Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Kauli ya Halima Mdee Baada ya Askofu Gwajima Kumtaka Amuombe Radhi Spika wa Bunge

0
0
Askofu Mkuu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Dr. Josephat Gwajima jana  alijitokeza hadharani mbele ya waumini wa kanisa lake na kumtaka Halima Mdee Mbunge wa CHADEMA kumuomba radhi Spika wa Bunge Job Ndugai kwa maelezo kuwa alimtukana. Gwajima alisema, kama hatafanya hivyo, basi ataitumia Jumapili Ijayo 'kumchapa' Hadharani

 Kutokana na madai hayo, Halima Mdee amejitokeza hadharani na kumjibu Gwajima

"Namuheshimu sana Mch. Gwajima,sitajibizana nae kwenye mitandao. Niweke rekodi sawa sijamtukana na wala sitarajii kumkosea heshima Spika.

"Hayo ya J2 namwachia yeye! Yangu na yaliyojiri Bungeni.. Najua jinsi ya kuyahandle. Yawezekana yalishamalizwa kabla ya Ibada yake LEO."


Makamu wa Rais Samia Suluhu kunusuru Bonde la Mto Ruaha Mkuu

0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuongoza Kampeni ya kunusuru Bonde la Mto Ruaha Mkuu lililopo Iringa kutokana uharibifu mkubwa unaendelea, huku akiambatana na Mawaziri watano ambao watasaidia kuokoa uharibifu wa Mazingira.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Januari Makamba alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jana Jijini Dar es salaam.

Alisema kuwa Ofisi hiyo imeanzisha Kampeni hiyo kwa sababu Hifadhi ya Bonde la Mto Ruaha Mkuu ni kubwa kuliko yote hapa Afrika Mashariki.

Alisema kuwa uharibifu unafanywa kutokana na shughuli mbalimbali za kibinadamu katika Bonde hilo unasababisha kukauka kwa Mto Ruaha ambao ni tegemezi katika nyanja za kiuchumi.

Aidha, Makamba aliwataja Mawaziri watakaoongozana na Makamu wa Rais kuwa ni pamoja na Waziri wa Maji, Gerson Lwenge, Waziri wa Ardhi, William Lukuvi, Waziri wa Maliasili na Utalii, Jumanne Maghembe, Waziri wa Kilimo, Charles Tizeba.

Vile vile, aliongeza kuwa hali ya mazingira kwa sasa ni mbaya sana kwenye bonde hilo kwani ukifika wakati wa kiangazi mto huo wa Ruaha Mkuu hautirirshi tena maji kama ilivyokuwa zamani.

“Hali hii inasababisha kupungua kwa watalii, shughuli za kiuchumi na uzalishaji wa umeme ambao unamrahishia mwananchi wa kawaida kupata umema nafuu, pia uhalibifu huu wa Mazingira unahatarisha maisha ya wanyama,”alisema Makamba.

Hata hivyo alitoa wito kwa wananchi wote kutunza vyanzo vya maji, Mazingira ili viweze kuwaletea manufaa kwa sasa na vizazi vijavyo.

Kamanda Sirro atoa tahadhari kwa wauza CD zenya Maudhui ya Kigaidi

0
0
Katika kuhakikisha Jiji la Dar es salaam linakuwa katika hali ya usalama kwa wananchi na mali zao, Kamishna wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam, Simon Sirro amewatahadharisha wafanyabiashara wa CD ambazo zina viashiria vya ugaidi kuacha mara moja biashara hiyo vinginevyo hatua kali zitachuliwa dhidi yao.

Amesema hayo Jijini Dar es salaam wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari, amesema kama wasipotii amri hiyo ya kuacha kuuza CD hizo zenye viashiria vya ugaidi ndani yake basi Jeshi la Polisi litaanzisha msako mkali dhidi yao na kuwachukulia hatua kali za kisheria.

“Hizi CD zina viashiria ambavyo vinahamasisha watu kufanya uhalifu kama ujambazi na masuala ya ugaidi, natoa angalizo kwa wafanyabiashara hao kuziteketeza, hii ni kwa ajili tu ya kuliweka Jiji letu katika hali ya usalama zaidi,”amesema Sirro.

Aidha, katika hatua nyingine, Sirro amewataka wafanyabishara wote wa CD wanaotandaza kando kando ya barabara kuacha mara moja kwani siyo sehemu sahihi na salama ya kufanyia biashara hiyo.

Hata hivyo, amesema kuwa hatua mbali mbali zinaendelea kuchukuliwa za kuhakikisha Jiji linakuwa salama na shwari, pia ametoa wito kwa wazazi, walezi, viongozi wa dini na wananchi kwa ujumla kufuatilia nyendo za watoto wao ili wajue wanajishughulisha na nini.

Maalim Seif Amvaa Lipumba, Msajili wa Vyama.......Ataja Hujuma 4 Dhidi ya CUF

0
0
Licha ya Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) anayetambuliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Profesa Ibrahim Lipumba kudai kuwa Baraza la Uongozi la chama hicho limemvua madaraka Katibu Mkuu Maalim Seif Sheriff Hamad kwa madai kwamba ameshindwa kutekeleza majukumu yake.

Maalim Seif jana Aprili 9,2017 jijini Dar es Salaam aliibuka na kueleza hujuma 4 nzito alizodai zimetekelezwa na Lipumba kwa kushirikiana na vyombo vya dola, kwa kutumia mgongo wake kukidhoofisha chama hicho, huku akijinasibu kuwa hajashindwa kutekeleza majukumu yake na kuahidi kwamba mara baada ya kumaliza ziara ya ujenzi wa chama Zanzibar atahamia Bara ili kudhihirishia wanachama hajashindwa kufanya kazi.

Maalim Seif alitangaza vita dhidi ya Profesa Lipumba na kundi lake huku akisisitiza kuwa yeye bado Katibu Mkuu hadi pale atakaposimamishwa na Baraza Kuu la Uongozi halali la chama hicho au kufukuzwa uanachama na Mkutano Mkuu halali wa CUF.

“Tumevumilia vya kutosha sasa basi, tutailinda CUF kwa gharama yoyote ile na nyie mlio nyuma ya mgogoro huu mtabeba dhamana kwa mliyoyatenda. Hakuna tena cha kunitisha na kunikatisha tamaa na tulipofika tutapata ushindi,” amesema.

==>Miongoni mwa hujuma 4 alizotaja Seif dhidi ya CUF, ni pamoja na;
1.Vyombo vya dola kumzuia kufanya shughuli za kisiasa upande wa Tanzania Bara

2.Lipumba kuvamia na kuteka baadhi ya ofisi za CUF

3.Wizi wa fedha za ruzuku

4.Bunge kupokea wagombea feki wa chama hicho katika uchaguzi wa Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki.

Licha ya hayo, Maalim Seif ameitaka Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) kutokubali kushiriki njama ovu aliyodai kuwa imelenga kusajili wajumbe feki wa Bodi ya Wadhamini CUF kwa minajili ya kumlinda Lipumba na Kundi lake ikiwemo kufuta kesi zilizofunguliwa na Bodi ya Wadhamini ya chama hicho dhidi ya mwenyekiti huyo anayetambuliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa na wenzake ambazo zimelenga kukilinda chama hicho.

Hali kadhalika amesema kuwa, CUF imekwisha pitia migogoro mingi ambayo chama hicho imeshinda kwa kuwa ni taasisi imara na kudai kwamba mgogoro uliopo sasa haujalenga kukisambaratisha chama hicho pekee bali umelenga kuiua demokrasia nchini kwa kukandamiza na kuzuia taasisi za kidemokrasia Tanzania kutekeleza majukumu yake.

