Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Daladala Dodoma zagoma kupinga manyanyaso

$
0
0
Zaidi ya mabasi 70 ya daladala yanayosafirisha abiria katika baadhi ya njia za manispaa ya Dodoma, yamegoma kutoa huduma kwa siku nzima ya leo kutokana na madai ya kunyanyaswa na askari wa usalama barabarani.

Daladala hizo zinazotoa huduma kati ya Jamatini na Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) pamoja na Jamatini na Veyula, zilisimamisha huduma zake kwa siku nzima ya leo zikipinga manyanyaso ya askari hao.

Baadhi ya madereva wa mabasi hayo, wamesema wamechoshwa na manyanyaso kutoka kwa askari hao kwa vitendo vyao vya kuwakamata kiuonevu.

Wamesema sababu kubwa ya mgomo wao ni rushwa na manyanyaso wanayofanyiwa na baadhi ya askari hao wa usalama barabarani.

Hata hivyo, akijibu malalamiko ya madereva hao, Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani mkoa wa Dodoma, Marisone Mwakyoma, amesema sheria zipo wazi kama kuna mtu anaombwa rushwa na kutoa, wote wana makosa kwa sababu zipo ngazi za kuripoti matukio hayo.

Afisa Mfawidhi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra) mkoa wa Dodoma, Conrad Shio, amesema baada ya kutokea kwa mgomo huo waliweza kutoa kibali kwa magari mengine kuweza kubeba abiria wasipate shida ya usafiri.

Mahakama Kuu Yaamuru Mwanafunzi wa UDOM Aliyefukuzwa Chuo kwa Kuongoza Mgomo Arudishwe Masomoni

$
0
0
MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dodoma imetengua uamuzi wa Baraza la Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) ya kumfukuza mwanachuo Phillip Mwakibinga na kuamuru arudishwe ili kumalizia masomo yake.

Uamuzi huo ulitolewa jana na Naibu Msajili wa Mahakama Kuu, John Chaba kwa niaba ya Jaji Awadhi Mohamed aliyekuwa akisikiliza shauri hilo.

Mwakibinga alikuwa akisoma Shahada ya Kiswahili mwaka wa tatu wakati akisimamishwa na alikuwa Waziri Mkuu wa Kitivo cha Sayansi ya Jamii. Katika uamuzi huo, mahakama ilisema mlalamikaji hakupewa nafasi ya kusikilizwa na hivyo kukiuka haki ya asili ya mlalamikaji. Pia mlalamikaji hakupewa haki ya kusikilizwa na hakuandikiwa mashtaka rasmi.

“Baraza liliegemea upande moja bila kumhoji wala nafasi ya kusikilizwa na kujitetea,” alisema. 

Mwakibinga alifukuzwa Udom Januari 14, mwaka jana, kwa madai ya kuongoza mgomo ambapo siku hiyo baraza la chuo lilikaa na kumfukuza bila kupewa nafasi ya kusikilizwa.

Alifungua kesi Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma kutaka mahakama kutengua uamuzi huo. Kwa mujibu wa wakili wa Mwakibinga, Elias Machibya alisema awali waliomba ruhusa ya kufungua kesi na wakapewa Februari 5, mwaka jana wakiomba kutengua maombi ya baraza la Chuo Kikuu cha Dodoma.

“Tulipata kibali cha kufungua kuomba kutengua maamuzi ya Chuo Kikuu cha Dodoma kwa kumfukuza,” alisema.

Alizitaja sababu kuu tatu za kupinga mwanafunzi huyo kufukuzwa chuo kuwa ni pamoja na kutopewa nafasi ya kusikilizwa, hakuna hatua za nidhamu zilizochukuliwa, walimfukuza wakidai aliwahi kuhusika na migomo ya nyuma.

 Alidai barua ya kumfukuza ilisainiwa na Profesa Shaban Mlacha.

Januari 14, mwaka jana uongozi wa Udom ulimfukuza Mwakibinga ambaye wakati huo alikuwa Waziri Mkuu wa Serikali ya wanafunzi, Kitivo cha Sayansi ya Elimu ya Jamii, na kupewa barua ya kusimamishwa kutokana na kosa la kuhamasisha mgomo.

Uongozi huo ulisema Mwakibinga amefukuzwa kabisa kwa kuwa alishawahi kujihusisha na mgomo wa mwaka 2010/2011 akafukuzwa lakini akakata rufaa na kuomba msamaha kwenye Kamati nidhamu.

“Baada ya kukata rufaa Kamati ikamuonea huruma ikamrudisha kabla ya kurudi alitakiwa aje na kiapo kutoka kwa mwanasheria kwamba hatajihusisha na mgomo tena lakini akarudia tena kosa hilo."

Mwakibinga amesema amefurahia uamuzi huo kwani ndio sababu ya msingi ya kufungua kesi na mahakama imetenda haki. Alisema anasubiri barua ya hukumu ambayo itatoka kesho ndipo taratibu zake za kurudi chuo zitakapoanza.

Mkuu Brigedi ya Nyuki JWTZ afariki dunia

$
0
0
KAMANDA wa Brigedi ya Nyuki ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Brigedia Jenerali Cyril Mhaiki, amefariki dunia katika Hospitali ya Jeshi ya Lugalo, Dar es Salaam, alikokuwa akipatiwa matibabu.

Katika salamu zake za rambirambi kwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Tanzania, Davis Mwamunyange, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Ali Mohamed Shein, alisema jana kuwa, amepokea kwa huzuni kubwa taarifa za kifo cha Brigedia Jenerali Mhaiki aliyefikwa na mauti juzi.

Dk Shein kwa niaba yake na ya wananchi wote Zanzibar, alisema wamepokea kwa mshtuko, taarifa ya kifo cha Kamanda huyo hodari aliyetoa mchango mkubwa katika shughuli za ulinzi na usalama na maendeleo ya nchi.

Aidha, salamu hizo za rambirambi zilieleza kuwa Brigedia Jenerali Mhaiki ameacha pengo kubwa, si tu kwa familia yake, bali kwa Brigedi ya Nyuki, JWTZ na nchi kwa ujumla, huku akisisitiza kuwa mchango wake hautosahaulika.

Alimuomba Mwamunyange kuzifikisha salamu hizo za rambirambi kwa wanafamilia, maofisa na wapiganaji wa vikosi vyote vya ulinzi na usalama.

