Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Zitto Kabwe Asakwa na Jeshi la Polisi kwa Uchochezi.....ACT Wazalendo Wadai Yuko Salama, Wataka Polisi Wafuate Utaratibu

0
0
Naibu Katibu Mkuu wa ACT Wazalendo ndugu Msafiri A Mtemelwa ametoa taarifa kuwa kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo Mh Zitto Kabwe hajakamatwa na polisi na kusema yupo salama hapa hapa nchini.

Akitumia mtandao wa twitter wa Chama cha ACT Wazalendo Msafiri Mtemelwa anadai kuwa kiongozi huyo wa chama yupo salama lakini dereva wake ndg Patrick Muhidin pamoja na katibu wa Chama wa jimbo la Kahama ndg. Vincent Ikerenge ndio walikamatwa na walipelekwa kituo cha polisi Kahama na kuandikishwa maelezo.

"Tunawajulisha kuwa kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo ndg. Zitto Kabwe, Mb hajakamatwa na polisi na yupo salama hapa hapa nchini. Tarehe 21/1/2017 Polisi wilayani Kahama wakiwa na magari 7 kati yao manne ya FFU walivamia mkutano wa Kampeni wa Chama katika kata ya Isagehe, Halmashauri ya Mji wa Kahama. Kiongozi wa Chama alikuwa jukwaani wakati polisi wanafika na aliendelea na hotuba yake mpaka mwisho na kumnadi Mgombea ndg Ibrahim Masele. Baada ya kushuka jukwaani, Kama kawaida yake alipeana mikono na wananchi na baadaye alipotea katika eneo Hilo" alisema Msafiri Mtemelwa

Kwa mujibu wa Naibu Katibu Mkuu wa ACT Wazalendo ndugu Msafiri Mtemelwa anadai wamefuatilia polisi kutaka kujua kwanini kiongozi wa Chama chao anatafutwa na polisi na kusema wamejulishwa kuwa ana mashatka ya kutoa lugha ya uchochezi katika hotuba zake za kampeni.

"Tumejulishwa na polisi kwamba Kiongozi wa Chama  ana mashtaka ya kutoa lugha ya uchochezi katika hotuba zake za kampeni katika kata ya Isagehe Jimbo la Kahama Mjini. Polisi wanasema Zitto Kabwe amemchonganisha Rais na wananchi kwa kusema kuwa Rais anakula bure na kulala bure ndio maana hajali hali ngumu ya maisha ya wananchi wakati huu wa balaa la njaa" ameandika Mtemelwa

Hata hivyo mbunge huyo wa Kigoma mjini na kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo kupitia viongozi wa chama cha ACT Wazalendo amesema polisi wataweza kumkamata iwapo yeye atataka kukamatwa na siyo kwa kuvamiwa bali kwa kuitwa rasmi na polisi na kuelezwa makosa yake.

"Chama kinalitaka jeshi la polisi kufuata taratibu za kukamata raia kwa mujibu wa sheria na pia protokali za kuwaita polisi viongozi wa Kitaifa Kama ilivyo kwa ndg Zitto. Chama kinajiandaa na wanasheria wake ili kwenda na KC kituo chochote cha polisi nchini Mara watakapopata wito wa kwenda polisi.". Amesema Msafiri Mtemelwa

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu Ya January 23

Tazama Gari la kifahari la Yahya Jammeh lenye thamani ya TZS milioni 800.....Inadaiwa Kakomba Fedha zote kabla ya Kuondoka

0
0

Yahya Jammeh aliyeitawala Gambia kwa miaka 22, hatimaye jana aliondoka nchini humo na kwenda kuishi uhamishoni baada ya kushindwa katika uchaguzi mkuu wa Disemba Mosi mwaka jana.

Jammeh alishindwa na kiongozi aliyekuwa akiungwa mkono na vyama vya upinzani, Adama Barrow ambaye amekuwa akiishi nchni Senegal alipoapishwa kuwa Rais wa Gambia baada ya Jammeh kukataa kutoka madarakani awali.

Yahya Jammeh alipokuwa akiiongoza Gambia aliweza kujinunulia vitu vingi vya kifahari na moja wapo ni gari lake la kifahari aina ya Rolls Royce.

Gari hili ambalo kwenye viti vyake ameandika jina lake, lina thamani ya kati ya fedha za kitanzania milioni 500 hadi milioni 800. Rolls Royce ni moja ya magari ya kifahari na ya kipekee duniani ambayo mara nyingi hutumiwa na watu wenye uwezo mkubwa kifedha.

Gari hili la Yahya Jammeh liliwashangaza rais wengi wa Gambia lilipokuwa likikatisha katika viunga vya mji wa Banjul kumpeleka kiongozi huyo uwanja wa ndege tayari kuondoka nchini humo.

Licha ya kuwa Jammeh aliondoka nchini Gambia jana huku wananchi wakishangilia kwa furaha, imeelezwa kuwa kiongozi huyo alikomba fedha katika hazina ya nchini hiyo na kuiacha katika ukata mkubwa wa fedha.

Taarifa kutoka katika kambi ya Rais Adama Barrow zinaeleza kuwa dola za kimarekani milioni 11 zilichukuliwa katika hazina ya nchi hiyo.

Yahya Jammeh tayari amewasili nchini Equatorial Guinea ambapo ndipo ataishi.

Hapa chini ni picha zaidi za gari hilo la kifahari;

Hapa ni sehemu ya magari ya Yahya Jammeh yaliyopo uwanja wa ndege wa Banjul Gambia, baada ya ndege toka Guinea kuzuiliwa kuyachukua.

Profesa Lipumba Anusurika Kupigwa na Vijana wa UKAWA

0
0
Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi (CUF) anayetambuliwa na Msajili wa Vyama vya Siasa, Profesa Ibrahim Lipumba amenusurika kupigwa na vijana wanaoaminika kuwa ni wa Ukawa wakati akitoka kwenye mkutano wa kampeni mjini Morogoro.

Katika vurugu zilizotokea juzi jioni wakati vijana wa Ukawa na kikundi cha ulinzi cha CUF (blue guard) cha Dar es Salaam wakiwa na Profesa  Lipumba walikuwa wakitoka kwenye mikutano ya kampeni maeneo tofauti walipokutana barabarani na kuanza kurushiana maneno na hatimaye kupigana.

Katika vurugu hizo, vijana wa Ukawa waliwazidi wenzao wa blue guard na Profesa Lipumba kulazimika kukimbilia kwenye Msikiti wa Mungu Mmoja Dini Moja ili kujinusuru.

Ghasia hizo zilidumu kwa takribani saa moja na nusu ambapo baada ya Profesa Lipumba kukimbilia msikitini hapo, wafuasi wa Ukawa walibaki nje mpaka polisi walipofika na kuwatawanya.

Akizungumzia tukio hilo, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Leonce Rwegasira alikiri kutokea kwa vurugu hizo ambapo alisema wafuasi watatu wa CUF walijeruhiwa.

Alisema kuwa polisi wanaendelea na uchunguzi ili kuwabaini walioanzisha vurugu hizo ikiwa ni pamoja na kuweka doria kali katika mikutano ya vyama vya siasa.

Profesa Lipumba hakupatikana jana kuzungumzia suala hilo, baada ya simu yake kutokuwa hewani jana

CCM yashinda ubunge Dimani Zanzibar, yaiacha mbali CHADEMA matokeo ya Udiwani

0
0
Chama cha Mapinduzi (CCM) kimeibuka na ushindi katika uchaguzi mdogo wa ubunge jimbo la Dimani, Zanzibar huku wakijizolea Kata nyingi za udiwani na kuwaacha mbali UKAWA.

CCM iliibuka na ushindi jimboni hapo baada ya mgombea wake Juma Ali Juma kupata kura 4,860 dhidi ya mpinzani wake wa UKAWA, Abdulrazak Khatib Ramadhani aliyejizolea kura 1,234.
Kwa upande wa UKAWA wamelalamikia uchaguzi huo wakisema kuwa uligubikwa na udanganyifu mkubwa kwani hata majina ya marehemu yalitumika kupigishwa kura.

