Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Jinsi Wachawi Wanavyo Tumia Miti Ya Kwenye Kitanda Cha Sokwe Mtu Katika Kutengeneza Na Kutuma Uchawi Hatari Wa Kuwafilisi Watu .

$
0
0
Na. DOKTA  MUNGWA  KABILI……..0744  000  473
Haya  ni  maelezo  yanayo patikana  ndani  ya  kitabu  “ Kitanda  Cha  Sokwe  Mtu “


Lugwisha  aliletwa  kwangu  saa  nne  kamili  za  asubuhi  na  nikaanza  kumshughulikia  saa  saba  kamili  mchana.

 Zoezi  la  kwanza  lilikuwa  kupima  aina  na  kiwango  cha  uchawi  alicholishwa.

Zipo  njia  mbalimbali  za  kumpima  mtu  ili  kujua  kiwango  na  aina  ya  uchawi  aio  lishwa,  Njia  moja  wapo  ni  kulishwa  dawa  maalumu  ya  kutapisha  uchawi  au  kuumfanya  aharishe  uchawi  husika. 

 Njia  za  kutapisha  pia  zipo  za  aina  mbili, aina  ya  kwanza  ni  kutapisha  uchawi  kwa  njia  ya  kawaida  na  aina  ya  pili  ni  kutapisha  kupitia  nyongo.

Sasa  basi  kwenye  kutapisha  uchawi, huwa  kuna  mti  mmoja wa  porini  hatari  sana  katika  kutapisha  uchawi. Mti  huu  huwa  unatapisha  uchawi  wa  aina  yoyote  ile.

Ni moja kati  ya miti  iliyo  katika  daraja  la juu kabisa  katika  miti  ya  uganga. Mti  huu  una  maruhani  na  majini  wakali  zaidi  ya  mia  tatu.

Mti  huu  unapatikana  porini.  Unataka  kuujua  ni  mti  gani ?  Soma  maelezo  yafuatayo;

Porini  huwa  kuna  ndege  mmoja  mwenye  maajabu  makubwa  sana. Ndege  huyu  ana tumbo  la  rangi  nyekundu  au  rangi ya  pinki. Kichwa  chake  huwa kina rangi sawa  sawa  na  rangi  ya  tumboni  na  mgongo  wake  huwa  na  rangi  nyeusi  ambayo  hutapakaa  hadi  kwenye  mkia  wake.

 Ndege  huyu  ana  sifa  moja  kubwa  na  ya  kipekee.  Ni  kwamba, chochote  utakacho  mfanyia  kiwe  kibaya  au  kizuri, basi  kitarudia  wewe   mwenyewe . Kwa  mfano  ukimtoboa  jicho, basi  na  wewe  hazitapita  siku  saba  utatobolewa  jicho.

Ukimkata  mguu, na  wewe  ndani  ya  siku  saba  uta katwa  mguu  nakadhalika.

Kiota  chake  kina  maajabu  yanayo  fanana  na  ndege  mwingine  wa  porini  aitwae  fundi  chuma.

Ni  kwamba  uki haribu  kiota  chake, kama  una  nyumba  basi  nyumba  yao  nayo  itaharibiwa  eidha  kwa  mafuriko, kimbunga, moto  au  chochote  kile.

Na  kama  haujawahi  kujenga  basi  ndio  hautajenga katika  maisha  yao  yote.

Huyu  ndege  huwa  anakula  matunda  ya  kwenye  mti  mmoja  tu. Huu  mti  nao una majini  wengi   wabaya  kwa  wazuri.

Wachawi  huwa  wana  utumia  mti  huu  kwa  mambo mengi  sana, moja  wapo  ni  kumtupia  mtu  mkuli  wa  paka  kwa  lengo  la  kumtengeneza  awe  banda  la  kufugia  mapepo  wachafu.

Jinsi  wanavyo  fanya, mchawi  anatafuta  paka  mweusi. Paka  huyu  mweusi  lazima  akutane  nae  usiku  wa  kuanzia  saa  sita  na  awe  amekutana  nae  kwa  bahati  mbaya, asipange  kukutana  nae, vinginevyo  amuite  paka  huyu  kwa  kutumia  uchawi.

Paka  huyu  akisha patikana  huchukuliwa  na  kupelekwa  hadi  kwenye  mti  huu, na  kuchinjwa kisha  damu  yake  kumwagwa  kwenye  mti  huo  kwa  tambiko  maalumu.

Baada  ya  hapo    matawi  matatu  yatachukuliwa  kutoka  kwenye  mti  huo, kisha  mchawi  atakwenda  nao  mpaka  kaburini.

Akifika  kaburini anaenda  kuamsha  mkuli  wa  kwenye  kaburi  husika na  kuunganisha  na  mkuli  wa  paka  aliyetolewa  kafara  kisha  vyote  kwa  pamoja  vinaunganishwa  na  majini  ya  huo  mti  na  kutumwa  kwa  mtu  aiyekusudiwa  kwa  lengo  la  kumtupia  ugonjwa  wa  kumfanya  awe  analia  kama  paka  na  kujikuna  kama  paka.

Sasa  basi  mizizi  ya  mti  huu  ndio  kiungo  kikuu  kinacho  tumika  katika  kumtapisha  mtu  uchawi  kwa  lengo  la  kugundua  kiwango  cha  uchawi  na  aina  ya  uchawi  alio tupiwa.

Mtu aisha  lishwa  dawa  hii  atatapika  ama  kuharisha  uchawi  wote  alio  lishwa, muchaw  huu  utachukuliwa  na  kwenda  kuchomwa  njia  panda  kwa kutumia  miti  maalumu.

Katika  zoezi  la  kuchoma  uchawi  huu  kwa  kutumia  miti  hiyo  maalumu  ndipo  itajulikana  aina  ya  uchawi alio  tupiwa  mtu.

Kwa  kutumia   njia  ya  kuteketeza  uchawi  huu  kwa  kutumia  miti  maalumu  unaweza  kugundua  aina  ya  uchawi  ulio  tumika  na  kijiji  ulipo  tumiwa.

Katika   ulimwengu   wa   wachawi  kila  kijiji  kina  kazi yake.

Mfano  mchawi   anapotaka  kumwambia  mwenzake  anataka  kuzungumzia  uchawi  wa aina  Fulani, badala  ya  kutaja  uchawi  huo,  yeye  atataja  jina  la  kijiji  kinacho  husiana  na  uchawi  huo  na  moja  kwa  moja  mchawi  mwenzake  ataelewa  anamaanisha  nini.

Sasa  basi  baada  ya zoezi  la  kuteketeza  kwa  moto  maalumu  uchawi  alio tumiwa  kijana  Lugwisha,  niligundua  kuwa  ametupiwa  uchawi   kutoka  kijiji  kimoja  cha  wilaya  ya  Rufiji  na  mwingine  umetumwa  kutoka  kwenye  kijiji  kimoja  cha  wilaya  ya  Kasulu  mkoani  kibondo.

Uchawi  alio  tumiwa  kutoka  Rufiji  ni  aina  ya  uchawi  ambao  hujulikana  kama  Sunkwa.

Asili  ya  ya  uchawi  huu  ni  kijiji  kimoja  cha  wilaya  ya  Handeni  mkoa  wa  Tanga.

Sunkwa  ni  uchawi ambao  lengo  lake  ni  kumfukuza  mtu kwa kutumia  uchawi na  kumfunga  asirudi  tena  katika  eneo  alilo  fukuzwa.

Zipo  njia  nyingi  sana  ambazo  wachawi  huzitumia  kutengeneza  uchawi  wa  sunkwa  na  kuutuma  kwa  watu walio wakusudia.

Katika  kitabu  hiki  nitaelezea  njia  moja wapo. Njia  hii ndio  ambayo   imetumika  dhidi  ya  Lugwisha .

Jinsi  uchawi  wa  sunkwa  unavyo  fanyika; Kwanza  inachukuliwa  miti  saba  ambayo  hutumiwa  na  sokwe  kutengeneza  kitanda .

  Miti  hii  lazima  ichukuliwe  katika  maeneo  tofauti  tofauti  saba  na  huchukuliwa  kwa  tambiko  maalumu.

Porini  sokwe  mtu  huwa  na  vitanda  vyao. Hutengeneza  vitanda  vyao  kwa  kutumia  miti  mbalimbali.  

Kuhusu  vitanda  vya  sokwe  mtu  huwa  kuna  sifa  moja  kuu  nayo  ni  kwamba, sokwe  mtu  huwa  hawezi  kutengeneza  kitanda  cha  kudumu  na  wala  hawezi  kukaa  sehemu  moja  kwa  muda  mrefu.

Sokwe  mtu  anapotengeneza  kitanda  chake  huwa  anakaa  kwa  muda  mfupi  sana  na  baada  ya  hapo  huhama  katika  eneo  hilo  na  kuhamia  sehemu  nyingine  ambako  nako  huko  ataenda  kutengeneza  kitanda  kingine.  Hali  hii  huwa  hivi  katika  maisha  yote  ya  sokwe  mtu.

