Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

CHADEMA Yalia na Wahisani......Yataka Waungane Kuinyima Tanzania Misaada

$
0
0
Siku moja baada ya kuachiwa kwa dhamana viongozi wake, Chadema imetaka jumuiya ya kimataifa kuacha kuifadhili Tanzania, ikidai kuna ukiukwaji wa demokrasia na haki za binadamu.

Tamko hilo lilitolewa na mwanasheria wa Chadema, Tundu Lissu alipozungumza na waandishi wa habari jana kuhusu kuendelea kukamatwa kwa viongozi wa chama hicho, akiwemo Dk Vicent Mashinji, ambaye ni katibu mkuu aliyekamatwa Jumamosi akiwa Mbambabay wilayani Nyasa.

Wengine waliokamatwa ni Cecil Mwambe, ambaye ni mwenyekiti wa Kanda ya Kusini na mbunge wa Ndanda, Philbert Ngatunga (katibu wa kanda) na Manawa Samuda (ofisa wa operesheni na mafunzo).

Pamoja nao ni Zubeda Sakuru (mbunge wa viti maalum, Ruvuma), Asia Mohamed (ofisa wa kanda), Ireneus Ngwatura (mwenyekiti wa Mkoa wa Ruvuma), Delphin Ngaiza (katibu wa Mkoa wa Ruvuma), Cuthbert Ngwata (mwenyekiti wa Wilaya ya Nyasa) na Charles Makunguru (katibu wa uenezi wa Wilaya ya Nyasa).

Ilikuwa ni siku chache baada ya viongozi na wanachama 51 kukamatwa Julai 8 wakiwa kwenye kikao cha ndani wilayani Chato mkoani Geita.

Vitendo hivyo viliifanya Chadema itoe tamko zito jana.

“Nchi zinazoupa fedha uongozi wa Rais (John) Magufuli, hazina budi kuacha,” alisema Lissu akitoa mfano wa jinsi Afrika Kusini ilivyotengwa wakati wa siasa za ubaguzi.

“Hawatakiwi kupewa fedha ambazo zitakandamiza Watanzania, ambazo zitauza demokrasia.”

Lissu, ambaye anajulikana kwa kutumia maneno mazito, alito mifano mingi aliyodai inaonyesha kukandamizwa kwa demokrasia.

“Wao wanafanya mikutano ambayo sisi tumezuiwa, wanafanya mikutano ya ndani ambayo sisi tumezuiwa,” alisema Lissu, ambaye ni mbunge wa Singida Mashariki.

Lissu alisema sasa ni wakati wa kuacha woga na badala yake kupaza sauti kimataifa kupinga, kile alichoita ni ukandamizaji wa demokrasia ili wahisani wainyime misaada Serikali ya Tanzania.

Mwanasheria huyo alihoji kitendo cha majaji wa Mahakama Kuu kujiuzulu bila kujulikana sababu licha ya baadhi yao kuhusishwa na sakata la uchotwaji fedha kutoka Akaunti ya Tegeta Escrow iliyokuwa Benki Kuu (BoT).

Lissu pia alizungumzia matumizi ya Jeshi la Polisi akishauri lisiendelee kutumika kukamata wanasiasa wa upinzani ambao wanafanya mikutano na vikao vya ndani kwa kuzingatia sheria na Katiba, badala yake litumike kukamata wahalifu.

“Kila Polisi aliyenikamata anasema ‘bwana we tumeagizwa kutoka juu’. Sasa hili ni jeshi la maagizo au ni Jeshi la Polisi?” alihoji Lissu, ambaye amewahi kukamatwa mara kadhaa na kulala mahabusu.

Mwanasheria huyo wa kujitegemea alisema kupinga Serikali si dhambi na haijawahi kuwa dhambi wala kosa la jinai. Pia, alisema kama unatoa kauli kwa kuonyesha ubovu au kukosoa, si uchochezi.

Akijua kuwa alikuwa akitoa kauli kali dhidi ya Serikali, Lissu alisema anaamini waandishi wa habari hawataandika yote aliyosema kwa sababu wanaogopa sheria zilizopo, maonyo na vitisho.

Polepole: Lowassa Sio Tishio kwa CCM......Amechuja na Akigombea Tena 2020 Tutamshinda

$
0
0
Siku moja baada ya mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Edward Lowassa kusema atagombea tena urais katika uchaguzi ujao, CCM imesema inamsubiri na ina uhakika itamshinda tena kwa kuwa tayari ameshachuja na wala sio tishio.

Lowassa aliweka rekodi ya kuwa mgombea wa upinzani aliyepata kura nyingi baada ya kugombea kwa tiketi ya Chadema na kuungwa mkono na vyama vingine vitatu vya upinzani katika Uchaguzi Mkuu uliopita.

