Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Jinsi Punyeto Inavyo Sababisha Ukosefu Na Upungufu Wa Nguvu za Kiume

$
0
0

Ukosefu  na/ama  upungufu  wa  nguvu  za  kiume, ni  tatizo  linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume  duniani.  Zipo  sababu  nyingi  zinazo  sababisha  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume.  

Miongoni  mwa  sababu  hizo  ni  pamoja  na  maradhi  kisukari, presha,shinikizo  la  damu, moyo, figo, matatizo  kwenye  mishipa  ya  ubongo  &  mishipa  ya  uti  wa mgongo, matatizo  kwenye  mishipa itumikayo  kusafrisha damu  mwilini, maradhi  ya  ngiri,  pamoja  na   upigaji  punyeto  kwa  muda  mrefu.

Katika  makala  yetu  ya  leo, tutaangalia  namna   suala  la  upigaji  punyeto linavyo  athiri  nguvu  za  kiume.

Kabla  hatujaangalia  namna  suala la upigaji  punyeto linavyo  maliza  nguvu  za  kiume, ni  vyema  tukafahamu  kwanza  kuhusu  SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME.

Kufahamu   kuhusu   SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME  tafadhali  tembelea :

Ukisoma  vizuri  kuhusu  mfumo  wa  nguvu  za  kiume, utagundua  kuwa   Suala  la  nguvu  za  kiume  ni  suala  la  kimfumo.  Ili  mwanaume  awe na nguvu  za  kiume, aendelee  kuwa  na  nguvu  za  kiume na  azilinde  nguvu  zake za  kiume, ni  lazima  ogani  zote zinazo  husika  na  mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ziwe  na  afya  njema  na  ziwe  na  ushirikiano   thabiti  na  wenye  afya.

Vile  vile , utagundua  kuwa , mambo  makuu  muhimu  katika   mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ni  kama  ifuatavyo:

i.Mishipa  imara  ya  ubongo  na  yenye  afya  njema

ii. Mishipa  imara  ya  uti  wa  mgongo  (  spinal  cords )

iii.Mishipa  imara  itumikayo  kusafirisha  damu  mwilini  (  Blood Vessels )

iv. Mfumo  imara  wa  usafirishaji  damu  mwilini

v. Mishipa  ya  uume  iliyo  imara  na  yenye  afya  njema

vi. Uhusiano  imara  na  wenye  afya  kati  ya  mishipa  ya  fahamu  iliyopo  katika  ubongo, mishipa  ya  kwenye  uti  wa  mgongo  pamoja  na  misuli & mishipa  ya  kwenye  uume.

Hivyo  basi, ili  mwanaume  aweze  kuwa  na  nguvu  imara  za  kiume, na  aendelee  kuwa  na  nguvu  hizo ni  lazima  mambo  yote  muhimu  katika  mfumo  wa  nguvu za  kiume  yawe  imara  pasi na  hitilafu  yoyote.

Hitilafu  yoyote  katika  mambo  hayo, itasababisha  ukosefu na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume  kwa  mwanaume  huyo.  Pale inapotokea    hitilafu  ama  mapungufu  katika  ogani  zaidi  ya  moja  kati  ya  zilizo  tajwa hapo  juu, basi  tatizo  kwa  muhusika  huwa  kubwa  mara  dufu.

JINSI  PUNYETO  INAVYO  SABABISHA  TATIZO  LA  UKOSEFU &  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.
Mwanaume   anapopatwa na  wazo  la  kufanya  tendo  la  ndoa, ubongo  hutoa  ishara  kwenye  mishipa  ya  uti  wa  mgongo  ambayo  nayo  husafirisha  taarifa  hadi  kwenye  mishipa &  misuli  ya  uume.

Mishipa  ya  uume inapopokea  taarifa  hiyo, hutanuka. Na  mishipa  ya  uume  inapotanuka, hufanya  mambo  mawili  muhimu  sana :

i.Husababisha  mishipa  ya  ateri  kupanuka  na  hivyo  kuruhusu  damu  kuingia kwa  kasi  sana   ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  hivyo  kuufanya  uume  usimame  na  kuwa  imara  bara bara.

ii. Huibinya na  kuiziba  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kuzuia  kunyonya  ama  kufyonza  damu  iliyo  ingia  ndani  ya  mishipa ya  uume.  (  KAZI  KUBWA  YA  MISHIPA  YA  VENA  ILIYO  KARIBU NA  MISHIPA  YA  UUME  NI KUHAKIKISHA  HAKUNA  DAMU NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME. HIVYO  BASI  DAMU  INAPOINGIA  NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME, MISHIPA  YA  VENA  HU “SENSE” JAMBO  HILO  KWA  HARAKA  NA HIVYO  KUIFYONZA  DAMU  HIYO  KUTOKA KWENYE MISHIPA  YA UUME  YA  KUITOA  NJE YA MISHIPA  YA  UUME.  NA  DAMU INAPOKOSEKANA  NDANI  YA  MISHIPA  YA  UUME, HUUFANYA  UUME  KUSINYAA  NA  KULEGEA )

Mtu  anayepiga  punyeto  husababisha  mambo  yafuatayo  katika  mwili  wake :

1. Huuwa  nguvu  ya  mishipa  & misuli ya  uume ambayo  ndio  inayo husika  na  kusimama  kwa  uume

2. Mishipa  ya   uume  inapo  sinyaa  na  kukosa  nguvu  yake  ya  asili, husababisha  mambo  yafuatayo :

i.Huondoa  uwezo  wa  mishipa  &  misuli  ya  uume  kutanuka, na  hii  ndio  sababu  inayo  wafanya  waathirika  wa  punyeto  kutumia  nguvu  nyingi  sana  katika  kuufanya  uume  usimame.

ii.Huondoa  uwezo  wa  mishipa &  misuli  ya  uume  kuibana  na  kuiziba  mishipa  ya  vena, na  hii ndio  sababu  inayo  fanya  waathirika  wa  punyeto  kufika  kileleni  haraka  sana, kwani damu  inayo  ingia  kwenye misuli  ya  uume   hufyonzwa  ndani ya  muda  mfupi sana. 
 
