Baada ya Dkt. Mwele Malecela kutumbuliwa, Prof. Yunus Mgaya ateuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu NIMR
↧
↧
Mahakama yatupa pingamizi la serikali katika kesi ya mbunge Godbless Lema.
Uamuzi wa kuongezewa muda wa kuwasilisha notisi ya nia ya kukata rufaa dhidi ya dhamana ya Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema, unatarajiwa kutolewa Desemba 20, mwaka huu na Mahakama Kuu Kanda ya Arusha.
Uamuzi huo utatolewa baada ya Lema jana kufanikiwa kuwasilisha maombi yake ya kuongezewa muda wa kuleta notisi hiyo ya rufaa dhidi ya dhamana yake baada ya mahakama hiyo kutupilia mbali pingamizi mbili za mawakili wa Serikali waliokuwa wakitaka maombi hayo yasisikilizwe.
Mbele ya Jaji Dk. Modesta Opiyo wa mahakama hiyo, upande wa Jamhuri ulikuwa ukiwakilishwa na Wakili Hashim Ngole, Matenus Marandu, Elizabeth Swai na Adelaide Kasala huku Lema akitetewa na Wakili Sheck Mfinanga na Faraji Mangula.
Katika maombi hayo namba 69 ya mwaka huu, baada ya kusikiliza hoja za pande zote mbili, Jaji Dk. Opiyo alisema kuwa atatoa uamuzi huo siku hiyo saa sita mchana.
“Baada ya kusikiliza hoja za pande zote nitatoa uamuzi Jumanne ijayo saa sita mchana, msije asubuhi ili nipate muda wa kupitia hoja zenu,” alisema Jaji Dk. Opiyo.
Awali, akitoa uamuzi wa pingamizi mbili zilizotolewa Desemba 14, mwaka huu na mawakili hao wa Jamhuri, Jaji Dk. Opiyo, aliyesoma uamuzi huo kwa muda wa dakika 50 kuanzia saa 5:30 asubuhi hadi saa 6:20 mchana, alisema ameamua kuzitupa pingamizi hizo baada ya kuziona hazina mashiko ya kisheria.
Alisema kuwa hakuna maombi kama hayo yaliyoacha kusikilizwa mahakamani kwa kushindwa kuonyesha kifungu namba 392 A cha sheria ya uendeshaji wa mashauri ya jinai hivyo akalitupa pingamizi la kwanza la mawakili wa Serikali waliodai maombi hayo hayakufuata utaratibu wa kisheria ikiwemo kutoonyesha vifungu vya sheria waliyoitumia kuleta maombi hayo.
“Baada ya kupitia hoja za pande zote, mahakama imeamua kutupa pingamizi hizo za Jamhuri baada ya kuziona kuwa hazina mashiko kisheria na hata upande wa Jamhuri ulishindwa kurejea shauri lolote ambalo limewahi kufanyiwa uamuzi na mahakama za juu kuhusu suala hilo,” alisema Jaji Dk. Opiyo.
Akizungumzia hoja ya pili ambayo Jamhuri ilidai ya kiapo kinachounga mkono maombi yaliyowasilishwa mahakamani hapo kimekosewa hivyo hakifai kwa sababu wamejumuisha mambo yasiyotakiwa kisheria ikiwemo maoni, mabishano na hitimisho na kubeba hoja za rufaa alisema mahakama hiyo imeondoa aya ya 11 na 12.
Alisema kuwa aya nyingine za 9, 10, 13 na ile ya 17 zitabaki katika hati hiyo ya kiapo kwa sababu hazibebi hoja za rufaa, maoni, mabishano wala hitimisho hivyo mahakama hiyo haiwezi kukataa hati hiyo ya kiapo iliyoambatanishwa na maombi hayo.
Akiwasilisha hoja za maombi ya kuongezewa muda wa kuwasilisha notisi hiyo ili rufaa hiyo iweze kusikilizwa, Wakili Mfinanga, alidai mahakamani hapo kuwa maombi hayo yamewasilishwa mahakamani hapo chini ya kifungu 361(2) cha sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai.
Alidai kuwa uamuzi wanaotarajia kukatia rufaa ni uliotolewa Novemba 11, mwaka huu katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha na Hakimu Desderi Kamugisha, ambapo Lema anakabiliwa na kesi namba 440 na 441 za uchochezi dhidi ya Rais Dk. John Magufuli.
Alitaja sababu mbili za msingi za kukatia uamuzi huo rufaa kuwa ni kuiomba mahakama hiyo ipitie makosa ya kisheria yaliyofanywa na mahakama ya chini na kusema kuwa uamuzi huo ulimpa mleta maombi (Lema) dhamana ila kabla hajapewa masharti ya dhamana upande wa Jamhuri ulitoa notisi ya nia ya kukata rufaa.
“Kwa msingi huo mahakama ilisema imefungwa mkono na hawawezi kuendelea na jambo lolote kuhusu suala hilo hata uamuzi wake wa kumpa dhamana haukuwezwa kutimizwa na mahakama haikueleza upande wowote ambao haujaridhika na uamuzi huo una haki ya kukata rufaa,” alidai Mfinanga na kuongeza:
“Kuna vitu muhimu na vitasahihishwa iwapo tutaleta notisi ya nia ya kukata rufaa na rufaa yenyewe kusikilizwa na mahakama yako ambayo ni msimamizi wa haki na sheria ikatoa ruksa ili tuweze kusikilizwa na rekodi ya mahakama ya chini iweze kurekebishwa, ni muhimu mahakama kuzingatia maombi haya pasipo kuzingatia mambo mengine.”
Huku akirejea mashauri mbalimbali ya mahakama za juu, aliendelea kueleza mahakama hiyo kuwa mahakama ikishasema imempa mtu haki ya dhamana lazima itaje masharti ya dhamana.
“Tunaomba mahakama itupatie muda tena mfupi ambao hautazidi hata saa 1:30 kwa ajili ya kuleta notisi hiyo ili mahakama iweze kurekebisha makosa hayo,” alisema.
Akiwasilisha hoja ya pili, Wakili Mangula, alidai mahakamani hapo kuwa tangu kutolewa kwa uamuzi huo hawajapumzika na muda wote walikuwa mahakamani.
Alidai kuwa walikuwa wanaenda mahakamani kwa njia tofauti ili kuiomba mahakama irekebishe makosa hayo ya kisheria.
Alidai kuwa baada ya uamuzi huo kutolewa muda wa kazi ulishaisha na ilikuwa Ijumaa hivyo Novemba 14, mwaka huu walipeleka barua ya malalamiko mahakamani hapo na walipoitwa pande zote mbili katika shauri namba 6 lakini walikumbana na pingamizi zilizowasilishwa na mawakili wa Serikali.