“Huu ni wakati wa wapenda demokrasia na wapenda amani wote kusimama pamoja kuilinda demokrasia na taasisi zetu zinazohamasisha demokrasia,” alisema.

Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli Alivyosherehekea Siku yake ya Kuzaliwa Ambayo Ilikuwa ni Jana April 9

0
0
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli jana  aliadhimisha siku yake ya kuzaliwa kwa kutoa msaada wa vitu mbalimbali kwa wagonjwa katika Taasisi ya Magonjwa ya Saratani ya Ocean jijini Dar es salaam na kutoa wito kwa Watanzania kusaidia watu wenye mahitaji.

Akiwa hospitalini hapo, Mama Magufuli, alisema ameamua kuwatembelea na kuwafariji wagonjwa hospitalini hapo kwa kutoa msaada huo kwa kuwa yeye alizaliwa katika hospitali hiyo tarehe na mwezi kama wa huu ambapo pia alipata fursa ya kuwaombea afya njema wagonjwa wote na kuwatia moyo ndugu wanaouguza kuendelea na jukumu hilo zito.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road, Dk. Julius Mwaisalage alimshukuru  Mama Janeth Magufuli kwa moyo wake wa kujitolea kwa kusaidia wagonjwa hospitalini hapo kwa kuwa kitendo hicho kinawatia moyo wao kama wauguzi lakini pia kinarudisha imani kwa wagonjwa na kujiona kuwa hawapo peke yao.

Mama Janeth Magufuli kwa kushirikiana na wanawake wa Wilaya ya Ilala na Temeke wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema walitoa msaada wa vitu mbalimbali kama vile mchele, maharage, sabuni za kufulia, sabuni za kuogea, maziwa ya unga,juisi, taulo za kike, vitenge, kanga, misuli,mafuta ya kujipaka na dawa za meno.

Askofu Gwajima Atishwa na Matukio Ya Utekaji......Atishia Kumwanika Diamond Alivyojiunga Freemasons Kama Ataendelea Kumchokoza

0
0
Matukio  ya utekaji yanayodaiwa kutokea nchini, yamemtisha Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima, ambaye amesema Tanzania imeanza kuwa mahala pa hatari, huku akitaka vyombo vya dola vichukue hatua kuyakomesha.

Akihubiri jana katika kanisa lake lililopo Ubungo, Dar es Salaam, Gwajima  aligusia tukio la kupotea kwenye mazingira ya kutatanisha kwa Msaidizi wa Mwenyekiti wa Chadema, Ben Saanane, uvamizi wa Kituo cha Televisheni cha Clouds Group na kutekwa kwa msanii wa muziki wa Hiphop, Ibrahim Mussa maarufu Roma Mkatoliki.

Katika orodha hiyo, Gwajima pia alimtaja  mdogo wake, Mchungaji Samson Gwajima ambaye alidai alitekwa wiki iliyopita mkoani Mwanza.

Gwajima ambaye ibada yake hiyo ilikuwa ikirushwa mubashara na redio mtandao iliyokuwa ikisikilizwa na takribani watu 850,000 na mtandao wa Youtube uliokuwa ukifuatiliwa na watu 8,000, alilaani matukio hayo na kusema kwa sasa hata wazazi wana wasiwasi na usalama wa watoto wao, ikiwamo yeye mwenyewe ambaye wazazi wake wanamtaka aende  nje ya nchi. 

 “Tanzania inaanza kuwa nchi ya watu kupotea kama mzuka, Ben Saanane hajaonekana hadi leo, Meneja wa Diamond alisema wa kuulizwa aliko Roma ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, wakaenda akasema atapatikana kabla ya Jumapili.

“Aliyesema atapatikana Jumapili ama alijua, ana jeshi la kumfuatilia alipo, amemficha, amempa kazi maalumu ama alikuwa naye.

“Nazungumza haya kwa sababu hata mdogo wangu (Mchungaji Samson Gwajima) naye alitekwa, lakini alifanikiwa kujinasua, hivyo naunganisha watekaji wa Dar es Salaam na Mwanza,” alisema.

Alisema baadhi ya wazazi na walezi sasa wameanza kuwa na hofu na watoto wao kutokana na matukio ya utekaji yanayoendelea nchini.
 
Kwa mujibu wa Askofu Gwajima, wazazi wake (baba yake mzazi na baba mkwe wake), tayari wameingiwa na hofu juu ya matukio hayo.

“Ni nani anayewateka watu, anatumwa na nani, anawateka kwa manufaa gani, nani atakayefuata… mimi sitekwi ng’o, ila kama ni polisi nitakwenda.

“Tutafanya kazi saa ngapi, tutajenga nchi saa ngapi, nampenda sana Rais wangu, lakini mambo haya yanaleta picha mbaya, lazima utekaji ukome,” alisema Askofu Gwajima.

Alimtaka Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba na Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Ernest Mangu, kuchukua hatua dhidi ya matukio hayo yaliyoanza kuzoeleka nchini.

Alisema kwa hali ilivyo, waliovamia kituo cha televisheni Clouds na waliovamia studio aliyokuwamo Roma na kumchukua ni watu walewale kwa kuwa zote zilizovamiwa ni studio.

Alisema inatia shaka pale ambapo polisi wanasema mtu hayupo katika kituo chochote cha polisi, lakini baada ya muda uliotajwa na mtu asiye polisi, anayetafutwa anaibukia katika kituo cha polisi.

Gwajima alisema kwa mazingira kama hayo, inaonyesha aliyesema mtu huyo atapatikana kwenye muda huo alikuwa anajua alipo anayetafuwa, hivyo kumshauri Rais kumchukulia hatua kwa kumwondoa kwa maelezo kwamba atazidi kuiaibisha Serikali.

“Hata mimi nawaza, hivi akiondolewa ataenda wapi, lakini nishauri tu labda apelekwe hata nje ya nchi, huko mpaka arudi huku sisi tunaojua kuwa alipata zero (sifuri) tutakuwa na miaka 60 labda, na akiwa huko nje anaweza kusoma mpaka chuo kikuu, ama akasoma hata Memkwa (Elimu ya watu wazima),” alisema Gwajima.

Katika hatua nyingine, Askofu Gwajima pia alimshambulia  msanii wa muziki wa Bongo flava,  Naseeb Abdul, maarufu Diamond, kwa kumwimba katika wimbo wake alioutoa hivi karibuni.

Akimzungumzia Diamond kuhusu wimbo wake uliosambazwa katika mitandao ya kijamii, alisema alikuwa amejiandaa kugeuza dhahabu kuwa maji taka kwa aliyeimba wimbo na kumtaja kwa lengo la kuunga mkono wenye vyeti feki.

Alisema hata hivyo, ameamua kumsamehe Diamond kwa sababu Biblia inakataza kumshambulia mtu aliyeomba msamaha.

Juzi baada ya wimbo huo kusambaa katika mitandao ya kijamii na kuibuka taarifa kwamba jana Gwajima angezungumzia suala hilo, Diamond kwenye ukurasa wake wa Instagram aliandika:“Yala, yala jamani mwenzenu nimeyatimba, chonde chonde mzee wangu Bishop (Askofu) Gwajima usinigeuze maji kesho (jana).

“Maana nakujua ukimuamulia mtu… naweza Jumapili ya kesho (jana) nikaiona chungu mwaka mzima.”

Jana katika ibada yake, Askofu Gwajima alisema alipanga kueleza kuhusu siri ya mafanikio ya mwanamuziki huyo na mambo yanayoendelea katika maisha yake, lakini aliamua kumsamehe baada ya kuombwa radhi.

