Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Masoud Kipanya: Hakuna mwanaume Anayeridhika na Mwanamke mmoja. ....Ukiona katulia na mmoja basi ana matatizo au uchumi umekaa vibaya

$
0
0
Mtangazaji na Mchoraji katuni maarufu nchini Tanzania,Masoud Kipanya amewaaacha watanzania midomo wazi kwa kuweka wazi maoni yake kuwa mwanaume hawezi kuridhika na mwanamke mmoja.

Masoud amesema tangia zamani wanaume ni Watu mwenye tamaa hivyo hakuna mwanaume ambae anapenda kuwa na mwanamke mmoja ila ni vitu vidogo vidogo tu vinavyozuia kama dini ya Kikristo na masuala mengine ya kiuchumi.

“Hakuna mwanaume anaependa kuwa na mwanamke mmoja,na hiyo ndiyo huruka ya uanaume,tunajizuia tu kwa sababu!! hivyo kwa mfano kwa wenzangu wakristo utaratibu unawazuia lakini angalia vidumu vilivyo nje unaona eeehh??“Amesema Masoud Kipanya kwenye Mahojiano yake na Kwanza TV.

Hata hivyo Masoud alizungumzia suala la idadi ya kuzaa watoto kwenye familia na kusema kuwa kwa upande wake  yeye hana kikomo kwenye kuzaa kwani anaamini watoto hawarishwi na yeye bali wanarishwa na mwenyezi Mungu.

Masoud Kipanya kwa mujibu wa Takwimu za mwaka jana zilizofanywa na kituo cha Clouds FM kupitia kipindi cha XXl ni moja ya watu watatu maarufu nchini Tanzania wanaoendesha magari ya kifahari akiwa anamiliki gari aina ya Hummer H3.

==>Msikilize hapo chini akiongea

Sugu: Bashite Amekataliwa na Jamii Yote, Wasanii Acheni Kutumika

$
0
0
Mbunge wa mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (Chadema), amewataka wanasiasa kutowatumia vibaya wasanii kwa manufaa yao binafsi. Amesema Bashite ni mtu aliyekataliwa na jamii, hivyo wasanii wasikubali kutumika kumsafisha.

Ameyasema hayo jana Bungeni Mjini Dodoma alipokuwa akisoma hotuba ya kambi rasmi ya upinzani kuhusu Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo.

Aidha, Sugu amemtaka msanii ‘Roma’ kujitokeza hadharani kusema ukweli ni kipi kilichotokea na ni nani aliyehusika katika tukio hilo la utekwaji wake na wenzie.

“Wanasiasa tunatakiwa tuwaheshimu wasanii kwani ni kioo cha jamii, kuwatumia na kuwaterekeza mtakuwa hawatendei haki,”amesema Mbilinyi.

==>Msikilize Hapo Chini Akiongea

Habari Mbaya: Wanafunzi 20 wahofiwa kufa katika ajali ya basi Karatu

$
0
0
Wanafunzi zaidi ya 20 wanahofiwa kupoteza maisha katika ajali ya basi iliyotokea wilayani Karatu leo asubuhi.
Habari zinaarifu kuwa , basi hilo limeanguka kabla ya kuingia karatu mjini na kuua watoto wengi .

Inaarifiwa kuwa Wanafunzi hao  ni wa shule inayoitwa Lucky Vicent ya Arusha ambao walikua wanaenda karatu kufanya mitihani ya mashindano na shule za karatu.

Picha za utupu za Diane Rwigara anayetaka kuwa Rais Rwanda zavuja

$
0
0
Picha za utupu za Diane Shima Rwigara zimezagaa katika makundi ya Whatsapp mjini Kigali, Rwanda.

Rwigara, 35, ni msichana ambaye juzi alitangaza nia yake ya kugombea urais katika uchaguzi utakaofanyika Agosti, 2017.

Picha zake za utupu zimetumwa kama barua-pepe kwa vyombo vya habari na mtu aliyejiita Twahirwa Emmy.

Bw Twahirwa amejitambulisha kuwa ni mwandishi wa habari aliyechukizwa na maadili ya mgombea huyo mtarajiwa.