 Hii  hutokea  kwa  sababu  mishipa na  misuli  ya  uume inakuwa  imelegea,na  mishipa  ya  vena inakuwa  imepwaya, hivyo  msuguano wowote ule  hufanya  mishipa  ya  vena  kufunguka  na  kufyonza  damu  kutoka  kwenye mishipa  ya  uume  na hivyo  kuufanya  uume  kusinyaa  ndani ya dakika ama sekunde  chache sana.

3. Vile  vile  punyeto  hufanya  uume  kusinyaa na  kurudi ndani  na  kuufanya  uonekane kama  uume  wa  motto mdogo.

Kwa  ufupi  punyeto  husababisha  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  sababu  kuu  zifuatazo :

i.Kwanza   hudhoofisha  na  kuharibu  mishipa  ya  uume,  ambayo  ndio  hufanya  uume kusimama.

ii.Pili  hudhoofisha  utendaji  kazi  wa  mishipa  ya  ateri, ambayo  ndio  hutumika  kama  njia  ya  kusafirisha  damu kupeleka kwenye  misuli  ya  uume  na  ivyo  kuufanya  uume  usimame

iii. Tatu, punyeto  hupelekea  kuvuja  kwa  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kusababisha  damu  kufyonzwa  kwa  haraka  sana  kila  iingiapo ndani  ya  misuli ya  uume  na  matokeo  yake  ni  uume   kusimama  kwa  muda  mfupi  sana  wakati wa  tendo  la  ndoa.

iv. Punyeto  huathiri  mtiririko  wa  damu  kwenda  kwenye  mishipa  ya  uume, kwa  sababu  hudhoofisha  misuli &  mishipa  ya  uume  pamoja  na mishipa ya  ateri  ambayo  ndio  hutumika  katika  kusafirisha  damu kwenda  kwenye  uume

DALILI  ZA  MTU  ALIYE  ATHIRIWA  NA  PUNYETO
Dalili  kuu  za  mtu  aliye athiriwa  na  punyeto  ni  kama  ifuatavyo:

i.           Uume  kusinyaa  na  kuwa  kama  wa  mtoto
ii.         Uume kurudi  ndani
iii.       Uume  kusimama  ukiwa  legelege
iv.       Kufika  kileleni  haraka  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

TIBA   YA   NGUVU  ZA  KIUME  KWA MTU  ALIYE  ATHIRIKA  NA  PUNYETO.
Dawa   asilia  ya  nguvu  za  kiume iitwayo JIKO  ni tiba  bora  na  ya  uhakika  kabisa  kwa  mtu  aliye  athiriwa   na  punyeto.  Dawa  hii, pamoja  na  mambo  mengine  mengi, husaidia  kufanya  mambio  yafuatayo  katika  mwili  wa  mwanaume  aliye  athiriwa  na  punyeto :

i.Kuimarisha  mishipa  & misuli  ya  uume  ulio  legea na  hivyo  kuurejeshea  uwezo wake wa  asili

ii. Hutibu   tatizo  la  uume  kurudi  ndani

iii.Humaliza  tatizo  la  kusimama  kwa  uume  ukiwa  legelege

iv.Hutibu  na  kuponya  kabisa  tatizo  la  kufika  kieleleni  haraka.

BEI  YA  DAWA  :  Dawa  hii  inapatikana  kwa  gharama  ya  SHILINGI  ELFU  THEMANINI  TU (Tsh. 80,000/=)

MAHALI  INAPOPATIKANA :  Dawa  hii  inapatikana  katika  duka  la  dawa  asilia  liitwalo  NEEMA  HERBALIST  &  NUTRITIONAL  FOODS  CLINIC  lililopo  jijini  DAR  ES  SALAAM  katika  eneo  la  UBUNGO   nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA   karibu  na SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING.

Kwa  wateja  wasio  weza  kufika  ofisini  kwetu. Watafikishiwa  dawa  mahali  popote  walipo  jijini  DAR  ES  SALAAM.

Kwa   wateja  waliopo  mikoani  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  MABASI

Kwa  wateja  waliopo   Zanzibar  wata fikishiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa boti.

Na  kwa  wateja  waliopo  UGHAIBUNI  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  ama  DHL.

MAWASILIANO :  WASILIANA  NASI   KWA  SIMU  NAMBA  0766  53  83  84.

Kwa  taarifa  zaidi  kuhusu  huduma  zetu, tutembelee kila  siku  kwenye  blogu  yetu :


Korea Kaskazini yafyatua Kombora zito, latua eneo Muhimu Japan

$
0
0
Korea Kaskazini imeendelea na mpango wake wa majaribio ya silaha nzito ambapo jana usiku imeripotiwa kufyatua kombora lingine zito kutoka Magharibi mwa eneo lake.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na maafisa wa Japan na Korea Kaskazini, kombora hilo lilifyatuliwa majira ya saa tatu na dakika arobaini usiku kwa saa za eneo hilo, na lilitua katika eneo muhimu la kiuchumi la bahari nchini Japan.

Shirika la habari la Yonhap limekariri tamko la jeshi la Japan kuwa kombora lililofyatuliwa lilisafiri umbali wa kilometa 930 na lilichukua dakika 40 kabla ya kutua, kitendo kilichozua taharuki.

Hili ni jaribio la 11 la makombora ya Korea Kaskazini kwa mwaka huu, ingawa majaribio ya hivi karibuni yanaonekana kufanikiwa kwa kiasi kikubwa.

Jaribio la mwisho lilikuwa mwezi Mei mwaka huu, katika maeneo mawili tofauti ambayo yote yalielekezwa baharini nchini Japan.

