Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Ridhiwani Kikwete ajibu shutuma ya kutajwa kwenye orodha ya watuhumiwa wa dawa za kulevya

$
0
0
Mbunge wa jimbo la Chalinze mkoani Pwani kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Ridhiwani Kikwete amekanusha vikali shutuma zilizotolewa dhidi yake kuhusu kujihusisha na biashara haramu ya dawa za kulevya.

Moja ya magazeti ya leo yamechapisha habari inayomtaja mbunge huyo kujihuisha na bishara ya dawa za kulevya ambayo imekuwa ikipigwa vita kila kona ya nchi kutokana na kupoteza nguvu kazi ya taifa.

Gazeti hilo limeandika kuwa, jina la Ridhiwani limetajwa katika orodha ya watuhumiwa wa dawa za kulevya na kuwa uchunguzi utafanyika. Pia limesema mbunge huyo ametoa kauli nzito kwa hadhara.

Kiongozi huyo kupitia ukurasa wake wa Twitter amesema kuwa, hafanyi biashara hiyo haramu wala hakuwahi kufikiria kuifanya na kwamba nafsi yake i tayari kufa masikini kuliko kupata utajiri kupitia njia hiyo.

Aidha, ameeleza kuwa, anaamini kwamba uchunguzi utafanywa ili kuweza kuweka mambo sawa kwani yeye hana kitu chochote cha kuficha. 

Amesema kwamba, maneno hayo ya shutuma juu yake ni ya uongo na kwamba yametolewa na watu wasiomtakia mema na wasio na haya.



Jalada La Masogange Lakwama Kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG)

$
0
0
Msanii  maarufu anayepamba  video za wasanii wa muziki wa bongo Fleva (Video Queen) Agnes Gerald maarufu Masogange ameendelea kusota rumande, huku jalada lake likiendelea kuwa mikononi mwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG).

Masogange (25), alikamatwa na Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam kwa tuhuma za kujihusisha na uuzaji, usafirisha na kutumia dawa za kulevya.

Masogange alitarajiwa kupandishwa kizimbani Ijumaa wiki iliyopita lakini ilishindikana kutokana na majibu ya Mkemia Mkuu wa Serikali dhidi ya vipimo vyake kuonesha kama anatumia au hatumii dawa hizo kutokamilika.

Hata hivyo alitarajiwa kufikishwa tena Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu juzi ambapo alikwama tena kutokana na jalada lake kupelekwa kwa AG.

Wakili wa Masogange, Nick Kitege  amesema bado jalada la Masogange lipo kwa AG na anaendelea kulifanyia kazi na pindi litakapokamilika muda wowote anaweza kupelekwa mahakamani.

Alisema jalada hilo limechelewa kutokana na taratibu za kisheria zinazofanywa ili kukamilisha uchunguzi.

 “Bado tupo tunafuatilia na jalada la kesi yake kwa sasa lipo kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali pindi taratibu zitakapokamilika atafikishwa mahakamani kati ya leo au kesho.

“Kuhusu ucheleweshwaji wa kesi hiyo ni kutokana na taratibu za kisheria, hivyo  Polisi waachwe wafanye kazi yao na sisi tunaangalia hatua zinazoendelea.

“Unajua hivi ni vyombo vya sheria na wanafanya kazi yao, wanahitaji muda kuchunguza na kutoa hoja zilizojitosheleza, bado wanahangaika kushughulikia suala hilo naamini leo tutapata jibu kamili,” alisema Kitege.

Julai mwaka 2013 Masogange alikamatwa Afrika Kusini katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Oliver Tambo, akiwa na mwenzake aliyejulikana kwa jina la Melisa Edward wakiwa na mzigo wa dawa za kulevya wenye thamani ya zaidi ya Sh bilioni 6.8.

Wanafunzi wanne kizimbani kwa kumkashifu Rais

$
0
0
Wanafunzi  wanne wa Chuo Kikuu cha Kampala Dar es Salaam, wamefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala, wakikabiliwa na shitaka la kuchapisha picha zinazoonyesha Rais Dk. John Magufuli amevaa hijabu kama mwanamke wa Kislamu na kuzisambaza kwenye mtandao wa WhatsApp.

Shtaka jingine ni kusambaza taarifa za uongo kwenye mitandao ya  amii (WhatsApp) kwa lengo la kumuudhi Rais.

Washitakiwa hao ni Amenitha Kongo (19), Maria Tweve (20), Agnes Gabriel (21) na Anne Mwansasu(21).

Walifikishwa mahakamani hapo jana   mbele ya Hakimu Mkazi, Catherine Kiyoja.

Akisoma mashitaka hayo, Wakili wa Serikali,  Florida Wenceslaus, alidai washitakiwa walitenda kosa hilo Juni 9, mwaka jana  Dar es Salaam.

Florida alidai washitakiwa kwa pamoja walitengeneza picha hizo kwa kutumia kompyuta na baadaye kuisambaza kwenye WhatsApp kwa lengo la kumuudhi Rais.

