MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA
“LUKASSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSS…………………………………………..!!!!”
Askari huyo alipiga ukelele wa maumivu na uchungu baada ya kumshudia mwenzake huyo akikata roho, yeye akiwa gorofani, kelele hizo zikawafanya askari wangine walio kuwa wakiwa huduma ya kwanza wezo kukimbilia alipo mwenzao. Agnes akatabasamu kwa dharau kisha akamnyooshea kidole cha kati askari huyo anaye lia kwa uchungu kisha akaondoka zake kwa kujiamini sana.
ENDELEA
Agnes akaanza kushuka chini kwa kutumia ngazi katioka gorofa aliyo ingia huku mara kwa mara akifanya mawasiliano na Jaquline ambaye aliamua kusitisha zoaezi la kumteka raisi, akatoka nje, gari aliyo kuja nayo ikamchukua na moja kwa moja akaelekea sehemu ambayo Agnes alimuelekeza
***
Hadi kuna pambazuka Eddy, hakuweza kupata hata lepe la usingizi, akanyanyuka kwenye kiti alicho kuwa amekaa usiku kucha, akatoka nje na moja kwa moja akaelekea kwenye makaburi ya familia yeka. Akasimama kwa dakika kadhaa akiyatazama makaburi hayo, hakuamini kwamba ni kweli familia yake imeweza kupotea gafla na kubaki akiwa peke yake, kila alipo mfikiria mzee Godwin machozi ya hasira na uchungu ndivyo yalivyo zidi kumwagika. Akastukia akishikwa mkono wake wa kushoto taratibu akaigeuza shingo yake na kumkuta Shamsa akiwa amesimama pembeni yake huku naye akionekana kuwa na huzuni nyingi sana usoni mwake.
“Madam Mery ameondoka”
Shamsa alizungumza kwa sauti ya unyonge huku macho yake akiwa ameyaelekezea kwenye makaburi hayo matatu
“Amekwenda wapi?”
“Hakuniambia ni wapi alipo kwenda”
“Achana naye”
“Ila baba, kuna mambo mengi muhimu amaniambia nikuambia”
“Mambo gani?”
Eddy alizungumza huku akimtazama Shamsa usoni aliye onekena kusita kwa kile ambacho anahitaji kwenda kukizungumza mbele ya Eddy anaye mchukulia kama baba yake mlezi.
“Mbona umekaa kimya huwezi kuzungumza?”
“Ni ni kuhusiana na baba yako?”
“Baba yangu……!!”
“Ndio mzee Godwin”
Eddy akatazama kila kona, akamshika mkono Shamsa, wakatafuta sehemu iliyo tulia kwenye moja ya bustani zilizopo ndani ya njumba lake la kifahari.
“Alikuambia kuhusiana na nini?”
“Jana usikua alinieleza kila kitu kuhusiana na kikundi cha D.F.E. Hicho ni kikundi ambacho kimeanzishwa na mzee Godwin mwenyewe, kazi yake kubwa ni kuhakikisha kwamba wanalipiza visasi kwa wale wote ambao waliweza kuwatemndea ubaya katika maisha yao.”
“Aliniambia kwamba hicho ni kikundi kikubwa sana na kina wafuasi wengi ambao wengine wamo ndani ya serikali yetu ya Tanzania, na anashirikiana nao”
“Amekutajia majina?”
“Hapana hajanitajia majina. Ila anadai wafuasi hao ni watu wakubwa sana serikalini, si Tanzania pekee bali nchi nyingi za Afrika pamoja na nchi za Amerika, ikiwemo Marekani”
Shamsa akanyamaza kimya kidogo kisha akaendelea kuzungumza kwa umakini kile alicho ambiwa kukizungumza kutoka kwa madam Mery ambaye alihofia kufanya hilo.
“Watu hao wana chata ndogo kwenye sehemu za miili yao, yenye maandishia meusi D.F.E. Ameneniambia kwamba msaidizi wa mambo yote ya kikundi hicho ni mtu ambaye anakujua vizuri kuanzia A hadi Z, ukimuachilia kiongozoi wao mzee Godwin”
“Ni nani huyo?”
“Alinitajia kwa jina moja tu……..JONH”
Eddy akatumbua macho yake huku akimtzama Shamsa, akiwa haamini kitui alicho kizungumza kwani kumbukumbu ya mwisho anakumbuka jinsi alivyo vikata viungo vya John kwa kulipiza kisasi cha mambo yote aliyo mfanyia.
