Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Spika wa Bunge Naye Kamkana Maalim Seif

$
0
0
Ofisi ya Bunge Leo  imeeleza kuwa Spika Job Ndugai amepokea barua kutoka kwa Maalif Seif Sharif Hamad yenye maelezo ya kuwafuta uanachama wabunge wawili Magdalena Hamis Sakaya na Maftaha Abdallah Nachuma akidai wamekosa sifa ya kuendelea na Ubunge.

Taarifa ya ofisi ya Bunge  imeeleza kuwa ofisi ya Spika inayo barua ya Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha CUF Prof. Ibrahim Lipumba yenye kumbukunbu namba CUF/AK/DSM/MKT/05/2017 ya March 22, 2017 ikiliarifu Bunge kuwa Maalim Seif ameshindwa kutekeleza majukumu yake kama Katibu Mkuu hivyo kwa mujibu wa Katiba ya CUF, majukumu ya Katibu Mkuu yatatekelezwa kuanzia tarehe hiyo na Magdalena Sakaya.

==>Soma barua nzima hapo chini 

Kesi ya Yusuf Manji Yashindwa Kuendelea Kisutu.....Wenzake Warudishwa Rumande

$
0
0
Kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili mfanyabiashara,Yusuf  Manji (41) na wenzake watatu imeahirishwa hadi Agosti 9, mwaka huu.

Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi, aimeiahirisha kesi hiyo leo baada ya Wakili wa Serikali Mwandamizi, Kishenyi Mutalemwa, kueleza kuwa ingawa kesi ilipangwa kutajwa lakini mshtakiwa wa kwanza, Manji, yupo Mahakama Kuu

Manji aliwakilishwa na Mawakili, Mpaya Kamala, Seni Malimi na Hudson Ndusyepo.

Wakili Kishenyi aliiomba mahakama kesi hiyo itajwe Jumatano ya Agosti 9, 2017 na upande wa utetezi haukuwa na pingamizi. Upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika.

Katika kesi hiyo, Manji na wenzake wanakabiliwa na mashtaka saba chini ya sheria ya uhujumu uchumi na Usalama wa Taifa kwa kukutwa na vitambaa vinavyotumika kutengeneza sare za Jeshi la Wananchi wa Tanzania vyenye thamani ya zaidi ya Sh200 milioni na mihuri.

Washtakiwa wengine ambao walikuwapo mahakamani ni Deogratius Kisinda (28), Abdallah Sangey (46) na Thobias Fwere (43).

Awali, akiwasomea hati ya mashtaka inayowakabili washtakiwa hao, Wakili wa Serikali, Tulumanywa Majigo alidai kuwa Juni 30, 2017 katika eneo la Chang’ombe ‘A’ wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam, washtakiwa hao kwa pamoja walikutwa na askari polisi wakiwa na bunda 35 za vitambaa vinavyotumika kutengenezea sare za Jeshi la Wananchi Tanzania vyenye thamani ya Sh 192.5 milioni na kwamba mali hiyo ilipatikana kinyume cha sheria.

Katika shitaka la pili, Majigo alidai kuwa Julai Mosi, 2017 huko Chang’ombe ‘A’ washtakiwa hao walikutwa na polisi wakiwa na mabunda nane ya vitambaa vinavyotumika kutengenezea sare za Jeshi la Wananchi Tanzania vyenye thamani ya Sh44 milioni mali ambayo ilipatikana isivyohalali.

Katika shtaka la tatu, inadaiwa pia kuwa katika eneo hilohilo, mnamo Juni 30, 2017, washtakiwa hao kwa pamoja walikutwa na muhuri wa Jeshi la Wananchi Tanzania wenye maandishi ‘Mkuu 121 kikosi cha JWTZ’ bila ya kuwa na uhalali, kitendo ambacho kingehatarisha usalama wa nchi.

Katika shitaka la nne, Wakili Majigo anadai kuwa Juni 30, 2017 kwenye eneo hilo la Chang’ombe ‘A’ Manji na wenzake hao watatu walikutwa wakiwa na mhuri wenye maandishi ‘Kamanda Kikosi 834 KJ Makutupora Dodoma’ wakati hawana uhalali wa kuwa na muhuru huo kitendo ambacho kingehatarisha usalama wa nchi.

