Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Live: Yanayojiri Bungeni Dodoma leo Aprili 27, 2017

0
0
Tazama hapa moja kwa moja kutoka Bungeni Dodoma kipindi cha Maswali na Majibu katika Bunge la 11, Mkutano wa Saba leo Aprili 27, 2017.

==>Tazama hapo chini

Ray Kigosi afunguka Mambo Mazito kuhusu marehemu Kanumba Kuhusishwa na Uchawi na Freemason

0
0
Msanii wa filamu nchini Ray Kigosi amefunguka na kusema kuwa baadhi wa Watanzania ni wanafiki na wamekuwa wakikatisha tamaa watu katika mambo yao kutokana na unafiki wao.

Ray Kigosi amesema hayo kupitia ukurasa wake wa Instgram na kusema kutokana na unafiki huo wa baadhi ya watu ulimfanya mpaka marehemu Kanumba kuvunjwa moyo katika kazi yake.

==>Ray Kigosi ameandika;
1. Kanumba alipoanza kuona mwanga wa kufanikiwa bila kujali juhudi zake kuna watu walimuita Freemanson, Mara anatumia nguvu za Giza. that is to say films zake hazikuwa nzuri but ziliuza sababu ya nguvu za Freemanson na nguvu za giza!!

2. Kanumba alipoenda Big Brother alipondwa Sana na kuitwa bogus kwa Madai hajui kiingereza, Ni watanzania Hawa Hawa walibebea bango hili huku baadhi ya waandishi uchwara wakieneza ujinga huu bila kujali juhudi zake. But Leo wanamsifia hakuna Kama Kanumba!

3. Kuna wakati Kanumba alionekana wazi kuvunjwa moyo na kukatishwa tamaa kwa kuonekana juhudi zake si kitu. But Alisema maneno machache Kuwa mtanikumbuka kama si Leo basi Ni Kesho.
And alichosema kimetimia, wale wale waliokuwa wakisema Ni Freemanson bila hata kujali juhudi zake kwenye game Leo ndio kwa unafiki wanasema hakuna Kama Kanumba !….. HAO NDIO BINADAMU NA TABIA ZAO
Je Kanumba kaondoka na Bongo Movie yake ya Freemanson ? Kama wengine mnavyodhani industry Ni Mtu sio system !

4. Diamond Platnumz nae baada ya kuona Njia ya mafanikio kuna watanzania, wasanii wenzake na hata baadhi ya wanahabari wanasema Ni Freemanson, wengine wanaonyesha chuki ya wazi kwake. Wanasema Hana muziki mzuri, Mara Ni Kiki tu ambazo hata Kanumba alikuwa akiripotiwa magazetini na kina Wema.

Hawaoni juhudi na thamani ya Diamond sasa ! Hatuombi baya limpate Diamond ili kudhibitisha tabia na unafiki wa binadamu. But HAO NDIO BINADAMU siku zote hawana Jema unafiki ni sehemu ya Maisha.

5. kila siku Ni kuzua hii na kile, Mara ooh Diamond Ni mchawi, kasema mleteni huyo mganga wangu mkashindwa kumleta, akajitokeza mganga fake sijui na Madai juu Kuwa Diamond atashuka kimuziki kwa sababu ananipuuza niliyempa nyota, Diamond akasema sawa namtegemea Mungu. Miaka 4 sasa tangu yaliyoitwa ya mganga Diamond hashuki ndio anazidi kupaa. HAO NDIO BINADAMU kusema lolote Ni haki Yao.

Kazi za Kanumba sasa zinapewa thamani na ubora uliovuka mipaka na viwango ambao hakupewa kipindi yupo hai ! HAO NDIO BINADAMU na tabia zao. Ni tabia tu ya baadhi ya watu kubebea mabango mabaya ya Mtu au uzushi na kuacha mazuri yake then baadaye wakishikwa Uchawi wanageuza walichoamini Ni nyeusi kiwe nye.

SORRY MADAM -Sehemu ya 57 & 58 (Destination of my enemies)

0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWAILIPOISHIA
ILIPOISHIA
“Kusema kweli, ndani ya gari hatukukuta mwili wa mtu yoyote. Hata tulipo jaribu jaribu kutazama pembeni kuona kwamba labda mtu au watu walio kuwemo ndani ya gari hilo watakuwa wameangukia pembeni hatukuweza kuwapata”
“Unasema kweli?”
“Ndio Mrs Ranjiti, siwezi kukutania”
Kidogo hata nguvu za miguu zikamjia Phidaya, akajikongoja kongoja kwenda kuchungulia kwenye korongo hilo huku akiongozana na askari huyo sehemu alipo onyeshwa gari ilipo kutwa, alijikuta akitoa macho kwani ina umbali mrefu sana.
‘Sasa kama wametoka watakuwa wapi’
Phidaya aliiuliza huku akiendelea kuchhungulia chungulia bondeni kwenye korongo hilo.

ENDELEA
   Phidaya hakuhitaji kuondoka katika eneo hilo hadi apate ripoti ya mwisho kutoka kwa Polisi kwamba kijana wake Lee Si pamoja na Shamsa hawakuwemo kwenye ajali hiyo. Hadi yanatimu majira ya saa nne usiku, baridi ikiwa kali katika eneo la eneo hilo pamoja na ukungu mwingi, ulio tanda kila mahali hapakuweza kuonekana mtui wa aina yoyote aliye kuwamo kwenye ajali hiyo. Jambo hilo kwa upande mmoja liampa matumaini makubwa sana Phidaya. Akaagana na mkuu wa polisi aliye fika katika eneo hilo kushuhudia kazi ya vijana wake. Kwa usalama na kutona ni usiku sana, Phidaya akapewa gari mbili za polisi ziweze kuongozana naye hadi takapo fika mjini, gari mmoja ikatangulia mbele, huku ikiwa na askari wawili na gari moja ikafwatia kwa nyuma nayo ikiwa na askari wawili.

Safari yao haikukumbwa na tatizo la aina yoyote hadi walipo mfikisha Phidaya kwenye jumba lake la kifahari, lenye ulinzi madhubuti. Akaagana na askari hao wakimuahidi watampatia ripoti kwa kila jambo ambalo litatokea kwa wakati wowote katika uchunguzi wanao endelea kuufanya juu ya chanzo cha ajali hiyo. Mfanyakazi wake wa ndani, akampokea koti alilo livua na kulishika mkononi, taratibu Phidaya akangoza hadi kwenye meza ya chakula na kuketi.

“Dokta hajarudi?”
Phidaya alimuliza mfanyakazi wake wa ndani baada ya kukuta hapakuwa na chakula ambacho kimeweza kuguswa.
“Hajarudi bado”
“Hembu nitolee simu kwenye hilo koti langu”
Mfanyakazi wake akafanya kama alivyo agizwa, Phidaya akaipokea simu yake hiyo, kitu cha kwanza alipo minya batani ya kuwashia mwanga kwenye simu yake hiyo aina ya Iphone 6, akakutana na sura ya Black Shadow. Kwa haraka kumbukumbu zake zikarudi kwa mgonjwa huyo.
Akakurupuka kwenye kiti kama kichaa, hata kula hakutamani tena, akatoka nje na kuingia kwenye gari lake, walinzi wa getini wakamfungulia geti na kuondoka kwa mwendo wa kasi sana akiwahi hospital;ini.
                                                                                                               ***
    Majira ya saa tano kasoro usiku, Kim akiwa amevalia mavazi ya udaktari, pamoja na kitambaa cha kijani alicho jifunga puani na kuziba mdomo, huku kikiwa kimembakisha macho tu. Akaanza kutembea kuelekea kwenye kordo inayo kupeleka kwenye litio ya kushukia kwenye chumba cha siri.
Mavazi yote aliyo yavaa aliweza kukabidhiwa na dokta Yan. Huku dokta Ranjiti aki nje kabisa ya hospitali yake gari lake akiwa amelisimamisha sehemu ambayo anaweza kuliona geti la hospitalini kwake na endapo gari ya kubebea wagonjwa litatoka, basi ataungana nalo kuhakikisha kwamba Black Shadow wanamuua na kumzika.