Pamoja na hayo, salamu hizo zilimuomba Mwenyezi Mungu awape moyo wa subira ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huku akimuomba Mwenyezi Mungu kumlaza mahala pema Kamanda huyo.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Disemba 16

Waziri Mkuu Acharuka....Asema NGO Chonganishi Zitafutwa

$
0
0
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa ametoa miezi sita ya kujitathimini mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs) yanayofanya kazi zake wilayani Ngorongoro mkoani Arusha, kama yanafanya kazi kwa misingi ya sheria na maadili.

Baadaye, yatahakikiwa na kama yatabainika yanachochea migogoro, yatafutwa.

Pia, Majaliwa amezicharukia NGOs nyingine zinazoitangaza vibaya Tanzania kimataifa kwa kupiga picha za kudhalilisha watoto wakiwa wanatembea kwenye mawe huku wamevaa kandambili kubwa, kuonesha nchi ni masikini. Ametaka NGOs hizo kuondoka nchini, la sivyo serikali itazishughulikia.

“Hizi NGOs zingine si muondoke, nendeni kwingine mkafanye kazi. Halafu nyie mnaotuma picha za kudhalilisha watoto wakiwa wamevaa kandambili kubwa, kudai nchi za nje eti Tanzania ni masikini, tutawashughulikia,” alisema Majaliwa alipozungumza na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro jana.

Aidha alisema Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) atakuja wilayani hapo kukagua kazi walizozifanya, wanazozifanya na miradi wanaosaidia jamii.

Majaliwa aliwaambia watumishi hao wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro pamoja na wadau mbalimbali wakiwemo wakurugenzi wa mashirika yasiyo ya serikali, yanayofanya shughuli zake wilayani hapo, kuwa serikali haitaki mashirika chochezi wa migogoro na itayafuta.

Alisema serikali haitasita kuyafuta mashirika yanayofanya kazi wilayani humo, ambayo yapo kwa nia ya uchochezi na kuacha kufanya kazi katika malengo yaliyokusudiwa.

Waziri Mkuu alisema wilaya hiyo, ina mashirika yasiyo ya serikali 30 ambayo yamesajiliwa, lakini yanayofanya kazi ni 19 tu.

Alisisitiza kuwa haiwezekani serikali isajili mashirika hayo, lakini utendaji kazi wake uwe hafifu.

Alisema ukifuatilia, mashirika hayo utagundua kuwa yanapokea fedha nyingi, lakini hakuna cha maana wanachokifanya kwa wananchi. Alisema serikali ina taarifa ya NGOs hizo zinazopewa fedha na wafadhili.

“Najua taarifa zenu mnapokea kiasi gani cha fedha na mnazifanyia nini, lakini namleta Mkaguzi wa serikali ili akague mnatumiaje fedha zenu, nawapa miezi sita tu halafu ukaguzi utaanza, maana kuna mashirika mengi lakini kazi mnazofanya hazionekani,” alisema Majaliwa.

Alisema baadhi ya mashirika, yana akaunti nchi jirani ya Kenya na mengine kama PWC anapewa Sh bilioni 2.5 kwa mwaka na shirika la UCRT linapokea Sh bilioni 1.5 kwa mwaka, lakini hajui yanafanya nini.

“Nina taarifa zenu mnapata hela nyingi, lakini mnahudumia vipi jamii hakuna, sasa ngojeni ukaguzi ufanyike halafu nitachukua maamuzi maana kila siku Loliondo kuna nini hapa mnasajiliwa halafu hakuna cha maana,” alisema.

“Kuna nini Loliondo, kwani kila mara Loliondo nina taarifa za kila NGOs zinazofanya kazi hapa, najua mnachokifanya, sasa nawaambia serikali haitawafumbia macho kuona hiki ninachokifanya hapa na ikigundulika mnafanya kinyume na matakwa ya usajili tutazifuta”.

Alisema serikali itazifuta NGOs zote, ambazo zitabainika ni kiini cha migogoro Loliondo. Alitoa hadhari kwa kampuni zinazofanya kazi zake bila usajili, kuwa zikigundulika, zitachukuliwa hatua.

Aliwageukia watumishi wa umma na kuwatahadharisha wale wanaotoa taarifa za migogoro ya ndani kwa wahusika wa NGOs na kisha kuzituma nje ya nchi kwenye mitandao ya kijamii na barua pepe.

Alisema kuwa nao watashugulikiwa, kwa kuwa wanapaswa kuwa majibu ya migogoro na si wasambazaji wa habari mbaya za nchi.

Alisisitiza watekeleze kikamilifu kauli ya ‘Hapa Kazi Tu’ ; na si kutumia NGOs kwa ajili ya kudai kuwasaidia wananchi, huku wakijua kuwa wananchi hawanufaiki na fedha hizo wanazopewa na wafadhili Awali akizungumza na watumishi wa halmashauri ya Wilaya hiyo, Majaliwa alitoa tahadhari kwa madiwani kuacha kushirikiana na watu wa Uhasibu wanaotoa hela kwaajili ya miradi mbalimbali ya maendeleo.

Alisema baadhi ya madiwani, wanakwamisha miradi ya maendeleo kwa kula fedha kwa sababu ya ukaribu walionao.

Akizungumzia nidhamu ya fedha, Majaliwa alisisitiza kila mtumishi lazima afanye kazi kwa bidii, ikiwemo kutoa huduma bila kuwabagua wananchi kwa itikadi zao za vyama.

Afande Sele aanika sababu za kuitosa ACT Wazalendo

$
0
0
Mwanamuziki mkongwe, Selemani Msindi maarufu kama Afande Sele ameeleza sababu zilizopelekea jana kutangaza kung’atuka ndani ya Chama Cha ACT – Wazalendo mwaka mmoja baada ya harakati za uchaguzi Mkuu ambao aliutumia kugombea ubunge wa Morogoro Mjini.

Afande Sele ameeleza kuwa moja kati ya sababu zilizopelekea yeye kung’atuka ni kutofikia malengo yake ya kuingia ndani ya chama hicho ya kupata ubunge.

“Nimejitoa ACT- Wazalendo kwa makusudi kabisa na hili lilikuwa ni jambo tarajiwa, kitu cha kwanza moja ya matarajio yalikuwa baada ya mimi kuingia ACT nakuwa Mbunge ila sasa sikupata Ubunge na kama ningeupata Ubunge basi nisingejitoa ndani ya chama,” Anasema Afande Sele .

Jana, kupitia ukurasa wake wa Facebook, mwanamuziki huyo alieleza kuwa amechukua uamuzi huo sio kwa bahati mbaya hivyo uamuzi wake uheshimiwe. Alisisitiza kuwa hatajiunga na chama chochote cha siasa hadi pale ambapo ataamua vinginevyo.