Katika shitaka la tano, Manji na wenzake hao wanadaiwa kuwa Juni 30, 2017 huko Chang’ombe ‘A’ walikutwa na mhuri wa Jeshi la Ulinzi la Tanzania wenye maandishi ‘Commanding Officer 835 KJ Mgambo P.0. Box 224 Korogwe’ kinyume cha sheria.

Katika shtaka la sita, washtakiwa hao kwa pamoja wanadaiwa kuwa Julai Mosi, 2017 katika eneo hilo la Chang’ombe ‘A’ walikutwa na askari polisi wakiwa namba za usajili wa gari SU 383 ambayo ilipatikana kwa njia isiyo halali.

Kwenye shtaka la saba washtakiwa hao wanadaiwa kuwa Julai Mosi, 2017 kwenye eneo hilo la Chang’ombe ‘A’ washtakiwa hao walikutwa na askari polisi wakiwa na namba za usajili wa gari SM 8573 ambayo ilipatikana kwa njia isiyohalali.

Maamuzi ya Mahakama ya Kisutu kuhusu kielelezo cha mkojo wa Wema Sepetu

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imetupilia mbali maombi ya Wema Sepetu ya kutaka kielelezo cha sampuli ya mkojo wake kisipokelewe mahakamani. 

Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba amesema anakubaliana na upande wa mashtaka kwamba kielelezo cha mkojo wa Wema kipokelewe na Mahakama kama sehemu ya ushahidi.

Pingamizi la Wema kupitia wakili wake Kibatala ni kwamba ripoti iliyowasilishwa na Mkemia kutoka Ofisi ya Mkemia Mkuu, Elias Mlima ya kwamba mkojo wa Wema una chembe chembe za dawa za kulevya aina ya Bangi haikukidhi  matakwa ya kisheria. Kutokana na hatua hiyo, Hakimu Simba ameahirisha kesi hiyo hadi Agosti 16/2017.

Wema Sepetu na wengine wawili wanakabiliwa na makosa  ya kukutwa na dawa za kulevya aina ya bangi Februari mwaka huu .

Serikali Yawasilisha Pingamizi la Awali Kupinga Dhamana ya Yusuf Manji

$
0
0
Upande wa serikali umewasilisha pingamizi la awali Mahakama Kuu ya Tanzania kupinga maombi ya dhamana ya mfanyabiashara Yusuf Manji. 

Pingamizi hilo limewasilishwa leo na wakili wa serikali, Paul Kadushi mbele ya Naibu Msajili, Sian Mustafa kutokana na Jaji Isaya Arufan anayesikiliza maombi hayo kutokuwepo.

Katika pingamizi hilo, wakili Kadushi amedai kuwa Mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza maombi ya dhamana ya Manji. 

Pia kiapo kilichowasilisha cha kuhusu dhamana kinadosari kisheria, pamoja na kuwepo kwa vifungu visivyo sahihi. 

Baada ya kuwasilisha pingamizi hilo, Msajili Mustafa ameahirisha kesi hiyo hadi August 7/2017 kwa ajili ya kusikilizwa.

==>>Huu ni Muonekano wa Manji kwa sasa 

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya August 5

Bangi Za Mponza Mbunge wa jimbo la Tarime vijijini John Heche

$
0
0
Mbunge wa jimbo la Tarime vijijini, kwa tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) John Heche jana alikamatwa na polisi  alipokwenda kituo cha polisi cha Tarime  kufuatilia kukamatwa kwa Katibu wake.

Mbunge wa Jimbo la Serengeti Marwa Ryoba amesema kuwa polisi walimkamata Heche kutokana na kauli zake ikiwepo kauli ya kutaka kilimo cha bangi kihalalishwe pamoja na kauli yake ya kuzuia shughuli za ACACIA.

