Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Acacia wakutana na Rais Magufuli Ikulu leo, wakubali kulipa fedha wanazodaiwa

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amekutana na kufanya mazungumzo na Mwenyekiti wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation ambayo ni mmiliki mkubwa wa kampuni ya Acacia Mining Limited Prof. John L. Thornton na kukubaliana kuwa kampuni hiyo ipo tayari kufanya mazungumzo na Serikali ya Tanzania ili kulipa fedha ambazo Tanzania imezipoteza kutokana na kampuni hiyo kuendesha shughuli zake hapa nchini.

Prof. John L. Thornton ambaye amesafiri kwa ndege binafsi kutoka nchini Canada hadi Tanzania amekutana na Mhe. Rais Magufuli leo Juni 14, 2017 Ikulu Jijini Dar es Salaam na mazungumzo yao yamehudhuriwa na Balozi wa Canada hapa nchini Mhe. Ian Myles na Waziri wa Sheria na Katiba Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi.

Baada ya Mazungumzo hayo Prof. John L. Thornton amesema kampuni yake ipo tayari kufanya mazungumzo na Tanzania yatakayozingatia maslahi ya pande zote mbili na pia ipo tayari kulipa fedha zote ambazo inapaswa kulipa kwa Tanzania.

Kwa upande wake Mhe. Rais Magufuli amesema Serikali inakaribisha mazungumzo hayo na itaunda jopo la wataalamu watakaofanya majadiliano na kampuni ya Barrick Gold Corporation ili kufikia makubaliano ya kulipwa fedha zinazodaiwa na namna kampuni hiyo itakavyoendesha shughuli zake nchini maslahi ya pande zote mbili.

Mhe. Rais Magufuli amesema pamoja na kukubali kulipa fedha zinazodaiwa Prof. John L. Thornton amekubali kushirikiana na Tanzania kujenga mtambo wa kuchenjulia dhahabu (smelter) hapa nchini.

Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli amevionya vyombo vya habari vinavyowataja Marais wastaafu Mhe. Benjamin William Mkapa na Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete na kuwahusisha na taarifa za kamati mbili za uchunguzi wa madini yaliyo katika makontena yenye mchanga wa madini (Makinikia) ambao ripoti zimekabidhiwa kwake na kamati hizo.

“Nimesoma ripoti zote mbili hakuna mahali ambapo Mzee Mkapa na Mzee Kikwete wametajwa, vyombo vya habari viache kuwachafua hawa wazee, wamefanya kazi kubwa ya kulitumikia Taifa letu, viwaache wapumzike” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
14 Juni, 2017

Habari Zilizopp Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi ya June 15

Rais Magufuli Amemteua Prof. Longinus Rutasitara kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Kituo cha Uwekezaji nchini(TIC).

TANESCO yautahadharisha umma kuhusu matapeli wanaodai watawawezesha kupata ajira walizoomba

Kipindi Maalum : Rais Magufuli Alivyotana Na Mwenyekiti Wa Barrick Gold Corporation June 14,2017

$
0
0
Kipindi Maalum :  Rais  Magufuli Alivyokutana Na Mwenyekiti Wa Barrick Gold Corporation June 14,2017 

==>Tazama Full Ripoti Hapo Chini

Taarifa Kwa Umma Kuhusu D9 Club

'Pedeshee Ndama mto wa ng'ombe' Alipa Milioni 200 na Kuachiwa huru kwa dhamana.

$
0
0
Baada ya kufanikiwa kulipa faini ya milioni 200 hatimae jana  mfanyabiashara , Ndama Shabani Hussein, maarufu kama Pedeshee Ndama mtoto ya Ng'ombe amepata dhamana.

Ndama amepata dhamana baada ya kuwa na wadhamini wawili na kuwasilisha hati ya mali isiyohamishika yenye thamani zaidi ya shilingi milioni 600.

Wiki iliyopita Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ilimtia hatiani Ndama na kumuhukumu kwenda jela miaka mitano au kulipa faini ya milioni 200 baada ya kukiri shtaka la kutakatisha USD 540,000.

Aidha mahakama hiyo iliyoketi chini ya Hakimu Mkazi Victoria Nongwa ilimsomea masharti ya dhamana mshtakiwa huyo iwapo angefanikiwa kulipa kiasi hicho cha milioni 200 ili awe huru katika mashtaka matano yanayoendelea kumkabili mahakamani hapo ambayo upelelezi wake bado haujakamilika.

Katika masharti hayo, Ndama alitakiwa kuwa na wadhamini wawili wanaoaminika na atoe fedha taslimu kiasi cha USD 270,200 ambacho ni sawa na zaidi ya milioni 600 mahakamani hapo ama mali isiyohamishika yenye thamani ya kiasi hicho cha fedha

Licha ya kupata dhamana, Ndama alirudishwa gerezani kukamilisha taratibu kabla ya kuachiwa huru.

Hukumu hiyo ya shtaka la sita la kutakatisha fedha ilitolewa baada ya Wakili wa Serikali, Christopher Msigwa kumsomea maelezo ya awali (PH) Ndama na kuyakubali maelezo ya awali na maelezo yote yanayounda shtaka hilo la kutakatisha fedha, akapatikana na hatiani na kupewa adhabu hiyo.

Kabla ya kutolewa kwa hukumu hiyo, Wakili Msigwa aliiambia mahakama kuwa mshtakiwa amekubali shtaka la sita la kutakatisha fedha na maelezo yanayounda shtaka hilo, hawana kumbukumbu za nyuma za makosa dhidi ya Ndama ila ni rai ya upande wa mashtaka kuwa wakati mahakama ikitoa adhabu izingatie matakwa ya kifungu cha 13(a) cha sheria ya kuzuia utakatishaji fedha.

Serikali Yatoa Onyo.......Yavitaka vyombo vya habari kuacha kuwahusisha Marais wastaafu na mchanga wa madini

$
0
0
Serikali ya Tanzania kupitia Waziri ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo imevitaka vyombo vya habari na mitandao ya kijamii kuacha kuwatuhumu Marais wastaafu kwenye sakata la mchanga wa madini kwani majina yao hayajatajwa kwenye ripoti ambayo Rais Magufuli ameipokea.

