Rais Magufuli wewe ni jembe sana na wewe umeletwa na Mungu katika watu ambao watasema katika halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM ambayo mimi ni mjumbe, basi mimi nitasema wewe uongezewe miaka hii miaka kumi haikutoshi, uongezewe miaka ufanye kazi miaka 20 na hilo pendekezo la Ilani ya uchaguzi lije mapema Mashekh wapo hapa, viongozi wa dini wapo hapa na sisi waganga wa kienyeji tupo hapa tutakuombea hilo wazo litapita, mtu anayefanya kazi hakuna kumbadilisha badilisha, unafanya kazi ambayo Watanzania wanaipenda tukibadilisha badilisha tunaweza kupata mtu ambaye ataimaliza nchi yetu" alisema Mbunge wa Korogwe Vijijini

Aidha Professa Majimarefu amesema kuwa wananchi wake wamekuwa wanyonge sana na kudai kuwa wao kama viongozi wa Chama Cha Mapinduzi wanashiondwa kusema baadhi ya mambo ambayo yanawarudisha nyuma kwa kuwa wanahofia kuchafua hali ya hewa.

"Rais tunaonewa sana na sisi hatupendi kusema hili kwa sababu ni viongozi wa CCM na serikali ya awamu ya tano haishikilii wabadhirifu, tumefanya mambo mengi Rais lakini kwa nguvu ya wananchi, leo wananchi wangu wanakuwa wanyonge kwa sababu hakuna mahali popote pakuwaletea maendeleo, maendeleo yanaletwa na wakulima, maendeleo yanaletwa na wafugaji lakini watu hawa wahawana maeneo ya kufanya maendeleo yao kwa kuwa maeneo yote yamechukuliwa na wawekezaji" alisisitiza Majimarefu.

Mbali na Profesa Majimarefu Rais wa Awamu ya pili nchini Tanzania Alhaj Ali Hassan Mwinyi amewahi kuzungumza na kutoa maoni yake kuwa kama isingekuwa Katiba ya Jumhuri wa Muungano wa Tanzania kuweka ukomo wa Rais kuongoza nchi basi Rais Magufuli angeongezewa muda wa kuongoza kwa kuwa amekuwa akifanya mambo mengi ambayo wao hawakuweza kufanya wakati wakitumikia nafasi hiyo ya Urais. 

Rais Magufuli: Ni Bora Njaa Kama Hamtaki Kufanya Kazi

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ameendelea kuwaonya Watanzania wenye tabia ya uvivu na kupenda kubweteka bila kujituma, huku akisema wakati wa utawala wake hakutakuwa na vitu vya bure.

Rais Magufuli ameyasema hayo leo alipokuwa akihutubia wananchi wa wilaya ya Korogwe mkoani Tanga waliohudhuria uzinduzi wa kituo cha mabasi (Stand) wilayani humo, na kusema kuwa watu wanaopenda kukaa vijiweni bila kujishugulisha huku wakilalamika njaa na hakuna pesa, ni bora wafe na njaa.

" Wakati wa kukaa kwenye magenge na kupiga maneno umepitwa na wakati, mnakaa kwenye pool unasubiri vitakuja hakuna, vya namna hiyo nataka kuwaeleza havitakuja kwenye utawala wangu, mnakaa mnasubiri tuna njaa tunataka mtuletee, mimi njaa nafuu ikuue kuliko nikuletee chakula, kwa sababu kama mwenzako ana chakula wewe una njaa, hatuwezi tukavumilia vitu vya namna hiyo", alisema Rais Magufuli.

Rais Magufuli aliendelea kusema ni lazima awaeleze Watanzania ukweli kuhusu hilo, bila kujali kuchukiwa kwani atasimamia haki huu akiwa na dhamira ya kwenda mbele.

"Ni lazima niwaeleze ukweli, nafuu mnichukie lakini niwaeleze ukweli, lakini hata mkinichukia hata sura yangu wala haipendezi, lakini mimi nitasimamia haki ya kuwaeleza ukweli, tunataka twende mbele, tunataka tubadilishe nchi, serikali itafanya juhudi zake zote kuwasaidia Watanzania", alisema Rais Magufuli

Rais Magufuli Amgomea Maji Marefu.......Asema hayupo tayari kukaa madarakani kwa muda wa miaka 20.