Mgombe huyo wa CUF alisema kuwa dada yake ambaye amefariki tangu Januari 15 naye jina lake lilitumia katika kupigisha kura.

Jimbo hili la Dimani lilikuwa wazi baada ya aliyekuwa mbunge wake, Hafidh Ally Tahri (CCM) kufariki Novemba mwaka jana akipatiwa matibabu mjini Dodoma.

Kwa matokeo ya Kata 13 yaliyokuwa yametolewa hadi leo asubuhi, CCM ilikuwa imeshinda udiwani katika Kata 12 huku CHADEMA ikiambulia Kata 1

Rais Mstaafu Jakaya Kikwete akutana na Mabilionea, Aliko Dangote na Bill Gates

0
0
Rais wa awamu ya nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Jakaya Mrisho Kikwete amepata nafasi ya kukutana na mabilionea wawili wakubwa duniani akiwa ziarani Davos nchini Uswisi.

Dr. JK ameshiriki katika uzinduzi wa baraza la kutokomeza Malaria Duniani (End Malaria Council) uliofanyika tarehe 19 January 2017 huko Davos Uswisi ambapo baraza la kutokomeza Malaria linaundwa na Wajumbe 9 ambao ni watu mashuhuri katika sekta ya umma na sekta binafsi duniani na orodha yenyewe ya Wajumbe ndio hii hapa chini

1. Bill Gates – Mwanzilishi na mmiliki wa Bill Gates Foundation
2. Ray Chambers – Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Malaria
3. Peter Chermin –Mwanzilishi wa Chermin  Entertainment na Chermin Group
4. Aliko Dangote – Rais na Mtendaji Mkuu wa Dangote Group
5. Idrisa Deby –Rais wa Chad kwa nafasi yake ya Mwenyekiti wa Taasisi ya ALMA
6. Jakaya Kikwete –Rais Mstaafu wa Tanzania
7. Graca Machel – Mwanzilishi wa Foundation for Community Development,Msumbiji
8. Luis Alberto Moreno –Rais wa Inter-American Development Bank
9. Ellen Johnson Sirleaf – Rais wa Liberia.


Rais mstaafu Jakaya Kikwete akisalimiana na Bill Gates ambaye mpaka January 2017 jina lake limetajwa kuwa ndio anashika namba 1 kwa utajiri duniani

Lengo la Baraza hilo ni kuunganisha nguvu za wadau na mataifa duniani kukabiliana na hatimaye kutokomeza kabisa ugonjwa wa Malaria ifikapo mwaka 2030 ambapo kuanzishwa kwa Baraza hilo kumetokana na mafanikio makubwa yaliyopatikana katika vita dhidi ya malaria katika miaka 15 iliyopita.

Katika kikao chake cha kwanza kilichofanyika Davos, Baraza hilo limejadili kuhusu upatikanaji wa rasilimali za kutosha za kuwezesha kutoa msukumo katika upatikanaji wa vifaa tiba, dawa, tafiti na uvumbuzi wa mbinu na nyenzo za kisasa za kuzuia, kupambana na hatimaye kutokomeza ugonjwa wa Malaria katika nchi za Afrika, Asia na Amerika ya Kusini.


Jakaya Kikwete na  Ray Chambers na Bill Gates
Akizungumza mara baada ya uzinduzi wa Baraza hilo, Rais Mstaafu Jakaya Kikwete, ambaye utotoni kwake alipoteza kaka yake kwa ugonjwa wa  Malaria pamoja na ndugu wengine wengi katika maisha yake amesema, ” Kutokomeza Malaria iliwahi kuwa ndoto isiyotekeleza, lakini sasa kuifikia ndoto hiyo ni dhahiri…..tunawea kuifanya Malaria kuwa historia na kuutokomeza ugonjwa huu katili katika uso wa dunia”.

Tanzania ni moja ya nchi zinazosifika barani Afrika na duniani kwa kuweza kupiga hatua kubwa katika kutokomeza ugonjwa wa Malaria. Katika kipindi cha miaka 10 iliyopita, takwimu zinaonyesha kuwa maambukizi ya malaria yamepungua kwa asilimia 70 na vifo vimepungua kwa asilimia 50.

SORRY MADAM -Sehemu ya 21 & 22 (Destination of my enemies)

0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA

ILIPOISHIA  
Kwa haraka Shamsa akalichukua faili na kulifungua mbele ya askari huyo hata kabla hajaondoka. Shamsa akastuka kukuta picha ya msichana ambaye alisha wahi kumuona sehemu ila kumbukumbu zake hazikumbuki ni sehemu gani ambayo aliweza kumuona. Shamsa akajikuta akiusukuma mlango na kuingia dani ya chumba hicho. Akamkuta Madam Mery akiwa amepiga magoti, wote wakamtazama Shamsa ambaye ameingia gafla,
“Dady huyu ndio aliye muua Junio”
Eddy kusikia taarifa hiyo, akastuka, kwa haraka akalichukua faili hilo na kulifunua, kitu alicho kiona picha ya Manka pamoja na jina lake pembeni.
“MANKA……..!!!! MANKA SI ALIKUFA…….??.”
  
ENDELEA
“Manka………!!!”
Madam Mery alizungumza huku akinyanyanyuka, Eddy na Shamsa wote wakamgeukia na kumshangaa.

“Hembu nione”
Madam Mery akachukua faili alilo lishika Eddy, macho yakamzidi kumtoka huku akimtazama Manka kwenye picha,
“Unamfahamu huyo?”
Eddy aliuliza huku akimtazama Madam Mery ambaye anaonekana kuwa na wasiwasi mkubwa sana. Madam Merya akajibu kwa kutingissha kichwa akionekana kumfahamu Manka.
“Hakufa”
Madam Mery alizungumza huku akimtazama Eddy usuoni kwa macho ya wasiwasi mwingi.
“Una maana gani?”
                                                                                              ***
“Ila Eddy ni chanzo cha mume mume wangu kufa”
Manka alizungumza huku akimtazama Mzee Godwin.
“Kwani, kwani uliolewa?”
“Hapana baba, ila nilikuwa na mwanaume ambaye nilimpenda sana, na alikuwa anafanana sana na Eddy”
“Nilimpenda sana yule mwanume, nakumbuka Eddy aliamua kumpa mume wangu kazi ya kwenda kumuoa Sheila aliye kuwa ni mpenzi wake, ila haikuwa hivyo kwani siku ya harusi yao ndipo walipo vamiwa na mume wangu kutekwa na kuuawa”

Maneno ya Manka yakamkumbusha Mzee Godwin, tukio ambalo yeye ndio alikuwa ni muhusika mkuu katika kupanga mpango mzima wa kuweza kumteka Eddy kwenye harusi yake yeye pamoja na mke wake. Huku akimtumia John kuweza kukamilisha mipango yote hiyo. Ila kitu ambacho kilimchanganya Mzee Godwin ni siku alipo gundua kwamba mtu waliye weza kumuu si Eddy, ila swali lililo muumiza sana kichwani mwake kijana huyo ni nani, na ametoka wapi. Leo ndio anapata jibu kamili kwamba yeye ndio muhusika mkuu wa kifo cha mpenzi wa mwanae kipenzi Manka.

Mzee Godwin taratibu akamvuta Manka hadi kifuani mwake na kumkumbatia taratibu, akaanza kumbembeleza ili asimwagikwe na machozi.
“Hatuna jinsi ya kufanya mwangu, tambua ninatafutwa ina bidi niweze kurudi makao makuu haraka iwezekanavyo”
“Makao makuu?”