Katibu Mkuu wa Baraza la Mawazili la Japan, Yoshihide Suga ameeleza kuwa uchokozi unaofanywa na Korea Kaskazini hauvumiliki. Ameongeza kuwa taifa hilo linalaani kwa nguvu zote vitendo hivyo na hatua stahiki zitachukuliwa.

Naye Rais wa Korea Kusini, Moon Jae ametoa wito wa kufanyika kwa kikao cha dharura cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kujadili hatua za Korea Kaskazini, wito aliousisitiza pia wakati wa kikao chake na Rais wa Marekani, Donald Trump ndani ya Ikulu ya Marekani.

Rais Trump pia aliendelea na mfululizo wa maonyo kwa Korea Kaskazini, akisema kuwa uvumilivu umefika kikomo na sasa ‘inatosha’.

Picha: Rais Magufuli Alivyotua Jijini Mwanza na Kisha Kuingia Uwanjani Kutazama Mpira

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Wachezaji wa Buhongwa Fc mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Nyamagana jana Jumatatu ya July 3

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongela mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Mwanza.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Viongozi wa Dini mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Mwanza.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwasalimia wakazi wa Kona ya bwiru katika barabara ya Airport wakati akitokea uwanja wa ndege wa Mwanza.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwasalimia wakazi wa katikati ya jiji la Mwanza waliokusanyika kumpokea.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akinunua Karanga kutoka kwa Mmachinga anayefanya biashara katikati ya jiji la Mwanza
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia mkono washabiki waliohudhuria mechi kati ya Buhongwa United na Timu ya Nyamwaga katika uwanja wa Nyamagana jijini Mwanza.

VIDEO: Mapokezi Ya Rais Dkt John Pombe Magufuli Alipowasili Jijini Mwanza

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, jana tarehe 3 Julai, 2017 amewasili mkoani Mwanza kwa ziara ya kikazi ya siku mbili na kupokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongela pamoja na viongozi mbalimbali wa Mkoa wa Mwanza.

==>Tazama tukio zima hapo chini

Taarifa Muhimu Toka Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais IKULU

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, jana tarehe 3 Julai, 2017 amewasili mkoani Mwanza kwa ziara ya kikazi ya siku mbili na kupokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongela pamoja na viongozi mbalimbali wa Mkoa wa Mwanza.

Akiwa mkoani hapa Mhe. Rais Magufuli atakuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa mradi wa  uboreshaji wa huduma ya maji safi na usafi wa mazingira mjini Sengerema leo  tarehe 4 Julai, 2017.

Katika Uwanja wa Ndege wa Mwanza Mhe. Rais Dkt. Magufuli alikutana na kamati ya amani ya viongozi wa dini na  kuwashukuru viongozi hao kwa sala na dua zao na amewataka waendelee kuwahimiza waumini wao kuliombea Taifa ili liepukane na vitendo vya rushwa ambavyo ni adui wa maendeleo.

Akiwa njiani kutoka Uwanja wa Ndege wa Mwanza katika eneo la Bwiru kuelekea Ikulu ndogo ya Mwanza, Mhe. Rais Magufuli msafara wake ulisimamishwa mara kwa mara na wananchi waliojaa barabarani na kuamua kuzungumza nao ambapo aliwahakikishia kuwa Serikali ya Awamu ya Tano imepania kupambana na ufisadi kwa lengo la kuwaletea maendeleo Watanzania bila kujali tofauti za dini au Siasa.

Aidha, aliwahakikishia wananchi hao kuwa Serikali yake imedhamiria kuondoa kero mbalimbali ikiwa ni pamoja na kufuta baadhi ya kodi zenye kero na kuwapatia vitambulisho wafanyabishara wadogo wadogo, maarufu kama Wamachinga, ili waweze kufanya biashara zao bila kusumbuliwa.

Akiwa eneo la Nyamagana jijini Mwanza, Mheshimiwa Rais alitembea kwa miguu huku kuwasalimu wananchi waliokuwa wakimshangilia na kuzuia msafara wake. 

Rais Magufuli pia alikwenda  Uwanja wa Mpira wa Nyamagana na kuungana na baadhi ya wananchi waliokuwa wakiangalia mechi ya mpira wa miguu  kati ya timu ya Buhongwe na Nyamwaga.

Mhe. Rais Dkt. Magufuli pia amefurahishwa na maendeleo ya ujenzi wa barabara ya kutoka Uwanja wa Ndege wa Mwanza hadi katikakati ya jiji ambao gharama za ujenzi wake zilitokana na fedha zilizokuwa zimetengwa kwa ajili ya sherehe za Muungano.

Jaffar Haniu Naibu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Mwanza

Tangazo la nafasi za kazi 400 kutoka serikalini

$
0
0
Tangazo la nafasi za kazi 400 kutoka serikalini

Taarifa Ya CCM Kuhusu Mambo Yaliyozuiwa katika Uchaguzi wa ndani wa Chama hicho.

Jipatie Dawa za Asili za Kuongeza Maumbile, Nguvu za Kiume......Kuondoa Mvi na Mkanda kwa Ajili ya Kupunguza Tumbo

$
0
0
OFFER OFFER OFFER
Natural beauty product inakupa OFFER ya EID kwa punguzo la %10 kwa kila product.  
 
Tatizo la upungufu wa nguvu za kiume na maumbile madogo ni kwa watu wengi sana lakin NATURAL BEAUTY imepata uvumbuzi wa tatizo hilo na tiba zake zilizotengenezwa kwa mimea na matunda hazina kemiko wala madhara yoyote. 
 
