Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Rais Magufuli Amvaa Mbunge wa CCM Morogogoro.........Amtaka Arudishe Viwanda. Pia Kasema Machinga Stendi ya Msamvu Wasisumbuliwe

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amebadilikia Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini Mh Aziz Abood na kumtaka arudishe viwanda mbalimbali ambavyo alibinafsishiwa na serikali kama ameshindwa kuviendesha.

Rais Magufuli amesema hayo leo alipokuwa Morogoro mjini na kuwataka watu waliobinafsishiwa viwanda na serikali mkoani humo na wameshindwa kuviendesha wavirudishe kwa serikali ili serikali iweze kuwapa watu wengine ambao wataweza kuviendesha.

“Ninarudia wito wangu niliokwisha kuutoa huko nyuma, kwamba wenye viwanda hapa Morogoro ambao wameshindwa kuviendesha, na leo nataja akiwemo Mbunge wa hapa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), narudia akiwemo Mbunge wa hapa wa CCM ambaye alibinafsishiwa viwanda vingi, kama ameshindwa kuviendesha avirudishe ili tuwape watu wengine kwa sababu vijana hawa wanakosa ajira, nazungumza kwa uwazi kwa sababu msema kweli ni mpenzi wa Mungu” amesisitiza Mhe. Rais Magufuli.

Mbali na hilo Rais Magufuli amemuagiza Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Morogoro SACP - Ulrich Onesphory Matei kuhakikisha askari Mgambo hawawasumbuli wafanyabiashara wadogo wadogo na amewataka wafanyabiashara hao kutofanya vurugu wakati utaratibu mzuri unaandaliwa kwa ajili yao.

Rais Magufuli wakati akiwa katika ziara mkoani Singida aliweka wazi kuwa yeye anauchukua sana ubinafsishaji na kusema ndiyo umeturudisha nyuma na kuharibu mipango mizuri ambayo alikuwa nayo Mwalimu Nyerere, huku akitolea mfano viwanda kadhaa ambavyo vipo Morogoro na vimeshindwa kuendelezwa na majengo yake kugeuka magodauni ya watu.

==>>Hii ni taarifa ya Ikulu

Makontena 10 Ya Kemikali Bashirifu ( Ethanol )Yakamatwa Bandarini

$
0
0
Mamlaka ya kudhibiti na kupambana na dawa za kulevya nchini imekamata makontena 10 yaliyokuwa na kemikali aina ya ethanol yenye ujazo wa lita 200000 (Laki mbili) kupitia bandari ya Dar es salaam kutokea nchini Swaziland.

Taarifa iliyotolewa na Kamishna Mkuu wa kupambana na dawa za kulevya nchini Rogers Sianga inasema kuwa kemikali ziliingizwa nchini na kampuni ya 'Hamid Ibrahim Saambaya' na kusema kwamba makontena hayo yamekamatwa kutokana na kampuni hiyo kutofuata miongozo na ya sheria zilizopo kutoka katika mamlaka husika za kujihusisha na kemikali bashirifu.

Taarifa ya Sianga imedai kuwa kampuni hiyo imekuwa ikiingiza kemikali hizo nchini tangu mwaka 2016 na kufikia jumla ya ujazo wa lita milioni moja na nusu na kwamba kampuni hiyo haijawahi kusajiliwa wala kuweka kumbukumbu wapi kemikali hizo zinakopelekwa.

"Pamoja na kwamba kemikali hizo zinatumika kwa matumizi mengine viwandani kama kutengeneza pombe na vinginevyo pia kwa kutumia kemikali hizi zikichepushwa zinaweza kutengeneza dawa za kulevya" Taarifa iliyotolewa na Kamishna Sianga ilieleza.

Hata hivyo mamlaka kwa kushirikiana na mamlaka nyingine zinaendelea na uchunguzi juu ya uhalali wa biashara za kampuni hiyo na kufahamu mahali sahihi kemikali hizo zinapopelekwa na baada ya hapo hatua za kisheria zitachukuliwa.

Nzega: Wanawake watano wachomwa moto hadi kufa kwa Imani za Kishirikina

$
0
0
Watu watano wameuwawa kwa kuchomwa moto katika kata ya Uchama Wilayani Nzega Mkoani Tabora na watu wanaosaidikiwa kuwa ni Sungusungu huku wakidaiwa wameuliwa kutokana na imani za kishirikina.

Kufuatia Mauaji hayo Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Agreya Mwanri, amezitaka Kamati za Ulinzi na usalama ngazi ya Mkoa na ile ya Wilaya ya Nzega kusitisha shughuli zote zilizokuwa zikifanywa na sungusungu katika kijiji hicho.