"Mhe. Heche alifika Polisi Tarime kwa ajili ya kufuatilia kukamatwa kwa Katibu wake, katika hali ya kushangaza naye akawekwa chini ya ulinzi na RCO na baadae kuelezwa kuwa alikuwa akitafutwa kwa makosa mawili 

"Kosa la kwanza ni  Kauli aliyoitoa mapema mwaka huu katika mkutano wa hadhara Sirari ya kwamba atapeleka hoja bungeni aiombe serikali ihalalishe kilimo cha bangi na pili kauli yake ya hivi karibuni kuhusu kuzuia shughuli za ACACIA Nyamongo kufuatia Kauli ya Rais kwamba mgodi huo haupo kihalali nchini." alisema Marwa Ryoba

Aidha Mbunge Marwa anasema kuwa Heche alikataa kutoa maelezo yoyote polisi na jeshi la polisi limechukua simu zake zote

"Walimwachia Heche ila wakachukua simu zake zote na kumtaka afike polisi Jumatatu kwa mahojiano. Alikataa kuchukuliwa maelezo yoyote kwa kuwa hakuwa amekwenda Polisi kwa mambo hayo bali kushughulikia kukamatwa kwa Katibu wake, hivyo amejidhamini na kuondoka ila simu zimebaki Polisi" alisema Marwa Ryoba

Rais Paul Kagame ashinda uchaguzi kwa asilimia 98

$
0
0
Tume ya Uchaguzi nchini Rwanda inasema kuwa Paul Kagame ameshinda uchaguzi wa uraisi uliyofanyika jana nchini humo.

Tume hiyo imesema matokeo ya awali yameonyesha kuwa Rais Kagame alishinda kwa asilimia 98 ya kura zilizohesabiwa. Rais Kagame ambaye amekuwa madarakani kwa miaka kumi na saba sasa atahudumu muhula wa tatu wa miaka saba.

Wafuasi wake wanamsifu Kagame kwa kuleta utulivu na maendeleo ya kiuchumi nchini humo baada ya mauaji ya kimbari ya mwaka 1994 ambapo maelfu ya watu waliuaawa.

Wapinzani wa bwana Kagame walikuwa ni Frank Habineza na Philippe Mpayimana

Rais Kagame aliingia madarakani mwaka 1994 wakati kundi lake la waasi lilichukua udhibiti wa mji mkuu Kigali na kukomesha mauaji ya kimbari ambapo watu 800,000 watusi na wahutu wenye msimamo wa wastani waliuawa.

Katiba ya Rwanda ilifanyiwa mabadiliko mwaka 2015 na kumpa Kagame fursa ya kusalia madarakani hadi mwaka 2034.

Wapinzani wa Kagame wamelalamika kuwa wafuasi wao wanahangaishwa, wakisema kuwa ndiyo imesababisha kuwepo watu wachache katika mikutano yao ya kabla ya kura. Hata hivyo chama tawala kimekana madai hayo.

Gwajima Kununua Ndege ya Kisasa

$
0
0
Baaada ya kimya cha muda mrefu Askofu Mkuu wa kanisa la ufufuo na uzima, Mchungaji Josephat Gwajima ameibuka na kutangaza kuleta ndege aina ya 'Jet' Tanzania kwa ajili ya kutoa huduma kwa watumishi wake.

Mchungaji Gwajima ambaye hivi sasa yupo mjini Birmingham, Alabama nchini Marekani kwa shughuli zake za injili na mikutano mbalimbali ameahidi ataleta ndege aina ya 'Jet'

"Muda si mrefu nitaleta Tanzania ndege hii 'Jet' kwa lengo la kukuza falme ya Mungu" alisema Gwajima

Mbali na hilo Mchungaji Gwajima akiwa katika ziara zake hizo za kiroho alidai kuwa amepata umeme megawati 250 kutoka nchini Ujerumani ambazo anaamini zitasaidia taifa letu la Tanzania katika kukuza sekta ya viwanda.

"Nimepata Umeme Megawati 250 kutoka Ujerumani kwa ajili ya Taifa letu katika juhudi za kuunga mkono Tanzania ya Viwanda. Nilimtuma Engineer Mkuu wa Ufufuo na Uzima Duniani Eng.Yeconia Bihagaze huko Ujerumani kufanya ufuatiliaji, Umeme huu ni kwa ajili ya Watanzania wote na ujenzi wa uchumi imara wa Tanzania ya Viwanda" alisema Mchungaji Gwajima

Hata hivyo mchungaji Gwajima aliwahi kuahidi pia ataleta treni la kisasa linalotumia Umeme Tanzania.

