Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

SORRY MADAM -Sehemu ya 17 & 18 (Destination of my enemies)

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA

ILIPOISHIA  
. Akiwa gorofa ya kwanza kwenda gorofa ya pili, akakutana na askari wawili wakishiuka chini, akaishusha kofia yake chini kidogo, akapisha na askari hao wakimtazama.
“Ngoja kwanza”
Askari mmoja alizungumza baada ya kushuka ngazi sita kwenda chini, akatoa picha iliyopo mfukoni mwake.
“Ndio huyu tunaye mtafuta”
Askari mmoja alizungumza na kuanza kupandisha kwenda ngazi za juu huku akikimbia, kwa bahati nzuri akafanikiwa kumuona mzee Godwin akitembea kwenye moja ya kordo.
“Simama polisii”  
Askari huyo alizungumza huku bunduki yake akiwa amemnyooshea mzee Godwin kwa nyuma.

ENDELEA
“Nyoosha mikono yako juu”
Watu walio karibu na eneo alipo simama Mzee Godwin pamoja na askari hao walipo nyuma yake mita chache kutoka sehemu alipo, wakabaki wakishangaa tukio hilo kwani hawakujua ni kwanini askari hao wamemshikia mtutu mtu huyo. Taratibu Mzee Godwin akanyoosha mikono yake juu, huku akiwa bado hajageuka kuwatazama askari hao. Askari mmoja akamkonyeza mwenzake amfwate mzee Godwin, kwenda kumfunga piungu.

Kwa umakini mkubwa askari huyo akaanza kutembea kwa kunyata huku bunduki yake aina ya SMG akiwa ameishika vizuri mikononi mwake. Kitendo cha kumfikia Mzee Godwin, ikawa ni moja ya kosa kubwa sana, mzee Godwin akageuka na teke la mguu wa kustoto, lililo mchota askari huyo miguu yake na kujikuta akianguka kama mzingo na bunduki yake akiitupia pembeni, kwa uharaka wa hali ya juu, mzee Godwin, akaichomoa bastola yake iliyo ichomeka kiunoni mwake kwa nyuma.

Hakuhitaji hata kuwa na huruma na askari aliye mshikia bunduki, akibabaika. Akapimga risasi moja ya paja askari huyo, akaanguka huku akilia kwa uchungu na maumivu makali sana.

Mlio wa bastola yake ukawafanya watu kutawanyika, si madaktari wala wagonjwa walio jiweza, kila mmoja akaikoa roho yake, hata kushangaa kwao kukaingia doa. Askari wengine walio kuwa kwenye maeneo tofauti ya hospitali, baada ya kusikia mlio huo wakakimbilia katika jengo hilo la maabara.

Askari aliye anguka chini, baada ya kuona mwenzie ametandikwa risasi ya paja na anaendelea kuhangaika hangaika chini, huku akilia, akajaribu kurusha teke la chini, ambalo lilimuangusha mzee Godwin. Askari huyo akanyenyuka, huku akikunja ngumi, mzee Godwin akasimama huku akitabasamu, kwani akimuangalia askari huyo, umri wake wapata miaka ishirini na tatu hadi tano.

Askari akaanza kurusha ngumi zake, zilizo mkosa Mzee Godwin, kwani aliweza kuzikwepa zote huku akiendelea kumuonea huruma kijana huyo. Mzee Godwin akakimbia kwa kasi, askari huyo akanzanza kumfukuza, mzee Godwin akafika hadi karibu ya ukuta, kwa uwezo mkubwa alio kuwa nao akakanyaga ukutani, na kujigeuza kwa kasi, askari huyo akakutana na teke zito la kichwa lililo muangusha chini, na kupoteza fahamu hapo hapo.

“Nice job, kijana”
Mzee Godwin alizungumza huku akijiweka sawa koti lake. Akiwa katika kordo hiyo, askari mmoja akajitokeza akiwa na bunduki. Askari akaanza kufyatua risasi kwa mawenge yaliyo muingia baada ya kumuona wezake wakiwa wamelala chini, mmoja akiwa ametulia kimya na mwengine akiendelea kulia huku damu nyingi zikiwa zimesambaa kwenye sakafu.

Mzee Godwin, akauvamila mlango ulipo mbele yake, na kuingia ndani ya chumba hicho, alicho wakuta madaktari wawili wakiwa wamelala chini ya meza kwa woga. Mzee Godwin akaufunga mlango kwa ndani kisha akaichomoa bastola yake.
“Simameni”
Aliwaamrisha askari hao, wakatoka chini ya meza huku kila mmoja akionekana kuwa ni muoga kupindukia, kwani haja ndogo ilianza kuitotesha suruali yake.

“Vueni nguo haraka”
Kila walicho ambiwa ndicho ambacho madaktari hao waliweza kukifanya, Mzee Godwin naye akaanza kuvua nguo zake na kubakiwa na nguo za ndani.
“Wewe kikojozi vaa hizi”
Akamrushia daktari nguo zake, kisha yeye akachukua nguo za daktari mwengine. Alipo maliza kuvaa mavazi hayo ya kidaktari pamoja na miwani, akamuamrisha daktari huyo kuvaa, kofia yake aliyo kuwa ameivaa.

       Gari za polisi wa vikosi vya kutuliza ghasia F.F.U, zikazidi kuongezeka katika hospitali ya muhimbili, hii ni baada ya kupata habari kwamba, gaidi Mzee Godwin ameweza kuonekana katika hospitali hiyo na kuwashambulia askari wawili. Wananchi walipo katika eneo la hospitali wakawekwa chini ya ulinzi mkali, hapakuwa na aliye ruhusiwa kuingia ndani ya hospitali, wala aliye ndani ya hospitali hakuruhusiwa kuweza kutoka nje. Hii yote ni kuhakikisha gaidi wao hajichanganyi na wananchi na kuweza kutoweka katika eneo la hospitali.
                                                                                                   ***
       Nguvu na umahiri wa kikosi cha bwana Rusev kikazidi kuongezeka siku hadi siku, akazidi kuchukua vijana mbali mbali katika mataifa ya kiafrika, akawaingiza katika kikosi chake ili kuhakikisha mipango yake anayo ipanga inakwenda vizuri sana.
“Muheshimiwa mipango yako ni nini?”
Mshauri wake wa karibu alimuuliza bwana Rusev mara baada ya vijana zaidi ya ishirini kutoka nchi ya Afrika kuweza kuingizwa kwenye kambi yake, iliyopo chini ya bahari.
“Nahitaji kuifanya dunia nzima kuwa na kiongozi mmoja tu, ambaye ni mimi”

“Ila muheshimiwa itawezekana kweli, kutokana mataifa mengi yana nguvu sana”
“Kwa ukimya ambao tumeufanya tangu kifo cha Pual Hennry Jr, sasa ninakwenda kuitingisha dunia. Nahitaji ndoto za Adolf Hitler niweze kuzitimiza mimi”
Bwana Rusev alizungumza huku akitabasamu. Akiendelea kuwaangalia vijana hao, wakinza kupatiwa mafunzo maalumu katika ngome yake, ambayo ni ngumu sana kwa mtu kuweza kuifahamu.
Simu ya mshauri wake, ikaingia ujumbe wa video ulio mstua sana, ikabidi amuonyeshe bosi wake bwana Rusev.

