Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya January 30


Jipatie Dawa za Asili za Kupunguza Maziwa, Kutoa Michirizi, Kuondoa Chunusi, Kuongeza Maumbilie na Nguvu za Kiume

$
0
0
NATURAL BEAUTY COSMETICS ni kampuni inayoongoza kwa kutoa bidhaa original za asili zenye matokeo mazuri bila kemiko wala madhara yoyote pia tunatoa punguzo la bei la %10 kwa ajili ya Xmas and new year pata bidhaa kwetu uweze kufurahia matokeo mazuri kwa bidhaa original.

     Tunazo za:👇👇👇👇
1. Kutengeneza shepu hipsi na makalio kwa:- (a) Dawa ya kunywa au Botcho yakupaka @ 150,000/= (b)Vidonge maalum @ 150,000/=
 
2. Kupunguza au kuongeza maziwa @ 90,000
3. Kushepu miguu kuwa (Chupa ya bia) @ 100,000
( Kuludisha bikra (@) 100,000/=
 
4. Kuondoa mipasuko au michirizi @90,000/=
5.Kuwa softi na mweupe mwili mzima kwa mafuta @10,000/= vidonge maalum @150,000
 
6.Kuongeza unene wa mwili mzima @130,000/=
7.kupunguza tumbo na manyama uzembe kwa:-
(a)Dawa ya kunywa au kupaka @ 130,000/=
(b) Mkanda original wa MICRO COMPUTER @200,000/=
 
8.Kuondoa chunusi na madoa sugu (@) 100,000/=
9.Kuondoa mvi milele na zisiludi tena @ 120,000
 
10.Kuongeza maumbile kwa:- (a)Gel ya kupaka @120,000/= Mashine original ya HANDSOME UP @170,000/=
11.Kuondoa vinyweleo @90,000/=
 
12.kuotesha nywele kwenye kipara @120,000/=
13.Kuongeza nguvu za kiume na hamu ya tendo @100,000/=
14.Kuondoa makovu sehemu yoyote @90,000/=

     WASILIANA NASI KWA NAMBA :-
          065 9618585 au
             0759029968.
 
Popote ulipo utapata huduma zetu. BIDHAA  zetu zote ni GARANTII  na risiti unapewa ili kuhakikisha mafanikio yako
           Follow us 
   👇👇👇👇👇👇
@natural2162
@natural2162
@natural2162
@natural2162
@natural2162
      👆🏻👆🏻👆🏻👆🏻👆🏻👆🏻

Makamu wa Rais atuma salamu za pole na pongezi kwa Mkuu wa Mkoa wa Geita kwa Kuwaokoa Wachimbaji Waliofukiwa na Kifusi

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan amemtumia salamu za pole na pongezi Mkuu wa Mkoa wa Geita Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Kyunga kwa kazi nzuri na kubwa waliyoifanya ya kuwaokoa wachimbaji wadogo 15 waliofukiwa na maporomoko ya udongo kwenye Mgodi wa Dhahabu wa RZU uliopo katika Kijiji cha Nyarugusu, wilaya ya Geita katika mkoa wa Geita.

Tukio hilo la kufukiwa wachimbaji hao wadogo 15 wakiwemo Watanzania 14 na raia Mmoja wa China lilitokea usiku wa Tarehe 26 Januari mwaka 2016.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan amesema amepokea kwa furaha taarifa za kuokolewa kwa wachimbaji hao wadogo na amesifu na kupongeza jitihada za kuwaokoa wachimbaji hao  zilizofanywa na Serikali ya Mkoa wa Geita, Jumuiya ya Wachimbaji Wadogo wa mkoa wa Geita, Wamiliki wa Migodi ya Dhahabu na wananchi kwa ujumla kwa kutoa vifaa mbalimbali vya uokoaji jitihada ambazo zimepelekea kuokolewa kwa wachimbaji hao wakiwa hai.

Makamu wa Rais amesisitiza kuwa “jitihada ,Umoja na Mshikamano ulioonyeshwa na makundi mbalimbali katika kuwaokoa ndugu zetu waliofukiwa na maporomoko ya Udongo wakiwa kazini huko Geita ni mfano mzuri na wakuigwa na wananchi na taasisi nyingine nchini katika kujitolea kwa hali na mali hasa vifaa vya uokoaji kwa ajili ya kusaidia watu wanaopatwa na majanga ili kuepusha madhara yanayoweza kutokea kama walivyofanya ndugu zetu wa mkoa wa Geita nawapongeza Sana”.

 Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amewataka wamiliki wa migodi kote nchini wahakikishe wanafanya kazi zao za uchimbaji wa madini kwa kuzingatia kanuni,taratibu na sheria kama hatua ya kuepuka madhara yanayoweza kutokea wakiwa wanafanya shughuli zao za uchimbaji wa madini.

Kupitia kwako Mkuu wa mkoa wa Geita napenda kutuma salamu za pole kwa ndugu, jamaa na marafiki kufuatia kutokea kwa tukio hilo na nawaombea kwa Mwenyezi Mungu wachimbaji hao ambao kwa sasa wanapatiwa matibabu Katika Hospitali ya Serikali ya mkoa wa GEITA matibabu mema ili waweze kupona haraka na kurejea kwenye kazi zao za kujitafutia riziki.

