Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Malawi Yaichokonoa Tena Tanzania Kuhusu Ziwa Nyasa

$
0
0
Rais wa Malawi, Peter Mutharika ameanza tena chokochoko baada ya kutangaza kuwa hakuna nchi ambayo inamiliki kwa pamoja Ziwa Nyasa na kwamba haijafikia makubaliano na nchi yoyote, hivyo ameahidi kulinda umiliki na masilahi yake.

Kauli hiyo ni tofauti na mazungumzo ya Mutharika na Rais John Magufuli yaliyofanyika Januari 30 jijini Addis Ababa, Ethiopia wakati walipokuwa wakihudhuria kikao cha Umoja wa Afrika (AU).

Katika taarifa iliyotolewa na Idara ya Mawasiliano ya Rais baada ya kikao hicho, ilisema marais wote wameridhishwa na jitihada zinazofanywa na jopo la usuluhishi lililoteuliwa na Umoja wa Maendeleo wa Nchi za Kusini mwa Afrika (Sadc).

Jopo hilo linaongozwa na rais wa zamani wa Msumbiji, Joachim Chisano.

Mkuu wa kitengo cha mawasiliano katika wizara ya  Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mindi Kasiga amekiri kuiona taarifa hiyo na alisema anayeweza kulizungumzia suala hilo ni Naibu Waziri.

“Tumeiona hiyo taarifa ila jaribu kumtafuta Naibu Waziri maana Waziri atakuwa nje ya nchi. Ninachofahamu baraza la usuluhishi bado linaendelea na vikao vyake. Ukimpata naibu waziri atakuwa na maelezo ya kina.”alisema Mindi.

Lakini, akihudhuria Siku ya Maji Duniani Jumatano iliyopita mjini Mangoshi, Rais Mutharika alisisitiza msimamo wa Malawi kulinda umiliki wa ziwa hilo dhidi ya watu aliowaita wavamizi.

Mutharika alisema Malawi ndiye mmiliki pekee wa Ziwa Malawi, ambalo huku linajulikana kama Ziwa Nyasa, na kuonya kuwa utawala wake hautavumilia watu watakaokuwa na nia ya kuyumbisha taarifa za umiliki.

“Hebu tulilinde ziwa letu. Hili ni ziwa letu na ninaposema ziwa letu namaanisha ziwa lote. Mtu yeyote asifanye kosa la kubadili umiliki ambao umekuwepo kwa miaka 124 iliyopita,” alisema Mutharika akikaririwa na tovuti ya Nyasa Times ya Malawi juzi wakati wa mkutano huo uliofanyika ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Nkopola Lakeshore mjini Mangochi.

“Tunathamini ziwa letu na tutahakikisha tunachukua hatua za kulilinda kwa gharama zozote,” alisema.

Mutharika aliwataka wananchi kupunguza matumizi mabaya ya maji ili yapatikane kwa ajili ya kilimo na viwandani wakati wa msimu wa ukame.

Hivi karibuni, Malawi na Tanzania zimejikuta katika mzozo wa umiliki wa Ziwa Nyasa lililo kusini mwa Tanzania, mzozo ambao umesababisha kuanza kwa mazungumzo ya usuluhishi kumaliza kutokubaliana huko baada ya nchi hizo mbili kushindwa kufikia muafaka. Mzozo wa mpaka kwenye Ziwa Nyasa umekuwepo tangu mwaka 1967.

Lakini, mzozo wa hivi karibuni umeibuka baada ya Malawi kuanza utafiti wa mafuta na gesi kwenye ziwa hilo.

Hata hivyo, Mutharika alisema uchimbaji mafuta utaendelea katika ziwa hilo licha ya wanaharakati wa mazingira kuitaka Malawi iache mpango huo.

“Wale wanaohofia kuhusu mipango yetu ya kutafuta na kuchimba mafuta hawana sababu ya kuhofia. Kama tutaamua kuchimba mafuta katika ziwa, tutahakikisha tunatumia teknolojia safi,” alisema akikaririwa na Nyasa Times.

Nape Akabidhi Ofisi Kwa Mwakyembe

$
0
0
Aliyekuwa Waziri wa Habari Nape  Nnauye amemkabidhi ramsi ofisi Waziri mpya wa Habari, Dkt Harrison George Mwakyembe.

Watuhumiwa wa Ugaidi Watishia Kugoma Mahakamani

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha leo imesikiliza malalamiko ya watuhumiwa 61 wanao kabiliwa na kosa la ugaidi, ambapo ni shauri lililofunguliwa mwaka 2014.

Wakizungumza leo mahakamani hapo watuhumiwa hao wamesema kuwa leo ndiyo itakuwa mwisho wao kufika kwenye viwanja vya mahakama hiyo mpaka upande wa jamuhuri utakapo kamilisha upelelezi wao.

Wamesema wamekuwa wakifika mahakamani kwa muda ambapo wengi wao familia zinateseka na kusambaratika sababu ya kukaa mahabusu kwa miaka minne kwa makosa ya kusingiziwa.

Aidha wamesema wamekuwa wakipewa ahadi  hewa na mkuu wa upelelezi  kuwa angeshughulikia shauri hilo ndani ya miezi mitatu na kwamba suala la mahakama kushindwa kutekeleza wajibu wake  wa kikatiba linaleta ukakasi kwa wananchi.