Ingawaje hakuna chombo cha habari kilichorusha picha hizo kufikia sasa, lakini zimekuwa ‘habari ya mjini’ baada ya kutapakaa katika mitandao ya kijamii hususan Whatsapp.

Picha moja inamuonesha msichana huyo akiwa amekaa kwenye sofa nyumbani sehemu isiyojulikana, akiwa hajavaa chupi wala sidiria.

Picha nyingine inamuonesha akiwa amesimama huku ameyashika maziwa yake.

Ni picha ambazo zitakuwa zimepigwa na mtu wake wa karibu kwani inavyoonekana hazijapigwa kipaparazi.

Msichana huyo anaonekana pichani akiwa anamuangalia mpiga picha.Picha ya tatu inawaonesha watu wanne wakiwemo waandishi wa habari watatu wanaojulikana nchini Rwanda.

Mtuma picha ameahidi kutuma nyingine akidai lengo lake ni kuufahamisha umma kuwa mtu anayepiga picha za utupu hafai kupewa dhamana ya kuongoza nchi.

Rwigara ni msichana wa mfanyabiashara mashuhuri Asinapol Rwigara aliyefariki katika ajali ya barabarani mnamo Februari 2015.

Juzi, Jumatano, alitangaza nia yake ya kuwania urais, akiwaahidi Wanyarwanda kupambana na umaskini huku akiupa kipaumbele uhuru wa maoni endapo watamchagua.

Credit: Habari Pevu

Update: Wanafunzi Waliofariki Katika Ajali Leo Wafika 31

$
0
0
Kamanda wa Polisi, mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo amesema wanafunzi 31 na walimu wao wamefariki katika ajali iliyotokea wilayani Karatu, ulipo mto Mlera.

Mkumbo amesema wanafunzi waliopoteza maisha katika ajali hiyo ni wa shule ya mchepuo wa Kiingereza, iitwayo Luck Vicent ya mjini Arusha.

Kati ya wale waliofariki 28 walikuwa wanafunzi huku watatu wakiwa ni dereva na walimu wao

Ripoti zinasema kuwa basi hilo liliteleza na kukosa mwelekeo ,likatoka katika barabara na kuanguka katika mto katika eneo la Marera eneo la Rhotia, kilomita chache kabla ya karatu katika barabara ya Arusha

Lowassa awalilia wanafunzi Waliofariki katika Ajali........Maiti 32 zapelekwa mochwari katika Hospitali ya Lutheran Karatu.

$
0
0
Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa ametuma salamu za rambi rambi kutokana na tukio la watu 32 kufariki dunia katika ajali ya basi.

Waliofariki katika ajali hiyo iliyotokea leo asubuhi Karatu, ni wanafunzi 29, walimu wawili, pamoja na dereva wa gari hilo.

“Nimepokea kwa masikitiko taarifa ya ajali hiyo, ni ajali mbaya ambayo inaifanya siku hii kuwa mbaya katika historia ya nchi yetu,”alisema

Miongoni mwa wanafunzi waliofariki ni pamoja na wanaume 11 na wasichana 18.

Kadhalika maiti 32 zikiwamo za walimu wawili, dereva mmoja na wanafunzi 29 zimepokelewa sasa hivi katika Hospitali ya Lutheran Karatu.


Majina ya wanafunzi waliofariki katika ajali ya basi Karatu

$
0
0
Wanafunzi 29 , walimu 2 na dereva wa gari la shule ya msingi iitwayo Lucky Vicent ya Arusha wamefariki dunia leo saa 3 asubuhi baada ya gari walilokuwa wakisafiria kupata ajali katika eneo Rhotia Marera, Wilaya ya Karatu Mkoani Arusha.

Wanafunzi na walimu hao walikuwa wakitoka shuleni kwao kwenda shule ya msingi iitwayo Tumaini kwa ajili ya kufanya mtihani wa ujirani mwema na walipofika katika eneo la Rhotia Marera basi walilopanda liliacha njia na kisha kutumbukia korongoni ambako limesababisha vifo hivyo na majeruhi watatu.