“Leo (jana) nilitaka kufundisha kuhusu Freemason na kuna bwana mmoja nitampiga ana uhusiano na Freemason. Nitaeleza tarehe aliyojiunga, mahala, alimtoa nani (kafara), ofisi yake ikoje na kinachoendelea kwenye maisha yake.
 
“Kabla hujamwimba Mchungaji Gwajima, lazima uwaze mara mbilimbili na wimbo wako uurudie mara mbilimbili kabla hujaupiga ili ujue madhara yake… nataka kumwonyesha namfahamu na nikikuongelea utabaki vipande vipande,” alisema.

Askofu Gwajima alisema  ana roho mtakatifu anayemsaidia kuwafyatua watu na akatahadharisha watu wanaojaribu kumshambulia wajue wanashambulia mdomo wa Jehova.

“Umetoa wapi ujasiri wa kusema juu ya masihi wa bwana? Ukinichokoza uwe umevaa suti ya chuma, mavazi ya kawaida nitayachana, watumishi wa Mungu unapotaka kuwachokoza tafakari mara mbilimbili,” alisema Gwajima.

Askofu Gwajima alisema amemsamehe Daiamond, lakini anampa onyo na kama akirudia tena hata akiomba msamaha hatamsamehe.

“Biblia inatuzuia kumpiga mtu aliyeomba msamaha na mimi namsamehe, lakini nampa onyo atakaposogeza pua yake tena, hata akiomba msamaha nitajua amezoea, hivyo atageuka sembe… ujumbe umeupata almasi,” alisema.

Katika ibada hiyo, pia Askofu Gwajima aliendesha maombi maalumu yaliyokuwa na lengo la kuiombea nchi iondokane na matatizo mbalimbali yakiwamo ya utekaji.

“Kama kuna kafara imetolewa watu wawe wanatekwa, tunafanya maombi maalumu juu ya nchi kwa ajili ya kuibomoa kafara hiyo,” alisema Askofu Gwajima na kushangiliwa na waumini wake.

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH .....Anasafisha Nyota, Anatafsiri Ndoto,Kinga ya Mwili, Biashara, Kizazi na Mengine Mengi

0
0
Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Maalim HUSSEIN Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..

==>JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. 

==>Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
 
Maalim Hussein Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
 
Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, na mengi zaidi

==>Whatsapp +255 674 835107 

==>Calls +255746757102
 
NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Rais Magufulin ateua kamati ya pili itakayofanya uchunguzi wa kiasi cha madini yaliyopo kwenye mchanga uliopo maeneo mbalimbali nchini

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 10 Aprili, 2017 ameteua wajumbe wa kamati maalum ya pili itakayofanya uchunguzi wa madini yaliyomo kwenye mchanga wenye madini ulio ndani ya makontena yaliyopo katika maeneo mbalimbali hapa nchini.

Kamati hiyo inajumuisha wachumi na wanasheria na imetanguliwa na kamati ya kwanza iliyoundwa na wataalamu wa masuala ya jiolojia, kemikali na uchambuzi wa kisayansi.

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imewataja wajumbe wa kamati hiyo kuwa ni;
  1.     Prof. Nehemiah Eliachim Osoro
  2.     Prof. Longinus Kyaruzi Rutasitara
  3.     Dkt. Oswald Joseph Mashindano
  4.     Bw. Gabriel Pascal Malata
  5.     Bw. Casmir Sumba Kyuki
  6.     Bi. Butamo Kasuka Philip
  7.     Bw. Usaje Benard Usubisye
  8.     Bw. Andrew Wilson Massawe
Wajumbe hao wataapishwa na Mhe. Rais Magufuli kesho tarehe 11 Aprili, 2017 saa 3:00 asubuhi Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
10 Aprili, 201

Jinsi Punyeto Inavyo Sababisha Ukosefu Na Upungufu Wa Nguvu za Kiume

0
0

Ukosefu  na/ama  upungufu  wa  nguvu  za  kiume, ni  tatizo  linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume  duniani.  Zipo  sababu  nyingi  zinazo  sababisha  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume.  

Miongoni  mwa  sababu  hizo  ni  pamoja  na  maradhi  kisukari, presha,shinikizo  la  damu, moyo, figo, matatizo  kwenye  mishipa  ya  ubongo  &  mishipa  ya  uti  wa mgongo, matatizo  kwenye  mishipa itumikayo  kusafrisha damu  mwilini, maradhi  ya  ngiri,  pamoja  na   upigaji  punyeto  kwa  muda  mrefu.

Katika  makala  yetu  ya  leo, tutaangalia  namna   suala  la  upigaji  punyeto linavyo  athiri  nguvu  za  kiume.

Kabla  hatujaangalia  namna  suala la upigaji  punyeto linavyo  maliza  nguvu  za  kiume, ni  vyema  tukafahamu  kwanza  kuhusu  SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME.

Kufahamu   kuhusu   SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME  tafadhali  tembelea :

Ukisoma  vizuri  kuhusu  mfumo  wa  nguvu  za  kiume, utagundua  kuwa   Suala  la  nguvu  za  kiume  ni  suala  la  kimfumo.  Ili  mwanaume  awe na nguvu  za  kiume, aendelee  kuwa  na  nguvu  za  kiume na  azilinde  nguvu  zake za  kiume, ni  lazima  ogani  zote zinazo  husika  na  mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ziwe  na  afya  njema  na  ziwe  na  ushirikiano   thabiti  na  wenye  afya.

Vile  vile , utagundua  kuwa , mambo  makuu  muhimu  katika   mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ni  kama  ifuatavyo:

i.Mishipa  imara  ya  ubongo  na  yenye  afya  njema

ii. Mishipa  imara  ya  uti  wa  mgongo  (  spinal  cords )

iii.Mishipa  imara  itumikayo  kusafirisha  damu  mwilini  (  Blood Vessels )

iv. Mfumo  imara  wa  usafirishaji  damu  mwilini

v. Mishipa  ya  uume  iliyo  imara  na  yenye  afya  njema

vi. Uhusiano  imara  na  wenye  afya  kati  ya  mishipa  ya  fahamu  iliyopo  katika  ubongo, mishipa  ya  kwenye  uti  wa  mgongo  pamoja  na  misuli & mishipa  ya  kwenye  uume.

Hivyo  basi, ili  mwanaume  aweze  kuwa  na  nguvu  imara  za  kiume, na  aendelee  kuwa  na  nguvu  hizo ni  lazima  mambo  yote  muhimu  katika  mfumo  wa  nguvu za  kiume  yawe  imara  pasi na  hitilafu  yoyote.

Hitilafu  yoyote  katika  mambo  hayo, itasababisha  ukosefu na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume  kwa  mwanaume  huyo.  Pale inapotokea    hitilafu  ama  mapungufu  katika  ogani  zaidi  ya  moja  kati  ya  zilizo  tajwa hapo  juu, basi  tatizo  kwa  muhusika  huwa  kubwa  mara  dufu.

JINSI  PUNYETO  INAVYO  SABABISHA  TATIZO  LA  UKOSEFU &  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.
Mwanaume   anapopatwa na  wazo  la  kufanya  tendo  la  ndoa, ubongo  hutoa  ishara  kwenye  mishipa  ya  uti  wa  mgongo  ambayo  nayo  husafirisha  taarifa  hadi  kwenye  mishipa &  misuli  ya  uume.

