Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Zitto Kabwe: Serikali Idhibiti Mfumuko wa Bei Kupunguza Ugumu wa Maisha kwa Wafanyakazi

$
0
0
Wakati wafanyakazi jana walisherehekea Siku ya Wafanyakazi Duniani ‘Mei Mosi’,  Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo,  Ziito Kabwe, ameleeza  kilio chake  kuhusu makato ya  mifuko ya hifadhi ya jamii pamoja na jinsi kampuni zinavyopoteza asilia 5 la pato la taifa.

*** Hizi ni  Salaam za Kiongozi wa ACT Wazalendo Kwa Wafanyakazi wa Tanzania, Mei Mosi 2017

Ndugu Wafanyakazi

Leo (JANA )ni siku yenu katika mwaka. Kama ilivyo kawaida siku hii husherehekewa kwa maadhimisho makubwa ambapo Waajiri (Serikali na Sekta Binafsi) na waajiriwa hutoa hotuba mbalimbali. Wakati mwengine ni siku kama siku nyengine tu za miaka ya nyuma, hotuba, ahadi, kula na kunywa. Hata hivyo Wafanyakazi wa Tanzania wana changamoto nyingi sana na ni vema kutumia siku hii kutafakari Kwa kina changamoto hizi na kutafuta majawabu yake.

Sisi ACT Wazalendo tunaamini katika siasa za Kijamaa, siasa zenye kupigania zaidi maslahi ya wanyonge, Wafanyakazi, Wakulima, Wavuvi na Wakwezi. Katika salaam zangu mwaka huu nawaomba mtafakari hotuba yangu hii niliyotoa Arusha tarehe Machi 25, 2017 na mapendekezo machache ninayoyatoa mwishoni mwa waraka wangu huu kwenu.

Nchini Tanzania Wafanyakazi kwenye sekta rasmi ni milioni 2.1 sawa na 9% tu ya nguvu kazi yote ya Taifa. Hawa wameajiriwa kwenye sekta binafsi (1.4m sawa na 67%) na sekta ya umma (700,000 sawa na 33%). Hawa wanalipwa mishahara na posho mbalimbali kama chanzo cha mapato yao.

91% ya Watanzania wapo kwenye sekta isiyo rasmi na rekodi ya mapato yao yaweza kuwa kizungumkuti kuipata. Hata hivyo tunajua kuwa wengi wameajiajiri wenyewe kwenye kilimo na biashara ndogo ndogo, uvuvi, ufugaji, uchimbaji wa madini na utoaji huduma.

Ni muhimu kusisitiza kuwa Watanzania wengi hawamo kwenye ajira rasmi au isiyo rasmi. Taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa ya mwaka 2015 inaonyesha kuwa Jijini Dar es Salaam kwa mfano ni asilimia 60 tu ya wakazi wake wapo kwenye ama ajira rasmi au ajira isiyo rasmi na asilimia 40 hawana kazi yeyote.

Uchambuzi pekee ambao tunaweza kuufanya kwa sasa ni kwa kutumia vyanzo vya mapato ya serikali ambapo tutaona mchango wa Wafanyakazi kwenye mapato ya Serikali kulingana na vyanzo yake vya mapato.

Kwa mfano, Kitabu cha Mapato ya Serikali Kuu cha mwaka 2016/17 kinaonyesha kuwa Wafanyakazi wote wa sekta ya Umma na Sekta Binafsi watachangia jumla ya shilingi trilioni 3 kwenye mapato yote ya Serikali kulinganisha na wenye mitaji (waajiri) ambao watachangia jumla ya shilingi bilioni 900 tu kutoka kwenye kodi za faida/gawio, ongezeko la mitaji na riba (taxes on income/interests, profits and capital gains).

Hata ukitazama miaka miwili ya nyuma utaona kwamba mwaka 2015/16 makampuni yalichangia shilingi 773 bilioni wakati Wafanyakazi walichangia shilingi 2.2 trilioni na mwaka 2014/15 makampuni yalichangia shilingi 600 bilioni na wafanyakazi shilingi 1.9 trilioni kama kodi zao kwenye mapato ya Serikali. Kwa kutumia kigezo cha Kodi za Mapato, matajiri (waajiri) wanachangia robo tu ya mapato yote ya serikali na wafanyakazi wanachangia robo tatu iliyobakia. Hii inachangia sana kuwepo kwa tofauti ya kipato ndani ya jamii.

Kwanini wafanyakazi wanachangia zaidi kuliko wenye mitaji ni swali ambalo tutalieleza. Sababu kubwa ni kuwa wenye Miraji/Mabepari wana fursa ya kukwepa kodi kisheria wakati wafanyakazi hawana uwezo huo. Kodi za wafanyakazi hukatwa moja kwa moja na waajiri kutoka kwenye mishahara yao.

Kwanini Kodi za Makampuni ni kidogo kuliko za Wafanyakazi?

Wafanyakazi wao hukatwa kodi zao kutoka kwenye mishahara yao moja kwa moja ikiwemo pia makato mengine kama michango kwenye mifuko ya Hifadhi ya Jamii na Bima ya Afya. Makato hayo huanzia asilimia 9 kwa mishahara ya ngazi ya chini mpaka asilimia 30 kwa wenye kulipwa mishahara ya juu kabisa. Kwa hiyo kodi ya wafanyakazi ni kodi ambayo serikali ina uhakika nayo moja kwa moja. Kwa takwimu ambazo tumeziona tayari, ni wafanyakazi wa sekta rasmi tu ndio hubeba mzigo wote wa kodi za wafanyakazi hapa nchini. Lakini kwanini kodi zinazotokana na mapato ya makampuni ziwe kidogo kuliko kodi zinazotokana na mapato ya wafanyakazi?

Kwenye makampuni, Kodi ya Mapato ni asilimia 30 ya faida ambayo kampuni imepata. Lakini mapato yanayokusanywa kwenye kodi hii ni kidogo sana kama tulivyoona, shilingi bilioni 900 tu kati ya mapato yote ya serikali mwaka 2016/17 sawa na asilimia nne tu ya mapato yote ya serikali yanayokusanywa na Mamlaka ya Mapato Tanzania. Hali halisi hii sio ya Tanzania peke yake.

Mwanazuoni Thomas Piketty anaeleza kuwa "Ingawa kodi za faida za makampuni ni kati ya asilimia 40 - 50 kwenye nchi za magharibi, mapato kwenye kodi hizi hayazidi asilimia 2.5 - 3 ya Pato la Taifa. Nadharia ya faida inayotozwa kodi ni nyembamba kuliko nadharia ya mapato ghafi ya ziada kwa sababu makampuni huondoa gharama za uchakavu wa mitambo, riba kwa mikopo na hata gharama za bima. Kodi kwenye faida imegubikwa na matundu mengi kwenye mfumo mzima wa kodi duniani" (msisitizo ni wangu).

Matundu haya ndiyo njia za ukwepaji kodi zinazofanywa na makampuni na hasa makampuni ya kimataifa (Multinational Corporations). Nchi za Afrika zimeathirika mno na mfumo wa kodi wa kimataifa na hivyo kupelekea fedha nyingi kutoka Afrika kutoroshwa kwenda ughaibuni. Azimio la Tabora la Chama cha ACT Wazalendo limeeleza kidogo kadhia hii ambayo Serikali za Afrika hazitilii maanani kabisa licha ya taarifa nzuri ya Rais mstaafu Thabo Mbeki wa Afrika ya Kusini.

Katika kitabu cha 'Africa’s Odious Debts: How Foreign Loans & Capital Flight Bled a Continet' waandishi Leonce Ndikumana na James Boyce, wameonesha kwamba katika kipindi cha miaka 40 iliyopita, jumla ya dola za Kimarekani bilioni 11.4 (wastani wa shilingi trilioni 24) zimetoroshwa kutoka Tanzania kwa njia mbalimbali.

