Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Sakata la Richmond Laibuka Tena Bungeni.......Mwakyembe Amtuhumu Joshua Nassari Kuingia na Chupa ya Konyagi Bungeni

$
0
0
Iikiwa imepita miaka tisa tangu alipojiuzulu aliyekuwa Waziri Mkuu wa kwanza wa Serikali ya Awamu ya Nne, Edward Lowasa, mzimu wake umeendelea kumtesa Dk. Harrison Mwakyembe, aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati Teule ya Bunge kuhusu suala la Richmond.

Hatua hiyo inatokana kuibuka   kwa suala la Richmond bungeni juzi, hali iliyosababisha kutupiana vijembe kati yake na Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari (Chadema).

Juzi, Dk. Mwakyembe ambaye sasa ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, akijibu matamshi ya Nassari,  alidai   mbunge huyo aliingia bungeni   akiwa amelewa.

Alidai  mkakati uliopo wa Chadema kumsafisha Lowassa   hautafanikiwa.

Jana, akizungumza bungeni wakati wa kutihimisha mjadala wa hotuba ya makadirio ya matumizi ya fedha  ya Ofisi ya Rais Tamisemi pamoja na ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dk. Mwakyembe, alijibu tena ‘makombora’ yaliyorushwa kwake na Nassari  juzi.

“Suala la Richmond limeibuliwa jana (juzi) na Mbunge wa Arumeru Mashariki, Mheshimiwa Nassari kwamba Kamati Teule iliyochunguza suala hilo, haikumtendea haki Mheshimiwa Edward Lowassa kwa sababu haikumuhoji.

“Mimi naelewa ni kazi mgumu sana leo (jana) hii kutaka kumsafisha Mheshimiwa Edward Lowassa na kesi ya Richmond ilikwisha na ndiyo maana sioni ajabu kusema aliyoyasema ilibidi Nassari anywe pombe kwanza.

Na nayasema haya kiongozi wa upinzani bungeni ajue kwamba tuna tatizo hilo na mimi nawapongeza sana vijana wetu wa usalama waliokamata hiyo chupa na angeruhusiwa na hiyo chupa huenda angeweza akatapikia hata rangi zetu za Taifa humu ndani ingekuwa ni scandal (kashfa) kubwa.

“Mheshimiwa mimi nimelezea mara nyingi sana katika Bunge hili, hata Bunge la tisa lililoshughulikia suala la Richmond kuwa Kamati Teule iliyoundwa na Bunge hili kazi yake ilikuwa kuchunguza siyo kutoa uamuzi,” alisema Dk. Mwakyembe.

Msomi huyo na mwalimu wa sheria, alisema wakati wa kufanya uchunguzi  suala la kusikiliza upande mwingine halipo, upo wakati wa uamuzi na ndiyo maana kamati yake iliwasilisha ripoti bungeni ikiwa na mashahidi 40 nje ya   Bunge.

“Aliyetakiwa kuhojiwa hapa akajiuzulu, unamlaumu Mwakyembe kwa hilo?  Naomba msipotoshe umma kuwa hakuhojiwa, ahojiwe vipi?

“Unajua ni aibu, ni sawa na mtu anaenda mahakamani anasema unajua polisi hawakunipa haki ya kuhojiwa….polisi?  Uko mahakamani ndiyo pa kukuhojiwa hapo,” alisema.

Alisema kamati yake ilikuwa na nyaraka za Serikali 104 na iliwahoji watu 75 ambao waliulizwa maswali 2,717.

Dk. Mwakyembe alisema, kwa sababu hiyo kamati yake haikuona sababu yoyote ya kumuhoji Lowassa kwa sababu ilikuwa na kila kitu.

“Mimi niombe Mheshimiwa mwenyekiti, kama kuna mtu yeyote hapa  bado anakereketwa na kesi ya Richmond, aache maneno maneno hapa, leta hiyo kesi hapa kama hatujawanyoa nywele kwa kipande cha chupa.

“Ileta hapa, acha maneno ya kienyeji hapa, tumeshachoka, jamani hee…ileteni hiyo kesi hapa, mnaruhusiwa na kanuni.

“Naomba nimalizie kwamba, mimi naahidi, siku ambayo kuna mmoja atakuwa jasiri wa kusema analeta suala la Richmond hapa, mimi naahidi nitamuomba Mheshimiwa Rais anipumzishe uwaziri niweze kuishughulikia hiyo kesi kwa ukamilifu iishe moja kwa moja.

“Mheshimiwa Mwenyekiti kuna hoja nyingine ambayo aliieleza kwenye andiko langu la Shahada ya Uzamivu  niliandika kuhusu Serikali tatu lakini   hivi sasa nasema kuhusu Serikali mbili,” alisema Dk. Mwakyembe.

Akizungumza matamshi ya Nassari juzi kuwa hiyo inaonyesha jinsi Waziri huyo alivyo kigeugeukwa  kuandika kuwa ili Tanzania iende mbele inahitaji serikali tatu, lakini akageuka wakati wa Bunge Maalumu la Katiba na kuunga mkono serikali mbili, Mwakyembe alisema: “Alilewa (Nassari), ndiyo maana alikuwa anasema tu, alikuwa ameambiwa, hajasoma hata hilo andiko,” na kuongeza:

“Na hapa ndiyo unaelewa watu wasio na integrity, unawajua hapa. Ambao wanakesha miaka mitano kumtukana mtu kwa kumwita fisadi, leo wanamkumbatia wanalamba na nyayo zake, ndiyo vigeugeu namba moja hao”. 

Hata hivyo, kabla hajamaliza kuzungumza  alisimama Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea (Chadema) na kuomba mwongozo na utaratibu kwa mujibu wa Kanuni ya 64(1).

Alisema: “Kwa mujibu wa Hansard za Bunge, Dk. Mwakyembe alisema Mheshimiwa Edward Lowassa alijiuzulu kwa mambo yaliyofanywa na walio chini yake, leo (jana) Dk. Mwakyembe anasema ana ushahidi wa asilimia 100 kwamba Lowassa alihusika 100 kwa 100 na jambo hilo.

“Naomba kwa idhini yako unipe muda niwasilishe Hansard hapa kwenye Bunge hili kuthibitisha maneno ya Dk. Mwakyembe ya Februari mwaka 2008”. 

Kubenea alisema  jambo la pili ni kuhusu tuhuma za Dk. Mwakyembe kwamba juzi Nassari   alikuwa na chupa ya  Konyagi na aliingia nayo bungeni.

“Siyo kweli, nina uwezo wa kulithibitishia Bunge hili kwamba Nassari jana hakuwa amelewa.  Tulikuwa naye mchana kutwa na alikuwa amekuja bungeni na soda ambayo ilikuwa imewekwa kwenye chupa,” alisema.

Baada ya maelezo hayo, Mwenyekiti wa Bunge, Andrew Chenge, alisema kwa taarifa alizo nazo, chupa anayodaiwa kuwa nayo Nassari  ilikuwa ni nje ya Bunge wala siyo ndani ya Bunge kama inavyodaiwa.