Mishipa  ya  uume inapopokea  taarifa  hiyo, hutanuka. Na  mishipa  ya  uume  inapotanuka, hufanya  mambo  mawili  muhimu  sana :

i.Husababisha  mishipa  ya  ateri  kupanuka  na  hivyo  kuruhusu  damu  kuingia kwa  kasi  sana   ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  hivyo  kuufanya  uume  usimame  na  kuwa  imara  bara bara.

ii. Huibinya na  kuiziba  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kuzuia  kunyonya  ama  kufyonza  damu  iliyo  ingia  ndani  ya  mishipa ya  uume.  (  KAZI  KUBWA  YA  MISHIPA  YA  VENA  ILIYO  KARIBU NA  MISHIPA  YA  UUME  NI KUHAKIKISHA  HAKUNA  DAMU NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME. HIVYO  BASI  DAMU  INAPOINGIA  NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME, MISHIPA  YA  VENA  HU “SENSE” JAMBO  HILO  KWA  HARAKA  NA HIVYO  KUIFYONZA  DAMU  HIYO  KUTOKA KWENYE MISHIPA  YA UUME  YA  KUITOA  NJE YA MISHIPA  YA  UUME.  NA  DAMU INAPOKOSEKANA  NDANI  YA  MISHIPA  YA  UUME, HUUFANYA  UUME  KUSINYAA  NA  KULEGEA )

Mtu  anayepiga  punyeto  husababisha  mambo  yafuatayo  katika  mwili  wake :

1. Huuwa  nguvu  ya  mishipa  & misuli ya  uume ambayo  ndio  inayo husika  na  kusimama  kwa  uume

2. Mishipa  ya   uume  inapo  sinyaa  na  kukosa  nguvu  yake  ya  asili, husababisha  mambo  yafuatayo :

i.Huondoa  uwezo  wa  mishipa  &  misuli  ya  uume  kutanuka, na  hii  ndio  sababu  inayo  wafanya  waathirika  wa  punyeto  kutumia  nguvu  nyingi  sana  katika  kuufanya  uume  usimame.

ii.Huondoa  uwezo  wa  mishipa &  misuli  ya  uume  kuibana  na  kuiziba  mishipa  ya  vena, na  hii ndio  sababu  inayo  fanya  waathirika  wa  punyeto  kufika  kileleni  haraka  sana, kwani damu  inayo  ingia  kwenye misuli  ya  uume   hufyonzwa  ndani ya  muda  mfupi sana. 
 
 Hii  hutokea  kwa  sababu  mishipa na  misuli  ya  uume inakuwa  imelegea,na  mishipa  ya  vena inakuwa  imepwaya, hivyo  msuguano wowote ule  hufanya  mishipa  ya  vena  kufunguka  na  kufyonza  damu  kutoka  kwenye mishipa  ya  uume  na hivyo  kuufanya  uume  kusinyaa  ndani ya dakika ama sekunde  chache sana.

3. Vile  vile  punyeto  hufanya  uume  kusinyaa na  kurudi ndani  na  kuufanya  uonekane kama  uume  wa  motto mdogo.

Kwa  ufupi  punyeto  husababisha  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  sababu  kuu  zifuatazo :

i.Kwanza   hudhoofisha  na  kuharibu  mishipa  ya  uume,  ambayo  ndio  hufanya  uume kusimama.

ii.Pili  hudhoofisha  utendaji  kazi  wa  mishipa  ya  ateri, ambayo  ndio  hutumika  kama  njia  ya  kusafirisha  damu kupeleka kwenye  misuli  ya  uume  na  ivyo  kuufanya  uume  usimame

iii. Tatu, punyeto  hupelekea  kuvuja  kwa  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kusababisha  damu  kufyonzwa  kwa  haraka  sana  kila  iingiapo ndani  ya  misuli ya  uume  na  matokeo  yake  ni  uume   kusimama  kwa  muda  mfupi  sana  wakati wa  tendo  la  ndoa.

iv. Punyeto  huathiri  mtiririko  wa  damu  kwenda  kwenye  mishipa  ya  uume, kwa  sababu  hudhoofisha  misuli &  mishipa  ya  uume  pamoja  na mishipa ya  ateri  ambayo  ndio  hutumika  katika  kusafirisha  damu kwenda  kwenye  uume

DALILI  ZA  MTU  ALIYE  ATHIRIWA  NA  PUNYETO
Dalili  kuu  za  mtu  aliye athiriwa  na  punyeto  ni  kama  ifuatavyo:

i.           Uume  kusinyaa  na  kuwa  kama  wa  mtoto
ii.         Uume kurudi  ndani
iii.       Uume  kusimama  ukiwa  legelege
iv.       Kufika  kileleni  haraka  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

TIBA   YA   NGUVU  ZA  KIUME  KWA MTU  ALIYE  ATHIRIKA  NA  PUNYETO.
Dawa   asilia  ya  nguvu  za  kiume iitwayo JIKO  ni tiba  bora  na  ya  uhakika  kabisa  kwa  mtu  aliye  athiriwa   na  punyeto.  Dawa  hii, pamoja  na  mambo  mengine  mengi, husaidia  kufanya  mambio  yafuatayo  katika  mwili  wa  mwanaume  aliye  athiriwa  na  punyeto :

i.Kuimarisha  mishipa  & misuli  ya  uume  ulio  legea na  hivyo  kuurejeshea  uwezo wake wa  asili

ii. Hutibu   tatizo  la  uume  kurudi  ndani

iii.Humaliza  tatizo  la  kusimama  kwa  uume  ukiwa  legelege

iv.Hutibu  na  kuponya  kabisa  tatizo  la  kufika  kieleleni  haraka.

BEI  YA  DAWA  :  Dawa  hii  inapatikana  kwa  gharama  ya  SHILINGI  ELFU  THEMANINI  TU (Tsh. 80,000/=)

MAHALI  INAPOPATIKANA :  Dawa  hii  inapatikana  katika  duka  la  dawa  asilia  liitwalo  NEEMA  HERBALIST  &  NUTRITIONAL  FOODS  CLINIC  lililopo  jijini  DAR  ES  SALAAM  katika  eneo  la  UBUNGO   nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA   karibu  na SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING.

Kwa  wateja  wasio  weza  kufika  ofisini  kwetu. Watafikishiwa  dawa  mahali  popote  walipo  jijini  DAR  ES  SALAAM.

Kwa   wateja  waliopo  mikoani  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  MABASI

Kwa  wateja  waliopo   Zanzibar  wata fikishiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa boti.

Na  kwa  wateja  waliopo  UGHAIBUNI  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  ama  DHL.

MAWASILIANO :  WASILIANA  NASI   KWA  SIMU  NAMBA  0766  53  83  84.

Kwa  taarifa  zaidi  kuhusu  huduma  zetu, tutembelee kila  siku  kwenye  blogu  yetu :

Watuhumiwa Watatu Waitwa Marekani Kwa Tuhuma Za Biashara Ya Dawa Za Kulevya

0
0
Waziri wa Katiba na Sheria amewasilisha maombi  ya kuwasafirisha washitakiwa watatu akiwemo Ally Hatibu Hassan maarufu kama Shkuba  kwenda nchini Marekani kwa ajili ya kujibu tuhuma za kusafirishaji dawa za kulevya.

Washitakiwa wengine ambao wanaungana na Shkuba ni Idd Mafuru na Lwitiko Emmanuel Adam.

Maombi hayo yamewasilishwa Katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu chini ya kifungu namba 5 (1) cha Sheria ya Usafirishaji wahalifu sura ya 368 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Katika maombi hayo upande wa waziri kupitia DPP wanaiomba mahakama hiyo isikilize ushahidi na itoe amri ya kuwahifadhi washitakiwa ndani wakiwa wanasubiri kibali cha Waziri huyo cha kuwasafirisha nje ya nchi kwa mashitaka hayo.

