Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Rais Magufuli azindua uwanja wa ndegevita wa Ngerengere

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe 06 Machi, 2017 amezindua uwanja wa kisasa wa ndegevita wa Ngerengere uliopo Mkoani Morogoro, uliofanyiwa ukarabati mkubwa baada ya miundombinu ya uwanja uliojengwa tangu mwaka 1970 kuharibika.

Sherehe ya uzinduzi wa uwanja huo imefanyika uwanjani hapo na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, Balozi wa China hapa nchini Mhe. Dkt. Lu Youqing, Viongozi wa vyombo vya ulinzi na usalama na Wakuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania wastaafu.

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Venance Salvatory Mabeyo amesema ukarabati wa uwanja huo ulioanza tarehe 15 Julai, 2013 umegharimu Shilingi Bilioni 137 na Milioni 631 ikiwa ni ufadhili wa Serikali ya China na umehusisha kujenga upya njia ya kuruka na kutua ndege yenye urefu wa mita 3,000 upana wa mita 45 na unene wa sentimeta 45 pamoja na maegesho ya ndege za kivita na ndege za abiria.

Jenerali Mabeyo ameongeza kuwa uwanja huo ni miongoni mwa viwanja bora zaidi duniani kwa sasa na una uwezo wa kutumiwa na ndege za aina zote zilizo chini ya Boeing 777 huku akibainisha kuwa pamoja na ndege za kivita pia unaweza kutumiwa na ndege za kawaida za abiria kwa dharula.

Nae Balozi wa China hapa nchini Mhe. Dkt. Lu Youqing amesema kujengwa kwa uwanja huo kumeimarisha zaidi uhusiano na ushirikiano kati ya Tanzania na China na amempongeza Mhe. Rais Magufuli kwa kuendeleza uhusiano huo.

Pamoja na kuzindua uwanja huo, Mhe. Rais Magufuli ameshuhudia maonesho ya ndege za kivita zilizorushwa kwa mbinu mbalimbali za kivita, kutoa heshima na kutua katika uwanja huo.

Katika hotuba yake, Mhe. Rais Magufuli amelipongeza Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kwa kazi kubwa linayofanya na pia amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Watu wa China Mhe. Xi Jinping na Serikali yake kwa msaada mkubwa iliyoutoa kujenga uwanja huo.

“Mhe. Balozi Lu Youqing naomba unipelekee shukrani zangu za dhati Mhe. Rais wa China kwa kutoa msaada huu mkubwa wa kujenga uwanja wa ndegevita wa Ngerengere, najua China imetusaidia kujenga Reli ya TAZARA, Kiwanda cha Urafiki na Uwanja wa Mpira, hii yote inathibitisha uhusiano wetu mzuri, urafiki na undugu” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Aidha, Mhe. Dkt. Magufuli ameahidi kujenga barabara ya lami ya kuunganisha Kamandi ya Jeshi la anga ya Ngerengere na barabara kuu ya Dar es Salaam – Morogoro.

Tundu Lissu Aachiwa Kwa Dhamana

0
0
Mwanasheria Mkuu wa Chama na Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu ameachiwa kwa dhamana (ya polisi) iliyowekwa na wanasheria wawili, Hekima Mwasipu na Nashon Nkungu baada ya kushikiliwa na polisi  kwa saa kadhaa leo.

Lissu alikamatwa ghafla leo alipokuwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu baada ya mashitaka yake ya uchochezo katika moja ya kesi zinazomkabili, kufutwa.

Kwa mujibu wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lissu alikamatwa na kushikiliwa kwa tuhuma za kutoa maneno ya uchochezi ambayo yangeweza kuibua mtafaruku wa kidini katika jamii wakati alipokuwa akihutubia mkutano wa kampeni za uchaguzi mdogo Jimbo la Dimani, Zanzibar, mwezi Januari mwaka huu.

Baada ya mahojiano ya leo, Lissu ameachiwa kwa sharti la kuripoti Kituo Kikuu cha Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Machi 13, mwaka huu.

Rais Magufuli Atengua uteuzi wa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Elimu Kibaha

0
0
Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ametengua uteuzi wa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Elimu Kibaha Dkt. Crispin Mpemba ili kupisha uchunguzi dhidi ya tuhuma za kiutendaji zinazomkabili ikiwemo uendeshaji wa shirika hilo

Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari Waziri wa nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI George Simbachawene amesema moja ya tuhuma zinazomkabili ni pamoja na kuingia mikataba kiholela.

