Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

VIDEO: Godbless Lema Afunguka Maneno Mazito Bungeni......Kaomba Walau Kila Mbunge Afungwe Miezi Minne ili Waone Karaha Yake

$
0
0
Jana mkutano wa saba wa bunge uliendelea ambapo wabunge walikuwa wakijadili mapitio ya mapato na matumizi ya fedha za ofisi ya Waziri mkuu na ofisi ya bunge kwa mwaka wa fedha 2017/2018

Kati ya Wabunge waliopata nafasi ya kusimama ni pamoja na mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema, ambaye alisimulia jinsi alivyotupwa selo miezi minne gerezani huku dhamana yake ikiwa wazi.

==>Msikilize hapo chini akiongea

Hussein Bashe Afunguka Sakata la Kutekwa Msanii Roma Mkatoliki

$
0
0
Jana usiku taarifa za kukamatwa kwa msanii wa hip hop Roma Mkatolikia zilianza kuenea katika mitandao ya kijamii kwa kuripotiwa kuwa Roma Mkatoliki na Moni wakiwa studio za Tongwe Records walikuja kukamatwa na watu wasiojulikana na kuwapeleka kusikojulikana.

Watu mbalimbali ikiwemo wasanii mbalimbali wamekuwa wakionesha hisia zao juu ya tukio hilo kwa kutumia kurasa zao za mitandao ya kijamii kuoneshwa kuguswa na tukio hilo, mbunge wa Nzega Hussein Bashe ni miongoni mwa watu waliyotumia kuraza zao za instagram kuandika anachowaza kuhusu Roma.

"Who is behind all this? Ni genge ambalo limejipa mamlaka ya kupandikiza woga na chuki miongoni mwa jamii na kuharibu Taswira ya CCM. Tunawajibu wa kukataa woga ,Tunawajibu wa kutoruhusu Misuse ya vyombo vya Ulinzi na usalama, Tunawajibu wa kulinda Taifa letu

“Tunawajibu wa kupigania Values zilizopiganiwa na waasisi wa Taifa letu kama Mzee Karume na Mwl Nyerere, Tunawajibu wa kukataa ukandamizaji tukikaa kimya kwa kufikiri kuwa hayanihusu mimi yanamhusu yule yatakapokufika wewe hatakuepo mtu wa kukutetea na halitakuepo Taifa la Tanzania

“Sote tusimame tuseme hapana kwa mfumo huu unaoanza kuota mizizi kama mtu Ana makosa ufuatwe utaratibu wa kisheria kumkamata na sio utekaji tunakabiliwa na vita kubwa ya kupambana na Umasikini na kujenga Taifa huru la kiuchumi . 

"Umasikini ni hatari kwa usalama wa taifa sio nyimbo
#FreeRoma"
Who is behind all this? Ni genge ambalo limejipa mamlaka ya kupandikiza woga na chuki miongoni mwa jamii na kuharibu Taswira ya CCM. Tunawajibu wa kukataa woga ,Tunawajibu wa kutoruhusu Misuse ya vyombo vya Ulinzi na usalama, Tunawajibu wa kulinda Taifa letu, Tunawajibu wa kupigania Values zilizopiganiwa na waasisi wa Taifa letu kama Mzee Karume na Mwl Nyerere, Tunawajibu wa kukataa ukandamizaji Tukikaa kimya kwa kufikiri kuwa hayanihusu mimi yanamhusu yule yatakapokufika wewe hatakuepo mtu wa kukutetea na halitakuepo Taifa la Tanzania. Sote tusimame tuseme hapana kwa mfumo huu unaoanza kuota mizizi. Kama mtu Ana makosa ufuatwe utaratibu wa kisheria kumkamata na sio utekaji. Tunakabiliwa na vita kubwa ya kupambana na Umasikini na kujenga Taifa huru la kiuchumi . "Umasikini ni hatari kwa usalama wa taifa sio nyimbo". #FreeRoma
A post shared by Hussein Mohammed Bashe (@bashehussein) on

Nape Nnauye Amlilia Roma Mkatoliki

$
0
0
Ikiwa leo ni siku ya pili tangu ilipotolewa taarifa kuwa msanii Roma Mkatoliki alitekwa na watu wasiojulikana akiwa pamoja na Moni Centrozone, mtayarishaji wa muziki wa Tongwe Records, Bin Laden katika studio za Tongwe Records, Waziri wa zamani wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye amemlilia msanii huyo.

Nape emetoa kilio chake kupitia ukurasa wake wa Twitter, akitumia maneno matatu pekee yanayosomeka kwa hisia za ndani kuwa ni mtu anayemlilia mpendwa wake.

“Roma! Oooooh No!” ametweet Nape.


Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa jana na uongozi wa Tongwe Records, watekaji walifika katika studio hizo na kuwahoji waliokuwepo, kisha kuondoka nao wote pamoja na baadhi ya vifaa vinavyotumika kurekodia muziki, kwenda kusikojulikana.

Mke wa Roma, Nancy ameeleza kuwa alifika katika vituo kadhaa vya polisi jijini Dar es Salaam kuulizia taarifa za mumewe, lakini alielezwa kuwa taarifa za Roma hazikuwepo.

Akizungumza kwa uchungu kwenye vyombo mbalimbali vya habari, Nancy aliwaomba Watanzania kwa ujumla pamoja na vyombo vya usalama kusaidia kufahamu alipo mumewe.

Leo mchana, wasanii wamekutana katika studio za Tongwe Records kwa lengo la kuzungumzia suala hilo zito ambalo limevunja mioyo ya wadau wa muziki, familia na ndugu wa Roma na wenzake.

Idriss Sultan Amwangua Rais Magufuli Sakata la Roma Kutekwa

$
0
0
Baada ya msanii wa muziki Roma Mkatoliki kupotea katika mazingira ya kutatanisha akiwa katika studio ya Tongwe Records wasanii mbalimbali wameonesha kuguswa na kuamua kutumia mitandao yao ya kijamii kuonesha masikitiko yao.

 Leo April 7 kupitia mtandao wa Instagram Idriss Sultan alikua na haya ya kusema,

"Hawa ni wasanii na ni maarufu, sitamani kujua ni wangapi tusiowajua waliopotea katika mfumo kama huu. Nina hofu sio kwa maisha yangu na uhuru wangu ila kwa kaka, dada, watoto, baba, mama na ndugu , wake, waume, na wapenzi wa watanzania wenzangu wasio na sauti niliyo nayo mim.

"Mwenyezi Mungu hakunipa nilichonacho ili niishie kupimisha misuli na wenzangu nani zaidi, watu kama mimi ndio wa kwenda motoni haraka zaidi tukishaulizwa ulifanyia nini ulichopewa. Raisi Magufuli, waziri Mwakyembe na Mkuu wa mkoa Makonda nina imani hili lipo mezani kwenu naombeni mlitolee tamko zaidi ya “Uchunguzi unafanyika

"Pia mlivalie njuga kuwapata ndugu zetu ili kutuliza amani ya hii nchi iliyopiganiwa iliyokuzwa kwa upendo na amani ya juu kabisa. We can’t call it the land of peace wakati ukilala hujui kama utaaamka sehemu unayoijua na ukiwa hata na hali yako ya kiafya ile ile.

