Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

CHADEMA Wampa Kazi Mke wa Lowassa

0
0
Wanawake wa Chadema wamemtwishwa Regina Lowassa mzigo wa kuongoza mapambano ya ushindi katika Uchaguzi Mkuu wa 2020.

Akizungumza na wajumbe wa Baraza Kuu la Wanawake wa Chadema (Bawacha) mjini Dodoma jana, Regina ambaye ni mke wa waziri mkuu wa zamani Edward Lowassa, alisema maandalizi ya uchaguzi huo yanapaswa kuanza sasa.

Katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, Lowassa aligombea urais kupitia Chadema kwa kushirikiana na vyama vilivyounda umoja wa katiba ya Wananchi (Ukawa) na hivyo kuweka ushindani mkubwa dhidi ya chama tawala, ingawa hakushinda.

Jana, Regina alisema ushindi wa chama hicho uko mikononi mwa wanawake wa Tanzania. “Kwanza niwashukuru sana kwa mapambamo mliyoyafanya mwaka 2015. Nataka mfahamu kuwa bado Chadema inapendwa na ina nguvu kubwa kuliko wakati mwingine. Msikatishwe tamaa bali tusonge mbele,” alisema Regina.

Mama huyo aliwataka wajumbe kujiamini zaidi na kupeleka ujumbe kwa wenzao ambao wamedhamiria kufanya mageuzi makubwa, lakini akawataka wasilale.

Mwenyekiti wa Bawacha, Halima Mdee aliwataka wanawake kujitoa zaidi katika kukisaidia chama hicho, hasa katika maandalizi ya uchaguzi ujao.

Mdee aliwashauri wanawake wenye nafasi, kama wabunge, kutumia nafasi zao kukisaidia chama.

Alisema wakati walionao kwa sasa si wa kujivunia nafasi walizonazo, bali wanapaswa kuongeza nguvu zaidi na kugombea nafasi za uongozi wa juu wa Chadema ili waendeleze mapambano ya ukombozi.

“Katika kipindi hiki ambacho tunaona demokrasia inaminywa kwa vyama vyote vya siasa, ni vema wanawake ambao ni jeshi kubwa tukawa mstari wa mbele katika mapambano si kurudi nyuma. Lazima kuwa na nidhamu ndani na nje ya chama ili tufanikiwe katika vita hii,” alisema Mdee.

Katika kuonyesha msisitizo huo, alimuagiza katibu mkuu wa Bawacha, Grace Tendega kuwaandikia barua wabunge ambao hawakuhudhuria kikao cha jana ili wajieleze kabla ya kuchukuliwa hatua.

Alisema ni jambo la aibu na fedheha kwa viongozi kutoka mbali wakasafiri hadi Dodoma kwa ajili ya kikao, lakini wabunge ambao wako mjini hapa wakashindwa kuhudhuria.

Mbunge wa Viti Maalumu, Devotha Minja alisema chachu ya ushindi na mapambano ndani ya chama hicho kwa sasa ni kubwa kwa kuwa wameamua kufanya kazi usiku na mchana kwa ajili ya kuisaidia Chadema.

LIVE: Kamati ya Pili ya Mchanga wa Madini Ikiwasilisha Ripoti Yake kwa Rais Magufuli

0
0
Leo Kamati ya Pili ya Mchanga wa Madini Inawasilisha Ripoti Yake kwa Rais Magufuli. Fuatilia Matangazo ya Moja Kwa Moja Hapo Chini

Serikali yabaini mbinu ya utakatishaji fedha kwa kutumia mifugo.

Kutana na Maajabu ya Mtabibu CHIEF SULTAN(MAKATA WA MAKATANI) Mganga wa Waganga Sasa Yupo Mikoa Yote Tanzania

0
0
Kutana Maajabu ya Mtabibu CHIEF SULTAN(MAKATA WA MAKATANI) Mganga wa Waganga Sasa Yupo Mikoa Yote Tanzania
 
Pia anatoa Tiba kwa Njia ya Simu ukiwa popote Pale Tanzania au Nje ya Tanzania..
CHIEF SULTAN ni Mtabibu na Mtafiti wa Dawa za Asili ya Africa, na Duniani Katika utoaji wa Tiba za Asili..
Je unasumbulia na Mapenzi..?


(Umeachwa na Umpendae awe Mume/ Mke au mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine na Bado Unampenda?) Umejaribu sehemu Nyingi bila Mafanikio?Wasiliana na CHIEF SULTAN Akusaidie Kumshika Umpendae Asikusaliti(LIMBWATA) Kumtawala Mpenzi wako kwa sababu Maalum..Anauwezo wa Kusambalatisha Mahusiano yao ndani ya siku Moja tu.


Je Unasumbuliwa na Madeni?
Biashara yako Haina wateja?
Unatatizo la kutokushika Mimba na umehangaika sehemu nyingi bila mafanikio?
Wasiliana na CHIEF SULTAN Kwa Majibu ya Maswali yako..
Anasafisha NYOTA na Kutoa PETE za BAHATI kuendana na NYOTA yako. UTAJIRI USIO NA MASHARTI.(Magic Wallet_Pochi ya Maajabu Isio Isha Hela)


KUWA MAARUFU na KUJULIKANA
Kupandishwa CHEO na HESHIMA Mahala pa KAZI.
Utapewa Nguvu ya Kujilinda na MALI ZAKO zako na Mwili wako.. Huzuia Chuma Ulete katika Biashara.. Hurudisha MALI zilizo Potea au KUDHULUMIWA..
Mvuto wa Biashara na Mwili wako.
Hutibu kabisa Nguvu za Kiume na Kurefusha Uume kwa saizi Unayotaka.

Magonjwa Sugu(Miguu Kufa Ganzi, kisukari, Presha, Pumu nk.)Humaliza Kesi za Muda mrefu ndani ya siku 14 tu.


Anatoa NDAGU Zisizokuwa na Masharti.. Kwa maelezo Zaidi wasilina nae kwa 

 
whatsapp +255 0658 316 976
Call +255 755 911 233

LIVE UPDATES: Yanayojiri Toka Ikulu Wakati Rais Magufuli Akipokea Ripoti ya Pili ya Madini ya Mchanga

0
0
1.Kamati ya wanasheria na wachumi ya kuchunguza mchanga wa madini iliteuliwa Aprili 10 ikiongozwa na Prof. Nehemiah Osoro.

2.Miongoni mwa hadidu za rejea ambazo kamati ilipewa ni kujua idadi ya makotena yaliyosafirishwa nje ya nchi tangu 1998.

3.Kamati pia ilitakiwa kuchunguza kama Tanzania inauwezo wa kutengeneza 'smelter' nchini, gharama zake na muda utakaotumika. 

4.Kamati ilitakiwa kuchunguza tofauti ya mapato ambayo Tanzania ilipata na ambayo ilitakiwa kuyapata tangu mwaka 1998. 

5.ACACIA inayojinasibu kama mmiliki wa migodi ya Bulyanhulu na Buzwagi haijawahi kuwasilisha nyaraka za umiliki huo.

6. Kamati imebani kwa mujibu wa nyaraka kuwa kampuni ya ACACIA PLC haikusajiliwa nchini 

7.Kamati imebaini kuwa wamiliki wa makampuni ya madini nchini wametenda makosa mbalimbali ya jinai. 

8.Kamati imeridhia baadhi ya watumishi wa serikali, makampuni ya usafirishaji na TMAA wameliingiza Taifa hasara kwa makusud. 

9.Makampuni ya Pangea na Bulyahulu yamepatikana na hatia ya kuliingizia Taifa hasara kwa kutokutoa taarifa sahihi juu ya uzito wa makinikia:. 

9.Idadi na uzito wa makontena ya mchanga ulionekana kuwa mkubwa kwenye meli tofauti na kwenye nyaraka za bandarini. 

10.Baadhi ya makampuni ya wakala wa meli ziliwasilisha nyaraka za uongo za usafirishaji wa madini kati ya 1998 na 2017. 

