Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Kijana afariki dunia baada ya Nyoka wake kupigwa hadi kufa

$
0
0
Mkazi wa Mtaa wa Mateka, Manispaa ya Songea, Denis Komba (26) afariki dunia baada ya nyoka wake aliyekuwa amembeba kwenye mfuko wa jaketi kuuawa na wananchi.

Komba alifariki dunia katika hospitali ya Rufaa Songea mkoa wa Ruvuma (Homso) ambako alilazwa baada ya watu wenye hasira kumuua kwa mawe na fimbo nyoka wake huyo.

Mashuhuda wanaeleza kuwa kabla ya wananchi kumuua nyoka huyo, Komba aliwasihi wasifanye hivyo kwa kuwa wakimuua na yeye angekufa, lakini ombi lake hilo halikusikilizwa.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, siku ya tukio Komba alikodi pikipiki ya Kassian Haule (24) ambaye ni mkazi wa Mpitimbi, yenye namba za usajili MC 724 AKB ili apelekwe nyumbani kwake mtaa wa Mateka.

Akisimulia tukio hilo, alisema alipofika katika eneo la Benki ya Posta ya zamani barabara kuu ya Sokoine, dereva wa pikipiki alihisi kuna kitu kinamtekenya na kumgonga gonga kwa nyuma, ndipo alipogeuka nyuma na kumwona abiria wake amebeba nyoka mkubwa huku amesimamisha kichwa.

Haule alisema, baada ya kumuona nyoka huyo aliruka kutoka kwenye pikipiki na kuanguka pembeni mwa barabara na abiria wake alimwachia yule nyoka ambaye alikimbilia kwenye kalavati la maji.

Aliongeza kuwa ndipo alipopiga kelele za kuomba msaada na kundi la vijana waendesha pikipiki wenzake walifika eneo hilo la tukio kwa lengo la kumsaidia mwenzao juu ya maswahiba yaliyompata hadi kumfanya apige kelele.

Alisema kabla ya vijana hao hawajafanya jambo lolote, Komba aliwaomba vijana hao na watu wengine waliofika katika eneo hilo wasimpige nyoka wake kwani iwapo watampiga na kufa yeye pia atapoteza maisha. Kutokana na maneno hayo, Haule alimtoa nyoka huyo ndani ya kalavati na kwa kushirikiana na vijana wenzake walianza kumpiga nyoka huyo hadi kufa.

Alisema wakati wanampiga nyoka huyo, Komba ambaye ndiye mmiliki wa nyoka huyo naye alianza kulegea kisha akaanguka chini huku akitokwa na mapovu mdomoni na puani.

Habari zinasema kuwa,baada ya Komba kuanguka alikimbizwa hospitali kwa ajili ya kupatiwa matibabu; hata hivyo juhudi za madaktari na wauguzi wa hospitali za kuokoa maisha yake zilishindikana kwani Komba alifariki.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma, Zuberi Mwombeji, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuongeza kuwa mwili wa marehemu haukuwa na jeraha lolote na umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya rufaa Songea.

Alisema nyoka aliyeuawa na wananchi amechukuliwa na idara ya maliasili na uchunguzi zaidi ya tukio hilo unaendelea ili kubaini kiini cha tukio hilo la kuuawa kwa nyoka na kisha mmiliki wake naye kufa. Kamanda Mwombeji alisema, kwa upande wa dereva wa pikipiki yeye anaendelea vizuri na anapatiwa matibabu katika hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Ruvuma.

Aidha Kamanda Mwombeji, ametoa rai kwa wananchi kuacha mara moja kumiliki nyara za serikali zinazoweza kuwaletea madhara kama vile majeraha au vifo.

Dhamana ya Mbunge Godbless Lema Yakwama.....Arejeshwa Gerezani

$
0
0
Mbunge Godbless Lema amerejeshwa tena rumande leo baada ya rufaa yake ya kupinga kunyimwa dhamana kushindikana kusikilizwa kama ilivyokuwa imepangwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Arusha leo.

Rufaa hiyo ya Lema iliyokuwa umepangwa kusikilizwa leo imeshindikana baada ya upande wa Jamhuri kukata rufaa kupinga kuongezwa muda wa kuwasilisha notisi ya rufaa.

Mawakili wa Lema waliomba kuongezewa  muda wa kuwasilisha notisi ya kukata rufaa kupinga kunyimwa dhamana baada ya kushindwa kufanya hivyo katika muda uliokuwa umepangwa awali.

Jaji aliyekuwa anasikiliza kesi ya rufaa hizo Salma Magimbi amesema kuwa mara baada ya upande wa jamhuri kuleta rufaa kwa njia ya maandishi upande wa mshtakiwa Lema wataijibu tarehe 30 Disemba 2016 ambapo tarehe 2 Januari watakutana pande zote kwa ajili ya kufanya majumuisho na maamuzi ya rufaa hiyo yatatolewa tarehe 4 Januari 2017.

Mbunge Godbless Lema ambaye alikamatwa Novemba 2 mwaka huu mjini Dodoma amerejeshwa rumande katika gereza la Kisongo jijini Arusha.

Video: Simu ya Rais yatoa kelele za watu wakifanya mapenzi mahakamani

$
0
0
Moja ya habari ambazo zimeandikwa sana na vyombo vya habari vya kimataifa ni pamoja na hii inayomhusu Rais wa Bolvia Evo Morales.

Rais Evo Morales akiwa mahakamani kwenye kikao pamoja na wanasheria wa kimataifa alianza kuchezea simu yake ambapo ghafla zilisikika sauti za watu wakifanya mapenzi kwenye simu yake. Bonyeza play hapa chini kutazama

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya Diseba 29

Bodi ya Mikopo yaja na mbinu nyingine ya kukusanya madeni kwa wadaiwa sugu

$
0
0
BODI ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imesema kuanzia mwanzoni mwa Januari mwakani, itaanza kuchapisha majina na picha za wadaiwa sugu kwenye vyombo vya habari waliohitimu katika vyuo mbalimbali vya elimu ya juu kuanzia wale wa miaka 10 iliyopita.

Bodi hiyo ilitoa muda wa zaidi ya siku 30 unaoisha kesho Desemba 30, mwaka huu, kwa wadaiwa hao sugu kulipa madeni yao ndani ya muda huo, vinginevyo hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao, ikiwemo kulazimika kulipia gharama za kuwasaka na kuendesha kesi.

Pamoja na hayo, bodi hiyo pia kupitia Sheria ya Bodi ya Mikopo iliyofanyiwa marekebisho hivi karibuni na Bunge, imeanza mkakati wa kuwabana waajiri wasiotimiza wajibu wao kisheria kwa kuunda kikosi kazi cha kuhakiki waajiriwa wasiowasilisha makato na majina ya waajiriwa waliokopa HESLB, na adhabu yao itakuwa ni faini au kifungo cha miezi 36 jela.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Mkurugenzi Mtendaji wa bodi hiyo, Abdul-Razaq Badru, alisema baada ya kuisha kwa muda huo wa siku 30 walioutoa, wadaiwa wote sugu, ambao mpaka sasa hawajajisalimisha wenyewe kwa hiari, kulipa madeni yao wataanikwa hadharani na picha zao.

“Tumeamua kuchukua hatua hii ambayo tunaamini itasaidia watu kuwatambua wadaiwa hawa wa bodi, na kuturahisishia kupata taarifa zao na kuwasaka ili waturejeshee fedha zetu,” alisema Badru.