Hakimu Mfawidhi Nestory Baro wa mahakama hiyo amewataka watuhumiwa kuwa na subira wakati wakishughulikia shauri lao ambapo kesi itatajwa April 11 mwaka huu na amewataka kufika mahakamani siku hiyo bila kukosa wakati akifanya utaratibu wa kumtafuta mkuu wa upelelezi na kuzungumza naye

AUDIO: Lipumba Amtimua Rasmi Maalim Seif Na Amchaguwa Sakaya Kukaimu Ukatibu Mkuu

$
0
0
Baraza Kuu la Uongozi Taifa la Chama cha Wananchi(CUF) leo limemvua Maalim Seif nafasi ya Ukatibu Mkuu na kumpa Magdalena Sakaya.

Tamko hilo limetolewa na mwenyekiti wa CUF anayeungwa mkono na  Msajili wa Vyama,  Prof. Ibrahim Lipumba ambapo amesema hatua hiyo imefikiwa baada ya Maalim Seif kukaidi na kususia ofisi kwa miezi kadhaa.

==>Msikilize hapo chini akiongea

VIDEO: Waziri Mkuu Majaliwa atua Buzwagi nakuondoka na mchanga wa Madini

$
0
0
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ametinga kwenye mgodi wa dhahabu wa Buzwagi uliopo Kahama mkoani Shinyanga na kuchukua sampuli za mchanga kwa lengo la kwenda kuyapima kwa wataalamu wa madini ili kubaini kiasi cha dhahabu kilichomo.

Amesema wanataka kuona mchanga unaosafirishwa na mwekezaji huyo una kiasi gani cha dhahabu, pia Serikali inataka kufahamu kama kodi inayolipwa ni sahihi.

“Tumeamua kuchukua sampuli za mchanga ambao mwekezaji anasema wanaupeleka nje ya nchi kwa ajili ya kwenda kutenganisha madini ya dhahabu na shaba. Hata hivyo nimemuhoji kwa nini mitambo hiyo isiletwe nchini ili kila kitu kifanyike hapahapa,” Amesema Majaliwa

Waziri Mkuu amesema sera ya uwekezaji inasema mtambo huo unatakiwa uwepo nchini ili kila hatua ya uchenjuaji ifanyike hapa hapa, hivyo tunataka kujiridhisha na mwenendo wa mwekezaji na mapato tunayoyapata kama yanastahili.

Aliongeza kwamba “Hili lipo miongoni mwa masharti ya uwekezaji kwenye sekta ya madini nchini kwamba mitambo hiyo ije kujengwa hapa nchini na itaongeza fursa ya ajira na kukuza sekta nyingine ikiwemo ya kilimo,”.

Kuhusu uzalishaji mgodini hapo
Kwa upande wake Meneja Uendelezaji wa mgodi huo Bw. George Mkanza alisema mgodi huo ulionzishwa mwaka 2009 umeajiri watumishi 720 pamoja na vibarua 500.
Alisema kwa siku wanachenjua makontena matatu hadi sita ambapo katika kila kontena moja wanapata kilo tatu za madini ya dhahabu na tani nne za madini ya shaba.

Bw. Mkanza alisema wanazalisha asilimia 50 ya madini ya dhahabu na asilimia 50 ya dhahabu iko kwenye mchanga na inakuwa imechanganyika na madini ya shaba ambayo ndiyo unaosafirishwa kwenda nje ya nchi kwa ajili ya kutenganishwa.

“Hapa Buzwagi tuna makontena 179, makontena mengine 152 yako Dar es Salaam kwenye bandari kavu ya Nazam na 21 yako bandarini. Kila siku tunapoendelea kuzalisha tunakuwa na makontena manne hadi sita. Ndugu zetu wa Bulyanhulu nao wanamakontena 108 yako mgodini na 104 yako Nazam Cargo Dar es Salaam,”alisema.

==>Video ya tukio hilo

Makamishna Wapya Wa Uhamiaji Waapishwa Leo Mjini Dodoma

$
0
0
Katibu Mkuu wa Wizara  ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira  aliyeketi katikati akishuhudia Makamishna wapya wa  Uhamiaji wakila kiapo cha Maadili ya Viongozi wa Utumishi wa Umma baada ya kuvishwa vyeo vipya katika hafla iliyofanyika leo katika ukumbi wa Mikutano wa  Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma,  Kulia ni Naibu  Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Balozi  Hassan Simba Yahaya na  kushoto ni Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dr. Anna Peter Makakala wote wakishuhudia tukio hilo.
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dr. Anna Peter Makakala ,akimvisha cheo kipya Kamishna wa Uhamiaji Utawala na Fedha,  Edward Peter Chogero  katika hafla iliyofanyika leo katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma. Anayeshuhudia ni Naibu Kamishna wa Uhamiaji Chrispin Ngonyani. Tukio hili linehudhuriwa na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Meja Jenerali Projest Rwegasira  na Naibu  Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Balozi  Hassan Simba Yahaya.
Kamishna mpya wa Uhamiaji Divisheni ya Sheria Hannerole Morgan Manyanga akila kiapo cha Utii mbele ya Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dr.  Anna Peter Makakala katika hafla iliyofanyika  leo katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma. Hafla hiyo imehudhuriwa na Katibu Mkuu wa Wizara  ya Mambo ya Ndani ya Nchi Meja Jenerali Projest Rwegasira   na Naibu  Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Balozi Hassan Simba Yahaya.
Kamishna wa Tume ya Maadili ya Utumishi wa Umma , Jaji Mstaafu Harold Nsekela wa kwanza kushoto akiwaongoza  Makamishna wapya wa Uhamiaji kuapa  kiapo cha Maadili ya Viongozi wa  Utumishi wa Umma baada ya Makamishna hao wapya kuvalishwa vyeo vipya katika hafla iliyofanyika  leo katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma.
Makamishna wapya wa Uhamiaji wakisaini Fomu za Maadili ya Viongozi wa Umma baada ya Makamishna hao kula kiapo cha Maadili ya Viongozi wa Utumishi wa Umma, katika hafla iliyofanyika leo katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma.
Katibu Mkuu wa Wizara  ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira  akitoa maelekezo kwa Makamishna wapya wa Uhamiaji wakati wa hafla ya kuvikwa Vyeo Vipya   iliyofanyika  leo katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma.
Katibu Mkuu wa Wizara  ya Mambo ya Ndani ya Nchi Meja Jenerali Projest Rwegasira   akizungumza jambo na Makamishna wapya wa Uhamiaji baada ya kumalizika shughuli ya kuapishwa Makamishna hao  leo katika viwanja vya Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma. 