Alipata kura milioni 6.07, takriban mara tatu ya kura ambazo wapinzani wamekuwa wakipata katika chaguzinne za awali. Mshindi alikuwa John Magufuli wa CCM aliyepata kura milioni 8.8.

Waziri huyo mkuu wa zamani ametangaza nia ya kusimama tena kugombea urais wakati alipofanya mahojiano na waandishi wa Nation Media Group jijini Nairobi, Kenya ambako alikwenda kuhudhuria mazishi ya aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani, lakini CCM imesema asitarajie ushindi.

Alipoulizwa kuhusu tamko la Lowassa, katibu wa itikadi na uenezi wa CCM, Humphrey Polepole alisema mbunge huyo wa zamani wa Monduli si tishio na hayuko katika fikra za chama hicho.

“Katika orodha ya vitu muhimu, Lowassa hatumfikirii kabisa na si tishio hata kidogo,” alisema Polepole ambaye katika uchaguzi uliopita aliapa kuzunguka nchi nzima kumpinga Lowassa.

Polepole alisema kwa sasa chama hicho kimejikita kutekeleza Ilani yake inayotokana na ahadi za wananchi, kama kushughulikia changamoto za uadilifu kwa viongozi ndani ya CCM na Serikali.

“Tunatimiza wajibu wetu vizuri tuliotumwa na Watanzania na kazi inaonekana. Nje ya hapo tunasubiri Watanzania watupatie haki yetu katika uchaguzi ujao, na tumeshajipangia kupata ushindi wa zaidi ya asilimia 70, kwa hiyo hatumfikirii kabisa,” alisema Polepole.

Hata hivyo, jina la Lowassa limekuwa gumzo katika vikao vya chama hicho tawala na alisababisha wajumbe watatu wa Kamati Kuu ya CCM kuchukuliwa hatua, wenyeviti wanne wa mikoa kuvuliwa uongozi na uanachama na wengine kadhaa kuadhibiwa kwa njia tofauti.

Hiyo ilitokana na baadhi kuendelea kumuunga mkono baada ya kujivua uanachama wa CCM na kujiunga upinzani, akiwa Waziri Mkuu wa kwanza kufanya hivyo tangu siasa za ushindani zirejeshwe mwaka 1992.

Kubenea Amvaa Spika wa Bunge, Job Ndugai

$
0
0
Mbunge wa Jimbo la Ubungo, Saed Kubenea amesema kuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai hatoshi kuendelea na nafasi hiyo ya kuliongoza bunge kwani amekuwa akiwakandamiza wabunge wa Chadema.

Kubenea amemtuhumu Spika kuwa hafai kwa sababu pia alishawahi kupata kashfa ya kumpiga ndugu yake aliyekuwa mgombea mwenzake wa nafasi ya ubunge Jimbo la Kongwa Mkoani Dodoma.

Ameyasema hayo wakati wa mkutano wake wa hadhara na wapiga kura wake wa kata ya Manzese Wilaya ya Ubungo Jijini Dar es salaam, ambapo amesema kuwa Ndugai alifanya tukio hilo wakati wa kinyang’anyiro cha kura za maoni ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM).

“Simshangai Ndugai kwa sababu alimchapa ndugu yake, Mgogo mwenzake, leo amewafungia wabunge wa upinzani akiwemo mbunge jimbo la Kawe, Halima Mdee na Ester Bulaya kutoshiriki vikao vya Bunge,”amesema Kubenea.

Hata hivyo, amewataka wapiga kura wake kutoshangaa kwa kukaa kimya bila mradi katika Manispaa mpya ya Ubungo kwakuwa Manispaa hiyo bado mpya na kulikuwa mgawanyo wa miradi hiyo

Polisi Akatwa Mkono Katika Ugomvi wa Kugombea Mwanamke

$
0
0
Jeshi la Polisi katika Mkoa wa Kipolisi wa Tarime-Rorya, linawashikilia watu wawili wakazi wa Mtaa wa Nkende mjini Tarime wakidaiwa kumkata mkono Mkaguzi wa Polisi wa Kituo cha Ngamba Tana-River cha nchini Kenya, James Mnuve (50), wakati wakimgombania mwanamke.

Kamanda wa Polisi Tarime Rorya, SACP Henry Mwaibambe, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo la kukatwa mkono Mkaguzi huyo wa Polisi wa nchini Kenya. 

Mwaibambe alidai kuwa tukio hilo lilitokea Julai 13 mchana katika mtaa wa Nkende mjini Tarime ambapo vijana hao walitenda kosa hilo. 

Aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Michael Omahe, anayedaiwa kumtorosha mwanamke huyo, Anne Njeri, kutoka Kenya na kumleta Tanzania kisha kuishi naye kinyumba huku akisaidiana na rafiki yake, Daniel Onchiri.

“Mwanamke huyo (Njeri) anadaiwa alikuwa na uhusiano wa kimapenzi pia na askari James Mnuve na walikuwa wakiishi huko Tana River nchini Kenya, baada ya kuondoka, Julai 13 mchana askari huyo alimfuatilia kutoka Kenya hadi Mtaa wa Nkende, Tarime alipokuwa anaishi na kijana aliyemtorosha (Michael Omahe),” alisema Kamanda.

Akaongeza,“Alipofika Mtaa wa Nkende alimkuta Michael, pamoja na rafiki yake huyo wakiwa na mwanamke huyo na hapo ndipo ugomvi ulipoanza kwani askari James alitaka kuondoka na mwanamke huyo na zikazuka vurugu kubwa na kusababisha Mnuve kukatwa kwa kutumia panga.”

Aidha Kamanada huyo alisema kuwa,“Jeshi la Polisi tulifika kwenye eneo la tukio mapema na kuweza kuwakamata watuhumiwa wote watatu; Marandi, Ochiri na mwanamke huyo na kisha tukawahoji kabla ya kuwafikisha mahakamani huku majeruhi akiwa amepelekwa katika Hospitali ya Wilaya ya Tarime kwa matibabu.” 

Majeruhi James anadai kuwa yeye ni Inspekta wa Polisi wa Kituo cha Ngamba Tana River nchini Kenya na mwanamke huyo, Njeri Wanjoi, ni mke wake.

IGP Sirro afanya mabadiliko Jeshi la Polisi....... Muliro Aondolewa Shinyanga na Kupelekwa Kinondoni

$
0
0
Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Murilo Jumanne Murilo 
 
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Saimon Sirro,  amefanya mabadiliko ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni pamoja na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Shinyanga.

Katika mabadiliko hayo, aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni Kamishna  Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Suzan Salome Kaganda amekuwa Mkuu wa kitengo cha Mafao na Fidia  Makao Makuu ya Polisi, na nafasi yake inachukuliwa na Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Murilo Jumanne Murilo ambaye alikuwa kamanda Polisi Mkoa wa Shinyanga.

Aidha, Nafasi ya aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga imechukuliwa na Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Simon Sylverius Haule, ambaye alikuwa Afisa Mnadhimu  wa Polisi wa Mkoa wa Mara.

Uhamisho huo ni mabadiliko ya kawaida yanayotokea ndani ya  Jeshi la Polisi katika kuongeza ufanisi wa utendaji kazi.

Imetolewa na:
Barnabus D. Mwakalukwa - ACP
Msemaji wa Jeshi la Polisi.
Makao Makuu ya Polisi.

Serikali Yaendelea Kujipanga Vizuri.......Watumishi Wote wa Umma sasa Kupokea Mishahara Kwa Wakati Mmoja

$
0
0
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala Bora), Angellah Kairuki, amesema katika mwaka huu mpya wa fedha watumishi wa umma watakuwa wanalipwa mishahara kwa wakati mmoja ili kupunguza matatizo ya mishahara yanayojitokeza.

Kairuki ametoa kauli hiyo leo Jumanne, Julai 18 wakati akizungumza na watumishi wa wilaya mpya ya Ubungo ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake aliyoianza jana katika halmashauri hiyo.

Amesema awali watumishi hao walikuwa wanapata mishahara yao kwa nyakati tofauti lakini sasa wataingizia mishahara yao moja kwa moja katika akaunti ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) badala ya kupitia benki za biashara.

"Hatutaki itokee huyu amewekewa mshahara tarehe 27, huku mwingine akienda kuangalia salio katika akaunti anaambiwa bado lakini sasa hivi itakuwa wakati mmoja," amesema Kairuki huku akishangaliwa na watumishi wa halmashauri hiyo.

Alisisitiza lengo la kuweka mfumo huo ni kuhakikisha watumishi wote wanapata mshahara wao wakati mmoja na hiyo itasaidia Serikali kusimamia kwa umakini mishahara.

Amefafanua kwamba siku tatu kabla mshahara haujaingizwa katika akaunti ya mtumishi, mwajiri sekta husika atapelekewa orodha ya watumishi watakaotakiwa kulipwa mishahara.

"Matumaini yangu waajiri watakuwa makini kuangalia orodha hizo ili isitokee hata mtumishi mmoja akaachwa," anasema Kairuki.

