MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWAILIPOISHIA
ILIPOISHIA
Kitendo hicho kikiwa kinaendelea Shamsa aliweza kushuhudia damu ikimtoka mtu ambaye anaamini amekuja kuwasaidia na kuwaokoa.Bila ya uwoga na wala pasipo kuhofia maisha yake, Shamsa akasimama wima na kuanza kupiga hatua za kwenda walipo simama watu hao walio muweka kati mtu aliye valia mavazi meusi tupu.
Eddy akabaki akiwa katika mshangao mkubwa, baada ya kumuona Shamsa akikaribia katika eneo hilo ambalo ni hatari kwa maisha yake. Eddy akajaribu kutingisha kichwa chake kumzuia Shamsa asiweze kusogelea eneo hilo, ila ndio kwanza Shamsa akaongeza mwendo wa kuwasogelea akiwa amejiandaa tayari kwa kupigania watu wote waliomo ndani ya jengo hilo.
ENDELEA
“Am sorry dady”(Samahani baba)
Shamsa alizungumza huku akiruka hewani na kushusha teke zito kwa Lukuman akitambua kwamba ni baba yake. Eddy akataka kuzungumza kitu ila akastukia akipigwa mtama na Briton, ulio mpeleka chini, hakutaka kupoteza hata sekunde moja kwa kofia lake kuweza kuanguka alicho kifanya ni kuliweka sawa na kunyanyuka huku akichechemea.
“Baba kwa nini umeamua kufanya hivi?”
Shamsa alizungumza huku machozi yakimwagika usoni, Lukuman akabaki akiwa ameshangaa kwa kuitwa baba, ili kupotezea akarusha ngumi nzito kifuani mwa Shamsa, na kumfanya binti huyo kuto ukelele wa maumivu huku akianguka chini na kujikunja. Briton na Eddy wakajikuta wote wakimtazama Shamsa anaye garagara chini kwa maumivu makali. Kumbukumbu na sura ya Shamsa vikaanza kumjia Briton, akaanza kufikiria ni wapi alipo isikia sauti hiyo ya maumivu ya msichana huyo mwenye asili ya kiasia.
Kumbukumbu zake zikatua kipindi ambacho, walikuwa ni miongoni mwa mateka walio weza kuingizwa katika kambi ya kundi la Al-Shababu, akiwa ni kijana mdogo mwenye umri wa miaka kumi na tano. Miongoni mwa mateka ambao waliokuwa kipindi hicho, Shamsa ni mmoja wapo kipindi hicho Shamsa alikuwa bado binti mdogo.
Anakumbuka siku moja wakiwa katika mazoezi ya lazima, Shamsa alipewa kijana mwengine ambaye walimkuta ndani ya kambi hiyo, apambane naye, kutokana Shamsa hakuwa mzoefu na alikuwa ni binti mdogo na mpole sana, kijana huyo pasipo huruma aliweza kumbutua vya kutosha Shamsa, na kitu ambacho anakikumbuka zaidi, ni pale kijana huyo alipo mpiga Shamsa ngumi ya kifuani na binti huyo akaanguka hivyo hivyo kama alivyo anguka sasa hivi.
Britona akakumbuka alipo jitoa katikati ya vijana wezake walio zunguka duara hilo wakiwatazama Shamsa na kijana mwengine jinsi walivyo kuwa wakipigna. Akamvaa kijana huyo na kumshindilia ngumi za hasira hadi kijana huyo akapoteza maisha yake.
‘Naitwa Shamsa’
Sauti hiyo ilipita masikioni mwa Briton na kukumbuka siku alipo muuliza jina bintyi huyo na kutokea kumpenda, kupita maelezo. Briton akastushwa na buti zito la Lukuman lililo tua tumboni mwa Shamsa, dadi akanyanyuka kidogo juu na kutua chini puu.
“Ahagraaaaaaaaaa”
Briton akamuacha Eddy na kwenda kumvaa Lukuman, na kumuangusha chini kama mzoga, hadi Eddy akabaki akishangaa. Briton akaanza kumshindilia mangumi ya uso Lukuman, kila alivyo zidi kumshindilia mangumi mazito hayo ndivyo alivyo kuwa akikumbuka tukio la Lukuman kumpiga msichana ambaye alizama ndani ya moyo wake na kuahidi atamtunza ndani ya moyo wake hadi siku ambayo atakuja kumuona. Eddy kwa haraka akapiga goti moja chini na kumnyanyua Shamsa aliye poteza fahamu.