   Hapakuwa na nesi wala mtu aliye weza kumstukia Kim, kutokana na jinsi alivyo vaa. Anaonekana kama daktari anaye toka katika chumba cha upasuaji. Kim akashuka na lifti hadi kwenye chumba ambacho amelazwa Black Shadow, akatembea kwa tahadhari kubwa hadi kwenye chumba ambacho ameelelezwa atamkuta Black Shadow.
Macho yake yakatua kitandani ambapo alitegemea kumkuta Black Shadow ila haikuwa hivyo kwani hakuwepo, kilicho bakishwa hapo ni kitanda na mashuka pekee. Akahisi labda amekosea, akatoka na kuanza kukagua vyumba vingine viwili, hakukuta kitu zaidi ya maboksi yenye dawa tu.

“Shitii…….”
Kim alizungumza kwa hasira huku akiitoa simu yake mfukoni akampigia dokta Ranjiti, hazikupita hata sekunde tano simu ikapokelewa.
“Vipi umefanikisha?”
Lilikuwa swali la kwanza kutoka kwa dokta Ranjiti mara tu alipo pokea simu ya Kim.
“Mbona hayupo mgonjwa mwenyewe”
“Uuuu….unasem…aje?”
“Hayupo nimeingia kwenye chumba mulicho niagiza nimekumta hayupo”

Dokta Ranjiti hakuonge kitu chochote zaidi ya kukaa kimya, Kim akakata simu na kumpigia dokta Yan, naye akaonekana kushangazwa na taarifa hiyo, kutokana yeye yupo ndani ya hospitali kwa haraka akashuka hadi kwenye chumba, akadhibitisha kwamba Black Shadow hayupo. Kila mmoja akili yake ikajikuta akichanganyikiwa haswa dokta Yan, kwani kwa ugonjwa alio kuwa nao Black Shadow ni vigumu sana kwa yeye kuondoka hapo hospitalini na isitoshe amemchoma sindano ya usingizi inayo chukua masaa mengi sana hadi kuisha kwake mwilini.
                                                                                                       ***
    Dokta Ranjiti, akataka kuliwasha gari lake na kwenda hospitali ila alipo liona gari la Phidaya likiingia katika geti la hospitalini, akasitisha zoezi lake la kwenda hospitalini, kwa jinsi alivyo changanyikiwa akahisi akili yake ikitaka kupasua kichwa chake, japo ndani ya gari lake kuna hewa ya kiyoyozi, ila jasho lilimtiririka usoni mwake kama mtu aliye kimbia mbio ndefu.

Phidaya akasimamisha gari lake kwenye maegesho, kwa haraka akashuka na kuanza kutembea kwa mwendo wa kasi kuelekea ndani. Hakuhihitaji kusemeshana na mfanyakazi yoyote, akili yake kwa wakati huo inamfikiria Black Shadow tu. Akiwa kwenye kordo akapishana na Kim akiwa ameifunika sura yake, hakumtilia maanani sana. Akaingia kwenye chumba chenye lifti, akashuka chini, akaanzaa kukimbia hadi kwenye chumba alicho lazwa Black Shadow.

Macho na sura yake vikabadilika, gafla baada ya kukuta kitanda kikiwa hakina mgonjwa, dura ikajaa mikunjo, macho yakamtoka. Mwendo kasi ukaisha, akajikuta akianza kutembea kwa taratibu kukifwata kitanda hicho. Dokta Yan aliweza kumuona Phidaya akiingia ndani ya chumba alilichokuwa amelazwa Black Shadow, yeye akiwa kwenye moja ya stoo, mara baada ya Kim kuondoka, aliingia kutafuta tafuta, kwani naye akili yake ilichanganyikiwa. Kwa woga wa kumuogopa Phidaya akajibanza kwenye maboksi mengi ya dawa akihofia kuonekana kwa maana kesi nzima itamuangukia yeye.

Phidaya akajikuta akiishiwa nguvu za miguu na kujikalia kitandani, hakujua alie, acheke au afanye nini kwa wakati huo, akili yake ikakosa kabisa maamuzi ya kufanya hali ya hatari ikamjaa moyoni mwake. Taratibu akajikuta akilala chali kwenye kitanda hicho na kutazama feni lililopo juu kwenye chumba hicho linavyo zunguka taratibu taratibu.
                                                                                                             ***
   Kitendo cha gari kuanza kwenda chini, kwenye makorongo, Shamsa akaona kupiga kelele haita kuwa jambo la msaada kwao, kwa haraka akajirusha kwenye siti ya mwisho alipo Sa Yoo, anaye endelea kupayuka kwa makelele. Kutokana kioo cha nyuma cha gari hilo kimepasuka kikampa upenyo mzuri wa yeye kujitoa kwa haraka, akamshika mkono Sa Yoo, akamchomoa kupitia katika upenyo huo. Lee Si alipo ona juhudi za wasichana hao zimezaa matunda na yeye bila kusubiria gari kufika chini kabisa, akafungua mlango na kujitosha nje na kuanza kubingiria kwenye majani marefu. Sa Yoo na Shamsa nao waakendelea kubingiria kwenda chini wakiporomoka kwenye majani marefu. Cha kumshukuru Mungu Shamsa akabahatika kushikilia kijimti kilicho mzuia kwenda chini, hivyo hivyo ikawa kwa Sa Yoo. Kwa umahiri wa mazoezi aliyo nayo Lee Si, akafanikiwa kujizuia kwenye moja ya jiwe.

Mlipuko wa gari hilo, uliwastua kila mmoja wao. Kila mmoja aliweza kulishuhudia gari hilo likiteketea kwa moto, kutokana na nyasi nyingi zilizo kuwepo katika eneo hilo, adui yao Kim, hakuweza kuwaona kwa urahisi akaamini kwamba wameteketea  kwa moto. Wakasubira kwa muda hadi walipo sikia mngurumo wa gari la adui yao Kim lilipo ondoka ndipo na wao walipo anza kufanya jitihada za kupandisha kilima hicho.

 Haikuwachukua muda sana, wakafanikiwa kufika juu barabarani, wakaanza kutembea kwa miguu wakirudi kutokea mjini, kwa mwendo wa dakika tano, wakafanikiwa kusimamisha gari la mizigo, wakapewa lifti iliyo wafikisha hadi mjini kabisa. Muda wote walitembea kwa kujihami wakihofia kuonekana na adui yao kwani hawakutambua kwamba ni sehemu gani anapatika. Wakaelekea katika nyumba ambayo Sa Yoo, alikuwa akiishi na bibi yake, na baada ya msiba wa bibi yake aliicha na kwenda kuishi na rafiki yake Shamsa.

