Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Askofu Gwajima Kununua Treni ya Umeme

$
0
0
Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima amesema amedhamiria kununu treni ya umeme baada ya Rais John Magufuli kuonyesha dhamira ya kujenga reli ya kisasa(standard gauge).

Amesema kuwa treni hiyo itatumika siku za ibada kubeba waumini huku wakiimba nyimbo za kumtukuza Mungu. Lakini pia alisema atakuwa tayari kuruhusu itumike kubeba abiria wa kawaida.

Askofu Gwajima aliyasema hayo jana kanisani kwake, ambapo alieleza gharama za treni hiyo ni TZS bilioni 11 lakini hakusema ni lini hasa atainunua.

“Siku moja nilimchukua mwalimu Bihagaze, alikuwa mwalimu wangu wa Biblia, nikamwambia twende nikakuonyeshe mji wa mwanakondoo, nikamchukua na helkopta hadi shambani ambapo ni mji utakuwa na mahoteli, universities, kituo cha mafuta na kila kitu,”  alisema.

Alifafanua kuwa katika mji huo, kuna ramani inaonyesha kuwa reli inapita katikati. “Alipopaona akasema mbona kuna reli inapita katikati, nikamwambia nitanunua treni, akashangaa akaniuliza, treni ni shilingi ngapi? Nikamwambia dola milioni nne na mabehewa yake dola milioni tano hivi, akasema nikulipie? Nikamwambia nitanunua mwenyewe. Akapiga magoti kusujudu nikamwambia yapo mengi yanakuja,” alisema Askofu Gwajima huku waumini wake wakimshangilia kwa shangwe.

Ujenzi wa reli uliozinduliwa na Rais Dkt Magufuli Aprili 12 mwaka huu, utakamilika ndani ya miezi 30, ambapo kwa awamu ya kwanza utaanzia Dar es Salaam hadi Morogoro, treni ikiwa na uwezo wa kukimbia umbali wa 160km/hr. Treni itakuwa na jumla ya mabehewa 100.




Uteuzi wa Jokate Mwegelo UVCCM Waibua Mfarakano

$
0
0
Uteuzi  wa Miss Tanzania namba mbili wa mwaka 2006, Jokate Mwegelo kuwa Kaimu Katibu wa Uhamasishaji wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, unaonekana kutaka kuivuruga jumuiya hiyo.

Mjadala mkubwa umeibuka kuhusu uteuzi huo, ambapo baadhi ya wanachama na viongozi wa juu wa jumuiya hiyo wamedai kuwa haukufuata kanuni na taratibu za umoja huo.

Vyanzo vya kuaminika kutoka katika umoja huo vimedai kuwa baadhi ya viongozi wa juu wa UVCCM hawakushirikishwa katika uteuzi huo uliofanywa na kigogo mmoja wa umoja huo.

Taarifa za ndani zinaeleza kuwa uteuzi huo haukushirikisha wajumbe wa Kamati ya Utekelezaji wala Baraza Kuu la UVCCM, ambalo halikukutana kumthibitisha Jokate kama kanuni zinavyoelekeza.

Kwa mujibu wa kanuni za jumuiya hiyo, wajumbe wa kamati ya utekelezaji hawazidi 10, ambapo miongoni mwao ni Mwenyekiti wa umoja huo Taifa, Makamu Mwenyekiti Taifa, Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu na mjumbe mmoja kutoka makao makuu ya chama.

Wajumbe wa baraza kuu ni wenyeviti na makatibu wa mikoa na mjumbe mmoja kutoka katika kila mkoa.

Kutokana na kile kilichodaiwa kuwa ni mvurugano ndani ya umoja huo, Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa, Shaka Hamdu Shaka, amesema kuwa uteuzi huo ulifuata taratibu zote za chama.

“Ni kweli amekaimishwa kwa kufuata taratibu zote za chama, kikao cha Kamati ya Utekelezaji kilikutana Aprili 18, mwaka huu, Dar es Salaam na ndicho kimewakaimisha wakuu wa idara watano akiwamo Jokate.

“Hao wanaolalamika hawajui kanuni na taratibu za jumuiya yetu, huwezi kupata nafasi kama kikao cha Kamati ya Utekelezaji hakijakaa,” alisema Shaka.

Hata hivyo alikiri kutoitishwa kwa kikao cha Baraza Kuu ili kuthibitisha uteuzi huo, akisema ni gharama kubwa kuitisha kikao hicho.

“Kwa kawaida Baraza Kuu huwa linakutana kila baada ya mwaka mmoja, kuita baraza kuu ni gharama sana hivyo ikitokea kuna nafasi wazi Kamati ya Utekelezaji ina mamlaka pia ya kumthibitisha,” alisema.

Kwa upande wake, Jokate alishukuru kwa uteuzi huo na kuahidi kuifanya jumuiya hiyo iwe karibu zaidi na vijana wa Kitanzania.

“Nashukuru kwa imani waliyoonyesha viongozi wangu ila zaidi kuona nina uwezo wa kuongoza idara hiyo nyeti na muhimu kwenye jumuiya.

“Kikubwa ni kuifanya jumuiya iwe karibu zaidi na vijana wa Kitanzania na kurudisha tumaini na kusimamia changamoto wanazozikabili vijana katika kujiletea maendeleo,” alisema Jokate.

Jokate pia alikuwa miongozi mwa wanachama 450 wa CCM waliojitokeza kuchukua fomu za kuwania ubunge wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA).

Jokate alianzia kwenye mashindano ya Miss Tanzania mwaka 2006 ambapo aliibuka mshindi wa pili.

Hivi sasa anajishughulisha na sanaa na ujasiriamali ambapo anamiliki Lebo ya Kidoti Fashion inayojihusisha na uuzaji wa nywele na mavazi.

Mgogo CUF Wazidi Kuwaka Moto......Wabunge Walaani, Polisi Wafuta Mkutano wa Maalim Seif

$
0
0
Siku  moja baada ya kutokea kwa vurugu kubwa katika mkutano wa viongozi wa Chama cha Wananchi (CUF) Wilaya ya Kinondoni, Dar es Salaam kwa kuvamiwa na genge la watu waliokuwa na silaha za moto, wabunge wa upinzani wameibuka na kuitupia lawama Serikali.

Kutokana na hali hiyo wabunge hao wamesema ukimya wa Serikali kuhusu uvamizi huo wa viongozi wa CUF, huku wakitangaza kumwandikia barua Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Ernest Mangu pamoja na taasisi nyingine za Serikali kuhusu tukio hilo.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma, Naibu Mnadhimu wa Kambi rasmi ya Upinzani bungeni, Ally Saleh alishangazwa na ukimya wa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe kwa kushindwa kujitokeza na kukemea hatua ya waandishi wa habari kupigwa katika mkutano huo.

Kutokana na hilo, wamelaani kitendo hicho cha uvamizi wa mkutano pamoja na waandishi wa habari kupigwa huku wakiitaka Serikali kutoa tamko na kuchukua hatua kali dhidi ya waliohusika.

Wakati wabunge hao wakitoa tamko hilo,  Dk. Mwakyembe  yeye amekana kuwa taarifa juu ya tukio hilo. 

“Mimi sijui chochote ndiyo nasikia kwako, kwani hao wabunge wamekwambia kama wameniletea taarifa hizo? Mimi niko Dodoma…sifahamu chochote,” alisema.

Akizungumzia hali hiyo Saleh, alisema chama cha CUF, kimeshamwandikia barua IGP Mangu pamoja na taasisi nyingine za Serikali kuhusu tukio hilo.

Alisema ukimya wa Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba na Dk. Mwakyembe juu ya tukio hilo umeonesha kuwa hawajatimizi majukumu yao ipasavyo.

 “Mambo haya yanavyotokea mawaziri wawili tunataka kuwavisha mnyororo, Waziri Mwigulu Nchemba na Mwakyembe.