Mbunge Hussein Bashe atumiwa ujumbe wa vitisho kuwa yeye ni miongoni mwa watu 11 waliopo hatarini kufanyiwa vitu vibaya

0
0
Mbunge wa Nzega Vijijini kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Hussein Mohamed Bashe amesema kuwa ametumiwa ujumbe wa vitisho na watu wasiojulikana wakisema kuwa watamfanyika kitu kibaya popote pale alipo.

Bashe ambaye yupo kwenye vikao vya bunge vinavyoendelea mjini Dodoma ameandika leo asubuhi kupitia akaunti yake ya Tiwtter na Instagram  kuwa, ametumiwa ujumbe huo uliosomeka;

“Kuna watu wamenitumia ujumbe kwamba mimi ni kati ya watu 11 waliopo hatarini kufanyiwa vitu vibaya popote pale tulipo.

"Bunge na Serikali haiwezi kulifumbia macho jambo hili la Haramu wakati Watanzania wanatekwa na watu wasiojulikana. "

Kufuatia vitisho hivyo, Mbunge Hussein Bashe amelitaka Bunge na Serikali kutofumbia macho vitendo hivi vya wananchi kutekwa na watu wasiojulikana.

Roma aelezea tukio zima la kutekwa na mateso waliyopata

0
0
Mwanamuziki Roma Mkatoliki amezungumza na waandishi wa habari leo kuhusu tukio la utekaji lililomkuta yeye pamoja na wenzake watatu usiku wa Jumatano wakiwa katika studio za Tongwe Records Masaki jijini Dar es Salaam.

Roma amesema kuwa walikuja watu waliokuwa na silaha za moto, wakawaamuru kuingia kwenye gari na kisha wakafungwa vitambaa usoni na pingu mkononi na kupelekwa eneo ambalo halijulikani. 

Wakiwa katika eneo hilo walihojiwa kwa siku tatu huku wakipigwa kabla ya kwenda kutupwa wakiwa wamefungwa katika eneo ambalo kwa haraka hawakujua ni wapi.

==>Haya ni baadhi ya Maneno ya Roma
1. Kwanza natoa shukrani kwa Mungu, kwenu, kwa wananchi na hasa wasanii wenzangu, nimeona mmesimama imara, pia serikali.

2.Kilichotokea ni kama case study maana kimetuunganisha wote bila kujali itikadi zetu, tuendelee kushikamana.

3.Niwaambie ukweli tu, mpaka sasa hatuna uhakika na usalama wetu, mahali tulipokuwa si pazuri kabisa.

4.Kama alifanyiwa daktari, baadaye akafanyiwa msanii, usishtuke kesho akafanyiwa mwandishi wa habari, au Mbunge.

5.Kinachotusikitisha zaidi ni maneno ya baadhi ya watu wanaodai kuwa tumepewa pesa ili tuitengeze hii, siyo sawa.

6.Ukweli ni kwamba tukio ni la kweli na tumepigwa sana, hadi sasa hatuko sawa kiafya.

7.Siku hiyo, walikuja watu wakiwa na silaha, na wamefunika nyuso zao, wakatuamrisha kuingia ndani ya gari.

8.Walitufunga macho na kutupeleka kusikojulikana, walitutesa sana, wametupiga sana.

9.Baada ya kupitia katika kipindi cha mateso makali, tuliachiwa usiku, tukaana kutembea bila kujua tuko wapi.

10.Siwezi kujua kama tukio hili linahusiana na muziki wangu, maana kuna hadi house boy wetu pia amehusika.

==>Hapo chini kuna Video wakiongea

Mwakyembe: Ntahakikisha Nawapata Waliomteka Roma ili Kukomesha Tabia Hii

0
0
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe amesikitishwa na vitendo walivyofanyiwa wasanii wa muziki Roma Mkatoliki na wenzake huku akisema hawezi kukubali kuona mambo kama hayo yakiwa yanaendelea kutokea.

Akizungumza na wanahabari leo Jijini Dar es Salaam, Waziri huyo amesema kilichotokea siyo hali ya kawaida kwa watanzania kamwe hawezi kukubaliana na jambo hilo huku akisisitiza kuwa atafuatilia kwa ukaribu sana ili aweze kupata majibu ya haraka kabla hajawasilisha bajeti ya wizara yake

"Hiki kilichotokea siyo hali ya kawaida kwa watanzania, hatuwezi kukubali kitu kama hiki kiendelee kutokea,nitalifuatilia kwa ukaribu sana, nitajitahidi nipate majibu kabla ya bajeti yangu Bungeni". Alisema Dk. Mwakyembe

Hata hivyo Dkt. Mwakyembe amewataka wananchi waache tabia ya kuamini kila maneno yanayosemwa na watu ambao hawana ujuzi katika masuala ya uchunguzi, hivyo wanapaswa kuvipa muda vyombo vya dola viweze kufanya kazi zake kwa ufasaha.

"Nilishasema kuwa nimeagiza vyombo vya dola vifanyeuchunguzi ili ajulikane aliyewafanyia hivi wakina Roma kama ni nani kama wa dola ntadili naye, tuache uchunguzi ufanyike, tuache kupiga ramli". Alisisitiza Mwakyembe

Pia Waziri huyo mwenye dhamana na wasanii ametoa ujumbe kwa vyombo vyote vilivyopo chini ya Wizara yake kutofanya mahojiano yoyote yanayowahusu wasanii hao bila ya kuwepo taarifa kamili kutoka kwake.

Kwa upande mwingine Roma ambaye ambaye amesimulia tukio lilivyokuwa amesema kwa sasa hawezi kuongea mambo mengi kwa kuwa kila kitu amekwisharipoti polisi kila kitu, na kwamba kuna mambo akiyaweka hadharani atakuwa anaingilia upelelezi wa polisi.

Pia amesema hawezi kujua kama kweli tukio hilo lililowatokea  linahusiana na muziki kwa kuwa ameweza kuhusishwa mpaka mfanyakazi wao wa ndani ambaye hana hata chembechembe za uimbaji.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya April 11

Mfumuko Wa Bei Wa Taifa Kwa Mwezi Machi 2017 Umeongezeka Hadi Kufikia Asilimia 6.4

0
0
Mfumuko wa Bei wa Taifa kwa mwezi Machi, 2017 umeongeza hadi kufikia asilimia 6.4 kutoka asilimia 5.5 mwezi Februari 2017.

Hayo yalibainishwa katika taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) kwa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam naja.

Taarifa hiyo ilieleza kuwa hali hiyo inamaanisha kuwa, kasi ya upandaji wa bei za bidhaa na huduma kwa mwaka ulioishia mwezi Machi 2017 imeongezeka ikilinganishwa na kasi ya upandaji ilivyokuwa kwa mwaka ulioishia mwezi wa Februari 2017.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo Fahirisi za Bei zimeongezeka hadi 108.44 mwezi Machi 2017 kutoka 101.93 mwezi Machi 2016.Mfumuko wa Bei wa bidhaa za vyakula na vinywaji baridi kwa mwezi Machi 2017 umeongezeka hadi asilimia 11.0 kutoka asilimia 8.7 ilivyokuwa mwezi Februari 2017.

Taarifa hiyo imeonesha kuwa kuongezeka kwa mfumuko wa Bei wa mwezi Machi 2017 kumechangiwa na kuongezeka kwa bei ya baadhi ya bidhaa za vyakula na bidhaa zisizo za vyakula kwa kipindi kilichoishia mwezi Machi 2017 zikilinganishwa na bei za mwezi Machi 2016.

