Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Walioghushi vyeti kuchukuliwa hatua za kinidhamu

$
0
0
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angellah Kairuki amesema watumishi wa umma walioghushi vyeti watachukuliwa hatua za kinidhamu.

Kairuki amesema hayo  jana (Julai 11) katika kikao kazi na watumishi na viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Temeke, Tarafa ya Mbagala.

Alisema wote walioghushi vyeti hawapo kazini na wameshafutwa katika orodha ya malipo ya Serikali.

Waziri alielekeza waajiri kuwafuta wote wasiostahili kuwepo katika orodha ya malipo na wasimsubiri hadi afike katika maeneo yao ya kazi ili kutekeleza agizo hilo.

“Baada ya uhakiki kukamilika, hatua za kinidhamu zitachukuliwa kwa walioghushi vyeti kwa kuzingatia sheria, kanuni, utaratibu na miongozo iliyopo katika utumishi wa umma,” alisema Kairuki kama alivyokaririwa katika taarifa iliyotolewa na wizara.

Aliwataka waajiri kuhakikisha wanahakiki taarifa za watumishi wapya wanapoajiriwa na wale wanaohamia ili kujiridhisha kama wana vyeti safi.

“Ni wajibu wa kila mwajiri kuhakikisha kuwa vyeti vya kila mwajiriwa mpya vinathibitishwa na mamlaka husika kabla ya kumwajiri na hatimaye kumuingiza kwenye orodha za malipo ya mshahara kupitia mfumo wa HCMIS na mifumo mingine ya mishahara ya kitaasisi,” alisema.

Akizungumzia watumishi wa umma walioajiriwa na sifa za darasa la saba, Kairuki alisema endapo aliajiriwa kabla ya Mei 20 mwaka 2004 anastahili kuendelea kuwa katika utumishi wa umma na endapo kajiendeleza abadilishiwe muundo kuendana na sifa za elimu aliyopata.

Alisema endapo mtumishi huyo aliajiriwa baada ya Mei 20 mwaka 2004 anatakiwa kuwa na sifa ya elimu ya kidato cha nne.

Kairuki pia alitoa ufafanuzi wa kazi inayoendelea inayohusu kuoanisha taarifa za watumishi na zile za usajili uliofanywa na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida).

“Uhakiki huu utaongeza usahihi wa taarifa za watumishi nchini, kudhibiti watumishi hewa, udanganyifu wa taarifa zinazomhusu mtumishi na kutekeleza azma ya Serikali ya kuunganisha mifumo ya kimkakati ya Tehama ili ibadilishane taarifa,” alisema.

Katibu Tawala Mkoa wa Dar e Salaam, Theresia Mbando alimpongeza Waziri Kairuki kwa kuboresha utumishi wa umma.

Mbando alisema sasa watumishi wa umma waliobaki kazini wameweza kuziba pengo la waliobainika kuwa na vyeti vya kughushi na kuondolewa kazini.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Atembelea Ujenzi Wa Daraja Mto Lukuledi ......Asema Watu Wengi Wamekufa Wakikatiza Katika Eneo Hilo

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametembelea mradi wa ujenzi wa daraja la mto Lukuledi lenye urefu wa kilomita 30.45 linalounganisha mikoa ya Lindi na Mtwara na na kusema kwamba ameridhishwa na maendeleo ya ujenzi wake.

Amesema ujenzi wa daraja hilo unatakaogharimu sh. bilioni 5.4 ni mkombozi kwa wananchi wa mikoa hiyo hasa wa wilaya za Ruangwa na Masasi ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakishirikiana katika masuala mbalimbali yakiwemo kilimo na huduma za kijamii.

Waziri Mkuu amesema hayo jana (Jumanne, Julai 11, 2017) alipotembelea mradi huo wa ujenzi wa daraja hilo katika kijiji cha Nandanga alipowasili wilayani Ruangwa akiwa katika siku ya pili ya ziara yake ya kikazi ya siku nne Mkoani Lindi.

“Watu wengi wamepoteza maisha kwa kuliwa na mamba walipokuwa wakikatiza katika eneo hilo. Ujenzi wa daraja hili ni muhimu, watu wengi wa Ruangwa wanavuka kufuata matibabu katika hospitali ya Ndanda, wilayani Masasi na wakazi wa Ndanda wanavuka kufanya shughuli za kilimo wilayani Ruangwa.”

Pia Waziri Mkuu aliwaomba wananchi wa maeneo hayo kuhakikisha wanatoa ushirikiano kwa mkandarasi anayejenga daraja hilo ili aweze kutekeleza majukumu yake ipasavyo na kumaliza mradi huo kwa wakati.

Kwa upande wake Mbunge wa jimbo la Ndanda, Mheshimiwa Cecil Mwambe ameipongeza na kuishukuru Serikali kwa jitihada zake za kuwaletea wananchi maendele0 na kubadilisha maisha yao.

Alisema mradi wa ujenzi wa daraja hilo ni faraja kwa wananchi wa mikoa hiyo kwa kuwa eneo hilo ni makazi ya mamba, hivyo kukamilika kwake kutaokoa maisha ya watu pamoja na kurahisisha usafiri wa watu na bidhaa.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu alisema changamoto ya upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama katika vijiji vya Litama, Luchelegwa, Nandanga, Ipingo na Chiapi kuwa historia baada kuungwanishwa na mradi wa maji wa Mbwinji.

Aliyasema hayo leo wakati akizungumza kwa nyakati tofauti na wananchi wa vijiji vya Litama, Chiapi, Nandanga, Luchelegwa alipowasili wilayani Ruangwa akiwa katika siku ya pili ya ziara yake ya kikazi ya siku nne Mkoani Lindi.

Waziri Mkuu alisema Serikali inatekeleza Kampeni yake ya kumtua mama ndoo, hivyo itahakikisha wananchi katika maeneo yote nchini, hususan ni ya vijijini wanapata huduma ya maji safi na salama katika umbali usiozidi mita 400.

Aliitoa kauli hiyo baada ya wananchi wa vijiji hivyo kumueleza changamoto mbalimbali zinazowakabili kwenye maeneo yao zikiwemo za maji, barabara, umeme, ambapo aliwahakikishia kwamba Serikali imeshaanza kuboresha huduma hizo.

Wakati huo huo, Waziri Mkuu amezindua Zahanati ya Nandanga ambayo imejengwa kwa fedha kutoka mfuko wa jimbo umegaharimu kiasi cha sh. milioni 73.47 na kuwahakikishia kwamba Serikali itawapelekea wataalam wa kutosha ili kuwahudumia.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

TRA yavuka lengo la makusanyo ya mapato kwa mwaka 2016/17

$
0
0
Mamlaka ya Mapato Tanzania imefanikiwa kukusanya kiasi cha shilingi Trilioni 14.4 kwa mwaka wa fedha 2016/17.

Makusanyo haya ni sawa na ukuaji wa asilimia 7.67 ikilinganishwa na makusanyo ya mwaka 2015/16 ambayo yalikuwa ni kiasi cha Shilingi Trilioni 13.3.

Sambamba na Makusanyo, Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa kodi TRA Bw. Richard Kayombo alisema Mamlaka imeendelea kukusanya kodi mbalimbali ikiwemo kodi ya majengo na muitikio wake umekuwa ni wa kiwango cha kuridhisha.

Mamlaka inapenda kuwashukuru walipakodi wote kwa muitikio huo na wengine wanaoendelea kujitokeza katika ofisi mbalimbali za Mamlaka nchi nzima ili kuweza kulipa kodi hiyo ambayo mwisho wa kulipa kodi hiyo ni tarehe 15 Julai, 2017.

Aidha, Mamlaka inapenda kutoa wito kwa wafanyabiashara wote kutoa risiti za EFD pindi wanapouza bidhaa au huduma na Wananchi wote kuhakikisha wanadai risiti pindi wanaponunua bidhaa au kupata huduma na kuwa, kinyume na hapo watakuwa wanatenda kosa kwa mujibu wa sheria ya usimamizi wa kodi.

Hivi sasa kuna zoezi la uhamasishaji na ukaguzi linaloendelea nchi nzima katika sehemu zote za biashara kukagua wafanyabiashara wasiotumia Mashine za Risiti za Kielektroniki za EFDs pamoja na wananchi wote wasiodai risiti baada ya kununua bidhaa au huduma.