Mwanri amesema kuwa amechukua hatua hiyo baada ya sungusungu hao kutekeleza mauaji hayo ya watu watano ambao wote ni wanawake wakituhumiwa kuwa ni washirikina.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora Wilbroad Mutafungwa amesema kuwa katika kuendelea kuchunguza tukio hilo jeshi hilo linawashikilia baadhi ya viongozi wa kijiji hicho ili kuweza kubaini waliotekeleza tukio hilo.

Maalim Seif Amvaa Spika wa Bunge Job Ndugai

$
0
0
Katibu Mkuu wa Chama cha CUF, Maalim Seif Sharif Hamad amesema kwamba hatua ya Spika kuwavua ubunge , udiwani na kuteua wengine wapya  inalenga kudhoofisha kambi ya wabunge wa  CUF na Ukawa.

Amesema Watanzania wanapaswa wajikumbushe kwamba hata kama hicho kinachoitwa ‘kuwafukuza uanachama’ wabunge halali wa CUF kingekuwa kiko sawa, hatua kama hiyo hufuata taratibu zote za kisheria na kikanuni za Bunge kujiridhisha kwanza.

Spika Job Ndugai anadhani Watanzania ni vichaa wamuamini kuwa alishachukua hatua ya kujiridhisha kuwa wabunge wanane wa Chama cha Wananchi (CUF) wamefukuzwa uanachama kulingana na taratibu za chama hicho na hivyo wamekosa sifa za kuendelea na Ubunge. Ndani ya siku moja?” amehoji Maalim.

Amesema Spika amejiridhisha vipi ikiwa hata hakuwasiliana na Katibu Mkuu wa Chama ambaye kwa mujibu wa Katiba ya CUF ndiye Mtendaji Mkuu wa shughuli za chama na pia kwa nafasi hiyo ndiye katibu wa vikao vya Mkutano Mkuu wa Taifa na Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la Chama?

Amesema yeye kama katibu, alimuandikia Spika Ndugai barua, Jumanne, Julai 25  akimueleza kwamba hilo lililoitwa Baraza Kuu la Uongozi la CUF halikuundwa na wajumbe halali wa Baraza Kuu.

“Angekuwa na nia ya kweli ya kutaka kujiridhisha si hapo ndipo pangekuwa pa kuanzia kwa kuwepo kile wanasheria wanachokiita shaka inayoweza kuingia akilini yaani ‘reasonable doubt’?’’ amehoji.

Amesema  Spika Ndugai aliyapuuza yote hayo kwa sababu ni kinyume na mkakati wa Dola wa kuihujumu CUF na kuua demokrasia Tanzania. Hapo ndipo Spika Job Ndugai alipolifikisha Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota........Anatoa Mvuto wa Biashara, Kupandishwa Cheo, Kurudishiwa Mali Uliyoibiwa na Mengne

$
0
0
Kutana Maajabu ya Mtabibu CHIEF SULTAN(MAKATA WA MAKATANI) Mganga wa Waganga Sasa Yupo Mikoa Yote Tanzania

Pia anatoa Tiba kwa Njia ya Simu ukiwa popote Pale Tanzania au Nje ya Tanzania..

CHIEF SULTAN ni Mtabibu na Mtafiti wa Dawa za Asili ya Africa, na Duniani Katika utoaji wa Tiba za Asili..
 
Je unasumbulia na Mapenzi..?
(Umeachwa na Umpendae awe Mume/ Mke au mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine na Bado Unampenda?) Umejaribu sehemu Nyingi bila Mafanikio?Wasiliana na CHIEF SULTAN Akusaidie Kumshika Umpendae Asikusaliti(LIMBWATA) Kumtawala Mpenzi wako kwa sababu Maalum..Anauwezo wa Kusambalatisha Mahusiano yao ndani ya siku Moja tu.
Je Unasumbuliwa na Madeni?
Biashara yako Haina wateja?
Unatatizo la kutokushika Mimba na umehangaika sehemu nyingi bila mafanikio?
 
Wasiliana na CHIEF SULTAN Kwa Majibu ya Maswali yako..
Anasafisha NYOTA na Kutoa PETE za BAHATI kuendana na NYOTA yako. UTAJIRI USIO NA MASHARTI.(Magic Wallet_Pochi ya Maajabu Isio Isha Hela)
KUWA MAARUFU na KUJULIKANA
Kupandishwa CHEO na HESHIMA Mahala pa KAZI.
Utapewa Nguvu ya Kujilinda na MALI ZAKO zako na Mwili wako.. Huzuia Chuma Ulete katika Biashara.. Hurudisha MALI zilizo Potea au KUDHULUMIWA..
Mvuto wa Biashara na Mwili wako.
Hutibu kabisa Nguvu za Kiume na Kurefusha Uume kwa saizi Unayotaka.
 
