Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya May 5
↧
↧
Mbunge John Heche Azidiwa Ghafla na Kukimbizwa Muhimbili
Mbunge wa Tarime Vijijini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), John Heche ameshindwa kuendelea kuhudhuria vikao vya Bunge vinavyoendelea mjini hapa, kutokana na matatizo ya kiafya na kulazimika kukimbizwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) jijini Dar es Salaam.
Heche alipata tatizo la afya na kufikishwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma jana alfajiri. Kwa mujibu wa Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo, Dk Caroline Damian alikiri kuwa Heche, alipokewa hospitalini hapo alfajiri ya jana na kuhudumiwa kwa muda kabla hajasafirishwa kupelekwa mahali ambako hakuwa tayari kupataja.
“Hatujampa rufaa ila matibabu yake yanaratibiwa na Kliniki ya Bunge, hivyo tulimpokea na kumhudumia kwa muda kabla taratibu za kumsafirisha hazijakamilika, tulipoambiwa ndege ya kumsafirisha ipo tayari, aliondolewa kwetu na kusafirishwa kwa ajili ya matibabu,” alieleza daktari huyo.
Awali, mbunge huyo alipata tatizo la afya na kulazimika kuwa chini ya uangalizi wa kitabibu. Awali, Naibu Katibu Mkuu wa Chadema Zanzibar, Salum Mwalimu, alikaririwa na vyombo vya habari hivi karibuni akijibu maswali ya wananchi walihoji hali ya mbunge huyo, ambaye ilikuwa ikielezwa kuwa hospitalini.
Kabla ya muda huo kuwadia, ilielezwa kuwa Heche alipata maumivu ya tumbo kabla hajapelekwa katika Hospitali ya Rufaa ya Taifa ya Muhimbili ambako alifanyiwa upasuaji.
Kwa upande wake, Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Chadema Taifa, Tumaini Makene jana alithibitisha taarifa ya kuugua ghafla kwa Heche na kuletwa jijini Dar es Salaam katika hospitali hiyo.
“Ni kweli Heche aliugua ghafla akiwa Bungeni huko Dodoma, alisafirishwa kwa ndege jana asubuhi saa moja na kuletwa Muhimbili ambako anaendelea na matibabu,” alisema Makene.
Ofisa Habari wa Muhimbili, Neema Mwangomo alithibitisha kupokelewa Heche jana saa nne asubuhi na kwamba anaendelea na vipimo kubaini nini tatizo lake.
↧
Jinsi Punyeto Inavyo Sababisha Ukosefu Na Upungufu Wa Nguvu za Kiume
Ukosefu na/ama upungufu wa nguvu za kiume, ni tatizo linalo wakabili mamilioni ya wanaume duniani. Zipo sababu nyingi zinazo sababisha tatizo la ukosefu wa nguvu za kiume.
Miongoni mwa sababu hizo ni pamoja na maradhi kisukari, presha,shinikizo la damu, moyo, figo, matatizo kwenye mishipa ya ubongo & mishipa ya uti wa mgongo, matatizo kwenye mishipa itumikayo kusafrisha damu mwilini, maradhi ya ngiri, pamoja na upigaji punyeto kwa muda mrefu.
Katika makala yetu ya leo, tutaangalia namna suala la upigaji punyeto linavyo athiri nguvu za kiume.
Kabla hatujaangalia namna suala la upigaji punyeto linavyo maliza nguvu za kiume, ni vyema tukafahamu kwanza kuhusu SAYANSI YA MFUMO WA NGUVU ZA KIUME.
Kufahamu kuhusu SAYANSI YA MFUMO WA NGUVU ZA KIUME tafadhali tembelea :
Ukisoma vizuri kuhusu mfumo wa nguvu za kiume, utagundua kuwa Suala la nguvu za kiume ni suala la kimfumo. Ili mwanaume awe na nguvu za kiume, aendelee kuwa na nguvu za kiume na azilinde nguvu zake za kiume, ni lazima ogani zote zinazo husika na mfumo wa nguvu za kiume ziwe na afya njema na ziwe na ushirikiano thabiti na wenye afya.
Vile vile , utagundua kuwa , mambo makuu muhimu katika mfumo wa nguvu za kiume ni kama ifuatavyo:
i.Mishipa imara ya ubongo na yenye afya njema
ii. Mishipa imara ya uti wa mgongo ( spinal cords )
iii.Mishipa imara itumikayo kusafirisha damu mwilini ( Blood Vessels )
iv. Mfumo imara wa usafirishaji damu mwilini
v. Mishipa ya uume iliyo imara na yenye afya njema
vi. Uhusiano imara na wenye afya kati ya mishipa ya fahamu iliyopo katika ubongo, mishipa ya kwenye uti wa mgongo pamoja na misuli & mishipa ya kwenye uume.
Hivyo basi, ili mwanaume aweze kuwa na nguvu imara za kiume, na aendelee kuwa na nguvu hizo ni lazima mambo yote muhimu katika mfumo wa nguvu za kiume yawe imara pasi na hitilafu yoyote.
Hitilafu yoyote katika mambo hayo, itasababisha ukosefu na/ama upungufu wa nguvu za kiume kwa mwanaume huyo. Pale inapotokea hitilafu ama mapungufu katika ogani zaidi ya moja kati ya zilizo tajwa hapo juu, basi tatizo kwa muhusika huwa kubwa mara dufu.
JINSI PUNYETO INAVYO SABABISHA TATIZO LA UKOSEFU & UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME.
Mwanaume anapopatwa na wazo la kufanya tendo la ndoa, ubongo hutoa ishara kwenye mishipa ya uti wa mgongo ambayo nayo husafirisha taarifa hadi kwenye mishipa & misuli ya uume.
Mishipa ya uume inapopokea taarifa hiyo, hutanuka. Na mishipa ya uume inapotanuka, hufanya mambo mawili muhimu sana :
i.Husababisha mishipa ya ateri kupanuka na hivyo kuruhusu damu kuingia kwa kasi sana ndani ya mishipa ya uume na hivyo kuufanya uume usimame na kuwa imara bara bara.
ii. Huibinya na kuiziba mishipa ya vena na hivyo kuzuia kunyonya ama kufyonza damu iliyo ingia ndani ya mishipa ya uume. ( KAZI KUBWA YA MISHIPA YA VENA ILIYO KARIBU NA MISHIPA YA UUME NI KUHAKIKISHA HAKUNA DAMU NDANI YA MISHIPA YA UUME. HIVYO BASI DAMU INAPOINGIA NDANI YA MISHIPA YA UUME, MISHIPA YA VENA HU “SENSE” JAMBO HILO KWA HARAKA NA HIVYO KUIFYONZA DAMU HIYO KUTOKA KWENYE MISHIPA YA UUME YA KUITOA NJE YA MISHIPA YA UUME. NA DAMU INAPOKOSEKANA NDANI YA MISHIPA YA UUME, HUUFANYA UUME KUSINYAA NA KULEGEA )
Mtu anayepiga punyeto husababisha mambo yafuatayo katika mwili wake :
1. Huuwa nguvu ya mishipa & misuli ya uume ambayo ndio inayo husika na kusimama kwa uume
2. Mishipa ya uume inapo sinyaa na kukosa nguvu yake ya asili, husababisha mambo yafuatayo :
i.Huondoa uwezo wa mishipa & misuli ya uume kutanuka, na hii ndio sababu inayo wafanya waathirika wa punyeto kutumia nguvu nyingi sana katika kuufanya uume usimame.
ii.Huondoa uwezo wa mishipa & misuli ya uume kuibana na kuiziba mishipa ya vena, na hii ndio sababu inayo fanya waathirika wa punyeto kufika kileleni haraka sana, kwani damu inayo ingia kwenye misuli ya uume hufyonzwa ndani ya muda mfupi sana.
Hii hutokea kwa sababu mishipa na misuli ya uume inakuwa imelegea,na mishipa ya vena inakuwa imepwaya, hivyo msuguano wowote ule hufanya mishipa ya vena kufunguka na kufyonza damu kutoka kwenye mishipa ya uume na hivyo kuufanya uume kusinyaa ndani ya dakika ama sekunde chache sana.
3. Vile vile punyeto hufanya uume kusinyaa na kurudi ndani na kuufanya uonekane kama uume wa motto mdogo.
Kwa ufupi punyeto husababisha ukosefu wa nguvu za kiume kwa sababu kuu zifuatazo :
i.Kwanza hudhoofisha na kuharibu mishipa ya uume, ambayo ndio hufanya uume kusimama.
ii.Pili hudhoofisha utendaji kazi wa mishipa ya ateri, ambayo ndio hutumika kama njia ya kusafirisha damu kupeleka kwenye misuli ya uume na ivyo kuufanya uume usimame
iii. Tatu, punyeto hupelekea kuvuja kwa mishipa ya vena na hivyo kusababisha damu kufyonzwa kwa haraka sana kila iingiapo ndani ya misuli ya uume na matokeo yake ni uume kusimama kwa muda mfupi sana wakati wa tendo la ndoa.
iv. Punyeto huathiri mtiririko wa damu kwenda kwenye mishipa ya uume, kwa sababu hudhoofisha misuli & mishipa ya uume pamoja na mishipa ya ateri ambayo ndio hutumika katika kusafirisha damu kwenda kwenye uume
DALILI ZA MTU ALIYE ATHIRIWA NA PUNYETO
Dalili kuu za mtu aliye athiriwa na punyeto ni kama ifuatavyo:
i. Uume kusinyaa na kuwa kama wa mtoto
ii. Uume kurudi ndani
iii. Uume kusimama ukiwa legelege
iv. Kufika kileleni haraka wakati wa tendo la ndoa.
