Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Mjadala wa BANGI Watikisa Bunge

$
0
0
Leo wakati mkutano wa saba , kikao cha 40 kikiendela bungeni Dodoma umeibuka mjadala wa dawa za kulevya aina bangi baada ya baadhi ya wabunge kusema kuna vitendo vinavyofanywa na baadhi ya polisi nchini vinatokana na polisi hao kuwa wamelewa bangi.

Katika mjadala huo Mh Spika Job Ndugai naye alichomekea kuwa huwa anasikia watu wanasema bangi zinaongeza nguvu, hivyo naye alitaka kujua hizo bangi zinaongeza nguvu za aina gani, huki akiwauliza wabunge ambao wanatokea maeneo ambayo bangi imekuwa ikiripotiwa sana.

Kufuatia mjadala huo kuendelea alisimama Mbunge Esther Matiko Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Mara na kusema yeye mwenyewe huwa anaona polisi wakichoma bangi katika maeneo hayo na kudai huenda baadhi ya vitendo vinavyofanywa na polisi wetu ni kutokana na kuathirika na moshi wa bangi wakiwa wanachoma bangi hizo. Lakini katika ufafanuzi wa Naibu Waziri wa Afya alisema polisi hao wao huwa hawaathiriki na moshi huo.

"Jamani tunapojadili juu ya suala la madawa ya kulevya si jambo la mzaha, ni kwamba polisi wanapokwenda kuchoma bangi mashambani huwa wanajifunika vifaa maalum lakini hata kama hawajifuniki vifaa hivyo bado ile bangi ikiingia kwenye miili yao itaondoka ndani ya siku 30 kwani inageuka na kuwa chumvi na kutoka kwa njia ya mkojo na jasho. Lakini kwa watu ambao wanatumia kila siku yaani leo, kesho, kesho kutwa na kuendelea wao wanakuwa ni clonic wa dawa hizo" alisema Kigwangalla

Licha ya Naibu Waziri wa Afya kutoa ufafanuzi juu ya uchomaji wa bangi lakini Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Jenista Joakim Mhagama alisimama na kutoa ufafanuzi wake pia akisema kuwa polisi hawajaathirika na bangi kutokana na namna ambavyo huwa wanachoma bangi hizo kwa kufuata utaratibu mzuri.

"Mh. Spika vikosi vya polisi vinavyofanya utekeketezaji wa bangi, zipo njia nyingi wanatumia kuteketeza bangi hizo, kwanza wakiwa wanafanya zoezi hilo huwa wanaangalia uelekeo wa upepo lakini pia maandalizi mengine ya vifaa vyao vya uteketezaji wa bangi, aina ya mafuta yanayotumia kwenye kuchomea bangi hizo vinawafanya kuwa salama kabisa, kwa hiyo siyo kweli kwamba likitokea tatizo kwenye jeshi la polisi kwamba polisi wetu wameathirika na matumizi ya bangi, kwani polisi wetu ni weledi na wanafanya kazi kwa kufuata utaratibu na sheria" alisisitiza Mhagama

Kwa kumalizia mjadala huo Spika wa Bunge, Job Ndugai alisema kuwa nchi nzima na viongozi wamesikia juu ya jambo hilo hivyo wanapaswa kuwa makini katika utekelezaji wa mambo hayo.

Kutanana na Maajabu ya Mtabibu CHIEF SULTAN(MAKATA WA MAKATANI) Mganga wa Waganga Sasa Yupo Mikoa Yote Tanzania

$
0
0
Kutanana na Maajabu ya Mtabibu CHIEF SULTAN(MAKATA WA MAKATANI) Mganga wa Waganga Sasa Yupo Mikoa Yote Tanzania

Pia anatoa Tiba kwa Njia ya Simu ukiwa popote Pale Tanzania au Nje ya Tanzania..

CHIEF SULTAN ni Mtabibu na Mtafiti wa Dawa za Asili ya Africa, na  Duniani Katika utoaji wa Tiba za Asili..
 
 Je unasumbulia na Mapenzi..?
(Umeachwa na Umpendae awe Mume/ Mke  au mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine na Bado Unampenda?) Umejaribu sehemu Nyingi bila Mafanikio?Wasiliana na CHIEF SULTAN Akusaidie Kumshika Umpendae Asikusaliti(LIMBWATA) Kumtawala Mpenzi wako kwa sababu Maalum..Anauwezo wa Kusambalatisha Mahusiano yao ndani ya siku Moja tu.
 
Je Unasumbuliwa na Madeni?
Biashara yako Haina wateja?
Unatatizo la kutokushika Mimba na umehangaika sehemu nyingi bila mafanikio?
 
Wasiliana na CHIEF SULTAN  Kwa Majibu ya Maswali yako..
Anasafisha NYOTA na Kutoa PETE za BAHATI kuendana na NYOTA yako. UTAJIRI USIO NA MASHARTI.(Magic Wallet_Pochi ya Maajabu Isio Isha Hela)
 
KUWA MAARUFU na KUJULIKANA
Kupandishwa CHEO na HESHIMA Mahala pa KAZI.
Utapewa Nguvu ya Kujilinda na MALI ZAKO zako na Mwili wako.. Huzuia Chuma Ulete katika Biashara.. Hurudisha MALI zilizo Potea au KUDHULUMIWA..
 
Mvuto wa Biashara na Mwili wako.
Hutibu kabisa Nguvu za Kiume na Kurefusha Uume kwa saizi Unayotaka.
 
Magonjwa Sugu(Miguu Kufa Ganzi, kisukari, Presha, Pumu nk.)Humaliza Kesi za Muda mrefu ndani ya siku 14 tu.
Anatoa NDAGU Zisizokuwa na Masharti.. Kwa maelezo Zaidi wasilina nae kwa  +255 0658 316 976

Mahakama Kuu ya Uganda yaamuru kaburi la Ivan Semwanga(Aliyekuwa Mume wa Zari) lifukuliwe

$
0
0
Wanasheria nchini Uganda wameamua kuifikisha familia ya Ivan Mahakamani kwa makosa ya kuzika pesa halali za Jamhuri ya Uganda katika kaburi la ndugu yao Ivan. Kwa nchi yoyote kitendo hicho hakikubaliki kwani pesa hizo zingeweza kutumika katika shughuli zingine na kukuza uchumi wa nchi.

Kitendo hicho kinakuja baada ya marafiki wa Ivan kumwaga mamilioni ya pesa ndani ya kaburi la Ivan kama njia ya kumuaga rafiki yao aliyekuwa maarufu kwa matumizi makubwa ya pesa.

Wanasheria wakiongozwa na Tugume Gideon wa Human Rights Defenders Association Uganda wamesema hawakufurahishwa na kitendo cha RICH GANG cha kuzika mamilioni ya pesa ndani ya kaburi, na kwa vile ni kinyume cha sheria,

wameamua kwenda mahakamani kuomba kaburi la Ivan lifukuliwe, pesa zitolewe zikafanye shughuli nyingine na waliohusika washitakiwe kwa kuharibu kwa makusudi alama ya taifa.