Wakati huo huo, Makamu wa Rais wa Jamhuri  ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan ameipongeza Ofisi ya Waziri Mkuu, Kitengo cha Kudhibiti Maafa nchini, Wizara ya Nishati na Madini pamoja na Wizara ya Mambo ya Ndani kwa ushirikiano mkubwa walioutoa kwa Ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Geita na kupekelea kuchukuliwa hatua za haraka katika kushughulikia ajali hiyo.

Imetolewa na
Ofisi ya Makamu wa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Dar es Salaam           

29-Jan-2017

Rais Magufuli Ahutubia Katika Kutangaza Jina Rasmi La Kituo Cha Amani Na Usalama Kilichopewa Jina La Mwalimu Julius Nyerere Addis Ababa Nchini Ethiopia

$
0
0
Jengo la amani na usalama lililopo makao makuu ya Umoja wa Afrika (AU) Mjini Addis Ababa nchini Ethiopia jana tarehe 29 Januari, 2017 limetangazwa rasmi kuwa litaitwa Mwalimu Julius Nyerere.

Jengo hilo limepewa jina hilo rasmi katika hafla ya chakula cha mchana iliyofanyika leo na kuhudhuriwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na Marais mbalimbali wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Mhe. Antonio Guterres, Mawaziri na Mabalozi mbalimbali wanaohudhuria Mkutano wa 28 wa wakuu wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika unaoendelea Mjini hapa.

Akizungumza katika hafla hiyo Mhe. Rais Magufuli aliwashukuru viongozi wote wa Umoja wa Afrika kwa kuamua jengo hilo liitwe jina la Mwalimu Julius Nyerere ikiwa ni kutambua mchango wake katika kupigania amani na usalama na amebainisha kuwa Mwalimu Nyerere alikuwa Mwafrika halisi na kiongozi mahiri na shupavu.

“Na kwa hakika naweza kusema kuwa alikuwa mmoja wa viongozi bora kabisa ambaye amewahi kutokea katika Bara letu, katika maisha yake yote Mwalimu Nyerere alipambana ili kujenga umoja na mshikamano miongoni mwa Afrika, alikuwa mmoja wa waanzilishi wa umoja huu, sisi Watanzania kwa hakika tunajivunia sana Mwalimu Nyerere kuwa Baba wa Taifa” alisema Mhe. Rais Magufuli.

Mhe. Dkt. Magufuli aliongeza kuwa Mwalimu Nyerere alitoa mchango mkubwa katika kupambana na ubaguzi na unyonyaji wa kila aina, alisaidia ukombozi wa nchi nyingi za Afrika, na hata alipong’atuka katika hatamu za uongozi wa Taifa la Tanzania aliendelea kutoa mchango wake kupigania amani katika nchi za Afrika.

“Wito wangu kwenu, waheshimiwa viongozi ni kwamba, sambamba na kumuenzi Mwalimu Nyerere kwa jengo hili, itakuwa ni jambo jema zaidi kama tutajitahidi kufuata nyayo zake pamoja na kuishi maisha ya viongozi wengine hodari wa Bara hili wakiwemo Hayati Kwame Nkhrumah, Ahmed Ben Bella, Sekou Toure, Gamal Abdel Nasser na bila kusahau shujaa wetu mwingine Hayati Nelson Mandela” alisisitiza Rais Magufuli.

Mkutano wa 28 wa wakuu wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika unaendelea leo  tarehe 30 Januari, 2017 hapa Addis Ababa.

Video: Rais Magufuli Alivyohutubia kwa Kiswahili Huko Ethiopia

$
0
0
Jengo la amani na usalama lililopo makao makuu ya Umoja wa Afrika (AU) Mjini Addis Ababa nchini Ethiopia jana tarehe 29 Januari, 2017 limetangazwa rasmi kuwa litaitwa Mwalimu Julius Nyerere.

Rais Magufuli alipewa heshima ya kutangaza rasmi kuanza kufanya kazi kwa jengo

==>Msikilize hapo chini akihutubia  kwa Kiswahili

Daktari Aandika Barua ya Kuacha Kazi Baada ya Mkuu wa Mkoa Kumuweka Rumande Kwa Kosa la Kipindupindu

$
0
0
Mganga  Mkuu wa Wilaya ya Singida Vijijini, Dk. Erick Bakuza ameandika barua ya kuacha kazi

Dk. Bakuza amechukua uamuzi huo ikiwa ni siku chache tangu alipopewa adhabu ya kuwekwa mahabusu na Mkuu wa Mkoa huo, Dk. Rehema Nchimbi.

Dk. Nchimbi alitoa amri ya kukamatwa kwa daktari huyo kutokana na kuzuka ugonjwa wa kipindupindu ambao ulisababisha vifo vya watu wawili mwishoni mwa mwaka jana.

Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, Rashid Mandoa jana alithibitisha kuacha kazi kwa Dk. Bakuza.

“Ni kweli amewasilisha barua ya kuacha kazi lakini ninavyojua mimi si kweli kwamba ameacha kazi kutokana na adhabu aliyopewa na Mkuu wa Mkoa ya kuwekwa ndani.