Sasa  basi,  miti  inayo  tumika  kutengeneza  kitanda  cha  sokwe  mtu , pamoja  na  kazi  nyinginezo,  huwa  pia  inachukuliwa  na  kutumika  katika  kutengeneza   uchawi  wa  kumfukuza  mtu  na  kumfanya  aishi  maisha  ya  kuhamahama  na  kutanga  tanga.

Kinacho  fanyika  huwa  hivi; Kwanza  inachukuliwa  miti  au  fimbo  zilizo  tumika  kutengeneza  kitanda  cha  sokwe  mtu, zinagawanywa  katika  mafungu  mawili, fungu  la  kwanza  linatumika  kutengeneza   kijimtumbwi  kidogo  na  fungu  la pili  linasagwa  pamoja  na  mafuta  ya  usiku.

Baada  ya  hapo  yanachukuliwa  majani  yaliyo peperushwa  na  kimbunga  ambayo  yaidakwa juu  kwa  juu  kabla  hayaja tua  chini, unachukuliwa  mchanga  na  uchafu  wa  kutoka  kwenye  njia  na  barabara  arobaini  zap  kutoka  sehemu  tofauti  tofauti,  mchanga  na  udongo  wa  kutoka  kwenye  mikoa  yote  ya  Tanzania,  anachukuliwa  kimburu; kimburu  ni  paka  aliye  asi nyumbani  na  kwenda  kuishi  porini, huyu  paka  anaunguzwa  kwenye  chungu  cha  kichawi   akiwa  mzima mzima  hadi  anaua  majivu,   kitu  kingine  wanachukuliwa  vibinya  mapumbu  saba  wa  kwenye  mgodo, vibinya  mapumbu  ni  wadudu   mijusi  aina  ya  gomamli  ambao  huishi  kwenye  miti  tu.

Sasa  katika  zoezi  hili  huwa  wanachukuliwa  gomamli  wanao  patikana  kwenye  mti  wa  porini  unaoitwa  mgodo.   Kitu  kingine  kinacho  ongezwa  hapo  ni  mpanzi  bukta  kumi  na  tatu. Hawa  mpanzi  bukta  ni  aina  ya  panzi  wanaoishi  porini.

Vitu  vyote  hivyo  vinasagwa  pamoja  kisha  vinachanganywa  na   dawa  inaitwa  kishinda  wachawi  na  mfalme  wa  pori  halafu  mhusika  anaenda  kuvichoma  njia  panda  pamoja  na  fusho  moja  chafu .

 Fusho  hili  ni  miongoni  mwa  mafusho  machafu  kabisa na  hufanana  na  lami  nyeusi.

Wakati  uchawi  huu  unachomwa  mchomaji  ana  hakikisha  moshi  haueleke  upande  wake.

 Ulozi  huu  unachomwa  kwa  manuizi  maalumu  ya  kumnuia  mkusudiwa  kwanza  ahame  katika  eneo  alilokusudiwa  kuhama  lakini  pili  awe  ni  mtu  wa  kuhamahama  na  kutanga  tanga  katika  kila  sehemu  atakayo  kwenda  katika  siku  zote  za  maisha  yake.

Uchawi  huu  huwa unafanya  kazi  kwa  haraka  sana  na  kinga  yake  ni  ima  uwe  na  zindiko  kali, au  uwe  mcha  Mungu.

Ile miti  iliyo  tumika  kutengenezwa  mtumbi, zinachukuliwa  dawa  zile  zilizounguzwa  pamoja  na  jina, nguo, au  picha  ya  mkusudiwa  na  karatasi  iliyo  andikwa  maneno  maalumu  ya  kilozi, kisha  mtumbw  huo  unaenda  kuwekwa  kwenye mtu  unao tembea   kwa  manuizi  maalumu  ya  kumhamisha  mhusika  na  kumfanya  atange  tange  katika  maisha  yake  yote.

Basi  unaambiwa  mtu  aiyefanyiwa  uchawi  huu  huwa  haichukui  muda  ataondoka  sehemu  aiyo  fukuzwa  kichawi  na  kuiona  kama jehanamu na  anaanza  kuwa  mtu  wa  kuhamahama  na  kutanga  tanga.

Ama  kwa  upande  wa  uchawi  wa  kumfilisi  mtu, huwa  upo  uchawi  wa  aina  nyingi  sana, kuanzia  uchawi  wa  kumlisha  mtu kumtegea  njia  panda, kuzika  uchawi mtoni  kadhalika.

Lakini  katika  kitabu  hiki  nitaelezea  kuhusu  aina  ya  uchawi  ulio  tumika  kumuumiza Lugwisha  pamoja  na  namna  ya  kujikinga  nao.

Uchawi  ulio  tumika  kumuumiza  Lugwisha   ni  uchawi  wa  kwanza  kumtia  nuksi, mikosi  na  mabalaa   na  pili  ni  kumfilisi, kumfilisi  ikiwa  ni  mojawapo kati  ya  matokeo  ya  mabalaa.

Ni  uchawi  hatari  sana  na  umeumiza  watu  wengi  sana. Kabla ya  kupiga  kombora  la  kumfilisi  mkusudiwa. Huwa  linaanza  kwanza  zoezi  la  kumtia  uchizi.

Katika  zoezi  la  kumtia  uchizi  huwa  vinakusanywa  vizimba  mbalimbali  vya  hatari. Baadhi  ya  vizimba  hivyo  ni  pamoja  na  uchafu  wa  binadamu. Hapa  kwenye  uchafu  wa  binadamu  ngoja  nifafanue  kidogo.

Katika  viumbe  wote  wa  Mwenyezi  Mungu, hakuna  kiumbe  mwenye  harufu  mbaya  kama  binadamu.

 Mbwa anaweza  kukaa  mwezi  mmoja  bila  kuoga  laini  harufu  yake  haiwezi  kufanana  na  binadamu  alie  kaa  wiki  moja  bila  kuoga. Binadamu  anapiga  mswaki  kila  siku  lakini  akikaa  masaa  kumi  bila  kuongea  kinywa  chake  kinakuwa  kinatoa  harufu  mbaya.

 Linganisha  harufu  ya  maiti  ya  mwanadamu  na  mzoga  wa  mnyama  yoyote  yule  unae  mfahamu.

Harufu  ya  mzoga  wa  mwanadamu  ni  kali  kuliko  kiumbe  yoyote  ile. Mfano  mzuri, unaweza  kukaa  kwenye  eneo  ambao  kuna  mzoga  wa  mbwa, paka , kuku  nakadhalika  hata  kwa  siku mbili  au  tatu  lakini  huwezi  kukaa  mahali kwenye  mwili  wa mwanadamu  ulio  fariki  na  kuachwa  kwa  siku  moja  tu.

Hata  katika  roho , mwanadamu  ndio  kiumbe  mwenye  roho  mbaya  kuliko  mnyama  yoyote  yule.

Simba  hawezi  kula  simba  mwenzake  lakini  binadamu  wanakulana  wao  kwa  wao.

Ndio  maana  wanasema  hata  silaha  kubwa  kubwa  kama  vile  mabomu  na  bunduki  vimewekwa  kwa  ajili  ya  kumdhibiti  mwanadamu  na  sio  wanyama.

Sasa  basi  wachawi  hutumia  uchafu  wa  mwanadamu kama moja  wapo  kati  ya  viambato  vikolezo  katika kutengeneza  ulozi  wa  kuwatia  watu  nuksi, mikosi  na  mabalaa.

Uchafu  wa  mwanadamu  huweza  kutumika  katika  ulozi  kwa  namna  nyingi  sana. Mfano  mchawi  mwenye  pepo  la  uchawi  linalo  tenda  kazi, anaweza  kulala  saa  moja  usiku  na  kuamka  sea  kumi  na  moja  alfajiri  mdomo  wake  ukiwa  unanuka  halafu  akaroga  biashara  ya  mtu , kuvunja  ndoa  ya  mtu  au  kumtia  mtu  mkosi  kwa  kutumia  harufu  ya  mdomo  wae  kama  kizimba  pamoja  na  mti  mmoja  wa  kichawi.

 Tukirudi  katika  uchawi  ulio tumika  kumuumiza  LUGWISHA. Hutafutwa  watu  arobaini  wenye  shida, nuksi na  mabalaa  ya  kutisha  ambayo  ni  tofauti  tofauti.  Watu  hawa  hupatikana  kwa  msaada  wa  wakonikoni.

Watu  hawa  hupiga  kambi  maalumu  ya  kichawi  kwa muda  wa  siku  arobaini bila  kuoga. Siku  ya  arobaini  ndio  linaanza  kufanyika  zoezi  la  kupika  uchawi  huu.

Watu  hao  wake  kwa  waume watajipaka  dawa  fulani  ya  kichawi  halafu  wataanza kukwangua  uchafu  wao  kutoka  kwenye  sehemu  mbalimbali  za  miili  yao  huku  yakitamkwa  maneno  maalumu  ya  kichawi. Kila  mmoja  wao  atapulizia  pumzi  yake  kwenye kitambaa  cheusi  ambacho  kitafungwa  baada  ya  hapo   na  atafanya  hivyo  huku  aitamka  maneno  maalumu  ya  kichawi.