TIBA YA NGUVU ZA KIUME KWA MTU ALIYE ATHIRIKA NA PUNYETO.
Dawa asilia ya nguvu za kiume iitwayo JIKO ni tiba bora na ya uhakika kabisa kwa mtu aliye athiriwa na punyeto. Dawa hii, pamoja na mambo mengine mengi, husaidia kufanya mambio yafuatayo katika mwili wa mwanaume aliye athiriwa na punyeto :
i.Kuimarisha mishipa & misuli ya uume ulio legea na hivyo kuurejeshea uwezo wake wa asili
ii. Hutibu tatizo la uume kurudi ndani
iii.Humaliza tatizo la kusimama kwa uume ukiwa legelege
iv.Hutibu na kuponya kabisa tatizo la kufika kieleleni haraka.
BEI YA DAWA : Dawa hii inapatikana kwa gharama ya SHILINGI ELFU THEMANINI TU (Tsh. 80,000/=)
MAHALI INAPOPATIKANA : Dawa hii inapatikana katika duka la dawa asilia liitwalo NEEMA HERBALIST & NUTRITIONAL FOODS CLINIC lililopo jijini DAR ES SALAAM katika eneo la UBUNGO nyuma ya jengo la UBUNGO PLAZA karibu na SHULE YA MSINGI UBUNGO NATIONAL HOUSING.
Kwa wateja wasio weza kufika ofisini kwetu. Watafikishiwa dawa mahali popote walipo jijini DAR ES SALAAM.
Kwa wateja waliopo mikoani watatumiwa dawa kwa njia ya MABASI
Kwa wateja waliopo Zanzibar wata fikishiwa dawa kwa njia ya usafiri wa boti.
Na kwa wateja waliopo UGHAIBUNI watatumiwa dawa kwa njia ya POSTA ama DHL.
MAWASILIANO : WASILIANA NASI KWA SIMU NAMBA 0766 53 83 84.
Kwa taarifa zaidi kuhusu huduma zetu, tutembelee kila siku kwenye blogu yetu :
↧
Wakandarasi wazalendo kupewa kipaumbele lakini Kwa Miradi Isiyozidi Bilioni 10
Serikali imeahidi kuendelea kuwapa kipaumbele wakandarasi wazalendo katika utekelezaji wa miradi mikubwa lakini imewaonya wale ambao wamekuwa wakitekeleza miradi chini ya viwango vilivyowekwa kwenye mikataba.
Hayo yalisemwa jana mjini Dodoma na Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan, wakati akifungua mkutano wa mwaka wa makandarasi ulioandaliwa na Bodi ya Usajili wa Wakandarasi (CRB).
Samia aliagiza kuwa miradi yote ya thamani isiyozidi Sh bilioni 10 wapewe wakandarasi wa ndani hasa kwa miradi inayotekelezwa kwa fedha za ndani kwani wakandarasi hao watasaidia kuongeza ajira kwa vijana wa Kitanzania na kuongeza uwekezaji ndani ya nchi.
Alisema kuwapa miradi mikubwa wakandarasi wazalendo kuna faida kubwa kwani kutasaidia kuwajengea uwezo hivyo kuweza kushindana na wakandarasi wa nje hivyo fedha nyingi za serikali kubaki ndani.
“Tanzania bora na yenye viwanda itatokana na wakandarasi bora na wenye uzalendo, hatuwezi kufikia huko tunakotaka kwenda wakati miradi mikubwa ya ujenzi inafanywa na wakandarasi wanje…. miradi ni yetu na fedha ni zetu hivyo lazima tuwape nyinyi,” alisema.
Aidha, aliwataka wakandarasi wazalendo wakamilishe kazi kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa pale wanapopewa miradi ili wajenge uaminifu kwa serikali kuendelea kuwaamini na kuwapa miradi mikubwa.
Makamu wa Rais aliwaonya baadhi ya wakandarasi wanaoshirikiana na maofisa wa serikali kuongeza gharama kubwa za ujenzi wa miradi kwa misingi ya rushwa hali ambayo imekuwa ikifuja fedha za serikali.
“Jamani kwenye mkutano huu tujitathimini na tuanze upya maana kuna wenzetu ambao hawana maadili na wanaendekeza rushwa, serikali ikitumia taasisi zake inatekeleza miradi mikubwa kwa gharama ndogo lakini nyinyi wengine mnaweka gharama kubwa ambazo si halisi,” alisisitiza.
Aliipongeza CRB kwa namna inavyoendelea kuratibu kazi za wakandarasi wazawa huku akiitaka kuendelea kuwajengea uwezo ili watekeleze miradi mikubwa kama kampuni ya nje.
“CRB mmefanyakazi kubwa sana kuandaa mkutano huu na kwa kuwa mmekutana hapa naomba mjadiliane kwa uwazi na muelezane ukweli kuhusu changamoto mlizonazo na namna mtakavyozitatua na sisi serikali mkituletea maazimio yetu sisi tunaahidi kuyafanyia kazi,” alisema.
Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi, Makame Mbarawa, yeye alisema asilimia 75 ya madeni ya wakandarasi yameshalipwa na yaliyobaki yatalipwa wakati ukifika na aliwaomba wawe wavumilivu wakati huu.
“Msidhani serikali imewasahau, tunafanya kazi kwa bidii kuhakikisha wote mnalipwa kwa sababu sisi tunaamini na tunafahamu kwamba ili makampuni yenu yaendelee lazima mlipwe hela zenu hivyo endeleeni kuchapa kazi hela zilizobaki zinakuja,” aliahidi Profesa Mbarawa.
Mwenyekiti wa CRB, Consolata Ngimbwa, aliomba serikali iharakishe malipo ya wakandarasi kwani wengi wao wako kwenye hali mbaya kifedha. Alisema baadhi ya wakandarasi walifariki dunia kutokana kabla hatajalipwa malimbikizo ya madeni wanayoidai serikali baada ya kukamilisha miradi mbalimbali ya ujenzi.
Alisema wakandarasi wengi wazalendo wana uwezo mkubwa wa kutekeleza miradi mikubwa ya ujenzi hivyo aliiomba serikali iweke kipaumbele kwa kuwapa miradi hiyo.
Vile vile, aliwageukia wakandarasi ambao wamekuwa na kawaida ya kutekeleza miradi chini ya kiwango na wengine kutokomea mara baada ya kulipwa fedha za awali za ujenzi.
Msajili wa CRB, Rhoben Nkori aliwataka wakandarasi kutekeleza miradi wanayopewa na kuahidi kuwa bodi yake itaendelea kuhakikisha mkandarasi asiye na viwango anafutiwa usajili.
↧
Waziri Mkuu: Majiji Yote Kujengwa Barabara za Kisasa
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali ina mkakati wa kufanya Majiji yote nchini yawe na barabara za viwango vya kimataifa na zinazopitika kwa urahisi.
“Tumeanza kujenga barabara za kisasa katika jiji la Arusha ambalo ni jiji la utalii, tutakwenda Mwanza na Dar es Salaam kwa kujenga barabara zenye njia za juu (flyovers) zikiwemo za magari na za waenda kwa miguu,” amesema.
Ametoa kauli hiyo Alhamisi, Mei 4, 2017 wakati akizumngumza na wananchi wa Tengeru, wilayani Arumeru, mkoani Arusha mara baada ya kukagua barabara ya Sakina- Tengeru yenye urefu wa km. 14.1 ambayo itakuwa na njia nne za magari.
“Nimekuja kukagua ujenzi wa barabara hii ya Sakina hadi Tengeru lakini mkandarasi akimaliza anajenga barabara nyingine ya kilometa 42.1 na hivyo hapa Arusha tutakuwa na kilometa 56.5 za awamu ya kwanza,” alisema.
Alisema maboresho ya barabara za Jiji la Arusha yanafanyika ili kuwezesha wafanyabiashara kusafirisha bidhaa zao kwa urahisi na viwanda vitakapoanza kujengwa, itakuwa hawana shida ya mawasiliano.
Akizungumzia tatizo la uhaba wa ardhi aambalo lililibuliwa na mbunge wa Arumeru Mashariki, Bw. Joshua Nassari, Waziri Mkuu alimuagiza Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Bw, Mrisho Gambo aendelee na zoezi la kuuzungukia mkoa wake ili kubaini maeneo yenye matatizo sugu.
Mapema, akitoa taarifa ya ujenzi wa barabara hiyo kwa Waziri Mkuu, Kaimu Meneja wa TANROADS Mkoa wa Arusha, Eng. Mgeni Mwanga alisema ujenzi wa barabara hiyo ambao ulianza Juni 2015, unatarajia kukamilika Juni 2018.
“Ujenzi wa barara ya Sakina –Tengeru ni wa awamu ya kwanza ya ujenzi wa barabara yenye urefu wa km. 230 ya kutoka Arusha –Holili- Taveta –Voi ambayo ujenzi wake unatarajiwa kugharimu sh. bilioni 139.34. Ujenzi huo unagharimiwa na Serikali ya Tanzania pamoja na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB).