"Leo ni Roma na Moni, kesho ni nani ? Kamanda Sirro sijasahau kabisa usalama wa huu mji upo mikononi mwako. Wake za hawa wawili wanaongea na watoto wao wanawaambia baba yupo ila amesafiri anarudi kesho. Kesho isipofika basi inshaallah tutajua Tanzania yetu ni nchi ya aina gani. Hata Mungu simuachii hili hatujalishindwa bado"
Hawa ni wasanii na ni maarufu, sitamani kujua ni wangapi tusiowajua waliopotea katika mfumo kama huu. Nina hofu sio kwa maisha yangu na uhuru wangu ila kwa kaka, dada, watoto, baba, mama na ndugu , wake, waume, na wapenzi wa watanzania wenzangu wasio na sauti niliyo nayo mimi. Mwenyezi Mungu hakunipa nilichonacho ili niishie kupimisha misuli na wenzangu nani zaidi, watu kama mimi ndio wa kwenda motoni haraka zaidi tukishaulizwa ulifanyia nini ulichopewa. Raisi Magufuli, waziri Mwakyembe, waziri Mwigulu na Mkuu wa mkoa Makonda nina imani hili lipo mezani kwenu naombeni mlitolee tamko zaidi ya "Uchunguzi unafanyika" na pia mlivalie njuga kuwapata ndugu zetu ili kutuliza amani ya hii nchi iliyopiganiwa iliyokuzwa kwa upendo na amani ya juu kabisa. We can't call it the land of peace wakati ukilala hujui kama utaaamka sehemu unayoijua na ukiwa hata na hali yako ya kiafya ile ile. Leo ni Roma na Moni, kesho ni nani ? Kamanda Sirro sijasahau kabisa usalama wa huu mji upo mikononi mwako. Wake za hawa wawili wanaongea na watoto wao wanawaambia baba yupo ila amesafiri anarudi kesho. Kesho isipofika basi inshaallah tutajua Tanzania yetu ni nchi ya aina gani. Hata Mungu simuachii hili hatujalishindwa bado #FreeRoma #FreeMoni
A post shared by Idris Sultan 🇹🇿 (@idrissultan) on

Kamanda Siiro Afunguka kuhusu kupotea kwa Msanii Roma Mkatoliki

$
0
0
Kamishna wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es salaam, Simon Sirro amesema kuwa tayari wameshapata taarifa za kupotea kwa Msanii wa Bongo Fleva hapa nchini, ‘Ibrahim Mussa’ maarufu kwa jina la Roma Mkatoliki na kuongeza kuwa tayari timu yake ya upelelezi imeshaanza kazi.

Ameyasema hayo mapema hii leo wakati akizungumza na Katibu wa Chama cha Wanamziki wa Kizazi Kipya Tanzania, Samweli Mbwana alipotaka kujua kama Jeshi la Polisi lina taarifa ya kupotea kwa mwanamziki huyo.

Sirro amesema kuwa taarifa za kupotea kwa msanii huyo tayari wameshazipata na Jalada la upelelezi tayari limeshafunguliwa kwa ajili ya upelelezi.

Ameongeza kuwa timu yake ya upelelezi iko mtaani kwa ajili ya kujua kinachoendelea, na amewaomba wasanii na baadhi ya watu kutokuwa wepesi wa kusambaza uvumi usiokuwa na ukweli ndani yake.

“Jamani mambo ya uvumi yaacheni, sio kitu kizuri unamvumishia mtu kitu ambacho hakijui na wengine wanasema kuwa Serikali inahusika kitu ambacho si cha kweli”,amesema Kamanda Sirro.

Aidha, Sirro amesema kuwa amepanga kukutana Waandishi wa Habari kesho saa tano Ofisini kwake ili kuweza kutoa ripoti kamili kuhusu kupotea kwa msanii huyo wa Bongo fleva kwani timu ya upelelezi tayari iko kazini.

Hata hivyo, amewatoa hofu wasanii na wananchi kwa ujumla kwamba suala hilo linafanyiwa kazi, hivyo hakuna haja ya kuogopa na kuendelea kuvumisha vitu visivyokuwa vya msingi.

Kisukari Ni Ugonjwa Unao Weza Kudhibitiwa Kwa Kutumia Tiba Asilia

$
0
0
Kisukari  ni  tatizo  la  kiafya  linalo wasumbua  na  kuwatesa  mamilioni  ya  watu  duniani. Miongoni  mwa  dalili  za  ugonjwa  wa  kisukari ni pamoja  na

i. Kukojoa  mara  kwa  mara  ( Watoto kukojoa  kitandani )

ii.Kunywa maji mengi kuliko kawaida na kusikia kiu kila wakati.

iii.Kuwa dhaifu, kukosa nguvu na kujisikia mchovu kila wakati.

iv.Kupungua uzito  kwa  kasi  au kukonda pamoja na kwamba unakula  vizuri  tena kila  wakati  kwa  sababu  ya  kusikia  njaa kila  wakati  kunakosababishwa  na  maradhi  ya  kisukari

v.Wanawake  kupatwa  na  tatizo  la kuwashwa ukeni.

vi.Kupoteza  uwezo  wa Kuona  vizuri.

vii.Wanaume  kupatwa  na  tatizo  la  ukosefu na / ama  upungufu  wa  nguvu  za  kiume  na  wanawake  kukosa  hamu  ya  tendo  la  ndoa.

viii.Kupatwa  na  ganzi,  kusikia  hali  ya  kama  kuchomwachomwa au kutohisi chochote  pindi  unapoguswa  kwenye  sehemu za miguu, viganjani na  kwenye  vidole.

ix.Miguu kuoza na hata kupata gangrini.

x.Kukaukwa na ngozi na pia kupata aina ya ngazi katika miguu.

xi.Vidonda au majeraha sehemu yoyote ya mwili kutopona haraka.

xii.Kutokwa  na   Majipu kwenye  sehemu  mbalimbali  mwilini.

Kwa  mujibu  wa  tafiti mbalimbali  za  kitaalamu , watu walio katika makundi yafuatayo  wapo katika  hatari  kubwa  ya  kupatwa  na  ugonjwa wa kisukari kuliko watu wengine.  Watu  hao  ni  kama  ifuatavyo :

i. Watu  wenye   uzito uliozidi,

ii.Watu  wanao  toka  katika  familia  zenye  historia  ya  kuwa  na  wagonjwa  wa  kisukari.

iii.Wanawake waliozaa watoto wenye kilo 4 au zaidi,

iv. Watu   wasio  fanya  mazoezi

v. Wagonjwa  wa  shinikizo la damu,

vi.Watu wenye  kiasi  kikubwa  cha  lehemu  mbaya  ( Bad  Cholestrol ) kwenye  damu.

vii.Watu  wenye   virimba  tumo (  vitambi):  Wataalamu  wa  afya  wanaeleza  kuwa, kuna hatari kubwa ya kupatwa na maradhi  ya  kisukari ikiwa mtu ana mafuta mengi katika tumbo na kiuno chake kuliko katika mapaja yake. Mafuta katika kongosho na ini huvuruga uwezo wa mwili wa kudhibiti kiasi cha sukari kwenye damu

viii.Watu  wenye msongo wa mawazo na

ix.Watu  wanao tumia  pombe  na kupita  kiasi  pamoja  na  wale  wavutaji  wa  sigara  kupita  kiasi: Wavutaji wa sigara wanakabiliwa na hatari kubwa zaidi ya kupatwa  na  tatizo  la  kisukari,kwani kwa  mujibu  wa  tafiti  mbalimbali za  kitaalamu, uvutaji  sigara huathiri  moyo na mfumo wa mzunguko wa damu na kubana mishipa ya damu.  Tafiti  mbalimbali  za  kiafya  zinaeleza  kwamba asilimia 95 ya watu wanaougua kisukari ambao hulazimika kukatwa viungo ni wavutaji wa sigara.

x. Kundi  jinginge  la  watu  walio  katika  hatari  ya  kupatwa  na  maradhi  ya  kisukari  ni  watu wenye  umri  mkubwa  kuanzia  miaka  55  na  kuendelea

Wataalamu  wa  afya  wanashauri  watu walio  kwenye   orodha  iliyo  tajwa  hapo  juu, kujiwekea  utaratibu  wa  kuwa  wanapima  afya  zao  walao  mara  moja  kila  mwakaili waweze  kuchukua  hatua  stahiki  za  kiafya endapo  watakutwa  na  tatizo  la  sukari.
TIBA   ASILIA   KWA   WAGONJWA   WA  KISUKARI
Zipo  tiba  asilia  mbalimbali  zinazo  saidia  kkupunguza  maradhi  ya  kisukari. Miongoni  mwa  tiba  hizo  ni  pamoja  na  tiba  ijulikanayo  kama  Mkatasukari. Tiba  hii  inasaidia kushusha  na  kudhibiti  kiwango  cha  sukari  kwa  mgonjwa mwenye  sukari  ya  kupanda. Kama  unasumbuliwa na  maradhi  ya  kisukari ( Sukari  ya  kupanda ), unaweza  kujaribu  kutumia  tiba  hii.