“Kwanza ujue hakuwekwa ndani, na ameamua kuacha kazi kwa sababu amepata sehemu nyingine ambayo anaona ina maslahi anayohitaji yeye,” alisema.

Juhudi za kumpata Dk. Bakuza kuzungumzia hatua yake hiyo hazikuzaa matunda.

Kauli ya Mkuu wa Mkoa
Wakati Mkurugenzi huyo akisema kwamba Dk. Bakuza hakuwekwa ndani, Mkuu wa Mkoa huyo, Dk. Nchimbi alithibitisha kwamba aliwekwa ndani kwa   saa tatu.

“Mimi nilitoa amri ya kukamatwa Daktari huyu na aliwekwa chini ya ulinzi kwa saa tatu.Nilimuweka ndani kwa sababu ya mazingira ambayo niliyakuta nilipokuja kuanza kuitumikia nafasi niliyoteuliwa ya ukuu wa mkoa, na nitatetea uamuzi wangu huo.

“Niliamuru akamatwe kwa sababu ya mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu, kesi ya kwanza ya kuwapo kwa mgonjwa wa kipindupindu iliripotiwa Novemba 26, mwaka jana.

“Utaratibu unajulikana wazi kwamba ikifika kesi tano DMO (Mganga Mkuu wa Wilaya) anatakiwa atoe taarifa kwa MRO (Mganga Mkuu wa Mkoa).

“Desemba 4   hakutoa taarifa, ilipofika Desemba 16 vikatokea vifo viwili hakutoa taarifa hadi Desemba 18 ndipo akatangaza.

“Nikaona hakuwa makini katika kazi yake kwa sababu alipaswa kutangaza mapema ili tuchukue hatua za kudhibiti ugonjwa huo na naamini hata hivyo vifo visingetokea,” alisema.

Dk. Nchimbi alisema suala la kipindupindu halipaswi kuchukuliwa kisiasa na kwamba lenyewe lipo kitaalamu zaidi.

“Kuna taratibu ambazo hufuatwa lazima tupate evidence ya kutosha, watu wachukuliwe vipimo, yeye alinyamaza kimya. Wataalamu walipokwenda kuchunguza wakagundua kuna kipindupindu kwenye wilaya yake,” alisema.

Aliongeza: “Kwa hali hiyo niliona hakuwa makini katika kazi yake, hivyo nilitaka kumshtua tu awe makini, hakuwa makini.

“Katika hali ya kawaida angesema mapema tungechukua hatua mapema, tungetibu maji, tungesafisha visima na hata vifo visingetokea,” alisema.

Maalim Seif Afunguka Mambo Mazito.......,Adai Muda si Mrefu Atakuwa Rais wa Zanziba, Asema Yupo Tayari Kwa Maridhiano

$
0
0
Aliyekuwa  mgombea urais Zanzibar kwa tiketi ya Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad, amesema yupo tayari kufanya tena maridhiano endapo pande zote mbili zitakubali kwamba Zanzibar kuna matatizo.

Maalim Seif aliyasema hayo jana katika kipindi cha Funguka kinachorushwa na Televisheni ya AZAM na kuongozwa na mtangazaji nguli nchini, Tido Mhando.

Alisema maridhiano yaliyofanyika akiwa na Rais Mstaafu wa Zanzibar, Dk. Amani Abeid Karume,  yalikuwa na manufaa makubwa kwa kuwa Zanzibar ilikuwa na amani na utulivu.

Maalim Seif alisema CUF iliamua kukaa na Karume baada ya kuona uchaguzi ulikuwa unakaribia kufanyika hivyo ikaamua kufanya kikao cha muafaka wa maridhiano na kuunda Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK) iliyozaa matunda.

Alisema baada ya kufanyika maridhiano na kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais alikuwa na nafasi kubwa ya kumshauri Rais mambo mbalimbali.

 “Hata kulipokuwa na SUK (Serikali ya Umoja wa Kitaifa),  mambo yalikuwa mazuri na maelewano na hata ilikuwa ikitokea mtu akifika ofisini anashindwa kufahamu CUF ni nani na CCM ni nani,’’ alisema Maalim Seif.

Alisema  hata sasa kama kuna nia njema ya kufanyika mazungumzo yafanyike kwa sababu  kwa sasa Zanzibar kuna matatizo na uhasama unazidi kupamba moto.

Maalim Seif pia alizungumzia suala la kufutwa  Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 25, mwaka 2015 na marudio yake Machi 20 mwaka jana.

Alisema yeye alishinda kwa kura nyingi na hivyo kama uchaguzi ungekuwa huru na haki yeye ndiyo alistahili kutangazwa kuwa Rais wa Zanzibar na si vinginevyo.

Alisistiza kwamba hatambui uchaguzi wa marudio uliofanyika Machi 20, mwaka jana  kwa kuwa hakushiriki na wala hakuwa na sababu ya kushiriki kwa kuwa mshindi alishapatikana Oktoba 25, mwaka juzi.

“Nisingeweza kukubali kurudia uchaguzi ule kwa kuwa mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi (ZEC) alifuta matokeo yale ili CCM kwa njia zozote zile ishinde kwenye uchaguzi wa marudio.

