Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Serikali Yawajibu ACACIA......Yasema TRA Iko Sahihi Kudai Kodi ya Trilioni 424 na Kama Hawaridhiki Wakate Rufaa

$
0
0
Siku Chache baada ya Kampuni ya Acacia kuonyesha kushitushwa na deni lililoelekezwa kwenye kampuni tanzu zinazodaiwa kodi ya dola za Marekani 190 (Sh trilioni 424) na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), serikali imesema kama hairidhiki iende kwenye bodi ya rufaa ya kodi.

Kampuni hizo ni  Bulyanhulu Gold mine (BGML) inayoendesha mgodi wa Bulyanhulu na Pangea Minerals (PML) inayosimamia mgodi wa Buzwagi,.

Serikali pia imeelezwa kushangazwa na jinsi Acacia ilivyojiingiza kwenye suala hilo ikizingatiwa TRA ilipeleka madai ya kodi hizo kwa  BGML na PML.

Wakati hayo yakiendelea, Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC),   limeripoti kuwa  baada ya Acacia   kutoa taarifa juu ya madai ya kodi iliyoainishwa   na TRA, jana asubuhi kwenye soko la hisa la London, hisa za kampuni hiyo ziliporomoka kwa asilimia 7.7.

Taarifa ya TRA kuzidai kampuni hizo matrilioni ya shilingi  imetolewa  ikiwa ni miezi michache baada ya Kamati ya Rais iliyoongozwa na Profesa  Nehemiah Osoro, kutoa taarifa yake   kuonyesha Acacia imekuwa ikiibia serikali  fedha nyingi kwenye mchanga wa dhahabu (makinikia) unaosafirishwa nje ya nchi.

Ilionyesha pia kuwa Acacia inaendesha shughuli zake nchini kinyume cha taratibu kwa sababu haijasajiliwa.

Baada ya taarifa hiyo kutolewa, Juni 14, Rais Magufuli alikutana na Mwenyekiti wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation Profesa John Thornton,    Dar es Salaam.

Baadaye Ikulu  ilitoa taarifa kuwa Barrick inayomiliki zaidi ya asilimia 60 ya migodi hiyo, ilisema  ipo tayari kufanya mazungumzo na Serikali kulipa fedha ambazo Tanzania imezipoteza.

Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano cha Wizara ya Fedha na Mipango, Beny Mwaipaja, jana  alisema deni hilo ni halali na lilikokotolewa kwa mujibu wa sheria  na endapo wadaiwa wana tatizo, wanajua sehemu ya kwenda.

“TRA iliwasilisha deni hilo kwa kampuni za Bulyanhulu na Pangea na wala siyo Acacia, kama wanaona wameonewa, wawasilishe malalamiko yao kwa Kamishna wa TRA au bodi ya rufani za kodi, yatafanyiwa kazi,”alisema Mwaipaja.

Alisema kampuni za uwekezaji zinajua utaratibu wa kufuata kama zinaona kuna tatizo, hivyo basi Acacia ina muda wa kutosha wa kuwasilisha malalamiko yake kwenye mamlaka zinazohusika kuliko kulalamika bila ya kufuata utaratibu.

“Kila mgodi umepelekewa bili yake kasoro Acacia ambao bado hawajapelekewa bili,”alisema.

Mkurugenzi wa Elimu kwa Mlipakodi wa TRA, Richard Kayombo amesema   masuala yanayohusu mlipakodi, kwa mujibu wa sheria Mamlaka  hairuhusiwi kuyajadili hadharani bali huwasiliana na mhusika moja kwa moja.

“Issue (suala) za mlipakodi kisheria haturuhusiwi kuzi-discuss in public (kuzijadili hadharani) huwa tunawasiliana na mlipakodi moja kwa moja,”alisema Kayombo.

Taarifa ya ACACIA
Taarifa ya Acacia juzi ilisema TRA  inaonyesha kuwa migodi yake ya Bulyanhulu inadaiwa kodi ya kati ya mwaka 2000 hadi 2017  wakati Pangea inadaiwa kodi ya kati ya 2007-2017.

Taarifa yake inasema uchambuzi uliofanywa na TRA umeonyesha Mgodi wa Bulyanhulu unadaiwa dola za Marekani bilioni 154 (Sh trilioni 344.8) na Mgodi wa Pangea dola bilioni 36 (Sh trilioni 76.1).

Inasema dola bilioni 40 (Sh trilioni 89.5 trilioni) ni malimbikizo ya kodi na dola bilioni 15 (Sh trilioni 335.9) ni adhabu na riba.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo iliyochapishwa kwenye tovuti ya kampuni hiyo, kodi hiyo imetokana na ripoti za kamati mbili za Rais zilizoonyesha kuwa kampuni hizo zimekuwa hazitangazi kiasi halisi cha mapato yake yanayotokana na makinikia.