Hapa chini ni majina ya wanafunzi waliofariki katika ajali hiyo

Rais Magufuli atuma salamu za rambirambi vifo vya wananfunzi 32

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amepokea kwa mshtuko na masikitiko makubwa taarifa ya vifo vya wanafunzi 32 wa darasa la saba, walimu 2 na dereva wa gari la shule ya msingi iitwayo Lucky Vicent ya Arusha vilivyotokea leo saa 3 asubuhi baada ya gari walilokuwa wakisafiria kupata ajali katika eneo Rhotia Marera, Wilaya ya Karatu Mkoani Arusha.

Wanafunzi na walimu hao walikuwa wakitoka shuleni kwao kwenda shule ya msingi iitwayo Tumaini kwa ajili ya kufanya mtihani wa ujirani mwema na walipofika katika eneo la Rhotia Marera basi walilopanda liliacha njia na kisha kutumbukia korongoni ambako limesababisha vifo hivyo na majeruhi watatu.

Kufuatia ajali hii, Mhe. Rais Magufuli amemtumia salamu za rambirambi Mkuu wa Mkoa wa Arusha Bw. Mrisho Gambo na kueleza kuwa ajali hiyo imezima ndoto za watoto waliokuwa wakijiandaa kulitumikia Taifa na imesababisha uchungu, huzuni na masikitiko makubwa kwa familia za marehemu na Taifa kwa ujumla.

“Ndg Mkuu wa Mkoa wa Arusha Bw. Mrisho Gambo naomba unifikishie pole nyingi kwa wazazi, ndugu, jamaa na marafiki wote wa wanafunzi, walimu na dereva waliopoteza maisha, hiki ni kipindi kigumu kwetu sote, na uwaambie naungana nao katika majonzi na maombi.

“Muhimu kwa sasa tuwaombee marehemu wote wapumzishwe mahali pema, majeruhi wapone haraka na wote walioguswa na msiba huu wawe na moyo wa subira, ustahimilivu na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu” Amesema Mhe. Rais Magufuli.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
06 Mei, 2017

Zitto na ACT Wazalendo watuma salamu za rambirambi kufuatia vifo vya wanafunzi 32

$
0
0
Picha: Wajumbe wa Kamati ya Chama cha ACT Wazalendo, wakiwa wamesimama kuomboleza na kuwakumbuka wote waliopoteza maisha katika Ajali hii.

Mbunge wa Kigoma mjini kwa tiketi ya ACT Wazalendo Zitto Kabwe na Chama Chake cha ACT Wazalendo wametuma salamu za rambirambi kufuatia kutokea kwa ajali mbaya ya basi dogo ambalo limepelekea vifo vya wanafunzi 29, walimu 2 na dereva mmoja wa gari hiyo.

Zitto Kabwe katika salamu zake za rambirambi anasema kuwa huu ni msiba mkubwa kwa taifa.

"Moyo wangu umesinyaa baada ya kusikia Taarifa za ajali ya watoto wetu huko Karatu. Natoa salaam zangu za rambirambi kwa Wazazi wa wanafunzi wa shule ya St. Lucky na Kwa ndugu na familia za walimu na wafanyakazi wa shule waliopoteza maisha. Huu ni msiba mkubwa sana. Huzuni haielezeki. Nawaombea Kwa Mola awape wazazi na ndugu wote moyo wa subira katika mtihani huu. Ni msiba wa Taifa zima" alisema Zitto Kabwe

Katika taarifa ya Chama Cha ACT Wazalendo pia imetoa pole kwa wanafamilia, walimu

"Chama cha ACT Wazalendo kimepokea kwa majonzi na simanzi kubwa taarifa ya vifo vya wanafunzi, walimu pamoja na wafanyakazi wa Shule ya awali na msingi ya Lucky Vicent ya Jijini Arusha, vifo vilivyotokana na ajali ya basi iliyotokea katika wilaya ya Karatu mkoani Arusha. ACT Wazalendo tunatoa pole kwa wazazi waliopoteza watoto wao, ndugu na jamaa waliopoteza walimu na wafanyakazi wa shule hiyo, pamoja na watanzania wote kwa ujumla. Pia tunawaombea majeruhi wote wa ajali hii wapate kupona kwa haraka" alisema Abdallah Khamis Afisa Habari wa ACT Wazalendo

CHADEMA watuma salamu za rambirambi kufuatia vifo vya Wanafunzi 32

$
0
0
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kupitia Mkurugenzi wa Itikadi, Mawasiliano na Mambo ya Nje, John Mrema wametuma salamu za rambirambi kufuatia kutokea kwa ajali mbaya iliyotokea leo na kusababisha vifo vya watu 32.