Ulaji Nyama Isiyo Na Kiwango Ni Chanzo Cha Magonjwa.

$
0
0
Na: Agness Moshi – MAELEZO.
Ulaji wa nyama una faida lukuki kwa afya ya binadamu ikiwa ni pamoja na upatikanaji wa virutubisho vya aina ya protini ambayo ni rahisi kutumika mwilini, madini mbalimbali (Calcium, Magnesium, Phosphorus, Zinc na Chuma); vitamini aina ya folic asidi, E, B na B12 ambayo inapatikana katika nyama pekee.

Nyama pia inasaidia katika ukuaji na kuongeza afya ya mlaji kutokana na uwezo mkubwa wa kujenga mwili, kukarabati seli za mwili zilizokufa, kuzalisha chembe hai mpya, kurekebisha kinga ya mwili, kuongeza damu na kuimarisha mifupa.

Hata hivyo faida zote hizo zinapatikana tu, kwa walaji wa nyama iliyo bora na yenye kiwango. Hivyo ni vizuri wananchi wakazingatia kanuni za ulaji wa nyama yenye kiwango ili kujiepusha na athari zinazoletwa na nyama isiyo na kiwango.

Msajili wa Bodi ya Nyama Tanzania (TMB) Bi.Suzana Kiango amesema kuwa nyama yenye kiwango na bora huanzia kwenye utunzwaji wa mifugo wenye kuzingatia kanuni za uzalishaji bora, unenepeshaji wa mifugo yenye umri mdogo kwa kuwalisha chakula mchanganyiko kwa muda usiopungua siku 90 kabla ya kuchinja.

Bi.Kiango amesema kuwa hatua nyingine ni katika uchinjaji ambapo inashauriwa ufanyike kwenye machinjio bora ambayo yanakidhi viwango vya usafi. Hii ni pamoja na kuwa na sakafu na kuta zinazosafishika, maji ya kutosha na sehemu za kuning’iniza wakati wa kuchuna na kupasua.

“Kanuni za uchinjaji ni pamoja na kupumzisha mifugo ili kuipoteza fahamu na kumfanya mnyama asiogope na kuzalisha asidi nyingi inayosababisha nyama kuwa ngumu, pia iwe rahisi kutoa damu yote katika misuli. Uning’inizwaji wa chune mara baada ya kuchinjwa unasaidia kuondoa damu iliyo mwilini. Endapo damu haitatoka yote kwenye chune itasababisha nyama kuwa na rangi nyeusi na kuharibika mapema”, alisema Bi.Kiango.

Madhara ya ulaji wa nyama isiyo na viwango na bora ni pamoja na kupata magonjwa ya tumbo, kuharisha na kutapika endapo nyama itapata vimelea vya magonjwa hayo, kuugua magonjwa ya kuvimba miguu, kifua kikuu, shinikizo la damu, kisukari na kansa.

Hata hivyo, Bi. Kiango amesisitiza kuwa magonjwa haya yanaweza kuwatokea pia watu ambao hawatumii kabisa nyama kwa hivyo si nyama pekee ndio chanzo cha magonjwa haya japo inaweza kuwa sababu ya mtu kuugua.

“Bodi imeendelea kutoa elimu kwa watumiaji na wachinjaji wa nyama kupitia vyombo mbalimbali vya habari kama vile, redio, televisheni na magazeti. Pia katika maonesho mbalimbali kama Saba saba na Nane nane ambapo wataalamu wa bodi hutoa elimu kwa wananchi wanaotembelea mabanda ikiwa ni pamoja na kusambaza vipeperushi” amesema Bi.Kiango.

Namna nyingine ya kutoa elimu ni pamoja na kutumia matamasha ya nyama choma, wiki ya mayai na maonesho ya kuku, wiki ya chakula salama na siku ya chakula duniani. Wakati wa shughuli hizi wanashiriki hupatiwa elimu kuhusu faida na athari za kula nyama isiyo na viwango ili kunusuru afya zao.

Aidha walaji huelekezwa maeneo mbalimbali wanayoweza kupata nyama hiyo, na kwa upande wa wafanyabiashara wa nyama hupewa maelekezo ya kuboresha miundombinu ya kuzalisha, kuchinja na kuuza kwa kuzingatia viwango vya ubora na usalama.