Serikali Yamjibu Tundu Lissu....Yadai ni Muongo, Mpotoshaji

Kutana na Mtaalamu wa Kusafisha Nyota........Anatoa Mvuto wa Biashara, Kupandishwa Cheo, Kurudishiwa Mali Uliyoibiwa na Mengne

$
0
0
Kutana Maajabu ya Mtabibu CHIEF SULTAN(MAKATA WA MAKATANI) Mganga wa Waganga Sasa Yupo Mikoa Yote Tanzania

Pia anatoa Tiba kwa Njia ya Simu ukiwa popote Pale Tanzania au Nje ya Tanzania..

CHIEF SULTAN ni Mtabibu na Mtafiti wa Dawa za Asili ya Africa, na Duniani Katika utoaji wa Tiba za Asili..
 
Je unasumbulia na Mapenzi..?
(Umeachwa na Umpendae awe Mume/ Mke au mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine na Bado Unampenda?) Umejaribu sehemu Nyingi bila Mafanikio?Wasiliana na CHIEF SULTAN Akusaidie Kumshika Umpendae Asikusaliti(LIMBWATA) Kumtawala Mpenzi wako kwa sababu Maalum..Anauwezo wa Kusambalatisha Mahusiano yao ndani ya siku Moja tu.
Je Unasumbuliwa na Madeni?
Biashara yako Haina wateja?
Unatatizo la kutokushika Mimba na umehangaika sehemu nyingi bila mafanikio?
 
Wasiliana na CHIEF SULTAN Kwa Majibu ya Maswali yako..
Anasafisha NYOTA na Kutoa PETE za BAHATI kuendana na NYOTA yako. UTAJIRI USIO NA MASHARTI.(Magic Wallet_Pochi ya Maajabu Isio Isha Hela)
KUWA MAARUFU na KUJULIKANA
Kupandishwa CHEO na HESHIMA Mahala pa KAZI.
Utapewa Nguvu ya Kujilinda na MALI ZAKO zako na Mwili wako.. Huzuia Chuma Ulete katika Biashara.. Hurudisha MALI zilizo Potea au KUDHULUMIWA..
Mvuto wa Biashara na Mwili wako.
Hutibu kabisa Nguvu za Kiume na Kurefusha Uume kwa saizi Unayotaka.
 
Magonjwa Sugu(Miguu Kufa Ganzi, kisukari, Presha, Pumu nk.)Humaliza Kesi za Muda mrefu ndani ya siku 14 tu.
Anatoa NDAGU Zisizokuwa na Masharti.. Kwa maelezo Zaidi wasilina nae kwa

whatsapp +255 0658 316 976
Call +255 755 911 233

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya July 19

Efatha Ministry Ruvuma: Huduma Zetu Pamoja na Raitiba za Ibada......Nyote Mnakaribishwa

$
0
0
EFATHA MINISTRY RUVUMA
EFATHA maana yake ni Funguka[MARKO 7:34], Efatha ni huduma iliyo chini ya Mtume na Nabii JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA,Huduma ilianzishwa mwaka 1997.

Huduma ya Efatha mkoa wa Ruvuma inaongozwa na Mchungaji kiongozi PHILIPO JAMES GUNI, Katika Mkoa wa Ruvuma Huduma ya Efatha inapatikana Songea eneo la Mkuzo na Wilaya zote za Mkoa wa Ruvuma.
 
Huduma ya Efatha Ruvuma chini ya Mchungaji kiongozi PHILIPO JAMES GUNI,Tunatoa Huduma ya Uponyaji na Ukombozi kwa damu ya Yesu, Uponyaji na Ukombozi katika Magonjwa,Kipato, Kazi, Mazingira, Utasa, Ugumba, Uchumi ulioyumba, Umaskini, Ndoa, Kuachwa, Kuachika, Kukataliwa na mengine yote yaliyoshindikana, Huduma inatolewa bureee kwa damu ya YESU.
 
RATIBA ZETU ZA IBADA NI KAMA IFUATAVYO:
1.JUMATATU-IJUMAA –NI USHAURI NA MAOMBEZ, I Muda wote
2.JUMAMOSI-IBADA YA MAOMBI, kuanzia saa 3:00 asubuhi-saa 6;00 mchana
3.JUMAPILI-IBADA KWA WATU WOTE, kuanzia saa 4:00 asubuhi- saa 8:00 mchana

Tunapatikana SONGEA-MKUZO, Kufika panda magari yaendayo MKUZO/MWENGEMSHINDO yanayopaki stendi kuu ya daladala Songea, shuka kituo kinachoitwa EFATHA uliza kanisa lililopo sio mbali kutoka barabarani.
 