Washitakiwa walikana shitaka hilo na kurudishwa rumande kutokana na kutotimiza masharti ya dhamana.  Kesi itatajwa tena Machi 13, mwaka huu.

Masogange apandishwa kizimbani, aachiwa kwa Dhamana ya Milioni 10

$
0
0

Msanii  Agnes Gerald 'Masogange' amepandishwa kizimbani leo katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kusomewa mashitaka ya kutumia dawa za kulevya.

Mrembo huyo ambaye ni maarufu kwa kupamba video za muziki wa wasanii wa bongo fleva, amekana tuhuma hizo na kesi yake kuahirishwa hadi Machi 2i mwaka huu.

Katika mashtaka yake mawili yaliyosomwa na mwendesha mashtaka Mashauri Wilboard chini ya wakili wa serikali Constatine Kokulwa, Agnes anadaiwa kutumia dawa za kulevya aina ya Heroin na Oxazepan kwa nyakati tofauti.

Mara baada ya kusomewa mashtaka yake, ameachiwa kwa dhamana ya wadhamini wawili pamoja na kusaini bondi ya shilingi milioni 10.

Pia mrembo huyo ambaye amewahi kukamatwa nchini Afrika Kusini akihusishwa na usafirishaji wa dawa za kulevya, ametakiwa kutotoka nje ya Dar es Salaam kwa kipindi chote cha kesi bila kibali cha mahakama.

Zitto Kabwe azidi kuibana Serikali Kuhusu ufisadi wa IPTL....Amtaka Rais Magufuli Achukue Hatua

$
0
0
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi wa ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, ameendelea kumtaka Rais Magufuli kuchukua hatua dhidi ya anachokiita ufisadi katika kampuni ya uzalishaji umeme ya IPTL, inayomilikiwa na Kampuni wa PAP.

Tangu Rais Magufuli alipoingia madarakani mwezi Novemba mwaka 2015, Zitto amekuwa mstari wa mbele kumsihi na kumuomba Rais Magufuli afanye maamuzi juu ya kampuni hiyo ambayo imekuwa ikilipwa milioni 300 kila siku bila kujali kama inazalisha umeme au la.

Kupitia mitandao ya kijamii, Zitto ameandika "Rais John Magufuli ana fursa ya kihistoria kumaliza kabisa huu mtandao wa wizi na utapeli uliodumu toka mwaka 1995. watanzania masikini na wanyonge tutakuwa nyuma yake kwenye hili. Atende sasa."

Mnamo tarehe 21, Septemba 2016 Mhe. Zitto Kabwe alimtaka tena Rais Magufuli aoneshe hasira zake dhidi ya hicho anachokiita ufisadi mkongwe wa IPTL huku akieleza masikitiko yake juu ya kutochukuliwa kwa hatua zozote hadi sasa.

Mhe. Zitto Kabwe ambaye amekuwa hachoki kulizungumzia sakata hilo la IPTL amehoji ni nini kipo nyuma ya pazia, na ni nani mfaidika hadi hatua zisichukuliwe, huku akitoa ushauri wa hatua zinazoweza kuchukuliwa na mahakama kwa sasa.

"Mahakama Ina uwezo wa kurejea maamuzi yake kwa kuitisha upya kesi zilizoamuliwa. Hivi hii Mahakama haioni suala la PAP kumiliki IPTL na kuchota mabilioni ya fedha zilizokuwa Benki Kuu na kuendelea kulipwa tshs 300m kila siku izalishe au isizalishe umeme? Ushahidi wote ulionyesha utapeli wa Kimataifa uliofanywa na Harbinder Singh Seth lakini kivuli cha uamuzi wa Mahakama umefanya matapeli hawa kuendelea kunyonya fedha kutoka TANESCO. Huu mrija wa PAP/IPTL upo kinywani mwa The Chato Inc? Ama ni jipu la mgongoni?". Alihoji Mhe. Zitto Kabwe

Wafanyakazi 14 wa Kampuni ya Quality Group ya Manji Wafikishwa Mahakamani

$
0
0
Raia  14 wa India ambao wanafanya kazi Quality Group iliyo chini ya Yusuf Manji leo wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kujibu mashtaka matatu likiwemo la kufanya kazi nchini bila ya kuwa na kibali.

Washtakiwa hao wamesomewa mashtaka mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Cyprian Mkeha.

Hati ya mashtaka, iliyosomwa na mwendesha Mashtaka, wa uhamiaji Method Kagoma imewataja washtakiwa hao kuwa ni Rojat Surkar, Jagadish Mamidu, Niladri Maiti, Sivarar Raja Sekaran, Mohammed Taher Shaikh, Bijenda Kumar, Prasoon Kumar Mallik na Nipun Dinbandhu Bhatt.

Wengine ni Pintu Kumar, Anuj Agurwa, Varun Boloor, Arun Kumar Kateel, Avinash Chandratiwari na Vikram Sankhala.