“JOHN…..JOHN…….!!!”
“Ndio huyo huyo John, pia ameniambia mtu wa kwanza kuweza kulengwa katika mikakati yao ni wewe, wanataka kukuangusha chini, ten echini kabisa ya aridhi”
Eddy akajikuta akishusha pumzi nyingi, woga wa gafla ukamuingia moyoni mwake, kajasho kembamba kakaanza kumwagika kwani hakujua ni jinsi gani ambavyo wanaweza kumuangusha.
“Ahaa….aaaa aahaame ame kwenda wapi Madam Mery?”
“Hakuaniambia ni wapi anapo elekea kwa sasa, ila kitu kingine cha mwisho alicho niambia nikuambia ni kwamba, ujiudhuru nafasi yako hiyo ya uongozi kwani ni rahisi kwa wao kuweza kukupata, pili kati ya watu ambao unafanya nao kazi serikalini wana kisasi na wewe, ikiwemo wale ambao uliwaharibia biashara zao kipindi ambapo iliingia madarakani, wana uchungu na kisasi kikubwa juu yako”
Eddy akahisi kichwa chake kinapasuka kwa maumivu makali ambayo anayapata kwa taarifa hiyo ambayo si nzuri kwa upande wake. Taratibu akanyanyuka kwenye kiti alicho kaa na moja kwa moja akaelekea ndani kwake. Akafungua kabati lake lenye baadhi ya vitu muhimu, akatoa kikopo kidogo chenye dawa za kutuliza mawazo, akatoa vidogo kadhaa na kuvimeza, pasipo kutumia maji, kisha akajitupa kitandani.
“Kwa nini kila kitu kinanitokea mimi tuuuuuuuuuuuuu”
Eddy alizungumza kwa sauti ya ukali iliyo jaaa jasira na uchungu ndani yake, akiwa katika kuhangaika hangaika kitandani kujaribu kuutafuta japo usingizi, mlango wake ukagongwa mara mbili.
“Nani?”
Mlango ukafunguliwa pasipo mtu huyo kujibu, Eddy akamkuta Rahab akiwa amesimama mlangoni peke yake, Rahab akapiga hatua moja mbela na kuufunga mlango kwa ndani.
“Umefwata nini huku ndani?”
Eddy alizungumza huku akishuka kitandani
“Nimekuja nahitaji kuzungumza na wewe?”
Rahab alizungumza huku akipiga hatua kadhaa kumfwata Eddy kitandani
“Twende tukazungumzie nje ila si ndani ya chumba ninacho lala na mke wangu”
Eddy alizungumza kwa ukali kidogo, hakujali Rahab ni mke wa raisi au laa, kabla Eddy hajafika mlangoni Rahab akamuita na kumfanya Eddy kugeuka na kutazama ni kitu gani ambacho Rahab anamuitia.
“Eddy ninakupenda?”
“Upo sawa wewe?”
“Ndio nipo sawa, na ninacho kizungumza ni kitu kitokacho moyoni mwangu”
Rahaba akapiga hatua kadhaa hadi alipo simama, wakatazama kwa muda, kitendo ambacho kikaanza kumfan ya Rahab kumwagikwa na machozi.
“Eddy nipo tayari kuacha kila kitu kwenye maisha yangu, ili niwe na wewe. Wewe ni mwanaume wa kwanza katika haya maisha yangu kukupenda, ni mwauaume abaye umeweza kuziteka hisia zangu tangu siku ya kwanza nilipo kuona picha yake nyumbani kwa mama yako”
“Eddy nimekuwa mtumwa kuanzia siku hiyo nimekuwa ni mtu wa kuishi na majuto ya kwanini niliamua kuolewa na Praygod, ambaye si chagua la moyo wangu”
***
Wasiwasi mwingi ukaanza kumtawala Raisi Praygod, kila alipo jaribu kuipiga simu ya mke wake, inaita hadi kukata, akamuita mlinzi wake mmoja anaye muamini sana.
“Mama yupo wapi?”
“Ametoka kama dakika kumi zilizo pita hivi”
“Ameenda wapi?”
“Hakuniambia, ila ngoja kwanza nimpigie dereva wake”
Kijana huyo akatoa simu yake mfukoni na kumpigia dereva wa madam Rahab, simu ikaita baada ya muda ikapokelewa
“Upo wapi?”