Mjumbe wa Baraza Kuu UVCCM Mkoa wa Arusha Ndg. Robert PJN Atoa Msaada wa Chakula Hospitali teule ya Wilaya ya Sengerema

$
0
0
Kutoka Sengerema - Mwanza.
Mjumbe wa Baraza Kuu UVCCM Mkoa wa Arusha Ndg. Robert PJN Kaseko  tarehe 27 Machi, 2017 ametembelea Hospitali teule ya Wilaya ya Sengerema na kutoa Msaada wa Chakula kwa Wagonjwa wenye hali ngumu ya Maisha & Wanaohitaji msaada kutoka kwa wasamalia wema.

Akikabidhi msaada  huo kwa Muuguzi Mkuu wa Hospitali hiyo  Sr. Mariojose kwa niaba ya Wagonjwa wamama na watoto Ndugu Kaseko ametoa Chakula Mahindi Kilo 100, Maharage Kilo 50, Soya Kilo 50, Sukari Kilo 25, Mafuta ya Kupikia Ndoo moja ya lita 20, Sabuni & Juice Vyenye thamani ya Tsh. 700,000/=

Mjumbe huyo wa Baraza Kuu UVCCM Mkoa wa Arusha amesema yeye ni mzawa wa Sengerema na amekuwa akitibiwa katika Hospitali hiyo wakati wote wa utoto wake hivyo anazifahamu sawia changamoto zinazoikabili huduma ya afya hospitalini hapo na kwamba ameguswa sana Matatizo hayo hivyo na kuamua kuunga Mkono Juhudi za Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli za kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili Watanzania katika sekta ya Afya.

Ndugu Kaseko ametumia nafasi hiyo kuwaomba wadau mbalimbaliwa maendeleo kuisaidia Serikali kuwaletea maendeleo wananchi kwani Serikali ina mambo mengi hivyo peke yake haiwezi ni lazima watu wenye moyo wa kujitolea na wanaopenda maendeleo wajitoe kuisaidia Serikali inaayoongozwa na Rais Magufuli ambayo ukweli inajikita haswaa kuwatumikia wananchi kwa kuwaletea maendeleo.

Mganga Mkuu wa Hospitali hiyo teule ya Wilayaya Sengerema Sr.Mariojose amemshukuru sana Ndugu Kaseko kwa msaada huo na kusema ni wachache sana wenye moyo huo na kumuomba aendelee na moyo huo huo wa kujitolea wa kuwasaidia wenye Shida hasa Masikini.

Katika hatua nyingine Ndugu Kaseko amekabidhi Madawati Kumi na Tano  manne  ( 4 ) Katika Shule ya Msingi Ibondo Wilayani Sengerema. Ndugu Kaseko ambaye ni Mjumbe wa Baraza Kuu UVCCM Mkoa wa Arusha amesema anaunga mkono Juhudi za Serikali ya Hawamu ya Tano Chini ya Rais Magufuli na Kwamba Elimu bure imekuja na changamoto kedekede kote nchini na kwamba  serikali inastahili kusaidiwa ili kuhakikisha Elimu bora inatolewa. Ndugu Kaseko ametaja baadhi ya Changamoto hizo ni Uchache wa  Madarasa ya kusomea, Maabara, Madawati, Vyoo vichache ikilinganishwa na Idadi kubwa ya Wanafunzi walioandikishwa.

Ndugu Kaseko amewaomba wadau mbalimbali wa Elimu kuendelea kuunga Mkono Sera ya Elimu Bure kwa Shule za Msingi na Sekondari kwa kujitoa kusaidia jamiI zinazotuzunguka.

Baada ya Makabidhiano hayo Afisa Elimu Kata hiyo ya Ibondo Ndugu Janerose amemshukuru sana Ndugu Kaseko kwa msaada huo wa Madawati, Madirisha na Katoni mbili za Madaftari.

Na kwa upande Mwingine Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo Bw. Emmanuel Mashili amemshukuru Diwani wa Kata hiyo Mh. Mathias Henyenge ambaye pia ni rafiki wa Ndg. Kaseko kwa Juhudi zake kubwa za kuwatumikia wananchi wa Kata ya Ibondo. 

