Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Waziri Ummy azindua Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto

$
0
0
Kwa mara ya kwanza mawaziri 11 wamekutana kwa ajili ya kutokomeza vitendo vya ukatili wa kijinsia, huku Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ikiweka wazi mpango wake wa kuanzisha madawati ya kuwalinda watoto katika shule za msingi na sekondari.

Aidha, ina mpango wa kuanzisha kamati za ulinzi na usalama wa mtoto katika kila mtaa na kijiji nchi nzima, lengo likiwa ni kutokomeza vitendo vya ukatili na unyanyasaji kwa watoto.

Mawaziri hao walikutana jana katika uzinduzi wa Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto wa miaka mitano 2017/18 hadi 2021/22 uliofanyika jijini Dar es Salaam.

Akizungumza kwenye uzinduzi huo, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu alisema hatua hiyo inatokana na kuwepo vitendo vya ubakaji pamoja na vitendo vya watoto wa kiume kulawitiana.

Aliongeza kuwa licha ya kuwepo walimu wa nidhamu lakini wamekuwa wakiogopwa hivyo madawati hayo yatakuwa ni rafiki pindi mtoto anapokutana na vitendo hivyo anakimbilia katika dawati hilo.

Alifafanua kuwa kamati za ulinzi na usalama wa mtoto kwa kila mtaa na kijiji pamoja na kuanzisha mtandao wa wanaume katika kila kata ambao watakuwa wakitetea na kulinda vitendo vya ukatili.

“Ukatili mashuleni tunazungumzia ubakaji wa wakubwa, kinachosikitisha watoto wa kiume wanalawitiana katika mazingira ya shule, sisi kama wizara tumeona tuanzishe dawati la kuwalinda watoto katika shule zetu zote za msingi na sekondari,” alisema.

Akizungumza kwenye mkutano huo, Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa (UN) nchini, Alvaro Rodriguez alisema dhamira ya serikali imechangia katika kuifanya Tanzania kuwa nchi ya kwanza katika Bara la Afrika chini ya mpango mpya wa ushirikiano wa kimataifa katika kukomesha ukatili dhidi ya watoto.

Rodriguez alisema malengo ya dunia yanataka kumaliza vitendo vya ukatili kwa wanawake na watoto na badala yake kuwekeza katika kuwawezesha na kuwalinda.

Alisema UN itaendelea kushirikiana na serikali katika kuzuia ukatili wa aina yoyote kwa wanawake na watoto.

Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango aliagiza wizara, taasisi za serikali, mikoa, wilaya pamoja na mamlaka za mitaa, kuhakikisha zinazingatia mpango kazi huo kwa kutenga fedha katika bajeti zao kuanzia mwaka wa fedha 2017/18 ili kukidhi utekelezaji wa mpango huo.

Alisema utekelezaji wa mpango huo utagharimu Sh bilioni 267.4 kwa miaka mitano, ambapo unatekelezwa na Serikali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo, sekta binafsi na wananchi kwa ujumla.

Kwa upande wake, waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu, Jenista Mhagama alisema mpango huo ni muhimu kwa taifa hasa kwa wakati huu, kwa kuwa vitendo vya unyanyasaji vimekuwa vikiongezeka.

Alisema imefika mahali ambapo vitendo hivyo vinatakiwa vikome na kwamba Ofisi ya Waziri Mkuu itasimamia mpango kazi huo ili kuhakikisha unatekelezeka na kuendana na gharama halisi ili kufikia malengo.

Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Harrison Mwakyembe alisema serikali inataka kupitia sheria ya mtoto ya mwaka 2009 ili kubaini mapungufu ambyo wadau wameyaona na kuyafanyia marekebisho.

Alisema pia wanaangalia namna ya kupanua wigo wa fursa kwa wanawake na watoto katika kutafuta haki na hatua mojawapo ya kufanikisha suala hilo ni kuanzisha mfumo wa msaada wa kisheria kwa wananchi wasio na uwezo.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Stella Manyanya alisema kuwa katika kutekeleza mpango huo, wizara hiyo itahakikisha inasimamia ipasavyo katika maeoneo yote inayohusika.

Naye Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani alisema, lengo la serikali ni kuhakikisha wanapeleka umeme katika vijiji vyote kupitia REA awamu ya tatu hasa katika zahanati ili kuwasaidia akinamama kujifungua katika mazingira salama.

Aidha, pia alisema shule nyingi zinaungua kutokana na matumizi ya vibatari hivyo wamekusudia kufikisha umeme katika shule zote. Dk Kalemani pia aliwaonya wamiliki wa migodi ambao wamekuwa hawawashirikishi wanawake katika shughuli za kiuchumi.

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Anastazia Wambura alisema wizara yake itatumia idara za sanaa na utamaduni ili kuhakikisha wanatokomeza vitendo vya ukatili.

Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi alimwakilisha waziri wa wizara hiyo, Mwigulu Nchemba alisema matukio ya ukatili yamekuwa ni mengi, na kuahidi kuwa wizara itaendelea kuhakikisha wanatumiwa wanakamatwa na kufikishwa katika vyombo vya sheria.

Mawaziri wengine waliozungumza katika mkutano huo ni Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Dk Charles Tizeba, Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage. Wizara nyingine zinazoshiriki ni Ofisi ya Rais, TAMISEMI.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii. Jinsia na Watoto Mh. Ummy Mwalimu akizungumza na wadau (hawapo pichani) kwa niaba ya Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan kabla ya uzinduzi wa Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto  jijini Dar es Salaam .
Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu Mh. Jenista Joakim Mhagama akiongea na  wadau (hawapo pichani) kabla ya uzinduzi wa Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto  jijini Dar es Salaam
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mh. Charles Mwijage akiongea na wadau (hawapo pichani) kabla ya uzinduzi wa Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto  jijini Dar es Salaam
Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Harrison Mwakyembe akiongea na wadau (hawapo pichani) kabla ya uzinduzi wa Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto  jijini Dar es Salaam
Mratibu Mkazi wa  Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akiongea na  wadau (hawapo pichani) kabla ya uzinduzi wa Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto  jijini Dar es Salaam
Naibu Waziri Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo Mh. Anastazia Wambura akiongea na  wadau (hawapo pichani) kabla ya uzinduzi wa Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto jijini Dar es Salaam
Naibu Waziri Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo Mh. Anastazia Wambura (Kulia) akifurahia jambo na  kwa Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Injinia Stella Manyanya baada ya uzinduzi wa Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto  jijini Dar es Salaam . (Picha zote na Benjamin Sawe-Maelezo)

CUF Yakubali Kushiriki Uchaguzi wa Mbunge Dimani.......Mwaka jana Walisusa Baada ya Jecha Kufuta Matokeo

$
0
0

Kamati ya Utendaji ya CUF imepitisha majina matatu ya wanaowania kuteuliwa kugombea ubunge katika Jimbo la Dimani, Mkoa wa Mjini Mgharibi kisiwani Unguja. 
Wakati CUF imepitisha majina hayo yatakayokwenda kwenye mchujo wa kura ya maoni ndani ya chama hicho kupata jina moja, CCM nao wamepitisha majina matatu ambayo ni Juma Ali Juma, Hussein Migoda Mataka na Abdalla Sheria yatakayopitia mkondo huohuo. 
Uchaguzi huo utakaofanyika Januari 22, mwakani umetangazwa na Tume ya Uchaguzi ya Taifa (NEC), kujaza nafasi ya Hafidh Ali Tahir aliyefariki dunia ghafla mkoani Dodoma hivi karibuni wakati akihudhuria vikao vya Bunge. 
 CUF itakuwa ikishiriki uchaguzi huo kwa mara ya kwanza baada ya kususa ule wa marudio uliofanyika Machi 20, kutokana na kitendo cha Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha kufuta uchaguzi uliofanyika Oktoba 25, mwaka jana. 
Naibu Katibu Mkuu wa CUF Zanzibar, Nassor Ahmed Mazrui alitaja majina hayo kuwa ni Abdulrazak Khatib Ramadhan, Asha Hamad Makungu na Ahmed Abass Haji, ambao watapigiwa kura jimboni huko ili kumpata mmoja atakayeiwakilisha CUF. 
Akizungumza baada ya kikao hicho kilichoongozwa na Katibu Mkuu, Maalim Seif Sharif Hamad, Mazrui alisisitiza kuwa chama hicho hakitazikubali hujuma zote, yakiwamo masharti hayo ya NEC aliyoyaita ya mfukoni. 
Katika hatua nyingine, CUF imesema inaendelea na mazungumzo na vyama vinavyounda Ukawa kuona namna bora ya kushiriki uchaguzi mdogo ujao jimboni humo ili kuhakikisha wanaibwaga CCM. 
Kaimu Naibu Katibu Mkuu wa CUF (Bara), Joram Bashange alisema chama hicho bado ni sehemu ya Ukawa na hakuna mtu yeyote mwenye uwezo wa kutengua uamuzi huo. 
“Suala hilo lilipitishwa na Mkutano Mkuu wa Taifa uliofanyika tarehe 23 mpaka 27 Juni, 2014 na mkutano mkuu ndicho chombo cha juu kabisa na chenye maamuzi ya mwisho katika chama,” alisema. 
Kikao hicho kilikuwa na ajenda moja ya maandalizi ya uchaguzi mdogo wa madiwani 22 Tanzania Bara na ubunge wa Dimani. 
Kamati ya Utendaji ilipitisha ratiba ya uchaguzi wa ndani ya chama kwa ajili ya kuwapata wagombea wa CUF katika nafasi hizo. 
Wakati huo huo, Bashange amesema Kamati ya Utendaji ya Taifa imeshangazwa na kauli ya Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC, Ramadhani Kailima kwamba wagombea wa CUF lazima fomu zao za uteuzi zithibitishwe na kutiwa saini na pande mbili zinazohasimiana. 
“Kailima amekitoa wapi kifungu cha sheria au kanuni, alichokitumia kuweka sharti hilo la ajabu tena kwa chama kimoja tu,” alisema na kuongeza:“Huwezi kuwa na sharti linalokihusu chama kimoja tu katika kuthibitisha uteuzi wa wagombea.” 
Alisema fomu za uteuzi wa wagombea kutoka NEC huthibitishwa na katibu wa chama wa ngazi inayohusika na kwa ubunge na madiwani ni katibu wa wilaya.