Nje ya Ukumbi wa Bunge, Nassari alisema alijibu tuhuma hizo za Dk. Mwakyembe  kwa sababu  kitendo cha Serikali kuhangaika naye tangu juzi ni kwamba amewagusa sehemu nyeti na Waziri huyo (Dk. Mwakyembe)  si mtu wa kuaminika.

Swali la Mama Salma Kikwete kwa Waziri Mkuu Kuhusu Ufisadi wa Bilioni 30 za Korosho

$
0
0
Mbunge wa Kuteuliwa, Salma Kikwete (CCM), ameeleza kushangazwa kwa kitendo cha Serikali kukaa kimya juu ya ubadhirifu wa Sh bilioni 30 Bodi ya Korosho.

Mke huyo wa Rais Mstaafu, Jakaya Kikwete, alitoa kauli hiyo bungeni jana wakati akiuliza swali la papo kwa hapo kwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

“Umekuwapo ushahidi wa kutosha kabisa kuhusiana na wizi unaofanyika kwenye biashara ya korosho, hasa katika mikoa ya Mtwara na Lindi, ukiachilia mbali kazi iliyofanywa na Takukuru iliyobainisha kwamba kumekuwa na upotevu wa kiasi kikubwa cha fedha shilingi bilioni 30 kutoka Bodi ya Korosho.

“Serikali hatujasikia, mimi binafsi na wengine hawajasikia juu ya jambo hili. Je, Serikali leo inatuambia nini kuhusu ubadhirifu huu uliotokea hapa nchini kwetu, hasa wananchi wa Mtwara na Lindi kwa sababu jambo hili linaweza kutokea sehemu yoyote nchini mwetu,” alihoji.

Akijibu swali hilo, Majaliwa alisema mienendo ya vyama vya ushirika nchini imeonyesha si mizuri kwa kuonyesha upotevu wa fedha na inawakatisha tamaa wakulima.

“Mienendo ya vyama vyetu vya ushirika nchini vimeonesha si mizuri kwa kuonesha upotevu wa fedha na unakatisha tamaa wakulima wetu na Serikali inafanya mapitio ya vyama vyote na tumeanza na vyama vya ushirika wa kilimo.

“Tulikuwa na kikao Bagamoyo kwa ajili ya ubadhirifu huo wa bilioni 30 na Serikali iliunda timu maalumu na ikagundua kuwa ni hasara ya Sh bil 6 si bilioni 30 na haikusababishwa na bodi bali vyama vikuu na vyama vya ushirika vilivyopo kata na wilaya, vyama vya msingi na vyama vikuu na vyote vilifanyiwa uchunguzi na hatua zimeanza kuchukuliwa,” alisema.

Pamoja na majibu hayo ya Waziri Mkuu, Salma aliuliza swali la nyongeza akisema haijalishi ni kiasi gani cha fedha kimechukuliwa, lakini watalipwa lini.

“Haijalishi ni kiasi gani cha fedha kimechukuliwa, hizi bilioni sita na hizi ni haki za wananchi je, wananchi wanazipataje fedha hizo?” alihoji mbunge huyo.

VIDEO: Msikilize Mwakyembe Akiongelea Sakata la Richmond, huku Akimtuhumu Nassari Kuingia na Konyagi Bungeni

$
0
0
Jana Waziri wa Habari, utamaduni, sanaa na michezo Dr. Harrison Mwakyembe alimtuhumu Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nassari kwa  kuingia bungeni akiwa amekunywa pombe  aina ya konyagi, huku akijibu tuhusa za sakata la Richmond

==>Msikilize hapo chini

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya April 22

Rais Magufuli afanya uteuzi wa Kamishna wa Madini na Mwenyekiti wa Bodi ya PURA

Mtuhumiwa wa Richmond Aachiwa Huru

$
0
0
Aliyekuwa  Wakala wa Kampuni inayodaiwa kuwa ni kampuni hewa ya kufua umeme wa dharura, Richmond Development LLC, Naeem Gire ameachiwa huru baada ya upande wa mashtaka kushindwa kuthibitisha mashtaka dhidi yake.

Akitoa uamuzi huo jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Hakimu Mfawidhi, Cyprian Mkeha alisema upande wa mashitaka umeshindwa kuthibitisha mashitaka mawili ya kughushi na kuwasilisha nyaraka za uongo.

Uamuzi huo ni wa pili kutolewa na mahakama hiyo dhidi ya mashitaka yaliyokuwa yakimkabili Gire. Awali, aliachiwa huru baada ya kuonekana hana kesi ya kujibu, ambapo Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) hakuridhika na uamuzi huo na kukata rufaa Mahakama Kuu.

Katika uamuzi wake, Mahakama Kuu ilisema haikuwa sahihi kumwachia, kabla hajajitetea katika mashitaka ya kwanza na ya pili, ambayo ni kughushi na kuwasilisha nyaraka za uongo. Hivyo, kesi hiyo ilirejeshwa Mahakama ya Kisutu, na Gire akapanda tena kizimbani akajitetea na Hakimu Mkeha ametoa uamuzi huo.

Katika kesi hiyo hiyo, Julai 28, 2011 Gire aliachiwa huru katika mahakama hiyo na Hakimu Mkazi, Waliarwande Lema kuwa hana kesi ya kujibu, lakini Mahakama Kuu ilimtaka apande kizimbani tena kwa ajili ya kujitetea.

Katika uamuzi wake wa kumwachia huru Gire, Hakimu Lema alisema kuwa ameridhika na hoja za utetezi kuwa mshtakiwa huyo hana kesi ya kujibu, kwa kuwa upande wa mashtaka umeshindwa kutengeneza kesi dhidhi ya mshtakiwa kwa mashtaka yaliyokuwa yakimkabili, kiasi cha kumlazimu ajitetee.

Hakimu Lema alisema baada ya kuupitia ushahidi uliotolewa mahakamani na mashahidi wa upande wa mashtaka , hoja za pande zote na vifungu vya sharia, aliridhika kuwa ushahidi huo hauna vigezo vya kuonesha kuwa mshitakiwa huyo ana kesi ya kujibu.

Uamuzi wa Mahakama Kuu ulitolewa na Jaji Lawrence Kaduri katika rufaa ya DPP aliyekuwa akipinga uamuzi wa Mahakama ya Kisutu, kumwachia huru kuwa hana kesi ya kujibu.

Jaji Kaduri alisema kuwa baada ya kupitia ushahidi wa upande wa mashtaka, ameridhika kuwa mshtakiwa huyo alikuwa na kesi ya kujibu na kwamba ushahidi huo unamlazimisha apande kizimbani kujitetea. 

Hata hivyo, aliamuru mshtakiwa huyo arudi kizimbani katika Mahakama ya Kisutu ili aanze kujitetea na kwamba kesi hiyo isikilizwe na hakimu mwingine.

Serikali Yatangaza Ajira Mpya 52,436

$
0
0
Serikali  inakusudia kuajiri watumishi wapya wa umma 52,436 katika mwaka ujao wa fedha. 