11.Makontena 30 ya futi 20 yenye makinikia yalionekana kwenye nyaraka yamesafirishwa, lakini ukweli yalisafirishwa 33. 

12.Kupitia hati ya usafirishaji wa makontena melini, idadi kubwa ya makontena yalikuwa yakisafirishwa bila kuorodheshwa. 

13.Migodi ya Bulyanhulu na Pangea imekuwa ikipata faida lakini faida halisi haikuwa ikionyeshwa. 

14.Kamati imebaini makontena 44,277 kwa kiwango cha chini yalisafirishwa nje ya nchi kati ya 1998 na 2017. 

15.Viwango vya dhahabu kwa kila kontena ni 28kg, kwa miaka yote ni tani 1,240 kwa kiwango cha chini, thamani yake Tsh 108tril 

16.Jumla ya thamani ya madini yaliyosafirishwa nje ya nchi kati ya 1998 hadi 2017 ni trilioni 132.56 kwa kiwango cha chini.

17.Jumla ya thamani ya madini yaliyosafirishwa nje ya nchi kati ya 1998 hadi 2017 ni trilioni 229.9 kwa kiwango cha juu.

18.Jumla ya thamani ya madini yaliyosafirishwa nje ya nchi kati ya 1998 hadi 2017 kwa Kiwango cha wastani ni trilioni 188.58

19.Kodi ya Mapato ambayo Tanzania imepoteza tangu 1998 hadi Machi 2017 ni trilioni 55 katika usafirishaji wa makinikia. 

20.Kodi ya Zuio ambayo Tanzania imepoteza tangu 1998 hadi Machi 2017 ni bilioni 94 katika usafirishaji wa makinikia.

21.Mh Rais jumla ya Kodi tulizopoteza ni Sawa na makadirio ya bajeti ya serikali kwa kiwango cha Mwaka 2017/18 kwa miaka 2.

22.Taarifa ambazo zimekuwa sikiwasilishwa TMAA kuhusu uchenjuaji wa makinikia hazina ukweli wowote. 

23.Mh Rais kamati imepata mikataba ya mauzo ya uuzwaji Wa makinikia nje ya nchi kuwa serikali haihusiki kabisa.

24.Mikataba hiyo Mh Rais haina Masharti kuwa Serikali inapaswa kupewa taarifa ya uuzwaji wa Makinikia kutoka ktk migodi.

25.Mh Rais katika uchunguzi wetu Serikali ina hisa asilimia 15 ikauza 5 na kila mwaka kamishna au Waziri wa Fedha hupokea dola laki 1. 

26.Pangea Gold mine ina mikataba miwili ilisainiwa na Mh Daniel Yona baadaye Mh Nazir Karamagi serikali haina hisa Yoyote.

27.Mh Rais Mkataba wa North Mara ulisainiwa na Waziri Daniel Yona Mwaka 1999 baadaye Nazir Karamagi Mwaka 2017 

28.Mh Rais katika Mkataba wa Geita Gold Mine ulisainiwa na Mh Abdallah Kigoda na serikali haina Hisa hata moja. 

29.Kamati imebaini kuwa kumekuwa na uongezaji wa muda wa leseni na maeneo uchimbaji kinyume na sheria.

30.Mh Rais kamati imebaini kuwa Mh William Ngeleja na Sospeter Muhongo walitoa mikataba mipya bila kufuata sheria za nchi

31.Mh Rais Mkataba wa North Mara ulisainiwa na Waziri Daniel Yona Mwaka 1999 baadaye Nazir Karamagi Mwaka 2007 

32.Mh Rais mwanasheria mkuu wa serikali pamoja na makamishina wa madini Mh Andrew Chenge na Dalali kafumu walihusika ktk mikataba ya madini. 

33.Makampuni ya uchimbaji yakilipwa fedha haziwekwi kwenye mabenki ya ndani badala yake huwekwa kwenye mabenki ya nje.

34.Uwekaji wa fedha kwenye mabenki ya nje badala ya mabenki ya ndani, umechochea utoroshaji mkubwa wa fedha.

35. Makapuni mengi yamekuwa hayaajiri wazawa, na mgodi mmoja ulitaka kuleta walinzi kutoka nje ya nchi.

36.Hakuna mfumo uliowekwa na serikali wa kuhakikisha kunakuwa na ufuatiliaji wa ajira zinazotolewa katika migodi nchini.

37.Sheria ya madini inatoa uhuru wa madaraka kwa Waziri wa Madini katika kuingia kwenye mikataba ya madini.

38.Mh Rais Kamati inatoa mapendekezo kuwa mikataba yote ya madini ipelekwe bungeni kujadiliwa na kisha kupitishwa kwa maslahi ya Taifa.

39.Kamati imeona hakuna haja ya kupelekwa migogoro nje ya nchi,badala yake migogoro isikilizwe hapa nchini.

40.Kamati imeona kuwa kuna uwezo wa kujenga 'smelter' hapa nchini kwa kupitia vyanzo mbalimbali vya fedha kama mikopo..

 41.Licha ya kuwapo taasisi nyingi zenye dhamana ya kusimamia sekta ya madini, Tanzania imekuwa ikipata hasara kila mara.

42.Tanzania imekuwa ikipata hasara bandarini kutokana na kutokuwa na wakala wa meli. 

Mapendekezo:
1.Kamati inapendekeza serikali kupitia msajili wa makampuni iichukulie hatua kampuni ya Acacia kwa kufanyakazi kinyume na sheria. 

2. Serikali izuie usafirishaji wa makinikia nje ya nchi, hadi hapo wadaiwa watakapolipa madeni yao. 

3.Serikali iwachukulie hatua waliokuwa Mawaziri, Wanasheria Wakuu wa Serikali, Manaibu na watumishi wote waliohusika. 

4. Serikali ijenge smelter hapa nchini ili kuokoa fedha zinazopotea kutokana na usafirishaji wa makinikia. 

5. Serikali ichunguze mwenendo wa watumishi wa Mabaraza ya Kodi kwa kuchukua muda mrefu kutoa maamuzi ya mashauri ya kodi. 

6. Sheria iongeze kiwango cha adhabu kilichoanishwa katika ukiukwaji wa sheria ya madini nchini.

7. Sheria iweke kiwango maalumu cha hisa ambacho zitamilikiwa na serikali na kuiwezesha serikali kununua hisa. 

8.Sheria itamke bayana kuwa madini ni mali ya Watanzania na yamewekwe chini ya ofisi ya rais. 

9. Mikataba ya madini isiwe ya siri ni lazima iridhiwe na bunge

10. Sheria iondoe mamlaka aliyonayo Waziri wa Madini na Kamishna wa Madini katika sekta ya madini. 

11. Serikali ifute au kubadili sheria ya kodi ya madini ili kuondoa vifungu ambavyo havina manufaa kwa mataifa. 

12. Serikali itoe elimu kwa watumishi wake kuhusu sekta ya madini. 

==>Rais Magufuli anazungumza.
1.Muda mwingine ni vigumu sana huwa uzungumze nini mara baada ya ripoti hii yenye kutia uchungu sana. 
2.Nisije kusahau nawapongeza kamati mmefanya kazi kubwa kwa ajili ya Watanzania wapo waliotaka kukatisha maisha yenu.

3.Nisije kusahau nawapongeza kamati mmefanya kazi kubwa kwa ajili ya Watanzania wapo waliotaka kukatisha maisha yenu. 

4.Ndugu zangu watanzania Mungu alitupenda katuweka katika nchi ya Tanzania akatupatia Maliasili nyingi. 

5.Nina Uhakika huko alipo shetani anatucheka nina imani shetani huyohuyo anatumia viongozi kuifanya Tanzania kuwa maskini. 

6.Wakati mwingine tunapewa mikopo kwa Masharti ya ajabu ajabu huku mali tunazo sisi wenyewe jamani.  

7.Kampuni inafanya biashara ya Trilioni of money lakini hata haijasajiliwa nchini mara ngapi tunawaumiza wamamchinga wasio na leseni. 