Shirika la Elimu Kibaha ni Shirika la umma linalotoa huduma mbalimbali likiwa na ofisi zake Mkoa wa Pwani kilomita 40 Magharibi mwa Mji wa Dar es salaam.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya March 7

Wanafunzi Wapingwa Mabomu ya Machozi Wakati Wakiandamana Kupinga Mwalimu Wao Kuhamishwa

0
0
Jeshi la Polisi katika Wilaya ya Bariadi mkoani  Simiyu, jana liliwapiga mabomu ya machozi wanafunzi wa Shule ya Sekondari Bariadi waliokuwa wakiandamana kupinga Mkuu wa Shule yao, Deus Toga, kuhamishwa.

Wakati wa maandamano hayo yaliyofanyika saa 6.00 mchana wanafunzi hao wapatao 600, walifunga barabara kuu ya Bariadi – Lamadi.

Pia, shughuli mbalimbali za  jamii mjini Bariadi zilisimama kwa zaidi ya saa mbili kwa kuwa hakukuwa na utulivu.

Taarifa zilizopatikana zinasema   wanafunzi hao waliandamana wakipinga Mwalimu Toga kuhamishiwa katika Shule ya Sekondari Giriku.

Kabla ya wanafunzi hao hawajapigwa mabomu hayo, walianza kuandamana kuelekea ofisi ya Mkuregenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Merkzedek Humbe, ambaye ndiye aliyemhamisha Mwalimu Toga.

Wakati wakielekea ofisini kwa mkurugenzi huyo, askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), waliwadhibiti kabla hawajafika walikokuwa wakielekea.

Taarifa zinasema   walipozuiwa kuelekea ofisini kwa mkurugenzi, walibadili mwelekeo na kuelekea ofisini kwa mkuu wa Mkoa wa Simiyu ili wakapeleke malalamiko yao.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, wanafunzi hao walisambaratishwa na askari hao baada ya kufika jirani na Hospitali Teule ya Mkoa wa Simiyu iliyoko Somanda.

Kutokana na hali hiyo, wanafunzi hao wa kidato cha kwanza hadi cha sita, walilazimika kutanda katikati ya barabara ya Bariadi – Lamadi.

Wakiwa barabarani hapo, walikuwa wakiimba nyimbo mbalimbali za kutomtaka Mkuu mpya wa Shule yao, Paul Lutema, aliyepelekwa  kushika nafasi ya Mwalimu Toga.

Pamoja na nyimbo hizo, walikuwa pia wamebeba mabango mbalimbali yenye ujumbe tofauti yakiwamo yaliyosema ‘mlimleta kuinua elimu shuleni kwetu mnamuondoa’, ‘D.E. O’ ni jipu na mengine yalisomeka ‘tunamtaka mkuu wetu Toga’.

Baada ya kukaa kwa muda barabarani hapo, walianza kuwarushia mawe polisi waliokuwa wamewazunguka wasielekee ofisini kwa Mkuu wa Mkoa Simiyu.

Polisi hao walipozidi kupigwa mawe, walilazimika kujibu mapigo kwa kuwarushia mabomu ya machozi   kuwatawanya wanafunzi hao.

Akizungumza kwa niaba ya wenzake, mmoja wa wanafunzi hao ambaye hakutaka jina lake litajwe , alisema walifikia uamuzi huo baada ya kutangaziwa na mwalimu wao wa zamu kwamba Mwalimu Toga, alikuwa amehamishwa.

“Baada ya kutangaziwa hivyo, tuligoma kuingia madarasani na kuamua kuandamana kwenda ofisini kwa mkurugenzi na ofisi ya mkuu wa mkoa kutaka mwalimu wetu arudishwe kwa sababu ni mchapa kazi.

“Wanafunzi wanamtaka Mwalimu Toga kwa sababu tangu afike shuleni kwetu, ufaulu umeongezeka na migogoro ya shule iliyokuwapo imekwisha.

“Hata duka la shule lililokuwa limefungwa kutokana na migogoro ya walimu, limefunguliwa, ndiyo maana wanafunzi wanamtaka mwalimu huyo,” alisema mwanafunzi huyo.

Kutokana na hali ilivyokuwa, Kaimu Mkuu wa Mkoa ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Festo Kiswaga na Ofisa Elimu wa Mkoa, Julius Nestory, walifika  shuleni hapo kuwatuliza wanafunzi kwa kuzungumza nao.