Sambamba na barabara hiyo, Eng. Mwanga alisema mkandarasi wa barabara hiyo ataanza kujenga barabara nyingine ya km. 42.1 inayoanzaia Usa River hadi Kisongo kwa kiwango cha lami ambayo itakuwa na madaraja saba wakati ile ya Sakina hadi Tengeru ina madaraja makubwa mawili.
Naye mbunge wa Arumeru Mashariki, Bw. Joshua Nassari alisems uhaba wa ardhi bado ni tatizo kubwa kwenye wilaya hiyo kiasi kwamba hawana hata eneo la kujenga shule au zahanati.
“Maeneo yote yameuzwa na wenyeviti wa vijiji na madiwani, hivi sasa ukitaka kujenga shule au zahanati hakuna eneo hata moja. Mheshimiwa Waziri Mkuu tunaomba utusaidie kufuatilia suala hilo licha ya kuwa Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi alishakuja na kuelezwa hali halisi ilivyo,” alisema.
↧
↧
Waziri Mkuu Aiomba Rotary Club Isaidie Kukabiliana Na Malaria
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameutaka uongozi wa Klabu ya Rotary nchini uangalie uwezekano wa kuisaidia Serikali kupambana na ugonjwa wa Malaria.
Waziri Mkuu Majaliwa ambaye jana Alhamisi, Mei 4, 2017 alikuwa mwanachana wa 651 kujiunga na klabu hiyo, alitoa wito huo wakati akifungua mkutano wa 92 wa mwaka wa Rotary unaojumuisha nchi za Uganda na Tanzania (District 9211) katika ukumbi wa AICC jijini Arusha.
"Ninatambua kazi nzuri inayofanywa na Rotary Club katika kuisaidia jamii kwa vile na mimi mwenyewe nimekuwa nikisaidia jamii. Kwa hiyo mimi na mke wangu Mary Majaliwa tunajiunga tukiwa ni wanachama wa 651 na 652 ili kuongeza nguvu ya Rotary kusaidia jamii," alisema huku akishangiliwa na washiriki zaidi ya 1,000 waliohudhuria mkutano huo kutoka Uganda, Tanzania, India, New Zealand na Australia.
Waziri Mkuu aliutaka uongozi wa klabu hiyo uongeze mikakati ya kutangaza kazi wanazozifanya ili kuondoa dhana iliyojengeka miongoni mwa watu wengi kwamba wanaojiunga na klabu hiyo ni watu matajiri na watu maarufu.
"Kazi mnazozifanya ni kubwa na nzuri mno kwa jamii. Lakini itabidi mjitangaze zaidi ili watu wengi zaidi watambue kazi zenu na waweze kuwaunga mkono," alisema.
Waziri Mkuu aliahidi kuwashawishi viongozi wengine wa Serikali, taasisi za umma pamoja na Wabunge wajiunge kwa wingi na klabu hiyo. Tanzania ina klabu za Rotary 36 zenye wanachama 650 wakati Uganda ina klabu za Rotary 93 zenye wanachama 2,700. Tanzania na Uganda zinaunda District 9211 katika mfumo wa kimataifa wa rotary.
Waziri Mkuu alitumia fursa hiyo kuwapongeza wana-Rotary kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kusaidia jamii hasa kwenye sekta za maji, elimu, na afya.
Alisema Rotary inatambulika duniani kwa kampeni yake ya kutokomeza ugonjwa wa polio; na kupitia michango ya wana-Rotary, Tanzania hivi sasa haina mgonjwa yeyote wa polio.
"Licha ya uchache wenu, natambua mchango mkubwa unaotolewa na Rotary Club hapa nchini. Hivi karibuni, Rotary Club saba ziliungana na Benki M na kujenga hospitali kubwa ya watoto pale Muhimbili (MNH) na Kituo cha Ujasiriamali kwa Vijana pale Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM)," alisema.
"Miradi mingine inayofadhiliwa na Rotary Club ni ujenzi wa hospitali ya akinamama wajawazito mkoani Dodoma, utoaji wa vitabu vya ziada 20,000 kwenye shule za sekondari zaidi ya 40 mkoani Tanga pamoja na miradi ya maji safi kwenye wilaya za Same na Mwanga mkoani Kilimanjaro.
Kwa upande wake, District Gavana wa Rotary 9211 ambaye anamaliza muda wake, Bw, Jayesh Asher wana-Rotary duniani wanaamini kwamba Serikali za nchi mbalimbali haziwezi kutekeleza majukumu yote kwa wananchi wake kwa hiyo wanajiunga na kutoa rasilmali zao ili kusaidia jamii zenye uhitaji.
Akizungumzia kuhusu uchahe wa wanachama hapa nchini, Bw. Asher alisema Rotary Club ya Uganda imepata umaarufu kwa sababu viongozi wengi wamejiunga na klabu hiyo wakiwemo Mawaziri, Spika wa Bunge la Uganda, wabunge na mabalozi.
“Hapa Tanzania itabidi tutangaze zaidi kazi zetu ili tuweze kuwavuta viongozi wa kisiasa na wa umma na pia kuongeza wanachama zaidi,” alisema.
Mkutano huo wa siku tatu, utamalizika Juni 6, mwaka huu.
↧
Fedha za mfuko wa jimbo zaibua mjadala mzito Bungeni
Mjadala mkubwa umetokea Bungeni mjini Dodoma mapema hii leo mara baada ya wabunge wa viti maalumu kuhoji uhalali wa kutokuwepo kwenye mgawo wa fedha za mfuko wa jimbo.
Mjadala huo umeibuka mara baada ya Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tamisemi, Suleiman Jafo kusema kuwa fedha hizo haziwahusu wabunge hao hali ambayo imeibua maswali mengi kwa wabunge hao.
Akijibu hoja hiyo Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tamisemi, George Simbachawene kuhusu mgawo wa fedha za mfuko wa Jimbo, amesema kuwa mfuko huo upo kwa ajili ya majimbo na si kuwalipa wabunge wa viti maalumu.
Amesema kuwa yeye yupo kwa ajili ya kusimamia mfuko huo uliopo kwa mujibu wa sheria za bunge hivyo hana nanma ya kubadilisha sheria hiyo ili kuwawezesha wabunge hao kupata fedha hizo.
Aidha, Katika hatua nyingine, Simbachawene ameongeza kuwa kwa upande wa Zanzibar kuhusu fedha hizo amesema kuwa atawasiliana na Ofisi ya Makamu wa Rais ili kuweza kuweka utaratibu maalum wa kuharakisha upatikanaji wa fedha hizo.
“Mfuko huu hauwahusu wabunge wa viti maalum, napata wakati mgumu kama Jimbo moja linakuwa na idadi kubwa ya wabunge wa viti maalum, ina maana fedha hizi zitaishia kwenye mgawo wa wabunge,”amesema Simbachawene.
↧
TANESCO Wakata Umeme Kambi ya JWTZ , Magereza na Polisi.......Ofisi ya Mkuu wa Mkoa nayo Nusura Ikatiwe
Agizo la Rais Dk. John Magufuli la kulitaka Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kuzikatia umeme taasisi za Serikali zinazodaiwa jumla ya Sh bilioni 8.6 limeanza kufanya kazi mkoani Arusha.
Ofisi zilizoanza kuonja machungu ya kukosa umeme kuanzia jana hadi zitakapolipa madeni ni Kambi ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Oljoro, Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Jeshi la Magereza, Hospitali za Serikali na Taasisi za Maji.
Nyingine zilizokatiwa umeme ni Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha ikiwamo Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha na Kituo Kikuu cha Polisi cha Arusha.
Wakati ofisi hizo zikikosa umeme, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha ilinusurika baada ya kuanza kulipia deni lake la Sh milioni sita 6 kwa awamu.
Akithibitisha kufanyika kwa operesheni hiyo iliyotajwa kuwa endelevu kwa ofisi hizo mkoa mzima, Ofisa Uhusiano wa Tanesco mkoani hapa, Saidy Mremi, alisema inalenga kukusanya madeni yote ya miaka iliyopita.
“Tunatekeleza agizo la Rais Magufuli, hatutaziacha salama ofisi zote zinazodaiwa. Tunafanya hivi ili kuiwezesha ijiendeshe pamoja na kutoa huduma bora kwa wateja wetu,” alisema.
Mremi alisema operesheni hiyo iliyoongozwa na Meneja wa Tanesco Kanda, Stella Hizza na Meneja wa Mkoa, Gasper Msigwa, ilikata umeme katika vituo vya polisi vilivyopo mjini hapa.
Pia alivitaja vituo vya polisi vingine vilivyokatiwa umeme kuwa ni vituo vya Polisi vya Unga Limited, Ngarenaro, Sakina na Ngaramtoni.
“Vituo vingine ni Sekei, Fire, Kijenge, Chekereni, Olorien na Mbauda. Na vituo vingine vya jeshi likiwamo Duka la Jeshi lililoko JKT Oljoro na Njiro Nane Nane. Hii ni operesheni endelevu itakayowezesha shirika kujiendesha,” alisema.
Akielezezea kuhusu Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha, alisema ofisi hiyo imeweza kutoa ushirikiano wa hali juu katika kulipia deni lao.