“Hawakuweka mpira  uwanjani urudiwe eti kwa sababu washindwe  si kweli, hivyo wangetumia mbinu zozote ili washinde ,’’alisema Maalim Seif.

Seif ambaye pia ni Katibu Mkuu wa CUF, alisema ni kosa kukaa kimya wakati bado suala   la uchaguzi linafanyiwa kazi ili ufumbuzi upatikane.

Alisema  hilo  ni kama bomu ambalo likiripuka  hali itakuwa mbaya.

Mtangazaji alimuuliza MaalimSeif kama hakuona kuwa ni kosa kujitangazia   ushindi?

Alisema alifanya hivyo baada ya kuona kwamba ZEC ilikuwa anataka kumtangaza Dk. Shein (Ali Mohamed Rais wa Zanzibar) kuwa ni mshindi  huku hakushinda.

Hata hivyo alisema kama waliona amefanya makosa basi wangemkamata na kumpeleka mahakamani.

Alisema bado ana matarajio ya kuwa Rais wa Zanzibar katika   muda mfupi ujao.

Kuhusu uchaguzi wa 2020, alisema  ataangalia hali ya siasa ijayo.

 Mgogoro ndani ya CUF
Akizungumzia mgogoro ndani ya chama hicho, alisema  unachangiwa na Msajili wa Vyama vya Siasa.

Alisema Profesa Ibrahimu Lipumba aliamua kuondoka yeye mwenyewe.  “Lakini cha kushangaza baada ya miezi 10 akarudi sijui ni kwa misingi gani?” alihoji.

Alisema Katiba iko wazi kwa mtu anayejiuzuru, ni kwamba anaandika barua kwa Katibu Mkuu na Katibu anapeleka barua kwenye Mkutano Mkuu.

Alipoulizwa mbona alipokabdhiwa barua hakuitisha mkutano wa kumridhia Lipumba kujiuzulu, alisema hawakuweza kuitisha mkutano ghafla kwa kuwa chama hicho ni kidogo na hakikuwa na fedha.

‘’Lakini tuliitisha Mkutano Mkuu akajadiliwa, cha kushangaza yeye anang’ang’ania kuwa ni mwenyekiti, hii inashangaza haiwezekani katika hili!’’ alisema.

Alisema hata Msajili anafahamu kurudi kwa Lipumba ni lazima akubaliwe na Mkutano Mkuu.

Hata hivyo, alisema katiba ya chama haisemi mtu anayeondoka akae na baadaye aamue kurudi kwa sababu  hawafahamu kama ana nia njema na chama au la ikizingatiwa  pia alikiacha chama  katika kipindi kigumu cha uchaguzi mkuu.

Seif alisema kutokana na Msajili wa Vyama vya Siasa kuendelea kumtambua Profesa Lipumba licha ya kujiuzuru yeye mwenyewe, CUF kimeamua kwenda mahakamani  kuweza kupata tafsiri ya sheria.

“Mgogoro huu ulipandikizwa kwa wazi kabisa na Lipumba wakati anajiuzuru  tulimfuata na viongozi mbalimbali, wa dini wa chama wazee na vijana asitoke lakini alikataa kuendelea kubaki kwenye nafasi hiyo,’’ alisema.

Maalim Seif alisema kwa kufanya hivyo imeonekana kuwa Lipumba hakuwa na msimamo kwa kuwa yeye ndiye aliyewaletea aliyekuwa mgombea urais akiwakilisha Ukawa, Edward Lowassa, huku akisema kuwa kila alipokuwa akipita vijiweni, Lowassa alikuwa akitajwa tajwa sana na wananchi.

Alisema  yeye na wenyeviti wenzake wa   Ukawa walimtangaza Lowassa, hivyo Lipumba kubadili msimamo kulionyesha dhahiri kwamba tayari kulikuwa na nguvu nyuma yake iliyokuwa ikimshawishi  na hata baada ya kujiuzuru iliendelea kufanya hivyo.

Maalim  alisema baada ya Lipumba kukaa pembeni CUF kilipata mafanikio makubwa kwa vile kilipata viti vya ubunge 10 upande wa Bara na halmashauri nne ambazo ziliundwa na chama hicho  peke yake.

Alisema  hata katika uchaguzi mdogo wa marudio wa hivi karibuni, Lipumba alisimamisha wagombea katika kata 11 lakini hakuambulia kiti hata kimoja zaidi ya wagombea kupata kura 10 ,11,12.

Alipoulizwa hatima ya CUF kwa sasa,   alisema hiyo si mara ya kwanza kwa vile  kuna migogoro mikubwa ilipita huko awali ukiwamo wa Hamad Rashid Mohamed lakini ulikwisha.

Kuhusu kama ana mpango wa kuunda chama kingine, alisema ni hisia za watu tu na kwamba hana mpango huo.

Alisema  yeye ni mmoja wa waanzilishi wa CUF akiunda chama kingine ataonekana kuwa ni msaliti.

“Siwezi kuunda chama kingine nikaachana na CUF, mimi ni CUF kindakindaki na nitaendelea kuwa CUF kindakindaki  ndani ya chama ,’’alisema.

Alisema CUF kimeamua  kupeleka mahakamani  mgogoro huo na hata kama mahakama itampa Lipumba ushindi  watakata rufaa ingawa hawatarajii hilo.