“Kaimu mkuu wa mkoa aliwasihi wanafunzi warejee madarasani kuendelea na masomo kwa kuwa madai yao ya kumtaka Mwalimu Toga yalikuwa yamekubaliwa.

“Lakini ofisa elimu alisema ofisi ya mkurugenzi ilimhamisha Mwalimu Toga kwa makosa kwa sababu haikuzingatia sheria na taratibu za uhamisho kwa sababu mwenye mamlaka ya kuwahamisha wakuu wa shule ni Katibu Tawala wa Mkoa.

“Ofisi ya katibu tawala wa mkoa na ofisi yangu ya elimu, hatukuwa na taarifa za uhamisho huu. Kwa hiyo, tumeamua kuutengua na tunawataka viongozi wenzangu wasifanye uamuzi bila kufuata utaratibu na sheria,”alisema ofisa elimu huyo.

Mwalimu Toga alipotakiwa kuzungumzia tukio hilo  alikataa kusema chochote ingawa alionyesha kushangazwa na uamuzi huo wa wanafunzi.

“Naomba nisizungumze lolote kwa sababu hata mimi nashangaa kusikia haya. Yaani sielewi ni nini kimesababisha yote haya mpaka wanafunzi kufikia uamuzi huu, niacheni,” alisema Mwalimu Toga.

Sasa Ni Rasmi Vodacom Tanzania Kuanza Kuuza Hisa Zake Kwa Wawekezaji

0
0
Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Vodacom Tanzania, Ian Ferrao
**
Kampuni ya simu za mkononi nchini Vodacom Tanzania itakuwa kampuni ya kwanza inayotoa huduma za mawasiliano kuuza hisa zake katika soko la hisa la Dar es Salaam maarufu kama “DSE”. 

Hii inafuatia rasimu ya waraka wa matarajio (Prospectus) na maombi yaliyotumwa kwenye Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA) kukubaliwa.  CMSA ndiyo mamlaka inayosimamia masoko ya mitaji na dhamana nchini.
 
Uuzaji wa hisa za awali wa Vodacom Tanzania Limited PLC ni katika utekelezaji wa Sheria ya Posta na Mawasiliano iliyofanyiwa marekebisho na sheria ya Fedha mwaka 2016 ambayo inaagiza kampuni zote za simu za mikononi kuuza 25% ya hisa zao kwa umma.
 
Hisa za kampuni hiyo inayoongoza kwa kuwa na wateja wengi zaidi nchini, huenda sasa zikaanza kuuzwa muda wowote kuanzia wiki hii au wiki ijayo. 

Vodacom Tanzania inatarajia kuorodhesha asilimia 25 ya hisa zake katika soko la mitaji ambayo ni sawa ni hisa milioni 560 zitakazokuwa na thamani ya shilingi bilioni 476 huku kila hisa ikiuzwa kwa Tsh 850. 
 
Hii ni hatua kubwa sana kwa Vodacom Tanzania ikizingatiwa kwamba kampuni nyingine za simu zinasuasua. Vodacom inatarajiwa kuwa miongoni mwa kampuni zitakazokuwa na mitaji mikubwa katika soko la DSE. 

Kampuni nyingine zenye mitaji mikubwa ni Acacia, EABL na TBL. Hadi hivi sasa DSE ina kampuni 25 zilizoorodheshwa ambapo kampuni za ndani ni 18 na zile zilizoorodheshwa kutoka masoko ya kigeni yakiwemo London na Nairobi ni 7.
 
Taarifa rasmi za mauzo ya awali ya hisa hizo milioni 560 lini zitaanza kuuzwa, na wawekezaji gani watakidhi vigezo zitatangazwa hivi karibuni. Tutazidi kukuletea taarifa hizi za uwekezaji kwa makampuni ya simu nchini.

Lipumba Amtumbua Maalim Seif......Amteua Magdalena Sakaya Kukaimu Nafasi ya Katibu Mkuu CUF

0
0
Mgogoro wa Uongozi wa Chama cha Wananchi CUF umeendelea kufukuta ambapo Mwenyekiti wa Chama hicho anayetambuliwa na Ofisi ya Msajili Vyama vya Siasa nchini Prof. Ibrahim Lipumba amemteua Naibu Katibu Mkuu Bara, Magdalena Sakaya kukaimu nafasi ya Katibu Mkuu Maalim Seif Sharif Hamad baada ya Maalim Seif kukaidi wito wa Mwenyekiti wake kwenda Ofisi kuu Buguruni kwa zaidi ya mara nne