JINSI   YA   KUANDAA  TIBA  ASILIA  YA  MKATASUKARI

Mahitaji  ;
i. Nanasi  moja  kubwa

ii. Majani  ya  chai  vijiko vitatu vya  chakula

iii. Maji  lita  tano

iv. Dawa asilia  ya  Mkatasukari  vijiko  vikubwa  vitatu.

MATAYARISHO:  Chukua  nanasi  lako  lililo  iva  vizuri, limenye  kisha  likate  vipande  vidogo vidogo,  kisha  liweke  kwenye  sufuria  halafu ndani  ya  sufuria  hilo, ongeza  lita  tano  ya  maji  safi.  Baada  ya  hapo  weka  majani ya  chai vijiko  vikubwa  vitatu, kisha  ongeza  vijiko  vikubwa vitatu  vya  dawa asilia  ya  Mkatasukari, kisha  chemsha  kwa  muda  wa  dakika  thelathini (30).

Baada  ya  dakika  thelathini, ipua   na  uchuje, makapi  weka  pembeni, kisha  hifadhi  kimiminika  chako  kwenye  chombo  safi.

MATUMIZI  :
Tumia  kunywa  kikombe  kidogo chenye ujazo milimita  mia  mbili  na  hamsini  ( 250 mills ) au  robo  lita  kwa  lugha  nyepesi. Utafanya  hivyo  mara  tatu  kwa  siku, asubuhi  mchana  na  jioni  hadi  dozi  yako  itakapo  kamilika.

Baada  ya  kutumia  dozi  hii, unashauriwa  kwenda  hospitali  kupima   tena  sukari  ili  ujue  sukari  yako  imeshuka  kwa  kiasi  gani  pamoja  na  kupata  ushauri  wa  daktari  wako.

Kwa  mahitaji  yako ya  tiba  asilia  ya  Mkatasukari, fika  katika  duka  la  NEEMA  HERBALIST. Tunapatikana  UBUNGO  jijini  DAR ES  SALAAM,  jirani  na  SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING  nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA.

Kwa wateja  wetu  waliopo  jijini DAR  ES  SALAAM, ambao  hawawezi  kufika  ofisini kwetu., tunatoa  huduma  ya  kuwapelekea  dawa  mahali  walipo  ( HOME & OFFICE  DELIVERY ), kwa  wateja  waliopo  Zanzibar  watasafirishiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa  boti, kwa  wateja  waliopo  mikoani  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa  mabasi mbalimbali. Wateja  waliopo NAIROBI  na  MOMBASA  watatumiwa  dawa  kwa  njia ya  usafiri  wa  mabasi  mbalimbali.

Na  kwa  wateja  waliopo  UGHAIBUNI  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  au  DHL.

Wasiliana  nasi  kwa  simu  namba  0766  53 83 84

Na  kwa  taarifa  zaidi  kuhusu  huduma  zetu, tutembelee  kila  siku  katika  blogu  yetu ;

VIDEO: Wasanii Wakutana Coco Beach......wapaza Sauti Na Kuiomba Serikali Ihakikishe Roma Anapatikana

$
0
0
Wasanii wa muziki wa Bongo Fleva nchini kwa pamoja wameungana na  kuviomba vyombo vya usalama nchini kufanya juhudi za kumtafuta msanii mwenzao ROMA Mkatoliki na wenzake wanaodaiwa kutekwa na kupelekwa kusikojulina.

Wasanii hao, leo wamekutana  COCO Beach na kulaani kitendo cha Roma kutekwa, huku wakiitaka serikali iwasaidie kumtafuta na kumpata akiwa salama.

==> Hii ni video ya mazungumzo yao na vyombo vya habari leo

Taarifa ya Wizara ya Habari kuhusu kutoweka kwa Roma Mkatoliki

$
0
0
Serikali kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, sanaa na Michezo imesema imepokea kwa mshtuko taarifa za kutoweka kwa Mwanamuziki Ibrahim Mussa kwa jina la kisanii “Roma Mkatoliki”  tangu tarehe 5 Aprili 2017.

Katika taarifa yake iliyotolewa  jana jioni na kusainiwa na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa wizara Zawadi Msalla, alisema kuwa wizara hiyo kwa dhamana yake katika tasnia ya sanaa, imefuatilia kwa karibu suala hilo kwa kuwa lina muelekeo wa jinai na kwamba hashikiliwi katika kituo chochote cha polisi.

"Hata hivyo taarifa kutoka vyombo vya dola zinathibitisha kuwa Roma Mkatoliki hashikiliwi katika kituo chochote cha polisi".Alisema Zawadi.

Alisema kutokana na hali hiyo, wizara imewaomba wadau mbalimbali na wananchi kwa ujumla kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi kwa kutoa taarifa zozote zitakazo saidia kujua alipo msanii huyo.


Wema awalaumu waigizaji Sakata la Roma.......Ray Amtolea Uvivu na Kumjibu

$
0
0
Baada ya wasanii Roma Mkatoliki, Moni pamoja na wenzao kuchukuliwa na watu wasiofahamika tangu usiku wa kuamkia juzi  wasanii mbalimbali wamekuwa wakitumia kurasa zao za mitandao ya kijamii kupost juu ya kusikitshwa na kitendo hicho, Wema Sepetu akiwa moja kati yao.

Lakini post ya Wema Sepetu ambayo aliiandika kupitia ukurasa wake wa Instagram imeonesha kutokumfurahisha muigizaji mwenzake Ray Kigosi ambaye amepost pia katika ukurasa wake wa instagram na kueleza kutokufurahishwa na namna Wema alivyoandika kuhusu ishu hiyo.

==> Wema Sepetu aliandika hivi;
"This Is Scary… Ni Janga kubwa sana kwa wasanii, kwa wananchi na Kwa Taifa letu kiujumla… Kinachonishangaza ni kuona baadhi ya wasanii wa Bongo movie wamekazana kupost eti wapo kwa Mkuu wa mkoa wakiongelea WaKorea na Waphilipino…. Mlikumbuka kumuuliza Mheshimiwa alipo Roma na Moni…??? Au ndo mambo ya kila mtu anaangalia lake…. 

"Au labda mpaka atekwe msanii wa Bongo movie pia ndo akili itatukaa sawa…??? Oh God help Us Please… Lakini pia wala sitoshangaa hata kama akitekwa msanii wa bongo movie hakuna atakaehangaika within Us zaidi ya wananchi peke yao na watu wetu wa karibu… Tumejawa sana Unafki…!!! All in All namuonea sana huruma Nancy…. 