Neema Wambura Amshukuru Rais Magufuli Kwa Kumsaidia.......Awapongeza Madaktari na Wauguzi

$
0
0
Mgonjwa Neema Wambura ambaye alikuwa akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) amemshukuru Rais John Pombe Magufuli baada ya afya yake kuimarika na kuruhusiwa leo kurejea nyumbani.
 
Neema amemshukuru rais kwa kumwezesha kupata matibabu tangu alipofikishwa katika hospitali hiyo Februari 23, mwaka huu.
 
“Namuomba Mwenyezi Mungu amuepushe Rais Magufuli na mambo mabaya yote. Sasa nipata nguvu, nina furaha na naoga mwenyewe tofauti na awali,” amesema Neema.
 
Pia, Neema amewashukuru madaktari na wauguzi wa Muhimbili kwa kumpatia huduma bora na kumwezesha kupona majeraha ya moto.
 
Neema ambaye ni Mkazi wa Mkoa wa Mara alimwagiwa maji ya moto na mumewe wakati alipokuwa akichemsha maji kwa ajili ya kupika ugali na kuungua sehemu ya kifuani, shingo na mkono.
 
Mkuu wa Idara ya Upasuaji na Daktari Bingwa wa Upasuaji, Dk Ibrahim Mkoma  amesema afya ya Neema inaendelea vizuri baada ya kufanyiwa upasuaji sehemu ya shingoni ili kutenganisha shingo na sehemu ya kifua na kuziba majera ya moto.
 
“Neema anaendelea vizuri sasa anaweza kunyanyua shingo vizuri kabla ya hapo alikuwa hawezi kuinyanyua wala kuizungusha,” amesema.

Serikali Kutengeneza Mwongozo Wa Kuwarudisha Shule Waliopata Mimba

$
0
0
Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO.
Serikali imejipanga kutengeneza mwongozo wa kuwarudisha shuleni wanafunzi waliopata mimba wakiwa masomoni ili kuhakikisha wanapata elimu hadi kufikia ngazi za juu.

Hayo yamesemwa jana Jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Msaidizi Masuala Mtambuka kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Venance Manori alipokuwa akifungua warsha ya kuwawezesha Maafisa Waandamizi wa Serikali kutoka nchi sita za Afrika katika kutengeneza mipango inayozingatia jinsia katika elimu kwa niaba ya Waziri wa Wizara hiyo Prof. Joyce Ndalichako.

Manori amesema Serikali ya Tanzania inajitahidi kuzingatia jinsia katika utoaji wa elimu ambapo takwimu zinaonyesha kuwa elimu ya Msingi na Sekondari uwiano wake ni moja kwa moja japo kuwa idadi ya wasichana hupungua kutokana na changamoto mbalimbali zinazowakumba hivyo lengo la warsha hiyo ni kuwasaidia wadau kuweka mipango ya elimu inayozingatia usawa wa kijinsia.

“Serikali yetu imejipanga kuhakikisha wasichana wanapata elimu hadi ngazi za juu lakini mpango huo unakumbwa na changamoto mbalimbali zikiwemo za mimba na ndoa za utotoni hivyo ili kuhakikisha mtoto wa kike anafikia ngazi za juu za elimu tuko kwenye mchakato wa kuandaa mwongozo kwa ajili ya wanafunzi waliopata mimba wakiwa bado wanasoma kupata nafasi ya kuendelea na masomo,”alisema Manori.

Mkurugenzi Msaidizi amezitaja changamoto zingine zinazowapelekea wanafunzi wa kike kuacha shule zikiwemo za umaskini, mazingira rafiki ya kusomea, mila na desturi zinazomkataza msichana kupata nafasi ya kusoma pamoja na kukosa muda wa kujisomea kwa sababu ya kufanya kazi nyingi wanaporudi majumbani.

Manori ametoa rai kwa Watanzania kuelewa kuwa kila mtoto ana haki na wajibu wa kupata elimu bila kujali jinsia pia ameiasa jamii kuacha kuwaozesha wasichana wenye umri chini ya miaka 18 ili waweze kufikia malengo yao waliyojipangia.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Plan International- Tanzania, Jorgen Haldorsen ameahidi kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kuhakikisha mipango ya elimu nchini inaangalia usawa wa kijinsia kwa kuwa ni njia moja wapo itakayochochea maendeleo ya elimu kwa watoto wa kike.

“Warsha hii imeandaliwa kwa ajili ya wadau wote kutoa mawazo yao juu ya changamoto za usawa wa kijinsia zinazoikumba sekta ya elimu pamoja na kuwapa fursa wadau hao kushauriana kuhusu mikakati mbalimbali ya kutatua changamoto hizo ili kuinua sekta ya elimu sio tu kwa Tanzania bali kwa Afrika nzima,”alisema Haldorsen.

Haldorsen ameongeza kuwa mfumo wa elimu umetambua uhusiano uliopo kati ya elimu na usawa wa kijinsia ndio maana wadau wa masuala ya elimu wa Serikali kutoka katika baadhi ya nchi za Afrika wameamua kuungana kwa pamoja kujadili juu ya tathmini, mpangilio na ufuatiliaji wa elimu unayozingatia jinsia.