Prof. Lipumba akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam pamoja na wafuasi wa chama hicho, amesema Maalim Seif amekaidi wito wa kwenda Makao Makuu Buguruni tangu Septemba 23 mwaka jana kwa ajili ya kusimamia mkutano wa kamati ya Utendaji ambao ulitakiwa kujadili mambo kadhaa ya chama hicho

Aidha, Prof. Lipumba amewavua madaraka wakurugenzi kutoka Zanzibar akiwemo Salim Bimani aliyekuwa Mkurugenzi wa Habari na Uenezi, Omar Ali Salehe Mkurugenzi Mipango na Uchaguzi, Abdalah Bakar Khamis Mkurugenzi wa Fedha na Uchumi, Pavu Juma Abdallah - Haki za Binadamu, Mahima Ali Mahima Katibu Mtendaji JUVICUF pamoja na Yusuph Salim Naibu Mkurugenzi Ulinzi na Usalama CUF wote kutoka Zanzibar.

Chama cha Wananchi CUF kimekumbwa na Mgogoro wa uongozi tangu Prof. Lipumba alipotangaza kujiuzulu uongozi wa chama hicho kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, ambapo baadaye alitangaza kurudi na kufanyika mkutano mkuu ambao ulivurugika na kusababisha mpasuko kati ya CUF bara na CUF Zanzibar.

Mrisho Mpoto awataka wananchi kuangalia utendaji kazi wa Makonda na siyo vyeti Vyake

0
0
Msanii wa muziki wa asili nchini Mrisho Mpoto ameamua kumkingia kifua RC Makonda ambaye kwa siku za karibuni amekuwa aki-trend kwenye mitandao ya kijamii akituhumiwa kufoji vyeti.

Mpoto amedai anashangaa kuona hata wale ambao walikuwa wanamsupport na kumsifia mkuu huyo wameshinndwa kufungua midomo yao.

“Hii nchi ya ajabu sana ukifanya vizuri lazima upate maadui mpaka wakushushe, ndiyo waanze kumpansisha mwingine. Wako wapi waliosema Makonda songa mbele usirudi nyuma? mko wapi mliomuita Makonda shujaa mkombozi wa Wa watoto wetu, leo kila mtu anamruka na kuona hakuna alichofanya This is not Fair at all,” alianidika Mpoto Instagram.

“Angalieni utendaji wake Wa kazi na siyo vyeti vyake guys!! Songa Songa Songa Makonda kama ulivyosema hii vita siyo ndogo na ina wanafiki wengi. @paulmakonda @paulmakonda unawaona waleeeeeee ndiyo siyo watu wazuri kabisa!!,” aliongeza Mpoto.

Mkuu huyo hivi karibuni alidai hayo yote yamezalishwa kutokana na vita yake dhidi ya madawa ya kulevya ambayo umezaa matunda kwa kiasi kikubwa.

Kituo cha Mafuta Tegeta Jijini Dar Chateketea Kwa Moto

0
0
Kituo cha mafuta kilichopo eneo la Tegeta Azania jijini Dar as Salaam kineteketea kwa moto.Chanzo cha ajali hiyo ni gari lililokuwa likishusha shehena ya mafuta kushika moto.

Mama Mlezi wa Rais Mstaafu Jakaya Kikwete Afariki Dunia

0
0
Mama mlezi wa aliyekuwa Rais Wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete, Bi Nuru binti Halfani Shomvi amefariki dunia katika Hospitali ya Muhimbili alipokuwa akitibiwa asubuhi ya leo.

Kupitia mtandao wa twitter, Rais Mstaafu Jakaya Kikwete akishukuru jamii kwa salamu za pole alizopokea amesema shughuli za msiba ziko nyumbani kwa marehemu Mzee Kikwete, Mtaa wa Caravan, Bagamoyo na maziko yatakuwa Bagamoyo mjini, kesho Jumatano Machi 8, 2017 saa 10 Alasiri.

"Mama amefariki jana usiku saa nane, akiwa na miaka 91. Baba yangu, Mzee Halfani Mrisho Kikwete alikuwa na wake wawili alipofariki 1998. Mama yangu mzazi Bi Asha binti Jakaya, aliyekuwa mke mkubwa wa Mzee Halfani Kikwete alifariki 1999; tukabaki na mama yetu huyu mdogo". Kauli ya Jakaya Kikwete

Naye Mbunge wa Chalinze Mhe. Ridhiwan Kikwete ambaye ni mjukuu wa marehemu ndiye aliyekuwa wa kwanza kuthibitisha kutokea kwa kifo hicho asubuhi ya leo.