Unaweza kutupata kupitia mitandao ya kijamii kama
Facebook @efatharuvuma
Instagram @efathaministryruvuma
Youtube Efatha Songea
na Wasiliana nasi kwa
Simu no. 0625 85 99 90, na 0714 21 49 36,
Barua pepe ruvuma@efathaministry.org
 
KARIBU KATIKA ZIARA YA KITUME NA KINABII

BAKWATA wataka anayejiitwa Mtume akamatwe

$
0
0
Baraza la ulamaa limetoa wito kwa vyombo vya dola kumchukulia hatua stahiki mtu aliyejitokeza katika Mkoa wa Pwani na kudai yeye ni Mtume.

Akizungumza  jana na waandishi wa habari kwa niaba ya Mufti wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeir Ally,  Mwenyekiti wa Halmashauri Kuu Bakwata, Sheikh Hamisi Said Mataka alisema, anachodai mtu  huyo anayefahamika kwa jina la Hamza Issa kuwa yeye ni Mtume  ni kitu ambacho hakipo kabisa katika mafundisho ya kiislamu.

Alisema kauli ya Issa kudai yeye ni mtume na kisha  kwamba ni muislamu na kutumia maandiko ya uislamu ni upotoshaji mkubwa ambao ukiachwa bila kudhibitiwa ni kuruhusu fujo na uvunjifu wa amani.

“Kwa mujibu wa maelezo yaliyoenea katika mitandao ya kijamii na ya kutoka baraza za Masheikh wa Mkoa wa Pwani chini ya kiongozi wake Sheikh na Qadhi wa Mkoa wa Pwani, amedai kuwa yeye ni Nabii Ilyasa kwa maana ya kwamba roho ya Nabii Ilyasa imemuingia yeye Hamza Issa na kwa hiyo yeye wamekuwa Nabii Ilyasa” alisema Sheikh

Aliongeza maelekezo na mafundisho ya uislamu yako wazi kuwa hakuna Mtume mwingine katika Uislamu baada ya Mtume Muhammad (S.A.W) na kwamba upatikanaji wa MTU ndani ya uislamu na kudai kuwa yeye ni Mtume ni kutaka kuamsha hisia Kali za waislamu nchini.

“Baraza la Ulamaa linapenda kuwafahamisha waislamu kwamba, yeyote atakayemfuata mpotoshaji huyu atakuwa ametoka ndani ya uislamu” alisema Sheikh Mataka.

Pia Baraza limetoa wito kwa Masheikh wa Mikoa, Wilaya na viongozi wa taasisi mbali mbali za Kiislam kutotoa fursa ya aina yoyote kwa huyo anayejiita Nabii ( Hamza Issa), ili kuzuia kuipotosha jamii.

DC Amuweka Ndani Dk Mary Nagu (Mbunge wa Hanang -CCM )

$
0
0
Mbunge wa Hanang (CCM), Dk Mary Nagu  jana alishikiliwa kwa muda polisi baada ya kutokea vurugu katika kikao cha kamati ya siasa ya chama hicho.

Dk Nagu aliyewahi kuwa waziri katika wizara kadhaa wakati wa utawala wa Serikali za awamu mbili zilizopita, alishikiliwa kwa muda  na kuachiwa baada ya kuhojiwa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara, Francis Masawe alisema Dk Nagu alifikishwa kituoni kutokana na vurugu zilizoibuka kwenye kikao cha kamati ya siasa ya CCM Wilaya ya Hanang baada ya makundi mawili kujitokeza.

Masawe alisema baada ya mahojiano kufanyika na kuandika maelezo, kwa kuwa mgogoro huo ulikuwa ni mambo ya ndani ya CCM walimwachia.

"Taarifa ambazo nimepata ameachiwa baada ya kuandika maelezo na tayari walifikia makubaliano wenyewe," alisema.

Awali, mkuu wa wilaya hiyo, ambaye pia ni mjumbe wa kamati ya siasa ya wilaya, Sara Msafiri alisema: "Ni kweli amekamatwa lakini nipo kwenye kikao siwezi kuzungumza.”

Habari kutoka ndani ya kikao hicho, zimeeleza Dk Nagu alikamatwa kutokana na malumbano ya kupitisha wagombea wa uchaguzi ndani ya CCM.

UVCCM: Magufuli Ametupunguzia Kazi 2020

$
0
0
Umoja  wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), umesema kuwa kazi kubwa inayofanywa kwa sasa na Rais Dk. John Magufuli, imeipunguzia kazi CCM katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020.

Kwamba Watanzania wamekuwa wakivutiwa na utendaji kazi wa kiongozi huyo wa nchi ikiwamo kusimamia rasilimali za nchi.

