Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Kivuko Kipya kilichozinduliwa na kukabidhiwa kwa Waziri Mbarawa

0
0
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa amepokea Kivuko cha MV Kazi kutoka kwa Kampuni ya kizalendo ya M/S Songoro Marine Transport Boatyard ya Mwanza iliyokuwa inafanya kazi ya ujenzi wa Kivuko hicho mara baada ya ujenzi wake kukamilika.

Akizungumza na wananchi, Prof Mbarawa jana alisema lengo la Serikali kuongeza Kivuko hicho  ni kuboresha huduma za kusafirisha abiria na magari kati ya Magogoni na Kigamboni.

“Uwepo wa vivuko vitatu kutasaidia utoaji wa huduma kwa wakati na kwa urahisi na ikitokea Kivuko kimoja kimepelekwa kufanyiwa ukarabati huduma zitaendelea kama kawaida bila kuathiri utaratibu wa kawaida”.Alisema Prof Mbarawa.

Aliongeza kuwa ili kuendana na kasi ya Mhe. Rais John Magufuli  Wizara yake itaendelea kuboresha huduma za Vivuko katika Mikoa mingine ikiwemo Mkoa wa Lindi , Kivuko cha Pangani, na Kivuko cha Kigongo Busisi Mkoani Mwanza.

Nae Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Dkt. Dkt. Mussa Mgwatu alisema Kivuko cha MV Kazi kimejengwa kulingana na viwango vinavyotakiwa Kimataifa na ukaguzi wake umefanywa na Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) na kuthibitishwa kuwa ni salama kwa ubebaji wa abiria na magari.

 Ujenzi wa MV KAZI umegharimu Shilingi Bilioni 7.3 za Kitanzania na kina uwezo wa kubeba abiria 800 magari 22 sawa na jumla ya tani 170.

Kivuko hicho kimekabidhiwa jana  kwa ajili ya kuanza kutoa huduma kati ya Magogoni na Kigamboni Jijini Dar es salaam na kuongeza idadi ya vivuko katika eneo hilo kufikia vitatu.


Rais Magufuli amuapisha Aliyekuwa Mwenyekiti wa ACT- Wazalendo Bibi Anna Mghwira Kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 06 Juni, 2017 amemuapisha Bibi Anna Elisha Mghwira kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro.

Bibi Anna Elisha Mghwira amejaza nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Saidi Meck Sadiki aliyekuwa Mkuu wa Mkoa huo.

Hafla ya kuapishwa kwa Bibi Anna Elisha Mghwira imefanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa.

Akizungumza baada ya kumuapisha, Mhe. Rais Magufuli amemtaka Bibi Anna Elisha Mghwira kwenda kuchapa kazi kwa juhudi na maarifa na kuondoa kero zinazowakabili wananchi wa Kilimanjaro bila kujali itikadi za vyama vyao vya siasa, dini, makabilia na kanda wanazotoka.

Mhe. Rais Magufuli amemhakikishia kuwa atapata ushirikiano wa kutosha wakati wote wa utekelezaji wa majukumu yake na asikubali kuyumbishwa na mtu yeyote katika majukumu yake ya kuwahudumia wananchi.

“Mimi huwa siteui watu hivi hivi, huwa naangalia uwezo wa mtu, na wewe nimekuchunguza na nimejiridhisha kuwa una uwezo wa kuwatumikia wananchi, nenda kachape kazi, kawaondolee kero wananchi wa Kilimanjaro, wapo watu watakaokusema na wengine watakuonea wivu, wewe kachape kazi” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Kwa upande wake Bibi Anna Elisha Mghwira amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kumuamini na kumteua kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro na amemuahidi kuwa yupo tayari kwenda kufanya kazi ya kuwatumikia wananchi na kujenga Taifa.

“Ninasema hii ni heshima kwa Taifa letu, ni heshima kwa umoja wa nchi yetu, ni heshima kwa siasa za umoja wa nchi yetu, kumekuwa na minong’ono mingi sana kuwa Rais analeta nini, kuteua watu wanaitwa wapinzani, mimi sio mpinzani wa maendeleo” amesema Bibi Mghwira. 

VIDEO: Alichozungumza Anna Mghwira baada ya kuapishwa na Rais Magufuli

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 06 Juni, 2017 amemuapisha Bibi Anna Elisha Mghwira kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro.

Bibi Anna Elisha Mghwira amejaza nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Saidi Meck Sadiki aliyekuwa Mkuu wa Mkoa huo.

==>Msikilize hapo chini

Video: Rais Magufuli atolea ufafanuzi kauli yake ya kutoteua kiongozi wa upinzani

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli amesema kuwa anafahamu watu wanamshangaa kwa sababu alishawahi kusema hatoteua kiongozi wa upinzani katika serikali yake, lakini tayari ameshateua kadhaa.

Rais amesema kuwa, ni lazima watu waelewe maneno hayo alizungumza akiwa mahali gani, aliyazungumza kwenye mkutano wa hadhara Zanzibar.

“Lakini siku zote nimekuwa nikisistiza, Tanzania kwanza. Of course wapo wengine wanaosema, mbona ulishangumza, hutashirikiana, sitateua mpinzani! Ni lazima watu waelewe nimezungumza hivyo mahali gani, nilizungumza nikiwa Zanzibari.”