Kila mmoja akaanza kutibu majeraha ya mwilini mwake, hususani Sa Yoo, yeye ndio amepata mikwaruzo mingi sana, sehemu za mikononi na migongoni.
“Shamsa hivi umejifunzia wapi mbinu zote zile?”
Sa Yoo aliuliza huku akitabasamu, Shamsa, hakumjibu kitu chochote zaidi ya kutabasamu na yeye.
“Haki ya Mungu nilijua leo nakufa, yaani ahaa wee acha tu. Ila kusema kweli asante rafiki yangu Shamsa, kwa maana ningekuwa sasa hivi sijui nipo kuzimu au laa”
“Unapaswa kuwa mwana mazoezi”
“Na kamwili haka kweli nifanye mazoezi gani mimi?”

“Ya kujilinda”
Muda wote wa mazungumzo Lee Si hakuzungumza kitu chochote, aliendelea kusikilizia maumivu ya vidonda vyake. Hata wazo la kumpigia simu bosi wake kumpa taarifa kwamba wapo salama wala halikuwepo akilini mwake, aliendelea kumshukuru Mungu kwa jinsi alivyo fanikiwa kutoka kwenye ajali hiyo.
Shamsa na Sa Yoo wakaandaa chakula, majira ya saa mbili usiku wote kwa pamoja wakajumuika mezani na kuanza kula.
“Wewe unaitwa nani?”
Sa Yoo, alimuuliza Lee Si, baada ya kumuona akiwa ametawaliwa na mawazo mengi kichwani mwake hata chakula hakukila kwa furaha.

”Lee Si”
“Asante pia kwa kutusaidia”
“Nanyi asanteni”
“Mimi naitwa Sa Yoo, huyu anaitwa Shamsa”
“Lee kwa nini uliamua kuhatarisha maisha yako na kutusaidia sisi”
Shamsa alimuuliza Lee Si.
“Ilikuwa ni moja ya kazi yangu niliyo weza kupewa na bosi wangu”
“Bosi wako ndio amekupa kazi ya kuhatarisha maisha yako?”
“Hapana bosi wangu aliweza kunipa kazi ya kukulinda wewe”
“Mimi…….!!”
Shamsa  alishangaa huku wakitazamana na Sa Yoo, kisha akamtazama Lee Si kwa macho hayo hayo ya mshangao
“Ndio bosi wangu ndiye aliye niagiza”
“Anaitwa nani?”
Sa Yoo alidakia mada

“Anaitwa Madam Phidaya mke wa Mr Ranjiti”
Shamsa akastuka kidogo, kijoko alicho kuwa akikipeleka mdomoni kikiwa na chakula akajikuta akikishusha taratibu na kukirudisha kwenye sahani yake.
“Laiti kama nisinge kulinda basi leo hii mungekuwa nyote walili maiti hususani wewe Shamsa”
Sa Yoo na yeye macho yakamtoka, kwa jinsi macho yake yalivyo na ukubwa fulani na yaduara, kwa jinsi yalivyo mtoka hadi Lee Si akacheka kidogo.
“Unacheke sisi kufa?”
Sa Yoo aliuliza kwa woga
“Hapana siwacheki, ila nimecheka kwa jinsi ulivyo yatoa macho yako”
“Sa Yoo una simu hapo?”
“Sina simu si tumeacha nyumba ile kule”
“Na wewe Lee Si”

“Sina nahisi simu yangu imeteketea kwenye moto kwa maana niliiangusha ndani ya gari”
“Kwani simu unaitaka ya nini na wewe?”
“Nahitaji tumpigie mama”
“Mama……!!”
“Ndio mama, Phidaya ni mama yangu”
Lee Si, habari aliyo isikia nayo ni mpya masikioni mwake,naye akajikuta akishangaa. Taratibu picha ya mazungumzo ya dokta Ranjiti na Kim ikaanza kumjia taratibu kichwani mwake.
“Sasa naanza kupata picha”
Lee Si alizungumza huku akitingisha kichwa chake
“Picha gani?”
“Mpango wote wa wewe kuuliwa ameupanga mume wake dokta Ranjiti?”
“What……?”(Nini…….?)
“Ndio, kitu kinacho takiwa kwa sasa hivi ni wewe kuwa makini kwani maisha yako yapo hatarini”
“Eheee hanijui huyu, ameingia pabaya”
Shamsa alizungumza huku akiacha kula na kunyanyuka, akaanza kutembea kwa haraka kuelekea nje, wezake nao wakamfwata huku Sa Yoo akimuita.

“Unakwenda wapi sasa?”
“Nakwenda kuonana na huyo Rnjiti”
“Nisikilize Shamsa, peke yako huwezi kupambana na Ranjiti, ni mtu mwenye pesa sana na endapo atakuona tena atakuua”
Lee Si alizungungumza huku akimzuia Shamsa aliye jawa na hasira, hakujua ni kwa nini daktari huyo anahitaji kumuu kwani hapakuwa na jambo lolote baya alilo weza kumfanyia daktari huyo. Lee Si akafanikiwa kumzuia Shamsa na kumrudisha ndani. Wote watatu wakakaa kwenye meza moja kwa mazungumzo zaidi.

“Kwa nini anataka kuniua”
“Nilisikia akizungumza na mtu aliye mpa hii kazi, kwamba wewe unatambua siri ya Phidaya”
“Siri…..! Siri gani?”
“Sijajua, ila nahisi kuna jambo ambalo Phidaya mwenyewe anahitaji kulitambua, ndio maana akaamua kukutafuta wewe ili uweze kumueleza ukweli”
Shamsa akashusha pumzi nyingi, kila kitu anacho kisikia kwa wakati huu kinamchanganya akili yake.
“Nahitaji kuonana na mama”

“Kwa leo itakuwa ni ngumu kuonana naye, kwa maana usiku huu atakuwa yupo nyumbani kwake”
“Kwani sasa hivi ni saa ngapi?”
Sa Yoo akasimama na kuingia kwenye chumba chake, akaitazama saa ya ukutani kisha akarudi sebleni
“Ni nne na dakika tano”
“Atakuwa amesha toka hospitalini”
Lee Si alisisitiza. Kutajwa kwa hospitalini, Shamsa akamkumbuka Black Shadow wake.
“Mungu wangu……!!”
“Nini?”
“Black Shadow lazima yule dokta atamuua, si anatambua kwamba yule ni mpenzi wangu, ili kuendelea kufivha mauvo yake atamuua tu”

“Ohooo sasa itakuwaje?”
“Itabidi twende hospitalini haraka”
Wote watatu wakakubaliana kwa pamoja wakatoka nje na kukodisha taksi, iliyo wapeleka hadi hospitalini. Taksi yao ikasimama pembeni na kulipisha gari la wagonjwa linalo toka kwenye hospitali hiyo, huku Kim akiwa ndio derava wa gari hilo, cha kumshukuru Mungu hapakuwa na mtu aliye weza kulifwatilia gari hilo la wagonjwa wala Kim, kuifwatilia taksi hiyo kwani Kim moyoni mwake amejawa na hasira sana, kwani kazi yake haijakwenda kama alivyo kusudia. Gari hilo lilipo toka taksi nayo ikaruhusiwa kuingia, moja kwa moja ikaenda kusimama kwenye maegesho ya magari. Lee Si akatoa waleti yake, mfuko wa nyuma wa jinzi alilo vaa. Akampa dereva taksi kiasi anacho wadai, kisha akashuka kwenye taksi, akiwa eneo hilo akaliona gari la Phidaya likiwa kwenye maegesho yake ya kila siku.
“Madam yupo ndani, gari yake hiyo hapo”
Lee Si alizungumza huku akianza kutembea kwa hatua ndefu kuelekea ndani ya hospitali huku akifwatwa nyuma na Sa Yoo na Shamsa.

