Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Mfanyabiashara Afikishwa Mahakamani Kwa Kukutwa na Sare 5000 za JWTZ

$
0
0
Mfanyabiashara  wa Kariakoo, Casto Ngogo (35) amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na mashitaka ya kukutwa na vifaa vya serikali ambavyo ni suruali 5,000 sare za Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Ngogo ambaye ni mkazi wa Tabata Segerea alifikishwa mahakamani hapo jana mbele ya Hakimu Mkazi, Victoria Nongwa na kusomewa mashitaka yake na Wakili wa Serikali, Hamisi Saidi.

Akisoma mashitaka, Wakili Saidi alidai Juni 15, mwaka huu maeneo ya bandari kavu ya Galco iliyopo Chang’ombe wilaya ya Temeke, Dar es Salaam, Ngogo alikutwa na suruali 5,000 za JWTZ kwenye kontena namba PCIU 82851 (5) za thamani ya Sh milioni 59 mali ya serikali bila kuwa na kibali.

Mshitakiwa alikana mashitaka hayo upande wa mashitaka ulidai kuwa upelelezi wa shauri hilo haujakamilika na kwamba hawana pingamizi ya dhamana. 

Hakimu Nongwa alitaja masharti ya dhamana kwa mshitakiwa kuwa na fedha taslimu Sh milioni 30 au hati ya mali isiyohamishika ya thamani hiyo pamoja na wadhamini wawili watakaosaini bondi ya Sh milioni 10 kila mmoja. 

Ngogo alitimiza masharti hayo na kuachiwa huru ambapo kesi hiyo imeahirishwa hadi Julai 17 mwaka huu kwa ajili ya kutajwa.

Kamisha Siang’a asema wauza ‘Unga’ walijaribu kumuua wiki iliyopita......Asimulia Wanavyoishi Kifahari Gerezani

$
0
0
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya, Rogers Siang’a amesema kuwa wafanyabiashara wa dawa za kulevya walitaka kumuua wiki iliyopita.

Kamishna Siang’a ameeleza hayo katika mahojiano maalum aliyofanya na gazeti la Mwananchi kuhusu maendeleo ya vita dhidi ya biashara hiyo haramu, ikiwa ni takribani miezi mitano tangu ateuliwa kuongoza kitengo hicho nyeti.

“Wiki iliyopita tu hapa [wauza dawa za kulevya] walitaka kuniua,” alisema Siang’a ingawa hakueleza kwa kina kuhusu jaribio hilo baya dhidi yake. “Wanaofanya biashara hii wana uwezo wa kufanya chochote wanachotaka. Kabla jamii haijatuhukumu ni vyema ikatambua kuwa tuna changamoto kubwa,” aliongeza.

Katika hatua nyingine, Kamishna Siang’a alisema kuwa wanaofanya biashara hii haramu ni watu wakubwa ambao hufadhili kazi za Serikali, viongozi wanaowalina na madhehebu mbalimbali ya dini.

Alisema kuwa yupo mfanyabiashara mkubwa wa dawa za kulevya ambaye alikuwa akionekana kama mtu mwema sana kwenye jamii, akifadhili taasisi moja ya Serikali pamoja na kuwasomesha watoto wa vigogo na kufadhili shughuli zao za harusi, lakini ameshakamatwa na anatumikia kifungo cha maisha jela.

Hata hivyo, Siang’a alisema kuwa wamepata taarifa kuwa mfanyabiashara huyo anaishi maisha ya kifalme gerezani na kwamba huenda hata usiku halali ndani ya gereza hilo.

“Tunapata taarifa kuwa anahudumiwa vizuri gerezani, na inavyosemekana kuwa huenda halali hata huko. Anachukuliwa usiku na kupelekwa kwake kulala, asubuhi anarudishwa,” alisema.

Alitoa mfano mwingine wa nguli wa dawa za kulevya aliyefungwa gerezani, kuwa kabla ya kuingia alikarabati gereza na kukodisha nyumba za jirani kwa ajili ya kuweka watu ambao watakuwa wanampikia vyakula, hivyo ameendelea kuwa na afya nzuri akiwa gerezani.

Alisema hayo yote hufanyika kwa ushirikiano wa baadhi ya askari wa gerezani na wakuu wa gereza husika.

Kamishna Siang’a alisema kuwa Mamlaka hiyo hairudishwi nyuma na kwamba hadi sasa wameshawakamata vinara 15 wa dawa za kulevya ambao amewataja kama watu wenye jeuri ya pesa.

Chanzo: Mwananchi

Mahakama yaruhusu kura ya siri ya kutokuwa na imani na Zuma

$
0
0
Mahakama ya juu zaidi nchini Afrika Kusini imeamuru kuwa kura ya kutokuwa na imani na Rais Jacob Zuma inaweza kufanywa kwa siri.

Akitoa uamuzi huo Jaji mkuu Mgoeng Mgoeng alisema kuwa spika wa bunge ana mamlaka ya kuamua ni njia gani kura hiyo itafanyika.

Bwana Zuma amekuwa chini ya shinikizo kufuatia shutuma nyingi ikiwemo madai ya ufisadi na mabadiliko kwa baraza la mawaziri yaliyokumbwa na utata.

Vyama vya upinzani vinaamini kuwa chini ya kura ya siri, wabunge kutoka chama cha Zuma cha ANC wanaweza kupiga kura ya kumpinga.

Spika wa bunge Baleka Mbete alikuwa amedai kuwa sheria za bunge haziruhusu kufanyika kura ya siri lakini sasa itatagazwa tarehe mpya ya kura hiyo.