Rais Magufuli aliyasema hayo mapema leo asubuhi alipokuwa akimuapisha Mwenyekiti wa Chama cha ACT-Wazalendo, Anna Elisha Mghwira kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro.

Rais amempongeza kiongozi huyo, akisema yeye ni mstaarabu na ni mtu anayejielewa hivyo anafahamu kabisa kuwa nafasi hiyo aliyompa ataweza kuitumikia vyema.

Wakati huo huo, Rais Magufuli alisema kuwa, wapo wabunge wa CHADEMA ambao wamekuwa wakimuomba awateue lakini yeye amewakatalia kwa sababu anataka upinzani uendelee kuwepo.

==>Msikilize hapo chini


Uamuzi wa ACT Wazalendo kuhusu uteuzi wa Mwenyekiti Anna Mghwira kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro

0
0
Tarehe 03 Juni 2017 Chama chetu kilipokea taarifa kuhusu uteuzi Mama Anna Elisha Mghwira, Mwenyekiti wa Taifa wa Chama chetu kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro. Uteuzi wa Mwenyekiti wetu umefanywa akiwa nje ya nchi na baada ya kurejea amefanya mazungumzo na viongozi wenzake wa juu wa Chama kuhusu uteuzi wake huo.

Kufuatia uteuzi huu na kwa kuzingatia unyeti na majukumu ya Mkuu wa Mkoa, Kamati ya Uongozi ya chama itakutana kesho tarehe 07 Juni 2016 kutafakari pamoja na mambo mengine, namna ambavyo Mama Anna Mghwira atatekeleza wajibu wake wa uenyekiti wa chama na majukumu yake mapya.

Chama kinatoa wito Kwa wanachama wote kuendelea na utulivu wakati vikao vya Chama vinachukua hatua stahiki kuhusu jambo hili.

Ado Shaibu,
Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mawasiliano kwa Umma,
ACT Wazalendo.
Imetolewa leo tarehe 06 Juni 2017

Rais Awapandisha Vyeo Maafisa Wa Magereza Leo

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mh. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli amewapandisha vyeo Maafisa watano wa Magereza kuwa Naibu Makamishna  na  wengine 24 kuwa Makamishna Wasaidizi Waandamizi  wa Magereza kuanzia tarehe  25 mwezi Mei, 2017.

Waliopandishwa vyeo kuwa Naibu Kamishna wa Magereza ni Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza Uwesu H. Ngarama,  Boharia Mkuu wa Jeshi la Magereza, Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza Gideon M. D. Nkana, Mkuu wa Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji Ukonga, Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza Jeremiah .M.C. Nkondo,  Mkuu wa Magereza Mkoa wa Kagera, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza Tusekile S. Mwaisabila, Mkuu wa Magereza Mkoa wa Lindi pamoja na Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza Augustine S. Mboje ambaye ni Mkuu wa Magereza Mkoa wa Dar es Salaam.

Waliopandishwa vyeo kuwa Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza ni Kamishna Msaidizi wa Magereza Mbaraka Sultan Semwanza, Mwalimu wa Hisabati na Kemia shule ya Sekondari Bwawani inayosimamiwa na Jeshi Magereza, Kamishna Msaidizi wa Magereza George Togholai Mwambashi, Mkuu wa Kitengo cha Sheria Makao Makuu ya Magereza Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi wa Magereza Charles R. Novat, Mkuu wa Kitengo cha Mafunzo Makao Makuu ya Magereza Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi wa Magereza Faustine Martin Kasike Mkufunzi Mwandamizi Chuo cha Ulinzi wa Taifa (NDC) Kunduchi Dar es Salaam.

Wengine ni Kamishna Msaidizi wa Magereza Joel Silverster  Bukuku, Mdhibiti wa Shirika la Magereza, Kamishna Msaidizi wa Magereza Deogratius Ndaboine Lwanga, Afisa Mnadhimu, Magereza Makao Makuu Ukonga, Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi wa Magereza Boyd Patric Mwambingu, Mkuu wa Magereza Mkoa wa Pwani, Kamishna Msaidizi wa Magereza Athuman Ambayuu Kitiku, Mkuu wa Magereza Mkoa wa Mwanza, Kamishna Msaidizi wa Magereza Hassan Bakari Mkwiche,  Mkuu wa Magereza Mkoa wa Kilimanjaro, Kamishna Msaidizi wa Magereza Luhende DAVID Makwaia, Mkufunzi Mkuu wa Mafunzo ya Kijeshi na Msaidizi wa Mkuu wa Chuo cha Magereza Kiwira Mbeya, Kamishna Msaidizi wa Magereza Hamza Rajab Hamza, Afisa Mnadhimu wa Magereza Mkoa wa Tabora na Kamishna Msaidizi wa Magereza Jeremiah Yoram Katungu, Msaidizi Ofisi ya Mkuu wa Jeshi la Magereza Makao Makuu Dar es Salaam.