“Hawa tulikuwa tunawadai shilingi milioni sita hadi sasa wameweza kulipia zaidi ya asilimia 80 ya deni lao, wametupa ushirikiano wa hali ya juu na wameahidi kuendelea kulipa ili kumaliza deni lao,” alisema.
Mremi alisema madeni hayo ni ya miaka ya nyuma na yalitokana na taasisisi hizo kuyalimbikiza kisha yakahamia mwaka mwingine.
Aliyataja madeni ambayo taasisi hizo zinadaiwa (kwenye mabano) kuwa JWTZ (Sh milioni 538), JKT (Sh milioni 57), Jeshi la Polisi (Sh milioni 490), Jeshi la Magereza (Sh Milioni 271), hospitali tofauti za Serikali (Sh milioni 58) na taasisi nyingine ikiwamo za maji (Sh milioni 106).
“Taasisi hizi za Serikali kwa ujumla wake zinadaiwa shilingi bilioni 8.6 sawa na asilimia 28 na asilimia 72 inayobakia ipo kwa taasisi, mashirika na watu binafsi,” alisema.
Kabla ya kufikia hatua hiyo ya kuzikatia umeme taasisi hizo pamoja na wateja wengine, alisema huwa wanatoa notisi kwa wateja wake ikiwamo kutangaza matangazo katika vyombo vya habari.
↧
Bunge lafuta maneno kwenye hotuba ya Sugu kabla ya kusomwa
Mwenyekiti wa Bunge, Mussa Zungu ameagiza Hotuba ya Kambi ya Upinzani kuhusu Bajeti ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ihaririwe na kufuta maneno yote katika kurasa 17.
Zungu ametoa uamuzi huo leo asubuhi baada ya kipindi cha maswali na majibu, hata kabla ya bajeti yenyewe kuwakilishwa na Waziri Dk Harrison Mwakyembe.
Zungu amesema amezipihitia hotuba zote na kubaini kuwa ile ya upinzani itakayowalishwa na Joseph Mbilinyi 'Sugu' ina masuala yaliyopo mahakamani ambayo yamekwishazuliwa katika bajeti zilizotangulia.
Amesema maneno yenye mwelekeo huo yakisomwa atachukua hatua.
↧
↧
Shilole Ataja Sifa za Mwanaume Anayemtaka
Zuwena Mohamed ' Shilole' anayetamba na hit ya 'hatutoi kiki' amefunguka na kudai kwamba haitaji kuolewa na mwanaume mwenye pesa kwani wengi wao hutumia mali zao kama fimbo ya kuwachapa na kunyanyasia wanawake zao.
Akiwa Kikaangoni kwenye ukurasa wa Facebook wa EATV, Shilole amefunguka kuwa yupo tayari kuolewa lakini mpaka atakapo pata mwanaume atakayekidhi vigezo vyake huku akitaja pesa siyo kitu anachokitanguliza bali heshima, upole na ukarimu.
"Natamani sana kuolewa lakini mpaka nimpate mtu mwenye vigezo ninavyohitaji mimi, napenda mwanaume anayejali, atakayeniheshimu lakini awe pia anafanya kazi kama hafanyi kazi simtaki. Lakini pia wanaume wenye pesa siwataki maana tunawaona huko majumbani wanavyotumia kama fimbo kuwanyanyasa wake zao" Shilole alifunguka.
"Mimi siangalii sana muonekano kwani unaweza kutengenezwa lakini ukiwa mfupi mimi sitakukubali nahitaji mwanaume mrefu na mwenye heshima na anayejituma kwenye utafutaji" aliongeza Shilole.
↧
VIDEO: Tazama Video Hii Kujua Yaliyojiri Bungeni Dodoma leo Mei 5, 2017
↧
Sakata la Vyeti Feki: Watusmishi 6 Wafungwa Jela, Zahati 2 Zafungwa kwa Kukosa Watumishi maana Wote Walifoji Vyeti
Uamuzi wa Serikali wa kuwafukuza kazi watumishi wanaodaiwa kughushi vyeti, umezidi kuchukua sura mpya, baada ya watumishi sita wa Halmashauri ya Kilwa mkoani Lindi kufungwa jela mwaka mmoja kila mmoja kwa kosa la kughushi vyeti vya kidato cha nne na kujipatia ajira.
Taarifa nyingine zinasema Katibu Tawala wa Wilaya ya Tandahimba (DAS), Mohamed Azizi naye ameguswa na sakata la vyeti feki baada ya kutajwa katika orodha ya watumishi wenye vyeti feki akiwa namba 5356.
Chanzo cha uhakika kutoka ofisi ya DAS kimesema kuwa, tayari kiongozi huyo ameshaondoka Mtwara kuelekea Dar es Salaam kupeleka malalamiko yake katika mamlaka za juu kwamba jina lake limeingizwa kimakosa katika orodha hiyo.
Taarifa nyingine kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Lindi Vijijini zinasema zahanati mbili zimefungwa baada ya watumishi wote waliokuwapo kukumbwa na sakata la vyeti feki.
Madereva hao, walihukumiwa jana na Mahakama ya Wilaya ya Kilwa, baada ya kupatikana na hatia ya makosa matatu ya kufoji vyeti vya kidato cha nne.
Hukumu hiyo, imetolewa na Hakimu wa Mahakama hiyo, Gabriel Ngaeje baada ya kuridhishwa na ushahidi uliotolewa na upande wa mashtaka.
Madereva waliohukumiwa ni Juma Sungura, Issa Juma Abdurahamani, Abdull Chubi, Dactuce, Ahamadi Selemani na Abdallah Kilolopera.
Kabla ya kutolewa hukumu hiyo, Hakimu Ngaeje aliwauliza washtakiwa kama wana sababu zitakazoishawishi mahakama isiwape adhabu kali.
Kila mmoja kwa wakati wake, aliomba mahakama iwaonee huruma, kwani wana familia zinazowategemea, hivyo iwapo watapewa adhabu kali kuna hatari ya kukosa matunzo yao.
Naye mwanasheria wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Emmanuel Camilius aliiomba mahakama kutoa adhabu kali ili iwe fundisho kwa watuhumiwa na watu wengine wenye tabia ya aina hiyo ndani ya Mkoa wa Lindi na Taifa kwa ujumla.
“Tabia ya aina hii si ya kuifumbia macho, kazi wanazozifanya zinahusu usalama wa watu, kugushi vyeti kwa ajili ya kujipatia ajira ni hatari,”alisema Camulius.
Hakimu Ngaeje, akitoa hukumu katika kesi hiyo namba 07/2014, alisema amesikiliza maombi ya pande zote mbili, hivyo akawahukumu kila mmoja kifungo cha nje cha miezi (12) kwa kila kosa na kufanya idadi ya miezi (196).
“Kwa vile adhabu inakwenda pamoja, mtatumikia kifungo cha nje miezi 12,”alisema.
Awali ilidaiwa mahakamani hapo na mwanasheria Camilius, kuwa watumishi hao wakijua wanachokifanya ni makosa, walifoji vyeti vya kidato cha nne na kujipatia ajira kinyume na sheria ya nchi.
Naye Mbunge wa Mchinga, Hamidu Bobali (CUF), alisema zahanati mbili katika Halmashauri ya Wilaya ya Lindi Vijijini mkoani Lindi, zimefungwa baada ya watumishi wake kutajwa katika orodha ya watumishi wa umma wenye vyeti feki.
Bobali alitoa taarifa hiyo bungeni mjini Dodoma jana, alipokuwa akichangia bajeti ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, kwa mwaka wa fedha 2017/18.
“Mheshimiwa mwenyekiti, hili suala la vyeti feki limeleta shida katika Halmashauri ya Wilaya ya Lindi Vijijini kwa sababu kuna zahanati mbili zimefungwa, baada ya watumishi wake wote kubainika wana vyeti feki.
“Kwa hiyo, namwomba mheshimiwa waziri, achukue hatua haraka,” alisema Bobali wakati alipokuwa akihitimisha mchango wake.
Pamoja na kusema hayo bungeni, nje ya bunge Bobali alisema a zahanati zilizofungwa ziko katika Jimbo la Mtama katika Halmashauri ya Wilaya ya Lindi Vijijini.
“Zahanati zilizofungwa ni za Mkanga 2 na Sudi ambazo zote ziko pembezoni kabisa ya mji, kiasi kwamba kitendo cha kuzifunga, kitaathiri mno wananchi.
“Kwa hiyo, ndiyo maana nilimwomba mheshimiwa waziri afanye kila analoweza kuhakikisha zinafunguliwa haraka ili kunusuru maisha ya wananchi,”alisema Bobali.
Kwa mujibu wa Bobali, zahanati hizo zilikuwa na watumishi watatu watatu kila moja.
Taarifa zaidi kutoka Lindi, zinasema watumishi 236 wa Serikali wamegundulika kutumia vyeti feki.
Katika sakata hilo, halmashauri za wilaya za Nachingwea na Kilwa zinaongoza kwa kuwa na idadi kubwa.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Godfrey Zambi alizitaja wilaya na idaidi ya watumishi kwenye mabano, kuwa ni Nachingwea (72), Kilwa (53), Ruangwa (45),Lindi Vijijini (25), Ofisi ya Katibu Tawala (RAS) (23), Manispaa (11) na Liwale (7).
Alisema katika idadi hiyo, idara za afya na elimu zinaongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya watumishi wa vyeti feki.