"Our prayers are with u mama… Inshallah mumeo atapatikana… Tuzidi kumuomba Mungu…..🙏🏼🙏🏼🙏🏼…. Kabla sijasahau, Tuwage tuna hata fikra za kujua tupo kwenye wakati gani na tupost vitu gani….!!! Yaani mtu kapotea siku ya pili mko busy na kupost Wakorea na Waphilipino…?? 🙄🙄🙄 SMH.. "
This Is Scary... Ni Janga kubwa sana kwa wasanii, kwa wananchi na Kwa Taifa letu kiujumla... Kinachonishangaza ni kuona baadhi ya wasanii wa Bongo movie wamekazana kupost eti wapo kwa Mkuu wa mkoa wakiongelea WaKorea na Waphilipino.... Mlikumbuka kumuuliza Mheshimiwa alipo Roma na Moni...??? Au ndo mambo ya kila mtu anaangalia lake.... Au labda mpaka atekwe msanii wa Bongo movie pia ndo akili itatukaa sawa...??? Oh God help Us Please... Lakini pia wala sitoshangaa hata kama akitekwa msanii wa bongo movie hakuna atakaehangaika within Us zaidi ya wananchi peke yao na watu wetu wa karibu... Tumejawa sana Unafki...!!! All in All namuonea sana huruma Nancy.... Our prayers are with u mama... Inshallah mumeo atapatikana... Tuzidi kumuomba Mungu.....🙏🏼🙏🏼🙏🏼.... Kabla sijasahau, Tuwage tuna hata fikra za kujua tupo kwenye wakati gani na tupost vitu gani....!!! Yaani mtu kapotea siku ya pili mko busy na kupost Wakorea na Waphilipino...?? 🙄🙄🙄 SMH...
A post shared by Wema Sepetu (@wemasepetu) on


==>Ray Kigosi  hakuipenda post hii, hivyo akajibu;
NAFIKIRI NI VEMA MTU KUELEZA HISIA ZAKE JAPO SIO BUSARA KWA MWENYE HISIA HIZO KUZIELEZA BILA WEREDI NAWASIHI WASANII WENZANGU KUPOTEA KWA ROMA ISIWE SABUNI YA KUTAKATISHA UCHAFU WA MTU SOTE TUMESIKITISHWA NA JAMBO HILO NA TUMEONYESHA KWA VITENDO. MIMI NIMEPOST INSHU YA ROMA TANGU JANA USIKU WEMA SEPETU WEWE ULIKUWA HUJAPOST CHOCHOTE TUSEME ULIKUWA HUNA UCHUNGU? ALAFU LEO UNAANDIKA KUWA BONGO MOVIE HAWAPO PAMOJA NA TUKIO LA ROMA HUKU NI KUTUGOMBANISHA NA WANANCHI WANAOTUAMINI. SISI BONGO MOVIE MARA NYINGI SANA TUNAKUWA PAMOJA KWENYE MATUKIO YA BONGE FLEVA TOFAUTI NA WAO. KAMA UNA UGONVI NA MTU HAYO NI MAMBO YAKO BINAFSI ILA USITUFANYE SISI TUONEKANA WABAYA MBELE YA JAMII UTAKUWA KICHAA KAMA USIPOPATA MAUMIVU KWA TUKIO LA ROMA NIMESIKITISHWA SANA POST YAKO @wemasepetu KAMA UNADHANI HUU NI MUDA MUAFAKA WA KUTAFUTIA POINT KATIKA TUKIO LA ROMA MKATOLIKI UMEFELI HILI NI JANGA LETU SOTE. @wemasepetu #(KINA ROMA WAKO WAPI?).

Maagizo Aliyoyatoa Waziri Nchemba Kwa Polisi Kuhusu Kutekwa kwa Msanii Roma

$
0
0
Msanii wa hip hop Roma Mkatolikia alikamatwa April 5 usiku ambapo taarifa zilianza kuenea katika mitandao ya kijamii kuwa alikamatwa studio za Tongwe Records  na watu wasiojulikana akiwa na wenzake na wakapelekwa  kusikojulikana.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mwigulu Nchemba ambaye ndio anahusika na usalama wa raia, ametumia ukurasa wake wa instagram kuonesha kuguswa na tukio la kutekwa kwa Roma Mkatoliki na Moni.

Waziri Nchemba ameeleza kuwa amewaagiza polisi kufuatilia na kutoa taarifa kwa umma.

“Nimeshtushwa kwa kutokuonekana kwa Msanii Roma na Wenzake mpaka sasa. Nimeshtuka zaidi nilipofuatilia na kuambiwa hakuna kituo chochote cha polisi kinachowashikilia. Nimeelekeza Polisi wafuatilie kwa karibu kujua undani wa tukio hili na hatima yao na kutoa taarifa kwa umma”

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya April 8

Je, Umeathiriwa na Punyeto Kiasi cha Kushindwa Kurudia Tendo la Ndoa???.....Bofya Hapa Kupata Tiba, Pia Tuna Handsome Up ya Kuongeza Maumbile

$
0
0
NATURAL BEAUTY COSMETIC ni kampuni inayotoa bidhaa ORIGINAL zenye matokeo mazuri bila kemiko wala madhara yoyote. Pata punguzo la bei kwa bidhaa hizi. 
 
1.HANDSOME UP ni kifaa kinachoongeza maumbile ya kiume  kwa 99% kwa size uipendayo wewe na kuimarisha misuli ya uume kwa @170,000/= tuu. 
 
2.MEN GELY kupaka. Hii inaongeza kwa wastani wa inch 6.5 na inapatikana kwa @120,000/=.  
 
3. MAX MAN 2. Ni vidonge kwa ajili ya nguvu ambavyo vinasaidia sana hata kwa watu wenye kisukari na waliokua wakifanya sana masturbation. Pia huongeza hamu ya tendo la ndoa kwa @130,000/=tu.     
 
Tupo DAR ES SALAAM  kariakoo na kinondoni kanisani.

Kwa mawasiliano zaidi piga  0759029968 au 0659618585.
Popote ulipo utapata huduma zetu.
 
Follow us
@natural2162
@natural2162
@natural2162
@natural2162
 
     Bidhaa zetu zote ni garantii na unapewa risiti
              Karibu

SORRY MADAM -Sehemu ya 47 & 48 (Destination of my enemies)

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWAILIPOISHIA

ILIPOISHIA
Rahab akamtazama raisi Praygod na kumkumbatia, wote wakajikuta wakimwagikwa na machozi, jambo lililo wafanya makachero wengine kuwa katika hali ya simanzi iliyo changanyikana na furaha.

Gafla Rahab akaanza kuisikia milio ya risasi masikioni mwake, alipo nyanyua kichwa chake akawaoa makachero walio mpiga risasi kwenye handaki. Macho yake gafla yakabadilika na kuzidi kuwa mekundu,  akamsukuma raisi Praygod pembeni na kumrukia kachero mmoja aliye mpiga risasi, akambwaga chini na kuanza kuliminya koo la kachero aliyeanza kutapatapa akijitahidi kuutoa mkono mmoja wa Rahab ulio mkaba shingoni

ENDELEA
  Kwa haraka makachero wakaanza kumtoa Rahab juu ya mwili mwa kachero anaye kabwa koo. Japo ni wanaume wa nguvu ila kijasho kilianza kuwamwagika kutoka na jinsi Rahab anavyo washinda nguvu.

Zoezi la kumtoa Rahaba likafanikiwa. Japo kachero aliye nusurika kuyaonja mauti hali yake kidogo ni mbaya. Hapakuwa na mtu aliye weza kuelewa ni kitu gani ambacho kimepata mke wa raisi. Kila mmoja akatokea kumuogopa sana Rahab, hata raisi Praygod mwenyewe hakusubutu kumsogelea karibu mke wake.