Aidha, madaktari wapya 258 waliokuwa waende kufanya kazi nchini Kenya, lakini wakakwama kutokana na kuwekewa pingamizi la kimahakama na wenzao wao huko na hivyo Rais, Dk John Magufuli kuamuru waajiriwe mara moja nchini, wanatarajiwa kuanza kazi keshokutwa Jumatatu.

Hayo yalisemwa bungeni juzi usiku na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais anayeshughulikia Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angellah Kairuki alipokuwa anatoa ufafanuzi wa lini Serikali itaendelea kuajiri watumishi wa kada nyingine, kama ilivyoulizwa na Mbunge wa Viti Maalumu, Anna Lupembe (CCM).

“Azma ya serikali, kwanza kabisa hatuwezi kuajiri wananchi wote, tumekuwa tukisikia hapa wahitimu hawana ajira, wengine wanaendesha bodaboda… tunapopanga idadi ya watumishi wa kuajiriwa, tunaangalia mambo mengi, kuanzia mahitaji, vipaumbele hadi uwezo wa kibajeti.

“Tayari tumeshaanza kutoa vibali vya ajira zaidi ya watu 9,700 na tutaendelea kufanya hivyo, na hivi karibuni Rais amebariki kuajiriwa kwa madaktari wapya 258 na Jumatatu (keshokutwa) wanaripoti kazini.

"Tutaendelea kuajiri na wataalamu wa kada nyingine, kabla ya kumalizika kwa mwaka huu wa fedha mwezi Juni tutakuwa tumejiajiri kwa idadi tutakayoipanga kwa awamu, na katika mwaka ujao wa fedha tutaendelea kuajiri watumishi wengine wa umma zaidi ya 52,436,” alisema.

Hata hivyo, alisisitiza Serikali itahakikisha hairudii makosa ya kuajiri watumishi hewa, wasio na sifa na weledi unaohitajika. 

Alisema kwa kiasi kikubwa uhakiki wa watumishi wa umma kwa ujumla umekwisha, lakini kazi hiyo ni endelevu, kwani serikali itaendelea kufanya hivyo mara kwa mara.

Alisema matunda ya uhakiki wa watumishi wa umma umebaini watumishi hewa 19,708 na ambao wameshaondolewa katika orodha ya mishahara ya watumishi wa umma. 

“Hawa wangeachwa, Serikali ingekuwa inapoteza kiasi cha Sh bilioni 19.8 kila mwezi, lakini fedha hizi zimeokolewa kupitia uhakiki wa watumishi wa umma.

"Tunafanya haya kwa nia njema. Mathalani tusingewatoa hawa, si wangeziba nafasi za ajira za wengine na fedha ngapi zingepotea?” alihoji. 

Alisisitiza kuwa, wizara hiyo itaendelea kutimiza majukumu yake kwa vitendo ili kurejesha nidhamu ya serikali na utumishi wa umma kwa kuongeza uwazi na kusimamia sheria, kanuni na taratibu za uwajibikaji wa viongozi wa watumishi wa umma ili wawajibike kwa wananchi ambao ndio wateja na waajiri wakuu wa watumishi wa umma.

Naye Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), George Simbachawene, akijibu hoja za wabunge, hasa la uhamisho wa watumishi wakiwemo wanandoa wanaotenganishwa, alikemea tabia ya maofisa watumishi kuzuia wenye ndoa kuhama kutoka kituo kimoja cha kazi kwa lengo la kuwafuata wenzao.

Alisema kuwazuia ni kuwanyima haki ya msingi, na kuwaagiza wabunge katika maeneo yao wasaidia kusimamia haki za watumishi. 

"Lazima sheria za utumishi zizingatiwe, walimu hawa au watumishi wanayo haki ya kutoka sehemu moja kwenda nyingine, lakini pia kuishi na wenza wao, lakini utadhani mtumishi anapoomba ni kama anasaidiwa, hapana ni haki yake ya msingi, waheshimiwa tusimamie haki za watumishi,” alisema Simbachawene

Waziri Mkuu Majaliwa apokea taarifa ya mgogoro wa Loliondo

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amepokea Taarifa ya Kamati Shirikishi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo ya kushughulikia mgogoro wa matumizi ya ardhi kwenye pori tengefu la Loliondo mkoani Arusha, ambapo atatoa maelekezo baada ya kuisoma.

Alipokea taarifa hiyo juzi katika kikao alichokiitisha kwenye ukumbi wa Spika, Bungeni mjini Dodoma. Waziri Mkuu aliiunda kamati hiyo, Desemba mwaka jana mara baada ya kumaliza ziara ya kikazi mkoani Arusha.

Kiini cha mgogoro huo ni eneo la pori tengefu la Loliondo ambalo linagombewa na wawekezaji, wakulima, wawindaji kwa sababu ni mapitio ya wanyama, chanzo cha maji, mazalia ya wanyama, malisho ya mifugo na makazi.

Kikao hicho kilihudhuriwa na Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Tate William Ole-Nasha, viongozi wa mkoa wa Arusha na wataalamu kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii. Wengine ni Mkuu wa wilaya ya Ngorongoro Rashid Taka, Kamati za Ulinzi na Usalama za Mkoa wa Arusha na wilaya ya Ngorongoro, wawakilishi wa wananchi, wawekezaji na asasi za kiraia ambao wote walishiriki katika uandaaji wa taarifa hiyo.

Waziri Mkuu alisema lengo la kamati hiyo ni kutaka kupata muafaka wa matumizi ya rasilimali zilizoko katika eneo hilo ili kila upande uweze kutekeleza majukumu yake bila ya kuathiri mwingine na kuwezesha wananchi wote kunufaika na rasilimali zilizoko katika eneo hilo.

“Serikali inataka watu wote tuwe kitu kimoja katika kutunza maeneo yetu, lakini pia shughuli za wananchi nazo ziweze kuendelea ili Watanzania wote tuweze kunufaika na rasilimali zilizoko kwenye maeneo yetu,” alisema.

Atembezwa Nusu UCHI Na Kisha Kulazimishwa Kula Kinyesi kwa Kosa la Kumtukana Mama Yake

$
0
0
Wanawake wa kijiji cha Kisungamile kilichopo katika Kata ya Matai wilayani Kalambo katika mkoa wa Rukwa wamemwadhibu Vitus Nyami (26) kwa kumtembeza nusu uchi na kulazimisha kula kinyesi cha ng’ombe kwa kosa la kumtukana mama yake mzazi matusi ya nguoni.

Aidha wanawake hao walitumia mfuko wa ‘salphate’ kufunika sehemu za siri za kijana huyo kisha wakaanza kumtembeza mitaani kijijini  humo huku wakiimba nyimbo za kabila la Kifipa wakilaani tabia ya kijana huyo ya kumtukana mama yake mzazi matusi ya nguoni kila kukicha .