Hata hivyo, Acacia ilisema inaendelea na msimamo wake wa kupinga matokeo ya kamati hizo ikisisitiza imekuwa ikitangaza mapato yake yote.

Kampuni hiyo ilisema bado haijapata nakala za ripoti za kamati ya kwanza na ya pili zilizowasilishwa kwa Rais Magufuli Mei 24 na Juni 12 mwaka huu.

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Jipatie Riwaya Kali ya Kusisimua ya PRESIDENT WIFE Toka kwa Mtunzi makini

$
0
0
NUNUA SASA KITABU CHA PRESIDENT WIFE kwa Tzsh 10000/= Upate muendelezo wa kitabu cha Sorry Madam Destination of My Enemies
 
"Baada ya utawala wa mzee GODWIN na MANKA kutolewa madarakani na EDDY DODWIN, adui mkubwa wa Eddy, JOHN anachukua madaraka ya Mzee Godwin na kuapa ni lazima ataamuangamiza Eddy aliye kuwa rafiki yake wa kipindi kirefu toka wakiwa sekondari. Rahab anaongoza nchi huku kijana machachari Adrus akiwa mlinzi makini kuhakikisha maisha ya mke wa raisi yanakuwa salama, ila K2 na kaka yake wanajawa na uchu wa madaraka na kuhakikisha kwamba wanauangusha uongozi wa Raahab, ila Eddy anasimama kama ngao na kupigania uongozi wa Rahab je atafanikiwa"
 
Ungana nami muandishi wako Eddazaria G.Msulwa katika hadithi hii ya kusisimua

Kitabu hichi kinapatikana katika mfumo wa softy copy kupitia Whatsapp 0657072588 au Email eddazariaM@gmail.com
Pia unaweza wasiliana nami muandishi wa story hizi kupitia simu namba 0657072588 au 0768516188

Usajili Simba, Yanga wazua utata

$
0
0
Shirikisho la Soka la Tanzania (TFF) limezikumbusha klabu zote ambazo zinasimamiwa na shirikisho hilo kuhakikisha zinamaliza zoezi lake la usajili mapema.

TFF imetoa tamko hilo kupitia kwa Ofisa Habari, Alfred Lucas kuwa katika timu 16 za Ligi Kuu ya Tanzania Bara ni mbili pekee ndizo ambazo zimewasilisha majina yao ya usajili kuelekea msimu ujao wa 2017/18.

Katika majina ya klabu hizo, Simba na Yanga siyo miongoni mwao, hiyo inamaana kuwa kumbe hata wachezaji wao wapya waliosajiliwa hivi karibuni bado hawatambuliki ndani ya mfumo wa usajili wa shirikisho hilo.

Baadhi ya wachezaji waliosajiliwa hivi karibuni ni Emmanuel Okwi kwa upande wa Simba na Ibrahim Ajibu upande wa Yanga.

Alfred amesema timu 24 za Ligi Daraja la Kwanza na 24 Ligi Daraja la Pili zinatakiwa kukamilisha mfumo wa usajili kwa kuwa imesalia wiki moja tu kabla ya mfumo kufungwa.

Dirisha la usajili lilifunguliwa Juni 15, mwaka huu na litarajia kufungwa Agosti 6, mwaka huu.

Mwanamke Mmoja Auawa Kibaha....Polisi Watangaza Vita

$
0
0
Baada ya mkazi wa Mharani kwa Matiasi wilayani Kibaha kukutwa amefariki dunia kwa kuuawa na watu wasiojulikana jana majira ya saa moja usiku, Kamanda wa Polisi mkoani Pwani Jonathan Shana ametangaza mapambano makali ya kuwatia nguvuni wahalifu.

Kamanda Shana amesema kuwa  mwili wa mwanamke huyo aliyetambuliwa kwa jina la Mariamu Omari (31) ulikutwa nje ya nyumba anayoishi mbele kidogo umbali wa mita 40 akiwa anavuja damu nyingi sehemu za usoni na jereha kichwani upande wa kushoto huku muuaji akiwa bado hajafahamika.

"Kufuatia tukio hili jeshi la polisi mkoani Pwani linafanya uchunguzi wa kina kuhakikisha wanaweza kuwabaini waliojihusisha na tukio hilo, Pia wananchi wanatakiwa watoe ushirikiano kwa kuwafichua wahalifu ili waweze kuchukuliwa hatua za kisheria.