Tanzania imekua nchi ya kwanza kuendesha warsha hiyo ya siku tatu iliyoshirikisha maafisa waandamizi wa Serikali wanaoshughulikia mipango ya elimu kutoka nchi za Mozambique, Zambia, Malawi, Uganda, Zanzibar na Tanzania Bara.

Imeandaliwa kwa ushirikiano wa shirika la Plan International- Tanzania, Global Partnership for Education (GPE), Dubai Cares pamoja na United Nations Girls’ Education Initiative (UNGEI).

Fedha za maendeleo zaongezeka kwa asilimia 36.......Tazama Hapa Ripoti Kamili Iliyowasilishwa Leo Bungeni na Waziri wa Fedha

$
0
0
Serikali imewasilisha mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa na kiwango cha ukomo wa bajeti ya mwaka wa fedha 2017/18 huku ikionyesha ukomo wa bajeti kufikia shilingi trilioni 31.6 kutoka trilioni 22 za mwaka wa fedha unaoisha Juni 30, mwaka huu

Katika bajeti hiyo, fedha za maendeleo zimeongezeka kutoka trilioni 11.8 mwaka 2016/17 hadi trilioni 11.9 mwaka 2017/18 sawa asilimia 38 ya bajeti yote.

Mapendekezo hayo yamewasilishwa hii leo bungeni mjini Dodoma ikiwa ni siku chache kabla ya kuanza kwa vikao vya bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Akiwasilisha mapendekezo hayo, Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango ametaja baadhi ya maeneo ya kipaumbele kuwa ni ujenzi wa reli ya kati, kuhuisha shirika la ndege Tanzania na shamba la kilimo na uzalishaji sukari la Mkulazi.

Aidha, Waziri Dkt. Mpango ametaja changamoto za utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2016/2017 hadi Februari mwaka huu kuwa ni mwamko mdogo wa kulipa kodi na hususani kuzingatia matumizi ya mashine ya kielektroniki.

Baadhi ya wabunge ambao ni wawakilishi wa wananchi, nje ya ukumbi wa bunge wamesema serikali imechukua jitihada kubwa katika kuhakikisha inaondokana na utegemezi kuliko kutegemea fedha kutoka nje.

Wabunge bado wanaendelea na vikao na shughuli za utekelezaji katika kamati mbalimbali hadi Aprili 2 mwaka huu kabla ya kuanza kwa vikao vya Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania April 4 mwaka huu mjini Dodoma.

==>Hii ndo Ripoti kamili iliyowasilishwa leo Bungeni

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya March 29

Wachimbaji Wadogo Wamwangukia Rais Magufuli

$
0
0
Wachimbaji, wauzaji na wasafirishaji wadogo wa madini, wamemwomba Rais Dk. John Magufuli kuondoa zuio la kusafirisha mchanga wenye madini alilolitoa wiki iliyopita, baada ya kutembelea Bandari ya Dar es Salaam.

Pia wachimbaji hao wamesikitishwa na hatua ya watendaji kutoka Wizara ya Nishati na Madini, kumpotosha Rais kuwa makontena yaliyozuiwa bandarini yana mchanga wa dhahabu, badala ya mchanga wenye madini mengine, ikiwa ni pamoja na shaba, chuma, salfa, mercury na nickel.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, kiongozi wa wachimbaji wa madini ya nickel kutoka Dodoma, Thobias Rweyemamu, alisema tangu Machi 2, mwaka huu walizuiwa kusafirisha mchanga na mawe jambo ambalo limewasababishia hasara kubwa.

Alisema hata shughuli za uzalishaji katika maeneo ya machimbo zimesimama na kusababisha hasara ya Sh milioni 4 kila siku.

“Tunapata hasara kubwa tangu Machi 2, tunapoteza Sh milioni 4 kila siku, wachimbaji waliokuwa wanaendelea na shughuli zao wamesimama, hali imekuwa ngumu, tutashindwa kuendesha maisha, familia zetu zinatutegemea na kundi kubwa la vijana migodini… hali hii ikiendelea tutawafanyaje?” alihoji Rweyemamu.

Alisema hadi sasa wachimbaji wadogo zaidi ya 110 wamezuiliwa, huku mchanga wenye nickel zaidi ya makontena 60 na copper makontena saba yakiwa na mchanganyiko wa madini yamezuiliwa.

Rweyemamu alisema kutokana na hali hiyo, bado wanaingia hasara ya kulipia ushuru wa Dola za Marekani 20 kila siku ambazo ni  sawa na Dola 12,000 kwa mwezi jambo linalowatia gharama kubwa.

Alisema wamekuwa wakifanya biashara hiyo kwa miaka mingi, baada ya kupata vibali halali kutoka Wizara ya Nishati na Madini na wapo kihalali si kama ilivyoelezwa.

Mchimbaji mwingine, Paul Kaliyemba, alisema Rais Magufuli alipotoa agizo hilo, hawakupaswa kuchanganywa na maelezo ya wataalamu wa wizara.

Kaliyemba alisema wanafanya biashara hiyo kihalali, hata wizara inatambua kwa sababu leseni zilitolewa na Wakala wa Ukaguzi wa Madini Tanzania (TMAA) na  walifanya ukaguzi na kujiridhisha.

Alisema kutokana na hali hiyo, wamemwandikia barua Rais Magufuli kupitia Wizara ya Nishati na Waziri Mkuu kupitia upya uamuzi wao na wachimbaji wadogo waruhusiwe kuendelea na biashara yao.