Mkuu wa Majeshi aahirisha ziara yake Kibiti

$
0
0
Mkuu wa Majeshi nchini, Jenerali Venance Mabeyo ameahirisha kufanya mazungumzo na wazee wa Kibiti.

Mkuu wa Wilaya ya Kibiti, Gullamuhusein Kifu amesema ni kutokana na mkuu huyo kupangiwa majukumu mengine ya kikazi.

Awali, Mabeyo alitarajiwa kufika Kibiti kufanya mazungumzo na wazee kwa ajili ya kuimarisha hali ya usalama mkoani humo ambamo kumekuwa na mfululizo wa mauaji hasa ya viongozi wa vijiji.

Rais Magufuli afanya ziara ya kushtukiza kiwanda cha viuatilifu vya malaria Kibaha

$
0
0
Rais John Magufuli amefanya ziara ya kushtukiza katika kiwanda cha kutengeneza dawa za kuulia vimelea vya mbu wanaosababisha malaria kilichopo Kibaha, Pwani.

Magufuli amevamia katika kiwanda hicho leo (Alhamisi) katika siku ya mwisho ya ziara yake mkoani Pwani na kuzipa siku 10 halmashauri, manispaa na majiji nchini kwenda kuchukua dawa hizo za kuua vijidudu vya malaria na kuzipulizia katika maeneo yao yalipo makazi ya watu.

“Sasa mimi nimeshatoa agizo dawa zilipiwe, sasa nione mkurugenzi ambaye atashindwa kutekeleza agizo langu la kufata dawa hizo kwa kipindi nilichotoa, nimesema natoa muda mpaka  mwisho wa mwezi, "amesema Rais Magufuli.

Kadhalika, Rais ameiagiza Wizara ya Fedha kutoa Sh1.3 bilioni  kwa ajili ya kulipia lita 100 ya dawa  hizo za kuua vimelea vya mbu zilizopo katika kiwanda hicho.

Awali, Kaimu Meneja wa kiwanda hicho, Samweli Mziray alimweleza Rais kuwa dawa takribani lita 100 zipo tu kiwandani hapo baada ya wanunuzi wakuuu ambao ni Halmashauri za Wilaya kushindwa kuzinunua kwa madai ya kukosa fedha.

Kadhalika, Mziray amefafanua zaidi na kumweleza Rais kuwa kushindikana kununuliwa dawa hizo kwa wakati kunaweza kusababisha zikaharibika  kwa sababu  zinatakiwa zisihifadhiwe zaidi ya miezi miwili tangu  zinapotengenezwa.

Profesa Muhongo Atoweka Bungeni

$
0
0
Aliyekuwa Waziri wa nishati na madini prof. Sospeter Muhongo, hajaonekana Bungeni mjini Dodoma bila ruhusa ya Spika tangu uteuzi wake katika baraza la mawaziri utenguliwe wiki tano zilizopita .
 
Mei 24, mwaka huu, Ris John Mgufuli alitengua uteuzi wa prof. Muhongo katika baraza la mawaziri, ikiwa ni muda mfupi baada ya kukabidhiwa ripoti ya kamati ya kwanza ya uchunguzi wa machanga wa dhahabu (makinikia)
 
Mtaalamu huyo wa jiolojia wa kimataifa hakuwapo bungeni wakati uteuzi wake wa uwaziri ukitenguliwa, huku taarifa zikidai kuwa alirudi nyumbani kwao, Musoma Mkoani Mara, kuhudhulia mazishi ya dada yake.

Katibu wa bunge DK. Thomas Kashililah, alisema ofisi yake haina taarifa ya mbunge huyo wa Msoma Vijijini (CCM) jambo ambalo ni kinyume na utaratibu.

Kiongozi huyo wa bunge pia alisema ofisi yake haijui aliko tangu alipoachishwa nafasi ya uwaziri mwishoni mwa mwezi uliopita

DK. Kashililah aliongeza kuwa kwa kawaida mbunge anapokuwa na udhuru , humwandikia Spika kumuelezea hatakuwa bungeni kwa muda Fulani na ofisi ya KAtibu wa Bunge hupewa nakala.

“Sijapata nakala yeyote ya udhuru, wa profesa Muhongo na wala sijui alipo tangu siku ile,” alisema DK. Kashililah.

Katibu wa Bunge huyo alisema hii ni mara ya pili kwa Muhongo kuondoka Bungeni kwa muda mrefu bila ya ruhusa kwani hata alipomwandikia barua ya kujiuzulu Rais wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete, hakuhudhulia bunge kwa muda mrefu.

Prof. Muhongo alijiuzulu nafasi ya uwaziri wa Nishati na Madini Januari 24,2015 kwa shinikizo la Bunge, kutokana na taarifa ya kamati moja ya chombo hicho juu ya kashfa ya uchotwaji wa fedha katika akaunti ya Tegeta Escrow.

Rais aagiza walioshindwa kuendeleza viwanda wakamatwe, wawekwe gerezani

$
0
0
Rais John Magufuli amemwagiza Waziri wa Viwanda na Biashara, Charles Mwijage, kuwanyang’anya viwanda wamiliki ambao wameshindwa kuviendeleza.

Ameyazungumza hayo leo (Alhamisi) akiwa katika ziara yake ya siku tatu mkoani Pwani ambako amezindua viwanda saba.

“Kipindi cha nyuma tulipofanya makosa ni pale tulipouza viwanda kwa watu binafsi, sasa  kuna  viwanda 197 vimeshakufa waliouziwa hawajishughulishi na vingine vipo kama magofu,” amesema.