Kada wa CCM Aliyetuhumiwa Kughushi Kitambulisho cha Usalama wa Taifa Aachiwa huru baada ya Jamhuri kusema hawana nia kuendelea na kesi

$
0
0
Miezi kadhaa iliyopita aliyekuwa mwenyekiti wa umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi ‘UVCCM’ Arusha, Lengai Ole Sabaya alishtakiwa kwa kosa la kujifanya ofisa usalama wa Taifa na kughushi kitambulisho cha usalama wa taifa.

Kesi hiyo imetolewa maaamuzi na mahakama ya hakimu mkazi Arusha leo December 14 2016 ambapo imemuachia huru Lengai Ole Sabaya baada ya upande wa Jamhuri kusema hawana nia ya kuendelea na kesi hiyo.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi ya Disemba 15

Jinsi Punyeto Inavyo Sababisha Ukosefu Na Upungufu Wa Nguvu za Kiume

$
0
0

Ukosefu  na/ama  upungufu  wa  nguvu  za  kiume, ni  tatizo  linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume  duniani.  Zipo  sababu  nyingi  zinazo  sababisha  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume.  

Miongoni  mwa  sababu  hizo  ni  pamoja  na  maradhi  kisukari, presha,shinikizo  la  damu, moyo, figo, matatizo  kwenye  mishipa  ya  ubongo  &  mishipa  ya  uti  wa mgongo, matatizo  kwenye  mishipa itumikayo  kusafrisha damu  mwilini, maradhi  ya  ngiri,  pamoja  na   upigaji  punyeto  kwa  muda  mrefu.

Katika  makala  yetu  ya  leo, tutaangalia  namna   suala  la  upigaji  punyeto linavyo  athiri  nguvu  za  kiume.

Kabla  hatujaangalia  namna  suala la upigaji  punyeto linavyo  maliza  nguvu  za  kiume, ni  vyema  tukafahamu  kwanza  kuhusu  SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME.

Kufahamu   kuhusu   SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME  tafadhali  tembelea :

Ukisoma  vizuri  kuhusu  mfumo  wa  nguvu  za  kiume, utagundua  kuwa   Suala  la  nguvu  za  kiume  ni  suala  la  kimfumo.  Ili  mwanaume  awe na nguvu  za  kiume, aendelee  kuwa  na  nguvu  za  kiume na  azilinde  nguvu  zake za  kiume, ni  lazima  ogani  zote zinazo  husika  na  mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ziwe  na  afya  njema  na  ziwe  na  ushirikiano   thabiti  na  wenye  afya.

Vile  vile , utagundua  kuwa , mambo  makuu  muhimu  katika   mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ni  kama  ifuatavyo:

i.Mishipa  imara  ya  ubongo  na  yenye  afya  njema

ii. Mishipa  imara  ya  uti  wa  mgongo  (  spinal  cords )

iii.Mishipa  imara  itumikayo  kusafirisha  damu  mwilini  (  Blood Vessels )

iv. Mfumo  imara  wa  usafirishaji  damu  mwilini

v. Mishipa  ya  uume  iliyo  imara  na  yenye  afya  njema

vi. Uhusiano  imara  na  wenye  afya  kati  ya  mishipa  ya  fahamu  iliyopo  katika  ubongo, mishipa  ya  kwenye  uti  wa  mgongo  pamoja  na  misuli & mishipa  ya  kwenye  uume.

Hivyo  basi, ili  mwanaume  aweze  kuwa  na  nguvu  imara  za  kiume, na  aendelee  kuwa  na  nguvu  hizo ni  lazima  mambo  yote  muhimu  katika  mfumo  wa  nguvu za  kiume  yawe  imara  pasi na  hitilafu  yoyote.

Hitilafu  yoyote  katika  mambo  hayo, itasababisha  ukosefu na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume  kwa  mwanaume  huyo.  Pale inapotokea    hitilafu  ama  mapungufu  katika  ogani  zaidi  ya  moja  kati  ya  zilizo  tajwa hapo  juu, basi  tatizo  kwa  muhusika  huwa  kubwa  mara  dufu.

JINSI  PUNYETO  INAVYO  SABABISHA  TATIZO  LA  UKOSEFU &  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.
Mwanaume   anapopatwa na  wazo  la  kufanya  tendo  la  ndoa, ubongo  hutoa  ishara  kwenye  mishipa  ya  uti  wa  mgongo  ambayo  nayo  husafirisha  taarifa  hadi  kwenye  mishipa &  misuli  ya  uume.

Mishipa  ya  uume inapopokea  taarifa  hiyo, hutanuka. Na  mishipa  ya  uume  inapotanuka, hufanya  mambo  mawili  muhimu  sana :

i.Husababisha  mishipa  ya  ateri  kupanuka  na  hivyo  kuruhusu  damu  kuingia kwa  kasi  sana   ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  hivyo  kuufanya  uume  usimame  na  kuwa  imara  bara bara.

ii. Huibinya na  kuiziba  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kuzuia  kunyonya  ama  kufyonza  damu  iliyo  ingia  ndani  ya  mishipa ya  uume.  (  KAZI  KUBWA  YA  MISHIPA  YA  VENA  ILIYO  KARIBU NA  MISHIPA  YA  UUME  NI KUHAKIKISHA  HAKUNA  DAMU NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME. HIVYO  BASI  DAMU  INAPOINGIA  NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME, MISHIPA  YA  VENA  HU “SENSE” JAMBO  HILO  KWA  HARAKA  NA HIVYO  KUIFYONZA  DAMU  HIYO  KUTOKA KWENYE MISHIPA  YA UUME  YA  KUITOA  NJE YA MISHIPA  YA  UUME.  NA  DAMU INAPOKOSEKANA  NDANI  YA  MISHIPA  YA  UUME, HUUFANYA  UUME  KUSINYAA  NA  KULEGEA )

Mtu  anayepiga  punyeto  husababisha  mambo  yafuatayo  katika  mwili  wake :

1. Huuwa  nguvu  ya  mishipa  & misuli ya  uume ambayo  ndio  inayo husika  na  kusimama  kwa  uume

2. Mishipa  ya   uume  inapo  sinyaa  na  kukosa  nguvu  yake  ya  asili, husababisha  mambo  yafuatayo :

i.Huondoa  uwezo  wa  mishipa  &  misuli  ya  uume  kutanuka, na  hii  ndio  sababu  inayo  wafanya  waathirika  wa  punyeto  kutumia  nguvu  nyingi  sana  katika  kuufanya  uume  usimame.

ii.Huondoa  uwezo  wa  mishipa &  misuli  ya  uume  kuibana  na  kuiziba  mishipa  ya  vena, na  hii ndio  sababu  inayo  fanya  waathirika  wa  punyeto  kufika  kileleni  haraka  sana, kwani damu  inayo  ingia  kwenye misuli  ya  uume   hufyonzwa  ndani ya  muda  mfupi sana. 
 