Kuibuka kwa wachimbaji hao, kumetokana na Rais Magufuli kupiga marufuku usafirishaji wa mchanga wenye madini ya dhahabu kwenda nje ya nchi.

Kutokana na agizo hilo, Rais Magufuli aliagiza Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) kuzuia makontena 262 yenye mchanga unaodaiwa kuwa na madini usisafirishwe kwenda nje ya nchi.

Mkurugenzi wa Bandari ya Dar es Salaam, Deusdedit Kakoko, alisema baada ya Rais kushuhudia makontena hayo, Alhamisi iliyopita walianzisha operesheni maalumu na kubaini makontena 262 yaliyokuwa na mchanga wa dhahabu tayari kwa kusafirishwa nje.

Alisema makontena hayo ni mali ya mgodi wa Buzwagi, unaomilikiwa na Kampuni ya Acacia yaliyokuwa yamehifadhiwa bandari kavu ya Mofed iliyopo Kurasini, Temeke.

Hata hivyo, Meneja Uhusiano wa Acacia, Asa Mwaipopo, alisema makontena hayo ni ya mchanga wa madini ya shaba na yalifikishwa bandarini kabla ya zuio la Rais Magufuli.

Nape Nnauye: Sina Mpango wa Kuhama CCM na Ntaendelea Kuwa Mtiifu Kwa Rais

$
0
0
Aliyekuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye amesema ataendelea kuwa mtiifu kwa Rais John Magufuli, Serikali na Chama cha Mapinduzi tofauti na maneno yanayosemwa mitandaoni.

Tangu alipoachwa kwenye mabadiliko madogo ya Baraza la Mawaziri, Machi 23, kumekuwa na taarifa nyingi feki kwenye mitandao ya kijamii kuhusu kuenguliwa kwake zikidaiwa kutolewa na mbunge huyo wa Mtama ambazo hata hivyo, amekuwa akizikanusha.

Akizungumza jana wakati akikabidhi ofisi kwa waziri mpya wa wizara hiyo, Dk Harrison Mwakyembe katika ofisi za wizara hiyo mjini hapa, bila kutaja maneno hayo ya mitandaoni, Nape alisema ataendelea kumuunga mkono Rais katika dhamira yake njema ya kuleta mageuzi nchini.

“Heshima aliyonipa Rais ni kubwa mno na nitaendelea kumuunga mkono katika dhamira yake njema ya kuleta mageuzi nchini” alisema.

Alimshukuru Rais kwa kumpa dhamana ya kusimamia wizara hiyo kwa miezi 15 baada ya kuchaguliwa kuwa mbunge kwa mara ya kwanza. “Nitaendelea kutoa ushirikiano kwa wizara hii kwa sababu mimi ni mdau mkubwa wa sekta hiyo,” alisema.

Waziri Mwakyembe alisema ataendeleza mazuri yote yaliyofanywa na Nape katika kuimarisha wizara hiyo na atahakikisha wizara hiyo inakuwa ya mfano nchini.

Alimsifu Nape akisema katika kipindi kifupi alichokaa katika wizara hiyo amefanya mabadiliko na watu wameanza kuifahamu.

Nape aliondolewa katika nafasi hiyo siku moja baada ya kamati aliyounda kuchunguza tukio la kuvamiwa kwa ofisi za Clouds kumkabidhi ripoti.

Mara baada ya kupewa ripoti hiyo, Nape aliahidi kuikabidhi kwa mamlaka zake za juu akizitaja kuwa ni Waziri Mkuu, Makamu wa Rais na Rais lakini asubuhi ya siku iliyofuata aliondolewa katika nafasi hiyo.

Makabidhiano hayo yalishuhudiwa na viongozi wengine wa wizara hiyo, naibu waziri, Anastazia Wambura, katibu mkuu, Profesa Elisante Ole Gabriel na naibu katibu mkuu, Nuru Millao.

==>Msikilize Hapo Chini Akiongea

Nay wa Mitego: Ntaurekebisha Wimbo Wangu Kama Rais Alivyoshauri Lakini Sitavuka Mipaka

$
0
0
Saa chache baada ya kuachiwa huru kutokana na amri ya Rais John Magufuli, Rapa Nay wa Mitego amesema kuwa atayafanyia kazi maoni ya Rais kuhusu kuboresha wimbo wake kwa namna ya pekee.

Rapa huyo alitiwa nguvuni wikendi iliyopita kwa tuhuma za kusambaza wimbo wake wa ‘Wapo’ ambao Baraza la Sanaa Tanzania (Basata) liliweka wazi kuwa haufai na una lugha za matusi, lakini mambo yalibadilika baada ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe kueleza kuwa amezungumza na Rais Magufuli na amesema anaupenda wimbo huo na kwamba ameagiza aachiwe huru na aufanyie maboresho kwa kuongeza mambo mengine bila kupunguza alichokiimba.

Akizungumzia suala hilo, Nay wa Mitego amesema kuwa ataufanyia marekebisho wimbo huo lakini atahakikisha havuki mipaka.

“Ninalifanyia kazi, mheshimiwa amesema anaupenda wimbo wangu na anausikiliza, yeye mwenyewe amewekwa kwenye huu wimbo ni jambo ambalo hawezi kupuuzia na hiki kinachoendelea labda amefurahishwa, hivyo nitaifanyia kazi kwa kuongeza mengi makubwa na kwa mapana zaidi bila kuvuka mipaka,” Nay wa Mitego anakaririwa.