Mei mwaka jana, Afande Sele alitangaza kugombea ubunge wa Morogoro mjini kupitia ACT-Wazalendo lakini hakufanikiwa kuupata ubunge wa jimbo hilo kupitia sanduku la kura, Oktoba 25 mwaka jana.

Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) Lataka Mmiliki wa Jamii Forums Aachiwe Mara Moja

$
0
0
Kwa muda wa siku tatu sasa Jeshi la Polisi Tanzania linamshikilia Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Jamii Media Limited, Maxence Melo katika Kituo Kikuu cha Polisi Mkoa wa Dar es Salaam.

Hadi sasa, si Melo, familia yake au wanasheria wake walioelezwa kosa linalomfanya ashikiliwe. Wanasheria wa Melo wameweka kambi katika Kituo Kikuu cha Polisi Dar es Salaam, lakini hakuna majibu ya maana wanayopewa na wala Melo hafikishwi mahakamani.

Taarifa wanazotoa askari waliopo kituoni hapo, ambazo si taarifa rasmi, ni kwamba Melo anashikiliwa kwa nia ya kumtaka awape polisi majina wanayoyahitaji ya wachangiaji wa masuala mbalimbali katika mtandao wa Jamii Forums kwa mujibu wa Sheria ya Makosa ya Mtandaoni huku wakidai ni maelekezo kutoka “juu”.

Siku ya Jumatano, Desemba 14, 2016 polisi wamefika ofisini na nyumbani kwa Melo wakapekua sehemu zote. Taarifa kutoka ofisini kwa Melo zinaonyesha polisi wamechukua nyaraka mbalimbali ikiwamo hati ya kusajili kampuni, leseni ya biashara na nyingine.

Pia polisi wameondoka na wafanyakazi wawili wa Kampuni ya Jamii Forums kwa mahojiano zaidi.

Taarifa nyingine zinaonyesha kuwa polisi wanaomshikilia Melo wanajiapiza kuwa hata kama mawakili wake watakwenda mahakamani hawatamwachia hadi atekeleze wakitakacho.

Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) linafuatilia kwa karibu mwenendo na utendaji wa Jeshi la Polisi juu ya suala la uhuru wa kujieleza na kutoa maoni unaotolewa na Ibara ya 18 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (1977).

Katika siku za karibuni, TEF na Watanzania kwa ujumla wanashuhudia ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu unaofanywa na Jeshi la Polisi linaloelekea kuacha kuheshimu misingi ya utawala wa Sheria na Katiba ya Tanzania.

Melo kama mtuhumiwa anayo haki ya kufikishwa mahakamani kujibu tuhuma katika muda usiozidi saa 24. Kitendo cha polisi kumshikilia kwa siku tatu, ambapo hatujui kama anateswa au la, ni uvunjaji mkubwa wa haki za binadamu.

Tamko la Haki za Binadamu la Mwaka 1948 linavitaka vyombo vya dola kuheshimu utawala wa sheria ambao pamoja na mambo mengine msingi wake ni kuheshimu mgawanyo wa madaraka (separation of power). Kitendo cha Polisi kuanza kuchukua sheria mkononi kwa kukamatakamata watu, kuwatisha waandishi wa habari na watetezi wa haki za binadamu hakikubaliki.

TEF inalitaka Jeshi la Polisi kumwachia mara moja Melo bila masharti au kumfikisha mahakamani na kumfungulia mashitaka kwa mujibu wa sheria ikiwa ana kosa. 

Tunamwomba Rais John Magufuli aingilie kati mzozo huu na kuwafahamisha polisi kuwa wanayoyatenda wanapalilia mbegu ya chuki katika nchi jambo ambalo si jema waliache mara moja.

TEF inaungana na Watanzania kulaani kitendo cha polisi kumkamata Melo kwa kutumia sheria mbaya isiyokubalika ya Makosa ya Mtandaoni. 

TEF inatetea haki ya uhuru wa kutoa mawazo na kukataa ukandamizaji huu wa polisi wanaodai wana maelekezo kutoka juu chini ya uongozi wa Serikali ya Awamu ya Tano. Mungu ibariki Tanzania.


Theophil Makunga,
Mwenyekiti,
Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF)
Dar es Salaam, Desemba 15, 2016

Ndalichako Asitisha Ajira za Walimu Wa Masomo ya Sanaa

$
0
0
WAZIRI wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako, ametoa masharti mapya ya ajira za ualimu nchini, huku akisema Serikali haitaajiri walimu wa masomo ya sanaa (arts) kwa kuwa wapo wa kutosha.

Akizungumza mjini Dodoma jana wakati akifungua mkutano mkuu wa mwaka wa Wakuu wa Shule za Sekondari Tanzania (TAHOSSA), Profesa Ndalichako, alisema Serikali kwa sasa haiwezi kuajiri walimu wa masomo hayo kwa kuwa inataka kuajiri walimu wa masomo ya sayansi na hisabati ambao idadi yao ni ndogo.

“Pamoja na uamuzi huo mpya, ajira za walimu wapya wa masomo ya sayansi nazo zimebadilika kwani wale wote waliohitimu ualimu wa sayansi na hisabati, wanatakiwa watume vyeti vyao kabla ya kupangiwa kituo cha kazi.

“Kuhusu wale walimu wa ‘arts’, kule tuna walimu wa ziada ambao tutajaribu kuwapanga kutokana na shule, kwani wengi walikuwa wamepangwa shule moja. Kwahiyo, tutaangalia utaratibu wa kuwapanga kulingana na mahitaji,’’ alisema Profesa Ndalichako.

Akizungumzia suala la ubora wa elimu nchini, Profesa Ndalichako aliwataka walimu wakuu hao kuhakikisha wanasimamia ubora wa elimu kwa kuwa wao ndio wanaowaandaa wanafunzi kabla hawajaenda vyuoni.

“Vilevile pelekeni takwimu sahihi za wanafunzi waliopo katika shule zenu kuisaidia Serikali katika kupanga bajeti ili iweze kutoa fedha sahihi.

“Hapa kuna kimbembe, yaani wakati mwingine huwa najifanya nimepoteza takwimu ya shule fulani, nikiziomba na kutumiwa, zinakuwa ni tofauti na zile za mwanzo.

“Hili nawaomba mkalisimamie ili iwe rahisi kwetu kupanga bajeti yenye tija,’’ alisema.

Kuhusu ujenzi wa maabara katika shule za sekondari, waziri huyo alisema kwamba kutokana na nyingi kukamilika, Serikali itatoa vifaa vya maabara kuanzia Januari mwakani baada ya kuwa vimeingia nchini kutoka vilikoagizwa.

