Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya July 20
↧
↧
Serikali kuwashughulikia wanaotoa matamshi ya kichochezi
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali itawashughulikia watu wote wanaotoa matamshi ya kichochezi nchini bila ya kujali nyadhifa zao.
Amesema ni vema watu wakawa makini na kijiepusha kutoa matamshi ambayo yataathiri mfumo wa maisha kwa wananchi wengine.
Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo jana (Jumatano, Julai 19, 2017) wakati wa ibada ya mazishi ya mke wa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe Bibi Linnah Mwakyembe iliyofanyika wilayani Kyela.
Alisema Serikali haitavumilia kuona baadhi ya watu wakitoa matamshi ambayo hayana tija kwa jamii na badala yake yanalenga kuwavuruga wananchi na kuchochea migogoro.
”Tutashughulika na watu wote wanaotoa matamshi ya kichochezi, popote walipo bila ya kujali uwezo wao, vyeo vyao na mamlaka walizonazo.”
Pia aliwaomba viongozi wa dini waendelee kuliombea Taifa na viongozi wake na kwamba Serikali inawategemea na iko pamoja nao.
Waziri Mkuu alitoa kauli hiyo baada ya Askofu wa Kanisa la Evarinjerical Brother Hood, Rabison Mwakanani kuonya vitendo vya baadhi ya watu kumtukana Mheshimiwa Rais Dkt. John Magufuli.
Alisema ni vema watu hao wakajifunza namna ya kuwasilisha hoja zao bila ya kutumia lugha za matusi.
“Rais Dkt. Magufuli amefanya mambo mengi makubwa kwa ajili ya maendeleo. Wanaofanya hivyo wasidhani kama wanamtukana Rais tu bali wanawatukana Watanzania wote waliomchagua wakiwemo viongozi wa dini.”
Pia aliwaomba wananchi kufanya maandalizi mapema kwa sababu wote ni wapitaji, hivyo waandae roho zao kwa kuacha kufanya dhambi na maovu yote ili wawe na mwisho mwema.
Vile Vile Waziri Mkuu aliwaomba wananchi wote washirikiane kwa pamoja kumuombea Dkt. Mwakyembe na familia yake ili Mwenyezi Mungu aweze kuwafariji katika kipindi hiki kigumu.
“Wajibu wetu sote ni kumuomba Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema. Tunajua kwa sasa Dkt. Mwakyembe yuko katika wakati mgumu, namuhakikishia kwamba hayuko peke yake kwani Serikali iko pamoja naye katika kipindi hiki kigumu.”
Naye, Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai alimpa pole Dkt. Mwakyembe huku akiitaka familia kuendelea kuwa na upendo kama ule uliokuwepo wakati wa uhai wa marehemu Bibi Linnah.
Kwa upande wake, Mtoto mkubwa wa marehemu, George Mwakyembe alisema anaamini mama yao, alijiandaa na kifo hicho kwa kuwa alikuwa mchamungu.
“Mama alikuwa na ratiba kila siku ifikapo saa nne usiku lazima afanye ibada, Hivyo nina matumaini makubwa kupitia Uchamungu wake, Mwenyezi Mungu atamuweka mahala pema.”
↧
Tundu Lissu Jana Alitoa Kali........Ni Baada ya Kugoma Kutoka Mahakamani Akihofia Kukamatwa na Polisi
Mbunge wa Singida Mashariki ambaye pia ni Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Tundu Lissu jana aligoma kutoka katika chumba cha mahakama kufuatia kuwepo kwa tetesi kuwa kuna baadhi ya polisi wametumwa kumkamata kiongozi huyo. .
Lissu alifika mahakamani hapo jana asubuhi kwa ajili kusimamia kesi ya migogoro ya ndani ya Chama cha Walimu Tanzania (CWT) iliyokuwa ikisikilizwa na Hakimu Proches Mushi.
Katika kesi hiyo, Kamati ya Utendaji ya CWT wilaya imefungua kesi dhidi ya Katibu Mkuu wa CWT, Yahaya Msulwa wakimtuhumu kwa matumizi mabaya madaraka.
Hata hivyo wakijadili muda wa kurudi tena kwa kesi hiyo, Lissu ambaye pia ni Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika, (TLS) alisema kuna polisi waliovalia kiraia waliokuwa wakimngojea nje ili wamkamate na kumsafirisha kwenda Dar es Salaam.
Habari za kutaka kukamatwa kwa Lissu zilisikika asubuhi katika mitandao ya kijamii baada ya kutumiwa ujumbe kuwa kuna maaskari waliovalia kiraia wanataka kumkamata.
“Mheshimiwa naomba kesi hii isisomwe tarehe 23 kwa sababu sitakuwepo nchini, natarajia kwenda Uganda kwenye kikao cha vyama vya Afrika Mashariki vya mawakili,”alisema na kuongeza:
“Lakini pia nimepewa taarifa kuwa hapo nje kuna polisi wananisubiri nikitoka wanikamate na kunisafirisha kwenda Dar es Salaam hivyo huenda tarehe hiyo (Julai 23) nisiwe huru kuhudhuria kesi.”