Kutokana na hilo, Rais amesema; "natoa wito kwa wote waliouziwa viwanda kipindi cha nyuma na sasa wameshindwa kuviendeleza , naagiza sasa basi mrudishe  na wewe Waziri Mwijage tumia hata nguvu kama kuwaweka ndani weka tu siku akitoka huko atakuta kiwanda kimeanza kazi."

Rais Magufuli: Katika Utawala Wangu Hakuna Atakayepewa Mimba na Kuruhusiwa Kurudi Shule

$
0
0
Rais John Magufuli amesema wakati wa utawala wake hakuna mwanafunzi atakayepata mimba na kuruhusiwa kurudi shule.

 Ameyasema hayo leo (Alhamisi) wakati wa ziara yake ya siku tatu mkoani Pwani ambako amezindua viwanda saba.

“Azae halafu aende kuwahubiria wenzake, unajua ilikuwa hivi, halafu nilifanya hivi,”amesema.

Amesema waliozaa shuleni wanaweza kwenda kupata elimu nyingine kama vyuo vya ufundi stadi (Veta) na kilimo badala ya kurudi shule na kuanza kuwafundisha wenzao yale waliyoyafanya.

“Mnataka niwaambie warudi shule halafu, ni bora wakalime ili ile nguvu waliyoitumia kujifungua waitumie kulima,” amesema.

Amesema; “Ni rahisi zaidi kuzalia chuo kikuu, ule mwaka wa kwanza, wa pili lakini sekondari, darasa la kwanza  kupeleka walio na watoto, tunapoteza maadili yetu, watazaa mno.”

 “Mtajikuta darasa la kwanza wote wanawahi nyumbani kwenda kunyonyesha. Hii tutalipeleka Taifa pabaya,” amesema.

Rais Magufuli: Nataka Wafungwa Walime Sana ili Wajifunze na Waogope Kufungwa Tena

$
0
0
Rais John Magufuli amesema ni vizuri magereza yakawa na maeneo mengi ili wafungwa walime na wajue maana ya kufungwa ni nini.

Ameyasema hayo leo (alhamisi) wakati akizungumza wilayani Bagamoyo katika ziara yake ya siku tatu, mkoani Pwani.

 “Nimechoka kuwalisha wafungwa, mtu afungwe halafu anunuliwe chakula. Nimeshatoa maagizo, wafungwa hawa wakalime ili waogope kufungwa,” amesema na kuongeza;

“Wakajifunze kulima, wajue kufungwa ni kufungwa na neno kufungwa ni kufungwa kweli. Tukianza kuwapunguzia maeneo magereza, mnataka wakalime wapi?” amehoji.

Rais amesema, hiyo ndiyo sababu ya kutunza maeneo ya magereza ili yatumike kwa uzalishaji mali.

 Ameongeza kuwa ni vizuri wahalifu wakatumia nguvu kama walizotumia kuiba, ili wakalime.

“Huko magereza wafanye kazi, bila kujali vyeo walivyokuwa navyo, umaarufu wao na wakafanye kazi,” amesema

Rais Magufuli Atoa Ekari 65 za Magereza na Kuwapa Wananchi

$
0
0
Rais John Magufuli amewapa wakazi wa Bagamoyo, eneo la Magereza lenye ukubwa wa heka 65.

 Rais Magufuli amechukua uamuzi huo leo (Alhamisi) wakati akihutubia katika mkutano wa hadhara katika ziara yake ya siku tatu, mkoani Pwani.

Alichukua hatua hiyo baada ya wanawake waliokuwa wamebeba mabango, kumtaka awape eneo lao kwa kuwa ni wazaliwa wa Bagamoyo, ni wajane na wana uhaba wa maeneo ya biashara.

“Akina mama mnaokaa huko na akina baba nimewapa hilo eneo lakini natoa tahadhari, mpaka wenu sasa ni barabara, msivuke mkaenda upande ule,” amesema.

Amelitaka Jeshi la Magereza kufanya mabadiliko katika hati ili eneo hilo liwe la wananchi.

Jipatie Dawa za Asili za Kupunguza Maziwa, Kupunguza tumbo, Kuongeza nguvu za Kiume na Mvi

$
0
0
OFFER OFFER OFFER
Natural beauty products inakupa OFFER ya EID kwa punguzo la %10 kwa kila product. 
Bidhaa zetu zote zimetengenezwa kwa mimea na matunda hazina kemiko wala madhara yoyote.
 
   🥝🥑🥒🧀🍉🍅🍓🍋
        Pia anatumia mtu wa aina yoyote. Tunazo za÷
1.HANDSOME UP ni kifaa kinachoongeza maumbile ya kiume  kwa 99% kwa size uipendayo wewe na kuimarisha misuli ya uume kwa @170,000/= tuu.
2.MEN GELY YA KUPAKA. Hii inaongeza kwa wastani wa inch 6.5 na inapatikana kwa @130,000/=. 
3. SHARK POWER. Hii pia ni kwa ajili ya kuongeza maumbile  wastani wa inch 7.5 inapatikana kwa @135,000/=.
4.. MAX MAN 2. Ni vidonge kwa ajili ya nguvu ambavyo vinasaidia sana hata kwa watu wenye kisukari na waliokua wakifanya sana master blashion. Pia huongeza hamu ya tendo la ndoa inapatikana kwa @130,000/=
5.DISCREET. Hii ni ya kuondoa mvi na zisiludi tena milele inapatikana kwa @130,000/=
🍅🍇🍉🍅🍍🍓🥒🥑🍒
Tupo DAR ES SALAAM  kariakoo na kinondoni kanisani. 
 