 “Madam”
Priscar aliita kwa mara nyingine tena ila safari hii hakudhubutu kusogea karibu na Rahab, aliye geuza shingo yake na kumgeukia na kumtazama. Gafla Rahab akapoteza nguvu za miguu na kuanguka chini, akapoteza fahamu.

 ***
Japo Eddy ana uwezo wa kupambana ila si kwa idadi kubwa ya vijana wa Kijapan walio mzinguka na kumuweka kati huku kila mmoja wao akiwa na silaha ya kisu mkononi mwake.

Vijana hao wanao onekana ni wahuni wa mtaani wakatulia wakimtazama Eddy, huku baadhi yao wa nyuma wakianza kumpisha kiongozi wao akisogea mbele taratibu. Kiongozi wao ni jitu moja refu lililo jazia misuli kifuani mwake pamoja na mikononi, kwa kimo cha Eddy anamfikia mtu huyo maeneo ya kifuani na kumlazimu Eddy kunyanyua sura yake juu ili kuweza kumtazama vizuri mtu huyo.

“Wewe ni NSS(Nation Securty Service)?”
Kiongozi wao huyo alimuuliza Eddy kwa kingereza, huku likikunja kunja vidole vyake vilivyo komaa.
“Hapana”
“Umefwata nini wewe mbwa mweusi?”
Eddy akatabasamu kisha akapiga hatua moja mbele kulisogelea jitu hilo karibu kabisa na sehemu alipo simama.
“Nimekufwata wewe mbwa Malaya wa kike”
“Nini……..!!!”
Jibu hilo likamkasirisha jamaa huyo, akamshika Eddy maeneo ya mabegani, akamnyanyua juu kama futi tano na kumsukumia chini. Wapambe wake wakataka kumvamia Eddy ila likawazuia ili apambane mwenyewe.

Eddy akapunguza uzito wa koti alilo livaa, akabakiwa na tisheti nyeusi iliyo mbana vizuri mwilini mwake na kulichora vizuri umbo lake la mazoezi. Akarudi hatua mbili nyuma, akavuta kasi ya kulivamia jitu hilo. Hata kabla hajalifikia akarudishwa na teke zito la kifua lililo mrusha kurudi alipo toka.
Wapambe wa jitu hilo hawakusita kushangilia kwa kitendo alicho kifanya mkuu wao. Eddy akajizoa zoa chini alipo anguka akajipanga tena kwa mashambulizi, akalitazama jitu hilo kuanzia chini hadi juu, kisha akakunya ngumi na kujiweka sawa.

Jitu hilo likaanza kurusha makonde ambayo Eddy alijitahdi kuyakwepa kwa maana endapo konde moja kitampata mwilini mwake ni sawa yeye akimpiga jitu hilo ngumi sehemu moja ya mwili si chini ya kumi tena mfululizo.

Kadri jinsi jitu hilo lilivyo zidi kurusha ngumu ndivyo jinsi Eddy alivyo zidi kujitahidi kumkwepa hadi jitu hilo likaanza kuchoka, na jasho jingi likaanza kumwagika. Ikawa ni kazi kwa Eddy kujipatia maujiko kama wasemavyo watoto wa mtaani. Kwa maana alizitambua sehemu zenye udhaifu kwa jitu hilo. Ngumi iliyo komaa kwa mazoezi makali ya miezi mingi ya nyuma, ikaanza kutua kwenye viungio vya mikono vya jamaa huyo.

   Kila lilipo jaribu kurusha ngumu ili mradi amfikie Eddy, ila ndivyo jinsi lilivyo zidi kupiga sehemu ya viungio vya mikono yake hadi ikafikia hatua likashindwa kabisa kurusha mikono yake. Likamlazimu kutumia mateke, ila hali ikawa ni hiyo hiyo, kila alipo rusha teka basi alijikuta akipigwa teke kwenye viungio vya miguu yake, taratibu likaanza kuyumba. Wapambe wake wakajikuta wakikaa kimya wengi wao wakiwa hawaamini kwamba kiongozi wao ndio huyo anaye pigika kama mtoto mdogo. Kwa mwili mkubwa wa jamaa hili likajikuta likipiga magoti yote mawili chini, huku likiwa limeorojeka twipwili tipwili.

“Ahaaaaa”
Jamaa hilo lilijikuta likipiga mayowe, huku likifumba macho, baada ya kuiona ngumu nzito ikija kuharibu pua yake. Likasubiria kwa sekunde kadhaa ngumi hiyo kutua kwenye pua yake ili isambaratike, ila haikuwa hivyo, taratibu likafumbua macho na kukutana na ngumi hiyo ikiwa imemsogelea karibu kabisa na uso wake.

“Nikubamize?”
Jitu hilo likatingisha kichwa huku woga mwingi ukiwa umemjaa, Eddy akaishusha ngumi yake, wapambe wote wakawa kimya wakikosa cha kuzungumza. Taratibu jitu hilo likainamisha kichwa chini likaishiria kwamba limemkubali Eddy. Wapambe wake nao wote wakapiga magoti na kuinamisha vichwa vyao chini wakimpa heshima Eddy.
Eddy akatabasamu kisha akaelekea alipo libwaga koti lake, akaliokota na kulikung’uta vumbi kisha akalivaa vizuri. Akaanza kupita katikati yao kabla hajawamaliza akasikia sauti ikimuita.
“Heei usiondoke kiongozi”
Jitu lile lilimsemesha Eddy kwa heshima kubwa.
“Kama hutojali tunakuomba tulifahamu jina lako”

Eddy akageuka na kulikukuta jitu hilo likisaidiwa na wapambe wake kunyanyuka kutoka chini.
“Unahitaji kulijua jina langu?”
“Eddy alizungumza huku akilifwata jitu hilo”
“Ndio”
Lilizungumza kwa kuto kujiamini sana.
“Black Shadow ndio jina langu”
“Mimi naitwa Sabogoo. U…uu unakwenda wapi?”
“Sina makazi popote mimi ninaishi”
“Basi twende kwangu ni jirani na hapa”
Sabogoo alizungumza huku akiachia tabasamu pana dharau zote alizo kuwa nazo zimeyanyuka kama barafu, heshima ikachukua nafasi yake juu ya Eddy.
                                                                                                  ***
  Kazi ya kumbembeleza Sa Yoo, ilichukua masaa kadhaa, hadi akaukubali ukweli kwamba bibi yake kipenzi amefariki dunia. Kwa tamaduni za Kijapan, endapo kunatokea msiba basi nyumbani kwamfiwa ama ndugu wa mfiwa. Kutaandaliwa sehemu maalumu ambayo watu watahudhuria kumpa pole mfiwa huku picha kubwa ya marehemu iliyo pambwa kwa maua pamoja na kuwashiwa ubani pembei yake. Ikiwa katika eneo hilo.

  Hivyo ndivyo ilivyo kuwa kwa Sa Yoo. Alirudi nyumbani akiwa ameongozana na Shamsa pamoja na dakari. Shamsa akajikuita akiwa na majukumu ya kuwa karibu sana na Sa Yoo. Urafiki wao wa muda mfupi tu, walijikuta kila mmoja akimpenda mwenzake hadi baadhi ya watu ambao ni watu wa karibu na Sa Yoo, wakabaki wakiwa wanamshangaa Shamsa kwani hawakujua ni wapi ametoke na ni nani katika familia ya Sa Yoo. Kwani Shamsa aliketi jirani kabisa na Sa Yoo na kila sehemu ambayo Sa Yoo alikwenda basi Shamsa yupo nyuma yake.