“RUSEV, RUSEV RUSEV, Umenimiss eheee”
Sauti na sura ya Jaquline, vinaoenekana kwenye simu hiyo. Bwana Rusev akajikuta akiitumbulia macho video hiyo aliyo tumwa na muda mchache ulio pita.
“Huyu Malaya yupo hai?”
Bwana Rusev alizungumza kwa hasira huku akiendelea kuitazama video hiyo.
“Najua utashangaa, kuniona nipo hai. Hahahaaaaaa, ngoja niende kwenye point muhimu. Niliapa kwamba nilazima nitakuua, na hii ni moja ya ahadi nitakayo ifanya siku na muda wowote.”

“Ila kabla ya kufanya hivyo kutana na mgeni rafiki yako mpendwa”
Video hiyo ikasogezwa pembeni, ambapo bwana Rusev akaiona sura ya Agnes akitabasamu.
“Umewaacha wezangu wamekwenda jela kwa ajili yako, sasa tambua kazi ni moja tu. Tutakupeleka kuzimu mw………”
Bwana Rusev kwa hasira akaizima video hiyo ya vitisho kutoka kwa mabinti ambao anawatambua vizuri sana.
“Muheshimiwa ut…..”
Bwana Rusev akamtandika ngumi nzito mshauri wake huyo, kisha akaondoka kwa hasira na kuwafanya baadhiya askari wake kushangaa tukio hilo.
                                                                                                     ***
       Mzee Godwin kuchungulia dirishani, akaona askari wengi wakiwa wamemiminika katika eneo la hospitalini, wakiwa na silaha nzito pamoja na mbwa wakali.
“Shitii”
Mzee Godwin alizungumza huku akijikuna kichwa chake
“Shika meza huko”
Aliwaamuru madkatari hao kuisukumia meza hiyo kubwa kwenye mlango, kwani alihisi muda wowote mlango unaweza kuvunjwa na askari walipo nje.

“Laleni chini”
Mzee Godwin aliendelea kuwaamrisha madaktari hao walio tii, kwani pasipo kuweza kufanya hivyo wanaweza kupoteza maisha yao. Katika kukichunguza chumba, kwa bahati nzuri akaona sehemu ya juu kuna sehemu inaweza kufunguka.
“Mukinyanya kichwa tu, ninawapasua ubongo”
Mzee Godwin alizungumza huku akipanda juu ya meza hiyo, akiendelea kutafuta ni jinsi gani anaweza kuifungua sehemu hiyo yenye mfuniko mgumu kiasi. Kwa bahati nzuri akafanikiwa kufungua mfuniko huo, akachungulia juu ya dari, akakuta uwazi mkubwa ambao unaweza kumruhusu yeye kuweza kupita pasipo wasiwasi.

“Hivi ni kwanini tusivunje mlango?”
Askari mmoja alishauri, wezake kwani ni muda umekatika wamekaa nje ya mlango huo wakishikilizia kitu kinacho endela ndani.
“Humo ndani kuna madaktari tukifanya hivyo tunaweza kuwapelekea wakauliwa
“Ila mkuu tutaendela kukaa hapa hadi saa ngapi?”
Hapakuwa na jibu lolote alilo litoa mkuu wao huyo, anaye hofia maisha ya madaktari hao.


Barua ya TEC Kwenda Kwa Maaskofu wa Makanisa Yote Kuombea Mvua Inyeshe

Ray Kigosi afunguka kuhusu Mimba na mapenzi yake na Chuchu Hans

$
0
0
Zikiwa zimebaki siku kadhaa msanii wa filamu nchini Chuchu Hans kujifungua msanii Ray Kigosi amefunguka na kumuomba Mungu mpenzi wake huyo ajifungue salama.

Ray amesema licha ya kupitia mambo mengi lakini Mungu amewapigania mpka sasa wanatarajia kupata mtoto wao wa kwanza kati ya mwezi huu wa kwanza kama siyo wa pili mwanzoni.

Ray Kigosi anasema ulikuwa ni kama utani vile lakini tayari leo umeshafika mwezi wa tisa toka mchumba wake huyo amepata ujauzito huo. 

"Kwanza kabisa napenda kumrudishia sifa na utukufu Mungu baba Muumba wa mbingu na ardhi tumepitia vingi vikwazo lakini yeye atutiaye nguvu aliendelea kusimama na sisi imara asante sana Mungu kwa kuwa mwema kwetu mengi yalisemwa juu yetu lakini Mungu baba umejibu ulikuwa mwezi mmoja kama utani vile hatimaye imefika miezi tisa na sasa kubaki siku chache. Nakuombea my lovely Mzungu Mungu akufanyie wepesi". Ray Kigosi

A photo posted by vicenti kigosi (@ray_kigosi) on

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili ya January 15

Taarifa kutoka Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) kuhusu Mhadhiri Msaidizi aliyekamatwa kwa tuhuma za rushwa ya ngono

Mkakati Mpya wa Kumtoa Godbless Lema Gerezani

$
0
0
Chadema imeamua kuja na mpango mpya wa kuhakikisha Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema anatolewa mahabusu.

Lema amekuwa mahabusu tangu Novemba mwaka jana, lakini chama hicho kimesema sasa kinataka apate haki ya kisheria na kuwa huru kwa kuwatumia wanansheria katika kesi mbalimbali zinazomkabili.

Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu amesema hayo baada ya yeye, mwenyekiti wake, Freeman Mbowe pamoja na viongozi wengine kumtembelea Lema mahabusu anakoshikiliwa tangu Novemba 2, mwaka jana kwa tuhuma za kutoa lugha za uchochezi dhidi ya Rais John Magufuli.

Lema amekuwa akikwama kupata dhamana kutokana na sarakasi za kisheria zilizosababisha upande wa utetezi uende hadi Mahakama Kuu katika kuhakikisha anapata haki hiyo, lakini hadi sasa bado vita hiyo ya kisheria haijaisha.

Lissu amewaambia waandishi wa habari mjini Arusha kwamba wataongeza nguvu ya mawakili wa Chadema katika kesi hiyo kila itakapokuwa ikitajwa mahakamani.