“Mwakyembe alipaswa kujitokeza kwa haraka na kutoa tamko, tunahisi jukumu la Serikali halijatekelezwa, Mwakyembe anapaswa kuhakikisha usalama wa waandishi unakuwapo,” alisema.

Saleh ambaye ni Mbunge wa Malindi alisema kikundi cha ‘Mungiki’ si kigeni hapa nchini na Serikali inakifahamu lakini hakuna hatua zozote ambazo zimeshachukuliwa hadi sasa.

Aidha alisema kutokana na tukio lililotokea juzi, ziara  iliyokuwa ifanywe na Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Shariff Hamad upande wa bara jana ilifutwa na Serikali.

“Kitendo cha Serikali kuufuta mkutano huo si sawa kwa sababu bwana yule (Profesa Ibrahim Lipumba) anabebwa na mbereko ya Serikali kwa kufanya mikutano ya ndani kila wakati.

“Serikali inalea Jamhuri ndogo ndani ya Jamhuri, vile vile Serikali imekuwa inalea kambi ndogo ndani ya Buguruni na kwamba wanufaika zaidi wa mgogoro unaoendelea ndani ya CUF ni Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambao dhumuni lao ni kuchukua majimbo yanayoongozwa na CUF katika uchaguzi mkuu ujao,”alisema.

Kwa upande wake Naibu Waziri Kivuli wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Devotha Minja alisema matukio wanayofanyiwa waandishi wa habari yanapaswa kukemewa.

“Waandishi wa habari ni kiungo cha serikali na wananchi, pia ni kiungo kati ya wanasiasa na wananchi, suala walilofanyiwa jana linapaswa kukemewa na halipaswi kuendelea kutokea,” alisema Minja.

Minja ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema), alisema waandishi wa habari wamekuwa wakionewa na kupigwa, akitolea mfano wa tukio la kuvamiwa kwa Kituo cha Televisheni cha Clouds, kutekwa na kuteswa kwa Absalom Kibanda, kuuawa kwa aliyekuwa mwandishi wa Channel Ten, Daud Mwangosi.

Kutokana na vurugu hizo ambazo zilisababisha mtu mmija anayedaiwa kuvamia mkutano huo kujeruhiwa,  Jeshi la Polisi limesema bado linaendelea na uchunguzi wa kina kuhusu tukio hilo na hadi sasa hakuna mtu yeyote anayeshikilia.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Suzan Kaganda, amesema bado wanaendelea na uchunguzi wa tukio hilo ikiwa ni pamoja na wahusika waliosababisha vurugu hizo.

“ Kwa sasa hatuwezi kuzungumzia jambo lolote kuhusu tukio hilo…tunaendelea na uchunguzi wa kina kuhusu vurugu hizo na baada ya uchunguzi wetu kukamilika tutatoa taarifa ,”alisema Suzan.

Tamko la serikali kuhusu kushambuliwa waandishi wa habari katika mkutano wa CUF

$
0
0
Serikali imepokea kwa masikitiko taarifa za kushambuliwa na kujeruhiwa baadhi ya waandishi wa habari katika mvutano uliotokea juzi jijini Dar es Salaam kati ya wafuasi wa pande mbili zinazokinzana za Chama cha Wananchi (CUF). Tumechukua muda kidogo kulifuatilia suala hili na kubaini licha ya baadhi yao kujeruhiwa na kuripoti polisi, wapo waandishi ambao vifaa vyao vya kazi pia vililengwa katika shambulizi hilo.

Tunachukua fursa hii kulaani kitendo cha kuumizwa wanahabari tena waliokuwa wamealikwa kuhudhuria mkutano huo. Ifahamike kuwa uandishi wa habari ni taaluma adhimu na nadhifu inayopaswa kuheshimiwa, kuenziwa, kulindwa na kutoingizwa katika migogoro ya pande zinazofarakana katika jamii.

Kifungu cha 7 (1) (a) cha Sheria ya Huduma za Habari Na. 12 ya mwaka 2016 kinaainisha uhuru wa wanahabari katika kukusanya habari kwa muktadha wa kuwepo katika maeneo ya matukio kama hakuna sababu nyingine za kuzuiwa. Misingi ya uhuru huu wa kitaaluma pia imesisitizwa katika Ibara za 18 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977 na 19 ya Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Kiraia na Kisiasa wa mwaka 1966 ambao nchi yetu imeuridhia.

Tunawatakia nafuu ya haraka wanahabari waliojeruhiwa na wenzao wengine waliopatwa na jakamoyo katika tukio hilo. Kwa kuwa suala hili tayari limeripotiwa polisi, tunawaomba wadau wote wa habari na wanasiasa kwa sasa kutulia na kuviachia vyombo husika vilifanyie kazi ili hatua stahiki za kisheria zichukuliwe.

Imetolewa na:
Dkt. Hassan Abbasi
Mkurugenzi, Idara ya Habari-MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali

SORRY MADAM -Sehemu ya 55 & 56 (Destination of my enemies)

$
0
0
 MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWAILIPOISHIA

ILIPOISHIA
“Mungu wangu…..!! Umezinduka?”
Phidaya alizungumza huku akipiga magoti chini, akakinyanyua kichwa cha Black Shadow, akakiweka kwenye mapaja yake, akijaribu kumpa huduma ya kwanza mgonjwa, macho ya Eddy yaliyo jaa machozi ya maumivu makali ya mbavu zake zilizo piga chini, alipo kuwa akijaribu kunyanyuka kitandani ili kumuona mwanamke mwenye sauti ya inayo fanana na Phidaya, yakatua usoni mwa nesi huyo, akajikuta akistuka kwani ni Phidaya mwenyewe, ndiye aliyepo mbele yake akimuhudumia.

ENDELEA
Kwa haraka Phidaya,  akakiweka kichwa cha Black Shadow chini, akamnyoosha ili asiendelee kujikunja na kusabaisha nyuzi alizo shonwa kwenye mbavu kuachia. Akatoa simua yake na kumpigia daktari msaidizi wa dokta Ranjiti, akamuelezea hali ya mgonjwa aliyo kuwa nayo.
“Phidaya……”
Black Shadow akajitahidi kumuita Phidaya na kumfanya astuke na kumtazama mgonjwa wake.

“Unalijua jina langu…..?”
“Phid….aa…ya mk……”
Black Shadow hakumalizia sentensi yake akatulia kimya akazimia tena. Phidaya akazidi kuchanganyikiwa ndani ya dakika moja mbeleni daktari akafika akiwa na dawa maalumu za kupunguza maumivu, wakasaidia na Phidaya kumnyanyua Black Shadow na kumrudisha kitandani mwake. Dokta akamfantia uchunguzi wa haraka, cha kumshukuru Mungu hapakuwa na itilafu iliyo weza kujitokeza kwenye mshono wake.

“Amepoteza fahamu kutokana na muumivu makali sana”
Dokta Yan alimuambia Phidaya aliye onekana kuwa na wasiwasi mwingi.
“Ila dokta Yan, huyu mgonjwa anaonekana kama kunijua mimi”
“Kukujua wewe kivipi?”
“Ameniita jina langu la Phidaya”
Dokta Yan akabaki akiwa na mshangao asijue ni kitu gani kinacho endelea. Kila mara Phidaya akajikuta akijifuta jasho usoni mwake na kitambaa chake, mapigo ya moyo wake hayakutulia kabisa kiasi cha kumfanya ahisi kuna jambo ambalo Black Shadow analitambua, isitoshe maneno yake ya mwisho yaliyo katika katika alipokuwa akizungumza ndio yalizidi kumchanganya.