Waziri Mkuu Amsimamisha Kazi Mkurugenzi Msaidizi Wa Pembejeo

0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemsimamisha kazi Mkurugenzi Msaidizi wa Pembejeo wa Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Bw. Shenal Nyoni ili kupisha uchunguzi wa tuhuma zinazomkabili kwa kuongeza gharama za pembejeo kwa kushirikiana na baadhi ya mawakala wa pembejeo za kilimo.

Amesema Serikali italipa madeni yote ya mawakala wa pembejeo za kilimo mara baada ya kukamilisha uhakiki na kujiridhisha juu ya uhalali wake, sababu bado inawahitaji mawakala ili kushirikiana nao katika kuhudumia wakulima kwenye maeneo mbalimbali nchini.
 
Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo jana (Jumatatu, Aprili 10, 2017) katika kikao alichokiitisha kwenye Makazi ya Waziri Mkuu mjini Dodoma kati yake na mawakala wa pembejeo za kilimo pamona na Maofisa kutoka Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi.
 
“Gharama ya madeni ni kubwa kuliko pembejeo zilizosambazwa. Hii inatokana na udanganyifu mkubwa unaofanywa na mawakala kwa kushirikiana na watendaji wa Serikali wanaohusika na masuala ya pembejeo,”
 
Amesema kuwa kwenye eneo la pembejeo kuna matatizo makubwa kutokana na baadhi ya Maofisa kuzungumza na mawakala na kuongeza gharama za pembejeo kwa lengo la kuibia Serikali na kisha kugawana fedha. 

“Sasa Serikali haiwezi kulipa madeni ya kutengenezwa bali tutawalipa stahili zenu baada ya uhakiki kukamilika kama nilivyosema awali,”.
 
Waziri Mkuu aliongeza mawakala wa pembejeo waliwasilisha Serikali deni la sh. bilioni 65.4 kwa huduma waliyoitoa katika mikoa 25 ambapo Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi imekamilisha uhakiki wa madeni hayo kwa mikoa 10 ya Morogoro, Iringa, Njombe, Ruvuma, Songwe, Rukwa, Katavi, Kigoma, Kilimanjaro na Arusha ambayo madeni yake ni asilimia 70 ya madeni yote.
 
Alisema ripoti ya uhakiki wa mikoa nane kati ya 10 imetoka (imebaki Katavi na Kigoma) na kubainisha kuwa mikoa hiyo inadai sh. bilioni 36 kati ya hizo sh. bilioni 11 bado zinaendelea kuhakikiwa, sh. bilioni 14 zimekataliwa hivyo siyo madeni halali, sh. bilioni 8.2 ndiyo deni halali na sh. bilioni 2.3 zinachungizwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU).
 
Waziri Mkuu alisema uhakiki wa madeni kwa mikoa 15 iliyobakia ambayo madeni yake ni asilimia 30 unaendelea ambapo amewasihi mawakala hao kuwa wavumilivu katika kipindi ambacho Serikali inafanya uhakiki kwa kuwa inataka itende haki kwa kila mtu kulipwa deni lake kwa kiwango kinachostahili na watakaobainika kufanya udanganyifu watachukuliwa hatua za kisheria.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
S.L.P 980, DODOMA

JUMATATU, APRILI 10, 2017.

Prof. Maghembe Apiga Marufuku Kusafirisha Mkaa Kutoka Wilaya Moja Kwenda Nyingine Kuanzia Mwezi Julai.

0
0
NA HAMZA TEMBA - WMU
Waziri wa Maliasili na Utalii Prof. Jumanne Maghembe ametangaza mabadiliko makubwa katika biashara ya mkaa nchini na kusema kuwa kuanzia mwezi Julai mwaka huu hakuna mkaa wowote utakaosafirishwa kutoka wilaya moja kwenda nyingine ili kunusuru misitu inayoteketea kwa kasi hapa nchini.

Amesema hayo jana  wakati akifungua mkutano wa 24 wa baraza la wafanyakazi wa Wizara ya Maliasili na Utalii uliofanyika katika ukumbi wa LAPF mjini Dodoma na kuhudhuriwa na wajumbe mbalimbali kutoka kwenye Idara, Vitengo na Taasisi mbalimbali zilizopo chini ya Wizara hiyo.

“Kuanzia mwezi Julai hakuna ruhusa ya kutoa vibali vya kuhamisha mkaa kutoka wilaya moja kwenda wilaya nyingine, mkaa utachomwa, utauzwa ndani ya wilaya kwa ajili ya matumizi ya watanzania wanaohitaji nishati ya mkaa, lakini biashara ya mkaa ya kutoa Dodoma kwenda Dar es Salaam mpaka Zanzibar marufuku.

“Wamekata misitu yetu yote, mito yetu imekauka, tunashindwa kupata maji ya umwagiliaji kwasababu watu wengi huko nje wanataka mkaa wetu, Tanzania jamani sio shamba la bibi, wale wote watakaotoa mkaa kutoka eneo moja hadi jingine kinyume na sheria hii watashuulikiwa kwa utaratibu wa uhujumu uchumi”, alisema Maghembe.

Alisema kuwa kwa upande wa miji mikubwa kama Dar es Salaam, Dodoma, Morogoro na Tanga vitaanzishwa viwanda maalumu vya kuzalisha mkaa ambao utauzwa kwa vibali maalumu katika mikoa mbalimbali hapa nchini. Amesema mkaa huo hautakuwa na athari nyingi za kimazingira kwa sababu utazingatia taratibu za uzalishaji endelevu.

Wakati huo huo, Waziri Maghembe amemuagiza Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania kumuhamisha kituo cha kazi Mkuu wa Kikosi cha Kufuatilia na Kuzuia Uharibifu wa Misitu wa Wakala hiyo, Arjason Mloge kutoka Makao Makuu ya Taasisi hiyo kwenda chuo cha Viwanda vya Misitu (FITI) kilichopo mkoani Kilimanjaro na badala yake atafutwe mtu mwingine muaminifu.

Alisema uamuzi huo ni kufuatia udhaifu uliojitokeza katika usafirishaji wa rasilimali za misitu ndani na nje ya nchi ikiwemo usafirishaji kwa kutumia nakala za vibali ambazo sio halisi, yaani “Photocopies”. 

“Agizo hili litekelezwe mara moja kabla ya saa sita mchana wa leo na niwe nimepewa nakala ya barua hiyo ya uhamisho” alisema.

Kufuatia uamuzi huo amepiga marufuku kuanzia sasa usafirishaji wa mazao ya misitu ndani na nje ya nchi kwa kutumia nakala zisizo halisi (Photocopies). Ameongeza kuwa katika kuunga mkono Sera ya Uchumi wa Viwanda ya Serikali ya awamu ya tano hakuna gogo litakalosafirishwa kwenda nje ya nchi.

“Wawekezaji wanahimizwa kujenga viwanda vya kuchakata magogo hayo hapa nchini ili kutoa ajira kwa Watanzania pamoja na kutoa faida halisi inayotokana na rasilimali hizo kwenye uchumi wa taifa”, alisema.

Akizungumzia changamoto ya mifugo kwenye maeneo ya hifadhi nchini amesema Sheria ya Uhifadhi wa Wanyamapori Na. 5 ya mwaka 2009 sehemu ya 21 (1) hairuhusiwi kabisha kuchunga mifugo katika Hifadhi za Taifa, Mapori ya Akiba, Mapori Tengefu na Hifadhi za Misitu. Aliwataka watumishi wa Maliasili kusimamia Sheria hiyo pamoja na kutoa wito kwa wananchi kuifuata kikamilifu.