8.Mali ni yangu mimi nakulinda wewe unanitisha kuwa tutashitakiwa kwa kisingizio cha ajira tuko hapa kulinda maslahi ya watanzania  

9.Hawa watu muda mwingine hawana hata huruma wamechukua madini na mchanga wote huo lakini hata kodi hawakulipa.  

10.Watanzania hapa Mawaziri na Wataalamu wote mioyo yao haiwaruhusu hata kwenda kukagua smelter nje ya nchi. 

11.Makampuni ya kujenga smelter ya dhahabu hayaruhusiwi lakini chuma, Cement na Tiles mnaweza hili ni soko la ajabu. 

12.Tulikuwa tunashare ya 15% lakini mtu akaona apunguze hii aweke asilimia 5 baadaye akaenda kuiondoa yote hiyo. 

13.Yupo mpiga Kelele mmoja ambaye anapiga Kelele kila siku tulipomchunguza huko nyuma anapiga simu kwa Mwanyika anaomba data.  

14.Sio kwamba mimi sina Damu ila Mungu alifawanyanyua mkaona mimi ndiyo ninafaa siwezi kuwasaliti hata kidogo. 

15.Mtu kama Dkt Kafumu alikwenda kufanya forgery yupo daktari mmoja pale Muhimbili naye tulimshika hata hausiki alileta ukabila 

16.Wahusika wote waliotajwa ndani ya Ripoti hii mimi nimeyakubali mapendekezo haya yote ntayasapoti kwa asilimia 100. 

17.Waziri Kabudi uwe na timu ya wanasheria waaminifu, rekebisheni hizi sheria tuzipeleke bungeni zifanyiwe mabadiliko

18.Wakikiri na kuomba msamaha tutakubali kuwasajili lakini kwa sasa hakuna kuwasajili na hakuna mchanga kutoka nje

19.Wizara zote zinazohusika wawaite Acacia wawadai fedha zetu zote na wakiri walituibia. Wakikubali tutaendelea


20.Tunahitaji wawekezaji, lakini katika uwekezaji ambao utatunufaisha wote, na si wawekezaji wezi.

21.Kama mtu ametajwa kwenye ripoti na yuko hai, muite umhoji kwanini alifanya aliyoyafanya

22.Mwl. Nyerere alisubiri hadi wakati utakapofika ndio tuchimbe. Nina uhakika huko aliko akituangalia machozi yanatoka
 

 

Ripoti: Kampuni ya Kuchimba Madini ACACIA Iliingia Kinyemela na Wala Haina Kibali Chochote

0
0
Taarifa ya pili ya  wachumi na wanasheria iliyofanya uchunguzi wa madini yaliyo kwenye makontena yenye mchanga wa madini iliyoundwa na Rais Joseph Magufuli, imebaini kuwa kampuni ya ACACIA Mining Plc haina kibali na inafanya kazi kinyume cha sheria.

Prof. Osoro amesema kwamba  Kamati yake imebaini kuwa Acacia haina uhalali wa kufanya shughuli zake hapa nchini  na imetenda makosa yakiwemo kujipatia mali kwa udanganyifu, uhujumu uchumi, jinai na kuitia hasara taifa.

Aidha Kamati ya Prof. Osoro imebaini kwamba  Makinikia yaliyouzwa nje ya nchi hayakuwa makinikia hasa, bali yalikuwa ni madini mbalimbali huku ikiongeza kwamba  katika mikataba ya uuzwaji wa makinikia hayo, serikali haikuwa sehemu ya mikataba hiyo.

Prof. Osoro ameongeza kwamba jumla ya mapato yote ambayo serikali imepoteza ni Tsh. trilion 68.6 sawa na bajeti ya miaka miwili ya nchi kodi ya mapato ambayo taifa imepoteza ni Tsh. tril 55.07, mrahaba tril 11, bandari tril 1.6. na kwamba jumla ya thamani ya madini kwenye makontena yote 44,277 tangu mwaka 1998 ni Tsh. tril 132.56.

Pamoja na hayo imebainika kuwa uongezwaji wa leseni kinyume cha sheria ambapo imedaiwa kuwa aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini  William Ngeleja na Sospeter Muhongo ndio waliohusika na uongezaji wa muda kwenye uchimbaji wa madini.

Kamati hiyo imetoa mapendekezo mbalimbali ikiwepo kuchukua sheria juu ya kampuni ya ACACIA iliyopo nchini kinyume cha sheria kupitia msajili wa makampuni ikiwa ni pamoja na Mawaziri wote walioshiriki kwa namna moja au nyingine juu ya mikataba ya uchimbaji madini huku ikiitaka Serikali iwe inafanya ukaguzi wa mara kwa mara kwenye makampuni ya madini

Wapinzani Walivyosimama Bungeni na Kuanza Kuimba Wana Imani na Mkapa, Kikwete

0
0
Bunge limezizima kwa makofi baada ya hotuba ya mpango wa bajeti ya kambi rasmi ya upinzani.Wabunge wa upinzani  ndiyo wengi waliobaki ukumbini baada ya wengi kwenda kufuatilia ripoti ya kamati ya pili ya Rais John Magufuli kuhusu usafirishaji wa makinikia.

Wabunge wamesimama na kuanza kuimba huku wakipiga makofi, marais wa awamu zilizopita; Benjamin Mkapa na Jakaya Kikwete wametajwa.

"Tuna imani na Mkaaapa...oya oya oya
Mkapa kweeeli...kweli
Kweli, kweli, kweli Mkapa.

Tuna imani na Kikweeetee...oya oya oya
Kikwete kweeli
Kweli, kweli, kweli Kikwete."

Wimbo huo umeimbwa baada ya Waziri Kivuli wa Fedha na Mipango, David Silinde kulitaka Serikali kuileta bungeni mikataba yote ya madini ili ijadiliwe.

Alichokisema Rais Magufuli Kuhusu Wabunge "Waropokaji"

0
0
Baada ya kupokea Ripoti ya pili ya mchanga wa madini Ikulu leo June 12, 2017 Rais Magufuli pia amezungumzia swala  ya Wabunge wanaoropoka bungeni

Rais  amemwambia Spika; "Nitakuletea huu mzigo ili muweze kuipitia kule kwa maslahi mapana ya taifa letu, kwa wale watakaokua wanaropokaropoka….. unaenda vizuri

"Tumia mbinu hiyohiyo ya kuwafanya wasiropokee Bungeni, waropokee nje na kule tutadili nao vizuri kwasababu wanapokua kule ndani wana kinga wanaweza wakatukana chochote, sasa kinga wanayoitumia vibaya bungeni kainyooshe wewe.

"Wawe wanatoka kule bungeni, ukishamfukuza hata mwezi mzima… atakuja aropokee huku, na mimi nakueleza waache waropokee huku nitadili nao, wala siwatishi lakini hatuwezi kuwa kwenye vita wewe unaanza kugeuka kupiga wale wanaokwenda mbele…. ni nafuu unyamaze ukalale

"Mimi muda wangu utapita, tena ningetamani kweli hata ingekua mwaka huu tu niondoke niwaachie na wengine niwe nachungulia tu, saa nyingine hulali usiku kucha unahangaika documents ziko nyingi… saa nyingine nauliza Mungu kwanini ulinipa hii kazi, ni kazi ngumu"

FULL RIPOTI: Hii Ndo Taarifa Yote Ya Kamati ya Pili ya Kuchunguza Madini Katika Mchanga Iliyowasilishwa Kwa Rais Leo

0
0
Leo June 12, 2017 Rais Magufuli amepokea Ripoti ya piti ya kamati aliyounda kuchunguza madini katika mchanga.

==> Ripoti yote iko hapo chini

Jipatie Dawa za Asili za Kupunguza Maziwa, Kupunguza tumbo, Kuongeza nguvu za Kiume na Mvi

0
0
(OFFER OFFER OFFER) NATURAL BEAUTY COSMETIC INAKUPATIA OFA YA PUNGUZO LA BEI KWA KILA BIDHAA PUNGUZO LA  %10 KWA MWEZI HUU WA RAMADHANI. 
 