Pata bidhaa hizi uweze kufurahia matokeo mazuri. Tunazo za÷
   🥝🥑🥒🧀🍉🍅🍓🍇
1.HANDSOME UP ni kifaa kinachoongeza maumbile ya kiume  kwa 99% kwa size uipendayo wewe na kuimarisha misuli ya uume kifaa hiki kinapatikana kwa @180,000/= tuu.
2.MEN GELY YA KUPAKA. Hii inaongeza kwa wastani wa inch 6.5 na inapatikana kwa @130,000/=. 
3. SHARK POWER. Hii pia ni kwa ajili ya kuongeza maumbile  wastani wa inch 7.5 kutoka size uliopo inapatikana kwa @140,000/=.
4.. MAX MAN 2. Ni vidonge kwa ajili ya nguvu ambavyo vinasaidia sana hata kwa watu wenye kisukari na waliokua wakifanya sana master blashion. Pia huongeza hamu ya tendo la ndoa inapatikana kwa @140,000/=
5.DISCREET. Hii ni ya kuondoa mvi na zisiludi tena milele inapatikana kwa @130,000/=
6.MICRO COMPUTER. Huu ni mkanda kwa ajili ya kupunguza tumbo pamoja na nyama za pembeni unapatikana kwa 180,000/=
7. YODI PILLS. Hii ni vidonge vya kuongeza (shepu hips na makakio) vinapatikana kwa 170,000/=
8.BODY BOOSTER. Ni dawa ya kuongeza mwili mzima pamoja na hamu ya kula vizuri 150,000/=
9.BOTCHO CREAM. Ni dawa ya kupaka ya kuongeza (makalio hips na mapaja) inapatikana kwa 150,000/=
10.BOTCHO MULTPLUS. Ni dawa ya kunywa ya kuongeza (shepu makalio mapaja na hips)  inapatikana kwa 200,000/=
🍅🍇🍉🍅🍍🍓🥒🥑🍒
 
      Tupo DAR ES SALAAM  kariakoo na kinondoni kanisani.
Kwa mawasiliano zaidi piga  0759029968 au 0659618585.
Popote ulipo utapata huduma zetu. 
 
Pia bidhaa zetu zote ni guarantee na hakikisha ununuapo bidhaa kampuni hii unapewa risiti harisi ya natural beauty
 
           Follow us Instagram
@natural2162
@natural2162
@natural2162
@natural2162
                            Karibu

Mbunge CCM ( Juliana Shonza ) nusura achapane na wabunge wa Chadema

$
0
0
Wabunge wa Chadema jana walipambana kwa maneno na mbunge wa viti maalumu (CCM), Juliana Shonza, ambaye baadaye alienda polisi kuripoti sakata hilo.

Wabunge hao walidai Shonza aliwatukana kwa kuwaita wapumbavu baada ya kumwambia kuwa anachokifanya bungeni, hasa kuwasilisha mapendekezo ya adhabu dhidi ya wabunge wa Chadema, Halima Mdee (Kawe) na Ester Bulaya (Bunda Mjini) ni chuki binafsi ya kuondoka upinzani.

Mzozo huo ulizuka jana mara baada ya kikao cha mchana wakati wabunge wa Ukawa wakisubiri kukaguliwa kuingia jengo la utawala kwa ajili ya kikao chao na waandishi wa habari.

Shonza, ambaye aliwahi kuwa mwanachama wa Chadema, alikuwa akitoka jengo la utawala na kukuta wabunge hao wakisubiri ukaguzi.

Mbunge huyo alisikika akisema, “hamuwezi kunipangia cha kusema, kwa sababu hamkunileta bungeni,” huku akimfuata kwa karibu mbunge wa Ubungo (Chadema), Saed Kubenea. Sekunde chache baadaye, Shonza alisikika akisema “mnataka kunipiga” (huku akielekeza mkono kwa Suzan Kiwanga (mbunge wa Mlimba, Chadema), ambaye alisikika akimtaka Shonza amtaje aliyetaka kumpiga.

Baadaye wabunge wa upinzani walisikika wakihoji sababu za Shonza kuwatukana.

“Wengine hapa sisi ni mama zako,” alisikika Suzan Lyimo (viti maalum, Chadema).

Hata hivyo, baadaye wabunge wa CCM waliokuwa jirani walisogea na kumsihi Shonza kuachana na ugomvi huo, lakini mbunge huyo aliendelea kuwa eneo hilo, lakini baadaye walimchukua na kwenda naye jengo la Pius Msekwa.

Wakati wakiondoka naye, Pauline Gekul (Babati Mjini, Chadema), alimtaka Zainabu Vullu (viti Maalumu (CCM), kumfunda mbunge wao.

Alipoulizwa chanzo cha ugomvi huo, Kubenea alisema Shonza aliwatukana kwa kuwaita “wapumbavu” baada ya Joseph Selasini (Rombo, Chadema) kumwambia Shonza anachokifanya bungeni ni chuki.

Spika Job Ndugai alisema baadaye kuwa alipata taarifa za tukio hilo na kumshauri Shonza aliripoti polisi kwa kuwa ni la jinai na kwamba atawafikisha wabunge nane mbele ya Kamati ya Maadili kwa hatua zaidi.

Kaimu kamanda wa polisi wa mkoa, Ernest Kimola alisema suala hilo limefunguliwa jalada la shambulio la kudhuru.

“Hatua inayofuata baada ya kuletwa kwa taarifa hii ni kuwatafuta wahusika ili tuweze kupata taarifa ya upande wa pili,” alisema Kamanda Kimola.

Credit: Mwananchi

Wabunge 6 CHADEMA Wahojiwa kwa Kumshambulia Mbunge wa CCM

$
0
0
Wabunge sita wa Chadema usiku wa kumkia leo wamehojiwa na polisi kwa tuhuma za kumshambulia Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Juliana Shonza.

Mwenyekiti mwenza wa wabunge wanaounda umoja wa katiba (Ukawa) James Mbatia amewataja wanaoshikiliwa kuwa ni Mbunge wa Mlimba Suzan Kiwanga, Saed Kubenea(Ubungo), Pauline Gekul (Babati Mjini), Frank Mwakajoka (Tunduma), Joseph Selasini (Rombo) na Cecilia Pareso (Viti Maalum).

Hadi saa 5.00 usiku wabunge hao bado walikuwa wakiandika maelezo katika kituo cha polisi. Wabunge hao ni kati ya wabunge wanane waliotajwa na Spika wa Bunge Job Ndugai alipokuwa akiahirisha kikao cha bunge jioni kuwa wanatuhumiwa kumshambulia Shonza.