"Ndugu na marafiki nasikitika kuwatangazia msiba/kifo cha Bibi yetu Bi. Nuru Khalfan Kikwete kilichotokea asubuhi hii katika Hospitali ya Muhimbili alipokuwa amelazwa kwa matibabu. Taratibu za mazishi tutajulishana" Amesema Ridhiwan Kikwete.
 
Ndugu wapendwa, nawashukuru sana kwa salamu za pole na upendo kufuatia kifo cha Mama yangu mdogo mpendwa Bi Nuru binti Halfani Shomvi. – JK
— Jakaya Kikwete (@jmkikwete) March 7, 2017




CUF ya Maalim Seif kuiburuza CUF ya Prof.Lipumba mahakamani

0
0
Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Wananchi (CUF ), imefungua kesi ya madai dhidi ya wanachama wake nane akiwemo Naibu Katibu Mkuu, Magdalena Sakaya

Kesi hiyo imefunguliwa leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ikitaka wanachama hao wasijihusishe na harakati  zozote za chama hicho.

Mbali ya Sakaya ambaye pia ni mbunge wa Kaliua mkoani Tabora, wadaiwa wengine ni Thomas Malima, mbunge wa Mtwara Mjini,Mafta Nachumu, Omar Mhina Masoud, Abdul Kambaya, Salama Masoud, Zainabu Mndolwa na Jafari Mneke.

Maombi hayo mbayo yametajwa mbele ya Hakimu Mkazi, Wilbard Mashauri yamewasilishwa na Wakili wa bodi, Hashim Mziray na yamepangwa kusikilizwa kesho.

Katika maombi hayo yaliyopewa namba 1 ya mwaka 2017, bodi inaiomba mahakama kutoa zuio kwa wadaiwa kutojihusisha katika masuala yeyote yanayohusiana na chama hicho.

Mbali ya maombi hayo, pia Wakili Mziray amewasilisha maombi madogo ya kuiomba mahakama kuwaamuru wadaiwa wasijihusishe na mikutano ya chama hicho.
 
Aidha, Mziray aliomba maombi yao madogo yasikilizwe kwa upande mmoja wa wadai tu kwa kuwa wamechelewa kuwapatia nyaraka za madai yao wadaiwa.

"Mheshimiwa tunaomba tusikilizwe upande mmoja ukizingatia maombi yameletwa chini ya hati ya dharula na kwa mujibu wa sheria mahakama hii... inayo mamlaka ya kufanya hivyo".

Hakimu Mashauri alisema anakubaliana na upande wa wadai na maombi hayo yatasikilizwa kesho mahakamani hapo.

Hatua ya Bodi ya CUF, kukimbilia mahakamani inakuja ikiwa ni siku moja baada ya upande unaomuunga mkono Katibu Mkuu wa chama hicho, Maalim Seif Shariff Hammad kupinga uteuzi wa Mwenyekiti wa chama hicho, Profesa Ibrahim Lipumba.

Uteuzi wa Profesa Lipumba ambao unapingwa ni ule alioufanya Machi 6, mwaka huu baada kuwaondoa katika nafasi zao, Mkurugenzi wa Mipango na Uchaguzi, Omar Ali Shehe.

Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mahusiano na Umma, Salim Abdull Bimani, Mkurugenzi wa Fedha na Uchumi, Abdullah Bakar Hassan.

Wengine ni Pavu Juma, Naibu Mkurugenzi wa Haki za Binadam na Sheria, Mahmoud Ali Mahindo na Katibu wa Jumuiya ya Vijana, Yusuph Salim.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya March 8

Sakata la Madawa: Vanessa Mdee Akamatwa na Polisi, Apelekwa kwa Mkemia Mkuu

0
0
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linamshikilia mwanamuziki Vanessa Mdee maarufu Vee Money kwa tuhuma za kujihusisha na biashara haramu ya dawa za kulevya.

Akizunguzumzia taarifa hiyo, Mwanasheria wa mwanamuziki huyo, Amin Tenga amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo amesema kuwa Vanessa alijisalimisha mwenyewe katika kituo cha polisi kama alivyoagizwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam wakati akitaja majina ya watuhumiwa wa dawa hizo mapema mwezi uliopita.

Vanessa ni miongoni mwa watu waliotajwa katika orodha ya watuhumiwa wa dawa za kulevya, lakini hakuweza kuripoti kwa wakati sababu alikuwa nchini Afrika Kusini kikazi.