Aidha, alisema nia ya kuchapisha majina na picha za wadaiwa hao ni kuutangazia na kuutarifu umma juu ya watu wanaokwamisha wanafunzi wengine kukosa fursa ya kupata mikopo ya elimu ya juu kwa kuwa fedha iliyopo bado haitoshelezi.

Alisema bodi hiyo ilitoa muda wa wiki nne kwa wadaiwa hao sugu na baadaye kuwaongezea tena muda wa wiki mbili, unaoishia Desemba 30, mwaka huu, hivyo kinachofuata ni utekelezaji kwa wale walioshindwa kuitumia fursa hiyo ya kujisalimisha.

Mkurugenzi huyo alisema baada ya muda huo kwisha na bodi hiyo kuanza kuchapisha majina na picha za wadaiwa hao, wale watakaopatikana kwa kushindwa kulipa madeni yao, watachukuliwa hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kulipia gharama za usumbufu wa kuwatafuta.

Alisema utaratibu wa kukopesha ni mfumo unaowezesha wanafunzi wengi zaidi, kupata fursa ya kuendelea na masomo yao ya elimu ya juu, hivyo ni vyema wanafunzi wote wanaopata fursa ya kukopa wahakikishe wanalipa kwa muda muafaka uliowekwa kisheria.

Badru alisema kwa mujibu wa marekebisho ya sheria hiyo ya Bodi ya Mikopo, imewaongezea muda wa kuanza kulipa wanafunzi walionufaika na mikopo kutoka miezi sita hadi miaka miwili ili kutoa fursa ya kujipanga na kutafuta ajira.

Aidha, alibainisha kuwa sheria hiyo pia imeongeza kiwango cha makato kwa waajiriwa walionufaika na mikopo ya HESLB kutoka asilimia nane ya mishahara yao hadi asilimia 15.

“Tunawashukuru sana wadau kwa kuwezesha kutoa maoni yao yenye tija kwenye sheria hii katika eneo hili sisi tulipendekeza kiwango cha makato kifikie hadi asilimia 30 na zaidi, lakini kupitia maoni mbalimbali ya wadau wakiwemo wa wabunge walipendekeza kiwango kiwe asilimia 15 tu,” alisema.

Alisema ili kuweza kutimiza lengo la kuhakikisha kila mnufaika na mikopo hiyo aliyeajiriwa analipa deni lake, pamoja na kuwabana wadaiwa, bodi hiyo imeanza mkakati wa kuwabana waajiri wasiotimiza wajibu wao kisheria kupitia marekebisho hayo ya sheria.

“Tumeunda kikosi kazi kinachojumuisha timu ya wataalamu kutoka sehemu mbalimbali nyeti, kitakachoanza kufanya kazi kuanzia Januari 2, mwaka huu, ya kuhakiki kila ofisi ya waajiri sugu ili kubaini kama ama wamewasilisha majina ya wanufaika wa mikopo hii au wanawakata bila kuwasilisha michango hiyo kwa bodi,” alisema.

Alisema waajiri watakaobainika kwenda kinyume na sheria hiyo kwa kutoisaidia bodi kupata waajiriwa wanaodaiwa au kutowasilisha makato yao, wataadhibiwa kwa mujibu wa sheria kwa kulipa faini isiyopungua makato hayo waliyoshindwa kuyawasilisha na endapo watashindwa watakabiliwa na adhabu ya kifungo cha muda wa miezi 36 jela.

“Lakini pia sheria hii imewawajibisha wale waliokopa kuhakikisha wanapeleka wenyewe taarifa zao kwa bodi ili waweze kuwekewa utaratibu wa makato, yeyote atakayebainika kutowasilisha taarifa zake naye atawajibishwa,” alisisitiza.

Halikadhalika, Badru alisema marekebisho hayo ya sheria, pia yamegusa wanufaika wa mikopo hiyo ya elimu ya juu, ambao hawako kwenye mfumo rasmi wa ajira, ambao nao wanatakiwa kurejesha kiasi kisichopungua Sh 100,000 kila mwezi.

Akizungumzia mafanikio tangu bodi hiyo itoe muda wa hiari kwa wadaiwa sugu kulipa wenyewe madeni yao, Mkurugenzi huyo alisema makusanyo ya fedha, yameongezeka kutoka Sh bilioni mbili mpaka nne kwa mwezi hadi Sh bilioni nane.

Alisema tangu muda huo utolewe jumla ya wanufaika 42,700 wamejitokeza wenyewe kwa hiari na kulipa madeni yao huku wengine wakilipa deni lote na wengine wakiyapunguza.

Hadi sasa bodi hiyo ya mikopo ina jumla ya Sh bilioni 300 zilizoiva, inazozidai kwa wadaiwa hao sugu na kati ya fedha hizo ni Sh bilioni 140 pekee ndio zimelipwa.

Kwa mujibu wa HESLB kuanzia Juni, mwaka huu, jumla ya wanafunzi 379,179 wamenufaika na mikopo ya elimu ya juu inayotolewa na bodi hiyo tangu ianzishwe Juni, mwaka 1994 na jumla ya Sh trilioni 2.6 zimeshatolewa kwa wanafunzi hao.

Jumla ya wahitimu wa elimu ya juu wa zamani 238,430 walionufaika na mikopo ya HESLB, wanatakiwa kuanza kulipa madeni yao, ambayo ni kiasi cha Sh trilioni 1.4, baada ya muda waliotakiwa kulipa kwa mujibu wa sheria kuisha.

Hapi Aishika Pabaya Kampuni Ya Zantel.......Yalipa Mapato Zaidi Ya Milioni 687 Ndani Ya Siku 7 Ilizopewa

$
0
0
KAMPUNI ya simu za mkononi ya Zantel Tanzania imelipa zaidi ya Sh milioni 687 baada ya kupewa siku saba na halmashauri hiyo iwe imelipa fedha hizo ambazo zilikuwa za kodi ya pango inazodaiwa na manispaa hiyo.

Fedha hizo zililipwa Desemba 21 na mkataba huo wa zamani unaisha Januari mwakani ambapo Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi amesema wanaandaa mpya wenye viwango vya malipo vya sasa.

Aidha halmashauri hiyo imeamua kuelekeza fedha hizo ambayo ni sh 687,931,040 katika ujenzi wa vyumba vya madarasa 40 katika halmashauri hiyo kwamba kama itaonekana inawezekana kujenga shule nyingine mpya ya sekondari.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Hapi alisema fedha hizo zimelipwa baada ofisi yake kubaini mchezo mchafu uliokuwa umefanywa na watendaji wa halmashauri yake waliokuwepo huko nyuma ambao walificha mkataba kati yake na Zantel.

Aidha aliipongeza Zantel kwa kutii maagizo waliyopewa na kulipa fedha hizo na tayari wamepewa risiti kuonesha kupokea fedha hizo na kwamba watu wote waliohusika katika jambo hilo watachukuliwa hatua za kisheria. 

Alisema baada ya malipo hayo, ameelekeza Manispaa kutumia fedha zote hizo kujenga vyumba vya madarasa katika halmashauri hiyo.

“Takwimu zinaonesha mwaka huu watoto 19,000 walifaulu katika Halmashauri ya Kinondoni waliochaguli kujiunga na Sekondari ni 12,889 na hadi sasa wanafunzi 3,169 hawajapata nafasi katika shule zetu kwasababu ya ufinyu wa madarasa,” alisema Hapi.

Waziri Mkuu Achangia Mabati Ujenzi Wa Zahanati

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewahimiza wakazi wa vijiji saba wilayani Ruangwa waharakishe kufyatua matofali ili waanze ujenzi wa zahanati na yeye atawachangia mabati.