Akijibu maombi hayo Mushi alisogeza kesi hiyo hadi Septemba 27-29 kwa ajili ya kuendelea na ushahidi.
Mara baada ya kesi kuahirishwa, Lissu akafanya mkutano na waandishi wa habari ndani ya ukumbi wa mahakama hiyo na kudai hatatoka mahakamani hapo ili aone kama polisi wana uwezo wa kuingia na kumkamata.
“Leo asubuhi nimepata taarifa kutoka Dar es Salaam kwa mama watoto wangu kwamba polisi walikuja nyumbani kwangu kunitafuta na wakaelezwa kwamba yuko Dodoma kwa muda wa siku tatu,” alisema.
“Baada ya hapo wasamaria wema walinitaarifu kuwa Jeshi la Polisi Dar es Salaam limewaomba wenzao wa Dodoma wanikamate pindi tu nitakapotoka hapa na kunirejesha Dar es Salaam.”
Alipoulizwa sababu inayofanya polisi watake kumkamata, Lissu amesema ni kutokana na maoni yake aliyoongea juzi ya kuukosoa uongozi wa Rais Magufuli.
“Rais Magufuli na chama chake wameshindwa siasa na wanachofanya sasa ni kutumia mabavu lakini wao kama Chadema kamwe hawataogopa wala kukaa kimya kwani kazi yao si kumsifia Rais bali ni kumkosoa anapofanya vibaya,”amesema.
Lissu ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki alisema hakuna sheria yoyote inayowaruhusu polisi kumkamata wakili akiwa katika shughuli zake mahakamani.
“Nakaa nione kama watavunja sheria ya kuja kunikamatia hapa hapa mahakamani. Nimeshazoea kukamatwa tangu mwaka huu uanze nimekamatwa mara nne,”alisema.
Baada ya kukaa mahakamani kwa saa nne, alifika Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Lazaro Mambosasa na kumweleza Lissu kwamba Jeshi la Polisi Dodoma halina taarifa yoyote wala mpango wowote wa kumkamata.
“Hatujapokea taarifa yoyote wala maelekezo yoyote ya kukukamata kutoka makao makuu. Hata ingekuwa hivyo tungeshakukamata kwa sababu muda wa mahakama umekwisha. Kwa sasa hivi yamebakia majengo tu kwa hiyo uwe huru uendelee na shughuli zako,” Mambosasa alimwambia mbunge huyo.
Baada ya Mambosasa kuondoka katika mahakama hiyo, Lissu naye aliondoka katika eneo hilo.
↧
Jinsi Kitambi Kinavyopatikana na Jinsi Kinavyoondolewa na Dawa ya Mkataa Kitambi
Kitambi ni ile hali ya tumbo kuwa kubwa na kuchomoza kwa mbele na wakati mwingine kufikia hatua ya kunin’ginia.
JINSI KITAMBI KINAVYO PATIKANA
Kwa mujibu wa tafiti mbalimbali za kitaalamu, mwili wa binadamu una seli kati ya bilioni 50 hadi 200 za mafuta zilizogawanyika katika sehemu mbalimbali za mwili wa binadamu.
Kwa wanawake seli hizo zipo sana katika maeneo ya matiti, kwenye nyonga, kiunoni na kwenye makalio.
Kwa upande wa wanaume seli hizo zinapatikana sana kwenye kifua, tumboni na kwenye makalio pia.
Mafuta ya tumbo yanayofanya kitambi hukusanywa kwa njia kuu mbili:
i.Njia ya kwanza ni mafuta kutoka kwenye tishu zilizo chini ya ngozi
ii.Na njia ya pili ni kutoka kwenye ogani za ndani kama moyo, kongosho n.k
SABABU ZA KUPATA KITAMBI
Sababu kubwa ya kitambi ni kukosekana ulingano wa nguvu(kalori) katika mwili wa mwanadamu, hali inayo sababishwa na mtu kula vyakula vinavyotia nguvu sana kuliko jinsi anavyoweza kutumia na kutoa kama taka mwili.
VYAKULA VINAVYO CHANGIA KULETA KITAMBI
Vyakula vinavyochangia kuleta kitambi ni pamoja na :
i.Vyakula vyenye mafuta mengi kama vile nyama nyekundu (iwe ni ya kuchemsha, kukaanga au kuchoma), nyama ya kuku wa kizungu ( iwe ya kuchemsha, kukaanga ama kuchoma ), mafuta ya kupikia, (hasa yale yatokanayo na bidhaa za wanyama, kama siagi, na jibini), viazi ya kukaanga kwa mafuta (chips) pamoja na pizza.
ii.Vyakula vyenye wanga mwingi kama vile ugali wa mahindi, mihogo, wali, mkate mweupe.
iii. Vyakula na vinywaji vyenye sukari nyingi iliyo ongezwa( added sugar ), kama vile soda na keki.
iv. Vyakula vilivyo tengenezwa kwa ngano na sukari kama vile keki, skonzi, chapatti, maandazi, mkate mweupe nakadhalika
v. Pamoja na vinywaji vilivyo tengenezwa kwa kutumia ngano kama vile bia za aina mbalimbali na kadhalika.
