Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Watanzania 180 Wafukuzwa Msumbiji

$
0
0
Idadi ya Watanzania wanaorudishwa kutoka nchi ya Msumbiji walikokuwa wakiishi, imezidi kuongezeka na kufikia 180 huku kukiwa na madai ya kuwafanyia vitendo vya kikatili.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Ofisa Uhamiaji mkoani Mtwara, Rose Mhagama alisema taarifa ambazo wamezipata hadi sasa ni kwamba bado Watanzania wengi wamefungiwa katika mahabusu za nchini humo na wanarudishwa kwa makundi.

Mhagama alisema sababu za kurudishwa kwa Watanzania hao bado hazijafahamika ila uchunguzi wa kina unaonyesha kwamba katika maeneo ya Mtepweshi na Nanyupu nchini humo, kuna migodi ya madini inayomilikiwa na raia kutoka moja ya nchi za Magharibi, anayedaiwa kufadhili askari wa nchi hiyo kuwafukuza Watanzania.

“Sijui ni kwanini na sifikirii sana kwamba Watanzania pekee ndio wapo kwenye maeneo hayo, kimsingi taarifa ambazo tunazo ni kwamba anaona kama Watanzania ndio wanakwenda kupora zile mali zilizopo katika machimbo hayo.

“Kiukweli zoezi hili linaleta sintofahamu nyingi kwa sababu unajiuliza kama kweli ni zoezi rasmi, kwanini wanawachania hati zao za kusafiria na kuwanyang’anya vitu vyao, inaonyesha wana nia ya kuwapora Watanzania mali zao au kutowatendea haki,” alisema.

Wakati ofisa hiyo akisema idadi ya Watanzania waliofukuzwa Msumbiji ni 180, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Dk Suzan Kolimba amesema idadi ni watu 132 na ikitarajiwa kuongezeka zaidi kutokana na operesheni ya kuwarudisha nyumbani wahamiaji haramu.

Alisema Februari 11, Watanzania 58 walirudishwa nchini kutoka Msumbiji, Februari 14 walirudishwa Watanzania 24 na jana walirudishwa wengine 50 ikiwa ni mwendelezo wa operesheni hiyo inayoendelea nchini humo.

Akizungumzia suala hilo jana jijini Dar es Salaam, Dk Kolimba alisema operesheni hiyo haijawalenga Watanzania pekee bali pia raia wa nchi nyingine walioingia Msumbiji kinyume cha taratibu.

Dk Kolimba alisema operesheni hiyo inaendeshwa katika mji wa Monte Puez uliopo Jimbo la Cabo Delgado na mji huo una Watanzania 3,000 wanaoishi huko na kwamba idadi ya watakaoondolewa huko inaweza kuongezeka zaidi.

“Tunaendelea kufuatilia tuhuma za baadhi ya Watanzania kwamba walifanyiwa ukatili wakati wanarudishwa nyumbani ili tujue hatua za kuchukua. Ubalozi wetu unashirikiana na serikali ya Msumbiji katika kuhakikisha Watanzania hawapati matatizo katika operesheni hiyo,” alisema Dk Kolimba.

Dk Kolimba alisema Serikali inaendelea kufanya mawasiliano ya kidiplomasia na serikali ya Msumbiji ili kuhakikisha usalama wa Watanzania na mali zao. Hata hivyo, alisisitiza kwamba uhusiano wa Tanzania na Msumbiji ni mzuri.

Diamond naye ajikuta mikononi mwa polisi

$
0
0
Mwanamuziki Diamond Platnumz jana ameripoti Kituo Kikuu cha Polisi cha Usalama Barabarani baada ya video yake kusambaa kwenye mitandao ya kijamii ikimuonyesha akiendesha gari bila kufunga mkanda huku akiachia usukani na kucheza ndani ya gari.

Daimond ambaye alikuwa ndani ya gari hilo pamoja na mpenzi wake, Zarinah Hassan, mama yake mzazi na mtoto wake walikuwa wakicheza wimbo mpya wa Diamond, Marry You aliomshirikika Ne-Yo.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Diamond ameweka picha akiwa na Kiongozi wa Kikosi cha Usalama Barabara, Kamanda Mpinga ambapo amewataka vijana wenzake kuhakikisha wanachukua tahadhari pindi wanapoendesha magari na kutumia barabara. Lakini pia ameeleza kuwa amelipa faini kwa mujibu wa sheria kutokana na kukiuka sheria za usalama barabarani.

“Leo nilireport kituo kikuu cha polisi wa usalama barabarani kutokana na Vidoe Clip tuliyopost naendesha gari barabarani bila kufunga mkanda na pia kuachia usukani na kucheza…. Nikapewa Onyo na Kulipa faini kulingana ya Mujibu wa sheria… tafadhali watanzania na Vijana wenzangu… tuhakikishe tunafunga mikanda pindi tupandapo na tuendeshapo Magari Maana ni Hatari kwa Maisha yetu na inaweza kukupeleka kunyea debe pia…🙏” ameandika Diamond

Waziri Mkuu Awabana Mkrugenzi na Mkuu wa Wilaya.......Awataka Wakajibu Kero za Wananchi

$
0
0
Waziri  Mkuu, Kassim Majaliwa, amewaagiza Mkuu wa Wilaya ya Kiteto, Mhandisi Tumaini Magesa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya hiyo, Tamim Kambona, kwenda kata ya Engusero keshokutwa kujibu kero za wananchi katika mkutano wa hadhara.

Mkuu huyo wa wilaya na mkurugenzi wametakiwa wafuatane na Mwenyekiti wa Halmashauri, Lairumbe Mollel kwenda kuitisha mkutano huo.

Majaliwa alitoa maagizo hayo jana katika kijiji cha Engusero baada ya kusimamishwa na wananchi wakati akiwa njiani kuelekea mji wa Kibaya, yalipo makao makuu ya wilaya hiyo kuanza ziara ya kikazi ya mkoa wa Manyara.