Sababu Iliyowafanya Wabunge wa Upinzani Wasuse na kutoka Nje

$
0
0
Mbunge wa Kibamba, John Mnyika ametolewa nje ya Bunge leo Ijumaa kwa agizo la Spika wa Bunge, Job Ndugai.

Licha ya adhabu hiyo, amemzuia kutohudhuria vikao vya Bunge kwa siku saba kuanzia leo.

Mnyika ametolewa baada ya mmoja wa wabunge kusema 'Mnyika mwizi' akimhusisha na wizi wa madini, hoja inayochangiwa na wengi kwenye mjadala wa Wizara ya Nishati na Madini unaoendelea.

Kutokana na hali hiyo Mnyika alimtaka Spika kuchukua hatua kwa mbunge aliyesema kuwa yeye ni mwizi lakini Spika akasema hajui hilo na haijaingia kwenye hansadi. Hata hivyo Mnyika alisisitiza kuwa mambo hayaweze kwenda hivyo.

Baada ya majibizano kati yake na Spika, Spika akaamuru walinzi wamtoe Mnyika nje ya Bunge na asihudhurie vikao saba vinavyofuata.

Mnyika alikuwa akitoa maelezo baada ya Mbunge wa Mtera, Livingston Lusinde kusema upinzani wa Tanzania ni wa ajabu kwani unatetea wezi wa madini.

Baada ya hatua hiyo, wabunge wa upinzani waliamua kutoka nje kupinga mnyika kutolewa nje.

Wakiwa nje ya ukumbi wa bunge, Mbunge wa Bunda, Esther Bulaya alizungumza na waandishi wa habari na kusema hawakubaliani hatua iliyochukuliwa na spika dhidi ya mwenzao kwani kuna mbunge wa CCM alisema wabunge wengine hawana akili lakini hakuchukuliwa hatua yoyote.

“Nadhani hata nyinyi mmeona mbunge aliyekuwa anachangia anasema kuwa wabunge wengine wapimwe akili, inawezekana hawana akili anaachwa kwa sababu tu ni mbunge wa Chama Cha Mapinduzi.”

Aidha, Bulaya alisema kazi ya upinzani ni kuikosoa serikali pale mambo yanapokuwa hayaendi sawa ni si kupongeza kila kitu. Alifafanua zaidi kuwa hawawezi kuwa wanaisifia tu serikali, bali watafanya hivyo pale panapopasa kama kwenye wizara ya ardhi ambapo walimpongeza waziri kwa kazi kubwa anayofanya.

“Msimamo wetu kama Kambi ya Upinzani tumeamua kutoka kwa sababu hatuwezi kujadili mambo ya msingi kwa kufanyiwa mambo haya, sisi kazi yetu ni kuishauri serikali lakini hatuwezi kuishauri serikali vile wanavyotaka wao. Kwenye Wizara ya Ardhi mbona wabunge wa upinzani walisimama na wakapongeza na Wizara ya Ardhi ilipita bila shida yoyote kwa pande zote mbili, sasa kwanini wao wanataka kupongezwa tu? Kazi yetu ni kuona pale ambapo mambo hayaendi sawa kwa mujibu wa sheria tunasema na hili liwe wazi watu waliokuwa wakipigia kelele mikataba mibovu ni upinzani bungeni” alisisitiza Ester Bulaya.

Wakati huo huo, Kamati ya Bunge ya Maadili itamjadili Mbunge Esther Bulaya kwa kosa la kushawishi wenzake kutoka nje.

Spika wa Bunge pia ameiagiza Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kujadili kitendo cha Mbunge wa Kawe, Halima Mdee cha kuzuia Askari wa bunge kumtoa nje Mbunge John Mnyika.

Yeriko Nyerere Afikishwa Mahakamani Kisutu

$
0
0
Mfanyabiashara na kada maarufu wa CHADEMA   Yericko Nyerere amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na mashtaka matano ya kutoa taarifa za upotoshaji kupitia mtandao wa Facebook.

Kwa mujibu wa kesi hiyo namba 184, 2017, Wakili wa Serikali, Elia Athanas alidai kwa Hakimu Mkazi Mkuu,Wilbard Mashauri kuwa mshtakiwa huyo alifanya makosa hayo kinyume na kifungu cha 16 cha Sheria ya Mtandao Namba 14 ya 2015

Ameachiwa kwa dhamana baada ya kukamilisha masharti ya kuwa na mdhamini mmoja ambaye amesaini bondi ya Sh 10milioni.

Kesi imeahirishwa Juni 5, 2017 kusomewa maelezo ya awali (PH)

Rais Magufuli Atoa Maagizo Mazito Kwa IGP Simon Sirro

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amelitaka Jeshi la Polisi nchini kutumia weledi wake kwa kiwango cha juu katika kutekeleza jukumu lake lakulinda raia na mali zao, hasa kukomesha vitendo vya uhalifu.

Mhe. Rais Magufuli ametoa agizo hilo leo tarehe 02 Juni, 2017wakati akizungumza na Makamanda Wakuu kutoka makao makuu ya polisi, Makamanda wa Mikoa na Vikosi vya Tanzania Bara na Zanzibar na viongozi wote wakuu wa polisi wa Mkoa wa Dar es Salaam waliokutanakatika Bwalo la Maofisa Wakuu wa polisi lililopo Oysterbay Jijini Dar es Salaam.

Mhe. Dkt. Magufuli amelipongeza Jeshi la Polisi kwa juhudi zake za kukabiliana na uhalifu lakini ametaka juhudi hizo ziongezwe hususanikukabiliana na matukio ya ujambazi na mauaji ya raia, dawa za kulevya na kuendesha operesheni zenye tija katika mikoa yote.

Amemuagiza Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro kujipanga vizuri yeye na safu yake ya Makamanda, Viongozi Wakuu wa Vikosi na Maofisa mbalimbali ili kuondoa dosari zote za utendaji kazi zinazoshusha ufanisi na heshima ya Jeshi la Polisi.

“Ni lazima ufanye mabadiliko makubwa, nataka kuona Jeshi la Polisi linakuwa Jeshi la Polisi, Wewe IGP Sirro na Makamnda wenzako hakikisheni mnakomesha uhalifu, komesheni mauaji dhidi ya raia, ujambazi na dawa za kulevya” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli amewataka Makamanda, Maofisana Askari wa jeshi hilo kujiepusha na rushwa, dawa za kulevya, kutumiwa na watu kwa maslai binafsi, kuingia mikataba isiyo na maslai kwa Jeshi na Taifa, ubadhirifu na kuacha upendeleo katika utoaji wa ajira na vyeo.

Mhe. Rais Magufuli pia ametaka Makamanda, Maofisa na Askari wote wa Jeshi la Polisi wampe ushirikiano wa kutosha IGP Simon Sirro ambaye hivi karibuni amemteua kuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini.