Vyakula vilivyo tajwa hapo juu, vikitumiwa bila kuzingatia kanuni za mlo kamili, huchangia kuleta tatizo la kitambi.
vi. Sababu nyingine ni kutofanya mazoezi ya mwili na viungo( physical exercises ) kwa muda mrefu.
JINSI YA KUJUA KAMA UNA KITAMBI
Kitambi kinaweza kuonekana kirahisi kwa macho. Ila kujua ni kwa kiwango gani kitambi chako kipo inabidi kufanya vipimo vya kiuno(waist) na nyonga (hips).
Mzingo wa kiuno ukiwa >102 cm au 40 kwa wanaume na >88 cm au 35 kwa wanawake, na uwiano wa kiuno na hips(Waist-Hip Ratio) ikiwa >0.9 kwa wanaume na >0.85 kwa wanawake.
BMI ya 30 au zaidi inaashiria 'Obese' uzito kuzidi kiasi. Kuwa na mzingo uliozidi kawaida ni kiashiria hatari cha matatizo ya kimetaboliki, kuliko hata cha BMI.
Kipimo kingine cha kitambi ambacho kimeonyesha uwezo zaidi kuliko BMI katika kutabiri uwezekano mkubwa wa magonjwa ya moyo ni Index Of Central Obesity(Waist-To-Height Ratio-WHtR) ambapo uwiano ukiwa sawa na 0.5 au zaidi, hii ikimaanisha mzingo wa kiuno angalau ni nusu ya kimo cha mtu.
Kipimo kingine ni Body Volume Index, kinachopima kitambi kwa kupima umbo la mtu na mgawanyo wa uzito wake.
MAMBO YANAYO MUWEKA MTU KATIKA HATARI YA KUPATWA NA KITAMBI
Tumekwisha ona hapo juu jinsi kitambi kinavyo patikana na vyakula pamoja na sababu nyinginezo zinazo sababisha kutokea kwa kitambi, sasa tutazame mambo yatakayo kufanya uwe katika hatari ya kupatwa na kitambi.
Kwa mujibu wa tafiti mbalimbali za kitaalamu, mambo yafuatayo huwaweka watu katika hatari kubwa ya kupatwa na kitambi :
1. Ulaji mbovu wa chakula; Ulaji mbovu wa chakula ni ulaji usio zingatia kanuni za mlo kamili. Hapa mtu hufululiza kutumia chakula cha aina fulani pekee bila kuzingatia aina nyinginezo za chakula. Mfano; mtu anaweza kuwa anakula mlo ufuatao :
Asubuhi : Mchemsho ama supu ya ng’ombe , chapatti tatu na soda moja. Mchana : Ugali nyama choma anashushia kwa maji na soda.
Jioni : Mchemsho wa kuku na bia mbili nakuendelea.
Usiku : Chips mayai au chips kuku au chips mishikaki na bia.
Mtu huyu akiendelea na utaratibu huu kwa muda mrefu, ni lazima atapatwa na kitambi.
2. Ulaji mfululizo wa vyakula vyenye mafuta mengi
3. Ulaji mfululizo wa vyakula vyenye wanga mwingi
4.Ulaji mfululizo wa vyakula vyenye sukari iliyo ongezwa ( added sugar ).
5.Ulaji mfululizo wa vyakula vya ngano.
6.Ulaji mfululizo wa vinywaji vyenye ngano na sukari.
7.Kutofanya mazoezi ya mwili na viungo ( physical exercises ).
Mhusika anapokuwa katika makundi yote yali yotajwa hapo juu, hali huwa mbaya zaidi.
NJIA ZA KUONDOA KITAMBI
Kuwa na kitambi ni lugha ya mwili ( body-language ) inayo leta ujumbe kwako kwamba “ Mwili wako haupo salama tena “
Kama una kitambi maana yake una mafuta yasiyo hitajika mwilini, mwili wako unatumika kuhifadhi mafuta usiyo yahitaji.
Hali hii kitabibu imaanisha kwamba, ogani nyinginezo zilizomo ndani ya mwili wako zinao gelea kwenye mafuta( fats ) yasihotika yaliyomo ndani ya mwili wako, jambo linalo kuweka katika hatari kubwa sana ya kushambuliwa na magonjwa hatari kama vile shinikizo kubwa la damu, kiharusi na kisukari na kwa kutaja machache.
Hivyo basi ili kuondokana na hatari hiyo, yakupasa kupambana kuondoa hayo mafuta yasiyo hitajika mwilini mwako.
NJIA ZA KUONDOA KITAMBI.
Unaweza kuondokana na kitambi kwa kufanya diet pamoja na mazoezi ya mwili na viungo.
Vilevile unaweza kuondoa kitambi na kupunguza mafuta mwilini kwa kutumia dawa asilia ya kuondoa kitambi na kuondoa mafuta yasiyo hitajika mwilini.
DAWA ASILIA YA KUONDOA KIAMBI NA MAFUTA MWILINI.
Hii ni njia ya uhakika kabisa ya kuondoa tatizo la kitambi pamoja na mafuta yasiyo hitajika mwilini.