Maalim Seif  alikiri kwamba bila vyama vya upinzani kuungana ni vigumu kukiondoa  CCM madarakani na ndiyo sababu ya kufanya hivyo.

Mgogoro wa ruzuku
Alimshangaa Msajili wa Vyama vya Siasa kwa kutoa ruzuku kwa Profesa Lipumba   kupitia akaunti nyingine ambayo si ya chama makao makuu.

Alisema Msajili aliwaandikia barua kusema kuwa  ruzuku isingetolewa kutokana na chama hicho kuwa na mgogoro, lakini  baada ya muda wakashangaa imepitishiwa katika akaunti ya wilaya ya Temeke.

Kuhusu kushindwa uchaguzi wa marudio, Dimani alisema siyo kwamba wameshindwa bali   Dimani ni jimbo la CCM  na hata hivyo kama   demokrasi CCM ingetumika isingeshinda.

Maisha baada ya kustaafu
Maalim Seif alisema licha ya kustaafu anapata haki zake zote kisheria siyo kuomba.

Haki hizo ni pamoja na gari, walinzi na posho kila mwezi ingawa alisema matibabu anajigharamia mwenyewe   kwa kuwa akiomba ananyanyaswa.

==>Zaidi, Msikilize Hapo Chini

Golikipa David Burhan wa Kagera Sugar, afariki dunia

$
0
0
Mchezaji wa timu ya Kagera Sugar, David Abdalah Burhan ambaye pia amewahi kuchezea klabu mbalimbali za bongo amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando.

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amethibitisha kutokea kifi hicho na kutuma salamu zake za pole kwa familia pamoja na klabu ya Kagera Sugar na kwa wote ambao wameguswa na kifo cha mchezaji huyo.

"Nimepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha David Abdalah Burhan mchezaji wa Kagera Sugar. Amefariki usiku wa kuamkia leo.Apumzike kwa amani"

Marehemu David Burhan ameshawahidakia Mbeya City na Majimaji, ikumbukwe kuwa Burhan ni mtoto wa mshambuliaji wa zamani wa Pan African ya Dar es Salaam, Abdallah Buruhan.


Picha: Meli kubwa ya kisasa ya Azam yatia nanga Bandari ya Tanga kwa mara ya kwanza

$
0
0
Meli mpya na ya kisasa iitwayo AZAM SEALINK 2 aina ya RORO yenye uwezo wa kubeba abiria wapatao 1650, mizigo uzito wa tani 717 sambamba na magari 150 imetia nanga
Bandari ya Tanga leo.

Meli hiyo inatarajiwa kufanya safari zake na kutoa huduma za kubeba abiria na mizigo ikiwemo magari kutoka Pemba kwenda Unguja hadi Tanga mara moja kwa wiki.

Wanachama 200 Waikimbia CHADEMA na Kujiunga CCM

$
0
0
Chama   cha  Demokrasia  na Maendeleo (Chadema), kimeendelea  kupata  pigo  baada  ya  wanachama  200, wakiwamo  viongozi  wa Kitongoji  cha Kwemghogho Mahezangulu kujitoa  na  kujiunga  na  Chama Cha Mapinduzi (CCM) .

Akizungumza  baaada ya  kupokea  wanachama  hao, Mbunge wa  Bumbuli, January Makamba (CCM),  alisema  wananchama  hao  wameamua  kurudi  wenyewe nyumbani   kutokana  na   kuona  ahadi  nyingi  za maendeleo zimetekelezwa  kwa  kiasi kikubwa.

Alisema  chama  chake kimefanya mambo mengi  hivyo  haoni  ajabu  ya  kupokea  wanachama kutoka  vyama  vingine  vya  upinzani.

January, ambaye pia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia Muungano na Mazingira, alisema  hivi sasa kuna kazi kubwa ya kuendelea kuleta maendeleo ambayo yanahitaji umoja  na mshikamano.

Alisema migogoro, majungu na fitina inatokana na kambi  zilizokuwapo huku akiwasisitiza wana CCM watambue ni hema kubwa na linavumilia tofauti za watu.

Aliyekuwa  Mwenyekiti wa  Chadema  Kitongoji cha Kwemghogho, Shabani Kahema,  aliwataka   vijana  na  wanachama  wengine  kubadilika kwa kuwa CCM ndiyo chama chenye ilani inayotekelezeka.

Waziri Mkuu Atua Dodoma Kwa Ndege ya Abiria

$
0
0
Waziri mkuu Kassim Majaliwa amewasili mkoani Dodoma leo asubuhi kwa ajili kuhudhuria vikao vya bunge  ambavyo vinatarajiwa kuanza kesho Jumanne

Waziri Mkuu ameongozana na mkewe Mary Majaliwa pamoja na viongozi mbalimbali ambao wametumia usafri wa ndege ya abiria ya ATCL inayopitia Dodoma kuelekea Kigoma

Katika Uwanja wa Ndege Waziri Mkuu amepokelewa na mkuu wa mkoa wa Dodoma Jordan Rugimbana pamoja na viongozi wa serikali na chama wa mkoa wa Dodoma

Vikao vya Bunge vinaanza kesho baada ya wiki mbili za shughuli za kamati za kudumu za Bunge, na sasa tayari wabunge wamekwishawasili Dodoma kwa ajili ya vikao hivyo vitakavyodumu kwa takriban wiki 2

Harmorapa Ajibu Mapigo Baada ya Moses Iyobo Kumuita NYANI

$
0
0
Baada ya Mtangazaji wa XXL ya Clouds FM, B Dozen kupost picha Instagram akiwa na mtafiti wa wanyama aina ya Sokwe, dancer wa Diamond Platnumz Mose Iyobo alicomment kwenye picha hiyo kuwa mtafiti huyo aje na Dar es salaam kumfanyia utafiti Harmorapa.