Hizi ni sawa na wastani wa dola za Kimarekani 285 milioni kutoroshwa kila mwaka kuanzia mwaka 1970 mpaka 2010. Sehemu kubwa ya fedha hizi zinatoroshwa na makampuni makubwa ya kigeni yanayofanya biashara na kuwekeza hapa nchin. Africa Progress Panel na kikosi kazi kilichoongozwa na Rais Thabo Mbeki ilieleza kuwa Afrika hupoteza zaidi ya dola za kimarekani bilioni 50 kila mwaka kutokana na utoroshaji wa fedha unaofanywa hususan na makampuni haya ya kimataifa.

Inasemekana asilimia 30 ya utajiri wa fedha wa bara la Afrika umewekwa kwenye pepo za kodi (tax havens) kwa mujibu wa kitabu cha 'The Hidden Wealth of Nations' kilichoandikwa na Gabriel Zucman, mhadhiri wa London School of Economics.

Katika kitabu hicho, Zucman ameonyesha takwimu kutoka Benki ya Taifa ya Uswisi zinazothibitisha kuwa takribani dola za kimarekani bilioni 150 kutoka Afrika zimehifadhiwa kwenye mabenki ya nchi hiyo. Jumla ya Pato la Taifa (GDP) ya nchi zote za Jumuiya ya Afrika Mashariki ni dola za kimarekani 147.3 bilioni, hivyo fedha za Afrika zilizopo Uswisi ni zaidi ya GDP ya Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi kwa pamoja. Fedha hii ni mara tano ya gharama za kujenga mradi wa Inga Dam kule Kongo ambao ungeweza kuzalisha umeme wa kutosha bara zima la Afrika.

Pamoja na mambo mengine, matundu haya ya ukwepaji kodi yamejengwa ndani ya mfumo wa kodi za kimataifa. Kuna kitu kinaitwa kwa lugha ya kigeni Base Erosion and Profit Shifting ikiwa na maana kuwa makampuni ya kimataifa yanapowekeza hapa nchini huhamisha faida kupeleka nchi zenye viwango vidogo vya kodi na hivyo kutolipa kabisa kodi hapa nchini ama kulipa kodi kiduchu sana.

Kwa mfano, katika kukokotoa kodi kampuni huondoa gharama za riba za mikopo, bima na gharama za utawala na kinachobakia ndio faida ambayo hutozwa kodi. Kampuni hizi huchukua huduma hizi za mikopo, bima na utawala kutoka kwa makampuni dada na kuongeza gharama maradufu na hivyo kuhamisha fedha hizi kana kwamba wanalipia hizi gharama na hivyo kupunguza sana wigo wao wa kodi. Ndio maana siku za nyuma tulisikia kampuni za madini hazilipi kodi ya mapato kwa sababu nyingi zilikuwa zikitumia mtindo huu wa kumomonyoa wigo wa kodi.

Wakati nikiwa mmoja wa wajumbe wa Kamati ya Madini ya Jaji Mark Bomani tulikuta ushahidi wa kampuni ya Geita Gold Mines ambayo uwiano wa mtaji wake na mikopo (debt-equity ratio) ulikuwa asilimia milioni 12. Hii iliifanya kampuni hii kumomonyoa kila walichokipata katika uchimbaji wa dhahabu nchini kwetu na kukihamishia njia kana kwamba ni malipo ya mikopo waliyochukua kumbe ni mbinu ya kukwepa kodi na kupora dhahabu ya Tanzania. Nilipokuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali, tuliagiza ukaguzi wa ukwepaji kodi unaofanywa na makampuni ya kimataifa na iligundulika kuwa karibia kila sekta ya uchumi ilihusika na ukwepaji kodi.

Mfano ambao huwa naukumbuka mara kwa mara ni mfano wa mauzo yetu ya Korosho kwenda nje. Hupenda kuurudia na nitaurudia tena hapa. Mwaka 2011 Tanzania iliuza Korosho kwa nchi ya India. Kwenye rekodi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania ilionyesha kuwa tuliuza tani 80,000 za korosho kwa bei ya dola za marekani 1000 kwa kila tani sawa na dola za kimarekani 80 milioni.

Uchunguzi ulionyesha kuwa katika nchi ya India rekodi yao ya Korosho walizonunua kutoka Tanzania ilikuwa ni dola za kimarekani 120 milioni kwa sababu wao walinunua tani 120,000 za korosho kutoka Tanzania. Hii ina maana kuwa tani 40,000 hazikurekodiwa kwenye forodha zetu na hivyo wauzaji kukwepa kodi ya ushuru wa korosho wa zaidi ya dola za kimarekani 12 milioni.

Pia kwenye kodi ya Mapato ya kampuni iliyouza korosho hizi mapato ya zaidi ya dola 40 milioni hayatoonekana na hivyo kufanikiwa kukwepa kodi. Huu ni mfano ninaopenda kuuleza katika kueleza namna mfumo wetu wa kodi ulivyojaa matundu na kuhitaji kufanyiwa kazi kubwa ya kuufumua.

Kwa hiyo makampuni yana njia nyingi za kukwepa kulipa kodi na hivyo wamiliki wake kujilimbikizia mali nyingi na kuongeza tofauti ya kipato miongoni mwa wananchi. Kama hatua madhubuti hazitachukuliwa tofauti ya kipato itazidi kuongezeka na kuleta hatari kubwa kwa ustawi wa wananchi na usalama wa nchi yetu.

Moja ya suala ambalo chama cha ACT Wazalendo ililieleza na halikuelezwa na chama kingine chochote katika kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 ilikuwa ni hili la kufanya marekebisho ya mfumo wa kodi ili kila anayepaswa kulipa kodi alipe kwa haki na kwa uwazi.

Tuliahidi "kuweka mfumo mpya wa kodi za kimataifa ili kuzuia makampuni ya kimataifa kumomonyoa wigo wa kodi kwa kushiriki kikamilifu katika kampeni za kimataifa za kurekebisha mfumo wa kodi za kimataifa, kupitia mikataba ya kikodi na nchi nyengine ili kuzuia ukwepaji kodi na kujengea uwezo kitengo cha kodi za kimataifa ili kudhibiti ukwepaji kodi".

Serikali ya Awamu ya Tano imefanya nini katika eneo hili?

Serikali ya Awamu ya Tano ilisifika kwa makusanyo makubwa ya kodi katika miezi yake ya mwanzo ya kuongoza nchi yetu. Lakini haijafanya juhudi yeyote ya ndani au ya nje kuhakikisha kuwa nchi inaondoa tofauti kubwa ya kipato kati ya wenye nacho na wasio nacho. Juhudi hizi za kukusanya kodi hazijaweza kupunguza mzigo Wa kodi kwa wafanyakazi wa Tanzania.

Juhudi za kuendesha kampeni ya kimataifa ili kuboresha mfumo wa kodi za kimataifa zimeshuka chini na kiukweli kama nchi tumerudi nyuma wakati dunia nzima inashiriki kwenye kampeni hizi. Juhudi za ndani za kuongeza makusanyo ya kodi kama hazitatazama mfumo wa kodi za kimataifa, basi hazitakuwa na faida yeyote na tutabakia na kodi za wafanyakazi na vibarua tu tukiwakamua zaidi ili kupata fedha za kuendesha nchi yetu.

Tunapendekeza nini?

1. Serikali ifanye marekebisho ya sheria mbalimbali za kodi zinazohusisha makampuni ya kimataifa (MNCs) ili kuzuia kumomonyoa wigo wa kodi ( Base Erosion and Profit Shifting) kunakofanywa na kampuni hizi. Hili linawezekana kwa Serikali kuchukua hatua ya kupitia mikataba ya kikodi (double taxation treaties) ambayo Tanzania iliingia na nchi nyingine duniani.