Unaweza kuondoa tatizo la kitambi pamoja na kupunguza mafuta mwilini kwa kutumia DAWA ASILIA IITWAYO YA MKATAA KITAMBI.
Dawa hii ni ya asili kabisa
“ Pure Herbal “, ambayo haijachanganywa na kemikali yoyote, haina side effect kwa mtumiaji na inaondoa kabisa tatizo la kitambi ndani ya siku kumi na nne.
JINSI DAWA YA MKATAA KITAMBI INAVYO FANYA KAZI.
1.Huyeyusha mafuta yasiyo hitajika mwilini.
2.Husaidia kupunguza hamu ya chakula.
3.Inazuia kutengenezwa kwa seli za mafuta ( fat cells ) katika mwili wa mwanadamu. Unapokula chakula chenye mafuta mengi, dawa hii asilia hupambana kuyafanya mafuta hayo yasitengeneze seli za mafuta mwilini mwako. Hali hii huuepusha mwili wako kuhifadhi mafuta yasiyo hitajika mwilini.
4. Husaidia kupunguza uzito wa mwili kwa haraka sana endapo itatumika pamoja na diet ya kabechi.
UFANISI WA DAWA.
Ufanisi wa dawa hii ni wa asilimia mia moja. Dozi ya dawa hii hutumika kwa muda wa siki ishirini na moja.
MATOKEO YA DAWA:
Dawa hii huondoa kabisa kitambi ndani ya siku kumi na nne.
BEI YA DAWA :
Dawa hii inaoatikana kwa kiasi cha SHILINGI ELFU HAMSINI TU (Tshs. 50,000/=)
MAHALI TUNAPO PATIKANA.
Tunapatikana jijini DAR ES SALAAM, katika eneo la UBUNGO karibu na SHULE MSINGI UBUNGO NATIONAL HOUSING nyuma ya jengo la UBUNGO PLAZA.
KWA WATEJA WASIO WEZA KUFIKA OFISINI KWETU.
Kwa wateja wasio weza kufika ofisini kwetu Tabata, tunao utaratibu wa kuwafikishia dawa mahali popote walipo ndani ya jiji la Dar Es salaam.
KWA WATEJA WA NJE YA DAR ES SALAAM.
Kwa wateja waliopo nje ya Dar Es salaam, tunawatumia dawa kwa njia ya MABASI.
Kwa wateja wa ZANZIBAR tunawatumia dawa kwa njia ya boti.
KWA WATEJA WA NJE YA NCHI:
Kwa wateja wa nje ya nchi, tunatumia dawa kwa njia ya POSTA au DHL.
WASILIANA NASI KWA SIMU NAMBA : 0766 53 83 84
TUTEMBELEE:
↧
Zitto Kabwe Ampinga Tundu Lissu.....Kasema Kuomba Nchi Ikatiwe Misaada ni UHAYAWANI
Mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Kabwe amekuja juu na kutoa ya moyoni akionekana kutofurahishwa na taarifa iliyosambaa kwenye vyombo mbalimbali vya habari ikiwemo mitandaoni ikitokea Chama cha demokrasia na maendeleo- CHADEMA.
Kauli za Zitto zilifuatia taarifa aliyoiona kwenye ukurasa wa Twitter iliyosema; “CHADEMA waitaka Jumuiya ya kimataifa kuinyima misaada Tanzania kutokana na ukiukwaji wa Demokrasia mfano, kukamatwa kwa viongozi wa upinzani”
Baada ya kuiona hiyo taarifa Zitto Kabwe aliandika “Huu ni uhayawani, hii ni nchi huru, kukaribisha wageni kuingilia mambo yetu ni upuuzi na umazwazwa, tupambane ndani kuleta demokrasia .NDANI”
Baada ya Zitto kuonyesha dhahiri msimamo wake, baadhi ya Followers wake kwenye Twitter walimuandikia kila mmoja na maoni yake na yeye akawajibu kama inavyoonekana hapa chini.
↧
↧
ADC Nao Wampinga Tundu Lissu
Chama cha Alliance For Democratic Change (ADC) wameitaka Chadema itoe msimamo wake kuhusu kauli ya mwanasheria wa chama hicho, Tundu Lissu kutaka jumuiya za kimataifa zisitishe misaada kwa Tanzania.
Katibu Mkuu wa ADC, Doyo Hassan amesema kama huo hautakuwa msimamo wa Chadema ,Lissu anapaswa kuomba radhi.
Amesema kauli ya kutaka misaada isitishwe hailengi kuwatakia mema Watanzania.
"Tunadhani matatizo yetu ya ndani ni vema tukapambana nayo kuliko kutangazia ugomvi wako kwa mtu asiyekuhusu.’’
"Kwa kauli hii hizi za Chadema ni wazi wameshindwa mapambano ya ndani na sasa wanafikiria njia nyingine ambazo ni hatari zaidi katika nchi yetu,"amesema Hassan.
Amesema kama Chadema imeshindwa kupambana na CCM na Serikali yake ni wazi wawaeleze wafuasi wao kuliko kutoa matamshi ambayo yanahatarisha ustawi wa taifa letu.