Awali, akisoma risala ya walimu hao, Rais wa TAHOSSA, Bonus Nyimbo, aliiomba Serikali itoe waraka wa kupiga marufuku matumizi ya simu kwa wanafunzi shuleni kwa kuwa zimekuwa zikichangia kushuka kwa ufaulu kwa baadhi ya wanafunzi.

“Ili kuboresha elimu, tunaiomba Serikali itoe waraka wa kupiga marufuku matumizi ya simu kwa wanafunzi kwani simu nyingi tunazozikamata tunakuta mule hakuna taaluma,’’ alisema Nyimbo.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Global Education Link, Abdulmalik Molel, ambaye pia kampuni yake ilipewa tuzo ya heshima katika kuendeleza elimu nchini, alisema ni jukumu la kila mmoja kutimiza wajibu wake ili kuiendeleza elimu ya Tanzania.

“Kila mmoja anapaswa kutimiza wajibu, wazazi, walezi na walimu, waambieni wanafunzi wasiwe na ‘expectation’ (matarajio) makubwa kwani wanapokuwa na matarajio hayo, wakienda vyuo vikuu wanakuwa wasumbufu,” alisema.

Wakati hayo yakiendelea, juzi taarifa ilitolewa jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Maimuna Tarishi, ikisema kwamba, walimu wahitimu wa masomo ya sayansi na hisabati waliohitimu shahada na astashahada mwaka 2015, wanatakiwa kuwasilisha nakala za vyeti vya elimu ya sekondari vya kidato cha nne na sita na taaluma ya ualimu kwa uhakiki.

Pamoja na hayo, hivi karibuni Serikali ilitangaza kusitisha ajira zote nchini ili kukabiliana na wimbi la watumishi hewa.

Sambamba na uamuzi huo, nyongeza za mishahara kwa watumishi wa Serikali nazo zilisimamishwa ili kukabiliana na watumishi hao hewa ambao walikuwa wakiingizia hasara Serikali.

Mwanzilishi wa JamiiForums afikishwa mahakamani....Ashindwa Kutimiza Masharti ya Dhamana

$
0
0
Mwanazilishi wa Mtandao wa JamiiForums aliyekamatwa na Polisi kuanzia juzi Maxence Melo, leo amefikishwa mahakamani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisitu Jijini Dar es Salaam leo asubuhi na kusomewa mashtaka matatu.

Melo amefikishwa mahakamani leo ikiwa ni baada ya sitofahamu kubwa iliyokuwa imetanda kuhusu kosa hasa la kukamatwa kwake ambapo tangu alipokuwa amekamatwa zaidi ya saa 24 zilizopita hakuwa amefikishwa mahakamani huku Polisi wakiwa wamefanya upekuzi ofisini kwake na  nyumbani.

Maxence Melo amepandishwa kizimbani leo na kusomewa mashtaka matatu yanayomkabili likiwemo la kumiliki na kuendesha tovuti ambayo haijasajiliwa hapa nchini Tanzania (JamiiForums).

Mashtaka mengine ni kuzuia na kuharibu taarifa ambazo Jeshi la Polisi wamekuwa wakizitaka kwa ajili ya uchagunguzi chini ya kifungu cha 22 cha Sheria ya Makosa ya Mitandao na kushindwa kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi  na kuharibu uchunguzi chini ya kifungu cha namba 22 cha Sheria ya Makosa ya Mitandao.

Kwa mujibu wa taarifa zilizokuwa zimetolewa na tovuti ya JamiiForums jana, walisema kuwa ‘server’ ya tovuti yao haipo nchini Tanzania wala barani Afrika lakini hawakutaja ni nchi gani ilipo.

Melo apelekwa rumande Keko hadi Jumatatu Disemba 19 mwaka huu baada ya kukosa mdhamini katika shtaka la tatu la kumiliki na kuendesha tovuti ambayo haijasajiliwa nchini.

Utafiti wa NIMR Wagundua watu 83 waliougua ugonjwa wa zika Hapa Nchini

$
0
0

Watu 83 hapa chini wamegundulika kuwa na maambukizi ya virusi vya ugonjwa zika kati ya watu 533 waliochukuliwa sampuli za damu.

Utafiti uliofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu nchini (NIMR) kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Kanisa Katoliki Bugando, umeonyesha kuwa watu hao walipata maambukizi hayo kati ya mwaka 2015 na 2016.

Wakati NIMR ikitoa ripoti yake ya utafiti kuhusu kugundulika watu waliokuwa na virusi vya zika nchini, Januari 31 Serikali ilitoa taarifa kukanusha kuwapo kwa ugonjwa huo nchini.

Taarifa hiyo iliyotolewa kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ilitaarifu: “Kumekuwepo na taarifa kupitia vyombo mbalimbali vya habari vya kitaifa na kimataifa kuhusu Homa ya Zika ambao ni ugonjwa unaosababishwa na kirusi kijulikanacho kama “Zika Virus”.

“Ugonjwa wa Homa ya Zika bado haujaingia Tanzania. Wananchi waondoe hofu juu ya uwepo wa ugonjwa huu. Hata hivyo, ni muhimu kwa kila mmoja wetu kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya magonjwa ya zika, dengue na malaria ambayo huenezwa kwa namna inayofanana.”

Jana, Mkurugenzi Mkuu wa NIMR, Dk Mwele Malecela alikutana na waandishi wa habari kueleza ripoti ya utafiti wao ikionyesha zika ipo Tanzania na wanaendelea na utafiti kujua ukubwa wa tatizo.

“Utafiti huu ulifanyika kuanzia mwaka 2015 hadi 2016 katika mikoa nane, ambapo jumla ya sampuli 533 za damu zilipimwa na kati yao, watoto wachanga 80 walizaliwa na ulemavu wa viungo mbalimbali ambapo baada ya kufanya utafiti tulibaini asilimia 43.8 ya watoto hao wachanga walikuwa wameambukizwa virusi vya ugonjwa wa zika katika mikoa hiyo,” alisema Dk Malecela.

Aliitaja mikoa iliyofanyiwa utafiti huo kuwa ni Mwanza, Simiyu, Shinyanga, Geita, Kigoma, Tabora, Singida na Morogoro na kwamba bado taasisi hiyo na Chuo Kikuu cha Bugando wanaendelea na utafiti huo ili kujua ukubwa wa tatizo hilo katika mikoa hiyo.