Wabunge wengine waliotajwa katika sakata hilo lililotokea Jumatatu mchana mchana katika lango la kuingilia jengo la utawala ni Devotha Minja (Viti Maalum) na Cecil Mwambe (Ndanda).

Hata hivyo James Mbatia alipohojiwa Saa 5.45usiku alisema kuwa wabunge hao waliachiwa kwa dhamana baada ya mahojiano na kutakiwa kurud polisi Jumanne Saa 3 asubuhi.

Hata hivyo Mbatia ameshangazwa na kitendo cha kutajwa kwa Mwambe ambaye amesema hii ni wiki ya pili hayupo mjini Dodoma.

“Mimi nilikuwa msimamizi wa kambi yetu, Mwambe aliniaga tangu wiki mbili zilizopita anaenda jimboni na hajarudi sasa tunashangaa kutajwa alikuwepo wakati wa tukio,” amesema.

Wabunge hao walidakwa mmoja mmoja na askari waliokuwa wamevalia mavazi ya kiraia (askari kanzu) wanaolinda bunge.

Kukamatwa kwa wabunge hao kulifuatia Shonza kwenda kushtaki kwa Ndugai naye kutoa kibali cha kukamatwa kwa wabunge hao.

TRL Yavikataa vichwa vya treni Vilivyo Bandarini.......TPA Wanadai ni Vyao ila tu Kuna Mgogoro Ambao wao Hawakutaarifiwa

$
0
0
Kampuni  ya Reli Tanzania (TRL) imekanusha kuhusika na vichwa 11 vilivyoshushwa na kutelekezwa katika Bandari ya Dar es Salaam hivi karibuni. 

Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Deusdedit Kakoko, vichwa hivyo vilivyoshushwa na meli ya Mesina Line tangu wiki iliyopita, na kwamba ni mali ya TRL.

Mkurugenzi Mkuu wa kampuni hiyo, Masanja Kadogosa jana alisema TRL haihusiki kwa namna yoyote na vichwa hivyo kwa kuwa hakuna taarifa zozote zinahusu uagizwaji wake.

Alisema pia kwa mujibu wa Sheria ya Manunuzi, kampuni hiyo inapofanya manunuzi yoyote lazima kuwepo na mkataba wa makubaliano na kampuni husika inayouza bidhaa, lakini haina mkataba wowote unaohusu ununuzi wa vichwa hivyo.

Alieleza kuwa taratibu za manunuzi zinafahamika kwani endapo kampuni hiyo ingeagiza vichwa hivyo ingetakiwa kupeleka mtu wake kwa ajili ya ukaguzi wakati vinatengenezwa na mara baada ya kutengenezwa kabla ya kupakiwa kwenye meli. “Lakini hiyo kitu hakuna, hatukuwa na watu wetu kwa kuwa si mali yetu,” alieleza.

Pamoja na hayo, alisema ili mzigo wowote umfikie mhusika lazima kuwepo na nyaraka ya kutolea mzigo bandarini ambayo pia huwa na makubaliano mengine baina ya mnunuzi na muuzaji ambayo katika sakata hilo, TRL wamesisitiza hawana nyaraka hiyo.

Alisema TRL haivitambui vichwa hivyo kwa kuwa si mali yake. “Hivi ni vichwa vikubwa sasa kwanini tuvikatae kama ni vyetu, ila ukweli ni kwamba hatuvitambui kabisa,” alieleza mkuu huyo wa reli nchini.

Juzi wakati akizundua Mradi wa Uboreshaji wa Bandari ya Dar es Salaam (DSMGP), Rais John Magufuli aliibua hoja hiyo ya vichwa vya treni kushushwa bandarini na kutekelezwa bila kuwa na mwenyewe na kuitaka TPA pamoja na Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, kufuatilia kwa kina suala hilo.

Dk Magufuli alisema anazo taarifa za kushushwa kwa vichwa vya treni takribani 15 katika bandari hiyo, ambavyo mmiliki wake hafahamiki na meli iliyovileta imeshaondoka. 

Hata hivyo, mkurugenzi wa mamlaka hiyo ya TPA Kakoko pamoja na kuthibitisha kushushwa kwa vichwa hivyo kutoka kwa meli ya Mesina Line, iliyobeba mzigo huo kutoka kwa Komazi Trading Co, alibainisha wazi kuwa vichwa hivyo ni vya TRL.

Alisema vichwa hivyo ni awamu ya pili iliyoagizwa tangu serikali ya awamu ya nne miaka mitatu iliyopita, ambapo awamu ya kwanza ilishaletwa na vichwa vyake kuchukuliwa na hadi leo vinatumiwa na TRL.

Alifafanua kuwa baada ya uchunguzi wa TPA ilibaini kuwa kuna mgogoro unaoendelea kati ya TRL na kampuni ya Komazi na kwamba TRL ilishagoma kuvichukua vichwa hivyo lakini suala hilo, halikutaarifiwa kwa TPA

Miswada Mipya: Ni Marufuku kwa kampuni za madini kuweka fedha nje......Kesi Zote za Mikataba Zitaamuliwa Nchini

$
0
0
Sasa  kampuni za madini zinazofanya kazi zake nchini hazitaruhusiwa kuhifadhi fedha nje ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na pia mashauri ya mikataba hiyo yatafanyika ndani ya nchi na siyo katika mahakama na mabaraza ya nje, Bunge limepitisha katika kulinda rasilimali za nchi.

Aidha, Bunge limepewa nguvu ya kupitia makubaliano ya mikataba ya maliasili na rasilimali za nchi. 

Akiwasilisha Muswada wa Sheria ya Mamlaka ya Nchi kuhusiana na Umiliki wa Maliasili wa Mwaka 2017, Waziri wa Sheria na Katiba, Profesa Palamagamba Kabudi alisema sheria inaeleza kuwa mapato yote yanayotokana na rasilimali na maliasili na utafutaji, uchimbaji au umiliki na utumiaji wa rasilimali za Taifa, yanahifadhiwa katika taasisi za kifedha za ndani ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania.