Kwa mawasiliano zaidi piga  0759029968 au 0659618585.
Popote ulipo utapata huduma zetu.
           Follow us Instagram
@natural2162
@natural2162
@natural2162
@natural2162
 
     Bidhaa zetu zote ni garantii na unapewa risiti
              Karibu

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya June 23

Kutana Maajabu ya Mtabibu CHIEF SULTAN(MAKATA WA MAKATANI) Mganga wa Waganga Sasa Yupo Mikoa Yote Tanzania

$
0
0
Pia anatoa Tiba kwa Njia ya Simu ukiwa popote Pale Tanzania au Nje ya Tanzania..

CHIEF SULTAN ni Mtabibu na Mtafiti wa Dawa za Asili ya Africa, na Duniani Katika utoaji wa Tiba za Asili..
Je unasumbulia na Mapenzi..?
 
(Umeachwa na Umpendae awe Mume/ Mke au mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine na Bado Unampenda?) Umejaribu sehemu Nyingi bila Mafanikio?Wasiliana na CHIEF SULTAN Akusaidie Kumshika Umpendae Asikusaliti(LIMBWATA) Kumtawala Mpenzi wako kwa sababu Maalum..Anauwezo wa Kusambalatisha Mahusiano yao ndani ya siku Moja tu.
Je Unasumbuliwa na Madeni?
Biashara yako Haina wateja?
Unatatizo la kutokushika Mimba na umehangaika sehemu nyingi bila mafanikio?
 
Wasiliana na CHIEF SULTAN Kwa Majibu ya Maswali yako..
Anasafisha NYOTA na Kutoa PETE za BAHATI kuendana na NYOTA yako. UTAJIRI USIO NA MASHARTI.(Magic Wallet_Pochi ya Maajabu Isio Isha Hela)
KUWA MAARUFU na KUJULIKANA
Kupandishwa CHEO na HESHIMA Mahala pa KAZI.
Utapewa Nguvu ya Kujilinda na MALI ZAKO zako na Mwili wako.. Huzuia Chuma Ulete katika Biashara.. Hurudisha MALI zilizo Potea au KUDHULUMIWA..
 
Mvuto wa Biashara na Mwili wako.
Hutibu kabisa Nguvu za Kiume na Kurefusha Uume kwa saizi Unayotaka.
Magonjwa Sugu(Miguu Kufa Ganzi, kisukari, Presha, Pumu nk.)Humaliza Kesi za Muda mrefu ndani ya siku 14 tu.
Anatoa NDAGU Zisizokuwa na Masharti.. Kwa maelezo Zaidi wasilina nae kwa

Whatsapp +255 0658 316 976
Call +255 755 911 233

Jinsi Kitambi Kinavyopatikana na Jinsi Kinavyoondolewa na Dawa ya Mkataa Kitambi

$
0
0

Kitambi  ni  ile  hali  ya  tumbo  kuwa kubwa  na  kuchomoza  kwa  mbele  na  wakati mwingine  kufikia  hatua  ya  kunin’ginia.
JINSI  KITAMBI  KINAVYO  PATIKANA
Kwa  mujibu  wa  tafiti  mbalimbali  za  kitaalamu, mwili wa binadamu una seli kati  ya bilioni 50  hadi 200 za mafuta zilizogawanyika katika  sehemu  mbalimbali  za  mwili wa binadamu.

 Kwa wanawake  seli hizo  zipo sana katika maeneo ya matiti, kwenye  nyonga, kiunoni na kwenye makalio.

Kwa upande  wa  wanaume seli  hizo zinapatikana  sana kwenye kifua, tumboni na kwenye makalio pia.

Mafuta ya tumbo yanayofanya kitambi hukusanywa kwa njia kuu mbili:

i.Njia  ya kwanza ni mafuta kutoka kwenye tishu zilizo chini ya ngozi

ii.Na  njia  ya pili ni kutoka kwenye ogani za ndani kama moyo, kongosho n.k

SABABU ZA KUPATA KITAMBI
Sababu kubwa ya kitambi ni kukosekana ulingano wa nguvu(kalori) katika  mwili  wa  mwanadamu, hali  inayo  sababishwa  na  mtu  kula vyakula vinavyotia nguvu sana kuliko jinsi anavyoweza kutumia na kutoa kama taka mwili.

VYAKULA  VINAVYO  CHANGIA KULETA  KITAMBI

Vyakula vinavyochangia  kuleta  kitambi ni  pamoja  na :
i.Vyakula  vyenye  mafuta  mengi  kama  vile  nyama nyekundu  (iwe ni ya kuchemsha, kukaanga au kuchoma), nyama  ya  kuku  wa  kizungu  ( iwe  ya  kuchemsha, kukaanga  ama  kuchoma ), mafuta ya kupikia, (hasa yale yatokanayo na bidhaa za wanyama, kama siagi, na jibini), viazi ya kukaanga kwa  mafuta  (chips) pamoja  na  pizza.

ii.Vyakula vyenye wanga mwingi kama  vile ugali wa mahindi, mihogo, wali, mkate  mweupe.

iii. Vyakula  na  vinywaji  vyenye  sukari  nyingi  iliyo  ongezwa( added  sugar ), kama  vile  soda  na  keki.

iv. Vyakula  vilivyo  tengenezwa  kwa  ngano  na  sukari kama  vile  keki, skonzi, chapatti, maandazi, mkate  mweupe  nakadhalika

v. Pamoja  na  vinywaji  vilivyo  tengenezwa  kwa  kutumia  ngano  kama  vile  bia  za  aina  mbalimbali  na  kadhalika.