Katika taarifa ambayo imetolewa na Waziri Mwakyembe imeeleza kuwa kuna baadhi ya vyombo vya habari na mitandao ya kijamii wamekuwa wakituhumu Marais wastaafu bila kujua athari zake kiasiasa na kijamii

==>Msikilize Waziri Mwakyembe Akiongea Hapo chini

Jinsi Ya Kuandaa Na Kutayarisha Lishe Maalumu Ya Kuongeza Na Kunenepesha Mwili

$
0
0
Kama umekonda  na  kudhoofika  mwili  kutokana  na  sababu  mbalimbali  kama  vile kuugua  magonjwa  na  maradhi  mbalimbali  au  kupatwa  na  msongo  mawazo, basi  fuata  maelekezo  yafuatayo  ili  upate  kujua  namna  ya  kuandaa  na  kutayarishe  lishe  maalumu  ya  asili  itakayo  kusaidia kunenepa  na  kurejesha  afya  ya  mwili  wako  katika  hali  yake  ya  kawaida.

MAHITAJI:
1.    Dawa  Lishe  ya  kuongeza  na  kunenepesha  mwili

2.   Asali  ya  tende

3.   Ufuta

4.     Ukwaju

5.    Kitunguu  swaumu

6.   Giligiliani

7.    Juisi  ya  Komamanga na  Asali

MATAYARISHO  NA  MATUMIZI
Matumizi  ya  lishe  hii, yame  gawanyika  katika  awamu  kuu  mbili. Awamu  ya  kwanza, itachukua  siku thelathini  na  awamu  ya  pili  itachukua  siku  thelathini pia.

Katika  awamu  ya  kwanza , mgonjwa  atatumia  DAWA  LISHE  YA  KUNENEPESHA  MWILI, ASALI  YA  TENDE  NA  UFUTA  na  awamu  ya  pili, mgonjwa  atatumia   UKWAJU, KITUNGUU  SWAUMU, GILIGILIANI  na  JUISI  YA  KOMAMANGA  & ASALI  kwa  kufuata  utaratibu  utakao  elezwa  hapo  chini.

AWAMU   YA   KWANZA
SIKU   THELATHINI  ZA  KWANZA

Mahitaji

1.   Dawa  lishe  ya  kuongeza  na  kunenepesha  mwili

2.   Ufuta

3.   Asali  ya  Tende  (   Dates  Syrup )

MATAYARISHO  , MAELEKEZO  NA  MATUMIZI
1.   Dawa –Lishe  ya  Kunenepesha  Mwili

Chukua  vijiko   vitatu vikubwa  vyenye  dawa  yako, kisha  changanya  na  maji  nusu  lita halafu chemsha  hadi  itokote, Ikiisha  tokota, ipua  acha  ipoe  kidogo kisha  tumia  kunywa  pamoja  na  machicha  yake.  Utafanya  hivyo  mara  mbili  kwa  siku  asubuhi  na  jioni  kwa  muda wa  siku  thelathini.

2.   Ufuta : Matayarisho : Chukua  vijiko  vikubwa  vinane  vyenye  ufuta, kisha  changanya  na  lita  moja  na  nusu  ya  maji. Kama  hauna  tatizo  na  sukari, unaweza  kuongeza  na  sukari  kiasi ili  kuipa  ladha.  Ikisha  tokota, ipua iache  ipoe  kiasi  kisha  tumia  kula  ufuta wote  pamoja  na  supu  yake  ama  juisi  yake. Utafanya  hivyo mara  mbili  kwa siku  asubuhi  na  jioni  kwa  muda  wa  siku  thelathini.

(N.B:   KAMA  UNA  NAFASI,  BADALA  YA  KUTUMIA  VIJIKO  VINANE  TU VYA  UFUTA  KWENYE LITA  MOJA  NA  NUSU  YA  MAJI, WEWE  TUMIA  ROBO KILO  YA  UFUTA  KWENYE  LITA  TATU  YA  MAJI, CHEMSHA  HADI  ITOKOTE,  IACHE  IPOE, KISHA  TUMIA  KULA . FANYA  HIVYO  MARA  MBILI  KWA  SIKU  ASUBUHI NA  JIONI  KWA  MUDA  WA SIKU  THELATHINI )

2.   ASALI  YA  TENDE
3.   Tumia  kula  vijiko vikubwa  vinne  vya  tende  mara  mbili  kwa siku  asubuhi  na  usiku   kwa  muda  wa  siku  thelathini. Yaani  asubuhi  kula  vijiko  vikubwa vinne  na  usiku  kula  vijiko  vikubwa vinne  vya  asali  ya  tende.

( HABARI  NJEMA  KWA  WATEJA  WETU  NI  KWAMBA, ASALI  YA  TENDE  SASA  INAPATIKANA  MOJA  KWA  MOJA  DUKANI   KWETU . UTAPATIWA  DAWA  LISHE  PAMOJA  NA  ASALI  YA  TENDE  UTAKAYO  ITUMIA  KWA  MUDA  WA  SIKU  THELATHINI  KWA  UTARATIBU  WA  MAELEKEZO  HAYO  HAPO  JUU )
AWAMU   YA  PILI
Awamu  ya  pili  ya  lishe  hii, itaanza  baada  ya  kukamilika  kwa  siku  thelathini  za  kutumia  dawa  lishe, ufuta  pamoja  na  asali  ya  tende. Kama  ilivyo  kuwa  kwa  awamu  ya  kwanza, awamu  ya  pili  pia  itachukua  muda  wa  siku  thelathini

MAHITAJI, MATAYARISHO   NA  MATUMIZI

1.  UKWAJU
Matayarisho na  Maandalizi
Chukua ukwaju  kiasi  cha  robo kilo , weka  kwenye  maji  kiasi  cha  lita  moja, ongeza pilipili  manga kiasi cha  kijiko kimoja kidogo  ( tea spoon ) halafu ongeza sukari  vijiko  vitatu vikubwa, ongeza karafuu  ya unga  kijiko kimoja kidogo, pamoja  na hiriki vijiko  vikubwa  viwili.

Ukisha  fanya  hivyo, chemsha  hadi  mchanganyiko  wako  utokote. Ukisha  tokota, ipua  na  kuchuja  kisha  weka  kwenye  chombo  kisafi.