“WOTE TOKENI NJEEEEEE”
Ikawa kama fungulia mbwa, kila mmoja aliye jiweza alijitahdi kutoka nje akikimbia, hapakuwa na mtu aliye hitaji kujihusisha na ugovi wa watekaji hao wawili, kila mtu alijitahidi kuizingatia roho yake kwanza mambo mengine yatafwata baadaye. Eddy akamuweka Shamsa kwenye moja ya meza, baada ya kugundua yupo hai, kisha yeye akandoka akihofia askari walio anza kuingia ndani ya jengo hilo kuweza kumkuta na kumtambua.
Ndani ya dakika moja Brina na watui wake wote wawili, walijikuta wakiwa wamelala chini, kila mmoja akishika eneo la mwili wake lililo tole pande la nyama, kwa kucha kali ambazo Samson alizitumia katika kuwadhuru waasi hao.
Mmoja wao koromeo lake liliweza kutolewa nje, na yupo katika hatua za mwisho mwisho za kuiaga dunia huku mikono yake miwili ikiwa imeshika sehemu koromeo lake lilipo chomolewa, ili damu isitoke.
Mwengine alitobolewa tumboni na utombo wake wote ukavutwa nje pasipo huruma. Brian miguu yake yote miwili, ilivunjwa vunjwa vipingili pingili zaidi ya kumi kwa kila mguu, na kuacha akiendelea kulia kwa maumivu makali.
Samson alipo hakikisha kazi yake imekamilika akatoka ndani ya chumba hicho na kuwaachia woga mwingi mafundi mitambo, kila mmoja akiwa haamini kama amepota, na hapakuwa na aliye weza kutoka katika sehemu aliyo jificha hadi walipo sikia sauti za polisi,walio jitambulisha mara baada ya kuingia ndani ya chumba hicho.
“Upo salama?”
Samson alimuuliza Eddy mara baada ya kumkuta akiwa amesimama juu ya paa akiwatazama jinsi wananchi wanavyo pokelewa na ndugu zao walio weka kambi katika eneo hilo kuhakikisha kwamba wanawaona ndugu zao.
Japo si desturi ya watu wengi kukumbatiana ila kila aliye muona ndugu yake alijikuta akimkumbatia kwa furaha, wengine wakiendelea kuita majina ya ndugu zao wakizidi kuwatafuta katikati ya mamia ya watu walio weza kutoka ndani ya jengo hilo. Wachache kati ya waliopo nje ya jengo, walijikuta wakiingiwa na wasiwasi mwingi na wengine wakiangua vilio baada ya kupata taarifa au kuona miili ya ndugu zao walio fariki.
“Ndio japo si sana”
Eddy alizungumza kwa ufupi huku akiendelea kutazama huku na huku, akabahatika kuweza kumuona Shamsa akiwa amebebwa kwenye machela na kuingizwa ndani ya gari ya wagonjwa, hapo roho yake ikaweza kutulia
“Tuondoke zetu muheshimiwa”
“Usiniite muheshiwa niite……..”
“BLACK SHADOW”
***
“I.T.V:WANANCHI WALIO TEKWA WAMEACHIWA USIKU HUU”
“T.B,C:MAMIA YA WANANCHI WALIO TEKWA NDANI YA JENGO LA BIASHARA MLIMANI CITY WAACHIWA HURU”
“Star Tv:GAIDI MMOJA AKAMATWA, NA ALIYE KUWA WAZIRI WA ULINZINA NDIO MTEKAJI MKUU AMEKUTWA AMEKUFA”
Kila muandishi wa kitua cha habari aliye kuwepo katika eneo la tukio la Mlimani City aliweza kuzungumza taarifa hiyo kwa jinsi ya habari aliyo weza kuipata kwa wakati huyo. Watu wote walio kuwemo ndani ya ofisi ya maalumu ya matukio ya raisi Praygod Makuya wakajikuta wakipiga makofi wakifurahia tukio hilo, kila mmoja alikumkumbatia raisi kwa furaha, wakimpongeza kwa kazi nzuri, Rahab naye wakampongeza kwa kuwa pamoja nao katika kazi nzito ya kushinda kwenye mativ makubwa yaliyomo ndani ya ofisi hiyo wakilifwatilia tukio zima.