“Hivi atazinduka kweli?”
“Ndio nesi atazinduka, ila itamchukua kama masaa mengine tisa hadi kumi, kwa maana sindano nilkiyo mchoma inapunguza mumivu taratibu taratibu”
“Isije akawa akaka kwa muda mrefu kama alivyo kaa?”
“Hapana atakuwa salama tu nesi, ila nikuulize swali?”
“Uliza tu”
“Mbona una wasiwasi mwingi sana juu ya huyu mgonjwa tofauti sana na mara ya kwanza?”
“Kusema kweli dokta Yan mimi sielewi kabisa kichwa change, nahisi kuna kitu ambacho najaribu kukikumbuka ila nashindwa kujua ni kitu gani hicho”

Macho yakamtoka dokta Yan, wasiwasi mwingi na yeye ukamtawala ila akajikaza asiweze kuuonyesha mbele ya Phidaya. Akamuomba Phidaya aondoke akaendelee na kazi zake. Phidaya hakuwa na hiyana yoyote kwa daktari huyo msaidizi wa mume wake. Akaondoka na kuelekea ofisini kwake akamuacha Phidaya akiwa amesimama jirani kabisa na kitanda cha Black Shadow.

Phidaya kwa mara nyingine, akajikuta akianza kumvua Black Shaodow kinyago alicho kivaa, akafanikiwa kumaliza kukivua kinyago hicho na kukishika katika mkono wake wa kushoto. Sura nzuri ya Black Shadow, ikamfanya aitazame kwa muda mwingi sana zaidi ya dakika kumi.
Wazo moja likamjia kichwani mwake, akatoa simu yake na kuingia upande wa kamera kisha akampiga Black Shadow picha nne, alipo maliza akamvalisha kinyago chake kama kilivyo kuwa na kutoka zake ndani ya chumba hicho.
                                                                                                 ***
“Ndio dokta kuna jambo nahitaji kukuambia”
Dokta Yan, alizungumza kwenye simu yake mara ya kuingia ofisini kwake na kujifungia kwa ndani. Simu hiyo iliyopo hewani, anazungumza na dokta Ranjiti akiwa ndani ya gari akirudi kutoka kwenye mgahawa alipo kwenda kuonana na Kim.
“Jambo gani hilo?”
“Ni kuhusiana na mke wako”
“Amefanyaje?”
“Nahisi anaanza kuutafuta ukweli juu yake”
“Umelijuaje hilo?”
“Anadai kwamba yule mgonjwa mpiganaji amezinduka, na amemuita jina lake”
“U…uuu..nasema mpiganaji amezinduka…..?”

“Ndio amezinduka na amemuita mkeo jina lake na hapa kunaonekana kuna kufamiana”
“Sasa umefanyaje wewe”
Dokta Ranjiti alizungumza huku akionekana kama amechanganyikiwa kwa taarifa aliyo pewa.
“Ilinibidi nimchome sindano ya usingizi, ili hadi utakapo rudi tuweze kujua tunafanyaje”
“Kazi nzuri Yan, nipo njiani nakuja sasa hivi”
Dokta Yan akakata simu na kukaa vizuri kwenye kiti chake akimfikiria mgonjwa waliye muweka katika chumba cha siri, kwani yeye ni mtu wa karibu wa dokta Ranjiti  na anafhamu kila kitu ambacho kimetokea kati ya Phidaya na Ranjiti.
                                                                                                    ***
   Mawazo ya Shamsa yote yakahamia kwa Phidaya, mwanamke aliye mchukulia kama mama yake, ambaye alimpatia upendo mkubwa  kama alivyo kuwa amepatiwa kwa marehemu mama yake. Tangu aweze kuishi na Phidaya kwa miaka zaidi ya mitatu, alitokea kumpenda mama huyo, kwani wote asili zao zimeenda na ilikuwa ni vigumu sana kwa watu kuwatofautisha hao kama si mtu na mama yake. Asili yao ya kihidi ndio ilizidi kuwafanya wafanane japo si sana.

“Shamsa una waza nini?”
Sa Yoo alimuuliza Shamsa aliye jilaza kwenye sofa ndani ya sebule yao, huku miguu yake akiwa ameiweka juu ya meza kubwa ya kioo iliyopo jirani naye. Shamsa akashusha pumzi kidogo kisha akaishusha miguu yake kwenye meza na kukaa sawa.

“Namfikiria yule nesi kule hospitalini”
“Sasa ndio anakufanya uwe katika mawazo kiasi hicho, kama ni ugomvi si ulisha isha”
“Hapana si hivyo Sa Yoo”
“Ila ni nini?”
Ýule ni mama yangu”
Sa Yoo macho yakamtoka kama ameona kitu cha kushangaza sana na chakutisha, taratibu Sa Yoo akajiweka vizuri kwenye sofa alilo kaa na kuendelea kumtumbulia macho Shamsa.

“Mbona unanitumbulia macho yako hivyo, unaniogopesha bwana”
“Hamna Shamsa, nashangaa, inakuwaje yule nesi awe mama yako?”
“Kweli ni mama yangu, ila cha kushangaza tulisha mzika, yeye, bibi na mdogo wangu wa kiume anaitwa Junio”
“Sasa, Shamsa unataka kuniambia siku hizi watu wanaweza kurudi kutoka wafu au….?”
“Sa Yoo sio hivyo hata mimi nashangaa kwanini imekuwa hivyo”

“Ahahaa hapana Shamsa bado hujanishawishi”
“Hembu lete Laptop”
Sa Yoo akanyanyuka na kuichukua Laptop ilipoto kwenye meza ya chakula akarudi nayo na kukaa kwenye sofa alilipo Shamsa. Akaiweka mezani na Shamsa akaifungua na kuiwasha, wakasubiria kwa sekunde kumi na tano ilipo waka, Shamsa akaingia kwenye mtandao wa ‘google’ akaandika jina lake, haikuchukua sekunde jina lake likawa limejitokea kwenye kioo cha laptop hiyo akaingia kwenye sehemu ya picha, zikafunguka picha nyingi, picha ya kwanza kabisa kuonekana ni yake  akiwa na Phidaya pamoja na Junio. Macho yakamtoka Sa Yoo.

Akaivuta laptop karibu kudhibitisha picha anayo inaoa kweli nesi aliye muoana anafanana kabisa na mtu anaye muona amesimama na Shamsa. Mwanga wa Laptop hiyo ukaanza kufifia huku taa nyekundu ndogo ikiwaka chini kidogo ya kioo hicho.
“Ohoo inaisha chaji, hujaichomeka kwenye kebo ya umeme hembu inama uivute hiyo kebo”

Sa Yoo alizungumza na Shamsa akafanya kama alivyo ambiwa, gafla Laptop hiyo ikarushwa mbali na kuangukia chini, huku kioo cha dirisha la karibu walipo kaa, likipasuliwa na risasi ambayo imeingia na kumkosa Shamsa aliye inama chini kuvuta kebo hiyo na kutua kwenye laptop.
“Sa Yoo inama chini”
Shamsa alizungumza kwa sauti kali, Sa Yoo bila hata kuuliza akalala chini kabisa ya sakafu.
“Shamsa ni nini hicho”
“Ni risasi hiyo”
Risasi mfululizo zikaanza kumiminika ndani ya sable yao, meza ya kioo ikapasuliwa, kila mmoja akawa amelala chini na kujibanza kwa chini kwenye sofa walilo kuwa wamelalia.
                                                                                                         ***
  Kim baada ya kukabidhiwa kazi na dokta Ranjiti ya kumuua Shamsa hakuona haja ya kupoteza muda wala kujipanga kwani mtu ambaye anakwenda kumuu kwake ni sawasawa na siafu mdogo ambaye anaweza kuminya minya chini kwa kidole chake kimoja.

Akarudi nyumbani kwake na kuingia kwenye compyuta yake, akalisaka jina la Shamsa Eddy, akafanikiwa kulipata, kwa utaalamu wake alio kuwa nao kwenye maswala ya mtandao akafanikiwa kufahamu hadi nyumba anayo ishi binti huyo alipo, hakikisha kwamba amefanikiwa kumpata, akafungua droo lake kubwa, ambapo akachukua budnuki yake aina ya L115A3 AWM yenye uzito usio pungua kilo 16 ikiwa na risasi zake tano ndani ya magazine.