Magonjwa Sugu(Miguu Kufa Ganzi, kisukari, Presha, Pumu nk.)Humaliza Kesi za Muda mrefu ndani ya siku 14 tu.
Anatoa NDAGU Zisizokuwa na Masharti.. Kwa maelezo Zaidi wasilina nae kwa

whatsapp +255 0658 316 976
Call +255 755 911 233

Sheikh Ponda Alaani Waumini 10 Kutekwa Msikitini

$
0
0
Jumuiya ya Taasisi za Kiislamu Tanzania imelaani waumini 10 wa dini hiyo kutekwa wakiwa katika msikiti wa Ali Mchumo wilayani Kilwa na sasa hawajulikani walipo.

Akizungumza leo Alhamisi Julai 27, Katibu wa jumuiya hiyo, Sheikh  Ponda Issa Ponda amesema Julai 21, mwaka huu usiku waumini hao wakiwa wanasali katika msikiti huo walivamiwa na watu waliokuwa kwenye magari matano.

Amesema wavamizi hao waliingia msikitini na kuanza kuwapiga waumini hao kisha wakaondoka nao.

Amesema kabla ya kuingia msikitini, walipiga risasi sehemu mbalimbali za msikiti huo.

Ponda amesema wakati wakitekeleza unyama huo, majirani walisikia mayowe ya waumini hao.

Amesema baada ya hapo majirani walishuhudia wavamizi hao wakiwa wamewabeba waumini hao na kuwaingiza kwenye magari na kuondoka nao.

Amesema baada ya tukio hilo majirani walishuhudia damu nyingi ndani ya msikiti huo.

"Sijui kama watu hao watakuwa wazima hadi sasa kwa kuwa waliondoka wakiwa wamebebwa" amesema.

Amesema hadi sasa Polisi bado hawajatoa taarifa zozote kuhusiana na waumini hao.

Rais Magufuli Awasili Jijini Dar......Awahutubia Wananchi Wa Tegeta Kwa Ndevu

$
0
0
Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akizungumza na wananchi wa eneo la Tegeta kwa Ndevu jijini Dar es salaam, baada ya wananchi hao kusimamisha msafara wake alipokuwa safarini akirejea jijini Dar es salaam kutokea Mkoani Dodoma, Julai 27, 2017.
Sehemu ya wananchi wa eneo la Tegeta kwa Ndevu jijini Dar es salaam, wakimsikiliza Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliposimama kuzungumza nao, alipokuwa safarini akirejea jijini Dar es salaam kutokea Mkoani Dodoma, Julai 27, 2017.
Sehemu ya wananchi wa eneo la Tegeta kwa Ndevu jijini Dar es salaam, wakimshangilia Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliposimama kuzungumza nao, alipokuwa safarini akirejea jijini Dar es salaam kutokea Mkoani Dodoma, Julai 27, 2017. PICHA NA IKULU.

Lipumba Amvaa Maalim Seif.....Kasema Yeye Ndo Aliyewaponza Wabunge Waliotimuliwa

$
0
0
Mwenyekiti wa (CUF) anayetambuliwa na ofisi ya Msajili wa Vyama vya siasa, Profesa Lipumba amefunguka na kusema kuwa Katibu Mkuu wa CUF Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad ana kesi ya kujibu na kudai yeye kawaponza wabunge nane waliovuliwa uanachama wa CUF

Profesa Lipumba amesema hayo leo alipokuwa akiongea na waandishi wa habari na kusema Katibu Mkuu wa (CUF)  Mhe. Maalim Seif na yeye anayake ya kujibu mbele za Kamati ya Maadili na Nidhamu ya CUF.

"Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu na kuna wananchama wengine wengi tu ambao pia wana makosa ya kuweza kujibu mbele ya Kamati ya Nidhamu na Maadili katika watu wote hao Katibu Mkuu yumo na yeye ndiye amewaponza hawa wabunge nane wa Viti Maalum ambao wamevuliwa uanachama na ndugu zangu wa Zanzibar na wale wabunge wengine wale msiwe mnasikiliza na kufuata kila anachosema Katibu Mkuu atakuponza kama alivyowaponza wajumbe wa baraza la wawakilishi" alisema Lipumba

Kwa upande wa Katibu Mkuu wa CUF Taifa  Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad amesema mpaka sasa wabunge wote nane ambao wanasemakama wamefukuzwa uanachama wameamua kufungua kesi Mahakama Kuu kupinga maamuzi feki ambayo yamefanywa na Baraza Kuu feki na kuitaka Mahakama itamke kuwa wao ni wanachama halali wa CUF na wabunge halali wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Lakini pia Katibu Mkuu amesema kuwa Baraza Kuu halali la CUF litakutana kwa dharura siku ya kesho Ijumaa tarehe 28/07/2017 kujadili mambo mbalimbali ambayo yanaendelea katika chama hicho na kutangaza hatua ambazo zitafuata.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

NEC imeteua Wabunge 8 kuziba nafasi ya waliotimuliwa CUF

Rais Magufuli aunga mkono uamuzi wa TCU kuvifungia vyuo 19

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amewasili Jijini Dar es Salaam leo tarehe 27 Julai, 2017 akitokea Mkoani Dodoma ambapo akiwa katika eneo la Tegeta Wilaya ya Kinondoni amezungumza na wananchi waliosimamisha msafara wake na kuwahakikishia kuwa Serikali inaendelea kuchukua hatua mbalimbali za kukabiliana na kero na kuimarisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi.