Wengine ni Kamishna Msaidizi wa Magereza Mzee Ramadhan Nyamka, Mkuu wa Magereza Mkoa wa Morogoro, Kamishna Msaidizi wa Magereza Afwilile Mwakijungu, Mkuu wa Gereza Isupilo Mkoa wa Iringa,  Kamishna Msaidizi wa Magereza Ally Abdallah S. Kaherewa, Mkuu wa Magereza Mkoa wa Ruvuma, Kamishna Msaidizi wa Magereza Salum Omar Hassan, Kaimu Mkuu wa Magereza Mkoa wa Singida, Kamishna Msaidizi wa Magereza Ismail T. Mlawa, Mkuu wa Magereza Mkoa wa Mtwara, Kamishna Msaidizi wa Magereza Chacha Bina Jackson, Mdhibiti wa Fedha Makao Makuu ya Magereza Dar es Salaam na  Kamishna Msaidizi wa Magereza Rajab Nyange Bakari, Mkuu wa Kikosi Maalum cha Kuzuia Ghasia Magereza Ukonga Dar es Salaam.

Wengine ni Kamishna Msaidizi wa Magereza Kijida Paul Mwankingi, Mkuu wa Magereza Mkoa wa Mbeya, Kamishna Msaidizi wa Magereza Julius Cosmas Ntambala, Msimamizi Mkuu wa Ujenzi wa Nyumba 320 za Kuishi Askari Gereza la Ukonga, Kamishna Msaidizi wa Magereza Mussa Musuluzya Kaswaka, Afisa Mkaguzi Makao Makuu Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi wa Magereza Justine M. Kaziulaya, Mratibu Msaidizi Baraza la Usalama la Taifa na  Kamishna Msaidizi wa Magereza Bertha Joseph Minde ambaye ni Mkuu wa Magereza Mkoa wa Manyara.   

Imetolewa na
Meja Jenerali Projest Rwegasira
Katibu Mkuu
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
6 Juni 2017

Waziri Mkuu Atoa ONYO Zito Kwa Wanaume Wanaowapa Mimba Wanafunzi

0
0
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema mtu yeyote atakayebainika amemkatisha mwanafunzi wa kike masomo kwa kumpa mimba au kumfanyia vitendo vya ukatili vitakavyopelekea kukatisha masomo yake ni lazima afungwe miaka 30 jela.

Majaliwa ametoa agizo hilo leo Lugalo jeshini Jijini Dar es Salaam wakati akizindua na kukabidhi vifaa vya maabara na vifaa vya wanafunzi wenye mahitaji maalumu vyenye jumla ya thamani ya Shilingi Bilioni 16.9 kwa ajili ya shule 1696 kwa nchi nzima kwa lengo la kuhakikisha uboreshaji wa masomo ya sayansi.

Vilevile Majaliwa ameiagiza TAMISEMI kuhakikisha wanakamilisha maabara za shule zote nchini 4587 ambazo bado hazijakamilika ili vifaa hivyo vianze kusaidia wanafunzi kwa haraka na kufikia malengo ya nchi ya kuwa ya uchumi wa kati.

Pamoja na hayo, Majaliwa amesema watendaji watakaoenda kinyume na maadili ya kazi zao ni lazima mkono wa sheria uchukue nafasi yake.

Mmea Wa Mmoyomoyo Katika Tiba Na Kinga Dhidi Ya Maradhi Ya Moyo

0
0
Mamilioni  ya  watu  duniani  wanasumbuliwa  na  maradhi  mbalimbali  ya  moyo.

 Inapotajwa  maradhi  ya  moyo  maana  yake  ni  uwepo  wa  hitilafu  mbalimbali  ndani ya  moyo  au  zinazo  husiana  na  moyo  ambazo  husababisha  moyo  kutokufanya  kazi  sawa  sawa.

 Kupanuka  kwa  moyo  , mapigo  ya  moyo  kwenda  kasi  na  shinikizo  kuu la  damu    ni  miongoni  mwa  maradhi  yanayo  tajwa  na  wataalamu  wa  afya  kama  maradhi  ya  moyo.

Katika   tiba  asilia,  mmea  wa   Mmoyomoyo  unatajwa  kuwa  na  uwezo mkubwa  wa  kudhibiti  na  kupambana  na  maradhi  mbalimbali  yanayo husiana  na   moyo . 

Watu   wanao  tumia  mmea  wa   Mmoyomoyo  katika  kupambana  na  maradhi  mbalimbali  ya  moyo  hupata nafuu  kubwa.

Mbali  na  kusaidia  katika  kutibu  maradhi  mbalimbali  ya  moyo, mmea  wa  Mmoyomoyo  unatumika  zaidi  katika  kinga  dhidi  ya  maradhi  mbalimbali  ya  moyo.

Matumizi  mabaya  ya  chakula, hasa  hasa  utumiaji  wa vyakula  vya  mafuta , vyakula  vyenye sukari, ulevi kupita  kiasi  pamoja  na  kutokufanya  mazoezi  ya  mwili  ( Physical  Exercises ) ni miongoni  mwa  mambo  yanayo  weza  kumuweka  mtu  katika  hatari kuu  ya  kupatwa  na  magonjwa  ya moyo.

Matumizi  ya  mara  kwa  mara  ya  mmea  wa   Mmoyomoyo  yanaweza   kupunguza  hatari  ya  kupatwa  na  maradhi  ya  moyo.

Mmea  huu  pia  unatumika  katika     kuondoa  na   kudhibiti  mafuta  yasiyo  hitajika  mwilini.

Makala  haya  yamekuja  kwenu  kwa  hisani  ya  NEEMA  HERBALIST. Duka  la  kuuza  dawa  mbalimbali  za  asili. Tunapatikana  jijini  DAR  ES SALAAM, katika  eneo  la UBUNGO  jirani  na  SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONA  HOUSING  nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA. 