Katika salamu zao cha CHADEMA wamesema wamepokea taarifa hizo kwa masikitiko makubwa kwani taifa limepoteza watu muhimu ambao wangelitumikia taifa katika siku zijazo.

"Tumepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za ajali mbaya Iliyotokea Leo tarehe 6 Mei,2017 Mkoani Arusha, Wilaya ya Karatu na kusababisha vifo vya wanafunzi 33 (watoto wa kike 16 na watoto wa kiume 17) waliokuwa wanafunzi wa Shule ya Lucky Vicent ya Mkoani Arusha.....Hakika taifa limepoteza watoto wake na vijana wa Kesho ambao wangelitumikia taifa letu siku zijazo". Alisema Mrema

Aidha, chama cha CHADEMA pia wametoa pole kwa familia ya wafiwa, uongozi wa shule ya Lucky Vicent pamoja na wananchi kwa ujumla.
 
"Kwa majonzi makubwa tunatoa salamu za pole kwa wazazi, wanafunzi wa Shule ya Lucky Vicent,  uongozi wa Shule hiyo pamoja na wananchi wote wa Tanzania kwa msiba huu mkubwa na wenye kutia simanzi na huzuni kubwa...CHADEMA tutakuwa pamoja na familia za Marehemu katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo , tunawataka wanachama na watanzania wote bila kujali imani zetu tuwakumbuke wafiwa katika Sala /Dua ili Mwenyezi Mungu awatie ujasiri wafiwa katika kipindi hiki kigumu". Alisema Mrema

Pamoja na hayo, CHADEMA wamelitaka jeshi la polisi kufanya uchunguzi wa kina juu ya chanzo cha ajali hiyo mbaya ili matokeo ya uchunguzi huo yatumike katika kuzuia ajali nyingine  isije kutokea katika siku zijazo.

TTCL kuzima mitambo yote ya CDMA kesho

Bunge latoa pole kwa wanafunzi 32 Waliofariki Arusha

$
0
0
Spika wa Bunge, Job Ndugai amemtumia salamu za rambirambi kwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo kufuatia vifo vya wananafunzi, walimu na dereva  wa Shule ya Msingi Lucky Vicent, baada ya gari walilokuwa wakisafiria kupata ajali leo asubuhi katika eneo la Rhotia Marera, wilayani Karatu mkoani Arusha.

“Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa nakupa pole sana, nimepokea kwa mshtuko taarifa hii ya ajali iliyogharimu maisha ya watoto wetu, hakika hili ni pigo kwa Taifa zima, namuomba Mungu azilaze roho za marehemu mahali pema peponi,” amesema Ndugai na kuongeza:

 “Natoa pole kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki waliopoteza wapendwa wao, Mwenyezi Mungu awape nguvu na faraja katika kipindi hiki kigumu, vilevile nawaombea majeruhi wote wa ajali hiyo wapate uponyaji wa haraka.”

LIVE: Taarifa ya Habari ya TBC Sa mbili Usiku huu wa May 6

$
0
0
Sikiliza hapa taarifa ya habari ya TBC saa mbili usiku huu

Barua ya Bodi ya Ligi kuhusu sakata la alama tatu kati ya Kagera Sugar na Simba SC.

$
0
0
Bodi ya Ligi ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) imewajibu rasmi Simba SC juu ya sakata lao la kupokwa pointi tatu za mezani walizopewa baada ya rufaa yao dhidi ya Kagera Sugar wakidai kumcheza mchezaji Mohamed Fakhi akiwa na kadi tatu za njano.
 
Kwa mujibu wa barua kutoka katika Bodi ya Ligi zimesema kuwa Fakhi hakuwa na kadi tatu za njano wakati akicheza mchezo dhidi ya Simba uliofanyikia uwanja wa Kaitaba, Bukoba Aprili 2 mwaka huu.