“Kwa sababu ni mara yangu ya kwanza kusimama hapa Tegeta, nianze kwa kuwashukuru sana, kwa kura nyingi mlizonipa ili niwe Rais wa Awamu ya Tano, nawashukuru CCM, nawashukuru CHADEMA, nawashukuru CUF, nawashukuru ACT na hata wale ambao hawana chama kwani wote kwa umoja wenu mlitanguliza maslahi ya Taifa na kumpa kura mtu ambaye atalisaidia Taifa, na mimi nitafanya kazi kwa nguvu zangu zote na kwa kumtanguliza Mwenyezi Mungu ili Watanzania wote hasa wanyonge ambao siku zote walikuwa wakionewa” amesema Mhe. Rais Magufuli

Baadhi ya juhudi alizozitaja kufanyika tangu aingie madarakani ni pamoja na kuondoa ada kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari, kuongeza mikopo ya wanafunzi wa vyuo vikuu kutoka Shilingi Bilioni 371 hadi kufikia Shilingi Bilioni 483, kukabiliana na vitendo vya rushwa na ufisadi na kulinda mali za umma hasa madini.

“Kwenye madini tumeibiwa sana, nchi yetu ni kati ya nchi zinazoongoza kwa kuibiwa, tumeibiwa kwa miaka 18, sasa imetosha” amesema Rais Magufuli.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli ameipongeza Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) kwa kuzuia udahili wa wanafunzi wote wa mwaka kwanza katika vyuo vikuu 19 na kuzuia udahili wa wanafunzi wa kozi 75 katika vyuo vikuu 22 kutokana na dosari zilizobainika wakati wa ukaguzi wa ubora vyuo hivyo uliofanyika Oktoba 2016.

“Ndugu zangu nchi hii ilishakuwa kila kitu hewa hewa, tumegundua wafanyakazi hewa zaidi ya 19,500, kulikuwa na mikopo hewa ya wanafunzi, na naipongeza TCU kwa kufungia baadhi ya vyuo kudahili wanafunzi, nafanya yote haya kwa ajili yenu, nataka tuwe na nchi nzuri” amebainisha Mhe. Rais Magufuli.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
27 Julai, 2017

==>Ulizisoma hizi>


Waziri Mhagama Awapa Siku 30 Waajiri Wote Nchini

$
0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu, Bunge, Kazi,Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu, ametoa siku 30 kwa waajiri wote nchini ambao hawajasajili, kujisajili katika mfuko wa fidia kwa wafanyakazi (WCF) na kutoa michango kwa wakati.

Mh. Mhagama ametoa agizo hilo leo jijini Mbeya wakati wa ukaguzi wa kushtukiza jijini humo na kuwabaini waajiri ambao bado hawajatekeleza Sheria ya fidia kwa Wafanyakazi Sura 263 Marejeo ya Mwaka 2015 kifungu cha 5, ambayo inawataka waajiri wote kutoka sekta ya Umma na binafsi Tanzania Bara kujisajili kwenye mfuko huo.

Mhagama amefafanua kwamba, mwajiri ambaye hajajisajili kwenye mfuko, anaweza kufikishwa mahakamani na adhabu ni pamoja na kutozwa faini ya kiasi cha fedha kisichozidi shilingi milioni 50 au kifungo kisichozidi miaka 5 jela au vyote kwa pamoja,

Katika ziara hiyo ya ukaguzi wa kushtukiza Mh. Mhagama alifuatana na Mkurugenzi wa Huduma za Tiba na Tathmini wa Mfuko wa fidia kwa wafanyakazi, Dk. Abdulsalaam Omar, na aliikagua hospitali ya K’s iliyoko eneo la Mafyati na Shule ya Sekondari ya Saint Aggrey iliyoko Uyole na kubaini kuwa taasisi hizo hazijajisajili katika mfuko.

Mwanzilishi wa Amazon Jeff Bezos atangazwa tajiri namba 1 duniani baada ya kumpita Bill Gates leo

$
0
0
Mwanzilishi wa Kampuni ya Amazon, Jeff Bezos amempita Bill Gates na kuwa tajiri namba moja duniani akimiliki utaji wa dola za kimarekani 90.6 bilioni (Tsh 203 trilioni).