Ametoa ahadi hizo jana (Jumatano, Desemba 28, 2016) wakati akizungumza na wananchi wa vijiji vya Namilema, Mbuyuni, Nandandara, Namkonjera, Muhuru, Chikundi na Chibula na viongozi wa wilaya ya Ruangwa, mkoa wa Lindi ambako anapita kuwasalimia wananchi wa jimbo lake na kuhimiza kazi za maendeleo. 

Waziri Mkuu yuko Ruangwa kwa siku nne kwa mapumziko ya mwisho wa mwaka.Alisema sera ya Serikali ni kuwa na zahanati kwa kila kijiji na kituo cha afya kwa kila kata na kwamba umefika wakati wa kuanza kutekeleza kaulimbiu ya jimbo hilo inayosema “Ruangwa kwa maendeleo, inawezekana.”

Katika kuhimiza ujenzi wa zahanati hizo, alichangia mabati kati ya 50 na 150 kwa kila kijiji na akawahimiza wahakikishe wanakamilisha mapema ujenzi wa maboma ili aweze kutimiza ahadi yake ya mabati.

Alisema katika awamu iliyopita, alikazania sana suala la elimu kwa kusimamia ujenzi wa nyumba za walimu na madarasa kwenye shule ambazo hazikuwa na madarasa ya kutosha. Pia alisimamia ukarabati wa majengo chakavu katika baadhi ya shule.

“Kuanzia awamu hii na miaka minne iliyobakia, mkakati wangu ni kusimamia upatikanaji wa maji safi na suala la kuboresha sekta ya afya katika jimbo zima nikishirikiana na uongozi wa Halmashauri yetu,” alisema.

Pia alimwagiza Mganga Mkuu wa Wilaya hiyo, Dk. Japhet Simeo ahakikishe anawasiliana na viongozi wa vijiji hivyo ili wapatiwe michoro ya ramani zilizoidhinishwa na Wizara ya Afya.

Wakati huohuo, Mkurugenzi wa kampuni ya Umemejua ya Baraka Solar Specialist, Bw. Ansi Mmasi alisema atajitolea kuweka mfumo wa umemejua wa watts 300 pamoja na nyaya zake kwenye zahanati inayotaka kujengwa kwenye kijiji cha Namilema.

Alisema anaishukuru kwa kuwapa kazi makandarasi wazawa na akawataka wakandarasi wenzake watumie vifaa bora na imara pindi wanapopewa kazi ya kutoa huduma na taasisi mbalimbali ikiwemo halmashauri na idara za Serikali.

“Tujitahidi kufanya kazi hizi kwa weledi na tutumie vifaa bora na imara ili watu wanaotarajia huduma zetu waweze kuridhika na kuendelea kuwa na umani na wakandarasi wazawa kwamba tunaweza kufanya kazi nzuri na zenye ubora unaotakiwa,” alisema.

Naye Mkurugenzi wa kampuni ya ujenzi ya Wanyumbani Construction, Bw. Fakihi J. Bakili alisema atachangia mifuko 50 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa zahanati hiyo ya kijiji cha Namilema. Pia alichangia mifuko 100 kwenye zahanati ya kijiji cha Manokwe na mifuko mingine 50 kwa ajili ya ujenzi wa zahanati ya kijiji cha Chikundi.


IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Watu 7 Wafikishwa Mahakamani kwa kumchoma mkuki mdomoni mkulima

$
0
0
POLISI mkoani Morogoro imewafikisha mahakamani watu saba kati ya 12, kujibu tuhuma za kumjeruhi kwa kumchoma mkuki mdomoni hadi kutokea shingoni, Augustino Mtitu (35).

Walipandishwa kizimbani jana katika Mahakama ya Wilaya ya Kilosa huku wengine watano, wote wakazi wa kitongoji cha Upangwa wilayani Kilosa wakisubiri kufikishwa mahakamani baada ya uchunguzi kukamilika.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Ulrich Matei, alisema jana alipokuwa anazungumzia msako uliofanywa na polisi na kufanikisha kukamatwa kwa watuhumiwa hao baada ya kutokea kwa tukio hilo Desemba 25, mwaka huu, majira ya saa tano asubuhi eneo la kitongoji cha Upangwa, Kijiji cha Dodoma Isanga, Kata na Tarafa ya Masanze wilayani Kilosa.

Kamanda Matei alisema katika msako huo, watu 12 walikamatwa na saba kati yao tayari wamefikishwa mahakamani. Wengine watano watafikisha mahakamani baada ya kukamilika kwa uchunguzi.

Hata hivyo, Kamanda huyo aliwataja majeruhi wa tukio hilo mbali na Mtitu ambaye bado anaendelea na matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro, kuwa ni George Andrew (68) aliyejeruhiwa kichwani.

Wengine ni Yohana Wisa (26) aliyejeruhiwa mkono wa kulia, Mathayo Elia (34) aliyejeruhiwa kichwani na bega la kushoto, Josephat Mtitu (55) aliyejeruhiwa begani na shavuni na mwingine ni Paulo Thomas (56) aliyejeruhiwa mbavu na mkono wa kushoto.

Wote ni wakazi wa kijiji cha Dodoma Isanga na wanaendelea vizuri. Hivi karibuni, baadhi ya wafugaji wa jamii ya kimasai waliwashambulia kwa silaha za jadi na kuwajeruhi watu sita akiwemo Mtitu mara baada ya kukamata mifugo ya mtu mmoja aitwaye Ngoyoni Kimang’ati, iliyokuwa ikiharibu mahindi shambani.

Mapya Yaibuka Sakata la Kijana Aliyefariki Baada ya Nyoka wake Kuuawa na Wananchi

$
0
0
Tukio  la kushangaza lililohusishwa na kifo cha Denis Komba (24) baada ya nyoka aliyekuwa naye kuuawa, limechukua sura mpya baada ya mambo kadhaa kuibuka.

Hayo ni pamoja na familia kudai mzoga wa nyoka na kwenda nao kuuzika nyumbani, jambo lililoendelea kuhusisha suala hilo na imani za kishirikina.

Imeelezwa kuwa familia ilielezwa na mganga wa kienyeji kuwa mwili uliohifadhiwa hospitali, si wa mtoto wao, jambo lililowafanya kuuchukua mzoga wa nyoka na kwenda kuuweka katika mfuko wa sarandusi (kiroba) na kuuzika.

Hata hivyo, mashuhuda walieleza kuwa, familia hiyo ilikikata kichwa cha nyoka na kukizika kivyake na kiwiliwili sehemu nyingine huku mwili wa Komba ambaye naye alizikwa jana, ukizikwa katika kaburi eneo lingine tofauti. Tukio hilo ni la juzi na lilimhusu Komba, mkazi wa Mateka, manispaa ya Songea mkoani Ruvuma.

Nyumbani kwao ni kilometa tano kutoka katikati ya mji wa Songea. Kabla ya maziko, baadhi ya vijana waliokuwa wamebeba jeneza, walikuwa wakikimbia nalo mwendo wa mchakamchaka huku wakiimba “mkimbize mkimbize nyoka awahi asije kudhuru watu wengine”.

Katika maziko hayo, hakuna ndugu aliyeonekana kulia wala hakukuwa na ibada yoyote wakati jina la marehemu linadhihirisha kuwa ni wa imani ya Kikristo. 

Wakati hayo yakiendelea msibani, baadhi ya watu wake wa karibu walidai alikuwa na tabia ya kucheza na nyoka mara kwa mara.

Hata hivyo, baba mzazi alikana kumuona mwanawe na nyoka. Naye daktari aliyechunguza mwili, alisema kifo cha Komba kinatokana na kugongwa na nyoka mwenye sumu kali, lakini hakuna jeraha wala alama yoyote iliyoonekana katika mwili huo.