Tunapatikana  kwa  simu  namba  0766  53  83 84

Na  kwa  makala  kuhusu  tiba  asilia  ya  magonjwa  mbalimbali, tembelea   blogu yetu kila  siku :


Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya June 7

Msajili wa Vyama Azungumzia Sakata la Maalim Seif Kufungua Ofisi Mpya za CUF

0
0
Kutokana na Chama cha Wananchi (CUF) kufungua ofisi mpya za chama hicho katika eneo la Mtaa wa Idrisa Kata ya Mzimuni, Magomeni wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, Msajili wa Vyama vya Siasa amesema anaamini chama hicho kinafanya mambo yake kwa kuzingatia sheria.

Jana  Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi, alisema hajapata taarifa yoyote ya chama hicho, kufungua ofisi mpya zaidi ya kuona katika vyombo vya habari.

“Ukiondoa taarifa za kwenye media sijapata taarifa yoyote kutoka CUF labda wawe wameleta leo (jana), lakini naamini chochote wanachofanya wanaelewa taratibu wataleta taarifa, “ alisema Jaji Mutungi.

Jaji Mutungi alisema sheria inawataka wanapofungua ofisi watoe taarifa ndani ya siku 14, ambazo hazijaisha hivyo anaamini wanajua hilo. 

Upande wa Katibu Mkuu, Maalim Seif Sharif Hamad wamefungua ofisi hizo, baada ya tukio la kuvamiwa katika Ofisi Kuu za Buguruni na kundi la Profesa Ibrahim Lipumba.

Jaji Mutungi alisema atakapopokea taarifa rasmi ataangalia kama taratibu zilifuatwa kwani ufunguaji wa ofisi mpya una taratibu zake. 

“Nikiletewa taarifa ndio nitajua kama walifata taratibu au la, ufunguaji wa ofisi una taratibu zake najua wanazijua pia, “ alisema Jaji Mutungi.

Alisema taarifa hiyo ataipata kutoka kwa mwenyekiti au msemaji wa chama, ambaye ni katibu mkuu ambao wanatambuliwa na ofisi ya msajili wa vyama vya siasa. 

Akizindua ofisi hiyo Juni 4 mwaka huu, Maalim Seif alisema ofisi hiyo imetolewa na wabunge 40 wa CUF.

Alisema uamuzi wa wabunge hao kumpatia ofisi ya kufanyia kazi hapo ni kitendo cha kiungwana na kiungwe mkono na wanachama wote. 

Alisema kwa miezi 10 sasa, wamekuwa wakishindwa kufanya kazi kwa upande wa Tanzania Bara, jambo ambalo limewaathiri hivyo kupatiwa ofisi kutamsaidia kutimiza majukumu bila hofu yoyote.

Katibu huyo alisema ana imani na mahakama kuwa itawapatia haki stahiki hivyo kuwataka wanachama kuendelea kuwa na subira.

IGP Sirro afanya ziara Kibiti na Rufiji.....Atangaza msako mkali

0
0
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Simon Sirro  jana alifanya mazungumzo na wazee pamoja na viongozi wa dini wilayani Kibiti mkoani Pwani ili kubaini waalifu wanaotekeleza mauaji ya watu wilayani humo na kusema vyovyote itakavyokuwa lazima watawarudisha kwenye msitari.

IGP Sirro alisema kupitia mazungumzo hayo tayari amepata taarifa za wahalifu hao ingawa ni mapema kuziweka wazi ila amewakikishia wananchi kuwa waalifu wao ni lazima watapatikana.

“Kubwa ni kwamba wazee wetu wa Kibiti wametueleza taarifa nyingi sana na mnavyojua hawa waalifu wanaishi ndani ya Kibiti, ndani ya Ikwiriri, kwa hiyo wazee wetu wamejaribu kutueleza ni wapi tunaweza kuwapata na chanzo cha mambo yote haya,” alisema IGP Sirro na kuongeza;

“Kwa hiyo kimsingi mambo mengine mengi ni ya kipelelezi ambayo siwezi kuyasema kwa sasa, lakini kikubwa wametupa dira, muelekeo kwa maana kwamba wale ndugu zetu au maadui zetu kwa lugha nyepesi tumepata njia nzuri ya kudeal nao. Kwa hiyo nitume salamu kwao kwamba waendelee kukimbia lakini njia ya muongo ni fupi na mwisho wa siku tutawarudisha kwenye mstari"

Halima Mdee na Ester Bulaya Kulipwa nusu mshahara kwa miezi 10 nje ya Bunge

0
0
Wabunge wa Chadema, Halima Mdee (Kawe) na Ester Bulaya (Bunda Mjini) ambao wamesimamishwa kuhudhuria vikao vya Bunge, watalipwa nusu mshahara na posho zinazoambatana nao kwa miezi kumi.

Stahiki hizo ni kwa mujibu wa kanuni ya 75 ya Bunge inayosema, “mbunge aliyesimamishwa hataingia tena sehemu yoyote ya ukumbi na maeneo ya Bunge kwa muda wote atakapokuwa amesimamishwa na atalipwa nusu mshahara na nusu posho zinazoambatana na mshahara huo.”