Walidai kukasirishwa na tabia ya kijana huyo wa kiume kumtukana mzazi wake wa kike matusi ya nguoni, hivyo walilazimika kumfunga kamba na kumtembeza mitaani kijijini humo akiwa nusu uchi.

Mwenyekiti wa kijiji cha Kisungamile, Didas Musa alikiri kutokea kwa mkasa huo juzi ambapo mtuhumiwa huyo alitembezwa mitaani kwa saa sita kuanzia saa 1:00 asubuhi hadi saa 6:00 mchana.

Akifafanua alisema kuwa licha ya adhabu hiyo ya kutembezwa nusu uchi mitaani na kucharazwa viboko 15, pia ameamriwa kulipa mbuzi mmoja, unga wa sembe debe moja na mafuta ya kupikia lita moja.

“Adhabu hii kwa kijana hutolewa na akina mama ambapo mimi kama kiongozi kazi yangu ni kuibariki tu,” alisisitiza . Mkazi wa kijiji hicho, Obedi Mwanakatwe alisema kijana huyo amekuwa akimtukana mama yake mara kwa mara , tabia ambayo imekuwa ikiwachukiza akinamama kijijini humo ambapo waliandamana na kumkamata kijana huyo .

“Baada ya akinamama hao wenye hasiri kumkamata kijana huyo walimpeleka kwenye shimo lililojaa kinyesi cha ng’ombe kisha wakampaka kinyesi hicho mwili mzima wakiwa wamechanganya na unga wakisaidiwa na wanaume, walimtembeza uchi kijana huyo mitaani kijijini humo,” alieleza.

Stela Tenganamba alisema baada ya kumtembeza kwa muda mrefu waliamua kumlisha kinyesi cha ng’ombe na kumpaka mwili mzima sambamba na kumroweka kwenye matope.

Adhabu hiyo iliwekwa enzi za mababu zao , ambapo mtu yeyote anayetukana matusi hadharani huchukuliwa hatua hiyo sambamba na kulipishwa ng’ombe mmoja, mbuzi, unga debe moja na mafuta ya kupikia lita moja.

Akifafanua alisema kuwa baada ya kutembezwa mitaani akiwa uchi hupelekwa kwa Mwenyekiti wa Kijiji ambaye hutoa adhabu kulingana na akinamama watavyoona inafaa

Mfanyabiashara Auawa kwa Risasi Singida

$
0
0
Mauaji ya kutumia silaha za moto yameendelea kushamiri nchini,baada ya mfanyabiashara mmoja mjini Singida kufariki dunia baada ya kupigwa risasi ya bunduki aina ya bastola wakati akitaka kuondoka dukani kurejea nyumbani.

Mfanyabiashara huyo na mkazi wa Itungukia tarafa ya Mungumaji manispaa Singida ni Simon Charles (49).

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Kamanda wa jeshai la polisi mkoa wa Singida,ACP Debora Magiligimba, alisema tukio hilo la kusikitisha limetokea Aprili, 20 mwaka huu saa 3.30 usiku.

Alisema siku ya tukio baada ya mfanyabiashara huyo kufunga duka lake la madawa ya binadamu lililopo standi ya zamani ya mabasi alianza kuelekea kwenye gari lake ili aweze kurejea nyumbani kwake.

“Wakati akikaribia gari lake ghafla muuaji huyo ambaye alijificha upande mwingine wa gari hilo alinyanyuka na kumpiga risasi titi la upande wa kulia na kutokea nyuma na kisha kudondoka pale pale. Wasamaria wema waliweza kumkimbiza hospitali ya mkoa lakini alifariki akipatiwa matibabu.Kifo chake kinatokana na kuvuja damu nyingi,” alisema Magiligimba. 

Kamanda huyo alisema kwenye eneo la tukio kulipatikana ganda moja la risasi ya bastola. Hadi sasa chanzo cha mauaji hayo, bado hakijajulikana.

Katika hatua nyingine, Magiligimba alisema kuwa Jeshi la Polisi linaendelea na msako mkali kubaini watu waliojihusisha na tukio hilo ili waweze kukamatwa na sheria ziweze kuchukua mkondo wake.

“Jeshi la polisi linatoa wito kwa wananchi wote mkoani kutoa ushirikiano kwa jeshi hilo ili kusaidia kukamatwa kwa wauaji hao. Pia wafanyabiashara tunawakumbusha umuhimu wa kuajiri walinzi, watakaowalinda wao na mali zao,” alisisitiza.

Habari kutoka eneo la tukio, zinaeleza kwamba mfanyabiashara huyo ambaye kitaaluma ni daktari wa binadamu ameauwa na mtu mmoja ambaye alivalia suruali. Baada ya mauaji hayo, mtu huyo aliondoka kwa miguu na kutokomea kusiko julikana.

Mashuhuda wengine wanadai kuwa muuaji huyo hakuweza kukamatwa wala kufukuzwa, kwa madai kuwa mlio wa risasi ya bastola haukuwa mkubwa hivyo wakahisi kuwa ni tairi la pikipiki limepasuka na hivyo walipuuzia.

Chanzo: Modewji

Mkutano wa CUF ya Maalim Seif Wavamiwa na Watu wenye Silaha......Wananchi Wafanikiwa Kumnasa mmoja

$
0
0
Watu wasiofahamika wamevamia mkutano wa wanachama wa CUF upande unaomuunga mkono, Katibu Mkuu wa Chama hicho, Maalim Seif Sharif Hamad.

Mkutano huo uliokuwa ukifanyika katika Hoteli ya Vina, Mabibo, ulipangwa kuanza leo saa tano asubuhi lakini kabla haujaanza watu waliovalia soksi nyeusi usoni(mask) walivamia na kuanza kuwapiga wanachama wa CUF na waandishi waliokuwa kwenye mkutano huo.

Mtu mmoja miongoni mwa waliovamia mkutano wa wanachama wa CUF ameshambuliwa na wananchi wakati akijaribu kutoroka.

Mtu huyo, ambaye hajafahamika alikuwa akitoroka pamoja na wenzake katika eneo hilo la Vina Hotel Mabibo mara baada ya kutekeleza uvamizi huo katika mkutano wa wanachama wa CUF.

Watu hao waliovamia mkutano huo, walikuwa na bastola.

SORRY MADAM -Sehemu ya 53 & 54 (Destination of my enemies)

$
0
0
 MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWAILIPOISHIA

ILIPOISHIA
Shamsa akajikuta akistuka baada ya kumuona Phidaya akimfwata katika sehemu alipo shikiliwa na polisi.
“Hawa ndio majambazi eheee?”
Phidaya alizungumza kwa sauti ya ukali, askari mmoja akamuitikia, Phidaya bila hata kujiuliza mara mbili, akamzaba kofi Shamsa, aliye kuwa akimshangaa, pasipo kuamini kwamba huyo ni Phidaya au laa, kwa maana wamefanana kila kitu. Ilibidi baadhi ya askari wamzuie Phidaya asiendelea kuwashambulia majambazi hao walio ivamia hospitali yake.