 “Napenda kuwakumbusha wananchi wote kuhakiki risiti zao ili kuona usahihi wa tarehe na kiasi walicholipa kabla ya kuondoka na risiti hiyo” alisistiza Kayombo

 ‘Pamoja Tunajenga Taifa Letu’

Richard Kayombo

MKURUGENZI WA HUDUMA NA ELIMU KWA MLIPAKODI

Diwani Arusha aitosa Chadema akieleza anamuunga mkono Rais Magufuli

$
0
0
Diwani wa Ngabobo (Chadema), Solomon Laizer ameandika barua ya kujiuzulu udiwani na kujiunga na CCM kwa maelezo anamuunga mkono Rais John Magufuli.

Laizer ni diwani wa tano katika Halmashauri ya Meru kujiuzulu kwa kutoa sababu kuwa anamuunga mkono Rais Magufuli.

Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo, Christopher Kazeri amethibitisha jana  (Julai 11) kupata taarifa za kujiuzulu kwa Ngabobo.

Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari amesema kujiuzulu kwa diwani huyo ni mchezo mchafu akidai  amenunuliwa.

Amesema tayari walipata taarifa za diwani huyo kushawishiwa kujiuzulu na kwamba, alifuatwa na viongozi wa wilaya na kanda wa chama hicho aliowaeleza kuwa ameshawishiwa.

"Baadaye alieleza hataondoka lakini naona wamefanikiwa kumshawishi, tunashangaa viongozi wa Serikali badala ya kufanya kazi za maendeleo wanafanya kazi za kushawishi madiwani wa upinzani kuhama," amesema.

Hata hivyo, madiwani wanaohama wanapinga kuwa wameshawishiwa kufanya hivyo.

Hadi sasa madiwani watano wa Chadema waliojiuzulu ni Credo Kifukwe wa Kata ya Murieti jijini Arusha.

Wengine waliojiuzulu katika Jimbo la Arumeru Mashariki na kata zao kwenye mabano ni Anderson Sikawa (Leguruki), Emmanuel Mollel (Makiba), Greyson Isangya (Maroroni) na Josephine Mshiu (Viti Maalumu).

Jinsi Ya Kuandaa Na Kutayarisha Lishe Maalumu Ya Kuongeza Na Kunenepesha Mwili

$
0
0
Kama umekonda  na  kudhoofika  mwili  kutokana  na  sababu  mbalimbali  kama  vile kuugua  magonjwa  na  maradhi  mbalimbali  au  kupatwa  na  msongo  mawazo, basi  fuata  maelekezo  yafuatayo  ili  upate  kujua  namna  ya  kuandaa  na  kutayarishe  lishe  maalumu  ya  asili  itakayo  kusaidia kunenepa  na  kurejesha  afya  ya  mwili  wako  katika  hali  yake  ya  kawaida.

MAHITAJI:
1.    Dawa  Lishe  ya  kuongeza  na  kunenepesha  mwili

2.   Asali  ya  tende

3.   Ufuta

4.     Ukwaju

5.    Kitunguu  swaumu

6.   Giligiliani

7.    Juisi  ya  Komamanga na  Asali

MATAYARISHO  NA  MATUMIZI
Matumizi  ya  lishe  hii, yame  gawanyika  katika  awamu  kuu  mbili. Awamu  ya  kwanza, itachukua  siku thelathini  na  awamu  ya  pili  itachukua  siku  thelathini pia.

Katika  awamu  ya  kwanza , mgonjwa  atatumia  DAWA  LISHE  YA  KUNENEPESHA  MWILI, ASALI  YA  TENDE  NA  UFUTA  na  awamu  ya  pili, mgonjwa  atatumia   UKWAJU, KITUNGUU  SWAUMU, GILIGILIANI  na  JUISI  YA  KOMAMANGA  & ASALI  kwa  kufuata  utaratibu  utakao  elezwa  hapo  chini.

AWAMU   YA   KWANZA
SIKU   THELATHINI  ZA  KWANZA

Mahitaji

1.   Dawa  lishe  ya  kuongeza  na  kunenepesha  mwili

2.   Ufuta

3.   Asali  ya  Tende  (   Dates  Syrup )

MATAYARISHO  , MAELEKEZO  NA  MATUMIZI
1.   Dawa –Lishe  ya  Kunenepesha  Mwili

Chukua  vijiko   vitatu vikubwa  vyenye  dawa  yako, kisha  changanya  na  maji  nusu  lita halafu chemsha  hadi  itokote, Ikiisha  tokota, ipua  acha  ipoe  kidogo kisha  tumia  kunywa  pamoja  na  machicha  yake.  Utafanya  hivyo  mara  mbili  kwa  siku  asubuhi  na  jioni  kwa  muda wa  siku  thelathini.

2.   Ufuta : Matayarisho : Chukua  vijiko  vikubwa  vinane  vyenye  ufuta, kisha  changanya  na  lita  moja  na  nusu  ya  maji. Kama  hauna  tatizo  na  sukari, unaweza  kuongeza  na  sukari  kiasi ili  kuipa  ladha.  Ikisha  tokota, ipua iache  ipoe  kiasi  kisha  tumia  kula  ufuta wote  pamoja  na  supu  yake  ama  juisi  yake. Utafanya  hivyo mara  mbili  kwa siku  asubuhi  na  jioni  kwa  muda  wa  siku  thelathini.

(N.B:   KAMA  UNA  NAFASI,  BADALA  YA  KUTUMIA  VIJIKO  VINANE  TU VYA  UFUTA  KWENYE LITA  MOJA  NA  NUSU  YA  MAJI, WEWE  TUMIA  ROBO KILO  YA  UFUTA  KWENYE  LITA  TATU  YA  MAJI, CHEMSHA  HADI  ITOKOTE,  IACHE  IPOE, KISHA  TUMIA  KULA . FANYA  HIVYO  MARA  MBILI  KWA  SIKU  ASUBUHI NA  JIONI  KWA  MUDA  WA SIKU  THELATHINI )

2.   ASALI  YA  TENDE
3.   Tumia  kula  vijiko vikubwa  vinne  vya  tende  mara  mbili  kwa siku  asubuhi  na  usiku   kwa  muda  wa  siku  thelathini. Yaani  asubuhi  kula  vijiko  vikubwa vinne  na  usiku  kula  vijiko  vikubwa vinne  vya  asali  ya  tende.

( HABARI  NJEMA  KWA  WATEJA  WETU  NI  KWAMBA, ASALI  YA  TENDE  SASA  INAPATIKANA  MOJA  KWA  MOJA  DUKANI   KWETU . UTAPATIWA  DAWA  LISHE  PAMOJA  NA  ASALI  YA  TENDE  UTAKAYO  ITUMIA  KWA  MUDA  WA  SIKU  THELATHINI  KWA  UTARATIBU  WA  MAELEKEZO  HAYO  HAPO  JUU )
AWAMU   YA  PILI
Awamu  ya  pili  ya  lishe  hii, itaanza  baada  ya  kukamilika  kwa  siku  thelathini  za  kutumia  dawa  lishe, ufuta  pamoja  na  asali  ya  tende. Kama  ilivyo  kuwa  kwa  awamu  ya  kwanza, awamu  ya  pili  pia  itachukua  muda  wa  siku  thelathini

MAHITAJI, MATAYARISHO   NA  MATUMIZI

1.  UKWAJU
Matayarisho na  Maandalizi
Chukua ukwaju  kiasi  cha  robo kilo , weka  kwenye  maji  kiasi  cha  lita  moja, ongeza pilipili  manga kiasi cha  kijiko kimoja kidogo  ( tea spoon ) halafu ongeza sukari  vijiko  vitatu vikubwa, ongeza karafuu  ya unga  kijiko kimoja kidogo, pamoja  na hiriki vijiko  vikubwa  viwili.

Ukisha  fanya  hivyo, chemsha  hadi  mchanganyiko  wako  utokote. Ukisha  tokota, ipua  na  kuchuja  kisha  weka  kwenye  chombo  kisafi.