↧
SORRY MADAM -Sehemu ya 59 & 60 (Destination of my enemies)
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWAILIPOISHIA
ILIPOISHIA
. Taratibu akapiga hatua za uwoga, akaingia, ndani, mtoto huyo akaufunga mlango huo ulio kaa kama ukuta.
“Umepajuaje huku?”
“Babu yangu ndio alinionyesha huku”
“Babu yako”
“Ndio.”
“Kwanza unaitwa nani?”
“Naitwa Soroo”
Walizidi kushuka chini, wakakuta kordo moja ndefu iliyo jaa taa pembeni kwa juu, mbele yake kwa mbali kuna mlango wa kuingilia kwenye chumba kimoja tu kilichopo kwenye eneo hilo. Wakazidi kupiga hatua, wakiwa umbali fulani kutoka kilipo chumba hicho, taa zikaanza kufifia. Wote wakajikuta wakiogopa, gafla taa zote zikazima na kujikuta wakipiga kelele za woga kwani giza zito lilitanda kwenye mboni za macho yao.
ENDELEA
Haikupita hata dakika moja taa hizo zikawaka, wote wakanyamaza na kushusha pumzi zao. Kila mmoja woga ulimtawala.
“Turudi zetu”
Phidaya alizungumza huku akimshika mkono Soroo, habari ya kwenda alipo Black Shadow, ikayayuka moyoni mwake, hakutamani kuona anafia kwenye sehemu hiyo chini kabisa ya ardhi. Wakaanza kutembea kwenye kordo kurudi walipo tokea tena safari hii waliongeza hata mwendo wa kutembea. Kila mara Phidaya alitazama nyuma kuona kama kuna kitu kinakuja. Wakazipandisha ngazi kwa haraka, Soroo akafungua mlango, wakapita na kutokezea katika choo walicho ingia.
Wakarudishia kila kitu sehemu yake, na kutoka kwenye mabweni hayo. Moja kwa moja wakarudi katika sehemu ya mkusanyiko walipo watoto wengine pamoja na walezi wao.
“Mumefanikiwa kuona kitanda chake?”
Mlezi mmoja alimuuliza, huku akiachia tabasamu pana usoni mwake.
“Ndio, nimefurahi sana kuona mabweni yao. Nitahalkikisha kwamba tunaongeza mabweni ili mumweze kuchukua vijana wengi wamaoishi kwenye maisha magumu”
“Tutashukuru sana madam”
“Nipo pamoja nanyi. Naona muda wangu hautoshi basi ngoja niwaache muendelee na majukumu”
Phidaya alijikaza kuzungumza hivyo, ila mwili mzima alihisi kama umekufa ganzi kwa woga. Phidaya akamuaga Saroo, na kumuahidi atarejea kisha akangia kwenye gari lake na kuelekea hotelini wanap ishi Shamsa na mwenzake. Wakawakuta wakiwa wanafanya mazoezi ya viungo. Wakasalimiana kwa furaha, huku Phidaya akimbusu Shamsa kwenye paji la uso.
“Vipi mbona mupo kwenye mazoezi makali?”
“Kuna kitu mama nahitaji uweze kunisaidia”
“Kitu gani hicho?”
“Nihitaji kutafuta ukweli kuhusiana na kitu ambacho kilikupata wewe kwa maana inavyo onekana hukumbuki mambo ya nyuma”
Shamsa alizungumza huku akimtazama Phidaya usoni, anaye onekana kumsikiliza kwa umakini sana.
“Nahitaji kufahamu maeneo ambayo dokta Ranjiti anapenda kuyatembelea?”
“Kwa sasa yupo Korea Kusini”
“Mama hujanielewa swali langu, yaani sihitaji kujua yupo wapi ila nahitaji kufahamu maeneo anayo penda kwenda kutulia”
“Kusema kweli sifahamu, huwa Ranjiti muda mwingi anapenda kuutumia akiwa hospitalini, na hata akitoka ni sehemu chache sana ambazo anakwenda na kurejea”
“Au labda Yan yule rafiki yake aliye kuwa naye katika chumba cha Black Shadow anaweza kufahamu maeneo ambayo Ranjiti anapenda kuyatembelea kwa sana”
“Eheee umenikumbusha mama hivi siku ambayo uliwasikia wakizungumza kwenye chumba cha Black Shadow, Yan si alihusika?”
“Ndio lihusika”
“Basi mama nimeshapata kwa kuanzia, kila jambo kwa sasa litakwenda sawa, niachie mimi hiyo kazi”
“Sawa. Ila unataka kufanya nini?”
“Mama kila kitu nimekuambia niachie mimi, nikiimaliza kazi yangu nitakuletea ripoti kamili”
“Sawa ila kuwa makini kwa maana hawa watu mimi wala siwaamini sana”
“Usijali mama yangu, hivi nyumbani kwa Yan si unapafahamu?”
“Ndio napafahamu”
Phidaya akamuelekeza Shamsa na Sa Yoo nyumbani kwa daktari Yan, kutokana Sa Yoo ni mwenyeji sana katika nchi hiyo ya Japan, eneo hilo alilifahamu.
***
Majadiliano ya dokta Ranjiti, dokta Yan na Kim ndani ya ndege, yalimchanganya rubani wake ambaye alikuwa ndani ya ndege hiyo pasipo bosi wake kuweza kufahamu. Mpango wa kwenda kumteka Black Shadow, kwenye hospitalini na kwenda kumuua kwa kumchoma moto. Aliweza kuisikia vizuri, rohoni mwake akajikuta akishindwa kuvumilia kuona tukio hilo likiwa linatendeka.
Mzee Yo, aliyasikiliza mazungumzo hayo hadi mwisho, bosi wake alipo ondoka katika eneo la karakana kwa haraka akashuka kutoka ndani ya ndege. Hakumuaga mtu, akapanda pikipiki yake, iliyo mpeleka moja kwa moja hadi nyumbani kwake. Kichwani kwake mawazo mengi yalizidi kukiandama kichwa chake, kila alipo jaribu kufikiria jinsi ya kumuokoa Black Shadow, alijikuta akishindwa kupata jibu kabisa.
“Nitafanyaje wakati kazi hii ni hatari sana. Laiti bosi akitambua nitakuwa sina kazi na pia anaweza kuniua”
Mzee Yo alizungumza peke yake akiwa chumbani kwake amejiinamia kwenye sofa lake. Japo ni rubani wa muda mrefu katika kampuni ya dokta Ranjiti, ila leo ndio aliweza kufahamu kwamba dokta huyo ni mtu katili sana. Kila alipo mfikiria Black Shadow, kijana ambaye ana ujuzi mkubwa wa kupigana, hadi akamteka kihisia, hakukubali kuona anakufa mikononi mwa dokta Ranjiti ambaye amepewa jukumu la kumtibu. Hakuhitaji kufahamu ni kitu gani ambacho Black Shadow amekifanya kwa daktari huyo ila kitu alicho kihitaji ni kuhakikisha kwamba kijana huyo anakuwa hai.
Kwa haraka haraka, akilini mwake akafikiria ni mtu gani anayeweza kumsaidia katika kazi hiyo, kura yake ikatua bibi Eyna. Mwanamke aliye kuwa na mahusiano naye miaka mingi ya nyuma, kabla hawajatengana. Akakumbuka kwamba bibi Eyna anafanya kazi katika hospitali ya dokta Ranjit, kwa haraka akachukua kitabu chake cha kuhifadhia kumbukumbu. Akaanza kufungua kurasa kadhaa, akiitafuta namba ya simu ya bibi huyo. Akabahatika kuipata namba hiyo. Akaingiza namba hizo kwenye simu yake ya mkononi, akaiweka sikioni simu yake na kusikiliza, kwa bahati nzuri simu hiyo iliita kwa muda kisha ikapokelewa.
“Habari yako Eyna”
Sauti ya Mzee Yo, haikuwa ngeni masikioni mwake, moyo wa bibi Eyna ukajikuta ukikubwa na furaha kubwa.
“Safi tu Yo habari za siku nyingi?”
“Safi upo wapi kwa sasa?”
“Nipo kazini”
“Naweza kuja kukuona mpenzi?”
“Mmmm jamani, mpenzi si usubiri nikitoka”
“Hapana ni muhimu sana, nahitaji kukuona mida hii nina hamu sana na wewe”
“Waooo njoo basi nakusubiria”
Mzee Yo, akakata simu baada ya kutumia mameno ya ulaghai kwa mpenzi wake huyo, ambaye aliweza kuachana naye kutoka bibi Eyna enzi za ujana wake hakutulia na mwanaume mmoja. Ndani ya dakika thelathini akawa amefika katika hospitali ya dokta Ranjiti, hakupata tabu sana kuweza kukutana na Bibi Eyna, ambaye alimkumbatia kwa furaha mara baada ya kumuona.
Japo ni mzee ila bibi Eyna bado ana hulka za ujana, hakusita kumpiga mzee Yo busu la mdomoni.
“Baby nimefurahi kukuona jamani”
“Hata mimi, ila unaonekana una joto kali”
Mzee Yo, alitania, huku kiganja chake akiwa amekiweka shingoni mwa bibi Eyna.
“Ni joto la kulimisi penzi lako?”
“Kweli?”
“Ndio”
“Ninaweza kukupatia ubaraidi wakati huu?”