Vyakula  vilivyo  tajwa  hapo  juu, vikitumiwa  bila  kuzingatia  kanuni  za  mlo  kamili, huchangia  kuleta  tatizo  la  kitambi.

vi. Sababu nyingine ni  kutofanya  mazoezi  ya  mwili  na  viungo(  physical  exercises  )  kwa  muda  mrefu.

JINSI YA KUJUA KAMA UNA KITAMBI
Kitambi kinaweza kuonekana kirahisi kwa macho. Ila kujua ni kwa kiwango gani kitambi chako kipo inabidi kufanya vipimo vya kiuno(waist) na nyonga (hips).

Mzingo wa kiuno ukiwa >102 cm au 40  kwa wanaume na >88 cm au 35  kwa wanawake, na uwiano wa kiuno na hips(Waist-Hip Ratio) ikiwa >0.9 kwa wanaume na >0.85 kwa wanawake.

BMI ya 30 au zaidi inaashiria 'Obese' uzito kuzidi kiasi. Kuwa na mzingo uliozidi kawaida ni kiashiria hatari cha matatizo ya kimetaboliki, kuliko hata cha BMI.

Kipimo kingine cha kitambi ambacho kimeonyesha uwezo zaidi kuliko BMI katika kutabiri uwezekano mkubwa wa magonjwa ya moyo ni Index Of Central Obesity(Waist-To-Height Ratio-WHtR) ambapo uwiano ukiwa sawa na 0.5 au zaidi, hii ikimaanisha mzingo wa kiuno angalau ni nusu ya kimo cha mtu.

Kipimo kingine ni Body Volume Index, kinachopima kitambi kwa kupima umbo la mtu na mgawanyo wa uzito wake.

MAMBO  YANAYO  MUWEKA  MTU  KATIKA  HATARI  YA  KUPATWA  NA  KITAMBI
Tumekwisha  ona  hapo  juu jinsi  kitambi  kinavyo  patikana  na  vyakula  pamoja  na  sababu  nyinginezo  zinazo  sababisha  kutokea  kwa  kitambi, sasa  tutazame  mambo  yatakayo  kufanya  uwe  katika  hatari  ya  kupatwa  na  kitambi.

Kwa  mujibu  wa  tafiti  mbalimbali  za kitaalamu, mambo  yafuatayo  huwaweka  watu  katika  hatari  kubwa   ya  kupatwa  na  kitambi :

1. Ulaji  mbovu  wa  chakula; Ulaji  mbovu  wa  chakula  ni  ulaji  usio  zingatia  kanuni  za  mlo  kamili. Hapa  mtu  hufululiza  kutumia  chakula  cha  aina  fulani  pekee  bila  kuzingatia  aina  nyinginezo  za  chakula.  Mfano; mtu  anaweza  kuwa  anakula  mlo  ufuatao :

Asubuhi :  Mchemsho  ama    supu  ya  ng’ombe , chapatti  tatu  na  soda  moja.  Mchana :   Ugali  nyama  choma anashushia  kwa  maji  na  soda.

Jioni :  Mchemsho  wa  kuku  na  bia  mbili  nakuendelea.

Usiku  :  Chips  mayai  au  chips  kuku  au  chips  mishikaki  na  bia.

Mtu  huyu  akiendelea  na  utaratibu  huu  kwa  muda  mrefu, ni  lazima  atapatwa  na  kitambi.

2. Ulaji  mfululizo  wa  vyakula  vyenye  mafuta  mengi

3. Ulaji  mfululizo  wa  vyakula  vyenye wanga  mwingi  

4.Ulaji  mfululizo  wa  vyakula  vyenye  sukari  iliyo  ongezwa ( added  sugar  ).

5.Ulaji  mfululizo  wa  vyakula  vya  ngano.

6.Ulaji  mfululizo  wa   vinywaji  vyenye ngano  na  sukari.

7.Kutofanya  mazoezi  ya  mwili  na viungo  ( physical  exercises  ).

Mhusika  anapokuwa  katika  makundi  yote  yali yotajwa  hapo  juu, hali  huwa  mbaya  zaidi. 

NJIA ZA KUONDOA KITAMBI
Kuwa  na  kitambi  ni  lugha  ya  mwili  ( body-language )  inayo  leta  ujumbe  kwako  kwamba  “ Mwili    wako  haupo  salama  tena “

Kama  una  kitambi   maana  yake  una  mafuta  yasiyo  hitajika  mwilini, mwili  wako  unatumika  kuhifadhi  mafuta  usiyo  yahitaji.

Hali  hii  kitabibu  imaanisha  kwamba, ogani  nyinginezo  zilizomo  ndani  ya  mwili  wako  zinao gelea  kwenye  mafuta( fats  )  yasihotika  yaliyomo ndani  ya  mwili  wako,  jambo  linalo  kuweka  katika  hatari  kubwa  sana  ya  kushambuliwa  na  magonjwa  hatari  kama  vile  shinikizo  kubwa  la  damu, kiharusi  na kisukari  na  kwa kutaja  machache.

Hivyo  basi  ili  kuondokana  na  hatari  hiyo, yakupasa   kupambana  kuondoa  hayo  mafuta  yasiyo  hitajika  mwilini  mwako.

NJIA  ZA  KUONDOA  KITAMBI.
Unaweza  kuondokana  na  kitambi  kwa  kufanya  diet  pamoja  na  mazoezi ya  mwili  na  viungo.

Vilevile  unaweza  kuondoa  kitambi  na  kupunguza  mafuta  mwilini  kwa  kutumia  dawa  asilia  ya  kuondoa  kitambi  na  kuondoa  mafuta  yasiyo  hitajika  mwilini.