Kumbuka  hawa  watu  hupatikana  kwa  msaada  wa  wakonikoni.  Watu  hawa  wanakuwa  wameenda  kwa  wakoni  koni  kwa  ajili  ya  kutolewa  mabalaa, nuksi  na  mikosi  mbalimbali.

Kwa  wakoni  koni  nuksi  na  mabalaa  ya  watu  ni  bidhaa  adimu.  Badala  ya kuitoa  wao  huvichukua  kwa  ajili  ya  kutengeneza  uchawi  wa  kuwaumiza  watu.

Siku  hiyo yakwenda  kutoa  hizo  nuksi, kila  mmoja  kati  ya  watu  hao  wenye  nuksi  hutamka  maneno  maalumu  wakati  anatoa  uchafu kwenye sehemu  mbaimbali  zap  mwli  wake  kama  vile  kwenye  masikio, mdomoni, kwapani, sehemu  zap  siri  nakadhalika.

Kwa  mfano, mimi  fulani  Bin  Fulani  ambae  ninasumbuliwa  na  magonjwa kadha  wa  kadha, ninasumbuliwa  na  matatizo  kadha  wa  kadha, ninayatoa  magonjwa  yangu  yote, nuksi  zangu  zote pamoja  na  matatizo  yangu  yote  na  kuyahamishia  kwa  fulani  bin  fulani  nakadhalika.

Uchafu  wote  huu  utausanywa pamoja na  kuhifadhiwa  kwenye  chombo  maalumu. Zile  harufu  zitatumika  wakati  wa  kupika  hii  nuksi  katika  hatua  ya  mwisho  kabisa.

Baada  ya  hapo  vitachukuliwa  vitu  vingine  kama  vile  mavi  ya  sokwe, mavi ya nyani, mavi ya ngedere, mavi ya  bundi, mavi  ya  ndege  wa  porini  ajulikanae  kama  mpambe  wa  bundi, mavi  ya  ndege  wa  porini  anaitwa  Mkatasanda   “ Ndege  huyu  mkatasanda  akilia  kwenye  nyumba  yenu  lazima  msiba  mkubwa  utokee”, uchafu kutoka  kwenye  majalala  arobaini, uchafu  kutoka  kwenye misiba  arobaini, vizimba  vya wanunguli , mafusho  sea  machafu pamoja  na  miti  mingine  kumi  na  tatu  ya porini.

Vitu  vyote  hivi  vinasagwa  pamoja  na  kwenda  kunuizwa  makaburini. Wakati  wa  manuizo  wale  watu  arobaini  wanakuwa  wanalia  na  kuimba  nyimbo  za  kichawi  na  maombolezo  huku  waitaja  jina  la  mkusudiwa  kana  kwamba  amefariki  dunia.

Baada  ya  zoezi  la  kumtumia  nuksi, balaa  na  mikosi  mkusudiwa, zoezi  linao  fuata  huwa  ni   kufanya  tambiko  au  uchawi  wa  kumfilisi  mkusudiwa.

Katika  tambiko  hili wachawi  huchukua  mzizi  wa  mbono  kaburi, mzizi  wa  mti  unaitwa  mshindwi , mzizi  wa  mtopetope , mzizi  wa  mfausiku, mzizi  wa  mgodo, pamoja  na  mizizi  ya  miti  mingine 33.  Mizizi  yote  hiyo  niliyo  itaja  hapo  juu  husagwa  kwa  pamoja na  kuhifadhiwa  kwenye  kitambaa  cheusi.

Baada  ya  hapo   unachukuliwa  mzizi au  mizizi  iliyo okotwa  wakati kaburi linachimbwa. Mzizi  huu wakati  unachukuliwa  huwa  hauchukuliwi  na  mhusika  mwenyewe  bali  hutuma  mtu   akauchukue..  Huu  ni  uchawi  mkubwa  sana  na  unatumika  kwenye  mambo mengi  sana  ya  kichawi,. Ni  hatari  sana. Narudia  tena  ni  uchawi  sana.

 Huo  mzizi    ulio   chukuliwa  wakati  kaburi  linachimbwa, unapaluliwa  vizuri  kwa    tambiko  maalumu  la kichawi, wakati  mzizi  huu  unapaluliwa   mpaluaji  anakuwa  amejipaka  dawa  maalumu na  anakuwa  amevaa  vazi  maalumu.

  Mzizi  huu  ukishapaluliwa  unawekwa  kwenye   chungu  cheusi.

Halafu  anatafutwa  ogoo  mwekundu  au  mweusi . Huyu  jogoo  mweusi  au  mwekundu  analishwa  dawa  maalumu  ya  kichawi  na  kwenda   kufungwa  porini chini  ya  mti wa mgodo   kwa  muda  wa  siku saba. Atauwa  anapelekewa  mchele  kila  siku  kwa  muda  siku  hizo  saba.

Baada  ya  siku  saba  mchawi  atamchukua  yule  jogoo  na kulala  nae  ndani.  Mahali  atakapo  kuwa  amelala  huyo  mchawi  lazima   pembeni  yake  kuwe   na  kile  chungu  cheusi  chenye  ile  mizizi  ya  kaburini  iliyo  paluliwa  na kusagwa  kisha   kuwekwa  ndani  yake.

Ikifika  alfajiri, jogoo  akiwika  mara  moja , anakamatwa  na  kuchinjwa  kisha  damu  yake  inawekwa  kwenye  kile  chungu  cheusi  chenye  ile  dawa  ya  kichawi.

Mchawi  huyu  anakuwa  makini mno kuhakikisha kuwa   jogoo hawiki   zaidi  ya  mara  moja. Yaani  jogoo  akiwika  mara  moja  tu,anakamatwa   hapohapo  na kuchinjwa  na  kisha   damu  yake  inamiminwa  kwenye  hicho  chungu  chenye  huo  uchawi. Hapa  sasa  damu  ya  kuku  inakuwa  imechanganyikana  na  hii  dawa.

Zoezi  hili  likikamilika, yule  jogoo  anaachwa  sakafuni  pale pale  alipo chinjwa   na  ile  damu  yake  ambacho  imechanganywa  na  ile  dawa  inaachwa  kwenye  chungu  kisha  mchawi  huyu  anaenda  kulala  na  kuamka  jua  litakapo  chomoza.

Akisha  amka  anaenda  kukausha  dawa  ile  pamoja  na  damu  kisha  anaisaga  hadi  inakuwa  unga  unga.  Ukisha  patikana  unga  unga  wa  dawa  hii  unahifadhiwa  kwenye  chungu  cheusi.

Ndani  ya  chungu  hicho  cheusi  vinaongezwa  vitu  vifuatavyo ;  sindano  saba,  viwembe  saba  ambavyo  vyote   vinakatwa, mafuta  ya  maiti  vichupa  saba  ( mafuta  haya  hutumika kuwapaka maiti, karafuu  maiti ya  kidonge  vidonge  saba, mafuta  ya  usiku  kiasi cha  kifuniko  kimoja  cha  soda,  kishinda  wachawi  kijiko  kimoja, mti  mkuu  kijiko  kimoja, mfalme  wa  porini  kijiko  kimoja,   unga  wa  mdudu  kusahau kijiko kimoja, Huyu  mdudu  kusahau  hupatikana  porini na  nyikani. Sifa  yake  ni  kwamba, ukimkanyaga  utapotea  mahali  unapokwenda. Ana  majini  wakali  sana  wa  usahaulifu.

 Vitu  vingine  vinavyo  chukuliwa  ni  pamoja  na  magunzi  ya  maindi  yaliyo liwa  na  nyani  shambani, mabai  ya  mazao  na mchanga  wa  kwenye  shamba  lililo  liwa  na  nyani, mabaki  ya  mazao  mchanga  wa  kwenye  shamba  la  mihogo  lililo vamiwa  na  kuliwa  na  nguruwe  mwitu , nzige  walio kaushwa  na  kusagwa,  mabaki ya  mazao  au  mimea  iliyo  shambuliwa na kuliwa  na  nzige, ubao  au  vitu  vilivyo toka  kwenye  mafuriko pamoja  na  vizimba  vingine  vingi.

Vyote  hivi  vinasagwa  kwa  pamoja  na  kuchanganywa  kwenye  chungu  cheusi.

Baada  ya zoezi  hili , mchawi   anachukua  zile  dawa alizo  saga  pamoja  mara  ya  kwanza  ambazo  ni  mizizi ya mbono kaburi, mfausiku, mshindwi,mtopetope  na  miti mingine  33  ya  kichawi,na  kuzichangaya  kwenye  hicho  chungu  ambacho  uchawi  huo  hapo  juu  umewekwa.

Baada  ya  hapo  chungu  hicho  kinafungwa  kwa  kitambaa  cheusi juu  na  kwenye  shingo.

Zoezi  hili  hufanyika  kwa  kufuata  hatua  zote  bila  kuruka  au  kusahau  hata  hatua  moja.