Kikao hicho kimehudhuriwa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Mwigulu Lameck Nchemba na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Meja Jenerali Mstaafu Projest Rwegasira.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
02 Juni, 2017
 

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya June 3

Bodaboda Achinjwa Kinyama na Kuporwa Pikipiki

$
0
0
Mwanaume mmoja (30) mkazi wa Nyankumbu wilayani Nyamagana mkoani Geita anashikiliwa na jeshi la polisi kwa kosa la mauaji ya dereva bodaboda yaliyotokea majira ya 3:00 Usiku tarehe 06.05.2017.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza ACP Zarau Mpangule amemtaja mtuhumiwa huyo kuwa ni Andrea anayedaiwa kupora pikipiki na kumuua dereva wa pikipiki Bw. Alphonce Sekagi (32) mkazi wa wilayani Sengerema wakilishirikiana na wenzake wawili kisha kutoroka na pikipiki kusikojulikana.

Taarifa zinaeleza kuwa marehemu alikuwa dereva bodaboda wa mji wa Sengerema na siku ya tukio alipakia abiria watatu kwenye pikipiki yake wakitokea Sengerema mjini kwenda kijiji cha Tabaruka na kwamba wakati wakiwa njiani abiria hao walimkata dereva huyo na kitu chenye ncha kali shingoni kisha wakamchinja kwa kutumia panga shingoni na kupelekea kupoteza maisha papo hapo.

Kamanda Mpangule amesema wananchi walitoa taarifa polisi kuhusiana na tukio hilo ambapo askari walifanya ufuatiliaji wa haraka hadi eneo la tukio na kufanya msako mkali wa kuwatafuta watuhumiwa wa mauaji hayo katika maeneo mbalimbali kwa kushirikiana na wananchi ndipo  tarehe 01.06.2017 majira ya saa 8:30 mchana wakafanikiwa kumtamata mtuhumiwa mmoja akiwa na pikipiki waliyoipora katika mauaji hayo.

Kamanda Mpangule ameendelea kwa kusema upelelezi na msako wa kuwatafuta watuhumiwa wengine wawili ambapo wanadaiwa kushiriki katika mauji hayo pamoja na uporaji unaendelea huku mtuhumiwa aliyekamatwa anafanyiwa mahojiano na uchunguzi ukikamilika atapandishwa mahakamani.

Serikali kusafirisha mwili Mzee aliyechora Nembo ya Taifa Francis Maige Kanyasu

$
0
0
Mwili wa Mzee Francis Maige Kanyasu alimaarufu kwa jina la Mzee Ngosha ambaye anayetajwa kuwa ni moja wa wachoraji wa nembo ya Taifa aliyefariki tarehe 30 mwezi wa 5 unatarajiwa kusafirishwa leo  kuelekea Misungwi Mwanza.

Kwa mujibu wa taarifa ya Katibu Mkuu Wizara ya Afya (Maendeleo ya Jamii) imesema kuwa ndugu wa Mzee Kanyasu wamepatikana na sasa serikali itagharamia kusafirisha mwili wa mzee huyo mpaka Mwanza ambapo atakwenda kuzikwa huko.

Mwili wa Mzee Francis Maige unatarajiwa kuagwa leo  Jumamosi saa 2 asubuhi Hospitali Taifa ya Muhimbili kabla ya kuanza safari ya kuelekea Mwanza.

Marekani Yaionya China

$
0
0
Marekani imeionya China kuhusu mpango wake wa kupeleka wanajeshi wake katika visiwa ilivyojenga baharini kusini mwa nchi hiyo kwaajili ya kujilinda na maadui wa taifa hilo.

Onyo hilo limetolewa na Waziri wa ulinzi wa Marekani, James Mattis katika mkutano wa kujadili masuala ya usalama uliofanyika Singapore, ambapo amesema kupeleka wanajeshi katika visiwa hivyo kutahatarisha amani ya dunia.

Aidha, ameongeza kuwa kama China itaendelea na mpango wake wa kupeleka wanajeshi katika visiwa hivyo, kuha hatari kubwa uhusiano kati ya nchi hizo kuvurugika na kuhatarisha amani ya eneo hilo.

Hata hivyo, hatua hiyo ya Marekani imekuja mara baada ya Baraza la Usalama kuiongezea vikwazo Korea ya Kaskazini kufuatia kufanya majaribio kadhaa ya makombora ya masafa marefhu.

Mwigulu Nchemba Awataka Chenge, Werema Waeleze Maslahi Yao Mchanga wa Madini

$
0
0
Waziri  wa Mambo ya Ndani  ya Nchi, Mwigulu Nchemba, ametaka wanasheria wakuu wa Serikali wastaafu waeleze hadharani maslahi waliyonayo kwenye kampuni za madini zinazosafirisha mchanga nje ya nchi.

Hatua hiyo ya waziri imekuja siku chache baada ya wanasheria wakuu wastaafu waliofanya kazi kwa nyakati tofauti wakati nchi ikiingia kwenye mikataba ya madini ‘kujivua lawama’ kuhusu udanganyifu uliogunduliwa kuhusa sakata la usafirishaji wa mchanga.

Wanasheria hao wakuu wa Serikali wastaafu ni Andrew Chenge na Jaji Frederick  Werema na amewataka wamwache Rais Dk. Magufuli aendelee kulinda rasilimali za umma zisiliwe na watu wachache.

Mwigulu amesema hayo juzi, wakati akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliohudhuriwa na mamia ya wananchi wa Tarafa ya Ndago, Jimbo la Iramba.

Alisema Chenge na Werema kwa nyakati tofauti wakiwa wanasheria wakuu wa serikali, pamoja na majukumu yao mengine, wameshiriki kusaini  mikataba mikubwa mikubwa, ikiwamo ya makampuni ya kuchimba madini.

“Kwa akili ya kawaida tu, baadhi ya mikataba mikubwa, ikiwamo ya makampuni ya madini, haikuwa sawa… ndiyo maana imelalamikiwa kwa muda mrefu.” alifafanua Mwigulu, Mbunge wa Jimbo la Iramba.

Alisema juzi juzi magazeti yameeleza kuwa akina Chenge na Werema wamedai kuwa Rais wetu Magufuli amedanganywa na tume maalumu ya Profesa Mruma.

 “Wao ndio waliosaini mikataba ambayo imechangia Taifa kupoteza mabilioni ya fedha kupitia usafirishaji wa michanga nje ya nchi. Sasa wamegeuka na kuwa upande wa pili wa watu waliosaini pamoja mikataba hiyo mibovu. Nawashauri watoke hadharani…. waeleze wana maslahi gani na kampuni wanazozitetea,”alifafanua zaidi.

Aidha, Mwigulu amesema Chenge na Werema wakishindwa kuweka wazi maslahi waliyonayo, basi ni vema wakakaa kimya na kumwacha Rais wa vitendo aendelee kuinyoosha nchi.

“Hivi ukimpa mtu kazi ya kuuza duka, halafu kila siku awe anakuambia hajauza kitu na huku akilalamika kuwa kila siku anapata hasara. Unamshauri aachane na biashara inayompatia hasara, haachi…anaendelea kuwepo tu, utamwalewaje. Si atakuwa si mkweli, mwongo ananufaika na hilo duka,” alisema.

Akiijengea nguvu hoja yake, alisema Chenge na Werema wanaishi Masaki, jijini Dar es Salaam, hawa hawawezi au watakuwa wamesahau maisha ya Watanzania wengi maskini waliopo vijijini. Hivyo wamwache Rais Magufuli ambaye ameonyesha uzalendo wa kweli, aendelee kulinda rasilimali za umma.

