Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Marekani: Hatuna Muda Tena wa Kuivumilia Korea Kaskazini

0
0
Rais wa Marekani, Donald Trump amesisitiza kwamba muda wa kimkakati wa uvumilivu kwa Korea Kaskazini umekwisha.

Katika hotuba ya pamoja juzi, akiwa na mwenzake wa Korea Kusini, Moon Jae katika bustani ya Rose kwenye Ikulu ya White house, Trump aliahidi ‘kuchukua hatua madhubuti’ dhidi ya programu ya nyuklia na makombora ya Korea Kaskazini  akisema vitisho vyake vinafaa kupatiwa majibu ya kijasiri.

“Hizi si zama za kuvuta subira juu ya Serikali ya Korea Kusini ambayo imeshindwa kutekeleza wajibu wake,” alisema Trump.

“Imechukua miaka mingi na imeshindikana, na kwa kweli hakuna kuvuta subira hivi sasa.”

Hata hivyo, Trump amesema ni muhimu kuwe na ushirikiano katika kugawana mzigo wa kuhakikisha usalama.

Kadhalika, Rais wa Korea Kusini amesema kwamba Taifa lake litaweka marekebisho ya kiusalama na kujenga msingi dhabiti wa kujikinga.

Kiongozi huyo ameshauri kuwa ni muhimu kuendelea na majadiliano na viongozi wa Korea Kaskazini.

Trump na Moon walitofautiana jinsi wanavyotakiwa kuweka shinikizo juu ya Korea Kaskazini ili iweze kuacha kabisa programu yake ya nyuklia.

Wakati hayo yakiendelea, Korea Kaskazini imeendelea kushikilia msimamo wake wa kufanya majaribio ya makombora ya kinyuklia, huku ikiongeza ubora zaidi wa makombora yake na kudai kuwa yanafika katika kona nyingi za dunia ikiwa ni pamoja na sehemu ya Marekani.

Watanzania 18 watekwa na waasi wa Congo

0
0
Waasi wanaodaiwa wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) wamewateka madereva 21, wakiwamo Watanzania 18 wanaofanya kazi kwenye kampuni ya malori ya mizigo ya Alistair ya nchini.

Meneja usimamizi wa Tanzania na DRC wa kampuni ya Alistair , Anna Joyce Mbise aliliambia gazaeti la Mwananchi  jana kuwa  madereva hao walitekwa asubuhi ya Juni 29, baada ya mapambano kati ya askari wa Serikali ya Congo na waasi hao.

“Kwa mujibu wa maelezo ya madereva hao ni kwamba askari wa Serikali waliokuwa wanawasindikiza kabla ya msafara kuvamiwa, walizidiwa kwenye mashambulizi hayo ndipo wakatekwa,” alisema Mbise na kuongeza:

“Wametueleza kuwa hakuna aliyejeruhiwa katika tukio hilo, waasi wamekuwa wakizungumza nao vyema, lakini gari zetu tatu zimeharibika kwa risasi kutokana na mashambulizi hayo,” alisema.

Alisema kampuni hiyo imewasiliana na viongozi husika wa Serikali kwa kuandika barua Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, ili wasaidie madereva hao kuachiwa huru wakiwa salama.

“Tumejawa na hofu kuhusu usalama wao, kwani tunaamini kwamba askari wa jeshi la Serikali lazima wanajipanga kurejea kupambana ili kulikomboa eneo hilo, hapo tuna wasiwasi na usalama wa madereva hao ,” alisema.

Mratibu wa Shirikisho la Wasafirishaji Afrika Mashariki (FEARTA), Emmanuel Kakuyu alisema taarifa walizonazo ni kwamba madereva hao wamekumbwa na mkasa huo katika eneo la kijiji cha Lulimba kilichopo kati ya Ziwa Tanganyika na Kindu Manyema.

Alisema waasi hawa hawajawadhuru madereva hao, lakini alifafanua kuwa madereva watatu kati ya 21 wanatoka Uganda.

“Watekaji wamekuwa wakizungumza nao vizuri ikiwamo kuwahakikishia usalama wao wakidai kwamba hawana ugomvi nao, bali wana ugomvi na Serikali ya Congo,” alisema.

Umbali kati ya Lulimba na Kigoma ni kilomita 448, lakini ili ufike Lulimba ni lazima ulizunguke Ziwa Tanganyika upande wa mashariki mwa DRC.

Kaimu Mkurugenzi wa dawati la Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Suleiman Saleh alijibu kwa kifupi kwamba wamepokea taarifa za utekaji huo na tayari wameanza kushughulikia.

Rais Magufuli: Tanzania ni Yetu, Selous Iko Tanzania......Tuna Uhuru wa Kuamua Mambo Yetu maana Tumechoka Kuchezewa

0
0
Rais  John Magufuli amesema ujenzi wa mradi wa umeme katika maporomoko ya maji ya mto Rufiji (Stiegler’s Gorge) mkoani Pwani lazima ufanyike, akiapa kuwa inyeshe mvua au liwake jua, lazima utajengwa.

Alisema hayo jana alipokuwa akifungua Maonesho ya 41 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere (Sabasaba), barabara ya Kilwa.

Aliwaeleza wawekezaji kuwa changamoto ya umeme wa uhakika itakwisha, kwani Tanzania itakuwa na umeme wa megawati kati ya 4,000 na 5, 000 utakapokamilika mradi huo.

“Inyeshe mvua, liwake jua Stiegler’s Gorge itajengwa, tumeamua kuchukua juhudi za makusudi kuifufua na ninawahakikishia wawekezaji tunaifufua... na tunaanza kwa fedha yetu,” alisema Rais Magufuli.

Aliwahakikishia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kuwa Tanzania imejipanga vizuri, kuweka mazingira mazuri kutatua changamoto za sekta ya viwanda. 

“Moja ya changamoto kubwa ni suala la umeme, kama serikali tumeamua kuchukua jitihada za makusudi kutekeleza ahadi za Mwalimu Nyerere ya kuendeleza Stiegler’s Gorge kwa kujenga bwawa kubwa,” alisema.

Alisema ameshatoa maelekezo kwa wizara husika, pia imeundwa timu ya wataalamu wa kufuatilia na kwamba zabuni itakapotangazwa, watu wajitokeze kwa ajili ya ujenzi. 

Alisema ujenzi wa bwawa hilo, utawezesha kupatikana umeme wa megawati 2,100, ikimaanisha kuwa ni umeme utakaotosheleza mahitaji mengi, yakiwemo ya matumizi ya kawaida, viwandani na mengineyo.

“Najua wapo watakaojiuliza fedha kweli wanazo? Nataka kuwaambia fedha tunazo, haiingii akilini tunazungumzia viwanda wakati umeme hatuna,” alisema. 

Aliongeza kuwa, Serikali ikiomba fedha za mradi huo kwa wafadhili, wataweka masharti makubwa na kuambiwa mradi huo una matatizo ya kimazingira.

“Nataka kuwaambia kuwa hatutasikiliza suala la environmental impact (athari za kimazingira), Selous iko Tanzania, tunawajibu wa kuamua jambo la kufanya ambapo,”alisema Rais na kuongeza kuwa mradi huo, utatumia asilimia tatu tu ya hifadhi hiyo.

Alisema kwa watu ambao wanazingatia mambo ya kimazingira, wataona kwamba Tanzania inatunza mazingira, kwani yatapatikana maji kwa ajili pia ya uvuvi, viumbehai wengine watatumia pia maji hayo kwa kilimo.