ENDELEA
   Shamsa na majambazi wengine watatu wakaingizwa ndani ya gari tatu tofauti za polisi, tukio hilo Sa Yoo aliweza kulishuhudia ila hakujau ni kitu gani kimetokea hadi Shamsa kukamatwa na askari, isitoshe akiwa katika mavazi ya unesi, wakati si mavazi ambayo alikuwa nayo.

Gari za polisi zilizo beba wahalifu zikaondoka Sa Yoo naye akaingia kwenye gari lake na kuzifwatilia hadi kituoni. Shamsa na waalifu wengine wawili wakaingizwa mahabusu, kusubiria mahojiano yatakayo fwanywa dhidi yao.
Akilini mwa Shamsa kumbukumbu za Phidaya, zilizidi kujirudia kichwani mwake. Hakuelewa ni jambo gani ambalo limetokea hadi Phidaya kuwa hai.

“Au sio yeye?”
Alijiuliza mwenyewe, huku akiwa amesimama kwenye moja ya kona ya mahabusu, huku mahabusu wezake wengine wakike wakiwa wamejilaza, kwenye sakafu.
“Kwa usiku huu hautaweza kumuona”
Askari mmoja alimueleza Sa Yoo, ambaye alihitaji kukutana na rafiki yake ili amuhoji kuhusu jambo lililo jitokeza muda mchache ulio pita. Sa Yoo kwa haraka akampigia simu daktari wa Shamsa, akamueleza kila kitui kilicho tokea, daktri hiyo aliye kabidhiwa jukumu la kumuangalia Shamsa, kwa haraka akafika kituo cha polisi akiwa ameongozana na mwanasheria wake kuhakikisha kwamba Shamsa anaachiwa huru.
                                                                                                           ***
  Maisha ya madam Mery yalizidi kuwa mazuri kadri siku zilivyo zidi kwenda, jeraha la risasi aliyo pigwa na Manka lilisha pona muda mrefu sana. Maisha yake aliamua kuyahamishia mkoani Mwanza, ambapo alifanikiwa kufungua mgahawa mmoja mkubwa wa kisasa, ambao kwa siku una uwezo wa kuhudumia wateja mia tisa hasi alfu moja kwa siku.

Umaarufu wa mgahawa wake uliendana moja kwa moja na jina lake, jumba kubwa la gorofa la kifahari, lililopo maeneo ya majango mapya. Aliliwekea ulinzi mkali kutoka katika mashirika mawili tofauti yanayo jishuhulisha na ulinzi. Uzuri wake uliwanyima usingizi wanaume wengi wa jijini Mwanza, umri wa miaka arobaini na moja alio nao, kwa haraka haraka ukimtazama utahisi ni msichana mwenye umri wa miaka ishirini na tano.

  Kwa siku hiyo, madam Mery alijawa na furaha sana moyoni mwake, pale alipo toka katioka banki ya Bacrays, na kukuta kiasi cha miliomi moja dola za kimarekani zikiwa zimeingizwa kwenye akaunti yake hiyo.
“Ranjiti nitakutesa hadi kufa kwako”
Madam Mery alizungumza baada ya kupokea risiti yake inayo onyesha kiasi hicho kikubwa cha pesa kikiwa kimeingizwa kwenye akaunti yake. Kwa mwendo wa madaha akaanza kutembea huku mlinzi wake wa kike akiwa ameibeba pochi lake kubwa. Wakaingia kwenye gari, walipo muacha dereva wake.

“Nirudishe nyumbani nahitaji kupumzika kwa sasa”
“Sawa madam”
Safari ya kutoka benk hadi nyumbani kwake iliwachukua dakika ishirini, geti kubwa linalo funguliwa na umeme likafunguka. Gari yake aina ya Hammer, likaingia na dereva akalisimamisha kwenye maegesho ya magari, ambapo kuna gari nyingine nne za kifahari zikiwemo, Range rover sport, Aud Q7, Ferrari spider na BMW X6. Milinzi wake kwa haraka akashuka na kumfungulia mlango.

“Lete tu pochi pumzika”
Madam Mery alizungumza huku akiichukua pochi yake kwa mlinzi wake huyo, akaelekea ndani, alipo pokelewa na mfanyakazi wake wa ndani.
“Mama utakula nikuandalie chakula?”
Hapana sijisikii kula”
Kwa furaha ambayo madam Mery anayo, hakutamani siku hiyo kuweza kuingiza kiu chochote mdoni mwake, kwani utajiri wake unazidi kuongezeka mara dufu, akaingia chumbani kwake, ajitupa kwenye tanda lake kubwa linalo nesa nesa.

“Mery sasa hivi mimi ni milionear”
Alizungumza huku akiliachilia tabasamu lake pana, akakaa kitako, akaichukua rimoti ya Tv yake kubwa ilipo ukutani, akaiwasha na kuanza kutafuta chaneli ambayo ina kipindi kizuri cha kutazama. Chaguo la chaneli likaangukia katika chaneli ya ITV, ambapo amekuta mwenyekiti wa chama cha upinzani cha  TDPP(Tanzania Democras People Party), bwana Kibwila, akizungumza na waandishi wa habari.
Masikio na macho ya Madam Mery yote yakaelekea kwenye Tv yake, mapigo ya moyo yakaanza kumdunda pale alipo muona Manka akiwa pembeni ya kiongozi huyo.

“Huyu mtoto amefwata nini kwenye hichi chama?”
Madam Mery aalijiuliza huku akiongeza kidogo sauti ya Tv hiyo. Mwenyekiti wa chama hicho bwana Kibwila, akafikia wakati wa kumtangaza mgombea uraisi wa chama chake.
“Mgombea wetu atakaye ipeperusha bendera ya chama chetu atakuwa ndugu Godwin, gererali mstaafu wa jeshi la wananchi Tanzania”
Madama Mery, akahisi kizunguzungu kikali kikitaka kumchukua, baada ya kulisikia jina la Mzee Godwin, kwa kudhibitishiwa kwamba mwenyekiti huyo hajakosea kabisa, akaonyesha picha ya Mzee Godwin, hapo ndipo furaha yote ya Madam Mery ikayeyuka kama barafu liwekwapo juani.
                                                                                                                ***
  Taratibu Rahab akamfikia Raisi Praygod kwenye mlango alipo simama, kwa haraka akamkumbatia, na kuanza kumwagikwa na machozi jambo lililo mshangaza raisi Praygod.
“Mume wangu nisamehe”

Rahab alizungumza huku machozi yakimwagika, raisi Praygod, alizidi kuendelea kushangaa, kumuona Rahab akiwa amerejea katika hali ya kawaida. Rahab, hakusita kuanza kuzinyonya lipsi za mume wake, joto la hisia za kimapenzi likaanza kupanda katikati yao. Kila mmoja akajikuta akiwa na hamu ya kupata penzi la mwenzake, ambalo walilikosa kwa kipindi fulani. Ndani ya dakika kadhaa wote wawilili wakajikuta wakiwa hawana nguo katika miili yao.
Kila mmoja alipo hakikisha kwamba amemuandaa mwenzake vya kutosha, mechi ikaanza, si raisi wala Rahab aliye onekana kuchoka, kila mmoja alihakikisha kwamba anampa mwenzake kile kitu roho inapenda, huku wote wakiwa wamejawa na furaha mioyoni mwao.
                                                                                                             ***
   Iliwalazimu Black Shadow kuhamishiwa katika chumba kingine cha siri, kilichopo chini ya ardhi ndani ya hospitali hiyo. Kazi hiyo ilifanywa na dokta Ranjiti na wasaidizi wake, usiku huo huo, baada ya tukio la uvamizi kutokea katika hospitali yake. Polisi wakatoa tamko kwa watu ambao walijitokeza kumuombea shujaa huyo, kwamba warudi majumbani kwao na kuanzia siku hiyo watu hawata ruhusiwa kuja kujazana katika hospitali hiyo, hadi pale afya ya Black Shadow itakapo imarika.