“Mmmm jamani, mbona unanisisimua”
“ Sikusisimui ila ninacho kizungumza nina kimaanisha baby”
Mzee Yo, aliweza kuutambua udhaifu wa mwanamke huyo, kwani anapenda sana ngono kuliko hata kula ndio maana walishindwana kipindi cha ujana wao.
“Sasa hapa tutafanyia wapi mume wangu?”
“Kwani hakuna chumba cha siri tukafanya mambo?”
Bibi Eyna akaichekecha akili yake kwa haraka huku akifikiria sehemu gani, akakumbuka kwamba ndani ya hospitali hapo kuna vyumba vya siri ambavyo vipo ardhini ila havitumiki kwa muda mrefu sasa. Hakujua uwepo wa Black Shadow ndani ya moja ya vyumba hivyo, kwani uwepo wa Black Shawod ni siri iliyopo kwa madaktari wakubwa tu, hata madaktari wengine hawatambui.
“Hembu kaa hapo niandae mazingira kisha naja kukuchukua”
“Mazingira gani baby”
“Ngoja kuna vyumba vipo huko ardhini nahisi huko kutatufaa mpenzi wangu”
Bibi Eyna akaondoka katika eneo hilo akiwa mwingi wa furaha na amani sana, haraka haraka akaelekea kweye ofisi ya dokta Ranjiti akagonga kwa muda, hakuitikiwa, akausukuma mlango na kukuta haujafungwa kwa funguo.
Akachungulia ndani hapakuwa na mtu, akaelekea ofisi ya Phidaya, akagonga pia akukuta hakuna mtu. Akaelekea katika ofisi ya dokta Yan, ambaye ni msaidizi wa dokta Ranjiti naku huko pia hakukuta mtu. Siku hiyo akajiona ni mtu mwenye bahati sana, akarudi sehemu alipo muacha Mzee Yo. Akamuomba amfwate kwa nyuma.
Wakaingia kwenye chumba ambacho kina lifti iliyo washusha chini. Kitendo cha kufika eneo hilo, bibi Eyna akamkumbatia kimahaba mzee huyo na kuanza kumpiga mabusu mfululizo.
“Baby tulia kwanza tuchunguze kuna weza kukawa na mtu humu akatuona ikawa tatizo”
“Baby hakuna mtu bwana”
Mzee Yo, akitazama saa yake ya mkononi inamuonyesha ni saa mbili usiku. Muda wa Black Shadow kuja kutolewa kwenye eneo hilo ni saa nne usiku. Kutokana na yeye ni mwanaume rijari, hakuona vibaya akampatia haki bibi Eyna, haraka haraka ili kuzidi kumchanganya na kumuweka karibu pale ataka anza kufanya mpango wake, kwa maana anatambu lazima Black Shadow yupo kwenye chumba hicho, kutokana alisikia jinsi Kim alivyo kuwa akielekezwa chumba alicho Black Shadow, kila alama aliyo isikia kwenye ndege ipo kwenye moja ya mlango.
Kwa haraka, akalipandisha gauni la bibi Eyna hadi kifuani, akamshusha chupi aliyo ivaa, na yeye akashusha suruali na nguo yake ya ndani. Agamshikisha ukuta bibi Eyna, bila hata maandalizi, ya kumuandaa mwenza wake, akaanza kumpa haki yake.
Bibi Eyna, akaanza kutoa miguno ya mahaba, kwa kasi ambayo anakwenda nayo Mzee Yo, ilimfanya apagawe na zaidi ya mara nne, bibi Eyna alijikuta anafika kileleni. Mzee Yo akafunga goli lake dakika kumi baada ya mchezo kuanza. Bibi Eyna akajikuta akikaa chini kwa jinsi alivyo choka kwani ni muda mrefu hajakutana na mwanaume wa kumpeleka kasi namna hiyo.
Mzee Yo akapandisha nguo zake, akajiweka sawa, bila ya kupotaza muda akaanza kufungua mlango ambao alisikia maelekezo yake yakiwa yanatolewa. Kweli akamkuta Black Shadow akiwa amelala kwenye kitanda hicho akiwa hajitambui, ili kuhakikisha ni yeye akamsogelea karibu, kinyago cha Black Shadow alicho kivaa kilimuhakikishia kwamba ndio mwenyewe.
“Haaaa…….!!!”
Sauti ya Bibi Eyna ilimstua akageuka na kumkuta akiwa amesimama kwenye mlango huku mdomo wake ukiwa mdomoni.
“Shiiiii”
“Huyo si ndio mgonjwa mbaye alivamiwa majuzi?”
Bibi Eyna alizungumza huku akienda kumtazama Black Shadow kitandani alipo lala.
“Nahitaji kumtorosha hapa hospitalini”
“Kwa nini?”
“Kuna watu wanahitaji kumuua”
Macho yakamtoka bibi Eyna kwa kushangaa
“Usishangae, dokta Ranjiti anahitaji kumua, sasa nahiyaji tumtoe kiakili pasipo mtu mwengine kutambu”
“Si unanitafutia matatizo jambo hili likijulikana”
“Una nipenda ua hunipendi?”
“Nakupenda”
“Fanya kama ninavyo hiaji akiendelea kukaa hapa ninaimani wakuu wako watakuja kumuua”
“Ina maana dokta Ranjiti anahitaji huyu kijana kumuua?”
“Hilo ni jibu na si swali, hatuna muda wa kupoteza nilaziama kumtoa humu ndani”
“Sasa utambeba wapi, kwa maana hivi hivi ataonekena”
Mzee Yoo akatoka kwenye chumba hicho, akaingia kwenye chumba kingine, ambapo akakuta maboksi mengi makubwa yakiwa yamepangwa, akalifunua boksi moja na kukuta likiwa halina kitu ndani yake, kwa ukubwa wa boksi hilo akamini kwamba litamsaidia katika mpango wake.
Akarudi nalo kwenye chumba alipo Black Shadow, akamkuta bibi Eyna akiwa amelifunua shuka lililo kuwa limemfunika Black Shadow nusu mwili, msho uliopo kwenye mbavu zake ukmfanya Mzee Yoo aumize kichwa kufikiria jinsi ya kumuingiza humo.
“Unataka kumingiza kwenye boksi?”
“Ndio”
↧
↧
Mavazi Yaibua Mjadala Bungeni.....Naibu Waziri Ajibu Madai ya Wanawake Kuvuliwa Hijabu na Polisi
Naibu Waziri, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akiwa bungeni leo amefunguka na kusema hakuna tafsiri ya mavazi ya kike au kiume kwa kuwa mavazi hayo kama suruali yanavaliwa na watu wote wanaume hata wanawake.
Masauni alitoa ufafanuzi huo bungeni kufuatia Mbunge kutaka kujua serikali inachukua hatua gani kwa baadhi ya wanaume ambao wamekuwa wakijipamba na kujilemba kwa kuvaa nguo za kike.
"Ni kweli kuna wanaume wanavaa mavazi ya kike hata wanawake pia wapo wanavaa mavazi ya kiume, ila sidhani suala la mavazi kama lina tafsiri kuwa vazi hili ni la kike tu na hili ni la kiume tu, nadhani suala hili la Mbunge linahitaji ufafanuzi wake wa kina ili tujue yeye alikuwa anamaanisha nini zaidi katika jambo hili" alisema Masauni
Mbali na hilo Naibu Waziri huyo alitolea ufafanuzi malalamiko ambayo yametolewa kuwa wapo baadhi ya wanawake huvuliwa hijabu zao na kusema si kweli kwani polisi wanafanya kazi zao kwa weledi na kufuata sheria.
"Si kweli kwamba wanawake wanavuliwa hijjabu na nikabu zao na polisi wa kiume pindi wanapokaguliwa kwani polisi wanafanya kazi zao kwa kufuata sheria na umakini mkubwa, ila kama wapo watu wanafanya hivyo niwaombe wanawake wote pindi wanapofanyiwa hivyo wapeleke malalamiko yao kwenye vyombo husika tutalifanyia kazi, natambua kule Zanzibar kuna changamoto katika kufanya ukaguzi lakini hatukuona wanawake wakivuliwa mavazi yao" alisisitiza Masauni
↧
Zitto Kabwe Aikosoa Serikali Kwa Kuamua Kujenga Reli ya Kati Toka Dar Hadi Moro
Mbunge wa Kigoma mjini kupitia tiketi ya ACT, Zitto Kabwe ameukosoa mpango wa serikali kuanza kujenga reli ya kati baina ya Dar es Salaam na Morogoro na kusema serikali inapaswa kuangalia vipaumbele vya maeneo ambayo shughuli za reli hiyo itasaidia
Zitto amebainisha hayo wakati akichangia hotuba ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano katika mkutano wa Bunge Jijini Dodoma kwa kumtaka Waziri Profesa Makame Mbarawa aangalie takwimu ni wapi anapaswa apeleke reli ili aweze kupata pesa ya kujenga reli nyingine.
"Toka mwaka jana tumelalamika kuhusu jambo hili...Nawashukuru wabunge wemametoa tafsiri mpya ya reli ya kati, reli ya kati tafsiri yake ni Kigoma Dar es salaam au Dar es salaam Kigoma maeneo mengine yote ni matawi ya reli ya kati......