MATUMIZI :
Tumia  kunywa  mchanganyiko  huu kila  siku  asubuhi  baada  ya  kunywa  chai. Utafanya  hivyo  kwa  muda  wa  siku  thelathini  mfululizo.

2.   JUISI   YA  KOMAMANGA  NA  ASALI
Matayarisho  na  Matumizi

Tayarisha  juisi  ya  komamanga  kiasi  cha  nusu  lita, changanya  na asali ya  kawaida  vijiko vikubwa    vinane, kisha  ongeza  chumvi kijiko kidogo( tea spoon)

Koroga  mchanganyiko  wako  halafu  tumia  kunywa. Utafanya  hivyo  mara  moja   kwa  siku kwa  muda  wa  siku thelathini.

Matunda  ya  makomamanga  yanapatikana  masokoni, ingawa  mara  nyingi  hupatikana  kwa  uchache. Kama  utabahatika  kupata matunda  mengi, basi  unashauriwa  kuyachukua  kwa  wingi  na  kuyahifadhi, sehemu  salama ili usipate  usumbufu  wakati  wa  kutumia  tiba  yako.

Mbali  na  kutumika  katika lishe  ya  kuongeza  na  kunenepesha  mwili, tunda  la  komamanga, linasaidia  kuondoa  harufu  mbaya  ya  kinywa. Kwa  kuondoa  harufu  mbaya  ya  kinywa, kula  walau  tunda  moja  la  komamanga  kwa  siku  kwa  muda  wa  siku  thelathini  mfululizo. Utapata  matokeo  mazuri . ( HII  ITAWASAIDIA  ZAIDI  WALE  AMBAO  TATIZO  LAO  LA  KUTOKWA  NA  HARUFU  MBAYA  YA  KINYWA  LIMEANZIA  KINYWANI  NA  SIO  TUMBONI

ALTERNATIVE (MBADALA )  WA JUISI  YA  KOMAMANGA  ILIYO  UNGWA  NA  ASALI.

Kama  utashindwa  kupata makoma manga, basi  utafanya  kama  ifuatavyo :

KITUNGUU  SWAUMU
Chukua punje  nne  za  vitunguu  swaumu, zitwange kisha  tia  kwenye  maji nusu lita halafu ongeza  juisi  ya  ndimu  moja  au  limao  moja kisha  chemsha hadi mchanganyiko  wako  uchemke.

Matumizi :  Tumia  hivyo kila  siku  usiku baada  ya  kula  chakula cha  usiku. Utafanya  hivyo  kwa  muda  wa  siku  thelathini mfululizo.

AU
Vile vile , mbadala  mwingine wa  kutumia  juisi  ya komamanga  iliyo  changanywa  na  asali, unaweza  kutumia  JUISI  YA  GILIGILIANI  kwa  kufuata  utaratibu  ufuatao :

JUISI   YA   GILIGILIANI
MATAYARISHO   NA   MATUMIZI YA  JUISI  YA  GILI GILIANI

Chukua giligiliani  fresh, kisha zi -blend ( ZISAGE ) ili  kupata  juice  yake  kiasi  cha  robo  lita.

 Ndani  ya  juisi  yako  ya  giligiliani, kamuliamo ndimu fresh moja, halafu  ongeza  chumvi  kiasi robo  kijiko  kidogo ( tea spoon), koroga  kisha  tumia  kunywa.  Utakunywa  usiku  baada  ya  kula  chakula  cha  usiku. Utafanya  hivyo mara   moja  kwa  siku  kwa  muda  wa  siku  thelathini  mfululizo.

PIA : Jenga  utaratibu  wa  kuwa  unakula    giligiliani kwa wingi. Hakikisha  katika  kila  mlo  wako, inakuwepo  mboga  ya  giligiliani  pembeni.

VITU   VINGINE VYA   KUZINGATIA..
Pamoja na kutumia  lishe  hii  ya  asili  kwa  kufuata  utaratibu  huo  hapo  juu, unashauriwa  kuzingatia  matumizi  ya  vyakula  vifuatavyo:

TANGAWIZI
Jenga  tabia  ya  kuwa  una tumia  tangawizi, kila  mara  upatapo  nafasi.  Utaratibu  wa  jinsi  ya  kutayarisha  tangawizi ni  kama  ifuatavyo :

Chukua kipande  kimoja  cha  tangawizi, kisha  kitwange  halafu ongeza  vikombe  viwili vya  maji  vyenye  ujazo  wa  milimita  mia  mbili  na  hamsini ( 250 mills). Chemsha pamoja  kisha ongeza  maziwa  kiasi cha  robo lita  na  sukari ili kupata  ladha.  Fanya  hivi  kila  mara  uapatapo  nafasi. Ukiweza kufanya  hivyo walau  mara  mbili  kwa  siku, itakuwa  vizuri  zaidi.

  AU  chukua  kipande  kimoja  cha  tangawizi, kitwange kisha  chemsha pamoja  na  chumvi nusu  kijiko  kidogo  kwenye  maji kiasi  cha  nusu   lita  halafu tumia  kunywa  kikombe  kimoja  nusu  saa  kabla  ya  kula  chakula chako  cha  asubuhi, mchana  na usiku.

HIRIKI
Jenga utaratibu  wa  kuwa  unakunywa  mara  kwa  mara  chai  iliyo  changanywa  na  hiriki.

MACHUNGWA
Jenga utaratibu  wa  kuwa  unakula  machungwa kwa  wingi,  kwa  kadri utakavyo  weza. Unashauriwa  kuwa  unachanganya na  chumvi  kidogo  pamoja  na  pilipili  manga.

KWA  MAHITAJI  YAKO  YA  DAWA-LISHE  YA  KUNENEPESHA  & KUONGEZA  MWILI  PAMOJA  NA  ASALI  YA  TENDE.

Kwa  mahitaji  yako  ya  DAWA-LISHE ya  kuongeza & kunenepesha  mwili, pamoja  na  asali  ya  tende, fika  katika  duka  la  NEEMA  HERBALIST.

Tunapatikana  UBUNGO  jijini  DAR  ES  SALAAM, jirani  na  SHULE  YA  MSINGI   UBUNGO  NATIONAL  HOUSING  nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA.

WASILIANA  NASI  KWA  SIMU  NAMBA  0766 53 83 84.

Kwa wateja  wetu  waliopo  jijini  Dar  Es  Salaam, ambao  hawana  nafasi  ya  kufika  dukani  kwetu  Ubungo, tunayo  huduma  ya  kuwapelekea  dawa  mahali  walipo ( HOME & OFFICE  DELIVERY  )

Kwa wateja  waliopo  nje  ya  mkoa   wa  Dar  Es  Salaam,  watatumiwa  dawa  kwa  kutumia  mabasi  mbalimbali.

Kwa  wateja  waliopo  Zanzibar, watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa  boti.

Kwa  wateja  waliopo  ughaibuni, watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  au  DHL.

Na kwa  taarifa  zaidi  kuhusu  huduma  zetu, tutembelee  kila  siku  katika  blogu  yetu :

Ombi la Msukuma kwa Rais Magufuli

$
0
0
Mbunge wa Geita Vijijini, Joseph Msukuma (CCM) amemtaka Rais Magufuli kutosikiliza kelele za baadhi ya viongozi hususani wapinzani na kusema anapaswa kushikilia hapo hapo aliposhikilia kwani anafanya vizuri na mambo anayotenda yameanza kuonekana.

Msukuma alisema hayo juzi wakati wa makabidhiano ya nyumba 50 zilizojengwa na taasisi ya The Benjamin William Mkapa Foundation (BMF) na kusema wao Geita wapo mstari wambele kuhakikisha wanaunga mkono kila jambo ambalo linafanywa na Rais Magufuli.

"Mhe. Rais sisi huku Geita tunakuunga mkono na tupo tayari kujitolea hata bure katika mambo unayofanya katika nchi hii, nakuomba tu usisikilize zile kelele za watubali wewe fanya kazi kwa ajili ya Watanzania, maana kuna watu wengine wanasimama bungeni na kuanza kupiga kelele tu, wengine wanasimama bungeni na kusema eti unajenga uwanja wa ndege Chato, usiwasikilize na wala kelele zao zisikukatishe tamaa, ukiona kitu kingine kizuri chochote usiusahau mkoa wa Geita" alisisitiza Msukuma

Mbali na hilo Msukuma alikuwa na ombi kwa Rais Magufuli pindi wawekezaji waliokuwa wakisafirisha makinikia kwenda nje ya nchi wakilipa deni hilo basi awakumbuke watuwa Geita japo kwa barabara za lami kwani barabara anadai zimekuwa hazina kiwango kizuri na ni mbovu.