“Ohoo mjukuu wangu Lee Si mbona umeadimika siku hizi upo wapi?”
Bibi Eyna, alizungumza huku akiweka ndoo yake na ufagio wake wa kusafishia sakafu chini. Akamkumbatia Lee Si, kijana anaye mchukulia kama mjukuu wake.
“Nipo bibi, madam alinipa kazi kidogo nikawa nimebanwa banwa”
“Mbona umechubuka chubuka, alafu ni nyote watatu mumepatwa na nini?”
“Ahaa bibi nitakuambia badaye, vipi madam Phidaya yupo ofisini kwake?”
“Hapana nilimuona kwenye kordo akielekea chumba cha siri huko chini”
 

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa ya April 28

Rais Magufuli kupokea taarifa vyeti feki LEO

0
0
RAIS John Magufuli leo anatarajiwa kupokea taarifa ya zoezi la uhakiki wa vyeti kwa watumishi wa umma katika Ukumbi wa Chimwaga mkoani Dodoma.

Taarifa iliyotolewa jana na Naibu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais katika Ikulu Ndogo ya Chamwino Dodoma, Jaffar Haniu ilisema taarifa hiyo itawasilishwa kwa Rais Magufuli na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angella Kairuki.

Zoezi la uhakiki wa vyeti kwa watumishi wa umma liliendeshwa na Serikali kuanzia Oktoba, 2016. 

Hivi karibuni wakati akifungua rasmi nyumba mpya za makazi ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Rais Magufuli alisema anasubiri ripoti kuhusu watumishi wa umma wenye vyeti feki wapatao 9000.

“…Kwa hiyo mnaweza mkaona shida zilizopo katika nchi hii, huku wafanyakazi hewa karibu 19,000, wanafunzi hewa ni zaidi ya 56,000, kila mahali unapokwenda ni matatizo, lakini ni lazima niyatatue matatizo kwa sababu mlinichagua kwa ajili hiyo,” alisisitiza Rais katika hotuba yake hiyo.


Jinsi Punyeto Inavyo Sababisha Ukosefu Na Upungufu Wa Nguvu za Kiume

0
0

Ukosefu  na/ama  upungufu  wa  nguvu  za  kiume, ni  tatizo  linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume  duniani.  Zipo  sababu  nyingi  zinazo  sababisha  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume.  

Miongoni  mwa  sababu  hizo  ni  pamoja  na  maradhi  kisukari, presha,shinikizo  la  damu, moyo, figo, matatizo  kwenye  mishipa  ya  ubongo  &  mishipa  ya  uti  wa mgongo, matatizo  kwenye  mishipa itumikayo  kusafrisha damu  mwilini, maradhi  ya  ngiri,  pamoja  na   upigaji  punyeto  kwa  muda  mrefu.

Katika  makala  yetu  ya  leo, tutaangalia  namna   suala  la  upigaji  punyeto linavyo  athiri  nguvu  za  kiume.

Kabla  hatujaangalia  namna  suala la upigaji  punyeto linavyo  maliza  nguvu  za  kiume, ni  vyema  tukafahamu  kwanza  kuhusu  SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME.

Kufahamu   kuhusu   SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME  tafadhali  tembelea :

Ukisoma  vizuri  kuhusu  mfumo  wa  nguvu  za  kiume, utagundua  kuwa   Suala  la  nguvu  za  kiume  ni  suala  la  kimfumo.  Ili  mwanaume  awe na nguvu  za  kiume, aendelee  kuwa  na  nguvu  za  kiume na  azilinde  nguvu  zake za  kiume, ni  lazima  ogani  zote zinazo  husika  na  mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ziwe  na  afya  njema  na  ziwe  na  ushirikiano   thabiti  na  wenye  afya.

Vile  vile , utagundua  kuwa , mambo  makuu  muhimu  katika   mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ni  kama  ifuatavyo:

i.Mishipa  imara  ya  ubongo  na  yenye  afya  njema

ii. Mishipa  imara  ya  uti  wa  mgongo  (  spinal  cords )

iii.Mishipa  imara  itumikayo  kusafirisha  damu  mwilini  (  Blood Vessels )

iv. Mfumo  imara  wa  usafirishaji  damu  mwilini

v. Mishipa  ya  uume  iliyo  imara  na  yenye  afya  njema

vi. Uhusiano  imara  na  wenye  afya  kati  ya  mishipa  ya  fahamu  iliyopo  katika  ubongo, mishipa  ya  kwenye  uti  wa  mgongo  pamoja  na  misuli & mishipa  ya  kwenye  uume.

Hivyo  basi, ili  mwanaume  aweze  kuwa  na  nguvu  imara  za  kiume, na  aendelee  kuwa  na  nguvu  hizo ni  lazima  mambo  yote  muhimu  katika  mfumo  wa  nguvu za  kiume  yawe  imara  pasi na  hitilafu  yoyote.

Hitilafu  yoyote  katika  mambo  hayo, itasababisha  ukosefu na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume  kwa  mwanaume  huyo.  Pale inapotokea    hitilafu  ama  mapungufu  katika  ogani  zaidi  ya  moja  kati  ya  zilizo  tajwa hapo  juu, basi  tatizo  kwa  muhusika  huwa  kubwa  mara  dufu.

JINSI  PUNYETO  INAVYO  SABABISHA  TATIZO  LA  UKOSEFU &  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.
Mwanaume   anapopatwa na  wazo  la  kufanya  tendo  la  ndoa, ubongo  hutoa  ishara  kwenye  mishipa  ya  uti  wa  mgongo  ambayo  nayo  husafirisha  taarifa  hadi  kwenye  mishipa &  misuli  ya  uume.

Mishipa  ya  uume inapopokea  taarifa  hiyo, hutanuka. Na  mishipa  ya  uume  inapotanuka, hufanya  mambo  mawili  muhimu  sana :

i.Husababisha  mishipa  ya  ateri  kupanuka  na  hivyo  kuruhusu  damu  kuingia kwa  kasi  sana   ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  hivyo  kuufanya  uume  usimame  na  kuwa  imara  bara bara.

ii. Huibinya na  kuiziba  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kuzuia  kunyonya  ama  kufyonza  damu  iliyo  ingia  ndani  ya  mishipa ya  uume.  (  KAZI  KUBWA  YA  MISHIPA  YA  VENA  ILIYO  KARIBU NA  MISHIPA  YA  UUME  NI KUHAKIKISHA  HAKUNA  DAMU NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME. HIVYO  BASI  DAMU  INAPOINGIA  NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME, MISHIPA  YA  VENA  HU “SENSE” JAMBO  HILO  KWA  HARAKA  NA HIVYO  KUIFYONZA  DAMU  HIYO  KUTOKA KWENYE MISHIPA  YA UUME  YA  KUITOA  NJE YA MISHIPA  YA  UUME.  NA  DAMU INAPOKOSEKANA  NDANI  YA  MISHIPA  YA  UUME, HUUFANYA  UUME  KUSINYAA  NA  KULEGEA )