DAWA   ASILIA  YA  KUONDOA  KIAMBI  NA  MAFUTA  MWILINI.
Hii  ni  njia  ya  uhakika  kabisa  ya  kuondoa  tatizo  la  kitambi  pamoja  na  mafuta  yasiyo  hitajika  mwilini.

 Unaweza  kuondoa  tatizo  la  kitambi  pamoja  na  kupunguza  mafuta  mwilini  kwa  kutumia  DAWA  ASILIA   IITWAYO YA  MKATAA  KITAMBI.

 Dawa   hii  ni  ya asili  kabisa
“  Pure  Herbal “, ambayo  haijachanganywa  na  kemikali  yoyote, haina  side  effect kwa  mtumiaji  na  inaondoa  kabisa  tatizo  la  kitambi  ndani  ya  siku  kumi  na  nne.

JINSI  DAWA  YA  MKATAA  KITAMBI  INAVYO  FANYA  KAZI.
1.Huyeyusha  mafuta  yasiyo  hitajika  mwilini.

2.Husaidia  kupunguza  hamu  ya  chakula.

3.Inazuia  kutengenezwa  kwa  seli  za  mafuta  ( fat cells  ) katika  mwili  wa  mwanadamu. Unapokula  chakula  chenye  mafuta  mengi, dawa  hii asilia  hupambana  kuyafanya  mafuta  hayo  yasitengeneze  seli  za  mafuta  mwilini  mwako. Hali  hii  huuepusha  mwili  wako  kuhifadhi  mafuta   yasiyo  hitajika  mwilini.

4. Husaidia  kupunguza  uzito wa mwili  kwa  haraka  sana  endapo  itatumika  pamoja  na  diet  ya  kabechi.

UFANISI  WA  DAWA.
Ufanisi  wa  dawa  hii  ni  wa  asilimia  mia  moja. Dozi  ya  dawa  hii  hutumika  kwa  muda  wa  siki  ishirini  na  moja.

MATOKEO  YA  DAWA:
Dawa  hii  huondoa  kabisa  kitambi  ndani  ya  siku  kumi  na  nne.

BEI  YA  DAWA :
Dawa  hii  inaoatikana  kwa  kiasi  cha  SHILINGI  ELFU  HAMSINI  TU  (Tshs. 50,000/=)

MAHALI  TUNAPO  PATIKANA.
Tunapatikana  jijini  DAR  ES  SALAAM, katika  eneo  la  UBUNGO  karibu  na  SHULE  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING  nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA.

KWA  WATEJA  WASIO  WEZA  KUFIKA  OFISINI  KWETU.
Kwa  wateja  wasio  weza  kufika  ofisini  kwetu  Tabata, tunao  utaratibu  wa  kuwafikishia  dawa  mahali  popote  walipo  ndani  ya  jiji  la  Dar  Es  salaam.

KWA  WATEJA  WA  NJE  YA  DAR  ES  SALAAM.
Kwa  wateja  waliopo  nje  ya  Dar  Es  salaam, tunawatumia  dawa  kwa  njia  ya  MABASI.

Kwa  wateja  wa  ZANZIBAR  tunawatumia  dawa  kwa njia  ya  boti.

KWA  WATEJA  WA  NJE  YA  NCHI:
Kwa  wateja  wa  nje  ya  nchi, tunatumia  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  au  DHL.

WASILIANA  NASI  KWA  SIMU  NAMBA : 0766  53 83 84

TUTEMBELEE:

Madiwani na Naibu Meya CHADEMA Watiwa Mbaroni Arusha

$
0
0
Naibu Meya wa Jiji la Arusha, Viola Likindikoki, pamoja na madiwani wengine wawili wa Chadema wamekamatwa jana na Jeshi la Polisi mkoani humo kwa sababu ambazo mpaka sasa hazijafahamika.

Meya wa Jiji la Arusha, Kalist Lazaro amesema Viola pamoja na madiwani hao wawili walikamatwa  jana Alhamisi  wakiwa katika mkutano wa ndani uliokuwa ukisikiliza kero za wananchi.

“Nipo Tanga kikazi na nilimkaimisha nafasi yangu Viola, kwa kawaida Alhamisi tunasikiliza kero za wananchi, wakati wakiendelea kusikiliza kero ndipo walipokamatwa,” alisema.

Wengine waliokamatwa katika tukio hilo ni diwani wa viti maalumu (Chadema), Kata ya Ngarenaro Happiness Charles na diwani wa Viti Maalumu kata ya Olorieni, Sabrina Francis.

Kamanda wa Polisi mkoani Arusha, Charles Mkumbo amesema kwa kifupi kwamba jeshi lake linawashikilia kwa uchunguzi.

Diwani wa viti maalumu (Chadema), Jenipher Lomayan  amesema madiwani hao walikamatwa   jana saa 9 alasiri  wakiwa ndani ya ofisi ya Meya wa Jiji la Arusha wakisikiliza kero za wananchi.

Lomayan, amesema  wakiwa ndani ya ofisi hizo polisi waliovalia nguo za kiraia waliingia na kuwaeleza kwamba wako chini ya ulinzi na wanatakiwa kufika mbele ya makao maku ya jeshi hilo kwa uchunguzi zaidi.

“Wale polisi walitaka kuichukua simu ya Naibu Meya na ndipo madiwani wawili (Sabrina na Happiness) wanaoshikiliwa waliingilia kati na kuwazuia polisi wasimnyanganye simu hiyo na ndipo na wao wakaunganishwa katika tukio hilo,” amesema.