Katika hatua nyingine, Waziri Maghembe aliwataka majangili wote nchini kuachana na biashara hiyo haramu ambayo hailipi kwa sasa na badala yake wachukue matrekta wakalime.

“Mtu ambaye alikuwa anaishi kwa kutegemea ujangili sasa atafute trekta akalime, kwa sababu akifanya ujangili tukamkamata tu, na tukimkamata atakaa kwenye hoteli ya mkuu wa magereza (magereza) kwa zaidi ya miaka 25”.

Aidha, Waziri Maghembe alitoa pongezi kwa watumishi wote wa Wizara ya Maliasili kwa kazi nzuri wanayofanya ya kupambana na ujangili nchini pamoja na ulinzi wa maliasili za taifa (Misitu, Wanyamapori na Mambo ya Kale) ambazo kwa pamoja zinachangia asilimia 20.5 kwenye pato la taifa. Amesema matokeo chanya ya kupambana na ujangili yameanza kuonekana japo ujangili bado upo.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Aloyce Nzuki alimueleza Waziri Maghembe kuwa maelekezo yote aliyoyatoa yamepokelewa kwa ajili ya kuyafanyiwa kazi, huku Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori, Prof. Alexandre Songorwa akimueleza Waziri huyo kuwa watalinda na kusimamia Malisili za Taifa na kwamba katu hawapo tayari kuandikwa kwenye vitabu kuwa walishiriki katika kutoweka kwa maliasili hizo.

Kitanda cha Sokwe Mtu

0
0
Ni  simulizi  la  ukweli  linalo  husu  maisha  ya kijana  Lugwisha , kutoka  kitongoji cha  Goweko, wilayani  Uyui  mkoani  Tabora.

 Kijana  Lugwisha, baada  ya  kumaliza  shule  ya  msingi  mnamo  mwaka  1994 huko  kijijini  kwao, alifunga  safari  hadi  jijini  Dar  Es  Salaam, kwa  ajili  ya  kutafuta  maisha.

Miaka  kumi  baadae  , kijana  Lugwisha  akawa  amepata  mafanikio  makubwa  yaliyo badilisha  maisha  yake.

Mafanikio  katika  maisha  ya  Lugwisha  yanasababisha  kuinuka  kwa  maadui  ambao hawapendezwi   na  kufanikiwa  kwake.

Maadui  hawa  wanapanga  njama mbalimbali  za  kupambana dhidi ya  mafanikio  ya  Lugwisha.

Kati  ya  maadui  wa  Lugwisha,  ni  maadui  wawili tu  ndio wanaonekana  kuwa  na  nia thabiti  nay a  dhati  katika mapambano  dhidi  ya  Lugwisha.

Maadui  hao  ni  Beka  Msangi  pamoja  na  Bundala.

Beka  Msangi  alikuwa  mmiliki  wa  bar  iliyo  kuwa  jirani  na  bar  iliyo  milikiwa  na  Lugwisha.

Bar hii  ya  Lugwisha  ilikuwa  ni  moja  kati ya  makumi  ya  vitega  uchumi  vyake vilivyo  muingizia  fedha nyingi.

Bar ya  Lugwisha  ilikuwa maarufu  sana  jijini  Dar  Es  Salaam  na ilikuwa  ikifurika  wateja  kuanzia  Jumatatu hadi  Jumapili.

Bar  hii  ya  Lugwisha  ilikuwa  katika  eneo  lenye  bar  nyingi. Uwepo   wa bar  ya  Lugwisha  katika eneo  hilo uliua  biashara  ya  karibu  bar  zote  zilizo kuwepo  katika  eneo ikiwemo  bar ya  Beka  Msangi.

Beka  Msangi  hakutaka  kukubaliana  na  hali  hiyo  na hivyo  kufikia  uamuzi  wa  kusafiri  hadi  katika  kijiji  cha  Mchukwi  wilayani  Rufiji mkoani  Pwani,   kwa ajili ya  kumroga  Lugwisha.

 Baada  ya  kupiga  ramli, wachawi  wa Rufiji  wanaona  njia  pekee  ya  kupambana  na  Lugwisha  ni kumuhamisha  kichawi   yeye  na  bar  yake  kwa  kutumia  uchawi  wa  kizigua, ujulikanao  kama  “Sunkwa”.

Lengo  la skadi  hili  la  kichawi  lilikuwa  kumfanya  Lugwisha, yeye  mwenyewe  kwa  hiari  yake    afunge  bar  yake  katika  eneo  hilo  na  kuhamia  katika  eneo  jingine  na  wala  asipate  kabisa  wazo la  kurudi  tena  kufanya  biashara  katika  eneo  hilo,  hali  ambayo  ingemfanya  Beka  Msangi  aweze  kufanya  biashara  yake  ya  Bar  bila  ya  kupata  upinzani  wowote  mkubwa.

Ama  kwa  upande  wa  Bundala, huyu  ni  mdogo  wa  damu  wa Lugwisha.  Lugwisha  na  Bundala wamezaliwa  kwa baba  mmoja  lakini  mama  tofauti.

Baada  ya  kujaribu  kuomba  misaada  ya  mara  kwa  mara  kwa  Lugwisha  bila  mafanikio  yoyote, Bundala , mama  yake  ( ambae  ni  mama  wa  kambo  wa  Lugwisha  )  pamoja  na dada  yake  aitwae  Kalunde  ambae  alikuwa  Mwalimu  wa  shule  moja  ya  msingi  huko  mkoani  Kigoma, walijiridhisha  pasi  na  shaka  yoyote  kwamba, Lugwisha   anawadharua  sana  kwa  sababu  Mwenyezi  Mungu  amemjalia  fedha  na  mali  na  kwamba, anawabagua  wao  kwa  sababu  ni  watoto  wa  mama  wa  kambo.

Hivyo  basi Bundala, Kalunde  pamoja  na  mama  yao alieitwa   Bi. Mkamiti  wakaamua  kusafiri  hadi  wilaya  ya  Kasulu  mkoani  Kigoma  kwa  ajili  ya  kwenda  kumroga  Lugwisha  ili afilisike  kabisa, awe  kama  wao  au  awe  chini  yao.

------------------------------------------------------------------

JE   BEKA     MSANGI   ATAFANIKIWA   KUMUHAMISHA  LUGWISHA  KWA  KUTUMIA  UCHAWI ? JE  BUNDALA, KALUNDE  NA  BI MKAMITI   WATAFANIKIWA  KUMFILISI  LUGWISHA  KWA  KUTUMIA  UCHAWI  KUTOKA  KIGOMA ?

Jiandae  kusoma  kitabu  “  KITANDA  CHA  SOKWE  MTU “  upate  kujua  ukweli   kuhusu  kisa  hiki  cha  ukweli.   Kitabu  hicho  kitatoka  hivi  karibuni  na  utakipata  kwa  gharama  ya  SHILINGI  ELFU  KUMI  TU  ZA  KITANZANIA .

Katika  kitabu  hicho  utapata  kufahamu  mambo  mbalimbali  kama  vile ;

A. Jinsi  wachawi  wanavyo  tengeneza  uchawi  wa  kumuhamisha  na  kumfukuza  mtu   kwa  kutumia  uchawi, kutoka  sehemu  moja  na  kwenda  sehemu  nyingine  na  kumfanya  mtu  huyu  asirudi  tena  katika  eneo  hilo  hadi  anaingia  kaburini, pamoja  na jinsi ya  kujiepusha  dhidi  ya  uchawi  huo.