Akijibu baadhi ya maswali aliyoulizwa na wananchi wa Engusero, Waziri Mkuu alisema analichukua na kwenda kulifanyia kazi ombi la wakazi hao la kujengewa soko la kimataifa katika kata hiyo ili wauze mahindi hapo hapo.

“Nitaawagiza Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi wa Halmashauri waje hapa Jumamosi hii na kufanya mkutano ili wawaeleze wana mpango gani kuhusiana na ujenzi wa soko hilo,” alisema.

Awali, mkazi wa kata hiyo, Ali Athumani, alimuomba Waziri Mkuu awasaidie ili wajengewe soko la kimataifa kwa sababu wao ni wazalishaji wakubwa wa mahindi, lakini hawafaidiki nayo kwa sababu yote huuzwa katika soko la Kibaigwa mkoani Morogoro.

Naye Said Shabani, alimuomba Waziri Mkuu awasaidie kufuatilia upatikanaji wa gari la wagonjwa na ujenzi wa wodi nyingine ya wagonjwa pamoja na chumba cha kuhifadhia maiti kwenye zahanati yao.

Wakati huo huo, Waziri Mkuu, amewaagiza viongozi wa serikali za vijiji kuanzia sasa kuwakamata wote wanaojihusisha na biashara ya dawa za kulevya katika maeneo yao.

Alitoa agizo hilo jana katika kijiji cha Engusero wilayani Kiteto, baada ya kusimamishwa na wananchi wakati akiwa njiani kuelekea mji wa Kibaya.

Majaliwa alisema serikali imeweka nia ya dhati ya kupambana na dawa za kulevya na amewataka watendaji wote kuanzia ngazi ya vijiji kudhibiti suala hilo.

“Serikali haiwezi kuona vijana wanaangamia kwa dawa za kulevya. Tumeamua kudhibiti hali hiyo. Hii vita ni ya nchi nzima," alisema Waziri Mkuu.

“Tunataka vijiji vyetu, kata zetu, wilaya zetu na mikoa yetu iwe safi bila hata chembe ya dawa za kulevya.

"Tukikuona kijana unayumbayumba au kuweweseka, tunakupima na tukikuta umetumia ile kitu, tunakukamata ili utuambie ni nani amekupa.

“Sisi tunataka vijana wafanye kazi za kujiletea maendeleo. Kijana hawezi kuwa na maendeleo wakati hufanyi kazi, huwezi kuwa na ndoto za maendeleo wakati umelewa bangi au dawa za kulevya.

"Kila mmoja afanye kazi kwa ajili ya maendeleo ya nchi yetu.”

Wafuasi wa Steven Wassira Waendelea Kumng'ang'ania Ester Bulaya....

$
0
0
Wapigakura wanne wa Jimbo la Bunda waliofungua shauri kupinga matokeo ya Uchaguzi Mkuu uliopita wameendelea kumng’ang’ania mbunge wa jimbo hilo, Ester Bulaya kwa kukata rufaa kupinga uamuzi wa Mahakama Kuu wa kutupa maombi yao.

Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, Francis Kabwe alisema jana kuwa rufaa ya wapigakura hao, Magambo Masato, Matwiga Matwiga, Janes Ezekiel na Acetic Malagila iliyosajiliwa kwa namba 199 ya mwaka 2016, itasikilizwa mfululizo kuanzia Februari 20.

Alisema rufaa hiyo itasikilizwa jijini Mwanza na jopo la majaji watatu wa Mahakama ya Rufani, Salim Mbarouk, Augustine Mwarija na Shabani Lila.

Katika maombi ya msingi waliyofungua Mahakama Kuu, wapigakura hao wanaowakilishwa na Wakili Constantine Mutalemwa, wanaiomba Mahakama kutengua ushindi wa Bulaya dhidi ya aliyekuwa mgombea wa CCM, Stephen Wasira kwa madai kuwa uchaguzi wa Oktoba 25, mwaka 2015 haukuwa huru na wa haki.

Pamoja na madai mengine, Masato na wenzake wanadai kuwa mchakato wa kampeni, upigaji kura na utangazaji wa matokeo uligubikwa na ukiukwaji wa sheria na utaratibu wa uchaguzi, vikiwamo vitendo vya rushwa, msimamizi wa uchaguzi kumnyima haki Wasira kwa kukataa ombi lake la kura kuhesabiwa upya.

Hoja nyingine ni msimamizi wa uchaguzi kutangaza matokeo bila Wasira kuwapo ukumbini na kuchanganya tarakimu za idadi ya wapigakura walioshiriki uchaguzi.

Novemba 17, mwaka jana, Jaji Noel Chocha wa Mahakama Kuu alimtangaza Bulaya kuwa mshindi halali wa uchaguzi huo baada ya kutupilia mbali maombi ya wapigakura hao.

Manji athibitika kutumia Madawa ya Kulevya, kupandishwa kizimbani leo

$
0
0
Hatimaye imedhibitika kuwa Mwenyekiti wa Timu ya soka ya Yanga na Mfanyabiashara mkubwa nchini Tanzania Yusuph Manji anatumia madawa ya kulevya na leo atapandishwa kizimbani kwa tuhuma hizo akiwa pamoja na watuhumiwa wengine wanaoshikiliwa kwa sakata kama hilo.

Katika Kipindi cha michezo katika redio moja nchini Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Kamishna,  Simon Sirro amethibitisha kuwa vipimo vya Mkemia Mkuu wa Serikali alivyofanyiwa Manji vinaonyesha kuwa ni Mtumiaji wa Madawa ya kulevya (Hakuyataja aina yake) na kusisitiza kuwa leo mtuhumiwa huyo atapandishiwa kizimbani kujibu shitaka hilo.

Akielezea afya yake tangu alazwe Hospitali, Kamanda Sirro amesema kuwa mwenyekiti huyo wa yanga yuko vizuri na sasa ameruhusiwa kutoka Hospitalini na kurejeshwa mahabusu polisi kusubiri kupandishwa kizimbani.