Leo  January 30 2017 kupitia YOU HEARD ya XXL clouds FM, Soudy Brown ameongea na kuhusu  issue ya  Mose Iyobo kumfanisha Harmorapa na Nyani ambapo haya ni majibu ya Harmorapa baada ya hiyo comment.

"Asante sana Mose kwa kuniita nyani ila akae atambue anamkufuru Mungu kwa sababu ndio aliyeniumba kwa hiyo anavyonifananisha na nyani na mimi nafananishwa na Harmonize pia na Hamornize ni nyani kwa hiyo tuko nyani wawili." amorapa

Mose Iyobo kwa upande wake amesema: "Mimi sioni cha ajabu, kuna mtu anaitwa Simba na anafurahi, kuna mtu anajiita Dudu baya na anafurahi leo mtu kumuita mtu nyani yanakuja maneno mengi, wao wanatukana maneno mangapi na hujasikia nimeenda kusema sehemu"

==>Wasikilize Hapo Chini

Gazeti La Mwanahalisi Lapewa Saa 24 Liombe Radhi

Hatimaye Njia Ya Reli Kati Ya Dar Es Salaam Na Ruvu Yafunguliwa

$
0
0
Uongozi wa Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) umetoa taarifa kuwa kuanzia saa 9 alasiri leo Januari 30, 2017 njia ya reli kati ya Kituo Kikuu cha Dar es salaam na Ruvu imefunguliwa rasmi kwa shughuli za uendeshaji wa reli.

Taarifa hiyo imesema kuwa kazi ya ufunguaji njia imewezekana baada ya Wahandisi na Mafundi wa reli kuyaondoa Mabehewa yaliopata ajali  kutoka relini na pia kuikarabati sehemu iliyoharibika . Kazi hiyo imefanyika kuanzia usiku wa Januari 29, 2017 hadi mchana wa Januari 30, 2017.

Aidha treni ya abiria iliyoahirisha safari ya kuondoka kwenda bara jana imeondoka leo saa 9:05 alasiri kutoka kituo kikuu cha Dar es Salaam kwenda bara..

Wakati huo huo imefahamika kuwa msafiri mmoja aliyetambulikana kama Nd Basekena O. Bango kutoka Bujumbura Burundi akiwa anasafiri kutoka Kigoma amelazwa katika Hospitali ya Tumbi Kibaha mkoani wa Pwani kwa ajili ya matibabu zaidi. Aligunduliwa kuwa amechanika mguu wake wa kulia hivyo basi kuhitaji kushonwa mguu wake huo.

Taarifa kutoka Muhimbili zinaeleza kulazwa kwa majeruhi wawili waliopokelewa hospitalini hapo usiku wa Januari 29, 2017. Majeruhi wamefahamika kuwa ni Nd. Stephania Mbona (46) kutoka Kigoma alikuwa amekuja Muhimbili kuendelea na matibabu ya ugonjwa wa tumbo, hata hivyo alitibiwa majeraha ya kawaida na anaendelea kulazwa kwa ajili ya matibabu ya ugonjwa wake wa tumbo.

Mgonjwa wa pili Nd Alice Jovin (37) mkazi wa Salasala Dar es Salaam alikuwa anatoka Kigoma kuja Dar es Salaam amepata majeraha ya kawadia ametibiwa na alitarajiwa kuruhusiwa leo asubuhi.

Kuhusu idadi ya wasafiri treni ya Deluxe yenye uwezo wa kusafirisha abiria zaidi ya 1000 wakati inapata ajali ilikuwa na abiria 480.

Aidha imefahamika kuwa ili kufahamika hasara na sababu za ajali hiyo taarifa rasmi itatolewa baada ya uchunguzi wa Kamati maalum inayoundwa kwa mujibu wa sheria, taratibu na kanuni za uendeshaji reli za kimataifa. Taarifa hiyo itatolewa baada ya wiki mbili.

Imetolewa na Afisi ya Uhusiano:
Kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa TRL
Ndugu Masanja Kungu Kadogosa
Januari 30, 2017
DAR ES SALAAM

Waziri Mkuu Azitaka Halmashauri Zifanye Kazi Kwa Weledi

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassm Majaliwa amesema wakati umefika wa kuwa na watumishi wenye weledi wa kutosha kwenye Halmashauri zote nchini na pia hazitakiwi kuwa pango la wezi, wazembe au jalala la kutupa wabadhilifu walioshindikana kwingineko.