PATA BIDHAA HIZI ZILIZOTENGENEZWA KWA MIMEA NA MATUNDA UFURAHIE MATOKEO MAZURI BILA KEMIKALI WALA MADHARA YOYOTE PIA NI GUARANTEE. Bidhaa tulizonazo÷
 
🍉🍓🍇🍅🍊🍒🍍🌴🍐🧀🧀🧀🧀🍅🍇🍇🍇🍇🍇🍇🍐🍍🌳🍏🍐🌶🍉🍆🍆🍒.
Pata punguzo la bei kwa bidhaa hizi.
1. YODI PILLS _ Ni vidonge vya kuongeza hips na makalio @170,000/=
2. BOTCHO CREAM_ Ni dawa ya kupaka ya kuongeza shepu (hips na makalio) @150,000/=
3. BOTCHO MULT PLUS_ Hii ni dawa ya kunywa ya kuongeza shepu (hips makalio na mapaja) @200,000/=
4. PANNAMAS BREAST_ Ni dawa ya kupunguza maziwa na kuyasimamisha hata kwa walio nyonyesha. Inapatikana kwa Tsh @120,000/=
5. DISCREET_Hii ni kwa ajili ya kuondoa mvi milele na zisiludi tena. @120,000/=
6. BODY BOOSTER_Ni dawa ya kuongeza mwili mzima na kukupa hamu ya kula vizuri. Inapatikana kwa Tsh @130,000/=
7. LEG BOOSTER_Ni dawa ya kuongeza miguu kuwa (Chupa ya bia) @120,000/=
8. HAIR GROWTH STIMULATOR_ Ni mafuta ya kulefusha nywele na kuzuia kukatika ovyo. Yanapatikana kwa Tsh @100,000/=
9. MICRO COMPUTER_ Ni mkanda wa kupunguza tumbo na manyama uzembe. @170,000/=
10.HANDSOME UP ni kifaa kinachoongeza maumbile ya kiume  kwa 99% kwa size uipendayo wewe na kuimarisha misuli ya uume kwa @170,000/= tuu.
11.MEN GELY YA KUPAKA. Hii inaongeza kwa wastani wa inch 6.5 na inapatikana kwa @120,000/=. 
12. SHARK POWER. Hii pia ni kwa ajili ya kuongeza maumbile  wastani wa inch 7.5 inapatikana kwa @135,000/=.
15. MAX MAN 2. Ni vidonge kwa ajili ya nguvu ambavyo vinasaidia sana hata kwa watu wenye kisukari na waliokua wakifanya sana master blashion. Pia huongeza hamu ya tendo la ndoa inapatikana kwa @130,000/=
🌳🍉🍌🍅🍍🍐🍓🍆🍐🍒🍒🍓🍓🍑🍍🍍🍓🍓🍓🍍🍐🍐🍈🍉
Tupo DAR ES SALAAM  kariakoo na kinondoni kanisani.
Kwa mawasiliano zaidi piga  0759029968 au 0659618585. 
 
Popote ulipo utapata huduma zetu.
                 Follow us
@natural2162
@natural2162
@natural2162
@natural2162
     Bidhaa zetu zote ni garantii na unapewa risiti
              Karibu

Profesa Muhongo Kitanzini Tena.....Ni Baada ya Rais Magufuli Kuviagiza Vyombo vya Dola Vimuhoji Kwa Kusaini Mikataba Mibovu ya Madini

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano, Dkt Magufuli ameagiza viongozi wa Wizara ya Nishati na Madini, Manaibu wake, Wanasheria Wakuu wa Serikali, Makatibu Wakuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Maafisa wa TRA, na watumishi wengine waliohusika katika upotevu wa matrilioni ya fedha kupitia sekta ya madini wahojiwe.

Rais Magufuli ameyasema hayo leo Ikulu alipokuwa akipokea ripoti ya pili ya kamati iliyokuwa ikichunguza makinikia yaliyopo kwenye makontena bandarini iliyoundwa na wanasheria ya wachumi.

Akizungumza kwa uchungu, Rais Magufuli alisema kuwa Tanzania imejaliwa na kila aina ya madini ambayo unaweza kuyataja hadi ukasahau lakini bado sisi ni maskini. 

Akitaja baadhi ya madini alisema kuna dhahabu, almasi, tanzanite, gesi za kila aina na vitu vingine mbalimbali lakini tumebaki masikini kutokana na viongozi kutokuwa wazalendo.

Akisoma ripoti hiyo Ikulu leo, Mwenyekiti wa Kamati, Prof. Nehemiah Osoro alisema kuwa Mawaziri wa Wizara ya Nishati na Madini wa kipindi kilichopita walisaini mikataba ya madini ambayo haikuwa na faida kwa taifa na hivyo kusababisha nchi kupoteza mapato kwa kutoa misamaha ya tozo mbalimbali.

Prof. Osoro alieleza zaidi kuwa kwa kutumia mamlaka aliyonayo, Mawaziri waliopita wamekuwa wakiwaongezea muda wa kufanyakazi au eneo la uchimbaji makampuni ya madini bila kufuata sheria. Akitolea mfano hapa, Prof. Osoro alisema kuwa, Waziri Prof. Muhongo alifanya hivyo kwa mgodi wa North Mara.

Aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini kipindi cha mwisho cha Rais Mkapa, Daniel Yona amewahi kushtakiwa kwa kosa la kuongezea  mkataba  wa  ukaguzi  wa  madini  kampuni MS  ALEX  STUWART  kwa  miaka  miwili zaidi  kuanzia  tarehe  14 Juni 2005  hadi  tarehe  23 Juni 2007 bila kufuata utaratibu.

Rais ameagiza viongozi hao wahojiwe ili waeleze kwanini walifanya waliyoyafanya na kwa manufaa ya nani kitu kilichopelekea taifa kupoteza fedha nyingi.

Miongoni mwa watakaohojiwa kufuatua amri hii ya Rais ni, William Ngeleja, Prof. Sospeter Muhongo, Nazir Karamagi, Daniel Yona, Andrew Chenge, Fredrick Werema, Johnson Mwanyika.

MAPOVU Ya Diamond Platnumz Baada ya Mpnz wake Kupost Picha ya Nusu Uchi Akiwa na Mwanaume Mwingine

0
0
Diamond Platnumz  ameonesha kukerwa na kitendo  cha  Zari  ambaye ni mpenzi wake waliezaa nae watoto wawili.

Kumekua na picha zinazosambaa mitandaoni zikimuonyesha Zari akiwa ndani ya maji nusu uchi  ambapo kwenye picha alizopost yeye Zari, alionekana mwenyewe lakini kuna nyingine zimesambaa zikimuonyesha akiwa na Mwanaume.
Diamond Platnumz  ameonesha kuchukizwa na kitendo hicho na kuamua kuandika yafuatayo “Ndio maana wakati mwingine naonaga bora tu nile na kusepa…. maana hawathaminikagi wala kuaminika hawa“

Spika Job Ndugai kuunda timu ya kuchunguza suala la madini ya Almasi

0
0
Spika wa Bunge, Job Ndugai amesema ataunda timu yake itakayofuatilia suala la madini ya almasi.

Ndugai ameyasema hayo leo baada ya kamati ya pili kutoa ripoti yake kuhusu mchanga wa madini katika makontena 277 yanayoshikiliwa.

Amesema kwa kushirikiana na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ambaye ni kiongozi wa shughuli za bunge, watasaidiana kuunda timu hiyo ili kumsaidia Rais katika masuala ya madini.

“Kwa pamoja, rais ukienda huko na sisi tukienda huku, tutafika

Tayari Spika alishaunda kamati kuchunguza suala la madini ya Tanzanite.