Pia, watakiandikia Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS) barua rasmi kukitaka kitoe tamko kwa namna yoyote ili kiseme katika kesi ya Lema kipo upande upi na kama kikisema hakihusiki, basi hakutakuwa na chama cha wanasheria nchini na wakiona kuna hoja, basi watawataka watoe mawakili waliopo Arusha kusaidia kesi zinazomkabili Lema.

 “Hawa wanasheria wasijidai hamnazo wakati mbunge wao yupo mahabusu. Tutawaambia wawepo mahakamani kwa kuwa wananchi  wa kawaida hawaruhusiwi kuja kusikiliza kesi hiyo, basi wajae wanasheria,” amesema Lissu.

Awali, Mbowe amesema chama na viongozi waliamua kwenda kumuona Lema na familia yake kwa kuwa yupo mahabusu kinyume na haki za binadamu.

“Lema ana moyo mkuu sana na amejifunza mambo mengi kwa mujibu wa maelezo yake. Anasema wapo mahabusu asilimia 70 wenye makosa yanayostahili kupewa dhamana, lakini hawajapewa,” amesema.

Tazama show ya Diamond kwenye ufunguzi wa AFCON 2017

$
0
0
Jumamosi hii Diamond Platnumz na dancers wake, akishirikiana na wasanii wengine akiwemo Mohombi na Lumino, walitumbuiza kwenye ufunguzi wa kombe la AFCON 2017 nchini Gabon. Tazama video hiyo chini.

AFCON Yaanza kwa sare sare

$
0
0
Michuano ya Kombe la Mataifa Afrika (AFCON 2017) imeanza usiku wa jana kwa kushuhudia sare mbili ikiwemo ya mwenyeji Gabon ambaye amelazimishwa sare ya bao 1-1 na Guinea Bissau katika mchezo wa ufunguzi

Guinea Bissau walisawazisha bao la Aubameyang lililofungwa dakika ya 51 kunako dakika ya 89 kupitia Soares

Katika mchezo wa pili, Cameroon pia imelazimishwa sare ya bao 1-1 na Burkina Faso.

Leo zinapigwa mechi mbili ya kundi B, ambapo saa 1:00 jioni Algeria inakipiga na Zimbabwe huku Tunisia ikikipiga na Senegal saa 4:00 Usiku.

Haya ndiyo makundi

Matokeo ya Kidato cha Pili Yatangazwa....... St. Franscis, Kilimanjaro Islamic na Kaizerege Zaongoza

$
0
0
Baraza la Mitihani nchini – NECTA limetoa matokeo ya mitihani ya upimaji kwa wanafunzi wa darasa la nne kwa shule zote za msingi nchini pamoja na ule wa kidato cha pili kwa wanafunzi wa shule za sekondari yanayoonesha ufaulu kuongezeka kwa 1.9%.

Katibu Mtendaji wa Baraza lza Mitihani nchini Dkt Charles Msonde ndiye aliyetoa taarifa hiyo leo jijini Dar es Salaam ambapo katika hali isiyo ya kawaida, shule tisa kati ya kumi zilizofanya vibaya katika mtihani wa kidato cha pili nchini, zimetoka mkoani Mtwara kama zinavyoonekana hapa

Amesema ufaulu umeongezeka kwa asilimia 1.9 kutoka 89.12% mwaka 2015 hadi kufikia 91.02% mwaka 2016 ambapo wanafunzi 372,228 wamepata alama zinazowawezesha kuingia kidato cha tatu huku wanafunzi 36,737 wakishindwa kufikisha alama hizo.

Shule ya St. Francis Girls ya Mbeya imeongoza katika shule 10 bora kitaifa katika matokeo ya mtihani wa kidato cha pili mwaka 2016

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, idadi ya watahiniwa waliopata ufaulu mzuri wa madaraja ya I, II, na III ni 178,115 sawa na asilimia 43.55

Kuhusu ufaulu wa masomo, amesema, katika masomo ya Civics, History, Geography, Kiswahili, Phiysics, Chemistry, Chemistry, Biology na Basic Mathematics umepanda ikilinganishwa na mwaka 2015.

Aidha ufaulu kwa somo la English Language pekee ndio ambao umeshuka ikilinganishwa na mwaka 2015.

Somo lililofanyika vizuri zaidi ni Kiswahili ambapo asilimia 90.06 ya wanafunzi wote, wamefaulu na soko lenye ufaulu wa chini zaidi ni Basic Mathematics ambapo asilimia 21.55 wamefaulu.

Mwanafunzi aliyefanya vizuri zaidi ni Teckla Erasmo Haule kutoka Canosa ya Dar es Salaam akifuatiwa na Joseph Fabian Kalabwe wa Kwema Modern ya Shinyanga na Mirable Rayner Matowo wa Canosa ya Dar es Salaam.

Katika wanafunzi 10 bora kitaifa, wanafunzi 9 ni wasichana, na watano kati yao wanatoka Feza Girls.

Matokeo ya wanafunzi 31 yamefutwa baada ya kubainika kuwa walifanya udanganyifu
.


******

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatatu Ya January 16

Mazombi Yavamia ofisi za CUF Zanzibar......Yapora Mali na Kujeruhi Watu

$
0
0
Watu wasiojulikana maarufu kama mazombi wameivamia ofisi ya Chama cha Wananchi (CUF) katika Jimbo la Dimani Wilaya ya Magharibi B. 

Katika tukio hilo lililotokea saa 6.30 usiku wa kuamkia jana, inadaiwa mazombi hayo yalipora mali, kujeruhi watu na kuwateka wengine wa nyumba jirani na ofisi hiyo. 

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi, Hassan Nassir Ali alithibitisha kuwepo kwa tukio hilo huku CUF wakitaka uchunguzi uanze mara moja kuwabaini wahalifu.

 “Ni kweli taarifa tunazo za watu kuvamia ofisi hiyo ya CUF na kuwapiga pamoja na kuwahujumu watu na huo ni uharamia unaoripotiwa mara kwa mara,” alisema Kamanda Ali. 

Katika tukio hilo, watu hao walioripotiwa kuwa na bunduki na silaha za jadi kama mashoka, mapanga, mashanuo, chupa, spoku za baiskeli na nyundo, walidaiwa kuvunja milango ya jengo la ofisi hiyo katika kijiji cha Bweleo kabla ya kutembeza kipigo kwa majirani na kuondoka na vitu kadhaa. 

Katika tukio hilo inadaiwa mazombi walitoweka na watu kadhaa akiwamo Mwenyekiti wa CUF Tawi la Bweleo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazee wa chama hicho Wilaya ya Magharibi, Juma Ali Juma.