Sirro amesema kuwa habari kamili kuhusu sakata hilo na watuhumiwa wengine wakiwemo wasanii waliokamatwa zitatolewa leo mbele ya wanahabari Jijini Dar es Salaam.

==>Msikilize kamanda Sirro akiongea hapo chini

Tundu Lissu: Serikali haiwezi kuifuta TLS

$
0
0
Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt Harrison Mwakyembe jana alisema kuwa atakifuta Chama cha Wanasheria Tanganyika (Tanganyika Law Society (TLS)) kwa madai kuwa kimesahau misingi yake na kuanza kufanya kazi kama chama cha siasa.

Waziri Mwakyembe alisema kuwa, kama wanataka kufanykazi kama chama cha siasa, basi yeye ataongea na msajili wa vyama vya siasa nchini ili cha hicho kipya kisajiliwe.

Kufuatia kauli hiyo, Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA, Mbunge wa Singida Mashariki na mgombea Urais wa TLS, Tundu Lissu ameandika waraka huu kwenda kwa wanasheria wenzake.

Mawakili wenzangu. Mimi binafsi sijashangazwa na kauli ya Dkt. Mwakyembe kwamba ataifuta TLS kama itajiingiza katika harakati za kisiasa. Hii sio mara ya kwanza kwa viongozi wa serikali ya Tanzania kutoa vitisho vya kuifuta TLS.

Waziri Mkuu hayati Edward Sokoine aliwahi kutishia hivyo katika kilele cha vita dhidi ya wahujumu uchumi miaka ya mwanzo ya ’80. Na hata kabla ya hapo katika miaka ya ’60 na ’70 watangulizi wa Sokoine walijaribu kufanya hivyo hivyo. In fact, kuanzishwa kwa Tanzania Legal Corporation kipindi hicho kulikuwa driven in part na jitihada za kuondoa the private bar.

Vitisho dhidi ya TLS vilirudi miaka ya ’90 wakati wa Lyatonga Mrema. Kitu kimoja kiko common katika vitisho hivyo vyote. Vitisho hivi vimetolewa kila wakati TLS na private bar wanapo-assert their independence na wanapoanza kutetea utawala wa sheria na kupinga state lawlessness and impunity of the rulers.

Mawakili wakiwa kimya na TLS ikiwa mfukoni mwa serikali na wasipohoji matumizi mabaya ya madaraka basi wanakuwa darlings wa serikali.

Kuna kitu kingine ambacho ni common katika vitisho hivi. Havijawahi kufanikiwa na havitafanikiwa. Sheikh Abeid Amani Karume alipiga marufuku private legal practice mara baada ya Mapinduzi ya Zanzibar ya ’64. Tanzania ya leo sio Zanzibar ya miaka ya ’60 na ’70, hatutakubali udikteta wa aina ya Karume au wa aina nyingine yoyote kwenye Tanzania ya leo.

Inaelekea Dkt. Mwakyembe hafahamu au anajisahaulisha jinsi ambavyo TLS na mawakili binafsi walivyo embedded kwenye mfumo wetu wa kikatiba na kisheria. Simply put, ukifuta TLS maana yake ni kwamba hakuna wakili binafsi hata mmoja nchi nzima. Mfumo mzima wa kimahakama unategemea uwepo wa mawakili na kwa hiyo uwepo wa TLS. Mahakama karibu zote zitashindwa kufanya kazi kusipokuwa na mawakili binafsi. The same applies to various tribunals and other judicial and quasi judicial bodies.

Aidha, kuna taasisi nyingi zilizoundwa na Katiba yetu kama vile Judicial Service Commission na Law Reform Commission ambazo zinakuwa properly constituted kukiwa na uwakilishi wa TLS. Kuna taasisi nyingine nyingi ambazo zimeanzishwa na sheria za kawaida ambazo composition yake inakamilika kukiwa na representation ya TLS. Hiyo legal, constitutional and political upheaval itakayotokana na kufutwa kwa TLS will be unprecedented and unimaginable kwa mtu mwenye akili timamu.

Dkt. Mwakyembe ana akili timamu. He must be joking. Hawezi kufuta TLS. Anachotaka kufanya ni kuwatisha mawakili ili wachague watu wale wale wa miaka yote kuongoza TLS. Anatutisha ili tuendelee na status quo katika uongozi wa TLS. Hataki tufanye mabadiliko yanayohitajika ili TLS yetu isichukue nafasi yake stahiki katika kuamua mustakbala wa nchi yetu na wa taaluma yetu.

Nawataka viongozi na wanachama wa TLS wamkemee Dkt. Mwakyembe in the strongest possible terms. Nawataka wagombea wenzangu wa nafasi mbali mbali za uongozi katika TLS wajitokeze hadharani na kulaani kauli ya Dkt. Mwakyembe in no uncertain terms. Wakinyamaza tutawajua wako upande wa nani: status quo au mabadiliko. And I’ll ask you all to vote accordingly.

 Tundu Lissu.

Zitto Afunguka kuhusu kufungiwa kwa wimbo ‘I’m Sorry JK’ wa Nikki Mbishi

$
0
0
Wimbo mpya wa rapper Nikki Mbishi, I’m Sorry JK umefungiwa.

Uamuzi huo umekuja saa chache baada ya rapper huyo kuitwa na Baraza la Sanaa la Taifa, BASATA Jumatano hii kujielezea kuhusiana na wimbo huo. Kupitia Instagram, Nikki amewaonya watu dhidi ya kuusambaza wimbo huo kwakuwa mkono wa sheria utawaangukia.

“Naomba niombe radhi kwa vyombo vyote vya habari kuwa sitoweza kuwapa ushirikiano wowote kuhusu wimbo wangu wa “I’M SORRY JK” uliositishwa na hii ni kwa usalama wao na wangu pia,” ameandika kwenye Instagram. 

“Napokea simu nyingi sana zikihitaji maelezo juu ya suala hilo ila kiukweli kwa watakaohitaji taarifa kamili wanaweza kufika ofisi za BASATA,naomba nisiwe msemaji tena juu ya jambo hili,” ameongeza.