Dk Malecela alisema hayo jana wakati akitoa taarifa ya mafanikio ya taasisi hiyo katika kipindi cha mwaka mmoja ambapo alisema kati ya watu 533 waliopimwa, watu 83 sawa na asilimia 15.6 waligundulika kuwa na maambukizi ya virusi vya ugonjwa wa zika na hivyo kupatiwa matibabu ya haraka.

“Kwa wale watoto wachanga 80 waliozaliwa na ulemavu, asilimia 43.8 walikuwa wameambukizwa virusi vya zika na mpaka sasa bado tunaendelea na utafiti kubaini ukubwa wa tatizo hili na kuchukua hatua za haraka,” alisema Dk Malecela.

Alisema kwa sasa wanaendelea na utafiti katika mikoa hiyo kwa wanawake waliopata matatizo ya kuharibika kwa mimba ili kujua ukubwa wa tatizo hilo.

Dk Salvatory Florence kutoka Idara ya Magonjwa ya Watoto ya Hospitali ya Hubert Kairuki alisema ugonjwa huo hauna tiba ni kama ugonjwa wa dengue ulivyo ambapo mgonjwa anapaswa kunywa maji mengi.

Dk Florence ambaye pia ni Mhadhiri Chuo cha Kumbukumbu ya Hubert Kairuki, alisema wajawazito wa miezi mitatu wapo katika hatari ya kuzaa watoto wenye matatizo ya mtindio wa ubongo na watoto wenye vichwa vidogo (microcephalus) endapo wataambukizwa virusi hivyo kupitia kwa mama zao.

“Zika ni ugonjwa unaosababishwa na kirusi kijulikanacho kama “Zika Virus na unaenezwa na mbu aina ya Aedes ambaye huwa ana tabia ya kuuma asubuhi na pia nyakati za mchana na wakati mwingine jioni,” alisema Dk Florence.

Pia, utafiti wa Nimr ulionyesha kuwa waendesha bodaboda katika mkoa wa Dar es Salaam, wapo hatarini kupata virusi vya Ukimwi.

Utafiti huo uliofanyika katika jiji hilo Agosti mwaka huu, umeonyesha kuwa licha ya madereva hao wa pikipiki kuwa na maambukizi madogo ya VVU kwa asilimia 2.5, bado wapo hatarini kutokana na kuwa na wapenzi wengi huku wengi wao wakigoma kutumia kinga.

Vodacom Tanzania Na WCB (Wasafi) Waja Na ‘Nogesha Upendo’

$
0
0
Katika muendelezo wa kuwapatia wateja wake na watanzania wote kwa ujumla burudani za sikukuu, Vodacom Tanzania kwa kushirikiana na wasanii wa WCB imeandaa matamasha mawili ya kukata na shoka ambayo yatafanyika katika msimu huu wa sikukuu katika Mikoa ya Dar es Salaam na Iringa.

Akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa kampuni hiyo, Nandi Mwiyomella, alisema matamasha hayo makubwa ya muziki wa kizazi kipya yatafanyika katika mikoa ya Dar e salaam na Iringa chini ya wasanii Diamond Platinumz, Rayvanny, Rich Mavoko, Harmonize  na Queen Darleen.
 
“Kama mnavyoelewa msimu huu huwa umeambatana na shamrashamra mbalimbali za sikukuu na mitoko ukiwa  na familia yako, Desemba 24 kutashushwa shoo ya nguvu katika fukwe za Jangwani Sea Breeze Hotel ambapo kutakua na tamasha la kihistoria la  “Vodacom Wasafi Beach Party” na Iringa tamasha litafanyika siku ya Krismasi katika uwanja wa  Samora na matamasha yote yataanza saa nane mchana”. Alisema.
 
Mwiyombella alisema burudani hii ya muziki inakwenda sambamba na promosheni ya “Nogesha Upendo” http://vda.cm/nogeshaupendo ya Vodacom inayolenga kuwapatia wateja wote wa mtandao wa Vodacom zawadi za sikukuu ikiwa ni shukrani kwa wateja ambapo pia wateja wanayo fursa ya kujishindia tiketi za bure za kushiriki katika matamasha haya makubwa katika msimu huu wa sikukuu.
“Ili kujishindia tiketi ya bure anachotakiwa kufanya mteja wa Vodacom ni kupiga*149*01# kisha nunua kifurushi chochote cha Vodacom na moja kwa moja atakua ameingia katika droo ya kuweza kujishindia tiketi.  Zawadi nyingine kemkem kupitia promosheni ya Nogesha Upendo ni fedha taslimu, muda wa maongezi, Vifurushi vya intaneti (Mb)”.Alisema.
 
Naye Msanii wa muziki wa kizazi kipya anayetamba katika anga za kimataifa, Diamond Platinumz akiongea kwa niaba ya wasanii wa WCB alitoa wito kwa wakazi wa jiji la Dar es Salaam na Iringa kujitokeza kwa wingi siku ya shoo hizo kwani zitakuwa ni shoo za kihistoria katika mikoa hii miwili kufanywa na Vodacom kwa kushirikiana na WCB,Napenda kuwahakikishia mashabiki wetu kwamba tutakamua vilivyo tukiwa na wasanii wenzangu wote wa WBC kwa “Kunogesha Upendo” Alisisitiza Diamond.
 

Kafulila ahama NCCR, ahamia Chadema

$
0
0

Mbunge wa zamani wa Jimbo la Kigoma Kusini kwa tiketi ya Chama cha NCCR-Mageuzi, David Kafulila leo ametangaza kukihama chama hicho na kusema kuwa atajiunga na Chama cha Demokrasia na Manendeleo (CHADEMA).

Kafulila ambaye alijizolea umaarufu mkubwa katika bunge la kumi kwa kufichua hoja mbalimbali za ufisadi amesema kuwa ameshawasilisha barua ya kujiuzulu kwa uongozi wa chama hicho.

Akieleza sababu iliyomsukuma kujiunga na CHADEMA, Kafulila alinukuliwa akisema kuwa kikubwa ni kuhakikia wanaleta mabadiliko nchini Tanzania. 

"Ili kufanya safari kuwa fupi, kuondoa vikwazo vya huyu yuko chama hiki mwingine kile nimemamua kujiunga na CHADEMA ili kurahisisha uletaji mabadiliko katika nchi yetu sababu nimeona uhitaji huo," alisema Kafulila.

Katika uchaguzi uliopita Kafulila alipoteza jimbo la Kigoma Kusini ambalo lilikwenda wa Hasna Sudi Katunda Mwilima aliyekuwa akigombea kupitia Chama cha Mapinduzi.