Akaiingiza kwenye begi lake kubwa, akachukua na bastola zake mbili, akazichomeka kwa kiunoni kwa nyuma, akajiweka sawa na kutoka nje ya nyumba yake. Akaliweka begi lake ndani ya gari lake aina ya Range Rover, na taratibu akaanza kuondoka kuelekeaeneo la tukio.

Lee Si, aliweza kumuona Kim akiwa anatoka nyumbani kwake, kama alivyo agizwa na bosi wake Madam Phidaya, akaendelea kumfwatilia mtu huyo ambaye amepewa kazi na dokta Ranjiti.
Kim hakustuka kwamba anafwatiliwa hadi alipo fika katika eneo la karibu kabisa na nyumba ambayo anaishi Shamsa. Kwa uzuri karibu na nyumba hiyo kuna moja ya dorofa linalo endelea kujengwa ila ni takribani wiki mbili ujenzi wa jengo hilo umesimamishwa kutokana na uchunguzi unao fanyiwa mkandarasi wa gorofa hilo.

Kim akapanda hadi gorofa ya tano akiwa na begi lenye bunduki yake hiyo kubwa, ambayo mara nyingi anaitumia kwa mauaji ya mtu mmoja mmoja. Akaitoa bunduki yake hiyo na kuifunga, akaiweka sawa kwenye moja ya dirisha linalo elekea kwenye nyumba ya Shamsa.
   Kwa kutumia Lensi ya bunduki hiyo akafanikiwa kuwaona mabinti wawili wakiwa wamekaa kwenye sofa huku wakionekana vichwa kwa nyuma. Kitu kilicho mchanganya hakujua kati ya hao mabinti wawili yupi ni muhusika anaye paswa kuuawa.

Akamlenga shabaha binti wa kwanza upande wa kushoto kwake, ila binti huyo alipo inama kidogo aliweza kuina sura yake, na kutambua kwamba sio ambaye anatakiwa kumuu. Akaihamishia shabaha yake kwa binti wa kulia kwake, alipo hakikisha kwamba amemuweka vizuri kwenye tageti, akafyatua risasi, ila binti huyo aliinama chini kabla ya risasi hiyo kufika na kutua kwenye laptop ambayo hapo mwanzo binti huyo alikuwa ameiziba.

”Shitii…….”
Kim alizungumza huku akiwa ameyakaza meno yake, kwani tangu aanze kuifanya kazi ya mauaji hakuwahi kumkosa shabaha yule aliye kusudia kumuua, hata iweje, ila kwa huyu binti sijui imekuwaje. Binti wa pili naye akapotea kwenye tageti yake na risasi aliyo kuwa amemlenga ikatua kwenye meza ya kioo na kupasuka pasuka. Sofa ndilo lililo haribu mpango mzima wa Kim kumuua Shamsa, kila alipo jaribu kuwatafuta hakuweza kuwaona.

Lee Si, alishushudia mpango mzima ukiwa unaendelea kwa muuji na wanao paswa kuuliwa, akiwa amekaa ndani ya gari lake mbali kidogo na nyumba ambayo ishi Shamsa.
“Hapa ndipo atakapokuwa anaishi yule binti”
Lee Si alizungumza huku akitazama jinsi Kim akipiga risasa zinazo toka kimya kimya kutokana na bunduki anayo itumia kufungwa kiwambo cha kuzuia risasi.

“Hapana naweza kufanya kitu”
Lee Si akawasha gari lake, akakanyaga mafuta kwa kasi na kwenda kulipaki mbele ya mlango wa nyumba ya Shamsa, kwa utaalamu mkubwa akajirusha nje ya gari baada ya kulisimamisha, akaupiga teke mlango huo na ukafunguka, jambo lililo washangaza Sa Yoo na Shamsa, hata Kim mwenyewe akashangaa kuona gari nyekundu ikiwa imesimama nje ya mlango wa Shamsa.
                                                                                                     ***
“Vipi mwenzetu tulisikia kwamba unaumwa?”
Halima alimuuliza Rahab huku akijipangusa machozi ya furaha yaliyo mtiririka usoni mwake.
“Yaa kweli nilikuwa ninaumwa?”
“Nini zaidi”
Fetty alimuuliza Rahab huku akiwa ameupitisha mkono wake mmoja mabegani mwa Rahab.
“Ahaa ni malaria tu ilinishika nusu iniue”
Rahab aliongopea

“Doo pole sana”
“Sasa mke wa raisi inakuwaje anaumwa Malaria hadi ikulu kuna mbu kweli?”
Anna alitania huku akicheka, wote wakajikuta wakiangua kicheko, wakamkaribisha Rahab na kuketi naye kwenye masofa yaliyomo ndani ya chumba chao.
“Vipi unatumia kilevi, au ndio umestaarabika Mrs President”
“Hapana jamani, bado nina dozi musije mukaniua mwana wa mwenzenu. Haya niambieni yaliyo wakuta kwa maana nasikia mulikufa nyinyi?”
“Ni kweli kama tetesi ulivyo sizikia kwamba tumekufa ila ndivyo dunia inavyo jua, ila ukweli hatujakufa”

Fetty akaanza kuadisia mkasa wa wao tangu walipo achana, wakiamini kwamba rafiki yao huyo alikamatwa kwenye tukio la mwisho la wao kuvamia benki hadi wao walivyo pitia matatizo mengi pamoja na mateso. Hawakumficha ujuzi walio upata kwa bwana Rusev, na jinsi alivyo watelekeza na kuangukia mikononi mwa Wamarekani. Mateso makali waliyo pitia wakiwa gerezani hadi kuokolewa na Mzee Godwin na kurudi tena Tanzania.
Machozi yakamwagika, Rahab, kwani historia hiyo iliyo wapata wezake imemsikitisha kupita maelezo, na yeye akawaadisia mambo yote yaliyo mpata kwenye maisha yake hadi kuolewa na raisi Praygod, ila kitu alicho waficha wezake na nguvu zake za ajabu alizo kuwa nazo.

“Ila unampenda huyo mumeo”
Agnes aliuliza huku akiwa amekazia macho Rahab.
“Ahaaa hivyo hivyo tu maisha yanasonga”
“Mmmmm ila kunaonekana ikulu ni kuzuri, mwenzetu huna hata doa”
Wote wakacheka, Rahab akatambulishwa kwa Jaquline na Manka. Wakaendelea kupiga piga stori kuhusiana na mpango wao wa kuingia ikulu kupitia kura za wananchi.

“Musijali nitahakikisha munaingia ikulu na si munatambua raisi Praygod ni mmoja wa target yetu ambaye bado hatujafanikiwa kuiangusha?”
Rahab alizungumza huku akiwatazama wezake wote ndani ya chumba, Fetty akatingisha kichwa akimaanisha kwamba anakumbuka.
“Basi nitakuwa nikiwaeleza kila kitu ambacho kitakuwa kinaendelea ndani ya ikulu”
Wote wakampigia makofi Rahab, kila mmoja akaamini ushindi wa Mzee Godwin kuingia ikulu upo karibu kuiva.
                                                                                                       ***
   Dokta Ranjiti akasimamisha gari lake eneo la maegesho na kushuka kwa haraka, akaanza kutembea kwa kasi kueleka ofisini kwake, akili yake alihisi inakwenda kuchanganyikiwa, swali kubwa alilo jiuliza, imekuwaje Black Shadow, alitambue jina la mke wake. Kila alipo jaribu kuhisi labda Black Shadow, aliweza kusoma koti la mke wake, ambalo kila mfanya kazi wa hospitalini kwenye nguo yake ya kazi huwa kuna jina.