 Hii  hutokea  kwa  sababu  mishipa na  misuli  ya  uume inakuwa  imelegea,na  mishipa  ya  vena inakuwa  imepwaya, hivyo  msuguano wowote ule  hufanya  mishipa  ya  vena  kufunguka  na  kufyonza  damu  kutoka  kwenye mishipa  ya  uume  na hivyo  kuufanya  uume  kusinyaa  ndani ya dakika ama sekunde  chache sana.

3. Vile  vile  punyeto  hufanya  uume  kusinyaa na  kurudi ndani  na  kuufanya  uonekane kama  uume  wa  motto mdogo.

Kwa  ufupi  punyeto  husababisha  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  sababu  kuu  zifuatazo :

i.Kwanza   hudhoofisha  na  kuharibu  mishipa  ya  uume,  ambayo  ndio  hufanya  uume kusimama.

ii.Pili  hudhoofisha  utendaji  kazi  wa  mishipa  ya  ateri, ambayo  ndio  hutumika  kama  njia  ya  kusafirisha  damu kupeleka kwenye  misuli  ya  uume  na  ivyo  kuufanya  uume  usimame

iii. Tatu, punyeto  hupelekea  kuvuja  kwa  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kusababisha  damu  kufyonzwa  kwa  haraka  sana  kila  iingiapo ndani  ya  misuli ya  uume  na  matokeo  yake  ni  uume   kusimama  kwa  muda  mfupi  sana  wakati wa  tendo  la  ndoa.

iv. Punyeto  huathiri  mtiririko  wa  damu  kwenda  kwenye  mishipa  ya  uume, kwa  sababu  hudhoofisha  misuli &  mishipa  ya  uume  pamoja  na mishipa ya  ateri  ambayo  ndio  hutumika  katika  kusafirisha  damu kwenda  kwenye  uume

DALILI  ZA  MTU  ALIYE  ATHIRIWA  NA  PUNYETO
Dalili  kuu  za  mtu  aliye athiriwa  na  punyeto  ni  kama  ifuatavyo:

i.           Uume  kusinyaa  na  kuwa  kama  wa  mtoto
ii.         Uume kurudi  ndani
iii.       Uume  kusimama  ukiwa  legelege
iv.       Kufika  kileleni  haraka  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

TIBA   YA   NGUVU  ZA  KIUME  KWA MTU  ALIYE  ATHIRIKA  NA  PUNYETO.
Dawa   asilia  ya  nguvu  za  kiume iitwayo JIKO  ni tiba  bora  na  ya  uhakika  kabisa  kwa  mtu  aliye  athiriwa   na  punyeto.  Dawa  hii, pamoja  na  mambo  mengine  mengi, husaidia  kufanya  mambio  yafuatayo  katika  mwili  wa  mwanaume  aliye  athiriwa  na  punyeto :

i.Kuimarisha  mishipa  & misuli  ya  uume  ulio  legea na  hivyo  kuurejeshea  uwezo wake wa  asili

ii. Hutibu   tatizo  la  uume  kurudi  ndani

iii.Humaliza  tatizo  la  kusimama  kwa  uume  ukiwa  legelege

iv.Hutibu  na  kuponya  kabisa  tatizo  la  kufika  kieleleni  haraka.

BEI  YA  DAWA  :  Dawa  hii  inapatikana  kwa  gharama  ya  SHILINGI  ELFU  THEMANINI  TU (Tsh. 80,000/=)

MAHALI  INAPOPATIKANA :  Dawa  hii  inapatikana  katika  duka  la  dawa  asilia  liitwalo  NEEMA  HERBALIST  &  NUTRITIONAL  FOODS  CLINIC  lililopo  jijini  DAR  ES  SALAAM  katika  eneo  la  UBUNGO   nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA   karibu  na SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING.

Kwa  wateja  wasio  weza  kufika  ofisini  kwetu. Watafikishiwa  dawa  mahali  popote  walipo  jijini  DAR  ES  SALAAM.

Kwa   wateja  waliopo  mikoani  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  MABASI

Kwa  wateja  waliopo   Zanzibar  wata fikishiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa boti.

Na  kwa  wateja  waliopo  UGHAIBUNI  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  ama  DHL.

MAWASILIANO :  WASILIANA  NASI   KWA  SIMU  NAMBA  0766  53  83  84.

Kwa  taarifa  zaidi  kuhusu  huduma  zetu, tutembelee kila  siku  kwenye  blogu  yetu :

Kauli ya CHADEMA kufuatia kutoweka kwa kada wao Bwana Ben Sanane

$
0
0

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimesema hadi sasa hakijui alipo msaidizi wa Mwenyekiti wa chama hicho, Ben Saanane.

Kimevitaka vyombo vya dola, kuchukua hatua za haraka kuhakikisha msaidizi huyo anapatikana haraka. 

Saanane inadaiwa alitoweka katika mazingira ya kutatanisha tangu Novemba 18, mwaka huu. Juhudi za kumtafuta katika vituo vya polisi, hospitalini na vyumba vya kuhifadhia maiti, zimefanyika bila mafanikio.

Kauli hiyo imetolewa na Mwanasheria Mkuu wa chama hicho, Tundu Lissu wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu Saanane ambaye hajulikani aliko. 

Alisema hata wao hawajui alipo, hawafahamu kama yuko hai au ameshikiliwa mahali. Kwamba wanachokijua ni kwamba hawajui aliko.

“Katika mazingira haya, tunaiomba serikali na vyombo vyake vya ulinzi, ituambie kama imemkamata na inamshikilia Ben Saanane tuanzie hapo…lakini kama hawajamkamata na hawamshikilii, serikali na vyombo vyake watueleze mawasiliano yake ya mwisho yalikuwa lini, na nani, wapi na yalihusu nini,” alisema.

Alisema kwa kuwa serikali ndiyo yenye udhibiti wa mipaka yote nchini, iwaeleze kama kuna rekodi yoyote inayoonesha Ben aliondoka nchini kwa kupitia mipaka hiyo, kama ni mipaka ya nchi kavu, majini au viwanja vya ndege.

Katika hatua nyingine, alisema pamoja na majibu hayo, lakini pia wanaitaka serikali pamoja na vyombo vyake vya dola, kufukua miili ya watu waliokufa katika mto Ruvu na ifanyiwe uchunguzi ili wajulikane watu hao ni akina nani, ili isije kuwa miongoni mwa watu hao ni Saanane.

Lissu alisema kuwa mawasiliano ya mwisho kati ya Saanane na Mbowe, yalikuwa ni Novemba 14, mwaka huu wakati Saanane akiwa Dar es Salaam na mwenyekiti huyo akiwa Dodoma.

“Alimwambia mwenyekiti uko wapi, akamwambia nakwenda kwenye maziko ya Samuel Sitta, mawasiliano ya mwisho ni ya tarehe 14 Novemba,” alisema Lissu.

Alisema pamoja na kwamba Saanane alikuwa ni msaidizi wa Mbowe katika masuala ya kisiasa na kijamii, lakini hakuwa akitembea na mwenyekiti huyo na kwamba shughuli zake alikuwa akifanyia katika Makao Makuu ya chama hicho.

Lissu alisema kuwa wapo watu wanahoji inawezekanaje Mwenyekiti hajui mahali alipo msaidizi wake, lakini wanapaswa kufahamu kuwa Mbowe hakuwa akitembea na Saanane.

Alisema baada ya maziko ya Sitta, viongozi wote wa chama hicho walikuwa wakizunguka katika mikoa mbalimbali kwa ajili ya kufanya shughuli za chama, lakini katika kipindi chote hicho, mwenyekiti huyo hakuwa na msaidizi wake huyo, kwa kuwa hatembei naye na si jambo la ajabu.

“Baada ya hizi ziara, tulienda nchi za nje…katika kipindi chote hiki Mwenyekiti hakuwa na Ben na vilevile nataka niweke hii vizuri, Mwenyekiti hakupata wasaa wa kusema Ben yuko wapi, kwa sababu hatembei naye, hayuko naye muda wote.”

 “Sasa kuna watu wanaosema Mwenyekiti ndiye anayejua, atuambie yuko wapi, Mwenyekiti hajui, mimi sifahamu aliko Ben, tungekuwa tunafahamu tungeshasema,” alisema.

Alisema kwa mara ya kwanza alipigiwa simu na mdogo wake Ben, aliyemtaja kwa jina la Dorice Desemba 4, lakini hakumpata na alimtumia ujumbe kumwambia kuwa kaka yao Ben amepotea, hawajui aliko na alikuwa akitaka ushauri ambapo alimjibu waliripoti jambo hilo polisi na kwenye vyombo vya habari.

Alisema si kwamba wamenyamaza kimya, kwa kuwa wanajua alipo msaidizi huyo na kwamba watu wanaodai hivyo si sahihi. 