Tafiti mbalimbali katika eneo hili zinaonyesha kuwa Tanzania hupoteza 5% ya Pato la Taifa kutokana na vitendo vya kampuni kubwa kukwepa kodi kwa kutumia mbinu za kihasibu (tax planning measures). Serikali yetu inapaswa kushirikiana na Serikali nyengine za nchi mbalimbali duniani katika kampeni ya kimataifa ya haki za kodi (International Tax Justice Movement).

Vyama vya Wafanyakazi nchini vinapaswa kuwa mbele kuishinikiza Serikali kushiriki kwenye kampeni hizi na pia kufanya mabadiliko makubwa kwenye sheria zetu za kodi ili kulinda wigo wetu wa kodi.

2. Serikali itazame upya michango ya wafanyakazi kwenye Mifuko ya Hifadhi ya Jamii. Viwango vya michango Kwa Tanzania vipo juu mno na vinapunguza kipato cha mfanyakazi na kuongeza gharama kwa waajiri. Michango ya Hifadhi ya Jamii ishushwe mpaka jumla ya 12% ya mshahara; kwa Waajiri kuchangia 7% na Wafanyakazi kuchangia 5% ya mishahara yao.

Hii itasaidia kupunguza gharama za kuajiri kwa Waajiri. Vile vile Tozo ya mafunzo SDL ishushwe mpaka 3% . Eneo hili ni muhimu liangaliwe kwa muktadha wa kukuza ajira nchini hivyo ajira zinapoongezeka mapato kwenye maeneo haya yanaongezeka pia.

3. Serikali idhibiti mfumuko wa bei kuhakikisha inapunguza gharama za maisha kwa wafanyakazi. Katika wakati kama huu ambao bei za vyakula zimepanda zaidi ya mara 2 kipato cha wafanyakazi wengi nchini kimebaki palepale, hali hii inaongeza ugumu wa maisha kwao. Ni muhimu Serikali kuchukua hatua mahsusi kudhibiti mfumuko wa bei za vyakula nchini.

Mwisho, Wafanyakazi wa Tanzania, nawakumbusha kuwa kuna mahusiano chanya kati ya maslahi yenu na aina ya uongozi wa kisiasa uliopo kwenye nchi. Msikae pembeni kwenye harakati za mabadiliko ya kisiasa nchini. Vyama vya Wafanyakazi vina nguvu zaidi ya kuhamasisha na kuweka mazingira mazuri ya kidemokrasia na utawala wa kikatiba nchini.

Nawatakia Mei Mosi Njema.

Kabwe Z. Ruyagwa Zitto
Kiongozi wa Chama, ACT Wazalendo
Dar Es salaam.
Mei 1, 2017

Video: Kipindi cha Maswali na Majibu Bungeni leo May 2, 2017

$
0
0
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limeendelea leo May 2, 2017 mjini Dodoma kwa kipindi cha maswali na majibu katika Bunge la Kumi na Moja, Mkutano wa Saba na Kikao cha Kumi na Tano.

==>Unaweza kutazama video hapo chini

Maamuzi ya Kamati Ya Maadili Baada ya Paul Makonda Kukutwa na kosa la kuingilia uhuru wa Bunge

$
0
0
Kamati ya Maadili, Haki na Madaraka ya Bunge la Tanzania, leo imewasilisha bungeni taarifa za matukio mbalimbali ambazo imezifanyika kazi ikiwa ni pamoja na kuwaita na kuwahoji wahusika kwa kukiuka kanuni za bunge nje na ndani ya bunge hilo.

Miongoni mwa taarifa hizo ni pamoja na ile ya kuingilia uhuru wa bunge kosa lililofanywa na Paul Christian Makonda na Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Alexander Mnyeti.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka bungeni, viongozi hao wate wawili wamesamehewa kutokana na kukiri makosa yao na kuliomba radhi bunge la Tanzania.

Aidha, Kamati ya Maadili ya Bunge imemsamehe Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe baada ya kukiri kutoa lugha ya kudharau mamlaka ya bunge.

Pia Kamati ya Maadili ya Bunge imemuadhibu Mbunge Halima Mdee  kutohudhuria vikao vya Bunge la Bajeti vilivyosalia kwa kudharau mamlaka ya bunge.

Hata hivyo, Bunge limeazimia kumsamehe mbunge huyo  baada ya Wabunge wa pande zote kumuombea msamaha .

Katika hatua nyingine,Mbunge wa Bunda Mjini, Ester Amos Bulaya amepewa karipio kali na Kamati ya Maadili ya Bunge kwa kosa la kudharau Mamlaka ya Spika wa Bunge.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya May 3

Kesi ya Wema Sepetu Kutumia BANGI Yapigwa Kalenda

$
0
0

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imeambiwa kwamba upelelezi wa kesi ya kukutwa na bangi inayomkabili Muigizaji maarufu, Wema Sepetu na wenzake umekamilika.

Hatua hiyo imefikiwa   ambapo upande wa Jamhuri mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba alisema kwamba upelelezi umekamilika dhidi ya msanii huyo na wakili wa Serikali Helleni Mushi aliomba kesi hiyo kuarishwa  na kupangwa tarehe ya kuanza kusikilizwa ili watuhumiwa waanze kusomewa maelezo ya awali.

Katika kesi ya msingi, Wema anatuhumiwa kukutwa na msokoto mmoja wa bangi na vipande viwili vidogo vya bangi vyenye uzito wa gramu 1.08. 

Mbali na Wema washitakiwa wengine ni wafanyakazi wake wa ndani Angelina Msigwa (21) na Matrida Abas (16), ambapo wote wanashtakiwa kwa kosa moja la kukutwa na kiasi hicho cha dawa za kulevya.

Inadaiwa kuwa Wema na wenzake walitenda kosa hilo Februari 4 mwaka huu, nyumbani kwao Kunduchi Ununio , Wilaya ya Kinondoni Mkoa wa Dar es Salaam.

Hakimu Simba alisema  kesi hiyo itaanza kusikilizwa, Juni Mosi, mwaka kwa watuhumiwa kuanza kusomewa maelezo ya awali.

Jinsi Punyeto Inavyo Sababisha Ukosefu Na Upungufu Wa Nguvu za Kiume

$
0
0

Ukosefu  na/ama  upungufu  wa  nguvu  za  kiume, ni  tatizo  linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume  duniani.  Zipo  sababu  nyingi  zinazo  sababisha  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume.  

Miongoni  mwa  sababu  hizo  ni  pamoja  na  maradhi  kisukari, presha,shinikizo  la  damu, moyo, figo, matatizo  kwenye  mishipa  ya  ubongo  &  mishipa  ya  uti  wa mgongo, matatizo  kwenye  mishipa itumikayo  kusafrisha damu  mwilini, maradhi  ya  ngiri,  pamoja  na   upigaji  punyeto  kwa  muda  mrefu.

Katika  makala  yetu  ya  leo, tutaangalia  namna   suala  la  upigaji  punyeto linavyo  athiri  nguvu  za  kiume.

Kabla  hatujaangalia  namna  suala la upigaji  punyeto linavyo  maliza  nguvu  za  kiume, ni  vyema  tukafahamu  kwanza  kuhusu  SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME.

Kufahamu   kuhusu   SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME  tafadhali  tembelea :

Ukisoma  vizuri  kuhusu  mfumo  wa  nguvu  za  kiume, utagundua  kuwa   Suala  la  nguvu  za  kiume  ni  suala  la  kimfumo.  Ili  mwanaume  awe na nguvu  za  kiume, aendelee  kuwa  na  nguvu  za  kiume na  azilinde  nguvu  zake za  kiume, ni  lazima  ogani  zote zinazo  husika  na  mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ziwe  na  afya  njema  na  ziwe  na  ushirikiano   thabiti  na  wenye  afya.