“Ndio makao makuu ya kikosi changu cha DFE(Destination of my enemies)”
“Sawa, ila kuna Madam Mery yupo wapi?”
Mzee Godwin akamtazama Tom, kisha akamgeukia Manka. Kwa jinsi macho yam zee Godwin yanavyo oenekana Manka tayari akagundua kuna kitu cha tofauti kinacho endelea baina ya Mzee Godwin na Madam Mery, ambaye alisha tambulishwa na baba yake kama mama yake mdogo.
“Kuna kazi nahitaji nikupe kabla hatujaondoka”

“Sawa baba”
“Tom, huyu ni Manka ni dada yako, kuanzia hivi sasa. Jiandaeni kwa kuondoka”
Tom na Mzee Godwin wakaingia kwenye chumba amacho kimehifadhiwa pesa nyingi, wakaanza kuvikusanya vibunda vya pesa  na kuviweka kwenye mabegi yaliyo kuwa na nguo. Manka akaanza kupitia pitai vitu ambayo vipo kwenye computer ambayo baba yake alikuwa anafwatilia baadhi ya kesi ikiwemo ya kwake, hapo ndipo akakutana na sura ya binti ambaye, anakumbuka alisha wahi kuwa rafiki yake enzi za utoto.

“Huyu si Fetty?”
Manka alijiuliza huku akiendelea kuiangali picha ya Fetty, akasoma maelezo ya msichana huyo na kukuta habari ambayo ilimshangaza sana.
“Fetty ni gaidi?”
Mzee Godwin na Tom wakamaliza kukusanya pesa hizo, kisha wakaanza kuchukua baadhi ya silaha ambazo Tom hakujua kazi yake ni nini.

“Babu hizi za kazi gani?”
“Ni kwaajili ya kujilinda unaweza kutumia?”
“Hapana, nimezoea kuona kwenye video, wakina Van dame, kina Rambo wakizitumia”
“Je unahitaji kujua kuzitumia?”
“Ndio”
Tom alijibu kwa shahuku kubwa akionekana anahitaji kufahamu kutumia bunduki, jambo lililo mfanya mzee Godwin kuachia tabasam pana. Wakatoka na kumkuta Manka akiendelea kuwa bize akisoma historia ya wasichana waliopo kundi moja na Fetty wanao sadikika kuwa chini ya mikono ya serikali ya kimarekani.

  **
       Ni usiku ulio tawala shamra shamra nyingi katika ikulu ya Marekani ijulikana Whaite house, ulinzi mkali umeimarishwa kwenye kila kona ya eneo zima la ikulu. Wageni rasmi kutoka maeneo mbali mbali ya nchi ya Marekani na hata nje ya nchi ya Marekani wameudhuria, katika sherehe ya kuzaliwa kwa raisi Markn Tosh.

“Nimefika”
Sauti ya Jaquline ilisikika kwenye sikio la Agnes kupitia kifaa, maalumu alicho kifaa kwenye sikio lake, Agnes kwa kutumia mitambo maalumu ya Satelaite, anaweza kumuona Jaquline kila sehemu anapo pita, akitumia gari ndogo ya kifahari anai ya Ferrari Spider. Kwa kutumia kadi maalumu ya mualiko waliyo ipata kwa binti mmoja anaye fanya kazi ndani ya ikulu hiyo, aliweza kuionyesha kwa walinzi wanao kagua kadi ya kila mmoja anaye katika katika eneo hilo.
Wakamtazama Jaquline kwenye computer kama ni miongoni mwa waalikwa, kwa bahati nzuri wakamkuta ni mualikwa mmoja wapo.

“Welcome miss”
“Thank you”
Baada ya kumkagua, taratibu Jaquline akanza kupiga hatua kuelekea ndani ya ukumbi, wa ikulu. Macho ya Jaquline yakakutana na macho ya Lidya, binti aliye weza kuwasaidia katika kuingia katika sherehe hiyo, huku wakiwa wamemshirikisha katika mpango wao mzima wa kumteka raisi.

Lidya ni binti wa kikorea aliye kulia Marekani tangu akiwa na umri wa miaka sita, baba yake Mr Jang Woo, aliweza kuhamishiwa kikazi nchini Marekani, kama mpelelezi kwenye kitengo cha CIA. Jambo lililo mlazimu kuweza kuhamia na binti yake Lidya, aliye mbadili jina kutoka katika Jang Woo hadi Lidya, hii ni kutokana na sababu za kimsingi alizo weza kuziona ni muhimu kwa yeye kufanya hivyo ili binti yake kuweza kuwa salama.

Lidya akiwa katika umri wa miaka kumi na mbili, baba yake aliweza kupoteza maisha kwenye shambulizi la kigaidi la kulipuliwa kwa magorofa ya kiuchumi ya Marekani yaitwayo Twin Tower, na gaidi la kimataifa Osama bin Laden. Kuanzia hapo, Lidya akaanza kulelewa chini ya uangalizi wa serikali ya kimarekani katika kikosi cha CIA(Central Intrligrnce Agency).

Katika kukua kwake, wakiwa katika mafunzo ya ujasusi nchini Russia ndipo, alipo weza kukutana na Jaquline aliye muokoa kwenye ajali ya bomu lililo tegwa kwenye gari lao na magaidi walio tumwa na bwana Rusev, Jaquline akiwa ni miongoni mwa magaidi hao, ila aliweza kufanya hivyo kutokana na kutokea kumuoenea hurua binti huyo mdogo kuangamia katika kifo hicho.

Kuanzia hapo Lidya akatokea kumpenda sana Jaquline na kumuheshimu kama dada yake.
Jaquline akajichanganya na wageni wengine, huku akifwata maelekezo kutoka kwa Agnes, aliye muacha hotelini akitumia laptop yake kuweza kuona kamera zote za ikulu hiyo zinavyo fanya kazi, hii ni baada ya kupewa namba maalumu(Code) na Lidya zinazo tumia na askari walipo chumba maalimu cha ulinzi.

“Jiweke karibu na raisi”
Agnes alimpa maelekezo Jaquline naye akafanya hivyo, muda wote watu wakiwa wanaendelea kupiga stori za hapa na pale, ndivyo jinsi Jaquline alivyo zidi kuendelea kuwasoma walinzi wote walipo kwenye ukumbi huo.

 Wakati huo huo, askari mmoja akaanza kumtilia mashaka Jaquline, kwani muda wote Jaquline yupo peke yake, hana mtu wa kuzungumza naye. Askari huyo ambaye ni miongoni mwa askari wanao mlinda raisi moja kwa moja akaelekea chumba cha ulinzi, ili kufwatilia taafa muhimu za binti huyo kwani kila mgeni aliye ingia ndani ya ukumbi huo ana taarifa muhimu zinazo julikana na ikulu, na endapo kutajitokeza tatizo lolote basi, kukamatwa kwake ni rahisi.

“Mvute karibu huyo binti”
Askari huyo alimuamuru mmoja wa mafundi mitambo waliomo kwenye chumba hicho cha ulinzi kilicho jaa computer nyingi, za kisasa na zenye uwezo wa hali ya juu katika matumizi yake.
“Tafuta taarifa muhimu za huyu binti”
Kijana huyo mwenye utaalamu wa mkubwa katika maswala ya coputer, akaanza kufanya kazi aliyo agizwa. Kila kilicho anza kufanyika, Agnes aliweza kukiona, kwenye laptop yake, jinsi askari huyo wanavyo jaribu kutafuta taarifa za Jaquline.
“Jina lake ni Livna Livba, uraia ni Senegal, ni mfanya biashara mkubwa”

Kija huyo alimjibu askari huyo, kwani Lidya yeye ndiye aliye weza kuandika taarifa hizo za uaongo na kuzituma kwenye mtandao, na endapo kutatokea kitu chochote kuhusiana na Jaquline basi iwe ni rahisi kwa yeye kuto weza kujulikana uhalisia wake halisi zaidi ya sura yake tu.
“Kuna mgeni yoyote kutoka Afrika?”
“Ngoja nicheki orodha ya wageni”
Kijana huyo anaendelea kufanya alicho agizwa. Kwa bahati nzuri akakuta jina la Livba Livna katika orodha ya wageni walio weza kuhuzuria katika sherehe hiyo”
Agnes akajikuta akishusha pumzi nyingi, baada ya kuona tukio hilo, limeweza kutatulika.