 Baada  ya  zoezi  hili  kukamilika  mchawi  huyu pamoja  na timu  yake, watavaa  kaniki  nyeusi  na  kujipaka  unga  wa  mti  maalumu  wa  kichawi, bila  kuvaa  nguo  yoyote  ndani, watasubiri  hadi  saa  sita  za  usiku  na  kwenda  hadi   kwenye  makaburi  yaliyo  sahaulika.

Ninaposema  makaburi  yaliyo  sahaulika  nazungumzia  makaburi  ambayo  marehemu  walizikwa  zaidi  ya  miaka  20, 30  hadi  50   au  hata  mia  iliyopita, ambayo  ndugu  zao  wameisha  ya  sahau  au  na  wao  walisha  kufa  zamani,.

Ipo  njia  ya  kiganga  na  kichawi  ambayo  inatumika  kujua  kama  kaburi  fulani  limesahaulika  au  la.

Wanapokwenda  kwenye  makaburi  haya  ni  lazima  wawe  bila  viatu na  kama  makaburi  yapo  kwenye  maeneo  yenye  miba mingi basi  watavaa  viatu vya  asili  kama  vile katambuga, na  pia  lazima  wapitie  kwanza  njia  panda  kufanya  tambiko  maalumu.

Wakifika  kwenye  makaburi  hayo  huanza  kwa  kupiga  hodi  mara  saba  huku  wanajiitikia  wenyewe.  Husema “ HODI!”  na  kujiitikia  wenyewe  “ KARIBU! “. Watafanya  hivyo  hadi mara  saba . Baada  ya kufanya  hivyo  mara  saba , wataanza  kusema  maneno  yafuatayo :

“  WAZEE  NIMEKUJA  NINA  NGORANI  YANGU. WAZEE  NIMEKUJA  MIMI  FULANI  BIN FULANI, SHIDA  YANGU  NI  FULANI  BIN  FULANI. NATAKA  MTU  HUYU  AFILISIKE  NA  ASHUKE  HADI  CHINI  AWE  KAMA  MIMI AU  SISI  KAMA  WAPO WENGI  AU  AWE  CHINI  YETU  KABISA!

  FULANI  BIN FULAN  AMEPATA  PESA  AMEPATA  MALI, AMESOMA  SANA, NA  SASA  ANATUDHARAU   KWA  KUWA  AMESOMA  SANA!  ANATUONA  SISI  HATUNA  MAANA !

PESA  ZAKE  , ELIMU  YAKE, MALI  ZAKE  NDIO  ZINAMTIA  JEURI  NA KIBURI  NA  KUMFANYA  ATUDHARAU. TUNAOMBA  MUENDE MKAMFILISI  NA  KUMSHUSHA  CHINI  HADI  AWE  KAMA  SISI.

NINYI  MIZIMU  WA  HAPA. NINYI  WAFU  MLIOLALA  HAPA. WAZEE  KWA  VIJANA, WAKE  KWA  WAUME. SIKUWA  NAWAJUA  WAKATI  WA  UHAI, WENU  ILA  NIMEKUJA  KUWAAMSHA  NA  KUWATUMA  KWA  FULANI  BIN  FULANI, NENDENI  MKAMFILISI  NA  KUMSHUSHA  CHINI   KABISA  HADI AFANANE  NA  MIMI AU  ASHUKE  KABISA  AWE  CHINI  YANGU.

MAMBO  YAKE  YOTE  YAHARIBIKE., MALI ZAKE, PESA ZAKE, NA  KILA  KITU  CHAKE. VYOTE  VIFE KAMA  JINSI NINYI  MLIVYO KUFA  NA  KUJA KU LALA  MAHALI  HAPA. KAMA  N I MASHAMBA  YAFE. BIASHARA  ZOTE  ZIFE..N.K

AUZE  KILA KITU  CHAKE  NA  PESA  ATAKAZO ZIPATA  ZITUMIKE  KUMUANGAMIZA  YEYE  MWENYEWE. AKINUNUA  CHAKULA  NA KINYWAJI VIMLETEE  KISUKARI  NA  PRESHA, AKINUNUA  GARI  LIMLETEE  AJALI  NA  KUMSABABISHIA  ULEMAVU  WA  KUDUMU,  AKINUNUA  NGONO  BASI  IMLETEE  UKIMWI. AUGUE  KILA  AINA  YA  MARADHI. ADHALILIKE. AFEDHEHEKE..NAKADHALIKA.

Wakati  huyu  mtu  anazungumza  maneno  haya, mkonikoni  au  mchawi  anakuwa  anafanya  tambiko  maalumu  kwenye  makaburi hayo  huku  akipuliza  na  kutupa  dawa  maalumu  za  kichawi  kwenye  makaburi  hayo.

Na  kama  hawa  washirikina   walioenda  kumroga  ndugu, jamaa  au  rafiki  yao  wapo  zaidi  ya  mmoja, basi kila  mmoja  atatamka  maneno  yake.

Wakimaliza   mmoja  wao  anachukua  kile  chungu  na  kukiweka  sehemu   ya  kifua  kwenye kaburi  lolote  ambalo  atalichagua  lililopo  katika  eneo  hilo. Na  huwa  ni  mwiko  kuzika  chungu  hiki  cha  kichawi. Huwa  kinawekwa  tu  juu juu.

Sasa  basi  mtu  huyu  anapokuwa  anaweka  hungu  hiki, hutamka  maneno  yafuatayo :

“  NA  KAFARA  YENU  NDIO  HII  HAPA  NIMEWAPA !  HII NDIO NGORANI YANGU! AMKENI  MKATENDE  KAZI  YENU ! HII NI  VITA ! HAYA  NI MAPAMBANO! UENI KILA  KITU  CHAKE  CHOTE, ABAKI  KAMA  ALIVYO  ZALIWA !

Skadi  hili  huwa  linaondoka  hapo  hapo  na  huanza  kufanya  kazi  siku  hiyo  hiyo.

Ni  uchawi  mkubwa na  wa  hatari  sana. Usiombee  utupiwe  skadi  kama  hili.

Watu  walio tupiwa  skadi  hili  wote  walipata matatizo  katika  maisha  yao. Pona  pona  yako  ni  kama  una  kinga  kubwa au  ni  mtu  wa  maomba  au  swala  yaani  mtu  wa  ibada, vinginevyo  ndugu  yangu.Utadhalilika  na  kufedheheka  katika  maisha  yako.

Mtu  aliye  tupiwa  skadi  hili  kwanza  huwa  anapewa dawa  ya  kutapika  au  kuharisha uchawi  aio  tupiwa , baada  ya  hapo anasafishwa mwili, anapikwa   na  kisha  anapandishwa  nyota yake na kutambikiwa  upya. Aanze  maisha  yake  upya.  Kama  kuna  mali  alizo dhulumiwa  basi  zitaanza  kurejeshwa  moja  baada  ya  nyingine.

Tambiko  la  kumrejesha  muhanga  wa  uchawi  huu  katika  hali  yake  ya  kawaida  huwa  lina  hatua  ndefu  sana. Si rahisi  kuzielezea  zote  hapa. Hila  kwa  ufupi  tambiko  hili  hufanywa  na  mganga  chini  ya  mti  mmoja  wa  porini  ambao  haukaliwi  na  kitu  chochote  kichafu  au  kibaya  kiwe  jinni  au  awe  mdudu  mbaya  kama  vile  nyoka  nakadhalika.

Mambo  yanayo  fanyika  katika  tambiko  hilo  ni  pamoja  na  kupiga hodi  kwenye mti  huo  kwa tambiko  maalumu  linalo  husisha  kuku  weupe, kondoo, punda  na  pemba  nyeupe.

Kufanya  tambiko  maalumu  la  kumrudisha  upya  duniani  kwa  kutumia  mayai  ya  kuku . Tambiko  hilo  ni  kubwa  sana  na  lina  nguvu  sana.

Kwa  ufupi  tambiko  la kubatilisha  uchawi  huu  na  kumrudisha  mhusika  katika  hali yake  ya  kawaida  linahusisha  vizimba  vingi  sana.  Vichache  kati  ya  vizimba  hivyo  ni  pamoja  na  maji  ya  kwenye  chemu  chemu  ya  mlima  mrefu, maji  ya  kwanza  ya  mtoni,   Asali  ya  nimba, Nimba  ni  mnyama  wa  porini  anaefanana  kama  nyumbu, mnyama  huyu  huwa anatembea  na mzinga  wa  nyuki  kichwani. Ni mnnyama  mwenye  maajabu  sana na  haonekani  ovyo  ovyo pia  ana  sifa  ya  kupotea. Sasa  asali  ya  mnyama  huyu ndio  inayo  tumika  hapa.

Vitu  vingine  ni  pamoja  na  miko  iliyo  tumika  katika  maeneo  mbalimbali  yenye  mkusanyiko  mkubwa  wa  watu  kama  vile  gerezani  nakadhalika, mzizi  ulio kata  njia, mti  ulio  ungua  ukulunoni, maji  ya  mchele,  marashi  ya  waridi,  mafuta  ya  mcheka  na  mbingu, maji  makuu, mti  mkuu, kishinda  wachawi, mfalme  wa  pori, mzungu pori, Mkurungu, mkubashengelo, picha  yako  ya  utotoni,  kibiringisha  mavi; hawa  vibiringisha  mavi  hupatikana  sana  sana  kwenye  mavi  ya  ng’ombe  na  siku zote  hujongea  kinyume  nyume , msuswe  aliye  gongwa  na gari  akiwa  anakatisha  njia; msuswe  ni  aina  ya  panya  ambao  hutoa  sauti  inayo fanana  na  jina  lao.