Vilevile, kutokana na uamuzi huo wabunge hao watakosa siku 65 za Bunge zinazojumuisha siku 25 zilizobaki za Bunge la bajeti linaloendelea, Bunge la Oktoba na lile la Februari, 2018. Vikao vya mabunge hayo mawili; la Oktoba na Februari kila kimoja huwa na mikutano ya wiki mbili mbili.

Wabunge hao walisimamishwa juzi kwa azimio la Bunge licha ya kutokuwapo au kujitetea kutokana na tuhuma zilizokuwa zinawakabili za kudharau kiti cha spika.

“Tukutane Bunge lijalo la bajeti,” alisema juzi Spika wa Bunge, Job Ndugai. Bunge la bajeti huanza mwezi Aprili.

Kufikia uamuzi huo, kamati ya haki, maadili na madaraka ya Bunge ilisema iliwatafuta kwa simu wabunge hao, lakini haikuwapata. Pia, iliwatumia ujumbe mfupi ambao haukujibiwa na ilipowapelekea hati ya wito haikuwakuta majumbani kwao.

Kwa kutambua umuhimu wa agizo ililonalo na kuzingatia matakwa ya kisheria, hati hizo ziliachwa baada ya kuelezwa kwamba wahusika hawapo kwani wamesafiri. Baada ya jitihada hizo kushindwa kuzaa matunda, kamati iliendelea kuwajadili bila wao kuwapo na kutoa maazimio hayo.

Pedezyee Ndama Mtoto wa Ng'ombe akiri tena utakatishaji fedha

0
0
Mfanyabiashara Ndama Shabani Hussein maarufu kama ‘Pedezyee Ndama Mtoto wa Ng'ombe’, jana alikiri kwa mara ya tatu shtaka la kutakatisha fedha dola za Marekani 540,000 baada ya upande wa utetezi kuomba mshtakiwa kukumbushwa mashtaka yake.

Awali, Mei 23 mwaka huu, Ndama alikiri kosa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ilipanga kusikiliza maelezo ya awali Mei 29, lakini aliomba muda wa kujadiliana na mawakili wa utetezi hadi Mei, 30, mwaka huu alipokumbushwa mashtaka yake na kukana kutakatisha fedha hizo.

Hata hivyo, hali ilikuwa tofauti jana katika mahakama hiyo iliyoketi jana chini ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Victoria Nongwa, baada ya Ndama kuomba kukumbushwa mashtaka yake na aliposomewa, alikiri kwa mara nyingine kutakatisha fedha hizo.

Wakili wa Serikali, Esterzia Wilson, alimkumbusha Ndama mashitaka yanayomkabili baada ya wakili wa utetezi, Jeremiah Ntobesya, kuomba mteja wake kukumbushwa mashitaka hayo.

Mahakama iliridhia ombi hilo na aliposomewa hati ya mashtaka sita, alikana mashtaka matano na kukiri shtaka la sita la kutakatisha fedha.

Katika shitaka la kutakatisha fedha, Ndama anadaiwa kuwa kwa tarehe tofauti jijini Dar es Salaam, kati ya Februari 26 na Machi 31, 2014, akiwa mwenyekiti na mtiaji saini pekee wa kampuni ya Muru Platnum Tanzania Investment Company Limited na akaunti ya benki ya kampuni hiyo iliyoko benki ya Stanbic, alijihusisha moja kwa moja katika uhamishaji fedha dola za Marekani 540,000.

Ilidaiwa kuwa alizitoa fedha hizo taslim huku akijua au alipaswa kujua kuwa fedha hizo ni za kosa la kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.

Hata hivyo, Ndama alikana mashitaka mengine ikiwamo la kudaiwa kuwa Februari 20,2014, akiwa jijini Dar es Salaam, alighushi nyaraka ya kibali cha kusafirisha madini na sampuli za madini kwa kusudi la kuonyesha kuwa kampuni ya Muru Platnum Tanzania Investment Company Limited iliruhusiwa kusafirisha maboksi manne ya dhahabu ya kilogramu 207, yenye thamani ya Dola za Marekani 8,280,000 kwenda Australia kwa kampuni ya Trade TJL DTYL Limited wakati akijua si kweli.

Pia Ndama anadaiwa kuwa Machi 6, 2014, Dar es Salaam, alighushi kwa kutengeneza hati ya kibali cha Umoja wa Mataifa Ofisi ya Dar es Salaam, akijaribu kuonyesha kuwa kilogramu 207 za dhahabu kutoka nchini Congo zinazotarajiwa kusafirishwa na kampuni ya Muru Platnum Tanzania Investment Company Limited kwenda Australia kwa kampuni ya Trade TJL PTYL Limited, zimesafirishwa bila jinai
yoyote wakati akijua ni kosa kisheria.

Aidha, anadaiwa kuwa Februari 20, 2014, alighushi fomu ya forodha yenye namba za usajili R.28092 akionyesha kampuni ya Muru imeilipa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) dola za Marekani 331,200 kama kodi ya uingizaji wa bidhaa ambazo zina uzito wa kilogramu 207 za dhahabu zenye thamani ya dola za Marekani 8,280,000 kutoka Congo.

Katika shitaka jingine, Ndama anadaiwa kuwa Februari 20, 2014, alighushi nyaraka ya bima kutoka Phoenix of Tanzania Assurance Company Ltd, akionyesha kampuni ya Muru imeyawekea bima makasha manne yaliyokuwa na dhahabu hizo.