Baada ya kujisalimisha, Jeshi la Polisi lilifanya upekuzi nyumbani kwake kabla ya kumpeleka kwa Mkemia Mkuu wa Serikali kwa ajili ya uchunguzi zaidi.

Jeshi la Polisi hadi sasa halijatoa taarifa kuhusu tukio hilo na kama walikuta ushahidi wowote nyumbani kwa mwanamuziki huyo.

Rais Magufuli na mkewe wawasili mkoani Dodoma

0
0
Rais wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, amewasili Mkoani Dodoma ambako pamoja na mambo mengine ataongoza Kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa, Mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa na Mkutano Mkuu Maalum wa Chama Cha Mapinduzi.

Mhe. Dkt. Magufuli ambaye ni Mwenyekiti wa CCM ataongoza kikao na mikutano hiyo kuanzia tarehe 10 - 12 Machi, 2017 Mjini Dodoma.

Mhe. Rais Magufuli akiwa na Mkewe Mama Janeth Magufuli waliwasili jana katika Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma akitokea Mkoani Morogoro ambako jana tarehe 06 Machi, 2017 alizindua uwanja wa kisasa wa ndegevita wa Ngerengere.

Saida Karoli Asimulia Alivyoporwa Haki Zake Katika Muziki Kisa Kutojua Kusoma na Kuandika

0
0
Jana kupitia kipindi cha Take One  cha Clouds TV, mtangazaji Zamaradi  alimuhoji mwimbaji wa muziki wa asili  Saida Karoli ambapo alikiri kuwa hana haki kwenye nyimbo zake kutokana na mikataba aliyosainishwa na Meneja wake sababu na yeye hakuwa anajua kusoma na kuandika na akadai zaidi ya album tano hana haki nazo na meneja wake wa zamani ndio mwenye haki nazo.

Kingine alichozungumza Saida ni kuhusu wimbo wa Salome ambao Diamond Platnumz aliurudia  ambapo alisema ana hesabu kama alitoa bure kwani hata fedha aliyopewa ni kidogo na haifai kuongelea.

”Siwezi kulalamika hata kidogo, mara nyingi naulizwa nasema sina tatizo, sina haki na zile nyimbo maana yeye ndio alinipa mikataba na yeye ndio alinitengenezea, hata hii ya Diamond naweza nikasema ikawa mbaya zaidi maana fedha niliyoipata siyo ya kuongelea, kwahiyo mimi najiona nimetoa bure

”Waandishi kila siku wanakuwa wananiuliza nawambia nimempa Diamond nyimbo bure na nimetoa kwa moyo mmoja kweli, roho yangu moja

“Meneja wa zamani aliniuliza nyimbo yako inatakiwa kutumika lakini nipe idhini yako japo ni nyimbo zangu zote lakini sikuwa na haki licha ya kuwa sauti yangu imesikika kule, mimi nilimjibu nimeshakata tamaa na kuimba naona muziki kwangu hauna faida na thamani bora kuwa hata mkaanga vitumbua au maandazi kuliko kuimba

”Nilikuwa na mpango wa kurudi kijijini nyumbani nikae mtu akihitaji show atanikuta kijijini lakini meneja akanambia hapana, alisema nyimbo tumpe Diamond kwa sababu itaniinua na kunipa moyo na kuniamsha upya kama mtu aliyekufa

“Walizushaga nimekufa na nilihisigi nimekufa kweli kutokana na hali ya maisha na nilikuwa nimekata tamaa nikajua nimekufa kweli” Alisema Saida Karoli

Kwa sasa Saida yupo Dar na amekuja rasmi kwa ajili ya kufanya muziki upya kama zamani na yupo tayari kufanya kolabo na wasanii kama Ben pol, Bell 9, Diamond na Darassa.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamidi ya March 9

Zanzibar kukatiwa umeme baada ya siku 14

0
0

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limetoa siku 14 kwa Shirika la Visiwani Zanzibar (ZECO) kulipa deni lote la ankara za umeme wanalodaiwa na endapo halitafanya hivyo basi hatua kali za kisheria zitachukuliwa ikiwa ni pamoja na kukatiwa umeme.

Kauli hiyo imetolewa leo na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa shirika hilo Dkt. Tito Mwinuka alipokuwa anaongea na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam ambapo amesema hadi kufikia mwezi Januari mwaka 2017, Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO) lilikuwa linadaiwa zaidi ya shilingi bilioni 127.8.