Rais Magufuli aliwaomba wadau wa maendeleo ambao wana nia ya kuisaidia Tanzania, wajitokeze ili Watanzania wanufaike na maliasili zao. 

Alisema umeme unaopatikana sasa hapa nchini ni megawati 1,460, lakini jitihada mbalimbali zimefanyika katika kuongeza kiwango hicho, ambapo ni pamoja na kuongeza umeme katika miradi ya Kinyerezi I, II na III iliyopo Dar es Salaam, itakayoongeza upatikanaji wa umeme nchini.

Rais Magufuli waliwaomba pia mabalozi wa nchi zote zenye uwakilishi hapa nchini, kuisaidia Tanzania kupitia nchi zao katika miradi mikubwa ambayo ina tija kwa taifa zima.

 “Kwa sababu tukishaweza kuzalisha megawati 2,100 watu wengi watakuwa na umeme, nina uhakika Waziri wa Mambo ya Nje atakuwa amechukua hiyo, na pia nawaomba mabalozi wote tunahitaji msaada katika miradi mikubwa,” alisema.

Rais Magufuli alipongeza maandalizi ya maonesho hayo, ambapo baada ya kuhutubia alipita kuangalia baadhi ya mabanda na kupata maelezo mbalimbali. 

Alisema maonesho hayo yana faida kubwa kwa wafanyabiashara, kwani huwakutanisha na wateja wao na pia kukutana na kampuni nyingine za nje na ndani ya nchi, kujifunza mambo mbalimbali na pia kubadilishana uzoefu na kuanzisha uhusiano wa kibiashara.

Alizipongeza pia kampuni za ndani na zile za nje takribani 3,000, zinazoshiriki katika maonesho hayo, zikiwemo 515 kutoka katika nchi 30 duniani. Rais Magufuli alisema Tanzania ni salama na ya amani na kwamba ipo kwa ajili ya wawekezaji.

Aliwataka Watanzania kutumia maonesho hayo, kama chachu ya kuibadili Tanzania. 

“Tumechoka, tumechezewa sana, lakini tulichezewa kwa sababu tuliamua sisi kuchezewa lazima tubadilike na moyo wa kubadili Tanzania tuanze sasa,” alisema Rais Magufuli.

Waziri Mkuu Atoa Ufafazi Sakata la Kuzuia Mahindi Kuuzwa Nje ya Nchi

0
0
WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amejibu hoja zinazosambazwa na wanasiasa wa kambi ya upinzani juu ya zuio la chakula nje ya nchi, akisema Serikali haizuii fursa ya wakulima kuuza mazao nje.

Bali, amesisitiza serikali inataka mazao hayo yatosheleze nchini na kama ni lazima, basi kwanza yasindikwe, yabanguliwe, yachakatwe kwa kuyakoboa ili kuyaongezea thamani. Majaliwa alitoa kauli hiyo wakati akijibu hoja ya wapinzani, walioitisha mkutano wa waandishi wa habari juzi na kuilaumu serikali.

Alhamisi wiki iliyopita, wakati Waziri Mkuu akijibu swali la papo kwa hapo la Mbunge wa Viti Maalumu, Ritha Kabati aliyetaka kuruhusiwa kuuzwa mahindi nje ya nchi, alikataza kuuza mahindi nje ya nchi.

Alisema ni marufuku kuuza mahindi nje ya nchi; na kama ni muhimu lazima kibali kitoke kwa Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa ajili ya kuuza nje ya nchi; na uuzwe unga uliosagwa na kamwe yasiuzwe mahindi.

Waziri Mkuu alitetea kauli hiyo ya serikali jana wakati akikagua banda la Ushirika wa Wakulima Wadogo wa Kilimo cha Umwagijiaji Dakawa (UWAWAKUDA) kabla ya kufunga Maadhimisho ya Siku ya Ushirika Duniani (SUD), yaliyofanyika katika Ukumbi wa CCM wa Jakaya Kikwete mjini hapa.

Alimpongeza na kumsifu mkulima Nassib Katoto kwa niaba ya wakulima wenzake wa Mpunga Dakawa mkoani Morogoro, kutokana na kulima kilimo cha umwagiliaji, lakini hasa kuvuna mpunga, kuukoboa na kuusindika ili kupata mchele na kuuweka katika mifuko na kuuza baada ya kuongeza thamani, badala ya mpunga.

Majaliwa alisema nia ya serikali si kuzuia fursa ya wakulima kuuza mahindi nje ya nchi, bali inataka kuhakikisha kila eneo nchini linakuwa na chakula, kwani baadhi ya maeneo nchini hayana chakula kutokana na kukosa mvua na hivyo kukumbwa na ukame.

Lakini, kama ni lazima kuuza chakula nje ya nchi, basi ni vema kibali kikatolewa na Waziri mwenye dhamana kwa kuuza unga badala ya mahindi. 

Alisema mazao yakisindikwa, yakichakatwa, yakabanguliwa na yakikobolewa kama vile mahindi, viwanda vya kukoboa na kusaga vitapata kipato, watu watapata ajira na mabaki yake yaani pumba yatatumika kulisha mifugo, kuliko kama yangeuzwa mahindi, kwani viwanda visingepata kazi, vijana wasingepata ajira na mifugo isingepata chakula.

Rais Magufuli Atoa ONYO Kwa Wanasiasa Waropokaji.......Awataka Polisi Wafanye Kazi Bila Kumuogopa Mtu

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk John Pombe Magufuli ametoa onyo kali kwa wanasiasa wanaotaka sifa za kisiasa kwa kushabikia waovu hapa nchini.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa upanuzi wa bandari ya Dar es Salaam Rais amesema kuna watu wanashabikia maovu kwa kutoa matamko bila kuyapima madhara yake.

"Niwaombe wanasiasa wanaoshindwa kuzuia midomo yao, wanaosema kuwa hawa watu wameshikiliwa kwa muda mrefu, tunashindwa kujua hata kuna watu kule Marekani walikaa Guantanamo muda mrefu, katika hali hiyo kwanini usifanye watu wafikiri na wewe ni mmoja wao.Msitufanye tukafika huko"

"Kwanini hata siku moja mtu asijitokeze kulaani watu wanaouawa bila hatia kule. Lakini kwa kutaka sifa za kisiasa, mtu anatoka anasema hawa watu wako ndani muda mrefu, kuna ndugu zetu wanakufa kule...nataka polisi mfanye kazi yenu, hawa wanaoropoka waisaidie polisi, msiogope sura, awe na mwendo wa haraka, polepole au kukimbia, mkamateni ili kusudi aisaidie polisi akiwa kule ndani," amesema Rais John Magufuli na kuongeza;

"Juzi mtu amekamatwa na uniform 5000 za jeshi na inaonekana anahusika na hao walioko ndani, halafu unasema wamekaa muda mrefu, au na wewe ni miongoni mwa walioagiza hizo uniform za jeshi.

"Endeleeni kujenga heshima ya bandari, rushwa iwe ni marufuku, halafu muda pia... mtu akifika hapa akae muda mfupi na aondoke, hata kama anasafirisha pini ifike inapokwenda na sio ipotelee njiani

"Kuna vichwa 13 vya treni vimeshushwa hapa lakini havijulikani ni vya nani, tena inasemekana ni vibovu na TRL wamesema hawajaagiza na wala hawajasaini mkataba wowote.