Lilikuwa ni pigo kwa mashabiki wa Black Shadow, ila hawakuwa na jinsi, ni lazima waweze kutii tamko hilo la askari. Ulinzi ukazidi kuimarishwa kwenye hospitali hiyo, hata dhiara ya raisi, ikakatishwa hadi pale mambo yatakapo kuja kuwa sawa ndipo raisi aweze kumtembelea mpiganaji huyo.

Uwepo wa Black Shadow katika chumba cha siri ulijilukana kwa watu wachache tu akiwemo Sabogo, ambaye yeye pekee ndiyo alipewa ruhusa ya kwenda kumuona Black Shadow katika chumba hicho. Asubuhi na mapema, Sabogo akawa yupo ndani ya chumba hicho cha siri kilicho jaa taa nyingi zenye mwanga mweupe.
    Sabogo akatoa kinyago kingine kilicho tengenezwa, kwa ajili ya Black Shadow, akamvua kinyago cha mwanzo na kumvalishi kingine kipaya lilicho mkaa vizuri, alipo hakikisha rafiki yake yupo salama, akatoka ndani ya chumba hicho na kurudi kwa daktari mkuu wa hospitali bwana Ranjiti.

“Itamchukua muda gani hadi kupata fahamu?”
“Itamchukua kipindi kidogo, ila kutokana bado tunaendelea kumuangalia kwa usalama mkubwa, basi tumuombe Mungu, kila jambo litakwenda sawa”
“Sawa dokta ila hakikisha kwamba hakuna mtu ambaye atagundua kwamba yupo chumba cha siri”
“Usijali kwa hilo”
Yote yakiwa yanazungumza ndani ya ofisi ya dokta Ranjiti Phidaya aliweza kuyasikia akiwa nje ya mlango, moyo wake ulizidi kumsumbua kila alipo fikiria juu ya donge nono ambalo polisi walilitangaza kwa mtu ambaye angelisaidia jeshi hilo kumkamata Eddy.

Phidaya akarudi kwenye ofisi yake akiwa na mawazo mengi, akilini mwake akaanza kulifikiria tukio la jana alipo weza kuiona sura ya Black Shadow, pili akafirikiria jinsi, majambazi walivyo vamia kwenye hospitali yake, na kutaka kumuua Black Shadow.
“Ina maana wanamjua kwamab ni Eddy nini?”
Phidaya alizungumza huku akinyanyuka kwenye kiti chake na kuanza kuzunguka zunguka ndani ya ofisi yake.
“Ngoja nikamueleze kila kitu mume wangu”
Phidaya alizungumza, kwa haraka akaanza kupiga hatua hadi mlangoni kwake, akavuta kitasa cha mlango huo, akaufungua na kuanza kutembea kuelekea katika ofisi ya mume wake.
                                                                                                 ***
   Baada ya Sabogo kutoka ofisini kwake, dokta Ranjiti, akawasha Tv yake, moja ya taarifa aliyo ikuta ni jinsi hospitali yake ilivyo vamiwa. Ila kati ya majambazi walio kamatwa, mmoja wao akamstua kidogo. Akajikuta akisimama kabisa na kwenda kuikodolea macho Tv hiyo. Jina la Shamsa Eddy, ndio kabisa zikazidi kumpagawisha. Na moja ya picha ikapita kwenye taarifa hiyo ya habari jinsi mke wake alivyo mtandika kofi jambazi huyo wa kike.

‘Mungu wangu siri inakwenda kufichuka’
Dokta Ranjiti alizungumza huku kijasho kikianza kumpiga na mapigo yake moyo yakizidi kwenda mbio. Akaanza kujipapasa kuitafuta simu yake ya mkononi sehemu alipo iweka, kwa bahati nzuri akaikuta kwenye koti lake, akaichomoa kwa haraka na kuminya baadhi ya namba kisha akaiweka sikioni, baada ya muda ikapokelewa upande wa pili.
“Ehee mkuu habari yako bwana”
‘Salama vipi dokta nikusaidie nini?’
“Naamini hao majambazi walio kuja kuvamia hospitalini kwangu wapo mikononi mwako”
‘Ndio na wanaendelea kufanyiwa mahojiano, ila huyu mmoja wa kike hana hatia ndio tumemuachia mida hii’
“Mungu wangu…….!!!”
‘VVipi kuna tatizo kwani?’
“Aha…ahaaa hapana”
‘Basi kila litakalo kuwa linaendelea nitakujulisha’
“Sawa mkuu”

Dokta Ranjiti baada ya kukata simu alipo maliza kuzungumza na mkuu wa kituo cha polisi, akili yake ikaanza kufanya kazi kama compyuta pale inapo tafuta, majina yaliyo hifadhiwa kwenye kumbukumbu zake. Kwa haraka mkumbukumbu zake zikatua kwenye moja ya mtu ambaye kazi zake ni umafia na huzifanya kazi za matajiri wengi ndani na nje ya Japani, pasipo kukosea wala kukamatwa na askari polisi kutokana na kujibadilisha badilisha sura na yeye huwa mara nyingi huwa ndio mtu anaye mfanyia upasuaji wa kumbadilisha sura.

“Ndio Kim upo wapi?’
‘Yokoma, vipi kuna tatizo dokta?’
“Ndio kuna tatizo bwana, kuna binti anaitwa Shamsa Eddy nahitaji uweze kumuondoa dunia”
‘Amekufanyaje tena dokta?’
“Ni binti ambaye anaitambua siri ya yangu juu ya mke wangu Phidaya, si unatambua kwamba huyu Phidaya ni mwanamke niliye mpora waziri mmoja nchini Tanzania”
‘Yap nalitambua hilo ulisha wahi kuniambia’
“Ndio basi binti huyo ni kati ya wale majambazi walio kamatwa jana na polisi na yeye anamtambua vizuri Phidaya kutokana ni mama yake”
  Mazungumza ya simu ya dokta Ranjiti yakamfanya Phidaya kusimama nje ya mlango, aliweza kusikia kila kitu alicho kizungumza mume wake, ila hakuweza kusikia mazungumzo na mtu wa pili.