    Msiba ukachukua siku kadhaa hadi kumalizika. Kutokana Shamsa alisha zoeana na Sa Yoo, ikawalazimu kuishi pamoja katika nyumba ambayo Shamsa amepangishiwa kwa ajili ya mapumziko yake. Furaha ya urafiki ikazidi kutawala kati yao, Sa Yoo akazidi kumtembeza Shamsa sehemu mbali mbali ndani ya Japan. Walitembelea sehemu nyingi za vivutio vya asili na vilivyo tengenezwa na binadamu.
“Hivi Shamsa huwa unapendelea kutazama mchezo wa mapambano?”
Sa Yoo alimuuliza wakiwa ndani ya gari lao wakirudi kutoka kwenye jengo la mauonyesho ya mashujaa walio pigana vita ya kwanza na yapili ya dunia.
“Ndio napenda kutazama”

“Basi leo usiku tutaelekea kwenye ukumbi mmoja unaonyesha mapambano ya ulingoni”
“Sawa ila hakuna fujo?”
“Hapana hakuna fujo kila kitu huko kina ulinzi wa kutosha. Tena ngoja tupitie kwenye ukumbi huo tununue tiketi mapema za kwenda kwenye maonyesho”
“Hakuna tatizo”
   Ndani ya dakika kumi Sa Yoo akasimamisha gari kwenye moja ya ukumbi mkubwa wenye mapicha picha mengi ya mapambano yatakayo fanyika usiku wa siku hiyo. Idadi ya watu wanao nunu tiketi katika siku hiyo ni kubwa sana.
“Huyu BLACK SHADOW ni nani?”

Sa Yoo alimuuliza  mmoja wa wauzaji wa tiketi baada ya kuona picha kubwa ya mpiganaji huyo, aliye valia kinyago cheusi usoni mwake na kuyaacha macho yake tu.
“Huyu ni mpiganaji mwengine mpya kabisa anazaminiwa na Sabogoo. Nasikia kwamba huyu jamaa ni mkali sana japo sijawahi kumuona na mimi”
Muuza tiketi huyo alizungumza kwa shauku iliyo zidi kuwatamanisha Sa Yoo na Shamsa. Wakanunua tiketi mbili za siti za mbele kabisa kisha wakaondoka kurudi nyumbani wanapo ishi kujiandaa kwa ajili ya usiku.
                                                                                                         ***
     Eddy hakuwa na jinsi ikamlazimu kukubaliana na Sabogo kujiunga katika kikosi chake, ambacho mara nyingi kinajishuhulisha na maswala ya upambanaji wa ulingoni. Eddy kutokana anatafutwa na polisi wa Japani, ikambidi atumie kikundi hicho kama sehemu ya kujihifadhia huku akiendelea na upelelezi wake wa maeneo kuweza kutafuta sehemu ambayo alipaswa kwenda kukutana na mwalimu ambaye angeendelea kumfundisha mafunzo ya upiganaji.
“Ila kabla sijaingia ulingoni na kupambana inabidi tukubaliane mambo mawali”
Eddy alizungumza akiwa na Sabogo kwenye ndani ya ofisi zikiwa zimebakia siku chache kabla mashindano ya kumtafuta mpambanaji wa ulingoni ndani ya Japan hayajaanza.

“Mambo gani tena kiongozi”
“Nahitaji kwa kila pambano munilipe asilimia ishirini ya pesa ambayo nitashinda. Mbili nitahitaji kuwa na mavazi ambayo ni meusi na yenye kinyago cheusi sihitaji sura yangu kuweza kuonekana na watu wa aina yoyote”
“Hayo yote mawili hayana tatizo nakuahidi kiongozi kila jambo litakwenda vizuri, swala la mavazi kuna mwana mitindo nitamuita sasa hivi aje akupime kisha leo leo hii hii mambo yatakwenda safi”

“Sawa”
Sabogo akampigia simu mwanamitindo anaye tengeneza nguo za wapambanaji katika maonyesho hayo makubwa ndani ya Japan. Akaifanya kazi hiyo ndani ya masaa kadhaa ambapo nguo imare za Eddy zikamalizika kutengenezwa huku kinyago chake anacho kivaa kichwani mwake kikimkaa vizuri kabisa hadi mwenyewe akajikubali.
“Unaonekana vizuri kiongozi”
Sabogoo alimsifia Eddy baada ya kumuona akiwa amevalia mavazi hayo, yenye maandishi makubwa mngongoni BLACK SHADOW.
“Huyu jamaa ni mtaalamu sana”

“Ndio maana nikaamua kumpa tenda yeye, na endapo utafanya vizuri basi nguo zako zinaweza kutengenezwa nyingi na kuuzwa kwa watu wa kila rika. Ukajikuta ukiingiza pesa nyingi sana”
“Kweli?”
“Ndio huku kwetu kila jambo zuri basi ni fursa ya kuingiza pesa”
“Basi nitahakikisha ninafanya kazi nzuri kadri ya uwezo wangu”
    Siku iliyo fwata wakaelekea kwenye studio za kupigia picha ambapo, Eddy akapiga picha zipatazo mia moja, akiwa amevalia mavazi yake hayo, na picha hizo zikapelekwa moja kwa moja kwa waandaaji wa mashindano hayo makubwa kwa ajili ya matangazo.

Siku na masaa yuakakatika, watu wengi ndani ya Japan, wakiisubiria siku ya mashindano ya mapambano ya ulingoni. Vituo vingi vya redio na televishion, vikazidi kutangaza juu ya mashindano hayo ambayo yana zawadi kubwa kwa mshindi, ikiwemo mkanda wa dhahabu wenye dhamani ya dola za kimarekani milioni ishirini.

Watu wengi kutoka maeneo mbali mbali ya Japan wakaanza kuingia kwenye ukumbi mkubwa unao ingiza watui zaidi ya laki sita kwa wakati mmoja, tiketi nyingi sana ziliuzwa majira ya asubuhi na mchana, wengi wakiwa na hamu ya kwenda kumuona mpiganaji mpya black shadow, ambaye anadhaminiwa na mpiganaji mbabe Sabogo, ambaye amewashangaza watu wengi sana kuto kushiriki katika mapambano hayo, na kusimamisha mtu mwingine kabisa.

Kila mmtu alisikika akisema yake, wengine wakidai labda Sabogo amestafu kupigana, wengine wakidai labda ameishiwa kutokana na kupoteza pambano la fainali mwaka jana na mpinzani wake ajulikanaye Young Poo.

   Eddy na wapamba wake Sabogo, wakaingia ndani ya jengo la mapambano, kupitia mlango wa nyuma ili asionekane na watu wengi akiwa amevalia mavazi yake ya kazi. Wakaelekea kwenye vyumba maalumu vya wapambanaji, wakakuta chumba chake kikiwa kimendaliwa vizuri na Sabogo akiwa na baadhi ya wadhamini wezake.

Akamtambulisha Black Shadow kwa wazamini wezake na kutoa majigambo mengi kwamba lazima mtu wake ataibuka mshindi na kuchukua mkanda, huku mamilioni ya dola ya ushindi yakiingia mikononi mwake.
“Kiongozi namba yako ya ushindani ni kumi na mbili”
Sabogo alimumbia Eddy huku akimpa kikaratasi mkoni mwake chenye namba.
“Sawa”
“Ukiingia usiwasikilize mashabiki, wewe hakikisha kwamba unacheza na mpinzani wako. Natambua mashabiki wako humu ndani ni wachache haswa ni hawa vijana wangu”
“Usijali kwa hili kila kitu kitakwenda poa”
“Nakuaminia”
                                                                                              ***
   Sa Yoo na Shamsa hawakupoteza muda baada ya kurudi nyumbani, wakaingia bafuni na kuoga kisha kila mmoja akavalia vazi ambalo anaona linaweza kumtoa kutona na umbo lake alilo jaliwa na Mungu. Kila mmoja alionekana kuwa katika hali ya kupendeza sana, walipo jitazama kwenye kioo kikubwa kilichomo ndani mwao kila mmoja alijikuta akimsifia mwenzake kwa alivyo pendeza.

