Takribani miezi kadhaa iliyopita star wa filamu Diana Kimaro
alikaririwa akisema kuwa yeye ni bikira na hajawahi kulala na mwanaume
yeyote kwani yupo busy na shule....
Diana aliyasema hayo katika kuweka wazi
kuwa baadhi ya watu walikuwa wanamuona ni mcharuko kutokana na
baadhi ya filamu alizoigiza kama mcharuko na kucheza vizuri hivyo
wengine kudhani ni kweli. ...
Hata hivyo
Diana Kimaro wa bongo movie ajuta kuianika BIKRA yake mitandaoni
↧
↧
Taarifa kuhusu bei mpya za umeme zitakazoanza kutumika tarehe 1 /1/ 2014
Tarehe 11 Oktoba 2013, Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) liliwasilisha maombi ya kurekebisha bei ya umeme kwa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA). TANESCO ilipendekeza kuongeza bei kwa asilimia 67.87 kuanzia tarehe 1 Oktoba 2013, asilimia 12.74 kuanzia tarehe 1 Januari 2014 na asilimia 9.17 kuanzia tarehe 1 Januari 2015.
Vilevile TANESCO waliomba kuidhinishwa kwa
↧
Watu saba wakamatwa wakijiandaa kulipua nyumba za Ibada
Na
Oscar Assenga, Korogwe -- JESHI la Polisi mkoani hapa kwa kushirikiana
na wakazi wa Kijiji cha Maili kumi wilayani Korogwe wamefanikiwa
kuwakamata watu saba kwa tuhuma za kuhusika na kuweka mabomu yaliyokuwa
yameandaliwa tayari kwa kulipuka kwenye nyumba mbili tofauti za ibada.Pamoja
na mabomu hayo, watuhumiwa hao ambao majina yao yanahifadhiwa kwa sababu
za kiuchunguzi
↧
"Nilijazwa mimba nikiwa na umri mdogo sana....Jamii ilinitenga, ila ujasiri ulinisaidia"....Madam Rita
Mkurugenzi wa Benchmark Production, Rita Paulsen aka Madam Rita
amesema yeye ni miongoni mwa wanawake waliopata ujauzito wakiwa na umri
mdogo lakini alikuwa jasiri wa kukabiliana na hali hiyo hadi
akafanikiwa.
Kupitia Facebook, Madam Rita amewashauri wasichana wanaojikuta katika
katika hali hiyo kutokata tamaa kwakuwa bado wanaweza kufanikiwa.
“Jambo moja msilofahamu
↧
Dr. Slaa akerwa na mapokezi ya Zitto Kabwe Kigoma na kuamua kumzuia kufanya mikutano......Zitto amjibu na kudai kuwa katiba ya nchi inamruhusu kufanya mikutano hiyo
Zitto Kabwe jana amefanya mkutano wa 3 ndani ya Mkoa wa
Kigoma,mikutano hii ilianza siku ya Jumamosi kwa sehemu ya Mwandiga
mahali alipozaliwa na kukulia,Kasulu ilikua juzi na jana kafanya Kigoma
mjini eneo la Mwanga kwenye uwanja wa Community Centre....
Mkutano
ulianza sa 10 kiitifaki ulitanguliwa na viongozi wa Chadema wa
mkoa,kisha Zitto Kabwe kupanda Jukwaani na moja kati ya
↧
↧
Wahamiaji haramu warejea kwa kasi Kagera....Ni wahamiaji wanaojiita M23 na wanadaiwa kuwatisha wananchi na kupora mali zao
Katika hali isiyo ya kawaida, wahamiaji haramu waliorejeshwa nchini mwao na serikali katika ‘Operesheni Kimbunga’ wameanza kurejea kwa wingi katika Wilaya ya Kyerwa, mkoani Kagera wakijiita M23 na kupora mali za wananchi kwa nguvu.