 Alisema kwa wao wanaomfahamu Rais Magufuli, kwa hili la kuchokonoa kwenye madini na kubaini upotevu mkubwa wa fedha za umma, ni mwanzo tu, kazi bado ipo mbele ya kuchokonoa zaidi ubadhirifu na wizi wa mali ya umma katika sehemu mbalimbali.

 Mwigulu ametumia fursa hiyo kuwaomba Watanzania wazalendo wa madhehebu ya dini mbalimbali waendelee kumwomba Mungu ampe Rais Magufuli afya njema na ujasiri wa kuziba mwinya yote inayotia hasara Taifa letu.

Rais Magufuli amteua Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 03 Juni, 2017 amemteua Bibi Anna Elisha Mghwira kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro.

Bibi Anna Elisha Mghwira anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Saidi Meck Sadiki aliyekuwa Mkuu wa Mkoa huo.

Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli amemteua Meja Jenerali Issah Suleiman Nassor kuwa Balozi.

Kabla ya uteuzi huo Meja Jenerali Issah Suleiman Nassor alikuwa Mkuu wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ).

Halikadhalika, Mhe. Rais Magufuli amemteua DIGP Abdulrahman Omari Juma Kaniki kuwa Balozi.

Kabla ya uteuzi huo DIGP Abdulrahman Omari Juma Kaniki alikuwa Naibu Mkuu wa Jeshi la Polisi.

Tarehe ya kuapishwa kwa wateule wote itatangazwa baadaye.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
03 Juni, 2017

CHADEMA Wazuiwa Kumuaga Mzee Ndesamburo Uwanja wa Mashujaa

$
0
0
Mbunge wa Arusha mjini, Mh. Godbless Jonathan Lema amedai Vyombo vya usalama vimezuia kuaga mwili wa aliyekuwa Mbunge wa Moshi mjini Mh. Philemon Ndesamburo kwenye uwanja wa Mashujaa. 

Hatua hiyo inakuja ikiwa tayari maandalizi yameanza kufanywa katika Uwanja wa Mashujaa kwa ajili ya kuuga mwili wa Ndesamburo lakini OCD Moshi  amezuia na kusema shughuli hiyo itafanyika Majengo badala ya Mashujaa kuepuka kuzuia shughuli za kila siku.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya June 4

SORRY MADAM -Sehemu ya 66 & 67 (Destination of my enemies)

$
0
0
 MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWAILIPOISHIA

ILIPOISHIA
Ukelele wa kulia kwa uchungu ulio tokea juu kabisa ya gorofa ukawafanya wote watatu kustuka hususani Shamsa ndio alishtuka zaidi, akajitoa mikononi mwa madam Mery na kuanza kukimbilia kuelekea gorofani, huku Madam Mery na Sa Yoo wakimfwata kwa nyuma. Wote watatu wakamkuta Black Shadow akiwa amepiga magoti chini, akilia kama mtoto huku sura yake akiwa ameiinamisha kwenye mwili wa Sabogo ulio lala chini kwa kunyooka ukishiria kwamba Sabogo amepoteza maisha.
“Babyyyy……..”
Shamsa aliita huku akikimbilia sehemu alipo Black Shadow, na kuwaacha Sa Yoo na Madam Mery wakiwa wamesimama wasijue ni nini cha kufanya.

ENDELEA
Shamsa akazidi kumsogelea Black Shadow, taratibu akamgusa begani jambo lililo mfanya Black Shadow kujiifikiria kwa muda kabla hajainyanyua sura yake kwa maana anamtambua vizuri Shamsa kwamba ni mwanae wa kumlea japo Shamsa hatambui ukweli wa aina yoyote.

‘Liwalo na liwe’
Black Shadow alizungumza huku taratibu akinyanyua kichwa chake kutoka katika mwili wa Sabogo aliye iaga dunia kwa kupigwa risasi na Lee Si. Taratibu Black Shadow akaigeuza sura yake na kumtazama Shamsa aliye stuka na kuyatoa macho yake, mstuko huo haukuwa kwa Shamsa peke yake, bali Madam Mery pamoja na Sa Yoo nao wakabaki wakimkodolea macho Eddy kwani wote walili wanamtambua vizuri hususani madam Mery aliye kuwa mwalimu wa Eddy tangu akiwa kijana mdogo.
“EDDY………”
Shamsa aliita huku akiwa bado hayaamini macho yake, mwili mzima Shamsa akahisi unamuishia nguvu. Taratibu Shamsa akajikuta akianguka kwenda chini, kabla hajafika chini Eddy akamdaka, Shamsa akazimia.

“Shamsa, Shamsa, Shamsaa”
Eddy alimuita Shamsa ila hakuitika kwa haraka Eddy akamnyanyua Shamsa na kumuweka begani mwake na kuanza kutoka kushuka kwenye jengo hilo huku Madam Mery na Sa Yoo wakifwata kwa nyuma wote wakionekana kuchanganyikikwa. Wakafika chini Eddy akataka kupanda pikipiki yake, ila Sa Yoo akamuomba watumie gari ambalo walikuja nalo.

“Lete funguo”
Eddy alizungumza mara baada ya kumuingiza Shamsa ndani ya gari, Sa Yoo akamkabidhi Eddy funguo na wote wakaingia kwenye gari, wakaondoka eneo hilo. Hapalukwa na mtu aliye weza kuzungumza kitu cha aina yoyote, kila mmoja alimfikiria Shamsa aliye laza kichwa mapajani mwa Madam Mery huku Sa Yoo akiwa siti ya mbele mara kwa mara aligeuka nyuma kuwez akumuangalia Shamsa.

“Unaelekea wapi?”
Sa Yoo aliuliza baada ya kuona wanaelekea nje ya mji. Eddy hakujibu kitu chochote zaidi ya kuongeza mwendo kasi wa gari hadi wakafika kwenye msitu mmoja mkubwa. Eddy akakunja kushoto kwenye barabara ndogo iliyo jaa nyasi nyingi. Akaongeza mwendo kasi hadi wakafanikiwa kufika kwenye pango kubwa, ambapo Eddy kwa haraka akshuka kwenye gari na kumtoa Shamsa, akambeba begani, Madam Mery na Sa Yoo wakamfwata kwa nyuma pasipo kuuliza ni wapi wanapo ingizwa.