  Wakatoka hadi nje, ila Shamsa akarudi ndani alipo isahau simu yake. Akaingia chumbani kwake na kuichukua simu yake, akakuta pia wamesahau kuizimi tv kubwa iliyomo ndani ya chumba chao. Akiwa anaangaza macho yake huku na kule kuitafuta rimoti ya kuzimia tv hiyo, taarifa ya habari ikaonyesha picha ya Eddy kwamba bado anaendelea kutafutwa na polisi.

   Mwili wa Shamsa ukawa kama umeingiwa na ganzi alipo isikia taarifa hiyo. Hakujua ni wapi alipo Eddy, hakujua ni kwa nini anazidi kutafutwa na polisi wa nchi ya Japani. Honi ya gari kutoke nje, ikamstua na kumtoa katika hali hiyo ya kujiuliza maswali mengi, kwa haraka akaizima tv na kutoka zake nje, akaingia ndani ya gari na wakaondoka zao.

VIDEO: Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda Aahid Msanii Roma Atapatikana Kabla ya Jumapili Hii

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda, ameahidi Roma Mkatoliki, Moni pamoja na wengine wawili watapatikana Jumapili hii baada ya wasanii hao kutekwa na watu wasiojulikana Jumatano hii wakiwa Tongwe Record.

Alisema hayo jana akiwa nyumbani kwake Masaki jijini Dar es salaam, muda mchache baada ya kutembelewa na wasanii ambao walimtaka mkuu huyo kuwasaidia kupatikana kwa wasanii hao.

Akiongea na waandishi mbele ya wasanii hao, RC Makonda alisema kila mtanzania ana nafasi ya kumtafuta Roma na wenzake kwa kuwa hakuna anayejua watu hao wako wapi.

“Natoa pole kwa ndugu pamoja na marafiki, hakuna mtu ambaye anaweza kupotelewa na mtu akawa na furaha na bahati mbaya tunahangaika kujua wapi waliko. Nitumie fursa hii kuwaambia wananchi wa mkoa wa Dar es salaam kwamba tunapopotelewa na ndugu zetu katika mazingira ambayo hatuyafahamu sio wakati ya kuyarusha rusha maneno na kufika hatua tunapoteza ushahidi,” alisema RC Makonda.

Alisema tayari ameliagiza jeshi la polisi kufuatia suala hilo kwa ukaribu zaidi ili kupata ufumbuzi mapema huku akiahidi mpaka Jumapili hii watu wao watakuwa wamepatikana.

==>Msikilize hapo chini akiongea

Kamanda Sirro Azungumza na Waandishi wa Habari kuhusu Sakata la Msanii Roma

$
0
0
Msanii wa hip hop Roma Mkatoliki alikamatwa April 5 usiku ambapo taarifa zilianza kuenea katika mitandao ya kijamii kuwa alikamatwa studio za Tongwe Records  na watu wasiojulikana akiwa na wenzake na wakapelekwa  kusikojulikana.

Akizungumza na waandishi wa habari mapema leo asubuhi kuhusu kutekwa kwa msanii huyo na wenzake, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Simon Sirro alisema kuwa hawezi kusema ni lini wasanii hao watapatikana kwani ni hadi pale upelelezi wanaouendesha utakapokamilika.

Sirro alikuwa akijibu swali la mwandishi wa habari aliyekuwa akiuliza kuhusu lini wasanii watapatikana kufuatia kauli ya Mkuu wa Mkoa aliyoitoa jana kuwa hadi Jumapili wasanii hao watakuwa wamepatikana.

==>Haya ni mambo machache aliyoyazungumza
“Matukio ya utekaji hayajaanza leo, yamekuwepo na tukafanyakazi tukapata majibu. Tukio hili la kutekwa wasanii ni la kawaida.

“Tukio hili la utekaji ni kama matukio mengine ya uhalifu ambayo tumeyashungulikia, hatuwezi kusema hali mbaya kwa tukio hili.

“Mimi ni Kamishna wa Polisi siwezi kusema wasanii watapatikana lini, kama kuna kiongozi alitaja siku watakayopatikana, muulizeni yeye.

“Upelelezi ndio utakao amua hawa watu watapatikana lini. Tunafanya kazi kufuata taaluma ni si kutoa maneno tu.

“Wanaosema simu ya Roma ilikuwa inapatikana na kuhoji kwanini hatukwenda TCRA, wasitufundishe kazi, wamejuaje hatukwenda TCRA?

“Wengine walalamika wasema leo ni siku ya tatu tumechelewa kutoa majibu walipo, wajue majibu ya polisi kuuawa tulipata baada ya mwezi mmoja.

“Hawa watu hawakuja kuniambia kuwa Kamishna Sirro sasa tunakwenda kuwateka, kwamba ninajua walipo lakini sitaki kuwakamata."

==> Msikilize hapo chini akiongea

Breaking News: Msani Roma Mkatoliki na wenzake waliotekwa wapatikana Wakiwa Salama

$
0
0
Muda mfupi  baada ya Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Simon Sirro kuwaambia waandishi wa habari kuwa hawezi kusema ni lini mwanamuziki  Roma na wenzake watapatikana, taarifa kutoka kwa mmiliki wa studio walipokamatiwa, amethibitisha kuwa wamepatikana.

J Murder ambaye ndiye mmiliki wa Tongwe Records walipokuwa Roma na wenzake kabla ya kukamatwa na watu wasiojulikana, amesema kuwa wasanii hao wamepatikana na wapo katika Kituo cha Polisi Oysterbay jijini Dar es Salaam.

Aidha,Mkuu wa polisi (OCD) wilaya ya Kinondoni, Abubakar Kunga amethibitisha kupatikana kwa wasanii hao, lakini kwa sasa amesema wanafanya nao mahojiano ya kipolisi katika kituo cha Oysterbay.

Kupatikana kwao kumefuatia wito mkubwa uliokuwa ukipaishwa na wasanii wenzake na mashabiki kuhusu kuachiliwa huru.

Awali, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam, Kamishina Simon Sirro alisema bado walikuwa wakiendelea na upelelezi wa tukio la kupotea (kutekwa) kwa msanii Roma Mkatoliki na wenzake.

“Mimi ni Kamishna wa Polisi siwezi kusema wasanii watapatikana lini, kama kuna kiongozi alitaja siku watakayopatikana, muulizeni yeye.

“Upelelezi ndio utakao amua hawa watu watapatikana lini. Tunafanya kazi kufuata taaluma ni si kutoa maneno tu."
Alisema kamanda Sirro mapema Asubuhi wakati akiongea na waandishi wa habari

Nape Atema Cheche Kwa Wapiga Kura Wake

$
0
0
Mbunge wa Jimbo la Mtama mkoani Mtwara kupitia tiketi ya CCM, Mhe. Nape Nnauye amtaka Rais Magufuli aunde tume huru ambayo itaweza kuchunguza matukio ya uhalifu ya uvamizi wa studio unaoendelea nchini.

Hatua hiyo inatokana na matukio ya kiuhalifu yanayoendelea Tanzania na kuacha maswali mengi vichwani mwa wananchi kushindwa kufahamu kuwa watu hao na vikundi hivyo vya kihuni vinavyofanya vitendo hivyo vinapata wapi mamlaka hayo kuwa na nguvu kushinda Dola.