"Hamkuuliza vya nani baada ya meli kuondoka ndio mnauliza, siku nyingine si watakuja kushusha hata na vifaru au makontena ya sumu?

"Sijui haya mavichwa mtafayanyia nini, lakini hili ni lazima lisemwe ili Watanzania wafahamu. Tutangulize uzalendo wa nchi yetu."

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu Ya July 3

Jinsi Ya Kuandaa Na Kutayarisha Lishe Maalumu Ya Kuongeza Na Kunenepesha Mwili

0
0
Kama umekonda  na  kudhoofika  mwili  kutokana  na  sababu  mbalimbali  kama  vile kuugua  magonjwa  na  maradhi  mbalimbali  au  kupatwa  na  msongo  mawazo, basi  fuata  maelekezo  yafuatayo  ili  upate  kujua  namna  ya  kuandaa  na  kutayarishe  lishe  maalumu  ya  asili  itakayo  kusaidia kunenepa  na  kurejesha  afya  ya  mwili  wako  katika  hali  yake  ya  kawaida.

MAHITAJI:
1.    Dawa  Lishe  ya  kuongeza  na  kunenepesha  mwili

2.   Asali  ya  tende

3.   Ufuta

4.     Ukwaju

5.    Kitunguu  swaumu

6.   Giligiliani

7.    Juisi  ya  Komamanga na  Asali

MATAYARISHO  NA  MATUMIZI
Matumizi  ya  lishe  hii, yame  gawanyika  katika  awamu  kuu  mbili. Awamu  ya  kwanza, itachukua  siku thelathini  na  awamu  ya  pili  itachukua  siku  thelathini pia.

Katika  awamu  ya  kwanza , mgonjwa  atatumia  DAWA  LISHE  YA  KUNENEPESHA  MWILI, ASALI  YA  TENDE  NA  UFUTA  na  awamu  ya  pili, mgonjwa  atatumia   UKWAJU, KITUNGUU  SWAUMU, GILIGILIANI  na  JUISI  YA  KOMAMANGA  & ASALI  kwa  kufuata  utaratibu  utakao  elezwa  hapo  chini.

AWAMU   YA   KWANZA
SIKU   THELATHINI  ZA  KWANZA

Mahitaji

1.   Dawa  lishe  ya  kuongeza  na  kunenepesha  mwili

2.   Ufuta

3.   Asali  ya  Tende  (   Dates  Syrup )

MATAYARISHO  , MAELEKEZO  NA  MATUMIZI
1.   Dawa –Lishe  ya  Kunenepesha  Mwili

Chukua  vijiko   vitatu vikubwa  vyenye  dawa  yako, kisha  changanya  na  maji  nusu  lita halafu chemsha  hadi  itokote, Ikiisha  tokota, ipua  acha  ipoe  kidogo kisha  tumia  kunywa  pamoja  na  machicha  yake.  Utafanya  hivyo  mara  mbili  kwa  siku  asubuhi  na  jioni  kwa  muda wa  siku  thelathini.

2.   Ufuta : Matayarisho : Chukua  vijiko  vikubwa  vinane  vyenye  ufuta, kisha  changanya  na  lita  moja  na  nusu  ya  maji. Kama  hauna  tatizo  na  sukari, unaweza  kuongeza  na  sukari  kiasi ili  kuipa  ladha.  Ikisha  tokota, ipua iache  ipoe  kiasi  kisha  tumia  kula  ufuta wote  pamoja  na  supu  yake  ama  juisi  yake. Utafanya  hivyo mara  mbili  kwa siku  asubuhi  na  jioni  kwa  muda  wa  siku  thelathini.

(N.B:   KAMA  UNA  NAFASI,  BADALA  YA  KUTUMIA  VIJIKO  VINANE  TU VYA  UFUTA  KWENYE LITA  MOJA  NA  NUSU  YA  MAJI, WEWE  TUMIA  ROBO KILO  YA  UFUTA  KWENYE  LITA  TATU  YA  MAJI, CHEMSHA  HADI  ITOKOTE,  IACHE  IPOE, KISHA  TUMIA  KULA . FANYA  HIVYO  MARA  MBILI  KWA  SIKU  ASUBUHI NA  JIONI  KWA  MUDA  WA SIKU  THELATHINI )

2.   ASALI  YA  TENDE
3.   Tumia  kula  vijiko vikubwa  vinne  vya  tende  mara  mbili  kwa siku  asubuhi  na  usiku   kwa  muda  wa  siku  thelathini. Yaani  asubuhi  kula  vijiko  vikubwa vinne  na  usiku  kula  vijiko  vikubwa vinne  vya  asali  ya  tende.

( HABARI  NJEMA  KWA  WATEJA  WETU  NI  KWAMBA, ASALI  YA  TENDE  SASA  INAPATIKANA  MOJA  KWA  MOJA  DUKANI   KWETU . UTAPATIWA  DAWA  LISHE  PAMOJA  NA  ASALI  YA  TENDE  UTAKAYO  ITUMIA  KWA  MUDA  WA  SIKU  THELATHINI  KWA  UTARATIBU  WA  MAELEKEZO  HAYO  HAPO  JUU )
AWAMU   YA  PILI
Awamu  ya  pili  ya  lishe  hii, itaanza  baada  ya  kukamilika  kwa  siku  thelathini  za  kutumia  dawa  lishe, ufuta  pamoja  na  asali  ya  tende. Kama  ilivyo  kuwa  kwa  awamu  ya  kwanza, awamu  ya  pili  pia  itachukua  muda  wa  siku  thelathini

MAHITAJI, MATAYARISHO   NA  MATUMIZI

1.  UKWAJU
Matayarisho na  Maandalizi
Chukua ukwaju  kiasi  cha  robo kilo , weka  kwenye  maji  kiasi  cha  lita  moja, ongeza pilipili  manga kiasi cha  kijiko kimoja kidogo  ( tea spoon ) halafu ongeza sukari  vijiko  vitatu vikubwa, ongeza karafuu  ya unga  kijiko kimoja kidogo, pamoja  na hiriki vijiko  vikubwa  viwili.

Ukisha  fanya  hivyo, chemsha  hadi  mchanganyiko  wako  utokote. Ukisha  tokota, ipua  na  kuchuja  kisha  weka  kwenye  chombo  kisafi.

MATUMIZI :
Tumia  kunywa  mchanganyiko  huu kila  siku  asubuhi  baada  ya  kunywa  chai. Utafanya  hivyo  kwa  muda  wa  siku  thelathini  mfululizo.

2.   JUISI   YA  KOMAMANGA  NA  ASALI
Matayarisho  na  Matumizi

Tayarisha  juisi  ya  komamanga  kiasi  cha  nusu  lita, changanya  na asali ya  kawaida  vijiko vikubwa    vinane, kisha  ongeza  chumvi kijiko kidogo( tea spoon)

Koroga  mchanganyiko  wako  halafu  tumia  kunywa. Utafanya  hivyo  mara  moja   kwa  siku kwa  muda  wa  siku thelathini.

Matunda  ya  makomamanga  yanapatikana  masokoni, ingawa  mara  nyingi  hupatikana  kwa  uchache. Kama  utabahatika  kupata matunda  mengi, basi  unashauriwa  kuyachukua  kwa  wingi  na  kuyahifadhi, sehemu  salama ili usipate  usumbufu  wakati  wa  kutumia  tiba  yako.