Alitaka mtu yeyote mwenye taarifa kuhusu Saanane alipo, azitoe taarifa hizo hadharani, polisi, kwenye chama, vyombo vya habari au kwa ndugu zake.

Aliyetobolewa macho uso kwa uso na Scorpion mahakamani......Atoa Ushahidi Jinsi Alivyo Shambuliwa na Kuporwa

$
0
0
Kwa mara ya kwanza mshitakiwa katika kesi ya unyang’anyi wa kutumia silaha na kujeruhi, Salum Njwete maarufu Scorpion, amekutana na mlalamikaji katika kesi hiyo, Said Mrisho katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala, iliposikilizwa jana.

Mrisho, ambaye ndiye shahidi wa kwanza katika kesi hiyo, aliieleza mahakama hiyo kuwa alichomwa visu tumboni na mgongoni kabla ya kutobolewa macho.

Akiongozwa na Wakili wa Serikali, Nassoro Katuga mbele ya Hakimu Mkazi, Flora Haule, Mrisho alidai kuwa wakati tukio hilo linaendelea, alimkariri mshitakiwa kwa kumuangalia usoni.

Akielezea tukio lilivyotokea, alidai Septemba 6, mwaka huu saa nne usiku alikuwa kazini kwake Tabata Segerea kwa kazi yake ya kinyozi na baada ya kufunga ofisi, alikwenda kituoni kusubiri usafiri wa kwenda nyumbani kwake Makuburi, karibu na Ubungo.

Alidai wakati anasubiri usafiri, ilipita bajaji na kumuuliza anakokwenda, ambapo alimwambia kwamba anakwenda Ubungo na mwenye bajaji alidai anakwenda Buguruni, ila anaweza kumsogeza hadi Tabata Relini ili akapande magari ya Ubungo.

‘’Wakati nishapanda bajaji na tumeelewana anifikishe Tabata Relini ghafla dereva huyo aliniomba apite njia ambayo ni fupi kutokezea Buguruni, ambapo hapo ndiko nitakapochukulia magari ya Ubungo kwani naishi Makuburi,” alidai Mrisho.

Alidai baada ya kufikishwa Buguruni Kwa Mnyamani, aliona wauza kuku na kusogea kwa ajili ya kununua ili kupeleka nyumbani kwake.

‘’Kulikuwa kuna wafanyabiashara wengi wa kuku eneo la Buguruni kituo kinaitwa Kwa Mnyamani kama saa 4:40 usiku ambapo nilinunua kuku mmoja kwa Sh 6, 000,” alidai.

Akiendelea kutoa ushahidi, Mrisho alidai wakati anaendelea na manunuzi na kuongea na muuzaji, aliona mtu amesimama upande wake wa kulia na alianza kumuita.

‘’ Aliniambia ‘broo’ nina shida. Nami nilimgeukia na kumuuliza una shida gani kama una shida sema nakusikiliza kama naweza kukusaidia nikusaidie, lakini mtu huyo hakujibu ambapo niliendelea na manunuzi,’’alidai.

Shahidi alidai wakati anaendelea na manunuzi alishikwa na hofu, kwani mkono wake alikuwa amevaa cheni ya silva na mfuko wa suruali, ulikuwa na fedha iliyokuwa inaonesha kutuna.

‘’Ghafla nilishtukia ninachomwa visu mkononi na bega la kushoto ambapo nilipogeuka niliendelea kuchomwa na nikaanza kupiga kelele ya mwizi lakini sikupata msaada, kwani nilishangazwa kuona watu wananiona lakini hawanipi msaada,’’alidai na kuongeza: 

‘’Yule mtu alijibu hakuna mtu wa kumsaidia ambapo aliendelea kumchoma visu vinne tumboni na kuanguka chini wakati huo kuna watu walikuwa wanamwita Scorpion, kwamba tayari umeshaua huku akiendelea kunikagua mfukoni,’’alidai.

Alidai wakati anaendelea kukaguliwa, mshitakiwa alimkanyaga mkono wake na kumkata cheni ambayo alikuwa amevaa mkononi na shingoni. Pia, alidai kuwa alivyodondoka chini alidondoka chali kwa hiyo alikuwa na nafasi ya kumkariri vizuri jinsi alivyo, kwa kuwa kulikuwa na mwanga wa taa.

Aliiambia mahakama kuwa, mshitakiwa aliendelea kumkagua mfukoni na kuchukua fedha zote na kwamba alisikia sauti kuwa, “Salum mwache huyo keshakufa sasa ukimchukulia na simu ndugu zake watajulishwaje?” Shahidi alidai baadaye alivuliwa fulana na kumfunga mkononi kisha akamburuza kumpeleka barabarani huku akiwaambia wenye magari wamgonge.

“Muda huo nilikuwa sijatobolewa macho ambapo niliwekwa barabarani ili nigongwe na gari, lakini yalikuwa yananipita nilikaa barabarani kama nusu saa wakati huo yeye kasimama pembeni. “Baada ya muda alinivuta pembeni na kunipiga kisu cha jicho la kushoto ambapo nilipoteza fahamu kwa muda na baadaye nilisikia mtu anadai yeye ni raia mwema anataka kunisaidia ambapo nilimpa simu na kuanza kuwasiliana na ndugu zangu,’’alidai.

Shahidi huyo alidai baada ya muda alisikia gari la polisi limefika na kumchukua hadi kituoni kwa ajili ya kupewa Fomu Namba Tatu(PF3) kwa ajili ya matibabu. 

Aidha, alidai kwa kuwa alikuwa anasikia maumivu, alichukuliwa maelezo akiwa ndani ya gari ambapo baadaye alifikishwa Hospitali ya Amana na kupewa huduma ya kwanza.

Shahidi huyo alidai alipofika Amana, alikutana na ndugu zake na baada ya muda alipelekwa Hospitali ya Taifa Muhimbili, ambapo alipewa kitabu cha kusaini kwa ajili ya kufanyiwa upasuaji tumboni. 

Pia alidai baada ya muda, daktari wa macho alimfanyia uchunguzi na kueleza kuwa macho yametobolewa, ambapo alikaa hospitali kwa siku sita.

Kabla ya kuanza kutoa ushahidi huo, mshitakiwa ambaye alipandishwa kizimbani saa 3.35 asubuhi, aliomba mahakama isianze kusikiliza shauri hilo hadi wakili wake wa utetezi afike. 

Mahakama hiyo ilikubaliana na ombi hilo, ambapo baada ya dakika 15 kupita wakili alifika na kuanza na usikilizwaji.

Kwa mujibu wa hati ya mashitaka, mshitakiwa ambaye ni mwalimu wa karate, alitenda kosa hilo Septemba 6, mwaka huu maeneo ya Buguruni Sheli wilayani Ilala.

Ilidaiwa mshitakiwa aliiba cheni ya dhahabu gramu 38 yenye thamani Sh 60,000, kibangili cha mkononi na Sh 331,000 pamoja na pochi, vyote vina thamani ya Sh 476,000, mali ya Said Mrisho.

Ilidaiwa kabla ya wizi huo, alimchoma na kisu tumboni mgongoni na machoni. Kesi hiyo itaendelea na ushahidi Desemba 28, mwaka huu na mshitakiwa alirudishwa rumande.

Wafuasi wa Lipumba na Maalim Seif wapigana tena mahakamani

$
0
0

Mahakama  Kuu Kanda ya Dar es Salaam, jana iligeuka kuwa uwanja wa masumbwi, baada ya wafuasi wa Chama cha Wananchi (CUF) kupigana na kusababisha watu watatu kujeruhiwa.

Wafuasi hao ni wa Bodi ya Wadhamini ya Chama walio upande wa Katibu Mkuu, Maalim Seif Sharif Hamad na wanaomuunga mkono Mwenyekiti wa chama hicho, Profesa Ibrahim Lipumba.

Tukio hilo la aina yake, lilitokea kabla ya kuingia kwenye chumba cha mahakama, tayari kwa kusikiliza uamuzi wa kujitoa au kuendelea kwa Jaji Sekiet Kihiyo kusikiliza kesi hiyo na baada ya kutoka mahakamani.

Hata hivyo, Jaji Kihiyo alitupilia mbali maombi ya bodi ya wadhamini kwamba asiendelee na kesi hiyo, kwa madai kwamba hawana imani naye, kwa kusema kuwa maombi hayo, hayana msingi kwa kuwa sheria inamruhusu kutojitoa kirahisi kwenye kesi.

Alieleza kuwa wadau hawana nafasi kujichagulia jaji wanayemtaka. Kabla ya kuingia kwenye chumba cha mahakama, mfuasi mmoja wa Profesa Lipumba na wanaodaiwa kuwa wafuasi wa Maalim Seif, walianza kurushiana ngumi na kuleta mtafaruku katika eneo la watu wanaosubiria kesi zao kuitwa huku Lipumba akionekana kulindwa na walinzi mbalimbali.