“Itakuwa ni kosa kuweka fedha hizo nje ya nchi isipokuwa gawiwo ambalo mwekezaji ataruhusiwa kutoa nje ya nchi kwa mujibu wa sheria za nchi za Tanzania,” alieleza Profesa Kabudi na kuongeza kuwa pia sheria inatamka kuwa mashauri kuhusu maliasili na rasilimali za nchi chini ya mamlaka ya nchi hayatafanyika chini ya mahakama na mabaraza ya nje.

Aidha, alibainisha kuwa sheria itatumika pande zote mbili za Muungano, bila kuathiri mamlaka ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar juu ya usimamizi wa rasilimali za nchi. 

Alisema muswada huo pia unazuia usafirishaji wa maliasili bila kuongeza thamani, lengo ni kuleta maendeleo na kutekeleza azma ya serikali ya kuwa na Tanzania ya viwanda.

Akiwasilisha Muswada wa Sheria ya Mapitio na Majadiliano kuhusu masharti hasi katika Mikataba ya Maliasili za Nchi wa Mwaka 2017, Profesa Kabudi alisema unawezesha wananchi kupitia Bunge, kupitia mikataba inayohusu rasilimali na malisiali ya nchi ambayo imefungana na Jamhuri ya Muungano kwa lengo la kujiridhisha kama masharti, makubaliano na mikataba haina masharti hasi na yanakinzana na maslahi ya wananchi na taifa kwa ujumla na kuishauri serikali.

“Sheria imeipa nguvu bunge kupitia mikataba yote inayohusiana na malisili za nchi na rasilimali zake iliyoingiwa na Jamhuri ya Muungano ili kujiridhisha masharti yaliyomo kwenye mikataba hiyo yamezingatia maslahi ya Watanzania. 

"Na endapo mikataba haitii maslahi ya Watanzania, basi Bunge liweze kuishauri serikali kufanya majadiliano na wahusika wengine katika mikataba kwa lengo la kuondoa masharti hasi yasiyokuwa na manufaa kwa Taifa,” alifafanua.

Aliongeza“Endapo itapita kuwa sheria, serikali haitafikia makubaliano yenye tija kwa wananchi na taifa ndani ya muda utakaokubaliwa na pande zote basi masharti yote hasi yatachukuliwa kwamba yamefutwa, na si sehemu ya mikataba, na serikali haitakuwa na wajibu wowote wa kutekeleza masharti ambayo yamebainika kuwa hasi.” 

Profesa Kabudi alisema serikali itapitia mikataba yote ya madini ya sasa kwa kuzingatia sheria mpya zitakazopitishwa na Bunge katika Mkutano wa Bajeti unaoendelea.

Alisema mikataba yote ya madini iliyopo sasa itapitiwa upya kwa kuzingatia sheria mpya zitakazopitishwa na Bunge. 

 “Miswada hii inalenga kuleta mapinduzi makubwa katika kulinda rasilimali na maliasili ya nchi, dhana ya miswada hii ni ukombozi wetu na mapinduzi ya Watanzania wote,” alieleza Profesa Kabudi na kusisitiza umuhimu wa wabunge kupitisha miswada hiyo.

Alinukuu insha ya falsafa ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere aliyesema, “Mapinduzi haya yanayotakiwa ni kwa wote na si kwa wachache, tulipoonewa tulionewa wote, tuliponyonywa tulinyonywa wote, tulipopuuzwa tulipuuzwa wote, ni unyonge wetu sote kwa pamoja ndio uliotufanya tukaonewa, tukanyonywa na kupuuzwa, mapinduzi tunayoyafanya sasa, ni lazima yawe yetu kwa pamoja ili Mtanzania asiwe mnyonge, na unyonge wake ukatumiwa kumnyonya, na kupuuza.”

Kambi ya Upinzani 
Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni imepinga kitendo cha Serikali au Bunge kutumia kifungu cha 5 (2) cha muswada muswada wa sheria ya mamlaka ya nchi kuhusiana na umiliki wa maliasili wa mwaka 2017 ambacho kimeweka umiliki wa rasilimali na maliasili za nchi mikononi mwa Rais kwa niaba ya wananchi wa Tanzania.

Kambi rasmi bungeni imesema kuwa kifungu hicho ni hatari ambacho kinaweza kuleta madhara makubwa kwa taifa kisipoangaliwa kwa nidhamu ya hali ya juu na kwa uzalendo uliotukuka kwani endapo anaweza kupatikana rais ambaye si mzalendo nchi inaweza kutumbukia pabaya.

“Mikataba hii imezipa kinga kubwa sana kampuni za madini ambazo zimesaini mikataba na serikali na ikiwa ni pamoja na kuzuia kutumika kwa sheria mpya ambazo zinapitishwa na Bunge kwa kampuni hizo kuanzia mikataba hiyo inaposainiwa,” yalikuwa maoni ya Upinzani yaliyosomwa na Mbunge wa Viti Maalumu, Cecilia Paresso.

Akichangia, Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (Chadema) alisema Bunge linapotunga sheria ni wakati muhimu wa kuwa makini na kwamba miswada hiyo ilihitaji muda wa kutosha.

Alisema anataka kuamini kuwa Rais aliyepo ni mzalendo na anapenda watu. “Najiuliza kwa mamlaka aliyopewa Rais siku akija mtu si mzalendo kama Magufuli nataka kuamini hivyo akatokea hata upande huu hata Chadema kwa sababu huku hakuna malaika au akitokea CUF nako hakuna malaika, akatokea rais sio mwaminifu na amepewa mamlaka kubwa ya kusimamia rasilimali basi atauza taifa hili,” alieleza Lema.