‘Phidaya kutokana ni mama yake’
Maneno hayo yakaanza kujirudia kwa nguvu akilini mwake, machozi yakaanza kumlanga lenga Phidaya, hakuona haja ya kuendelea kukaa mlangoni mwa mume wake kwa haraka akaanza kutembea kurudi ofisini mwake. Akaufunga mlango wake kwa ndani, akavuta kiti chake, akawa kama mtu aliye changanyikiwa mara kadhaa akijiuliza maswali mengi kuhusiana na kitui alicho kisikia.
“Shamsa Eddy”
‘Ni binti ambaye anaitambua siri yangu juu ya mke wangu Phidaya’

Phidaya akajikuta akizidi kuyakumbuka maneno ya mume wake bwana Ranjiti, kiu na hamu ya kumuona Shamsa, ikaanza kumjaa moyoni mwake, kwani anatambu ni kati ya majambazi ambao walikamatwa jana na ni yule aliye mtandika kibao jana usiku. Kwa haraka Phidaya akavua koti lake na kuvaa koti la baridi, akajifutamachozi usoni mwake, wala hakuhitajki tena kuzungumza na mumewe kwa kitu alicho wahi kukiona. Kwani roho ya kumchukia mwanume huyo ilianza kumvaa. Swali ambalo mara kwa mara alijiuliza kichwani mwake, kwamba yeye ni nani, taratibu alihisi linaanza kupata jibu.
“Lazima nijijua mimi ni nani”
Phidaya alizungumza peke yake huku akitembea kwenye kordo ya kuelekea nje ya hospitali.
                                                                                                        ***
    Kwa juhudi za mwana sheria aliye msimamia Shamsa, kwenye mahojiano kati yake na polisi, yalizaa matunda, kwani hadi inatimu alfajiri tayari Shamsa alionekana kwamba hana hatia kutokana na maelezo yake aliyo yatoa. Uchunguzi ulio fanywa kwa nesi ambaye aliuawa na Shamsa, ulionyesha kwamba hakuwa ni nesi wa hospitali hiyo kutokana na kukutwa na michoro mingi(tattoo) mwilini mwake.

Pia katika kubanwa kwa waalifu wawili wa kiume walio kamatwa, walidhibitisha kwamba Shamasa sio mwenzao, hilo pia lilichangia kwa Shamsa kuachiliwa huru.
“Inabidi sasa twende nyumbani ukapumzike”
Sa Yoo alizungumza mara baada ya Shamsa kuachiliwa huru, kwani naye pia alishinda kituoni hapo kuhakikisha kwamba rafiki yake anaachiwa huru.
“Hapana nahitaji kwenda hospitali kumuona Black Shadow ndio niweze kwenda nyumbani’

Kutokana Shamsa ni mtu wa kung’ang’ania maamuzi yake mwanzo mwisho,  Sa Yoo na daktari hawakuwa na hiyana zaidi ya kuanza safari kuelekea katika hospitali aliyo lazwa Black Shadow. Akilini mwa Shamsa hakumfikiria Phidaya kutoka alihisi labda alimfananisha, isitoshe tayari walisha mzika mama yeka huyo. Kutokana ni asubuhi, barabara ilijaa foleni nyingi, kwa hiyo iliwachukua muda mwingi sana hadi kuweza kufika katika hospitali hiyo. Wakiwa getini, wakapishana na gari aina ya Aud A4. Hakuna aliye weza kuifwatilia sana, haswa Shamsa ambaye muda wote alimuwaza Black Shadow wake.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya April 23

Msemaji wa Simba afungiwa kujihusisha na soka kwa mwaka mmoja

$
0
0
Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), imemfungia Haji Manara (Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa klabu ya Simba) kutojihusisha na masuala ya soka kwa mwaka mmoja na pia anatakiwa kulipa faini ya Shilingi  Milioni tisa.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Nidhamu, Jerome Msemwa amesema hatua hiyo imefikiwa baada ya Manara kukutwa na makosa matatu dhidi ya TFF ambao ni walalamikaji.

Makosa hayo ya Manara dhidi ya mlalamikaji TFF ni kuituhumu na kuidhalilisha TFF, kueneza chuki za ukabila na la tatu kuingilia utendaji wa shirikisho hilo.
 
Siku chache zilizopita  Manara aliituhumu TFF kufanya njama za waziwazi ili kuwabeba wapinzani wao Yanga kwenye Ligi Kuu.

Manara pia aliwatuhumu viongozi wakuu wa TFF, Jamal Malinzi na Katibu wake, Selestine Mwesigwa ni wahaya na viongozi wa zamani wa Yanga, ambao wanataka kuipendelea Kagera Sugar.

Skyner Ampa Makavu Nay wa Mitego

$
0
0

Msanii wa hip hop, Nay wa mitego amechezea kichambo kutoka kwa mzazi mwenzake ambaye ni muigizaji wa filamu za bongo, Skyner Ally kuwa ameshindwa kuwa baba bora kwa binti yake.

Kwenye ukurasa wake wa instagram Skyner amefunguka maneno hayo akiwa anamtakia heri ya kuzaliwa mtoto wake ambaye amefikisha miaka mitano na kudai kuwa alikuwa na dukuduku kutoka moyoni ndani ya miaka mitano na baada ya kuongea tayari limetoka.

"Thats face you make when you see your 'daddy jina' anakufanyia promotions na kudanganya watanzania kama Oooh my Twin sijui nanunua pisto, hata chupi unayovaa hajui thamani yake maskini. nimevumilia sana It's 5 Years now nimejiskia kutapika na nimetapikaa.  Am done Mungu wa mbinguni nakuomba unijaalie maisha marefu uwezo nizidishie riziki..... uzima wa afya nikuleee mwanangu aje akuone baadae Inshallah umekuja kuwa Waziri wa nchi & Raisi wa nchi then alete pua yake" aliandika Skyner.

Aidha skyner ameendelea kufunguka kuwa "Endelea na drama zako ila please shobo na mwanangu sitaki...Please unapost picha za mtoto wangu za nini...shobo dundo zanini? Sitaki shobo na mwanangu koma kama ulivyo komaaa...Je, Wababa anaojisifu kama wanapenda watoto wao then hata hawajui mtoto anakula nini anasoma wapi anavaaa nini Wapooooooo? Drama nyingi sana mtandaoni halafu i love You Nyingi Hana Analofanya Wapooooooooo ??? Am done"- Aliongeza Skyner.

Skyner hakuishia hapo  aliendelea kutoa usia kwa binti yake kwa kuonyesha jinsi alivyo na umuhimu katika maisha ya binti yake "Hakuna anayejua thamani yako zaidi yangu hata huyo anayejita baba'ko hana analolijua kuhusu wewe, si shule, malazi wala chakula kutwa kucha kukupost na kuongopea jamii kama anakujali, ninayehangaika nimie nakuhakikishia na kumuomba Mola wangu anijaalie uhai nguvu uwezo riziki nizidi kukulea kwa nguvu zangu Inshallah nakuonea gere sana umepata mama bora na sio bora mama uko mikono salama mwanangu wa uchungu. Happy Birthday My Happiness"- Skyner alimaza

Maneno hayo makali kwa Skyner yalikuja muda mfupi baada ya Nay kuweka picha ya binti yake na kumtakia heri ya kuzaliwa na kudai kuwa amenunua bastola kwa ajili ya kumlinda.