Kitu  kingine  unachukua  mzizi  ulio jitokeza  nje  ambao  majani  na  matunda  yake huliwa na  ndege  mmoja  wa  porini.  Huyu ndege  wa  porini  ana  sifa  moja  kubwa, wachawi  wanapenda  sana  kumtumia kwenye  shughuli  zao. Ukichukua  nyoya  lake, ukaweka  kwenye  mto wa kitanda  ambacho  analalia mgonjwa  basi  mgon jwa  huyo  atafariki  dunia. Kuweni  makini  sana  na  mito  mnampokuwa  na  wagonjwa  iwe  ni hospitalini  au majumbani.

Pamoja  na  vizimba  vingine  vingi.

Vitu  vyote  hivyo  vinatumika  katika  kutengeneza  tambiko  la  kubatilisha  uchawi  wa aina  hii  pamoja  na  kumrejesha  muhanga  katika  hali  yake  ya  awali.

Hatua  ya  mwisho  ya  tambiko  hili, mganga  humchukua  mgonjwa  na  kumtamkia  maneno  mbalimbali. Baadhi  ya  maneno  hayo  ni  pamoja  na :

“ KUANZIA  LEO NIMEKUTOA  CHINI WALIKOKUWA  WAMEKUWEKA  WACHAWI,  MAJINI, MASHEITWANI  NA  WATU  WABAYA. NAKUWEKA  JUU  NA  UTABAKI  KUWA  JUU  KATIKA  SIKU ZOTE  ZA  MAISHA  YAKO

iIi  kuepukana  na  kutupiwa  na  uchawi  wa  aina  hii au  uchawi  wa  aina  yoyote  ile, unatakiwa  uwe  Mcha  Mungu na  kama  sio Mchanga  Mungu basi  ni  lazima uwe  na  kinga  kubwa.  Baadhi  ya  kinga  hizo  ni  kama  nilivyo  zielezea katika  sehemu  zap  mwanzo zap kitabu  hiki..

Rais Dkt Magufuli ateua Naibu Kamishna Mkuu wa TRA

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Bw. Adolf Hyasinth Mohondela Ndunguru kuwa Naibu Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Uteuzi wa Bw. Adolf Hyasinth Mohondela Ndunguru umeanza  tarehe 22 Mei, 2017.

Kabla ya uteuzi huo Bw. Adolf Hyasinth Mohondela Ndunguru alikuwa Kamishna wa Sera, Wizara ya Fedha na Mipango.

Bw. Adolf Hyasinth Mohondela Ndunguru anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Charles Edward Kichere ambaye hivi karibuni aliteuliwa kuwa Kamishna Mkuu wa TRA.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

Binti wa miaka 15 abakwa na vijana wanne Jijini Mwanza

$
0
0
Watu watatu wanashikiliwa na jeshi la polisi huku mwingine mmoja akiendelea kutafutwa kwa tuhuma za kumbaka binti mmoja mwenye umri wa miaka 15 wilayani Ilemela, mkoani Mwanza.

Akitoa taarifa hiyo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza DCP Ahmed Msangi amesema kwamba tukio hilo limetokea tarehe 21/05/2017 majira ya saa moja kamili jioni katika maeneo ya mamlaka ya pamba, kata ya Kirumba ambapo inadaiwa kuwa binti huyo ambaye pia ni mkazi wa Kirumba alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na mtuhumiwa aliyejulikana kwa jina moja la Phili na walipanga wakutane katika maeneo hayo.

Inasemekana kuwa binti huyo alikutana na mpenzi wake mahali hapo kisha walikwenda sehemu yenye jumba bovu kuzungumza, wakiwa kwenye eneo hilo ghafla walitokea vijana wengine watatu wakishirikiana na Phili na kuanza kumfanyia ukatili kwa kumbaka.

Inasemekana kuwa wakati wakiendelea na ukatili huo binti alipiga yowe akiomba msaada kutoka kwa wananchi, wananchi walifika eneo la tukio na kumuokoa binti na kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa mmoja aitwaye Fredy Remigius kisha walitoa taarifa polisi kuhusiana na tukio hilo.

Askari walifika katika eneo la tukio na kufanya msako mkali wa kuwatafuta watuhumiwa wengine huku wakishirikiana na wananchi na kufanikiwa kuwakamata watuhumiwa wengine wawili huku mmoja aliyekuwa na mahusiano ya kimapenzi na binti akifanikiwa kutoroka.

Amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Fredy Remigius miaka 20, mkazi wa Kitangiri, Jackson Joseph miaka 17, mkazi wa Mlimani B na Frank Haruni miaka 18.

Kamanda Msangi amesema mahojiano na watuhumiwa waliokamatwa yanaendelea na pindi uchunguzi ukikamilika watafikishwa mahakamani na kwamba majeruhi aliyebakwa amepelekwa hospitali ya mkoa wa Mwanza Sekou Toure kwa ajili ya matibabu na hali yake inaendelea vizuri.

Kutana Maajabu ya NGWIZUKULU KARORE Mganga wa Waganga Sasa Yupo Mikoa Yote Tanzania

$
0
0
Kutana Maajabu ya NGWIZUKULU KARORE Mganga wa Waganga Sasa Yupo Mikoa Yote Tanzania

Pia anatoa Tiba kwa Njia ya Simu ukiwa popote Pale Tanzania au Nje ya Tanzania..

Ngwizukulu karore ni Mtabibu na Mtafiti wa Dawa za Asili ya Africa mwenye Uzoefu wa Miaka 19 na Ametembea Zaidi ya Nchi 43 Duniani Katika utoaji wa Tiba za Asili..
Je unasumbulia na Mapenzi..?
 
(Umeachwa na Umpendae awe Mume/ Mke au mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine na Bado Unampenda?) Umejaribu sehemu Nyingi bila Mafanikio?Wasiliana na Ngwizulu Karore Akusaidie Kumshika Umpendae Asikusaliti(LIMBWATA) Kumtawala Mpenzi wako kwa sababu Maalum..Anauwezo wa Kusambalatisha Mahusiano yao ndani ya siku Moja tu.
 
Je Unasumbuliwa na Madeni?
Umepotelewa na Mali au Kudhulumiwa?
Biashara yako Haina wateja?
Unatatizo la kutokushika Mimba na umehangaika sehemu nyingi bila mafanikio?
Wasiliana na Ngwizukulu karore Kwa Majibu ya Maswali yako..
Anasafisha Nyota na Kutoa Pete za Bahati kuendana na Nyota yako.
 
Kupandishwa Cheo na Heshima Mahala pa Kazi.
Wanaotaka Kuwa Maarufu na Kujulikana.
pia Utapewa Nguvu ya Kujilinda na Mali zako na Mwili wako.. Huzuia Chuma Ulete katika Biashara..
Mvuto wa Biashara na Mwili wako.
Hutibu kabisa Nguvu za Kiume na Kurefusha Uume kwa saizi Unayotaka.
 
Magonjwa Sugu(Miguu Kufa Ganzi, kisukari, Presha, Pumu nk.)Humaliza Kesi za Muda mrefu ndani ya siku 14 tu.
 
Anatoa NDAGU Zisizokuwa na Masharti(Mali Bila Mashrti) Kwa maelezo Zaidi wasilina nae kwa
 
Whatsapp+255 654 876 841
Call .. +255 759 084996

Wanafunzi wengine watatu wapoteza maisha leo Geita Baada ya Mtumbwi Wao Kuzama

$
0
0
Watu watatu ambao ni wanafunzi wa Shule ya Msingi Butwa mkoani Geita wamefariki dunia baada ya mtumbwi waliokuwa wakisafiria kuzama katika Ziwa Victoria, mkoani Geita.

Kamanda wa Polisi Mkoani Geita amesema tukio hilo lilitokea jana majira ya saa 10 jioni wakati wanafunzi hao walipokuwa wakivuka maji kwa kutumia mitumbwi miwili wakitoka shuleni katika kisiwa cha Isimacheli  kurudi majumbani kwao katika kisiwa cha Lulegea.

Amesema wanafunzi hao jumla walikuwa 24 ambao walijigawa kwa kupanda wanafunzi 12 katika kila mtumbwi ambapo mtumbwi wa kwanza ulifanikiwa kuvuka salama, lakini mtumbwi wa pili ulielemewa mawimbi na hatimaye kuzama.

Amesema kwamba kabla mtumbwi huo haujazama, nahodha wa mtumbwi huo baada ya kuona anaelemewa aliamua kurudi nyuma ili aurudishe ufukweni lakini wakati akijaribu kurudi mtumbwi ulizidiwa na kuzama ambapo wanafunzi 9 wote wa kiume walinusurika baada ya kufanikiwa kuogelea huku watatu ambao wote ni wa kike wakipoteza maisha.