Kupanda wa hisa za Amazon kwa asilimia 1.5 leo Alhamisi Julai 27 kulimaanisha kuwa tajiri huyo amempita mwanzilishi mwenza wa Microsoft, kwa mujibu wa taarifa za jarida la Forbes la nchini Marekani.

Forbes wameeleza kuwa Bezos ana utajiri wa $90.6 bilioni akimzidi Bill Gates aliyekuwa anashikilia nafasi hiyo akiwa na utajiri wa $90 billioni sawa na Tsh 201.5 trilioni.

Bezos ananakadiriwa kumilikia hisa milioni 80 za Amazon akiwa ni mwenye hisa nyingi zaidi ya mwingine yeyote.

Kwa miaka ya hivi karibuni amekuwa akijikita zaidi katika mradi wake wa Blue Origin unaohusika na urushaji wa rocket kwenda angani pamoja na Washington Post ambazo zote anazimiliki.

Bezos ambaye ni Mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji Mkuu (CEO) wa Amazon alizaliwa mwaka 1964 Albuquerque Jimbo laNew Mexico na alisoma Sayansi ya Kompyuta na Uhandisi wa Umeme katika Chuo Kikuu cha Princeton.

Alipohitimu alikwenda kufanya kazi na Wall Street lakini mwaka 1994 aliacha kazi na kwenda kuanzisha Amazon ambapo kwa mara ya kwanza Amazon ilianzishiwa katika karakana ya kutengenezea magari. Baada ya kampuni hiyo kuanza kufanikiwa na kujipanua katika nchi mbalimbali, mwaka 2000 alianzisha kampuni ya Blue Origin inayojishughulisha na masuala ya anga.

Mwaka 2013 akiendelea kujipanua, aliinunua Kampuni ya Washington Post kwa $250 milioni na ilipofika Mei 2017 alitajwa kuwa na utajiri wa $ 84.8 bilioni, lakini leo Julai 27, 2017 amefikisha utajiri wa $90.6 bilioni na kushikilia usukani wa mtu tajiri zaidi duniani.

Kwa mujibu wa Forbes, hawa ndio matajiri 10 wanaoongoza duniani;
  1.    Jeff Bezos (53)- Amazon.com
  2.     Bill Gates (61)- Microsoft
  3.     Amancio Ortega (81)- Zara
  4.     Warren Buffett (86)- Berkshire Hathaway
  5.     Mack Zuckerberg (33)- Facebook
  6.     Carlos Helu (77)- telecom
  7.     Larry Ellison (72)- software
  8.     Michael Bloomberg (75)- Bloomberg LP
  9.     Bernard Arnault (68)- LVMH
  10.     Charles Koch (81)- diversified

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya July 28

Serikali Kuunda Kamati ya Kukagua Viwanda Vyote Nchini

$
0
0
Serikali  imeteua kamati maalumu yenye kushirikisha wataalamu pamoja na wakuu wa mikoa wa kila mkoa, itakayozunguka kukagua utendaji wa viwanda vilivyobinafsishwa, na kisha ndani ya siku 15 itatoa maamuzi.

Imesema viwanda watakavyoshughulika navyo ni vile vilivyobinafsishwa na ambavyo havifanyi kazi, lakini pia kuhakikisha uzalishaji wa kiwanda husika kama ndio ulioruhusiwa. 

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage alisema hayo jijini Dar es Salaam jana na kuongeza kuwa wapo waliopewa viwanda kwa shilingi moja na wengine kwa Sh milioni 10, vingine vikifanya kazi, vingine vikiwa havifanyi kazi iliyokusudiwa na vingine kutokufanya kazi kabisa.

Alisema Kamati hiyo itafuatilia na tayari ameandika barua kwa wakuu wote wa mikoa nchini, na kupewa hadidu za rejea ili waweze kupitia kiwanda kimojakimoja kuhakikisha utendaji kazi wake. 

“Wakati Kamati hiyo ikikagua, wakikiona kiwanda wanapiga simu kwake na kwa msajili wa hazina ili kwenda kuhakikisha kiwanda hicho kinafanya kazi na baada ya hapo Augusti 15 watafanya maamuzi,” alisema.

Alisema yeyote aliyepewa kiwanda ni lazima kifanye kazi na kwamba kama anayehusika ameshindwa, atafute mtu mwingine ili kifanye kazi, la hasha ameagizwa akakichukue, kwani wapo watanzania ambao ni vijana wanatafuta kazi wakihitaji kutolewa vijiweni na kupewa viwanda waviendeshe na taasisi za kuwaelekeza zipo.