“Novemba 22, mahakama ilitoa uamuzi na kututaka waleta maombi tukate rufaa na hapo mleta maombi alipata haki yake ya kukata rufaa ambayo haikuelezwa mahakama ya chini na tulitoa notisi tukiamini tuko ndani ya muda na hatimaye rufaa ililetwa mbele ya Jaji Mfawidhi Fatuma Masengi,” alidai.
Alieleza mahakama hiyo kuwa katika rufaa hiyo namba 113, walikutana tena na pingamizi la Serikali kuwa wametoa notisi ya rufaa hiyo nje ya muda wa siku moja hivyo hizo ni jitihada walizokuwa wakifanya na si wazembe, wajinga wa sheria kama ilivyodaiwa na wakili wa Serikali.
Akijibu hoja za waleta maombi hao, Wakili Ngole, alidai kuwa ni wazembe, wajinga wa sheria na kuwa hata uamuzi wanaolalamikia mahakamani hapo ambao awali ulimpa mleta maombi dhamana, lakini kabla hajapewa masharti ya dhamana mahakama iliingiliwa mamlaka yake hawajawasilisha na maombi hayo.
Wakili huyo alidai mahakamani hapo kuwa hakukuwa na makosa yoyote ya kisheria kama inavyodaiwa na waleta maombi hao na kudai kuwa baada ya hakimu kusema mahakama inampa mshtakiwa dhamana Jamhuri kwa haki yake walisimama na kuifahamisha mahakama wana nia ya kukata rufaa.
“Ni utaratibu wa kisheria kuwa panapokuwa na notisi ya nia ya kukata rufaa mahakama haiwezi kuendelea na jambo lolote kuhusiana na kesi hiyo, hivyo hakimu asingeweza kuendelea na kesi na inafahamika notisi inasimama badala ya rufaa,” alidai na kuongeza:
“Kwa mujibu wa kifungu 359(1) na 361(1) cha sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai, vinaeleza mtu ambaye hajaridhika na hatua yoyote au uamuzi uliotolewa au kupitishwa anaweza kukata rufaa mahakama za juu.”
Lema anashikiliwa kwa zaidi ya mwezi mmoja katika mahabusu ya Gereza Kuu la Kisongo baada ya kukamatwa Novemba 2, mwaka huu nje ya Viwanja vya Bunge mjini Dodoma ambapo alifikishwa mahakamani Novemba 8, mwaka huu akikabiliwa na mashtaka ya uchochezi dhidi ya Rais Dk. Magufuli.
↧
Waziri Simbachawene atoa agizo jipya kwa machinga
Waziri wa TAMISEMI George Simbachawene amewataka wamachinga kutotafsiri vibaya agizo la Rais Magufuli kuwa halikumaanisha wafanye biashara kiholela mahala popote bila utaratibu bali wazingatie sheria zilizopo zikiwamo za mipango miji na usafi.
Simbachawene pia amewaagiza wakuu wa mikoa na wilaya pamoja na mamlaka za serikali za mitaa, kuhakikisha wanatekeleza agizo la Rais John Magufuli la kuwatafutia maeneo ya kufanyia biashara wafanyabiashara hao na kuwashirikisha kwenye mchakato mzima wa kubaini maeneo yenye wateja na miundombinu rafiki.
Aidha, watendaji nao wametakiwa kutotumia tafsiri hiyo kususa na kuwaacha wamachinga wafanye biashara zao kiholela.
Amesema endapo utaratibu huo utafuatwa pamoja na mambo mengine utaweza kurasimisha shughuli za wamachinga hali itakayosaidia pia kundi hilo kuchangia mapato ya halmashauri kwa kiasi kikubwa na kuondoa kabisa tabia ya kufukuzana fukuzana kila kukicha.
↧
Dr Mwele Malechela(Aliyetumbuliwa) : Safari itasonga kwa msaada wa Mungu
Aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu, NIMR, Dr Mwele Malechela, ametoa kauli yake baada ya uteuzi wake kutenguliwa na Rais Dkt John Magufuli, Ijumaa hii.
Kutenguliwa kwake kumekuja siku moja tu baada ya kuzungumza na waandishi na kudai kuwepo kwa virusi vya Zika nchini. Alisema kati ya watu 533 waliopimwa wakati wa utafiti walioufanya, asilimia 15.6 waligunduliwa kuwa na virusi hivyo. Taarifa yake, ilikuja kukanushwa na Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu.
Akijibu tweet iliyosema, ” Pole sana @mwelentuli safari yako na isonge mbele Dada,” Dr Mwele amesema, “Ahsante na itasonga kwa msaada wa Mungu.”
Tweet nyingine alijibu: Ahsante Mathew. Nilipewa dhamana nimetumikia ninamshukuru Mungu kwa nafasi ya kutumikia WaTanzania kupitia utafiti.”
Ahsante Mathew. Nilipewa dhamana nimetumikia ninamshukuru Mungu kwa nafasi ya kutumikia WaTanzania kupitia utafiti https://t.co/ZIXeN2p2q9— Mwele Malecela (@mwelentuli) December 16, 2016
Ahsante na itasonga kwa msaada wa Mungu https://t.co/L6ZNQOF5UX— Mwele Malecela (@mwelentuli) December 16, 2016
↧
Mbunge Sugu anusurika ajali, mtoto afariki kwenye ajali hiyo
Taarifa zilizoripotiwa na kituo cha runinga cha ITV leo December 17 2016 zinasema kuwa mbunge wa Mbeya mjini ‘CHADEMA’, Joseph Mbilinyi amenusurika kifo katika ajali ya gari iliyotokea eneo la Iyunga jijini Mbeya baada ya gari lake kufeli break na kumgonga mtoto ’15’ ambaye amefariki wakati akipelekwa hospitali.
Aidha taarifa hiyo inaeleza kuwa askari polisi wanne wamejeruhiwa baada ya kupata ajali wakati wakielekea kwenye ajali hiyo aliyopata mbunge Joseph Mbilinyi ‘sugu’
Gari hilo lilikuwa linaendeshwa na dereva wake, Gabriel Andrew (43) ambaye anashikiliwa na polisi.
↧
↧
Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili ya Disemba 18
↧
CCM yashinda Umeya Manispaa Mpya ya Kigamboni
Uchaguzi wa kumpata Meya wa Manispaa ya Kigamboni jijini Dar es Salaam, umefanyika na hatimaye Diwani wa Kata ya Pemba Mnazi kutoka Chama cha Mapinduzi (CCM), Maabadi Hoja amechaguliwa kuwa Meya wa kwanza.