Mtu  anayepiga  punyeto  husababisha  mambo  yafuatayo  katika  mwili  wake :

1. Huuwa  nguvu  ya  mishipa  & misuli ya  uume ambayo  ndio  inayo husika  na  kusimama  kwa  uume

2. Mishipa  ya   uume  inapo  sinyaa  na  kukosa  nguvu  yake  ya  asili, husababisha  mambo  yafuatayo :

i.Huondoa  uwezo  wa  mishipa  &  misuli  ya  uume  kutanuka, na  hii  ndio  sababu  inayo  wafanya  waathirika  wa  punyeto  kutumia  nguvu  nyingi  sana  katika  kuufanya  uume  usimame.

ii.Huondoa  uwezo  wa  mishipa &  misuli  ya  uume  kuibana  na  kuiziba  mishipa  ya  vena, na  hii ndio  sababu  inayo  fanya  waathirika  wa  punyeto  kufika  kileleni  haraka  sana, kwani damu  inayo  ingia  kwenye misuli  ya  uume   hufyonzwa  ndani ya  muda  mfupi sana. 
 
 Hii  hutokea  kwa  sababu  mishipa na  misuli  ya  uume inakuwa  imelegea,na  mishipa  ya  vena inakuwa  imepwaya, hivyo  msuguano wowote ule  hufanya  mishipa  ya  vena  kufunguka  na  kufyonza  damu  kutoka  kwenye mishipa  ya  uume  na hivyo  kuufanya  uume  kusinyaa  ndani ya dakika ama sekunde  chache sana.

3. Vile  vile  punyeto  hufanya  uume  kusinyaa na  kurudi ndani  na  kuufanya  uonekane kama  uume  wa  motto mdogo.

Kwa  ufupi  punyeto  husababisha  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  sababu  kuu  zifuatazo :

i.Kwanza   hudhoofisha  na  kuharibu  mishipa  ya  uume,  ambayo  ndio  hufanya  uume kusimama.

ii.Pili  hudhoofisha  utendaji  kazi  wa  mishipa  ya  ateri, ambayo  ndio  hutumika  kama  njia  ya  kusafirisha  damu kupeleka kwenye  misuli  ya  uume  na  ivyo  kuufanya  uume  usimame

iii. Tatu, punyeto  hupelekea  kuvuja  kwa  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kusababisha  damu  kufyonzwa  kwa  haraka  sana  kila  iingiapo ndani  ya  misuli ya  uume  na  matokeo  yake  ni  uume   kusimama  kwa  muda  mfupi  sana  wakati wa  tendo  la  ndoa.

iv. Punyeto  huathiri  mtiririko  wa  damu  kwenda  kwenye  mishipa  ya  uume, kwa  sababu  hudhoofisha  misuli &  mishipa  ya  uume  pamoja  na mishipa ya  ateri  ambayo  ndio  hutumika  katika  kusafirisha  damu kwenda  kwenye  uume

DALILI  ZA  MTU  ALIYE  ATHIRIWA  NA  PUNYETO
Dalili  kuu  za  mtu  aliye athiriwa  na  punyeto  ni  kama  ifuatavyo:

i.           Uume  kusinyaa  na  kuwa  kama  wa  mtoto
ii.         Uume kurudi  ndani
iii.       Uume  kusimama  ukiwa  legelege
iv.       Kufika  kileleni  haraka  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

TIBA   YA   NGUVU  ZA  KIUME  KWA MTU  ALIYE  ATHIRIKA  NA  PUNYETO.
Dawa   asilia  ya  nguvu  za  kiume iitwayo JIKO  ni tiba  bora  na  ya  uhakika  kabisa  kwa  mtu  aliye  athiriwa   na  punyeto.  Dawa  hii, pamoja  na  mambo  mengine  mengi, husaidia  kufanya  mambio  yafuatayo  katika  mwili  wa  mwanaume  aliye  athiriwa  na  punyeto :

i.Kuimarisha  mishipa  & misuli  ya  uume  ulio  legea na  hivyo  kuurejeshea  uwezo wake wa  asili

ii. Hutibu   tatizo  la  uume  kurudi  ndani

iii.Humaliza  tatizo  la  kusimama  kwa  uume  ukiwa  legelege

iv.Hutibu  na  kuponya  kabisa  tatizo  la  kufika  kieleleni  haraka.

BEI  YA  DAWA  :  Dawa  hii  inapatikana  kwa  gharama  ya  SHILINGI  ELFU  THEMANINI  TU (Tsh. 80,000/=)

MAHALI  INAPOPATIKANA :  Dawa  hii  inapatikana  katika  duka  la  dawa  asilia  liitwalo  NEEMA  HERBALIST  &  NUTRITIONAL  FOODS  CLINIC  lililopo  jijini  DAR  ES  SALAAM  katika  eneo  la  UBUNGO   nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA   karibu  na SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING.

Kwa  wateja  wasio  weza  kufika  ofisini  kwetu. Watafikishiwa  dawa  mahali  popote  walipo  jijini  DAR  ES  SALAAM.

Kwa   wateja  waliopo  mikoani  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  MABASI

Kwa  wateja  waliopo   Zanzibar  wata fikishiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa boti.

Na  kwa  wateja  waliopo  UGHAIBUNI  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  ama  DHL.

MAWASILIANO :  WASILIANA  NASI   KWA  SIMU  NAMBA  0766  53  83  84.

Kwa  taarifa  zaidi  kuhusu  huduma  zetu, tutembelee kila  siku  kwenye  blogu  yetu :

Waziri Masauni: Waliolipua Bomu Nyumba ya Kamishna wa Polisi Zanzibar ni Viongozi wa CUF

0
0
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni amesema viongozi waandamizi wa chama cha wananchi (CUF) ndiyo walihusika na tukio la kulipua bomu katika nyumba ya Kamishna wa Jeshi la Polisi Zanzibar baada ya kufanyika uchaguzi mkuu

Mhe. Masauni alieleza hayo Bungeni Jijini Dodoma jana pindi alipokuwa akijibu swali la nyongeza kutoka kwa Mbunge wa Gandu kupitia tiketi ya (CUF) visiwani Pemba, Mhe. Othuman Omary Hajji alipotaka kujua kwanini mpaka leo hajizachukuliwa hatua stahiki kwa wafuasi wa CCM waliochoma nyumba za wanachama wa CUF huko visiwani Tumbatu, huku akidai serikali iliyopo madarakani siyo halali ni haramu kwa kuwa Jeshi la Polisi lilichangia kumuweka madarakani Dkt. Ali Mohamed Shein.

"Ni kweli baada ya uchaguzi mkuu baadhi ya vyama vya upinzani ikiwemo chake, viongozi walijitokeza kuhamasisha wananchi kufanya mambo yanayokiuka sheria za nchi yetu.