"Sahizi ukizinguka sehemu ukisema tumetoka Geita kidogo tunakuwa na heshima kwa ajili yako Rais Magufuli, tunakuomba uendelee hivyo hivyo ombi letu watu wa Geita, mgodi huu hatufadiki nao, kwa kuwa tulipitisha asilimia 6 tunaomba asilimia 1 tubaki nayo, lakini ombi letu la pili tumekusikia mara nyingi unasema wawekezaji wakubwa wamekuwa na maeneo makubwa maeka na maeka, tunaomba vijana wako waruhusu wawekezaji wapunguze maeneo ili vijana wachimbaji wadogo wakachimbe madini," alimalizia Msukuma

Mbali na hilo Rais Magufuli alimsifu sana mbunge msukuma na kusema hata bungeni huwa anamsikia anasimamia sana chama chake (CCM) na kusema kuwa yupo vizuri sana kwa jambo hilo, kwani anawakilisha vizuri sana.

Rooney atua Bongo na kikosi kizima cha Everton.....Tazama Picha na Video Hapa

$
0
0
Klabu ya Everton tayari imewasili Jijini Dar es Salam dakika chache zilizopita ikiwa inatokea nchini Uingereza huku ikiwakosa wachezaji wake watatu muhimu katika kikosi hicho kutokana na majeruhi waliyokuwa nayo.

Pamoja na hayo, timu ya Everton imeongozwa na mchezaji nyota Wayne Rooney pamoja na Davy Klaassen na Michael Keane ambao pia wamejiunga na klabu hivi karibuni.

Kikosi kamili cha Everton kilichotua leo ni Maarten Stekelenburg, Mateusz Hewelt, Chris Renshaw, Tom Davies, Phil Jagielka, Ashley Williams, Callum Connolly, Jonjoe Kenny, Michael Keane, Muhamed Besic, Leighton Baines, Morgan Schneiderlin, James McCarthy, Davy Klaassen.

Wengine ni Gareth Barry, Idrissa Gana Gueye, Joe Williams, Kieran Dowell, Kevin Mirallas, Wayne Rooney, Aaron Lennon, Dominic Calvert-Lewin, Ademola Lookman, Matthew Pennington, Yannick Bolasie.

Everton imewasili Tanzania kwaajili ya mchezo wa kirafiki dhidi ya timu ya Gor Mahia ya nchini Kenya mchezo unaotarajiwa kuchezwa katika dimba la Uwanja wa Taifa Jijini Dar es salaam siku ya Alhamisi ya wiki hii.

Kivutio kikubwa katika mapokezi ya timu hiyo inayoshiriki Ligi Kuu ya Uingereza ni wananchi wengi waliojitokeza kumshabikia Wayne Rooney.


==>Tazama VIDEO hapa jinsi walivyopokelewa

Halima Mdee: Mapambano yanaendelea

$
0
0
Mbunge wa Kaw, Halima Mdee baada ya kuachiwa kwa dhamana ya shilingi milioni 10 kwa kudaiwa kutoa lugha chafu kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amewashukuru wote waliopaza sauti zao ili haki itendeke kwake huku akisema mapambano bado yanaendelea.

Halima mdee ametumia ukurasa wake wa Tweeter kutweet shukrani hizo huku akisema mapambano yanaendelea.

Mhe. Halima ametweet

Kwa heshima KUBWA niwashukuru sana wote mliopaza sauti zenu kutaka haki itendeke kwangu na kwa watoto wetu wa kike! #Mapambano yanaendelea!
Halima Mdee alidaiwa kutoa maneno hayo ya kukashifu na ya uchochezi katika mkutano wake wa Baraza la Wanawake Chadema uliofanyika katika ofisi za baraza hilo wakati akizungumza na wanahabari.

Waziri Mpango akifunga kituo cha GBP kilichopo eneo la Uwanja wa Ndege, Dar

$
0
0
Benny Mwaipaja, WFM, Dar es Salaam 
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, amefanya ziara ya kushitukiza katika eneo la Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam na kuamuru kituo cha Mafuta cha GBP kifungwe hadi hapo kitakapo funga mashine maalumu za kutolea risiti baada ya kubainika hakitumii ipasanyo mashine za kieletroniki za kukusanyia kodi (EFD)

Dkt. Mpango amechukua hatua hiyo baada ya kujionea kituo hicho kikiwa na pampu nne za mafuta lakini kuna mashine moja pekee ya mkononi ya kutolea risiti jambo linasababisha wateja wao wengi kutopewa risiti na hivyo kuikosesha Serikali mapato yake na ni kinyume cha sheria za nchi.

“Sasa nawachukulia hatua ili liwe fundisho kwa wengine wote wanaouza mafuta nchini bila kufuata taratibu, na nitaanza na wewe, biashara yako isimame mpaka mashine zifungwe kwenye kituo chote na utekeleze mara moja,” alisema Dkt. Mpango

Katika ukaguzi wa Kituo cha Mafuta cha Puma, Dkt. Mpango amesifu utaratibu mzuri uliowekwa na kituo hicho kwa kufunga mashine maalumu za kutolea risiti zilizounganishwa na kila pampu za mafuta kitu ambacho ndicho Serikali inavitaka vituo vyote vya mafuta vitumie mfumo huo

“Kituo hiki kimezingatia sheria sheria kwa kufunga mashine kwa kuzingatia maelekezo ya Serikali na hapa tunauhakika wa kupata fedha za kuwatumikia wananchi, kinyume kabisa na kituo cha mafuta nilichokifungia, hapa ndio ningeomba Watanzania wanunue mafuta” aliongeza Dkt. Mpango.

Ameiagiza Mamlaka ya mapato Tanzania-TRA kufanya ukaguzi nchi nzima ili kubaini wamiliki wa vituo vya mafuta wanaokiuka maagizo ya Serikali yaliyowataka wafunge mashine hizo maalumu tangu mwaka uliopita.

Waziri wa Fedha na Mipango amewageukia wenye vyombo vya moto wanaonunua mafuta kwenye vituo vya mafuta kote nchini kudai risiti wanapopata huduma ya kuwekewa mafuta kwenye vituo hivyo ili kuokoa fedha za Serikali zinazoishia mikononi mwa wajanja wachache wanaokwepa kodi kwa makusudi na kuikosesha Serikali mapato yake.

Baadhi ya wananchi wamepongeza uamuzi wa Serikali kupitia Waziri wa Fedha na Mipango wa kufanya ziara za kushitukiza kwenye vituo vya mafuta na kutaka hatua hiyo iwe endelevu kwa maafisa wengine wa Serikali ili kukomesha vitendo vya wenye vituo vya mafuta kukwepa kodi ya Serikali.

Katika siku yake ya kwanza ya ziara za namna hiyo, Julai 10 mwaka huu, Dkt. Mpango alikifungia kituo cha Mafuta cha Mawenzi kilichoko Kigamboni, Jijini Dar es Salaam baada ya kubaini kuwa kituo hicho kimefunga mashine maalumu za kutolea risiti za kielektroniki lakini hazitumiki na kuamuru kituo hicho kifungwe hadi kitakapo rekebisha kasoro hiyo na kuvionya vituo vya mafuta vya OilCom kufunga mashine za aina hiyo mara moja.

Maofisa CDA wapangiwa kazi nyingine......Ni Baada ya Rais Magufuli Kuivunja

$
0
0
Wafanyakazi 260 wa iliyokuwa Mamlaka ya Ustawishaji wa Mji wa Dodoma (CDA) wamepangiwa vituo vipya vya kazi.

Kwa mujibu wa Waziri Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), George Simbachawene wafanyakazi 150 kutoka kundi hilo wanabaki Manispaa ya Dodoma huku wengine 66 wakipelekwa katika halmashuri na mikoa mbalimbali nchini.