Akisoma hati ya mashtaka, Kagoma amedai kuwa, Februari 13, mwaka huu, huko katika ofisi ya Quality Group Ltd iliyopo katika Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam, washtakiwa hao walikutwa wakiwa na viza zilozoghushiwa za kufanyia kazi.

Katika shtaka la pili ilidaiwa kuwa siku na mahali hapo washtakiwa hao wakiwa raia wa India walikutwa wakiishi nchini Tanzania bila ya kuwa na kibali.

Kagoma aliongeza kuwa, Februari 13 mwaka huu, katika jengo la Quality Group washtakiwa hao wakiwa raia wa India walikutwa wakijihusisha na kufanya kazi katika kampuni hiyo kama washauri bila ya kuwa na kibali cha kufanya kazi nchini.

Hata hivyo, washtakiwa hao ambao wanatetewa na mawakili watatu, Alex Mgongolwa na Hudson Ndusyepo wamekanusha kujihusisha na tuhuma hizo na wako nje kwa dhamana baada ya kutimiza masharti ya dhamana.

Mahakama iliwaamuru washtakiwa hao kuweka dhamana ya milioni tano kila mmoja na kuleta mdhamini mmoja kila mtu atakayeweka  kiasi hicho cha fedha.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Machi 7, mwaka huu.

Wema Sepetu Atinga Maahakamani....Kesi Yaahirishwa Hadi March 15

$
0
0
Mwigizaji Wema Sepetu leo alienda tena  Mahakamani baada ya kuachiwa kwa dhamana kwenye sakata la dawa za kulevya baada ya kutajwa na mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi  15 March 2017 baada ya upande wa Mashtaka kusema upelelezi bado  haujakamilika 

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya February 23


TCU Yatoa majina ya wanafunzi wa vyuo vikuu ambao hawana sifa ya kuendelea na masomo

$
0
0
Hapa chini ni majina ya wanafunzi wanaoendelea na masomo katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) ambao hawana sifa.
Kuweza kuona majina zaidi ya wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali, bonyeza jina la chuo husika hapa chini kwenye orodha.

Polisi aua mwenzake kwa Kumpiga Risasi na Kisha na Yeye Kujiua

$
0
0
Polisi  amemuua mwenzake kwa kumpiga risasi usiku wa kuamkia leo na yeye amejiua baada kutazama mechi ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya kati ya Manchester City na Monaco.

Kabla ya polisi huyo, Konstebo Constable Patrick Kihagi kujiua kwa kujipiga risasi kichwani, alimjeruhi polisi mwingine kwa kumpiga risasi begani.

Polisi aliyekufa ametajwa kwa jina la Konstebo James Makokha, na kabla ya kifo alikuwa akifanya kazi Jogoo House.

Inadaiwa kuwa Makokha alipigwa risasi wakati akitaka kumaliza ubishani kati ya Kihagi na Ng’etich.

Kabla ya tukio hilo saa saba na nusu usiku kwenye eneo la Tassia, Nairobi nchini Kenya, polisi hao watatu walikuwa baa wakitazama mpira na kisha wakaanza kubishana, wakatoka nje.

Mashuhuda wanadai kuwa, walipotoka nje walizidi kubishana, Kihagi akatoa bastola na kumjeruhi mwenzake, Konstebo Dominic Ng’etich kwa risasi.

Kihagi alikuwa akifanya kazi katika kituo cha Embakasi, Ng’etich anafanya kazi kwenye kituo cha polisi kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta.

Mwanafunzi akipata mimba mzazi jela miaka 30

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, amesema serikali itatoa adhabu kali ya kifungo cha miaka 30 jela kwa wazazi wote wawili wa mtoto wa kike atakayekatishwa masomo na kulazimishwa kuolewa ama akipata ujauzito.

Aidha amesema Serikali itamfunga jela miaka 30 kijana anayetaka kumuoa msichana anayesoma pamoja na wazazi wake.

Amesema Serikali ya awamu ya tano imedhamiria kumlinda mtoto wa kike katika kuhakikisha kuwa anapata haki yake ya msingi ya kusoma kufikia elimu ya chuo kikuu kwa kujenga mabweni na kuwachukulia hatua kali za kisheria watu watakaowapa mimba na kuwaozesha katika umri mdogo na kukatisha masomo yao.

Majaliwa aliyasema hayo jana wilayani Hanang, mkoani Manyara katika ziara yake ya kikazi ya siku sita kwa mkoa huo.

Alisisitiza kuwa kupitia sera ya kuboresha elimu nchini serikali imeondoa michango ya fedha za kulipia bili za maji, umeme, gharama za mlinzi na mitihani ili kumpunguzia gharama mzazi na mlezi na kuwaacha wazazi kushughulikia maeneo mengine muhimu kwa mtoto wao.