$
0
0
Rais Magufuli akiwa Korogwe Tanga amesema hayuko tayari kuendelea kuongoza baada ya miaka 10 iliyowekwa kikatiba.

 Ameyasema haya baada ya Mbunge wa Korogwe Vijijini, Steven Ngonyani (Prof. Maji Marefu) kusema Rais anastahili kuongezwa muda ili afanye mambo mengi zaidi.

Maamuzi ya Mahakama kuu kuhusu dhamana ya Manji

$
0
0
Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam Leo imeyatupilia mbali maombi ya dhamana yaliyowasilishwa na   Mfanyabiashara maarufu Tanzania Yusuf Manji baada ya kukubaliana na mapingamizi yaliyowasilishwa na DPP.

Maombi hayo yametupiliwa mbali na Jaji Isaya Arufani.

Kabla ya kutupiliwa mbali, maombi hayo, Manji alisimama na kuieleza mahakama kukataa kuwakilishwa na Wakili Peter Kibatala kwa sababu za kisiasa.

Amedai, alipopeleka maombi ya dhamana alimpa maelekezo wakili Joseph Tedayo lakini alishangaa kesi ilipofika mahakamani hapo kwa ajili ya kisikilizwa maombi yake ya dhamana wakili Kibatala ndiyo alifika kumuwakilisha.

Kutokana na hayo, Manji ameiomba Mahakama mawakili, Alex Mgongolwa, Hudson Ndusyepo na Seni Malimi ndio wawe wanamuwakilisha katika maombi hayo.

 Hivyo DPP akiwakilishwa na mawikili Paul Kadushi na Simon Wankyo walidai kuwa, wamesilisha kiapo kinzani kupinga maombi hayo ya dhamana wakiwa na hoja tatu.

Hoja hizo ni kuwa, Mahakama Kuu haina mamlaka ya kusikiliza maombi hayo ya dhamana na kwamba yanapaswa kusikilizwa na mahakama ya kifisadi kwa kuwa mshtakiwa anakabiliwa na makosa ya uhujumu uchumi.

Ameongeza kiqa vifungu vya kisheria vilivyotumika kuleta maombi hayo siyo sahihi na pia hati ya kiapo iliyoambatanishwa  kuunga mkono maombi hayo ina dosari kisheria ambazo haziwezi kurekebishika.

Kadushi aliiomba mahakama kusikiloza kwanza mapingamizi ya DPP kabla ya kuanza kusikiliza maombi ya dhamana.

Hata hivyo Wakili Mgongolwa akiwakilisha jopo la mawakili wa Manji walikubaliana na mapingamizi ya DPP kuwa ni kweli yana msingi na maombi ya dhamana yanadosari.

Kufuatia kukiri huko, Kadushi aliiomba mahakama kutupilIa mbali maombi hayo ya dhamana.

Akitoa uamuzi, Jaji Arufani amekubaliana na mleta Maombi (Manji) kuwa hawakilishwi na Kibatala. Pia amesema mahakama kuu haina mamlaka ya kusikiliza maombi hayo hivyo ameyatupilia mbali.

Katika maombi hayo ya dhamana, Yusuf Manji anaiomba Mahakama Kuu itengue hati ya kunyimwa dhamana iliyowasilishwa na Mkurgenzi wa Mashtaka (DPP) kwa kuwa ana matatizo ya kiafya akisumbuliwa na matatizo ya moyo.

Kwa mujibu wa hati ya maombi hayo, Manji anadai kuwa anasumbuliwa na maradhi ya moyo  na kwamba ameambatanisha vyeti vya daktari katika maombi yake.

Katika kesi ya msingi,  Manji na wenzake wanatuhumiwa kukutwa na mihuri ya mbalimbali ya JWTZ isilivyo halali vyote vikiwa na thamani ya Sh. milioni 236.5.

Mbali na Manji, washtakiwa wengine ni,  Ofisa Rasilimaliwatu Deogratias Kisinda (28), Mtunza Stoo, Abdallah Sangey (46) na Mtunza Stoo msaidizi, Thobias Fwele (43)

Maelezo ya Waziri wa Viwanda Charles Mwijage Baada Rais Magufuli Kutamka Hadharani kwamba Haridhiki na Utendaji Wake

$
0
0
Jana (August 6, 2017) Rais Magufuli  alitoa kauli ya kutoridhishwa na hatua zinazochukuliwa na Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji dhidi ya watu waliouziwa viwanda na kuvitelekeza ambapo alimtaka Waziri Mwijage kuwanyang’anya na kuwapatia wawekezaji watao viendeleza.