MATUMIZI :
Tumia  kunywa  mchanganyiko  huu kila  siku  asubuhi  baada  ya  kunywa  chai. Utafanya  hivyo  kwa  muda  wa  siku  thelathini  mfululizo.

2.   JUISI   YA  KOMAMANGA  NA  ASALI
Matayarisho  na  Matumizi

Tayarisha  juisi  ya  komamanga  kiasi  cha  nusu  lita, changanya  na asali ya  kawaida  vijiko vikubwa    vinane, kisha  ongeza  chumvi kijiko kidogo( tea spoon)

Koroga  mchanganyiko  wako  halafu  tumia  kunywa. Utafanya  hivyo  mara  moja   kwa  siku kwa  muda  wa  siku thelathini.

Matunda  ya  makomamanga  yanapatikana  masokoni, ingawa  mara  nyingi  hupatikana  kwa  uchache. Kama  utabahatika  kupata matunda  mengi, basi  unashauriwa  kuyachukua  kwa  wingi  na  kuyahifadhi, sehemu  salama ili usipate  usumbufu  wakati  wa  kutumia  tiba  yako.

Mbali  na  kutumika  katika lishe  ya  kuongeza  na  kunenepesha  mwili, tunda  la  komamanga, linasaidia  kuondoa  harufu  mbaya  ya  kinywa. Kwa  kuondoa  harufu  mbaya  ya  kinywa, kula  walau  tunda  moja  la  komamanga  kwa  siku  kwa  muda  wa  siku  thelathini  mfululizo. Utapata  matokeo  mazuri . ( HII  ITAWASAIDIA  ZAIDI  WALE  AMBAO  TATIZO  LAO  LA  KUTOKWA  NA  HARUFU  MBAYA  YA  KINYWA  LIMEANZIA  KINYWANI  NA  SIO  TUMBONI

ALTERNATIVE (MBADALA )  WA JUISI  YA  KOMAMANGA  ILIYO  UNGWA  NA  ASALI.

Kama  utashindwa  kupata makoma manga, basi  utafanya  kama  ifuatavyo :

KITUNGUU  SWAUMU
Chukua punje  nne  za  vitunguu  swaumu, zitwange kisha  tia  kwenye  maji nusu lita halafu ongeza  juisi  ya  ndimu  moja  au  limao  moja kisha  chemsha hadi mchanganyiko  wako  uchemke.

Matumizi :  Tumia  hivyo kila  siku  usiku baada  ya  kula  chakula cha  usiku. Utafanya  hivyo  kwa  muda  wa  siku  thelathini mfululizo.

AU
Vile vile , mbadala  mwingine wa  kutumia  juisi  ya komamanga  iliyo  changanywa  na  asali, unaweza  kutumia  JUISI  YA  GILIGILIANI  kwa  kufuata  utaratibu  ufuatao :

JUISI   YA   GILIGILIANI
MATAYARISHO   NA   MATUMIZI YA  JUISI  YA  GILI GILIANI

Chukua giligiliani  fresh, kisha zi -blend ( ZISAGE ) ili  kupata  juice  yake  kiasi  cha  robo  lita.

 Ndani  ya  juisi  yako  ya  giligiliani, kamuliamo ndimu fresh moja, halafu  ongeza  chumvi  kiasi robo  kijiko  kidogo ( tea spoon), koroga  kisha  tumia  kunywa.  Utakunywa  usiku  baada  ya  kula  chakula  cha  usiku. Utafanya  hivyo mara   moja  kwa  siku  kwa  muda  wa  siku  thelathini  mfululizo.

PIA : Jenga  utaratibu  wa  kuwa  unakula    giligiliani kwa wingi. Hakikisha  katika  kila  mlo  wako, inakuwepo  mboga  ya  giligiliani  pembeni.

VITU   VINGINE VYA   KUZINGATIA..
Pamoja na kutumia  lishe  hii  ya  asili  kwa  kufuata  utaratibu  huo  hapo  juu, unashauriwa  kuzingatia  matumizi  ya  vyakula  vifuatavyo:

TANGAWIZI
Jenga  tabia  ya  kuwa  una tumia  tangawizi, kila  mara  upatapo  nafasi.  Utaratibu  wa  jinsi  ya  kutayarisha  tangawizi ni  kama  ifuatavyo :

Chukua kipande  kimoja  cha  tangawizi, kisha  kitwange  halafu ongeza  vikombe  viwili vya  maji  vyenye  ujazo  wa  milimita  mia  mbili  na  hamsini ( 250 mills). Chemsha pamoja  kisha ongeza  maziwa  kiasi cha  robo lita  na  sukari ili kupata  ladha.  Fanya  hivi  kila  mara  uapatapo  nafasi. Ukiweza kufanya  hivyo walau  mara  mbili  kwa  siku, itakuwa  vizuri  zaidi.

  AU  chukua  kipande  kimoja  cha  tangawizi, kitwange kisha  chemsha pamoja  na  chumvi nusu  kijiko  kidogo  kwenye  maji kiasi  cha  nusu   lita  halafu tumia  kunywa  kikombe  kimoja  nusu  saa  kabla  ya  kula  chakula chako  cha  asubuhi, mchana  na usiku.

HIRIKI
Jenga utaratibu  wa  kuwa  unakunywa  mara  kwa  mara  chai  iliyo  changanywa  na  hiriki.

MACHUNGWA
Jenga utaratibu  wa  kuwa  unakula  machungwa kwa  wingi,  kwa  kadri utakavyo  weza. Unashauriwa  kuwa  unachanganya na  chumvi  kidogo  pamoja  na  pilipili  manga.

KWA  MAHITAJI  YAKO  YA  DAWA-LISHE  YA  KUNENEPESHA  & KUONGEZA  MWILI  PAMOJA  NA  ASALI  YA  TENDE.

Kwa  mahitaji  yako  ya  DAWA-LISHE ya  kuongeza & kunenepesha  mwili, pamoja  na  asali  ya  tende, fika  katika  duka  la  NEEMA  HERBALIST.

Tunapatikana  UBUNGO  jijini  DAR  ES  SALAAM, jirani  na  SHULE  YA  MSINGI   UBUNGO  NATIONAL  HOUSING  nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA.