Madam Mery na Sa Yoo wakaonekana kushangaa mazingira ya ndani ya pango hilo lililo jengwa kwa ndani vizuri na kuna taa nyingi ambazo zinapendezesha mandhari ya ndnai ya pango hilo.
Eddy akamlaza Shamsa kwenye moja ya sofa, lililopo sebleni. Akamfungua kifungo cha suruali yake kisha akamvua tisheti aliyo vaa akabakiwa na sidiria.
“Mpeni muda wa kupumzika amepoteza fahamu huyo”
Eddy alizungumza huku jasho likimwagika usoni mwake, akashusha punzi na kuanza kuwatazama Madam Mery pamoja na Sa Yoo binti aliye msaidia kipindi anatafutwa na askari wa hapa nchini Japan.
“Kweli wewe ndio Black Shadow?”
Sa Yoo aliuliza huku macho yake akiwa amemtumbulia Eddy.
“Ndio mimi”

Eddy akamtazama Madam Mery ambaye anaonekana anajambo ambalo anahitaji kuzungumza ila anashindwa kulizungumza kwa wakati huo kutokana na uwepo wa Sa Yoo. Eddy baada ya kuligundua hilo akaanza kutembea kuelekea nje na Madam Mery akamfwata kwa nyuma.
“Umefikaje huku?”
Eddy alimuuliza Madam Mery kwa sauti nzito iliyo jaa hasira ndani yake, kwa maana kumbukumbu ya chanzo cha mtu aliye haribu maisha yake, ikamjia Eddy kichwani na Madam Mery ndio muhusika mkuu wa maisha ya Eddy kuharibika wakishirikiana na Mzee Godwin.

Taratibu Madam Mery akapiga magoti chini, huku machozi yakimwagika, kwani anamuelewa Eddy vizuri na anatambua hali aliyo kuwa nayo kwa sasa ni hali ya hasira na endapo atazungumza jambo baya basi maisha yake yapo hatarini kuondoka.
“Eddy, ninahaki ya kufa mikononi mwako, nipo tayari hata sasa hivi maisha yangu yatoke, ila nina kitu kimoja ninahitaji kuzungumza na wewe kabla hujaniua”

Madam mery alizungumza kwa sauti ya unyonge, machozi yakiendelea kumwagika usoni mwake. Kitendo cha sauti ya Madam Mery kupenya masikioni mwa Eddy kikazidisha hasira yake na kujikuta akikunja ngumi, mkono wa kulia huku mmkono wa kushoto ukimtetemeka sana.
“Sinto hitaji kusikia kitu chochote kutoka kwako, niliyaacha maisha yako kwa mara ya kwanza kwa kuheshimu msiba wa mke wangu, mwanangu na mama yangu. Ila kwa sasa nitakuua kisha atafwata Godwin”

Eddy alizungumza huku akimgeukia Madam Mery aliyepiga magoti pembeni yake. Akatamani alichomoe koo la Madam Mery kwa mkono wake wa kushoto unao tetemeka kwa hasira, ila akajikuta mkono huo ukiwa ni mzito sana kufanya jambo hilo. Madam Mery akatulia kimya, huku macho yake ameyafumba kwani anatambua ni nini anacho stahili kufanyiwa. Zikapita sekunde kadhaa za ukimya, Madam Mery akayafumbua macho yake na kumuona Eddy akiwa anaondoka kuingia ndani ya pango hilo na hajamfanya kitu chochote.
“Eddy tunatakliwa kumuua Godwin”

Eddy akasimama, kisha akageuka taratibu na kumtazama Madam Mery aliye piga magoti. Macho ya Eddy yaliyo jaa uwekundu wa hasira huku kwa mbali yakilengwa lengwa na machozi ya hasira, yakaanza kumpandisha na kumshusha madam Mery. Kisha sauti mbili moyoni mwake zikawa zinabishana kwenye kufanya maamuzi. Sauti yake ya kwanza inamtuma kumuua madam Mery muda huo huo, huku sauti yake ya piliikimuomba asifanye mauaji ya mwana mama huyo na amsikilize kwa kile ambacho Madam Mery anahitaji kumuambia.
“Tanzania pamoja na raisi Praygod wapo matatani, muda wowote na saa yoyote wanaweza kupoteza maisha……”
“Kutokana Godwin amekuwa……….Raisi wa nchini Tanzania”
“NINI…..?”
Eddy alistuka sana kusikia habari hiyo ambayo ni mbaya sana ndani ya masikio yake. Akamfwata Madam Mery kwa kasi hadi sehemu alipo piga magoti, jambo lililo mfanya madam Mery ajikute amekaa chini kutokana na kumuogopa Eddy.

“Umesemaje………..?”
“Ni…nini….memee..eeesema baa…ba yak…o Go…d……win amekuwa raisi wa Tanzania”
Madam Mery alizungumza huku mwili mzima ukimtetemeka, japo kuna baridi Eddy akajikuta jasho likimwagika kwa hasira. Kila alicho kifikiria juu ya Mzee Godwin kilimchanganya akilini mwake.
“Na Phid….aya bado yupo hai”
Maneno ya Madam Mery yakazidi kumumshangaza Eddy akilini mwake na kuanza kumkumbuka Nesi Phidaya ambaye alimfananisha na mke wake ila kitu kilicho mchanganya ni kwamba tayari alisha mzika mkewe Phidaya.
                                                                                                            ***
    Matajario mazuri ya watanzania juu ya uongozi wa Raisi Godwin, yakaanza kupotea kadri siku zilivyo zidi kwenda. WWengi walitarajia ugumu wa maisha utapungua ila ndio kwanza ukazidi kuongezeka mara kumi ya awali walivyo kuwa.

Nchi haikuwa ya watanzania wote bali, ikageuka kuwa nchi ya watanzania wachache, wenye nguvu ya kipesa na wenye maamuzi ya kufanya chochote kwa wakati wowote na kwamtu yoyote. Uonevu ukazidi kuongezeka kwa wananchi wa hali za chini, watu wote walio msaidia mzee Godwin kuingia madarakani, walikabidhiwa madaraka makubwa ambayo, hata watu wengine walio kua katika serikali ya raisi Praygod na kumuunga mkono, waliweza kupigwa chini, huku baadhi yao wakibambikiwa kesi na kusekwa magerezani, huku wengine wakifilisiwa na kubaki kuwa masikini kabisaa.

“Mzee tunatakiwa kidogo tuwajali wananchi, hata miaka mingine mitano ukigombania uraisi wakupatie kura zao”
Mshauri wa raisi wa Mzee Godwin, alizungumza huku akimtazama raisi Godwin usoni mwake. Mzee Godwin akatabasamu kidogo kisha akaachia kicheko cha dharau na kumtazama mshauri wake bwala Mgwira
“Ni nani aliye kudanganya kwamba kutakuwa na kupiga kura tena nchini Tanzania?”