"TFF ambayo ndiyo yenye dhamana ya usimamizi wa mpira nchini na ambayo ndiyo iliyokaimu madaraka kwa TPLB kuendesha ligi kuu iliitisha kikao cha Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ambayo ilichunguza kwa undani sakata hili na baada ya uchunguzi wao ambao walihoji watu mbalimbali, walituandikia kutujulisha kuwa wamebaini mchezaji Mohamed Fakhi anayelalamikiwa na Simba hakuwa na kadi 3 siku ya mchezo wa Kagera Sugara dhidi ya Simba hivyo alikuwa halali kucheza mchezo huo". Ilisema barua hiyo

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya May 7


Rais Magufuli Awapa Tumaini Jipya Wafanya Biashara

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli jana tarehe 06 Mei, 2017 alizindua Baraza la Taifa la Biashara (TNBC) na kuongoza Mkutano wa 10 wa Baraza hilo uliofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Baraza hili ni la tatu na mkutano huu ni wa kwanza kuongozwa na Mhe. Rais Magufuli tangu aingie madarakani ambapo tofauti na mikutano mingine, Mhe. Rais Magufuli aliendesha majadiliano ya pamoja ambapo wajumbe wa baraza na wawakilishi wengine kutoka sekta binafsi walipata fursa ya kutoa maoni, mapendekezo na dukuduku, kisha kupatiwa majibu kutoka kwa Mawaziri, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa na Mhe. Rais.

Miongoni mwa yaliyojitokeza ni kuiomba Serikali kuendelea kushirikiana na sekta binafsi katika upangaji na utekelezaji wa mipango, sera na sheria mbalimbali za uwekezaji na biashara, kuendelea kuondoa vikwazo na urasimu ambao unachangia kupunguza ufanisi katika biashara na uwekezaji, kuongeza vivutio vya uwekezaji na kuendelea kushirikisha sekta binafsi katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo ujenzi, utalii na viwanda.

Aidha, wawakilishi wa sekta binafsi waliipongeza Serikali ya Awamu ya Tano kwa juhudi kubwa inazozifanya kujenga miundombinu muhimu kwa uwekezajina biashara kama vile ujenzi wa reli, barabara, meli na ununuzi wa ndege, kukabiliana na rushwa, kusimamia mpango wa ujenzi wa viwanda, kujenga nidhamu na uwajibikaji wa watumishi wa umma na kujenga uhusiano mzuri na mataifa mbalimbali duniani.

Pamoja na majibu yaliyotolewa na Mawaziri ambao ni wajumbe wa Baraza la Taifa la Biashara, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa amewaahidi wawakilishi wa sekta binafsi waliohudhuria mkutano huo kuwa Serikali itahakikisha maoni yao yote yanafanyiwa kazi ili Taifa liweze kunufaika na rasilimali zake na kusonga mbele kimaendeleo.

“Naomba niwahakikishie kuwa hisia zenu tumezipata, maoni yenu tutayazingatia na tutahakikisha tunayafanyia kazi haraka iwezekanavyo ili kwa pamoja tufanye kazi ya kuijenga nchi yetu” alisema Mhe. Majaliwa.

Mhe. Rais Magufuli aliwapongeza wajumbe wa Baraza la Taifa la Biashara pamoja na Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) inayoongozwa na Mwenyekiti wake Dkt. Reginald Mengi kwa juhudi kubwa zinafanywa kuendeleza biashara na uwekezaji nchini na amewaahidi kuwa Serikali ya Awamu ya Tano itaendelea kuwathamini na kushirikiana na wawekezaji na wafanyabiashara kwa manufaa ya Taifa.

Mhe. Rais Magufuli alielezea kufurahishwa na maoni, mapendekezo na dukuduku alizozipata kutoka kwenye mkutano huo na amewakikishia kuwa Serikali anayoiongoza itafanyia kazi maoni yote yaliyotolewa ikiwemo kuondoa usumbufu unaosababishwa na uwingi wa taasisi zinazomhudumia na kumtoza mfanyabiashara na mwekezaji, kuongeza vivutio, kuboresha mifumo ya ukusanyaji wa kodi mbalimbali na kuishirikisha sekta binafsi katika mipango na utekelezaji wa miradi.

Kuhusu tatizo la ucheleweshaji wa mizigo bandarini Mhe. Rais Magufuli aliagiza kuanzia Jumatatu tarehe 08 Mei, 2017 taasisi zote zinazotoa huduma katika bandari ya Dar es Salaam ziungane na Mamlaka ya usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kutoa huduma kwa muda wote wa saa 24.