Kutokana na baadhi ya wafanyabiashara ya nyama kuendelea kuwauzia walaji nyama isiyo na viwango kwa kujua au kutojua madhara ya nyama hizo, Bi.Kiango alisema kuwa Bodi inachukua hatua za kuhakikisha wafanyabiashara hao wanapata uelewa wa kutosha.

“Bodi imeanza kutoa mafunzo kwa watumishi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa ambao watashiriki katika kutekeleza majukumu ya Bodi ikiwa ni pamoja na kusimamia uzalishaji wa nyama na kuelimisha wachinjaji ,walaji na wadau wengine wanaojishughulisha na uzalishaji wa nyama”alifafanua Bi.Kiango.

Aliendelea kusema mafunzo hayo yameshatolewa kwa vitendo kwa watumishi wanne kutoka katika kila Mamlaka za Serikali za Mitaa za mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Morogoro na Dodoma ambapo hadi sasa jumla ya wadau 490 katika maeneo tajwa wamekwisha patiwa elimu hiyo. Pia mafunzo yanatolewa na wadau wengine ambao ni Chuo cha nyama cha VETA, Dodoma na Kampuni ya nyama ya jijini Arusha.

Taarifa ya Polisi kuhusu watu wanaojifanya kuwa maafisa wa Polisi

$
0
0
Katika siku za hivi karibuni kumejitokeza kikundi cha watu wanaotumia vibaya jina la Jeshi la Polisi kwa kujifanya ni Maafisa wa Jeshi la Polisi na kuwatapeli watu kwa kigezo cha kuwapatia ajira.

Watu hao wamesambaza taarifa kupitia mitandao ya kijamii inayosomeka ‘Vigezo sifa za kujiunga na Jeshi la Polisi’, huku ndani yake ikitaja sifa ambazo kwa mujibu wa kikundi hicho ndizo anazopaswa kuwa nazo mtu anayeomba nafasi ya kujiunga na Jeshi la Polisi.

Jeshi la polisi linapenda kuwafahamisha wananchi kuwa taarifa hizo ni za uongo na zenye lengo la kupotosha Umma kwa madhumuni wanayoyajua wao wenyewe. Pia zipo taarifa ambazo hazijathibitishwa kuwa wapo watu wanaoombwa kutoa fedha na matapeli hao ili waweze kuwapatia nafasi ya ajira hizo.

Wananchi watambue kuwa Jeshi la Polisi lina utaratibu wake mzuri na wa wazi wa kuajiri. Pale Serikali itakapotoa idhini ya kuajiri watumishi wapya  utaratibu huo utatangazwa kwa  wananchi ili waweze kuufuata kuomba nafasi hizo.

Jeshi la Polisi linawataka wananchi kutoa taarifa juu ya kikundi hicho kupitia kituo chochote cha Polisi kilicho karibu nawe au ofisi za Serikali ili watu hao waweze kukamatwa na hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao.

Wananchi mnashauriwa kupata taarifa sahihi za Jeshi la Polisi kupitia website yake ambayo ni www.policeforce.go.tz au akaunti ya twitter www.twitter.com/tanpol pamoja na Facebook www.facebook.com/tanpol

Imetolewa na:

Barnabas David Mwakalukwa - ACP
Msemaji wa Jeshi la Polisi,
Makao Makuu ya Polisi,
S.L.P. 9141,
Dar es Salaam

Pata Tiba ya Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FUUl POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM .HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Lowassa Atua Kenya Kumnadi Uhuru Kenyatta

$
0
0
Zikiwa zimebaki siku mbili nchi ya Kenya kufanya Uchaguzi Mkuu, Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Edward Lowassa amefunguka sababu kuu zinazofanya amtetee na kumnadi mgombea Urais kupitia chama cha Jubilee Uhuru Kenyatta kuwa ni kiongozi shupavu.

Lowassa ambaye jana alishiriki katika mkutano wa chama cha Jubilee alisema kuwa kuna watu wanauliza kwanini yeye pamoja na CHADEMA wanamnadi kwa kuwa kiongozi huyo ni shupavu na mpenda watu.