Pia ameonya, “Kwa yeyote atakayeendelea kuusambaza au kuucheza popote pale mimi sitohusika naye maana technology iko huru popote duniani na siwezi kuzuia watu wasiupate kwa kuwa ushasambaa,hivyo chukua tahadhari ili usijikute mikononi mwa sheria. Asanteni sana,naomba msubiri ujio wangu mpya wa #SINGELI na aina nyingine za muziki kama #NAIJA #MCHIRIKU n.k.”

Mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Kabwe ameandika kwenye Facebook: Serikali imepiga marufuku wimbo wa msanii Nikki Mbishi. Wallah nilidhani ni utani kumbe Kweli? Serikali hii inachoogopa ni nini? Dah kua uyaone.”

Waziri Mkuu: Hatutakubalina Na Wachochezi ...... Amani Kwanza, Masuala Mengine Baadaye

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali haitakubali kuona watu wachache wanachochea vurugu na kusababisha watu wengine wapoteze maisha ilhali wao hawadhuriki.

Ametoa kauli hiyo jana jioni (Jumatano, Februari 15, 2017) wakati akizungumza na maelfu ya wananchi waliohudhuria mkutano wa hadhara kwenye uwanja wa michezo wa mjini Kibaya, wilayani Kiteto, mkoani Manyara.

Waziri Mkuu ambaye alikuwa katika siku ya kwanza ya ziara yake ya siku sita mkoani Manyara, alisema: “Hatutakubaliana na wachochezi. Hatutakubaliana na yeyote atakayesababisha kifo. Tukibaini kuna uchochezi, tutawasaka wahusika na kuwashughulikia,” alisema.

“Hapa kulikuwa na majina ya ajabuajabu, hatutakubali Kiteto iitwe Soweto au Kossovo, hapa ni Tanzania. Hatuwezi kuishi kwa kubaguana, ni lazima tuheshimu maamuzi ya wazee wetu wa kimila ambao wamesimamia zoezi hili ili kurejesha amani ya Kiteto,” alisema.
 
Alisema zamani Kiteto kulikuwa hakuna lugha ya amani lakini hali kwa sasa imebadilika na kuwa nzuri na akasisitiza kwamba hakuna kurudi nyuma.

Alisema anamshukuru Waziri Mkuu mstaafu, Mhe. Mizengo Pinda kuwa kufuatilia suala hilo na kuunda tume ya kutafuta amani wilayani Kiteto. “Nilipoingia madarakani, nami nilianza kufuatilia suala hilo ili nijue chanzo hasa ni nini. Nikabaini kuwa mgogoro mzima umechangiwa na chokochoko tu za watu wachache,” alisema.

Mapema, viongozi wa kimila walimkabidhi Waziri Mkuu rungu, jembe dogo na jani la mti wa asili (Kimasai unaitwa elisibie) ikiwa ni ishara amani ya kukomesha mapigano baina ya wafugaji na wakulima. Pia alishiriki dua ya kuombea amani ambayo iliongozwa na viongozi wa dini.

Idadi ya waliokamatwa kwa dawa za kulevya hadi sasa Dar yatajwa..... mwanafunzi aliyetaja majina ya viongozi naye atiwa mbaroni

$
0
0
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limetoa taarifa ya kukamatwa kwa jumla watuhumiwa 349 katika oparesheni ya kuwasaka watu wanaohusika na dawa za kulevya

Akizungumza leo Jijini Dar es Salaam, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Simon Sirro amesema kati ya watuhumiwa hao, wamo wauzaji, wasafirishaji na watumiaji wa dawa za kulevya, na kwamba wataanza kufikishwa mahakamani siku ya kesho, huku mmoja akipandishwa kizimbani leo.

Pia ametoa taarifa ya kijana mmoja anayedaiwa kusambaza taarifa za uongo, ambapo amesema kuwa jeshi hilo linamshikilia kijana huyo ambaye ni mwanafunzi mwenye umri wa miaka 23, anayedaiwa kutaja majina ya viongozi na kuwatuhumu kuwa wanahusika na dawa na dawa za kulevya.

Kuhusu askari 9 waliotuhumiwa kuhusika na dawa hizo, Kamanda Sirro amesema askari hao wamekabidhiwa kwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya kwa ajili ya kuchukuliwa hatua za kisheria.

Kamanda Sirro amesema hadi sasa jumla ya kete 612 pamoja na bangi vimekamatwa na kwamba kuna watu wengine 17 ambao bado jeshi hilo linawafuatilia na watakuwa mbaroni wakati wowote.

Agness Masogange apelekwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali kupimwa utumiaji wa madawa ya kulevya

$
0
0
Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu Dar es Salaam, Simon Sirro amesema mtuhumiwa Agness Gerald, maarufu Masogange amepelekwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali kwa ajili ya kuchukua vipimo vya damu ili kubaini kama anatumia dawa za kulevya.

Masogange ambaye ni mrembo maarufu anayetamba katika video za wasanii mbalimbali wa bongo fleva alikamatwa na polisi juzi.

Kamishna Sirro amewaambia wanahabari leo kuwa Masogange amepelekwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali na kwamba majibu yakipatikana kesho atafikishwa mahakamani

"Tunamchunguza Masogange katika mambo matatu ili kujua kama anauza , anatumia au anasafirisha dawa za kulevya, " amesema Kamishna Sirro.

Yusufu Manji Afikishwa Mahakamani Mchana huu

$
0
0
Mfanyabiashara maarufu nchini na mwenyekiti wa klabu ya Yanga, Yusufu Manji amefikishwa mahakamani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kusomewa shitaka moja la kutumia dawa za kulevya aina ya heroine..

Manji amefikishwa mahakamani leo ikiwa ni siku ya nane tangu alipojisalimisha na kushikiliwa katika Kituo Kikuu cha Polisi Dar es Salaam, alopoitikia wito wa Mkuu wa Mkoa, Paul Makonda ili kuhojiwa.