Aidha, Waziri Mkuu amesemma Serikali za Mitaa na Halmashauri zote nchini zinatakiwa zianze kujitathmini na kujipanga vizuri zaidi kuona ni kwa namna gani zitakuwa chachu ya maendeleo ya viwanda vinavyotarajiwa.

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo (Jumatatu, Januari 30, 2017) wakati akifungua Kikao cha Baraza la Mashauriano (RCC) mkoani Dodoma. Amesema kikao ni chombo muhimu na endapo kitatumika vizuri kitaweza kusaidia kusukuma maendeleo ya Mkoa na kupunguza migogoro kwenye Halmashauri.

Amesema Serikali itaendelea kuongeza kiwango cha ruzuku kwa Halmashauri zote nchini kwa kadiri uwezo utakavyoruhusu na kusisitiza kwamba fedha hizo lazima zisimamiwe vizuri na zielekezwe kwenye miradi ya maendeleo inayowagusa wananchi.

“Endapo itabainika kwamba kuna baadhi ya Sheria zinazokwamisha utendaji katika Mamlaka za Serikali za Mitaa, hatutasita kuzifanyia mapitio na hatimaye kuzibadili ili ziendane na azma yetu ya kutoa huduma bora kwa wananchi,” amesema.

Amesema Serikali ina maslahi makubwa kwa Serikali za Mitaa, sio tu kwa kuwa ni Serikali kamili katika ngazi hiyo, bali pia kutokana na ukweli kwamba kero nyingi za wananchi ziko katika ngazi hiyo.

Waziri Mkuu amesema vyanzo vingi vya mapato ya Serikali vinapatikana kwenye Halmashauri huku changamoto kubwa ikiwa ni kulegalega kwa  Halmashauri nyingi katika ukusanyaji wa mapato ya kodi na yasiyo ya kodi jambo linalozorotesha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Hivyo Waziri Mkuu ametoa rai kwa Halmashauri hizo kuendelea kuboresha huduma kwa wananchi na kutatua kero zao kikamilifu na kwa wakati pamoja na kubuni vyanzo vipya vya mapato na kuongeza kasi ya ukusanyaji wa mapato.

Pia zihakikishe malipo yote yanafanyika kwa njia za kielektoniki na zihamasishe vijana na akina mama wajiunge kwenye vikundi vya uzalishaji mali na kuwapatia stadi za kazi na mikopo yenye masharti nafuu ili waweze kuwa chanzo cha mapato hapo baadaye.

Amesema watendaji wa Halmashauri wanatakiwa  kujiepusha na vitendo vya rushwa na ubadhilifu wa mali za umma na uzembe kazini na watakaobainika kufanya vitendo hivyo  wachukuliwe hatua kali za kisheria na kinidhamu.

“Someni taarifa ya CAG (Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali) na kutoa majibu ya kina ya namna mtakavyodhibiti mianya ya rushwa na ubadhilifu kama ilivyoainishwa kwenye ripoti hizo,” amesema.

Hata hivyo amesema kila Halmashauri iandae mpango wa utekelezaji wa Ilani ya CCM kwenye maeneo makubwa ya kipaumbele kama vile ujenzi wa miundombinu ya shule,  maboresho kwenye sekta ya afya (ujenzi wa hospitali, zahanati na vituo vya afya).

“Endeleeni kuwa na mahusiano mazuri miongoni mwenu, mfanye kazi kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu.  Kila mmoja kwa nafasi aliyonayo atimize wajibu wake na kuzingatia mipaka ya nafasi yake. Punguzeni migogoro, matusi, dharau, bezo na vitisho. Mshirikiane na jamii ione mpo wamoja,” amesema.

Rais Magufuli Akutana Na Kufanya Mazungumzo Na Katibu Mkuu wa Umoja Wa Mataifa (UN)

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa(UN) Antonio Manuel Olveira Guterres katika Ofisi za  Makao Makuu ya Umoja wa Umoja wa Afrika (AU), Addis Ababa nchini Ethiopia.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa(UN) Antonio Manuel Olveira Guterres mara baada ya mazungumzo yao.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Rais wa Malawi Peter Mutharika kabla ya kuanza mazungumzo yao katika Ofisi za  Makao Makuu ya Umoja wa Umoja wa Afrika (AU), Addis Ababa nchini Ethiopia.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa ameshikana mikono na Rais wa Malawi Peter Mutharika pamoja na viongozi wengine mara baada ya kumaliza mazungumzo yao katika Ofisi za  Makao Makuu ya Umoja wa Umoja wa Afrika (AU), Addis Ababa nchini Ethiopia.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Rais wa Jamhuri ya Kiarabu ya Kidemokrasia ya Sahrawi(SADR) Brahim Ghali katika Ofisi za  Makao Makuu ya Umoja wa Umoja wa Afrika (AU), Addis Ababa nchini Ethiopia.

PICHA NA IKULU

Mkutano Wa 6 Wa Bunge Kuanza Kesho.....Wabunge 4 Kula Kiapo, Maswali 125 Kuulizwa Na 16 Ya Papo Kwa Papo Kwa Waziri Mkuu

$
0
0
Mkuu wa Kitengo cha Habari, Elimu na Masiliano Ofisi ya Bunge, Owen Mwandumbya akizungumza na wanahabi mjini Dodoma leo akitoa taarifa ya yale yatakayojiri katika Mkutano wa sita wa Bunge la 11 unaotaraji kuanza kesho Januari 31 hadi Februari 10 mwaka huu mjini Dodoma.