WASILIANA  NASI  KWA  SIMU  NAMBA  0766 53 83 84.

Kwa wateja  wetu  waliopo  jijini  Dar  Es  Salaam, ambao  hawana  nafasi  ya  kufika  dukani  kwetu  Ubungo, tunayo  huduma  ya  kuwapelekea  dawa  mahali  walipo ( HOME & OFFICE  DELIVERY  )

Kwa wateja  waliopo  nje  ya  mkoa   wa  Dar  Es  Salaam,  watatumiwa  dawa  kwa  kutumia  mabasi  mbalimbali.

Kwa  wateja  waliopo  Zanzibar, watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa  boti.

Kwa  wateja  waliopo  ughaibuni, watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  au  DHL.

Na kwa  taarifa  zaidi  kuhusu  huduma  zetu, tutembelee  kila  siku  katika  blogu  yetu :

Viongozi wa Dini Watangaza Siku Saba za Kumwombea Rais Magufuli

$
0
0
Na Jonas Kamaleki- MAELEZO
Viongozi wa dini wametangaza maombi ya siku saba nchi nzima kumwombea Rais John Pombe Magufuli ili aendelee na juhudi zake za kulinda raslimali za watanzania kwa manufaa ya Taifa kwa ujumla.

Hayo yalisemwa jana jijini Dar es Salaam katika mahojiano maalum na Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa ya Maadili, Amani na Haki za Binadamu kwa jamii ya dini zote, Askofu William Mwamalanga kwa niaba ya viongozi wa dini.

“Tumeamua kufanya maombi ya siku saba kwa kumtaka kila mtanzania popote alipo kutembea hatua saba kila siku akimwombea Mhe. Rais Magufuli ili Mungu amlinde pamoja na anaofanyanao kazi kwa usahihi (uaminifu)”, alisema Askofu Mwamalanga.

Ndani ya siku hizo saba kila mtanzania atakuwa ametembea jumla ya hatua 49 akimwombea Rais Magufuli na wazalendo wenzake.

Kwa mujibu wa Kiongozi huyo wa Dini, maombi hayo yataanza leo Alhamisi Juni 15 nchi nzima na yatajumuisha watu wa dini zote nchini, yaani madhehebu ya Kiislam, Kikristo, Kihindu, Budha na madhehebu mengine.

Maombi haya yanafanyika baada ya kuona kuwa Mhe. Rais Magufuli anachukua hatua madhubuti za kutaka waliohusika kwa namna yoyote kuiba raslimali za Taifa hususani madini, wanachukuliwa hatua na kuitaka kampuni ya ACCASIA kulipa kile ambacho walichukua kinyume cha sheria.

Askofu Mwamalanga alisema kuwa Kamati yake inamwomba Rais Magufuli achukue hatua za haraka kudhibiti raslimali za nchi kwa upande wa Wizara ya Maliasili na Utalii ambako mali nyingi zinatoroshwa na wajanja wachache.

Kamati hiyo ya Kitaifa ya Maadili, Amani na Haki za Binadamu kwa jamii ya dini zote imemwomba Mhe. Rais aziunganishe Wizara za Nishati na Madini na Maliasili na Utalii na kuunda wizara moja ambayo itasimamia kwa karibu raslimali za watanzania.

“Tunamwomba Rais Magufuli amchague mtu makini na mzalendo mwenye uchungu na nchi hii ili asimamie wizara hiyo, na nina hakika wizara hiyo ikisimamiwa vizuri, ndoto ya Rais ya kuifanya Tanzania kuwa nchi mhisani itatimia kwa kuwa hapa Mungu ametujalia kila kitu”,alisema Askofu Mwamalanga.

Viongozi hao wamempongeza Rais Magufuli kwa Uzalendo na Ujasri alionao katika kulinda raslimali za Taifa na kupambana na maovu. Wamesema ni kiongozi wa kuigwa na Marais au viongozi Duniani kote.

Kuhusu suala la walioachishwa kazi kutokana na kuwa na vyeti feki, Askofu Mwamalanga alisema kuwa Kamati inamwomba Mhe Rais kuwasamehe wale ambao wameitumikia nchi hii kati ya miaka mitano na 30 ili walau wapatiwe kifuta jasho licha ya kwamba walitumika bila kuwa na vyeti halali vya Kidato cha nne.

“Msamaha tunaoomba si wa kuwarudisha kazini bali tunaomba kwa ajili ya kupata kiinua mgongo kwani wengine walitumika kwa uaminifu na hata kupewa tuzo za ufanyakazi hodari (bora) hasa katika sekta za Afya,wauguzi, Elimu na maeneo mengine”, alisema Askofu Mwamalanga.

Mapema wiki hii, Rais Magufuli alipokea ripoti ya pili ya uchunguzi wa makinikia ambayo iliwajumuisha wanasheria na wachumi. Katika ripoti hiyo ilibainika kuwa kiasi kikubwa cha madini kilichukuliwa bila watanzania kupata chochote. Takriban madini yenye thamani ya shilingi trilioni 108 yalisafirishwa nje ya nchi bila Tanzania kupata faida kutokana na madini hayo.

Mama Amuua Mwanae Kwa Kumtupa Ziwa Victoria

$
0
0
Jeshi la polisi mkoani Mwanza linawashikilia wanawake wawili katika matukio mawili tofauti likiwemo la mwanamke mmoja kumuua mwanaye.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi alisema katika tukio la kwanza, mwanamke mmoja mkazi wa Kisiwa cha Nyamango, Kijiji cha Soswa katika Tarafa ya Buchosa, Nyamisi Bahati (27) anashikiliwa na polisi akituhumiwa kumuua mtoto wake, Sakimu Hassan mwenye umri wa miezi saba kwa kumtupa ndani ya Ziwa Victoria.

Msangi alisema tukio hilo lilitokea juzi saa moja usiku wakati mtuhumiwa alipotoka nyumbani kwake kwenda kuwasalimia wazazi wake huku ikidaiwa kuwa aliondoka akiwa na mtoto wake.