Habari zinaeleza kuwa juzi familia ilikwenda kuzungumza na watu wa Idara ya Maliasili, waliochukua mzoga wa nyoka kwa uchunguzi kama nyara ya serikali. Walikubaliana kuwa familia itakwenda kuufukia na ndipo Maliasili walimrudisha nyoka hadi eneo la tukio na familia kumchukua.

Ilielezwa kuwa hatua hiyo, inatokana na madai kuwa kuna mganga amehusisha mzoga wa nyoka huyo na mwili wa Komba.

Watu wa karibu wa familia hiyo, ambao hawakutaka kutaja majina yao wakiwemo mafundi seremala na majirani, walieleza kuwa familia wakiongozwa na baba mzazi Sevelin Komba, walirudi eneo la tukio baada ya kutoka kwa mganga wa kienyeji na kumchukua nyoka na kumpeleka nyumbani.

Habari zinaeleza kuwa familia baada ya tukio hilo, walikwenda kwa mtaalamu wa mambo ya asili (mganga wa kienyeji) ambaye hakufahamika mara moja na kuelezwa kwa nini wamekubali kumuacha mtoto wao akiteseka juani kwani mwili walioupeleka nyumbani kutoka hospitali si wa Denis (Komba).

Aidha familia baada ya kumchukua nyoka huyo eneo la tukio alikouawa, baada ya kufikishwa nyumbani alikatwa kichwa kwa makubaliano ya familia ya marehemu na kiwiliwili kuzikwa tofauti na kichwa katika mfuko wa sarandusi. Baba mzazi alikanusha suala hilo la kwenda kwa mganga.

Katika maziko hayo, hakukuwa na chakula wala matanga na watu wengi walijitokeza ili kushuhudia kitakachoendelea. 

Mikoa ya Njombe, Iringa na Mbeya yaongoza kwa maambukizi ya Virusi Vya UKIMWI

$
0
0
Kutokana na maambukizi mapya ya virusi vya Ukimwi kupungua kwa asilimia 50 duniani kote na kupelekea watu milioni 2.1 tu kuambukizwa Virusi vya Ukimwi katika mwaka 2015,kumeibua matumaini mapya ya kuwa na watu wasio na maambukizi ya virusi vya Ukimwi ifikapo mwaka 2030.

Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi nchini Tanzania (TACAIDS) Dkt. Leonard Maboko aliwaambia waandishi wa habari jana Jijini Dar es Salaam kuwa, nchini Tanzania maambukizi mapya ya virusi vya Ukimwi nayo yameshuka kwa asilimia 20 ambapo watu 54,000 wameambukizwa virusi hivyo kwa mwaka 2015 pekee.

Dkt. Maboko alisema, Ukimwi bado ni janga kubwa duniani na taifa kwa ujumla huku akitaja kundi la wanawake kuwa ndilo lina kiwango cha juu cha maambukizi ya VVU huku mikoa ya Njombe, Iringa na Mbeya ukiwa na kiwango cha juu cha maambukizi hayo kitaifa.

Aidha, alisema serikali imejiwekea mikakati kuhakikisha kuwa waliogundulika kuwa wameathirika wanaanzishiwa dawa, kuhimiza matumizi ya mpira wa kiume, kupunguza maambukizi mapya kwa asilimia 29 na kutoa elimu kwa wanawake wanaojihusisha na ngono, kupunguza maambukizi ya virusi vya Ukimwi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto.

Mke wa anayedaiwa kutobolewa macho na ‘Scorpion’ atoa ushahidi Mahakamani

$
0
0
Stara Sudi, mke wa Saidi Mrisho ameieleza Mahakama ya Wilaya ya Ilala, jinsi alivyoshtuka baada ya kupokea simu aliyopiga mumewe kuwa amevamiwa na kuchomwa visu machoni, mgongoni na tumboni. 

Akiongozwa na Wakili wa Serikali, Nassoro Katuga kutoa ushahidi dhidi ya mshtakiwa Salum Njwete (34) maarufu ‘Scropion’, Stara alimueleza Hakimu Mkazi, Flora Haule kuwa Septemba 6, saa tano usiku akiwa amelala alipokea simu yenye sauti ya mumewe ikieleza kuwa amevamiwa. 

“Aliniambia mama Nancy nimechomwa visu hata kuona sioni hapa nilipo nipo Buguruni,” alidai Stara ambaye ni shahidi wa pili wa upande wa mashtaka. 

Alidai tangu wafunge ndoa na mumewe Oktoba 2015 , Said alikuwa akifanya kazi ya kinyozi katika saluni ya Rodgers iliyopo Tabata Sanene. 

“Baada ya kuongea na mume wangu, simu ilikatika lakini wakati natafuta nguo nivae simu ileile ilipiga na nilipopokea sauti ya mtu mwingine iliongea ambaye ndiye mwenye simu na aliniambia kuwa mume wangu ana hali mbaya hivyo nifanye haraka niende Hospitali ya Amana,” alidai Stara. 

Baada ya kupata taarifa hizo, alidai alimweleza mtoto wao mkubwa, Abdul Said (12) kuwa anaelekea Amana. Lakini kabla ya kwenda huko alichukua pikipiki na kwenda Mabibo Hosteli anakoishi mama mkwe wake kumweleza taarifa hiyo na kwamba waliambatana hadi Amana. 

Alidai wakiwa njiani, walimjulisha mdogo wa Saidi, Yahaya Kisukari (23) kuwa kaka yako amepata matatizo ya kuvamiwa na mtu akachomwa visu na yupo Hospitali ya Amana. 

“Tulipofika Amana, tuliruhusiwa kuingia wodini na kumuona mume wangu akiwa amefungwa bandeji machoni na sehemu nyingine za mwili, huku damu ikivuja sehemu mbalimbali za mwili. Hata nguo aliyovaa ilikuwa imejaa damu,” aliiambia Mahakama na kuongeza: “Baada ya kumvua nguo zilizo- kuwa zimetapakaa damu, tulipewa rufaa kwenda Muhimbili kwa ajili ya matibabu na wakati huo ilikuwa imeshafika saa sita usiku.” 

Stara alidai baada ya kumuona mumewe aliyechomwa visu na mtu aliyemtaja kwa jina la Scorpion, alikwenda kutoa taarifa Kituo cha Polisi Buguruni. 

“Baada ya kutoa maelezo Polisi Buguruni na askari kwenda kuchukua maelezo ya mume wangu Muhimbili, tulikwenda kumkamata mshtakiwa Salum Njwete,” alidai. 

Alidai: “Septemba 8, tulirudi tena Muhimbili na kupewa taarifa na daktari wa macho aliyemfanyia upasuaji Said kuwa macho yake hayataona tena.” Stara alidai tangu waoane na mumewe, hajawahi kupata malalamiko yoyote kuwa mwenza wake huyo ni mwizi.

Wassira akimbilia Mahakama ya Rufaa kumpinga Bulaya

$
0
0
WAZIRI mwandamizi wa serikali ya Tanzania kwa awamu nne za uongozi, Stephen Masato Wassira, kupitia kwa wafuasi wake watatu, amekata rufaa Mahakama ya Rufaa, akipinga uamuzi wa Mahakama Kuu kwa kuhalalisha ushindi wa Mbunge wa Bunda Mjini, Esther Bulaya (Chadema).