“Kama alivyosema Waziri Mkuu, tunataka kufanyia kazi maoni yenu mara moja, kuanzia Jumatatu nataka taasisi zote za pale bandarini zitoe huduma saa 24, haiwezekani bandarini kwetu mizigo ichukue siku 13 kuitoa bandarini wakati bandari za wenzetu majirani inatoka baada ya siku 3, tutashindana vipi?” alihoji Mhe. Rais Magufuli.

Hata hivyo Mhe. Dkt. Magufuli aliwataka wafanyabiashara na wawekezaji wajirekebisha kwa kasoro ambazo baadhi yao wanazo ikiwemo ukwepaji wa kodi, kupandisha viwango vya bei kwa huduma wanazotoa Serikalini, kujihusisha na rushwa, kutaka faida kubwa isiyostahili bila kuwajali wananchi na kutochangamkia fursa za uwekezaji za ndani na nje ya nchi licha ya juhudi zake za kuwaleta viongozi na wafanyabiashara kutoka nchi mbalimbali.

“Nataka mjiulize amekuja Waziri Mkuu wa India, amekuja Rais wa Vietnam, amekuja Rais wa Uturuki, amekuja Rais wa Kongo (DRC), amekuja Rais wa Zambia, amekuja Rais wa Uganda, amekujaMfalme wa Morocco na wengine wengi, tumenufaikaje? Mbona wao wanakuja kuwekeza hapa nyie kwa nini hamuendi kwao?” alihoji Mhe. Rais Magufuli.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

Sakata la Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana Laibuka Bungeni.............Ni baada ya Godbless Kulianzisha Huku Akidai Amefichwa

$
0
0
Kauli aliyoitoa bungeni juzi usiku mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema kuwa Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana amefichwa ilisababisha mawaziri wawili wa sasa na mmoja wa zamani wamkomalie kuifuta.

Bunge lilikuwa likijadili Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.

Awali, Lema alisema ameona kwenye mitandao juu ya Kinana kufichwa na kupaza sauti akitaka kumtetea akiwa kama Waziri Kivuli wa Mambo ya Ndani.

Hata hivyo, kauli hiyo ilimsimamisha Waziri wa Tamisemi, George Simbachawene akitumia kanuni ya 64 (2) ambayo alisema inatoa nafasi kukumbusha Bunge kwamba kuna kanuni inayovunjwa.

“Mbunge anayezungumza anasema jambo ambalo hana uhakika nalo, linatia mashaka, sidhani kama ana uhakika kwamba Kinana amefichwa. Alithibitishie Bunge hili na kama hawezi kuthibitisha, kupitia kanuni ya 72 (2) nakuomba Mwenyekiti umtake afute maneno hayo,” alisema Simbachawene.

Ufafanuzi huo ulimuinua kitini Tundu Lissu na kusema Simbachawene hajui atendalo, Mungu amsamehe.

“Kanuni ya 72 (2) inasema mbunge atakayekiuka utaratibu uliowekwa na kanuni hizi anaweza kutakiwa na Spika hapohapo afuate utaratibu au mbunge atasimama kwa kutumia utaratibu huo na kutaja kanuni iliyokiukwa,” alisema Lissu.

Baada ya maelezo hayo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenister Mhagama ambaye ni mnadhimu mkuu wa Serikali aliweka msisitizo kwenye kanuni ya 64 (1) (a) ambayo inakataza mbunge kutotoa taarifa ambazo hazina ukweli.

“Naomba nimthibitishie mheshimiwa Lema kwamba Kinana tumezungumza naye wakati wa maadhimisho ya Muungano, wakati wa maadhimisho ya Mei Mosi. Kinana ametoka kwenye matibabu na sasa anapumzika nyumbani kwake.

Alipomaliza kuzungumza Jenister aliinuka Mbunge wa Newala (CCM), George Mkuchika ambaye aliwahi kuwa waziri wa wizara mbalimbali katika Serikali ya Awamu ya Nne na kuomba mwongozo wa mwenyekiti kuwa tangu Lema aanze kuchangia hakuwa anazungumzia jambo lililoko mezani, yaani bajeti ya wizara ya habari.