"Lakini ujenzi wa 'Standard Gauge' kwa hatua hizo wanazoziita za awali unatoka Dar es salaam kwenda Mwanza....Namuomba Waziri aangalie takwimu ni wapi atapeleka reli ili apate pesa ya kujenga reli nyingine.......
"Takwimu zinaonesha kwamba mizigo ambayo Tanzania inahudumia kwa nchi za maziwa makuu ni tani Milioni tano kwa mwaka kwa mujibu taarifa ya hali ya uchumi mwaka 2015/2016.
"Katika hizo asilimia 34 ni Zambia, asilimia 34 ni Kongo, asilimia 12 Rwanda, aslimia 6 Burundi, asilimia 2.6 Uganda...
"Unapoanza na 'Standard Gauge' matailion ya fedha ukaipeleka Isaka na Mwanza maana yake ni kwamba unaenda kuhudumia mizigo aslimia 15 ya mizigo yote tunayoipitisha unaacha kwenda kuhudumia mizigo asilimia 40 kwa maana ya Kongo na Burundi ambayo yote inapita Kigoma". Alisema Zitto
Aidha, Zitto amehoji wizara pamoja na serikali kuwa ni njia gani walizozitama mpaka kuamua kupeleka sehemu ambayo wanajua haiwezi kuleta faida kwa taifa.
"Economics' gani ambazo mmetumia katika kuhakikisha kwamba reli inaelekea mahali ambako hakuna mzigo..
"Sipendi kusema kwamba Kigoma inatengwa siyo lugha ambayo mimi kiongozi napenda kuzungumza lakini hili takwimu zote zinaonesha reli inapaswa kwenda kule ambako kuna faida, hampeleki kule ambako kuna faida ambako kuna faida hii maana yake nini ?...
"Lakini siyo hivyo tu Waziri, kuna fedha za Benki ya Dunia ...kwaajili ya ukarabati wa reli hata hizi Bilioni 200 za ukarabati wa reli ambao upo sahizi na zenyewe mmepeleka kule kule mnapopeleka 'Standard Gauge', mnashindwa hata kutudanganya kwa pipi". Alihoji Zitto
↧
Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya May 6
↧
VIDEO: CCM Yazungumzia Kutoonekana Hadharani kwa Katibu mkuu wa Chama Abdulrahman Kinana
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimesema kimempa mapumziko ya muda ambao hakijautaja Katibu Mkuu wake, Abdulrahman Kinana.
Kwa mujibu wa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole, kiongozi huyo ameruhusiwa kupumzika ili kuangalia afya yake hadi hapo itakapoimarika.
Polepole alitoa kauli hiyo jana, alipokuwa akifanya majumuisho ya ziara yake iliyolenga kukagua uhai wa CCM mkoani Arusha, ikiwa ni eneo linalotajwa kuwa ngome ya chama kikuu cha upinzani, Chadema.
Kauli hiyo ya Polepole imekuja ikiwa ni muda sasa Kinana hajaonekana hadharani, hatua ambayo imezusha maneno mengi, huku baadhi wakienda mbali na kuhusisha kitendo hicho na mgomo kutokana na uamuzi wa Serikali ya Rais Dk. John Magufuli kumvua uwaziri wa Habari, Vijana Sanaa na Michezo ‘kijana wake’, Nape Nnauye.
Kuwapo kwa hisia za namna hiyo kunatokana na kile ambacho CCM ilidai kuwa ni uvumi, kwamba Kinana alitaka kuitisha mkutano na wanahabari siku moja baada ya Nape kuondolewa kwenye wadhifa huo na saa chache baadaye wakati akielekea kuzungumza na vyombo vya habari kutishiwa kwa bastola na mtu ambaye haijajulikana anafanya kazi wapi.
Ni wakati huo Rais Magufuli alilazimika kuzungumzia mahali alipo Kinana, akisema alikuwa amemtuma kwenda nchini India kwa ajili ya matibabu.
Rais Magufuli alitoa ufafanuzi huo wakati akiwaapisha Mawaziri Profesa Palamagamba Kabudi kuwa Waziri wa Katiba na Sheria na Dk. Harrison Mwakyembe aliyechukua nafasi ya Nape.
Hadi sasa hakuna picha yoyote inayomwonyesha kiongozi au mtu yeyote amefika nyumbani kwa Kinana kwa ajili ya kumjulia hali, jambo ambalo limezidi kuzua maswali.
“Hili swali la Katibu wetu Mkuu ndugu Komrade Abdulrahmani Kinana limesemwa sana na mimi ninafurahi kwamba tunaanza kurejesha utamaduni ambao maisha ya viongozi wetu yanakuwa sehemu na maslahi ya umma wa Watanzania,” alisema Polepole na kuongeza:
“Lakini unapoona Katibu wetu Mkuu wa CCM anaulizwaulizwa yuko wapi na hata watu wasiokuwa wana CCM, hii inaonyesha kiwango cha imani cha Watanzania kinarejea kwa kasi kubwa, hasa katika kipindi hiki tunapofanya mageuzi makubwa ndani ya chama chetu.
“Na kwa hakika najua viongozi wa vyama vingine wasioonekana hawauliziwi na mtu yeyote, kwetu sisi ni dalili njema sana. Nipende tu kuwaambia jana nimeongea na Komrade Kinana bado yuko kwenye mapumziko ya kujitizama afya yake.
“Ninyi wote ni mashahidi mzee wetu huyu alifanya kazi kubwa ndani ya CCM na kwenye Serikali na pia kwenye wigo wa kimataifa, hasa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki.
“Lakini amefanya kazi kubwa zaidi kwenye chama ya kukijenga na kukiimarisha, hasa kwenye uongozi na utendaji kama Mtendaji Mkuu wa Chama.
“Leo labda niseme kwa sehemu mpaka wakati tunamaliza Mkutano Mkuu Maalumu ambao ulipitisha marekebisho na mabadiliko ya Katiba Ndugu Komrade Kinana alikuwa anafanya yote haya, lakini akiwa mgonjwa, akiugulia na sisi kwenye chama tuna utaratibu na tunawapenda viongozi wetu.
“Kwa hiyo ikakubalika achukue muda wa kutosha wa kuitazama afya yake nje ya nchi na kiongozi wa aina yake anaporejea, mgonjwa akitoka hospitali hakimbilii kazini au shambani moja kwa moja, inashauriwa kitaalamu atumie muda wa kupumzika ili kuimarisha afya yake.
“Na jana (juzi) nimezungumza naye anaendelea vizuri, yuko madhubuti kabisa kuliko jana, kwa hiyo nashukuru wale wote wanaofuatilia habari zetu za CCM na iwe mfano kwa vyama vingine,” alisema. .
Kwa mujibu wa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole, kiongozi huyo ameruhusiwa kupumzika ili kuangalia afya yake hadi hapo itakapoimarika.
Polepole alitoa kauli hiyo jana, alipokuwa akifanya majumuisho ya ziara yake iliyolenga kukagua uhai wa CCM mkoani Arusha, ikiwa ni eneo linalotajwa kuwa ngome ya chama kikuu cha upinzani, Chadema.
Kauli hiyo ya Polepole imekuja ikiwa ni muda sasa Kinana hajaonekana hadharani, hatua ambayo imezusha maneno mengi, huku baadhi wakienda mbali na kuhusisha kitendo hicho na mgomo kutokana na uamuzi wa Serikali ya Rais Dk. John Magufuli kumvua uwaziri wa Habari, Vijana Sanaa na Michezo ‘kijana wake’, Nape Nnauye.
Kuwapo kwa hisia za namna hiyo kunatokana na kile ambacho CCM ilidai kuwa ni uvumi, kwamba Kinana alitaka kuitisha mkutano na wanahabari siku moja baada ya Nape kuondolewa kwenye wadhifa huo na saa chache baadaye wakati akielekea kuzungumza na vyombo vya habari kutishiwa kwa bastola na mtu ambaye haijajulikana anafanya kazi wapi.
Ni wakati huo Rais Magufuli alilazimika kuzungumzia mahali alipo Kinana, akisema alikuwa amemtuma kwenda nchini India kwa ajili ya matibabu.
Rais Magufuli alitoa ufafanuzi huo wakati akiwaapisha Mawaziri Profesa Palamagamba Kabudi kuwa Waziri wa Katiba na Sheria na Dk. Harrison Mwakyembe aliyechukua nafasi ya Nape.
Hadi sasa hakuna picha yoyote inayomwonyesha kiongozi au mtu yeyote amefika nyumbani kwa Kinana kwa ajili ya kumjulia hali, jambo ambalo limezidi kuzua maswali.
“Hili swali la Katibu wetu Mkuu ndugu Komrade Abdulrahmani Kinana limesemwa sana na mimi ninafurahi kwamba tunaanza kurejesha utamaduni ambao maisha ya viongozi wetu yanakuwa sehemu na maslahi ya umma wa Watanzania,” alisema Polepole na kuongeza:
“Lakini unapoona Katibu wetu Mkuu wa CCM anaulizwaulizwa yuko wapi na hata watu wasiokuwa wana CCM, hii inaonyesha kiwango cha imani cha Watanzania kinarejea kwa kasi kubwa, hasa katika kipindi hiki tunapofanya mageuzi makubwa ndani ya chama chetu.