Wassira (71 ) alikuwa waziri kwa mara ya kwanza tangu Desemba 07, 1973 akiwa naibu waziri wa Kilimo na ameendelea kuwa kiongozi mwandamizi wakati wa serikali ya Mwalimu Julius Nyerere, akarithiwa wakati wa Rais Ali Hassan Mwinyi, baadaye Rais Benjamin Mkapa na hatimaye uongozi wa awamu ya nne wa Rais Jakaya Kikwete.

Tayari wafuasi hao wa Wassira; Magambo Masato, Matwiga Matwiga na Ascetic Malagaila, wamefungua kesi hiyo na imesajiliwa katika ofisi za mahakama ya rufaa jijini Mwanza tarehe 16 Desemba, 2016 na itakuwa ni kesi ya rufaa namba 199 ya mwaka 2016.

Katika rufaa hiyo iliyoandikwa na wakili wao, Constatine Mutalemwa, wametoa sababu kadhaa kama hoja zao za kukata rufaa.

Kwanza, wanadai kwamba jaji hakuzingatia makosa yaliyofanyika baada ya zoezi la kupiga kura.

Pili, Wassira au wakala wake wanadai hakuitwa kwenye majumuisho kujulishwa siku, mahali wanafanyia majumuisho.

Tatu, wanadai kuwa jaji hakutilia maanani kesi zinazofanana na hii zilizotolewa kama mfano mahakamani.

Nne, Jaji alikosea kutoa uamuzi kwa misingi ya maoni binafsi badala ya kuzingatia mambo ya maana.

Wanadai kuwa jaji alisema wananchi wa Bunda ni maskini waachwe wafanye shughuli za maendeleo kwa sasa.

Tano, wanadai jaji alikosea kuamua kuhusu sheria ya viapo na matamko iliyotajwa katika kanuni za kuendesha kesi za uchaguzi.

Novemba 18, mwaka huu, Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza ilitoa uamuzi wa kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa ubunge uliompa ushindi Mbunge wa Bunda Mjini, Esther Bulaya (Chadema) dhidi ya Stephen Wassira (CCM).

Kesi hiyo ya kupinga matokeo ya uchaguzi ilifunguliwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, lakini ilikuwa inasikilizwa mjini Musoma, mkoani Mara.

Mahakama hiyo ilieleza kutoridhishwa na ushahidi wa kupinga matokeo hayo uliowasilishwa na upande wa walalamikaji, hivyo ikamthibitisha Bulaya kuwa mbunge halali wa jimbo hilo.

Kesi ya kupinga matokeo hayo ilifunguliwa na wafuasi wa Wassira ambaye alikuwa mbunge wa jimbo hilo kabla ya kuondolewa kupitia uchaguzi mkuu uliofanyika mwaka jana.

Katika kesi ya msingi, walalamikaji ambao ni wakazi wa Bunda walidai kuwa uchaguzi haukuwa huru na haki kwakuwa uligubikwa na vitendo vya rushwa, mgombea wanaemuunga mkono kunyimwa fursa ya kuhakiki matokeo pamoja na kuongezeka kwa idadi ya vituo vya kupigia kura visivyo halali.

Katika kesi hiyo, Bulaya alitetewa na mwanasheria wa Chadema, Tundu Lissu.

Credit: FikraPevu

Bodi ya Mikopo yawatosa Watanzania wanaosoma China

$
0
0
Watanzania waliopata ufadhili wa kusoma nchini China, hawatapata mikopo baada ya Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) kuwaondoa kwenye orodha ya wanufaika. 

Taarifa iliyotolewa na HESLB, ikijibu Ubalozi wa Tanzania nchini China, kuhusu madai ya kuchelewa kwa fedha za mikopo kwa wanafunzi wanaosoma nchini humo imeeleza kuwa hatua hiyo inatokana na maelekezo ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwamba wanafunzi wote wanaopata ufadhili kutoka nchi rafiki watajitegemea ikiwamo gharama za tiketi za ndege.

Barua hiyo ya Desemba 20, 2016 iliyomnukuu Mkurugenzi Mtendaji wa bodi hiyo, Abdul Razaq Badru inaeleza kuwa mwaka huu wanafunzi hao hawatanufaika na mikopo kama ilivyokuwa ikitolewa miaka ya nyuma.

Jana, akizungumza na waandishi wa habari, Badru aliitambua barua hiyo huku akisita kutolea ufafanuzi wake kwa madai ilikuwa ni majibu kwa wanafunzi hao wa China.

Hata hivyo, alisema endapo kutakuwa na madai kutoka kwa wanafunzi hao watalazimika kutolea ufafanuzi.

Akizungumzia suala hilo Naibu Waziri Elimu, Stella Manyanya alisema ni hekima zaidi kuangalia au kusaidia wanafunzi wa ndani wasiokuwa nacho kuliko wanaopata ufadhili wa nje ya nchi.

Aliyemkashifu Mtume Z’bar Kufikishwa Kortini

$
0
0
JESHI la Polisi Zanzibar linatarajia kumfikisha mahakamani mtu anayedaiwa kumkashifu Mtume Muhammad (S.A.W).

Mtuhumiwa huyo, Dk. Abdallah Saleh Abdallah (50), mkazi wa Kikwajuni mjini Unguja, baada ya kutoa maneno hayo ya kashfa juzi na kusambaa kwenye mitandao ya kijamii.

Akizungumza na waandishi wa habari jana mjini Unguja, Kamishna wa Jeshi la Polisi visiwani hapa, Hamdan Omar Makame, alisema walimtia mbaroni daktari huyo wa binadamu baada ya taarifa zake kusambaa kwenye mitandao ya kijamii, ikiwamo wa Facebook.

Mtuhumiwa huyo anadaiwa kumkashifu Mtume Muhamad na waumini wa dini ya Kiislamu.

“Tumemkamata mtuhumiwa na tayari tumeshakamilisha kila kitu, ikiwamo taarifa za upelelelezi. Hivyo kilichobaki ni kumfikisha makahamani tu ili aweze kujibu mashtaka yake,” alisema Kamishna Makame.

Akiongezea kuhusu ukusanyaji wa taarifa za upelelezi, alisema wamelazimika kumshikilia kijana Ali Juma Makame (30) mkazi wa Michenzani mjini hapa ambaye anatuhumiwa kusambaza video hizo mitandaoni.

“Tunawanasihi waumini wa dini ya Kiislamu kutokubali kuyumbishwa na kufanya maandamano kwani kufanya hivyo ni kwenda kinyume na sheria, ni bora kujiepusha na jambo hili kwani tayari vyombo vya ulinzi vimeshachukua hatua kwa mujibu wa sheria,” alisema.

Kutokana na video hiyo, taasisi mbalimbali za dini ikiwamo Jumuia ya Maimamu Zanzibar (JUMAZA) na Ofisi ya Mufti, zimelaani tukio hilo na kutoa wito vyombo vya sheria kuchukua hatua na kufanya kazi bila upendeleo.

Amuua Rafiki Yake....... Ala Ubongo wake na Sehemu Za Siri

$
0
0
JESHI la Polisi Mkoa wa Mbeya, linamshikilia mchimba dhahabu, Shija Salum (38), mkazi wa Kahama mkoani Shinyanga kwa tuhuma za kumuua rafiki yake na kula ubongo wake.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Dhahiri Kidavashari, aliwaambia waandishi wa habari jana kwamba pamoja na mtuhumiwa huyo kula ubongo wa rafiki yake huyo aliyetambuliwa kwa jina moja la Shija, pia alitafuna sehemu zake za siri baada ya kuzikata.

Kwa mujibu wa Kamanda Kidavashari, tukio hilo lilitokea Desemba 25, mwaka huu, usiku katika Kijiji cha Manyanya, Kata ya Makongorosi, Wilaya ya Chunya mkoani Mbeya.