Vile  vile , utagundua  kuwa , mambo  makuu  muhimu  katika   mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ni  kama  ifuatavyo:

i.Mishipa  imara  ya  ubongo  na  yenye  afya  njema

ii. Mishipa  imara  ya  uti  wa  mgongo  (  spinal  cords )

iii.Mishipa  imara  itumikayo  kusafirisha  damu  mwilini  (  Blood Vessels )

iv. Mfumo  imara  wa  usafirishaji  damu  mwilini

v. Mishipa  ya  uume  iliyo  imara  na  yenye  afya  njema

vi. Uhusiano  imara  na  wenye  afya  kati  ya  mishipa  ya  fahamu  iliyopo  katika  ubongo, mishipa  ya  kwenye  uti  wa  mgongo  pamoja  na  misuli & mishipa  ya  kwenye  uume.

Hivyo  basi, ili  mwanaume  aweze  kuwa  na  nguvu  imara  za  kiume, na  aendelee  kuwa  na  nguvu  hizo ni  lazima  mambo  yote  muhimu  katika  mfumo  wa  nguvu za  kiume  yawe  imara  pasi na  hitilafu  yoyote.

Hitilafu  yoyote  katika  mambo  hayo, itasababisha  ukosefu na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume  kwa  mwanaume  huyo.  Pale inapotokea    hitilafu  ama  mapungufu  katika  ogani  zaidi  ya  moja  kati  ya  zilizo  tajwa hapo  juu, basi  tatizo  kwa  muhusika  huwa  kubwa  mara  dufu.

JINSI  PUNYETO  INAVYO  SABABISHA  TATIZO  LA  UKOSEFU &  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.
Mwanaume   anapopatwa na  wazo  la  kufanya  tendo  la  ndoa, ubongo  hutoa  ishara  kwenye  mishipa  ya  uti  wa  mgongo  ambayo  nayo  husafirisha  taarifa  hadi  kwenye  mishipa &  misuli  ya  uume.

Mishipa  ya  uume inapopokea  taarifa  hiyo, hutanuka. Na  mishipa  ya  uume  inapotanuka, hufanya  mambo  mawili  muhimu  sana :

i.Husababisha  mishipa  ya  ateri  kupanuka  na  hivyo  kuruhusu  damu  kuingia kwa  kasi  sana   ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  hivyo  kuufanya  uume  usimame  na  kuwa  imara  bara bara.

ii. Huibinya na  kuiziba  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kuzuia  kunyonya  ama  kufyonza  damu  iliyo  ingia  ndani  ya  mishipa ya  uume.  (  KAZI  KUBWA  YA  MISHIPA  YA  VENA  ILIYO  KARIBU NA  MISHIPA  YA  UUME  NI KUHAKIKISHA  HAKUNA  DAMU NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME. HIVYO  BASI  DAMU  INAPOINGIA  NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME, MISHIPA  YA  VENA  HU “SENSE” JAMBO  HILO  KWA  HARAKA  NA HIVYO  KUIFYONZA  DAMU  HIYO  KUTOKA KWENYE MISHIPA  YA UUME  YA  KUITOA  NJE YA MISHIPA  YA  UUME.  NA  DAMU INAPOKOSEKANA  NDANI  YA  MISHIPA  YA  UUME, HUUFANYA  UUME  KUSINYAA  NA  KULEGEA )

Mtu  anayepiga  punyeto  husababisha  mambo  yafuatayo  katika  mwili  wake :

1. Huuwa  nguvu  ya  mishipa  & misuli ya  uume ambayo  ndio  inayo husika  na  kusimama  kwa  uume

2. Mishipa  ya   uume  inapo  sinyaa  na  kukosa  nguvu  yake  ya  asili, husababisha  mambo  yafuatayo :

i.Huondoa  uwezo  wa  mishipa  &  misuli  ya  uume  kutanuka, na  hii  ndio  sababu  inayo  wafanya  waathirika  wa  punyeto  kutumia  nguvu  nyingi  sana  katika  kuufanya  uume  usimame.

ii.Huondoa  uwezo  wa  mishipa &  misuli  ya  uume  kuibana  na  kuiziba  mishipa  ya  vena, na  hii ndio  sababu  inayo  fanya  waathirika  wa  punyeto  kufika  kileleni  haraka  sana, kwani damu  inayo  ingia  kwenye misuli  ya  uume   hufyonzwa  ndani ya  muda  mfupi sana. 
 
 Hii  hutokea  kwa  sababu  mishipa na  misuli  ya  uume inakuwa  imelegea,na  mishipa  ya  vena inakuwa  imepwaya, hivyo  msuguano wowote ule  hufanya  mishipa  ya  vena  kufunguka  na  kufyonza  damu  kutoka  kwenye mishipa  ya  uume  na hivyo  kuufanya  uume  kusinyaa  ndani ya dakika ama sekunde  chache sana.

3. Vile  vile  punyeto  hufanya  uume  kusinyaa na  kurudi ndani  na  kuufanya  uonekane kama  uume  wa  motto mdogo.

Kwa  ufupi  punyeto  husababisha  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  sababu  kuu  zifuatazo :

i.Kwanza   hudhoofisha  na  kuharibu  mishipa  ya  uume,  ambayo  ndio  hufanya  uume kusimama.

ii.Pili  hudhoofisha  utendaji  kazi  wa  mishipa  ya  ateri, ambayo  ndio  hutumika  kama  njia  ya  kusafirisha  damu kupeleka kwenye  misuli  ya  uume  na  ivyo  kuufanya  uume  usimame

iii. Tatu, punyeto  hupelekea  kuvuja  kwa  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kusababisha  damu  kufyonzwa  kwa  haraka  sana  kila  iingiapo ndani  ya  misuli ya  uume  na  matokeo  yake  ni  uume   kusimama  kwa  muda  mfupi  sana  wakati wa  tendo  la  ndoa.

iv. Punyeto  huathiri  mtiririko  wa  damu  kwenda  kwenye  mishipa  ya  uume, kwa  sababu  hudhoofisha  misuli &  mishipa  ya  uume  pamoja  na mishipa ya  ateri  ambayo  ndio  hutumika  katika  kusafirisha  damu kwenda  kwenye  uume

DALILI  ZA  MTU  ALIYE  ATHIRIWA  NA  PUNYETO
Dalili  kuu  za  mtu  aliye athiriwa  na  punyeto  ni  kama  ifuatavyo:

i.           Uume  kusinyaa  na  kuwa  kama  wa  mtoto
ii.         Uume kurudi  ndani
iii.       Uume  kusimama  ukiwa  legelege
iv.       Kufika  kileleni  haraka  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

TIBA   YA   NGUVU  ZA  KIUME  KWA MTU  ALIYE  ATHIRIKA  NA  PUNYETO.
Dawa   asilia  ya  nguvu  za  kiume iitwayo JIKO  ni tiba  bora  na  ya  uhakika  kabisa  kwa  mtu  aliye  athiriwa   na  punyeto.  Dawa  hii, pamoja  na  mambo  mengine  mengi, husaidia  kufanya  mambio  yafuatayo  katika  mwili  wa  mwanaume  aliye  athiriwa  na  punyeto :

i.Kuimarisha  mishipa  & misuli  ya  uume  ulio  legea na  hivyo  kuurejeshea  uwezo wake wa  asili

ii. Hutibu   tatizo  la  uume  kurudi  ndani

iii.Humaliza  tatizo  la  kusimama  kwa  uume  ukiwa  legelege

iv.Hutibu  na  kuponya  kabisa  tatizo  la  kufika  kieleleni  haraka.