 Akilaani tukio hilo, Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mahusiano ya Umma wa CUF, Salim Abdallah Bimani alisema,“Huu ni uvunjifu wa amani na tunataka Rais John Magufuli iwapo anayo nia ya dhati afuatilie hujuma hiyo ambayo watekelezaji wake wanajulikana lakini hawakamatwi.” 

Bimani alisema, “Mazombi wameshawapiga sana wananchi hasa wafuasi wa CUF ambao hawana hatia, wengine mpaka walipo-teza maisha, wameshawapiga watu na kuwajeruhi vibaya na pia kuwaibia watu mali zao na hatuoni hatua yoyote ikichukuliwa.” 

Bimani alisema, “Tunamwambia Rais Magufuli kwa mujibu wa Katiba yeye ndiye mwenye mamlaka ya kuwalinda raia wote wa nchi hii, achukue hatua.” 

Naibu Mkurugenzi wa Haki za Binadamu wa CUF, Pavu Juma Abdalla aliwataja waliojeruhiwa kutokana na vipigo vikali kuwa ni pamoja na Juma Shani Mwita, Ali Saleh Shani, Kessi Khatib na Ame Mahmoud, wote wakazi wa Bweleo. 

Pavu alisema kuwa tukio hilo liliripotiwa katika Kituo cha Polisi cha Fumba na wahusika walipewa RB Na.18/2017. 

Kwa mujibu wa Mkurugenzi huyo inadaiwa kuwa miongoni mwa mali walizotoweka nazo ‘mazombi’ kutoka ndani ya ofisi hiyo, ni simu nne, fedha taslimu Sh300,000, viti 20, kifaa cha kudhibiti umeme, friji na bendera na mlingoti wake. 

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi, Hassan Nassir Ali alisema, “Ni kweli taarifa tunazo za watu kuvamia ofisi hiyo ya CUF na kuwapiga pamoja na kuwahujumu watu na huo ni uharamia unaoripotiwa mara kwa mara.” 

Nassir alisema,“Pamoja na juhudi tunazozichukua ili kuukomesha kwa kushirikiana na vikosi vingine, inaonekana hauwezi kuondoka kwa mara moja.” 

Alisema kuwa jana walifanikiwa kuwashikilia watu wawili ili kusaidia polisi wakati ambapo jeshi hilo likiendelea na upelelezi. 

Shambulio hilo lilitendeka saa chache baada ya makamu mwenyekiti mstaafu wa CUF, Juma Duni Haji na Mbunge wa Ubungo (Chadema), Saed Kubenea kuwasili Dimani ili kuendelea na kampeni za kumnadi mgombea wao, Abdulrazaq Khatib Ramadhan.

NSSF Yaanza kutekeleza Agizo la Rais Magufuli La Kujenga Viwanda Badala ya Majengo

$
0
0
Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) katika kuhakikisha inatatua changamoto ya ukosefu wa ajira hasa kwa vijana umeamua kuachana na uwekezaji wa majengo makubwa na badala yake imeanza kuelekeza nguvu katika kufufua viwanda. 

NSSF imeazimia kuunga mkono malengo ya Rais John Magufuli ya kukuza uchumi kwa kufufua viwanda na kwa kuanzia mfuko huo umeamua kufufua viwanda vya usagishaji vilivyokuwa katika mikoa ya Iringa, Mwanza, Dodoma na Morogoro. 

Hivi karibuni, Rais Magufuli aliagiza mifuko hiyo kuachana na ujenzi wa majengo badala yake ikijike katika ujenzi wa viwanda. 

Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji wa NSSF, Bathon Mmuni alisema hayo mjini Morogoro katika mkutano uliowakutanisha wadau wa mfuko huo kutoka taasisi za Serikali na binafsi ili kujadili masuala mbalimbali kuhusiana na mfuko huo. 

“Lazima fedha wanazochanga wanachama zizalishe haziwezi kukaa tu, uwekezaji ni moja ya faida kwa mwanachama wetu, hivyo lazima tubadilishe uwekezaji ili kupata faida,” alisema. 

Mmuni alisema kwa muda mrefu nchi imekuwa na changamoto ya ajira hasa kwa vijana, hivyo wameamua kufanya uwekezaji upande mwingine ikiwa katika kufufua na kujenga viwanda.

 Alisema ili kumsaidia Rais Magufuli katika kukuza uchumi, mbali na usagishaji wanaelekeza nguvu katika viwanda vya sukari. 

Alisema mfuko huo pia unalenga kuwawezesha Watanzania kupata ajira, hususani kwa vijana na kwa kuanzia shirika litaanza na ujenzi wa kiwanda cha sukari katika eneo la Mkulazi kwa kushirikiana na Mfuko wa Pensheni wa PPF kupitia kampuni tanzu ya Mkulazi Holding.

 Kaimu Mkurugenzi wa Fedha wa NSSF, Tikyeba Alphonce alitaja baadhi ya changamoto zinazoukabili mfuko huo kuwa ni baadhi ya waajiri kuchelewa kuwasilisha fedha za wanachama.

Mkuu wa Kanisa la KKKT Aonya Upungufu wa Chakula Nchini...........Lowassa, CHADEMA Waahidi Kugawa Chakula Kwa Wananchi

$
0
0
Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk Frederick Shoo ameiomba Serikali kufanya tathmini ya haraka kubaini upungufu wa chakula nchini uliosababishwa na ukame wa muda mrefu. 

Akizungumza wakati wa ibada ya kumweka wakfu Askofu wa Dayosisi ya Meru, Elias Nassari katika Usharika wa Usa River, Wilaya ya Arumeru alisema kuwa Serikali haitakiwi kungoja hadi watu wafe ndiyo waanze kutafuta chakula. 

Dk Shoo ametoa kauli hiyo siku moja baada ya Mwenyekiti wa Baraza la Maaskofu Katoliki (TEC), Tarcisius Ngalalekumtwa kuwaandikia maaskofu wote wa kanisa hilo kuwataka waumini wao wafanye maombi, hija, mfungo kwa lengo la kukabiliana na ukame unaolikabili taifa. 

Vilevile, hivi karibuni Baraza la Waislamu Tanzania (Bakwata) lilitoa wito kama huo kwa waumini wake, huku Serikali ikisisitiza kuwa hakuna njaa nchini na kuwa haitatoa chakula cha msaada. 

Askofu Shoo aliitaka Serikali iwajibike kufanya tathimini za haraka ili kubaini watu walioathirika na njaa pamoja na kujua idadi kamili ya familia pamoja na kaya zitakazoathirika na njaa ili kupata kiwango sahihi cha misaada ya chakula kitakachoitajika nchini.

 “Mikoa ya Kaskazini njaa ni tishio, kuna familia tunajua hazina chakula na tumeanza kutoa misaada,” alisema Dk Shoo. 