“Ila hili ni fundisho inaonyesha ni jinsi gani serikali yetu haijajipanga katika kuimarisha ulinzi. Hivyo basi kuanzia leo maeneo yote ya mipaka nitahakikisha ninaongeza vikosi vya ulinzi na usalama, ili kuhakikisha hawa maharamia hawawezi kuingia tena ndani ya nchi yetu”
Raisi Praygod alizungumza kwa sauti ya juu, watu wote wakampiga makofi kwa wazo hilo alilo weza kulitoa.
‘KUSEMA KWELI MIMI NIMSHUKURU YULE MTU ALIYE VALIA NGUO NYEUSI, KWELI ALIAMUA KUJITOA YAANI HUWEZI AMINI MWANANGU ALIMUONA AKI…………”
Dada huyo anaye hojiwa na mundishi alijikuta akimwaga machozi huku akiwa ameshikilia mkono mwanye wa kike, akajipungusa machozi kidogo kisha akendelea kuzungumza,
‘YAANI KUSEMA KWELI YULE KAKA NI JASIRI SANA, NITAMSHUKURU TENA SANA’
Muandishi wa habari akamuhoji mtu mwengine aliye vua shati lake na kulishika mkononi, akionekana kuwa katika hali ya furaha.
‘AISEE CHALAA WANGU MIMI HUKU DAR SIRUDI TENE, YAANI NIMEKUJA FANYA SHOPING HATA UKINIULIZA SASA HVI SIKUMBUKI NI KIPI KILICHO NILETA HAPA, TENA YULE MAN WANGU ALIYEKUWA ANARUSHA RUSHA MATEKE YANII YULE MAN NIME MMAINDI KICHIZI, YAANI CHALAA ANARUSHA VISU HUYO, JAPO NILIKUWA NIMELALA CHINI, ILA NIKAWA NACHABO MARA KWA MARA KUONA JINSI JAMAA ANAVYO WAANGUSHA WALE NGEDERE YANII CHALAA WANGU NAKUKUBALI SANA’
Kijana huyo mwenye lafudhi ya kichaga alizungumza bila hata ya kupumzika kwa furaha aliyo kuwa nayo hadi ikamlazimu muandishi wa habari kumkatisha na kumuhoji mtu mwengine.
***
Eddy na Samson wakafika nyumbani, moja kwa moja wakelekea kwenye chumba cha siri cha Eddy, ikawa ni kazi ya Samson kuhamisha vitu baadhi vilivyomo ndani ya chumba hicho na kuviingiza ndani ya gari. Mamumivu makali yakazidi kuutesa mguu wa Eddy, jasho jingi likanza kumwagika mwilini mwake, kwani hakuweza kumumbia Samson kama ana jeraha kwenye mguu wake, kwa kiasi cha damu kilicho weza kumtoka akajikuta akilegea na kupoteza fahamu.
“Eddy Eddy”
Samson aliita huku akimtingisha Eddy aliye jilaza kwenye kochi mara baada ya kuingia ndani ya chumba hicho, akitoka kupoleka baadhi ya vitu. Katika kumtazama vizuri suruali yeka mguu mmoja umelowana na damu nyingi, katika kumkagua kagua akakuta shimo lililo ingia risasi.
“Shitttttt”
Samson akanyanyuka kwa haraka na kukimbilia kwenye kabati lenye sawa pamoja na vifaha vya kutibia majeraha kwa haraka akaanza kumuhudumia kujaribu kuitoa risasi iliyomo ndani ya paja kabla hata sumu yake kusambaa kila eneo la mwili. Ndani ya muda mchache akafanikiwa kuitoa risasi hivyo na kulifunga jeraha hilo.
“Damu”
Samson akataka kutoa damu yake ili amuongezee Eddy, ila akasita akachukua simu yake na kumpigia Rahab ila simu yake haikuwa hewani, ikabidi atume ujumbe wa maandishi mafupi(massage).
Akataka kumbeba Eddy na kumpeleka ndani ya gari, ila akasikia vishindi vya kama watu wakikimbia nje ya nyumba, kwa haraka akaufunga mlango, akachukua moja ya kiti cha chuma kilichopo ndani ya chumba hicho, akakisogeza karibu na ukutani kisha akapanda juu yake kuchungulia kwenye kijidirisha kidogo kilichopo upande wa juu kabisa wa dirisha hilo. Kundi kubwa la wanajeshi wenye silaha wapo nje ya nyumba ya Eddy wakijiandaa kuvamia ndani ya nyumba hiyo.