“Nipo nyumbani kwa muheshimiwa Eddy”
“Upo na madam?”
“Ndio, ameingia ndani?”
“Mlinzi wake yupo wapi?”
“Yupo nje ya gari, kwani vipi?”
“Ahahaa hakuna kitu”
Kijana huyo akakata simu, na kumtazama raisi Praygod anaye onekena kujawa na wasiwasi kwani si kawaidia ya mke wake kuto kupoke simu kwa kipindi kirefu.
“Yupo kwa waziri wa ulinzi bwana Eddy Godwin”
‘Eddy Eddy’
Wivu wa mapenzi ukaanza kuusumbua moyo wa raisi Praygod, kila alipo jaribu kuvuta baadhi ya kumbukumbu, siku jinsi alivyo wakuta Eddy na mke wake kwenye chumba cha waziri huyo kijana mdogo, alihisi kitu kilicho kuwa kikiendelea ila hakuweza kukiweka kichwani mwake akiamini kwamba ni jambo la kawaida.
‘Kwanini leo tena aende kama walisha maliza kuzungumza jana?’
Raisi Pryagod alijiuliza tena kichwani mwake swali ambali jibu lake likajaa wasiwasi mwingi, akakumbuka kitu kimoja kilicho mstua, wakati Rahab anamueleza anakwenda kuonana na Eddy kwenye chumba chake, rangi ya mdomoni mwake, ilikuwa imekolea vizuri tu. Ila alipo ingia na kuwakuta rangi hiyo ya mdomoni haikuwa kama vile alivyo ingia nayo.
‘Au alimkiss mke wangu kilazima?’
Hapo ndipo raisi Praygod akahisi kuna kitu ambacho kinaendelea kwa watu wawili hao, asira na uchungu mkali ukampanda moyoni mwake.
“Andaa ndege nahitaji Eddy na mwanae aliye baki wapelekwe mbali na Tanzania”
“Sawa muheshima na tuwapeleke wapi?”
“Popote ila mbali na Tanzania, na hii taarifa umpelekee baada ya kila kitu kuwa sawa”
“Sawa muheshimiwa”
“Ila Lube, hakikisha kwamba hili jambo umuelezi mke wangu, iwe siri yako mimi na wewe”
“Sawa muheshimiwa”
“Pia hakikisha unawafwatilia hatua moja hadi nyingine, na kila kinacho endelea hakikisha kwamba unaniambia”
Raisi Praygod akajikuta akiachia tusi zito, lililo jaa hasira, akihisi hali ya mahusiano kati ya Eddy na Rahab
“Nitakuuaa wewe mshezi Eddy”
***
Madam Mery akiwa ndani ya basi la Ngorika liendalo mkoani Arusha, mawazo mengi yakamtawala moyoni mwake, kila alipo jaribu kufikiria mambo aliyo mfanyia Eddy, roho yake ilizidi kumuuma sana hadi wakati wingine akatamani kufa kwani hastahili kabisa kuwa binadamu anaye paswa kusamehewa.
Akaanza kukumbuka jinsi mahusiano mazuri yaliyo kuwepo kati yake na Mzee Godwin, kipindi alipo mleta Eddy shuleni kwake kumuanzisha kidato cha tano. Ni siku ambayo mzee Godwin aliweza kumkabidhi Eddy kwake awe anamtzama kwa kila kitu na hata baadhi ya pesa ya matumizi ya Eddy aliweza kumuachia endapo Eddy ataishiwa na pesa iwe rahisi kumsaidia.
Uchshi, ukaribu na uzuri wa Eddy, ndivyo vitu ambavyo vilimkosesha ujasiri na ustahimilivu wa kuzuia hisia zake za mapenzi juu ya Eddy. Kitu kilicho muumiza akili ni jinsi gani ambavyo angeweza kumuanza Eddy katika swala zima la mahusiano isitoshe yeye alikuwa ni mwalimu wake.
Siku ambayo aliweza kumkuta Eddy chumbani kwake akiwa ameshika mdoli wake ulio kaa kama jinsia ya mwaume, alio kuwa akiutumia katika kujichua pale hamu, zinapo mzidi, ndipo ikawa nafasi yake ya kuweza kufanya kila kitu kwa ajili ya kumpata kijana huyo aliye tokea kuutesa moyo wake.