Alisema mtuhumiwa na marehemu walifika kijijini hapo wakitokea Shinyanga miezi mitatu iliyopita.

“Inasemekana wawili hao walikuwa ni marafiki kwani walifika wilayani Chunya, Kata ya Makongolosi kwenye machimbo ya dhahabu yanayomilikiwa na mfanyabiashara mmoja aitwaye Teddy Mwantega.

“Siku hiyo ya tukio, marehemu Shija, alikuwa amejilaza mahali na hapo ndipo alipofika rafiki yake huyo, akiwa na panga mkononi na kumkata kwa nguvu kichwani.

“Baada ya hapo, alimvua nguo na kuzikata sehemu zake za siri na kuzishika mkononi.

“Wakati akiwa na sehemu hizo za siri mkononi, alichukua ubongo wa marehemu na kuula, kisha akatafuna zile sehemu za siri.

“Kwahiyo, mtuhumiwa atafikishwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika,” alisema Kamanda Kidavashari.

Ofa ya Kufunga Mwaka: Jipatie Vitabu Vya Riwaya za Kusisimua Toka kwa Mtunzi Aliyebobea, Eddazaria G.msulwa

$
0
0
Ninawashukuru wasomaji wangu wote ndani na nje ya Tanzania hasa  mlio soma story zangu za SORRY MADAM na SHE IS MY WIFE

Tukiwa tumebakisha siku chache kabla hatujamaliza mwaka. Ninawakaribisha kununua kitabu changu cha AM NOT A DOCTOR kwa sh 7000 TU huku kitabu cha HARD DAY kikipatikana kwa sh 4000 TU.

Njia za kuvipata vitabu hivi ni WHATSAPP 0657072588 na EMAIL: eddazariaM@gmail.com Wahi sasa ofa hii ya kufunga mwaka 2016.

SORRY MADAM -Sehemu ya 9 & 10 (Destination of my enemies)

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA

ILIPOISHIA  
“Muheshimiwa tumemkosa”
Askari walio agizwa kwenda kumfwatilia Mzee Godwin walikuja huku wakihema kana kwamba ni kweli waliweza kumfwatilia ila ukweli ni kwamba walipo toka ndani ya chumba cha walicho kuwepo na kwenda nje ya geti, wakatazama kila upande na kushauriana wakimbie kimbie, kama nusu saa ili kuitoa miili yao jasho, ili wakirudi watoe ripoti ya kwamba hawakufanikiwa kumuona mzee Godwin. Eddy akawatazama kwa muda jinsi wanavyo hema
“Hamuna kazi, kuanzia sasa rudishni magwanda kwenye vituo vyenu vya kazi”
Askari hao wakabaki wamemtumbulia mimacho Eddy na mmoja akaanza kuangua kilio kikubwa cha kujutia
  
ENDELEA
“Muheshimiwa mimi kwetu ninategemewa, na mimi itetezi change ni hii kazi”
Askari huyo alizungumza huku akiendelea kulia kwa machozi, Eddy hakuhitaji kusikiliza kitu cha aina yoyote zaidi ya kuwasisitiza wakalilie mbele ya safari kwani hawana sifa ya kuwa maaskari.
Hali ya Phidaya ikaendelea kuwa tata huku daktari na manesi wakindelea kuyastua mapigo ya moyo yaweze kufanya kazi, ila haikuwa rahisi kama wanavyo zoea kufanya kwa wagonjwa wengine

“Dokta vipi?”
Nesi Maria aliuliza huku akiwamgikwa na jasho jingi kwani nimara nyingi wamejaribu kumstua Phidaya ila juhudi zao hazikuzaa matunda
“Atakuwa amekufa nini?”
Doktar Khan alimuuliza nesi Maria kwa sauti ya chini ili waziri Eddy aliyopo nje asiweze kusikia kinacho endelea ndani ya chumba hicho
“Hata mimi pia nahisi hivyo kwani si kawaida”
“Sasa utamuambiaje huyo waziri hapo nje?”
“Nani niwaziri?”
Nesi Maria alizungumza kwani kwa kipindi chote alicho kuwa anazungumza na Eddy hakujua kwamba ni waziri

“Mungu wangu, mimi sijajua……!!!”
“Ohooo hapo sasa na wewe unaharibu, mimi nimesikia watu hapo nje wakiangua vilio baada ya kuambiwa hawana kazi”
“Mmmmm ehee Mungu sijui itakuwaje”
Wakiwa wakiendelea kujadilia, taratibu mashine ikaanza kuonyesha vimishale viwili vya kijani ikiashiria mapigo ya moyo ya Phidaya ayamesha anza kudunda japo kwa utaratibu bali anaashiria kwamba yu hai na si mfu kama wanavyo hisi
“Ohhh asante Mungu wewe baba wa majeshi, hakuna lishindikanalo kwako”
Nesi Maria alisali kwani kupona kwa Phidaya ndio kupona kwa kazi zao wanazo zitegemea maishani mwao.
                                                                                             ***
    Upasuaji wa kutoa risasi zilizo kuwa kwenye kifua cha Madam Mery, ukafanikiwa kwa kiasi kikubwa na madaktari wakafanikiwa kuweza kuzitoa risasi hizo kwa usalama kisha wakamshona vizuri Madam Mery na kumpeleka kwenye chumba maalumu cha wagonjwa mahututi. Kwa msaada wa mashine akaendelea kupumua huku dripu la maji na damu yakiendelea kufanya kazi ya kuongeza maji na damu vilivyo pungua mwilini mwa Madam Mery.

Usiku wa manane Madam Mery akaweza kufumbua macho yake kwa mara ya pili, kwani mara ya kwanza alikua wakiomba kuzungumza na Eddy, pale alipo pata hofu kwamba anaweza kupotea maisha yake muda wowote kuanzia pale

Akayazungusha macho yake kwenye kila kono ya chumba, kwaufahanu wake unao fanya kazi vizuri akagundua kwamba pale ni hospitali. Pameni ya kitanda akaona kuna kifaa maalumu ambacho ukikiminya nesi au daktari aliye karibu mtambo huo wa kisasa unao weza kuwataarifu manesi na madaktari kwamba mgonjwa wa chumba Fulani ana hitaji msaada.
Hazikupita dakika tano mlango wa chumbani kwakr ukafunguliwa na kuingia nesi mrefu kiasi aliye jazia maungo yake ya nyuma
“Nikusaidie nini?”  
Nesi huyo alizungumza kwa sauti ya upole huku akimtazama Madam Mery.
“Eddy, Eddy waziri namuhitaji”

Madam Mery alizungumza, kutokana na uwepo wa Eddy kwenye hospitali hii uliwafanya watu wengi kuutambua uwepo wake. Hakuwa na kipingamizi nesi huyo, aliye vaa kagauni kalisho ishia kenye maagoti na kuyafanay makalio yake makubwa kutingishika vibaya mno kila anapo tembea
Nesi akaongoza hadi sehemu alipo Eddy, nje ya chumba, kwaheshima zote akasimama mbele ya Eddy
“Muheshimiwa kuna mwana mama anakuhitaji kwenye chumba cha wagonjwa mahuti”
Kabla Eddy hajamjibu neno lolote nesi huyo mlango wa chumba alicho lazwa mke wake, ukafunguliwa akatoka doktar Khan, akiwa na tabasamu usoni mwake
“Dokta vipi mke wangu?”
Doktar Khan akashusha pumzi nyingi kisha akaanza kuzungumza