Mbunge wa Geita Vijiji, Joseph Msukuma (CCM) aliwashangaa wabunge wanaopinga miswada hiyo kuletwa kwa hati ya dharura na kuhoji kuwa mbona mgombea wa urais kupitia Ukawa, Edward Lowassa alipatikana kwa hati ya dharura.

“Hata mgombea urais wa upande mwingine (Chadema) walipata mgombea kwa hati ya dharura, walimuona anafaa kwa dharura waliyokuwa nayo, walimpata bila kumchunguza huku wakijua kuwa walileta mtu ambaye wanataka akabidhiwe nchi, na hajui chochote kuhusu Chadema na wananchi hawakuwahoji,” alisema.

Picha 5 za Mbunge wa CCM Alivyotaka Kupigana na Wabunge wa CHADEMA Jana Bungeni

$
0
0
MBUNGE wa Viti Maalum (CCM) Juliana Shonza, jana alizua timbwili nje ya viwanja vya bunge na kunusurika kupigwa na wabunge wa upinzani kutokana na kuwatambia kwamba atahakikisha Mbunge wa Kawe, Halima Mdee ambaye yuko kifungoni anaendelea kusota huko.

Wabunge hao wa Chadema  waliitwa Polisi kuhojiwa usiku wa kuamkia leo

Hapo chini ni picha za tukio hilo

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Aagiza Halima Mdee Akamatwe

$
0
0
Mkuu wa Wilaya (DC)  Kinondoni, Ally Hapi amemwagiza Kamanda wa Polisi mkoa wa Kinondoni, Suzan Kaganda kumkamata mbunge wa Kawe, (Chadema) Halima Mdee na kumweka mahabusu kwa saa 48 kutokana na kutoa maneno ya uchuchezi kwa Rais John Magufuli.

Mdee anadaiwa kutoa maneno hayo ya kukashifu na ya uchochezi katika mkutano wake wa Baraza la Wanawake Chadema (Bawacha) uliofanyika jana katika makao makuu ya chama hicho.

Akizungumza na wanahabari ofisini kwake leo (Jumanne Julai 4) Hapi amesema kauli za Mdee kuhusu wanafunzi waliopata mimba kurudi shuleni, imemshtua yeye kama mwenyekiti wa  Kamati ya Ulinzi na Usalama wa wilaya hiyo.

Amesema ameamua kuchukua hatua hiyo hasa baada ya Mdee, alipomshushia kashfa hizo kiongozi wa nchi ambaye ni Amiri Jeshi Mkuu wa nchi.

 
"Mh. Mdee amemtaja kwa jina rais kwamba ana tabia za hovyo, na kwamba tabia zake za hovyo zimempelekea kuona kwamba maneno yake ndiyo sheria ya nchi. Pia amesema kwamba ipo siku rais ataagiza watanzania watembee vifua wazi yaani wanawake kwa wanaume. Nimeshtushwa sana", amesema Mh. Happi na kuongeza;

 "Maneno yake ni ya kichochezi ambayo hayakubaliki, hayafai kutolewa na kiongozi kama yeye hivyo namuagiza kamanda amkamate Mdee amweke ndani kwa saa 48 ili ahojiwe yale yote aliyoyaongea ili afikishwe kwenye vyombo vya usalama,"

Mwanamke amwaga machozi mbele ya Rais Magufuli Mwanza

$
0
0
Rais John Magufuli amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongela kuyafanyia kazi malalamiko ya mwanamke mmoja mkazi wa Sengerema aliyedai kunyanyaswa na kuvunjiwa nyumba yake.

Rais ametoa agizo hilo leo (Jumanne Julai 4) wakati akizindua mradi wa maji, wilayani Sengerema na kumtaka Mongela kuchukua namba ya simu ya mwanamke huyo aliyejitambulisha kwa jina la Rosemary Simon, ili atatuliwe tatizo lake.

 Kabla ya Rais Magufuli kuchukua hatua hiyo, mwanamke huyo alikwenda mbele ya jukwaa alimoketi Rais, huku akilia kuwa ananyanyaswa na viongozi wa Chadema na kuwa wanataka kumbomolea nyumba yake, bila kufafanua ni kwa vipi.

“Mpe simu yako Mkuu wa Mkoa, halafu atakutafuta na wala usijali, nitamtuma Mkuu wa Mkoa  na haki yako itatendeka, nitalifanyia kazi suala lako,” amesema Rais.

Rais Magufuli: Mwalimu Atakaye Mrudisha Mwanafunzi Aliyepata Mimba Ntamfukuza Kazi

$
0
0
Rais John Magufuli amesema mwalimu mkuu atakayeruhusu mwanafunzi aliyejifungua kurudi shuleni kuendelea na masomo katika shule za Serikali, atafukuzwa kazi.

Rais ameyasema hayo leo (Jumanne, Julai 4) alipokuwa akihutubia wananchi wakati akizindua mradi wa maji Sengerema.

“Ni ukweli pia kuwa wanafunzi waliopata mimba hawarudishwi shuleni, kuna ujanja ujanja wa walimu, wanaandika cheti kuwa alikuwa amelazwa,” amesema na kuongeza:

“Nikimuona Headmaster, amerudisha mwanafunzi aliyepata mimba, kwenye shule za Serikali, yule mwalimu anaondoka.”

Rais amehoji: “Wote waliopata mimba wamebakwa?” Alihoji na kuendelea,“wanafanya mambo haya kwenye picha, wakipata mimba kwa namna hiyo arudi shule.”

Ameongeza:“Niwaombe wazazi wawachunge watoto, hizi mimba zinatokana na wazazi wetu ni lazima wazazi tujifunze kulea, tumechagua kueleza ukweli, tuambiane ukweli.

Rais Magufuli: Mnaotaka wenye Mimba Warudi Shule Muanzishe Shule Zenu

$
0
0
Rais John Magufuli amezitaka Asasi za Kiraia (NGO’s) kufungua shule kwa wanafunzi wanaopata mimba shuleni kama kweli zinawapenda wanafunzi hao.