“Shirika la umeme linashindwa kutekeleza majukumu yake mbalimbali kwa wakati ikiwemo uendeshaji wa shirika, matengenezo ya miundombinu pamoja na utekelezaji wa miradi, hayo yote yanasababishwa na malimbikizo ya madeni kwa wadaiwa sugu hivyo tunatoa siku 14, wasipoweza kulipa tutawakatia huduma ya umeme”. Alisema Dkt Mwinuka

Aidha mbali na ZECO, Tanesco imewataja wadaiwa sugu wengine ikihusisha Wizara na Taasisi za serikali zikiwa zinadaiwa zaidi ya bilioni 52.5, makampuni binafsi pamoja na wateja wadogo wanaodaiwa zaidi ya bilioni 94.9

Kwa upande mwingine Dkt. Mwinuka amesema shirika hilo linatarajia kuanza oparesheni maalum ya kukusanya madeni hayo na matarajio yao ni kulipwa kwa malikimbizo yote ili yalisaidie kujiendesha kiushandani na kwa ufanisi mkubwa zaidi na kuchochea kasi ya ukuaji sekta mbalimbali zinazotegema nishati ya umeme nchini.

Hatua hii imekuja ikiwa ni takriban siku 4 tangu Rais Magufuli kuagiza TANESCO kufuatilia madeni yote ikiwemo deni ambalo TANESCO inalidai ZECO, na kuitaka kuwakatia umeme wote watakaoshindwa kulipa kwa wakati.

Mfanyabiashara Ajiua baada ya kukamatwa na viroba

0
0
Kamatakamata ya wafanyabiashara wa viroba nchini, imesababisha kifo cha mfanyabiashara maarufu mjini Dodoma, Festo Mselia anayedaiwa kujiua kwa risasi baada ya kukaguliwa mara mbili na polisi kutokana na kumiliki bidhaa hiyo.

Kampeni ya kukamata wafanyabiashara wa viroba nchini, inayosimamiwa na Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) ilianza Machi mosi mwaka huu, baada ya Serikali kutoa taarifa ya mwisho wa biashara hiyo tangu Mei, mwaka jana.

Mei mwaka jana, Serikali ilibainisha kuwa kuanzia kipindi hicho hadi Januari mosi mwaka huu, ungekuwa mwisho wa kuzalisha biashara ya pombe kali inayohifadhiwa katika vifungashio hivyo (viroba).

Hata hivyo, Januari Serikali iliongeza muda hadi Machi mosi ili kutoa nafasi tena kwa wafanyabiashara waliokuwa na shehena ya vinywaji hivyo waliofuata taratibu, kumaliza, lakini wengi wamekamatwa wakiwa nazo katika msako unaoendelea hivi sasa.

Mfanyabiashara huyo anayemiliki kampuni ya Mselia Enterprises na duka la bia za jumla, baa na nyumba za kulala wageni mjini Dodoma, alijipiga risasi kwenye shavu la kushoto juzi, Jumanne akiwa shambani kwake Veyula, nje kidogo ya mji wa Dodoma.

Daktari wa zamu katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma, Carolyn Damian alisema alimpokea Mselia hospitalini hapo akiwa mahututi saa 7 usiku, na kumweka katika chumba cha uangalizi maalumu (ICU) na robo saa baadaye alifariki.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Lazaro Mambosasa alithibitisha kupewa taarifa na mtu kuhusu kusikika kwa mlio wa risasi saa 3 usiku na baadaye saa 5 aliwatuma askari na kwenda kuchunguza na ndipo walipomwona mfanyabiashara huyo, amejipiga risasi na alikufa kutokana na kutokwa na damu nyingi.

Mambosasa alisema baada ya kupewa taarifa, askari walifuatilia eneo ambalo risasi zilisikika katika shamba la mfanyabiashara huyo eneo la Veyula na walipofika, waliokota maganda matano ya risasi alizotumia kujiua.

Mfanyakazi wa mfanyabiashara huyo, Leslie Msigwa alisema ni kweli polisi walikwenda mara mbili dukani kwake Barabara ya 11, karibu na Ofisi za TFDA, na mara ya mwisho waliondoka naye akiwa kwenye gari lake prado likiendeshwa na mteja wao, Mazengo hadi waliposikia kwamba amejiua shambani kwake, Veyula Dodoma.

Msigwa alisema ni kweli kwenye stoo yake, kulikuwa na katoni 1,269 za viroba pamoja na vinywaji vingine, ambavyo huwa wanasambaza katika baa na maduka mbalimbali.