Anadaiwa kuwa kati ya Februari 26 na Machi 3, 2014, akiwa Dar es Salaam, kwa njia ya udanganyifu alijipatia kutoka kwa kampuni ya nchini Australia ya Trade TJL DTYL Limited dola za Marekani 540,000 baada ya kudanganya atawapa na kusafirisha dhahabu hizo.

Awali, Ndama aliposomewa maelezo ya awali, baada ya kukiri kosa hilo, alikana maelezo mengi ya msingi yanayounda shitaka hilo.

Kutokana na hali hiyo, Hakimu Nongwa aliamuru kesi hiyo kuendelea kusikilizwa kwa kuwa nia ya Ndama ya kukiri kosa
ilikuwa na shaka.

Ushahidi wa Baba Yake Wasababisha Ahukumie Kunyongwa Hadi Kufa

0
0
Mahakama  Kuu kanda ya Mbeya, kwa kusaidiwa na ushahidi wa baba mzazi wa mshitakiwa, imemhukumu kunyongwa hadi kufa, Geoffrey Sichizya (27) baada ya kumtia hatiani kwa kosa la kumua babu yake ili achukue ng’ombe wake tisa.

Akisoma hukumu hiyo kwenye Mahakama ya Wilaya ya Mbozi mkoani Songwe jana, Jaji wa Mahakama Kuu Atuganile Ngwala alisema baada ya kusikiliza ushahidi wa pande zote mbili ameridhika pasipo kuacha shaka kuwa mshitakiwa alimuua babu yake Labson Sichizya kwa kukusudia.

Alisema ameridhika na ushahidi uliotolewa na Meas Sichezya ambaye ni baba mzazi wa mshitakiwa huyo, pamoja na Mashaka Sichizya ambaye ni ndugu wa damu, ambao kwa pamoja walimkamata siku ya tukio wakiwa na viongozi wa vijiji na kumpeleka polisi.

Jaji Ngwala alisema Geofrey kwenye maelezo yake kwa mlinzi wa amani alidai kuwa alimuua babu yake ili achukue ng’ombe tisa waliokuwa wanamilikiwa na babu huyo.

Awali, ilidaiwa mahakamani hapo na Wakili wa Serikali, Ofmedy Mtenga kwamba mshitakiwa alimkaba koo babu yake Sichizya hadi kufa Novemba 19, 2012 saa 2:00 asubuhi katika kijiji cha Sakamwela, wilaya ya Mbozi mkoani Songwe.

Aliendelea kusema kuwa mshitakiwa huyo baada ya kumuua babu yake huyo kwa kumkaba koo na kufariki, alimfunga na kamba ya chandarua shingoni na kumning’niza kwenye mti nyuma ya nyumba yake ili ionekane kama marehemu alijinyonga.

Mshitakiwa huyo alikuwa akitetewa na wakili Kamru Habibu, ambaye baada ya hukumu kutolewa hakuwa na hoja yoyote mbele ya mahakama hiyo.

JWTZ yatoa ONYO kwa matapeli wa ajira

0
0
Mkuu wa utumishi Jeshi la Wananchi Tanazania (JWTZ), Meja Jenerali  Harrison Masebo amekanusha taarifa  zinazoenea mitandaoni kuhusu kutangazwa kwa nafasi za ajira na kwamba watu wanaotangaza hivyo ni matapeli waepukwe.

Meja Jenerali Masebo amebainisha hayo baada ya kuenea uvumi mitandaoni na mitaani kwa baadhi ya watu kujifanya wanahusika na jeshi hilo katika idara ya kutoa ajira kwa wananchi.

"Kumekuwa na vikundi ama watu ambao kwa namna moja ama nyingine wamekuwa wakijitangaza wao wanauwezo kutoa ajira, vikundi hivyo msivisikilize siyo vikundi rasmi ama watu hao siyo rasmi kwa niaba ya Mkuu wa Majeshi nasema kuanzia leo mtu akisiikia kuna mtu anamfuata anamwambia kuna nafasi ya kujiunga na mafunzo ya JKT ajue huyo mtu siyo halali ni muongo na tapeli" -alisema Meja Jenerali Masebo.

Pamoja na Hayo Meja Jenerali Masebo amesema mara zote Jeshi limekuwa likitoa ufafanuzi kuhusiana na masuala ya ajira lakini wanashangazwa na kundi hilo namna wanavyofanya kutaka kupitia 'shortcut'.

"Jeshi limekuwa likifafanua mara kwa mara kuhusu taratibu za kujiunga nafasi za mafunzo JKT na taratibu za kujiunga na jeshi la wananchi lakini katika mazingira ambayo tunashindwa kuyaelewa hawa watu au vikundi ndiyo wamekuwa wajanja kiasi cha kuwarubuni vijana, wazazi na wazazi wakaamini kwamba zipo njia mbadala za kujiunga 'shortcut' napenda kusema hakuna shortcut hapa" - alisisitiza Meja Jenerali Masebo

Pamoja na hayo, Meja Jenerali Masebo aliendelea kufafanua baadhi ya mambo kwa kusema "Kwa vyombo vyote vya ulinzi na usalama hata wakiwa Uhamiaji, Zima moto, Magereza, Polisi, TANAPA na Jeshi lenyewe ukitaka kujiunga na Jeshi la Wananchi maana yake ni kwamba kuna utaratibu maalumu ambapo kwanza kuna kikao ambacho wenyekiti wa kikao hicho ni mimi Mkuu wa Utumishi Jeshini kwa hiyo vyombo vingine vya ulinzi na usalama vinaleta wawakilishi ambao ni maofisa watumishi tunakaa pamoja kila taasisi, wanaleta idadi ya watu wanaowahitaji" - Meja Jenerali Masebo aliongeza.