Pamoja na hayo Kamanda Shana amewatahadharisha watu wote wanaojishughulisha na vitendo vya uhalifu kuacha mara moja  kwani jeshi limejipanga kuwasaka na kuwafikisha katika vyombo vya sheria

Mwana FA na AY Waendelea Kutamba Mahakamani

$
0
0
Wasanii wakongwe wa Bongo Flava, Ambwene ‘AY’ Yesaya na Hamisi ‘Mwana FA’ Mwinjuma wameendelea kupeta mahakamani wakitarajiwa kulipwa kiasi cha shilingi bilioni 2.1 na kampuni ya Mic Tanzania Limited.

Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam imetupilia mbali maombi ya Kampuni hiyo ya huduma za simu za mkononi iliyotaka kukata rufaa katika Mahakama ya Rufaa kupinga amri ya kutakiwa kuwalipa wasanii hao kiasi hicho cha fedha.

Hivi karibuni, Mahakama Kuu ilihalalisha uamuzi wa Mahakama ya Wilaya iliyoikuta na hatia ya kutumia bila kibali nyimbo za wasanii hao kama miito ya simu na kuitaka kuwalipa kiasi hicho cha fedha.

Wakili wa wasanii hao, Albert Msando aliweka pingamizi akiiomba Mahakama Kuu kuyakataa maombi yaliyowasilishwa na wanasheria wa kampuni ya Mic kwa madai kuwa ni batili kwani yalikuwa na makosa ya kisheria.

Jaji Isaya Arufani wa Mahakama Kuu alikubaliana na maelezo ya Wakili Msando na kuyatupilia mbali maombi ya wanasheria wa kampuni hiyo. Bado haijafahamika kama watafanya marekebisho na kurejesha maombi mapya au la.

AY na Mwana FA wanadai kuwa kampuni ya Mic Tanzania Limited ilitumia bila ruhusa yao nyimbo zao ‘Usije Mjini’ na ‘Dakika Moja’.

Baada ya Msiba wa Mkewe......Mwakyembe Leo Kaongea na Waandishi wa Habari

$
0
0

Leo Jumatano ya July 26 ikiwa ni siku 11 zimepita toka utokee msimba wa mke wa waziri wa habari, sanaa, utamaduni na michezo Dr Harrison Mwakyembe, leo ameongea na vyombo vya habari nyumbani kwake Kunduchi Dar es Salaam.

Mwakyembe amewashukuru Watanzania kwa ushirikiano mkubwa waliompa katika kuombeleza kifo cha mkewe Linah Mwakyembe kilichotokea usiku wa Julai 15 mwaka huu kwenye Hospitali ya Aga Khan.

Dk Mwakyembe pia amemshukuru Rais John Magufuli, Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kwa mchango mkubwa walioutoa katika kumuuguza mkewe.

Mbali na hao, Dk Mwakyembe ambaye pia ni Mbunge wa Kyela Mkoani Mbeya, amewashukuru viongozi wote wa dini akiwamo Mufti Mkuu wa Tanzania, Sheikh Aboubakar Zuberi na maaskofu.

"Wanafamilia tutakumbuka moyo adhimu na upendo na ushirikiano tulioupata kutoka Katibu Mkuu wa wizara hii Profesa Elisante Ole Gabriel na viongozi wengine waandamizi wa Serikali. Mwisho kabisa Wanakyela kwa uvumilivu wao katika kipindi hiki kigumu," amesema Dk Mwakyembe.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Madiwani 3 wa CHADEMA Wajiuzulu LEO na Kujiunga CCM

$
0
0
Wakati Wimbi la Madiwani wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kujiunga na Chama cha Mpinduzi (CCM) likiwa limepamba moto mkoani Arusha, majirani zao wa Kilimanjaro nao wameanza kutimka kwa kile wanachodai kuwa ni kuweza kumuunga mkono Rais Dkt John Pombe Magufuli.

Mapema leo mchana Julai 26, 2017, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole amewapokea madiwani watatu kutoka katika Halmashauri ya Wilaya ya Hai ambao wametangaza kujiuzulu nyadhifa zao na kujiunga CCM.

Madiwani waliojiuzulu ni, Diwani wa Kata ya Machame Magharibi, Goodluck Kimaro, Diwani wa Kata ya Weruweru, na  Diwani wa Kata ya Mnadani, Everist Peter Kimati.

Akizungumza wakati wa kutangaza azma hiyo, Goodluck Kimaro alisema kwamba CHADEMA hakuna demokrasia kama ambavyo chama hicho kimekuwa kikijinasibu. 