“Tumejitahidi kadri ya uwezo na..”
“Mke wangu amekufa doktar?”
Eddy aliuliza kwa wasiwasi mwingi
“Hapana hajafa, tumeweza kuyaokoa masha yake, ila kwa sasa atakuwa chini ya uangalizi wa manesi watau, mutamuona kesho asubuhi kwa sasa nitaomba mumuache apumzike”
“Sawa”
Eddy alijubu kwa unyonge huku akitamni kuzungumza kitu kwa daktari huyo, ila akajikuta akisahau ni kitu gani alihitaji kukizungumza. Hapakuwa na jinsi yoyote ikambidi Eddy amuombe Mzee Mboho kukaa nje ya chumba hicho hadi yeye pale atakapo rejea, yeye akaongozana nesi aliye kuja kumuita na kufikishwa kwenye chumba alichopo Madam Mery
                                                                                                ***
      Mzee Godwin baada ya kutoka kwenye geti la hospitali akakodi taksi iliyo mfikisha kwenye hoteli aliyo kuwa amefikizia na Madam Mery, akaingia bafuni na kunyoo ndevu zake zote alizo kuwa nazo na kumfanya arudi kwenye sura ya ukijana japo ni mzee, akakushanya nguo zake na kuziingiza ndani ya begi alilo kuja nalo, akiamini anaweza kuifanya kazi yake na kuimaliza ila hali tayari ilisha kuwa mbaya kwani mwanae Eddy anamamlaka makubwa serikalini na endapo atamtia nguvuni nilazima atahukumiwa.

Mzee Godwin akatoa kwenye chumba cha hoteli na kuanza kutembea kwenye kordo ndefu, hakuhitaji kutumi lifti kuhofia kukamatwa kizembe pale lifti itakapo funguka na kukumbana na kundi la askari. Akaanza kushuka kwenye ngazi akitokea gorofa ya saba kushuka chini, na kila mara akawa na kazi ya kuchungulia chini kuona kama atakutana na mtu yoyote.

Mzee Godwin akafanikiwa kufika nje ya hoteli pasipo kustukiwa akakodi taksi nyingine na kumuomba dereva kumpeleka kwenye uwanja wa ndege wa mwalimu Julias K.Nyerere ili aweze kuondoka nchini Tanzania haraka iwezekanavyo na kuelekea brazil alipo weka makazi yake ya maficho.
Mzee Godwin akastushwa kukuta gari zipatazo sita za polisi zikiwa zimefunga barabara ambayo walihitaji kupita kuelekea uwanja wa ndege. Na kundi hilo la askari wote walionekana kuwa na silaha mikononi mwao na wawili wakiwa namatochi makubwa yakiimulika taksi hiyo
                                                                                                   ***
     Eddy akafungua mlango na kuingia ndani ya chumba alicho lazwa Madam Mery na kumkuta akiwa yupo macho. Taratibu Eddy akaka kwenye kiti cha pembeni ya kiti cha Madam Mery, huku akiwa na maswali mengi ni kwanini amemkuta Madam Mery akiwa amepigwa risasi nyumbani kwake na kama alikuja na mzee Godwin imekuwaje wameanza kushirikiana na mzee huyo. Ila kutokana Madam Mery ni mngonjwa hakuhitaji kuuliza swali lolote zaidi ya kusubiria kitu kilicho mfanya yeye kuitwa hapo

Madam Mery alipo mtazama Eddy, akajikuta akimwagikwa na machozi, kila alivyo lia maumivu kwa mbali akaanza kuyasikia kwani dawa ya maumivu aliyo chomwa ndio ilikuwa ina kwenda kuishia kupoma.
“Eddy kwanza nahitaji kukuambia kitu kitu kitakacho tokea muda wowote, Godwin amepanga kutegesha bumu kwenye uwanja wa ndege wataifa na kuteka ndege ambayo, atataka kuitumia kwa shuhuli zake binafsi”

Maneno ya Madam Mery yakamfanya Eddy kustuka kwani hajafanikiwa kumtia mikononi mzee Godwin, Eddy kwa haraka akaitoa simu yake mfukoni, akajaribu kuiwasha akakuta imezima
“Mungu wangu”
Eddy alionekana kuchanganyikiwa, akajaribu mara kadhaa kuiwasha simu yake ila haikukubali kuwaka, kwa haraka akatoka nje ya chumba pasipo kumuaga madama Mery kwa bahati nzuri akakutana na nesi aliye kuwa amemuita

“Lete lete simu yako”
Eddy alizungumza na kumfanya nesi huyo kuanza kujipapasa papasa ila akajikuta akishangaa
“Ahaa nimeicha kule mapokezi ninaichaji”
Alizungumza na kuanza kukimbi kuelekea mapokezi, huku Eddy akifwata kwa nyuma. Kila walio pishana naye alihisi kuna jambo linalo endelea, wakafika kwenye chumba cha mapokezi, nesi huyo akaingia ndani naichomo simu yake kwenye chaji na kumkabidhi Eddy aliye onekean kuchanganyikiwa.

“Unafunguaje hiii”
Eddy alizungumza baada ya kushindwa kufungua mfuniko wa simu ili kuweza kubadilisha line za simu na aweke yakwake. Nesi akamsaidia kufungu simu hiyo, kisha akatoa line yake na kumpa Eddy, akaweka line yake na kuchua batrii na kuiweka na kuiwasha simu hiyo pasipo pasipo kuurudishia mfuniko wa nyuma. Eddy kwa haraka akatafuta namba ya mkuu wa polisi, kisha akaipiga. Ikaita kwa muda  na kupokelewa na sauti iliyo jaa usingizi
“Haloo”
“Kuna tukio la ugaidi lanataka kutendeka muda wowote kuanzia sasa, huku uwanja wa ndege wa JK unatakla kulipuliwa”

Eddy alizungumza kwa haraka haraka huku akihema
“Wewe nani kwani?”
Mkuu wa askari aliuliza
“Unataka kunijua mimi ni nani?”
“Ndio kwa maana wewe ugaidi Tanzania utokee wapi, hembu acha upuuzi wako. Acha tulale sisi”
“Kabla hujakata simu, kuanzia sasa huna kazi pumbavu wewe. Unazungumza na waziri wa Ulinzi Eddy, Eddy Godwin”
“Muhe……”
Eddy akaakata simu na kutafuta simu ya makamu msaidizi wa kamanda huyo wa kanda maalumu, akaipiga namba hiyo hata sekunde tano hazikupita, simu ikaokelewa

“Ndio muheshimiwa”
Kamanda huyo alizungumza kwa wasiwasi mwingi, na kumuomba dereva wa gari anaye muendesha kusimamisha pembeni
“Kuna tiukio la uwanja wa ndege kulipuliwa hakikisheni munafunga barabara ya kwenda uwanja wa taifa na gari zote munazisimamisha na kuzikagua na mumkamate Godwin aliye kuwa mkuu wa jeshi la ulinzi”
“Sawa mkuu nimekuelewa, kwanza nipo doria muda huu na vijana”
“Fanya hivyo kuanzia sasa hivi unachukua nafasi ya mkuu wako, nimefukuza kazi muda huu”
“Ohh asante sana muheshimiwa”