Alisema lengo la kubinafsisha viwanda ni ili vizalishe bidhaa ambazo zitatumika nchini na nyingine ziweze kuuzwa nje ya nchi na kuleta fedha za kigeni, vifanye kazi viweze kutoa ajira kwani asilimia 65 ya idadi ya watu nchini n I vijana na wengi wao hawana ajira.

“Kuna viwanda vilivyobinafsishwa na vinafanya kazi, hivyo hatuna shida navyo bali vile ambavyo havifanyi kazi, kwani malengo yetu ni wote wenye viwanda vifaye kazi hata vile vilivyosimama ili vikidhi malengo yaliyotakiwa,” alisema Mwijage na kuongeza kuwa viwanda vingi vilitolewa kwa Shilingi moja na vingine hadi Shilingi milioni 10.

Alitoa wito kwa wakuu wa mikoa, kukagua kiwanda kimoja baada ya kingine na hata kuhoji umiliki, hivyo mhusika anatakiwa kuwa na nyaraka stahiki, kwani ubinafsishaji dhamira yake kubwa ilikuwa ni kuwepo kwa ajira.

Mawaziri 5 watembelea mpaka wa Tanzania na Uganda

$
0
0
Mawaziri watano wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wametembelea mpaka wa Tanzania na Uganda ili kutatua changamoto zinazoukabili mpaka huo na kuuboresha.

Mawaziri hao ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni, Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Suleman Jaffo.

Pia alikuwapo, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Suzan Kolimba na Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Isack Kamwelwe.

Miongoni mwa maeneo yaliyotembelewa na mawaziri hao jana Alhamisi, Julai 27 ni eneo la mpaka ya Tanzania na Uganda kwa upande unapopita Mto Kagera na eneo la kivuko cha mpaka wa Tanzania na Uganda kilichopo Mtukula mkoani Kagera.

Katika ziara hii mawaziri hao wameweza kujionea hali halisi ya maisha ya wakazi wa mipakani na jinsi wanavyohusiana na wenzao wa nchi ya jirani ya Uganda ambapo wamekuwa wakishirikiana na kuishi kwa amani katika shughuli zao za kila siku.

Aidha, ziara hii ni maandalizi ya mkutano wa ujirani mwema kati ya mawaziri wa Serikali ya Uganda na mawaziri kutoka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambao unatarajiwa kufanyika Julai  29 , Bukoba mkoani Kagera.

Jiwe la mpaka wa Tanzania na Uganda

TCU Yawatoa Hofu Wanafunzi Wanaotarajia Kujiunga Vyuoni Mwaka Huu

$
0
0
Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) imesema kuwa haitegemei kufutiwa udahili kwa wanafunzi kwa baadhi ya vyuo, kutawakosesha baadhi ya wanafunzi watarajiwa nafasi au kozi walizodhamiria kwenda kuzisoma.

Akizungumza kwenye Viwanja vya Maonesho, Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam jana, Ofisa Habari Mwandamizi, Edward Mkaku alisema TCU haitahusika na wanafunzi ambao watakosa vyuo kwa sababu kwa sasa wameratibu udahili na hivyo ni jukumu la mwanafunzi kutafuta chuo kulingana na ufaulu alionao.

“Hatutarajii mwanafunzi kukosa chuo, na pia kufutiwa udahili kwa baadhi ya vyuo siyo sababu ya wanafunzi kukosa nafasi kwenye vile vyuo vilivyopo,” alisema.

Ndugai Aula....Achaguliwa Kushika Wadhifa Mzito Afrika

$
0
0
Ofisi ya Bunge inapenda kuuarifu umma kuwa Spika wa Bunge Mhe. Job Yustino Ndugai (Mb), amechaguliwa kuwa Mwenyekiti  wa Maspika na Viongozi wa Bunge katika Umoja wa Mabunge ya Jumuiya ya Madola Barani Afrika. 

Uchaguzi huo umefanyika  katika Mkutano wa Maspika wa Mabunge ya Jumuiya ya Madola Barani Afrika uliomalizika jana Mjini Abuja.

Kwa wadhifa huo, Mhe Ndugai ataongoza Maspika wenzake toka Mabunge na Mabaraza ya kutunga Sheria  63 yaliyoko katika nchi 18 za Jumuiya ya Madola kwenye Bara la Afrika. 

Wadhifa huo ni wa miaka miwili kuanzia sasa hadi mwaka 2019 kutakapofanyika uchaguzi mwingine.

Nchi wanachama wa Umoja wa Mabunge Barani Afrika ni pamoja na Afrika  ya Kusini, Botwana, Cameroon ,Ghana, Kenya, Lesotho,   Msumbiji, Mauritius, Malawi, Nigeria, Namibia, Rwanda, Seychelles, Sierra Leone, Swaziland, Tanzania, Uganda na Zambia.