Mwanasheria Mkuu wa TBS Afikishwa Mahakamani

0
0
Mwanasheria Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Baptister Marco (54) amepandishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kujibu mashtaka matatu ya kuishi na kufanya kazi nchini bila kuwa na  kibali.

Mwendesha Mashtaka wa Uhamiaji, Novatus Mlay alimemsomea mashtaka hayo leo Jumatano kwa Hakimu Mkazi Mkuu, Victoria Nongwa.

Akisoma hati ya mashtaka,  Mlay alidai kuwa  Mei 19, 2017  huko Kinondoni katika ofisi ya uhamiaji,  Marco akiwa raia wa Burundi alikutwa nchini bila kuwa na kibali cha kumuwezesha kuishi.

Marco katika shtaka la pili amedaiwa kuwa siku hiyo alikutwa akifanya kazi kama Mwanasheria Mkuu wa TBS bila ya kuwa na kibali kinachomruhusu kufanya kazi hapa nchini.

Katika shtaka la tatu, Mlay alidai kuwa, Julai 6 mwaka 2011 katika ofisi ya Uhamiaji ya Dar es Salaam iliyopo Wilaya ya Ilala, mshtakiwa huyo akiwa raia wa Burundi alitoa taarifa za uongo kuhusu maelezo yake binafsi wakati akijaza fomu ya kuomba hati ya kusafiria namba CT (5)(Ai).

Wakili Mlay alisema kitendo hicho cha kutoa taarifa za uongo kilimuwezesha Marco kupata hati ya kusafiria ya Tanzania yenye namba AB 474856 huku akijua kufanya hivyo ni kinyume cha sheria za nchi.

Baada ya kusomewa mashtaka hayo, alikana na upande wa mashtaka ulidai kuwa upelelezi bado haujakamilika.

Mshtakiwa alitakiwa kuwa na wadhamini wawili wanaoaminika ambao kila mmoja atasaini bondi ya Sh 20 milioni na alikamilisha. Kesi imeahirishwa hadi Juni 21, 2017 kwa ajili ya kutajwa.

Jipatie Dawa za Asili za Kupunguza Maziwa, Kupunguza tumbo, Kuongeza nguvu za Kiume na Mvi

0
0
(OFFER OFFER OFFER) NATURAL BEAUTY COSMETIC INAKUPATIA OFA YA PUNGUZO LA BEI KWA KILA BIDHAA PUNGUZO LA  %10 KWA MWEZI HUU WA RAMADHANI. 
 
PATA BIDHAA HIZI ZILIZOTENGENEZWA KWA MIMEA NA MATUNDA UFURAHIE MATOKEO MAZURI BILA KEMIKALI WALA MADHARA YOYOTE PIA NI GUARANTEE. Bidhaa tulizonazo÷
 
🍉🍓🍇🍅🍊🍒🍍🌴🍐🧀🧀🧀🧀🍅🍇🍇🍇🍇🍇🍇🍐🍍🌳🍏🍐🌶🍉🍆🍆🍒.
Pata punguzo la bei kwa bidhaa hizi.
1. YODI PILLS _ Ni vidonge vya kuongeza hips na makalio @170,000/=
2. BOTCHO CREAM_ Ni dawa ya kupaka ya kuongeza shepu (hips na makalio) @150,000/=
3. BOTCHO MULT PLUS_ Hii ni dawa ya kunywa ya kuongeza shepu (hips makalio na mapaja) @200,000/=
4. PANNAMAS BREAST_ Ni dawa ya kupunguza maziwa na kuyasimamisha hata kwa walio nyonyesha. Inapatikana kwa Tsh @120,000/=
5. DISCREET_Hii ni kwa ajili ya kuondoa mvi milele na zisiludi tena. @120,000/=
6. BODY BOOSTER_Ni dawa ya kuongeza mwili mzima na kukupa hamu ya kula vizuri. Inapatikana kwa Tsh @130,000/=
7. LEG BOOSTER_Ni dawa ya kuongeza miguu kuwa (Chupa ya bia) @120,000/=
8. HAIR GROWTH STIMULATOR_ Ni mafuta ya kulefusha nywele na kuzuia kukatika ovyo. Yanapatikana kwa Tsh @100,000/=
9. MICRO COMPUTER_ Ni mkanda wa kupunguza tumbo na manyama uzembe. @170,000/=
10.HANDSOME UP ni kifaa kinachoongeza maumbile ya kiume  kwa 99% kwa size uipendayo wewe na kuimarisha misuli ya uume kwa @170,000/= tuu.
11.MEN GELY YA KUPAKA. Hii inaongeza kwa wastani wa inch 6.5 na inapatikana kwa @120,000/=. 
12. SHARK POWER. Hii pia ni kwa ajili ya kuongeza maumbile  wastani wa inch 7.5 inapatikana kwa @135,000/=.
15. MAX MAN 2. Ni vidonge kwa ajili ya nguvu ambavyo vinasaidia sana hata kwa watu wenye kisukari na waliokua wakifanya sana master blashion. Pia huongeza hamu ya tendo la ndoa inapatikana kwa @130,000/=
🌳🍉🍌🍅🍍🍐🍓🍆🍐🍒🍒🍓🍓🍑🍍🍍🍓🍓🍓🍍🍐🍐🍈🍉
Tupo DAR ES SALAAM  kariakoo na kinondoni kanisani.
Kwa mawasiliano zaidi piga  0759029968 au 0659618585. 
 