B. Utapata  kufahamu  jinsi  wachawi  wanavyo tengeneza  uchawi  wa  kumfilisi  mtu  fedha  na  mali  zake  zote  kwa kutumia  uchawi  pamoja  na  jinsi  ya  kujikinga  dhidi  ya  uchawi  wa  namna  hiyo  hali kadhalika  jinsi  ya  kumzindua  mtu  aliye  tupiwa  uchawi  wa  aina  hiyo.

Vile  vile  katika  kitabu  hiki  utapata  kujua  matumizi  ya  kichawi  na  kiganga  kuhusu  vitu  na  mambo  mbali  mbali  kama  vile :

1.  Miti  ya  kwenye  kitanda  cha  sokwe  mtu

2. Mizizi iliyookotwa wakati kaburi linachimbwa

3. Dawa  chafu  ya  kiarabu  ambayo  inafanana  na  lami : Dawa hii  ya  kiarabu  ni  miongoni  mwa  madawa  machafu  kabisa  yatumikayo  kwa  ajili  ya  mambo  ya  shari  za  aina  mbalimbali. Utafahamu pia jinsi ya  kujikinga  na  heri  za  dawa  hiyo.

4.   Mzizi  ya  mti uitwao  Mbono  Kaburi

5.   Mizizi  ya  mti uitwao  Mtopetope

6. Mizizi  ya  mti  uitwao  Mshindwi

7.Marashi  ya  waridi

8. Sindano

9.Nyembe  zilizo  katwa  na  kwanini  huwa  zinakatwa

10.Makaburi  ya zamani  yaliyo  kwisha  kusahaulika

11. Jogoo  mweusi  au  jogoo  mwekundu  aliye wekwa  porini kwa  muda  wa  siku  saba.

12.Chungu  cheusi  kilicho  kesha  kaburini kwa  muda  wa  siku saba

13.Kaniki  nyeusi  pamoja  na  kamba  za  kaniki  nyeusi

14.Ngorani  yangu : Utapata  kujua  neno la  lugha  ya  kiha  “ NGORANI” lina maanisha  kitu  gani  katika  ulimwengu  wa  waganga  na  wachawi  na  linatumikaje, wakati  gani, kwa  sababu, gani, namna  gani  nakadhalika.

15.Mwiko  uliotumika  kupika  kwenye  msiba  mkubwa

16.Mzizi  wa  mti  ulio katisha  njia : Kwa  ufupi  tu  hiki  ni  kizimba  kikubwa  sana chenye  matumizi  mengi  sana  katika  ulimwengu  wa  kiganga. Ni kizima  kinacho tumika kufungua  vifungo  vingi  sana  vya  kichawi. Kila  mtu anapaswa  kufahamu  kuhusu  kizimba  hiki.

17. Maji  ya  mchele  yaliyo  kesha

18.Maji  ya  zamzam

19.Mizizi ya mti  wa  mkurungu

20.Jogoo  aliye  wika  alfajiri  mara  moja  tu na  kuchinjwa  hapo  hapo, huku damu  yake  ikiwekwa  kwenye  chungu  cheusi

21. Mizizi  ya  mti  uitwao  Mkubashengelo

22. Mizizi  ya  mti uitwao Mzungupori

23.Maseko :  Hii  ni dawa   ipatikanayo  kwa  kuchanganya  dawa  saba  za  porini ambazo, kati  ya  dawa  hizo  ni  pamoja  na  magamba  ya  mti  wa  ukwaju pori, pamoja  na  mafuta  ya  mnyama fulani  afugwae

24.  Mkuki  mdogo  wa  asili

25.Sarafu  ya  fedha

26. Asali  mbichi  ya  nyuki  wadogo

27.Panya  mdogo  aitwae  Msuswe

28. Mafuta  ya  simba

29.Mafuta  ya  nyuki  wa  Nimba : Nimba  ni  mnyama  wa  porini  ambae  anafanana  na  nyumbu. Mnyama  huyu  huwa  anatembea  na  mzinga  wa  nyuki  kichwani  kwake. Yupo  katika  kundi  la  wanyama  washirikina. Hapatikani  wala  kuonekana  kwa  urahisi na huwa  anapotea  kimiujiza.

30. Nywele  za  saluni

31. Punda, kondoo,  au  mbwa  aliye  pita  duniani  bila  kuonekana

PAMOJA   NA  MAMBO  MENGINE  MENGI.

KITABU  HIKI  KITAFUNGUA  UFAHAMU  WAKO  KUHUSU  MAMBO MENGI  KATIKA  ULIMWENGU  USIO ONEKANA.

SABABU  YA  KUTOA  KITABU : Wafuatiliaji  wa  makala  zangu  wamekuwa  wakilalamika, ninachelewa  sana  kutoa  matoleo  yanayo  fuata  ya  makala  mbalimbali  zilizo  andikwa  au  kusimuliwa  nami. Hii  imekuwa  ikisababishwa  na  kutingwa  na  shughuli  nyingi  na  hivyo kukosa  muda  wa  kutosha  wa  kuandika  makala.  Watakao  pata  bahati ya  kusoma  kitabu  hiki, watapata  fursa  ya  kukisoma  kuanzia  mwanzo  hadi  mwisho  wake.

WEKA  ODA  YAKO MAPEMA : Weka  oda  yako  mapema . Utaratibu  wa  kuweka  oda  ni  kama  ifuatavyo :  ANDIKA  UJUMBE  MFUPI  WA  MANENO  KUPITIA  SIMU  YANGU  YA  MKONONI

0744  000  473  UKISEMA  “ KITANDA  CHA  SOKWE  MTU”. Nami  nitahifadhi  namba  zako, na  kitabu kitakapo  toka  jikoni  basi utakuwa  miongoni  mwa  watu  wa  kwanza  kupata  nakala  yako.

Au  unaweza  kuandika  ujumbe  mfupi  wa  maneno  ukiambatanisha  na  namba  zako  simu  kupitia  barua  pepe  yengu : mungwakabili@gmail.com.

Kwa  maelezo  zaidi  kuhusu kitabu  hiki  na  mambo mengine  kuhusu  ulimwengu  usio onekana. Nitembelea  :  www.mungwakabili.blogspot.com

Aeshi asema yeye ni mmoja wa wabunge waliotishwa na Mkuu wa Dar es Salaam

0
0
Mbunge wa Sumbawanga Mjini (CCM), Aeshi Hillaly amesema yeye ni mmojawapo wa wabunge waliotishwa na Mwenyekiti wa Ulinzi na Usalama wa Mkoa wa Dar es Salaam ,Paul Makonda  mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni.

Amesema hayo leo wakati akichangia hotuba ya bajeti waziri mkuu na taasisi zake kwa mwaka 2017/18.

Amesema yuko tayari kutoa ushahidi ukihitajika na kwamba anaogopa kwenda mkoa huo hivi sasa ingawa anapatamani.

Hussein Bashe awataka wabunge wa CCM Waache Unafiki.....Kasema Yupo Tayari Kufukuzwa hata Uanachama wa CCM

0
0
Mbunge wa Nzega Mjini(CCM) Hussein Bashe amewataka wabunge wa CCM  kuacha unafiki kuhusu kuwateka watu na kwamba yeye ni mmoja wa watu waliokamatwa  na usalama wa taifa wakati wa mkutano Mkuu wa CCM.

"CCM acheni unafiki mimi nimeshakamatwa na watu wa usalama mnasema hawakamati, kwa hili nipo tayari mniondoe kwenye chama". Amesema Bashe

Bashe alikuja juu baada Waziri wa Tamisemi, George Simbachawene kumtaka Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe kuthibitisha kuwa matukio ya ukamataji yanafanywa na usalama wa Taifa

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images