Msanii huyo aliwataka wananchi na vyombo vya habari kuendelea kuzungumza ukweli na kutoa maoni yao lakini wazivuke mipaka.

‘Wapo’ haukuwa wimbo wa kwanza kumuweka matatani Nay wa Mitego kwani baadhi ya nyimbo zake kama ‘Pale Kati Patamu’ na ‘Shika Adabu Yako’ ziliwahi kufungiwa na Basata na kupewa onyo kali.

Makonda ahojiwa na kamati ya madaraka ya bunge

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda leo amefika mbele ya kamati ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge kufuatia wito wa Kamati hiyo kumtaka afike mbele ya kamati kujibu tuhuma zinazomkabili za kuingilia Haki, Uhuru na Madaraka ya Bunge kutokana na matashi aliyoyatoa mapema mwezi februari 2017 jijini Dar es Salaam yaliyokuwa na madai ya kudharau Bunge.

Wito wa kufika mbele ya Kamati hiyo unafuatia Azimio la Bunge lilitolewa tarehe 8 Februari 2017 ambapo Bunge liliazimia Mhe. Spika aweze kukubali Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe. Alexandra Mnyeti na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Mhe Paul Makonda wahojiwe kutokana na Matamshi yao ya Kudharau Bunge.

Jipatie Dawa za Asili za Kupunguza Maziwa, Kutoa Michirizi, Kuondoa Chunusi, Kuongeza Maumbilie na Nguvu za Kiume

$
0
0
NATURAL   BEAUTY COSMETICS

Ni kampuni inayotoa bidhaa original na zenye matokeo mazuri bila madhara wala kemiko ya aina yoyote. Bidhaa zetu zote zimetengenezwa kwa mimea na matunda. Tunawaletea punguzo la bei la %10 bidhaa tulizonazo ni kama zifuatazo.
 
     👇👇👇👇
1. Kutengeneza shepu hipsi na makalio kwa:- (a) Dawa ya kunywa au Botcho yakupaka @ 150,000/= (b)Vidonge maalum @ 170,000/=
2. Kupunguza au kuongeza maziwa @ 100,000
3. Kushepu miguu kuwa (Chupa ya bia) @ 110,000
( Kuludisha bikra (@) 100,000/=
4. Kuondoa mipasuko au michirizi @100,000/=
5.Kuwa softi na mweupe mwili mzima kwa mafuta @100,000/= vidonge maalum @150,000
6.Kuongeza unene wa mwili mzima kwa vidonge au dawa ya kunywa @150,000/=
7.kupunguza tumbo na manyama uzembe kwa:-
(a)Dawa ya kunywa au kupaka @ 130,000/=
(b) Mkanda original wa MICRO COMPUTER @200,000/=
8.Kuondoa chunusi na madoa sugu (@) 100,000/=
9.Kuondoa mvi milele na zisiludi tena @ 120,000
10.Kuongeza maumbile kwa:- (a)Gel ya kupaka @120,000/= Mashine original ya HANDSOME UP @170,000/=
11 Kuongeza nguvu za kiume na hamu ya tendo la ndoa @120,000
12.Kuondoa vinyweleo @80,000/=
13. kuotesha nywele kwenye kipara @120,000/=
14.Kuondoa makovu sehemu yoyote @100,000/=
15. Kuongeza hamu ya tendo la ndoa kwa wanawake @100,000/= NK. [ Bidhaa zetu zote ni garantii pia hakikisha unapewa risiti ununuapo bidhaa kampuni hii popote ulipo utapata huduma zetu]
 
     WASILIANA NASI KWA NAMBA
        {065 9618585 au 0759029968.}
           Follow us
   👇👇👇👇👇👇
@natural2162
@natural2162
@natural2162
@natural2162
@natural2162
                               Karibu sana

Mwakyembe Aimwagia Sifa Taifa Stars.....Adai Imemkaribisha Vizuri

$
0
0
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt Harrison Mwakyembe ameipongeza timu ya Taifa ya Mpira wa miguu(Taifa Stars) kwa kushinda mechi zao zote mbili za kirafiki dhidi ya Botswana na Burundi.

Ameyasema hayo mapema hii leo wakati akizungumza na waandishi wa habari Mjini Dodoma mara baada ya kukaribishwa rasmi Wizarani hapo.

Mwakyembe amesema kuwa Taifa Stars imempa ukaribisho mzuri katika Wizara hiyo kwa kumpa zawadi ya ushindi kwa michezo yote miwili iliyofanyika mwishoni mwa Juma lililopita na katikati mwa Juma hili.

“Nawapongeza sana wachezaji makocha na viongozi wa Taifa Stars kwa kujituma na kuipeperusha bendera ya Taifa kwa kushinda mechi zao zote mbili za kimataifa,”amesema Dkt Mwakyembe.

Aidha amewahimiza pia watanzania kuendelea kuiunga mkono Timu ya Taifa  ya Mpira wa miguu kwa vijana walio chini ya miaka 17 Serengeti Boys kwa kuichangia timu hiyo ili iweze kushinda nafasi ya kwenda kushindana katika kombe la dunia kwa vijana litakalofanyika mwezi Novemba mwaka huu nchini India.