ACACIA wapinga vikali matokeo ya kamati ya pili ya Rais

0
0
Mwitikio wa Acacia kwenye matokeo ya kamati ya pili ya Rais

Acacia imeona matokeo ya kushtua ya kamati ya pili ya Rais iliyowasilishwa kwa Rais wa Tanzania Mh. Dk John P. Magufuli leo asubuhi ambayo imeangalia nyanja za historia za kiuchumi na kisheria ya mauzo ya nje ya makanikia ya madini.

Kamati ya Pili imetoa matokeo yake kwa kutumia matokeo ya Kamati ya Rais ya Kwanza, iliyotangazwa tarehe 24 Mei 2017, ambayo Acacia imeikanusha vikali. Kamati hiyo ilipata matokeo yake kwa kutumia sampuli ya kontena 44. Kwa mujibu wa data za zaidi ya miaka 20 tulizonazo ni vigumu kuoanisha matokeo yetu na yaliyokutwa na kamati, na kamati imetoa thamani ya juu kwa zaidi ya mara 10 kuliko thamani halisi ya makanikia

Kamati ya Pili inadai kuwa Acacia imetangaza kiasi cha chini cha mapato kuliko inavyopata na kulipa kodi kidogo kuliko inavyostahili kwa miaka mingi na kuficha mabilioni ya dola ya Marekani. Na hivyo imefanya mapendekezo kadhaa ikiwa ni pamoja na Acacia kulipa kodi inayodaiwa na mirahaba, kufanya majadiliano upya ya mikataba mikubwa ya uchimbaji madini, umiliki wa Serikali katika migodi, na muendelezo wa marufuku ya kuuza nje.

Acacia inakanusha vikali tuhuma hizi mpya zisizo na ushahidi. Sisi tumefanya biashara zetu kwa utaratibu bora kabisa na kwa kufuata sheria zote za Tanzania. Tunarudia kusema tena tumeweka wazi kila kitu chenye faida tulichokuwa tunazalisha tangia tuanze uchimbaji Tanzania na tumelipa kodi na mirabaha yote inayotakiwa kulipwa, na kwa kuongezea mahesabu yetu tunayotoa yanakaguliwa kila mwaka kwa viwango vya kimataifa vinavyoendana na IFRS.

Acacia kwa muda mrefu tulitaka kushirikiana na Serikali ya Tanzania kwa kuwa tunaamini wote tuna malengo sawa katika kuimarisha maendeleo ya kijamii na kiuchumi nchini. Hata hivyo, ushirikiano huu lazima uwe na misingi ya haki kwa wadau wote, ikiwa ni pamoja na 96% ya wafanyakazi katika migodi yetu ambao ni Watanzania, na wanahisa wetu ambao wamechangia dola bilioni 4 za uwekezaji ambazo Acacia imefanya ndani ya nchi hadi sasa.

Acacia bado inakaribisha mazungumzo na Serikali kuhusu suala hili na inaendelea kutathmini nini inaweza kufanya . Tutatoa taarifa zaidi kwa soko kadri tutakavyoweza kufanya .

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya June 13


Neema Herbalist: Mzigo Mpya Umeingia, Bofya Hapa Kujipatia Fasta

0
0
Tunapenda  kuwafahamisha  wateja  wetu  wapendwa  kuwa, mzigo  mpya  wa  dawa  mbalimbali  za  asili  umeingia.

Dawa  zilizopo  ni  pamoja na :

1.Dawa  asilia ya  kuunganisha  mifupa, pingili  na kukomaza mifupa.

2.Dawa  asilia ya kuondoa  maumivu ya  misuli, kurekebisha  mishipa  na  misuli

3.Dawa  asilia  kwa  wagonjwa wa  kiharusi (Kupooza)

4. Dawa  asilia ya  kutibu  majeraha

5.Dawa  asilia  ya  kutibu  vidonda ndugu

6.Dawa asilia  ya  kuondoa  uchovu na  kuwashwa

7.Dawa  asilia  ya  kuondoa mafuta  kwenye damu ( kolestrol /lehemu)

8.Dawa  asilia  ya  kutibu tatizo  la  nyongo

9.Dawa  asilia  ya  kutibu  gauti

10.Dawa  asilia  ya  uzazi  wa  mpango

11.Dawa  asilia  ya  kutibu  tatizo  la  Goita

12.Dawa asilia ya  kutibu  tatizo  la  change  la watoto wachanga.

13.Dawa  asilia  ya kutibu  vidonda  vya  tumbo

14.Dawa  asilia  ya  kutibu mzio     ( Allergy)

15.Dawa asilia  ya  kutibu  tatizo  la  degedege  kwa watoto  wenye  umri  wa  kati  ya  miezi  6  hadi  tisa.

16.Dawa asilia  ya  kurutubisha  mayai  ya  uzazi  na  kuzibua  mirija  ya  uzazi  kwa  wanawake.

17.Dawa  asilia  ya  kutibu  tatizo  la  utasa  kwa  wanaume.

18.Dawa  asilia  ya  kusaidia  kugeuza  mtoto  aliye  kaa  vibaya  tumboni ( Mfano: Katanguliza mikono, makalio n.k )

19.Dawa  asilia  ya kupunguza  kitambi, uzito  na  unene  uliozidi.

20.Dawa  asilia  ya  kutibu  tatizo  la  vinyama  vya  puani.

21.Dawa asilia  ya  kutibu  tatizo  la  bawaziri.

22.Dawa  asilia  ya  kutibu  tatizo  la  uchungu  wa  pili  baada  ya  kujifungua.

23.Dawa  asilia  ya  kutibu  majeraha ya moto  pamoja na  makovu yatokanayo  na  moyo.

24.Dawa  asilia  ya  kutiu  tatizo  la  kwikwi

25.Dawa asilia  ya  kutibu  tatizo  la  kutokwa  na  harufu  mbaya  kinywani

26.Dawa  asilia  ya  kutibu  tatizo  la  kutoa harufu  mbaya mwilini

27.Dawa  asilia  ya  kusaidia  kunenepesha  mtu  aliye  dhoofu  mwili

28.Dawa  asilia ya kutibu  tatizo  la  uvimbe  wa  tumboni  ( FIBROID )

29.Dawa  asilia  ya  kisukari

30.Dawa  asilia  kwa  watu  wenye  tatizo  la  moyo, presha  ya  kupanda, presha ya  kushuka, moyo  kupanuka  na  matundu  kwenye moyo.

31.Dawa  asilia  ya  kutibu  tatizo  la  U.T.I, kaswende, kisonono sugu  na  Taifodi.

32.Dawa  asilia  ya  kutibu  magonjwa  mbalimbali ya  ngozi

33.Dawa  asilia  ya  kutibu  tatizo la  kubanwa mkojo na  maumivu  kwenye  njia  ya  mkojo

34.Dawa  asilia  ya  kutibu  tatizo  la  kujikojolea

35.Dawa  asilia  ya  kusafisha  figo  na  kibofu  cha  mkojo

36.Dawa  asilia  ya  kuondoa  sumu  mwilini

37.Dawa asilia  ya  kuondoa  maumivu  ya  hedhi

38.Dawa  asilia  za  kuondoa  sumu  ya  nyoka, na  nge.

39.Dawa  asilia  ya  kutibu  tatizo  la  pumu

40.Dawa  asilia  ya  kuyeyusha uvimbe  kwenye  lango  la  uzazi.

41.Dawa asilia ya kutibu  malaria  sugu

42.Dawa  asilia  ya kutibu  tatizo  la  upara

43.Dawa  asilia ya  kutibu  tatizo la  kikohozi sugu  na  kimeo.

44.Dawa  asilia  ya  kutibu  tatizo  la  ngiri

45.Mawe  kwenye  figo

46.Kukosa  choo

47.Kukosa  hamu  ya  kula

48.Chango  la  kike

49.Kutanua  nyonga ( Kuzaa  bila  kupasuliwa )

50.Nguvu za  kiume

51.Hamu  ya tendo  la  ndoa  kwa  wanawake.