 Hilo nalo halikumuingia kabisa akilini, akafungua ofisi yake na kukaa kwenye kiti chake cha kuzunguka, kwa haraka akampigia simu dokta Yan, ndani ya dakika tatu akawa amefika kwenye ofisi ya dokta Ranjiti.
“Hembu nieleze ilikuwaje kuwaje?”
Dokta Ranjiti alizungumza kwa sauti ya chini ya kunong’oneza, kwani swala hilo ni nyeti sana na halikupaswa mtu yoyote kuweza kulisikia.
“Kwa madai yake amesema kwamba mgonjwa alimuita baada ya kuzinduka”

Naye dokta Yan alizungumza kwa sauti ya chini.
“Sasa huyo Black Shadow amemjuaje mke wangu?”
“Hata mimi sitambui dokta, au anaweza kuwa ni rafiki wa karibu wa huyo mume wake uliye niambia?”
“Yaweza kuwa, au unaonaje tukamfunue sura yake, kwa maana najishangaa tumemfanyia mgonjwa upasuaji hata kuiona sura yake”

“Hapo kweli umenena dokta”
Dokta Ranjiti akashusha pumzi nyingi, huku akimtazama dokta Yan, rafiki yake wa muda mrefu sana. Kwa pamoja wakanyanyuka, na kutoka ndani ya ofisi kuelekea katika chumba cha siri walipo mlaza Black Shadow.
   Phidaya akaitazama picha ya Black Shadow kwenye simu yake, akayafumba macho yake kwa muda mrefu, huku akihakikisha kwamba anajaribu kumkumbuka mtu huyo, kwani kila alipo jaribu kuitazama picha hiyo mapigo yake ya moyo yalimuenda kasi sana.

Naibu Waziri wa Afya Hamis Kigwangalla Ammwagia Sifa Diamond Platnumz

$
0
0
Siku chache baada ya staa mwimbaji Diamond Platnumz kuzindua Perfume yake mpya “Chibu Perfume” na kuonesha kupokelewa kwa nguvu kubwa nchini Tanzania, Naibu Waziri wa Afya, Hamis Kigwangalla ameandika ujumbe kuhusu perfume hiyo huku akimsifia Diamond kwa kufanya vitu vikubwa pamoja na kukiri kuwa yeye sio shabiki wake isipokuwa anaupenda muziki wake.

“Sikuwahi kuwa mshabiki wa msanii huyu kijana @diamondplatnumz, kama nilivyosema hapo nyuma kidogo, japokuwa nimekuwa nikifuatilia na ku-enjoy muziki wake; Ila toka nimeanza kumfuatilia nimegundua kuwa, this young man is not only a good entertainer, but also a talented entrepreneur and businessman.

"He does business in music, he does a business of entertainment. Sasa naona kupitia kipaji chake cha ujasiriamali, naona ameamua kuwa muwekezaji, an investor! This is incredible. Keep stepping up your game son, that’s the way to do it! Hakika wewe umetoka #NjeYaBox, na Mungu akuongoze ubaki huko huko juu, usishuke!

"I wish wasanii wenzako pia watoke nje ya box kifikra, wafanye biashara kwenye vipaji vyao, wageuze changamoto kuwa fursa, waache kulalamika, wapige kazi tu! #HapaKaziTu! Kwa sababu nyie watu mashuhuri mkigeuza crowds zenu kama chanzo cha solo la bidhaa zenu, kwa hakika mtafanikiwa sana!

"Changamoto kwenu wadogo zangu…#chibudangote #chibu #diamondplatnumz 💪🏾#MzeeWaField #Dr_Kigwangalla #HamisiKigwangalla #SiasaNiVitendo #supportingourown #MadeInTanzania #Tanzanian #ProudlyTanzanian – Hamis Kigwangalla (Naibu Waziri wa Afya)
Sikuwahi kuwa mshabiki wa msanii huyu kijana @diamondplatnumz, kama nilivyosema hapo nyuma kidogo, japokuwa nimekuwa nikifuatilia na ku-enjoy muziki wake; Ila toka nimeanza kumfuatilia nimegundua kuwa, this young man is not only a good entertainer, but also a talented entrepreneur and businessman. He does business in music, he does a business of entertainment. Sasa naona kupitia kipaji chake cha ujasiriamali, naona ameamua kuwa muwekezaji, an investor! This is incredible. Keep stepping up your game son, that's the way to do it! Hakika wewe umetoka #NjeYaBox, na Mungu akuongoze ubaki huko huko juu, usishuke! I wish wasanii wenzako pia watoke nje ya box kifikra, wafanye biashara kwenye vipaji vyao, wageuze changamoto kuwa fursa, waache kulalamika, wapige kazi tu! #HapaKaziTu! Kwa sababu nyie watu mashuhuri mkigeuza crowds zenu kama chanzo cha solo la bidhaa zenu, kwa hakika mtafanikiwa sana! Changamoto kwenu wadogo zangu...#chibudangote #chibu #diamondplatnumz 💪🏾#MzeeWaField #Dr_Kigwangalla #HamisiKigwangalla #SiasaNiVitendo #supportingourown #MadeInTanzania #Tanzanian #ProudlyTanzanian Pongezi nyingi kwa team nzima nyuma ya Diamond 💎 @sallam_sk @babutale @mkubwafellatmk
A post shared by Dr. Hamisi Kigwangalla (@hamisi_kigwangalla) on

Wapinzani Wagoma Kusoma Hotuba Yao Bungeni

$
0
0
Msemaji wa upinzani katika Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira na Muungano, Ally Salehe amesusa kusoma hotuba yake ya upinzani kuhusu wizara hiyo baada ya kulazimishwa kuacha kusoma baadhi ya maneno yakiwamo yanayohusu Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar na mgogoro wa CUF.

Hali  hiyo imetokea bungeni leo Jumatatu baada ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali(AG), George Masaju kusimama na kupinga baadhi ya maneneo aliyotumia kama “Kila wizara imekiona cha moto, wamebanwa mpaka wamevunjwa mbavu” na kuwa Ofisi ya Makamu wa Rais imeathirika vibaya na kisu cha ngariba kwa kukata bajeti yake.

Baada ya malumbano, Mwenyekiti wa Bunge, Musa Zungu alitoa uamuzi kuwa maneno yaliyoandikwa kuanzia ukurasa wa tatu hadi wa saba kwenye hotuba hiyo yasisomwe wala kurekodiwa kwenye kumbukumbu rasmi za Bunge.

Baada ya uamuzi huo, Salehe alisema basi asingeendea kuisoma hotuba yake na yaliyobaki anamwachia ngariba afanye anavyotaka

Msajili wa Vyama vya Siasa Aibuka na Kulaani Vurugu za CUF

$
0
0
Nimesoma na kuona katika vyombo mbalimbali vya habari kuhusu vurugu zilizotokea tarehe 22 Aprili, 2017 katika hoteli ya Vina, Mabibo hapa Dar es salaam, zinazosemekana kuhusisha wanachama wa CUF.

Ni ukweli usiopingika kuwa, suala la mgogoro wa uongozi katika chama cha CUF lipo mahakamani, lakini nikiwa msimamizi wa Sheria ya Vyama vya Siasa na kutambuliwa na jamii kuwa ni mlezi wa vyama vya siasa; nimelazimika kuwasihi wadau wa siasa hususani wanachama wa chama cha CUF, kutambua kwamba, kuwapo kwa shauri mahakamani siyo fursa ya kufanya vitendo vya uvunjifu wa amani, kwani jambo hili ni uvunjifu wa sheria na linaleta sura mbaya kwa jamii.

Hivyo, ninalaani vurugu hizo, ambazo zilionekana kuvunja amani na utulivu na watu kuumizwa, tofauti na tunu zetu za taifa za amani na utulivu. Pia, nawaasa wanachama wa CUF pamoja na tofauti walizonazo, madhali masuala haya yapo mahakamani hebu tuheshimu utawala wa Sheria.

Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa na hata Jeshi la Polisi lipo kushughulikia malalamiko yoyote yanayohusu uendeshaji na shughuli za chama chochote cha siasa. Hivyo, hakuna haja ya wanachama wa chama cha CUF kukiuka taratibu za kuendesha chama hicho au kujichukulia Sheria mkononi.