Mbali  na  kutumika  katika lishe  ya  kuongeza  na  kunenepesha  mwili, tunda  la  komamanga, linasaidia  kuondoa  harufu  mbaya  ya  kinywa. Kwa  kuondoa  harufu  mbaya  ya  kinywa, kula  walau  tunda  moja  la  komamanga  kwa  siku  kwa  muda  wa  siku  thelathini  mfululizo. Utapata  matokeo  mazuri . ( HII  ITAWASAIDIA  ZAIDI  WALE  AMBAO  TATIZO  LAO  LA  KUTOKWA  NA  HARUFU  MBAYA  YA  KINYWA  LIMEANZIA  KINYWANI  NA  SIO  TUMBONI

ALTERNATIVE (MBADALA )  WA JUISI  YA  KOMAMANGA  ILIYO  UNGWA  NA  ASALI.

Kama  utashindwa  kupata makoma manga, basi  utafanya  kama  ifuatavyo :

KITUNGUU  SWAUMU
Chukua punje  nne  za  vitunguu  swaumu, zitwange kisha  tia  kwenye  maji nusu lita halafu ongeza  juisi  ya  ndimu  moja  au  limao  moja kisha  chemsha hadi mchanganyiko  wako  uchemke.

Matumizi :  Tumia  hivyo kila  siku  usiku baada  ya  kula  chakula cha  usiku. Utafanya  hivyo  kwa  muda  wa  siku  thelathini mfululizo.

AU
Vile vile , mbadala  mwingine wa  kutumia  juisi  ya komamanga  iliyo  changanywa  na  asali, unaweza  kutumia  JUISI  YA  GILIGILIANI  kwa  kufuata  utaratibu  ufuatao :

JUISI   YA   GILIGILIANI
MATAYARISHO   NA   MATUMIZI YA  JUISI  YA  GILI GILIANI

Chukua giligiliani  fresh, kisha zi -blend ( ZISAGE ) ili  kupata  juice  yake  kiasi  cha  robo  lita.

 Ndani  ya  juisi  yako  ya  giligiliani, kamuliamo ndimu fresh moja, halafu  ongeza  chumvi  kiasi robo  kijiko  kidogo ( tea spoon), koroga  kisha  tumia  kunywa.  Utakunywa  usiku  baada  ya  kula  chakula  cha  usiku. Utafanya  hivyo mara   moja  kwa  siku  kwa  muda  wa  siku  thelathini  mfululizo.

PIA : Jenga  utaratibu  wa  kuwa  unakula    giligiliani kwa wingi. Hakikisha  katika  kila  mlo  wako, inakuwepo  mboga  ya  giligiliani  pembeni.

VITU   VINGINE VYA   KUZINGATIA..
Pamoja na kutumia  lishe  hii  ya  asili  kwa  kufuata  utaratibu  huo  hapo  juu, unashauriwa  kuzingatia  matumizi  ya  vyakula  vifuatavyo:

TANGAWIZI
Jenga  tabia  ya  kuwa  una tumia  tangawizi, kila  mara  upatapo  nafasi.  Utaratibu  wa  jinsi  ya  kutayarisha  tangawizi ni  kama  ifuatavyo :

Chukua kipande  kimoja  cha  tangawizi, kisha  kitwange  halafu ongeza  vikombe  viwili vya  maji  vyenye  ujazo  wa  milimita  mia  mbili  na  hamsini ( 250 mills). Chemsha pamoja  kisha ongeza  maziwa  kiasi cha  robo lita  na  sukari ili kupata  ladha.  Fanya  hivi  kila  mara  uapatapo  nafasi. Ukiweza kufanya  hivyo walau  mara  mbili  kwa  siku, itakuwa  vizuri  zaidi.

  AU  chukua  kipande  kimoja  cha  tangawizi, kitwange kisha  chemsha pamoja  na  chumvi nusu  kijiko  kidogo  kwenye  maji kiasi  cha  nusu   lita  halafu tumia  kunywa  kikombe  kimoja  nusu  saa  kabla  ya  kula  chakula chako  cha  asubuhi, mchana  na usiku.

HIRIKI
Jenga utaratibu  wa  kuwa  unakunywa  mara  kwa  mara  chai  iliyo  changanywa  na  hiriki.

MACHUNGWA
Jenga utaratibu  wa  kuwa  unakula  machungwa kwa  wingi,  kwa  kadri utakavyo  weza. Unashauriwa  kuwa  unachanganya na  chumvi  kidogo  pamoja  na  pilipili  manga.

KWA  MAHITAJI  YAKO  YA  DAWA-LISHE  YA  KUNENEPESHA  & KUONGEZA  MWILI  PAMOJA  NA  ASALI  YA  TENDE.

Kwa  mahitaji  yako  ya  DAWA-LISHE ya  kuongeza & kunenepesha  mwili, pamoja  na  asali  ya  tende, fika  katika  duka  la  NEEMA  HERBALIST.

Tunapatikana  UBUNGO  jijini  DAR  ES  SALAAM, jirani  na  SHULE  YA  MSINGI   UBUNGO  NATIONAL  HOUSING  nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA.

WASILIANA  NASI  KWA  SIMU  NAMBA  0766 53 83 84.

Kwa wateja  wetu  waliopo  jijini  Dar  Es  Salaam, ambao  hawana  nafasi  ya  kufika  dukani  kwetu  Ubungo, tunayo  huduma  ya  kuwapelekea  dawa  mahali  walipo ( HOME & OFFICE  DELIVERY  )

Kwa wateja  waliopo  nje  ya  mkoa   wa  Dar  Es  Salaam,  watatumiwa  dawa  kwa  kutumia  mabasi  mbalimbali.

Kwa  wateja  waliopo  Zanzibar, watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa  boti.

Kwa  wateja  waliopo  ughaibuni, watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  au  DHL.

Na kwa  taarifa  zaidi  kuhusu  huduma  zetu, tutembelee  kila  siku  katika  blogu  yetu :

Makamu wa Rais apaa kuelekea Ethiopia kuhudhuria mkutano wa 29 wa AU

0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan ameondoka nchini jana  jioni  kuelekea Addis Ababa, Ethiopia ambapo atahudhuria Mkutano wa 29 wa Wakuu wa  Nchi na Serikali  wa Umoja wa Afrika (AU).

Katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam, Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan aliagwa na Viongozi mbalimbali  wa Serikali.

Katika Mkutano huo wa siku mbili kuanzia tarehe 03-hadi 04 Julai-2017, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan atamuakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwenye mkutano huo.

 Kabla ya ufunguzi rasmi, Mkutano huo ulitanguliwa na vikao vya Baraza la Utendaji linalowashirikisha Mawaziri wa Mambo ya Nje na Kamati ya Uwakilishi wa Kudumu  inayowahusisha Makatibu Wakuu wa Wizara za Mambo ya Nje kutoka nchi Wanachama wa Umoja wa Afrika.

Mkutano huo wa Wakuu wa Nchi  na Serikali  utafunguliwa rasmi leo tarehe 03-Julai-2017 katika Makao Makuu ya Umoja wa Afrika Jijini Addis Ababa, Ethiopia na  utajikita katika kujadili masuala mbalimbali yanayohusu umoja huo.

Miongoni mwa mambo yatakayojadiliwa katika Mkutano huo ni pamoja na taarifa  kuhusu Maboresho katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na maboresho ya kitaasisi katika AU na  hali ya Ulinzi na Usalama katika bara la Afrika.