52. Mtoto kuchelewa  kutembea

DAWA   ZOTE  HIZI  NI  ZA  ASILIA KABISA  NA  HAZINA   KEMIKALI ZA  VIWANDANI.

Tunapatikana  UBUNGO  jijini  DAR ES  SALAAM, jirani  na  SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING, nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO PLAZA.

Kwa  wateja  waliopo  Dar  Es  Salaam, ambao  hawana  nafasi  ya  kufika  ofisini  kwetu, watapelekewa  dawa  mahali  popote  walipo.

Kwa  wateja  waliopo  mikoani, watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  mabasi.

Kwa wateja  waliopo  Zanzibar, watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa  boti.

Kwa wateja  waliopo Mombasa, watatumiwa  dawa  kupitia  basi  la  TAHMEED.

Kwa  wateja waliopo  jijini  Nairobi, watatumiwa  dawa  kupitia  basi  la  DAR  EXRESS.

Na kwa  wateja  waliopo  ughaibuni, watatumiwa  dawa  kwa  njia ya  POSTA  au  DHL.

WASILIANA  NASI  KWA  SIMU  NAMBA:

0766 – 53 83  84.

Kwa  taarifa  zaidi  kuhusu huduma zetu, tutembelee  kila  siku, kupitia :

Prof. Muhongo, Andrew Chenge na Wahusika Wengine Wazuiwa kutoka nje ya Mipaka ya Tanzania

0
0
Serikali imeagiza, Mawaziri, Wanasheria Wakuu wa Serikali na Manaibu wao, Wakurugenzi wa idara za mikataba, na Makamishna wa madini, wanasheria wa Wizara ya Nishati na Madini na watumishi wengine wa Serikali na watu wote waliohusika katika kuingia mikataba ya uchimbaji madini, utoaji wa leseni za uchimbaji wa madini na kuongeza muda wa leseni, watumishi na wamiliki wa makampuni ya madini kuto toka nje ya mipaka ya Tanzania.

Agizo hilo lilitolewa jana  na Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba ambaye alisema kuwa, wote waliotajwa kuhusika katika kulisababishia taifa hasara kupitia sekta ya madini, hawaruhusiwi kutoka nje ya mipaka ya Tanzania isipokuwa kwa kibali maalum kutoka serikalini.

“Naelekeza wote waliotajwa kuhusika hakuna kutoka nje ya mipaka ya nchi yetu isipokuwa kwa kibali maalum kutoka serikalini. Vyombo vitekeleze maagizo ya Rais kwa utimamu,” aliandika Waziri Nchemba kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii.

Agizo hili limekuja ikiwa ni saa chache tangu Rais Magufuli alipoagiza kuwa, viongozi wote na watumishi mbalimbali waliohusika katika kusaini mikataba mibovu na kushiriki kwa namna yoyote ile, wahojiwe.

Miongoni mwa watakaoathiriwa na zuio hilo, ni pamoja na Maafisa wa TRA, Mwanasheria Mkuu wa Serikali Andrew Chenge, Mwanyika, na Werema, Mkurugenzi Idara ya Mikataba, Mary Ndosi, Kamishna Dalali Peter Kafumu, Waziri Prof. Muhongo, Waziri Daniel Yona, Waziri Nazir Karamagi, Jaji Julius Malaba, Waziri William Ngeleja.

Awali Waziri Nchemba alimpongeza Rais Magufuli kwa jitihada alizozichukua katika kuhakikisha analinda rasilimali za wanyonge na kusema kuwa hakuna uzalendo kama huo.

“Hakuna uzalendo zaidi ya kulinda rasilimali za Taifa, Hakuna utetezi wa wanyonge zaidi ya kulinda rasilimali zao.Hongera sana Mh.Rais kwa uzalendo wa vitendo kwa Taifa letu.”

Jipatie Dawa za Asili za Kupunguza Maziwa, Kupunguza tumbo, Kuongeza nguvu za Kiume na Mvi

0
0
NATURAL BEAUTY COSMETICS inatoa OFFER SPECIAL kwa ajili ya SIKUKUU YA EADY kwa kila bidhaa. Bidhaa zetu zote zimetengenezwa kwa mimea na matunda hazina kemiko wala madhara yoyote pia matokeo ni GUARANTEE. Pata bidhaa hizi kwa punguzo la %10 uweze kufulahia matokeo mazuri. Bidhaa tulizonazo ni kama zifuatavyo÷
🍉🍓🍇🍅🍊🍒🍍🌴🍐🧀🧀🧀🧀🍅🍇🍇🍇🍇🍇🍇🍐🍍🌳🍏🍐🌶🍉🍆🍆🍒.
1. YODI PILLS _ Ni vidonge vya kuongeza hips na makalio @170,000/=
2. BOTCHO CREAM_ Ni dawa ya kupaka ya kuongeza shepu (hips na makalio) @150,000/=
3. BOTCHO MULT PLUS_ Hii ni dawa ya kunywa ya kuongeza shepu (hips makalio na mapaja) @200,000/=
4. PANNAMAS BREAST_ Ni dawa ya kupunguza maziwa na kuyasimamisha hata kwa walio nyonyesha. Inapatikana kwa Tsh @120,000/=
5. DISCREET_Hii ni kwa ajili ya kuondoa mvi milele na zisiludi tena. @130,000/=
6. BODY BOOSTER_Ni dawa ya kuongeza mwili mzima na kukupa hamu ya kula vizuri. Inapatikana kwa Tsh @130,000/=
7. LEG BOOSTER_Ni dawa ya kuongeza miguu kuwa (Chupa ya bia) @120,000/=
8. HAIR GROWTH STIMULATOR_ Ni mafuta ya kulefusha nywele na kuzuia kukatika ovyo. Yanapatikana kwa Tsh @100,000/=
9. MICRO COMPUTER_ Ni mkanda wa kupunguza tumbo na manyama uzembe. @170,000/=
10.HANDSOME UP ni kifaa kinachoongeza maumbile ya kiume  kwa 99% kwa size uipendayo wewe na kuimarisha misuli ya uume kwa @170,000/= tuu.
11.MEN GELY YA KUPAKA. Hii inaongeza kwa wastani wa inch 6.5 na inapatikana kwa @120,000/=. 
12. SHARK POWER. Hii pia ni kwa ajili ya kuongeza maumbile  wastani wa inch 7.5 inapatikana kwa @135,000/=.
15. MAX MAN 2. Ni vidonge kwa ajili ya nguvu ambavyo vinasaidia sana hata kwa watu wenye kisukari na waliokua wakifanya sana master blashion. Pia huongeza hamu ya tendo la ndoa inapatikana kwa @130,000/=🌙💫🌟⭐
🌳🍉🍌🍅🍍🍐🍓🍆🍐🍒🍒🍓🍓🍑🍍🍍🍓🍓🍓🍍🍐🍐🍈🍉
 
Tupo DAR ES SALAAM  kariakoo na kinondoni kanisani. 
 
Kwa mawasiliano zaidi piga  0759029968 au 0659618585.
Popote ulipo utapata huduma zetu.
                 Follow us
@natural2162
@natural2162
@natural2162
@natural2162
     Bidhaa zetu zote ni garantii na unapewa risiti
              Karibu

Walichokisema Dr Kafumu, Ngeleja na Andrew Chenge Baada ya Kutakiwa Kuhojiwa Na Vyombo vya Dola

0
0
Vigogo waliotajwa katika ripoti ya pili ya kuchunguza makontena yenye mchanga wa madini (makinikia)  kuisababishia Serikali hasara ya matrilioni ya fedha kupitia sekta ya madini, walipokuwa wakihudumu katika nyadhifa zao serikalini wamevunja ukimya.

Vigogo hao wamezungumzia ripoti hiyo ya pili iliyowasilishwa kwa Rais Dk. John Magufuli Ikulu Dar es Salaam jana, ambapo kamati husika ilichunguza hasara ambayo nchi imepata tangu 1998 usafirishaji wa mchanga wa dhahabu nje ya nchi ulipoanza.