BEI  YA  DAWA  :  Dawa  hii  inapatikana  kwa  gharama  ya  SHILINGI  ELFU  THEMANINI  TU (Tsh. 80,000/=)

MAHALI  INAPOPATIKANA :  Dawa  hii  inapatikana  katika  duka  la  dawa  asilia  liitwalo  NEEMA  HERBALIST  &  NUTRITIONAL  FOODS  CLINIC  lililopo  jijini  DAR  ES  SALAAM  katika  eneo  la  UBUNGO   nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA   karibu  na SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING.

Kwa  wateja  wasio  weza  kufika  ofisini  kwetu. Watafikishiwa  dawa  mahali  popote  walipo  jijini  DAR  ES  SALAAM.

Kwa   wateja  waliopo  mikoani  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  MABASI

Kwa  wateja  waliopo   Zanzibar  wata fikishiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa boti.

Na  kwa  wateja  waliopo  UGHAIBUNI  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  ama  DHL.

MAWASILIANO :  WASILIANA  NASI   KWA  SIMU  NAMBA  0766  53  83  84.

Kwa  taarifa  zaidi  kuhusu  huduma  zetu, tutembelee kila  siku  kwenye  blogu  yetu :

Kauli ya Mrisho Mpoto baada ya kutukanwa mtandaoni kwa kumuunga mkono Rais Magufuli

$
0
0
Msanii Mrisho Mpoto jana  May 2 ameamua kutumia ukurasa wake wa instagram kuandika kuhusiana na wale wanaomtusi na kumponda kutokana na kuonesha kuunga mkono utendaji wa Rais Magufuli.

 Mrisho Mpoto ameeleza kwa nini ameamua kumuunga mkono Rais Magufuli na  amesema ataendelea kumuunga mkono.

“Nimepokea matusi mengi, kebehi, na maneno machafu juu ya mimi kuunga mkono utendaji wa Rais Magufuli, kitu ambacho nakiamini kuna “KUKUBALIANA KWA KUTOKUBALIANA” lakini siyo kumtukana mtu mwingie siyo busara hata kidogo

“Kwakuwa tu hakusema au hakufanya ambacho nafsi yako ilipenda kusikia. Kilichonifanya niandike ujumbe huu ni kuwa nisiwekewe maneno mdomoni yakuwa nimesema Rais Magufuli ni Mungu, kwa wale ambao hawakuangalia sherehe za MEI MOSI jana

“Naomba niseme kuwa hayo maneno siyo kweli na yamebadilishwa kutoka kwenye ukweli wa niliosema, Mimi ni mtu mwenye hofu na Mungu siwezi kusema hivyo, kumekuwa na utamaduni ikitokea mtu anauunga mkono utendaji wa Rais kuna ibukuka kundi la wapinga Maendeleo na kuanza kutukana

“Naomba ijulikane kuwa sababu za kumuunga mkono Rais, yale niliyokuwa nayaongea huko nyuma naona yanafanyiwa kazi hivi sasa!! MRISHO MPOTO mpaka sasa namuunga mkono Rais MAGUFULI, Iwe nachumia tumbo kama inavyosemwa au nimevimbilwa kwa shibe
Nimepokea matusi mengi, kebehi, na maneno machafu juu ya mimi kuunga mkono utendaji wa Rais Magufuli, kitu ambacho nakiamini kuna "KUKUBALIANA KWA KUTOKUBALINA" lakini siyo kumtukana mtu mwingie siyo busara hata kidogo, kwakua tu hakusema au hakufanya ambacho nafsi yako ilipenda kusikia. Kilichonifanya niandike ujumbe huu ni kuwa nisiwekewe maneno mdomoni yakua nimesema Rais Magufuli ni Mungu, kwa wale ambao hawakuangalia sherehe za MEI MOSI jana, naomba niseme kuwa hayo maneno siyo kweli na yamebadilishwa kutoka kwenye ukweli wa niliosema, Mimi ni mtu mwenye hofu na Mungu siwezi kusema hivyo, kumekuwa na utamaduni ikitokea mtu anauunga mkono utendaji wa Rais kuna ibukuka kundi la wapinga Maendeleo na kuanza kutukana. Naomba ijulikane kuwa sababu za kumunga mkono Rais, yale niliyokua nayaongea huko nyuma naona yanafanyiwa kazi hivi sasa!! MRISHO MPOTO mpaka sasa namuunga mkono Rais MAGUFULI, Iwe nachumia tumnbo kama inavyosemwa au nimevimbilwa kwa shibe.
A post shared by mjombampoto (@mrishompoto) on

Kigogo Dawa za Kulevya Aondolewa Nchini.......Apelekwa Marekani

$
0
0
Anayedaiwa kuwa Kiongozi wa Taasisi ya Kusambaza Dawa za Kulevya nchini, Ally Haji, maarufu Shikuba na wenzake wawili, wamesafirishwa kimya kimya kwenda nchini Marekani usiku wa kuamkia jana.

Pamoja na rufaa iliyokatwa Mahakama Kuu ya Tanzania kupinga uamuzi huo, Serikali imewaondoa bila kutoa taarifa kwa mawakili wala ndugu wa watuhumiwa hao.

Taarifa za kupelekwa Marekani Shikuba na wenzake; Iddy Mfuru na Tiko Adam, zilipatikana jana kutoka vyanzo mbalimbali vya kuaminika, akiwamo mke wa mfanyabiashara huyo na mawakili wao.

Aprili 12, mwaka huu, Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, ilikubali maombi ya aliyekuwa Waziri wa Katiba na Sheria, Harrison Mwakyembe ya kutaka Watanzania hao washikiliwe na kusafirishwa kwenda Marekani kujibu mashtaka ya kusafirisha na kusambaza dawa za kulevya yanayowakabili nchini humo.

Baada ya uamuzi huo, Aprili 13, mwaka huu, mawakili wa Shikuba na wenzake; Hudson Ndusyepo, Majura Magafu na Adinani Chitale, waliwasilisha katika mahakama hiyo nia ya kukata rufaa na tayari waliwasilisha sababu za kukata rufaa Mahakama Kuu ya Tanzania kama sheria inavyowataka endapo hawakuridhika.

Mke wa Shikuba, Munira Ally, alipoulizwa, alikiri kwamba mumewe alishasafirishwa na hawakupewa taarifa kuhusu kuondoka kwao.

“Waliondoka jana (juzi) saa tano na dakika kumi na ndege ya KLM kuelekea Marekani, sisi tumepata taarifa wakiwa wameshaondoka, hatuna jinsi walishaondoka.

“Baba mkwe hali yake ni mbaya baada ya kupata taarifa hizi, pale nyumbani watu wanajua wanazungumza anasikia… huwa anasumbuliwa na ugonjwa wa sukari na shinikizo la damu.

 “Tunataka tukutane na mawakili tuzungumze nini cha kufanya, gerezani atakuwa kaacha vitu vyake, napanga utaratibu niende Gereza la Ukonga kufuata vitu mbalimbali zikiwemo nyaraka za rufaa,” alisema Munira.

Wakili Ndusyepo, akizungumzia hilo, alisema amesikia wateja wao wameondoka nchini juzi usiku, huku Serikali ikijua kwamba kuna rufaa Mahakama Kuu.

“Serikali inajua kuna rufaa imekatwa kupinga uamuzi wa Mahakama ya Kisutu, inaacha kuheshimu, sheria inadharauliwa, Katiba haifuatwi, leo wamefanyiwa hawa kesho watafanyiwa wengine, kuna haja ya kupiga kelele,” alisema.

Wakili Magafu alipotakiwa kuzungumzia suala hilo, alisema alipata taarifa ya kuondoka kwao kutoka kwa Ndusyepo.