Hata hivyo, alisema kama kanisa wataendelea kufanya maombi ya mvua lakini ameitaka Serikali kuchukulia suala la ukame kwa umakini kwa kuwa viashiria vya kuwepo na njaa nchini vimeanza kuonekana. 

Awali, akizungumza kwenye ibada hiyo, Dk Shoo aliwataka viongozi wa dini na taasisi mbalimbali kutokuwa na kiburi pindi wanapopata madaraka badala yake wawatumikie waumini na wananchi kama walivyopewa dhamana hiyo. 

“Kiburi ni tishio sana hasa pale kiongozi atakapoonyesha, tuombe Mungu sana tabia hiyo isiwepo kwa viongozi wetu wa makanisa na taasisi mbalimbali nchini,” alisema Dk Shoo katika ibada iliyohudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kisiasa. 

Viongozi waliokuwapo ni Waziri Mkuu mstaafu, Mizengo Pinda, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo, Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na Meya wa Jiji la Arusha, Calist Lazaro na wabunge Lazaro Nyalandu (Singida Kaskazini) na Joshua Nassari wa Arumeru Mashariki. 

Alipopata fursa ya kuzungumza, Gambo ambaye alimwakilisha Rais John Magufuli aliyataka makanisa yote nchini kuwashauri wananchi wake kuweka akiba ya chakula ili kukabiliana na ukame uliopo kwa sasa. 

Pia aliwataka wawashauri wananchi kupanda mazao ambayo yanastahimili ukame ili kuepusha tishio la njaa linalotokana na ukame na wakulima ambao wanasafirisha mazao nje ya nchi kuacha mara moja. 

Kuhusu migogoro ya ardhi inayoendelea nchini, Gambo alizitaka taasisi za kidini kuyalinda maeneo yao akisema kumezuka mtindo kwa baadhi ya watu kuingilia maeneo ya taasisi hizo. 

Akitoa shukrani baada ya kusimikwa, Askofu Nassari aliwataka viongozi mbalimbali wa kidini kuhakikisha malengo ya kanisa yanatimia. 

Pia alisema atashirikiana na viongozi wa kisiasa na kijamii kuhakikisha changamoto mbalimbali za kijamii zinatatulika. 

Chadema kugawa chakula 
Wakati huohuo, Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Edward Lowassa alisema kwa kuwa Serikali haina utaratibu wa kutafuta ufumbuzi wa tatizo la chakula nchini, chama chake kitaandaa utaratibu wa kuhakikisha chakula kinapatikana. 

Alisema Chadema ina uwezo wa kuomba chakula hata kutoka nje ya nchi ili kuhakikisha hakuna mwananchi atakayepoteza maisha kwa tatizo hilo. 

Alisema hayo katika hotuba yake aliyoitoa mjini Bukoba kwa viongozi wa chama hicho kuanzia ngazi ya matawi hadi wilaya. 

Alisema jambo kubwa linalomvutia kwa Rais mteule wa Marekani Donald Trump ni uwezekano wa kuwabana viongozi wa Afrika wanaochezea demokrasia.

 “Nawaambia viongozi wa dunia wajue demokrasia ni lazima ipewe nafasi yake katika nchi za Kiafrika na si kuacha iendelee kuchezewa,” alisema Lowassa aliyegombea urais akaibuka wa pili nyuma ya Rais Magufuli mwaka jana. 

Pia, Lowassa aliwaeleza kuwa haina maana kusema kuna  amani na utulivu wakati hakuna demokrasia na kudai kinachoendelea nchini kwa sasa ni kuwajenga hofu wananchi. 

“Kinachofanyika hivi sasa ni kujenga watu hofu na kupandikiza chuki, kufanya hivyo ni kujenga mazingira ya udikteta,” alifafanua Lowassa. 

Pia, alikosoa matamko yanayotolewa na Rais Magufuli akisema haoni kama yanazingatia ushauri wa wataalamu wengine. 

Alidai kuwa hakuna sababu ya kujivunia ununuzi wa ndege mpya wakati kuna matatizo mengine sugu yanayowatesa Watanzania.

 “Rais anatakiwa kutumia wataalamu kabla ya kutoa misimamo yake sioni sehemu anaposhauriwa na mawaziri, sioni cabinet inayomshauri kuhusu suala la njaa,” alisema Lowassa aliyewahi kuwa waziri mkuu. 

Alisema ununuzi wa ndege ungesubiri na badala yake fedha hizo kutatua tatizo la maji linalowakabili wananchi wengi huku akirejea alivyoshughulikia tatizo hilo akiwa Waziri wa Maji. 

Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho Profesa Mwesiga Baregu alisema nguvu kubwa inayotumika kubana vyama vya upinzani inatia shaka na kujenga hofu kwa wananchi.

 Alitoa mfano wa nguvu kubwa iliyotumika kuzuia mikutano ya Ukuta kuwa ni dalili za kutojiamini kwa Serikali kiasi cha kuvuruga utaratibu wa kidemokrasia.

Zitto Kabwe: Watanzania wakifa njaa Tutaiwajibisha Serikali kwa mujibu wa Katiba ibara ya 46A

$
0
0
Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe amesema endapo Mtanzania yeyote atakufa kwa njaa watachukua jukumu la kumwajibisha Rais kwa kusema waziwazi kwamba hajatimiza wajibu wake.

Akihutubia mkutano wa kampeni katika Kata ya Kijichi jana,  kiongozi wa chama cha ACT-Wazalendo, Zitto alisema, “Tunamkumbusha Rais kwamba kwa mujibu wa ibara ya 46A ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambayo yeye amekula kiapo kuilinda, kuihifadhi na kuitetea, Bunge laweza kumshtaki kwa kosa la mwenendo unaodhalilisha kiti cha Rais. "

Kauli hiyo ya Zitto ilitokana na msimamo wa Rais Magufuli kuwa hakuna njaa nchini na kwamba Serikali haitatoa chakula cha msaada, huku makundi mengine ya wananchi, wakiwamo  wanasiasa na viongozi wa dini wakisema kuna upungufu wa chakula uliotokana na ukame. 

Zitto ambaye kabla ya kuhutubia alipita nyumba za jirani na uwanja akisalimia, alisema, “Tumesema hili la njaa katika kutekeleza wajibu wetu, Rais na Serikali wamejibu na kufunga mjadala. Wakati utaamua na kuonyesha mkweli nani na mpiga propaganda nani.” 

“Tunamwambia Rais kwamba, Mtanzania yeyote akifa kwa njaa kwa sababu Serikali imeshindwa kutekeleza wajibu wake, Watanzania tutapaswa kuchukua hatua, Katiba inatulazimisha kumtoa Rais madarakani. 