“Una maana gani muheshimiwa?”
“Maana yangu ni kwamba hakuna mtu ambaye atanitoa madarakani kwa kupiga kura. Hii nchi kwa sasa ni yangu na nitaiongoza hadi pale nitakapo fariki na endapo itatokea nitakufa basi atakaye tawala atakuwa ni Manka mwanangu kipenzi”
Bwana Mgwira akabaki amemtumbulia macho mzee Godwin, anaye zungumza kwa kujiamini sana.
“Nahitaji nchi hii nibadilishe mfumo wa utawala, uwe utawala wa kifalme na si utawala wa kiraisi”
“Muheshimiwa……………..!!!”
“Ndio, na tena wasiliana na viongozi wote kesho ninahitaji kufanya nao mkutano sawa”

“Sawa muheshimiwa”
Mzee Mgwira hakuwa na kitu cha kuzungumza zaidi ya kukubaliana na raisi Praygod ambaye siku zote akizungumza haitaji mtu yoyote aweze kukipinga. Manka akaingia kwenye sebule ya baba yake na kumkuta akiwa amekaa na Mzee Mgwira, ambaye baada ya kumuona Manka akanyanyuka na kuondoka, kuwapisha baba na mwana kuzungumza.
“Baba mbona unaonekana leo una furaha sana?”
“Ninafuraha mwanangu kwa maana nimefikiria kitu ambacho nina imani kitakuweka wewe kwenye mazingira mazuri sana”
“Kitu gani hicho baba, wakati unamiliki kila kitu kwa sasa?”
“Ninakwenda kubadilisha mfumo wa serikali kutoka katika mfumo wa serikali ya uraisi na kuingia katika serikali ya ufalme”

Mzee Godwin alizungumza huku akifurahia sana.
“Ufalme, ufalme wa aina gani?”
“Nahitaji kuwa mfalme, nitakuwa nikiongoza katika maisha yangu yote na hata mimi nikifa basi wewe mwanangu utatawala katika kiti cha ufalme na utakuwa ni malkia”
Manka naye aklajikuta akitabasamu na kufurahi sana, juu ya wazo ambalo baba yake amelifikiria. Kwa nguvu walio kuwa nayo walijiamini kwamba kila kitu ndani ya Tanzania ni chakwao.
“Wezako wanaendeleaje?”
“Wapo salama tu, kila mtu anaendelea na majukumu yake kwenye wizara ambayo umewapatia”

“Basi wasiliana nao na kesho uwaambie kwamba nina kikao ambacho kitakuwa kinakwenda kuihalalisha serikali ninayo ifikiria”
“Sawa baba”
Manka akanyanyuka kwenye sofa alilo kalia akamsogelea baba yake na kumbusu shavuni na kuondoka zake sebleni na kumuacha Mzee Godwin akifikiria mambo yake.
   Siku iliyo fwata, mkutano wa viongozi wote ndani ya serikali ya Mzee Godwin wakakutana kwenye kikoa ambacho kila mmoja alishangazwa na ukubwa wa kikao hicho kwa maana tangu uongozi wa raisi Godwin uanze hajawahi kuitisha kikao kikubwa kama hicho.

“Habari za asubu”
Raisi Godwin alizungumza kupitia kipaza sauti kilichopo kwenye meza yake, kila kiongozi aliye kuwepo kwenye eneo hilo aliitikia. Raisi Godwin akawatizama viongozi walio chini yake kisha akakohoa kidogo na kuanza kuzungumza kitu ambacho alikusudia kukizungumza.
“Ninahitaji kubadilisha mfumo wa serikali”
“Serikali ambayo ninahitaji iwe kwa sasa, itakuwa ni serikali ya ufalme, na hili swala sinto hitaji mtu wa iana yoyote kuweza kulipinga hili”

Minong’ono ya chini chini ikaanza kutawala ndani ya chumba cha mkutano, kila mmoja aliweza kuzungumza chake juu ya kitu kilicho zungumza na Raisi Godwin.
“Kuna baadhi ya sekta nitazifuta rasmi kuanzia leo na sekta ya kwanza itakuwa ni Tume ya taifa ya uchaguzi”
“Eheee bwana Luka unahitaji kuzungumza nini?”
“Muheshimiwa raisi wazo lako ulilo litoa si baya, ila itakuwaje kwa hao wananchi ambao tuna waongoza, watakubaliana kweli na hili?”

“Jeshi tunalo, nguvu ya pesa tunayo ni nani anayewezakupinga kauli yangu?”
Raisi Godwin alizungumza na kuwafanya viongozi wote kuwa kimya wasizungumze neno la aina yoyote.
“Ninaagiza waziri wa mawasiliano, vijulishe vyombo vya habari namuwatangazie juu ya hili nililo zungumza sawa”
“Sawa mkuu”
“Na kitu cha mwisho ambacho labda nitawahurumia wananchi wangu, waweze ku[iga kura za ndio na hapana kupitisha serikali ninayo itaka na watakao kataa. NITAJUA NI NINI CHAKUFANYA”


Jinsi Kitambi Kinavyopatikana na Jinsi Kinavyoondolewa na Dawa ya Mkataa Kitambi

$
0
0

Kitambi  ni  ile  hali  ya  tumbo  kuwa kubwa  na  kuchomoza  kwa  mbele  na  wakati mwingine  kufikia  hatua  ya  kunin’ginia.
JINSI  KITAMBI  KINAVYO  PATIKANA
Kwa  mujibu  wa  tafiti  mbalimbali  za  kitaalamu, mwili wa binadamu una seli kati  ya bilioni 50  hadi 200 za mafuta zilizogawanyika katika  sehemu  mbalimbali  za  mwili wa binadamu.

 Kwa wanawake  seli hizo  zipo sana katika maeneo ya matiti, kwenye  nyonga, kiunoni na kwenye makalio.

Kwa upande  wa  wanaume seli  hizo zinapatikana  sana kwenye kifua, tumboni na kwenye makalio pia.

Mafuta ya tumbo yanayofanya kitambi hukusanywa kwa njia kuu mbili:

i.Njia  ya kwanza ni mafuta kutoka kwenye tishu zilizo chini ya ngozi

ii.Na  njia  ya pili ni kutoka kwenye ogani za ndani kama moyo, kongosho n.k

SABABU ZA KUPATA KITAMBI
Sababu kubwa ya kitambi ni kukosekana ulingano wa nguvu(kalori) katika  mwili  wa  mwanadamu, hali  inayo  sababishwa  na  mtu  kula vyakula vinavyotia nguvu sana kuliko jinsi anavyoweza kutumia na kutoa kama taka mwili.

VYAKULA  VINAVYO  CHANGIA KULETA  KITAMBI

Vyakula vinavyochangia  kuleta  kitambi ni  pamoja  na :
i.Vyakula  vyenye  mafuta  mengi  kama  vile  nyama nyekundu  (iwe ni ya kuchemsha, kukaanga au kuchoma), nyama  ya  kuku  wa  kizungu  ( iwe  ya  kuchemsha, kukaanga  ama  kuchoma ), mafuta ya kupikia, (hasa yale yatokanayo na bidhaa za wanyama, kama siagi, na jibini), viazi ya kukaanga kwa  mafuta  (chips) pamoja  na  pizza.

ii.Vyakula vyenye wanga mwingi kama  vile ugali wa mahindi, mihogo, wali, mkate  mweupe.

iii. Vyakula  na  vinywaji  vyenye  sukari  nyingi  iliyo  ongezwa( added  sugar ), kama  vile  soda  na  keki.

iv. Vyakula  vilivyo  tengenezwa  kwa  ngano  na  sukari kama  vile  keki, skonzi, chapatti, maandazi, mkate  mweupe  nakadhalika

v. Pamoja  na  vinywaji  vilivyo  tengenezwa  kwa  kutumia  ngano  kama  vile  bia  za  aina  mbalimbali  na  kadhalika.