“Akiwa nyumbani kwao ghafla alitoka nje akiwa na mtoto wake, ilionekana kama anaenda kumbembeleza baada ya muda alirejea akiwa hana mtoto ndipo bibi yake alipoanza kuhoji alipo mtoto,” alisema Msangi.

Alisema baada ya kumhoji zaidi, baadaye mtuhumiwa alikiri kumtupa ndani ya Ziwa Victoria.

Baada ya bibi kupokea taarifa hiyo ilimshtua na kuanza kupiga kelele kuomba msaada kwa watu ili waweze kusaidia kumuokoa mtoto huyo.

Kamanda huyo aliendelea kueleza kuwa majirani waliokusanyika katika tukio hilo walisaidia kutoa taarifa kituo cha polisi ambao nao walifika eneo hilo na kuanza shughuli ya uokozi hadi walipofanikiwa kuupata mwili wa marehemu.

Msangi alisema uchunguzi wa awali umebainisha kuwa mtuhumiwa ana matatizo ya akili ingawa bado wapo kwenye upelelezi na mahojiano kujua ukweli wa jambo hilo.

Katika tukio la pili, polisi wanamshikilia mkazi wa mtaa wa Malulu, Kata ya Igogo wilayani Nyamagana, Ghati Chacha (36) kwa madai ya kukutwa na pombe haramu ya gongo lita 23.

UKATILI: Msichana Asimulia Jinsi Kondakta na Dereva Walivyombaka Kwa Zamu Ndani ya Daladala

$
0
0
Dereva na kondakta wa daladala zinazofanya safari ndani ya Manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro, Soweto–Mbuyuni wanatuhumiwa kumbaka abiria wao kwa zamu na kumuumiza sehemu za siri.

Tukio hilo lililotokea Juni 12 saa moja jioni maeneo ya Veta katika uchochoro uliopo karibu na shule ya Northen Highland iliyo umbali wa mita 400 kutoka barabara ya lami.

Akielezea tukio hilo, binti huyo mwenye umri wa miaka 20 alisema alitumwa na bosi wake kwenda kununua mahitaji ya nyumbani Soko la Mbuyuni na kumuelekeza kuwa akimaliza apande basi la Soweto sokoni hapo na ashukie mwisho ambako angechukua bodaboda ya kumfikisha nyumbani.

“Nilipomuuliza konda akaniambia ndiyo na nikampigia bodaboda ambaye nilipewa namba na bosi wangu ili ampe maelekezo huyo kondakta sehemu ambayo watanishusha ili yeye anichukue hapo na wakazungumza na baadaye akanirejeshea simu yangu,” alisema msichana huyo.

Alisema baada ya hapo safari ya kutoka Mbuyuni kwenda Soweto ilianza.

“Kwa kuwa nilikuwa mgeni, sikuelewa hata kituo kipi cha kushukia. Niliendelea kukaa hadi nilipoona watu wote wameisha kwenye (Toyota) Hiace, ndipo nikamuuliza konda kwa nini hanishushi akasema bado sijafika,” alisema.

Anasema alishangaa kuona dereva anaenda kuegesha gari uchochoroni na aliposimama, kondakta akashuka, akidai anaenda kujisaidia. “Aliporudi kwanye gari alifunga mlango na wakazima taa na kuanza kuniambia kuwa wamenipenda kama ninataka kuwa hai nikubaliane na wanachokitaka na nikikataa wataniua,” alisema binti huyo.

Alisema baadaye dereva alitoka kwenye usukani na kumfuata alipokaa na kuanza kumpapasa.

Alisema alipoona hivyo alijaribu kutoka nje kupitia dirishani, lakini walimvuta ndani huku wakimfunga mdomo asipige kelele na kumtishia kumuua.

“Nilikubali yaishe na nikatulia. Akaanza dereva huku kondakta akinishika mikono na baada ya kumaliza alichofanya, konda naye akaja akafanya hivyohivyo. Nilisikia maumivu, lakini nilishindwa kupiga kelele kwa kuwa walinitisha kuwa wangeniua,” alisema dada huyo.

“Walipomaliza kufanya ukatili huo, konda alimwambia dereva kuwa waniue kwa kuwa nimeshawatambua, lakini dereva akasema hakuna haja.”

Alisema katika mabishano hayo alijikaza na kuwaambia kuwa yeye ni mgeni na hajui popote kwa hiyo hatamwambia mtu kwa kuwa hilo ni tukio la aibu.

“Walikubaliana na mimi na wakaniambia kuwa ni kweli kubakwa ni kitendo cha aibu kwa hiyo nikimwambia mtu nitatengwa na jamii. Nikawaomba wanisaidie sehemu ya kupata msaada niweze kufika nyumbani,” alisema.

Alisema baadaye aliwaomba aende kuchukua kiatu chake kilichokuwa kimedondoka dirishani wakati akitaka kuruka, na walipomruhusu akatumia nafasi hiyo kusoma namba za gari.

Mlezi wake, Abdi Massawe alisema baada ya kufika nyumbani akiwa na bodaboda, binti huyo alimweleza tukio hilo na akatoa taarifa polisi ambako alipewa fomu ya matibabu aliyoitumia Hospitali ya Mawenzi, ambako vipimo vilithibitisha kuwa alibakwa.

“Huyu binti ni mgeni kutoka mkoani Singida. Hapa Moshi ana mwezi mmoja tu,” alisema Masssawe.

Massawe alisema baada ya hapo alianza kusaka daladala hilo kwa kutumia namba alizopewa na binti huyo na kufanikiwa kuikuta maeneo ya Soweto. Baadaye aliwapigia simu polisi ambao walifika na kushusha abiria waliokuwamo na kuipeleka kituoni.

Alisema wakati dereva akiendelea na mahojiano kondakta alitoroka.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Koka Moita alisema derava wa gari hilo aliyemtaja kuwa ni Salimu Abdalla (30) anashikiliwa na polisi ambao wanaendelea kumtafuta kondakta ambaye alitoroka akiwa katika kituo cha polisi.

Kwa sasa binti huyo anatibiwa Hospitali ya Mawenzi.

Tundu Lissu,Abdallah Mtolea Wapinga Azimio la Bunge Kumpongeza Rais Magufuli

$
0
0
Azimio la Bunge la kumpongeza Rais John Magufuli kwa hatua anazochukua kukabiliana na upotevu wa mapato ya serikali katika sekta ya madini jana liligawa Bunge baada ya wabunge wa upinzani kulikataa wakati wenzao wa CCM wakilikubali.