Umati mkubwa wa watu wanaodhaniwa kuwa ni mashahabiki wa Klabu ya Yanga, ndugu jamaa na marafiki wamefurika katika chumba cha mahakama

Yusuf Manji Kaachiwa Huru Kwa Dhamana ya Milioni 20

$
0
0
Mfanyabiashara maarufu Yusufu Manji amepata dhamana baada ya kusomewa shtaka moja la kutumia dawa za kulevya aina ya heroine.

Manji amesomewa shtaka hilo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu  baada ya wakili wake Alex Mgongolwa kuiomba dhamana na Jamhuri kusema haina pingamizi kwani shtaka hilo linadhaminika.

Hakimu Cyprian Mkeha amesema Manji atakuwa nje kwa dhamana kwa sharti la kusaini  bondi ya dhamana ya Sh10 milioni na awe na mdhamini mmoja ambaye atasaini bondi ya Sh10 milioni.

Amedhaminiwa na Katibu Mkuu wa Yanga Charles Mkwassa.Kesi itasikilizwa tena March 16

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya February 17

Waziri Mwakyembe afichua kilichofanya azidiwe kete na Agnes Masogange katika sakata la dawa za kulevya, amtaja kijana wake ambaye yuko hatarini kuuawa gerezani

$
0
0

Waziri wa Sheria na Katiba Dkt. Harrison Mwakyembe ameendelea kufunguka jinsi alivyokwama kudhibiti upitishwaji wa dawa za kulevya katika Uwanja wa Ndege wa Dar es Salaam wakati alipokuwa Waziri wa Uchukuzi hadi kuzidiwa kete na Agnes Masogange

Waziri Mwakyembe akiwa kwenye kipindi cha East Africa Breakfast amesimulia kilichotokea wakati alipotaka kumdhibiti binti mmoja aliyedaiwa kupitisha masanduku matano ya 'materials' za kutengenezea dawa za kulevya aliyekamatwa nchini Afrika Kusini akitokea Tanzania.

Amesema baada ya kufuatilia sakata lile mbali na kuchukua hatua kwa watu waliomsaidia kupitisha mzigo uwanja wa ndege, aliamua kufanya jitihada za kumkamata binti huyo ili achukuliwe hatua, lakini muda mfupi baada ya binti huyo kurejea nchini, yeye alihamishwa wizara, hivyo kukosa nguvu ya kumshughulikia, hatua iliyofanya binti huyo kumfanyia "nyodo".

Kumbukumbu zinaonesha kuwa binti ambaye alikamatwa nchini Afrika Kusini wakati huo kwa madai hayo, na kisha Waziri Mwakyembe kumfuatilia hadi kutimua baadhi ya watumishi wa uwanja huo Mwezi Agost mwaka 2013 alikuwa ni 'video queen' maarufu nchini, Agnes Gerald 'Masogange'.

Vilevile Mwakyembe amesema kijana wake mmoja anayefahamika kwa jina la Jingu ambaye yuko gerezani, anapaswa kuongezewa ulinzi kwa kuwa yeye ndiye aliyekuwa jemedari wa kudhibiti dawa za kulevya uwanjani hapo, lakini baadaye aliundiwa kesi na sasa huko gerezani anakutana na watu ambao wanaweza kumdhuru kutokana na kwamba yeye ndiye aliyesababisha wafungwe.

Mtazame hapa Dkt. Mwakyembe akifafanua zaidi....

Mchezaji wa Yanga na Taifa Stars afariki dunia

$
0
0
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Yanga, Prisons na Taifa Stars, Geofrey Bonny 'Ndanje' (37), amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Jijini Mbeya alikokuwa akipatiwa matibabu baada ya kusumbuliwa kwa muda mrefu na maradhi ya kifua kikuu

Awali taarifa za kuugua kwa kiungo huyo zilianza kusambaa kwenye mitandao ya kijamii, watu wakichangishana pesa kwa ajili ya kumsaidia mchezaji huyo kuendelea kupata matibabu katika hospitali hospitali ya Makandana - Tukuyu wilayani Rungwe mkoani Mbeya.

Dada wa mchezaji huyo aliyepewa nafasi katika timu ya Taifa Stas na kocha Marcio Maximo, Neema amesema, wamempoteza kipenzi chao baada ya kuhangaika naye kumuuguza kwa muda mrefu.

"Tumempoteza ndugu yetu ambaye amefariki usiku wa kuamkia leo, sisi tumekwenda majira ya saa 11:00 alfajiri tukakuta tayari amekwishafariki. Tumekuwa tukimuuguza kwa muda mrefu lakini Mungu amepanga yake, msiba upo nyumbani mjini Mbeya ambako taratibu za mazishi zimekwishaanza," amesema Neema Dada yake Marehemu Bonny.

Bonny alikuwa mchezaji wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars enzi za kocha Mbrazil, Marcio Maximo na wengi wanamkumbuka kwa soka lake maridadi katika sehemu ya kiungo, licha ya kwamba aliibuliwa wakati umri wake umekwishaenda.

Alicheza Yanga chini ya kocha Mserbia, Profesa Dusan Kondic na akaendelea hata alipoondolewa mwalimu huyo na kuletwa Mseribia mwingine, Kostadin Papic.

Ni kati ya wachezaji walioiwezesha Taifa Stars kukata tiketi ya kucheza fainali pekee za michauno ya Ubingwa wa Afrika (CHAN) zinazohusisha wachezaji wanaocheza ligi za nchini mwao pekee. 

Hata hivyo, Maximo akamtema katika kikosi cha Stars baada ya fainali za CHAN nchini Ivory Coast mwaka 2009 kutokana na kuwa majeruhi.

Maumivu hayo yalimfanya aachwe na Yanga mwaka 2011 akaenda kumalizia soka yake Simrik SYC ya Nepal.     


TRA Yakusanya Sh Trilioni 8.42 Kwa Miezi Sita

$
0
0
Mamlaka  ya Mapato Tanzania (TRA), imekusanya Sh trilioni 8.41 kuanzia Julai mwaka jana hadi Januari mwaka huu.