Kauli hiyo imetolewa jana wilayani Uvinza mkoani hapa na Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM, Shaka Hamdu Shaka, alipokuwa akizungumza na wana-CCM kwenye mkutano wa ndani uliofanyika katika kata za Kazuramimba na Nguruka.

Alisema kwa sasa njia imekuwa nyeupe kuelekea mwaka 2020 kwani kazi kubwa inayofanywa na Rais Magufuli ni kielelezo tosha kwa kiongozi huyo kuwa anastahili kupewa nchi na kuongoza kwa awamu ya pili.

Shaka aliwataka wanachama wa CCM kutobweteka na uhakika huo na badala yake wajitume kwa bidii, kufanya kazi ya kisiasa kisayansi na kizalendo kama njia ya kuwatumikia Watanzania wote.

“Utendaji wa Serikali ya Rais Dk. John Magufuli katika kipindi kifupi, kwa hakika umewakosha Watanzania pamoja na kuitikisa dunia na kwa sasa wanyonge nao wanajiona wana thamani na hadhi katika nchi yao.

“Dk. Magufuli ametupunguzia hekaheka na kazi nzito ya kusaka kura za ushindi wa mwaka 2020, hata viongozi na wanachama wa CCM tusibweteke na kujiamini, wajibu wetu ni kufanya kazi na kuwatumikia wananchi,” alisema.

Aidha Shaka alivichambua vyama vya upinzani na kusema vingine ni mabaki ya ukoloni mamboleo katika ardhi ya Tanzania.

Alisema vyama hivyo vimekuwa vikiongozwa na wanasiasa uchwara waliojitahidi kwa miaka mingi kuvipinga vyama vya TANU, ASP na Serikali baada ya Uhuru wa Tanganyika mwaka 1961 na Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964.

Shaka alisema kwa sasa upinzani uliokuwapo nchini hauna lolote zaidi ya kupoteza muda kutokana na vyama hivyo kurithi sera na mipango ileile ya wakoloni na Sultan kwa kuwagawa wananchi.

Unasumbuliwa na Kiharusi,Ngiri au Kifafa?......Unatatizo la Nguvu za Kiume, Kuachika au Tatizo la Uzazi? . Kutana na Mtalaamu Huyu Akusaidie

$
0
0
SASA YUPO DAR; Anauwezo wa kutabiri nyota yako na kukuletea mafanikio makubwa katia biashara yako, kazini na malengo yako ya maisha.Pia anatoa pete ya bahati yenye uwezo wa kukuletea mafanikio makubwa na kutimiza ndoto zako.

Je, Umedhurumiwa? unamdai na hakulipi?...Njoo upatiwe dawa ulipwe haraka. Anadawa ya kumvuta mpenzi wako popote alipo kwa masaa 6 tu na kumtuliza asitoke kwako

Je, unaugomvi usioisha na mpenzi wako na unaachwa mara kwa mara? Njoo upate dawa ufurahie penzi tulivu la umpendae.

Anadawa za nguvu za kiume, kuimarisha mishipa iliyolegea, kuongeza homoni na kukufanya udumu katika tendo hadi dakika 45 na unaweza kurudia tendo hata mara 4 bila kuchoka.

Anatibu Busha bila kupasua,uzazi, mshipa wa ngiri,kiharusi,kifafa,kuondoa majini machafu nakadhalika.

Mpigie kwa simu: 0755505099

Mghwira amvaa Lowassa, asema kuhama chama ni ufisadi wa kisiasa

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira amesema kuwa njia aliyoitumia aliyekuwa mgombea kiti cha urais katika uchaguzi mkuu uliopita kupitia Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Edward Lowassa ilikuwa ni aina fulani ya ufisadi wa kisiasa.

Ameyasema hayo mwishoni mwa wiki wakati akifanya mahojiano na Gazeti la Mwananchi ambapo amesema kuwa Mjumbe huyo wa Kamati Kuu ya Chadema njia aliyoitumia ilikuwa ni aina mojawapo ya ufisadi kwakuwa hakupitishwa na chombo chochote ndani ya chama chake.

Amesema kuwa hata katika Kampeni za uchaguzi mkuu, Ukawa haikuzungumzia suala la ufisadi kwakuwa kiongozi huyo teyari alikuwa ameshajiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

“Kwenye Kampeni za mwaka 2015 chama kikuu cha upinzani (Chadema) hakikuwa tena kinazungumzia suala la ufisadi, labda kwa hofu kuwa mshtumiwa wa ufisadi alikuwa mgombea wao, kwa bahati mbaya wao ndio waliibua tuhuma za ufisadi, lakini kuondoka kwa Dkt. Slaa nako kulikuwa ni tatizo, ingawa watu hawakutaka kulifuatilia,” amesema Mghwira.