Aidha, baada ya jaji kutoa uamuzi huo, wafuasi wote walitoka nje, ambapo wakati Profesa Lipumba akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kesi hiyo, wafuasi hao walianza kupigana na kujeruhi watu watatu, ambapo mmoja wao, aliyejulikana kwa jina la Robert Samson, alijeruhiwa kwa kutumia kitu chenye ncha kali shingoni na kusababisha kuvuja damu nyingi.

Hali hiyo iliendelea kwa wafuasi wa bodi ya udhamini, kulalamikia walinzi wa mahakama, kwamba ni kwa nini wanakagua watu, lakini wameshindwa kuwaona wenye silaha, ikiwemo visu na kusababisha watu wao kujeruhiwa.

Pia walidai kuwa licha ya kuwepo kwa askari wengi mahakamani hapo wakiwa na silaha, walishindwa kutuliza ghasia hiyo, ambayo imeleta madhara, kwa kuwa kila mfuasi aliyemuona adui yake alishikana naye shati na kupigana.

Kabla ya vurugu hizo kuisha, Profesa Lipumba na wafuasi wake walipanda magari yao huku wakimwimbia nyimbo za kumsifu mwenyekiti huyo na kuondoka. Waliwaacha wafuasi wa bodi ya wadhamini, wakilalamikia kitendo cha kupigwa.

Walijiapiza kwamba watajipanga ili siku kesi hiyo itakapoitwa tena, watahakikisha wanawadhibiti wapinzani wao na kwamba wataleta madhara makubwa mahakamani hapo.

Awali, akitoa uamuzi huo, Jaji Kihiyo alisema kuwa Novemba 10 mwaka huu, mawakili wa bodi ya wadhamini ya CUF, wakiwakilishwa na Rahim Khalfan, waliandika barua kwa Msajili wa mahakama hiyo, kuomba jaji huyo ajitoe, kwa kuwa wateja wao hawana imani naye.

Alisema kuwa hawezi kujitoa, kwa sababu zisizo za msingi, kwamba anaupa upendeleo upande wa washitakiwa na kuwaacha waombaji wakati hakukuwa na mazingira ya kuruhusu kutolewa hoja kwa pande zote.

“Mahakama ya Rufaa inasema majaji au mahakimu hawatakiwi kujitoa kwa urahisi kwenye kesi. Pia sheria hairuhusu wadau ambao wanakuja kwa mara ya kwanza mahakamani na hawajui taratibu za mahakama watake kujichagulia jaji,” alisema Jaji Kihiyo.

Alisisitiza kuwa jaji au hakimu ana mamlaka chini ya sheria, kujitoa au kuendelea kusikiliza shauri, kama ataridhika kwamba sababu zilizotolewa, zina nguvu ya kushawishi afanye hivyo.

Tamko la LHRC na THRDC kuhusu kukamatwa mwanzilishi wa JamiiForums

TCRA Wafanya Ukaguzi Wa Mwisho Na Kuiruhusu Radio 5 Kurudi Hewani Dec. 16

$
0
0
Mamlaka ya Mawasiliano Nchini Tanzania (TCRA) , jana December 14 imefanya Ukaguzi wa mwisho, kujiridhisha na kuruhusu Kituo cha Utangazaji cha Radio5 Arusha kurudisha Matangazo yake hewani ifikapo December 16 mwaka huu 2016.
 
Akiongea na Viongozi na baadhi ya Wafanyakazi wa Radio 5 baada ya kukamilisha ukaguzi wao, Mkurugenzi wa Utangazaji wa TCRA Bw. Fredrick Ntobi alisema wao kama Mamlaka Waliamua kuja kufanya ukaguzi wao kwa ajili ya kujiridhisha kurudisha Matangazo ya Kituo hicho hewani December 16 ambapo ndiyo tarehe rasmi ya kuisha kwa adhabu waliyokuwa wametoa kwa  kituo hicho.
 
Kituo cha Radio 5 kilisimamishwa na TCRA kurusha matangazo yaketoka  tarehe 16 September 2016 kwa kukiuka baadhi ya kanuni.
 
Mamlaka hiyo ilifanya ukaguzi wa Studio ya Kurusha Matangazo (On air Studio), Studio ya kuzalisha Vipindi (Production Studio), Chumba cha Habari (News room), Control Room, ofisi zote za Kituo pamoja na Mnara wa Kurushia Matangazo ambapo kote wamekuta kila kitu kiko sawa kwa kazi kama Mamlaka inavyotaka.
 
Hata hivyo Bw. Fredrick Ntobi akiwa ameongozana na Viongozi wa  TCRA kanda ya Kaskazini, aliwakumbusha Watangazaji na Waandishi kufuata Maadili ya uandishi wa habari ili kulinda Vituo vyao na Kulinda taaluma zao kwa ajili ya kuendelea kuhabarisha na kuelimisha Jamii nzima ya Watanzania.
 
“Mimi niwasisitize tu kuendelea kufuata maadili ya taaluma yenu ya uandishi wa habari, kufuata sheria na kanuni za uandishi wa habari ambao mmesomea, tumieni lugha Sanifu ambayo inakubalika kwa jamii na tasnia yenu na niwatakie maandalizi mema ya kurudi hewani pamoja na Sikukuu zinazokuja”. Alimaliza kwa Msisitizo Bw. Fredrick Ntobi.
 
Hata hivyo kwa upande wa Mkurugenzi wa Tan Communication Media inayomiliki kituo cha Radio5, Bw. Robert Francis, aliwataka Wasikilizaji wa Radio5 kukaa mkao wa Kuhabarika, Kupata Burudani na kuelimika zaidi kupitia Radio5 kwani Wamejipanga vyakutosha kurudi hewani kwa Kishindo.
 
“Mimi niwaombe tu wasikilizaji wetu ambao najua wametumiss sana, wakae tayari Kuhabarika, kuelimika na kuburudika zaidi sababu mimi na Wafanyakazi wangu tumejipanga vya kutosha haswa ukizingatia kwamba mwaka mpya ndo huu unakuja. 

"Kingine niwape pole tu wasikilizaji wetu wote kwa kutotusikia hewani kwa kipindi cha miezi mitatu, pamoja na Wadau ambao tumekuwa tukishirikiana kwa pamoja katika mambo mbali mbali niwaambie tu tunarudi rasmi Ijumaa ya tarehe 16 December 2016”. Alisema Mkurugenzi wa Radio5 Robert Francis.

RC Paul Makonda Atimiza Ahadi yake ya Misaada ya Milioni 164

$
0
0
Mkuu  wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, amekabidhi vitu vyenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 164 alivyoahidi kwenye ziara zake na pikipiki tano kwa Saidi Mrisho aliyetobolewa macho na ‘Scorpion’.

Kuanzia Novemba 19 hadi 28, Makonda alifanya ziara katika wilaya za Dar es Salaam kujua matatizo ya wananchi na kuahidi kutekeleza baadhi ya mambo.

Akizungumza jana, Makonda alisema ameona ni vema akaanza kutekeleza baadhi ya ahadi zake kabla mwaka kumalizika, huku mambo mengine yakisubiri utekelezaji kutoka ngazi za juu za uongozi.

Makonda alikikabidhi kituo cha kurekebisha tabia cha Kigamboni magodoro 50, runinga, king’amuzi, mitungi miwili ya gesi na jiko.

Pia alikabidhi gari la kubeba wagonjwa kwa Jeshi la Polisi Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) Ukonga, na tumba za kwaya ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Sekondari ya Jitegemee ilipewa mabati 2,000, shule ya msingi Mbagala Annex mabati 1,000, shule ya Katoliki mifuko 10,000 ya saruji, soko la samaki Msasani mabati 300, kanisa la AIC matofali 10,000 na mabati 200 kwa ajili ya Uwanja wa Taifa.

Katika kuthamini viongozi wanaojituma, alitoa pikipiki kwa mtendaji wa kata ya Mbuyuni na Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Buguruni.

Pia hakuwaacha nyuma wajasiriamali kwani alimkadidhi Lumino Evance mtaji wa Sh milioni moja na mama muuza machungwa Zuhura Waziri mtaji wa Sh 200,000.

Kutokana na changamoto ya maji Ukonga, Makonda alikabidhi Sh milioni 13 ili wananchi wa Gongo la Mboto na Pugu wapate maji. Pia alitoa Sh 500,000 kwa ajili ya kukamilisha tangi la maji kwa wananchi wa Buyuni, kata ya Pemba Mnazi.