Hii ndiyo 'Post' ya Nay iliyosababisha mama watoto wake kumtolea povu kwa hasira.

Kauli ya Jerry Muro baada ya Haji Manara wa Simba kufungiwa na TFF

$
0
0
Muda mfupi  baada ya shirikisho la soka Tanzania TFF kupitia kamati ya nidhamu ya TFF kutangaza kumfungia mkuu wa idara ya habari na mawasiliano wa Simba Haji Manara kwa utovu wa nidhamu na kukutwa na makosa matatu.

Afisa habari wa zamani wa Yanga ambaye nae alifungiwa mwaka mmoja Jerry Muro ametumia ukurasa wake wa instagram kuandika “Mtuache sasa tupumzike, tuliyofanya kwa taifa hilo haswa kwenye mpira nadhani yametosha, Waswahiba karibu kijiweni @hajismanara“

Mkuu wa idara ya habari na mawasiliano wa Simba Haji Manara amefungiwa mwaka mmoja kujihusisha na soka pamoja na faini ya Tsh Milioni 9.

Kamati ya nidhamu ya TFF imetoa adhabu hiyo licha ya Haji Manara kushindwa kufika kwa madai ya kupata dharura lakini anayo nafasi ya kukata rufaa.

TFF Yaipokonya Simba Pointi 3 za Kagera Sugar

$
0
0
Hatimaye Kamati ya Katiba, Sheria na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imeipokonya pointi tatu Simba SC, ilizokuwa imepewa kutoka kwa Klabu ya Kagera Sugar.

Awali, Simba ilikuwa imepewa ushindi wa mezani wa pointi tatu na magoli matatu dhidi ya Kagera Sugar, baada ya mchezo wake na timu hiyo ya mkoani Kagera kumalizika ikiwa imepigwa magoli 2-1.

Ushindi huo wa mezani ulitokana na malalamiko kuwa Kagera Sugar ilimchezesha mchezaji aliyekuwa na kadi tatu za njano, hivyo hakuwa na sifa za kushiriki mchezo huo kwa mujibu wa kanuni na sheria za Soka.

Akitangaza uamuzi wa kurejesha matokeo ya awali ya uwanjani leo katika ukumbi wa Habari wa TFF, Katibu Mkuu wa shirikisho hilo, Selestin Mwesigwa alisema kuwa sababu zilizopelekea Kamati kuchukua uamuzi huo, ni pamoja na kucheleweshwa kwa malalamiko ya Simba SC dhidi ya Kagera Sugar, Simba kushindwa kulipia ada ya rufaa dhidi ya maamuzi ya mechi hiyo na kukosekana kwa uhalali wa Kamati ya Saa 72 kwa kuwahusisha wajumbe waalikwa ambao hawakuwa na sifa za kuwa kwenye kamati hiyo.

Kutokana na uamuzi huo, Simba imeendelea kuwa kileleni mwa Ligi Kuu Tanzania Bara (VPL), ikiwa na pointi 59 badala ya 62 za awali.

Hali hiyo inawapa nafuu ya kupumua watani wao wa jadi, Young Africans ambao wana pointi 56 huku wakiwa na michezo miwili nyuma ya Simba FC.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya April 24

Mti wa Mchocho na Tiba ya Watoto Kukojoa Kitandani

$
0
0

Kukojoa  bila  kukusudia  ama  kujikojolea  ni  tatizo  linalo  wakabili  watu wengi duniani .

Kukojoa  bila  kukusudia  ama  kujikojolea  ni  ile  hali  ya   mtoto  mwenye  umri  wa  miaka  mitano  au zaidi  kushindwa  kuzuia  mkojo  wakati  wa  mchana  au  usiku  na  hivyo  kujikojolea  kitandani wakati  wa  usiku  au kujikojolea   kwenye  nguo  wakati  wa  mchana.

Tafiti  mbalimbali  za  kitaalamu  zinaeleza  kuwa  watoto wengi wanaacha kukojoa kitandani wakati  wa usiku katika umri wa miaka mitatu.  

Kuchelewa kukomaa kwa uwezo wa kibofu kuzuia mkojo kunaelezwa  kuwa  ndio  chanzo  kikuu  cha  tatizo  la  kujikojolea  kitandani kwa  watoto  wadogo.

Katika  tiba  asilia, ipo  mimea  mbalimbali  inayo  tajwa  kuwa  na  uwezo  wa  kutibu  tatizo  la  mtoto  kukojoa  kitandani.

Kati    ya  mimea  hiyo, upo  mti  wa  mchocho. Mmea  huu  umekuwa  ukitumiwa  na  wenyeji  wa  mkoa  wa Pwani  nchini  Tanzania  katika  kuwatibu  watoto  wenye tatizo  la  kukojoa  kitandani  au  kujikojolea.

Jinsi  unavyo  tumika, mizizi, magamba  na  majani ya  mmea  huu  wenye  ukubwa  kama  mti  wa  muembe  huchukuliwa  hukaushwa  na  kusagwa  kupata  unga  unga  wake,. Unga  wa  mti  huu  huchemshwa  kwenye  maji  kisha  kimiminika  chake  hupewa  kunywa  mtoto  mwenye  tatizo  la  kukojoa  kitandani  kwa muda  wa  siku  ishirini  na  moja. Mtoto  huanza  kuonyesha  nafuu kuanzia  siku  ya  saba  na  inapofika  siku  ya  ishirini  na  moja, mtoto huyu  anakuwa  amepona  kabisa  tatizo  la  kukojoa  bila  kukusudia  ama  kujikojolea  kwa  lugha  nyingine.

MAKALA  HAYA  YAMEANDALIWA  NA  DUKA  LA  NEEMA  HERBALIST. TUNAPATIKANA  UBUNGO  JIJINI  DAR  ES  SALAAM, NYUMA  YA  JENGO  LA  UBUNGO  PLAZA  JIRANI NA  SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING.

TUNAPATIKANA  KWA  SIMU  NAMBA  0766 53 83 84.  KUFAHAMU  ZAIDI  KUHUSU  TIBA ASILIA  YA  MAGONJWA  MBALIMBALI. TUTEMBELEE  KUPITIA  BLOGU  YETU:

www.neemaherbalist.blogspot.com

Live: Yanayojiri Bungeni Dodoma leo Aprili 24, 2017

$
0
0
Tazama hapa moja kwa moja kutoka Bungeni Dodoma kipindi cha Maswali na Majibu katika Bunge la 11, Mkutano wa Saba leo Aprili 24, 2017.

Bofya hapo  chini Kutazama.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images