Bunge lapinga ongezeko la ushuru vinywaji baridi

$
0
0
Serikali  imewasilisha bungeni Muswada wa Sheria ya Fedha wa Mwaka 2017 wenye marekebisho ya sheria 15 ikiwamo Sheria ya Ushuru wa Bidhaa.

Kwa mujibu wa marekebisho hayo, ushuru wa bidhaa kwenye vinywaji baridi umeongezeka kutoka Sh 58 kwa lita hadi Sh 61 ikiwa ni sawa na ongezeko la shilingi tatu. 

Aidha, Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti imepinga ongezeko hilo la shilingi tatu kwenye vinywaji baridi ikisema hatua hiyo itazorotesha ukuaji wa viwanda nchini.

Akiwasilisha Muswada huo jana, Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango alisema sheria hizo zinahusu masuala ya fedha, kodi, ushuru, tozo, na mawasiliano ili kupunguza, kurekebisha, au kufuta viwango vya kodi, ushuru, ada na tozo mbalimbali ili kuboresha ukusanyaji wa kodi.

Dk Mpango alisema marekebisho hayo yamezingatia mkakati wa taifa wa kukuza uchumi wa viwanda, na kwamba kiwango cha ushuru kwa baadhi ya bidhaa zinazozalishwa nchini kimepunguzwa au kubakia ilivyo sasa.

Mengine aliyozungumzia ni ongezeko la ushuru katika mafuta ya petroli, dizeli na mafuta ya taa kwa Sh 40, Sheria ya Benki Kuu inayorekebishwa ili kuweka sharti la ulazima kwa taasisi za serikali kufungua akaunti na kuhifadhi mapato na fedha Benki Kuu.

Alisema katika marekebisho hayo, pia ipo Sheria ya Posta na Mawasiliano ya Kielektroniki ili kutoa wigo mpana kupanua wigo wa mauzo ya hisa za asilimia 25 zitakazouzwa na kampuni ya mawasiliano kwenye soko la hisa kwa kutoa fursa kwa Watanzania walio ndani na nje ya nchi, taasisi ya Kitanzania, kampuni zinazomilikiwa kwa pamoja baina ya Watanzania na raia wa nje, raia, kampuni na taasisi za nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki au raia na kampuni kutoka nchi nyingine.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bajeti, Hawa Ghasia alipinga kuongezeka ushuru kwa vinywaji baridi akisema hatua hiyo itapunguza uzalishaji. 

Alitolea mfano hatua ya serikali ya kutoongeza kodi kwenye bidhaa hiyo kwa miaka mitatu iliyopita kuwa uzalishaji na uchumi uliongezeka na serikali kupata kodi; huku akipendekeza tozo 14 zilizobakia katika shule na vyuo binafsi zizidi kuondolewa ili wapunguzia gharama.

Mbunge wa Vwawa, Japhet Hasunga (CCM), alisema muswada huo umejumuisha asilimia 80 ya mapendekezo ya wabunge na kutaka asilimia 15 ya fedha ambazo mashirikia ya umma hutakiwa kuchangia mfuko mkuu wa serikali, zisitozwe kodi kwani mashirika ya umma yanalipa kodi mara mbili.

Mbunge wa Nzega Mjini, Hussein Bashe (CCM) alipendekeza kuongezwa tozo ya asilimia sita hadi 12 kwenye mapato yatokanayo na michezo ya kubahatisha, na asilimia nane hadi 20 kwenye zawadi na pia kuongeza tozo ya leseni.

Shahidi ( OCCID) Asimulia Jinsi Alivyomkamata Tundu Lissu

$
0
0
Mkuu  wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai wa Wilaya (OCCID), Yustino Mgonja ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa alimkamata Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu baada ya Mkuu wa Upelelezi Kanda Maalumu (ZCO), Camilius Wambura kumtaka afanye hivyo.

Mgonja ambaye ni shahidi wa nne katika kesi ya kutumia lugha ya uchochezi inayomkabili Lissu, alidai hayo jana mbele ya Hakimu Mkazi, Godfrey Mwambapa kesi hiyo ilipokuja kwa ajili ya kusikilizwa.

Akiongozwa na Wakili Mwandamizi wa Serikali, Mutalemwa Kishenyi, shahidi huyo alidai kuwa Juni 28, mwaka jana, Wambura alimpa maelekezo ya kumkamata Lissu kwa kosa la kutoa lugha za uchochezi katika viwanja vya mahakama hiyo.

Alidai kuwa Juni 29 mwaka jana saa 7 mchana alienda nyumbani kwa Lissu maeneo ya Tegeta wilayani Kinondoni, ambapo alimkamata na kumfikisha katika ofisi ya ZCO na kumkabidhi.

“Nilipewa amri na ZCO nikukamate hivyo kwa mamlaka hayo bila kuwa na hati ya ukamataji naweza kukukamata; kwani makosa yoyote ya jinai unaruhusiwa kukamata bila kuwa na hati hiyo,” alidai Mhonja.

Pia alidai kuwa kumpinga Rais anapokosea sio kosa na kwamba tafsiri ya maneno aliyoyatoa, ndio yamesababisha kukamatwa na kushitakiwa kwa kutumia lugha za kichochezi.

Katika mashitaka yake, Lissu anadaiwa kuwa Juni 28, mwaka huu akiwa katika viwanja vya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, alitoa kauli za uchochezi kuwa “Mamlaka ya Serikali mbovu ni ya kidikteta uchwara inahitaji kupingwa na kila Mtanzania kwa nguvu zote, ‘huyu diktekta uchwara lazima apingwe kila sehemu’. Kama uongozi utafanywa na utawala wa kijinga nchi inaingia ndani ya giza nene.’’