“Muheshimiwa kuna tatizo”
Kijana mwengine alimwambia askari huyo, aliye kimbilia moja kwa moja kwenye sehemu alipo kaa kijana huyo na computer yake, hapo ndipo alipo weza kuiona sura ya Agnes na akionekana yupo kwenye moja ya hoteli kubwa iliyopo karibu na ikulu hiyo.
“Securty code zimeibwa, narudia tena Securty code zimeibwa, number 99902, kuna tatizo narudia tena kuna tatizo”
Askari huyo alitoa taarifwa kwa walinzi wote waliopo katika eneo la ikulu, huku akitoka kwenye chumba hicho, kwa haraka sana.

“Kuwa makini naona kama kuna jambo linalo endelea”
Agnes alimuambia Jaquline aliye endelea kuwatazama askari waliopo katika ukumbi, akagundua baadhi ya askri wanaondoka katika ukumbi huo wakieelekea nje. Agnes akawashuhudia askari baadhi wakiingia kwenye magari na kuondoka ikulu.
“Wanakwenda wapi hawa”
Agnes alijiuliza mwenyewe pasipo kugundua kwamba tayari amesha stukiwa kwamba yupo kwenye hoteli moja iliyopo karibu na ikulu, na amejulikana kwamba yeye ndio aliye husika na mauaji ya kiongozi wao bwana Paul Henry Jr.
                                                                                                  ***
“Maana yangu huyu binti yupo hai”
Eddy akamtizama Madam Mery huku akiwa amemkazia macho makali, Eddy akakumbuka siku ambayo alirudi katika kazi ya kuwaokoa Phidaya, alipo rudia nyumbani kwa Amina, rafiki wa Manka aliye kwenda kufanya naye kazi ya kuikomba familia yake, alikuta nyumbani kwa Amina kumetulia sana, akakumbuka jinsi alivyo weza kushuka na masanduku ya pesa na kuingia nayo ndani, ndipo alipo weza kukuta michirizi mingi ya damu kwenye sakafu pamoja na ukutani, ila kabla hajagundua lolote ndipo alipo weza kuvamiwa na kikundi cha kigaidia huku, Shamsa akiwa ni miongoni mwa magaidi hao.
 

ECOWAS: Hakuna makubaliano yoyote ya Jammeh kutoshtakiwa

0
0
==>Yahya Jammeh mwenye vazi jeupe akiondoka mjini Banjul, kulia ni mlinzi wake akiwa analia. Januari 21, 2017
 ***
Viongozi wa nchi za Afrika Magharibi wamesema kuwa, hakuna makubaliano yoyote ya kutoshtakiwa kwa rais Yahya Jammeh yaliyofikiwa mwishoni mwa juma, makubaliano yaliyomshawishi kiongozi huyo kuondoka mwenyewe kwa hiari nchini mwake, amesema waziri wa mambo ya Kigeni wa Senegal.

Jammeh, ambaye anatuhumuwa kwa uvunjifu mkubwa wa haki za binadamu wakati wa utawala wake, aliliongoza taifa la Gambia kwa miaka takriban 22, lakini akakataa kukubali matokeo ya uchaguzi mkuu wa Desemba mosi mwaka jana.

Jammeh aliondoka mjini Banjul siku ya Jumamosi, saa chache kabla ya vikosi vya ukanda wa ECOWAS kuingia mjini Banjul kudhibiti hali ya usalama na kuandaa mazingira ya rais Adama Barrow kurejea.

Kuondoka kwa Yahya Jammeh nchini Gambia kunatoa nafasi sasa kwa rais Barrow kurejea nchini mwake baada ya kuwa amekula kiapo katika ubalozi wa nchi yake nchini Senegal.

Uamuzi wa Jammeh kuondoka nchini mwake, ulizua maswali kuhusu makubaliano yaliyofikiwa kati yake na wakuu wa nchi za ECOWAS katika mazungumzo ya siku mbili mfululizo mwishoni mwa juma, mazungumzo yaliyoongozwa na rais wa Guinea, Alpha Conde na mwenzake wa Mauritania, Mohamed Ould Abdel Aziz.

Akizungumza na shirika la habari la Reuters, waziri wa mambo ya kigeni wa Senegal, Mankeur Ndiaye, amesema kuwa, wakuu wa nchi za ECOWAS hawakukubaliana chochote kuhusu kutoshtakiwa kwa Jammeh licha ya kufikia makubaliano.

Waziri Mankeur amesema kuwa Jammeh na timu yake walikubali kuondoka baada ya kuahidiwa usalama na kupewa hakikisho chini ya makubaliano yaliyopendekezwa na umoja wa Mataifa, ECOWAS na umoja wa Afrika, makubaliano ambayo hata hivyo hayakutiwa saini na upande wowote.

Waziri huyu amesema haya baada ya kutolewa kwa chapisho la makubaliano ya umoja wa Afrika na umoja wa Mataifa kuhusu mapendekezo ya kufikia suluhu ya amani ya kisiasa nchini Gambia.

Katika hatua nyingine, vikosi vya nchi za ECOWAS tayari vimewasili mjini Banjul, Gambia, ambako vimeenda kwaajili ya kutoa usalama kwa rais Barrow na raia wa Gambia.

Chanzo:RFI

Hotuba ya Rais Magufuli na Rais wa Uturuki leo Dar es salaam

0
0
Serikali za Tanzania na Uturuki zimesaini mikataba 9 ya ushirikiano wa kimaendeleo katika nyanja za Afya, Usafiri wa Anga na Viwanda. Rais Endorgan amualika Rais Magufuli kufungua ubalozi nchini Uturuki.

Amemuomba kusaidia kutokomeza watu waliotaka kumpindua madarakani.

Zaidi, tazama hii video ya hotuba zao

Mikataba 9 Iliyosainiwa na Serikali ya Tanzania na Uturuki Leo

0
0
Na Beatrice Lyimo-MAELEZO
Serikali ya Tanzania na Serikali ya Uturuki zimesaini mikataba tisa ya makubaliano ya kiuchumi inayolenga katika kuimarisha uhusiano na ushirikiano wa maendeleo baina ya nchi hizo.

Mikataba hiyo inahusisha sekta za uchukuzi, mawasiliano, habari, elimu, utalii, utafiti, viwanda, afya na ulinzi.

Akizungumza mara baada ya kusaini kwa mikataba hiyo  leo Ikulu Jijini Dar es Salaam, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli alisema ujio wa Rais wa Uturuki na ujumbe wake ni kielelezo cha ukuaji wa mahusiano baina ya Tanzania na Uturuki katika nyanja ya biashara na kimaendeleo baina nchini hizo.

Rais Magufuli alisema katika mazungumzo yake aliyofanya na Rais Recep Erdogan kuhusu ujenzi wa Reli ya Standard Gauge nchini, alimjulisha kiongozi huyo kuwa miongoni mwa wakandarasi walioomba zabuni ya ujenzi wa reli hiyo kuwa ni kampuni kutoka Uturuki, hivyo endapo itashinda zabuni hiyo itasaidia kukuza uhusiano uliopo baina ya nchi hizi mbili.

Aidha, Rais Magufuli alisema kuwa, Serikali ya Tanzania inatarajia kuomba  mkopo kupitia Benki ya Exim ya Uturuki katika kujenga sehemu ya kipande cha ujenzi wa reli hiyo.

Rais magufuli alisema Tanzania inaendelea kunufaika na uwepo wa Shirika la Ndege la Uturuki kwa kufanya safari zake za moja wka moja kutoka nchini Uturuki, kwa kuwa utasaidia kuongezeka kwa idadi ya watalii nchini na hivyo kukuza uchumi wa nchi hizo.