Mbunge wa Bariadi, Andrew Chenge (CCM), alipoulizwa maoni yake juu ya kutajwa na kamati hiyo, alisema hataki kuzungumza chochote juu ya ripoti hiyo, huku Mbunge wa Sengerema, William Ngeleja (CCM), akisema sheria ya madini ya 2010 ingefuatwa, nchi isingekuwa hapa ilipo.

Kwa upande wake Kamishna wa Madini wa zamani, Dk. Dalaly Kafumu, alisema kwa sasa  hawezi kuzungumza jambo lolote kwa kuwa na yeye ni mmoja wa watuhumiwa waliotajwa kwenye ripoti hiyo.

Baada ya kutoka kwenye kipindi cha asubuhi cha Bunge ambacho alikuwa akikiendesha, Chenge alipotakiwa kuzungumzia ripoti hiyo, alijibu kwa ufupi.

“Sizungumzi na mtu,” na alipoulizwa kama hata salamu hataki, alisema. “Sizungumzi na mtu mimi,” alisema Change ambaye aliwahi kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Chenge alikuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali kati ya 1972 na 1990, ambapo mwaka 1993 aliteuliwa na Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali nafasi ambayo alidumu nayo hadi mwaka 2005.

Mbunge wa Igunga, Dk. Dalaly Kafumu (CCM), ambaye ametajwa kutaka kuingilia ripoti ya kamati ya kwanza iliyochunguza mchanga huo, alisema hataki kuzungumza chochote kwa sasa ingawa anaamini kila kitu kiko sawa.

“Kwa kuwa nimetajwa kama mtuhumiwa, sitaki kusema kitu kwa sasa kwa sababu hili ni sawa na jambo lililo mahakamani tu kwa kuwa wamesema tutahojiwa, lakini kila kitu kiko sawa,” alisema Dk. Kafumu.

Alipoulizwa kama ni kweli alikutana na Profesa Abdulkarim Mruma, aliyekuwa mwenyekiti wa kamati hiyo ya kwanza na ni nini walichozungumza, Dk. Kafumu alisema. “Nimeshasema no comment (sina la kusema ),” alisema Dk. Kafumu.

Dk. Kafumu ni moja ya watumishi waliohudumu ndani ya Wizara ya Nishati na Madini ambapo alifanyakazi kazi ndani ya wizara hiyo kuanzia mwaka 1983 hadi 2011, alipoacha na kwenda kugombea ubunge katika uchaguzi mdogo wa marudio wa Igunga, baada ya kujiuzulu kwa aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo Rostam Aziz.

Taarifa zilizopo kwenye tovuti ya Bunge zinaonesha, mwaka 1983 mpaka 1987, Dk. Kafumu alikuwa mtaalamu wa miamba na madini wa wizara hiyo, mwaka 1987 mpaka 1992, mkufunzi na mtafiti wa madini, mwaka 1992 mpaka 2002 akawa mtaalamu mwandamizi wa madini, mwaka 2002-2004, mtaalamu wa miamba mkuu na mbobezi  wa madini, mwaka 2004-2006, alikuwa ofisa mawasiliano na mwaka 2006 mpaka 2011, alikuwa kamishna wa madini.

Kwa upande wake Ngeleja aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, kuanzia mwaka 2008 hadi 2012, alisema hataki kuzungumzia juu ya kilichoelezwa na kamati hiyo ikiwamo kutajwa kwake, bali anachoweza kusema ni kuwa, Rais Magufuli ameonesha uzalendo.

“Sitaki kuzungumza yaliyo kwenye ripoti ya uchunguzi, ila tu nisema kwa wale tuliosikiliza wakati ripoti inawasilishwa na wakati Rais mwenyewe anazungumza, unaona hisia za uzalendo ambazo Rais anazo, na ameeleza kwa uchungu mkubwa namna ambavyo tunastahili kupata zaidi kuliko tunachopata sasa.

“Lakini jambo kubwa alilolifanya, amesema atamkabidhi taarifa (Spika wa Bunge), kwa sababu msingi wa mambo yote haya ni sera na sheria za nchi.

“Kwamba sisi kama Bunge tutimize wajibu wetu tuhakikishe mapungufun yote yaliyo pale tunayafanyia kazi, lakini kikubwa  amesema chenji (fedha zilizokwepwa na migoni) yetu irudi na amewakaribisha wawekezaji wakae mezani, lakini baada ya kuzingatia masilahi ya upande wetu, ni jambo jema.

 “…wakati nachangia bajeti ya Wizara ya Nishati nilisema, sheria hata tuliyo nayo sasa tungekuwa tumeitekeleza vizuri tusingekuwa hapa tulipo na moja ni kuhusu mikataba iliyofungwa kabla ya mwaka 2010,” alisema

Alisema kifungu cha 116 cha Sheria ya Madini, kinasema mikataba yote iliyofungwa kabla ya kutungwa kwa sheria ya madini ya mwaka 2010, inatakiwa iheshimu na  itambulike kwa utaratibu wa sheria hiyo.

“Kwenye kifungu cha 11 cha hii sheria ya madini, inasema kila baada ya miaka mitano baada ya kuanza kutumika hii sheria, mikataba yote ya madini ipitiwe upya.

“Mimi nilijiuzulu uwaziri Mei 4, 2012, sasa ni miaka mitano imepita, na wakati najiuzulu mimi tulikuwa tumemaliza kutunga kanuni, ninachotaka kusema ni kwamba kupitia hicho kifungu cha 11 hilo ndilo dirisha la kujadiliana yale ambayo kipindi kile kilishindikana,” alisema

Waziri huyo wa Nishati na Madini wa zamani, alisema kuwa kifungu cha 10 cha sheria hiyo kimeweka wazi namna Serikali inavyoweza kumiliki hisa kimkakati kwa kutumia dirisha hilo.

“Utaratibu huo ndiyo tumeutumia kwa Mchuchuma na Liganga, ambapo serikali ina asilimia 20 za bure, Ngaka ina asilimia 30 za bure, hayo ndiyo niliyosema,” alisema Ngeleja.

Maoni ya Tundu Lissu baada ya Rais Magufuli kupokea ripoti ya pili ya kamati maalum ya uchunguzi wa madini

0
0
For the Record: What Goes Around Comes Around!!!

Leo wapinzani wa Serikali ya Magufuli tumesemwa sana na kutishiwa kushughulikiwa bungeni na nje ya Bunge.

Kwa sababu hiyo, naomba niweke rekodi ya masuala haya sawa sawa.

Mwezi Machi '97 Bunge lilipitisha Sheria 2 kwa siku moja kwa kutumia Hati ya Dharura.

1) Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbali mbali za Fedha ya '97 ilifuta au kupunguza kodi nyingi kwa ajili ya makampuni ya kigeni ya madini.

2) Sheria ya Uwekezaji Tanzania '97 iliwapa wawekezaji wa kigeni ulinzi mkubwa na manufaa mengi kama vile kuondosha nje fedha na faida yote wanayopata kwa uwekezaji wao nchini.

Mwaka '98 Bunge lilipitisha Sheria ya Madini '98 ambayo ilitamka kwamba mwenye milki ya madini na fedha yote itokanayo na mauzo ya madini ni mwenye leseni ya kuchimba madini hayo.

Sheria hizo tatu nimeziita 'Utatu Usio Mtakatifu' (Unholy Trinity) katika maandiko yangu mbali mbali, na nimezichambua sana tangu mwaka '99 nilipoanza harakati dhidi ya sekta ya madini ya aina hii.

Kwa miaka yote hii hadi leo, Sheria hizi za madini zimeungwa mkono na kupigiwa debe na kila kiongozi na mbunge wa CCM, Magufuli included.

Watu hawa, with very few and minor exceptions, ndio wamekuwa washangiliaji wakubwa wa unyonyaji wa makampuni ya kigeni ya madini katika nchi yetu.

Na ukweli ni kwamba watu hawa na Chama chao ndio wamefaidika sana na utaratibu huu katika sekta ya madini.