Vyakula  vilivyo  tajwa  hapo  juu, vikitumiwa  bila  kuzingatia  kanuni  za  mlo  kamili, huchangia  kuleta  tatizo  la  kitambi.

vi. Sababu nyingine ni  kutofanya  mazoezi  ya  mwili  na  viungo(  physical  exercises  )  kwa  muda  mrefu.

JINSI YA KUJUA KAMA UNA KITAMBI
Kitambi kinaweza kuonekana kirahisi kwa macho. Ila kujua ni kwa kiwango gani kitambi chako kipo inabidi kufanya vipimo vya kiuno(waist) na nyonga (hips).

Mzingo wa kiuno ukiwa >102 cm au 40  kwa wanaume na >88 cm au 35  kwa wanawake, na uwiano wa kiuno na hips(Waist-Hip Ratio) ikiwa >0.9 kwa wanaume na >0.85 kwa wanawake.

BMI ya 30 au zaidi inaashiria 'Obese' uzito kuzidi kiasi. Kuwa na mzingo uliozidi kawaida ni kiashiria hatari cha matatizo ya kimetaboliki, kuliko hata cha BMI.

Kipimo kingine cha kitambi ambacho kimeonyesha uwezo zaidi kuliko BMI katika kutabiri uwezekano mkubwa wa magonjwa ya moyo ni Index Of Central Obesity(Waist-To-Height Ratio-WHtR) ambapo uwiano ukiwa sawa na 0.5 au zaidi, hii ikimaanisha mzingo wa kiuno angalau ni nusu ya kimo cha mtu.

Kipimo kingine ni Body Volume Index, kinachopima kitambi kwa kupima umbo la mtu na mgawanyo wa uzito wake.

MAMBO  YANAYO  MUWEKA  MTU  KATIKA  HATARI  YA  KUPATWA  NA  KITAMBI
Tumekwisha  ona  hapo  juu jinsi  kitambi  kinavyo  patikana  na  vyakula  pamoja  na  sababu  nyinginezo  zinazo  sababisha  kutokea  kwa  kitambi, sasa  tutazame  mambo  yatakayo  kufanya  uwe  katika  hatari  ya  kupatwa  na  kitambi.

Kwa  mujibu  wa  tafiti  mbalimbali  za kitaalamu, mambo  yafuatayo  huwaweka  watu  katika  hatari  kubwa   ya  kupatwa  na  kitambi :

1. Ulaji  mbovu  wa  chakula; Ulaji  mbovu  wa  chakula  ni  ulaji  usio  zingatia  kanuni  za  mlo  kamili. Hapa  mtu  hufululiza  kutumia  chakula  cha  aina  fulani  pekee  bila  kuzingatia  aina  nyinginezo  za  chakula.  Mfano; mtu  anaweza  kuwa  anakula  mlo  ufuatao :

Asubuhi :  Mchemsho  ama    supu  ya  ng’ombe , chapatti  tatu  na  soda  moja.  Mchana :   Ugali  nyama  choma anashushia  kwa  maji  na  soda.

Jioni :  Mchemsho  wa  kuku  na  bia  mbili  nakuendelea.

Usiku  :  Chips  mayai  au  chips  kuku  au  chips  mishikaki  na  bia.

Mtu  huyu  akiendelea  na  utaratibu  huu  kwa  muda  mrefu, ni  lazima  atapatwa  na  kitambi.

2. Ulaji  mfululizo  wa  vyakula  vyenye  mafuta  mengi

3. Ulaji  mfululizo  wa  vyakula  vyenye wanga  mwingi  

4.Ulaji  mfululizo  wa  vyakula  vyenye  sukari  iliyo  ongezwa ( added  sugar  ).

5.Ulaji  mfululizo  wa  vyakula  vya  ngano.

6.Ulaji  mfululizo  wa   vinywaji  vyenye ngano  na  sukari.

7.Kutofanya  mazoezi  ya  mwili  na viungo  ( physical  exercises  ).

Mhusika  anapokuwa  katika  makundi  yote  yali yotajwa  hapo  juu, hali  huwa  mbaya  zaidi. 

NJIA ZA KUONDOA KITAMBI
Kuwa  na  kitambi  ni  lugha  ya  mwili  ( body-language )  inayo  leta  ujumbe  kwako  kwamba  “ Mwili    wako  haupo  salama  tena “

Kama  una  kitambi   maana  yake  una  mafuta  yasiyo  hitajika  mwilini, mwili  wako  unatumika  kuhifadhi  mafuta  usiyo  yahitaji.

Hali  hii  kitabibu  imaanisha  kwamba, ogani  nyinginezo  zilizomo  ndani  ya  mwili  wako  zinao gelea  kwenye  mafuta( fats  )  yasihotika  yaliyomo ndani  ya  mwili  wako,  jambo  linalo  kuweka  katika  hatari  kubwa  sana  ya  kushambuliwa  na  magonjwa  hatari  kama  vile  shinikizo  kubwa  la  damu, kiharusi  na kisukari  na  kwa kutaja  machache.

Hivyo  basi  ili  kuondokana  na  hatari  hiyo, yakupasa   kupambana  kuondoa  hayo  mafuta  yasiyo  hitajika  mwilini  mwako.

NJIA  ZA  KUONDOA  KITAMBI.
Unaweza  kuondokana  na  kitambi  kwa  kufanya  diet  pamoja  na  mazoezi ya  mwili  na  viungo.

Vilevile  unaweza  kuondoa  kitambi  na  kupunguza  mafuta  mwilini  kwa  kutumia  dawa  asilia  ya  kuondoa  kitambi  na  kuondoa  mafuta  yasiyo  hitajika  mwilini.

DAWA   ASILIA  YA  KUONDOA  KIAMBI  NA  MAFUTA  MWILINI.
Hii  ni  njia  ya  uhakika  kabisa  ya  kuondoa  tatizo  la  kitambi  pamoja  na  mafuta  yasiyo  hitajika  mwilini.

 Unaweza  kuondoa  tatizo  la  kitambi  pamoja  na  kupunguza  mafuta  mwilini  kwa  kutumia  DAWA  ASILIA   IITWAYO YA  MKATAA  KITAMBI.

 Dawa   hii  ni  ya asili  kabisa
“  Pure  Herbal “, ambayo  haijachanganywa  na  kemikali  yoyote, haina  side  effect kwa  mtumiaji  na  inaondoa  kabisa  tatizo  la  kitambi  ndani  ya  siku  kumi  na  nne.

JINSI  DAWA  YA  MKATAA  KITAMBI  INAVYO  FANYA  KAZI.
1.Huyeyusha  mafuta  yasiyo  hitajika  mwilini.

2.Husaidia  kupunguza  hamu  ya  chakula.

3.Inazuia  kutengenezwa  kwa  seli  za  mafuta  ( fat cells  ) katika  mwili  wa  mwanadamu. Unapokula  chakula  chenye  mafuta  mengi, dawa  hii asilia  hupambana  kuyafanya  mafuta  hayo  yasitengeneze  seli  za  mafuta  mwilini  mwako. Hali  hii  huuepusha  mwili  wako  kuhifadhi  mafuta   yasiyo  hitajika  mwilini.