↧
Unasumbuliwa na Kiharusi,Ngiri au Kifafa?......Unatatizo la Nguvu za Kiume, Kuachika au Tatizo la Uzazi? . Kutana na Mtalaamu Huyu Akusaidie
SASA YUPO DAR; Anauwezo wa kutabiri nyota yako na kukuletea mafanikio makubwa katia biashara yako, kazini na malengo yako ya maisha.Pia anatoa pete ya bahati yenye uwezo wa kukuletea mafanikio makubwa na kutimiza ndoto zako.
Je, Umedhurumiwa? unamdai na hakulipi?...Njoo upatiwe dawa ulipwe haraka. Anadawa ya kumvuta mpenzi wako popote alipo kwa masaa 6 tu na kumtuliza asitoke kwako
Je, unaugomvi usioisha na mpenzi wako na unaachwa mara kwa mara? Njoo upate dawa ufurahie penzi tulivu la umpendae.
Anadawa za nguvu za kiume, kuimarisha mishipa iliyolegea, kuongeza homoni na kukufanya udumu katika tendo hadi dakika 45 na unaweza kurudia tendo hata mara 4 bila kuchoka.
Anatibu Busha bila kupasua,uzazi, mshipa wa ngiri,kiharusi,kifafa,kuondoa majini machafu nakadhalika.
Mpigie kwa simu: 0755505099
↧
Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota........Anatoa Mvuto wa Biashara, Kupandishwa Cheo, Kurudishiwa Mali Uliyoibiwa na Mengne
Kutana Maajabu ya Mtabibu CHIEF SULTAN(MAKATA WA MAKATANI) Mganga wa Waganga Sasa Yupo Mikoa Yote Tanzania
Pia anatoa Tiba kwa Njia ya Simu ukiwa popote Pale Tanzania au Nje ya Tanzania..
CHIEF SULTAN ni Mtabibu na Mtafiti wa Dawa za Asili ya Africa, na Duniani Katika utoaji wa Tiba za Asili..
Je unasumbulia na Mapenzi..?
(Umeachwa na Umpendae awe Mume/ Mke au mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine na Bado Unampenda?) Umejaribu sehemu Nyingi bila Mafanikio?Wasiliana na CHIEF SULTAN Akusaidie Kumshika Umpendae Asikusaliti(LIMBWATA) Kumtawala Mpenzi wako kwa sababu Maalum..Anauwezo wa Kusambalatisha Mahusiano yao ndani ya siku Moja tu.
Je Unasumbuliwa na Madeni?
Biashara yako Haina wateja?
Unatatizo la kutokushika Mimba na umehangaika sehemu nyingi bila mafanikio?
Wasiliana na CHIEF SULTAN Kwa Majibu ya Maswali yako..
Anasafisha NYOTA na Kutoa PETE za BAHATI kuendana na NYOTA yako. UTAJIRI USIO NA MASHARTI.(Magic Wallet_Pochi ya Maajabu Isio Isha Hela)
KUWA MAARUFU na KUJULIKANA
Kupandishwa CHEO na HESHIMA Mahala pa KAZI.
Utapewa Nguvu ya Kujilinda na MALI ZAKO zako na Mwili wako.. Huzuia Chuma Ulete katika Biashara.. Hurudisha MALI zilizo Potea au KUDHULUMIWA..
Mvuto wa Biashara na Mwili wako.
Hutibu kabisa Nguvu za Kiume na Kurefusha Uume kwa saizi Unayotaka.
Magonjwa Sugu(Miguu Kufa Ganzi, kisukari, Presha, Pumu nk.)Humaliza Kesi za Muda mrefu ndani ya siku 14 tu.
Anatoa NDAGU Zisizokuwa na Masharti.. Kwa maelezo Zaidi wasilina nae kwa
whatsapp +255 0658 316 976
Call +255 755 911 233
↧
Katibu Mkuu CHADEMA Dk Vincent Mashinji Apandishwa Kortini na Kisha Kurudishwa Rumande
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk Vincent Mashinji pamoja na viongozi watano wa chama hicho wakiwemo wabunge wawili, wamefikishwa katika Mahakama ya Mkoa wa Ruvuma, wakikabiliwa na makosa mawili ikiwemo kufanya mkusanyiko uliotishia usalama wa nchi.
Dk Mashinji alifikishwa mahakamani hapo jana na wanachama wengine watano wakiwa chini ya ulinzi mkali wa askari Polisi wa Kituo Kikuu cha Polisi Songea Mjini.
Walisomewa mashitaka mawili ya kufanya mkusanyiko usio halali na kufanya maandamano kinyume cha sheria, ambayo yanaweza kuhatarisha usalama wa nchi.
Akisoma mashitaka mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Mkoa wa Ruvuma, Simon Kobelo, Wakili Mfawidhi wa Serikali kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Kanda ya Songea, Renatus Mkude alidai Julai 15, mwaka huu mjini Mbamba Bay wilayani Nyasa, washitakiwa walikamatwa na Polisi wakiwa katika maandamano bila kuwa na kibali.
Aidha, Mkude alifafanua kuwa kosa lingine ni kufanya mkusanyiko kinyume cha sheria, hivyo kuhatarisha usalama wa nchi.