“Mheshimiwa Lema tangu ameanza hakuzungumza habari zozote kuhusu wizara. Mimi kwa umri huu hata ukinizomea siachi kuzungumza. Mheshimiwa Mwenyekiti naomba muongozo wako kuhusu kanuni ya 64 (b) inayosema mbunge hatazungumzia jambo nje ya mjadala.

Akitoa mwongozo wake Mwenyekiti wa Bunge, Azzan Zungu alisema kwa mujibu wa kanuni hizi 68 (10) Spika ndiye mwenye uamuzi wa mwisho kuhusu masuala yote ya kanuni, kwa hiyo akamtaka Lema afute maneno hayo na Lema aliyafuta akisema anafanya hivyo kwa kuwa waziri amemhakikisha kwamba Kinana hajatekwa.

Bashe awalilia wanafunzi 32 waliofariki Katika Ajali

$
0
0

Mbunge wa Nzega Mjini (CCM), Hussein Bashe ametoa pole kwa familia zilizopatwa na msiba kufuatia ajali iliyotokea jana Jijini Arusha na kusababisha vifo zaidi ya 30.

Mbunge huyo kupitia ukurasa wake wa Instagram amesema kwa niaba ya wananchi wa jimbo la Nzega amewatia moyo wanafamilia wote na Taifa kwa ujumla kufuatia msiba huu na kuwataka watanzania wote kuwa tayari kwa safari hii.

"Kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Nzega niwape pole familia za watoto hawa waulim na madereva ambao mwenyezi Mungu amewaita mbele ya haki" - Hussein Bashe.

"Kila nafsi itaonja mauti na mwenyezi Mungu amewaita hawa binadaam wenzetu katika umri mdogo wakati wazazi wao, familia zao na Taifa likiwa na matarajio makubwa na matumaini makubwa, ila Allah hutupima imani zetu kwa majaribu makubwa kama haya, tumshukuru kwa kila jambo na sisi tujiandae kwa safari hii ya asili na kimaumbile" - aliongeza Bashe.

"Poleni wanafamilia, poleni walimu, poleni watanzania wote"- Hussein Bashe.

Serikali yagharamia msiba wa wa Wanafunzi 32 Waliofariki Arusha

$
0
0
Serikali ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania imegharamia Sanda pamoja na majeneza kwa ajili ya Wanafunzi wa Shule ya Lucky Vicent waliopoteza maisha mapema jana kwenye ajali iliyokuwa ikihusisha safari ya kimasomo.

Akitoa taarifa hiyo leo Meya wa Jiji la Arusha , Mh. Calist Lazaro amesema kuwa taarifa za awali zinaonyesha kuwa tayari Serikali imekwishalipia gharama za majeneza na sanda ya kuhifadhia miili ya marehemu ambao kesho wanatarajiwa kufanyiwa ibada katika Uwanja wa mpira wa Sheikh Amri Abeid.

Shule ambayo wanafunzi wake wamefariki yafungwa

$
0
0
Shule ya Lucky Vicent imefungwa kwa siku saba kufuatia vifo vya wanafunzi wake 32 vilivyotokea kwenye ajali ya gari jana Karatu.

Kutokana na ajali hiyo Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema na wabunge wengine wa Chadema wamefika shuleni hapo kutoa pole.

Lema kwa niaba wabunge ameeleza kusikitishwa na msiba huu na amewapa pole wafiwa lakini akatoa angalizo kusiingizwe siasa katika msiba huu mkubwa.

Meya wa jiji la Arusha Kalist Lazaro ameeleza kuwa Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu, Waziri wa Tamisemi, George Simbachawene na Waziri wa Elimu, Profesa Joyce Ndalichako watafika jioni kuzungumza na wafiwa.

Kesho Makamu wa Rais Samia Suluhu kwa niaba ya Rais John Magufuli ataongoza kazi kuaga miili ya wanafunzi hao Uwanja wa Sheikh Amri Abeid.

Mkuu wa shule hiyo, Ephraem Jackson amesema  hadi sasa vifo ni 36 na wanafunzi wawili bado wamelazwa Hospitali ya Mkoa ya Mount Meru. Wanafunzi hao ni Sadiely Ismail na Wilson Tarimo.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images