Awali Aprili 10, mwaka huu, Serikali iliwasilisha maombi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu pamoja na vielelezo mbalimbali, ikiomba watuhumiwa wazuiliwe na kusafirishwa kwenda Marekani kujibu tuhuma za kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya.

Mahakama ilisikiliza maombi hayo Aprili 11, mwaka huu na kutoa uamuzi Aprili 12, ikibariki watuhumiwa hao kwenda nchini humo baada ya kujiridhisha kwa ushahidi uliotolewa mahakamani.

Hakimu Mkazi Mfawidhi, Cyprian Mkeha aliposoma uamuzi baada ya kusikiliza hoja za pande mbili, alisema mahakama kabla ya kuamua ilijiuliza maswali kadhaa, ikiwamo kama mashtaka wanayohusishwa nayo wajibu maombi yako katika utaratibu wa kubadilisha wahalifu.

Pia mahakama ilijiuliza na kubaini kuwa kuna makubaliano ya kubadilishana wahalifu kati ya nchi hizo mbili.

Hakimu Mkeha alisema kama wajibu maombi watakuwa wanapingana na uamuzi huo, mahakama inawapa nafasi ya kukata rufaa ndani ya siku 15 na walifanya hivyo.

Mwakyembe aliwasilisha maombi Februari 15, mwaka huu, akiomba mahakama hiyo kuamuru Shikuba, Mfuru na Adam washikiliwe wakati wakisubiri kibali cha kuwasafirisha kwenda Marekani kujibu tuhuma za kula njama, kusafirisha na kusambaza dawa za kulevya nchini humo.

Jamhuri ikiwakilishwa na Wakili wa Serikali Mkuu, Edwin Kakolaki, katika kuiridhisha mahakama iliwasilisha maombi na ushahidi dhidi ya wajibu maombi, kuonyesha kujihusisha kwao katika matukio hayo.

Ushahidi ulionyesha kwamba Marekani iliwachunguza wajibu maombi kwa miaka minne na walitumia Dola 10,000 kununua dawa hizo kutoka kwa taasisi yao ili kubaini ukweli.

Wajibu maombi ilibainika walikuwa wakisafirisha heroin na cocaine kwa kutumia magari, na wakifikisha dawa hizo Marekani huwatumia watu kusambaza kwa kutumia ndege binafsi na Shikuba ndio kiongozi wa taasisi hiyo.

Kakolaki alidai maombi yaliambatana na kiapo kilichoapwa na Richard Magnes ambaye anadai wajibu maombi wanatuhumiwa kuingiza dawa za kulevya zaidi ya kilo 1.78 Marekani.

Shikuba, ambaye amekuwa akihusishwa na biashara kubwa ya usafirishaji dawa za kulevya kati ya Afrika Mashariki, Asia, Ulaya na Marekani, alikamatwa mwaka 2014 nchini, akihusishwa na shehena ya kilo 210 za heroin zilizokamatwa mkoani Lindi mwaka 2012.

Serikali ya Marekani iliamua kutaifisha mali za mfanyabiashara huyo na kupiga marufuku kampuni za nchi hiyo kujihusisha na biashara zake.

Taarifa iliyotolewa na Kitengo cha Udhibiti wa Mali za Nje cha Wizara ya Fedha ya Marekani, ilieleza kuwa Shikuba ametambuliwa kama kinara wa usafirishaji wa dawa za kulevya kwa mujibu wa Sheria ya Utambuzi wa Vinara wa Dawa za Kulevya wa Nje ya nchi hiyo.

Kwa mujibu wa gazeti la The New York Times, sheria hiyo imekuwa ikitumiwa na Marekani kufuatilia wahalifu kadhaa wanaojihusisha na biashara hiyo duniani na kwamba Shikuba amekuwa akijaribu mara kadhaa kurubuni viongozi wa Serikali za Afrika kuepuka kukamatwa na kufunguliwa mashtaka kutokana na biashara zake haramu.

Imeelezwa kuwa tangu mwaka 2006, Shikuba amekuwa akiongoza wanachama wa mtandao wake kutuma shehena za dawa za kulevya kwenda sehemu kadhaa duniani kama China, Ulaya na Marekani.

VIDEO: Maalim Seif Afunguka Mambo Mazito Kuhusu Mgogoro wa CUF

$
0
0
Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad amesema kuwa Msajili wa Vyama vya Siasa Nchini ndiye anayejaribu kupandikiza mgogoro ndani ya chama hicho kwa maslahi yake binafsi.

Ameyasema hayo mapema hii leo alipokuwa akizungumza katika kipindi cha 360 kinachorushwa na CloudsTv. kilichopo Jijini Dar es salaam.

Amesema kuwa hakuna haja ya wanachama kuwa na hofu kuwa chama hicho kinaweza kusambaratika hivyo amewataka kuimarisha mshikamano uliopo ndani ya chama hicho.

“Nachojua mimi hakuna mgogoro ndani ya CUF kama inavyoelezwa na baadhi ya watu, isipokuwa Msajili wa Vyama vya Siasa Nchini anajaribu kupandikiza mgogoro huo kwa maslahi yake binafsi,”amesema Seif.

Aidha, ameongeza kuwa kuna baadhi ya watu ambao wanatumiwa kutaka kukivuruga chama hicho, hivyo amesema kamwe hawatafanikiwa.

Hata hivyo, amesema yeye kama kiongozi ataendelea kufanya shughuli zake za chama na kuwataka walio chini yake wasivunjike moyo.

Ofisi ya Rais (Utumishi) Yatoa Tahadhari ya Uwepo wa Matapeli Wanaotumia njia ya simu Kutapeli Watumishi wa Umma.

Mambo MUHUMU 8 Aliyoyazungumza Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Mh. Humphrey Polepole Huko Longido......Lipo pia la Serikali kusambaza tani 500 za Mahindi

$
0
0
Jana tarehe 02, Mei 2017 tumekuwa na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Mh. Humphrey Polepole ambaye amefanya ziara ya kukiimarisha chama chetu cha mapinduzi CCM  katika wilaya yetu ya Longido na kuzungumza na wanaCCM wakiwamo wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM wilaya ya Longido, wajumbe kamati ya siasa ya wilaya.

Mh. polepole amesema yafuatayo:
1. Serikali imedhamiria haswaa kuimarisha sekta ya usafiri wa anga ( ATCL ) kwa kuagiza ndege zingine ili kufikia ndege saba ikiwamo ndege kubwa ya kubeba abiria wasiopungua300, ndege tatu zenye uwezo wa kubeba abiria 102 kila moja ambazo zitasaidia kukuza  sekta ya utalii nchini ili kuliingizia taifa fedha za kigeni.

2. Serikali italeta kwa wananchi tani 500 za chakula kwa bei nafuu ili kuwasaidia wananchi wasio na uwezo  wa kumudu bei za chakula sokoni. kwa mujibu wa mheshimiwa Polepole Chakula hicho kitaanza kuingia juma lijalo.

3. Tutapambana kufa na kupona ili kurejesha ccm jimbo la longido na kata zake zote zilizobebwa na wapinzani.

4. Mradi mkubwa wa maji kusainiwa tarehe 06/05/2017 ili kuwaletea wanachi wa longido huduma ya maji na kuwaondolea kabisa shida ya maji na tatizo kuwa historia. Mradi huo utatoa maji kutoka West Kilimanjaro wilaya ya Siha.

5. Kiwanda kikubwa haswaa cha kutengeneza viatu kujengwa moshi Kilimanjaro na kwamba wamasai sasa wajiandae kupata soko kubwa la ngozi ya ng’ombe zitakazohitaji katika kiwanda hicho.

6. Chama cha mapinduzi kimepanga kujenga chuo kikubwa cha uongozi kwa ajili ya wanaccm na kwamba yeyote mwenye ndoto ya kuwa kiongozi ni lazima apitie chuo hicho.