"Kuna matukio mbalimbali yalijitokeza ikiwemo kuchomwa moto nyumba, kuchoma mashamba, kurusha mabomu ikiwemo nyumba ya Kamishna wa Jeshi la Polisi wa Zanzibar ambayo kwa uchunguzi uliofanyika mpaka sasa, watu waliokamatwa kwa kuhusika urushaji bomu katika nyumba ya Kamishna ni viongozi waandamizi wa Chama cha Wananchi (CUF)". Alisema Masauni

Pamoja na hayo, Masauni alisema Jeshi la Polisi limeshakamilisha uchunguzi wake na jalada la mashtaka  lipo kwa DPP muda wowote kuanzia sasa litapandishwa Mahakamani ili sheria ichukuliwe.

Mwenyekiti Mstaafu wa CCM Atiwa Mbaroni

0
0
Jeshi la Polisi mkoani Iringa linamshikilia mwenyekiti wa zamani wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Iringa, Jesca Msambatavangu, kwa tuhuma za kumshambulia mwanamke mmoja na kumsababishia maumivu makali mwilini.
 
Msambatavangu, ambaye alikuwa miongoni mwa wanaCCM waliofukuzwa uanachama katika Mkutano Mkuu Maalum wa chama hicho uliofanyika mwezi Machi, alikamatwa  jana mchana
 
Kamanda wa Polisi mkoani Iringa, Julius Mjengi, alisema kuwa kiongozi mstaafu anatuhumiwa kutenda kosa hilo wiki iliyopita.
 
Akifafanua, Kamanda Mjengi alibainisha kuwa kiongozi huyo alitenda kosa hilo akiwa na wenzake ambao asingeweza kuweka majina yao hadharani kwani wanaendelea kuwatafuta.
 
"Ni kweli tunamshikilia Jesca Msambatavangu, tumemkamata leo(jana)  saa nane mchana na tunaendelea na uchunguzi dhidi yake," alisema Mjengi na kuongeza:
 
"Jesca pamoja na wenzake wanatuhumiwa kumshambulia mwanamke mmoja mkazi wa Kibwabwa, walimshambulia na kisha kumchoma sindano ambayo mwanamke huyo hajui ni ya kitu gani," alisema Mjengi.
 
Alipohojiwa zaidi, Mjengi alikataa kuweka wazi jina la mwanamke na idadi ya watuhumiwa wengine kwa maelezo kuwa kufanya hivyo kunaweza kuharibu upelelezi unaoendelea.

CUF Lazima Kuchafuke....Wabunge Upande wa Maalim Wamepanga Kufanya Usafi Ofisi Kuu, Kambi ya Lipuma Imejipanga Kuwazuia

0
0
Wapinzani wawili katika mgogoro wa uongozi wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad na Profesa Ibrahim Lipumba sasa wamefikia pabaya baada ya kuamua kupambana kuichukua ofisi ya makao makuu iliyopo Buguruni.

Kwa sasa ofisi hiyo inatumiwa na Profesa Lipumba, ambaye uamuzi wake wa kurejea madarakani mwaka mmoja baada ya kujiuzulu uenyekiti na nyadhifa nyingine zote, unapingwa na kundi lililopanga kuzichukua ofisi hizo Jumapili.

Jana, kundi linalompinga Profesa Lipumba lilitangaza kuwa litakwenda ofisi hizo Jumapili kwa ajili ya kusafisha “kila kitu ambacho hakitakiwi kiwepo”, lakini mwenyekiti huyo amesema ameshajiandaa kukabiliana nao na ameripoti suala hilo polisi.

Profesa Lipumba alisema hayo jana, ikiwa ni siku moja tangu Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) limtake ajitokeze kuzungumzia kitendo cha walinzi wa CUF kuwashambulia waandishi wa habari waliokuwa kwenye mkutano ulioandaliwa na viongozi wa chama hicho Kinondoni.

Profesa Lipumba alikuwa akiwajibu wabunge wa CUF wanaomuunga mkono Maalim Seif waliowaambia wanahabari katika viwanja vya Bunge mjini Dodoma jana kuwa wamepanga kwenda ofisi za Buguruni Jumapili ijayo na wataungana na wanachama wengine kufanya usafi.

“Tulianza kufanya usafi soko la Buguruni, tukamalizia katika ofisi yetu. Kwa hiyo katika hali nzuri, hatuhitaji wabunge wasumbuke kufanya usafi siku hiyo,” alisema Profesa Lipumba

Profesa Lipumba alisema watu hao hawana nia ya dhati ya kufanya usafi, bali wamepanga kufanya vurugu katika ofisi hizo kwa kushirikiana na watu wa chama kingine cha upinzani.

“Wanataka kuleta vurugu ili CUF ionekane na taswira mbaya kwa Watanzania. Naomba wanachama waepuke mtego huu, namshauri (Mbunge wa Temeke, Abdallah) Mtolea akafanye usafi huo Temeke mbona kuna masoko mengi tu machafu?” alisema.

Awali mjini Dodoma, wabunge wanaomuunga Maalim Seif walisema watakwenda na vifaa vya usafikuondoa kila uchafu watakaoukuta

“Wanachama wa Chama cha Wananchi (CUF) ambao hawamkubali Profesa Ibrahim Lipumba kuwa mwenyekiti, wameamua kwenda kufanya usafi kwenye ofisi zao za Buguruni, ofisi kuu ya CUF Buguruni,” alisema Mtolea akiwa ameambatana na wabunge wenzake katika mkutano na waandishi uliofanyika chumba cha habari cha Bunge.

“Na hatua hii imekuja baada ya kuona ofisi ile inatumika vibaya. Imekuwa ndio kijiwe cha wahuni kupanga matukio ya kihalifu. Kwenda kuvamia mikutano, kwenda kuwavamia watu na kadhalika. Sasa sisi kama wanachama tumeona hatuwezi kuiacha hali hiyo iendelee.”

Aliwataka wanachama kutoka maeneo ya Dar es Salaam, Pwani na mikoa mingine wafike kufanya usafi huo.

Alipoulizwa aina ya uchafu wanaoenda kuuondoa, Mtolea alijibu “ni kitu chochote ambacho hakiko mahali pake” na kwamba hata Profesa Lipumba hayuko mahali pake.

“Tangu Msajili amtambue Profesa Lipumba kuwa mwenyekiti, hatujawahi kwenda katika ofisi yetu ya Buguruni, matokeo yake ofisi hiyo imekuwa na uchafu mwingi na kuwa pango la wahuni,” alisema Mtolea.

Alipoulizwa uwezekano wa kutokea vurugu, Mtolea alisema hawajiandai kufanya fujo, bali kufanya usafi.

Kuhusu kesi iliyopo mahakamani kuhusu mgogoro huo, alisema ile inapinga msajili kumtambua Lipumba na haizuii kusafisha ofisi yao.

Alisema hawaendi kuteka ofisi hizo, bali wanakwenda kwenye ofisi zao hivyo hawahitaji kuomba ruhusa kwa mtu yeyote.

“Ofisi ni chafu, sisi tunataka tukaisafishe kwa sababu imekuwa sehemu ya kupanga mipango mibaya kwa mustakabali wa chama,” alisema.

Akiweka msisitizo wa jibu hilo, Mbunge wa Chambani, Yusuf Salim Hussein alisema hakuna silaha ya moto inayoshinda nguvu ya umma.

Awali, wabunge hao walitoa tamko la kuunga mkono tamko la TEF kuhusu kulaani kitendo cha wafuasi wa Profesa Lipumba kuwashambulia waandishi wa habari.