Waziri Mkuu: Ni Marufuku Wazee wa Miaka 60 Kutozwa Kodi za Majengo

$
0
0
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amewataka maofisa wa Mamlaka ya Kodi ya Mapato Tanzania (TRA) wakusanye kodi za majengo kwa kuzingatia sheria na wasitoze kodi ya majengo wazee wenye umri zaidi ya miaka 60.

“TRA ijipange kukusanya kodi za majengo kuanzia Julai mosi 2017. Katika kutekeleza jukumu hilo, zingatieni sheria. Tusisikie mnawadai kodi ya majengo wazee wenye umri zaidi ya miaka 60 kwa majengo wanayotumia kama makazi yao,” alisema Majaliwa.

Alitoa agizo hilo jana wakati akizungumza na wananchi na viongozi wa Wilaya ya Chato waliohudhuria uzinduzi wa jengo la TRA wilayani humo mkoani Geita. Waziri Mkuu amewataka moafisa hao wakusanye kodi ya majengo kwenye maeneo ya mjini na siyo vijijini kwani kodi hiyo haiwahusu.

“Msiende vijijini. Nyumba za nyasi au za tembe hazihusiki. Tembeleeni nyumba za mijini. Piteni kwenye mitaa, muainishe aina zote za nyumba zinazostahili kulipiwa kodi. Mkishafanya sensa, wekeni utaratibu wa kuwawezesha wananchi kulipia kodi hizo,” alisema huku akishangiliwa.

Pia aliwataka wananchi wanaonunua bidhaa wadai risiti lakini wahakikishe wanapewa risiti yenye kiwango halisi walicholipia. 

“Ukipewa risiti uiangalie kama ina kiwango halisi cha fedha uliyotoa.Kuna watu wachache wasio waaminifu wanaamua kukupa risiti, lakini imeandikwa bei ndogo kuliko ile uliyolipia, ukitoa laki moja anakupa risiti ya shilingi elfu kumi,” alieleza.

 Mapema, akitoa taarifa ya ujenzi wa jengo hilo la ghorofa moja, Kamishna Mkuu wa TRA, Charles Kicheere alisema ujenzi huo ulianza Julai 12, mwaka jana na ulikamilika Juni 12, mwaka huu.

“Ujenzi wa jengo hili umegharimu Sh bilioni 1.4 na ulichochewa na ongezeko kubwa la idadi ya walipakodi wa Chato kutoka watu 150 mwaka 2010/11 hadi kufikia watu 600 mwaka 2016/17,” alieleza.

Pia alisema wamejenga ofisi hizo ili kuwapunguzia umbali wafanyabiashara wa wilaya hiyo ambao walilazimika kwenda Geita mjini kupata huduma za TRA ambako ni umbali wa zaidi kilometa 120.

Alisema hivi karibuni watakamilisha ukarabati wa ofisi za mikoa ya Mara, Iringa ikiwemo kujenga ofisi kwenye mikoa mipya ya Simiyu, Katavi, Njombe na Manyara. “Pia tutajenga ofisi kwenye mkoa mpya wa kikodi wa Kahama,” alieleza.

Alizitaja wilaya ambazo ziko mbioni kupatiwa ofisi zake kuwa ni Kondoa, Longido, Bunda na Arumeru. Alisema katika mwaka ujao wa fedha, TRA imelenga kukusanya Sh trilioni 17.106 na watahakikisha wanafikia lengo hilo.

Usikose Ofa Hii Kwa Sh. 7000 tu Upate Kitabu cha President Wife( Shadow of Destination of my Enermies)

$
0
0
Jipatie kitabu cha President wife kupitia, Whatsapp 0657072588 ay email eddazariaM@gmail.com  Unachotakiwa kufanya, wasiliana nami kisha nieleze ni wapi ninaweza kukutumia kitabu hicho(Mfano Whatsappp au kwenye Email). Nipigie kwa no 0657072588 au 0768516188.
 
Ofa hii y ash 7000 ni kwa siku ya leo  23 June 2017. Wahi sasa kwani ofa hiii ni kwa ajili yako msomaji wangu.Kumbuka President wife ni muendelezo wa SORRY MADAM Destination of my Enemies.
 
Namba za malipo MPESA 0768516188 JOYCE MBWAMBO au TIGOPESA 0657072588 AZARIA MSULWA                        KARIBUNI SANA

Picha: Rais Magufuli alivyozindua Kiwanda cha TAMCO kinachounganisha Matrekta

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli amezindua kiwanda cha kuunganisha matrekta cha Ursus na kiwanda cha Nondo cha Kiluwa ambapo  amewataka wawekezaji kujitokeza kwa wingi kwani Serikali iko nao bega kwa bega.

"Kiwanda ni kikubwa na kinatoa nondo ambazo zinaweza kujenga daraja lolote Tanzania au Ulaya.Tanzania tuna chuma, kwa nini tuagize chuma kutoka Brazil au China.

"Wawekezaji watafute njia ya kutumia chuma cha Tanzania badala ya kuagiza nje ya nchi  na nashauri Ajira zianze kwanza kwa vijana wa Mkoa wa Pwani'',  amesema Rais Dkt. Magufuli na kuongeza kuwa serikali inampango  wa kujenga barabara kubwa ya lami ya njia sita kutoka Dar mpaka Chalinze ambapo amewataka watanzania kuvilinda viwanda  na  amani ya Tanzania

 
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images