7. Mheshimiwa Polepole ameguswa na Changamoto mbalimbali zinazoikabili CCM Longido ikiwamo Kukosa Ofisi ya Chama yenye kukidhi mahitaji ya sasa na hivyo Kuchangia Tsh. 500,000/= kwa ajili ya Shughuli za Ujenzi. Tuungane pamoja kukijenga Chama.

8.Mheshimiwa Polepole ametoa rai kwa Wanaccm kushiriki kikamilifu katika uchaguzi wa ndani wa Chama cha mapinduzi unaendeleaje nchini kote. Ametutaka tuchague viongozi wenye mapenzi mema na nchi yetu na Taifa kwa Ujumla, wenye vigezo stahiki & Waadirifu. Tusiwape nafasi Watoa rushwa ambao hutumia pesa zao kusaka uongozi. Hili halikubaliki hata kidogo.

Kidumu Chama Cha Mapinduzi...Hii ndiyo ccm bwana, tukiahidi tunatekeleza. HAPA KAZI TU.

Robert PJN Kaseko
Mjumbe Baraza Kuu UVCCM (M) Arusha.
Mei 02, 2017

Mchungaji Anayedaiwa Kuuawa Akutwa Akibatiza Watu Kanisani

$
0
0
Mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania  (KKKT) Usharika wa Mbinga, Leonard Kambo ambaye alidaiwa kuuawa na watu watano wa kanisa hilo amekutwa akitoa ubatizo katika usharika wa KKKT Kitandilo, Makambako, Mkoani Njombe.

Wakati Mchungaji huyo aliyedaiwa kuuawa mwaka 2011 akionekana akitoa ubatizo kanisani, watu waliodaiwa kumuua mchungaji huyo wamo mahabusu tangu mwaka huo 2011.

Ndugu wa watuhumiwa wa mauaji hayo ndio waliohaha kusaka picha ya mchungaji huyo baada ya kupata taarifa kwamba alihamishiwa eneo la Makambako baada ya kutokea tuhuma kwamba ameuawa.

Kwa mujibu wa habari hizo, baada ya ndugu kupata taarifa kwamba mchungaji huyo yupo hai, walitumia kila njia kupata picha yake ili itumike kama ushahidi kwamba yupo hai na tuhuma dhidi ya wauaji si za kweli.

Muumini mmoja wa kanisa hilo alieleza kuwa ndugu wa watuhumiwa hao walihakikisha wanamnasa mchungaji huyo kwa kamera popote alipo ili wasitishe kifungo cha ndugu zao na uongo dhidi yao.

Mmoja wa watuhumiwa wa kesi hiyo ambaye alikamatwa kisha kuachiliwa huru, Leonard Myale alisema kuwa baada ya kumuona na kupata picha ya mchungaji huyo akiwa hai, watathibitisha Polisi ili akamatwe na watuhumiwa wengine waachiwe huru.

“Tumeteswa sana, tumedhalilishwa, tumepuuzwa na kusemwa vibaya na Wakristo wenzetu, ndugu zetu na hata jamii haikutuamini juu ya tuhuma hizi za uongo ambazo hata Polisi walitubambikiza kesi bila kufanya utafiti wa kina. Tulikanusha kuhusika na mauaji hayo lakini Polisi hawakutuamini. Sasa tunaamini tuko huru, wenye mamlaka watachukua hatua za kutusaidia” alisema Elenia Mhoka mtuhumiwa mwingine wa mauaji hayo.

Aidha aliyewahi kuwa Mchungaji wa KKKT Kitandililo, Geofrey Mtweve, alitafutwa ili kueleza kuhusiana na suala hilo, lakini hakutaka kuzungumza chochote na kusema kuwa yeye siyo msemaji wa kanisa hilo.

“Mimi si msemaji wa kanisa ila ni kweli nilikuwa Kitandililo, uongozi umenihamisha kuja Ilembula, nimebadilishana na Mchungaji Leonard Kambo, ambaye ndiye nimemkabidhi usharika, mengine sifahamu lolote. Wasiliana na uongozi wa Jimbo,” alisema Mtweve.

Aidha mchungaji Kambo alipotafutwa na kuulizwa kuhusiana na yeye kutuhumiwa kifo na kama ni kweli aeleze kuwa alifufuka lini, lakini mawasiliano yakawa mabovu.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma, baada ya kuelezwa tukio hilo aliomba kupatiwa picha na namba ya RB na kuahidi kuwa atalifanyia kazi suala hilo.

Credit: TanzaniaDaima

CHADEMA Yatangaza Majina 6 ya Watu Watakaogombea Ubunge wa Bunge la Afrika Mashariki

$
0
0
Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) imewateua washiriki sita kugombea ubunge wa Bunge la Afrika Mashariki (Eala).

Katika kikao kilichofanyika jana mjini Zanzibar walioteuliwa ni Profesa Abdalla Safari, Salum Mwalimu, Ezekiel Wenje, Josephine Lemoyan, Lawrence Masha na Pamela Massay.

Taarifa ya leo iliyotolewa na Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano ya Chadema, Tumaini Makene imesema wateule hao watakamilisha hatua zingine za uteuzi kwa mujibu wa utaratibu, Kanuni za Bunge na Uchaguzi wa Bunge la Afrika Mashariki.

Masha na Wenje, walishiriki uchaguzi uliofanyika Aprili 4 ambao Chadema ilipeleka majina yao pekee jambo lililozua mjadala bungeni na kuhitimishwa kwa wao kupigiwa kura za Hapana.

Katika uchaguzi huo, wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano waliwachagua wajumbe saba wa Eala.

Kwa upande wa CCM, walioshinda ni Fancy Nkuhi, Happiness Legiko, Maryam Ussi Yahya, Dk Abdullah Makame, Dk Ngwaru Maghembe na Adam Kimbisa na kutoka CUF iliyokuwa na wagombea watatu kwa ajili ya nafasi moja, aliyeshinda ni Mohamed Habib Mnyaa akiwashinda Twaha Taslima na Sonia Magogo.

Video: Msikilize Spika Jobu Ndugai Akielema Maana ya Neno FALA

$
0
0
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Job Ndugai jana ameonyesha aliumizwa na kitendo cha Mbunge wa Kawe kwa tiketi ya CHADEMA Mh. Halima Mdee kumwambia 'fala' bungeni na kusema hata kama mtu humpendi lakini si vyema kumtusi matusi.

Job Ndugai alisema hayo alipokuwa akitoa maana ya neno fala bungeni ambapo ilibidi arejee maana hiyo kwa kusoma kupitia kamusi ya Kiswahili ambayo ilitoa maana kuwa fala ni mtu ambaye akili zake hazifanyi kazi vizuri.

"Kwa neno ambalo alilisema Halima Mdee humu ndani, kamati imeenda kwenye tafsiri ikachukua Kamusi kwa neno lile alilosema ambalo maana yake kwa yule unayemwambia 'Fala' ni mtu ambaye akili zake hazifanyi kazi vizuri, ni mtu mpumbavu, ni mtu bwege, ni mtu mjinga, ni mtu bozi, ni gulagula. Ndiyo maana nikasema sisi Waafrika hata kama humpendi namna gani mwenzako huwezi kumfanyia hivyo" alisisitiza Job Ndugai 

==>Msikilize hapo chini akiongea

Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) Yatoa Tahadhari ya Uwepo wa Mvua Kubwa


VIDEO: NEC yatangaza nafasi iliyoachwa na mbunge Elly Macha

$
0
0
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetangaza nafasi  ya mbunge wa viti maalumu kwa tiketi ya Chadema.