Leo August 7, 2017 Waziri wa Viwanda Charles Mwijage amehojiwa kwenye Clouds 360 Clouds TV na kuelezea kuhusu hiyo kauli ya rais na kutoa hizi kauli.

”Kujenga viwanda sio mchezo, yapo maelekezo ya Rais viwanda vilivyo binafsishwa na havitumiki virudishwe, Rais alichokitegemea kwangu sio kile anachokiona sababu viwanda haviendi kwa kasi anayoiona na hii kuna sababu kadhaa.

“Hii sekta ya viwanda ni multi-sector maana kuna viwanda vipo chini ya Wizara ya Mifugo, vingine maliasili…. kuna viwanda vimechukuliwa lakini havipo kwenye orodha ya viwanda vilivyobinafsishwa, nahitaji Wakuu wa mikoa waingie hapa.

“Kuna watu wengine wameingia kwenye sekta ya viwanda lakini hawajui shughuli yake wengi wanang’ang’ania faida tu…. moja ya masharti ya viwanda watu walitakiwa kuviendeleza lakini kuanzia Ijumaa mimi nitaanza kutenda bila kuwa na maneno.

“Suala la kiwanda cha Mang’ula tayari mgogoro wake umefika Bungeni na mmiliki wake tayari ameitwa Bungeni kuhojiwa, kiwanda cha matairi Arusha tumekiongezea nguvu lakini tunahitaji muwekezaji ataekuwa na nguvu zaidi kwenye uzalishaji.

“Kiwanda cha General Tyre kina historia kubwa zaidi kilikuwa cha jumuiya ya Afrika Mashariki lakini sasa ni mali yetu, siwezi kumsemea Mh Rais najua ana imani na mimi sana ndio maana nilimuomba asinikumbushe tena siku nyingine.

“Anayetaka kujua viwanda vingapi vipo mkoa wa Pwani aanzie mkuranga mpaka zegereni kuna zaidi ya viwanda 20 hapo, kiwanda cha Mgololo mufindi kinafanya kazi lakini kuna baadhi ya shughuli nyingine za uzalishaji zinaendelea nje ya nchi.”  Amesema Waziri  Mwijage

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Tundu Lissu Ampa Makavu Mwijage

$
0
0
Rais wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS) na Mwanasheria wa CHADEMA, Tundu Lissu amefunguka na kumchana Waziri Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Bw. Charles Mwijage kuwa anahamasisha vijana kujiajiri wakati yeye analialia.

Mh Tundu Lissu amesema hayo baada ya kuona video ya Waziri Mwijage akisema kuwa yeye anaipenda sana kazi yake ya Uwaziri na kusema watu ambao wamepewa viwanda wasitake kumponza akapoteza nafasi hiyo.

"Niwaambie watu wote mniepushe na kikombe hiki wote mliopewa viwanda kwa bei ya kutupwa nimepewa amri hivyo viwanda vifanye kazi, naomba msiniponze nina watoto na hii kazi ninaipenda" alisikika Waziri Mwijage.

Baada ya kuona video hiyo Mh Tundu Lissu anasema kuwa mawaziri mbalimbali wamekuwa vinara kuhubiri majukwani na kuwahamasisha vijana waliomaliza vyuo mbalimbali kwamba wanatakiwa kujiajiri wakati wao wenyewe wameshindwa kufanya hivyo.

"Waziri analia kuwa ni yatima, ana watoto, anaipenda kazi, Majukwanii wanahamasisha vijana waliokopeshwa fedha za kugharamia masomo wajiajiri" alisema Tundu Lissu

Jana Rais Magufuli amemsifu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa kuanzisha viwanda mbalimbali lakini amesema kuwa anachukizwa na Waziri huyo anapokuwa mzito kufanya maamuzi ya kupokonya viwanda mbalimbali ambavyo havifanyi kazi na kusema sasa anataka kusikia watu wakinyang'anywa viwanda hivyo.