Kuhusu  hali ya  ulinzi na usalama katika Bara la Afrika majadiliano ya Viongozi hao yatajikita zaidi kwenye nchi za Sudan Kusini, Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo- DRC na Libya.  Aidha, majadiliano hayo pia yatagusa  hali ya usalama kwenye baadhi ya nchi ambazo ziliathiriwa na kundi la Boko Haram za  Nigeria, Niger, Chad na Cameroon.

Mkutano huo 29 wa AU, unatarajiwa kuhuduhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres na Rais wa Mamlaka ya Palestina Mahmoud Abbas.

Mkutano huo 29 wa AU utakaofanyika Jijini Addis Ababa, Ethiopia utaongozwa na Mheshimiwa  Alpha Conde  Rais wa Jamhuri ya Guinea ambaye ndiye Mwenyekiti wa AU.

Kauli Mbiu ya Mkutano huo ni Kuimarisha Mgawanyiko wa Idadi ya Watu Kupitia Uwekezaji katika Vijana (Harnessing Demographic Divident Through Investments in the Youth)

Imetolewa na Ofisi ya Makamu wa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
ADDIS ABABA- ETHIOPIA.   

Uchaguzi mkuu TFF wasimamishwa

0
0
Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Soka nchini (TFF) imesimamisha shughuli zote za uchaguzi kuanzia jana Jumapili hadi Julai 4 ambapo watakaa kikao cha kamati hiyo na kutoa maamuzi yatakayofikiwa kuhusu mchakato huo.

Sababu kubwa imeelezwa kuwa ni wajumbe wa kamati ya uchaguzi ya TFF kukataa majina ya baadhi ya wagombea kwa sababu binafsi. 

Revocatus Kuuli ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi amesema kutokuwa na maelewano kumemsababisha achukue uamuzi wa kuuandikia barua Kamati ya Utendaji akiiomba isitishe mchakato wa uchaguzi (kwakuwa kanuni zilizopo zinamruhusu kufanya hivyo) japo kumekuwa na taarifa kuwa Bwana Kuuli alitofautiana na wajumbe wengine wa Kamati ya Uchaguzi kuhusu hatma ya Rais wa Shirikisho hilo, Jamal Malinzi ambaye alichukua fomu kutaka kutetea kiti chake.

Mgogoro uliosababisha kutoelewana huku umetokana na wajumbe wanne kati ya watano kutaka jina la Rais wa sasa, Jamal Malinzi, lipitishwe bila kuwapo – jambo ambalo Revocatus Kuuli anasema si sahihi kikanuni.

 Kamati ya Uchaguzi ya TFF ina wajumbe watano. Kwa sababu hiyo, Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi Mkuu wa TFF Revocatus Kuuli akaiandikia barua Kamati ya Utendaji ya TFF akitaka mchakato mzima wa uchaguzi usimamishwe na kuangalia kama Sheria za zoezi zima zinazingatiwa.

“Kikao chetu cha leo kimefanyika lakini hakijatoa maamuzi ya matatizo yaliyotokea jana.”

“Mimi kama Mwenyekiti wa Kamati nimechukua maamuzi ya dhamana niliyonayo. Nimemuandikia Katibu juu ya dhamira yangu kuangalia upya mwenendo mzima wa kamati. Wamekubaliana na maombi yangu na wamenipa barua kwamba wanaona sahihi mchakato mzima usimame mpaka matatizo yaliyotokea yatakapopelekwa kwenye Kamati ya Utendaji ambayo ndio yenye mamlaka ya mwisho.”

“Wamesema wataitisha kikao Julai 4, 2017 (Jumanne ijayo). Matatizo yalikuwa mengi, kuna watu wamekatakata majina kwa uonevu tu. Taratibu zinataka kupindishwa kwa sababu ya kutaka kupendelea watu fulani.”

“Mimi siwezi kuwa sehemu ya kamati ambayo ipo namna hii, kwa hiyo nashukuru barua yangu imepokelewa na imefanyiwa kazi kama nilivyokuwa nimetaraji.”

Julai 4, 2017 baada ya Kamati ya Utendaji kukaa na kujadili mgogoro huo uamuzi wa kuendelea au kutoendelea kwa mchakato wa uchaguzi huo utatolewa.

Kaimu Katibu Mkuu wa TFF Salum Madadi amesema amekubali ombi la Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi kuhusu kusimamisha mchakato wa uchaguzi wa TFF kutokana na kutofautiana kwa wajumbe wa kamati hiyo.

Madadi amesema Kamati ya Utendaji ya TFF itakutana Jumanne Julai 4, 2017 kwa ajili ya kulitolea uamuzi suala hilo.

“Kumetokea mgawanyiko ndani ya kamati yetu ya uchaguzi, Mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi ametuandikia barua na tumeshauriana naye kusitisha mchakato wa uchaguzi na tumeitisha kikao cha dharura cha kamati ya utendaji ya TFF tarehe 4 Julai, 2017 saa 7:00 mchana.”

“Baada ya kikao cha dharura cha Kamati ya Utendaji tutakuwa na cha kusema kuhusu mchakato wa uchaguzi,” alisema Madadi.

Rais Magufuli Kuzindua Mradi Mkubwa wa Maji Sengerema Kesho

0
0
Rais John Magufuli anazindua mradi mkubwa wa maji katika kijiji cha Nyamazugo wilayani Sengerema kesho.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, Mkuu wa Wilaya ya Sengerema, Emmanuel Kipole alisema jana kuwa, Rais Magufuli atafika wilayani hapo saa mbili kwa ajili ya uzinduzi huo.

Mradi huo ulioanza kutekelezwa tangu mwaka 2014 kwa gharama ya Sh23 bilioni utawanufaisha zaidi ya wakazi wa wilaya hiyo zaidi ya 13,000.

“Lakini akiwa njiani kuelekea katika tukio la kuzindua mradi huo atasalimiana na wananchi barabarani kadri itakavyowezekana na baada ya kuzindua mradi huo atawahutubia wananchi wa Sengerema na viunga vyake hivyo wananchi wajitokeze kwa wingi,” alisema Kipole.

Kipole alisema wilaya hiyo ina jumla ya wakazi 74,186 kutokana na Sensa ya Watu na makazi ya mwaka 2002, hivyo mradi huo kwa sasa utahudumia kata 11.

Kata hizo ni Sima, Nyatukala, Ibisabageni, Mwabaruhi, Nyampulukano, Misheni, Tabaruka, Nyampande, Nyamazugu, Nyamazeze na Ibondo.

Mhandisi wa Maji Wilaya ya Sengerema, Nikas Ligombi alisema mradi huo uliofadhiliwa na Benki ya Afrika umekamilika kwa asilima 100 na utakapozinduliwa rasmi tatizo la maji katika mji wa Sengerema litakuwa limepatiwa ufumbuzi.

“Lita za ujazo 150,000 zitakuwa zinasukumwa kila siku kutoka kwenye chanzo cha maji kwenda kwenye matanki ya kusambaza mitaani,” alisema Ligombi.

Mkuregenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Sengerema, Magesa Mafuru alisema ni fahari kubwa kukamlika kwa maradi huu ambao utamaliza matatizo ya maji yaliyokuwa yakiukabili mji huo na kuwataka wananchi kuutunza na kuuthamini ili udumu kwa muda mrefu.

Mmoja wa wakazi wa mjini humo, Jumanne Kashiba alisema baada ya mradi huu kukamilika tatizo la maji mjini hapo lilokuwa likiwakabili litakoma na kuipongeza serikali kwa jitihada hizo.