Aidha, ninaviasa vyama vya siasa kuelewa kuwa havipo juu ya Sheria, vinapaswa kuheshimu na kufuata Sheria za nchi, ikiwamo kutunza amani na utulivu tulionao.

Mwisho, ninaomba vyombo vya ulinzi na usalama katika nchi yetu kulifanyia kazi tukio hilo, ili wahusika wafahamike na kuchukuliwa hatua za kisheria. Kwa upande wa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa inayosimamia utekelezaji wa Sheria ya Vyama vya Siasa, haitasita kuchukua hatua stahiki kwa mujibu wa Sheria.

Jaji Francis S.K. Mutungi                              
MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA
24 Aprili, 2017

Mtu mmoja Amejinyonga hadi kufa kwa Kutumia Kamba ya Katani Mkoani Mwanza

$
0
0
****Mtu mmoja amejinyonga hadi kufa kwa kutumia kamba ya katani wilayani nyamagana.

****Mtu mmoja anashikiliwa na jeshi la polisi kwa kosa la kupatikana akiwa na pombe iliyohifadhiwa kwenye vifungashio vya plastiki almaarufu viroba pakiti 103 wilayani ilemela.

Kwamba tarehe 23.04.2017 majira ya 18:45hrs jioni katika mtaa wa mkuyuni sokoni kata ya mkuyuni wilaya ya nyamagana jiji na mkoa wa mwanza, mtu mmoja mwanamume aliyrfahamika kwa jina la faraja anselem miaka 31, mkazi wa mtaa wa mkuyuni sokoni, alikutwa akiwa amejinyonga chumbani kwake hadi kufariki dunia kwa kutumia kamba ya katani aliyokua ameifunga kwenye paa la chumba, kitendo ambacho ni kosa kisheria.

Inasemekana kuwa taraehe tajwa hapo juu marehemu alibaki mwenyewe nyumbani, aidha inadaiwa kuwa kabla ya kufanya tukio hilo marehemu alionekana akiingia chumbani kwake kisha akafunga mlango ndipo baada ya muda kupita watoto waliokua wakicheza maeneo hayo waliona miguu ikining’inia dirishani ndipo walitoa taarifa kwa wazazi wao.

Majirani baada ya kuona tukio hilo walitoa taarifa polisi, ambapo askari walifanya ufuatiliaji wa haraka hadi eneo la tukio na kuukuta mwili wa marehemu ukining’inia mahali hapo, mwili wa marehemu umehifadhiwa hospitali ya rufaa ya bugando kwa ajili ya uchunguzi pindi uchunguzi ukikamilika utakabidhiwa kwa ndugu wa marehemu kwa ajili ya mazishi. Aidha upelezi kuhusiana na kifo hicho bado unaendelea.

Kamanda wa polisi mkoa wa mwanza naibu kamishina wa polisi ahmed msangi anatoa wito kwa wakazi wa jiji na mkoa wa mwanza, akiwaomba kuwa pale watakapoona mtu amekuwa na msongo wa mawazo kwa muda mrefu hadi inapelekea kuweza kufanya kitu kisicho cha kawaida cha kuweza kujidhuru yeye mwenyewe au watu wengine, wamfikishe kwa wataalamu wa ushauri nasaha ili waweze kumshauri na kumwaondoa katika hali hiyo ya msongo wa mawazo na kisha kurudi katika hali ya kawaida na kuweza kuendelea na maisha.

Katika tukio la pili,
Kwamba tarehe 23.04.2017 majira ya saa 14:33hrs katika mtaa wa kiloleli kata ya nyamanoro wilaya ya ilemela jiji na mkoa wa mwanza, askari wakiwa doria na misako walifanikiwa kumkamata mtu aliyefahamika kwa jina la donatus sebastina miaka 16, mkazi wa kiloleli akiwa na pombe iliyeowekwa kwenye vifunganishio vya plastiki almaarufu viroba aina ya empire pakiti 103, kitendo ambacho ni kosa kisheria.

Awali askari wakiwa kwenye doria na misako walipokea taarifa kutoka kwa wasiri kwamba maeneo tajwa hapo juu yupo mtu anayefanya biashara ya kuuza pombe ya viroba kwa siri, kutokana na taarifa hizo askari walifanya upelelezi wa kimyakimya huku wakiendelea na doria ndipo baada ya muda waliweza kufahamu mahali anapoishi mtuhumiwa na kufanikiwa kumkamata akaiwa na pakiti 103 za pombe iliyohifadhiwa kwenye vifungashio vya plastiki almaarufu viroba aina ya empire.

Mtuhumiwa yupo katika mahojiano na polisi, pindi uchunguzi ukikamilika atafikishwa mahakani, aidha upeleezi na misako ya kuwatafuta watu wengine wanaojihusisha na biashara hiyo ya pombe za viroba bado unaendelea.

Kamanda wa polisi mkoa wa mwanza naibu kamishina wa polisi ahmed msangi anatoa wito kwa wakazi wa jiji na mkoa wa mwanza akiwataka kuendelea kutoa taarifa mapema kwa jeshi la polisi ili watu wanaojihusisha na biashari hiyo ya pombe za viroba waweze kukamatwa na kifikishwa katika vyombo vya sheria.

Imetolewa na:
Dcp: Ahmed Msangi.
Kamanda wa Polisi (m) Mwanza

Ufafanuzi wa TFDA kuhusu Uwepo wa Sumu Katika Mafuta ya alizeti

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya April 25

Alichokisema Nape Nnauye Kuhusu CCM

$
0
0
Usiku wa kuamkia Leo  Mbunge wa Jimbo la Mtama mkoani Lindi kupitia tiketi ya CCM Nape Moses Nnauye ametumia ukurasa wake wa twitter kuandika ujumbe wake wa wazi aliyowahi kuandika kipindi cha nyuma kuhusu CCM, lengo likiwa ni kuweka kumbukumbu sawa kwa watu kuhusu CCM.

“Watu wengi wanaamini nimeisaidia sana CCM lakini ukweli ni kuwa CCM imenisaidia sana mimi kuliko mimi nilivyoisaidia, CCM ni SHULE.

“Bahati niliyopata kwa kuwa muenezi CCM ni kufanya kazi na ndg Kinana ni mwema, mzalendo, hodari, uwezo mkubwa, upendo na maarifa mengi”  Ameandika  Nape

Bunge Laibana Serikali Kuhusu Wachimbaji Waliofukiwa Machimbo ya Kitunda

$
0
0
Bunge limeiagiza serikali kufuatilia na kupeleka majibu kuhusu tukio la kufukiwa kwenye mgodi kwa wananchi wanaochimba madini katika machimbo ya Kata ya Kitunda, wilayani Sikonge, Tabora pamoja na kupata idadi kamili ya waliofukiwa.

Agizo hilo lilitolewa bungeni jana na Mwenyekiti wa Bunge, Mussa Zungu (pichani) wakati akijibu mwongozo ulioombwa na Mbunge wa Sikonge, Joseph Kakunda (CCM) aliyeomba mwongozo kwa kuwa alikuwa na jambo zito la kitaifa kutokana na kufukiwa kwa wachimbaji hao, hivyo kuiomba serikali ilifanyie kazi na kupatiwa ufumbuzi wakina.

Zungu alimpa pole mbunge huyo na wote waliofikwa na tukio hilo, huku akiiagiza serikali kulifanyia kazi kupitia wizara zinazohusika kwa kushirikiana na mbunge na wananchi wa maeneo hayo ili kupata uhakika wa idadi kamili ya waathirika.

 Pia aliwataka kuhakikisha maeneo kama hayo hayapati tena madhara makubwa, na wabunge kwa umoja wao katika maeneo yao waisaidie serikali.

Alisema wakati mwingine wabunge wamekuwa wakivunja sheria na masharti ambayo yanawekwa na serikali kuhusu mambo mbalimbali ili tu wapate kukubalika kwa wapiga kura wao. 