Amesema wafanyakazi 16 wamepelekwa Tamisemi, DART (14), Hospitali ya Benjamini Mkapa Dodoma (4), Chuo Kikuu cha Dodoma (3), Ofisi ya Waziri Mkuu (3), Wizara ya Ardhi (2) Ofisi ya Bunge (1) na Utumishi wa Umma (1).

Waziri Simbachawene amewataka wafanyakazi hao kuripoti katika vituo vyao vya kazi mara baada ya kupata barua na Serikali haitasita kufuta ajira ya mtumishi yeyote ambaye atakaidi agizo hilo.

Rais wa John Magufuli aliivunja rasmi CDA Mei mwaka huu  na kuagiza mali na shughuli zote zilizokuwa zikifanywa na CDA zihamishiwe Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma.

Rais Magufuli alisema ameamua kuivunja CDA na kuhamishia majukumu yake katika Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma ili kuondoa mkanganyiko wa utoaji wa huduma kwa wananchi.

Alisema mkanganyiko huo ulikuwa ukisababishwa na mgongano kati ya vyombo hivyo viwili.

Aidha, alisema mahitaji ya sasa yamedhihirisha kuwa hakuna haja ya kuwepo kwa CDA.

“Wananchi wa Dodoma wamelalamikia tatizo hili kwa muda mrefu, hata nilipokuwa kwenye kampeni zangu za uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 walilalamika sana, sasa nimetekeleza niliyowaahidi,” alisema Dk Magufuli.
 
“Naamini kwa uamuzi huu malalamiko ya wananchi yatapata utatuzi na pia tutakuwa tumeondoa kikwazo cha umiliki wa muda mfupi wa ardhi uliosababisha wawekezaji kushindwa kujenga viwanda Dodoma.

CDA ilianzishwa kwa Amri ya Rais ya Aprili Mosi, 1973 na kutangazwa kupitia tangazo la Serikali namba 230.

Waziri Mkuu: Vijiji vyote Nchini kupatiwa umeme

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema hakuna kijiji nchini kitakachoachwa bila ya kuunganishiwa umeme katika awamu ya tatu ya mradi unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (Rea).

Amesema Serikali imetenga Sh1 trilioni kwa ajili ya kusambaza umeme katika vijiji 8,000 ambavyo bado havijaunganishiwa na nishati hiyo.

Waziri Mkuu amesema hayo Jumanne, Julai 11  alipozungumza kwa nyakati tofauti na wananchi wilayani Ruangwa.

Amesema hayo katika mikutano aliyoifanya kwenye vijiji vya Chiapi, Nandanga, Mbecha na Luchelegwa, ikiwa ni siku ya pili ya ziara yake ya kikazi ya siku nne mkoani Lindi.

 “Rais John Magufuli anajali wananchi, hivyo ametenga fedha nyingi zitakazotosheleza kusambaza umeme katika vijiji vyote vikiwemo vya Wilaya ya Ruangwa. Gharama za kuunganishiwa umeme huo ni Sh27,000 tu,” amesema katika taarifa iliyotolewa na ofisi yake.

Amesema wananchi hawatawajibika kulipia nguzo na fomu za maombi ya kuunganishiwa umeme, kwa sababu tayari gharama hizo zimebebwa na Serikali.

Amesema lengo la Serikali ni kufikisha umeme kwenye vijiji vyote Tanzania na kwa vile ambavyo viko kwenye maeneo yaliyo mbali na gridi ya Taifa, vitafungiwa umeme jua (sola) hivyo kufungua fursa za ajira na kukuza uchumi.

Waziri Mkuu amesema huduma hiyo ni muhimu kwa kuwa mbali ya kutumiwa majumbani lakini pia kwa kusogezwa karibu na maeneo ya pembezoni itawezesha zahanati, shule, viwanda na vituo vya afya kuwa na umeme.

Meneja wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) Mkoa wa Lindi, Johnson Mwigune amesema hadi kufikia mwishoni mwa mwezi huu mkandarasi aliyepangwa kufanya kazi katika vijiji hivyo atakuwa ameanza kusambaza umeme.

Japan yakabidhi kiwanda cha mafuta kwa Chama cha Ushirika Chato......Kinauwezo wa kuzalisha lita 700 za mafuta kwa siku.

$
0
0
Na,Emmanuel Twimanye     Geita,
Serikali ya Japan imekabidhi kiwanda cha kuchakata na Kuzalisha Mafuta ya Alizeti kwa chama cha Ushirika wa Kilimo na Masoko wilayani Chato Mkoani Geita chenye uwezo wa kuzalisha lita 700 za mafuta kwa siku.

Akikabidhi kiwanda hicho,Balozi wa Japani nchini Bw. Masaharu Yoshida amesema Serikali ya Japan itaendelea kuimarisha ushirikiano huo baina ya nchi hizo mbili katika kuleta maendeleo kwa wananchi Tanzania.

Mbunge wa Jimbo la Chato, Dk. Medard Kalemani aliyeshiriki kwenye makabidhiano hayo amesema serikali ya Japani licha ya kujenga kiwanda hicho Chenye Thamani ya Sh. 170 milioni, pia Japan inatekeleza ujenzi wa mradi wa soko la samaki la Kimataifa katika kijiji cha Kasenda litakalogharimu Sh. 320 milioni.

Awali mwenyekiti wa Chama cha Ushirika na Masoko, Elias Kaswahili na Meneja wa Mradi huo Faidaya Misango wamesema uzalishalishaji wa Mafuta ni mkubwa ukilinganisha na upatikanaji wa Alizeti na hivyo kutoa wito kwa wananchi kulima zao hilo ili kuwezesha kiwanda hicho kufanya kazi.

Aidha, kwa niaba ya Wananchi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli ameipongeza serikali ya Japan ambayo imekuwa mstari wa mbele katika kufadhili miradi mbalimbali ya maendeleo hapa nchini.

Japan ni nchi ambayo imetajwa kuwa rafiki wa karibu na Tanzania na hii inajidhihirisha katika kutoa ufadhili wa miradi ya mbalimbali ya maendeleo katika sekta ya miundombinu ya barabara, masoko, reli na elimu.

Lissu ataka wote waliopata fedha za Escrow wakamatwe

$
0
0
Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika TLS, Tundu Lissu amesema kuwa watu wote waliopata mgawo wa fedha hizo wakamatwe kwakuwa wameuthibitishia umma kuwa ni wala rushwa.

Lissu amesema kuwa kwa sasa hakuna ubishi kuwa watu hao ni wala rushwa na walitumia madaraka yao vibaya kujipatia fedha hizo na kuwa watu hao ni sehemu ya mafisadi ambao wamekuwa wakihujumu nchi.

Ameyasema hayo baada ya aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini wa Serikali ya awamu ya nne na mbunge wa Sengerema, William Ngeleja kurudisha Serikalini kiasi cha shilingi milioni 40.4 za mgawo wa Escrow hali ambayo imeibua mijadala mingi.

Ngeleja ambaye aliwahi kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria, juzi alisema kuwa amefikia hatua hiyo ya kuzikabidhi fedha hizo kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ili kujiweka kando na kashfa hiyo kwakuwa aliyempa ni mtuhumiwa.

“Sheria inasema kuwa ukikutwa umeiba unakamatwa unafikishwa kwenye vyombo vya dola ukikutwa na hatia unafungwa na fedha unarudisha, kwa hiyo hawa wote waliochukua mgawo huo wakamatwe wafikishwe katika vyombo vya dola na sio kurudisha tu hizo fedha hawa ni wezi,”amesema Lissu

Hata hivyo, ameongeza kuwa bila kujali nafasi ya watu hao katika jamii waliopata mgawo huo wanapaswa kwakuwa hata unapokuwa kiongozi wa dini hupaswi kula rushwa au kuchukua fedha za rushwa.

Ngeleja Aeleza kwanini hakumrudishia fedha za Escrow Rugemalira na Badala yake Alizipeleka TRA

$
0
0
Siku chache baada ya kutangaza kuwasilisha shilingi milioni 40 katika Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Mbunge wa Sengerema, William Ngeleja amefafanua sababu za kutomrejeshea fedha huyo mfanyabiashara, James Rugemalira ambaye alimpa awali kama msaada.