Uchaguzi huo ulifanyika jana kwenye ukumbi wa Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
Katibu Tawala wa Wilaya ya Kigamboni, Rahel Mhando, ambaye alikuwa msimamizi wa uchaguzi, alisema mgombea huyo wa CCM ndiye aliyeshinda.
Washiriki wengine walitoka vyama vya CCM, Chama cha Wananchi (CUF) na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema). Mhando alisema Hoja alipata kura tisa dhidi ya Celestine Maufi (CUF) aliyepata kura tano na kura moja iliharibika.
Pia, Mhando alisema katika uchaguzi huo, Amini Sambo ambaye ni Diwani wa Kata ya Kibada, pia kutoka CCM, alishinda nafasi ya Naibu Meya, akipata kura 10 dhidi ya Ernest Mafimbo wa CUF, aliyepata kura tano. “Tunashukuru uchaguzi umefanyika vizuri Kigamboni, sasa tumepata Meya na Naibu Meya,” alisema Mhando.
Uchaguzi wa Meya na Naibu wake kwa upande wa Kigamboni, umefanywa baada ya Wilaya ya Temeke kugawanywa na kuwa wilaya mbili za Temeke na Kigamboni.
Mhando alieleza kuwa uchaguzi huo ambao ni wa mara ya kwanza kwa halmashauri hiyo, ulifanyika kwa amani bila kuwapo na malalamiko.
↧
Waziri Mkuu Apiga Marufuku matajiri kuwatumia polisi kupiga mabomu wananchi
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amepiga marufuku watu binafsi wenye uwezo kifedha kutumia Jeshi la Polisi kuwapiga mabomu na kuwanyanyasa wananchi kwa kuwapiga mabomu wananchi wasio na silaha.
Ameagiza nguvu hizo wazitumie kwenye maeneo ambayo yanahatarisha usalama wa nchi na wananchi.
Aidha amewaambia wananchi wa Kata ya Bwawani Kitongoji cha Omapinu kuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi atafika kijijini hapo wiki ijayo, kuzungumza nao namna ya kutatua mgogoro wa shamba la Tanzania Plantation na wananchi hao.
Waziri Mkuu Majaliwa aliyasema hayo baada ya kusimamishwa na wananchi wa kitongoji hicho, wakati alipokuwa akiendelea na ziara yake mkoani Arusha jana.
“Kuanzia sasa ni marufuku kwa watu binafsi wenye uwezo wa fedha kutumia Jeshi la Polisi kuwapiga mabomu na kuwanyanyasa wananchi kwa kuwapiga mabomu wakati hawana silaha.
“Polisi wanaruhusiwa kutumia nguvu hizo kwenye maeneo ambayo yanahatarisha usalama wa nchi na wananchi na si vinginevyo,” alisema Waziri Mkuu.
Kuhusu mgogoro wa shamba la Tanzania Plantation, Waziri Mkuu alihoji; “Ni kwanini polisi wawapige mabomu wananchi wanaozuiwa kulima au kuchota maji katika eneo hilo la shamba hadi kufikia hatua ya wanawake kuharibu mimba?
“Nyie polisi kwanini mnawapiga mabomu hawa watu, nani anatoa amri ya kupigwa mabomu wananchi hawa. Nasema kuanzia leo msiwapige mabomu watu hawa na pia nawasihi nyie wananchi msifanye fujo, subirini Waziri Lukuvi anakuja wiki ijayo kwa ajili ya kutatua mgogoro huu wa shamba.”
Alisema polisi wanaruhusiwa kutumia nguvu, pale tu panapotokea jambo linaloweza kuhatarisha maisha au vurugu, ila si kuwanyanyasa wananchi wanaodai ardhi yao kwa kuwapiga mabomu.
Alisema Lukuvi atafika mkoani humo kwa ajili ya kushughulikia migogoro ya ardhi, ambayo ipo zaidi wilayani Arumeru, na atakaa muda mwingi kwa ajili ya kutatua kero za wananchi.
Alisema kuanzia sasa mwekezaji ambaye ana mashamba wilayani humo na hayaendelezi, mashamba hayo yatachukuliwa na serikali ili kugawanywa kwa wananchi.
Alisema Waziri Lukuvi akiwa wilayani humo pamoja na kushughulikia migogoro mingine, pia atatatua mgogoro huo baina ya shamba la Tanzania Plantation na wanachi hao.
Awali, Ofisa Ardhi Wilaya ya Arumeru, Rehema Jato alikiri kuwepo kwa mgogoro wa ardhi kati ya mwekezaji wa wa Shamba la Tanzana Plantation, Pradeep Lodhia na wananchi.
Alisema kuna kesi mahakamani na wanachosubiri sasa ni uamuzi wa Mahakama ndipo hatua zingine zichukuliwe.
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Alexander Mnyeti alisema wilaya hiyo ni moja ya wilaya nchini zenye migogoro mingi ya ardhi na wakati mwingine watu wanauana.
↧
Makamu wa Rais: “Kila Jumamosi ya pili ya mwezi ni siku ya Mazoezi nchi nzima”
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ametoa muda wa miezi Mitatu kwa halmashauri zote nchini kurudisha serikalini haraka maeneo ya michezo yalivamiwa na watu kwa ajili ya kufanya shughuli zao binafsi ambapo pia ametoa agizo kuwa kila Jumamosi ya pili ya mwezi iwe ni siku ya mazoezi kwa watanzania wote ilikujiimalisha afya zao.
Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan ametoa agizo hilo baada ya kushiriki matembezi na kuzindua wa kampeni ya Kitaifa ya kudhibiti Magonjwa yasiyo ya kuambukiza kwenye viwanja wa Leaders Club jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais ameonya kuwa kama watendaji wa mikoa na halmashauri watakaoshindwa kurudisha maeneo hayo basi watenge haraka maeneo mengine kwa ajili ya wananchi kufanya mazoezi kama hatua ya kukabiliana na magonjwa yasiyo ya kuambukiza.
Katika kuunga mkono utaratibu wa kufanya mazoezi, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amewaagiza viongozi wa mikoa na wilaya zote kuweka utaratibu wa kufanya mazoezi angalau kwa mwezi mara Moja.
“Nitamke kuwa kila Jumamosi ya pili ya mwezi itakuwa siku ya mazoezi kwa afya kwa sababu mazoezi ni afya na nawaasa wananchi kufanya mazoezi na kuanzisha na kujiunga na vikundi vya mazoezi na serikali itatimiza wajibu wake wa kuweka mazingira mazuri ya kufanyia mazoezi kote nchini”
Makamu wa Rais pia ameagiza watendaji wa Wizara ya elimu, Sayansi na Teknolojia kurudisha mchakamchaka mashuleni kulingana na maeneo yalivyo. Amesema mchakamchaka utasaidia kuimarisha afya za wanafunzi na kukabiliana na magonjwa mbalimbali.