Tangaza Biashara Yako Au Bidhaa Yako Kwenye Mtandao huu Kwa BEI NZURI Kabisa

$
0
0

Tunakaribisha  matangazo  ya  aina  zote.Bei  zetu  ni  nzuri  sana  na  kamwe  hutajuta  kutangaza  biashara  yako  kupitia  mtandao  huu....

Kwa Siku tunafunga na Pageviews zaidi  ya  laki tano kama graph  inavyoonyesha  hapo  chini
Kama  una  tangazo, basi  wasiliana  nasi  kwa  kutuandika  email  ambapo  tutakutumia  bei  ya  matangazo.

Email  yetu:  mpekuziblog@gmail.com

Pata Dawa za Asili za Kupunguza Maziwa, Kuondoa Michirizi, Kuongeza Unene, Kuondoa Chunusi na Zingine Nyingi Toka Beauty Cosmetics

$
0
0
NATURAL BEAUTY COSMETICS Ni wauzaji wa vipodozi aina mbali mbali na vyenye matokeo mazuri na ya haraka zaidi bila kemikali wala madhara yoyote
 
     Tunazo za:👇👇👇👇
1. Kutengeneza shepu hipsi na makalio kwa:- (a) Dawa ya kunywa au Botcho yakupaka @ 150,000/= (b)Vidonge maalum @ 150,000/=
2. Kupunguza au kuongeza maziwa @ 90,000
3. Kushepu miguu kuwa (Chupa ya bia) @ 100,000
( Kuludisha bikra (@) 100,000/=
4. Kuondoa mipasuko au michirizi @90,000/=
5.Kuwa softi na mweupe mwili mzima kwa mafuta @90,000/= vidonge maalum @150,000
6.Kuongeza unene wa mwili mzima @120,000/=
7.kupunguza tumbo na manyama uzembe kwa:-
(a)Dawa ya kunywa au kupaka @ 120,000/=
(b) Mkanda original wa MICRO COMPUTER @200,000/=
8.Kuondoa chunusi na madoa sugu (@) 90,000/=
9.Kuondoa mvi milele na zisiludi tena @ 100,000
10.Kuongeza maumbile kwa:- (a)Gel ya kupaka @100,000/= Mashine original ya HANDSOME UP @170,000/=
11.Kuondoa vinyweleo @80,000/=
12.kuotesha nywele kwenye kipara @100,000/=
13.Kuongeza nguvu za kiume na hamu ya tendo @100,000/=
14.Kuondoa makovu sehemu yoyote @90,000/=
 
     WASILIANA NASI KWA :-
          065 9618585 au
             0759029968.
 
Popote ulipo utapata huduma. BIDHAA  zetu zote ni GARANTII  na risiti ili kuhakikisha mafanikio yako
 
           Follow us
   👇👇👇👇👇👇
@natural2162
@natural2162
@natural2162
@natural2162
@natural2162
      👆🏻👆🏻👆🏻👆🏻👆🏻👆🏻

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumamosi ya Disemba 17


Waziri Mkuu: Waliouza Kiwanja Cha Shule Wachukuliwe Hatua

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro, Bw. Rashid Taka na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Bw. Raphael Siumbo kufanya uchunguzi na kuwachukulia hatua watendaji wote watakaobainika kuhusika katika uuzwaji wa kiwanja cha shule ya msingi Waso.

Ametoa agizo hilo Alhamisi, Desemba 15, 2016 wakati akihutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye kata ya Waso Wilaya ya Ngorongoro akiwa katika ziara ya kikazi mkoani Arusha.

Waziri Mkuu alisema Serikali haiwezi kuvumilia kuona watendaji wachache wasiokuwa waadilifu  wanamega kiwanja cha shule na kukiuza kwa maslahi yao, hivyo aliwataka viongozi hao kufuatilia na kumpa taarifa ya hatua za kisheria walizochukua kwa wahusika.

“Mkuu wa wilaya na Mkurugenzi hapa kuna malalamiko ya viwanja fuatilieni viwanja hivyo vinavyolalamikiwa na wananchi ni viwanja gani je hiyo ya kwamba mmeuza viwanja vya shule ameuziwa nani,” alisema.

Aidha, Waziri Mkuu amemtaka Bw. Taka ahakikishe Mkuu wa Idara ya
Ardhi, Maliasili na Mzingira, Bw. Switbeth Byorushengo anatekeleza majukumu yake ipasavyo. Ametoa agizo hilo baada ya wananchi kudai Ofisa huyo ameshindwa kufanya kazi na kumuomba Waziri Mkuu aondoke naye.
Alisema Bw. Byorushengo anatakiwa kuhakikisha halmashauri hiyo inapima viwanja vya kutosha na kutoa hati kwa wananchi ili waweze kupata maeneo ya kujenga makazi na shughuli zingine za kijamii.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu alimuagiza Mkurugenzi wa halmashauri hiyo Bw. Byorushengo kuhakikisha halmashauri hiyo inaanza ujenzi wa hospitali ya wilaya na ifikapo Aprili, 2017 awe amepewa taarifa za ulipofikia ujenzi huo.Kwa upande wake Mkurugenzi huyo alisema tayari wapo katika mchakato wa ujenzi wa hospitali ya wilaya ambapo wametenga sh. milioni 800 za kuanzia.

Akizungumzia kuhusu mgogoro wa ardhi kati ya vijiji vya Tarafa ya Loliondo na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Waziri Mkuu alitoa muda wa siku 30 kwa uongozi wa Shirika la Hifadhi za Taifa Nchini (TANAPA) wawe wamekamilisha uhakiki wa mpaka huo.

Naye Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi ambaye ni Mbunge wa Ngorongoro Mheshimiwa William Ole Nasha alimuomba Waziri Mkuu kuwasaidia kutatua mgogoro huo wa ardhi kwa kuwa ni wa muda mrefu na unakwamisha shughuli za maendeleo.

Awali, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Bw. Mrisho Gambo alisema Wilaya ya Ngorongoro inachangamoto nyingi ikiwemo ya ardhi na sasa kuna mgogoro kati ya Kampuni ya Thomson Safari na wananchi ambao wanadai kuwa ardhi hiyo ilichukuliwa kinyemela na mwekezaji huyo bila ya wao kushirikishwa.