Amewataja waliofariki dunia kuwa ni pamoja na Kumbuka Bahati (13) mwanafunzi wa darasa la 3, Anastazia Mwita mwanafunzi wa darasa la 3 na Sophia Lusala mwanafunzi wa darasa la Kwanza.

Amesema mwili wa mwanafunzi mmoja ulipatikana jana majira ya jioni na miili miwili imepatikana leo ikiwa imeharibika vibaya

Jeshi hilo linamshikilia nahodha wa mtumbwi huo anayefahamika kwa jina la Hulugu Kayalenda na uchunguzi bado unaendelea.

Yussuf Manji Ajiuzulu Uenyekiti Club ya Yanga

$
0
0
Mwenyekiti wa Yanga, Yussuf Manji amejiuzulu wadhifa  huo akidai kuwa anatoa nafasi kwa watu wengine kuiongoza.

Kupitia barua yake, Manji amesema kuwa anaondoka akiamini ameiacha Yanga ikiwa timu yenye mafanikio kisoka nchini.

"Muda wangu wa kutangaza kuwa ninakaa pembeni kutoka kwenye nafasi ya uenyekiti ni sasa. Tayari tumekuwa mabingwa watetezi mashindano tena tuna kizuri cha wachezaji na makocha. Tumeungana kwa pamoja haijawahi kutokea, " imesema sehemu ya barua hiyo.

Akizungumza kwenye kipindi cha Sports Headquarters kinachoendeshwa na kituo cha radio cha EFM, Manji amekiri kujiuzulu.

"Hiyo taarifa ni sahihi na sababu za kujiuzulu zipo humo, " amejibu Manji kwa kifupi.

Kwa mujibu wa barua ya Manji iliyoisaini Mei 22, inasema amejiuzuru uenyekiti na sasa majukumu yote hadi pale uchaguzi mpya utakapofanyika wa kujaza nafasi yake majukumu yote ya timu yatakuwa chini ya Makamu wa Rais, Sanga.
 
Sanga alithibisha kupokea barua ya Manji kujizuru akisema ni kweli nimepokea barua ya mwenyekiti juu ya uamuzi wake wa kupumzika kwa sasa.
 
Katika barua Manji aliisema huwa kunafika muda tukiwa tunafuata wito fulani, wakati mimi nikiwa sehemu ya Yanga ilinibidi nijitokeze mbele kwa ajili ya umoja wa klabu yetu tuipendayo na kuongoza. Kulikuwa na wanachama waliokuwa wakigombana, ndipo ilikuwa muda wangu wa kutoa msaada kwa Yanga.
 
"Sisi sote ni sehemu ya ukoo mkubwa wa Yanga na ukweli mnaufahamu, imani ndiyo jambo ambalo tulilihitaji ndani ya Yanga kuturudisha katika mwelekeo sahihi wa miaka 11 iliyopita."
 
Taarifa hiyo iliendelea kusema "Kama Mungu alivyotuonyesha kwa kubadili jiwe kuwa mkata, hivyo msaada wangu kwa uwezo wa neema zake, naamini ulifanya mabadiliko chanya na klabu iko imara na huru. Lakini umefikia wakati wangu wa kuachia wengine na wengeni wasifikirie nilikuwa kiongozi aliyetaka cheo chochote au umashuhuri, ila ni upendo uliomgusa kuitumikia Yanga yetu. Pamoja tulifanikiwa mengi sana, na kuandika historia ndani ya Yanga na nilipolea baraka zenu mimi binafsi na familia yanga kupitia furaha japo ndogo, iliyoweza kuwaletea, ambao ninawashukuru sana.
 
"Nilisema tangu mwaka 2014, kuwa sitagombea katika uchaguzi wa uongozi kwenye nafasi yoyote ndani ya klabu na nikaonyesha mfano kuwa klabu yetu siyo mtu mmoja ila ni yetu sote, na uongozi ni lazima utoke kutoka kwenye kizazi kimoja kwenda kingine.
 
Iliongeza taarifa hiyo kuwa "Lakini mwaka jana tulikuwa katika mashindano ya mabara na kuacha pengo isingekuwa sahihi, hivyo kinyume na msimamo wangu niligombea uenyekiti wa Yanga na kupata ushindi bila ya kupigwa, lakini kama nikiendelea, nitakuwa ninaonyesha mfano upi kwa watoto wetu ambao wanaipenda Yanga kwa sababu yetu? Kwani Yanga siyo klabu yao kama ilivyokuwa yenu na mimi?"
 
Muda wangu wa kutangaza kuwa ninakaa pembeni kutoka kwenye nafasi ya mwenyekiti wa Yanga ni sasa, tayari tumekuwa mabingwa wa mashindano tena, tuna kikosi kizuri na wachezaji na makocha, tumeungana kwa umoja haijawahi kutokea, tumerudisha heshima ya kuwa washindano wa ukweli katika klabu Afrika, na kuwa imara zaidi kiuchumi na mkataba wa ufadhili  ya Sportspesa.
 
Nafahamukuwa bado kuna mengi yanayohitajika kutimizwa, lakini barabar ya mambo yanayotakiwa kutimizwa haiwezi kuisha, na siwezi kuwa mroho wa kuamini kuwa ni mimi pekee nitakayeweza kutufikisha mwisho wa safari.
 
Muda wangu kama mwenyekiti wa klabu yetu ulikuwa umeongezwa tu na haikumaanisha katika demokrasi yetu uwe ni ule usiokuwa na kikomo.

Nay Wa Mitego Amjibu Waziri Mwakyembe Kuhusu Kutoimba Siasa

$
0
0
Rapa Nay wa Mitego amefunguka na kumtaka Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe kutoa ufafanuzi juu ya kauli yake aliyotoa kuwa wasanii wasijihusishe na masuala ya siasa.

Nay wa Mitego akiongea kwenye kipindi cha Planet bongo ya East Africa Radio, amesema kuwa yeye anaamini muziki ni siasa na siasa ni muziki hivyo ni ngumu kutofautisha vitu hivyo viwili, hivyo amemuomba Waziri mwenye dhamana kutoa ufafanuzi juu ya kauli hiyo na kudai yeye hajawahi kuimba wimbo wa siasa bali anaimba mambo yaliyopo kwenye jamii.

"Nachoamini mimi muziki ni siasa na siasa ni kama muziki, siasa ni maisha ya watu ambayo wanaishi kila siku na muziki pia ni maisha ya watu ambayo wanaishi kila siku kwa hiyo anahitaji kutoa ufafanuzi wa kutosha juu ya hili. Siasa ni maisha ya watu na muziki ni maisha ya watu, mimi binafsi naamini sijawahi kuimba wimbo wa siasa hata siku moja bali ninaimba maisha ya watu ambayo yanaendelea kila siku na ndiyo maana wengi wanathubutu kusimama upande wangu endapo linatokea tatizo lolote" alisema Nay wa Mitego.

Mbali na hilo Nay aliendelea kusisitiza kuwa kuna haja Waziri kutoa ufafanuzi wa jambo hilo

"Mh. Waziri anatakiwa kutoa ufafanuzi juu ya jambo hili ili watu wajue kipi hawatakiwi kuimba na kipi wanatakiwa kuimba sababu siasa ni maisha ya watu ya kila siku na muziki wa Hip hop ni maisha ya watu ya kila siku, kwangu mimi muziki wangu hauwezi kubadilika zaidi nitazidi kuongeza vitu ili nisiwaudhi watu na nizidi kuongeza idadi ya mashabiki" alisisitiza Nay wa Mitego

OFA: Jipatie Kitabu cha Riwaya Kali ya President Wife Toka Kwa Mwandishi Makini Eddazaria

$
0
0
OFA HII SI YA KUKOSA KWA KWELI
Nununa kitabu cha PRESIDENT WIFE kwa sh 10000 upate kitabu cha HARD DAY Bureeeeee kabisa. Kumbuka kitabu hivi hupatikana Whatsapp 0657072588 kwa mfumo wa PDF. Au email eddazariaM@gmail.com


==>"Baada ya utawala wa mzee GODWIN na MANKA kutolewa madarakani na EDDY DODWIN, adui mkubwa wa Eddy, JOHN anachukua madaraka ya Mzee Godwin na kuapa ni lazima ataamuangamiza Eddy aliye kuwa rafiki yake wa kipindi kirefu toka wakiwa sekondari. 

"Rahab anaongoza nchi huku kijana machachari Adrus akiwa mlinzi makini kuhakikisha maisha ya mke wa raisi yanakuwa salama, ila K2 na kaka yake wanajawa na uchu wa madaraka na kuhakikisha kwamba wanauangusha uongozi wa Raahab, ila Eddy anasimama kama ngao na kupigania uongozi wa Rahab je atafanikiwa"
 
Ungana nami muandishi wako Eddazaria G.Msulwa katika hadithi hii ya kusisimua
 
●Wasiliana nami 0657072588 au 0768516188 

KARIBU SANA UZIDI KUNIUNGA MKONO KWENYE KAZI YANGU YA UANDISHI

Nape Amvaa Tena Makonda kuhusu Sakata la Kuvamia Kituo cha Clouds

$
0
0
Miezi michache ikiwa imepita tangu kutokea tukio la uvamizi wa kituo cha Clouds Media Group na kuundwa kwa kamati ya kuchunguza tukio hilo, hatimaye aliyekuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye  amemvaa  tena  Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kwa kusema kwamba hakuunda kamati ya kumchunguza yeye, bali aliunda kamati ya kuchunguza tukio la kuvamiwa kwa kituo cha utangazaji cha Clouds Media Group.