Fedha hizo ni sehemu ya shilingi bilioni 306 zilizotolewa katika akaunti maalum ya Tegeta Escrow mwaka 2014 iliyofunguliwa Benki Kuu ya Tanzania, fedha zizotolewa kimakosa wakati kesi ya mgogoro wa kati ya Tanesco na Kampuni ya kufua umeme ya IPTL ikiwa bado haijatolewa maamuzi.

Kwa mujibu wa taratibu, fedha hizo zilipaswa kutolewa baada ya kesi husika kukamilika na pande zote mbili kukaa pamoja kukokotoa kiasi cha fedha ambacho kila upande ungepaswa kupata kwa mujibu wa maamuzi.

“Kwa mazingira halisi yanayomkabili aliyenipa msaada, mahali salama pa kurejesha hizo fedha sasa ni serikalini. Serikali itajua kuwa fedha hizo zinastahili kwenda kwa Rugemalira sasa au wasubiri hatima ya kesi,” Ngeleja anakaririwa na Gazeti la Mwananchi .

“Ningerudisha kwa Rugemarila watu wangeweza kuibua hoja kwamba labda napiga changa la macho tu,” aliongeza.

Mfanyabiashara huyo maarufu ambaye kampuni yake ya VIP Engineering ilikuwa inamiliki asilimia 30 ya IPTL, pamoja na Mwenyekiti wa Pan African Power Solution (PAP), Harbinder Singh Seth wanakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi na bado wako mahabusu.

Mgao wa fedha hizo pia uliwafikia Anna Tibaijuka aliyekuwa waziri wa Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Andrew Chenge ambaye ni Mbunge wa Bariadi Magharibi, Askofu Msaidizi wa Kanisa Katoliki, Methodiu Kilaini, Jaji John Ruhangisa na wengine.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya July 13


Jinsi Punyeto Inavyo Sababisha Ukosefu Na Upungufu Wa Nguvu za Kiume

$
0
0

Ukosefu  na/ama  upungufu  wa  nguvu  za  kiume, ni  tatizo  linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume  duniani.  Zipo  sababu  nyingi  zinazo  sababisha  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume.  

Miongoni  mwa  sababu  hizo  ni  pamoja  na  maradhi  kisukari, presha,shinikizo  la  damu, moyo, figo, matatizo  kwenye  mishipa  ya  ubongo  &  mishipa  ya  uti  wa mgongo, matatizo  kwenye  mishipa itumikayo  kusafrisha damu  mwilini, maradhi  ya  ngiri,  pamoja  na   upigaji  punyeto  kwa  muda  mrefu.

Katika  makala  yetu  ya  leo, tutaangalia  namna   suala  la  upigaji  punyeto linavyo  athiri  nguvu  za  kiume.

Kabla  hatujaangalia  namna  suala la upigaji  punyeto linavyo  maliza  nguvu  za  kiume, ni  vyema  tukafahamu  kwanza  kuhusu  SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME.

Kufahamu   kuhusu   SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME  tafadhali  tembelea :

Ukisoma  vizuri  kuhusu  mfumo  wa  nguvu  za  kiume, utagundua  kuwa   Suala  la  nguvu  za  kiume  ni  suala  la  kimfumo.  Ili  mwanaume  awe na nguvu  za  kiume, aendelee  kuwa  na  nguvu  za  kiume na  azilinde  nguvu  zake za  kiume, ni  lazima  ogani  zote zinazo  husika  na  mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ziwe  na  afya  njema  na  ziwe  na  ushirikiano   thabiti  na  wenye  afya.

Vile  vile , utagundua  kuwa , mambo  makuu  muhimu  katika   mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ni  kama  ifuatavyo:

i.Mishipa  imara  ya  ubongo  na  yenye  afya  njema

ii. Mishipa  imara  ya  uti  wa  mgongo  (  spinal  cords )

iii.Mishipa  imara  itumikayo  kusafirisha  damu  mwilini  (  Blood Vessels )

iv. Mfumo  imara  wa  usafirishaji  damu  mwilini

v. Mishipa  ya  uume  iliyo  imara  na  yenye  afya  njema

vi. Uhusiano  imara  na  wenye  afya  kati  ya  mishipa  ya  fahamu  iliyopo  katika  ubongo, mishipa  ya  kwenye  uti  wa  mgongo  pamoja  na  misuli & mishipa  ya  kwenye  uume.

Hivyo  basi, ili  mwanaume  aweze  kuwa  na  nguvu  imara  za  kiume, na  aendelee  kuwa  na  nguvu  hizo ni  lazima  mambo  yote  muhimu  katika  mfumo  wa  nguvu za  kiume  yawe  imara  pasi na  hitilafu  yoyote.

Hitilafu  yoyote  katika  mambo  hayo, itasababisha  ukosefu na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume  kwa  mwanaume  huyo.  Pale inapotokea    hitilafu  ama  mapungufu  katika  ogani  zaidi  ya  moja  kati  ya  zilizo  tajwa hapo  juu, basi  tatizo  kwa  muhusika  huwa  kubwa  mara  dufu.

JINSI  PUNYETO  INAVYO  SABABISHA  TATIZO  LA  UKOSEFU &  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.
Mwanaume   anapopatwa na  wazo  la  kufanya  tendo  la  ndoa, ubongo  hutoa  ishara  kwenye  mishipa  ya  uti  wa  mgongo  ambayo  nayo  husafirisha  taarifa  hadi  kwenye  mishipa &  misuli  ya  uume.

Mishipa  ya  uume inapopokea  taarifa  hiyo, hutanuka. Na  mishipa  ya  uume  inapotanuka, hufanya  mambo  mawili  muhimu  sana :

i.Husababisha  mishipa  ya  ateri  kupanuka  na  hivyo  kuruhusu  damu  kuingia kwa  kasi  sana   ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  hivyo  kuufanya  uume  usimame  na  kuwa  imara  bara bara.

ii. Huibinya na  kuiziba  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kuzuia  kunyonya  ama  kufyonza  damu  iliyo  ingia  ndani  ya  mishipa ya  uume.  (  KAZI  KUBWA  YA  MISHIPA  YA  VENA  ILIYO  KARIBU NA  MISHIPA  YA  UUME  NI KUHAKIKISHA  HAKUNA  DAMU NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME. HIVYO  BASI  DAMU  INAPOINGIA  NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME, MISHIPA  YA  VENA  HU “SENSE” JAMBO  HILO  KWA  HARAKA  NA HIVYO  KUIFYONZA  DAMU  HIYO  KUTOKA KWENYE MISHIPA  YA UUME  YA  KUITOA  NJE YA MISHIPA  YA  UUME.  NA  DAMU INAPOKOSEKANA  NDANI  YA  MISHIPA  YA  UUME, HUUFANYA  UUME  KUSINYAA  NA  KULEGEA )

Mtu  anayepiga  punyeto  husababisha  mambo  yafuatayo  katika  mwili  wake :

1. Huuwa  nguvu  ya  mishipa  & misuli ya  uume ambayo  ndio  inayo husika  na  kusimama  kwa  uume

2. Mishipa  ya   uume  inapo  sinyaa  na  kukosa  nguvu  yake  ya  asili, husababisha  mambo  yafuatayo :

i.Huondoa  uwezo  wa  mishipa  &  misuli  ya  uume  kutanuka, na  hii  ndio  sababu  inayo  wafanya  waathirika  wa  punyeto  kutumia  nguvu  nyingi  sana  katika  kuufanya  uume  usimame.

ii.Huondoa  uwezo  wa  mishipa &  misuli  ya  uume  kuibana  na  kuiziba  mishipa  ya  vena, na  hii ndio  sababu  inayo  fanya  waathirika  wa  punyeto  kufika  kileleni  haraka  sana, kwani damu  inayo  ingia  kwenye misuli  ya  uume   hufyonzwa  ndani ya  muda  mfupi sana. 
 
 Hii  hutokea  kwa  sababu  mishipa na  misuli  ya  uume inakuwa  imelegea,na  mishipa  ya  vena inakuwa  imepwaya, hivyo  msuguano wowote ule  hufanya  mishipa  ya  vena  kufunguka  na  kufyonza  damu  kutoka  kwenye mishipa  ya  uume  na hivyo  kuufanya  uume  kusinyaa  ndani ya dakika ama sekunde  chache sana.