Mwenyekiti wa Bunge, Musa Zungu alipowahoji wabunge kama wanakubali azimio hilo, wabunge wote wa CCM waliitikia "ndiyooo" wakati wale wa upinzani walisema "siyooo".

Azimio hilo lenye kurasa mbili liliwasilishwa bungeni jana na Mbunge wa Newala Mjini (CCM), George Mkuchika na baada ya hapo wabunge walipata nafasi ya kulijadili.

“Bunge linamuunga mkono Rais John Magufuli na lipo tayari kutoa ushirikiano wa dhati kadri itakavyohitajika kuhakikisha juhudi hizi hazipotei bure na sekta ya madini inachangia maendeleo ya wananchi na Taifa kwa ujumla,” alisema Mkuchika ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Haki, Kinga, Maadili na Madaraka ya Bunge.

Lakini, aliposimama akiwa wa kwanza kuchangia hoja ya maazimio hayo, Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu alipinga akisema ni kinyume na majukumu ya Bunge hivyo kulitaka lisiendelee na taratibu za kumpongeza Rais akisema alichokifanya si kipya.

“Kazi ya Bunge ni kuishauri Serikali, siyo kuipongeza au kuiimbia mapambio. Hili siyo azimio la Bunge, bali wana-CCM kumpongeza mwenyekiti wao,” alisema mnadhimu huyo wa Kambi ya Upinzani Bungeni.

Alisema kinachofanywa na Rais Magufuli kilifanywa pia na watangulizi wake waliounda tume kadhaa na kwamba mpaka azimio hilo linajadiliwa, bado usafirishaji wa dhahabu inayochimbwa kwenye migodi mbalimbali nchini unaendelea.

“Dhahabu na madini mengine yanaendelea kusafirishwa hivi sasa. Ripoti za Profesa Mruma na Profesa Osoro ni professorial rubbish. Ni uongo, uongo, uongo,” alisema Lissu.

Ingawa alitakiwa kufuta neno rubbish kwenye mchango wake, Lissu alifafanua kwamba ripoti za wenyeviti hao wa kamati mbili za Rais za kuchunguza makontena 277 ya mchanga wa dhahabu, hazina taarifa sahihi.

Kuhusu azimio hilo kutokuwa na jipya, alisema Rais mstaafu, Benjamin Mkapa aliunda kamati ya Jenerali (Robert) Mboma mwaka 2002, ya Dk (Jonas) Kipokola mwaka 2004 kisha ya Dk (Enos) Bukuku mwaka 2005. Alisema hata Rais wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete naye aliunda mbili za Lawrence Masha na Jaji Mark Bomani.

Alisema kama Bunge linataka kupongeza kuhusiana na kamati zilizoundwa na Rais Magufuli, basi halina budi kuanza na watangulizi hao ambao walifanya kama anachokifanya sasa kwa masilahi ya Taifa huku akipendekeza semina itolewe kwa wabunge ili kuwaongezea uelewa wa masuala ya madini na kuwafanya wachangie wakiwa na ufahamu wa kutosha kuhusu sekta hiyo.

Lissu alipingwa na Mbunge wa Mtera (CCM), Livingstone Lusinde ambaye alitoa sababu za kumpongeza Rais Magufuli akisema kuna tofauti kati ya kamati alizoziunda na zile za watangulizi wake.

“Rais ameenda mbali zaidi. Ripoti imepokewa hadharani na wananchi wote wameisikia. Hii ni hatua ya mbele. Haiwezekani Taifa lisimpongeze Rais anapofanya mambo yanayoonekana,” alisema.

Alisema ameona clip (video fupi) za mawaziri wakuu wastaafu waliohamia upinzani; Edward Lowassa na Frederick Sumaye wakimpongeza Rais kwa hatua zake.

Lakini, Mbunge wa Temeke (CUF), Abdallah Mtolea alionekana kuungana na Lissu akiongeza kwamba maazimio hayo hayakuwa sawa kwa maelezo kwamba kilichofanywa na Rais Magufuli mpaka sasa hakijapiga hatua kubwa zaidi ya kilichofanywa na watangulizi wake.

Alisema suala la msingi ni kudhibiti wizi wa rasilimali nchini akikumbusha kwamba Kikwete pia aliunda tume lakini hata baada ya kupelekewa ripoti, hakufanya chochote hatua ambayo Rais Magufuli amefikia mpaka sasa kwenye vita aliyoianzisha.

Alisema hoja ya wizi wa madini ilianzishwa siku nyingi na wabunge ambao walionekana kuwa si wazalendo. “Kama Mkapa na Kikwete tungewapongeza kwa kuunda tume leo ingekuwaje? Bunge tusiwe washangiliaji,” alisema.

Alikumbusha pia kwamba Mbunge wa Kigoma Kaskazini (CCM), Peter Serukamba alipiga kelele, Dk Hamis Kigwangallah wa Nzega Vijijini (CCM) aliteswa, Tundu Lissu, Zitto Kabwe wa Kigoma Mjini (ACT Wazalendo) na John Mnyika wa Kibamba (Chadema) walilizungumza suala hilo lakini walibezwa.

Alisema kwa kuwa suala hilo sasa linazungumzwa na mtu anayependwa, linaungwa mkono.

Katika mchango wake, Hasunga ambaye ndiye aliyekuwa mtoa hoja alisema hatua ya Rais kuzuia usafirishaji wa mchanga nje ni muhimu inayopaswa kuungwa mkono na Watanzania wote.

“Jimboni na mkoani kwangu kuna madini mengi, hatustahili kuwa maskini,” alisema.

Akiunga mkono hoja hiyo, Mbunge wa Mwibara (CCM), Kangi Lugola alisema anachokifanya Rais Magufuli ndicho alichoahidi hata kabla hajashika wadhifa huo,

“Aliahidi watu watalima kwa meno, tunaona mafisadi wakilima kwa meno. Namuomba hata watu wanaowatetea wezi hawa awalimishe kwa meno pia.”