Mnadhimu wa chama hicho na Mbunge wa Malindi, Ally Salehe alisema TEF imetoa tamko zito la kutaka waandishi wa habari kufanya kazi kwa usalama na uhuru.

“Na isiwe TEF tu, tunataka watu wote waliokerwa na tukio hilo watoe tamko la kulaani,” alisema.

Kuhusu tamko la TEF, Profesa Lipumba alisema atatoa tamko kuhusu suala hilo ifikapo leo.

“Mimi ni muumini wa demokrasia. Hapa ninavyoongea na wewe nipo katika hatua ya mwisho ya kumalizia kuandika barua kuelekea TEF ambayo itafika kati ya leo (jana) jioni au kesho,” alisema.

Hata hivyo, alisema mkurugenzi wa habari, uenezi na mawasiliano kwa umma, Abdul Kambaya alitoa tamko kuhusu tukio hilo.

Katika tamko lake, Kambaya alisema mmoja wa watu walioshiriki kushambulia mkutano ni mlinzi wao na kwamba alikuwa katika doria kudhibiti wanachama wanaofanya mikutano hotelini.   

TANAPA watolea ufafanuzi taarifa zilizosambaa mitandaoni kuhusu Mwalimu wa Chuo Sinon Dar kujeruhiwa na Simba.

Taarifa za kuitwa kazini kwa madaktari waliokuwa wamekidhi vigezo kwenda kufanyakazi nchini Kenya.

LIVE: Rais John Magufuli akipokea taarifa ya zoezi la uhakiki wa Vyeti vya Watumishi wa Umma

0
0
Fuatilia matangazo ya moja kwa moja ya Rais John Magufuli akipokea taarifa ya zoezi la uhakiki wa Vyeti vya Watumishi wa Umma kutoka kwa Waziri Angellah Kairuki- ukumbi wa Chamwino, Chuo kikuu cha Dodoma

Wakuu wa Mikoa, Wilaya Wanusurika Sakata la Vyeti FEKI

0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi Bora Mhe. Angellah Kairuki amebainisha baadhi ya mambo waliyokuwa wameyapa kiupambele katika zoezi zima la uhakiki wa vyeti feki kwa kusema zoezi halikuweza kuhusika na viongozi wa kisiasa.

Kairuki amebainisha hayo leo katika ukumbi wa Chimwaga uliopo ndani ya Chuo Kikuu cha Dodoma, wakati anatoa taarifa ya uwasilishaji wa uhakiki wa vyeti feki kwa Watumishi wa Umma lilioendeshwa na Serikali kuanzia mwezi Oktoba mwaka 2016.

"Zoezi hili la uhakiki wa vyeti feki halikuwahusisha viongozi wa kisiasa kama Wabunge, Mawaziri, Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya, kwa sababu kwa mamlaka za uteuzi wao wanahitajika kujua kusoma na kuandika tu...Watumishi 9,932 wamebainika kuwa na vyeti vya kughushi sawa na asilimia 2.4 . Wenye vyeti vya utata ni 1,538 vilikuwa vikitumiwa na jumla ya watu 3,076, wenye vyeti halali pekee ni asilimia 94...Hatua hazitachukuliwa kwa wenye vyeti feki tu, bali hata kwa wanaohusika kutengeneza vyeti hivyo". Alisema Kairuki

Aidha Mhe. Kairuki amewataka wale wote wanajijua wanatumia vyeti vya kughushi waache mara moja kwa kuwa ni kosa la jinai huku akisisitiza kuwa adhabu yake ni kufungwa jela miaka saba.

Pamoja na hayo, Kairuki amepongeza serikali inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli kwa kuamua kushughulika na zoezi hilo na kulimaliza kwa awamu moja tofauti na nchi nyingine zilichukua awamu tatu huku akitolea mfano wa kwa kuzitaja nchi hizo kwamba ni South Africa na Nigeria.

Kwa upande mwingine,  Rais Dkt. Magufuli amewaagiza Waziri Kairuki na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kuwaondoa watumishi wote waliobainika kuwa wanatumia vyeti vya kughushi 'hewa' huku akisisitiza kwamba yeye hawezi kuwasemehe watu walioghushi kwani wataondoka mara moja.

Rais Maguli Afuta Zaidi ya Ajira Elfu 9 Za Walioghushi Vyeti

0
0
Rais  Dk. John Pombe Magufuli, ameiagiza Wizara ya Fedha kufuta mara moja ajira za  watumishi wa umma 9,932 waliobainika kughushi vyeti, kwenye orodha ya malipo ya watumishi wa umma.

Akiongea leo mara baada ya kupokea ripoti ya uhakiki wa vyeti vya watumishi wa umma mjini Dodoma, Rais Magufuli pia amewataka watumishi hao kuondoka wenyewe na iwapo watakaidi wakamatwe na vyombo vya dola na kushtakiwa.

Rais Dk. Magufuli pia ameziagiza mamlaka husika kujumuisha nafasi 9,932 za ajira ambazo zimeachwa wazi na watumishi wa umma walioghushi vyeti, kwenye ajira mpya zaidi ya elfu 52 za serikali ili ziweze kuchukuliwa na watu wenye sifa na uwezo wa kumudu nyadhifa zilizoachwa.

Akizungumza wakati akiwasilisha ripoti hiyo Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, Angela Kairuki, amesema, kwa Mujibu  wa Kanuni na Sheria za nchi zinabainisha wazi kuwa mtu atakaebainika kughushi vyeti au kutoa taarifa za uongo adhabu yake ni pamoja na kifungo cha Jela.

Polisi Yawazuia CUF Upande wa Maalim Kufanya Ufsafi.......Abdul Kambaya na wenzake 6 Watiwa Mbaroni kwa Kuvamia Mkutano wa CUF

0
0
Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam imezuia wanachama wa CUF kufanya usafi katika makao makuu ya chama hicho yaliyopo Buguruni kutokana na kuwepo kwa viashiria vya uvunjifu wa amani kutokana mvutano wa makundi mawili.

Akizungumza na waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Simon Sirro amesema ombi la kufanya usafi katika mazingira ya ofisi za chama hicho, liliwasilishwa na Mbunge wa Temeke, Abdallah Mtolea Aprili 27 mjini Dodoma.

Amesema kutokana na sababu za kiusalama pamoja na mgogoro wa muda mrefu unaoendelea ndani ya chama hicho, Mbunge huyo pamoja na wanachama wengine  wanashauriwa kila mmoja kufanya usafi katika eneo lake analoishi au analofanyia kazi.

"Kitendo hicho cha wanachama wa CUF kukusanyika kutoka katika maeneo mbalimbali kwa kigezo cha kufanya usafi kinaweza kusababisha uvunjifu wa amani na atakayethubutu kujitokeza atachukuliwa hatua za kisheria," amesema Sirro.

Wakati huo huo Kamanda Sirro amesema sakata la watu waliovamia mkutano wa iongozi wa CUF wilaya ya Kinondoni na wanahabari hadi sasa wanawashikilia watu saba akiwemo Mkurugenzi wa Mahusiano wa wa chama hicho, Abdul Kambaya.

Amesema upelelezi wa kesi hiyo, umefanyika vizuri na tayari jalada limefikishwa kwa Mwanasheria wa Serikali kwa ajili ya hatua zaidi ikiwemo kufikishwa mahakamani.
 