3. Vile  vile  punyeto  hufanya  uume  kusinyaa na  kurudi ndani  na  kuufanya  uonekane kama  uume  wa  motto mdogo.

Kwa  ufupi  punyeto  husababisha  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  sababu  kuu  zifuatazo :

i.Kwanza   hudhoofisha  na  kuharibu  mishipa  ya  uume,  ambayo  ndio  hufanya  uume kusimama.

ii.Pili  hudhoofisha  utendaji  kazi  wa  mishipa  ya  ateri, ambayo  ndio  hutumika  kama  njia  ya  kusafirisha  damu kupeleka kwenye  misuli  ya  uume  na  ivyo  kuufanya  uume  usimame

iii. Tatu, punyeto  hupelekea  kuvuja  kwa  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kusababisha  damu  kufyonzwa  kwa  haraka  sana  kila  iingiapo ndani  ya  misuli ya  uume  na  matokeo  yake  ni  uume   kusimama  kwa  muda  mfupi  sana  wakati wa  tendo  la  ndoa.

iv. Punyeto  huathiri  mtiririko  wa  damu  kwenda  kwenye  mishipa  ya  uume, kwa  sababu  hudhoofisha  misuli &  mishipa  ya  uume  pamoja  na mishipa ya  ateri  ambayo  ndio  hutumika  katika  kusafirisha  damu kwenda  kwenye  uume

DALILI  ZA  MTU  ALIYE  ATHIRIWA  NA  PUNYETO
Dalili  kuu  za  mtu  aliye athiriwa  na  punyeto  ni  kama  ifuatavyo:

i.           Uume  kusinyaa  na  kuwa  kama  wa  mtoto
ii.         Uume kurudi  ndani
iii.       Uume  kusimama  ukiwa  legelege
iv.       Kufika  kileleni  haraka  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

TIBA   YA   NGUVU  ZA  KIUME  KWA MTU  ALIYE  ATHIRIKA  NA  PUNYETO.
Dawa   asilia  ya  nguvu  za  kiume iitwayo JIKO  ni tiba  bora  na  ya  uhakika  kabisa  kwa  mtu  aliye  athiriwa   na  punyeto.  Dawa  hii, pamoja  na  mambo  mengine  mengi, husaidia  kufanya  mambio  yafuatayo  katika  mwili  wa  mwanaume  aliye  athiriwa  na  punyeto :

i.Kuimarisha  mishipa  & misuli  ya  uume  ulio  legea na  hivyo  kuurejeshea  uwezo wake wa  asili

ii. Hutibu   tatizo  la  uume  kurudi  ndani

iii.Humaliza  tatizo  la  kusimama  kwa  uume  ukiwa  legelege

iv.Hutibu  na  kuponya  kabisa  tatizo  la  kufika  kieleleni  haraka.

BEI  YA  DAWA  :  Dawa  hii  inapatikana  kwa  gharama  ya  SHILINGI  ELFU  THEMANINI  TU (Tsh. 80,000/=)

MAHALI  INAPOPATIKANA :  Dawa  hii  inapatikana  katika  duka  la  dawa  asilia  liitwalo  NEEMA  HERBALIST  &  NUTRITIONAL  FOODS  CLINIC  lililopo  jijini  DAR  ES  SALAAM  katika  eneo  la  UBUNGO   nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA   karibu  na SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING.

Kwa  wateja  wasio  weza  kufika  ofisini  kwetu. Watafikishiwa  dawa  mahali  popote  walipo  jijini  DAR  ES  SALAAM.

Kwa   wateja  waliopo  mikoani  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  MABASI

Kwa  wateja  waliopo   Zanzibar  wata fikishiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa boti.

Na  kwa  wateja  waliopo  UGHAIBUNI  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  ama  DHL.

MAWASILIANO :  WASILIANA  NASI   KWA  SIMU  NAMBA  0766  53  83  84.

Kwa  taarifa  zaidi  kuhusu  huduma  zetu, tutembelee kila  siku  kwenye  blogu  yetu :

Jipatie Dawa za Asili za Kuongeza Maumbile, Nguvu za Kiume......Kuondoa Mvi na Mkanda kwa Ajili ya Kupunguza Tumbo

$
0
0
Tatizo la upungufu wa nguvu za kiume na maumbile madogo ni kwa watu wengi sana lakini.  (NATURAL BEAUTY) imepata uvumbuzi wa tatizo hilo na tiba zake zilizotengenezwa kwa mimea na matunda hazina kemiko wala madhara yoyote. 
 
Pata bidhaa hizi uweze kufurahia matokeo mazuri na bidhaa salama kabisa. Tunazo za÷
 
   🥝🥑🥒🧀🍉🍅🍓🍇
1.HANDSOME UP ni kifaa kinachoongeza maumbile ya kiume  kwa 99% kwa size uipendayo wewe na kuimarisha misuli ya uume kifaa hiki kinapatikana kwa @180,000/= tuu.
2.MEN GELY YA KUPAKA. Hii inaongeza kwa wastani wa inch 6.5 na inapatikana kwa @130,000/=.  
 
3. SHARK POWER. Hii pia ni kwa ajili ya kuongeza maumbile  wastani wa inch 7.5 kutoka size uliopo inapatikana kwa @140,000/=.
 
4.. MAX MAN 2. Ni vidonge kwa ajili ya nguvu ambavyo vinasaidia sana hata kwa watu wenye kisukari na waliokua wakifanya sana master blashion. Pia huongeza hamu ya tendo la ndoa inapatikana kwa @140,000/=
 
5.DISCREET. Hii ni ya kuondoa mvi na zisiludi tena milele inapatikana kwa @130,000/=
 
6.MICRO COMPUTER. Huu ni mkanda kwa ajili ya kupunguza tumbo pamoja na nyama za pembeni unapatikana kwa 180,000/=
 
7. YODI PILLS. Hii ni vidonge vya kuongeza (shepu hips na makakio) vinapatikana kwa 170,000/=
 
8.BODY BOOSTER. Ni dawa ya kuongeza mwili mzima pamoja na hamu ya kula vizuri 150,000/=
 
9.BOTCHO CREAM. Ni dawa ya kupaka ya kuongeza (makalio hips na mapaja) inapatikana kwa 150,000/=
 
10.BOTCHO MULTPLUS. Ni dawa ya kunywa ya kuongeza (shepu makalio mapaja na hips)  inapatikana kwa 200,000/=
 
🍅🍇🍉🍅🍍🍓🥒🥑🍒
      Tupo DAR ES SALAAM  kariakoo na kinondoni kanisani.
Kwa mawasiliano zaidi piga  0759029968 au 0659618585. 
 
Popote ulipo utapata huduma zetu.
           Pia bidhaa zetu zote ni guarantee na hakikisha ununuapo bidhaa kampuni hii unapewa risiti harisi ya natural beauty
 
Follow us Instagram
@natural2162
@natural2162
@natural2162
@natural2162
                            Karibu

Kutana Maajabu ya Mtabibu CHIEF SULTAN(MAKATA WA MAKATANI) Mganga wa Waganga Sasa Yupo Mikoa Yote Tanzania

$
0
0
Kutana Maajabu ya Mtabibu CHIEF SULTAN(MAKATA WA MAKATANI) Mganga wa Waganga Sasa Yupo Mikoa Yote Tanzania

Pia anatoa Tiba kwa Njia ya Simu ukiwa popote Pale Tanzania au Nje ya Tanzania..

CHIEF SULTAN ni Mtabibu na Mtafiti wa Dawa za Asili ya Africa, na Duniani Katika utoaji wa Tiba za Asili..
 
Je unasumbulia na Mapenzi..?
(Umeachwa na Umpendae awe Mume/ Mke au mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine na Bado Unampenda?) Umejaribu sehemu Nyingi bila Mafanikio?Wasiliana na CHIEF SULTAN Akusaidie Kumshika Umpendae Asikusaliti(LIMBWATA) Kumtawala Mpenzi wako kwa sababu Maalum..Anauwezo wa Kusambalatisha Mahusiano yao ndani ya siku Moja tu.
Je Unasumbuliwa na Madeni?
Biashara yako Haina wateja?
Unatatizo la kutokushika Mimba na umehangaika sehemu nyingi bila mafanikio?
 