"Kuna watu wananiuliza kwanini mnamnadi Uhuru Kenyatta, nasema tena hadharani bila aibu yoyote huyu ni kiongozi shupavu anayependa watu, anaweza kuongoza watu wetu, lakini cha pili Uhuru Kenyatta anapenda Afrika Mashariki akiingia madarakani ataturuhusu tuendelee kuzunguka zunguka kwenye mipaka hii kama Namanga pale bila hata shida, la tatu ni kwamba aliingia madarakani nchi ikiwa kwenye vita lakini amewapa suluhu ameingoza nchi imekwenda taratibu na akafanikiwa" alisema Lowassa

Mbali na hilo Lowassa alisema kuwa licha ya mambo yote hayo lakini bado ukweli utabaki palepale kuwa Uhuru Kenyatta anapenda Demokrasia

"Tangu Demokrasia ya vyama vingi Uhuru Kenyatta hajaleta shida ya aina yoyote, siku moja nimeona kwenye TV yenu mama mmoja amemtukana mpaka matusi ya nguoni lakini asubuhi Rais anasema nimemsamehe bure, nawaambia huyu ndiye anawafaa, naondoka nikiwa na matumaini" alisema Lowassa

Siku ya Jumapili tarehe 8/8/2017 Wananchi wa Kenya watakuwa wakifanya uchaguzi kuchagua viongozi wao mbalimbali 

Sherehe Za Uwekaji Wa Jiwe La Msingi Bomba La Mafuta Ghafi Kutoka Hoima Mpaka Chongoleani, Tanga

$
0
0
 Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Rais wa Uganda, Yoweri  Kaguta Museveni  wakiwasili katika viwanja vya Chongoleani, Mkoani Tanga tayari kwa sherehe za uwekaji wa jiwe la Msingi la ujenzi wa  mradi mkubwa wa usafirishaji wa Mafuta ghafi kutoka Hoima nchini Uganda mpaka katika bandari ya Tanga.
Rais Dkt. John Pombe Magufuli na mgeni wake Rais wa Uganda, Yoweri  Kaguta Museveni  wakifurahi jambo na Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan wakiwa katika viwanja vya Chongoleani, Mkoani Tanga tayari kwa sherehe za uwekaji wa jiwe la Msingi la ujenzi wa  mradi mkubwa wa usafirishaji wa Mafuta ghafi kutoka Hoima nchini Uganda mpaka katika bandari ya Tanga.

==>Tazama hapo chini

Huduma ya fomu ya maombi ya pasipoti mtandaoni kuanzia Agosti 7, 2017

$
0
0
Idara ya Uhamiaji inapenda kuutangazia umma kuwa imezindua rasmi huduma ya fomu ya maombi ya pasipoti mtandaoni (Online Passport Application Form). Huduma hii inapatikana katika tovuti ya Idara kupitia link ifuatayo: https://www.immigration.go.tz/ppt_application/ na itaanza kutumika rasmi kuanzia siku ya Jumatatu tarehe 07 Agosti, 2017.

Kufuatia kuzinduliwa kwa huduma hii, waombaji wote wa pasipoti wanashauriwa kuzijaza fomu hizo mtandaoni, Kisha kuzichapisha (Printing) na kuziwasilisha katika Ofisi za Uhamiaji.

Hata hivyo, matumizi ya huduma hii yataenda sambamba na huduma inayotumiwa sasa ya fomu za maombi ya pasipoti mpaka pale itakapotangazwa vinginevyo.

Utaratibu wa namna ya kujaza fomu hizo umeelekezwa katika fomu husika mtandaoni, na pia wateja wanaweza kupata ufafanuzi au maelezo zaidi kuhusu huduma hiyo kupitia anuani ya Idara ambayo ni  info@immigration.go.tz au katika Ofisi yoyote ya Uhamiaji iliyo karibu nao.

Taarifa zaidi kuhusu huduma hii zitaendelea kutolewa kupitia vyombo mbalimbali vya habari.

Imetolewa na:
KITENGO CHA UHUSIANO,
MAKAO MAKUU, IDARA YA UHAMIAJI,
04 AGOSTI, 2017.