Wachache tuliopinga utaratibu huu tuliitwa kila aina ya majina mabaya na uzalendo wetu ulihojiwa kama unavyohojiwa leo na Magufuli.

Kwa mfano, Rais Mkapa alidai, wakati anazindua Mgodi wa Bulyanhulu, kwamba upinzani wetu ulikuwa ni 'ujinga uliofichama katika kivuli cha taaluma.'

Baadhi yetu, kama mimi na Dr. Rugemeleza Nshala, tulikamatwa na kushitakiwa mahakamani kwa uchochezi. Tulikabiliwa na kesi hiyo kuanzia Mei '01 hadi '08 ilipofutwa kwa kukosekana ushahidi.

Kama ilivyokuwa wakati wa Mkapa mwaka '01, leo pia Rais Magufuli ametukebehi na kuahidi kutushughulikia 'tukiropoka' nje ya Bunge.

Tunaambiwa ni lazima tumuunge mkono Rais wetu katika hii 'vita ya uchumi.' Ni sheria ipi ya Tanzania inayotulazimu kumuunga mkono Rais wetu hata kama tunaona amekosea???

Hebu naomba tuitafakari hii 'vita ya uchumi' kidogo. Je, nani hasa ni maadui zetu katika 'vita' hii??? Ni makampuni ya madini ya kigeni??? Kama ni hivyo, fikiria yafuatayo:

1) Wakati tuko vitani, Rais Magufuli na serikali yake wameiruhusu Acacia Mining (tunayoambiwa hata haijasajiliwa!!!) kuendelea kuchimba, kusafisha na kusafirisha nje ya nchi dhahabu kutoka Bulyanhulu, Buzwagi na North Mara Tarime.

Amezuia magwangala yasisafirishwe nje kwenye makontena lakini dhahabu yenyewe hamna shida ikisafirishwa na wezi hawa!!!!!

2) Wakati mapambano ya 'vita ya uchumi' yakiendelea, dhahabu yote inayochimbwa Geita Gold Mine (Mgodi mkubwa kuliko yote nchini) inaendelea kuchimbwa, kusafishwa na kusafirishwa nje ya nchi.

3) Wakati tuko vitani, Rais Magufuli na serikali yake ameruhusu kila mgodi wa dhahabu nchini kuwa na kiwanja chake binafsi cha ndege ili wezi hawa waweze kutorosha 'dhahabu yetu' kwa urahisi zaidi.

4) Wakati tungali vitani, 'Utatu Usio Mtakatifu' wa sheria zetu za kodi, uwekezaji na madini uko pale pale ulipokuwa mwaka '97-'98, cosmetic changes excepted.

Aidha, licha ya kuwa vitani, sisi bado ni signatories wa MIGA Convention na bilateral investment treaties (BITs) zinazowalinda hawa tunaoaminishwa kuwa ni wezi na maswahiba wao wa miaka yote.

5) Wakati tuko kwenye hii vita kubwa ya uchumi, jemedari wetu mkuu na serikali yake hawajatengua mkataba hata mmoja wa uendelezaji madini (Mineral Development Agreements - MDAs) walizosaini hawa anaowaita wanyonyaji na serikali za watangulizi wake Jakaya Kikwete na Ben Mkapa.

6) Wakati tunahamasishwa kumuunga mkono jemedari huyu shupavu, bado hatujaonyeshwa mkataba hata mmoja waliosaini na wanyonyaji hawa tangu miaka ya mwanzo ya '90.

Leo Jemedari Mkuu ameahidi kwamba mikataba hiyo italetwa bungeni. Safi sana.

Lakini je, hii ni mara ya kwanza tunaahidiwa hayo???

Mwaka '08 Jemedari Mkuu wa kabla yake alituahidi hivyo hivyo. Tuwe na subira kabla ya kuanza kushangilia prematurely.

7) Nimemsikia Magufuli akielekeza wahusika wote wa uchafu huu washughulikiwe. Kweli???

(a) Je, Jakaya Kikwete aliyesaini leseni za Bulyanhulu na Nzega mwaka '94 anaponaje???

(b) Je, Ben Mkapa aliyekuwa Rais na Mwenyekiti wa Cabinet wakati haya yanafanyika anaachwaje???

(c) Je, waliokuwa mawaziri na manaibu wao wote wakati haya yanatokea wanasalimikaje???

(d) Je, wale washangiliaji na wapiga meza wa bungeni, ambao waliunga mkono kila walicholetewa bungeni na kukipitisha kilivyo wanakosaje lawama???

8) Nimesikia Acacia Mining hawana hata leseni/usajili wa kuendeshea shughuli zao hapa nchini. Labda. Hata hivyo, jiulize yafuatayo:

(a) Hivi wamekuwa wanalipa kodi kama PAYE, SDL, income tax, withholding tax, mrahaba, n.k., kwa kutumia jina gani miaka yote hii???

(b) Je, wana akaunti yoyote katika benki za Tanzania??? Kama ndio, wamezifungua kwa jina gani???

Kama hapana, wanalipaje mishahara ya wafanyakazi wao wa Kitanzania au watoa huduma mbali mbali wa Kitanzania???

(c) Je, wanalipa bili za umeme kwa TANESCO au za simu kwa Vodacom, Tigo, Airtel, n.k. kwa kutumia jina gani???

(d) Je, wamesajiliwaje katika Soko la Hisa la Dar kama Acacia kama wanaendesha shughuli zao kihuni hivi???

(e) Kuna kitu kinaitwa 'estoppel' katika Sheria yetu ya Mikataba (the Law of Contract Act, Cap. 345) na katika Sheria yetu ya Ushahidi (the Law of Evidence, Cap. 6).

Je, estoppel haituhusu kwenye suala hili la leseni au usajili ya Acacia???

Kama estoppel inahusika, je, hoja hii ya ukosefu wa usajili ina uzito gani, kama upo, kisheria???

9) Nimesikia Sheria za Madini zinatakiwa kufanyiwa marekebisho makubwa. Sawa kabisa.

Lakini je, kwanini Rais Magufuli hajasema chochote juu ya Sheria za Gesi Asilia na Mafuta ambazo zilipitishwa haraka haraka kwa Hati ya Dharura baada ya sisi 'waropokaji' kutimuliwa bungeni na Spika Anna Makinda mwaka '15???

Au Rais wetu anaamini kwamba Sheria za Gesi Asilia na Mafuta hazina matatizo licha ya kupitishwa kwa utaratibu ule ule uliotumika kwa Sheria za Madini???

10) Wakati tunaingojea kwa hamu mikataba ya madini iletwe bungeni, hebu na tujiulize yafuatayo:

(a) Mikataba ya uchimbaji gesi asilia na mafuta nayo iko wapi???

(b) Mikataba ya manunuzi ya Bombardier na Dreamliner za Magufuli nayo italetwa bungeni au itabidi tusubiri aondoke madarakani kwanza kama ilivyokuwa kwa JK na BM???

(c) Mikataba ya ujenzi wa airport Chato na Reli ya Standard Geji ya Waturuki au Wachina na mabarabara kibao nayo italetwa bungeni au ndio basi tena tusubiri Bwana mkubwa atakapoondoka madarakani???

Wakati tukisubiri kufukuzwa bungeni na Spika Ndugai kwa maelekezo ya bosi wake, na wakati tukisubiri dhahama ya Bwana Mkubwa nje ya Bunge, hebu na tujiulize hivi nani hasa ndiye mzalendo wa kweli wa nchi hii???

Hebu na atutajie majina na namba za simu za wale wote ambao amedai wamekuwa wanawasiliana na Acacia na lini walifanya mawasiliano hayo na yalihusu kitu gani. Kutoa hukumu kwa innuendo peke yake haitoshi, tunahitaji ushahidi thabiti kutoka kwa Rais Magufuli.

Sijazungumzia bado plagiarism ya taarifa mbali mbali za kiserikali na zisizo za kiserikali katika Taarifa ya Kamati ya Prof. Osoro. Hili ni la baadae.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images