Kwa upande wake Rais wa Uturuki, Recep Erdogan alisema kuwa uwepo wa mikataba hiyo baina ya Tanzania na Uturuki itasaidia kupata matokeo mazuri ya uhusiano pamoja na fursa mbalimbali za ushirikiano katika nyanja ya Kilimo, Utalii, Ulinzi, Reli ambazo zitawezesha kukuza uchumi wa mataifa hayo.

Rais Erdogan alisema kuwa Uturuki imelenga kukuza ushirikiano uliopo baina yake na  Tanzania kupitia makongamano ya wafanyabiashara yenye malengo ya kukuza uchumi, kuongeza ajira pamoja na kukuza ujasiriamali baina ya Tanzania na Uturuki.

“Kiwango cha Biashara ya uwekezaji katika nchi ya Uturuki ni Dola za kimarekani 150 ambapo lengo letu ni kufika Dola za kimarekani 500,” alisema Rais huyo.

Aidha Rais Erdogan alisisitiza kuwa kufanya kazi kwa pamoja kutasaidia nchi hizi kusonga mbele na kufanikiwa katika nyanja mbalimbali.

Nae Waziri wa Maliasili na Utalii Prof. Jumanne Maghembe alisema kuwa makubaliano ya mkataba baina ya Tanzania na Uturuki katika Sekta ya Utalii yatasaidia katika kutangaza vivutio vilivyopo nchini, kubadilishana wataalamu, kubadilishana taarifa na kuongeza idadi ya watalii nchini.

Prof. Magembe aliongeza kuwa makubaliano hayo yatakuza sekta ya utalii katika kuvutia uwekezaji wa katika maeneo ya hoteli, fukwe na mbuga za wanyama zilizopo nchini.


Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumanne ya January 24

Mshindi wa Ubunge Dimani aahidi kuwa daraja

0
0
Mshindi wa nafasi ya Ubunge katika Jimbo la Dimani Visiwani Zanzibar Juma Ali Juma ameahidi kuzibeba kero za wananchi wa jimbo hilo na kuwasilisha serikalini kwa ajili ya kupatiwa ufumbuzi wa haraka

Ametoa ahadi hiyo mara baada ya Msimamizi wa Uchaguzi jimbo hilo, Fatma Gharib Ali kumtangaza rasmi kuwa mshindi katika uchaguzi huo na kusema kuwa kuwa Ubunge ni daraja la wananchi na serikali

Uchaguzi huo mdogo umefanyika kutokana na kifo cha aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo Hafidh Ali Tahir akiwa Bungeni Dodoma na umehusisha wagombea kutoka vyama 11 vya siasa.

Juma Ali Juma amepata kura 4,860 na kumshinda mpinzani wake kutoka CUF, Abdulrazak Khatib Ramadhan aliyepata kura 1,234.

Katika Uchaguzi huo wapiga kura walikuwa 6, 172 kati ya wapiga kura 9,275 waliojiandikisha katika daftari la wapiga kura jimboni humo.

Katibu wa Idara Maalum ya NEC, Itikadi na Uenezi Zanzibar amesema ushindi wa mgombea wa Chama hicho katika uchaguzi huo umekuwa mkubwa kuliko ule wa uchaguzi wa mwaka 2015, ishara inayotoa matumaini ya kuwa wananchi wa jimbo hilo wanaendelea kuiunga mkono CCM.

TCRA yatahadharisha Utapeli kupitia simu za mikononi

0
0
Mamlaka  ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imetoa tahadhari kwa watumiaji wa huduma za mawasiliano juu ya utapeli unaofanywa kwa kutumia simu za mkononi.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Kaimu Meneja wa Mawasiliano kwa Umma wa TCRA, Semu Mwakyanjala alisema kumekuwa na ongezeko la matapeli wanaoghushi utaratibu wa mawasiliano na kuwalaghai watu kutuma pesa kwa simu za mkononi.

Mwakyanyala alisema kumekuwa na ongezeko kubwa la matumizi ya huduma za kifedha na kwa miezi miwili iliyopita ya Novemba na Desemba, 2016 kwa wastani kiasi cha jumla ya fedha iliyopita katika mitandao ya kampuni zinazotoa huduma za kifedha kwa njia ya simu za mikononi ni Sh trilioni 13.07.

Aliongeza kuwa ni vyema wananchi wakazingatia mambo mbalimbali kabla ya kutuma fedha, ikiwemo kutokutekeleza maagizo yoyote yanayohusu fedha kwa mawasiliano ya simu hata kama yanatoka kwenye namba ya mtu anayemfahamu badala yake ampigie aliyemtumia ujumbe kwa namba nyingine kufanya uhakiki.

Pia aliwataka wananchi pale wanapopokea taarifa kwa njia ya simu au ujumbe mfupi wa maandishi kuwa ametumiwa fedha kwa makosa na kufuatiwa na kutumiwa ujumbe mfupi unaofanana na ujumbe unaotumwa na watoa huduma na kutakiwa kurudisha fedha hizo, asifanye haraka badala yake wachukue tahadhari zote kujiridhisha na uhalali wa taarifa hiyo.

“Omba taarifa fupi ya akaunti yako kwa mtoa huduma uhakiki miamala yako na salio lako ikibidi wasiliana na kituo cha huduma kwa wateja cha mtoa huduma wako kwa kuwa kumekuwepo na uhalifu wa kulaghai watoa huduma za mawasiliano kwa kutumia ujumbe mfupi unaokaribia kufanana na ujumbe unaotumwa na watoa huduma,” alieleza.

Wanasiasa wanaoeneza taarifa za uongo kuhusu njaa kukamatwa

0
0
Naibu  Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni ameonya kuwa watu wakiwemo wanasiasa wanaoeneza taarifa za uongo za kuwepo kwa baa la njaa, ni kosa na wachukuliwe hatua ikiwemo kukamatwa.

Masauni amesema bado kuna watu wanajichukulia mamlaka ambayo sio yao na kueneza uongo kuwa kuna njaa nchini, hilo ni kosa kwa kuwa kwa kueneza propaganda hiyo kunaweza kusababisha uvunjifu wa amani nchini.

“Hizo ni propaganda za watu wasioitakia mema nchi hii ….. mtu anapofanya kosa lazima achukuliwe hatua …… Jeshi la Polisi liangalieni hili,” alisisitiza.

Masauni alitoa onyo hilo wakati wa ziara yake ya siku moja aliyoifanya jana mkoani Rukwa ambako Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Zelothe Steven alimhakikishia kuwa mkoa huo hauna njaa, bali una ziada ya kutosha.

“Nyie wenyewe mmemsikia mkuu wa mkoa (Zelothe) amethibitisha kuwa hakuna njaa mkoani hapa lakini sio hapa tu, pia mikoa ya Mbeya na Songwe wamenithibitishia kuwa hawana njaa,” alisema Naibu Waziri Masauni na kuongeza: 

“Sasa wapo wanasiasa uchwara wanaeneza propaganda kuna njaa, sio mamlaka yao kutangaza kuwa kuna njaa, kueneza uongo kama huo ni si sawa kwa kuwa kunaweza kusababisha uvunjifu wa amani nchini, wanastahili kuchukuliwa hatua ikiwemo kukamatwa,” alisisitiza.

Awali Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Zelothe alimweleza Naibu Waziri Masauni kuwa hali ya kiusalama katika mkoa huo ni shwari ambapo amani na utulivu umeshamiri kwa kuwa una chakula cha kutosha.

Walimu Watatu Wakamatwa Kwa Kupiga Dili la Mishahara Miwili........Serikalini na Private!

0
0

Walimu watatu mkoani Mwanza wanashikiliwa na jeshi la polisi kwa kosa la  kukimbia vituo vyao vya kazi na kufanya kazi shule binafsi huku wakiendelea kupokea mishahara ya serikali

Taarifa ya jeshi la polisi mkoa wa Mwanza imewataja walimu hao waliokamatwa jana asubuhi katika mtaa wa Buhongwa wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza,kuwa ni pamoja na Richard Mgendi (30), Rwiza Ntare (27) na Gilbert Makwaya (33).