Alisema tayari kwa mwaka huu wa fedha, walimu 4,396 wa masomo ya sayansi wameajiriwa ambapo alisisitiza kuwa wazazi na walezi wanalo jukumu kubwa la kusimamia maendeleo ya shule ya watoto wao kwa lengo la kupandisha ufaulu wa elimu kwa wilaya,mkoa na taifa.

“Mtoto akiwa mtoro baba na mama wa mtoto huyo atashitakiwa,mtoto wa kike asiguswe,vijana waendesha bodaboda acheni kuwalaghai watoto hao kwa zawadi na usafiri, tutawasaka wote,” alisisitiza.

Akizungumza na watumishi wa umma katika halmashauri ya wilaya hiyo, aliwataka watumishi hao kujivunia serikali yao kwa kuienzi katika kufanya kazi kwa nidhamu katika kuwatumikia wananchi bila kujali uwezo wao, kabila wala rangi zao kwa kuwa wamepewa dhamana ya kusikiliza kero zao.

Majaliwa alifafanua kuwa wafanyakazi wana wajibu wa kuwatumikia watanzania kwa kuwa wao ni waajiriwa wa serikali hivyo ni muhimu wakatoka maofisini na kwenda vijijini kusikiliza kero na kuzitatua badala ya wananchi kungojea viongozi wa kitaifa kuja kusikiliza kero na malalamiko yao wakati wao ni watendaji wakuu katika maeneo yao.

“Utumishi wenu hauhitaji upendeleo ama ahadi za njoo kesho, utumishi wa awamu ya tano ni wa uwajibikaji zaidi na uwajibikaji ni pamoja na kuwa mwaminifu katika kulinda na kusimamia kikamilifu fedha za serikali zinazotengwa katika halmashauri husika kwa ajili ya maendeleo,” alisema.

Akizungumzia soko la kimataifa la Endagaw, aliwapongeza wananchi wa wilaya hiyo kwa kukubaliwa kujengewa soko kubwa la kimataifa ambako wakulima watapeleka mazao yao na kuyauza lakini pia wataweza kuingiza mapato kwa kukodisha makampuni makubwa yanayohitaji kukodi kuhifadhi mazao kama NRFA.

Aliwataka wakulima wa mazao mbalimbali wilayani Kateshi kulitumia soko la mazao la kimataifa la Endagaw lililojengwa na ofisi yake kuuza mazao yao kwa bei nzuri badala ya kuuza mazao majumbani ambako wamekuwa wakiuza kwa bei ya chini isiyowasaidia kukuza kipato chao.

Alieleza kuwa serikali itaendelea kjuimarisha miundombinu ya soko hilo kwa kujenga eneo la wazi la nje kudhibiti magari makubwa yanayoshusha na kupakia mizigo yasikwame kutokana na matope na kuwa na mizani ya kupimia mazao na magari.

Kuhusu kero ya maji katika mji wa Katesh, alisema marekebisho yanafanyika kurekebisha mashine ya kuvuta maji na kuhakikisha sera ya maji inatekelezwa kwa vitendo katika kumpatia maji kila mwananchi umbali usiozidi mita 400.

Awali katika taarifa yake Mkuu wa Wilaya ya Hanang, Sara Msafiri alimweleza Waziri Mkuu kuwa changamoto kubwa inayoikabili wilaya hiyo ni migogoro ya ardhi, kuanzisha gereza la wilaya kupunguza usumbufu wa kuwapeleka wahalifu Babati, jambo ambalo alisema atalipeleka wizara ya mambo ya ndani lipate kushughulikiwa.

Msafiri aliomba pia kujengewa mahakama ya wilaya ambapo alisema ni mchakato uliopo wa mahakama kuu kujenga mahakama katika ngazi za wilaya hivyo jambo hilo nalo litashughulikiwa.

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa, Ester Mahawe alibainisha tatizo la kuwa na shule ya kidato cha tano na sita moja kwa wilaya nzima ambapo alimwomba Waziri Mkuu kutoa kipaumbele katika bajeti zake za elimu ili shule zaidi zijengwe mkoani humo.

Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Manyara, Rose Kamili (Chadema) aliiomba serikali kufuatilia na kuyatolea maamuzi mashamba makubwa ambayo yamekuwa hayaendelezwi na wawekezaji kutoka Ngano Ltd wanayoyamiliki zaidi ya ekari elfu 45 ambapo wamekuwa wakilima ekari elfu 16 pekee na kuacha migogoro ya ardhi baina yao na wananchi na kukosesha mapato ya halmashauri.

Ziara hiyo ilipata baraka za mvua kubwa baada ya ukame wa muda mrefu ilishangiliwa na umati wa watu waliokuwa wakiimba kwa furaha kuashiria Waziri Mkuu kuja na baraka hiyo kuneemesha mazao yao.

Leo Waziri Mkuu anatarajiwa kuhitimisha ziara yake wilayani Babati ambapo pamoja na mambo mengine atafanya majumuisho ya ziara hiyo na kutoa maelekezo ya serikali kwa wananchi na viongozi ngazi ya mkoa.