“Jambo moja ni muhimu sana, Rais anapaswa kujua kuwa anafanya kazi kwa mujibu wa Katiba ya nchi. Na Katiba imetoa wajibu wa lazima kwa Serikali kulinda watu. Ndio kazi ya Serikali – kulinda wananchi pale ambapo yanatokea majanga ambayo yanazidi kimo wananchi hao,” aliongeza. 

Alisema Rais yupo chini ya Katiba na kwa idadi ya wabunge wa upinzani waliopo bungeni, na wakiamua kusimama na wananchi kulinda Katiba, anaweza kuwa wa kwanza wa nchi yetu kutolewa hoja ya kutokuwa na imani naye bungeni. 

“Katiba inahitaji asilimia 20 tu ya wabunge kuwasilisha hoja hiyo bungeni,” alisema. 

Mbunge huyo alitoa wito kwa Watanzania bila kujali vyama vyao, kuweka rekodi ya hali ya chakula popote walipo na kuweka takwimu ya maafa yeyote yanayotokana na njaa. 

Alimtaka Rais atumie lugha ya kujenga matumaini badala ya kujenga hofu kwenye jamii, aache kuonea watu kwa kutumia madaraka yake, na akumbuke cheo ni dhamana. 

Kiongozi huyo alisema ameamua kusema hayo kwa sababu baada ya siku saba hawatakuwa na nafasi ya kuzungumza majukwaani kama viongozi wa vyama vya siasa kwa sababu ya zuio lisilo la kikatiba la kuzuia mikutano ya hadhara. 

Hata hivyo, sheria inasema janga la njaa linaweza kutangazwa na Rais tu na si mtu mwingine.

Waumini Anglikana Nusura Wachapane Ngumi Kanisani

$
0
0
Baadhi ya waumini wa makanisa ya Anglikana   Dar es Salaam, nusura wazichape jana.

Hiyo ni baada ya mapadri wao kutaka kusoma waraka wa Halmashauri ya Kudumu ya Dayosisi ya Dar es Salaam unaomtetea Askofu wa Dayosisi hiyo, Dk. Valentino Mokiwa, ambaye ametakiwa kujiuzulu kwa sababu ya kashfa mbalimbali.

Waraka huo uliokuwa unasomwa jana ulilenga kujibu  uliotolewa na Askofu Mkuu wa Kanisa hilo nchini,  Dk. Jacob Chimeledya, ambao uliorodhesha tuhuma zilizokuwa zikimkabili Dk. Mokiwa ukisema kwa sasa dayosisi hiyo itakuwa chini ya Askofu Mkuu.

Baadhi ya makanisa ya Dar es Salaam, Januari 8, mwaka huu yalisomewa waraka huo wa Askofu Mkuu, Dk. Chimeledya huku mengine yakiwa hayajasomewa licha ya kutakiwa kufanya hivyo na ngazi ya taifa.

Jinsi ilivyokuwa
Katika baadhi ya makanisa, jana vurugu zilizuka mapadri walipoanza kusoma waraka wa Halmashauri ya Kudumu ya Dayosisi ya Dar es Salaam.

Hapo ndipo  baadhi ya waumini walipogoma wakisema wanataka kwanza kusomewa ule wa Askofu Mkuu wajue tuhuma zinazomkabili Dk. Mokiwa.

Katika Kanisa la Mtakatifu Batholomayo   Ubungo, hali ilikuwa mbaya zaidi baada ya baadhi ya waumini   kupiga kelele na kwenda kumzimia kipaza sauti Padri wa Kanisa hilo, James Hiza, huku wengine wakinyanyuka kwenye viti wakimtaka  kutokuusoma waraka huo wa Mokiwa.

Kutokana na kelele hizo ndani ya kanisa,   mmoja wa waumini hao alikwenda kuzima mfumo wa umeme na kusababisha vipaza sauti kutofanya kazi.

Hata hivyo, hatua hiyo  haikusaidia kwa kuwa Padri huyo   alikuwa akiendelea kusoma waraka huo.

Kuona hivyo, baadhi ya waumini walisikika wakisema ‘kama unasoma huo hakikisha unasoma waraka zote mbili’.

Hapo Katibu wa Kamati Tendaji ya Kanisa, John Mapunda, alisimama akiwa ameshikilia waraka wa Askofu Mkuu nao  kumtaka ausome mbele ya waumini na kuuacha aliokuwa akiusoma.

Hata hivyo, Padri huyo aliendelea kusoma waraka aliokuwa nao na kutowajali waliokuwa wakimtaka kuacha kusoma waraka huo.

Mbali na katibu huyo wa kanisa, pia mzee wa makamo alikwenda kumsihi Padri huyo kutosoma waraka huo.

Lakini juhudi zao hazikuzaa matunda kwani alisoma waraka huo mpaka mwisho ingawa waumini waliendelea kupiga kelele muda wote bila kumsikiliza.

Baada ya kumaliza kusoma waraka huo Padri,  Hiza alirudi na kukaa katika nafasi yake  huku akiwataka waumini kutulia.

Waondoka na sadaka
Baada ya kumaliza kusoma waraka huo na vurugu kutulia, baadhi ya waumini ambao hawakuridhika na yaliyotokea walionekana kususa shughuli nyingine ikiwa ni pamoja na kutoa sadaka.

Waumini hao licha ya kuwa na bahasha maalumu ambazo hutumika kutolea sadaka, muda wa matoleo ulipofika, waliendela  kukaa kwenye viti vyao wakiwa na bahasha zao.

Pia wengine walisusa kushiriki Meza ya Bwana ingawa  wahudumu waliwasihi wasifanye hivyo.

“Tusimfanyie hasira Mungu, hata kama mmekasirika vumilieni tuendelee na ibada yaani hata kupokea mwili hamtaki?” aliwauliza  mhudumu wa kanisani humo.

Baada ya ibada, Katibu wa Kamati Tendaji,  Mapunda aliwaambia waandishi wa habari   kuwa  walikuwa wamefanya kikao na kukubaliana kutosoma waraka wowote kwa sababu Jumapili iliyopita hawakuusoma   ule uliotolewa na Askofu Mkuu. Dk. Chimeledya.

“Waraka wa Baba Askofu Chimeledya hakuusoma wiki iliyopita, alisema hajaupata kumbe ulikuwapo.

“Siku chache badaye na Askofu Mokiwa ambaye ameshafukuzwa katoa waraka wake.

“Huo ndiyo alitaka kuusoma tukamwambia kwa kuwa ule wa kwanza haukusomwa kanisani na huu usiusome au usome zote ili tusiingie katika mgogoro huu.  Alikubali lakini kafika madhabahuni akatugeuka,” alisema Mapunda.

Padri Hiza alipofuatwa na waandishi  kuzungumzia suala hilo alisema, “Hili suala limefikia ngazi ya juu  ya dayosisi, mimi siwezi kuliongelea kwa kuwa si msemaji wa dayosisi.”