Akitolea mfano Halimashauri ya Wilaya ya Hai ambapo Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe ni Mbunge wa jimbo hilo, alisema chama hakina uwezo wa kufanya jambo lolote dhidi ya mbunge.

Endapo mbunge atashindwa kutekeleza majukumu yake, chama ndio kinatakiwa kumuadhibu, lakini kwa upande wetu wa Hai hakuna uongozi wa kuweza kufanya hivyo. 

Mbunge huwa hafanyi ziara za kutembelea jimbo kama anavyotakiwa, lakini bado chama hakina sauti, alisema Goodluck Kimaro.

Baada ya madiwani wote kuzungumza, Polepole alionya juu ya uwepo wa vitendo vya kihalifu kwa madiwani ambao wanahama CHADEMA na kusema jambo lolote likitokea kwa madiwani hao waliohama, watashughulikiwa ipasavyo na vyombo vya dola lakini pia chama hicho kingine ndio watakuwa wahusika.

Hadi sasa jumla ya madiwani 9 mkoani Arusha tayari wamejiunga na CCM na sasa watatu mkoani Kilimanjaro nao wamejiunga.

Breaking News: Bunge limeridhia kuvuliwa Uanachama Wabunge 8 wa CUF

$
0
0
Siku moja baada ya Spika wa Bunge Job Ndugai kupokea barua kutoka kwa Mwenyekiti wa CUF Taifa anayetambuliwa na Ofisi ya Msajili, Prof. Ibrahim Lipumba inayoeleza kuwafukuza uanachama Wabunge wanane wa Viti Maalum na Madiwani wawili, Bunge limeridhia.

Leo July 26, 2017 taarifa kutoka ofisi ya Bunge imeeleza kuwa Spika Job Ndugai ameridhia kufutwa uanachama kwa Wabunge hao na hivyo nafasi zao ziko wazi.

Pata Tiba ya Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FUUl POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM .HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamsi ya July 27

Waziri Mkuu Majaliwa avionya vyuo vilivyozuiwa kudahili wanafunzi

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameiagiza Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) na Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) kuhakikisha kwamba programu zote zinazotolewa na taasisi za elimu ya juu zinawawezesha wahitimu kujiajiri na kuwa na sifa za ushindani katika soko la ajira kimataifa.

Amesema wakati umefika sasa kwa wasomi katika vyuo vyetu vikuu tujiridhisha kuwa mitaala inayotolewa kama inawaandaa wahitimu kupata taaluma na stadi za kuweza kujiajiri na kupambana na changamoto za kimaisha.

Amesema taasisi za elimu ya juu nchini ziangalie mitaala yake na kuimarisha mfumo wa ithibati na udhibiti wa ubora wa elimu na mafunzo ili kwenda sambamba na dunia ya kazi inayoendana na agenda ya maendeleo ya Taifa.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo jana (Jumatano, Julai 26, 2017) wakati wa ufunguzi wa maonesho ya 12 ya Elimu ya Juu, jijini Dar es Salaam ambapo amevutaka vyuo hivyo badala ya kuendelea kulumbana kwenye makongamano na vyombo vya habari, vifanye maboresho yanayotakiwa ili viweze kuendelea na ufundishaji.

 Aidha alisema kuwa, lengo la serikali ni kuhakikisha elimu inayotolewa inakuwa bora na kwamba maboresho yanayotakiwa kufanyika yanawezekana.

Waziri Mkuu alisema maonesho hayo ni jukwaa la kipekee ambalo litaibua mjadala sahihi kuhusu uhalali wa kozi zinazotolewa na vyuo husika vya elimu ya juu. “Hivyo mnayo nafasi ya kuonesha kwa vitendo uwezo wenu katika utafiti, ubunifu na matumizi ya sayansi na teknolojia zinazotumika katika maendeleo ya viwanda.”

Alisema ni vema mfumo wa ithibati na udhibiti wa ubora wa elimu na mafunzo ukaimarishwa ili kuhakikisha asilimia 60 ya wanafunzi wanahitimu shahada kwenye sekta ambazo zinachangia kwa kiasi kikubwa kukua kwa uchumi.

Alisema taasisi za elimu ya juu ziweke mikakati ya kuinua na kuboresha taaluma wanayoitoa ili ilete tija kwa maendeleo ya Taifa na Dunia. Pia kuanzisha program za mafunzo zenye kukidhi mahitaji na kuleta maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa kuzingatia mahitaji ya kitaifa, kikanda na kimataifa.