Irene Uwoya kuwa mchungaji.....Atangaza kuanzisha kanisa

$
0
0
Msanii wa filamu Irene Uwoya amesema kuwa ana mpango wa kuwa Mchungaji pamoja na kumiliki kanisa lake yeye mwenyewe siku za usoni na kwamba anamuomba Mungu kila siku aweze kutimiza ndoto hizo.

Kauli hii imetoka kinywani mwa msanii huyo pindi alipokuwa akijibu maswali mubashara aliyokuwa anaulizwa na mashabiki zake kupitia katika ukurasa wa Facebook wa EATV katika kipindi cha Kikaangoni

"Nina ndoto ya kuwa mchungaji na kila siku huwa nina muomba Mungu anifanikishie suala hilo niweze kutimiza japokuwa sasa hivi bado nipo katika changamoto kubwa ila natumai ndoto zangu zitatimia. Natamani kuwa pastor ambaye ni mwalimu, niwafundishe watu Mungu anataka nini, lakini sitaki kuanzisha kanisa kama biashara, sitaki kucheza na Mungu, ndiyo maana najipanga kwanza sitaki kukurupuka, nataka niwafundishe watu Mungu anataka nini, na jinsi ya kumuomba Mungu". Alisema Uwoya

Uwoya pia amefunguka na kueleza kuwa kazi yake ya sanaa huwa inamtesa kiimani jambo ambalo linamfanya kila siku akiamka awe anatubu kwa ajili ya mambo anayoyafanya akiwa katika kazi zake za uigizaji .

Amesema katika tasnia ya uigizaji mara nyingi huwa wanaongea uongo na hata mambo mengi wanayoyafanya kufikisha ujumbe huwa ni vitu ambavyo havimpendezi Mungu.

"Mimi nina hofu ya Mungu sana pia napenda kusali linapokuja suala la kazi yangu ukweli naona kama inanisumbua imani yangu kwa sababu katika uigizaji mambo mengi tunayoyafanya siyo ya kumpndeza Mungu lakini ndiyo kazi sasa, kila siku asubuhi nikiamka huwa inabidi kumuomba msamaha mungu wangu ndiyo niendelee na kazi". Amesema Irene Uwoya.

Kwa waliotaka kujua kama Irene anatumia dawa za kulevya, amewajibu kuwa hatumii dawa za kulevya na hajawahi kutumia kwa kuwa ni mkristo na dini yake hairuhusu kutumia dawa za kulevya wala kushiriki katika ndoa za jinsia moja lakini pombe anakunywa

"Situmii dawa za kulevya lakini nakunywa bia, dini yangu haizuii kunywa, nina uwezo wa kumaliza hata kreti nzima, hata mapadre kwenye dini yetu wanakunywa, lakini hairuhusiwi kulewa"

Pia amefunguka kuhusu mapenzi yake ya kuvaa nguo fupi, ambapo amesema anapeda nguo fupi, kwa kuwa ana mzio 'allergy' na nguo ndefu, hivyo hawezi kuvaa nguo ndefu.

Maamuzi ya mahakama kuhusu rufaa ya Nangole kupinga kutenguliwa ubunge

$
0
0
Mahakama ya Rufani Kanda ya Arusha leo imetupilia mbali rufani ya aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Longido Onesmo Ole Nangole (Chadema), baada ya kukiuka amri ya Mahakama hiyo iliyomtaka afanye marekebisho kwa kuandika upya rufani yake.

Akisoma uamuzi wa Mahakama, Msajili wa Mahakama ya Rufani Tanzania, Amir Msumi, amesema, Ole Nagole alikiuka amri ya Mahakama iliyotolewa Oktoba 24, mwaka jana iliyomtaka aongeze majina ya Msimamizi wa Uchaguzi na Mwanasheria Mkuu wa Serikali katika rufani yake mpya kabla ya kesi kusikilizwa..

Mh. Jaji Msumi amesema Mahakama imeridhishwa na pingamizi lililowasilishwa na upande wa Mjibu Rufani, Dk. Masumbuko Lamwai, (CCM), aliyetaka rufani hiyo isisikilizwe kwa madai imeandikwa upya bila idhini ya Mahakama.

Matokeo ya Ubunge wa Onesmo Ole Nangole yalitenguliwa Juni 29 mwaka jana, kwa madai kulikuwa na dosari nyingi ikiwemo kujazwa matokeo ya Ubunge kwa kutumia fomu namba 21c za kujaza matokeo ya udiwani na kujaza matokeo ya Ubunge, badala ya kutumia fomu namba 21b.

Ole Nangole alikuwa akipinga kutenguliwa kwa matokeo hayo ambapo alikuwa akipambana na mgombea wa CCM Dk, Steven Kiruswa.

Mke Wa Bilionea Msuya Aachiwa Huru Na Kukamatwa Tena

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemuachia huru mke wa marehemu bilionea Erasto Msuya, Miriam Mrita na mwenzake Revocatus Muyela wanaokabiliwa na kesi ya mauaji ya Aneth Msuya.