“Natoa rai utaratibu wa mchakamchaka katika shule zetu urudishwe mara Moja katika Muda ambao utaonekana ni mwafaka kwa shule husika”.
Katika hatua nyingine, Makamu wa Rais ameiagiza Wizara ya Afya kukamilisha haraka mchakato wa kuunda kamati ya kushughulikia magonjwa yasiyo ya kuambukiza itakayojumuisha wadau kutoka wizara mbalimbali nchini.
Amesisitiza kuwa mchakato huo ni lazima ukamilike tarehe 1 machi mwaka 2017.
Kwa upande wake, Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amesema magonjwa yasiyo ya kuambukiza yamekuwa yanaongezeka sana duniani kote hasa kwenye nchi zilizo chini ya Jangwa la Sahara ikiwemo Tanzania ambapo magonjwa hayo mpaka sasa yanachangia asilimia 27 ya vifo Duniani.
Amesema utafiti uliofanyika mwaka 2012 uliohusisha wilaya 53 hapa nchini umeonyesha viashiria hatarishi vya magonjwa hayo ambapo asilimia 26 ya wananchi ni wanene kupita kiasi,asilimia 26 wana lehemu nyingi mwilini na asilimia 25.9 wanashinikizo kubwa la damu.
Utafiti huo pia ulionyesha kuwa asilimia 15.9 ya wananchi wanavuta sigara na asilimia 97.2 ya wananchi wanakula mboga mboga na matunda chini ya mara tano kwa siku.
Waziri wa afya Ummy Mwalimu amesema watanzania wanaweza kukabiliana na magonjwa hayo kwa kufanya mazoezi ya viungo angalau mara tatu kwa wiki kwa muda wa nusu saa, kuzingatia ulaji wa vyakula unaofaa,kupunguza matumizi ya pombe kupita kiasi na kujiepusha na matumizi ya tumbaku.
Kwa upande wake Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Alhaj Ali Hassan Mwinyi katika nasaha zake amewahimiza Watanzania kufanya mazoezi kwa ajili ya kulinda afya zao.
Amesema kama watanzania watafanya mazoezi wataepukana na magonjwa yasiyo ya kuambukiza ikiwemo ugonjwa wa moyo,kisukari,uti wa mgongo na mifumo ya neva na figo.
Kauli mbiu ya uzinduzi wa kampeni ya Kitaifa ya Kudhibiti Magonjwa yasiyo ya Kuambukiza ni “Afya yako,Mtaji wako”
↧
↧
RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 105 ( MWISHO )
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA
Daktari akaingia haraka, ndani ya chumba tulichopo. Kwa haraka akaanza kumuhudumia mama huku akiniomba niweze kutoka nje nimuache aifanye kazi yake kiufasaha. Nikatoka nje huku machozi yakinimwagika. Phidaya akanifwata kwa haraka baada ya kuniona ninatokwa na machozi mfululizo
“Baby kuna nini?”
“Mama anakufa”
Phidaya kwa haraka akaingia ndani ya chumba cha mama na kuufunga mlango, Shamsa akamchukua Junio na kumpeleka nje, kwani hakustahili kuendelea kushuhudia matukio yanayo endelelea kwa muda huu, ukitegemea kwamba umri wake bado ni mdogo sana. Blanka naye akaanza kutokwa na machozi, akanifwata na kunikumbatia
“Ohhh Mungu saidia mama yetu apone, kwa nini inakuwa ni hivi jamani?”
Blanka alizungumza huku akiwa ameendelea kunikumbatia, machozi yakimwagika. Tukaendelea kusubiri nje kwa muda mrefu pasipo Phidaya wala doka Angelina kutoka nje. Wasiwasi juu ya kifo cha mama ukazidi kunipanda, mara kadhaa nilihitaji kwenda kuufungua mlango ili kutazama hali ya mama ila Blanka alinizuia akiniomba niweze kuwapa muda walipo ndani kufanya wanacho kifanya kwa muda huu.
Baada ya masaa kama manne Phidaya akawa wa kwanza kutoka ndani ya chumba huku jasho likimwagika usoni mwake.
“Baby vipi?”
Nilianza kumuuliza Phidaya mara tu alipo simama mbele yetu, akatutizama kwa sekunde kadhaa, mimi na Blanka kisha akashusha pumzi nyingi, iliyo nizidisha kuchanganyikiwa.
“Tumejitahidi kadri ya uwezo wetu katika……katika kumuokoa mama, na…..naa….na….”
Kigugumizi cha Phidaya kikaanza kunipa wasiwasi ulio nifanya na mimi, kijasho chembaba kuanza kunimwagika usoni mwangu.
“Nini mbona huzungumzi?”
“Hali ya mama, si nzuri sana ila bado anapumua kwa kutumia mashine”
“Anasumbuliwa na nini?”
“Mmmmm alipata mstuko ulio pelekea mapigo yake ya moyo kwenda kwa spidi kubwa iliyo mfanya awe katika hali kama ile ila kwa sasa amerudi katika hali yake ya kawaida”
Niliona Phidaya akinichanganyia mada, mara aniambie hali yake ni mbaya mara aniambie hali yake imerudi kama kawaida. Nikataka kuingia chumbani ila Phidaya akanishika mkono.
“Kwa sasa mama anabadilishwa nguo na Angelina”
Nikamtazama Phidaya machoni, kwa kuhitaji kujua anacho kizungumza kina ukweli wowote ndani yake.
“Blanka nenda kamuangalie mama”
Nilimuagiza Blanka, taratibu akapiga hatua za kuelekea chumbani kwa mama, nikabaki na Phidaya tukiwa tumetazamana usoni. Baada ya muda Blanka akatoka akiwa ameongozana na dokta Angelina.
“Vipi?”
“Mama anaendelea vizuri kidogo”
Blanka alizungumza, jambo lililo anza kunipa faraja kidogo moyoni mwangu. Ila Angelina akaniambia siwezi kumuona mama kwa wakati huu kutokana amepumzika.
***
Hali ya mama ikaanza kurudi taratibu kadri ya siku zilivyo zidi kukatika, afya ya mwili wake ikaanza kujijenga taratibu baada ya matunzo mazuri anayo pewa na dokta Angelina pamoja na Phidaya. Kumbukumbu taratibu zikaanza kumrejea na kuwatambua watu baadhi jambo lililo zidi kutufurahisha katika familia yetu. Alipo kaa sawa nikamuelezea mama mpango wote alio kuwa ameupanga Sheila dhidi yake.
“Kumbe yule mtoto alikuwa mshenzi kiasi kile eheeee?”