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari jana na Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi, Richard Kayombo, inaonesha makusanyo ya Januari mwaka huu ni Sh trilioni 1.14.

Kayombo alisema pamoja na juhudi za kukusanya kodi mbalimbali, hivi sasa wameelekeza nguvu katika kukusanya kodi ya majengo kwa kutoa ankara kwa wamiliki wa majengo katika mikoa mbalimbali.

“Wamiliki wa majengo wanakumbushwa kwamba kodi ya majengo inakusanywa na TRA kuanzia Julai mwaka jana, hivyo tunawaomba watoe ushirikiano kwa kulipia ankara zao kwa wakati,” alisema Kayombo.

Kuhusu zoezi la uhakiki wa Namba ya Mlipakodi (TIN), alisema kuna mafanikio makubwa na kwamba wananchi wa mikoa ya Arusha, Mwanza, Kilimanjaro, Dodoma, Mbeya, Morogoro, Tanga na Pwani waitikie wito huo mapema kuepuka usumbufu.

Kamati ndogo ya KAmati Kuu ya CHADEMA Yabariki Mbowe Amshitaki Makonda kwa Kumdhalilisha

$
0
0
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimesema kimejipanga na kitampatia mawakili wa chama Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe katika hatua yake ya kumfungulia kesi ya kikatiba na ya madai Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda.

Februari 8 mwaka huu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, alitaja majina 65 kwa tuhuma za kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya akiwamo Mbowe na kuwataka kuripoti Kituo Kikuu cha Polisi Dar es Salaam kwa ajili ya kuhojiwa.

Lakini siku moja baadaye Mbowe aliitisha mkutano na waandishi wa habari akiwa mjini Dodoma ambapo alieleza kutofika polisi kwa wito wa Makonda akisema hana mamlaka hiyo isipokuwa pale tu taratibu za kisheria zitakapofuatwa.

Mbowe ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi ya Upinzani bungeni aliweka bayana nia yake ya kumfungulia mashtaka ya madai Makonda kwa kumkashifu na kumchafulia jina.

Akitoa maazimio ya kikao cha kamati ndogo ya Kamati Kuu ya Chadema jijini Dar es Salaam jana, Makamu Mwenyekiti wa chama hicho, Profesa Abdalah Safari alisema kamati hiyo inaunga mkono hatua ya Mbowe kumfungulia kesi ya kikatiba Makonda.

“Katika hili tumejipanga kweli kweli…tutaungana na Mbowe katika kesi hii na tutampatia mawakili wa chama akiwamo mimi na tuko wengi,”alisema.

Profesa Safari aliwataka wote ambao walitajwa na wanaamini kuwa walionewa kujihusisha na biashara au utumiaji wa dawa za kulevya wafungue mashauri mahakamani.

 “Tunatoa wito kwa wale wengine wote ambao walitajwa na wanaamini kuwa walionewa, kuchafuliwa majina na au kudhalilishwa wafungue mashauri mahakamani, kwani hii ndio njia pekee ya kuzuia wengine wasifanyiwe uonevu kama huu siku zijazo,”alisema Profesa Safari.

Pamoja na mambo mengine, Profesa Safari alisema tangu kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu 2015 viongozi na wanachama wa Chadema wamekuwa wakikamatwa na kushtakiwa kwa makosa ya kubambikiziwa kwa kisingizio cha uchochezi.

Alisema mpaka sasa jumla ya wanachama na viongozi 215 wamefunguliwa kesi zaidi ya 78 nchi nzima.

“Kati ya hao wengi wao wamenyimwa dhamana bila sababu za msingi huku wale ambao walipatikana na hatia walipewa adhabu za vifungo bila kupewa fursa ya faini.

“Kutokana na hilo, hivi sasa tunaandaa orodha kamili itakayoainisha kesi zote za jinai ambazo ziko mahakamani na kuonyesha aina ya mashtaka na vifungo vilivyotolewa ambayo itawekwa wazi kwa vyombo vya habari na taasisi za ndani na nje ya nchi kuthibitisha kuwa kuna mpango wa kuwafunga viongozi wa upinzani kwa kusudi ili kuwadhoofisha,”alisema Profesa Safari.

Katika hatua nyingine Profesa Safari aliwaomba marais wastaafu, mawaziri wakuu wastaafu na majaji wastaafu kuzungumza na Rais John Magufuli kutokana na yanayoendelea na kwamba wasiogope kwani wao hawatatumbuliwa.

 “Marais wastaafu Ali Hassani Mwinyi, Benjamin Mkapa na Jakaya Kikwete wanaogopa nini? Kwanini wasimwambie Rais Magufuli kuwa na wao waliapa kuilinda Katiba ya nchi hivyo na yeye afanye hivyo.

“Mawaziri wakuu wako wapi? Cleopa Msuya, Jaji Joseph Warioba, Dk. Salim Ahmed Salim huyu amekuwa kimya kabisa na alikuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Majaji wastaafu nao wako kimya. Tunaomba waache uoga wajitokeze wao hawatatumbuliwa,”alisema Profesa Safari.

Vituo vya UKIMWI vinavyochochea ushoga vyafutwa

$
0
0
Serikali imevifuta vituo vyote vya taasisi zisizo za kiserikali vinavyotoa huduma za afya ya VVU na Ukimwi, kwa makundi maalum kutokana na kubainika kuhamasisha mapenzi ya jinsia moja.

Baada ya kuvifuta, serikali imeelekeza huduma hizo sasa kutolewa tu kwenye vituo vya umma pamoja na vituo vya afya vya binafsi vilivyosajiliwa.

Tamko hilo limetolewa leo Jijini Dar es Salaam na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu ambapo amesema kuwa serikali imefikia uamuzi huo kutokana na maambukizi ya VVU na Ukimwi kwa makundi maalum kuongezeka ikilinganishwa na wastani wa kiwango cha maambukizi nchi nzima.