Aidha, Makonda alitoa zawadi kwa watumishi wanne waliokuwa  tayari kujitolea na kufanya kazi kwa ufanisi, ambao walizadiwa kulala  siku moja kwenye hoteli ya kifahari kwa gharama ya zaidi ya Sh milioni tano.

Kuhusu Mrisho ambaye alishindwa kuhudhuria hafla hiyo na kuwakilishwa, Makonda alisema utaratibu wa kumtafutia nyumba kama alivyoomba unaendelea.

Aliongeza kuwa kilichokwamisha ni eneo alilochagua ambalo walikuta lina mgogoro, hivyo alisema wanamtafutia sehemu nyingine kwa sasa.

Baada ya makabidhiano hayo baadhi ya wanufaika walimshukuru Makonda kuwa mwenye moyo wa uthubutu.

Kamanada wa FFU Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Stanley Kukaganeo alisema gari walilokabidhiwa litasaidia kuokoa maisha ya wananchi wengi wanaohitaji msaada wa dharura.

“Tumekuwa tukiumia sana mgonjwa kufia mikononi mwetu kwa sababu ya kukosa gari la kumwahisha hospitali ila Mkuu wa Mkoa tulikueleza hilo na sasa umetekeleza, ahsante sana,” alisema.

Zuhura alisema hakuwahi kufikiria kitu kama hicho katika maisha yake na anaona ni bahati kupata msaada huo.

“Niliomba Sh 20,000 ila wewe (Makonda) umenipa Sh 200,000, Mungu akubariki na uendelee na moyo huo huo wa kutusaidia,” alisema.
Kamanda wa kikosi cha kutuliza ghasia kanda maalum ya Dar es Salaam, Acp.Stanley Kulyamo akipokea gari la wagonjwa kutoka kwa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam ,Paul Makonda jana Jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam , Paul Makonda akikabidhi zawadi  tumba kwa ajili ya bendi ya jeshi la Wananchi mara baada ya kufanya vizuri katika mahadhimisho ya miaka 55 ya uhuru.
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam ,Paul Makonda , akikabidhi  shilingi laki mbili kwa mjasiliamali ,Zuhura Waziri mkazi wa Mwembe Yanga kwa ajili ya kuongeza mtaji wake wa Supu.
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam ,Paul Makonda akikabidhi mifuko ya Saruji kwa Mkuu wa shule ya St Joseph Goba , Sister Caroline Kokutekana, kama sehemu ya kutimiza ahadi yake wakati wa mahafali ya shule hiyo.
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam ,Paul Makonda akikabidhi mabati  kwa mkuu wa shule ya sekondari  Jitegemee kama sehemu ya ahadi yake katika kampeni ya Dar es Salaam mpya.

Lowassa Ahoji Uamuzi wa Rais Magufuli Kununua Ndege Badala ya Kutoa Huduma Kwa Jamii........Awataka Vijana Kuwa Imara 2020

$
0
0
Mjumbe  wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Edward Lowassa, ametaka vijana wa chama hicho kukabiliana na ukandamizaji wa demokrasia aliodai unafanywa na watawala.

Alisema hayo juzi alipokutana na vijana wa chama hicho ambao ni wanavyuo (CHASO) wa vyuo vikuu mkoani hapa.

Lowassa ambaye yuko Tabora  kwa ziara ya kuimarisha chama, aliwataka vijana hao kuwa na ujasiri wa kukabiliana na ukandamizaji wa demokrasia kwani vijana duniani ndio chachu ya mabadiliko.

“Nimekuja Tabora kuwashukuru kwa kura nyingi mlizonipigia na hamasa kubwa mliyoionesha kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka jana. Katika uchaguzi ule tulishinda, lakini ushindi mkubwa zaidi ni tulipofanikiwa kuvumilia na kuweka maslahi ya watoto, wazee na mama zetu mbele," alisema na kuongeza:

"Amani ni tunu muhimu sana kwa mustakabali wa Taifa kuliko kitu kingine chochote. Msikate tamaa, tumejipanga vema kwa uchaguzi ujao wa mwaka  2020 na hatutadhulumiwa tena haki yetu, kama ilivyokuwa mwaka jana,” alisema Lowassa.

Lowassa ambaye ni Waziri Mkuu wa zamani, alisema Jambo Kuu na la msingi ambalo wana Chadema wanatakiwa kuwa nalo sasa katika chama  ni umoja na mshikamano kati yao.

"Umuhimu wa umoja na mshikamano ndani ya chama chetu ni mkubwa sana, hasa katika kipindi hiki ambacho Serikali inajaribu kwa kila namna kukandamiza Upinzani na demokrasia na jambo hili si geni, ukirudi nyuma katika historia ya vyama vya siasa nchini, hata kabla ya Uhuru, unaweza kuona umoja ulivyoisadia TANU dhidi ya chokochoko za chama alichoanzisha mkoloni wakati ule - United Tanganyika Party (UTP) kukabiliana na kuidhoofisha TANU na kumzuia Mwafrika kupata Uhuru na kujitawala," alisema.

Aliwaambia vijana kwamba changamoto kama hizo ni za kawaida kwa vyama vingi vya upinzani hasa Afrika, ambavyo vinaungwa mkono na wananchi wengi wakiamini ni vya ukombozi.

Lakini pia alisema katika kujenga umoja na mshikamano huo ndani ya chama, ni lazima  nguvu kubwa ipelekwe kwenye matawi waliko wananchi.

"Katika chama chochote cha siasa watu wengi hawako ngazi za juu, bali mashinani. Ni lazima nguvu yetu kubwa ielekezwe huko kwa sasa, ili kuhakikisha chama kinakuwa na misingi madhubuti ambayo inaweza kutumika kukisaidia nyakati za uchaguzi," alisema.

Aidha, Lowassa ambaye katika uchaguzi mkuu wa mwaka jana alipata asilimia 38 ya kura, alihoji umuhimu wa Serikali kununua ndege zaidi, kuliko kupeleka huduma muhimu vijijini.

"Tumesikia nia njema yao ya kuagiza ndege nyingine zaidi miaka miwili ijayo, lakini tunajiuliza, je isingekuwa busara kutumia fedha hizo kupeleka maji safi na salama mijini na vijijini?" Alihoji.

Mwanzilishi wa Jamii Forums Jana Hakufikishwa Mahakamani.......Polisi Walivamia Ofisi zake na Kufanya Upekuzi

$
0
0
Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam  limevamia ofisi za mtandao wa Jamii Forums (JF) na kufanya upekuzi na  kuondoka  na  nyaraka za usajili wa Jamii Media ikiwemo cheti cha mlipa kodi, cheti cha BRELA, leseni ya biashara, n.k..

Askari hao walivamia ofisi hizo jana mchana wakiwa wamefuatana  na  na Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao  huo, Maxence Melo, wakafanya  upekuzi na kuwahoji baadhi ya wafanyakazi.

Baada ya kufanya upekuzi ndani ya ofisi hiyo walielekea nyumbani kwa mkurugenzi huyo,  kufanya upekuzi kabla ya kumrudisha  rumande kwa vile hakufikishwa mahakamani.

Melo alikamatwa  juzi  na   kupelekwa Kituo Kikuu cha Polisi  ambako aliwekwa selo.

Anakabiliwa na mashtaka ya kuzuia upelelezi wa makosa ya mtandao kwa kushindwa kutoa taarifa binafsi za watumiaji wa mtandao wa Jamii Forums ambazo polisi walizihitaji.

Taarifa iliyotolewa jana na mtandao huo iliwataka watumiaji wake kutokuwa na hofu yoyote na kwamba Jamii Forums haina server Tanzania wala Africa .

"Tunaomba umma utambue kwamba Jamii Media haina servers wala min-server ofisini kwake, nchini Tanzania wala Afrika. Pili, tunaomba watumiaji wa JamiiForums.com wasitiwe wasiwasi juu ya usalama wa taarifa zao. 

"Teknolojia tunayoitumia (encryption) kumsajili mtumiaji wa JamiiForums.com haituwezeshi kumfahamu mtumiaji yeyote labda yeye akubali kwa hiari yake kujiweka wazi mtandaoni." Ilieleza taarifa hiyo

Vodacom yawatengea wateja wake Bilioni 5/- kupitia promosheni ya NOGESHA UPENDO msimu huu wa Sikukuu.

$
0
0

Wateja wa Vodacom Tanzania wameletewa promosheni mpya inayojulikana kama “Nogesha Upendo” ambayo itawawezesha wateja wake kujishindia zawadi za fedha taslimu, muda wa bure wa maongezi na vifurushi vya intaneti kila siku  katika msimu huu wa sikukuu. 

Zawadi zenye thamani ya shilingi Bilioni 5 zitatolewa kwa wateja ambapo  wateja wapatao  500 wataweza kujishindia shilingi milioni 1( Tshs 1,000,000) kila mmoja katika kipindi chote cha msimu wa promosheni.