“Ndio mama, hata yule Fredy wamemuua wao”
“Aiseee, ila kama umesha waua hakuja haja tena ya kuwaadisia kwa maana, hicho ndicho walicho vuna kwa yale mauovu waliyo yafanya”
“Ni kweli mama”
“Pia nisamehe Eddy wangu, kwa kuto kukusikiliza na kumuona mke wako hana maana kwangu, nikidhani waarabu wote ni magaidi”
“Hakuna haja mama ya kuniomba msamaha kwa maana mimi pia nimekukosea mengi”
Nikamkumbatia mama, akiwa kitandani amelala, ikawa ni moja ya ukurasa mwengine tulio uanza kimaisha kama mama na mwanaye. Phidaya akamuanzishia mama mazoezi ya kujifunza kutembea asubuhi na mapema pamoja na jioni, kwani kutokana na kuparalaizi, aliweza kupoteza uwezo wa kutembea na kuzungumza vizuri.
Ndni ya miezi nane mfululizo ya mazoezi pamoja na kupewa dawa za kuipa nguvu mifupa yake pamoja na mwili kwa ujumla, mama akaanza kujimudu kutembea mwenyewe kwa kutimia fimbo maalumu inayo msaidia pale anapokuwa amechoka sana. Furaha ikazidi kuongezeka katika familia yetu, huku mama akizidi kuipenda familia yangu, hadi ikafikia hatua akaanza kutulazimisha mimi na Phidaya tuweze kufunga ndoa mapema, itakavyo wezekana.
“Mama tutafunga tu ndoa”
Phidaya alizungumza huku akiwa amemshika mkono mama, akimfanyisha mazoezi ya jioni ya kutembea tembea kuzunguka nyumba.
“Sawa, unajua mukikaa sana, pasipo kufunga ndoa mutapata uvizu wa kufunga ndoa”
“Ila mama tulikuwa tunakusubiria wewe upone ili nimuoe mke wangu, mtarajiwa”
“Ndio nimesha pona sasa, unaona ninaweza hata kutembea mwenyewe, ninakula mwenyewe”
“Hahaaaaaa”
Mimi na Phidaya tukacheka kwa jinsi mama alivyo kuwa akiruka ruka, akiashiria kwamba amepona kabisa
“Mama angalia usije ukaanguka”
“Siwezi kuanguka, hembu niachie uone leo situmii fimbo kutembea, nitatembea peke yangu”
Phidaya akamuachia mama, na mimi nikaishika fimbo yake anayo itumia kuitembelea. Taratibu mama akaanza kupiga hatua za kutembea. Jambo lililo tushangaza sote, kwani kutoka kitandani hadi leo anaweza kutembea mwenyewe ni kwa msaada wa mwenyezi Mungu ndio umemfikisha hapa.
“Munaona munaona naweza kutembea mwenyewe”
Kadri tulivyo zidi kwenda mbele ndivyo jinsi mama alivyo zidi kuongeza mwendo wa kutembea kwa haraka, japo ule mwendo wake nilio kuwa nimeuzoea haujarudi bado.
↧
Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatatu ya Disemba 19
↧
Jinsi Punyeto Inavyo Sababisha Ukosefu Na Upungufu Wa Nguvu za Kiume
Ukosefu na/ama upungufu wa nguvu za kiume, ni tatizo linalo wakabili mamilioni ya wanaume duniani. Zipo sababu nyingi zinazo sababisha tatizo la ukosefu wa nguvu za kiume.
Miongoni mwa sababu hizo ni pamoja na maradhi kisukari, presha,shinikizo la damu, moyo, figo, matatizo kwenye mishipa ya ubongo & mishipa ya uti wa mgongo, matatizo kwenye mishipa itumikayo kusafrisha damu mwilini, maradhi ya ngiri, pamoja na upigaji punyeto kwa muda mrefu.
Katika makala yetu ya leo, tutaangalia namna suala la upigaji punyeto linavyo athiri nguvu za kiume.
Kabla hatujaangalia namna suala la upigaji punyeto linavyo maliza nguvu za kiume, ni vyema tukafahamu kwanza kuhusu SAYANSI YA MFUMO WA NGUVU ZA KIUME.
Kufahamu kuhusu SAYANSI YA MFUMO WA NGUVU ZA KIUME tafadhali tembelea :
Ukisoma vizuri kuhusu mfumo wa nguvu za kiume, utagundua kuwa Suala la nguvu za kiume ni suala la kimfumo. Ili mwanaume awe na nguvu za kiume, aendelee kuwa na nguvu za kiume na azilinde nguvu zake za kiume, ni lazima ogani zote zinazo husika na mfumo wa nguvu za kiume ziwe na afya njema na ziwe na ushirikiano thabiti na wenye afya.
Vile vile , utagundua kuwa , mambo makuu muhimu katika mfumo wa nguvu za kiume ni kama ifuatavyo:
i.Mishipa imara ya ubongo na yenye afya njema
ii. Mishipa imara ya uti wa mgongo ( spinal cords )
iii.Mishipa imara itumikayo kusafirisha damu mwilini ( Blood Vessels )
iv. Mfumo imara wa usafirishaji damu mwilini
v. Mishipa ya uume iliyo imara na yenye afya njema
vi. Uhusiano imara na wenye afya kati ya mishipa ya fahamu iliyopo katika ubongo, mishipa ya kwenye uti wa mgongo pamoja na misuli & mishipa ya kwenye uume.
Hivyo basi, ili mwanaume aweze kuwa na nguvu imara za kiume, na aendelee kuwa na nguvu hizo ni lazima mambo yote muhimu katika mfumo wa nguvu za kiume yawe imara pasi na hitilafu yoyote.
Hitilafu yoyote katika mambo hayo, itasababisha ukosefu na/ama upungufu wa nguvu za kiume kwa mwanaume huyo. Pale inapotokea hitilafu ama mapungufu katika ogani zaidi ya moja kati ya zilizo tajwa hapo juu, basi tatizo kwa muhusika huwa kubwa mara dufu.
JINSI PUNYETO INAVYO SABABISHA TATIZO LA UKOSEFU & UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME.
Mwanaume anapopatwa na wazo la kufanya tendo la ndoa, ubongo hutoa ishara kwenye mishipa ya uti wa mgongo ambayo nayo husafirisha taarifa hadi kwenye mishipa & misuli ya uume.