Kwa upande wake Mganga Mkuu Prof. Muhammad Bakari Kambi amesema katazo hilo limelenga kupunguza maambukizi ya VVU na Ukimwi ambayo kwa sasa yameongezeka.

Wakati huo huo Waziri Ummy Mwalimu amewataka Watanzania kubadilisha kadi za homa ya manjano za zamani na kupatiwa kadi mpya na kusisitiza kuwa kuanzia tarehe 31 Machi mwaka huu kadi za zamani za homa ya manjano hazitatumika na kueleza gharama ya kubadilisha ni Shilingi 500 kwa Mtanzania na dola 10 kwa raia wa nje.

Mose Iyobo amchana tena Harmorapa

$
0
0
Dancer Mose Iyobo ambaye ni mpenzi wa Aunty Ezekiel amefunguka na kusema kuwa yeye haamini kama Harmorapa ana jina kubwa na wala hajawahi kusikia kazi yake yoyote ile na kusema hana ushauri wowote kwake, huku akimchana kuwa amekurupuka kwenye muziki.

Mose Iyobo alisema hayo kupitia eNewz ya EATV  na kudai kuwa muziki unahitaji mtu kujipanga ili uweze kumlipa lakini siyo kukurupuka kama ambavyo Harmorapa amefanya.

"Mimi ni mtu ambaye nipo kwenye muziki muda mrefu, kila siku nyimbo mpya zinapotoka ziwe za watu maarufu hata wasio maarufu nazisikia lakini mimi sijawahi kusikia kazi yoyote ya Harmorapa, kwa hiyo sina cha kumshauri ila hiyo kazi anayofanya inahitaji mtu makini, anayeenda na wakati na siyo kukurupuka tu na kufanya ghafla sababu hiyo kazi ina pesa nyingi sana na inatia umasikini kwa haraka sana kama haufanyi vile inavyotakiwa" alisema Mose Iyobo

Hii ni mara ya pili kwa Mose, kumchana Harmorapa, mara ya kwanza, alitoa kauli ya kumfananisha harmorapa na 'nyani'

SORRY MADAM -Sehemu ya 31 & 32 (Destination of my enemies)

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA

ILIPOISHIA
Vyombo vyote vya habari vikarusha tukio zima, ikiwa ni habari ya dharura(breaking news). Kwa kamera moja ya muandishi wa habari aliye kuwemo ndani ya jengo hilo na kujibanza kwenye moja ya kona pasipo kuonekana, aliitegesha kuelekea moja ya tv kubwa, na mawasiliano yakaruka moja kwa moja kwenye  kituao anacho kifanyia kazi, na kwakupitia video hiyo vituo vyote vya televishion nchini Tanzania vikawa vinaonyesha tukio hilo walilo liita la kigaidi, likiongozwa na waziri mstafu bwana Eddy Godwin, jambo lililo wastua wananchi wengi na kutambua maana ya waziri huyo kujiudhuru ndio hiyo.

ENDELEA
Shamsa akasimama wima pasipo kuwa na woga wowote
“Kaa chini wewe binti, kaa chini nitakupasua ubongo wako huo”
Mmoja wa watekeaji alizungumza huku bunduki yake akiwa ameielekezea kwa Shamsa, Dulla kwa haraka akamshika mkono Shamsa na kumvutia chini.

“Shamsa unataka kufanya nini, watakuua hawa watu”
“Nahitaji kuzungumza na baba yangu Eddy”
“Wasikilize watu wenyewe hawana akili kabisa hawa”
Dulla aliendelea kulalama kwa sauti ya chini, huku akiendelea kumshikilia Shamsa asiweze kunyanyuka kutoka katika sehemu aliyo lala.
“Funga mabakuli yenu wana haramu nyinyi”
Mtekaji huyo alizungumza kwa sauti ya kufoka na kuwafanya Dulla na Shamsa kunyamaza kimya.

  ***
“Madam”
Priscar alizungunza huku alimgeukia mdama Rahab aliye keti siti ya nyuma, akamkabidhi simu ambyo kuna ujumbe wa video uliingia. Rahab akaichukua simu hiyo na kutazama video hiyo.
“Ndugu wananchi, ninaimani kwa kufanya hivi serikali na wananchi kwa ujumla mutakuwa mumenielewa nini dhamira yangu, baada ya kujiudhuru”

Rahab akajikuta akistuka baada ya kumuona ni Eddy akizungumza kwenye video hiyo akiwa amevalia mavazi meusi pamoja.
“Eddy………!!”
Rahabu hakuamini macho yake kwani sura na sauti vya mtu anaye zungumza ni Eddy mwenyewe, ila kitu ambacho kinazidi kumshangaza zaid, Eddy amemuacha kwenye kwenye handaki mbalo kipindi walipo kuwa wakifanya kazi za ujambazi walikuwa wakijificha huko yeye na wezake.

“Serikali isipo hitaji kufwata matakwa yangu basi watu wote waliomo ndani ya jengo hili wateteketea kwa kupigwa risasi hadi kufa”
Ujumbe huo wa sauti ukaishia hapo, magari kwenye foleni yakaanza kuruhusiawa huku Rahab akiwa amepoteza amani ndani ya moyo wake. Kwani hiyo ni moja ya skendo ambayo itakuwa ni ngumu sana kuweza kujisafisha mbele ya wananchi ya Watanzania.

      Raisi Praygod akaitisha kikao cha dharura kwa maofisa wote wa ngazi za juu katika jeshi. Hali ya hatari inayo endelea katika jiji la Dar es Salaam kuhusiana na kutekwa kwa jengo la kibiashara la Mlimani City, ndio mada kuu ya kuweza kuzungumziwa ni jinsi gani ya kuweza kuwaokoa mateka wote wanao sadikika kutekwa na waziri  wa ulinzi, pasipo kujua kwamba mtu aliye panga mpango huo ni miongoni mwa washauri wa raisi walio panga kufanya kazi hiyo.