Akiongea wakati wa uzinduzi, Afisa Mtendaji Mkuu wa Mawasiliano na Uhusiano Vodacom Tanzania, Rosalynn Mworia alisema “Vodacom Tanzania tunayo furaha kuzindua promosheni ya msimu wa sikukuu ya Nogesha Upendo inayolenga kuleta shamrashamra za furaha ya sikukuu kwa wateja wetu. 
Tunajua sikukuu hizi zinaleta familia za kitanzania na marafiki pamoja kufurahi na kutumiana salamu za upendo, tumeleta promosheni hii kwa ajili ya kuwazadia wateja wetu wote kila wanaponunua vifurushi vya muda wa maongezi na Data kila siku.” 

Promosheni hii itawezesha wateja wetu 500 kujishindia kila mmoja shilingi milioni 1/- katika droo za wiki na wengine watajishindia shilingi 100,000/- katika droo za kila siku katika msimu huu wa sikukuu kupitia promosheni hii”.

Aliongeza kusema “Mbali na wateja kujishindia dakika tano za muda wa bure wa maongezi na kuperuzi internet,wateja wa Vodacom  pia kila watakaponunua vifurushi wataingizwa kwenye droo za kila siku na kila wiki za kujishindia vitita vya fedha.Kiasi cha shilingi milioni 700 zimetengwa kwa ajili ya kuwazawadia wateja wetu katika msimu huu wote wa sikuu”. 

Kwa ujumla, Vodacom imetenga zawadi zenye thamani ya zaidi ya shilingi Bilioni 5/- kwa ajili ya kuzawadia wateja wake kwa njia ya fedha taslimu, muda wa maongezi na bando za intaneti (MB) .Promosheni hii itakayodumu kipindi cha miezi 2 kuanzia leo ni kwa ajili ya wateja wote wa Vodacom ambao laini zao ziko hewani na watakanunua vifurushi vya kupata huduma mbalimbali za kampuni.

“Promosheni ya Nogesha Upendo imebuniwa kwa ajili ya kuwashukuru wateja wetu kwa kutuunga mkono muda wote,Tunawatakia heri katika msimu wa sikukuu na tunawakumbusha  wakati wote kufuatilia zawadi watakazokuwa wanazishindia kutoka mtandao wa Vodacom kuanzia muda wa maongezi na fedha taslimu zitakazowawezesha kufurahia sikukuu pamoja na familia zao na marafiki. Hivi ndivyo Vodacom tumejizatiti kufanya Maisha ya wateja wetu kuwa murua na kusambaza upendo.” Alisisitiza Mworia

Kanali wa JWTZ aeleza sababu za kuteuliwa na CCM kuwa Katibu wa NEC , Siasa na Uhusiano wa Kimataifa

$
0
0
Kanali Ngemela Lubinga (katikati), kulia ni Msaidizi wa Kanali Lubinga, Meja Joseph Masanja na kushoto ni Kapteni Swaleh Omar.
 ****
Wakati watu mbalimbali wakiwa na maoni tofauti kuhusu Chama cha Mapinduzi (CCM) kupitia Halmashauri Kuu yake kumteua Kanali wa Jeshi la Wananchi wa Tanzaia (JWTZ) kuwa Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, mwenyewe ameibuka na kutolea ufafanuzi uteuzi huo.

Kanali Ngemela Eslom Lubinga amesema kuwa alishastaafu utumishi wake jeshini na kuwa angeweza kutumikia chama cha siasa kwani si mtumishi wa jeshi hilo tena. Kanali Lubinga aliyekuwa Msemaji wa JWTZ alisema kuwa alistaafu utumishi katika jeshi kuanzia Disemba 2 mwaka huu. Aidha, alisisitiza kuwa alijiunga na Chama cha Mapinduzi mwaka 1979.

Kikubwa kilichozua maswali kuhusu uteuzi huu ni kwa sababu wanajeshi na watumishi wengine wa umma hawaruhusiwi kuwa wanachama wa vyama vya siasa. Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Waraka wa Utumishi wa mwaka 2015 unakataza watumishi wa umma kuwa wanachama wa vyama vya siasa lakini unatambua haki yao ya msingi ya kupiga kura.

Badhi ya maswali yaliyoulizwa na watumiaji wa mitandao ya kijamii ni lini Kanali Lubinga alijiunga na CCM kiasi cha kuweza kuteuliwa katika nafasi ya juu kiasi hicho? Kama alijiunga na chama mwaka 1979 inaonyesha wazi kuwa alikiuka katiba ya nchi inayowataka wanajeshi kutojiunga na vyama vya siasa.

Akijibu swali hilo Kanali Lubinga alisema kuwa wakati wa mfumo wa chama kimoja wanajeshi waliruhusiwa kujiunga na chama cha siasa na kuwa baada ya kuanza mfumo wa vyama vingi mwaka 1992 ndipo walizuiwa na kadi walizokuwa nazo zilichukuliwa. 

Kanali Lubinga aliendelea kusema kuwa kadi zile hazikutupwa bali zilihifadhiwa na hivyo baada ya kustaafu Disemba 2 mwaka huu akachukua kadi yake na kuendelea na uanachama wake.

Wengi waliokosoa uteuzi huo walitaka kuhakikisha kuwa siasa za nchi haziathiri utendaji  wa majeshi yetu na utumishi wa watumishi wengine wa umma.

Baba Achinja Wanawe Wawili na Kisha Kujinyonga

$
0
0
Watoto  wawili wenye umri wa miaka mitatu na sita wa Kijiji cha Patane Kata ya Mambamiamba wilayani Same,  wameuawa kwa kuchinjwa na panga na baba yao mzazi Yohana Greson (26) na yeye mwenyewe kujining’iniza kwenye paa la nyumba.

Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari jana Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Wilbroad Mutafungwa, alisema tukio hilo lilitokea Desemba 13, mwaka huu  majira ya saa tano asubuhi katika Kijiji cha Patane.

Kamanda alisema baba huyo alifanya tukio hilo la kutisha baada ya mkewe Eva Tumaini (29) mkazi Kijiji cha Ghona kwenda shambani na kumwacha mumewe nyumbani akiwa na watoto wawili, Esta Yohana na Tumaini Yohana, ambapo alichukua panga na kuwachinja na yeye kujinyonga kwa kamba.

Alisema Polisi inaendelea na uchunguzi wa tukio hilo na kwamba uchunguzi wa awali umebaini marehemu huyo alikuwa na tatizo la kifafa.

Alisema miili ya marehemu wote imehifadhiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Same kwa ajili ya uchunguzi zaidi na kwamba marehemu hakuacha ujumbe wowote na uchunguzi ukikamilika ndugu za marehemu watakabidhiwa miili hiyo kwa ajili mazishi.

RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 103 & 104 (Riwaya inawafaa kuanzia miaka 18 na kuendelea )

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA

ILIPOISHIA
Nikamvuta na kumuingiza chooni, mikamuonyesha bomu lilipo, Sote tukajikuta tunashangaa kutokana bomu hilo limebakisha sekunde hamsini na tisa, kabla halijalipuka na sote hapa hatujui jinsi ya kulitegua, na muhudumu akaanza kulia, akijaribu kunikumbatia kwani mwisho wetu umefika.

ENDELEA
"Una chochote cha kukatia"
Nilizungumza huku nikimtoa muhudumu huyu, mwilini mwangu, kwani kukumbatiana kwetu sio suhulisho la bomu hili kuacha kuacha kulipuka. Hakunijibu zaidi ya kubabaika, kwa mawenge yaliyo mchanganya kupita maelezo. Akaanza kujipapasa huku mwili mzima ukimtetemeka kwa woga, akatoa, kikatia kucha(Nail cutter), akaitupa chini huku akiendelea kuikagua mifuko ya nguo zake alizo zivaa. Kwa haraka nikaokota kikatia kucha, nikapiga magoti chini, huku nikiwa ninajiamini kwa lile ninalo kwenda kulifanya.

   Sekunde za bomu hili, zikazidi kurudi nyuma, huku zikiwa zimebakia sekunde thelathini na mbili kabla halijalipuka. Nikaanza kuzichambua nyaya nyingi ndogondogo zipatazo ushirini, zikiwa na rangi tofauti tofauti.