Walimu hao kila mmoja ana story yake kama ifuatavyo:-

Mwalimu Richard Mgendi alikuwa akifundisha shule ya sekondari ya Misasi wilayani Misungwi, mwaka 2012 alimuaga mkurugenzi wa wilaya hiyo kuwa anakwenda kusoma Masters ya lugha (Linguistic) katika chuo kikuu cha Mtakatifu Augustino, kwa kipindi chote hicho inadaiwa mwalimu huyo alikwenda kusoma na alipomaliza hakurudi katika shule yake ya awali bali alikuwa akifundisha shule binafsi ya sekondari iitwayo Musabe iliyopo Buhongwa huku akiendelea kulipwa mshahara kutoka serikalini.

Mwalimu Rwiza Ntare alikuwa akifundisha shule ya sekondari iitwayo Kigongo sekondari iliyopo wilaya ya Chato mkoani Geita ambapo mwaka 2015, alimuaga mkurugenzi wake kuwa anakwenda hospitali ya rufaa ya Bugando kupatiwa matibabu ya macho na vidonda vya tumbo lakini hakurudi tena bali inadaiwa alikuwa akifundisha shule binafsi ya sekondari iitwayo Musabe iliyopo mtaa wa Buhongwa huku akiendelea kulipwa mshahara na serikali.

Mwalimu Gilbert Makwaya alikuwa akifundisha Runima sekondari iliyopo maeneo ya Buhongwa na alimuaga mkurugenzi wa wilaya ya Nyamagana tarehe 27/09/2015 kuwa anakwenda kusoma Masters ya Hesabu katika chuo kikuu cha Mwenge kilichpo mjini Moshi lakini hakwenda bali alikuwa akifundisha shule binafsi ya Musabe iliyopo mtaa wa Buhongwa huku akiendelea kupokea mshahara kutoka serikalini.

Walimu wote watatu wapo katika mahojiano na jeshi la polisi na pindi uchunguzi ukikamilika watafikishwa mahakamani.

Jeshi la polisi linaendelea kuwatafuta baadhi ya walimu ambao wametoroka lakini inadaiwa wapo katika shule hiyo binafsi ya Musabe huku wakiendelea kulipwa mshahara na serikali pamoja na mkurugenzi wa shule hiyo.

Majambazi Wawili Wauawa Jijini Mwanza

0
0
Watu wawili waliokuwa wakituhumiwa kwa ujambazi wameuawa wakati wakitaka kujaribu kuwatoroka askari polisi wilayani Ilemela mkoani Mwanza

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza amesema kwamba tukio hilo lilitokea  tarehe 20.01.2016 majira ya saa 2:30  usiku, katika mtaa wa kiloleli “A” kata ya Nyasaka mkoa wa Mwanza na kuwataja majambazi waliouawa kuwa ni Eric Magese miaka 22, na aliyejulikana kwa jina moja la Peter miaka kati 25 hadi 27 wote wakazi wa Mecco jijini Mwanza.

Amesema majambazi hao waliuawa wakati wakijaribu kutoroka askari polisi pindi wakiwapeleka mahali ambapo wenzao wamejificha ili waweze kufanya uvamizi.

Amesema kuwa katika tukio hilo pia ilipatikana silaha moja aina ya short gun yenye namba TZ CAR 103283 ikiwa na risasi tatu ambayo inadaiwa walipora kwenye kampuni ya ulinzi iitwayo Malika Security Service Limited

Msangi amesema majambazi hao walikuwa wakitafutwa na polisi baada ya kufanya unyang’anyi wa kutumia silaha katika maeneo mbalimbali jijini Mwanza ilikiwemo tukio la Kitangiri mnamo tarehe 19.12.2016 na tukio la tarehe 02.01.2016 katika mtaa wa Nyasaka.

Jinsi walivyouawa
Msangi amesema baada ya upelelezi uliofanikisha kukamatwa kwa watuhumiwa hao, walikubali kuwapeleka askari katika eneo ambalo walikuwa wamepanga pamoja na wenzao wawili kwa ajili ya kufanya matukio zaidi ya ujambazi.

Amesema walipofika katika eneo hilo, watuhumiwa hao walipiga kelele kama ishara ya kuwatorosha wenzao na kuanza kuwakimbia askari.

Askari walifyatua risasi kadhaa hewani wakiwaamuru wasimame lakini waligoma ndipo waliwafyatulia risasi za mguuni kwa bahati mbaya ziliwalenga maeneo ya juu ambapo walifariki dunia wakati wakipelekwa hospitali.

Waraka wa Zitto Kabwe kuhusu marudio ya Uchaguzi

0
0
Nachukua fursa hii kuwapongeza Sana kwa kazi kubwa mliyoifanya kwenye chaguzi ndogo za udiwani na ubunge zilizomalizika hivi punde nchi nzima. Ingawa hatukushinda hata kata moja katika kata 20 zilizokuwa zinashindaniwa, lakini tumefanya vizuri kwenye matokeo.

Chama chetu kilisimamisha wagombea katika Kata 5 kati ya Kata 20 nchi nzima, Isagehe (Kahama), Kijichi (Dar es salaam), Kiwanja cha Ndege (Morogoro), Nkome (Geita) na Tanga (Songea). Na pia tulisimamisha Mgombea katika Uchaguzi wa Ubunge Dimani (Zanzibar).

Baada ya kufanya kampeni kubwa mzunguko wa kwanza tuliweza kutazama na kuamua kuwekeza kwa nguvu kwenye Kata 3.

Pamoja na kuwa hatukushinda Udiwani wala Ubunge katika Uchaguzi , matokeo yameonyesha kukua kwa kasi kubwa kwa Chama chetu. Tukishika nafasi ya 2 katika Kata ya Isagehe (Halmashauri ya Mji wa Kahama) kwa kupata mara 2 ya Kura ya zile ambazo tulipata katika Uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, hali hiyo ipo pia katika Kata ya Kijichi jijini Dar es salaam na Nkome mkoani Geita.

Ni dhahiri kuwa sauti yetu imesikika, Kampeni zetu zilizojikita juu ya masuala ya wananchi zimeleta matunda kiasi.Nawapongeza sana viongozi wetu wa Chama katika Jimbo la Kahama Mjini kwa kazi kubwa tulioifanya na kupiga hatua kubwa. Nawaomba wasikate Tamaa bali wawekeze kwenye kuimarisha uongozi wa Chama Jimbo zima, kwenye kata zote ili kuwa tayari kwa uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Katika Kata za Nkome mkoani Geita na Kijichi mkoani Dar Es salaam tumefanya kazi kubwa Sana. Wagombea na viongozi wetu wa Chama wa mikoa hii na kata hizi wamepigana kwenye mazingira magumu sana ya ushindani mkali wa kisiasa. Kata hizi zimetupa fundisho kuwa wananchi wanataka ushirikiano wa vyama vya upinzani. Ujumbe huo umefika na nawaomba viongozi wetu wa Chama wajiandae kufanya kazi na vyama vingjne. Ubinafsi, roho mbaya, chuki na kukomoana hakuwezi kutusaidia. Lazima tubadilike sisi wenyewe kwanza kabla ya kutaka kuleta mabadiliko kwa wananchi.

Katika Kata ya Tanga Manispaa ya Songea na kata ya Kiwanja cha Ndege Manispaa ya Morogoro wanachama wetu na viongozi walifanya kazi kubwa kuonyesha uwepo wa Chama kwenye maeneo yao. Wamepanda mbegu za Chama na kwa uwezo wa mungu mbegu hizi zitamea na kuzaa matunda.