Mbunge huyo ambaye aghalabu huzungumza kwa mbwembwe aliungwa mkono na Mbunge wa Rufiji (CCM), Mohamed Mchengerwa ambaye alitaka neno uzalendo liondolewe kwenye kamusi ya Kiswahili endapo kuna mtu atapinga yanayofanywa na Rais Magufuli.

“Tunaamini mambo haya yakitekelezwa vyema tutakuwa na barabara za lami na hatutakuwa na deni la Taifa,” alisema Mchengerwa.

William Ngeleja : Kutuhumiwa siyo kukutwa na hatia......Maisha yanaendelea

$
0
0
Mbunge wa jimbo la Sengerema, William Ngeleja, amesema kutuhumiwa siyo kukutwa na hatia na maisha yanaendelea.

Ngeleja ambaye ni mmoja wa watuhumiwa waliotajwa kwenye Ripoti ya pili Rais ya kuchunguza Makinikia, ameyasema hayo leo alipokuwa akichangia Bajeti Kuu ya Serikali ya 2017/18.

Wakati akiendelea na mchango wake, aliwataka wabunge kusimama ili kuonyesha kumuunga mkono Rais John Magufuli kwa kupambana na wizi wa rasilimali za Watanzania ikiwamo dhahabu.

Wakati akiendelea na mchango wake huo, Mbunge wa Mbozi, Pascal Haonga, aliomba kutoa taarifa kwa mzungumzaji akimtaka Ngeleja kueleza uhusika wake kwenye kashfa hiyo kwa sababu kamati imemtaja.

Baada ya kauli hiyo, Mwenyekiti wa Bunge, Mussa Azzan Zungu, alimtaka Ngeleja kuendelea na mchango wake na kuwa alichotoa Mbunge Haonga siyo taarifa.

Hata hivyo kabla ya kuendelea na mchango wake, Ngeleja alisema” kutuhumiwa siyo kukutwa na hatia na maisha yanaendelea”.

NCCR- Mageuzi Wataka CCM Iombe Radhi Sakata la Mchanga wa Madini

$
0
0
Baada  ya Rais, Dk. John Magufuli kukabidhiwa ripoti ya mchanga wa dhahabu, Chama cha NCCR-Mageuzi kimekitaka Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuwaomba radhi Watanzania.

Katibu Mkuu wa NCCR-Mageuzi, Juju Danda, alisema katika taarifa yake kwa vyombo vya habari jana, kwamba ripoti hiyo ya mchanga imeanika uozo uliosababishwa na CCM kwa kipindi kirefu ilichokaa madarakani.

“Kwa maana hiyo, ni vema CCM wakakaa, wajiulize na kujipima kwa kuwaomba radhi Watanzania ambao wamekuwa wakiishi maisha magumu yaliyosababishwa na CCM.

“Kamati mbili zilizoundwa na Rais Dk. John Magufuli, zimethibitisha pasipo shaka, kuwa Watanzania wameibiwa tena kwa kiwango kikubwa ingawa mwaka 2007, Kamati ya Bomani ilitoa maoni na mapendekezo kadhaa yaliyohusu sekta ya madini ingawa maoni hayo hayakufanyiwa kazi,”alisema.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, kukiri kosa ni uungwana na kwamba CCM wanatakiwa kujitokeza hadharani na kuwaomba radhi Watanzania, kuwa hawakuwatendea haki kutokana wizi uliokuwa ukifanyika katika sekta ya madini.

Pamoja na hayo, Danda aliiomba Serikali kuhakikisha inachukua hatua za kisheria kwa yeyote aliyeshiriki katika kuangamiza uchumi wa Taifa kwa kusaini mikataba mibovu katika sekta ya madini.

 “NCCR-Mageuzi, tunafarijika kuona tuliyokuwa tukiyapigania kwa miaka mingi, yanaendelea kufichuliwa waziwazi  na ukweli unazidi kubainika kupitia kamati zilizoundwa na Rais.

“Pia ni muda muafaka wa kupitia upya sheria zote zinazohusu masuala ya madini na ni wakati muafaka wa wataalamu wazalendo kuipitia tena Katiba iliyopendekezwa kwa kuwa inatoa mwelekeo wa kuwadhibiti wabadhirifu,” alisema.

RIPOTI YA TWAWEZA: Rais Magufuli Ameshuka Umaarufu kutoka asilimia 96 mwezi Juni mwaka jana hadi asilimia 71 ya June mwaka huu

$
0
0
Asilimia 71 ya wananchi wanaukubali utendaji wa Rais Magufuli tangu alipoingia madarakani. Kiwango hiki kimeshuka kutoka asilimia 96 mwezi Juni 2016.  Viwango vya kukubalika kwa Rais vinatofautiana katika makundi mbalimbali:
  • Asilimia 68 wenye umri chini ya miaka 30 wanamkubali Rais ikilinganishwa na asilimia 82 wenye umri zaidi ya miaka 50
  • Asilimia 75 ya wananchi wenye elimu ya msingi au chini yake wanamkubali Rais ikilinganishwa na asilimia 63 ya wale wenye elimu ya sekondari au zaidi
  • Asilimia 75 ya wananchi masikini wanamkubali Rais ikilinganishwa na asilimia 66 ya wananchi matajiri
Viwango vya kukubalika kwa viongozi wengine navyo pia vimeshuka katika kipindi hicho hicho.
  • Wabunge:  Kukubalika kwa utendaji wa wabunge kumeshuka kutoka asilimia 79 (Juni 2016) hadi asilimia 58 (Aprili 2017).
  • Madiwani: Kukubalika kwa utendaji wa madiwani kumeshuka kutoka asilimia 74 (Juni 2016) hadi asilimia 59 (Aprili 2017).
  • Wenyeviti wa vijiji/mitaa: Kukubalika kwa utendaji wa wenyeviti wa vijiji/mitaa kumeshuka kutoka asilimia 78 (Juni 2016) hadi asilimia 66 (Aprili 2017).
Matokeo haya yametolewa na Twaweza katika utafiti wake uitwao Matarajio na matokeo; Vipaumbele, utendaji na siasa nchini Tanzania. 

Utafiti huo unatokana na takwimu kutoka Sauti za Wananchi, utafiti wa kwanza barani Afrika wenye uwakilishi wa kitaifa unaotumia simu za mikononi. 