4. Husaidia  kupunguza  uzito wa mwili  kwa  haraka  sana  endapo  itatumika  pamoja  na  diet  ya  kabechi.

UFANISI  WA  DAWA.
Ufanisi  wa  dawa  hii  ni  wa  asilimia  mia  moja. Dozi  ya  dawa  hii  hutumika  kwa  muda  wa  siki  ishirini  na  moja.

MATOKEO  YA  DAWA:
Dawa  hii  huondoa  kabisa  kitambi  ndani  ya  siku  kumi  na  nne.

BEI  YA  DAWA :
Dawa  hii  inaoatikana  kwa  kiasi  cha  SHILINGI  ELFU  HAMSINI  TU  (Tshs. 50,000/=)

MAHALI  TUNAPO  PATIKANA.
Tunapatikana  jijini  DAR  ES  SALAAM, katika  eneo  la  UBUNGO  karibu  na  SHULE  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING  nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA.

KWA  WATEJA  WASIO  WEZA  KUFIKA  OFISINI  KWETU.
Kwa  wateja  wasio  weza  kufika  ofisini  kwetu  Tabata, tunao  utaratibu  wa  kuwafikishia  dawa  mahali  popote  walipo  ndani  ya  jiji  la  Dar  Es  salaam.

KWA  WATEJA  WA  NJE  YA  DAR  ES  SALAAM.
Kwa  wateja  waliopo  nje  ya  Dar  Es  salaam, tunawatumia  dawa  kwa  njia  ya  MABASI.

Kwa  wateja  wa  ZANZIBAR  tunawatumia  dawa  kwa njia  ya  boti.

KWA  WATEJA  WA  NJE  YA  NCHI:
Kwa  wateja  wa  nje  ya  nchi, tunatumia  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  au  DHL.

WASILIANA  NASI  KWA  SIMU  NAMBA : 0766  53 83 84

TUTEMBELEE:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya June 5

Makamu wa Rais: Wasiopeleka michango ya wanachama kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii wachukuliwe hatua

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan amewaagiza waajira wasiopeleka au kuchelewesha michango ya wanachama kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii nchini wachukuliwe hatua za kisheria ili kukomesha tabia hiyo.

Makamu wa Rais ametoa kauli hiyo 3-June-2017 Jijini Mwanza wakati anafungua semina ya maisha baada ya kustaafu,fursa ya mafao,uwekezaji iliyoandaliwa na Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF) kwa ajili ya wastaafu watarajiwa 450 kutoka wilaya zote za mkoa wa Mwanza.

Makamu wa Rais alisisitiza kuwa waajiri wakichangia kwa mujibu wa sheria kwenye mifuko hiyo watawezesha wanachama wao kupata mafao kikamilifu na kwa wakati.

Kuhusu madeni ya Serikali kwa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii nchini, Makamu wa Rais aliwahakikishia Wakurugenzi wa mifuko hiyo kuwa Serikali inashughulikia madeni hayo na baada ya kukamilika kwa zoezi la uhakiki wa madeni hayo basi malipo yatafanyika haraka iwezekanavyo.

Makamu wa Rais alisisitiza kuwa Serikali itaendelea kuhakikisha michango ya pensheni kwa wafanyakazi wa taasisi zinazopata ruzuku kutoka Serikalini inalipwa kwenye mifuko hiyo kwa wakati.

Aidha, Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan aliwahimiza wastaafu watarajiwa kote nchini waache tabia ya kukata tamaa baada ya kustaafu bali wajipange vyema na kuwekeza katika miradi mbalimbali ya kiuchumi ikiwemo viwanda vidogo, kilimo na biashara.

Alisema kuwa kama wastaafu hao watawekeza katika maeneo hayo watatoa ajira kubwa kwa vijana badala ya kutumia mafao yao kwenye matumizi yasiyo ya lazima.

“Wazee ni rasilimali na hazina kubwa kwa taifa kama waswahili wasemavyo panapo wazee hapaharibiki jambo hivyo basi ni matumaini yangu kuwa mfuko wa PSPF mtaendelea kufanya kazi kwa bidii na kwa uadilifu kuhakikisha kuwa hazina hii ya wazee wetu wanapata haki zao kwa mujihu wa sheria za nchi pale wanapohitaji huduma toka kwenu.”Alisisitiza Makamu wa Rais.

Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan alionya wastaafu hao watarajiwa kupunguza matumizi yasiyo ya lazima bali watumie fedha watakazopata katika shughuli za kiuchumi kwa ajili ya maslahi yao ya baadaye.

Makamu wa Rais pia alipongeza jitihada zinazofanywa na mfuko wa PSPF kwa kutoa mafunzo kwa wastaafu watarajiwa kwa ajili ya kuwasaidia kujipanga vyema pindi watakapostaafu utumishi wao.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dkt Ashatu Kijaji aliwahakikishia wastaafu hao watarajiwa kuwa wa mkoa wa Mwanza kuwa Serikali itaendelea kusimamia vyema mifuko ya hifadhi ya jamii ili iweze kutoa mafao bora na kwa wakati.

Dkt Ashatu Kijaji pia alihimiza wastaafu hao watarajiwa kutumia vizuri mafao wanayopata kwa ajili ya maisha yao ya baadaye.

Live: Yanayojiri Bungeni Dodoma leo Juni 5, 2017

$
0
0
Fuatilia hapa matangazo ya moja kwa moja ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yanayoendelea Mjini Dodoma leo Juni 5, 2017. 

Bofya hapa kutazama

Ally Kessy: Waliosaini Mikataba Mibovu ya Madini Wanyongwe

$
0
0
Mbunge wa Nkasi (CCM), Ally Kessy amefunguka na kusema watu waliohusika kusaini mikataba mibovu ya madini wanatakiwa kunyongwa kwani nchi ikitapoteza watu ishirini au thelathini hakuna hasara yoyote.

Mbunge Kessy anasema kama watu hao waliotia saini ya mikataba ya madini mwaka 1998 watakamatwa na mali zao kunyang'anywa na wakanyongwa itakuwa ni fundisho kubwa kwa watu wengine na baadhi ya wabunge wengine waliunga mkono hoja hiyo huku wakitaka mikataba hiyo ya madini iweze kupitiwa upya.

"Wakamatwe wote waliohusika na mikataba mibovu na kusababisha kuingizia serikali hasara, ikiwezekana wanyongwe hata ishirini au thelathini maana nchi hii wanazaliwa watu Muhimbili zaidi ya mia moja kwa siku, Bungando wanazaliwa mpaka Namanyele wanazaliwa kwa hiyo tukipoteza watu mia moja au mia mbili Mh. Spika hakuna kitu kitakachopotea katika nchi hii, tumeonewa vya kutosha haiwezekani" alisisitiza Ally Kessy na kuongeza;

"Mnasema mnarekebisha mikataba, mikataba kurekebisha ni kutafuta hao wote waliosaini wakamatwe, wanyang'anywe mali zao, wanyongwe tutabaki salama katika hii nchi, itakuwa mfano, nataka comment ya serikali kusikia kuwa tutashughulikia wote waliotia saini mikataba ya madini 1998 wakamatwe mara moja" alisema Kessy
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images