Hata hivyo, Waziri Mkuu amezitaka taasisi hizo kuendelea kuimarisha mfumo wa udahili na kujipanga kutumia fursa za elimu na mafunzo ndani na nje ya nchi kwa makundi yote ya jamii kwa usawa katika ngazi zote hususan ufundi, hisabati, sayansi na teknolojia.

Pia Waziri Mkuu alisema ni wakati muafaka kwa taasisi za elimu ya juu nchini kuandaa mikakati ya kuongeza udahili kwa kuzingatia mahitaji ya rasilimali watu na ujuzi unaohitajika katika sketa zinazokua haraka mfano mafuta, gesi na madini.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
ALHAMISI, JULAI 26, 2017

Zitto aijibu Chadema kuhusu kumsifia Rais Magufuli ziarani

$
0
0
 Na Regina Mkonde
 Mbunge wa Kigoma Mjini ambaye pia ni Kiongozi Mkuu wa chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe amewajibu baadhi ya watu wanaomkosoa na kumuita msaliti kutokana na kitendo cha kumsifia Rais John Magufuli alipokuwa ziarani jimboni humo.

Zitto alijibu mapigo hayo jana wakati akizungumza na wananchi wa Kigoma Mjini, ambapo alisema asingeweza kumkosoa Rais Magufuli wakati ule kwa kuwa alikuwa mgeni jimboni kwake, pia alikuwa anafanya shughuli za maendeleo ya wananchi wa jimboni kwake.

“Rais alikuja hapa akafungua mradi wa maji tukaenda ziwa Tanganyika, kuna watu walikasirika sababu Rais alinisifia sana, hawezi akaja Kigoma mtu akanisema mimi vibaya msingekubali, na mgeni akija siwezi nikaanza kumsema vibaya, mgeni akija unamkaribisha anafanya kazi yake anaondoka, kwani rais akienda kwenye majimbo yao wanamsema, rais alikwenda Bukoba Mjini wakati wa tetemeko, mbunge wa jimbo hilo alimsema ? alikwenda Arumeru kwa mdogo wangu Joshua Nasari, alimsema rais kwa nini akija kigoma mimi ndio nimseme,” alihoji Zitto.

Aliongeza kuwa “Mimi hamkunifundisha kuwa mazwazwa wazee mlinifundisha adabu na kuhakikisha maendeleo yanapatikana lakini sio kwamba rais akikosea hatutamsema tutamsema, na tumeshamsema sana, sisi ndio chama cha mwisho kufanya mkutano wa ziara, tukaja operesheni ya linda demokrasia tumemaliza mikutano ikapigwa marufuku.”

“Lakini toka serikali ya awamu ya tano iingie madarakani uhuru umeanza kuminywa sasa ni lazima, hatuwezi kukaa kimya haki ya watu kuwa na mawazo tofauti hatuwezi kuikalia kimya hata kidogo, lakini wakati huo huo hatuwezi tukasimamisha kila kitu kusubiri haki ya kuwa na mawazo huru, lazima haki ya mawazo huru ipiganiwe wakati tunapigania maendeleo,” amesema

 ==>Ulizisoma hizi??
    1. Employment Opportunity: Program Manager

    2.Job: Commercial Director is Needed 


    3.Vacancy: Assistant Project Manager 

Wagombea wa TFF wakamatwa na TAKUKURU.....Yupo Pia Mtangazaji wa Clouds

$
0
0
Wagombea katika nafasi mbalimbali za uchaguzi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na wadau wa soka wamekatwa na TAKUKURU kwa tuhuma za kujihusisha na rushwa jijini Mwanza.

Miongoni mwa waliyokamatwa ni pamoja na Mwenyekiti wa Chama cha Soka Dar es Salaam (DRFA), Almas Kasongo, Shafii Dauda  ambaye pia ni Mtangazaji wa Clouds Media Group, Elias Mwanjale, Leonald Malongo, Effam Majinge, Osuri Kasuli, Richard Kayenzi, Lazack Juma pamoja na Kelvin Shevi.

Hayo amebainisha Msemaji wa Takukuru Ernest Makale na kusema waliwakamata watu hao kwa kuweka mitego sehemu wanazofanyia vikao vyao vya siri.

"Tumewakamata kwa sababu hiki siyo kipindi cha kampeni na dalili zote kwamba walikuwa hapa kwa ajili ya uchaguzi unaotarajiwa zilikuwa zipo wazi, kama Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa tumeona kuna viashiria vya rushwa, tukaweka mitego katika sehemu walizokuwa wanaendesha vikao vyao vya siri tukaweza kuwakamata", amesema Makale.

Pamoja na hayo Makale amesema watuhumiwa hao wameachiwa kwa dhamana ila wanaendelea na uchunguzi wao endapo watakapopata ushahidi wa kutosha watafikishwa mahakamani.