Hata hivyo washtakiwa hao walikamatwa tena na jeshi la polisi.

Hakimu Mkazi Mkuu, Godfrey Mwambapa leo amewaachia huru washtakiwa hao baada ya upande wa mashtaka kushindwa kutimiza amri yake iliyowataka kufanyia marekebisho ya hati ya mashtaka

Washtakiwa hao walikuwa wanakabiliwa na kesi ya mauaji ya kukusudia.

Uamuzi wa mahakama kuifuta kesi hiyo umefikiwa leo baada ya jalada la kesi hiyo lililokuwa limeitwa Mahakama Kuu kurejeshwa mahakamani hapo.
 
Februari 20, mwaka huu, Hakimu Mwambapa aliupatia upande wa mashtaka muda wa siku tatu kurekebisha hati ya mashtaka.

Lakini mpaka siku hizo tatu zinaisha hawakuwa wamefanyia bali  Wakili wa Serikali, Hellen Moshi aliiambia mahakama kuwa baada ya ofisi yao kutafakari kwa kina wameamua kuwa hawana cha kubadilisha kwa hati hiyo ya mashtaka

Wakili wa utetezi,  Peter Kibatala alidai kuwa upande wa mashtaka licha ya kupewa muda wa kutosha kufanyia marekebisho hati hiyo lakini wamekaidi amri hiyo.

Kibatala aliiomba mahakama kuwaachia washtakiwa huru kwa kuwa amri ya mwisho ya mahakama ilisema kama wasipofanya marekebisho itachukua hatua  na pia hakuna rufaa yoyote iliyokatwa na Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kupinga uamuzi huo.

Hakimu Mwambapa amesema,kweli mahakama imeamuru upande wa mashtaka kufanyia marekebisho hati ya mashtaka pindi ilipoona inamapungufu lakini hawakufanya hivyo, akawaongezea muda hawakufanya hivyo, Ila leo wamekuja na maelezo ya kuwa hati ya mashtaka ni sahihi.

"Hati ipi ambayo ipo sahihi wakati mahakama ilisema haipo sahihi, nawaachia huru washtakiwa", amesema Mwambapa.

Awali ndugu wa marehemu waliwasilisha barua mahakamani hapo na Kwa mujibu wa barua hiyo walikuwa wanataka Hakimu huyo ajitoe kwa sababu hawana imani naye.

Hakimu Mwambapa alikuwa atoe uamuzi juu ya hoja zilizowasilishwa na upande wa utetezi pamoja na upande wa mashtaka ambapo Wakili John Malya aliomba washtakiwa hao waachiwe huru kwa sababu   hakuna hati ya mashtaka inayowashikilia washtakiwa hao mahakamani hapo.

Wakili wa Serikali Mwandamizi, Kishenyi Mutalemwa yeye aliiomba mahakama iwape muda ili waweze kutekeleza amri ya mahakama iliyotolewa Januari 9, mwaka huu

Washtakiwa Miriam na Revocutus  wanadaiwa kumuua kwa makusudi Aneth Msuya, kwa kumchinja, nyumbani kwake Kigamboni jijini Dar es Salaam.

Miriam  ambaye ni mshtakiwa wa kwanza katika kesi hiyo alikuwa mke wa aliyekuwa kaka wa Aneth, marehemu Erasto Msuya, maarufu kama bilionea Msuya.

Erasto Msuya, ambaye alikuwa mfanyabiashara bilionea wa madini ya Tanzanite, pia aliuawa kwa kupigwa risasi, Agosti, 2015 eneo la Mijohoroni,  kando ya barabara ya Arusha – Moshi wilayani Hai mkoani Kilimanjaro.

Hata hivyo washtakiwa hao walikamatwa tena na kuondoka na gari la polisi.

Rais Museveni Kuwasili Nchini Jumamosi

$
0
0
Na. Immaculate Makilika- MAELEZO
Rais wa Jamhuri ya Uganda, Yoweri Kaguta Museveni anatarajiwa kufanya ziara ya siku mbili nchini kuanzia Jumamosi wiki hii.

Taarifa hiyo imetolewa leo jijini Dar es salaam na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiao wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga wakati wa mkutano na waandishi wa habari.

Alisema kuwa lengo la ziara hiyo ni kuendeleza uhusiano mzuri uliopo baina ya Uganda na Tanzania, pamoja na kujadili masula mbalimbali ya kikanda, kimataifa na sekta mbalimbali za ushirikiano kati ya nchi hizi mbili hususani katika sekta za nishati, biashara na uchukuzi.

“ Mahusiano ya kibiashara kati ya Tanzania na Uganda yameendelea kuimarika katika miaka ya hivi karibuni, ambapo mwaka 2016 Tanzania ilifanya mauzo nje kwa Nchi hiyo ya kiasi cha shilingi bilioni 66.849, ikilinganishwa na shilingi bilioni 78.31 za mwaka 2015” alisema Waziri Mahiga.