Ni muhimu kukemea hali ya uchaguzi ya Dimani, Naibu Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mawasiliano ya Umma – Zanzibar, ndugu Seif Hamad, ni miongoni mwa waliojeruhiwa kutokana na kipigo baada ya kutolewa Kituoni alipokuwa Wakala wa Chama kwa kupinga udanganyifu wa uchaguzi. Bado uchaguzi kwa upande wa Zanzibar hauendeshwi katika misingi ya haki na demokrasia.

Nawapongeza na kuwashukuru sana wanachama wote wa ACT Wazalendo mliojitoa kwa Hali na Mali kushiriki kampeni katika uchaguzi huu. Shukran za dhati Kabisa kwa madiwani wetu waliotumia gharama zao kwenda kuishi vijijini kutafuta kura za Chama chetu. Sina cha kuwalipa mungu atawalipa. Mmeonyesha mapenzi ya dhati kwa Chama chenu. Mmeonyesha uzalendo wa dhati kwa vitendo.

Nawapongeza viongozi wa Chama wote wakiwemo wale kwa Kitaifa kuanzia Mwenyekiti wetu – Mama Anna Elisha Mghwira, Makamu Mwenyekiti – Mzee Shaaban Mambo, Kaimu Katibu Mkuu – ndugu Said Sanani, na Naibu Katibu Mkuu – ndugu Msafiri Mtelemwa kwa kazi kubwa walioiafanya. Nawapongeza pia makatibu wa Kamati za Makao Makuu ya Chama kwa kuwa waratibu wa kata zilizoshiriki uchaguzi na kwa wale waliokuwa makao makuu kwa kufanya kazi kubwa ya kuwasadia wenzao waliokuwa kwenye mapambano. Kwa Kweli tumefanya kazi kama timu na sote tumechangia matokeo haya tuliyoyapata.

Uchaguzi umekwisha. Badala ya kutumia muda wetu kujadili matokeo, tukubali tumeshindwa na kuanza kujipanga kujenga Chama kwenye maeneo yetu. Tuwaunge mkono walioshinda lakini pia tuwakosoe wanaposhindwa kuwajibika. Tusiache kuwasemea wananchi na kuhangaika na changamoto zao za maisha – msingi wetu wa Siasa zinazojikita juu ya masuala ya wananchi ni muhimu sana.

Ndio kazi yetu hii Kama Chama cha siasa. Tulitumia fursa ya kampeni za chaguzi ndogo kupaza sauti kwenye masuala ya kitaifa na tulifanikiwa Sana kwenye masuala mbalimbali na kutengeneza ajenda za kitaifa. Tusichoke kuendelea kuwa Chama cha masuala na sio matukio. Chama cha hoja Badala ya viroja. Chama cha UTU.

Tuendelee kutaka shughuli za kisiasa kuendelea kwa mujibu wa Sheria. Tuendelee kulaani vikali uamuzi wa Serikali kuzuia vyama vya siasa kufanya mikutano ya hadhara.

Ahsanteni Sana
Kabwe Z. Ruyagwa Zitto
Kiongozi wa Chama (KC)
ACT Wazalendo

Januari 23, 2017

Kauli ya Tundu Lissu baada ya upinzani kuburuzwa vibaya na CCM chaguzi ndogo

0
0
Na.Tundu Lissu 
Waheshimiwa na makamanda poleni kwa mapambano na hongereni kwa kazi kubwa mliyoifanya kwenye chaguzi hizi. Naona kila mmoja wetu anasikitika jinsi matokeo ambavyo yamekuwa tofauti na matarajio yetu na kazi tuliyoifanya.

Ni rahisi, katika mazingira haya ya kushindwa na kabla vumbi halijaisha, kuanza kulalamika, kunyoosheana vidole na kukatishana tamaa. Hii haitusaidii sana. Badala yake, tunachohitaji zaidi ni ‘brainstorming’ kuliko ‘blamestorming.’ Naomba nifanye ya kwanza. Chaguzi ndogo za ubunge au udiwani ni ngumu sana kushinda katika mazingira halisi ya nchi yetu.

Mifano michache inathibitisha ukweli huu. Katika election cycle ya ’05-’10, tulishinda Jimbo la Tarime lakini tukapigwa Biharamulo Magharibi na Busanda. Tarime lilikuwa Jimbo letu tangu Uchaguzi Mkuu wa ’05, Busanda lilikuwa la maCCM na Biharamulo Magharibi lilikuwa la TLP. Sikumbuki vizuri kama tulishinda Kata hata moja katika mzunguko wa uchaguzi wa kipindi hicho.

Katika election cycle ya ’10-’15, tulipigwa Igunga licha ya kazi kubwa tuliyofanya, lakini tukashinda Arumeru Mashariki iliyokuwa chini ya maCCM. Vile vile tulishindwa Kalenga, Chalinze na Ulanga Magharibi yaliyokuwa ya maCCM tangu Uchaguzi Mkuu wa ’10.

Kwenye chaguzi za Kata za ’12 kama mnakumbuka, licha ya kazi kubwa na rasilimali nyingi, tulipata Kata tatu tu kati ya 26 zilizokuwa zinagombaniwa. Ukiachia Ifakara Mjini ya Mh. Juakali, Kata nyingine mbili – Kiboriloni na Iseke – zilikuwa zetu tangu Uchaguzi Mkuu wa ’10.

Kwa mantiki hii, matokeo ya jana sio ya kushangaza sana. Kata ya Duru ilikuwa ya kwetu na tumeitetea, nyingine zote tulikopigwa zilikuwa za maCCM. Hatujanyang’anywa iliyokuwa yetu, hatujanyakua zilizokuwa zao. Hata hivyo, funzo kubwa zaidi la historia ya chaguzi hizi ni hili hapa: licha ya kupigwa kwenye chaguzi ndogo hizi, tumeendelea kufanya vizuri zaidi katika kila Uchaguzi Mkuu uliofuatia kipigo cha chaguzi ndogo.

Mwaka ’10 tulifanya vizuri zaidi licha ya kupigwa Busanda na Biharamulo Magharibi katika mzunguko wa ’05-’10. In fact, tulichukua Jimbo la Biharamulo Magharibi mwaka huo. Na tulipata Kata nyingi zaidi ’10 kuliko ilivyokuwa ’05. Mwaka ’15 tulipata ushindi mkubwa zaidi katika Kata na majimbo licha ya kupigwa kwenye chaguzi ndogo za mzunguko wa ’10-’15.

Hoja yangu hapa ni kwamba uchaguzi wa marudio hauna direct and negative bearing kwenye matokeo yetu ya Uchaguzi Mkuu unaofuatia. On the contrary, uchaguzi wa marudio unatupa fursa ya kupanda mbegu ambayo, ikitunzwa vizuri, inakuwa na mazao bora kwenye chaguzi zinazofuatia.

Kwa upande mwingine, chaguzi za marudio – kwa sababu ya udogo au uchache wa maeneo yanayogombaniwa – yanawapa maCCM fursa ya kutumia nguvu kubwa za rasilimali na za kidola ukilinganisha na tunazotumia sisi. Kwenye Uchaguzi Mkuu unaofuatia, nguvu hizo zinasambazwa nchi nzima na kwa hiyo effectiveness yake inapungua.

Ndio maana tumefanya vizuri zaidi kwenye Uchaguzi Mkuu kuliko kwenye chaguzi ndogo za marudio. Hili, kwa maoni yangu, ndilo fundisho kuu la chaguzi hizi za marudio. Hatuna sababu kubwa ya kushangilia kutokana na matokeo ya jana. Hata hivyo, hatuna sababu yoyote ya kuomboleza pia. Obviously, maCCM na wapambe wao wataandika ‘wasifu wa marehemu’ wa CHADEMA/UKAWA na kuutangaza dunia nzima na kwa sauti kubwa. Hilo lisitupofushe macho yetu, hata kama linakera sana.

Tutathmini kazi tuliyoifanya na matokeo tuliyoyapata. Tupate mafundisho sahihi ya kazi hiyo na matokeo yake. Tutumie mafundisho hayo kwa kujipanga vizuri zaidi kwa ajili ya ‘the real prize’: 2020.