Wakati hayo yakiendelea, polisi walikuwa wametanda  nje ya kanisa hilo.

Baada ya vurugu kutulia kanisani, polisi hao walionekena wakizungumza na Katibu wa Kamati ya Utendaji ya Kanisa, Mapunda na baadaye wakaondoka kwenye eneo hilo.

Hali ya sintofahamu ilitokea pia katika Kanisa la Hollyghost Kimara Mbezi ambako mgogoro wa kutaka kusoma waraka wa Dk. Mokiwa au usisomwe, uliibuka na mwisho Padri akaamua kuacha kuusoma.

Kabla ya Padri kuacha kuusoma, zilizuka  vurugu za hapa na pale kiasi cha   watu kufikia hatua   ya kutaka kupigana.

Katika Kanisa la Mtakatifu Mariam Padre wa kanisa hilo alitaka kuusoma waraka wa Mokiwa lakini waumini walikuja juu na kuusoma wa Askofu Mkuu Dk. Chimeledya.

Sumaye: Rais Magufuli Anatekeleza Sera za CHADEMA

$
0
0
Wakati Rais wa Awamu ya Tano, John Magufuli akitekeleza masuala mbalimbali aliyowaahidi Watanzania, ikiwa ni pamoja na kurejesha uwajibikaji na kupambana na ufisadi, Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye amesema hashtushwi na utendaji huo wa rais, kwani amekuwa akitumia baadhi ya hoja na mikakati ya Chadema kuongoza nchi.

Akizungumza wakati wa kumnadi mgombea wa udiwani katika kata ya Isagehe wilayani Kahama, Sumaye ambaye alijiunga Chadema Agosti mwaka juzi baada ya kuachana na CCM, alisema mengi anayofanya rais ni sera za Chadema ila chama hicho cha upinzani hakikuwa na sera ya kubana fedha.

Hata hivyo, Sumaye ambaye ni mjumbe wa kamati kuu ya Chadema hakuweka wazi hoja na mikakati ya Chadema inayotekelezwa na Rais Magufuli ambaye tangu aingie madarakani ameweka msimamo katika suala la kubana matumizi ya Serikali, kudhibiti watumishi hewa na safari za ndani na nje zisizo na tija na rushwa.

Katika mkutano huo ambao pia Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa alihutubia, Sumaye alisema kama wananchi, wangemchagua Lowassa kuwa Rais, angewaletea neema ya hali ya juu kwa kuwa angekuwa na misingi katika sera anazozitekeleza.

“Mmechagua Rais mzuri (Magufuli), lakini anafuata sera za chama chetu (Chadema) ambazo tungezitumia kama tungekuwa madarakani. Wananchi wa Kanda ya Ziwa mnatakiwa kumtumia Rais Magufuli ili kufanikisha malengo yetu,” alisema huku akisisitiza kuwa hata Lowassa wananchi wangeweza kumtumia kufanikisha malengo yao.

Huku akimnadi mgombea udiwani wa kata hiyo, John Luzinga, Sumaye aliwataka wananchi kutofanya makosa tena ya kuichagua CCM, ili wasije kujuta kwa maelezo kuwa watalazimika kuchagua diwani mwingine mwaka 2020.

Alisema Chadema kinaendeshwa kwa kufuata misingi ya demokrasia, huku akikosoa vyama kubanwa wakati nchi iriuridhia mfumo wa vyama vingi vya siasa.

Akizungumzia sababu za kuhama CCM, alisema kulitokana na nchi kukumbwa na hali mbaya ya uchumi sambamba na kukosekana kwa utawala bora.

“Serikali pamoja na kubana matumizi, hali ya uchumi imekuwa mbaya. Inatakiwa kuachia fedha ili kuwafikia wananchi waweze kumudu ugumu wa maisha unaowakabili kwa sasa. Haiwezekani kila Serikali isijifunze katika hili wakati hata wataalamu wanazungumza na kushauri masuala mbalimbali,” alisema Sumaye.

Alisema kitendo cha halmashauri tatu za wilaya ya Kahama kuongozwa na CCM, huku diwani mmoja tu ndio akiwa wa Chadema, kitawafanya wananchi hao kukosa watu sahihi wa kuwasemea mambo yao.

Uchaguzi katika kata hiyo utafanyika Januari 22 sambamba na kata nyingine 21 katika maeneo mbalimbali nchini.

UVCCM yawataka wananchi kuwapuuza Lowassa na Sumaye........Yadai Si Waadilifu, Wanasaka Madaraka

$
0
0
Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM), umewataka watanzania kuwapuuza Waziri Mkuu Mstaafu, Fredrick Sumaye na Waziri Mkuu aliyejiuzulu Edward lowassa kuwa wanaota ndoto za mchana .

Umoja huo umesema kuwa kuiombea CCM kushindwa uchaguzi mkuu wa mwaka 2020 ni sawa na kujivisha akili za Abunuasi,ambaye mipango haitimii, aidha umoja huo umesema upinzani  wa Tanzania haukubaliki mbele ya wananchi wazalendo.

Hayo yamesemwa na Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM Shaka Hamdu Shaka, alipokuwa akihutubia katika mkutano wa kampeni katika kata ya kiwanja cha ndege mkoani Morogoro.

Alisema kuwa wananchi hawana budi kuwapuuza Lowassa, Sumaye na chama chao kwa sababu sio viongozi waadilifu bali ni wasaka madaraka.

“Watanzania wapuuzeni watu hawa kwa sababu Sumaye ni Pwagu na mwenzake Lowassa ni pwaguzi, wanahaha usiku na mchana kusaka madaraka wakati wananchi wanawajua sio waadilifu na hawaaminiki katika jamii,”alisema Shaka.

Mkutano huo pia ulihudhuriwa na mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Morogoro Mjini,Fikiri Juma na Kaimu Katibu Mkoa wa Morogoro, Kulwa Milonge.

Mwanza: Mkuu wa Mkoa John Mongella Awasimamisha Watumishi Watatu Kwa Ufisadi wa Milioni 300

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongela amewasimamisha kazi watendaji watatu wa  Halmashauri ya Wilaya ya Magu mkoani hapa, ili kupisha uchunguzi wa matumizi ya fedha zaidi ya sh. milioni 300, zilizotolewa na Benki ya Dunia kwa ajili ya maendeleo wilayani humo.

Waliosimamishwa kazi ni pamoja na mweka hazina, mchumi na Mhandisi wa Halmashauri hiyo. Kwa pamoja wanadaiwa kubadili matumizi ya fedha za kutekeleza miradi ya SEDEP, zilizotolewa na benki hiyo kwa ajili ya kuboresha mazingira ya kusomea wanafunzi wa shule za sekondari.