Aliongeza kuwa Uganda ni muhimu katika Jumuiya ya Afrika Mashariki ambayo haina Bandari na hivyo inategemea Tanzania kwa ajili ya kupitisha mizigo yake.

Nchi ya Uganda imezidi kuwa na umuhimu kufuatia uamuzi wa kupitisha bomba la mafuta nchini Tanzania, kutoka Kabaale –Hoima, Uganda hadi Bandari ya Tanga, ambapo bomba hilo lina urefu wa kilimeta 1443 na kipenyo cha inchi 24.Bomba hilo la mafuta litakalokamilika mwaka 2020 limnatarajiwa kupatia nchi hizi mbili fursa mbalimbali.

“ Utekelezaji wa mradi huu utafungua fursa za ajira kwa watanzania, kuchochea shughuli za kiuchumi kwa mikoa inayopita bomba hilo, pamoja na kufungua ukanda wa biashara wa kaskazini mwa Tanzania na Uganda pamoja na kuimarisha uhusiano katika soko la Afrika Mashariki” alifafanua Waziri Mahiga.

Katika hatua nyingine, Waziri Mahiga alisema kuwa kuhusu mgogoro wa nchini Burundi, kumekuwepo na jitihada mbalimbali zinazofanywa na Rais Museveni pamoja na Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Benjamin Mkapa ili kuhakikisha amani inarejea nchini humo.

Katika ziara hiyo ya Rais Museveni nchini, atapokelewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Johm Magufuli ambapo atatembelea Bandari ya Dar es Salaam kwa lengo la kuangalia maboresho yaliyofanywa katika bandari hiyo, pamoja na Kiwanda cha kutengeneza Juisi cha Azam kilichopo Vingunguti jijini Dar es salaam.

Rais Magufuli awapongeza madaktari Muhimbili na amsaidia Neema Mwita Wambura aliyeunguzwa moto kifuani

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amewapongeza Madaktari wa Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa juhudi kubwa walizofanya kunusuru maisha ya Neema Mwita Wambura ambaye alijeruhiwa kwa kuunguzwa na maji ya moto kifuani, shingoni na mkononi.

Pongezi hizo za Mhe. Dkt. Magufuli zimetolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu Bw. Gerson Msigwa muda mfupi baada ya kumfikisha Neema Mwita Waitara katika Hospitali ya Taifa Muhimbili ambako Rais Magufuli ameagiza apelekwe kwa mara nyingine kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi wa maendeleo ya afya yake.

Katika Pongezi hizo Mhe. Dkt. Magufuli amesema Madaktari wa Hospitali ya Taifa Muhimbili wamefanya kazi kubwa na ya kizalendo kuhakikisha Neema anapona licha ya majeraha makubwa aliyoyapata miaka miwili iliyopita na ambayo yalitishia uhai wake.

Pia Mhe. Rais Magufuli amempongeza Mama Mariam Amir (Bibi Mwanja) kwa upendo wake wa kumchukua Neema na kisha kumpa hifadhi nyumbani kwake huko Tandika Devis Kona Jijini Dar es Salaam.

“Nakushukuru sana Mama na ninakupongeza, umeonesha mfano mzuri wa kujali umoja na upendo kwa Watanzania wenzako bila kujali dini, kabila wale kanda unayotoka na hivi ndivyo Watanzania wote tunapaswa kufanya” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Kabla ya kutoa pongezi hizo, mapema leo asubuhi Mhe. Rais Magufuli amewatuma wasaidizi wake wakiongozwa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu Bw. Gerson Msigwa kwenda Tandika Devis Kona katika Wilaya ya Temeke Jijini Dar es Salaam kumuona Neema Mwita Wambura ambaye alipatiwa hifadhi katika nyumba ya Mama Mjane aitwaye Mariam Amir (Bibi Mwanja) baada ya kuona picha na kusoma taarifa za mkasa uliomkuta katika mitandao ya kijamii.

Mhe. Rais Magufuli ametoa Shilingi laki 5 kwa Neema kwa ajili ya kumsaidia chakula yeye na watoto wake waliohifadhiwa na rafiki yake huko Bunda Mkoani Mara na pia ametoa Shilingi laki 5 kwa Mariam Amir aliyejitolea kumsaidia na kumpa hifadhi nyumbani kwake. Pia ameahidi kumsaidia wakati wote wa matibabu na pia familia yake.

Baada ya kumpokea daktari bingwa wa magonjwa ya dharula na ajali katika kitengo cha dharula cha Hospitali ya Taifa Muhimbili Dkt. Juma Mfinanga amesema wameanza kumfanyia uchunguzi ili kujua maendeleo yake na kama kumpa matibabu zaidi.