Msigwa alisema Ijumaa iliyopita, polisi walifika dukani kwake wakiwa kwenye magari mawili wakiwa na silaha, wakaingia kukagua ndani na wakaondoka na wao, wakaenda benki kuweka fedha na kulipia mzigo iliyoagizwa.

Alisema walimtaka aripoti polisi Jumatatu ya wiki hii na alifanya hivyo na akarudishwa na polisi dukani na aliingia chumba cha kupumzikia, akalala hadi saa 1 usiku waliondoka kwenda nyumbani eneo la Area D.

Mfanyakazi huyo alisema juzi, aliitwa polisi, kila alipopigiwa simu alidai anakuja hadi ilipofika saa 10 ndipo zilikuja gari za polisi mbili pamoja naye, akashuka akaingia ndani na baadhi yao wakatoka na kuondoka, yeye aliwafuata akiwa kwenye prado ikiendeshwa na mteja wake, Mazengo.

Habari kutoka shambani kwake Veyula, zilisema ni kweli siku ya tukio, Mselia alikwenda na Mazengo, akamwacha nyuma mahali ilipo mifugo, yeye akaendelea mbele na walipoona anachelewa, walimfuata na wakaona amejeruhiwa kwenye shavu.

Msigwa alisema, yeye na mkewe walipoona anachelewa kurudi, walifunga duka na wakarudi nyumbani hadi ilipofika saa 2.30, wakaanza kupata taarifa kutoka kwa ndugu zao kwamba Mselia amejipiga risasi shambani Veyula.

Mbowe alivyoshiriki msiba wa Mama Mdogo wa Rais Mstaafu Jakaya Kikwete

0
0
Msiba wa mama mdogo wa Rais Mstaafu, Jakaya Kikwete, umewakutanisha kwa mara ya kwanza hadharani kiongozi huyo wa Serikali ya awamu ya nne, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Bernard Membe.

Wakati wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, viongozi hao walionekana mahasimu zaidi baada ya aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, jina lake kukatwa katika kinyang’anyiro cha mbio za urais ndani ya CCM na kuhamia Chadema.

Baada ya Uchaguzi Mkuu kumalizika, Rais huyo mstaafu hakuwahi kuonekana hadharani akiwa na viongozi hao wa upinzani, huku Membe yeye akiwa haonekani kabisa kwenye mambo ya siasa wala mikusanyiko yoyote ile.

Lakini jana mazishi ya mama huyo, Nuru Khalfan, mbali ya kuwakutanisha viongozi hao, yaliwakutanisha pia Waziri Mkuu Mstaafu, Mizengo Pinda na Waziri wa Habari, Sanaa, Michezo na Utamaduni, Nape Nnauye.

Wengine walioudhuria ni Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP, Reginald Mengi na Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Evarist Ndikilo.

Waziri mkuu, Kassim Majaliwa, ndiye aliyeongoza mamia ya waombolezaji kwenye mazishi hayo yaliyofanyika Bagamoyo mkoani Pwani.

Mara baada ya kumalizika kwa mazishi hayo, Mbunge wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete, aliwashukuru wananchi wote waliojitokeza kushirikiana nao kwenye msiba huo.

Alisema madaktari na wauguzi wa Hospitali ya Muhimbili wamefanya kazi kubwa katika kipindi alichokuwa bibi yake amelazwa.

"Naomba niwashukuru madaktari na wauguzi wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) kwa sababu wamefanya kazi kubwa sana katika kipindi chote ambacho mgonjwa amelazwa hadi alipofariki," alisema Ridhiwani.

Rais Magufuli Aongoza Kikao Cha Baraza La Mawaziri Mjini Dodoma

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiongoza Kikao cha Baraza la Mawaziri mjini Dodoma leo tarehe 9/03/2017. Kikao hicho pia kimehudhuriwa na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan pamoja na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa. PICHA NA IKULU.

Rais Dkt Magufuli akiagana na Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan mapema leo mchana mara baada ya kumaliza kikao cha Baraza la Mawaziri mjini Dodoma,kulia ni Waziri Mkuu Kassim Majaliwa
Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan akijadiliana jambo na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa baada ya kutoka kwenye kikao cha Baraza la Mawazili,kilichofanyika leo mjini Dodoma
Waziri wa habari,Utamaduni Sanaa na Michezo,Nape Nnauye akizungumza jambo na Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji,Charles Mwijage kabla ya kuanza kikao cha Baraza la Mawaziri mjini Dodoma leo.PICHA NA OFISI YA MAKAMU WA RAIS.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images