“Niliunda kamati kuchunguza tukio la kuvamiwa kituo cha utangazaji sio kumchunguza RC. Kama RC alikuwa mmoja wa wavamizi, hayuko juu ya sheria,” ameandika Nape kupitia ukurasa wake wa Twitter.

Alipoulizwa kwanini Waziri wa Habari aunde kamati ya uchunguzi wa tukio la uvamizi badala ya kamati hiyo kuundwa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Nape alijibu kwa kuuliza swali kama kila kamati inaundwa na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Majibu haya ya Nape yamekuja ikiwa ni saa chache baada ya kuulizwa ni yapi maoni yake kuhusu kauli ya Makonda kwamba hakuwa akifahamu mipaka yake ya kazi ndio sababu alikwenda kuunda tume ya kumchunguza.
Kauli ya Nape kuhusu kuunda kamati imekuja ikiwa ni takribani saa 24 tangu Makonda aliposema kuwa aliyekuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo aliunda kamati ya kumchunguza.

Makonda alisema hayo jana, ambapo alidai kuwa kamati iliyoundwa na Waziri isingeweza kumhoji kwa sababu haikuwa na uwezo huo kutokana na wajumbe wa kamati hiyo kutofahamu mambo yanayohusiana na masuala ya uvamizi.

Aliyekuwa Rais wa Korea Kusini Afikishwa Mahakamani akiwa na Pingu Mikononi

$
0
0
Aliyekuwa Rais wa Korea Kusini, Park Geun-hye amefikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza kujibu mashtaka yanayomkabili, tangu alipokamatwa mwezi Machi mwaka huu.

Mwanasiasa huyo aliyeondolewa madarakani kwa kashfa nzito, anakabiliwa na mashtaka kadhaa ikiwa ni pamoja na rushwa, matumizi mabaya ya madaraka na kuvujisha siri za Serikali. Hata hivyo, Park aliyefikishwa mahakamani hapo na gari la magereza akiwa amefungwa pingu mikononi alikana mashtaka yote dhidi yake.

Park anatuhumiwa kushirikiana na rafiki yake, Choi Sonn-sil, kuchota fedha kinyume cha sheria kutoka kwa makampuni makubwa ya nchi hiyo ikiwa ni pamoja na kampuni ya Samsung, kwa malengo ya kupata mrejesho wa faida ya kisiasa.

Choi Soon-sil ambaye pia anakabiliwa na mashtaka alifikishwa mahakamani pamoja na mwanasiasa huyo lakini pia alikana mashtaka yote dhidi yake.

Kiwango cha juu zaidi cha adhabu kwa kosa la kupokea au kutoa rushwa nchini Korea Kusini ni kifungo cha maisha jela.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya May 24

Albert Msando Ajiuzulu......Ni Baada ya Video Yake Chafu Kuvuja Mtandaoni

$
0
0
Aliyekuwa mshauri wa Chama cha ACT Wazalendo, Albert Msando amejiuzulu nafasi yake hiyo kufuatia video chafu zilizomuhushisha kuvuja kwenye mitandao ya kijamii hivyo ameamua kujiuzulu ili kuwajibika na kuomba radhi kwa wananchi kwa kitendo hicho

Kiongozi wa Chama Cha ACT Wazalendo Zitto Kabwe, amethibitisha kupokea barua hiyo na kukubaliana na kiongozi huyo kwa kitendo chake hicho cha kuwajibika kisiasa huku akieleza kuwa, Bw. Msando amekuwa na mchango mkubwa katika Chama chao.

"Nimepokea barua ya Wakili Albert G. Msando kuomba kujiuzulu nafasi yake ya Ushauri wa Chama chetu cha ACT Wazalendo. Ndugu Msando anawajibika Kwani anapaswa, nanukuu kutoka katika barua yake, "kuishi Kama mfano Kwa jamii inayonizunguka". 

"Ndugu Albert Msando amekuwa kiongozi mwenye mchango mkubwa katika chama katika nafasi mbalimbali alizoshika ndani ya chama. Chama kinamshukuru kwa moyo wake wa uzalendo na mchango alioutoa katika Chama. Ni matumaini yetu ataendelea kushirikiana nasi katika ujenzi wa chama kwa kadri atakavyoweza na atakapohitajika kama mwanachama"- alisema Zitto Kabwe.

Zitto Kabwe pia ametumia nafasi hiyo kuwaomba wananchi wamsaidie katika jambo hilo analopitia saizi

"Nikiwa Kiongozi wa Chama nimekubali kuwajibika kwake na kumtakia kheri katika kujisahihisha kwake. Ndugu Msando Alberto ameomba msamaha Kwa jamii kwa uwazi na ni wajibu wetu kumsaidia kupita katika mitihani iliyomkumba" alimaliza Zitto Kabwe.

Rais Magufuli awahakikishia ushirikiano wawekezaji wa China

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amewahakikishia wafanyabiashara na wawekezaji kutoka Shirikisho la Taifa la Utengenezaji wa Mitambo ya Viwanda la China (China National Machinery Industry Federation – CNMIF) kuwa Serikali ya Awamu ya Tano itawapa ushirikiano wa kutosha katika mpango wao wa kuwekeza katika uzalishaji wa nishati ya umeme, viwanda na kilimo hapa nchini.

Mhe. Rais Magufuli ametoa kauli hiyo jana tarehe 23 Mei, 2017 Ikulu Jijini Dar es Salaam alipokutana na kufanya mazungumzo na Makamu Mwenyekiti wa CNMIF na Mbunge wa Bunge la Wananchi wa China Bw. Zhan Xin.

Mhe. Dkt. Magufuli alisema Tanzania imejiwekea malengo ya kuongeza uzalishaji wa umeme kutoka Megawatts kati ya 1,500 na 1,800 zinazozalishwa hivi sasa hadi kufikia Megawatts 10,000 na kwamba ili kufikia malengo hayo wawekezaji wanakaribishwa kuzalisha umeme kwa kutumia vyanzo vilivyopo kama vile gesi, makaa ya mawe na jua.

“Kwa hiyo Ndg. Zhang Xin kawaambie wawekezaji wenzako wa China waje Tanzania, nchini zetu ni ndugu na marafiki wa miaka mingi, itakuwa jambo jema wakija kuunga mkono juhudi zetu za kujenga viwanda kwa kuzalisha umeme mwingi na pia kushiriki katika miradi mingine ikiwemo ya ujenzi wa miundombinu ya reli na barabara” alisema Mhe. Rais Magufuli.

Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli amekutana na Balozi wa Ufaransa hapa nchini Mhe. Malika Berak ambapo viongozi hao wamezungumzia utekelezaji wa mambo mbalimbali ya ushirikiano pamoja na miradi ya maendeleo iliyotokana na makubaliano ya Mkutano wa wafanyabishara wa Tanzania na Ufaransa uliofanyika hivi karibuni.

Viongozi wengine ambao leo wamekutana na kufanya mazungumzo na Mhe. Rais Magufuli ni Kaimu Balozi wa Uturuki hapa nchini Bw. Yunus Belet na Kaimu Balozi wa Jamhuri ya Korea Bw. Songwon Shin.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

Rais Magufuli Atapokea Taarifa ya Kamati Maalum ya kuchunguza mchanga Saa Tatu Asubuhi Hii

$
0
0
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, inawataarifu wananchi wote kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo  tarehe 24 Mei, 2017 atapokea Taarifa ya Kamati Maalum aliyoiunda kuchunguza mchanga ulio katika makontena ya mchanga wa madini (Makinikia) yaliyopo katika maeneo mbalimbali hapa nchini Tanzania.

Tukio la kupokea taarifa hiyo litahudhuriwa na viongozi mbalimbali na kurushwa moja kwa moja kupitia vituo vya habari vya redio, televisheni na tovuti rasmi ya Ikulu ambayo ni www.ikulu.go.tz

Wananchi mnakaribishwa kutazama na kusikiliza matangazo hayo yatakayorushwa hewani kuanzia saa 3.30 Asubuhi kutoka Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Waziri Mkuu atembelea kiwanda cha kuunganisha matrekta wilayani Kibaha na Kuagiza Wakulima Wakopeshwe Ili Waweze Kununua Matrekta

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amezitaka benki mbalimbali nchini ikiwemo Benki ya Maendeleo ya Kilimo kutoa mikopo kwa vikundi vya kilimo ili viweze kupata fedha za kununulia matrekta.

Amesema Serikali imedhamiria kuimarisha Sekta ya kilimo ili kwenda sambamba na adhma yake ya kuwa nchi ya uchumi wa viwanda.