Katika kesi hiyo ya jinai namba 113 ya mwaka 2017, mbali na Dk Mashinji, washitakiwa wengine ni wabunge Zubeda Sakuro wa Viti Maalumu na Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Kusini Masasi na mbunge wa Ndanda kupitia chama hicho, Cecil Mwambe.
Wengine ni Katibu wa Ulinzi wa Taifa wa Chadema, Sanuda Madawa, Katibu Mwenezi Kanda ya Kusini Masasi, Charles Makunguru na Katibu wa Chadema Kanda ya Kusini Masasi, Filbert Ngatunga.
Washitakiwa baada ya kusomewa mashitaka yao, walikana kutenda makosa hayo.
Hata hivyo wakati wanasheria wa Chadema wakikamilisha taratibu ya dhamana, Jeshi la Polisi liliwachukua washitakiwa na kuwapandisha kwenye gari na kuwapeleka rumande hadi kesho, ambapo kesi hiyo itatajwa tena.
DK Mashinji na wanachama hao walikamatwa Julai 15, mwaka huu katika mji mdogo wa Mbamba Bay wilayani Nyasa na Jeshi la Polisi Wilaya ya Nyasa wakiwa katika maandamano na kufanya mkusanyiko kinyume cha sheria, licha ya serikali kuzuia mikutano yote vyama vya siasa.
Baada ya washitakiwa hao kushikiliwa na polisi wilayani Nyasa kwa saa 48, walipata dhamana kabla ya Jumanne na kupelekwa Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa mjini Songea, kabla ya jana kufikishwa mahakamani kujibu tuhuma hizo.
Upande wa utetezi ukiongozwa na Wakili Edson Mbogoro ulilalamikia kitendo cha wateja wao, kupelekwa mahabusu kwani hakimu tayari alishatoa ruhusa ya dhamana kwa washitakiwa, jambo ambalo alisema ni kinyume cha taratibu.
↧
↧
Lowassa Awasili Tena Polisi Kuhojiwa
Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa amewasili leo, Julai 20 saa mbili asubuhi makao makuu ya Jeshi la Polisi kwenye ofisi za Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Boaz.
Lowassa ameambatana na mkewe, Regina na mwanasheria wake, Peter Kibatala.
Hii ni mara ya nne kwa Lowassa kuripoti hapo akituhumiwa kutoa kauli za kichochezi wakati wa futari iliyoandaliwa Juni 23, na Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara.
Katika futari hiyo, Lowassa anadaiwa kutoa maneno ya uchochezi kuhusu masheikh wa Taasisi ya Uamsho wanaoshikiliwa gerezani akidai utaratibu wa kisheria ufanyike ili waachiwe huru.
Polisi wameimarisha ulinzi eneo hilo, huku Lowassa akiwa ndani tayari kwa kuhojiwa.
↧
NRM kubadili katiba ili Kumwongezea muda Rais Museveni
Chama tawala nchini Uganda cha National Resistence Movement (NRM) kimeapa kuhakikisha kwamba katiba ya nchi hiyo ina badilishwa ili kumruhusu Rais Yoweri Museveni kuitawala Uganda hadi mwisho wa umri wake.
Kwa mujibu wa taarifa iliyochapishwa leo katika mtandao wa Idhaa ya Kiswahili VOA inaeleza kuwa, NRM, imetangaza kutumia mbinu zote kuhakikisha kwamba katiba ya nchi inabadilishwa ili kumruhusu Rais Museveni kutawala hadi kifo chake. Hata hivyo Wanasiasa wa upinzani nao wameapa kuzima kila jaribio la kuifanyia katiba marekebisho.
Taarifa hiyo imeongeza kuwa, japokuwa Museveni amekaa kimya, viongozi wa NRM, wanasema wanasiasa wa upinzani wanamaliza muda wao kupinga nia ya chama tawala kuondoa ibara ya 102 B inayomzuia mtu yoyote aliyetimiza umri wa miaka 75 kuwania madaraka ya urais.
Viongozi hao wanaongozwa na mshauri wa Rais, David Mafabi ambaye amesema kuwa: “Hakuna wasiwasi kuhusu hilo. Tunataka katiba ibadilishwe na tunaieleza dunia ijue. wanaopinga wachunguze.
Kulingana na viongozi wa chama cha NRM, umri hauwezi kuwa kizuizi kwa kiongozi aliye na uwezo wa kuingoza nchi, na kwamba hakuna mtu yeyote nchini humo anayeweza kuwa rais isipokuwa Yoweri Kaguta Museveni.
Wanasiasa wa upinzani wakiongozwa na Dkt Kiiza Besigye wa FDC na Nobert Mao, kwa upande wao, wameendeleza kampeni ya kutaka raia kususia jaribio la serikali kuifanyia marekebisho katiba wakitishia kutumia mbinu zote kuzima hatua hiyo.
Katiba ya Uganda ilifanyiwa mabadiliko mnamo mwaka 2005 na kuondoa kizuizi cha mihula miwili, iliyomwezesha Museveni kuwania urais kwa mara nyingine. Museveni ameitawala Uganda tangu mwaka 1986.