Idara yake ya Uhamiaji yawahakikishia Watanzania kuwachukulia hatua raia wote wa kigeni wanaoingia nchini kinyume cha Sheria

$
0
0
Zimekuwepo taarifa za kuingia nchini kwa wahamiaji haramu kupitia mpaka wetu na Nchi ya Kenya. Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi  kupitia Idara yake ya Uhamiaji inawahakikishia Watanzania kwamba  hatua  kali za kisheria  zinachukuliwa  dhidi  ya raia wote wa kigeni  wanaoingia  nchini kinyume cha  Sheria  za Uhamiaji  na nchi yetu.

Kimsingi hakuna raia  yeyote wa kigeni anayeruhusiwa kuingia nchini kwa kisingizio cha  kuja kufanya kazi, biashara au Uwekezaji bila kufuata Sheria  na taratibu za Uhamiaji, na kwamba  wote wanaokiuka  Sheria hizo watarudishwa makwao mara moja.

Ni jambo lisilokubalika mtu atoke nchini kwake bila kibali cha kufanya kazi Tanzania kwa madai kwamba alishatuma maombi ya kibali husika na amekuja kusubiri majibu ya kibali hicho akiwa Tanzania. Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi haitavumilia ukiukwaji huu wa sheria za nchi na kwamba kila raia wa kigeni  anayekusudia kuingia nchini ahakikishe ana kibali cha kuingia nchini na anafanya kazi ambayo ndiyo aliyoiombea kwenye kibali chake.

Yapo matukio ya raia wa nchi jirani, hususan katika mipaka ya Kenya na Uganda ambapo kutokana na hali  ya muingiliano  wa kiuchumi na kijamii, raia  wa nchi zetu, wamekuwa  wakivuka mipaka  pande zote  kufuata huduma mbalimbali, Hii pia inachangiwa na mapungufu katika  usimamizi wa alama na maeneo ya wazi ya mipaka yetu. Hali hii inapelekea baadhi ya wananchi wetu kutumia mwanya huo kuwatengenezea  raia  wa kigeni mazingira ya kuingia nchini bila  kufuata taratibu au hata kutumiwa katika biashara haramu ya kusafirisha  binadamu.

Tahadhari inatolewa kwa Watanzania wote ambao wamekuwa wakiwapokea raia hao  wa kigeni na kuwahifadhi, kwani kufanya hivyo  ni kuvunja  sheria za nchi ikiwemo ile Sheria  ya usafirishaji  haramu wa binadamu.

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kupitia Idara yake ya Uhamiaji imeanza kuchukua hatua ili kuweza kushughulikia suala hili. Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dk. Anna Makakala, tayari ametembelea baadhi ya maeneo ya mipaka yetu hususani kijiji cha Jasini wilayani Mkinga mkoani Tanga ili kujionea hali halisi na kutoa Maelekezo ya hatua  za kuchukua  kudhibiti hali hiyo kwa mujibu wa Sheria, kwa kuwa eneo hilo linaonyesha kuwa na muingilino baina ya nchi ya Kenya na Tanzania kwa muda mrefu.

Wizara itaendelea na Mashauriano na Mamlaka nyingine zenye dhamana ya Kusimamia alama za mipaka ya nchi yetu kwa kuwa tatizo hili la muingiliano wa wananchi wa pande zote lipo kwenye mipaka mingi ya nchi.

Imetolewa na
Christina R. Mwangosi
Kaimu Msemaji
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
4 Agosti 2017

Kinana Ammwagia Sifa Rais Museven

$
0
0
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)  Ndugu Abdulrahman Kinana amefunguka na kusema kuwa hakuna Rais duniani kote ambaye awewahi kuja Tanzania mara nyingi na mkoa wa Tanga kama Rais Museveni.

Kinana amesema hayo leo katika sherehe za Uwekaji wa Jiwe la Msingi wa Ujenzi wa Bomba la Mafuta katika eneo la Chongoleani Tanga na kusema kuwa Museveni ni ndugu yetu na si rafiki wa Tanzania.