“Nilivyoingia bungeni tangu asubuhi nimepokea maswali na pole nyingi kutoka kwa wabunge kutokana na tukio la kufukiwa kwenye mgodi wa wananchi wa Tanzania wanaochimba kule Kitunda,” alisema Kakunda wakati wakiwasilisha mwongozo wake.

Kakunda alisema idadi kamili ya wachimbaji katika mgodi wa Kitunda haijulikani kwa sababu hakuna usajili wowote wa wanaoingia au kutoka katika mgodi huo. Alisema serikali inakadiria kwamba kuna wachimbaji kati ya 5,000 hadi 7,000. 

“Sasa mheshimiwa mwenyekiti usiku wa kuamkia Aprili 20 mwaka huu, machimbo hayo yalipata ajali na walifukiwa wananchi na mpaka jana (juzi) Aprili 23 mwaka huu ilifukuliwa miili sita.

"Mheshimiwa Mwenyekiti wananchi wanaamini, na wachimbaji wa eneo hilo wanaamini kwamba kuna wananchi zaidi bado wapo chini ya machimbo hayo, sasa mheshimiwa mwenyekiti ilitumika kijiko cha ujenzi wa barabara badala ya vifaa maalumu ambavyo huwa vinatumika kwenye migodi mikubwa kufukua ardhini kuokoa pamoja na kufukua maiti,” alisema.

Mbunge huyo, katika mwongozo wake aliomba kutoa hoja, Bunge hili lijadili hoja yake kwa kanuni kama kanuni zinavyowaongoza ili maazimio watakayofikiwa yatoe mwongozo kwa serikali na kuweka utaratibu wa usimamizi wa usajili na uratibu na msaada wa haraka wa tatizo kama hilo linapojitokeza ili kuondoa manung’uniko ya wananchi na hata wabunge yanapotokea majanga kama haya ya Kitunda kwenye migodi.

Waziri Mkuu: Tutahakikisha Wauza Madawa ya Kulevya Wote Wanakamatwa

$
0
0
Serikali imesema kuwa itahakikisha inashughulikia mtandao wa wafanyabiashara wakubwa wanaojihusisha na dawa za kulevya bila ajizi, ambapo vyombo vyote vya kisheria vimeagizwa kushirikiana kwa kusimamia sheria ipasavyo.

Hayo yalisemwa jana  Jijini Dar es salaam na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati wa ufunguzi wa kongamano linalohusu mmomonyoko wa maadili na athari za dawa za kulevya lililoandaliwa na Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) kwa kushirikiana na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya.

Alisema kuwa kila mzazi au mlezi aone aibu, uchungu na ajutie anapoona mtoto yoyote akienda kinyume na utaratibu wa kawaida wa maisha na ni vema wakatumia nafasi yao kwa kuwahimiza vijana hao waishi maisha ya nidhamu na yenye kumpendeza Mwenyezi Mungu.

“Ni ukweli usiopingika kuwa mmomonyoko wa maadili ni miongoni mwa vichocheo vinavyopelekea matumizi ya dawa haramu za kulevya,  hivyo ni matarajio yangu kuwa mtaliangalia kwa kina tatizo la mmomonyoko wa maadili ambalo kwa kiasi kikubwa linatuathiri kama Taifa katika mipango ya Serikali na maendeleo ya Taifa letu,” alisema Majaliwa.

Aidha, aliongeza kuwa Serikali ya Awamu ya Tano imedhamiria kujenga jamii yenye  kuzingatia maadili nchini na Rais, Dkt. John Magufuli amekuwa akisisitiza Watanzania wote kuzingatia maadili katika jamii kwa kufanya kazi kwa bidii na kujiepusha na vitendo vyote vya rushwa na ubadhirifu.

Naye Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini, Rogers Siang’a aliwaomba viongozi wa dini kuunga mkono Mamlaka hiyo kwa sababu inafanya kazi kubwa ambayo inahitaji msaada wa watu wote.

Kwa upande wake Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Alhaji Abubakary Zuberi alisema viongozi wa dini nchini wana jukumu la kukataza maovu na kuiamrisha jamii kufanya mambo mema badala ya kuiachia Serikali pekee kufanya kazi hiyo.

RAHCO Yabariki Ombi la Askofu Gwajima Kununua Treni ya Umeme

$
0
0
Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima amekaribishwa kuwa anaweza kuendesha huduma ya usafiri wa treni na kutaka wadau wengine wenye nia kama hiyo wajitokeze.

Katika ibada iliyofanyika juzi, Askofu Gwajima aliwaambia waumini wake kuwa amedhamiria kununua treni ya umeme itakayogharimu Sh11 bilioni, baada ya Rais John Magufuli kuzindua mradi wa ujenzi wa reli pana (standard gauge) itakayokuwa na kasi zaidi ya treni ya sasa na uwezo wa kuchukua shehena kubwa.

Ujenzi wa reli uliozinduliwa na Rais Magufuli Aprili 12, utakamilika ndani ya miezi 30 na awamu ya kwanza itaanzia Dar es Salaam hadi Morogoro, treni yake itakuwa na kasi ya kilomita 160 kwa saa, ikibeba mabehewa 100.

Msemaji wa Kampuni Hodhi ya Rasilimali za Reli (Rahco), Catherine  Moshi alisema kampuni hiyo  imebariki uamuzi huo wa kuwekeza katika usafiri wa reli, lakini askofu huyo anatakiwa kuomba kibali  Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

“Tunamkaribisha mchungaji, hii ni biashara kwetu na huyu ni mwekezaji tena wa ndani. Hatuwezi kumuangusha cha muhimu ni kufuata utaratibu tu,’’ alisema Catherine.

Polepole Aitaka CCM Imchukulie Hatua za Kinidhamu Nape Nnauye

$
0
0
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole amelaani vikali kauli iliyotolewa na mtangulizi wake ambaye ni mbunge wa jimbo la Mtama, Nape Nnauye kuwa alisaidia kukitoa chama hicho shimoni.

Nape alitoa kauli hiyo dakika chache baada ya mkutano wake na waandishi wa habari kuzuiwa na kutishiwa bastola na mtu mmoja, siku moja baada ya kuondolewa kwenye nafasi ya Uwaziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.

Polepole alisema kuwa kauli hiyo ya Nape sio kauli sahihi ya kiongozi na kwamba yeye pekee hawezi kukitoa chama shimoni huku kukiwa na wanachama milioni nane na maelfu ya viongozi.

“Mwanachama anayejitambua hawezi kusema anakibeba chama, wanachama wote milioni nane walikuwa wapi? Viongozi wote maelfu walikuwa wapi? Nape ni kiongozi wetu kwenye chama, kama kweli alisema maneno hayo alikengeuka sana,” Polepole anakaririwa na Mwananchi.

Katibu huyo wa Itikadi na Uenezi wa CCM alisema kuwa Kamati ya Maadili inapaswa kuliangalia suala hili na kumchukulia hatua Nape.

“Tuna kila sababu za kumshauri Mzee Mangula wa Kamati ya maadili kuwa hatuwezi kuwa na viongozi wa aina hii. Chama chenye watu milioni nane unakitoa shimoni na nini? Unakitoa na ngazi, ulitumia kamba kukitupia shimoni, uliita zimamoto? "Alihoji.

Hata hivyo, Polepole alisema kuwa hatua zinazopaswa kuchukuliwa kwa viongozi kama Nape sio za kuwawekea ukomo bali kuwalea kimaadili kwa kutumia hekima na busara ili watambue kuwa chama sio punda anayeweza kutumbukia shimoni. 

Hivyo, alisema CCM iko kwenye mpango wa kuanzisha chuo kikuu kitakachotoa mafunzo kwa makada wake kuhusu nidhamu na maadili.

Live: Yanayojiri Bungeni Dodoma leo Aprili 25, 2017

$
0
0
Tazama hapa moja kwa moja kutoka Bungeni Dodoma kipindi cha Maswali na Majibu katika Bunge la 11, Mkutano wa Saba leo Aprili 25, 2017.