Alisema baada ya ziara ya Waziri Mkuu kumalizika mkoani hapa atarudi wilayani Ngorongoro kwa ajili ya kutatua kero mbalimbali ikiwemo ya ardhi na matumizi mabaya ya fedha zinazotolewa na wawekezaji ambazo matumizi yake hayajulikani.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Waziri Mkuu Amsimamisha Kazi Mwekahazina Wa Wilaya Ya Bahi.......Aagiza arudishwe Longido kujibu tuhuma zinazomkabili

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemsimamisha kazi aliyekuwa Mwekahazina wa Halmashauri ya Wilaya ya Longido, Bw. Issai Mbilu ambaye kwa sasa amehamishiwa Wilaya ya Bahi mkoani Dodoma na kuagiza arudishwe haraka na kuja kujibu tuhuma za ubadhilifu sh. milioni 642.4 za miradi zinazomkabili.

“Tunaendelea kudhibiti na kuweka nidhamu ndani ya Serikali. Ukiharibu Longido usitegemee kuhamishiwa wilaya nyingine tunamalizana hapa hapa. Hatuwezi kuhamisha ugonjwa hapa na kuupeleka wilaya nyingine hivyo Mwekahazina huyu arudishwe haraka Longido,” amesisitiza.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo jana Ijumaa, Desemba 16, 2016 wakati akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Longido kwenye ukumbi wa Halmashauri hiyo akiwa katika ziara ya kikazi mkoani Arusha.

Pia amemuagiza Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha, Bw. Richard Kwitega kumuandikia barua Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) akimuomba amrudishe Mwekahazina huyo katika kituo chake cha kazi cha zamani ili aweze kujibu tuhuma zinazomkabili.

Amesema Serikali haitamvumilia mtumishi wa idara yoyote atakayeharibu jambo halafu kuhamishwa sehemu nyingine, “hivyo naagiza kuanzia sasa nimemsimamisha kazi Mwekahazina huyu na arudi hapa kujibu kwanini ameleta hasara ya hizi fedha. Na nyie watumishi wengine hili liwe funzo kwenu,” amesema.

Amesema miradi mingi ya maendeleo inakwama kwa sababu ya baadhi ya watumishi kuweka mbele maslahi binafsi badala ya kuzingatia maadili ya utumishi, hivyo amewaagiza Wakuu wa Idara wafuatilie kwa makini miradi inayotekelezwa katika maeneo yao kama inalingana na thamani halisi ya fedha zilizotolewa.

Akizungumzia kuhusu kushamiri kwa biashara haramu ya dawa za kulevya wilayani Longido, Waziri Mkuu amewaagiza wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya wilaya kufanya kufanya msako wa nyumba hadi nyumba na kuwakamata wote watakaokutwa wanafanya biashara hiyo.

“Wilaya hii ina sifa mbaya ya kuwa kitovu cha kusafirisha dawa ya kulevya zikiwemo bangi na mirungi. Hivyo nawaagiza wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama waendeshe msako kwa kila nyumba na atakayekamatwa achukuliwe hatua. Dawa za kulevya zinadhohofisha nguvu kazi ya Taifa,”.

“Ukivuta bangi unapishana na kauli mbiu ya Hapa Kazi Tu kwani unakwenda kulala jambo ambalo hatuwezi kulikubali. Watakaokutwa wanauza au kununua mirungi na bangi wakamatwe na kuchukuliwa hatua za kisheria ikiwa pamoja na kutaifisha magari yanayotumika kubeba bidhaa hiyo haramu,” amesema.

Awali, Mkuu wa Wilaya hiyo Bw. Daniel Chongolo akisoma Taarifa ya Wilaya amesema Longido inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo kutumika kama njia kuu ya kusafirisha dawa za kulevya aina ya bangi na mirungi kwenda nchi jirani ya Kenya ambako biashara hiyo imehalalishwa.

Changamoto nyingine ni ukosefu wa hospitali ya wilaya hali inayofanya wananchi kwenda kutibiwa Kenya, ambapo Waziri Mkuu alisema haiwezekani wakakosa hospitali ya wilaya hivyo amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kuhakikiusha anatenga fedha za ujenzi huo.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amesema Serikali ipo mbioni kujenga kiwanda cha kuchakata madini ya magadi soda ili yawe na ubora na thamani kubwa. Ametoa kauli hiyo aliposimamishwa na wananchi katika kijiji cha Loonolwo kilichopo Kata ya Gelai Merugoi Wilayani Longido akitokea wilayani Ngorongoro.

Amesema lengo la kujenga kiwanda hicho ni kuwawezesha wananchi wa wilaya hiyo hasa akinamama wanaoishi karibu na Ziwa Natron linalotoa magadi hayo waweze kunufaika na uwepo wa ziwa hilo.

Waziri Mkuu amesema ujenzi wa kiwanda hicho utawezesha vijana na akinamama hao wanaouza magadi maeneo ya pembezoni mwa barabara katika ziwa Natron kupata ajira kwa kuwa kitazalisha ajira zaidi ya 500 katika wilaya hizo mbili za Longido na Ngorongoro.

Pia amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Bw. Mrisho Gambo kushirikiana na wataalam wake kufanya tathimini ya uhaba wa chakula katika wilaya za Longido na Ngorongoro ili Serikali ijue Mkoa wa Arusha una ukosefu wa chakula kwa kiasi gani.

"Gambo fanya tathimini ya hali ya njaa katika wilaya hizi mbili ili tuweze kuwasaidia wananchi hawa. Hata hivyo nawaomba wananchi mtunze kiasi cha chakula mlichonacho na marufuku tumia nafaka kwa ajili ya kupika pombe,” amesema.

Awali, wananchi hao waliokuwa na mabango mbalimbali walilalamikia kero ya mipaka ya ardhi kati ya vijiji vya wilaya za Longido na Ngorongoro, ambapo Waziri Mkuu alimuagiza Afisa Ardhi Mkoa wa Arusha, Bw. Hamdoun Mansour kwenda katika vijiji hivyo vya mpakani na kukutana na viongozi wa kimila ili kumaliza mgogoro huo.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Taarifa ya Bodi ya Mikopo kwa wadaiwa sugu kuhusu mwisho wa kulipa kwa hiari

$
0
0
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu imeongeza muda kwa wadaiwa sugu kulipa madeni yao hadi Desemba 30, 2016.

Hatua ya Bodi inafuatia mwitikio chanya kutoka kwa wadaiwa ndani ya siku 30 za awali ambazo zinakamilika leo Desemba 14, 2016.

Akitoa taarifa ya kuongezwa kwa muda; Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi, Abdul_Razaq Badru amesema kuwa wadau wameomba kuongezewa muda kutokana na baadhi yao kukabiliana na changamoto za majukumu ya kazi na hivyo kushindwa kujitokeza ndani ya siku 30 zilizokuwa zimetangazwa awali.