“Hakuna Rais aliyewahi kutembelea Tanzania mara nyingi kama Museveni, hakuna Rais aliyewahi kutembelea Tanga mara nyingi kama Museveni, alikuwa akitusihi sana kujenga reli hapa Tanga  ila leo naona anafuraha kwamba reli haikuwezekana lakini bomba la mafuta limeonekana, lakini nampongeza  sana Rais Magufuli kwa sera zao nzuri na vyama vyao kuwezesha bomba la mafuta” alisema Kinana  na kuongeza;

“Nimemsikia Museveni akisema Tanzania na Uganda ni nchi ndugu na si marafiki, naona Rais Magufuli na Museveni wote wanasema siasa ni uchumi na uchumi ni siasa” alisema Kinana

Aidha Rais wa Uganda  Museven amesema kuwa Watanzania ni ndugu zake kabisa ila wazungu wote kwake ndiyo marafiki

“Mimi siwezi kusema Watanzania rafiki hapana ni ndugu zangu, mkinikubali nafurahi hata msiponikubali mimi nitabaki kuwa ndugu yenu, hao watu weupe (Wazungu)  ndiyo wabaki kuwa marafiki” alisisitiza Museveni

Unasumbuliwa na Kiharusi,Ngiri au Kifafa?......Unatatizo la Nguvu za Kiume, Kuachika au Tatizo la Uzazi? . Kutana na Mtalaamu Huyu Akusaidie

$
0
0
SASA YUPO DAR; Anauwezo wa kutabiri nyota yako na kukuletea mafanikio makubwa katia biashara yako, kazini na malengo yako ya maisha.Pia anatoa pete ya bahati yenye uwezo wa kukuletea mafanikio makubwa na kutimiza ndoto zako.

Je, Umedhurumiwa? unamdai na hakulipi?...Njoo upatiwe dawa ulipwe haraka. Anadawa ya kumvuta mpenzi wako popote alipo kwa masaa 6 tu na kumtuliza asitoke kwako

Je, unaugomvi usioisha na mpenzi wako na unaachwa mara kwa mara? Njoo upate dawa ufurahie penzi tulivu la umpendae.

Anadawa za nguvu za kiume, kuimarisha mishipa iliyolegea, kuongeza homoni na kukufanya udumu katika tendo hadi dakika 45 na unaweza kurudia tendo hata mara 4 bila kuchoka.

Anatibu Busha bila kupasua,uzazi, mshipa wa ngiri,kiharusi,kifafa,kuondoa majini machafu nakadhalika.

Mpigie kwa simu: 0755505099

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Rais Magufuli awapatanisha Ruge na Makonda

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli amewaunganisha marafiki waliogeuka kuwa mahasimu wakubwa, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda na Mkurugenzi wa vipindi wa Clouds Fm, Ruge Mutahaba.

Rais Magufuli amewaunganisha wawili hao leo kabla ya kuhitimisha hotuba yake jijini Tanga kuhusu uzinduzi wa mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta ghafi kutoka Hoima nchini Uganda hadi jijini humo.

Baada ya kumuomba muda mgeni wake Rais wa Uganda, Yoweri Museveni ili afanye kitu tofauti, Rais Magufuli aliwaita jukwaani Makonda na Ruge na kuwataka wamalize tofauti zao.

“Nimewaleta vijana wote ninawapenda na wao nataka wapendane,” alisema Rais Magufuli.

“Haya shikaneni mikono hapa. Nataka mambo yenu ninyi wawili yaishe. Nataka mfanye kazi kwa ajili ya Tanzania. Nakupongeza Ruge kwa nyimbo nzuri na Mungu awabariki sana,” aliwaeleza. kauli hiyo ikisababisha wananchi kulipuka kwa shangwe.

Makonda na Ruge waliingia katika mtafaruku baada ya Clouds Media Group kudai kuwa mkuu huyo wa mkoa alivamia katika studio zake usiku akiwa na askari wenye silaha na kulazimisha kipindi kisichokidhi sifa za kitaaluma za uandishi wa habari kurushwa kupitia kipindi cha Shilawadu kwa maslahi binafsi.

Kutokana na kitendo hicho, Kamati Maalum iliyoundwa na aliyekuwa waziri wa Habari, Michezo na Utamaduni, Nape Nnauye kiliwasilisha ripoti yake na kudai kuwa ni kweli tukio hilo lilitokea.

Kufuatia ripoti hiyo, Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) lilitangaza kumfungia Makonda kutangazwa au kuchapishwa na chombo chochote cha habari ambacho ni mwanachama wa Jukwaa hilo.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images