Bofya hapo  chini Kutazama.

Jeshi la Polisi Lasema Linawashikilia Watu 3 Kwa Kuvamia Mkutano wa CUF na Kuwapiga Watu

$
0
0
Saa  tatu baada ya viongozi wa CUF kukutana na Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Simon Sirro, kuhoji sababu za kutokamatwa watu waliofanya vurugu kwenye mkutano wa waandishi wa habari na viongozi wa chama hicho wa wilaya ya Kinondoni, Jeshi la Polisi limetangaza kushikilia watu watatu.

Wakiongozwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya Chama hicho Julius Mtatiro, viongozi hao waliwaeleza wanahabari kuwa ni ajabu kuona  Polisi haijachukua hatua huku ikijulikana wazi kuwa watu hao walijeruhi wanahabari na viongozi wa chama hicho katika tukio ambalo liliripotiwa na vyombo vya habari.

Viongozi hao walikutana na Sirro jana saa 5 asubuhi na kuzungumza kwa takribani saa moja, na kisha saa 8 mchana Kamanda huyo alizungumza na waandishi wa habari na kueleza kukamatwa kwa watu hao, wakituhumiwa kuhusika katika tukio hilo.

Jumamosi iliyopita takribani watu watano wakiwa kwenye gari lenye nembo na bendera za CUF, walivamia mkutano huo uliokuwa ukifanyika kwenye hoteli ya Vinna, Mabibo wilayani Kinondoni na kufanya vurugu.

Miongoni mwa watu hao, mmoja aliyekuwa amejifunika uso kininja alichomoa bastola na kutishia huku mwingine akishindwa kuondoka baada ya kuachwa na wenzake, jambo lililosababisha wananchi wamzingire na kumshushia kipigo.

Katika ufafanuzi wake, Mtatiro alisema tukio hilo ni la 13 dhidi ya upande unaomwunga mkono Katibu Mkuu wa Chama hicho, Maalim Seif Sharif Hamad lakini vyombo vya Dola viko kimya.

“Baada ya tukio la juzi (Jumamosi) tulikaa kimya ili kuona kama polisi watasema chochote ila imekuwa tofauti. Wako kimya tu,” alisema Mtatiro.

Akieleza kilichowapeleka kituoni hapo, alisema: “Tulitaka kujua yule mvamizi aliyekuwa na bastola mpaka sasa yuko wapi. Mvamizi mmoja tunajua alikamatwa na wananchi, akapigwa kidogo na kuokolewa. Tulitaka kujua alitoa maelezo gani.”

Alisema baada ya tukio hilo, Mkuu wa Upelelezi aliwapigia simu viongozi waliovamiwa akiomba waende kituo cha Polisi Magomeni  wakapatanishwe.

“Tulishangazwa na taarifa hiyo, kwa watu waliovamiwa kwenda kupatanishwa. Tulijihoji kama Jeshi la Polisi linaweza kupatanisha watu wenye makosa ya jinai, kwani mtu wa makosa hayo upelelezi unapokamilika hupelekwa mahakamani,” alisema Mtatiro.

Alisema sababu nyingine ya kwenda kituoni hapo ni kutaka kufahamu kama watu wanaofanya matukio hayo wako juu ya sheria.

“Tulimwonya Kamanda Sirro kwamba sisi (upande wa Maalim) tuna nguvu kuliko Lipumba na kuiomba Polisi kutekeleza majukumu yake kwa kuchukua hatua dhidi ya wavamizi hao,” alisema.

Katika mkutano wake na wanahabari, Sirro alisema Polisi inashikilia watu watatu wakituhumiwa kufanya vurugu kwenye mkutano huo.

“Tulipata taarifa ya kuvamiwa kwa mkutano wa wanachama wa CUF na watu wasiofahamika wakiwa na silaha. Baada ya taarifa hizo kupokewa askari walifuatilia na kukamata watu watatu,” alisema Sirro.

Alisema watuhumiwa hao wanaendelea kuhojiwa na upelelezi ukikamilika hatua za kisheria zitafuatwa.

Alisema hakuna mtu aliye juu ya sheria na kusisitiza kuwa waliohusika watasakwa kokote watakokuwa.

Taarifa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Nchi kuhusu Serikali kumuondoa nchini, Mkurugenzi wa UNDP, Bi. Awa Dabo.

$
0
0
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Serikali yamuondoa Mkurugenzi wa UNDP nchini 
 
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeliagiza Shirika la Umoja wa Mataifa la Programu ya Maendeleo (United Nations Development Programs – UNDP) kwa upande wa Tanzania kumuondoa nchini Mkurugenzi wa Shirika hilo Bi Awa Dabo.
 
Serikali ilifikia uamuzi huo kutokana na  Bi Dabo kutokuwa na maelewano mazuri na baadhi ya Watumishi wenzake na Menejimenti ya Shirika hilo, hivyo kupelekea kuzoretesha utendaji wa shirika hilo nchini na kupunguza kasi ya kuleta maendeleo kwa Watanzania endapo hatua za haraka zisingechukuliwa.
 
Baada ya kuthibitishiwa kuondoka nchini, Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nje imetoa rai kwa UNDP kuwakumbusha Watumishi wake kuwa kipaumbele chao ni kufanya kazi na Serikali ili kufikia malengo yaliyoainishwa kwenye Dira ya Maendeleo ya Mwaka 2025, Mpango wa Maendeleo wa Miaka mitano na Malengo ya Maendeleo Endelevu ambayo yamefafanuliwa katika Agenda ya Mwaka 2030. 

Mwisho.
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasili ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dodoma, 25 Aprili 2017.

Mtatiro: CUF haina walinzi wa chama wenye bastola

$
0
0
Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi, The Civic United Front (CUF) Julius Mtatiro amefunguka na kusema chama cha CUF hakina walinzi wa chama wenye bastola wala hakina walinzi wanaozunguka mitaani kufanya doria.

Julius Mtatiro ametoa ufafanuzi huo leo baada ya Mkurugenzi wa Habari CUF Taifa, ambaye anamuunga mkono Profes Ibrahim Lipumba  ndugu Abdul Kambaya kukiri kuwa ni kweli wao walituma vijana kwenda kwenye Kata ya Mabibo kufanya doria.

"Siku ambapo kikao kinafanyika Vinna Hotel, vijana wetu pia walikuwa kwenye doria, tulipozungumza na vyombo vya habari tulikiri na tunaendelea kukiri hatuna sababu ya kukataa kwamba tulituma vijana wetu na walikwenda kwenye doria" alisema Kambaya

Kufuatia taarifa hiyo ya Kambaya Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi, The Civic United Front (CUF) Julius Mtatiro amefunguka na kusema wao kama CUF hawana walinzi wa chama wenye bastola hivyo amelitaka jeshi la polisi limtumie huyu Kambaya kueleza kijana aliyekuwa na bastola yuko wapi na walikodishwa kutoka wapi.

"Leo amekiri kuwa lile Zombi lililopigwa na wananchi, Mabibo, eti lilitumwa na genge la Mungiki/Lipumba ili kufanya doria kwenye kata ya Mabibo. Yani eti Lipumba ana jeshi lake linalofanya doria na kupiga watu mitaani. Sasa Polisi wasitafute mchawi, huyu Abdul Kambaya aeleze lile zombi lililokuwa na bastola liko wapi na waliikodisha kutoka wapi? Alihoji Mtatiro

Mbali na hilo Mtatiro alizidi kusisitiza kuwa wao hawana walinzi wa chama

"Halafu, eti huyo msemaji wa Lipumba anasema "Zombi" hilo lililokamatwa ni "mlinzi wa chama". Napenda ifahamike kuwa CUF haina walinzi wa chama wenye bastola, na pia hakuna chama cha siasa chenye walinzi wanaozunguka mitaani kufanya doria, wameajiriwa na serikali ipi? Alihoji Mtatiro
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images