Matokeo hayo yanatokana na takwimu zilizokusanywa mwezi Aprili mwaka 2017 kutoka kwa wahojiwa 1,805 kutoka maeneo mbalimbali Tanzania Bara (Zanzibar haihusiki kwenye matokeo haya).
 
Kukubalika kwa vyama vya siasa kunatoa taswira mchanganyiko. Kukubalika kwa CCM kumeendelea kuimarika, ikiwa ni kati ya asilimia 54 na asilimia 65 kati ya mwaka 2012 na 2017, Baada ya kushuka mwaka 2013 na 2014 ambapo kiwango cha kukubalika kilifikia asilimia 54 kutoka asilimia 65 ya 2012. 

Kukubalika kwa CCM kumeendelea kubaki katika kiwango hicho hicho cha asilimia 62 tangu uchaguzi wa mwaka 2015 na asilimia 63 mwaka 2017. Kukubalika kwa Chadema kumeshuka hadi asilimia 17 mwaka 2017 kutoka asilimia 32 mwaka 2013.
 
CCM inakubalika zaidi miongoni mwa wazee (asilimia 80), ukilinganisha na asilimia 55 ya vijana. Wanawake (asilimia 68) wanaikubali CCM kuliko wanaume (asilimia 58), maeneo ya vijijini (asilimia 66) kuliko maeneo ya mijini (asilimia 57), na wananchi masikini (asilimia 69) kuliko matajiri (asilimia 53). Wananchi wenye elimu ya sekondari, elimu ya ufundi au elimu ya juu wanaikubali CCM kwa asilimia 46.
 
Kukubalika kwa Chadema kwa ujumla unafuata mtiririko tofauti: ni mkubwa miongoni mwa vijana, wanaume, watu matajiri na wenye kiwango kikubwa cha elimu.
 
Ndani ya kipindi cha miaka miwili tu, vipaumbele vya wananchi vimebadilika sana. Mwaka 2015, asilimia 34 ya wananchi walitaja umasikini na uchumi duni kama moja ya vipaumbele vyao vikubwa ikilinganishwa na asilimia 60 waliotaja masuala hayo mwaka 2017. 

Mwaka 2015, ni asilimia 9 waliotaja upungufu wa chakula au njaa kama kipaumbele chao ikilinganishwa na asilimia 57 mwaka 2017.
 
Katika kipindi hicho hicho, wasiwasi wa wananchi juu ya huduma za umma na rushwa umepungua.

Asilimia ya wananchi wanaotaja masuala yafuatayo kuwa miongoni mwa changamoto kuu tatu zinazoikabili nchi:
  • Afya: asilimia 40 mwaka 2017 ikilinganishwa na asilimia 59 mwaka 2015.
  • Elimu: asilimia 22 mwaka 2017 ikilinganishwa na asilimia 44 mwaka 2015.
  • Miundombinu: asilimia 21 mwaka 2017 ikilinganishwa na asilimia 32 mwaka 2015.
  • Huduma ya maji: asilimia 19 mwaka 2017 ikilinganishwa na asilimia 46 mwaka 2015.
  • Rushwa: asilimia 10 mwaka 2017 ikilinganishwa na asilimia 28 mwaka 2015.

==>Soma FULL  Ripoti Hapo Chini

Taarifa ya Kampuni ya Barrick baada ya kufanya mazungumzo na Rais Dkt Magufuli kuhusu sakata la mchanga wa madini.

AUDIO: Abdallah Ulega( Mbuge CCM) Awafananisha Wapinzania Na POPO

$
0
0
Mbunge wa Mkuranga kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Abdallah Ulega amewafananisha wabunge wa upinzani na popo kuwa hawaeleweki na kusema wamekuwa watetezi wa wawekezaji ambao wao wamewatuhumu kuwa ni wezi wa madini.

Mbunge huyo amesema hayo  bungeni akisema kuwa wapinzani hao leo limewashuka baada ya jana Rais Magufuli kukutana na  Mwenyekiti wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation ambayo ni mmiliki mkubwa wa kampuni ya Acacia Mining Limited Prof. John L. Thornton na kukubaliana kuwa kampuni hiyo ipo tayari kufanya mazungumzo na Serikali ya Tanzania ili kulipa fedha ambazo Tanzania imezipoteza kutokana na kampuni hiyo kuendesha shughuli zake hapa nchini.

"Popo hajafahamika kama ni mnyama au ndege mpaka hivi leo na hawa wenzetu hata sitaki kuwaita vinyonga naomba niwaite popo maanake hawajafahamika kama ndege au wanyama na leo limewashuka kwani walijigeuza kuwa mawakili wa wale ambao sisi tunawatuhumu kwamba ni wezi wetu na yule anayehusika Mkuu amewathibitishia mchana wa leo (jana) ameingia na amekiri mwenyewe kwa kinywa chake ya kwamba wapo tayari kulipa pesa ambazo tunawadai na tena lile lililokuwa linaonekana jambo gumu la kujenga kinu cha kuchenjua madini amelichukua na amesema yupo tayari kujenga" alisema Ulega

Mbunge huyo alikwenda mbali zaidi na kesema bara la Afrika limekuwa na bahati mbaya kwani wapinzani wa Afrika wamekuwa wakitumika na mabeberu miaka yote na kusema wao kama Chama Cha Mapinduzi wanakila sababu ya kutamba kwa kuwa Ilani ya Uchaguzi ya CCM imeweka sawa na kutamka namna nzuri ya kusimamia shughuli za madini. 

==>Msikilize hapo chini

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya June 16

Serikali yalifungia gazeti la MAWIO kwa kukiuka maagizo

$
0
0
Alhamisi ya Juni, 15 Serikali ilitangaza kulifunga gazeti la MAWIO kutochapishwa kwa muda wa miezi 24, sababu ikitajwa kuwa ni kuchapisha mbele picha ya Marais wastaafu, Mkapa na Kikwete na kuwahusisha na sakata la mchanga wa madini. 
 
==>Hapo chini kuna video ya Mkurugenzi Mtendaji wa Habari-MAELEZO, Dk. Hassan Abbas akitangaza kulifunga gazeti hilo.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images