Akizungumzia uchaguzi huo,  Mhe Ndugai amesema "Kwa hakika nawashukuru Maspika wenzangu kwa kunipa dhamana hii ya kuwa Mwenyekiti wao, ni heshima kwangu binafsi lakini zaidi Kwa Tanzania. Ni matumaini yangu kwamba Bunge letu litaendelea kung'ara kitaifa na kimataifa tukiwa Bunge moja lenye Upendo na mshikamano".

Huu ni wadhifa wa nne kwa Mhe. Ndugai katika masuala ya Bunge kwenye medani ya Kimataifa. Amewahi kuwa Mwakilishi wa Nchi za Afrika Mashariki katika Kamati ya Utendaji ya Umoja wa Mabunge ya Jumuiya ya Madola Duniani mwaka 2008-2011, Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma za Jamii ya Umoja wa Mabunge ya Afrika, Pacific na Carribbean na Jumuiya ya Ulaya  mwaka 2011-2014 na Rais wa Baraza la Mabunge ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC – PF)

Imetolewa na:
Kitengo cha Habari, Elimu na Mawasiliano
Ofisi ya Bunge
DODOMA

Waliovuliwa Ubunge na Lipumba CUF Wafungua Kesi Mahakamani

$
0
0
Siku chache baada ya Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF, Prof. Lipumba kuwavua uanachama Wabunge wanane wa Viti Maalum kisha Spika Ndugai kuridhia uamuzi huo, jana July 27, 2017 Wabunge hao wamefungua kesi katika Mahakama Kuu ya Tanzania.

Wabunge hao wamefungua kesi hiyo iliyopewa namba 143/2017 kupitia Wakili wao Peter Kibatala lakini hata hivyo bado haijapangiwa Jaji huku Wabunge hao wakidai hawajapewa muda wa kujitetea.

Mbali na kufungua kesi katika Mahakama Kuu Tanzania, pia wamekata rufaa ndani ya Chama chao kupinga utekelezaji huo na kuiomba Mahakama isitishe utekelezaji wa uamuzi wa kufukuzwa Uanachama wao.

Barrick (Acacia) Wakubali Yaishe.....Wiki Ijayo Wataanza Mazungumzo na Serikali

$
0
0
Kampuni ya Barrick Gold ya nchini Canada, imesema wiki ijayo timu ya wataalamu wake watakuja nchini kwa ajili ya kufanya mazungumzao na Serikali kuhusu uendeshaji wa migodi yake.

Tamko hilo limekuja siku chache baada ya Rais Dk. John Magufuli kutangaza kuwa iwapo Barrick inayoimiliki Kampuni ya Acacia itachelewa kuja kufanya mazungumzo ataifunga migodi yao.

Wakati kampuni hiyo ikijiandaa kuja nchini, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) tayari imepeleka madaia ya Dola za Marekani bilioni 190 ambazo ni sawa na Sh trilioni 424), kwa Kampuni ya Acacia, ikiwa ni malimbikizo ya kodi kutoka mwaka 2000.

Taarifa iliyochapishwa kwenye mtandao wa Financial Post juzi ilisema. “Kampuni ya Barrick Gold kupitia ripoti yake ya robo mwaka imesema itaanza majadiliano na Serikali ya Tanzania wiki ijayo kuhusu marufuku ya kusafirisha nje madini na masuala mengine yaliyoikumba kampuni inayoimiliki ya Acacia.

“Taarifa hiyo ya mazungumzo inakuja baada ya Jumatatu wiki hii Tanzania kuwasilisha bili ya dola bilioni 190 kwa Accacia yenye makao makuu Uingereza.

“Serikali ya Tanzania inaituhumu Acacia, ambayo inamilikiwa na Barrick kwa asilimia 63.9 kudanganya mapato yake ili kukwepa kodi na hivyo kuitaka ilipe malimbikizo pamoja na faini. Acacia imekana tuhuma hizo.

“Tanzania pia iliweka marufuku ya kusafirisha mchanga wa dhahabu (makinikia) na fedha Machi mwaka huu, hatua ambayo inaweza kuathiri asilimia sita ya uzalishaji wa wakia milioni 5.3 hadi milioni 5.6 ya dhahabu kwa mwaka katika migodi ya Acacia.

“Barrick ilisema inasubiri hadi Acacia itakaporekebisha mwongozo wake wa uzalishaji kabla ya kubadili mwelekeo mzima wa uzalishaji wake kwa mwaka,” ilisema taarifa hiyo.

Taarifa hiyo ilisema, Barrick yenye makao yake makuu Toronto, Canada iliripoti kuongezeka kwa mapato kufikia Dola bilioni 1.08 robo iliyoishia Juni 30, kutoka dola milioni 138 kwa mwaka mwaka jana.