Jeshi hilo pia limewataka wananchi waliowahi kuibiwa magari yao kujitokeza katika Kituo cha Polisi Mbezi ili kuangalia kutokana,na kupatikana kwa magari matano yanayodaiwa kuibiwa jijini Dar es Salaam.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya April 29

Uchaguzi wawakilishi wa Chadema Bunge la Afrika Mashariki (EALA) Kufanyika Mei 10

0
0
Bunge  limetangaza kuwa, uchaguzi mdogo wa kupata wawakilishi wawili wa nafasi ya ubunge kwa Bunge la Afrika Mashariki (EALA) kutoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), sasa utafanyika Mei 10, mwaka huu kwenye ukumbi wa Bunge, mjini Dodoma.

Kwa mujibu wa taarifa ya Katibu wa Bunge ambaye pia ni Msimamizi wa Uchaguzi huo, Dk Thomas Kashilillah, uteuzi wa wagombea utafanyika Mei 3. 

Watakaopigiwa kura na kuchaguliwa katika uchaguzi huo wataungana na wengine saba, sita wakiwa kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) na mmoja kutoka Chama cha Wananchi (CUF) ambao walishinda katika uchaguzi wa Aprili 4, mwaka huu.

Siku hiyo, Chadema licha ya kuweka wagombea wao Lawrence Masha na Ezekiah Wenje, kura zao hazikutosha hivyo kukosa sifa za kuchaguliwa. 

Walioshinda kwa upande wa CCM ni Fancy Nkuhi, Happiness Legiko, Maryam Ussi Yahya, Dk Abdullah Makame, Dk Ngwaru Maghembe, Alhaji Adam Kimbisa wakati kutoka CUF ni Habib Mnyaa.

Wabunge Watakiwa Kujisalimisha Bodi ya Mikopo (HESLB)

0
0
Wabunge  walionufaika na mikopo iliyotolewa na Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) kuanzia mwaka 1994 wametakiwa kujisalimisha na kuanza kulipa marejesho.

Agizo hilo limekuja baada ya HESLB kupeleka barua Ofisi ya Bunge inayowataka wabunge walionufaika na mikopo hiyo kuanza kujiorodhesha na kuanza kurejesha fedha hizo.

Akisoma tangazo hilo bungeni jana, Naibu Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson, aliwaambia wabunge hao kuwa watumishi wa Bunge wataanza kugawa fomu ili kila mbunge aanze kujiorodhesha.

Novemba 14, mwaka jana, HESLB kupitia Mkurugenzi wake, Abdul-Razaq, ilitoa notisi ya siku 30 kwa wadaiwa sugu wa mikopo wawe wameanza kulipa madeni yao kabla hatua zaidi hazijachukuliwa.

Notisi hiyo ilieleza kuwa inawalenga wanufaika waliokopeshwa na muda wa marejesho ukapita bila wao kuwasilisha taarifa zao.

Katika operesheni waliyoiendesha tangu kutolewa kwa notisi hiyo, wanufaika 93,500 walibainika na kupelekewa ankara ya madeni yao ili waweze kulipa.

Hata hivyo, HESLB ilikusanya Sh bilioni 25 zilizorejeshwa kwa mwaka wa fedha wa 2016/2017 kwa wadaiwa 81,085, huku wadaiwa sugu 142,470 wenye mikopo yenye thamani ya zaidi ya Sh bilioni 239 hawajajitokeza wala kuanza kulipa mikopo yao.

Jana, Dk. Tulia alisema wabunge ambao kwa nyakati tofauti walikuwa ni wanufaika wa mikopo ya elimu ya juu iliyotolewa kuanzia mwaka wa masomo wa 1994/1995 wanapaswa kujisalimisha.

“Ofisi ya Katibu wa Bunge inawaomba wabunge wote kujihakiki ikiwa miongoni mwenu wapo waliokuwa wanufaika na mkopo huo lakini hawajaweza kurejesha fedha walizokopeshwa na bodi,” alisema.

Dk. Tulia alisema utaratibu wa uhakiki huo unafanyika kwa kuwa wabunge wengi kabla ya Novemba, mwaka juzi walikuwa katika majukumu mengine ya kikazi na kusababisha makato ya mikopo kusimama na kuonekana kama wadaiwa sugu, jambo ambalo si sahihi.

“Tafadhali mnatakiwa kujihakiki kwa kujaza fomu zilizoambatanishwa na dokezo hili, hivyo vijana wetu watawaletea fomu ili mjiandikishe na wabainike wale wanaodaiwa, hata mimi nilikuwa ni mdaiwa lakini nimelipa deni lote,” alisema.

 Dk. Tulia alisema umuhimu wa kujihakiki utawasaidia wabunge ambao hawajarejesha mikopo ya elimu ya juu kuondokana na usumbufu usio wa lazima, ikiwamo kuchukuliwa hatua za kisheria na kudhalilika na kufikishwa mahakamani.

Kampuni ya Bia (TBL) yawafuta kazi wafanyakazi 100 ndani ya saa 24

0
0
Kampuni  ya Bia ya Tanzania Breweries (TBL), imepunguza watumishi wake takribani 100 ndani ya saa 24.

Kwa mujibu wa taatifa toka kwa  watumishi wa TBL,  watumishi waliopunguzwa ni wale wa kitengo cha masoko.

Mtoa taarifa mmoja kutoka kwenye duru za uongozi wa TBL ambaye hakutaka jina lake litajwe, alisema kuwa uamuzi huo ulitekelezwa Jumatatu ya wiki hii.

Alisema sababu kuu ya kupunguza wafanyakazi hao ni kulinda uchumi wa kampuni baada ya mauzo ya bidhaa kuporomoka kwa kasi katika kipindi cha mwaka jana hadi mwaka huu.

Ofisa masoko mmoja wa kampuni hiyo ambaye hajakumbwa na panga la kupunguzwa kazi, alidokeza kwamba uamuzi huo unatokana na hali ya mauzo na uchumi wa kampuni kutokuwa rafiki.

Aliongeza kuwa uamuzi wa Serikali wa kuzuia biashara ya pombe kali zinazofungashwa kwenye mifuko ya plastiki(viroba) umeathiri kwa kiasi kikubwa soko la bidhaa yao aina ya Konyagi.

“ Wameachishwa kinyama sana, waliitwa siku ya Jumatatu na kuachishwa papo hapo(on spot), wakaambiwa wayaache magari yao na kusaini fomu ya kuondoka, miye kwa bahati nzuri  nimepona. Na hili jambo la viroba ndio limepigilia msumali wa mwisho,” alisema ofisa huyo.

Msemaji wa Kampuni ya TBL, Georgia Mutagahwa alipotafutwa kwa ajili ya uthibitisho wa taarifa hiyo, hakupokea simu kila ilipopigiwa.

Credit: Mtanzania

PICHA: Rais Magufuli Awasili Mkoani Kilimanjaro kwa Ziara ya siku Tatu ....Pia Atakuwa Mgeni rasmi katika maadhimisho ya May Mosi

0
0
Rais John Pombe Magufuli leo Aprili 29, 2017 amewasili mkoani Kilimanjaro ambapo atafanya ziara ya kikazi kwa muda wa siku tatu.

Sambamba na ziara hiyo, Rais Magufuli anatarajiwa kuhudhuria sherehe za Sikukuu ya Wafanyakazi (Mei Mosi) ambapo atakuwa mgeni rasmi.

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images