Mishipa ya uume inapopokea taarifa hiyo, hutanuka. Na mishipa ya uume inapotanuka, hufanya mambo mawili muhimu sana :
i.Husababisha mishipa ya ateri kupanuka na hivyo kuruhusu damu kuingia kwa kasi sana ndani ya mishipa ya uume na hivyo kuufanya uume usimame na kuwa imara bara bara.
ii. Huibinya na kuiziba mishipa ya vena na hivyo kuzuia kunyonya ama kufyonza damu iliyo ingia ndani ya mishipa ya uume. ( KAZI KUBWA YA MISHIPA YA VENA ILIYO KARIBU NA MISHIPA YA UUME NI KUHAKIKISHA HAKUNA DAMU NDANI YA MISHIPA YA UUME. HIVYO BASI DAMU INAPOINGIA NDANI YA MISHIPA YA UUME, MISHIPA YA VENA HU “SENSE” JAMBO HILO KWA HARAKA NA HIVYO KUIFYONZA DAMU HIYO KUTOKA KWENYE MISHIPA YA UUME YA KUITOA NJE YA MISHIPA YA UUME. NA DAMU INAPOKOSEKANA NDANI YA MISHIPA YA UUME, HUUFANYA UUME KUSINYAA NA KULEGEA )
Mtu anayepiga punyeto husababisha mambo yafuatayo katika mwili wake :
1. Huuwa nguvu ya mishipa & misuli ya uume ambayo ndio inayo husika na kusimama kwa uume
2. Mishipa ya uume inapo sinyaa na kukosa nguvu yake ya asili, husababisha mambo yafuatayo :
i.Huondoa uwezo wa mishipa & misuli ya uume kutanuka, na hii ndio sababu inayo wafanya waathirika wa punyeto kutumia nguvu nyingi sana katika kuufanya uume usimame.
ii.Huondoa uwezo wa mishipa & misuli ya uume kuibana na kuiziba mishipa ya vena, na hii ndio sababu inayo fanya waathirika wa punyeto kufika kileleni haraka sana, kwani damu inayo ingia kwenye misuli ya uume hufyonzwa ndani ya muda mfupi sana.
Hii hutokea kwa sababu mishipa na misuli ya uume inakuwa imelegea,na mishipa ya vena inakuwa imepwaya, hivyo msuguano wowote ule hufanya mishipa ya vena kufunguka na kufyonza damu kutoka kwenye mishipa ya uume na hivyo kuufanya uume kusinyaa ndani ya dakika ama sekunde chache sana.
3. Vile vile punyeto hufanya uume kusinyaa na kurudi ndani na kuufanya uonekane kama uume wa motto mdogo.
Kwa ufupi punyeto husababisha ukosefu wa nguvu za kiume kwa sababu kuu zifuatazo :
i.Kwanza hudhoofisha na kuharibu mishipa ya uume, ambayo ndio hufanya uume kusimama.
ii.Pili hudhoofisha utendaji kazi wa mishipa ya ateri, ambayo ndio hutumika kama njia ya kusafirisha damu kupeleka kwenye misuli ya uume na ivyo kuufanya uume usimame
iii. Tatu, punyeto hupelekea kuvuja kwa mishipa ya vena na hivyo kusababisha damu kufyonzwa kwa haraka sana kila iingiapo ndani ya misuli ya uume na matokeo yake ni uume kusimama kwa muda mfupi sana wakati wa tendo la ndoa.
iv. Punyeto huathiri mtiririko wa damu kwenda kwenye mishipa ya uume, kwa sababu hudhoofisha misuli & mishipa ya uume pamoja na mishipa ya ateri ambayo ndio hutumika katika kusafirisha damu kwenda kwenye uume
DALILI ZA MTU ALIYE ATHIRIWA NA PUNYETO
Dalili kuu za mtu aliye athiriwa na punyeto ni kama ifuatavyo:
i. Uume kusinyaa na kuwa kama wa mtoto
ii. Uume kurudi ndani
iii. Uume kusimama ukiwa legelege
iv. Kufika kileleni haraka wakati wa tendo la ndoa.
TIBA YA NGUVU ZA KIUME KWA MTU ALIYE ATHIRIKA NA PUNYETO.
Dawa asilia ya nguvu za kiume iitwayo JIKO ni tiba bora na ya uhakika kabisa kwa mtu aliye athiriwa na punyeto. Dawa hii, pamoja na mambo mengine mengi, husaidia kufanya mambio yafuatayo katika mwili wa mwanaume aliye athiriwa na punyeto :
i.Kuimarisha mishipa & misuli ya uume ulio legea na hivyo kuurejeshea uwezo wake wa asili
ii. Hutibu tatizo la uume kurudi ndani
iii.Humaliza tatizo la kusimama kwa uume ukiwa legelege
iv.Hutibu na kuponya kabisa tatizo la kufika kieleleni haraka.
BEI YA DAWA : Dawa hii inapatikana kwa gharama ya SHILINGI ELFU THEMANINI TU (Tsh. 80,000/=)
MAHALI INAPOPATIKANA : Dawa hii inapatikana katika duka la dawa asilia liitwalo NEEMA HERBALIST & NUTRITIONAL FOODS CLINIC lililopo jijini DAR ES SALAAM katika eneo la UBUNGO nyuma ya jengo la UBUNGO PLAZA karibu na SHULE YA MSINGI UBUNGO NATIONAL HOUSING.
Kwa wateja wasio weza kufika ofisini kwetu. Watafikishiwa dawa mahali popote walipo jijini DAR ES SALAAM.
Kwa wateja waliopo mikoani watatumiwa dawa kwa njia ya MABASI
Kwa wateja waliopo Zanzibar wata fikishiwa dawa kwa njia ya usafiri wa boti.
Na kwa wateja waliopo UGHAIBUNI watatumiwa dawa kwa njia ya POSTA ama DHL.
MAWASILIANO : WASILIANA NASI KWA SIMU NAMBA 0766 53 83 84.
Kwa taarifa zaidi kuhusu huduma zetu, tutembelee kila siku kwenye blogu yetu :
↧
Waziri Mkuu Aunda Tume Ya Kuchunguza Taarifa Za Uhamisho Wa Faru John........Aagiza Kaburi Lake Litafutwe.
WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amesema Serikali imeunda tume kuchunguza taarifa inayoelezea utaratibu uliotumika kumhamisha faru John kutoka Hifadhi ya Ngorongoro kwenda Sasakwa Black Rhino Sanctuary iliyoko kwenye Hifadhi ya Grumeti Serengeti pamoja na kutafuta kaburi la faru huyo.
Amesema timu hiyo ya wataalamu tayari imeshafika Sasakwa VIP Grumet kwa ajili ya kutafuta kaburi na kuchukua vinasaba vya masalia ya faru John na kisha watakwenda kwenye Hifadhi ya Ngorongoro kuchukua vinasaba vya watoto wake na kuvilinganisha na pembe hiyo ili kubaini kama kweli pembe aliyopelekewa ni ya faru John au la.
Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo Jumapili, Desemba 18, 2016 wakati wa majumuisho ya ziara yake ya kikazi mkoani Arusha. Ziara hiyo ililenga kukagua utekelezaji wa shughuli za maendeleo na kuona utoaji wa huduma kwa wananchi.
"Tume niliyounda kwa ajili ya uchunguzi wa faru John imetua VIP Grumet Serengeti kujiridhisha kama kuna kaburi la faru John na kama lipo wachukue vinasaba na baada ya hapo watakwenda Creter na kuchukua vinasaba vya watoto wa faru John na kuvipima kwa pamoja. Lengo ni kutaka kubaini kama pembe iliyowasilishwa kwangu Disemba 9 mwaka huu ni ya faru John,” alisema.
Waziri Mkuu alisema wakati faru John akiwa V I P Grumet taarifa zilisema ni mgonjwa na daktari alipompima mara ya kwanza akabaini faru huyo hakuwa na ugonjwa wowote.”Daktari alimpima tena kwa mara ya pili taarifa zikasema tena si mgonjwa ghafla wakasema amekufa. Hili haliwezekani,”.
Waziri Mkuu alisema ameiagiza timu hiyo kufanya kazi ya uchunguzi wa taarifa hizo kikamilifu kwa sababu Serikali imetumia fedha nyingi kuwaleta faru hao kutoka nchini Afrika Kusini. Ni lazima nyara hizo za Serikali zilindwe kwa manufaa ya Taifa.
Waziri Mkuu alipokea taarifa inayoelezea utaratibu uliotumika kumhamisha faru John kutoka Hifadhi ya Ngorongoro kwenda Sasakwa Black Rhino Sanctuary iliyoko kwenye Hifadhi ya Grumeti Desemba 9, 2016 katika kikao kilichofanyika kwenye makazi ya Waziri Mkuu Oysterbay jijini Dar es Salaam.
Kikao hicho kilihudhuriwa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe na baadhi ya watendaji wa wizara yake, Baada ya kupokea taarifa hiyo Waziri Mkuu alisema taarifa hiyo itafanyiwa kazi na wataalamu wa ofisi yake.
Akisoma taarifa hiyo mbele ya Waziri Mkuu, Prof. Maghembe alisema hadi kufikia Desemba 2015 wakati faru John anahamishwa alikuwa na watoto 26 (sawa na asilimia 70.2) ya faru wote waliokuwepo ndani ya kreta.
“Kati ya faru 37 waliokuwepo ndani ya kreta, watoto wake walikuwa 26 sawa na asilimia 70.2. Uamuzi wa kumuondoa John ulikuwa ni muhimu ili kuwezesha kuongezeka kwa faru weusi na kupunguza tatizo la ‘inbreeding’ ndani ya Hifadhi ya Ngorongoro,” alisema Waziri Maghembe.
Baada ya kuhamishiwa Sasakwa, Waziri Maghembe alisema Julai 10, 2016 afya ya faru John ilianza kudorora na alikufa tarehe 18 Agosti, mwaka huu.
Taarifa hiyo iliandaliwa na Kamati ya Taifa ya Kuwalinda Tembo na Faru. Kamati hiyo inaundwa na Mkurugenzi Mkuu wa TAWIRI, Mkurugenzi Mkuu wa TANAPA, Mkurugenzi Mkuu wa NCAA na Mhifadhi Mkuu wa Ngorongoro.
Akikabidhi pembe za faru huyo mbele ya Waziri Mkuu, Kaimu Mkurugenzi Msaidizi wa Kitengo cha Kupambana na Ujangili wa Wanyamapori, Bw. Robert Mande alimweleza kwamba pembe kubwa ya faru John ilikuwa na uzito wa kilo 3.6 na pembe ndogo ilikuwa na uzito wa kilo 2.3.
Desemba 6, mwaka huu, akiwa ziarani mkoani Arusha, Waziri Mkuu aliuagiza uongozi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA), umletee nyaraka zote zilizotumika kumhamisha faru maarufu kwa jina la ‘John’ kutoka kwenye hifadhi hiyo ifikapo Alhamisi, Desemba 8.
Alitoa agizo hilo alipotembelea ofisi za makao makuu ya NCAA zilizoko wilayani Ngorongoro, mkoani Arusha na kuzungumza na watumishi wa mamlaka hiyo pamoja na Wajumbe wa Baraza la Wafugaji ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi mkoani humo.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
↧
↧
Picha: Mama Janeth Magufuli Alivyoshiriki ibada kwa mara ya kwanza tangu atoke hospitali
Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli jana Jumapili ameungana na Wakristo wenzake wa Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Petro iliyopo Oysterbay Jijini Dar es Salaam ikiwa ni wiki kadhaa tangu alipougua na kulazwa hospitali.
Akiwa mwenye afya njema na furaha Mama Magufuli aliyekuwa pamoja na Mke wa Waziri Mkuu Mama Mary Majaliwa walisali ibada ya asubuhi katika kanisa hilo na baadaye kusalimiana na waumini nje ya kanisa.
Baada ya kumalizika kwa Ibada, baadhi ya Waumini wa Kanisa hilo walielezea furaha yao ya kumuona Muumini mwenzao akiungana nao katika ibada na walimuombea afya njema.
“Nimejisikia furaha sana kumuona Mama Magufuli amekuja Kanisani akiwa na afya njema na uso wa bashasha, na ninamuombea kwa Mungu aendelee kumsimamia” alisema Mama Mabula.
“Nimeshukuru sana kumuona Mama yangu Mama Magufuli, Mwanajumuiya mwenzangu Kanisani, huku afya yake ikiwa imetengemaa zaidi, tunamshukuru sana Mwenyezi Mungu na tunamuombea aendelee kumpigania afya yake izidi kuwa imara” alisema Thomas Simon.
Mwezi uliopita Mama Janeth Magufuli aliugua na kulazwa katika wodi ya Sewahaji iliyopo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili ambako alipata matibabu kwa siku mbili na kisha kuruhusiwa.
↧
Picha 4 za Mwanamuziki Darassa Baada ya Kupata Ajali Kahama
Mwanamuziki Darassa ambaye kwa sasa anafanya vizuri na wimbo wake wa Muziki jana alipata ajali akiwa na Mtayarishaji wa video Hanscana walipokuwa njiani wakirejea Dar es Salaam kutoka Kahama.
Ajali hiyo inaelezwa kuwa ilitokea eneo la Ntobo barabara ya kuelekea mgodi wa Bullyanhulu, Wilaya ya Kahama mkoa wa Shinyanga.
Taarifa kutoka eneo la tukio zinaeleza kuwa hakuna aliefariki dunia
↧
Mugabe achaguliwa kugombea tena urais 2018
Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe amepitishwa na chama chake cha Zanu- PF kuwa mgombea urais katika uchaguzi mkuu wa nchi hiyo utakaofanyika mwaka 2018.