Eddy akakata simu, akakata simu na kumpigia simu mkuu wa ulizi katika uwanja wa ndege wa mwalimu Julius Nyerere, simu yake nayo ikapokelewa ndani ya muda mchache
“Haloo”
“Panga vijana wako, waimarishe ulizi kunahatihati ya uwanja wa ndege kulipuliwa kwa bomu”
“Haaaa…..!!!”
“Unashangaa nini?”
“Hapana nimekuelewa muheshimiwa”
Kilicho muokoa mkuu huyu kuto fukuzwa kazi ni kuweza kuikumbuka sauti ya Eddy aliyo toka kuisikia kwenye bunge mida ya saubuhi na wala hakufahamu namba yeka waziri huyo ameitolea wapi. Hakutaka makuu zaidi ya kupiga simu kwenye sekta nzima za ulinzi uwanja wa ndege kuwaamuru askari kudumisha ulinzi kwa anaye ingia na kutoka na kila waliye mtilia mashaka akamatwe kwa mahojiano

Rais Magufuli Ashiriki Msiba Wa Mzee Maarufu Wa Chato Admirabilis Mbabe Manyama (82) Chato Mkoani Geita

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 29 Desemba, 2016 ameungana na wananchi wenzake Wilayani Chato mkoani Geita kutoa pole kutokana na kifo cha Mzee Admirabilis Mbabe Manyama ambaye ni mzee maarufu wilayani hapa na Mzee James Lufunga Mchele ambaye ni jirani yake.
Rais Magufuli pamoja na kuwapa pole wafiwa na wananchi wa Chato kwa kuondokewa na mpendwa wao pia amitaka familia ya mzee Manyama kuendelea kuishi kwa kushikamana na kupendana kama ilivyokuwa enzi za uhai wa marehemu na kuwataka kuepukana na mifarakano.

''Unapotokea msiba kama huu katika familia nyingi huzuka mifarakano, ombi langu kwenu wewe Mama mkubwa na Mama mdogo kamwe msikubali kufarakanishwa kutokana na kifo cha mume wenu,muwaongoze watoto wenu ili muendelee kuishi kwa kupendana kama enzi za uhai wa mzee''

Aidha Rais Magufuli amemuelezea Marehemu Mzee Manyama kuwa alikuwa mzee maarufu kijijini hapa na miongoni mwa mafundi hodari wa kushona nguo ambaye pia alimshonea sare zake za shule wakati akisoma.

Kwa upande wake Mdogo wa marehemu ambaye ni msemaji wa familia Bwana Deodatus Manyama ambaye ni msemaji wa familia amemshukuru Rais Magufuli pamoja na ujumbe wake alioambatana nao kuwapa pole katika msiba huo, na kwamba kitendo hicho kinaonyesha kuwa Rais magufuli si mtu asiejikweza wala asiye na majivuno.

Marehemu Mzee Admirabilis Mbabe Manyama amefariki akiwa na umri wa miaka 80,ameacha wajane wawili,watoto 15 na wajukuuu kadhaa.

Jaffar Haniu
Naibu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Chato, Geita.

29 Desemba, 2016
.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpa pole Bi. Regina Mbabe mke mdogo wa Marehemu Mzee Maarufu Admirabilis Mbabe (82) Manyama mara baada ya kuwasili nyumbani kwa marehemu Chato mkoani Geita.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Deodatus Manyama wakwanza (kushoto) ambaye ni mdogo wa marehemu Marehemu Mzee Admirabilis Mbabe Manyama(82) mara baada ya kuwasili nyumbani kwa Marehemu Chato mkoani Geita.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Bi. Mugwe Mbabe mke mkubwa wa Marehemu Mzee Admirabilis Mbabe Manyama mara baada ya kuwasili nyumbani kwa marehemu Chato mkoani Geita.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisaini daftari la maombolezo mara baada ya kuwasili nyumbani kwa marehemu Mzee Admirabilis Mbabe Manyama (82) Chato mkoani Geita
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na kutoa pole katika msiba huo wa Marehemu MzeeAdmirabilis Mbabe Manyama mara baada ya kuwasili nyumbani kwake.

Majibu ya barua ya mkazi wa Dodoma aliyoandika kwa Rais Dkt Magufuli

Ufafanuzi kuhusu taarifa za kukamatwa kwa Watanzania wanaodaiwa ni majasusi nchini Malawi

$
0
0
Baadhi ya Vyombo vya habari vya hapa nchini hivi karibuni vilitoa taarifa kuwa, Watanzania 8 wanaodaiwa kuwa ni majasusi wa Serikali ya Tanzania wamekamatwa nchini Malawi kwa tuhuma za kuingia kwenye mgodi wa urani wa Kayerekera uliopo nchini Malawi kinyume cha sheria. 
 
Taarifa hiyo kwa mara ya kwanza ilitolewa na chombo cha habari cha Malawi ambacho kilidai kuwa watu hao wametumwa na Serikali ya Tanzania ili kuchunguza kama Serikali ya Malawi inatengeneza silaha za nyuklia kwa kutumia madini ya urani ya kutoka mgodi huo.
 
Kufuatia taarifa hizo, Wizara kupitia Ubalozi wa Tanzania nchini Malawi ulifuatilia ili kubaini ukweli wa tukio hilo. Baada ya kufuatilia ilibainika kuwa ni kweli Watanzania 8 kutoka taasisi ya CARTAS iliyo chini ya Kanisa Katoliki Songea mkoani Ruvuma walikamatwa na vyombo vya usalama katika Wilaya ya Karonga ambayo inapakana na Wilaya ya Kyela.

Watanzania hao mara moja walifunguliwa kesi kwa kutuhumiwa kufanya kosa la jinai la kuingia eneo la mgodi bila kibali (criminal trespass).
 
Ubalozi uliwasiliana na Taasisi ya CARTAS kutaka kufahamu madhumuni ya watu hao kufanya ziara nchini Malawi. Ubalozi ulielezwa kuwa ziara hiyo ilikuwa ni ya mafunzo ambapo walitaka kufahamu juu ya madhara yatokanayo na machimbo ya madini ya urani. Watanzania hao kwa sasa wapo katika gereza kuu la Mzuzu hadi kesi yao itakapotajwa tena tarehe 04 Januari 2017.
 
Ubalozi unaendelea kufanya mawasiliano na Kanisa Katoliki Songea ili kupata maelezo zaidi kuhusu ziara ya watu hao kwa madhumuni ya kuyawasilisha mamlaka husika ili watuhumiwa waweze kutolewa.
 
Aidha, Wizara kupitia Ubalozi umebaini kuwa CARTAS iliruhusu watu hao kufanya ziara nchini Malawi bila kupata kibali kutoka mamlaka husika na bila kutoa taarifa Ofisi ya Ubalozi kuhusu ziara hiyo.
 
Aidha, kipindi cha kufanya ziara hiyo nchini Malawi hakikuwa muafaka kwa kuwa watumishi wa Serikali ya Malawi wanakuwa katika likizo ya mwaka kuanzia tarehe 22 Desemba hadi 03 Januari 2017. Hii inakwamisha juhudi za kuwafuatilia watu hao ikiwa ni pamoja na kukwama kwa maombi ya kibali cha kuwatembelea watu hao tarehe 28 Desemba 2016.
 
Wizara inatoa wito kwa mara nyingine kwa taasisi za dini, vyuo vya elimu na watu binafsi kuomba vibali na kufuata sheria za nchi nyingine wanapofanya ziara za mafunzo au ziara nyinginezo ikiwa ni pamoja na kuwasiliana na ofisi za Balozi zetu kwa madhumuni ya kufahamishwa taratibu zinazotakiwa kufuatwa kabla ya kufanya ziara husika ili kuepuka usumbufu unaoweza kujitokeza.
 
Wizara, kupitia Ubalozi wa Tanzania nchini Malawi unaendelea na jitihada za kuhakikisha kuwa suala hilo linapatiwa ufumbuzi kwa haraka.
 
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Dar es Salaam, 29 Desemba  2016.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images