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Manji afungua maombi Mahakama Kuu akiiomba mahakama hiyo imuondolee zuio la dhamana

$
0
0
Mahakama Kuu ya Tanzania imesema inatarajia kuanza kusikiliza maombi ya dhamana yaliyotolewa na Mfanyabiashara maarufu Tanzania Yusuf Manji, August 4, 2017.

Jaji Isaya Arufani amesema hayo jana baada ya Mawakili wa Serikali Paul Kadushi na Simon Wankyo kuyapokea maombi hayo na kusema wana nia ya kuyapinga huku Jaji akisema anakubaliana na hoja zao na August 4, 2017 maombi hayo ya dhamana yataanza kusikilizwa.

Katika maombi hayo Yusuf Manji anaiomba Mahakama Kuu itengue hati ya kunyimwa dhamana iliyowasilishwa na Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kwa kuwa ana matatizo ya kiafya akisumbuliwa na matatizo ya moyo.

Breaking News: Tundu Lissu Kaachiwa Kwa Dhamana

$
0
0
Mbunge wa Singida Mashariki (CHADEMA) na Rais wa Chama cha Mawakili Tanzania, Mhe. Tundu Lissu ameachiwa kwa dhamana ya Milioni 10 leo katika kesi yake iliyokuwa inamkabili ya uchochezi.

Mahakama ya Kisutu imempa dhamana Mh Tundu Lissu kwa sharti la kuwa na wadhamini wawili watakaosaini dhamana ya thamani ya milioni kumi.

Aidha, Mahakama hiyo pia imemtaka Tundu Lissu kutokuondoka nje ya jiji la Dar es Salaam bila kuwa na kibali maalum cha mahakama. Uamuzi huo umetolewa mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Kisutu Jijini Dar es Salaam, Wilbard Mashauri.

Upande wake Tundu Lissu alikuwa anatetewa na jopo la mawakali 18 likiongozwa na Fatma Karume na Peter Kibatala ambapo katika shauri la kwanza waliomba Mahakama impe dhamana mteja wao.

Tundu Lissu alitiwa katika mikono ya dola mnamo Julai 20 siku ya Alhamsi katika uwanja wa ndege akiwa anaelekea nchini Rwanda. na siku iliyofuata  jeshi hilo lilikwenda kufanya upekuzi nyumbani kwa Mbunge huyo.

Aidha kesi yake imepangwa kusikilizwa Agosti 24 mwaka huu baada ya wadhamini wake kukamilisha taratibu zote za kumdhamini. 

 ==>Ulizisoma hizi??
    1. Nafasi za kazi: Program Manager Anahitajika

    2.Nafas za Kazi: Commercial Director Anahitajika


    3.Vacancy: Assistant Project Manager 


ACACIA yalipa Milioni 460 za ushuru

$
0
0
Mgodi wa dhahabu wa Acacia Bulyanhulu (BGML) uliopo katika Halmashauri ya Msalala, mkoa wa Shinyanga jana Jumatano Julai 26,2017 umekabidhi hundi yenye thamani ya Shilingi 460,732,841.08/= kwa ajili ya ushuru wa Huduma kwa halmashauri ya Msalala.

Akizungumza wakati wa kukabidhi hundi hiyo,Meneja Mkuu wa Mgodi wa Bulyanhulu Graham Crew alisema kiasi hicho ni asilimia 67 ya malipo ya ushuru wa huduma kwa ajili ya kipindi cha miezi sita kuanzia Januari hadi mwezi Juni mwaka huu ambacho ni asilimia 0.3 ya ukokotoaji wa ushuru wa huduma wa mgodi huo katika kipindi hicho.
 
 “Jumla ya malipo ya ushuru wa huduma kwa kipindi cha miezi sita iliyopita ni shilingi za Kitanzania 687,660,956.84/=,ambapo malipo hayo yamegawanywa katika halmashauri mbili ambazo ni Msalala inayopata asilimia 67 na Nyang’wale iliyopo mkoani Geita inapata asilimia 33”,alifafanua Crew.
 
Alisema kutokana na mgawanyo huo,halmashauri ya Msalala imelipwa shilingi milioni 460 (460,732,841.08/= ) na Nyang’wale shilingi Milioni 226 (226,928,115.76/=.
 
“Ushuru umepungua kwa kuwa mgodi haujafanya mauzo ya makinikia ambayo yamezuiwa tangu mwanzoni mwa mwezi machi mwaka huu, hivyo tunafahamu kuwa tutalipa zaidi tutakapouza makinikia ambayo yapo yanaendelea kukusanywa mgodini”,aliongeza Crew.
 