Aidha, Mghwira amesema kuwa watu walitakiwa kuhoji sababu za kuondoka kwa Dkt. Slaa na alikoelekea, nakuongeza kuwa ni ajabu kwa kiongozi anayepigania demokrasia anaingia kwenye chama na kugombea nafasi ya urais bila kupitishwa chombo chochote.

Hata hivyo, Mghwira ambaye ni kiongozi wa kwanza wa upinzani kushika wadhifa wa ukuu wa mkoa tangu kurejea kwa mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, amesema kuwa njia waliyotumia Chadema si tu inarudisha nyuma siasa za upinzani, bali haikutoa picha nzuri ya demokrasia ndani ya upinzani.

Alikerwa kuvuliwa uenyekiti
Katika mahojiano hayo yaliyofanyika nyumbani kwake Shanty Town mjini Moshi, Mghwira alikumbuka karaha aliyoipata baada ya furaha ya kuaminiwa na Rais na kupewa wadhifa huo.

Alisema kama si ubabaishaji wa kisiasa Tanzania, asingeondolewa kwenye uenyekiti wa ACT-Wazalendo.

“Changamoto niliyokutana nayo ACT-Wazalendo kama mwenyekiti ni kukosa wigo sahihi wa kisiasa kwa sababu kama tungekuwa tunafanya siasa sahihi, nisingeondolewa uenyekiti,” alisema.

Mghwira alisema, “Naapishwa tu kuwa RC (mkuu wa mkoa) kesho yake naondolewa tena tukiwa tumepanga kukutana kwenye kikao na mpaka leo hatujawahi kukutana.

“Nimesoma kwenye magazeti kuwa mrithi wa Mghwira kutembelea mikoa saba, yaani na mrithi ameshapatikana. Hizo si siasa, huo ni ubabaishaji. Ubabaishaji wa kisiasa Tanzania ni tatizo,” alisema.

Aliongeza, “Sisi kina mama tukisimama imara tunaweza kuondoa dhana hii ya siasa za ubabaishaji. Ni siasa za kipuuzi kabisa. Mmekubaliana mkutane muongee, hamuongei wenzako wanakaa pembeni. Umechaguliwa na mkutano mkuu unaondolewa na kamati ndogo. Watu 370 karibu 400 hivi walikuchagua, siku ya kuondolewa unaondolewa na watu watatu au wawili au mmoja. Hiyo si siasa ni dalili tosha kuwa hakuna siasa.”

Alisema mbaya zaidi ni kuwa watu wanaokuondoa hawakutumwa na mkutano mkuu, wala hawakukaimishwa na kamati kuu.

Hakuna upinzani nchini
Baada ya kujumuisha yote hayo na hasa alivyotimuliwa kwenye uongozi, mkuu huyo wa mkoa akawa na jibu moja kuhusu siasa za upinzani, “Hakuna siasa za upinzani, bali zilizopo ni za kurudishana nyuma maendeleo.

“Siasa ni kitu kizuri kwa maana ya ile mijadala, kubadilishana mawazo na kuzungumzia masuala ya itikadi, mipango ya kijamii... hakuna hiki kitu Tanzania.”

Badala yake alisema, “Tumeweka siasa kama ni uhasama kati ya chama tawala kilichoshinda kihalali na vyama hivi vingine. Kila siku watu wanatafuta makosa ya wenzao (Serikali) hata kama inafanya vizuri. Hiyo sio siasa.

“Vyama vya upinzani hapa hatuendeshi siasa. Awali, chama chochote kitakachoibuka na siasa inayoeleweka kinaweza kutawala nchi hii kwa miaka 100 ilimradi tu kitoke na siasa inayoeleweka.”

Mghwira alisema,“Vikitokea vyama vitatu vinaendesha siasa inayoeleweka tunakuwa mahali pazuri zaidi. Kwa maana kwamba wale wakiongea jambo lao, hata kama hawatawali, mtawala asikie na kuthamini.

“Sisi hapa Tanzania kuna aina ya siasa za kudidimizana. Kwa sisi wanawake wanaharakati tunaziita PhD (pool her down). Unavutwa tu chini hutakiwi kukua. Nchi haiwezi kwenda kwa staili hii.”


Alisisitiza,“Kuna watu wanafikiri kwamba ili kitu kiwe sahihi ni lazima wao wakifanye (upinzani) lakini kikifanywa na watu wengine hakiko sahihi. Hiyo ni kutokuwa mwanasiasa. Kuwa mwanasiasa si kugombana ni kuwa na uwezo wa kujenga hoja, kuitetea na kuisimamia. Mwenzako akija na hoja kubwa zaidi kubali.”