Mtatiro aeleza sababu ya upinzani ‘kuangukia pua’ uchaguzi mdogo

0
0
Na. Julius S. Mtatiro
Goodmorning. Katika uchaguzi huu mdogo CUF ilikuwa inatetea kata 1 ya Kimwani Muleba na CHADEMA ilikuwa inatetea kata 1 ya Duru, Babati. Kata zingine zote zilikuwa za CCM na zilikuwa zinatetewa na CCM.
 
Matokeo yanaonesha CCM imetetea viti vyake vyote vya udiwani (takribani 20), CUF imenyang’anywa kiti chake kimoja (Kimwani) na CHADEMA imelinda kiti chake kimoja (Duru).
 
Kwa vyovyote vile vyama mbadala haviwezi kujivunia matokeo haya kwani havikuweza kuishinda CCM, na CCM haina cha kutambia kwani imeongeza kata moja tu. Kwa sasa nina mambo kadha ya kuzungumza;
  1. Hali halisi inaonesha kuwa kama vyama mbadala vingeshirikiana vingelishinda kata si zaidi ya 7 hivi. Bahati mbaya mashirikiano haya yalikosekana tangu mwanzo baada ya upande wa “CUF ya Msajili na Bwana Yule” kusisitiza kuwa wataweka wagombea nchi nzima na hakuna UKAWA.
  2. Lakini pia, hata shajihisho la ushirikiano mkubwa zaidi lililokuja kuzuliwa na kaka yangu Prof. Kitila Mkumbo lilifanywa TOO LATE kwa lengo la kutafuta sababu ya kujificha baada ya matokeo. Niliwahi kusema, kiuzoefu vyama haviwezi kuachiana maeneo wiki moja kabla ya siku ya uchaguzi na kushauri hivyo si kwa nia njema.
  3. Baada ya CUF ya Msajili na Bwana Yule kujipanga kuvuruga uchaguzi huu na kushusha spirit ya UKAWA, vyama vya NCCR na CHADEMA pia vilionelea kila kimoja kijipiganie jambo ambalo ni kosa kubwa. Na madhara ya migawanyiko yote yalijulikana.
  4. Uzoefu unaonesha kuwa, kuishinda CCM kwenye chaguzi ndogo ni nadra mno. Kuliwahi kuwa na mfululizo wa chaguzi ndogo, Tarime, Busanda, Tunduru, Mbeya Vijijini n.k. na kote huko CCM ilishinda isipokuwa Tarime na baadaye Arumeru. Katika chaguzi ndogo CCM hutawanya rasilimali zake nyingi zikajaa kwenye majimbo au kata hadi POMONI.
  5. Mkakati wa DOLA na CCM kuvitumia baadhi ya vyama au baadhi ya viongozi kwenye vyama (mamluki) unaelekea kufanikiwa sana. Lakini, sera za “Self Protectionism” ndani ya vyama mbadala hata kwenye mambo yanayohitaji ushirikiano wa kitaifa zitaendelea kuvigharimu vyama vyetu.
  6. Good News kwa ACT Wazalendo kwamba huenda ndicho chama kilichofanikiwa kwenye uchaguzi huu kuliko vyama vyote (CCM inclusive) kwani pamoja na uchanga wake kimevishinda baadhi ya vyama vikongwe kwenye kata chache (kwa idadi ya kura na si ushindi wa jumla). Na hiyo ni alert call kwamba ACT is needed in the UKAWA basket na kwa hiyo ianze ku BEHAVE like a true party wakati UKAWA pia ikiiandalia mazingira kisaikolojia.
  7. Bado CCM inashinda chaguzi kwa kutumia mifumo ilele; rushwa, mabavu, hila, wawakilishi wa NEC na NEC yenyewe, uwezo wa uelewa wa wapiga kura (Mfano. CCM imepeleka uandikishaji wa Bima ya Afya kwa wananchi kata ya Nkome, wakati wa uchaguzi = Rushwa).
  8. Vyama vya upinzani vinashindwa chaguzi hizi kwa sababu ya kukosa ushirikiano wa kweli baina ya vyama hivyo, maelezo namba 7 hapo juu na sentensi ya kwanza ya maelezo yaliyo namba 5 hapo juu.
  1. Kwa hakika, matokeo haya hayana athari zozote za kufaulu kwa Magufuli katika sera zake au kushindwa kwa Magufuli katika sera zake. Yaani, CCM ya Magufuli haijawa na ushawishi wa ziada kwa wapiga kura ili kupata ushindi huu kwenye ngome zake. CCM bado inashinda chaguzi kibabe na kwa mkakati dola zaidi bila kujali nani yuko madarakani.
  2. Sijaona connection yoyote kati ya matokeo haya na siasa za 2020. Vyama vyote vinayo fursa ya kuendelea kujipanga na kama tutafanikiwa kuuvunja mfumo dola unaoathiri vyombo vya uchaguzi na uhuru wake, unaoondoa mazingira sawa kwa vyama kufanya siasa n.k, mabadiliko ya kikatiba kwenye NEC na sheria za uchaguzi na mengine mengi, siasa za 2020 zitakuwa mbichi sana.

Kauli ya Rais Magufuli Baada Ya CCM Kushinda Kwa Kishindo Uchaguzi Mdogo wa Marudio

0
0
Mwenyekiti  wa Taifa wa CCM, Rais John Magufuli amesema ushindi wa CCM wa ubunge na madiwani katika Uchaguzi Mdogo uliofanyika juzi nchini ni ishara ya ushindi wa chama chake katika uchaguzi ujao kutokana na wananchi kuonesha imani kwake na serikali yake.

Rais Magufuli aliyasema hayo kwa waandishi wa habari muda mfupi kabla ya kumpokea Rais wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan aliyefika Ikulu, Dar es Salaam jana akiwa kwenye ziara yake ya siku mbili nchini.

Rais Magufuli alisema ushindi huo ni kipimo cha utendaji wake kwa wananchi na hivyo umemuongezea ari ya kuwatumikia wananchi kwa moyo wake bila ya kujali changamoto mbalimbali zilizopo.

“CCM Oyee! Mnaonaje ushindi wa CCM? Hii inadhihirisha ni namna gani wananchi walivyo na imani na mimi na serikali yangu. Tumeshinda ushindi wa kishindo katika kata na Jimbo, wenyewe mmeshuhudia namna tulivyowapiga. Au mnasemaje?” Rais Magufuli aliwaambia waandishi wa habari na kisha akawashukuru na kuelekea eneo lake maalumu akimsubiria Rais wa Uturuki kwa ajili ya kumpokea.

CCM mbali ya kushinda kiti cha ubunge cha Dimani visiwani Zanzibar, imeshinda kata 18 kati ya kata 20 zilizofanya Uchaguzi Mdogo wa Udiwani juzi kutokana na sababu mbalimbali zikiwamo za kufa kwa waliokuwa wakishikilia nyadhifa hizo na kufutwa kwa matokeo kwa amri ya mahakama.

Kata ambazo CCM imeshinda ni Nyarenanyuki (Arumeru, Arusha), Isegehe (Kahama, Shinyanga), Nkome (Geita), Kiwanja cha Ndege (Manispaa Morogoro), Lembeni (Mwanga, Kilimanjaro), Ihumwa (Dodoma), Matevez (Meru, Arusha), Kimwani (Muleba, Kagera), Igombavanu (Iringa), Kijichi (Mbagala, Dar es Salaam), Ng’hambi (Dodoma), Kinampundu (Singida), Kasansa (Katavi), Malya na Kahumulo (Mwanza), Mkoma (Mara), Misugusugu (Kibaha, Pwani).

Aidha, CCM imeshindwa katika Kata ya Duru mkoani Manyara, ambako mgombea wa Chadema, Ali Shaaban ameibuka mshindi.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images