Wajumbe wa Zanu-FP walifikia uamuzi huo wa kumpa nafasi nyingine Mugabe mwenye umri wa miaka 92 kupitia mkutano wao uliofanyika katika mji wa kusini mashariki wa Masvingo.
Mugabe amelitawala taifa hilo tangu lilipopata uhuru mwaka 1980 lakini bado chama chake kinaonesha kuwa na imani naye huku kikieleza kuwa anafaa kuwa rais kwa maisha yake yote.
Chama hicho kimefikia uamuzi huo wakati ambapo kumekuwa na maandamano ya kupinga uongozi wa Mugabe kutokana na kile kinachoelezwa kuwa ni kupinga anguko la kiuchumi na hali mbaya ya maisha.
↧
Sugu Awaomba RADHI Wakazi wa Jiji la Mbeya Baada ya Gari Yake Kuua Mtoto
Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi maarufu kwa jina la Sugu jana aliwaomba radhi wakazi wa Mbeya, wanafamilia, ndugu wa marehemu Recho Lutumo (14) aliyefariki dunia baada ya kugongwa na gari lake juzi.
Ajali hiyo ilitokea wakati gari hilo lililokuwa likiendeshwa na Gabriel Andrew (43) mbunge huyo akiwamo lilipokuwa likitoka jijini hapa kwenda Uwanja wa Ndege Songwe (Sia).
Recho ambaye ni yatima na aliyekuwa akilelewa na bibi yake Neema Lutumo, aligongwa wakati akivuka kwenye alama za watembea kwa miguu eneo la Iyunga katika barabara kuu ya Zambia.
Sugu akiwa na baadhi ya viongozi wa Chadema jijini Mbeya alishiriki maandalizi na shughuli zote za mazishi ya mtoto huyo kuanzia nyumbani ambako ndiko alikoomba radhi.
↧
↧
Mwanzilishi wa mtandao wa JamiiForums Maxence Melo Aachiwa kwa dhamana
Mwanzilishi wa mtandao wa JamiiForums Maxence Melo ameachiwa kwa dhamana leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, baada ya kukaa mahabusu kwa takribani siku 5.
Melo anakabiliwa na mashtaka matatu likiwemo la kumiliki na kuendesha tovuti ambayo haijasajiliwa hapa nchini Tanzania (JamiiForums).
Mashtaka mengine ni kuzuia na kuharibu taarifa ambazo Jeshi la Polisi wamekuwa wakizitaka kwa ajili ya uchagunguzi chini ya kifungu cha 22 cha Sheria ya Makosa ya Mitandao na kushindwa kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi na kuharibu uchunguzi chini ya kifungu cha namba 22 cha Sheria ya Makosa ya Mitandao.
↧
Sungura Amtikisa Mbatia .....Amtaka Ajiuzulu Nafasi ya Mwenyekiti NCCR-Mageuzi ili Kukinusuru Chama
Aliyekuwa Mkuu wa Idara ya Kampeni ya Chama cha NCCR-Mageuzi, Faustine Sungura, amenzisha fukuto kwa kumtaka Mwenyekiti wa chama hicho, James Mbatia kujiuzulu nafasi yake kwa madai kuwa ameshindwa kukiongoza chama hicho tangu alipoingia madarakani.
Sungura anasema bila kufanya hivyo, atashirikiana na wanachama wengine kumwondoa, kwa sababu amekisahau chama na kujikita katika shughuli nyingine zisizo na tija, jambo ambalo limechangia chama hicho kupata mbunge mmoja kwenye uchaguzi uliofanyika Oktoba, mwaka jana.
Anasema hali ilipofikia hivi sasa, chama hicho kinaweza kufa na kubaki historia ambayo haiwezi kuwasaidia wanachama wengine wanaopigania uhuru na demokrasia ndani ya nchi yao.
“Hatumwondoi Mbatia kwa sababu tunamchukia, bali tunamwondoa kwa kushindwa kuangalia masilahi ya chama na kujikita kwenye shughuli zisizo na tija, jambo ambalo limechangia kupoteza wabunge na kubaki na mbunge mmoja ambaye ndiye yeye katika uchaguzi uliofanyika mwaka jana.
“Kwa sababu nafasi ya uenyekiti si ubatizo na wala si kiungo cha mwili wake, hata tuseme tutamuumiza, hivyo basi tunaamini vijana wenye mapenzi mema na chama wataungana na mimi kuhakikisha kuwa mwenyekiti anatoka madarakani ili tuweze kukiendesha chama,”- Sungura.
Anadai kuwa lengo lao ni kufanya siasa zenye tija, zikiwamo za kuzunguka mikoani kutafuta wanachama wapya na kuandaa viongozi ambao wataweza kukisimamia chama hadi uchaguzi ujao wa mwaka 2020.
Anasema kutokana na hali hiyo, nafasi yake itakabidhiwa kwa mwanachama mwingine kama alivyonyang’anywa mwenzake na kijiti kukabidhiwa yeye ili aweze kukiongoza chama.
Sungura alijunga na chama hicho tangu mwaka 1992, akiwa mwanachama mwenye kadi N0. 00011763.
Ofisa Utawala wa chama hicho, Frolian Mbeo, alipoulizwa kuhusu kauli ya Sungura, alisema hadi jana mchana hakuwa na taarifa yoyote ya kuwapo malalamiko ya mwanachama huyo.
Alisema uamuzi wa Sungura, umekuja baada ya kutolewa kwenye nafasi ya ukurugenzi wa kampeni, jambo ambalo limemfanya kuzunguka mikoani na kuanza kukisema vibaya chama.
↧
Picha: Mshindi wa shindano la Miss World 2016 lililofanyika jana Marekani
Jana, Jumapili Disemba 18, 2016 jijini Washington DC, Marekani lilifanyika shindano kubwa la kumsaka Mrembo wa Dunia (Miss World 2016) ambapo nchi mbalimbali zilishiriki kwa kuwapeleka warembo walioibuka na ushindi katika nchi hizo.
Shindano hilo lilimalizika kwa Mrembo kutoka nchini Puerto Rico, Stephanie Del Valle (19) kunyakuwa taji la Mrembo wa Dunia 2016 (Miss World 2016).
Mrembo huyo alitangazwa mshindi baada ya kuwashinda warembo wengine kutoka nchi 116 duniani kote na Tanzania ikiwa moja wapo.
Mshindi wa pili ni Yaritza Miguelina Reyes Ramirez kutoka Jamhuri ya Dominican huku nafasi ya tatu ikiwenda kwa Natasha Mannuela kutoka Indonesia.
Hapa chini ni picha za tukio hilo lililofanyika jana.
↧