Vikosi vya vitengo vyote vya jeshi kuanzia polisi, jeshi, zima moto pamoja na usala wa taifa, waliweza kutumwa katika jengo la Mlimani City kuhakikisha kwamba wanaweza kuwaokoa watu wote walio weza kutekwa ndani ya jengo hilo,

Waandishi wa habari, karibia vituo vyote vya habari nchini Tanzania wakaweka kambi katika jengo la Mlimani City kuweza kurusha habari kwa mambo ambayo yanaendelea katika eneo hilo.

Sio waandhishi pekee wa Tanzania, bali hata kutoka mashirika makubwa kama BBC, Sky news pamoja na CCN, waliweza kuweka kambi ili kuitaarifu dunia juu ya kuwepo kwa tukio hilo la ugaidi ambalo limejitokeza nchini Tanzania, huku tukio hilo walikifananisha na tukio lililo tokea nchini chini Kenya miaka kadhaa iliyo pita kwa kutekwa kwa jengo la kibiashara, ambapo ni watu wengi waliweza kutekwa na wengine waliweza kupoteza maisha yao katika shambulio hilo.

Ulinzi mkali ukazidi kuimarishwa nje ya jengo la Mlimani City, barabara inayo pita kuelekea Mwenge pamoja na Ubungo zote ziliweza kufungwa, hawakuruhusiwa watu kuweza kukatiza katika maeneo hayo.
Simu ya mezani iliyopo ndani ya chumba cha kuongozea kamera zate ndani ya jengo hilo, ikaanza kuita Briton na watu wake wote wakaitazama, kila mmoja akiwa katika hali ya kujiuliza ni nani anaye ipiga simu hiyo kwani hapakuwa na mtu aliye weza kufikiria kwa muda huo kuna simu ambayo inaweza kupigwa katika eneo hilo. Briton akajikaza na kuipokea simu hiyo, ila hakuzungumza kitu chochote.

“NYOTE MUMEKUFAAAAA”
Sauti nzito inayo kwaruza kwaruza ilisikika upende wa pili wa simu hiyo, jambo lililo muogopesha Briton na kujikuta akiutoa mkonga huo wa simu sikioni mwake na kuutazama kwa macho ya mshangao.
                                                                                                 ***
“Eddy…………!!”
Manka alijikuta akishangaa huku akitazama taarifa inayo rushwa kituo cha CNN, kuhusiana na kutekwa kwa jengo la Mlimani City.
“Ndio maana nikakuambia Eddy ni mtu hatari hafai kwenye hii jamii”

Mzee Godwin alizungumza huku akimtazama Manka machoni mwake, muda wote John alikaa kimya akiitazama taarifa hiyo kwani hakujua kwamba huo ni mchezo. Kitu kinacho muumiza kichwa zaidi ni jinsi gani ambavyo Eddy anaoeneka kuwa ni mtu hatari sana kwenye mipamgo yake kwani hadi kufikia hatua ya kuweza kuteka jengo hilo kubwa la biashara nchini Tanzania, basi amekamilika katika mipango yake, ila ukweli ni kwamba mpango huo wote mzee Godwin anaufahamu, ni njia moja ambayo inaweza kumfanya adui yake huyo kukimbia kimbia ndani ya nchi yake kama aliyo kuwa akiandamwa yeye kipindi Eddy alipo kuwa madarakani.

Katika taarifa hiyo, inayo endelea kuruka, hewani kukaonyeshwa kiongozi huyo ambaye amevalia sura inayo endana na Eddy, akiwachukua wanaume wawili alio wasimamisha mbele ya kamera pasipo huruma akawatandika risasi za kichwa, jambo lililo zidi kuwastua watu wote.
                                                                                               ***
“Eddy kuna tatizo”
Samson alimuambia Eddy aliye kuwa amesimama mbali kidogo na computer hizo mara baada ya kupiga simu ya vitisho kwa watekaji hao, kwa haraka akaelekea sehemu alipokuwa amekaa Samson, akashahudia watu wawili wakiwa wameuwa kwa kupigwa risasi kisha kiongozi wao huyo akizungumza kitu.

“Atendelea kufa mmoja baada ya mwengine”
Ujumbe huo mfupi ukazidi kuwachanganya Eddy na Samson ambao hawakujua wafanye nini kwa wakati huo, Eddy akaingia kwenye chumba alicho kuwa amelala, akachangua changua kwenye nguo zililzo wekwa bila ya mpangilio juu ya meza, akabahatika kuweka kulpata koti moja jeusi refu kuanzia chini hadi juu, ambapo lina kofia kubwa, na mtu akilivaa si rahisi kuweza kujulikana. Akalivaa, alipo ona limemtosha vizuri akatoka nje ya chumba hicho na kumuuliza Samson jinsi anavyo onekana.
“Unaonekana upo vizuri”
“Basi inatupasa kuweza kuifanya hii kazi ya kuwaokoa mamia ya watu walio weza kutekwa nyara ndani ya jengo hilo”

“Tutaifanya vipi hii kazi ikiwa, usalama umeimarishwa kila kona”
“Tutajua ni jinsi gani ya kuweza kufanya ila kwa sasa inatupasa kuweza kuondoka katika eneo hili, hakuna muda mwengine wa kuweza kupoteza”
Wakatoka na Samson na kuingia kwenye gari, safari ya kurudi jijini Dar es Salaam ikaanza, akilini mwa Eddy, akawa anafikiria ni jinsi gani anaweza kuifanya kazi hiyo ya kisiri pasipo mtu yoyote kumtambua.

Mwendo wa masaa manne wakafanikiwa kufika katika jumba lake la kifahari, ambapo hapakuwa na mlinzi wa aina yoyote anaye linda hapo, macho ya askari yote yapo kwenye jengo la Mlimani City. Wakaingia kwenye moja ya chumba cha siri cha Eddy kilichopo chini ya ardhi na chumba hicho mara nyingiu huwa anaficha silaha zake za siri za kupambana endapo kunakuwa na tatizo kubwa.

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images