Ongeza Makalio, Punguza Unene, Punguza Matit na Refusha Nywele kwa Dawa za Asili Kabisa

0
0
AFRICAN BEAUTY EXPRESS PRODUCTS
,dada kama unahitaji kuwa mrembo💃🏼na baba kama unahitaji kuonekana king👑ndani ya ndoa yako fika AFRICAN BEAUTY ndiyo habar ya wakali wote mjini,kwa products original na zenye matokeo yaharaka🔥
 
1)kuongeza hips na makalio@100000/=
2)kuongeza hipsi,makalio na mapaja@150000/=
3)kuongeza miguu(Chupa ya bia)@120000/=
4)kupunguza unene 25kg per wiki@150000
5)kuwa mweupe mwili mzima bila DOA,michiriz@150000
6)kuongeza unene na urefu wa uume
(a)inch7 kwa cm3@100000/=
(b)inch8 kwa cm4@130000/=
7)kuongeza nguvu za uume@100000/=
8)kupunguza au kuongeza matiti@100000/=
9)kurefusha nywele@100000/=
10)kungarisha meno,kufanya lips kuwa pink@80000/=
11)kuondoa michirizi sugu@100000/=huduma yetu niuhakika %na dawa zetu ni original matokeo wiki moja unaanza kuyaona,tuna tuma bidhaa mikoa yote,nje ya nchi tunatuma kwa DHL,dar free deliver,tunapatikana kariakoo Kongo na mlimani city ☎whatsapp+255756697906,📞0716805391 au unaweza kutufollow👇👇👇👇👇👇👇
@afric_is_beauty
@afric_is_beauty
@afric_is_beauty

SUMAYE: Watawala hawataki Madaraka yao Yadhibitiwe na Katiba.

0
0
Waziri  Mkuu wa zamani, Frederick Sumaye, amesema Katiba mpya imewekwa pembeni, kwani watawala hawataki madaraka yao yadhibitiwe na Katiba.

Sumaye, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Kanda ya Pwani, alisema hayo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam, kwenye mahafali ya vijana wa chuo kikuu wa chama hicho (Chaso).

Alisema Katiba inayopendekezwa ni ya wananchi na ilipitishwa na Bunge, lakini inaonekana si jambo la kipaumbele na wala haitashughulikiwa tena kwa sababu itawadhibiti watawala.

“Mchakato wa Katiba mpya umeigharimu nchi fedha nyingi za walipa kodi na kuitupa ni “makanikia” nyingine, najua Rais John Magufuli  amekwishasema yeye haambiwi la kufanya, lakini sisi tutaendelea kumkumbusha yale ambayo tunadhani ni muhimu kwa mustakabali wa Taifa letu.

“Si jambo la kupuuzwa. Kama ni la kupuuzwa basi awakamate wote waliohusika na uamuzi huo, maana ni ubadhirifu unaofanana na ule wa makanikia,” alisema.

Mwenyekiti huyo alisema chama hicho pamoja na washirika wake wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) wataendelea kudai Katiba mpya hadi itakapopatikana.

Alisema licha ya watawala kueleza kwamba Tanzania ina mfumo wa vyama vingi, hata hivyo si kweli, bali ina mfumo ‘bandia’ wa siasa za vyama vingi.

“Tuna mfumo ‘bandia’ wa siasa ya vyama vingi, mfumo wa chama kimoja kilichovaa ngozi ya vyama vingi, mfumo wa vyama vingi vya siasa ni lazima ufuate utawala wa sheria na unaolinda, unaoheshimu na kuitetea Katiba ya nchi ambayo watawala wameapa nayo wakati wa kukabidhiwa madaraka.

“Ukiona katika nchi watawala hawatii sheria wala katiba ya nchi, basi hakuna utawala wa kweli wa vyama vingi vya siasa, bali kuna utawala wa imla uliovaa ngozi ya demokrasia ya vyama vingi vya siasa.

“Tanzania leo hakuna uhuru wa watu kutoa na kupokea habari kama Katiba yetu inavyotaka. Ibara ya 18 ambayo inazungumzia “Haki na Uhuru wa Mawazo,” alisema.

Alisema mfumo au demokrasia ya vyama vingi haurusu ubabe katika utawala na uongozi wa nchi.

“Kama kiongozi anatawala kwa ubabe na vitisho, lazima tukubali kuwa ama Katiba tuliyonayo siyo sahihi au mfumo uliopo siyo wa demokrasia ya vyama vingi kivitendo,” alisisitiza.

Qatar yapewa masaa 48 kutimiza masharti

0
0
Qatar imepewa masaa 48 kutimiza masharti 13 iliyopewa na nchi za Kiarabu ikiwemo kukifunga kituo chake cha habari cha Alja Zeera vinginevyo itaongezewa masharti mengine ambayo yataisababishia matatizo makubwa ya mahusiano na nchi hizo.

Nchi hiyo  imesema kwamba leo itatoa majibu kuhusu masharti hayo.i.

Majibu hayo yatazingatia masharti 13 yaliyotolewa baadhi yakiwa ni kufunga televisheni ya Al Jazeera, kufunga kambi ya kijeshi ya Uturuki jijini hapa, kusitisha ufadhili kwa vikundi vya kigagidi na vyenye msimamo mkali, na kupunguza uhusiano wake na Iran.

Qatar iliwekewa masharti hayo na mataifa sita yakiongozwa na Saudi Arabia. Mataifa mengine matatu ya Kiarabu yaliwakilisha masharti 13 kwa Qatar kama milango ya kutatua mzozo unaoikumba ghuba hiyo.

Mataifa mengi ya ghuba yalitangaza kusitisha uhusiano wao wa kidiplomasia na Qatar kwa madai taifa hilo linajihusisha kuunga mkono makundi ya kigaidi, jambo ambalo Doha imekanusha na kutaka nchi hizo kutoa ushahidi wa kutosha. 

Mbali ya kuvunja uhusiano wa kidiplomasia, pia zilifunga mipaka na usafiri wa anga, bahari na ardhi.

Tarehe ya mwisho iliyowekwa na mataifa hayo kwa Qatar kutoa jibu ilikuwa jana Julai 2, lakini  iliongezewa  masaa 48

Yaliyojiri Bungeni Wakati Wa Uwasilishwaji Wa Maoni Na Ushauri Wa Kamati Ya Bunge Ya Pamoja Kuhusu Muswada Wa Sheria Ya Mamlaka Ya Nchi Kuhusiana Na Umiliki Wa Maliasili

0
0
*YALIYOJIRI BUNGENI WAKATI WA UWASILISHWAJI WA MAONI NA USHAURI WA KAMATI YA BUNGE YA PAMOJA KUHUSU MUSWADA WA SHERIA YA MAMLAKA YA NCHI KUHUSIANA NA UMILIKI WA MALIASILI WA MWAKA 2017,LEO TAREHE 03 JULAI, 2017*.

==>Mhe. Spika aliunda Kamati ya pamoja iliyojumuisha Kamati nne za Bunge.

#Kamati hizo ni:

(a) Kamati ya kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini;

(b) Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria;

(c)Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi,Maliasili na Utalii; na

(d) Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo.

==>Maudhui ya Muswada huu yanalenga kuzingatia matakwa ya kisheria ambavyo yanawekwa na Ibara ya 27 ya Katiba inayotoa wajibu kwa kila Mtanzania kulinda na kusimamia rasilimali za Umma.