***************
Mkutano wa Sita wa Bunge unatarajiwa kuanza siku ya Jumanne tarehe 31 Januari 2017 na kumalizika tarehe 10 Februari 2017 Mjini Dodoma. 

Mkutano huo utakuwa ni mahususi kwa ajili ya kupokea Taarifa za mwaka za Kamati za Kudumu za Bunge ambapo Kamati 14 za kisekta na mtambuka zitawasilisha taarifa zake Bungeni katika kipindi hiki. Shughuli nyingine zitakazofanyika katika Mkutano huu ni kama ifuatavyo:-
 
1.0         KIAPO CHA UAMINIFU
Kufuatia uteuzi wa wabunge watatu walioteuliwa na Mhe. Rais Dk. John Pombe Magufuli hivi karibuni na Uchaguzi Mdogo uliofanyika katika Jimbo la Dimani, Zanzibar Tarehe 22 Januari 2017, kutakuwa na Kiapo cha Uaminifu kwa Wabunge wapya wanne ambao ni:-
(i)         Mhe. Alhaji Abdallah Majula Bulembo
(ii)       Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi
(iii)      Mhe. Anne Kilango Malecela
(iv)    Mhe. Ali Juma Ali - (Jimbo la Dimani)
 
2.0         MASWALI
Katika Mkutano huu jumla ya maswali ya kawaida 125 yanatarajiwa kuulizwa na kujibiwa Bungeni. Aidha, kwa mujibu wa Kanuni ya 38 (1) ya Kanuni za Kudumu za Bunge wastani wa maswali 16 ya papo kwa papo kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu yataulizwa na kujibiwa pia siku za Alhamisi. 
 
3.0       KAULI ZA MAWAZIRI
Aidha, katika Mkutano huu wa Bunge Kauli mbili za Mawaziri zitawasilishwa  kama ifuatavyo:-
(i)     Kauli ya Serikali Kuhusu Hali ya Chakula Nchini itakayotolewa Tarehe 31 Januari, 2017.
(ii)   Kauli ya Serikali kuhusu Deni la Taifa na Hali ya Uchumi Nchini itakayotolewa Tarehe 31 Januari, 2017.
 
4.0       MISWADA YA SHERIA
Katika Mkutano wa Tano wa Bunge uliomalizika mwezi Novemba, 2016 Miswada mitatu (3) ya Sheria ilisomwa  kwa mara ya Kwanza Bungeni na kupelekwa kwenye Kamati husika ili ifanyiwe kazi. 
 
Hivyo katika Mkutano huu wa Sita Miswada hiyo inatarajiwa kuwasilishwa Bungeni kwa mara ya Pili, kujadiliwa na kupitishwa na Bunge kwa mujibu wa Kanuni ya 91. Miswada hiyo ni:-
  1. Muswada wa Sheria ya Sheria ya Madaktari wa Meno na Wataalam wa Afya Shirikishi wa mwaka, 2016 (The Medical, Dential and Allied Health Professionals Bill 2016).
  2. Muswada wa Sheria ya Huduma ya Msaada wa Kisheria wa mwaka 2016 (The Legal Aid Bill, 2016).
  1. Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria mbalimbali (Na.4) wa mwaka 2016. {The Written Laws (Miscellaneous Amendments)}, Bill, 2016)
Imetolewa na:
Kitengo cha Habari, Elimu na Mawasiliano
Ofisi ya Bunge
DODOMA
30 Januari, 2017.

Rais wa Chad achaguliwa kuwa Mwenyekiti Mpya wa Umoja wa Afrika (AU)

$
0
0
Rais wa Guinea, Alpha Conde amechaguliwa leo kuwa Mwenyekiti mpya wa Umoja wa Afrika (AU), uchaguzi uliofanyika katika vikao vya viongozi wa nchi wanachama vinavyoendelea katika Makao Makuu ya umoja huo mjini Addis Ababa nchini Ethiopia.

Rais Conde anapokea uongozi kwa Rais wa Chad Idris Deby ambaye alikuwa ndiye kiongozi wa umoja wa hadi.

Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika ni kiongozi asiye na maamuzi (ceremonial head of the Union). Mwenyekiti huyu huchaguliwa  na Marais wa Nchi wanachama wa AU ambaye hushika wadhifa huo kwa mwaka mmoja tu. Uongozi huu huenda wa zamu katika Kanda tano za bara la Afrika (Kaskazini, Kusini, Mashariki, Magharibi, na Afrika ya Kati).

Nafasi hii ilianzishwa mwaka 2002 ambayo Rais Mstaafu wa Afrika Kusini, Thabo Mbeki ndiye alikuwa mwenyekiti wa kwanza.

Rais wa Chad,  Idriss Deby (kushoto) akikabidhi madaraka kwa Mwenyekiti mpya wa Umoja wa Afrika, Rais Alpha Conde wa Guinea (kulia).

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya January 31

Wanafunzi 10 Waliofanya Vizuri Zaidi Kitaifa Katika Matokeo Ya Kidato cha Nne 2016

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images