“Hilo lilichochewa na mafanikio makubwa ya mauzo ya hisa katika mgodi wa Veladero na mradi wa Cerro Casale. Mtiririko wa fedha kwa kipindi hicho ulikuwa dola milioni 43 ukiwa umeshuka kutoka dola milioni 274 kwa kipindi kama hicho mwaka jana kutokana na kiwango cha juu cha kodi, ongezeko la mtaji na ongezeko lililopangwa kwa ajili ya matumizi ya ukuaji wa badaye,” ilisema.

Juni 14 mwaka huu, Rais Magufuli alikutana na kufanya mazungumzo na Mwenyekiti wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation Profesa John Thornton na Ikulu ikatoa taarifa kwa umma kwamba, katika mazungumzo hayo, kampuni hiyo imesema  ipo tayari kufanya mazungumzo na Serikali ya Tanzania ili kulipa fedha ambazo Tanzania imezipoteza kutokana na kampuni hiyo kuendesha shughuli zake hapa nchini.

Julai 21, 2017 akizungumza kwenye mkutano wa hadhara mkoani Kigoma, Rais Magufuli alisema.“Nitasimamia haki siku zote katika maisha yangu, na niliwaambia nimeanzisha vita hii ya kiuchumi, vita ya kiuchumi ni mbaya sana, wakubwa wale huwa hawafurahi, kuna viongozi wengi tu mliona yaliyowapata ni kwasababu nchi zao zilikuwa na mali.

“Lakini wale wakubwa wakataka kuchezea hizo mali, kwa manufaa yao na siyo kwa manufaa ya wananchi wa pale, walitumia mbinu nyingi za kila aina, lakini Mungu wangu ni mwema na Watanzania ni wema watasimama kwa ajili ya taifa hili.

“Ninayoongea nayajua ni matrilioni ya fedha ambayo yameibiwa, na kwasasa hivi tumewaita waje wafanye mazungumzo, wamekubali lakini wakichelewachelewa  nitafunga migodi yote.

“Ni mara 10 migodi hii tukaigawana Watanzania wachimbe wawe wanauza tuwe tunapata kodi, kuliko kuchimbwa na watu wanaojiita wawekezaji halafu hawalipo kodi.

“Walikuwa wanazungumza mle wanachimba dhahabu, madini machache tu, matatu. tumegundua mle kuna madini mengi.

“Tanzania hii ni nchi tajiri, lakini imekuwa ikiibiwa mno, tumechezewa sana, mimi nipo serikalini na mimi ndiye najua siri za serikali, tumechezewa sana kwa kuibiwa sana mali zetu, kwenye dhahabu huku tumeibiwa mno, ukiyajua yale yaliyokuwa yanafanyike mle unaweza ukalia.

“Unaweza ukatamani usiishi, mtu anachimba anapokea anapeleka na anashirikiana na baadhi ya watu tuliowaamini kwenda kulisimamia hili.

“Anasema hapa tunasafirisha mchanga na Watanzania wote tunaamini tunasafirisha mchanga, mbona hawajaja Kibondo kuchukua mchanga wa hapa mbona na penyewe tunao?

“Lakini tunaamini, wanaupeleka kwenye makontena wanapeleka Ulaya na wakisha enda kuusafisha kule ule mchanga unaobaki wala hawaurudishi, ulikuwa ni utapeli wa ajabu, na ni aibu kubwa kuona utapeli huu unafanywa na watu ambao ni wakubwa.

Julai 26 akiwa mkoani Singida, Rais Magufuli tena alisema “Haiingii akilini watu wanakuja wanachukua mali zetu na kuondoka nazo, ifike mahali tuamke, tumeibiwa vya kutosha, nendeni mkachimbe madini, hizo fedha tutagawana sisi, hata kama hatufanyi kazi hizo fedha tutagawana.

“Wapo wachina wanakuja kuchimba barabara hapa nchini, tunashindwaje kuwatumia hawa wakachimbe madini yetu kisha wakatuachia dhahabu yetu halafu wao wakaondoka?

“Mimi ndiye Rais, hakuna anayejua siri za serikali kama mimi na nawaambia mmepata mtu ambaye anazungumza ukweli, ningeweza kunyamaza kwa vingine ninavyoviona, lakini nataka kujenga Tanzania mpya.

“Yale makontena yote ningeweza kuwaambia tugawane mzee, hata kingereza ninajua, ningeweza kuwaambia give me ten percent (asilimia 10).

“Ningejenga mahoteli na kuwa na kampuni nyingi kwani wapo Watanzania wamejenga huko nje lakini nyumba za wazazi wao zimechakaa, mimi nimezaliwa hapa, ninaishi hapa na nitakufa hapa,” alisema Rais Magufuli.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images