Wasiliana na CHIEF SULTAN Kwa Majibu ya Maswali yako..
Anasafisha NYOTA na Kutoa PETE za BAHATI kuendana na NYOTA yako. UTAJIRI USIO NA MASHARTI.(Magic Wallet_Pochi ya Maajabu Isio Isha Hela)
KUWA MAARUFU na KUJULIKANA
Kupandishwa CHEO na HESHIMA Mahala pa KAZI.
Utapewa Nguvu ya Kujilinda na MALI ZAKO zako na Mwili wako.. Huzuia Chuma Ulete katika Biashara.. Hurudisha MALI zilizo Potea au KUDHULUMIWA..
Mvuto wa Biashara na Mwili wako.
Hutibu kabisa Nguvu za Kiume na Kurefusha Uume kwa saizi Unayotaka.
 
Magonjwa Sugu(Miguu Kufa Ganzi, kisukari, Presha, Pumu nk.)Humaliza Kesi za Muda mrefu ndani ya siku 14 tu.
Anatoa NDAGU Zisizokuwa na Masharti.. Kwa maelezo Zaidi wasilina nae kwa

whatsapp +255 0658 316 976
Call +255 755 911 233

Wakurugenzi 6, mameneja 6 NSSF waachishwa kazi

$
0
0
Bodi ya Wadhamini ya Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) imewaachisha kazi wafanyakazi 12 waliokuwa wamesimamishwa kwa mwaka mmoja sasa.

Wafanyakazi hao walisimamishwa kazi Julai 2016 kupisha uchunguzi kuhusu tuhuma za ubadhirifu na matumizi mabaya ya ofisi.

Taarifa ya NSSF iliyotolewa leo Alhamisi (Julai 13) kupitia vyombo vya habari walioachishwa kazi ni Yacob Kidula, aliyekuwa mkurugenzi wa mipango, uwekezaji na miradi.

Wengine na nafasi walizokuwa wakishikilia kwenye mabano ni Ludocick Mrosso (mkurugenzi wa fedha), Chiku Matessa (mkurugenzi wa rasilimali watu na utawala), Sadi Shemliwa (mkurugenzi wa udhibiti, hadhara na majanga), Pauline Mtunda (mkurugenzi wa ukaguzi wa hesabu za ndani).

Crescentius Magori (mkurugenzi  wa uendeshaji), Amina Abdallah (meneja utawala), Abdallah Mselli (meneja wa uwekezaji), Mhandisi John Ndazi (meneja miradi), Wakili Chedrick Komba (meneja kiongozi Mkoa wa Temeke) na Ramadhani Nassibu (meneja mkuu usalama).

Mbowe: Upinzani ni wito, Ningekuwa na Roho Nyepesi Ningekuwa Nishakimbia

$
0
0
Wakati diwani wa saba wa Chadema akijiuzulu jana, Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe amesema hata yeye kama angekuwa na moyo mwepesi na mpenda fedha, angekuwa ameshahama upinzani.

Mbowe alisema jana kwamba kuwa kiongozi wa upinzani awe mbunge, diwani, au mwenyekiti wa mtaa, kunahitaji roho ngumu na kwamba hiyo si kazi ya watu wenye kupenda fedha, bali ni ya maumivu, kudhalilishwa, kunyimwa ushirikiano, kufungwa wakati wowote na kunahitaji msimamo wa hali ya juu.

“Upinzani ni wito, wenye roho nyepesi hawawezi, kama ningekuwa napenda fedha, nina roho nyepesi, ningeshachukua hizo pesa na ningeshakimbia kabisa upinzani,” alisema.

Mbowe amesema hayo wakati chama hicho kikipitia misukosuko ya madiwani wake wa Mkoa wa Arusha kukihama na jana ilikuwa zamu ya Diwani wa Ambuleni, Arumeru, Japhet Jackson.

Diwani huyo aliwasilisha barua yake ya kuhama Chadema kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Meru, Christopher Kazeri jana mchana pia kama wenzake sita, akisema anamuunga mkono Rais John Magufuli.

Diwani wa karibuni kujiuzulu wa Ngobobo, Solomon Laizer pia wa wilaya hiyohiyo katika jimbo linaloongozwa na Joshua Nassari wa Chadema.

Akizungumza kwa simu jana, Mbowe ambaye pia ni Mbunge wa Hai alisema wanaowania nafasi za uongozi na viongozi wa Chadema wanahitaji kuwa na msimamo wa hali ya juu.

“Mara nyingi wanaowania nafasi kwa upande wa upinzani, ni wale waliokomaa, lakini katika uchaguzi uliopita, chama kilichopata watu wengi ni Chadema. Kutokana na mfumo huo wa kuwafungulia milango, wakaingia wengi, mbu, mende na mambo mengine,” alisema.

Kiongozi huyo wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni alidai kwamba kuondoka kwa madiwani hao wa Chadema kunasababishwa na baadhi ya watendaji wa Serikali hasa wakuu wa wilaya ambao wanataka kumfurahisha Rais.

“Inashangaza kuona wote wanaojiuzulu wanatoa kauli moja ya kumsifu Magufuli, ina maana hawana sababu nyingine labda pengine Chadema kuna matatizo, sera zao mbovu, kuna hiki na hiki hakijakaa sawa,” alisema.

Aliongeza kuwa juhudi za kuwarubuni viongozi wa Chadema zipo katika majimbo yote ya Chadema na juhudi hizo zinapata nguvu zaidi mahali ambako kuna mkuu wa wilaya dhaifu ambaye anatumia nguvu za ziada.

Alisema wamebaini kuwa baadhi ya wakuu wa wilaya ndiyo wanaotumiwa na wamewekwa kwa makusudi kwa ajili ya kuua upinzani nchini.

“DC anawahimiza wanachama na viongozi eti wapeleke barua za kujizulu kwake, kwa sababu ana jeuri ya mamlaka. Kisheria hana mamlaka ya kupokea barua ya kujiuzulu kwa mwanasiasa. Tumebaini hawa baadhi ya watendaji wanatumiwa na kuahidiwa makubwa endapo watawadhibiti wapinzani,” alisema.

Alisema walipata tetesi za kujiuzulu kwa madiwani hao lakini hawakutaka kuchukua uamuzi wa kuwafukuza kwani si vizuri kuishi kwa tetesi lakini kwa kuwa wameamua kuondoka anawatakia kila heri.

Alisema baadhi ya madiwani hao walionekana kwenye vikao vya CCM na kusema mtu anayezidiwa akili na kudanganywa kwa fedha hata akibaki katika chama hatakuwa na maana.

“Kuliko kubaki na watu wengi wanaopenda fedha, wanaohadaiwa kwa rushwa, bora tubaki watu wachache wenye maadili,” alisema.

Mbowe alisema, licha ya Serikali kuudhofisha upinzani, chama hicho kinaamini kuwa safari yake ni kama ya treni ya kwenda Kigoma ambayo wapo wanaopanda na wanaoshuka.

“Bado tunavuna maelfu ya wana CCM, alianza Edwin Mtei, lakini sasa tunazungumzia wanachama zaidi ya milioni sita. Muelewe kuwa upinzani haudhoofiki, bali unakua,” alisema.

Alisema wale waliodhani watapata ulaji kama wa fedha, ndiyo wanaokuwa wepesi kuondoka na kwenda kutafuta wanachokitaka.

“Tuna imani watabaki wachache wenye imani na nafasi za walioondoka zitachukuliwa na wengine walio bora zaidi,” alisema.

Kuhusu kuswekwa rumande kwa saa 48 kwa amri za wakuu wa wilaya, Mbowe alisema sheria za kumuweka ndani kiongozi zina masharti yake.

“Kuna utaratibu wa kufanya.DC sio polisi, anaweza kuagiza polisi, kamkamateni fulani kisha mumhoji na kisha afunguliwe mashtaka, lakini si kumuweka ndani kwa saa 48. Haya maagizo yote yanatolewa na ngazi za juu. Sisi sasa tunawashtaki hao Ma-DC wote na hata mimi nimemshtaki DC wa Hai, kwa kuharibu miradi yangu,” alisema.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live


Latest Images