Popote ulipo utapata huduma zetu.
                 Follow us
@natural2162
@natural2162
@natural2162
@natural2162
     Bidhaa zetu zote ni garantii na unapewa risiti
              Karibu

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya June 8

Anna Mgwhira avuliwa uenyekiti ACT- Wazalendo

0
0
Chama cha ACT Wazalendo  kimesitisha rasmi uenyekiti wa aliyekuwa Mwenyekiti wa chama hicho tangu kuanzishwa kwake, Anna Mghwira, baada ya kuteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro kuazia  jana  Juni 7.

Uamuzi huo umefanywa na kikao cha Kamati ya Uongozi ya chama hicho ambacho pia kimemteua Mwenyekiti wa Kamati ya Mafunzo, Oganaizesheni na Uanachama kuwa Kaimu Mwenyekiti wa chama hicho hadi uchaguzi mkuu utakapofanyika mwezi Machi mwakani.

Akitangaza uamuzi huo kwa wanahabari jana , Kaimu Kiongozi wa chama hicho, Samson Mwigamba amesema sababu kuu ya kusitisha uenyekiti wa Anna Mghwira, ni ili kumpa nafasi ya kutekeleza majukumu yake mapya aliyopewa na Rais wa Tanzania, pamoja na kumfanya asiwe na mgongano wa kimaslahi ya kichama wakati akitekeleza majumu yake kama kiongozi.

“Sisi kama ACT hatupingi uamuzi wa mamlaka ya Rais, isipokuwa kamati ya uongozi imeona ni busara kumpa nafasi Anna Mghwira kutumikia nafasi moja kama kiongozi, lakini ataendelea kuwa mwanachama wa ACT Wazalendo. Kabla ya kutangaza uamuzi huo tayari tumewasiliana naye na tumekubaliana hivyo. Tunamtakia kila la heri katika majukumu yake mapya,” alisema Ado Shaibu ambaye ni Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mawasiliano kwa umma.

Pamoja na hayo Mwigamba alimpongeza  Rais kwa kuvunja miiko ya siasa za Tanzania kwa kumpatia mpinzani nafasi hiyo ndani ya serikali yake  na kuongeza kuwa kama chama hawana tatizo kwa kiongozi huyo kukabidhiwa ilani ya CCM kwa sababu anakwenda kutumikia serikali kuu na Taifa.

Kutana Maajabu ya Mtabibu CHIEF SULTAN(MAKATA WA MAKATANI) Mganga wa Waganga Sasa Yupo Mikoa Yote Tanzania

0
0
Kutana Maajabu ya Mtabibu CHIEF SULTAN(MAKATA WA MAKATANI) Mganga wa Waganga Sasa Yupo Mikoa Yote Tanzania
 
Pia anatoa Tiba kwa Njia ya Simu ukiwa popote Pale Tanzania au Nje ya Tanzania..
CHIEF SULTAN ni Mtabibu na Mtafiti wa Dawa za Asili ya Africa, na Duniani Katika utoaji wa Tiba za Asili..
Je unasumbulia na Mapenzi..?


(Umeachwa na Umpendae awe Mume/ Mke au mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine na Bado Unampenda?) Umejaribu sehemu Nyingi bila Mafanikio?Wasiliana na CHIEF SULTAN Akusaidie Kumshika Umpendae Asikusaliti(LIMBWATA) Kumtawala Mpenzi wako kwa sababu Maalum..Anauwezo wa Kusambalatisha Mahusiano yao ndani ya siku Moja tu.


Je Unasumbuliwa na Madeni?
Biashara yako Haina wateja?
Unatatizo la kutokushika Mimba na umehangaika sehemu nyingi bila mafanikio?
Wasiliana na CHIEF SULTAN Kwa Majibu ya Maswali yako..
Anasafisha NYOTA na Kutoa PETE za BAHATI kuendana na NYOTA yako. UTAJIRI USIO NA MASHARTI.(Magic Wallet_Pochi ya Maajabu Isio Isha Hela)


KUWA MAARUFU na KUJULIKANA
Kupandishwa CHEO na HESHIMA Mahala pa KAZI.
Utapewa Nguvu ya Kujilinda na MALI ZAKO zako na Mwili wako.. Huzuia Chuma Ulete katika Biashara.. Hurudisha MALI zilizo Potea au KUDHULUMIWA..
Mvuto wa Biashara na Mwili wako.
Hutibu kabisa Nguvu za Kiume na Kurefusha Uume kwa saizi Unayotaka.

Magonjwa Sugu(Miguu Kufa Ganzi, kisukari, Presha, Pumu nk.)Humaliza Kesi za Muda mrefu ndani ya siku 14 tu.


Anatoa NDAGU Zisizokuwa na Masharti.. Kwa maelezo Zaidi wasilina nae kwa 

 
whatsapp +255 0658 316 976
Call +255 755 911 233
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images