==>Uchambuzi wa Muswada huu ulishirikisha wadau wa aina mbalimbali waliotoa maoni kwa njia ya majadaliano ya pamoja kwa moja kwa moja na kwa njia ya maandishi.

==>Kamati inashauri Serikali kuhakikisha utungaji wa Kanuni unafanyika mapema ili kuwezesha utekelezaji bora na wa haraka wa sheria itakayotokana na Muswada huu.

==>Serikali ianze haraka mchakato wa ujenzi wa mitambo ya kuchakata/kuchenjua Mali ghafi za raslimali nchini,ili kuwezesha wavunaji na raslimali hizo kupata huduma hiyo hapa nchini.

==>Serikali iimarishe Mfumo wa utendaji wa benki na taasisi za kifedha ili kuongeza ufanisi katika kuhudumia taasisi mbalimbali na makampuni makubwa ya uwekezaji nchini.

==>Serikali iboreshe zaidi mifumo na uwezo wa Mahakama na vyombo vingine vya utoaji haki nchini ili viweze kushughulikia mashauri yanayojitokeza na yatakayoweza kujitokeza kutokana na masharti ya uwekezaji yanayotamkwa katika Muswada huu.

*Imeandaliwa na Idara ya Habari-MAELEZO*.

Yaliyojiri Bungeni Katika Kikao Cha 58 Cha Mkutano Wa Saba Wa Bunge La 11 Leo Tarehe 03 Julai, 2017

0
0
*YALIYOJIRI BUNGENI KATIKA KIKAO CHA 58 CHA MKUTANO WA SABA WA BUNGE LA 11 LEO TAREHE 03 JULAI, 2017*.

1.Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ndiyo yenye jukumu kuu kisheria la kukusanya mapato ya Serikali.

2.TRA ilianza rasmi kukusanya kodi ya majengo kwa Halmashauri 30 kati ya 183 kuanzia Octoba 2016.

3.Katika kipindi cha Julai-Septemba, 2016,Halmashauri 30 ziliweza kukusanya shilingi milioni 3,399 sawa na asilimia 24 ya lengo la kukusanya milioni 14,502.

4.Kati ya Octoba 2016 hadi Aprili 2017, jumla ya Shilingi Milioni 10,652.6 zilikusanywa sawa na aslimia 22.0 ya lengo la kukusanya Shilingi Milioni 48,340.2.

5.Ufanisi huu ni sawa na wastani wa makusanyo ya Shilingi Milioni 1,521.8 kwa mwezi.

6.TRA imekusanya kodi ya majengo kwa ufanisi zaidi ikilinganishwa na Halmashauri.

7.Serikali imeaainisha maeneo yote nchini yanayofaa kwa Kilimo cha umwagiliaji na kuandaa Mpango Kabambe wa kuendeleza Kilimo cha umwagiliaji.

8.Mpango huu utahusisha matumizi ya maji ya maziwa makuu ikiwemo Ziwa Victoria kwa ajili ya umwagiliaji wa kutumia teknolojia zinazotumia maji kwa ufanisi.

9.Awamu ya tatu ya Mradi wa Usambazaji Umeme Vijijini (REA) umeanza kwa Nchi nzima tangu Mwezi Machi, 2017.

10.Serikali imeweka utaratibu ambapo posho za viongozi wa Serikali za Vijiji na Vitongoji zinalipwa na Halmashauri kupitia asilimia 20 inayotengwa kutokana na mapato ya ndani ya Halmashauri na kurejeshwa kwenye Vijiji.

11.Serikali inakusudia kuliweka kwenye Sheria ya Fedha suala la kutenga asilimia 20 kama posho za viongozi wa Serikali.

12.Serikali imetenga Shilingi Milioni *557.3* kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba pamoja na ujenzi wa vituo vya Afya na Zahanati.

13.Katika mwaka 2015/16 jumla ya meta za ujazo wa miti zipatazo *767,946.46* zilivunwa kutoka kwenye mashamba ya Serikali na kuingizia Serikali jumla ya Shilingi *58,312,894,416.20*

14.Mapato yanayotokana na zao la mbao,ni wastani wa Shilingi *Bilioni 18.3* kwa mwaka.

*Imeandaliwa na Idara ya Habari-MAELEZO*

Vigogo wa IPTL (Rugemarila na Seth) Wapandishwa Mahakamani Tena na Kuongezewa Mashitaka

0
0
Mfanyabiashara  Harbinder  Singh Sethi na James  Rugemalira wamepandishwa kizimbani kwa mara nyingine katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na mashtaka 12, badala ya mashtaka sita waliyosomewa awali.

Miongoni mwa mashtaka hayo 12 ya  uhujumu uchumi yamo mashtaka matano ya kutakatisha fedha na kuisababisha hasara ya USD 22, 198, 544.60 na Sh 309,461,300,158. 27.

Akiwasomea hati mpya ya mashtaka, Wakili wa Serikali Mwandamizi, Shedrack Kimaro kwa Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi alidai wanakabiliwa na mashtaka ya kula njama, kujihusisha mtandao wa uhalifu, kighushi,  kutoa nyaraka za kughushi, kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu, kuisababishia Serikali hasara na kutakatisha fedha.

Washtakiwa hao katika shtaka la kwanza wanadaiwa, Rugemarila ambaye ni Mkurugenzi wa VIP na mmiliki mwenza wa zamani wa IPTL, Sethi ambaye ni Mwenyekiti Mtendaji wa PAP wanadaiwa kuwa   kati ya Oktoba 18, 2011 na Machi 19, 2014 jiji Dar es Salaam walikula njama katika nchi za Afrika Kusini, Kenya na India ya kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.

Kimaro alidai katika shtaka la pili la kujihusisha na mtandao, washtakiwa hao kati ya Oktoba 18, 2011na Machi 19, 2014 jijini Dar es Salaam wakiwa siyo watumishi wa umma na watumishi wa umma  walitekeleza mtandao huo wa uhalifu kwa lengo la kujipatia faida.

Kwa upande shtaka la tatu, Sethi  anadaiwa  kuwa   Oktoba 10, 2011 katika mtaa wa Ohio Ilala Dar es Salaam akiwa na nia ya ulaghai alighushi fomu namba 14 ya usajili wa makampuni  na kuonyesha yeye ni mtanzania anayeishi Kitalu namba 887 Mtaa wa Mrikau Masaki wakati akijua ni uongo.

Seth katika shtaka la nne anadaiwa kutoa nyaraka ya kughushi ambayo ni fomu namba 14a ya usajili wa kampuni kwa ofisa msajili wa kampuni, Seka Kasera kwa njia ya kuonyesha kwamba yeye ni mtanzania na Mkazi wa Mtaa wa Mrikau.

Katika shtaka la tano, washtakiwa wote, wanadaiwa kuwa kati ya  Novemba 28/29, 2011 na Januari 23, 2014 makao makuu Benki ya Stanbic Kinondoni  na Benki ya Mkombozi Tawi St Joseph kwa ulaghai washtakiwa hao walijipatia kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BoT), walijipatia USD 22,198,544.60 na Sh 309, 461,300,158.27. 

Katika shtaka sita la kusababisha hasara,  washtakiwa hao wanadaiwa kuwa   Novemba 29, 2013 katika Benki ya Stanbic tawi la  kati Kinondoni kwa vitendo vyao waliisababishia Serikali hasara ya USD 22, 198, 544.60 na Sh 309,461,300,158.27.