TANZIA: Jaji Mstaafu wa mahakama Kuu, Upendo Msuya afariki dunia

$
0
0
Aliyekuwa Jaji wa Mahakama Kuu ambaye amejiuzulu  hivi karibuni, Upendo Msuya amefariki leo Julai 19 baada ya kuugua kwa muda mrefu ugonjwa wa kiharusi.

Mjomba wa marehemu, Niva Mbaga amethibitisha tarifa hizi na kusema kwamba marehemu amefariki akiwa Hospitali ya Kairuki alipokuwa amelazwa.

Amesema kwamba shughuli za mazishi zinafanyika nyumbani kwa marehemu Tegeta jijini Dar es Salaam.

“Amesumbuliwa kwa muda mrefu na ugonjwa wa kiharusi hivyo akawa anapelekwa hospitali na kurudi nyumbani zaidi ya miezi mitatu sasa na leo hii amefariki dunia’’ amesema Mbaga

Amesema marehemu ameacha watoto wanne.

Rais Magufuli Afungua Barabara ya Kagoma-Biharamulo-Lusahunga yenye urefu wa Kilometa 154

$
0
0
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa amesema Barabara ya Kagoma-Biharamulo-Lusahunga imegharimu Sh 190 bilioni.

Waziri Mbarawa ametoa tamko hilo leo wakati wa uzinduzi wa barabara hiyo mbele ya umati mkubwa wa watu ambao wamehudhuria uzinduzi wa barabara hiyo ya  kiwango cha lami yenye urefu wa kilometa 154.

Akizindua ujenzi wa barabara hiyo leo Rais John Magufuli amesema kwamba Biharamulo imeshika nafasi ya pili kwa umasikini na wananchi wanafanya ulinganisho na hali ilivyo tofauti katika wilaya jirani ya Chato.

Kwa upande wake Mbunge wa Biharamulo, Oscar Mukasa amesema wanaunga mkono msimamo wa Rais kupiga marufuku wanafunzi wanaobeba mimba kuendelea na masomo na wameanzisha shule ya wasichana ya bweni kuunga mkono kauli yake.

Muuguzi Aliyemchoma Sindano na Kumbaka Ndugu wa Mgonjwa Asimamishwa Kazi

$
0
0

Muuguzi wa Kituo cha Afya Kata ya Igurubi Wilaya ya Igunga mkoani Tabora, Damian Samson Mguya (26) amesimamishwa kazi na kufutiwa leseni yake ya uuguzi kwa tuhuma za kumbaka ndugu wa mgonjwa baada ya kumuwekea dawa za kulevya.

Kufuatia kitendo hicho Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imelaani kitendo ambacho muuguzi huyo amekifanya na kutaka leseni ya muuguzi huyo kusitishwa mara moja kwa kukiuka taratibu na kanuni za uuguzi.

Aidha msemaji wa Idara Kuu ya Afya, Nsachris Mwamwaja amewataka watumishi wote wa sekta ya afya nchini kuhakikisha wanafuata kanuni, utaratibu na maadili ya taaluma zao muda wote na siku zote. 

Muuguzi Damian Mguya anashikiliwa na polisi kwa tuhuma ya kumbaka binti wa miaka 18 mkazi wa Kijiji cha Mwagala, ambaye aliongozana na mgonjwa kwenda katika kituo hicho cha afya, upelelezi wa tukio hilo utakapokamilika muuguzi huyo atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma hizo. 

Rais Magufuli Atoa Siku 14 kwa Wamiliki wa Vituo vyote vya mafuta nchini

$
0
0
Rais John Magufuli ametoa siku 14 kwa wamiliki wa vituo vyote vya mafuta nchini, kuhakikisha wanaweka na kutumia mashine za kielektroniki za kutolea risiti (EFD) na atakayekiuka agizo hilo atafutiwa leseni ya biashara yake.

Rais Magufuli ametoa agizo hilo wakati wa ufunguzi wa barabara ya Kigoma-Biharamulo-Lusahunga yenye urefu wa KM 154 huku akiwataka mawaziri wenye dhamana kuhakikisha wanafuatilia maagizo hayo kuanzia sasa.

"Wanaolalamika kukosa mafuta waendelee kufanya hivyo, ni mara mia tukose mafuta kuliko kuwa na wafanyabiashara wanaokwepa kodi", amesema Rais Magufuli.

Kwa upande mwingine, Rais Magufuli amepiga marufuku wananchi kutozwa kodi kwa mzigo wenye uzito wa tani moja anapousafirisha kutoka wilaya moja kwenda nyingine.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live


Latest Images