Katika hatua nyingine Crew alisema tangu mwaka 2000 mpaka sasa mgodi huo umelipa zaidi ya shilingi 10,247,742,957/= za kodi ya ushuru wa huduma na kampuni ya Acacia ilianza kutoa malipo ya ushuru wa huduma wa asilimia 0.3 ya mapato ghafi kwa halmashauri husika mwaka 2014.
 
 “Mgodi wetu unaendelea kuwa na matarajio ya kuchangia kuimarisha sekta ya viwanda kwenye uchimbaji madini katika halmashauri ya Msalala huku tukiendelea kutekeleza mkakati wa Jamii Endelevu wa Acacia ulioanzishwa mwaka 2016 kwa kushauriana na wadau lengo likiwa ni kuchangia maendeleo ya Jamii Endelevu inayonufaika na kukua kwa uchumi ndani ya jamii ili kujenga mahusiano ya kuaminika”,alisema Crew.
 
Akipokea hundi hiyo kisha kuikabidhi kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Msalala, Mkuu wa wilaya ya Kahama Fadhili Nkurlu aliushukuru mgodi wa Acacia Bulyanhulu kwa kuendelea kuunga mkono jitihada za serikali katika kutoa huduma kwa jami.
 
“Hiki kiwango cha shilingi milioni 460 tulichopokea ni kiwango kizuri ingawa kimepungua ulikinganisha na kipindi cha miezi sita cha Mwezi Juni hadi Desemba 2016,furaha inatujaza kwamba ile shilingi milioni 300 na zaidi ipo ndani ya Makinikia, yatakapouzwa tutaipata na tutaendelea kuboresha huduma za kijamii”,alieleza Nkurlu.
 
Nkurulu alimuomba mkurugenzi wa halmashauri ya Msalala kuhakikisha fedha zilizotolewa na mgodi huo zitumike kwa huduma za kijamii kama zilivyokusudiwa ikiwemo kuboresha huduma za afya na miundombinu.
 
Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Msalala Simon Berege alisema mapato waliyopokea kutoka mgodi huo yako chini kwa shilingi milioni 300 ukilinganisha na kipindi kilichopita cha kuanzia Mwezi Julai hadi Desemba 2016 ambapo mgodi huo ulipokea shilingi milioni 760.
 
“Sisi tumepokea mapato haya kama tunavyopkea mapato mengine tunayopata katika halmashauri zetu,mapato haya ni yako chini ukilinganisha na kipindi kilichopita,tunaambiwa mapato yamepungua kutokana na Makinikia ambapo sasa yamesimama,hii inaleta changamoto katika ukusanyaji wa mapato katika halmashauri yetu, tunaamini mazungumzo baina Acacia na serikali yakiisha halmashauri yetu itapata mapato mengi Zaidi,” aliongeza Berege.
Meneja Mkuu wa Mgodi wa Bulyanhulu Graham Crew akizungumza wakati wa kukabidhi hundi yenye thamani ya Shilingi milioni 460 kwa ajili ya ushuru wa Huduma kwa halmashauri ya Msalala wilayani Kahama  jana Jumatano Julai 26,2017 katika ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Kahama.Kulia ni Mkuu wa wilaya ya Kahama Fadhili Nkurlu.
Hundi yenye thamani ya Shilingi milioni 460 iliyotolewa na Mgodi wa Acacia Bulyanhulu kwa ajili ya ushuru wa Huduma kwa halmashauri ya Msalala.
Kushoto ni Meneja Mkuu wa Mgodi wa Bulyanhulu Graham Crew akimkabidhi Mkuu wa wilaya ya Kahama Fadhili Nkurlu hundi yenye thamani ya Shilingi milioni 460 kwa ajili ya ushuru wa Huduma kwa halmashauri ya Msalala. 
Mkuu wa wilaya ya Kahama Fadhili Nkurlu (kulia) akishikana mkono na Meneja Mkuu wa Mgodi wa Bulyanhulu Graham Crew wakati wa zoezi la kukabidhi hundi yenye thamani ya Shilingi milioni 460 kwa ajili ya ushuru wa Huduma kwa halmashauri ya Msalala.
Mkuu wa wilaya ya Kahama Fadhili Nkurlu akimkabidhi Mkurugenzi wa Halmashauri ya Msalala hundi yenye thamani ya Shilingi milioni 460 kwa ajili ya ushuru wa Huduma kwa halmashauri ya Msalala. 
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Msalala Simon Berege akizungumza wakati akimkabidhi hundi hiyo Kaimu Mweka Hazina wa halmashauri hiyo Saleh Bugege (kushoto). Wa kwanza kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano ya Jamii mgodi wa Acacia Bulyanhulu Sarah Ezra Terry.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Msalala Simon Berege akizungumza baada ya kupokea hundi yenye thamani ya shilingi milioni 460 kwa ajili ya ushuru wa Huduma kwa halmashauri ya Msalala.
Mkuu wa wilaya ya Kahama Fadhili Nkurlu akizungumza wakati wa makabidhiano ya hundi yenye thamani ya shilingi milioni 460 kwa ajili ya ushuru wa Huduma kwa halmashauri ya Msalala.
 