Kimaro alidai katika la saba, kuwa kati ya Novemba 29, 2013 na Januari 23, 2014 maeneo tofauti Dar es Salaam kwa pamoja walitenda kosa la kutakatisha fedha kwa kuchukua fedha kutoka BoT USD 22,198,544.60 na Tsh 309,461,300, 158.27 wakati wakijua fedha hizo zao la kujihusisha na genge la uhalifu.

Shtaka la nane, Kimaro alidai kuwa Novemba 29, 2013 katika tawi la kati la Benji ya Stanbic Tanzania Wilaya ya Kinondoni Sethi alitakatisha fedha kwa kuchukua BoT USD 22,198,544.60 wakati akijua fedha hizo zimetokana na zao la kujihusisha na genge la uhalifu.

Kwa upande wa shtaka la tisa, Sethi anadaiwa kuwa kati ya Novemba 29, 2013 na Machi 14,2014 katika tawi la kati la Benji ya Stanbic Kinondoni Dar es Salaam alitakatisha fedha, Sh 309,461,300,158.27 kutoka BoT wakati akijua fedha hizo zimetokana na zao la kujihusisha na genge la uhalifu.

Shtaka ya kumi,  inadaiwa Januari 23, 2014 katika Benki ya Mkombozi tawi la St Joseph Cathedral, Rugemalila  alitakatisha fedha, Sh 73, 573, 500,000 kutoka kwa Seth wakati akijua fedha hizo zimetokana na zao la kujihusisha na genge la uhalifu.

Kwa upande wa shtaka la 11, Kimaro alidai kuwa Januari 23,2014 katika Benki ya Mkombozi tawi la St Joseph Cathedral, Rugemarila alitakatisha fedha USD 22,000,000 kutoka kwa Seth wakati akijua fedha hizo ni zao la uhalifu.

Shtaka la 12, Seth anadaiwa kuwa Januari 28, 2014 katika tawi la kati la Benki ya Stanbic Wilaya ya Kinondoni alihamisha Rand (zar 1,305,800 kwenda kwenye akaunti namba 022655123 katika Standard bank Land Rover Sandton Johannesburg wakati akijua katika kipindi anahamisha fedha hizo zimetokana na zao la kujihusha na genge la uhalifu.

Washtakiwa hawakuruhusiwa kuongea chochote kwa sababu mahakama ya Kisutu haina mamlaka ya kusikiliza kesi hao.

Upande wa mashtaka ulidai upelelezi bado haujakamilika na washtakiwa wamepelekwa rumande hadi Julai 14, 2017.

Hata hivyo mashtaka ya kutakatisha fedha yanayowakabili washtakiwa hao hayana dhamana.

CHADEMA Watishia Kuandamana....Polisi Watoa ONYO

0
0

Baraza la  Vijana la Chadema(Bavicha), wamesema wanatarajia kufanya maandamano ya amani yenye lengo la kuipongeza kambi rasmi ya upinzani bungeni.

Akizungumza leo Jumatatu katika mahafali ya Umoja wa Wanachama wa Chadema Vyuo Vikuu (CHASO), Mkoa wa Kilimanjaro, Katibu Mwenezi wa Bavicha, Edward Simbeyi alisema kuwa watafanya maandamano mapema mwa mwezi huu ili kuipongeza kambi hiyo ambapo amesema imekuwa ikipigania rasilimali za nchi.

Simbeyi ambaye ni mratibu wa CHASO taifa,alisema wanakusudia kufanya hivyo kama chama cha CCM  kilivyofanya maandamano ya kumpongeza Rais Magufuli kwa kuzuia mchanga wa madini (Makinikia).

Alisema kuwa wabunge wa upinzani wamekuwa wakipambana kwa kujenga hoja  bungeni kuhakikisha wananchi wananufaika na rasilimali zao wenyewe badala ya watu wachache kunufaika.

Hata hivyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Hamis Issah alisema kuwa maandamano yalishapigwa marufuku na  hayaruhusiwi kufanyika mahali popote.

“Kama walijitokeza watu wakitaka kufanya maandamano ya kumpongeza Rais wakazuiliwa na wao pia wasijaribu kufanya hivyo,”alisema Issah.

Rais wa TFF Jamal Malinzi na Katibu Wake Wanyimwa Dhamana na Kurudishwa Rumande

0
0
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi na Katibu Mkuu wa shirikisho hilo Selestine Mwesigwa wamenyimwa dhamana kwa kesi inayowakabili, wamerudishwa rumande mpaka Julai 17 mwaka huu shtaka lao litakaposomwa tena.

Uamuzi huo umetolewa na Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Kisutu Jijini Dar es Salaam, Wilbard Mashauri baada ya mabishano makali ya kisheria dhidi ya mawakili wa utetezi na mawakili upande wa jamhuri (serikali).

Malinzi na Mwesigwa walishikwa na Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU) mnamo Juni 27 kwa kutuhumiwa matumizi mabaya ya madaraka waliyokuwa nayo katika uongozi wao na kupandishwa Mahakamani kwa mara ya kwanza mnamo Juni 29 na kusomewa mashtaka 28 ya kughushi na kutakatisha fedha kupitia akaunti ya TFF.

Kutana Maajabu ya Mtabibu CHIEF SULTAN(MAKATA WA MAKATANI) Mganga wa Waganga Sasa Yupo Mikoa Yote Tanzania

0
0
Pia anatoa Tiba kwa Njia ya Simu ukiwa popote Pale Tanzania au Nje ya Tanzania..

CHIEF SULTAN ni Mtabibu na Mtafiti wa Dawa za Asili ya Africa, na Duniani Katika utoaji wa Tiba za Asili..
Je unasumbulia na Mapenzi..?
 
(Umeachwa na Umpendae awe Mume/ Mke au mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine na Bado Unampenda?) Umejaribu sehemu Nyingi bila Mafanikio?Wasiliana na CHIEF SULTAN Akusaidie Kumshika Umpendae Asikusaliti(LIMBWATA) Kumtawala Mpenzi wako kwa sababu Maalum..Anauwezo wa Kusambalatisha Mahusiano yao ndani ya siku Moja tu.
Je Unasumbuliwa na Madeni?
Biashara yako Haina wateja?
Unatatizo la kutokushika Mimba na umehangaika sehemu nyingi bila mafanikio?
 
Wasiliana na CHIEF SULTAN Kwa Majibu ya Maswali yako..
Anasafisha NYOTA na Kutoa PETE za BAHATI kuendana na NYOTA yako. UTAJIRI USIO NA MASHARTI.(Magic Wallet_Pochi ya Maajabu Isio Isha Hela)
KUWA MAARUFU na KUJULIKANA
Kupandishwa CHEO na HESHIMA Mahala pa KAZI.
Utapewa Nguvu ya Kujilinda na MALI ZAKO zako na Mwili wako.. Huzuia Chuma Ulete katika Biashara.. Hurudisha MALI zilizo Potea au KUDHULUMIWA..
 
Mvuto wa Biashara na Mwili wako.
Hutibu kabisa Nguvu za Kiume na Kurefusha Uume kwa saizi Unayotaka.
Magonjwa Sugu(Miguu Kufa Ganzi, kisukari, Presha, Pumu nk.)Humaliza Kesi za Muda mrefu ndani ya siku 14 tu.
Anatoa NDAGU Zisizokuwa na Masharti.. Kwa maelezo Zaidi wasilina nae kwa

Whatsapp +255 0658 316 976
Call +255 755 911 233

Habar Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya July 4

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images