Katika hatua nyingine, Bw. Badru amesema kuwa ndani ya siku za nyongeza Ofisi za Bodi ya Mikopo zilizopo Mwenge, jijini Dar es Salaam zitaendelea kuwa wazi kwa siku za Jumamosi, Disemba 17, 2016 na Jumapili, Disemba 18, 2016 kuanzia saa 3:00 asubuhi hadi saa 9:00 alasiri ili kutoa fursa muhimu kwa wadaiwa wote wa mikopo ya elimu ya juu ambao hawajaanza kurejesha mikopo yao kupata taarifa kuhusu madeni yao na kulipa.

Ili kuharakisha utoaji wa muhtasari wa deni la mdaiwa; mhusika aje na Majina yake kamili, Chuo alichosoma, Mwaka wa kuanza na wa kuhitimu, anuani yake ya barua pepe (email), nambari ya simu ya kiganjani, mwajiri wake na Check Number yake iwapo ameajiriwa serikalini.
‘Kuwa Mzalendo, Rejesha Mkopo wa Elimu ya Juu’

Kwa mawasiliano zaidi piga 0763 459165 au 0767 513208

Imetolewa na:
MKURUGENZI MTENDAJI
BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU
14/12/2016

Serikali Yakanusha Kuwepo Kwa Ugonjwa wa ZIKA Nchini

$
0
0
WIZARA ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, imesema hakuna uthibitisho wa kuwepo kwa ugonjwa wa Zika nchini.

Imeeleza kuwa utafiti uliofanyika ni wa kuangalia ubora wa kipimo cha ugonjwa huo.

Ufafanuzi wa Wizara hiyo umekuja siku moja baada ya Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), kutoa ripoti ya utafiti uliofanywa na taasisi hiyo kwa kushirikia na Chuo Kikuu cha Kanisa Katoliki Bugando, inayoeleza kuwepo wa maambukizi ya virusi vya Zika katika jamii ya Watanzania.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu alitoa ufafanuzi huo kwa waandishi wa habari jana, ambapo alisema wananchi wanapaswa kuondoa hofu kwa kuwa ugonjwa huo haujaingia nchini.

“Napenda kuwatoa hofu wananchi kwa sasa haijathibitishwa kuwepo kwa ugonjwa wa Zika nchini…wao walifanya utafiti nchini wa kuchunguza ubora wa kipimo cha kupima magonjwa ya Zika na Chikungunya, hawakupima kama zika ipo nchini au hakuna,” alisema Waziri Ummy.

Alisema wizara yake itaendelea kushirikiana na taasisi mbalimbali, kutafiti ili kubaini kama ugonjwa wa Zika upo nchini au la.

Wizara hiyo pia imeshaanda mkakati wa Zika nchini, unaoelekeza kufuatilia ugonjwa huo.

Mganga Mkuu wa Serikali, Mohammed Kambi alisema, NIMR walichokifanya ni kufanya utafiti wa kutathmini ufanisi na ubora wa kipimo, ambacho kinaweza kuja kutafiti magonjwa ya zika na mengine na kwamba kiutaratibu hizo ni hatua za awali.

Alisema, taarifa hiyo ya NIMR itafanyiwa tathmini ya kisanyasi ili wanasayansi wajiridhishe kama ilifuata taratibu zote na matokeo hayo yanaweza kuendelezwa mbele zaidi na baadae kuweka mikakati ya kuzidi kuthibisha uwepo wa ugonjwa huo.

“Tuna taratibu hizo za upande wa kitaalamu lakini kuna taratibu katika kutoa tamko, kuhusu uwepo wa ugonjwa kama huu kwasababu ni aina ya uginjwa unaotakiwa uripotiwe kimataifa…inabidi taarifa ije rasmi katika wizara, kuna mganga mkuu na Shirika la Afya tuangalie hizo na tukijidhihirisha taarifa rasmi inatolewa na mratibu wa magonjwa hayo,” alisema Dk Mohammed.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa NIMR, DK Mwele Malecela alisema taarifa aliyoitoa juzi, ilikuwa ni matokeo ya utafiti wa kubainisha uwezo wa kipimo hicho katika kuanisha virusi vya Zika, Dengue na Chikungunya na matokeo ya awali yalionesha uwepo wa virusi vya Zika.

Alisema pamoja na matokeo hayo, hawakuona dalili wala madhara yoyote yanayosababishwa na Zika ikiwemo Kichwa kidogo na mengine.

“Hili suala ni kwamba lilikuwa ni suala la kuainisha na katika uanishaji huo tukajikuta tumeona virusi hivyo, lakini hiyo haimanishi kuna uthibitishio, naomba nisisitize uthibitisho wa ugonjwa unatolewa na wizara ya afya kwa kufuata uatartibu maalumu uliowekwa,” alisema.

Alisema kuwa wataendelea kufanya utafiti hasa katika kuangalia magonjwa ya Zika, Dengue na Chikungunya na kutoa matokeo kwa kile watakachokipata katika utafiti huo.

Juzi NIMR ilitoa matokeo ya utafiti uliofanywa na taasisi hiyo pamoja na Chuo Kikuu cha Katoliki cha Bugando na utafiti kuanisha uwepo wa maambukizi ya virusi vya zika katika jamii ya Watanzania na kuangalia adhati ya maambukizi katika kusababisha watoto wanaozaliwa na ulemavu.

Sampuli za damu kutoka kwa watu 533 zilipimwa. Kati yao, watoto wachanga 80 walizaliwa na ulemavu wa viungo mbalimbali. Kati ya waliopimwa 533, 83 (15.6%) waligundulika kuwa wameambukizwa virusi vya Zika.

Kati ya wale watoto wachanga 80 waliozaliwa na ulemavu, 43.8% walikuwa wameambukizwa virusi vya Zika, utafiti unaendelea kujua ukubwa wa tatizo hili.

Rais Magufuli atengua uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR)

$
0
0
Taarifa kutoka IKULU inasema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, tarehe 16 Desemba, 2016 ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) Dkt. Mwele Malecela.

Uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa NIMR atakayejaza nafasi iliyoachwa wazi na Dkt. Mwele Malecela utatangazwa baadaye.

December 15 2016 Dr. Mwele alinukuliwa na vyombo vya habari akizungumza kuhusu uwepo wa ugonjwa wa ZIKA Tanzania na kwamba asilimia 15 ya waliopimwa walikutwa na virusi vya ugonjwa huo ambapo hata hivyo taarifa hizo zilikanushwa na wizara ya afya jana.

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images