Chanzo VOA Swahili
↧
Mkuu wa Polisi, Usalama Barabarani (RTO) Atumbuliwa
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, amelitaka Jeshi la Polisi kumuondoa katika nafasi ya Mkuu wa Polisi, Usalama Barabarani (RTO) Mkoa wa Pwani kutokana kwa kushindwa kusimamia sheria za usalama barabarani mkoani humo.
Masauni alitoa agizo hilo katika Kituo cha Mabasi cha mjini Kibaha Maili Moja baada ya kufanya ziara ya kushtukiza kituoni hapo jana, kwa ajili ya kufuatilia maelekezo yake aliyoyatoa alipofanya ziara kama hiyo mwaka jana.
“RTO ameshindwa kuendana na kasi ya awamu ya tano, nataka aondolewe katika nafasi hiyo na achukuliwe hatua ya kinidhamu, hatutaki uzembe, hatutaki kucheza na maisha ya watanzania,” alisema Masauni.
“Mwaka jana nilipofanya ziara kituoni hapa nilitoa maelekezo nilipokuta kuna mapungufu katika ukaguzi wa magari, tukakubaliana atayafanyia kazi haraka iwezekanavyo, lakini hakuna mabadiliko yoyote, magari hayakaguliwi, huku ni kuhatarisha usalama wa abiria.”
Aidha Masauni mara baada ya ukaguzi wa kituo hicho, aliendelea na ziara yake mkoani Pwani ambapo alifanya ukaguzi wa aina hiyo mjini Chalinze na baadaye Msata na kuimalizia ziara yake Bagamoyo.
↧
Mpenzi wa Diamond, Zari The Bosslady afiwa na mama yake mzazi
Mama mzazi wa Zari The Boss Lady ambaye ni mpenzi na mzazi mwenza wa mwimbaji wa Bongofleva Diamond Platnumz amefariki dunia asubuhi hii baada ya kuumwa..
Mrembo huyo wa Diamond amethibitisha taaifa hizo kupitia picha ya mama yake huyo aliyoiweka Instagram na kuandika, “It’s with deep sorrow that my family and I announce the death of our lovely mother who passed on this morning. May her soul rest in peace, May Allah forgive you your sins and grant you Jana.”
“You will forever be loved our Old Sun, us as your kids were given the best from God as our mother. We appreciate all you did for us. We will forever cherish you Mama.Sleep well😢,” ameongeza.
Huu ni msiba mkubwa wa pili kwa Zari kutokea mwaka huu baada ya takribani miezi miwili iliyopita alifiwa na mzazi mwenzake Ivan Ssemwanga.
↧
↧
Rais Magufuli Atua uwanja wa mpira wa Lemela kumsubiri Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza
Rais John Magufuli amewasili katika uwanja wa mpira wa Lemela Kata ya Kanazi Wilaya Ngara Mkoani Kagera ambapo atampokea Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza na baada ya hapo watakagua gwaride.
Mara baada ya kumaliza ukaguzi wa gwaride hilo viongozi hao watakuwa na maongezi maalum.
Rais Magufuli yuko ziarani Kanda ya ziwa na jana alizindua barabara ya kiwango cha lami ya Kagoma- Biharamulo-Lusahunga.
Pamoja na uzinduzi Rais Magufuli pia alihutubia wananchi ambako umati mkubwa umehudhuria uzinduzi wa barabara hiyo yenye urefu wa kilometa 154.
↧
Aliyeambiwa na Rais Magufuli astaafu apata mrithi wake
↧
Mbunge wa Jimbo la Temeke aswekwa rupango
Mbunge wa Temeke, Abdallah Mtolea yuko rumande tangu jana baada ya kukamatwa na Polisi akituhumiwa kuendesha gari ambalo bima yake ilikuwa imeisha muda.
Akithibitisha kukamatwa kwake leo Alhamis Julai 20, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Gilles Mrosso amesema mbunge huyo yuko rumande tangu jana jioni.
Amesema amekamatwa na askari wa usalama barabarani Temeke akiendesha gari ambalo bima yake ilikuwa imeisha muda wake.
“Askari wa usalama barabarani walipomhoji aliamua kuwapuuza na kuondoka zake,” amesema.
Amesema polisi walimfuatilia na kumkamata na sasa anaendelea kuhojiwa ili aweze kufikishwa mahakamani.
“Atafikishwa mahakamani kama tunavyofanya kwa raia yoyote, nafasi yake kama mbunge haiwezi kuwa sababu ya kutofuata sheria,” amesema.
↧
Wizara ya Mambo ya Ndani yakanusha upotoshaji unaohusu 'Kanuni/sheria za Wizara ya Ndani ya Nchi'
SERIKALI imesema itamchukulia hatua kali za kisheria mtu yeyote aliyesambaza taarifa za upotoshaji kwenye mitandao ya kijamii.
Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari Dar es Salaam jana na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasilino ya Serikali cha Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Christina Mwangosi, ilisema kumekuwapo na taarifa za uongo zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii zenye kichwa cha habari kinachosema “kanuni na sheria za Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi zitabadilishwa’.
Taarifa hizo, zimeanza zimeanza kusambazwa juzi zikidai kuanzia janana kuendelea kutakuwa kuna kanuni mpya za mawasiliano.
“Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, inapenda kuujulisha umma kuwa taarifa hii, ni ya uongo na uzushi,haina ukweli wowote na inalenga kuvuruga wananchi…tunaomba waipuuze.
“Wizara inatoa onyo kali kwa mtu yeyote aliyeanzisha na wale wanaoendelea kusambaza taarifa hii,hatua kali zitachukuliwa kwa watu wanaozusha mambo kwenye mitandao ya kijamii kwa kuwa Serikali inao mfumo rasmi wa utoaji wa taarifa kwa kutumia mfumo wa “kielectroniki na hardcopy,’’ ilisema taarifa hiyo.
↧
↧
Kubenea Aitwa Polisi Akidaiwa Kumtisha Profesa Lipumba
Mbunge wa jimbo Ubungo,(CHADEMA) Saed Kubenea ameitwa polisi na kutakiwa kuripoti leo tarehe 20/7/ 2017 kutoa maelezo kituo cha polisi kufuatia malalamiko aliyotoa Profesa Lipumba Mwenyekiti wa CUF anayetambuliwa na Msajili wa Vyama vya Siasa nchini.
Mbunge wa Ubungo Mh Saed Kubenea wiki iliyopita alifanya mkutano na vyombo vya habari kama Mwenyekiti wa Kanda ya Pwani akiwa pamoja na baadhi ya viongozi wa CUF iliyochini ya uongozi wa Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif na kutangaza oparesheni ya kumuondoa Profesa Lipumba katika ofisi za chama cha CUF Buguruni.
Baada ya Kubenea kutangaza oparesheni hiyo siku mbili mbele aliibuka Profesa Lipumba na kwenda kituo cha polisi kutoa malalamiko juu ya kile alichokisikia kutoka kwa kiongozi huyo na oparesheni hiyo aliyotangaza.
"Ni kweli Kubenea ameitwa na kuitwa kwake kumekuja baada ya wiki iliyopita kufanya mkutano na waandishi wa habari kama Makamu Mwenyekiti wa Kanda ya Pwani akiwa pamoja na viongozi wa CUF inayoongozwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi, Julius Mtatiro na Katibu Mkuu Maalim Seif na kutangaza operesheni inayoitwa 'Operesheni Ondoa Msaliti Buguruni (OMB). Operesheni hiyo itaendeshwa kwa ushirikiano wa vyama vinavyounda UKAWA" ilisema taarifa ya CHADEMA
Profesa Lipumba na baadhi ya viongozi wa CUF wapo katika mgogoro kutokana na kiongozi huyo kipindi cha uchaguzi mwaka 2015 kuandika barua ya kujiuzulu nafasi yake kama Mwenyekiti wa CUF taifa na kubaki mwanachama wa kawaida, lakini baada ya uchaguzi kupita kiongozi huyo akataka kubatilisha maamuzi yake ya kujiuzulu jambo ambalo viongozi wa CUF na baadhi ya wanachama wamekuwa wakilipinga na kukataa, japo Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi yeye bado anamtambua Lipumba kama Mwenyekiti wa CUF taifa.
↧
Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.
Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.
MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.
Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521
Tupo Mbagala
↧
Rais Magufuli Aagiza milioni 200 za mradi wa maji jeshini zitumike kwa wananchi
Rais John Magufuli ameagiza Sh200 milioni zilizopangwa kutumika katika mradi wa maji katika kambi ya jeshi zianze kuimarisha miradi ya maji kwa wananchi kwanza.
Akizungumza leo, Alhamisi Julai 20 katika ziara yake akiwa ameambatana na Rais wa Burundi, Pierre Nkurunzinza, Magufuli amesema amebaini kuwa pampu za maji wilayani Ngara zimeharibika kwa zaidi ya wiki tatu na kuwa wilaya hiyo ina uhaba mkubwa wa maji.
Alimuita, Mhandisi wa Maji ajieleze ni kwa nini pampu hizo hazifanyi kazi na baada ya kumsikiliza ndipo alipofanya uamuzi huo.
Akifafanua kuhusu hali ya maji, mhandisi huyo amesema awali visima vya maji wilayani hapo vilikuwa vikihudumia watu 400 lakini kwa sasa wilaya hiyo ina watu zaidi ya 240,000 na hivyo visima hivyo havitoshelezi.
“Tulikuwa tuna idadi ndogo ya watu sasa hivi imeongezeka, lakini tangu pampu iharibike, tumetengeneza mbili na kisima kimoja hakina pampu,” amesema.
Baada ya mhandisi huyo kufafanua hayo ndipo Rais alimuita Mkurugenzi wa Halmashauri kueleza mipango yake, ndipo Mkurugenzi huyo aliposema mradi wa maji wa Sh200 milioni utaanza kwanza katika kambi ya jeshi.
Kauli hiyo ndiyo iliyomfanya Rais Magufuli kushauri fedha hizo zitumike katika miradi ya maji katika makazi ya wananchi kwanza.
“Wanajeshi wapo 200 na wananchi wapo zaidi ya 20,000 sasa si bora waanze wananchi kwanza,” amesema.
↧
More Pages to Explore .....