Waziri Mkuu ameyasema hayo jana Jumanne, Mei 23, 2017 wakati alipotembelea kiwanda cha kuunganisha Matrekta URSUS-TAMCO, Kibaha mkoani Pwani.

Alisema kiwanda hicho kinalenga kuboresha sekta ya kilimo nchini na kuongeza uzalishaji wa malighafi za viwandani kwa kuwa wakulima watakuwa na zana za kisasa.

Aidha, amevitaka vyuo vya kilimo nchini kununua matrekta hayo kwa lengo la kufundishia wanafunzi wake ili wanapohotimu wawe na uwezo wa kutumia zana hizo vizuri na kwenda kuwasaidia wakulima katika maeneo yao.

Pia Waziri Mkuu alitoa wito kwa Halmashauri nchini kuendelea kupanga matumizi bora ya ardhi kwa kutenga maeneo ya kilimo, uwekezaji, makazi, biashara na huduma za jamii, hivyo kuepuka migogoro ya ardhi kwa siku zijazo.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) Bw. Mlingi Mkucha alisema wataunganisha matrekta 2,400, harrow 2,400 na majembe 2,400 katika mradi huo wa kiwanda cha kuunganisha matrekta URSUS-TAMCO ikiwa ni mkataba wa awali.

Alisema kiwanda hicho kina wafanyakazi 27 kwa hatua za mwanzo. Aidha, idadi hiyo itaongezeka kutokana na mahitaji ambapo baadhi ya wafanyakazi watapewa mafunzo nchini Poland na watakaporudi watakuwa wakufunzi wa watakaoajiriwa.

Mkurugenzi huyo aliongeza kuwa kiwanda hicho kimeazima wafanyakazi wengine wakiwemo watano kutoka Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, 10 kutoka vyuo mbalimbali vya ufundi nchini, wawili kutoka CAMARTEC ambao wanashirikiana na wataalamu 10 kutoka URSUS kuunganisha matrekta.

Bw. Mkucha alisema wafanyakazi 10 kutoka Tanzania wanatarajiwa kwenda nchini Poland kufanya mafunzo mahsusi na watakaporejea watakuwa wakufunzi kwa watumishi wengine watakaoajiriwa katika kiwanda hicho.

Alisema mbali na ujenzi wa kiwanda hicho cha kuunganishia matrekta ya URSUS, mradi unahusisha uanzishwaji wa vituo vinane kwa ajili ya kutoa huduma kwa wateja na kuuzia matrekta, zana na vifaa vingine.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Everest Ndikilo alisema miongoni mwa changamoto zinazoikabili sekta ya viwanda mkoani humo ni pamoja na kukatika kwa umeme, hivyo ameliomba Shirika la Umeme Tanzania (TANECO) kuongeza vituo vya kupozea umeme.

Awali Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mheshimiwa Charles Mwijage alisema kwa sasa nchini kuna viwanda vikubwa 393 kati yake 84 viko mkoani Pwani, ambapo amewaomba viongozi wa mkoa huo kutenga maeneo kwa ajili ya wanawake na vijana kuanzisha viwanda vidogo.

Mara baada ya kutembea kiwanda cha kuunganisha matrekta URSUS-TAMCO Waziri Mkuu alitembelea eneo la uwekezaji la Kamal (Kamal Indusrial Estate) lililoko katika Kata ya Kerege wilayani Bagamoyo.


Rais Magufuli Afanya Uteuzi wa Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI- Elimu)

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 24 Mei, 2017 amemteua Bw. Tixon Tuliangine Nzunda kuwa Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) -  anayeshughulikia Elimu.

Kabla ya uteuzi huo Bw. Tixon Tuliangine Nzunda alikuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa.

Bw. Tixon Tuliangine Nzunda anachukuwa nafasi ya aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) -  akishughulikia Elimu Bw. Bernard Makali ambaye ameteuliwa kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa.

Uteuzi huu unaanza mara moja.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

24 Mei, 2017

Taarifa ya TANESCO kuhusu katizo la umeme Mikoa ya Kinondoni Kaskazini, Ilala na Temeke.

LIVE: Rais Magufuli Anapokea Ripoti ya Madini Katika Makontena ya Mchanga

$
0
0
Fuatilia maangazo ya moja kwa moja toka Ikulu ambapo Mhe. Rais Magufuli anapokea Taarifa ya KAMATI Maalum aliyoiunda kuchunguza mchanga ulio katika makontena ya mchanga wa madini (Makinikia) yaliyopo katika maeneo mbalimbali Nchini.

Fuatilia moja kwa moja hapo chini

Jipatie Dawa za Asili za Kupunguza Maziwa, Kupunguza tumbo, Kuongeza nguvu za Kiume na Mvi

$
0
0
NATURAL BEAUTY COSMETIC ni kampuni inayotoa bidhaa ORIGINAL zenye matokeo mazuri bila kemiko wala madhara yoyote bidhaa zetu zote zimetengenezwa Kwa mimea na matunda
 
🍉🍓🍇🍅🍊🍒🍍🌴🍐🧀🧀🧀🧀🍅🍇🍇🍇🍇🍇🍇🍐🍍🌳🍏🍐🌶🍉🍆🍆🍒.
Pata punguzo la bei kwa bidhaa hizi.
1. YODI PILLS _ Ni vidonge vya kuongeza hips na makalio @170,000/=
 
2. BOTCHO CREAM_ Ni dawa ya kupaka ya kuongeza shepu (hips na makalio) @150,000/=
 
3. BOTCHO MULT PLUS_ Hii ni dawa ya kunywa ya kuongeza shepu (hips makalio na mapaja) @200,000/=
4. PANNAMAS BREAST_ Ni dawa ya kupunguza maziwa na kuyasimamisha hata kwa walio nyonyesha. Inapatikana kwa Tsh @120,000/=
 
5. DISCREET_Hii ni kwa ajili ya kuondoa mvi milele na zisiludi tena. @120,000/=
 
6. BODY BOOSTER_Ni dawa ya kuongeza mwili mzima na kukupa hamu ya kula vizuri. Inapatikana kwa Tsh @130,000/=
 
7. LEG BOOSTER_Ni dawa ya kuongeza miguu kuwa (Chupa ya bia) @120,000/=
 
8. HAIR GROWTH STIMULATOR_ Ni mafuta ya kulefusha nywele na kuzuia kukatika ovyo. Yanapatikana kwa Tsh @100,000/=
 
9. MICRO COMPUTER_ Ni mkanda wa kupunguza tumbo na manyama uzembe. @170,000/=
 
10.HANDSOME UP ni kifaa kinachoongeza maumbile ya kiume  kwa 99% kwa size uipendayo wewe na kuimarisha misuli ya uume kwa @170,000/= tuu. 
 
11.MEN GELY YA KUPAKA. Hii inaongeza kwa wastani wa inch 6.5 na inapatikana kwa @120,000/=.  
 
12. SHARK POWER. Hii pia ni kwa ajili ya kuongeza maumbile  wastani wa inch 7.5 inapatikana kwa @135,000/=.
 
15. MAX MAN 2. Ni vidonge kwa ajili ya nguvu ambavyo vinasaidia sana hata kwa watu wenye kisukari na waliokua wakifanya sana master blashion. Pia huongeza hamu ya tendo la ndoa inapatikana kwa @130,000/=
🌳🍉🍌🍅🍍🍐🍓🍆🍐🍒🍒🍓🍓🍑🍍🍍🍓🍓🍓🍍🍐🍐🍈🍉
         Tupo DAR ES SALAAM  kariakoo na kinondoni kanisani. 
 
Kwa mawasiliano zaidi piga  0759029968 au 0659618585.
Popote ulipo utapata huduma zetu.
 
                 Follow us
@natural2162
@natural2162
@natural2162
@natural2162
 
     Bidhaa zetu zote ni garantii na unapewa risiti
              Karibu

Breaking News Rais Magufuli amtaka Waziri Prof. Muhongo ajiuzulu

$
0
0
Rais John Magufuli amemtaka Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo kuachia madaraka kwa kushindwa kusimamia suala la mchanga wa dhahabu unaosafirishwa kwenye makontena.

Amemtaka waziri huyo kujitathimini na bila kuchukua muda mrefu aachie madaraka kutokana na suala hilo.

Rais Magufuli amesema hayo baada ya kamati iliyokuwa ikichunguza suala la mchanga kwenye makontena kukabidhi ripoti yao.

Kamati hiyo ya wataalamu wa jiolojia na uchambuzi wa kisayansi iliyoundwa Machi 29 mwaka huu, ilichunguza aina ya madini yaliyopo, kiasi na viwango vya ubora.

Akikabidhi ripoti hiyo, Profesa Mruma amesema uchunguzi huo umebaini uwepo wa madini ya kiasi cha kati ya Sh829.4 bilioni mpaka 1.439 Trillion kwa makontena yote 277.

"Licha ya uchunguzi uliofanywa kupitia makontena haya, tumegundua uwepo wa aina nyingi zaidi za madini ambayo hayakuwa yakijulikana na haya yamekutwa na thamani ya kati Sh129.5 bilioni mpaka261 bilioni," amesema Profesa Mruma.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images