Ofisi ya Taifa ya Takwimu Yapinga takwimu za GeoPoll kuhusu usikilizaji/utazamaji wa redio na runinga .......Yasema Mfumo wake Hautanbuliki

Mahakama Yatoa ONYO la Mwisho kwa Tundu Lissu

$
0
0
Mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu imempa onyo la mwisho Tundu Lissu kuhakikisha anafika katika kesi ya uchochezi inayomkabili Mahakamani hapo.

Onyo hilo limetolewa na Hakimu Mkazi Mkuu, Godfrey Mwambapa baada ya wakili wa serikali Mutalemwa Kishenyi kudai shauri hilo limeitishwa kwa ajili ya kusikilizwa lakini mshtakiwa Lissu hajafika Mahakamani.

Wadhamini wa Lissu hawakufika pia Mahakamani huku Wakili wa Lissu Jeremiah Ntobesya amedai kuwa mteja wake ana udhuru ambapo baada ya kuelezwa hayo, Hakimu Mwambapa amesema hii ni mara ya pili Lissu hajafika katika kesi hiyo hivyo anatoa onyo la mwisho ahakikishe anafika.

Hakimu huyo amesema kinyume na hapo hatua za kisheria zitachukuliwa ambapo baada ya maneno hayo  ameahirisha kesi hiyo hadi August 14/2017.

Katika kesi hiyo ya uchochezi (Dikteta uchwara) Lissu anadaiwa alitenda kosa hilo July 28/2016 katika eneo la Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Ilala Dar es Salaam.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya August 8

Wakenya milioni 19 kupiga kura Leo Kuchagua Rais na Viongozi Wengine

$
0
0
Wakenya milioni 19 wanashiriki kwenye uchaguzi wa kihistoria leo

Kiongozi wa chama tawala cha Jubilee, Rais Uhuru Kenyatta, anachuana tena na hasimu wake wa kisiasa, Raila Odinga wa muungano mkuu wa upinzani, NASA, kwenye kinyang'anyiro kinachotazamiwa kuwa cha vuta ni kuvute baina ya wawili hao, licha ya kuwepo wagombea wengine saba wa urais.

Uchaguzi huo unaowagharimu walipakodi wa Kenya shilingi bilioni 49 unaelezwa kuwa ghali zaidi ikilinganishwa na uchaguzi katika mataifa jirani.

Zaidi ya wagombea 1,000 watachaguliwa na Wakenya kwenye nafasi za urais, ugavana, useneta, ubunge, uwakilishi wa akinamama na wa kaunti mbalimbali.

Kuna vituo elfu 40,883 vya kupigia kura vitakavyolindwa na maafisa 150,000 wa idara za usalama, na zaidi ya waangalizi 9,000 wa kitaifa na wa kigeni wameidhinishwa kuangalia uchaguzi huu.

Zuma kitanzini tena.........Bunge la Afrika Kusini leo litapiga kura ya kutokuwa na imani nae

$
0
0
Wabunge nchini Afrika Kusini leo wanatarajia kupiga kura ya siri ya kuamua kuhusu hoja ya kutokuwa na imani na Rais wa nchi hiyo, Jacob Zuma.

Baleka Mbete ambaye ni spika wa bunge hilo amefikia uamuzi huo mara baada ya vyama vya upinzani kufungua kesi mahakamani wakitaka ipigwe kura ya siri dhidi ya Rais wa nchi hiyo ya kutokuwa na imani naye.

Aidha, Wabunge hao wanaamini kwamba iwapo kura ya siri itapigwa, basi wabunge wa chama tawala cha African National Congress (ANC) ambao wanampinga Zuma watakuwa na uhuru wa kupiga kura dhidi ya rais huyo.

Chama cha ANC, ambacho kimetawala Afrika Kusini tangu kumalizika kwa utawala wa ubaguzi wa rangi wa Wazungu mwaka 1994, kina idadi kubwa ya wabunge katika bunge la nchi hiyo.

Hata hivyo, hili ni jaribio la hivi karibuni la kutaka kumuondoa madarakani Rais Zuma na linatokea mara baada ya  kumfukuza kazi waziri wa fedha aliyekuwa anpendwa sana na wabunge wengi, Pravin Gordhan pamoja na mawaziri wengine katika mabadiliko yake kwenye baraza la mawaziri mwezi Machi.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live


Latest Images