Rais ameyasema hayo leo (Jumanne, Julai 4) alipokuwa akihutubia wakati wa uzinduzi wa mradi wa maji Sengerema.

“Si kwamba nawachukia wenye mimba, hata kwa bahati mbaya akapata mimba, kama hizo NGO zinawatetea sana, zifungue shule za wenye mimba, kwa sababu zinawapenda wenye mimba, wafungue shule zao,”amesema Rais leo.

Amesema hata hao wanaofanya makongamano ya kuhamasisha watu wapate mimba wafungue shule zao kwa ajili ya wanafunzi hao.

“ Haiwezekani fedha za walipa kodi, Sh 17 bilioni kila mwaka za kusomesha watoto wetu, kwenda kusomesha wakinamama, wazunguke, waimbe, waseme nini mimi ndiyo Rais, huo ndio ukweli,” amesema.

Amesema tatizo si wanaopata mimba, kwani wapo waliopata matatizo, kama kuugua kwa muda mrefu wakashindwa kwenda shule lakini ulianzishwa mpango maalum wa kuwasomesha katika mfumo usio rasmi.

Manji Afungua Kesi Akiomba Polisi Wamwachie Huru........Ni Baada ya Kukamatwa Tena Juzi Asubuhi

$
0
0
Mfanyabiashara maarufu na aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa Klabu ya Yanga Yusuf Manji na wenzake wawili wamefungua kwa hati ya dharura maombi katika Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar wakiomba waachiwe kwa sababu wamekamatwa isivyo halali.

Mbali na Yusuf Manji katika maombi hayo yaliyowasilishwa leo July 4, 2017 na kupangiwa mbele ya Jaji Lugano Mwandambo, walalamikaji wengine ni Deogratius Kisinda na Thobias Fwere ambapo wamefungua maombi hayo dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), George Masaju, IGP Simon Sirro na Mkuu wa Upelelezi Kanda ya Dar.

Kwa mujibu wa hati ya kiapo ambayo imewasilishwa na Wakili Gudson Ndusyepo, Manji na wenzake wanaiomba Mahakama Kuu iwaachie kutokana na kukamatwa isivyo halali huku wakiiomba Mahakama hiyo kutoa amri ya kuwataka walalamikiwa wawafikishe Mahakamani ili washughulikiwe kwa mujibu wa sheria.

Katika hati hiyo, Wakili Ndusyepo amebainisha kuwa Manji na wenzake walikamatwa nyakati tofauti tofauti ambapo mlalamikaji Kisinda alikamatwa June 30, 2017 saa 10 jioni wakati Manji na Fwere walimatwa July 1, 2017 saa 5 asubuhi katika Jengo la Quality Center Barabara ya Pugu, Dar.

Manji na wenzake walikamatwa kwa tuhuma za kukutwa na sare za Jeshi katika ghala la Quality Motors Group ambapo kupitia hati hiyo ya kiapo, Wakili Ndusyepo amebainisha kuwa kukamatwa kwa walalamikaji sio halali kwa sababu kosa linalodaiwa dhidi yao linahusiana na masuala ya Kampuni ya Quality Motors ambayo inaongozwa na Wakurugenzi wake na Manji.

Mara baada ya kukamatwa kwa walalamikaji hao waliombewa dhamana lakini ilikataliwa kwa sababu zisizojulikana
”Kama Wakili wa waombaji nimefuatilia suala la dhamana hadi sasa saa 48 zimeshapita tangu walipokamatwa, lakini hawajafikishwa Mahakamani. Jambo hilo ni kinyume na sheria.” – Wakili Ndusyebo.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya July 5

Kutana Maajabu ya Mtabibu CHIEF SULTAN(MAKATA WA MAKATANI) Mganga wa Waganga Sasa Yupo Mikoa Yote Tanzania

$
0
0
Pia anatoa Tiba kwa Njia ya Simu ukiwa popote Pale Tanzania au Nje ya Tanzania..

CHIEF SULTAN ni Mtabibu na Mtafiti wa Dawa za Asili ya Africa, na Duniani Katika utoaji wa Tiba za Asili..
Je unasumbulia na Mapenzi..?
 
(Umeachwa na Umpendae awe Mume/ Mke au mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine na Bado Unampenda?) Umejaribu sehemu Nyingi bila Mafanikio?Wasiliana na CHIEF SULTAN Akusaidie Kumshika Umpendae Asikusaliti(LIMBWATA) Kumtawala Mpenzi wako kwa sababu Maalum..Anauwezo wa Kusambalatisha Mahusiano yao ndani ya siku Moja tu.
Je Unasumbuliwa na Madeni?
Biashara yako Haina wateja?
Unatatizo la kutokushika Mimba na umehangaika sehemu nyingi bila mafanikio?
 
Wasiliana na CHIEF SULTAN Kwa Majibu ya Maswali yako..
Anasafisha NYOTA na Kutoa PETE za BAHATI kuendana na NYOTA yako. UTAJIRI USIO NA MASHARTI.(Magic Wallet_Pochi ya Maajabu Isio Isha Hela)
KUWA MAARUFU na KUJULIKANA
Kupandishwa CHEO na HESHIMA Mahala pa KAZI.
Utapewa Nguvu ya Kujilinda na MALI ZAKO zako na Mwili wako.. Huzuia Chuma Ulete katika Biashara.. Hurudisha MALI zilizo Potea au KUDHULUMIWA..
 
Mvuto wa Biashara na Mwili wako.
Hutibu kabisa Nguvu za Kiume na Kurefusha Uume kwa saizi Unayotaka.
Magonjwa Sugu(Miguu Kufa Ganzi, kisukari, Presha, Pumu nk.)Humaliza Kesi za Muda mrefu ndani ya siku 14 tu.
Anatoa NDAGU Zisizokuwa na Masharti.. Kwa maelezo Zaidi wasilina nae kwa

Whatsapp +255 0658 316 976
Call +255 755 911 233
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images