Nafasi hiyo imetangazwa baada ya kifo mbunge aliyekuwa anashikilia wadhifa huo, Dk Elly Macha kufariki dunia Machi 31, mwaka huu.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana  (Jumanne) na Mwenyekiti wa NEC, Jaji Semistocles Kaijage ni kuwa kwa mujibu wa Kifungu cha 37 (3) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amemjulisha kuwepo kwa nafasi hiyo.

“Kutokana na kuwepo kwa nafasi wazi ya Ubunge wa Viti Maalum, taratibu za kujaza nafasi hiyo zinaendelea kwa kuzingatia Ibara ya 78 (4) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, ikisomwa pamoja na kifungu cha 86A (8) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343,”amesema.

==>Msikilize hapo chini akiongea

VIDEO: Kipindi cha Maswali na Majibu Bungeni leo May 3, 2017

$
0
0
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limeendelea leo May 3, 2017 mjini Dodoma kwa kipindi cha maswali na majibu katika Bunge la Kumi na Moja, Mkutano wa Saba na Kikao cha Kumi na sita.

Bajeti ya Wizara ya Afya Yawasilishwa Leo Bungeni.......Waziri Ummy Aomba Kuidhinishiwa Sh. Trilioni 1

$
0
0
Bajeti ya Wizara ya Afya imewasilishwa bungeni leo na Waziri Ummy Mwalimu akisema kuwa malaria imeendelea kuwa changamoto nchini, licha ya kugawa vyandarua na kupulizia dawa katika mikoa mbalimbali.

Amegusia mambo mbalimbali ikiwemo  kuwataka wenye dalili za kifua kikuu wajitokeze kwa kuwa kinatibika.

"Wenye ukimwi kuanzia Juni wanapewa dawa za kupunguza makali bila kujali kupungua kwa CD4."

"Watoto 2020 wamefanyiwa upasuji wa vichwa vikubwa na mgongo wazi Muhimbili" Amesema Mwalimu

Pia amesema hudumu za kusafisha damu na figo zimeanza kupatikana katika hospitali za kanda. Amezilaani halmashauri zote ambazo hazikutoa fedha za mfuko wa maendeleo ya wamawake

Kuhusu mauaji ya wazee, Waziri Ummy amesema  yamepungua kutoka 190 mwaka 2015 hadi 134 mwaka 2016.

Waziri Ummy ametaja vipaumbele  vya wizara yake ambavyo ni  kuimarisha kinga na tiba, huduma za mama na watoto, upatijanaji wa dawa, kuimarisha vituo vya afya na hospitali, kuimarisha huduma lishe, matumizi ya tehama na kuongeza wanaotumia bima ya afya.

Ameeleza hakuna mjamzito atakayefariki kwa kukosa dawa ya kuzuia kifafa cha mimba na amesema zimetengwa Sh 7 bilioni kwa ajili yake.Amesema wajawazito 150,000 watapewa bima ya afya ili waweze kujifungua salama

Waziri Ummy amesema yeye si Daktari lakini ameshakuwa 'bush doctor' na ameomba Sh1,115,608,772,090.Fedha kwa ajili ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto ni Sh37,906,880,090.Jumla ya fedha za fungu la Afya ni Sh1,077,701,892,000

Waziri Mkuu Atembelea Kiwanda Cha Sukari TPC

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametembelea kiwanda cha sukari cha TPC kilichopo Arusha Chini, wilayani Moshi, mkoani Kilimanjaro na kukagua baadhi ya miundombinu ya kiwanda pamoja na mashamba.

Akiwa kiwandani hapo, Waziri Mkuu alielezwa kwamba hivi sasa msimu wa uzalishaji umefungwa na kiwanda kinafanyiwa matengenezo ambapo alishuhudia baadhi ya mitambo ikiwa imefunguliwa na kufanyiwa ukarabati.

Akitoa taarifa juu ya matengenezo hayo mwishoni mwa wiki, Meneja wa Kiwanda hicho, Bw. Pascal Petiot alimweleza Waziri Mkuu kwamba kiwanda hicho kimefungwa kwa zaidi ya wiki sita ili kujiandaa na msimu ujao wa uzalishaji ambao uko karibuni kuanza.

“Hivi sasa ni kipindi cha mvua, tumefunga msimu wa uzalishaji na tunaendelea na ukarabati wa mitambo ili kujiandaa na msimu ujao. Kila mwaka ni lazima tufunge msimu kwa kipindi kifupi, ili kufanya ukarabati kama huu,” alisema.

Akiwa kiwandani hapo, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alikuta mafundi wakifanya matengenezo katika sehemu mbalimbali za kiwanda. Hata hivyo, alionyeshwa mtambo wa kuzalisha umeme wa kiwanda hicho (boiler) ambao unatumia mabaki ya miwa yaliyokwisha kamuliwa juisi (bagasse) ambayo huchomwa na kuchemsha maji ili kupata mvuke unaosukuma jenereta.

“Tunatumia mabaki ya miwa badala ya kuni, joto linalozalishwa linafikia nyuzijoto 450 na kuweza kuzalisha megawati 17.5 wakati kiwanda kikiwa kinafanya kazi. Matumizi yetu kwa ajili ya kiwanda, makazi ya watumishi na vijiji vya jirani yanafikia megawati 12, na tunawauzia TANESCO megawati 4 ambazo wanaziingiza kwenye gridi ya Taifa,” alisema Bw. Jaffari Ali Omari ambaye ni Afisa Utawala Mtendaji.

Bw. Omari alimweleza Waziri Mkuu kwamba umeme unaozalishwa na kiwanda hicho ni mwingi kuliko unaozalishwa na mabwawa ya Hale na Nyumba ya Mungu yakijumuishwa kwa pamoja. “Hale inazalisha megawati nane na Nyumba ya Mungu inazalisha megawati tatu,” alisema.

Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu wa kiwanda hicho, Bw. Robert Baissac alisema uzalishaji wa sukari kwenye kiwanda hicho umepanda kwa asilimia zaidi ya 200 tangu wachukue kiwanda hicho mwaka 2000.

Alisema wakati wanaanza, kiwanda kilikuwa na uwezo wa kuzalisha tani 36,000 kwa mwaka na wakati wanakinunua walitakiwa kuongeza uzalishaji kwa asilimia 100 kwa kufikisha tani 72,000 za sukari.

 “Tuliweza kuvuka lengo hilo tangu mwaka 2007 na hivi sasa tumeweza kuzalisha tani 111,800 katika msimu uliopita,” alisema.

“Tunatumia mbegu bora zilizofanyiwa utafiti na majaribio hapa hapa kiwandani. Tunatumia mbolea na njia za umwagiliaji ili kuhakikisha hadhi ya miwa yetu ni ya kuridhisha, na inayoweza kutupatia kiwango kikubwa cha sukari,” alisema.

Akitoa maoni ya jumla, Waziri Mkuu aliwataka wafanyakazi wa kiwanda hicho wafanye kazi kwa bidii na kujituma na kuhakikisha wanaongeza tija katika uzalishaji wao.

“Msisitizo wa Serikali ni kuwasihi Watanzania tubadilike, tuchape kazi ili tuweze kuongeza tija mahali pa kazi,” alisema Waziri Mkuu.

Alikuwa akijibu hoja ya Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi kiwandani hapo (TASIWU), Bw. Bilal Omar Mchomvu ambaye aliomba Serikali iangalie uwezekano wa kuondoa makato ya kodi kwenye bonasi na overtime wanazolipwa na kiwanda hicho.

Kuhusu haki za wafanyakazi kiwandani hapo, Bw. Mchomvu alimweleza Waziri Mkuu kwamba chama cha wafanyakazi kina mahusiano mazuri na menejimenti ya kiwanda na kwamba kila miezi mitatu wanakutana na wafanyakazi hao kama sheria inavyotaka.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMATANO, MEI 3, 2017.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya May 4

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images