“Na kwa hakika najua viongozi wa vyama vingine wasioonekana hawauliziwi na mtu yeyote, kwetu sisi ni dalili njema sana. Nipende tu kuwaambia jana nimeongea na Komrade Kinana bado yuko kwenye mapumziko ya kujitizama afya yake.
“Ninyi wote ni mashahidi mzee wetu huyu alifanya kazi kubwa ndani ya CCM na kwenye Serikali na pia kwenye wigo wa kimataifa, hasa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki.
“Lakini amefanya kazi kubwa zaidi kwenye chama ya kukijenga na kukiimarisha, hasa kwenye uongozi na utendaji kama Mtendaji Mkuu wa Chama.
“Leo labda niseme kwa sehemu mpaka wakati tunamaliza Mkutano Mkuu Maalumu ambao ulipitisha marekebisho na mabadiliko ya Katiba Ndugu Komrade Kinana alikuwa anafanya yote haya, lakini akiwa mgonjwa, akiugulia na sisi kwenye chama tuna utaratibu na tunawapenda viongozi wetu.
“Kwa hiyo ikakubalika achukue muda wa kutosha wa kuitazama afya yake nje ya nchi na kiongozi wa aina yake anaporejea, mgonjwa akitoka hospitali hakimbilii kazini au shambani moja kwa moja, inashauriwa kitaalamu atumie muda wa kupumzika ili kuimarisha afya yake.
“Na jana (juzi) nimezungumza naye anaendelea vizuri, yuko madhubuti kabisa kuliko jana, kwa hiyo nashukuru wale wote wanaofuatilia habari zetu za CCM na iwe mfano kwa vyama vingine,” alisema. .
==>Msikilize hapo chini akiongea
↧
↧
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Anunua Hisa Zake Na Za Mke Wake Toka Vodacom Tanzania Zenye Thamani Ya Shilingi Milioni 20
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amenunua hisa za kampuni ya Vodacom Tanzania Plc zenye thamani ya sh. milioni 10 pamoja na nyingine za sh. milioni 10 kwa ajili ya mke wake, Mary Majaliwa.
Waziri Mkuu amechukua hatua hiyo Ijumaa, Mei 5, 2017 wakati akizungumza na waandishi wa habari mbele ya wakuu wa Masoko ya Hisa na Dhamana; Soko la Hisa la Dar es Salaam, viongozi wa Baraza la Uwezeshaji na kampuni ya Vodacom katika ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Magogoni jijini Dar es Salaam.
Waziri Mkuu amewasihi Watanzania walioko ndani na nje ya nchi wachangamkie fursa ya kununua hisa hizo ili waweze kuwa wamiliki wa kampuni kupitia hisa zao. “Hii ni fursa kwa Watanzania kumiliki kampuni. Ukinunua hisa, unashiriki kikamilifu kumiliki kampuni na pia unaboresha uchumi wako binafsi. Ninawasihi Watanzania wote tumieni fursa hii kununua hisa hizo kabla muda haujaisha,” alisisitiza.
Alisema watumishi wa umma wamepewa ya kununua hisa hizo kupitia mipango iliyowekwa na Makatibu Wakuu wao lakini pia amewasihi viongozi mbalimbali wa Serikali na taasisi wachangamkie fursa hiyo ili nchi iweze kupata kodi kupitia makampuni hayo.
“Hii ni fursa kwa kila Mtanzania, kwa viongozi kwa taasisi na mashirika ya umma, taasisi binafsi, wajasiriamali wadogo kama akinamama lishe au madereva wa bodaboda. Watanzania walioko nje ya nchi (Diaspora) nao pia wanunue hisa kwani watakuwa wanachangia uchumi wa nchi na wakati huo wanaweka akiba nyumbani,” aliongeza.
Akimkaribisha Waziri Mkuu kuzungumza na hadhira hiyo, Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Philip Mpango uwekezaji kwenye hisa ni njia mojawapo ya kuwawezesha Watanzania kumiliki uchumi wa nchi.
“Huko mtaani ukisema uchumi wa nchi unakua, watu wanabisha wakidai kuwa hawaoni unakua kwa sababu hawana fedha mifukoni. Hii ni fursa nyingine ya kuwawezesha kukua kiuchumi, ninaomba waichangamkie,” alisema.
Alisema sekta ya mawasiliano ni miongoni mwa sekta inayokua kwa kasi hapa nchini kwani katika robo tatu ya mwaka, sekta hiyo imekua kwa asilimia 11.3. “Niwasihi Watanzania wenzangu, tununue hisa za Vodacom ili tuweze kuboresha uchumi wetu,” alisema.
Alisema anatoa ombi maalum kwa wafugaji kukubali kuuza mifugo yao na kununua hisa ili kupunguza idadi ya mifugo yao, jambo ambalo alisema litapunguza migogoro baina yao na wakulima.
“Wakulima wa vitunguu, alizeti, maua au wafugaji wa samaki nao pia wanaweza kununua hisa na kuwa na mitaji kwa ajili ya shughuli zao. Ninawasihi wote watumie fursa hii ili kumiliki kampuni,” alisema.
Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Soko la Mitaji na Dhamana, Bi. Nassama Masinda alisema amefurahishwa kuona Waziri Mkuu akinunua hisa za kampuni ya Vodacom katika soko la awali.
Alisema uuzwaji wa hisa hizo ni utekelezaji wa Sheria ya Fedha ya mwaka 2016 kwa lengo la kuwawezesha Watanzania kuwa wamiliki wa makampuni ya simu za mikononi hapa nchini. “Marekebisho ya Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta sura ya 306 yanazitaka kampuni za simu na mawasiliano ya kielektroniki kuuza si chini ya asilimia 25 ya hisa zao kwa umma wa Tanzania kupitia masoko ya mitaji (IPO).”
Alisema baada ya hapo hisa hizo zinapaswa kuorodheshwa kwenye soko la Hisa la Dar es Salaam baada ya kukidhi matakwa ya Sheria ya Masoko ya Mitaji na Dhamana, sura ya 79. Kampuni ya Vodacom ilitoa hisa milioni 560 kwa umma kwa bei ya sh. 850 kila moja na hivyo kutarajia kukusanya sh. bilioni 476.
Alisema hivi sasa, wawekezaji kwenye masoko ya mitaji ni watu 500,000 tu ikilinganishwa na Kenya ambayo ina wawekezaji milioni 1.7; Uganda (40,000) na Rwanda (14,000). “Vodacom ina wateja milioni 6.2, iwapo nusu ya wateja wake wote watashiriki ununuzi wa hisa, idadi ya wawekezaji kupitia masoko ya mitaji na dhamana itaongezeka kwa asilimia 1,140. Na haya yatakuwa ni mageuzi makubwa katika sekta ya masoko ya mitaji si hapa nchini tu bali katika Afrika Mashariki,” alisema.
Mtendaji Mkuu wa Dodacom, Bw. Ian Ferrao alisema mauzo ya hisa yanayofanywa na kampuni hiyo ni makubwa mara nne ya mauzo ambayo yamewahi kufanyika hapa nchini.
Alisema kampuni hiyo ambayo imekwishafanya kazi kwa miaka 17 hapa nchini, imewekeza zaidi ya sh. trilioni mbili katika mtandao wa mawasiliano nchini Tanzania.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
IJUMAA, MEI 5, 2017.
↧
Video : Darassa aachia video Mpya ya ‘Hasara Roho’......Isikilize Hapa
Rapa aliyetikisa mitaa na vyombo vya habari na kuzipa shida baadhi ya nyimbo za wasanii wakubwa kushindwa kufanya vizuri kwa muda, Darassa wa ‘Muziki’ amerejea tena na ‘Hasara Roho’.
Ni ngoma ambayo bado inaendeleza mtindo usio na jina maalum wa rapa huyo, ulio na mchanganyiko wa asili ya Afrika na ngano za kisasa.
Video hiyo iliyoongozwa na Hanscana, ni moja kati ya video bora za Darassa zikiwa na matukio ya uswahilini, ushuani huku zikinogeshwa na mtindo wa kucheza alioubatiza jina la ‘Kuhangaika’. Hata hivyo, mtindo huo pia uliwahi kubatizwa jina la ‘flying swag’.
==>Itazame hapo chini
↧
AUDIO: Wolper na Harmonize Wapigana Chini......Msikilize hapa Harminize Akifunguka
Msanii wa muziki kutoka WCB, Harmonize Alhamisi alithibitisha kuachana na malkia wa filamu, Jacqueline Wolper.
Huenda wawili hao wamezinguana siku za karibuni, kwani Machi 16 mwaka huu Harmonize aliachia project yake ya wimbo ‘Niambie’ ambayo ndani yake Wolper alicheza vitendo na pia walishirikiana kwenye ishu ya promotion ya wimbo huo.
Akiongea katika kipindi cha Leo Tena, Harmonize amedai alikuwa na mipango mingi na Wolper lakini ameona bora aachane naye ili aupeshe shari.
“Sipo katika mahusiano, inshort kila mtu ana maisha yake ‘tumeachana'” alisema Harmonize .
Pia muimbaji huyo alikanusha taarifa za kwenye mitandao kuwa anatoka kimapenzi na msichana wa kizungu.
Hata hivyo hakuweka wazi sababu maalum ya kuachana na mpenzi wake huyo aliyedumu naye kwa muda mrefu pamoja na kumtambulisha kwao.
==>Msikilize hapo chini akiongea
↧
More Pages to Explore .....