Akizungumza akiwa katika ziara wilayani humo juzi, Mongela alisema ni lazima uchunguzi wa kina ufanyike, kwani thamani ya vyumba vya madarasa na vyoo vilivyojengwa kutokana na fedha za mradi huo, hailingani na fedha zilizotumika.

“Kunzia Jumatatu (leo), kuna timu ya wakaguzi itakuja hapa Magu kukagua na kuchunguza thamani ya fedha zilizotumika kwenye miradi hii ambayo nimeikagua. Miradi hii inajumuisha miradi ya ujenzi wa vyumba vya madarasa na vyoo ambayo inaonyesha wazi kuna uchakachuaji umefanyika,”alisema Mongela.

Mkuu Wilaya ya Magu, Hadija Nyembo alisema mambo yaliyokwamisha miradi ya ujenzi huo ni kuelekeza fedha hizo katika ujenzi wa maabara tofauti na matumizi ya fedha yalivyopangwa.

Hata hivyo, mabadiliko ya matumizi ya fedha hizo, yanadaiwa kuwa yalifanyika bila  kuthibitishwa na Wizara ya Fedha na Mipango ili yapewe baraka kwa kuwa Wizara hiyo, ndio yenye mamlaka ya kutoa idhini ya mwisho ya matumizi ya fedha za Umma.

Kutokana na sababu hizo mkuu huyo wa Mkoa aligoma kuzindua vyumba viwili vya madarasa vya shule ya msingi Nyanguge vilivyojengwa kupitia kiasi hicho cha fedha, kutokana na madai kuwa vyumba hivyo pamoja na ujenzi wa vyoo vimejengwa chini ya kiwango.

Zaidi ya Watu 32 Wafariki Dunia Baada ya Ndege ya Mizigo Kuanguka na Kugonga Nyumba za Watu

$
0
0
Watu zaidi ya 32 wamefariki baada ya ndege ya kubeba mizigo ya Uturuki, iliyokuwa safarini kutoka Hong Kong kuangukia nyumba za watu karibu na mji wa Bishkek nchini Kyrgyzstan.

Taarifa zinasema wengi wa waliokufa ni watu waliokuwa ardhini, ndege hiyo aina ya Boeing 747 ilianguka karibu na uwanja wa ndege wa Manas, takriban kilomita 25 kutoka mji mkuu Bishkek,

Nyumba zaidi ya 15 zimeharibiwa na watoto kadha wanaripotiwa kuwa miongoni mwa waliofariki. Imeelezwa kuwa hali ya hewa ilikuwa mbaya na kulikuwa na ukungu, ingawa chanzo hasa cha ajali hiyo hakijathibitishwa.

Kuna taarifa zinasema kuwa kwenye ndege hiyo kulikuwa na wahudumu wanne na mhudumu mmoja wa ndege amenusurika, watu kadhaa wamepelekwa hospitalini wakiwa na majeraha.

Msemaji wa huduma za dharura nchini humo Muhammed Svarov, ameambia AFP kwamba huenda idadi ya waliofariki ikaongezeka na juhudi za kuwasaka walionusurika zinaendelea.

Nauli ya Dar - Dodoma kwa Bombadier yatajwa....... Route ya Kwenda Dodoma Yazinduliwa Rasmi

$
0
0
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amezindua safari za ndege za Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) kutoka jijini Dar es Salaam kwenda Makao Makuu ya Nchi, Dodoma.

Akizindua safari hizo leo amesema safari hizo zitawezesha wafanyabiashara na wananchi wengine kutoka Dodoma na kwenda katika maeneo mengine kwa urahisi.

“Tuna ndege nzuri. Tuzitumie kwenda katika maeneo mengine kwani gharama zake ni nafuu. Kutoka Dodoma kwenda Dar es Salaam ni sh. 165,000, kwenda na kurudi ni  sh. 299,000,” amesema.

Amesema ndege nyingine kama hiyo inatarajia kuwasili nchini Juni mwaka huu jambo ambalo litaongeza idadi ya safari za ndege hizo nchini na maeneo mengine ya nchi jirani.

Kwa upande wake Kaimu Mtendaji Mkuu wa ATCL. Kapten Richard Shaidi ametumia fursa hiyo kuipongeza Serikali kwa ujio wa ndege hizo na kwamba hiyo ni moja ya mikakati ya Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli ya kufufua ATCL.

“Hivi karibuni tunaanza kwenda nchi jirani. Mwakani tutapata ndege nyingine kubwa itakajayokuwa inafanya safari za masafa ya kati na ya mbali” amesema.

Aidha, Mwenyekiti wa Bodi ya ATCL, Bw. Emmanuel Korosso amesema hivi karibuni shirika hilo linatarajia kuanza safari za kwenda katika miji ya Tabora, Songea, Mtwara, Mpanda, Mafia na Jiji la Tanga.

Akizungumzia kuhusu safari za Dodoma amesema zitafanyika mara mbili kwa wiki, siku ya Ijumaa na Jumatatu. Hata hivyo wanatarajia kuongeza safari hapo baadae.

Naye Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai ametoa wito kwa wakazi wa Dodoma kutumia vizuri fursa hiyo ya safari za ndege za ATCL kwa kuwa utawawezesha kusafiri kwa muda mfupi tofauti na vyombo vingine vya usafiri.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Bw. Jordan Rugimbana ameshukuru kwa uanzishwaji wa safari hizo kwa kuwa zitarahisisha kutoka katika Makao Makuu ya nchi na kwenda katika mikoa mingine nchini.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Waziri Mkuu Mstaafu, John Malecela baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Dodoma akitoka uwanja wa ndege wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam ikiwa ni uzinduzi wa safari za ndege za ATCL kati aya viwanja viwili hivyo, Januari 16, 2017.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Spika wa Bunge, Job Ndugai baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Dodoma akitoka uwanja wa ndege wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam ikiwa ni uzinduzi wa safari za ndege za ATCL kati aya viwanja viwili hivyo, Januari 16, 2017.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwapungia viongozi na wananchi wa Dodoma baada ya kutua kwenye uwanja wa ndege wa Dodoma akitoka uwanja wa ndege wa Julius Kambarage Nyerere jijini Dar es salaam Januari 16, 2017 ikiwa ni uzinduzi wa Safari za ndege za Shirika hilo kati ya viwanja viwili hivi.  
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisafiri kwa ndege ya Bombardier Q400 ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) kutoka uwanja wa ndege wa Julius Kambarage Nyerere kwenda Dodoma Januari 16, 2017. Alikuwa akizindua safari za ndege za ATCL katika viwanja viwili hivyo. Kushoto kwake ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Leonard Chamuriho.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images