Hata hivyo, amelipongeza pia Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kwa kushirikiana na Kamati ya kuhamasisha ushindi kwa Serengeti Boys iliyo chini ya Charles Hillary kuendelea kushirikiana kwa karibu na Wizara yake ili kufanikisha ushindi kwa timu hiyo

Mwakyembe: Huwezi Kuwa Hakimu wa Kesi Yako Mwenyewe.....Ripoti ya Uvamizi Clouds Media Inamapungufu, Sitaipeleka Ngazi za Juu

$
0
0
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt Harrison Mwakyembe leo amezungumza na waandishi wa habari Mjini Dodoma mara baada ya kukaribishwa rasmi Wizarani hapo..

Baada ya maongezi aliruhusu mwaswali ambapo moja ya swali aliloulizwa na wanahabari ni kuhusu ripoti iliyoachwa na Waziri wa zamani Nape Nnauye kuhusu uchunguzi wa mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda kudaiwa kuvamia ofisi za Clouds Media huku akiwa na Askari wenye silaha.

==>Haya ni majibu aliyoyatoa
"Wengi mnauliza nimeifanyia kazi gani ripoti ya Nape, mimi hiyo ripoti sijaiona na kama mwanasheria kwangu ni mwiko na sitapeleka taarifa ambayo haijakamilika.

"Kupitia vyombo vya habari taarifa imeeleza kuwa ushahidi ulitolewa na upande wa Clouds Media na mkakiri kuwa upande wa pili haukupatikana.
 
"Huwezi kuwa Hakimu kwenye suala lako wewe mwenyewe, kufanya hivyo ni ubatili kwahiyo hata mimi ningekuwa ni mwandishi wa habari ningesema hili jambo siliwezi kwakuwa linanihusu na mimi.

"Kanuni zinataka kusikiliza upande wa pili, sasa mmeshasema kitu kina upande mmoja alafu nimpelekee kiongozi wangu..NO, mimi kazi yangu ni kupata maelezo ya upande wa pili na nitapata.

"Hili jambo ni lakufa na kupona, yani niache kukutana na wakuu wa idara mbalimbali hapa kuhakikisha nakuza suala la sanaa na kuhakikisha vijana wetu hawaendelei kuibiwa nibaki kuhangaikia suala la ripoti.

"Mimi sikuapa kwa jambo hilo moja pekee lakini mimi ni mwanasheria mkongwe na nitahakikisha nalifuatilia lakini mimi sitaunda kamati katika jambo hilo.

"Lengo letu ni kuhakikisha hatutakuwa na matukio ya namna hiyo katika safari lakini tukitoka na kauli za papara tutakuwa tunajitafutia matatizo hapo mbeleni "

Mwenyekiti Wa Chama Cha Mapinduzi CCM Rais Dkt. Magufuli Aendesha Kikao Cha Kamati Kuu Ya Halmashauri Kuu Ya Taifa Ya CCM Jijini Dar Es Salaam.

$
0
0
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Rais  Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akijiandaa kuendesha Kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi CCM leo jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Rais  Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha na Rais wa Zanzibar ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti CCM (Zanzibar) Dkt. Ali Mohamed Shein, Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Spika wa Bunge Job Ndugai, Waziri Mkuu Mstaafu Dkt. Salim Ahmed Salim, Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi wakiwa pamoja na Wajumbe wengine wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi CCM, mara baada ya kumalizika kwa kikao hicho jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Rais  Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Rais wa Zanzibar ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti CCM (Zanzibar) Dkt. Ali Mohamed Shein mara baada ya kumalizika kwa kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama cha  Mapinduzi CCM kilichofanyika jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Rais  Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama cha  Mapinduzi CCM Dkt. Salim Ahmed Salim mara baada ya kumalizika kwa kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama cha  Mapinduzi CCM kilichofanyika jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU

Rais Magufuli Afungua Mkutano Wa Mawaziri Wa Tanzania Na Uganda Ulioongelea Maendeleo Ya Mradi Wa Ujenzi Wa Bomba La Mafuta Ghafi Kutoka Hoima Hadi Tanga

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifungua kikao cha pamoja cha Mawaziri wa Serikali za Tanzania na Uganda pamoja na wadau kuzungumzia mradi wa ujenzi wa Bomba la Kusafirishia Mafuta Ghafi kutoka Hoima nchini Uganda hadi Bandari ya Tanga.

Mkutano huo, uliofanyika Ikulu, Dar es salaam JANA  Jumanne Machi 28, 2017, ulihudhuriwa na Mawaziri wa Nishati na Madini pamoja na Mawaziri wa Ardhi wa nchi hizo mbili, Wanasheria wa Serikali  na kampuni washirika wa mradi huo Lake Albert (CNOOC, TOTAL na TULLOW).

Pamoja na mambo mengine, Mawaziri, Maafisa na Wataalam wa pande zote husika walikaa na kukubaliana kwamba rasimu ya  makubaliano rasmi ya kuanza kwa mradi yawe yamekamilika na kuwa tayari katika kipindi cha wiki mbili ili kuwezesha Marais wa Tanzania na Uganda kuweka jiwe la msingi kuashiria kuanza ujenzi wa kihistoria wa mradi huo wa bomba la mafuta kutoka Hoima nchini Uganda hadi Chongoleani mkoani Tanga, Tanzania. 

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images