Nae Daktari Bingwa wa Upasuaji Dkt. Ibrahim Mkoma ambaye amekuwa akimfanyia matibabu Neema Mwita Wambura tangu Julai 2015 alipofikishwa hospitalini hapo kwa mara ya kwanza amesema Neema anaendelea vizuri baada ya kufanyiwa upasuaji mara nne.

Dkt. Mkoma amesema baada ya upasuaji huo, sasa Neema anaweza kuinua na kugeuza shingo yake na kwamba kwa sasa wataendelea kumfanyia uchunguzi zaidi ili kujua maendeleo yake. Mhe. Rais Magufuli ameagiza vyombo vyote vinavyohusika kufanyia kazi mkasa uliomkuta Neema Mwita Wambura na kuhakikisha haki inatendeka.

Mrema Amshukuru Rais Magufuli Kwa Matibabu Nchini India

$
0
0
Na Eliphace Marwa -Maelezo
Mwenyekiti wa Bodi ya Parole ya Taifa, Dkt. Augustine Lyatonga Mrema amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwa kufanikisha safari ya kwenda nchini India kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi wa afya yake.

Dkt. Mrema ametoa kauli hiyo leo jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na waaandishi wa habari kuhusu uteuzi uliofanywa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Lameck Nchemba kwa kuwateua wajumbe wawili wa bodi hiyo.

“Nachukua nafasi hii kumshukuru Rais Magufuli , Waziri Mkuu, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Wizara ya Afya na Ikulu, kwa kunipeleka nchini India kufanyiwa uchunguzi wa afya yangu na kupatiwa matibabu na sasa afya yangu imeimarika na niko tayari kutekeleza majukumu yangu”, alisema Dkt. Mrema.

Akizungumzia uteuzi uliofanywa na Waziri Nchemba, Mrema amesema kuwa toka alivyoteuliwa na Rais Magufuli kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Parole Taifa, Bodi hiyo haikukaa vikao kutokana na baadhi ya wajumbe wa Bodi hiyo kumaliza muda wao.

“Nilipoteuliwa na Rais kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Parole Taifa, Bodi ilikuwa bado haijakutana na kufanya vikao kwasababu kuna wajumbe walikuwa wamemaliza muda wao na Waziri wa Mambo ya Ndani alikuwa bado hajateua wajumbe wengine lakini kwa sasa amakwisha fanya kazi ya uteuzi”, alisema Dkt. Mrema.

Mrema aliwataja walioteuliwa kuwa wajumbe wa Bodi ya Parole Taifa ni pamoja na Bwana Francis Kistola na Bwana John William Nyoka.

Aidha Mrema amempongeza Waziri wa Mambo ya Ndani kwa kukamilisha kazi ya uteuzi na amewapongeza wajumbe walioteuliwa na kuwakaribisha kwa mikono miwili kwenye bodi hiyo na kuomba ushirikiano wao na uzoefu wao ili kukamilisha majukumu ya bodi ya Parole.

Vilevile Mrema amesema kuwa kikao cha kwanza cha bodi mpya ya parole kitafanyika tarehe 3 na 4 Machi 2017 jijini Dar es Salaam na bodi hiyo mpya itazinduliwa siku hiyo na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Mwigulu Nchemba.

Wema Sepetu ahamia Chadema, aungana na Mbowe mahakamani

$
0
0
Chama cha Demokrasia na Maendeleo kunatarajia kuwakaribisha wanachama wapya waliojiunga leo na chama hicho akiwamo msanii maarufu nchini wa fani ya uigizaji wa filamu, Wema Sepetu (28).

Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasilianio wa Chadema, Tumaini Makene  amesema leo (Alhamisi) kuwa chama hicho kupitia Mwenyekiti wa Chama Taifa, Freeman Mbowe, baada ya kesi ya kikatiba namba 1 ya mwaka 2017 inayotarajiwa kuwasilishwa Mahakama Kuu leo, kitazungumza kwa umma kupitia waandishi wa habari kuwakaribisha wanachama wapya waliojiunga leo akiwemo Wema Sepetu.

Wema pamoja mama yake, leo aliongozana na Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe pamoja na viongozi wengine wa chama hicho kwenye mahakama kuu jijini Dar es Salaam.

Msanii huyo aliyeshinda taji la Miss Tanzania mwaka 2006, alikuwa kada wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kabla ya kuhamia Chadema.

Kutoka Mahakamani: Mbowe Kuendelea Kutokamatwa na Polisi Wala Kuwekwa Kizuizini

$
0
0
Mwanasheria wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Tundu Lissu ameongea na waandishi wa habari jioni hii  baada ya kutoka Mahakamani  kwenye kesi iliyofunguliwa na Freeman Mbowe dhidi ya Mkuu wa Mkoa w Dar Paul Makonda  na Kamshna Sirro.

Lissu amesema Amri ya kuzuia Freeman Mbowe asikamatwe na wala kuwekwa kizuizini na Polisi inaendelea isipokua wanaweza kumuita kwa Mahojiano ambapo pia Mahakama itatoa maamuzi Tarehe 2, March  2017

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya February 24

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images