“Ombi langu kwa Rais namuomba aunde tume huru ichunguze matendo haya yasijirudie tena kwa sababu yasipochukuliwa hatua yataharibu sura ya Tanzania pia yataweza kuibuka makundi ya wahuni kuanza kuteka watu nao kwa kuwa hakuna hatua zinazochukuliwa. Tumsaidie Rais Magufuli kwa kumwambia ukweli naimani atasikia na atafanyia kazi kwa kuwa Rais wetu anapenda kusikiliza watu”. Alisema Nape

Aidha Mbunge huyo amesema watu wanaofanya mambo hayo wanalengo la kuwagombanisha wananchi na Rais wao jambo ambalo sio zuri kwa taifa.

 "Juzi amepotea msanii Roma Mkatoliki na wengine lakini mpaka sasa haifahamiki wapo wapi, yaani kama vile amepotea Nzi, tulisikia kijana mmoja wa CHADEMA anaitwa Ben Sanane amepotea saizi miezi mitano imepita, matendo haya ya kina Ben Sanane, Roma Mkatoliki, na wengine yanajenga chuki ya wananchi kwa Rais, lakini pia yanajenga chuki kwa wananchi na Chama Cha Mapinduzi (CCM) ". Alisema Nape Nnauye

Vile vile Nape amesema yeye mpaka sasa haamini yule mtu aliyemtolea silaha siku ya mkutano wake na wanahabari kama alitumwa ila shida aliyokuwa nayo ni kutaka kujua vyombo vya ulinzi na usalama vinafanya nini mpaka matukio yote yanatokea.

==>Haya ni Maneno ya Nape
1.usema kuwa nilifanyakazi kubwa CCM haimaanishi kuwa wengine hawakufanya. Wote tunajua tulivyokipigania chama

2..Nilipopewa Uwaziri kwa miezi 15, sina mashaka, nilifanya kazi kwa umakini mkubwa kwa kutumia uwezo wangu wote

3.Kama ambavyo siku ya kuteuliwa hatukujadiliana, miezi 15 ilipopita aliyeniteua aliamua kufanya mabadiliko ya baraza.

4.Kama ikibainika kuwa alivamia kituo cha Clouds, alafu nisipochukua hatua, sitakuwa na sababu ya kuendelea kuwa waziri.

5.Nilipogundua ni kweli alivamia Clouds, niliamua kuchukua hatua na kusimamia maneno yangu nisionekane mpumbavu ni mimi.

6.potishiwa kwa bastola, nilimwambia yule mtu taratibu, unaharibu sababu tukio lile lilikuwa likirushwa mubashara.

7. yule aliyenitisha walisema si Polisi, mara hajulikani.Lakini mtu mwingine akinyanyua bastola hapa, Polisi hawatakuacha.

8..RPC alikuwa pale, kama hakuwa Polisi kwanini wasimkamate? Na mtu yule si kweli kwamba hajulikani, anajulikana.

9. Mazingira ya kupotea kwa Ben Saanane yanautata mkubwa sana. Watu wengi sana wanatishiwa sasa. Juzi studio wametekwa wanne.

10.Matukio yanayoendelea sasa nchini yanawafanya watu kuwa na hofu. Hawaamini kama wakitoka watarudi majumbani mwao salama.

11. Namuomba Rais wangu aunde tume huru ya kuchunguza matendo haya ili impelekee taarifa kamili aweze kuchukua hatua.

12.Tusipochukua hatua, yatajitokeza makundi ya wahuni nao watapitia mlango huo huo kwa sababu hakuna hatua zinazochukuliwa.

13.Matendo haya yasipokomeshwa haraka, CCM tutapata tabu sana kwenye uchaguzi wa mwaka 2020.

Wimbo Wamponza Diamond......Gwajima Aahidi Kupambana Nae

$
0
0
Mwanamuziki Diamond Platnumz amemuomba msamaha Askofu Gwajima kufuatia kile kilichodaiwa na askofu huyo kuwa ameimbwa kwenye wimbo wa mtu anayepotosha haki ili kutetea vyeti feki.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram mapema leo mchana  Askofu Gwajima aliandika, “Aliyeniweka kwenye wimbo wa lengo la kupotosha haki ili kusapoti vyeti feki, jiandae, Almasi itageuka maji kesho!”
Kauli hii ya Askofu Gwajima imekuja ikiwa ni saa chache tu tangu mwanamuziki Diamond Platnumz alipotoa wimbo wake unaokwenda kwa jina la Acha Nikae Kimya ambapo ndani ya waliotajwa ni pamoja na Askofu Gwajima. Katika wimbo huo, Diamond alisema kuwa, ugomvi kati ya Makonda na Gwajima unachcochewa na dada mmoja kwenye mitandao.

Baada ya Gwajima kutoka maneno hayo, Diamond amejitokeza na kuandika kwenye ukurasa wake wa Instagram akifafanua kile alichokiimba kuhusu Gwajima kuwa hakina lengo baya, huku akimtaka Askofu Gwajima kutomgeuza maji kesho kanisani kwake, kwani yeye akimpania mtu huwa hatoki

“Yala! Yala! Jamani Mwenzenu nimeyatimba😟….. lakini mi nafkiri watu wanatakiwa waiskilize hii nyimbo kwa umakini sana tena sana na wataelewa nini ilikuwa maana yangu haswa… Hususani kama kipengele nilichomtaja mzee wangu @Bishopgwajima nilisema:“mara nasikia vya aibu Konda na Gwajima eti ugomvi umekolea….ila kuchunguza kwa karibu ni kuna binti mmoja tu ndio kwa mitandao anachochea…” aliandika Diamond na kuongeza;

“Point yangu ni kwamba licha ya kweli kuna yaliyojiri nyuma, lakini kwa busara zao ninazoamini wamejaaliwa na Mwenyez Mungu muda si mref wangekaa chini na kumaliza…nawote kufurahi kwa pamoja, lakini kwakuwa kuna dada mwingine alikua anachochea hawa ndugu zetu wazidi kufarakana…ikapelekea hadi kufikia hapa…asa hapo kosa langu mie liko wapi?😭 Chonde chonde mzee wangu @Bishopgwajima usinigeuze maji kesho 👐, mana nakujua ukimuamulia mtu…. naweza jumapili ya kesho nikaiona chungu Mwaka mzima😁"
Yala! Yala! Jamani Mwenzenu nimeyatimba😟..... lakini mi nafkiri watu wanatakiwa waiskilize hii nyimbo kwa umakini sana tena sana na wataelewa nini ilikuwa maana yangu haswa... Hususani kama kipengele nilichomtaja mzee wangu @Bishopgwajima nilisema: "mara nasikia vya aibu Konda na Gwajima eti ugomvi umekolea....ila kuchunguza kwa karibu ni kuna binti mmoja tu ndio kwa mitandao anachochea..." Point yangu ni kwamba licha ya kweli kuna yaliyojiri nyuma, lakini kwa busara zao ninazoamini wamejaaliwa na Mwenyez Mungu muda si mref wangekaa chini na kumaliza...nawote kufurahi kwa pamoja, lakini kwakuwa kuna dada mwingine alikua anachochea hawa ndugu zetu wazidi kufarakana...ikapelekea hadi kufikia hapa...asa hapo kosa langu mie liko wapi?😭 Chonde chonde mzee wangu @Bishopgwajima usinigeuze maji kesho 👐, mana nakujua mzee wa single touch ukimuamulia mtu....... naweza jumapili ya kesho nikaiona chungu Mwaka mzima😁😆😅
A post shared by Chibu Dangote (@diamondplatnumz) on

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili ya April 9

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu Ya April 10

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images