Mkuu wa Wilaya hiyo, Mhandisi Benedict Kitenga, aliyasema hayo wakati akitoa taarifa kwa Mkuu wa Mkoa huo Kanali mstaafu, Fabian Massawe ambaye alitembelea
↧
Wastara awaomba mashabiki kuungana naye 28 Dec makaburini Kisutu kwaajili ya dua ya Sajuki
Msanii wa filamu, Wastara Juma amewaomba Watanzania na wadau
mbalimbali kuungana naye siku ya tarehe 28 December 2013 saa tatu
asubuhi makaburini Kisutu jijini Dar es Salaam kwaajili ya kufanya dua
maalum ya Sajuki
Wastara ametoa taarifa hiyo kupitia ukurasa wake wa Facebook.
“28 Jumamosi kuanzia saa 3 asubuhi naomba mashabiki wangu na wapenzi
wa kipenzi changu kipenzi chenu
↧
Kijana mmoja ashambuliwa hadi kufariki dunia maeneo ya Mbezi Luis jijini Dar es Salaam baada ya kusemekana kwamba ni mchawi aliyedondoka na ungo
Wananchi wakiwa hasira kali wamempiga hadi kumuua mwanaume
aliyedhaniwa kuwa ni mchawi baada ya kuanguka akiwa amepanda ungo maeneo
ya Mbezi Luis jijini Dar es Salaam.
Jamaa huyo mkazi wa Mwanza anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka
20 hadi 25, alianguka jana saa 12 asubuhi maeneo ya Mbezi Luis baada ya
kudai kuwa alikuwa kwenye safari zake za kishirikina.
Mashuhuda
↧
Tunawatakia sikukuu njema ya Christmas...
↧
↧
Wadau wapinga bei mpya za umeme
Baadhi ya wachumi na wadau mbalimbali wa nishati ya umeme
wameikosoa hatua ya Shirika la Ugavi wa Umeme Tanzania (Tanesco) baada
ya kuongeza gharama za umeme kwa maelezo kuwa hatua hiyo itamkandamiza
mwananchi wa kawaida.
Kauli hizo zimekuja siku moja baada ya Mamlaka ya
Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura) kutangaza bei mpya za
umeme huku kukiwa na ongezeko kubwa.
↧
Gazeti la Mtanzania litakuwa mtaani tena kuanzia ijumaa ya wiki hii baada ya serikali kulifunga kwa siku 90
GAZETI la Mtanzania ambalo serikali ililifungia kuchapishwa kwa
muda wa siku 90 kwa kile ilichokieleza kuwa ni kuandika habari za
uchochezi sasa litaanza tena kuchapishwa na kusambazwa nchini Ijumaa ya
Disemba 27, 2013.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na Mhariri
Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya New Habari (2006) Ltd, Absalom
Kibanda, kwa gazeti hili, uamuzi huo mpya umefikiwa
↧
Sura mpya ya baraza jipya la mawaziri litakaloundwa na JK muda wowote kuanzia sasa....
MABADILIKO makubwa ya Baraza la mawaziri yanayotarajiwa kufanywa wakati
wowote kuanzia sasa na Rais Jakaya Kikwete yameanza kuonyesha kila
dalili za kuibua sura mpya na ambazo hazitarajiwi na wengi sambamba na
kupanda kwa baadhi ya manaibu waziri...Dodoso
zilizofanywa na RAI kutoka kwa watu wa kada na rika mbalimbali
kuhusu muundo mpya wa Baraza la Mawaziri zimeonyesha kuwa iwapo rais
↧
Mazingaombwe ya CHADEMA jijini Mwanza....Vurugu kubwa zaibuka kati ya Meya na Madiwani wa CHADEMA
ILIKUWA ni kama uwanja wa vita na mipasho, ndivyo unavyoweza kusema,
baada ya kuibuka vurugu kubwa kati ya Meya wa Halmashauri ya Ilemela,
Henry Matata na madiwani wake wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo
(Chadema).
Vurugu hizo ziliibuka jana kwenye kikao cha Baraza la
Madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela baada ya Matata kuwataka
madiwani watatu wa Chadema kutoka nje ya
↧
↧
Kocha wa Simba afariki dunia....
Aliyekuwa kocha wa makipa wa Klabu ya Simba, James Kisaka amefariki
dunia leo asubuhi katika Hospitali ya Burhan, Dar es Salaam.