Picha zote na Kadama Malunde- Malunde1 blog

RC Gambo Ampa Onyo Godbless Lema

$
0
0
Wakati Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema akisema haogopi kusema ukweli, Mkuu wa mkoa huo, Mrisho Gambo amemtahadharisha kuwa hataacha kumchukulia hatua iwapo atamtukana Rais John Magufuli na Serikali yake.

Lema ambaye ameanza kufanya mikutano ya hadhara katika jimbo lake jana kwenye Soko Kuu la Arusha mjini alisema haogopi kusema ukweli hata kama akipingwa na baba yake mzazi.

“Taifa lipo kwenye mgawanyiko mkubwa, wakuu wa wilaya na mikoa wanafanya maamuzi kwa maelekezo kutoka ngazi za juu,” alisema.

Aliongeza kuwa hali ya demokrasia nchini ni mbaya kwa kuwa hakuna usawa na kuwataka viongozi kuomba hekima wanapopata mamlaka ya uongozi.

Kadhalika amezungumzia hatua ya kujiuzulu kwa Diwani wa Muriet, Credo Kifukwe akisema kuwa Chadema haihitaji jeshi la watu wengi bali la wachache wenye umoja. 

“Nimeteswa sana katika mji wa Arusha, lakini nawataka wafuasi wa Chadema msilipize kisasi kwa wanaohama chama. Leo wapinzani hawaruhusiwi kufanya siasa, lakini Rais anazunguka nchi nzima,” alisema.

Mbunge huyo alisema Tanzania inahitaji demokrasia ya kweli na amani ya nchi haiwezi kutunzwa na polisi isipokuwa kwa upendo wa Watanzania.

Pia, alimtaka Gambo kujipanga wakati wa uchaguzi mdogo wa madiwani kwa kuwa Chadema imejipanga kikamilifu. 

Katika mkutano huo, Lema aliwapandisha jukwaani madiwani wawili wa Chadema jijini Arusha, Obeid Meng’roriki wa Kata ya Terat na Ruben Ngowi wa Kimandolu huku akisema amesikia wanataka kujiuzulu nyadhifa zao.

Hata hivyo, madiwani hao waliposimama walisema wao hawana bei ya kuweza kununuliwa na mtu yeyote.

Wakati Lema akiyasema hayo, Gambo alisema Serikali ya Awamu ya Tano imejipambanua katika utendaji wake, hivyo mwanasiasa yeyote hataruhusiwa kutoa matamshi yenye kumdhihaki Rais na Serikali.

Akizungumza katika mkutano na viongozi wa madhehebu ya dini uliofanyika jana kwenye ukumbi wa mikutano wa AICC alisema: “Tumempa mbunge wa jimbo hili (Arusha Mjini) kibali cha kufanya mikutano na wananchi wake kwa sababu ni kiongozi aliyechaguliwa na wananchi, hatuna sababu ya kumzuia, ila hatutakubali kusikia kwenye mikutano yake akimtukana Rais wetu na Serikali yake. Akifanya hivyo tutamshughulikia.”

“Mtu yeyote anayetaka kuichezea Serikali na kutaka kukwamisha ajenda zake tutawang’oa iwe kwa greda au kwa namna nyingine yoyote, Rais Magufuli alipita nchi nzima akitoa ahadi zake na wamemchagua sasa wamwache atekeleze alichowaahidi wananchi.”

Gambo alitumia mkutano huo kuzungumzia kadhia ya rambirambi zilizotolewa kufuatia ajali ya wanafunzi wa Lucky Vincent iliyopoteza maisha ya watoto na wafanyakazi wapatao 35 na baadaye Meya wa Jiji la Arusha, Kalist Lazaro na Lema kutilia shaka matumizi yake.

 ==>Ulizisoma hizi??

     1. Ufafanuzi wa serikali kuhusu ajira 3,152 zilizotangazwa

    2.Nafas za Kazi: Commercial Director Anahitajika 
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live


Latest Images