Kisaka
aliyewahi kuwa kipa wa timu hiyo miaka ya nyuma, alikuwa akisumbuliwa na
maradhi ya kichwa, macho na miguu kwa muda mrefu.
Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi-Amina
<!-- adsense -->
↧
Video ya wapenzi wakingonoka vichakani yanaswa
Hakika mapenzi hayana heshima...Baba mtu mzima mwenye mke na watoto amefuamiwa live na Domo Langu akingonoka kichakani na binti yake wa kazi....
Kwa mujibu wa mtandao wa Domo Langu, wawili hao walifuniwa jana mchana katika kijiji cha mkwaju na kisha wakafikishwa ofisi ya mtendaji wakiwa chini ya ulinzi
<< VIDEO IKO HAPA >>
Kwa maelezo na
↧
Dk. Emmanuel Nchimbi ampigia magoti mwenyezi Mungu ili ampe moyo wa kusamehe kwa mambo aliyotendewa
SIKU chache baada ya aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk. Emmanuel
Nchimbi kuvuliwa wadhifa wake kwa tuhuma za kushindwa kusimamia wizara
yake, kiongozi huyo ametaka apewe moyo wa upendo na kusamehe.
Nchimbi ambaye ni mbunge wa Songea Mjini kwa tiketi ya CCM, alisema
hayo juzi kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa facebook, wakati
akisherehekea kutimiza miaka 42 ya
↧
Baada ya kumtema Penny...Diamond amtangaza rasmi Wema Sepetu kuwa ni Mchumba wake
Tukio hilo lilitokea jana pale Leaders club kwenye show ya Diamond ambapo
Wema Sepetu alipanda kwenye stage na kuongea na mashabiki waliofika
kwenye show hiyo....
Kwenye hiyo show, Diamond aliuliza,”Mnataka kumjua mchumba wangu”? Show ilivyoendelea Diamond alitaka kuimba wimbo wa "ukimwona" akasema:
“Nasikia ninayetaka kumuimbia wimbo huu yupo humuhumu ndani”.
Baada ya
↧
↧
Mwanafunzi abakwa kikatili mkoani Singida....Sehemu zake za siri na makalio vyote vimeoza na vinaoa usaha....Hili ni simulizi lake
Mwanafunzi wa kike,13, (jina linahifadhiwa) anayesoma
darasa la tano katika shule ya Msingi Unyakumi, mkoani Singida,
amefanyiwa unyama kwa kubakwa na kijana aliyemtaja kwa jina moja la
Mapunda ambaye ni dereva wa bodaboda.
Akizungumza kwa shida kutokana na maumivu makali aliyonayo akiwa
katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, denti huyo alisema kwamba mkasa
huo ulimpata Novemba 19,
↧
Rais Kikwete kuwasili leo nchini na SIRI nzito....Je, ataamua kuendelea kufanya kazi na Pinda??...Katiba inasemaje??
Rais Jakaya Kikwete anatua nchini leo akiwa na lake moyoni
kuhusu hatima ya baraza lake la mawaziri, baada ya kutengua uteuzi wa
mawaziri wake wanne, wiki mbili zilizopita.
Rais Kikwete alikwenda Marekani, Desemba 18, mwaka
huu kufanyiwa uchunguzi wa afya yake na akiwa huko, upepo wa kisiasa
ulibadilika na kumlazimisha kuchukua hatua hiyo ambayo inampa wajibu wa
kupanga upya safu
↧
Waziri Mkuu Mizengo Pinda, ambaye anakabiliwa na shinikizo la kujiuzulu amesema atazungumzia hatima yake baada ya sikukuu
Waziri Mkuu Mizengo Pinda, ambaye anakabiliwa na shinikizo la
kujiuzulu amesema atazungumzia hatima yake baada ya sikukuu za Krismasi
na Mwaka Mpya.
Gazeti la The Citizen,
lilimkariri Pinda jana akisema kwa sasa anahitaji amani na utulivu
katika kipindi hiki cha sikukuu baada ya shughuli za kikao kilichopita
cha Bunge.
Katika kikao hicho,
↧
More Pages to Explore .....