"Ishirini na tano"
Muhudumu aliniambia, huku macho yake akiwa ameyatumbulia kwenye bomu, linalo zionyesha sekunde hizo, zinavyo rudi nyuma.
"Mungu wangu"
Nilizungumza huku nikizidi kuchanganyikiwa, kwani sikujua ni waya upi unanipasa kuukata, ili kulizuia bomu hili kuto kulipuka.
"Kumi na tano"
Nikashika nyaya moja nyekundu na kuikata, chakushangaza, bomu likaendelea kurudisha sekunde zake nyuma.
"Nane"
Nikazidi kuchanganyikiwa, na kukata wanya mweusi, hali ikawa ni ile ile.
"Tano"
Mikono yote, ikazidi kutetemeka hadi nikaangusha kikatia kucha, nikakiokota kwa haraka, hata kukaa mkononi vizuri, nkawa ninashindwa kukishika.
"Tatu"

Nikamuona muhudumu, akipiga ishara ya msalaba akiashiria mwisho wetu ndio unakaribia, nikashika waya wa rangi ya kijani, sekunde ikawa imebaki moja, nami nikawa nimeukata. Sekunde hiyo ikasimama hapo hapo na bomu kuzima. Nikashusha pumzi nyingi, huku mwili wangu wote ukiwa umesha vuja jasho lakutosha hadi shati nililo livaa, likawa limelowana kabisa. Kumtazama muhudumu nikamkuta akiwa ameyafumba macho yake huku jasho likimwagika shingoni nwake.

"Tumefanikiwa"
Nilizungumza kwa sauti ya unyonge huku nikimtazama usoni muhudumu, akayafumbua macho yake taratibu, huku akihema. Akalitazama bomu nililo lichomoa na kulishika, akabaki akiwa ameduwaa. Akanishika mkono taratibu na kuninyanyua, akanikumbatia huku akilia kwa furaha.
"Asante Mungu, kweli wewe ni mwema. Hakuna kama wewe"
Alizungumza huku akiendelea kulia, nakunifanya na mimi machozi kunimwagika kwani sikutarajia kama nitaweza kufanikiwa kulitegua bomu hili, taratibu akaniachia, huku akijifuta machozi usoni

"Unaitwa nani?"
"Eddy, Eddy Godwin"
"Am Tasiana, from Arusha Tanzania"(Mimi ni Tasiana natokea Arusha Tanzania)
"Mimi pia natokea Tanzania, ila A leve nilisoma Arusha"
"Waooo, nashukuru kukufahamu"
Tasiana akanikumbatia kwa mara ya pili, akawasiliana na marubani wa ndege hii, kupitia kijisimu kidogo wanacho kitumia kuwasiliana, wakamuomba tuelekee kwenye chumba walipo, tukiwa na bomu hilo, ila tuhakikishe hakuna abiria atakaye liona, ili kuto hatarisha amani ya walio wengi.
Tasiana akachukua mfuko mtupu, mweusi. Akaliweka bomu, nikaongozana naye hadi chumba cha marubani. Tukawaelezea hali halisi juu ya tukio zima na jinsi mchungaji Frank, alivyo nipa vitisho nikiwa ninapishana naye kwenye mlango wa chooni.

"Hakuna aliye toka ndani ya ndege, ngoja tukifika Afrika kusini, tutafanya upelelezi kabla watu hawaja ruhusiwa kushuka kwenye ndege"
Rubani mmoja alizungumza huku akilitazama tazama bomu hilo nililo mpatia.
"Ukimuona si utamkumbuka?"
"Ndio, nilikuwa nimekaa naye ila simuoni kwenye siti yetu"
"Ulikaa siti gani?"
Nikamtajia rubani, huyo herufi ya siti niliyo kuwa nimekaa, akatazama mkanda mzima, kwenye kiji tv chao kidogo unao rekodiwa na kamera zilizo tegwa kila kona ya ndege. Tukamuona mzee huyo akiingia kwenye moja ya chumba walicho dai ni stoo, chenye gazi za kushukia chini, kunapo hifadhiwa mizigo mikubwa mikubwa.

"Ngoja nimfwate"
Nilizungunza kwa kujiamini, huku nikiwatazama marubani hawa wapatao wanne, huku wawili wakiwa niwasaidizi.
"Itaweza kumkamata?"
"Nitahakiksha nalifanikisha hilo"
Wakanitazama machoni, mkuu wao akanipa ruhusa.
"Tuongozane"
Tasiana aliomba tuongozane pamoja.
"Wewe baki, ngoja nikajaribu kulifanya na hili kama nitafanikiwa"
"Tafadhali twende pamoja"
Tasiana aling'ang'ania kwenda, ikanibidi nimkubalie tu. Tukaongozana hadi kwenye chumba hicho, pasipo wasafiri wezangu kuelewa kitu gani kinacho endelea, hakikuwa chumba kikubwa sana, kwani kina ngazi zakushuka chini kulipo na mizigo mikubwa. Tukafanikiwa kushuka chini, kwa wingi wa mizigo iliyo fungwa kwenye mifurushi mikubwa, ilitufanya tubaki tukiwa tumesimana na kuduwaa.

"Atakuwa wapi?"
Tasiana aliniuliza kwa sauti ya chini, huku tukiendea kupepesa pepesa macho yetu kila kona ya eneo hili lilolo kubwa.
"Nifwate nyuma na kuwa mkimya"
Tukaanza kupita kwenye vinjia, vilivyo tenganishwa kwa maburungutu makubwa ya mizigo. Nikaanza kupata wasiwasi, baada ya kukuta shati alilo kua amelivaa mzee yule, likiwa chini. Tasiana akataka kuliokota ila nikamzuia asifanye hivyo.
"Kwa nini nisiliokote?"
Nikatingisha kichwa nikimuashiria Tasiana asifanye chochote dhidi ya shati hilo.Tukalipita, hatua kumi mbele, tukakuta suruali aliyo kuwa ameivaa.
Kwa kutumia mguu nikaisogeza kuitazama kama kuna kitu kimefunikwa, ila hatukuona kitu.

Arufu ya moshi wa sigara, ukaanza kuingia kwenye pua zetu, ulitokea upande wa pili wa sehemu ilipo mizigo hiyo. Tukapiga hatua za tahadhari hadi sehemu inapo tokea harufu ya moshi huo wa sigara, tukakuta kipande cha sigara kikiwa chini, kikiendelea kuteketea taratibu.

Humphrey Polepole aeleza mikakati yake baada ya kukabidhiwa ofisi na Nape Nnauye

$
0
0
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Humphrey Polepole amesema atahakikisha chama hicho kinakuwa ni cha wanyonge na kuendelea kuwa kimbilio la wasio na sauti.

Polepole ametoa kauli hiyo leo wakati akikabidhiwa rasmi ofisi na  Katibu anayemaliza muda wake Nape Nnauye katika ofisi ndogo za Makao Makuu ya chama hicho Lumumba jijini Dar es Salaam.

Polepole alisema kwa misingi ya chama hicho imejengwa kuwasaidia na kuwa tete wanyongo hivyo katika muda wake wa uongozi atahakikisha chama kinasimama katima misingi hiyo ya kuanzishwa kwake.

“Msingi wa chama chetu ni utetezi wa wanyonge, tutahakikisha kinaendelea kuwa kimbilio la wasio na sauti,” alisema Polepole.

Aidha, katibu huyo alisema kuwa katika kutekeleza majukumu yake aliyokabidhiwa leo na mtangulizi wake, atahakikisha anajikita zaidi katika kazi za itikadi zaidi kuliko uenezi kwa kuwa itikadi ndiyo inayokibeba chama.

Polepole alitumia muda huo kumshukuru Nape Nnauye anayemaliza muda wake na kusema kuwa ni kiongozi imara na kuwa katika muda wake aliweza kuitumikia vyema nafasi yake. Lakini pia alisema japo anamaliza muda wake, lakini atakuwa akimuhitaji mara kwa mara kwa ajili ya ushauri na mambo mengine.

Wakati huo huo, Polepole amemshukuru Mwenyekiti wa CCM Dkt John Pombe Magufuli na Halmashauri Kuu ku kumwamini na kumpa majukumu hayo makuwa.

Nape awaaomba msamaha wapinzani.

$
0
0
Alikuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye amewaomba radhi viongozi na wafuasi wa vyama vya upinzani nchini kwa lolote ambalo aliwakwaza wakati akitekeleza majukumu yake katika nafasi hiyo.

Nape amewaangukia wapinzani pamoja na makundi mengine ya watanzania ikiwemo viongozi wenzake ndani ya chama leo wakati akikabidhi rasmi ofisi kwa kiongozi mpya anayechukua nafasi hiyo, ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Dar es Salaam, Humphrey Polepole katika ofisi ndogo za makao makuu ya chama hicho, Lumumba Jijini Dar es Salaam.

"Nawaomba msamaha viongozi wenzangu, wanachama, waandishi na hata wapinzani pale ambapo nimewaumiza katika kufanya kazi yangu, samahani sana. Nategemea ushirikiano niliopatiwa mimi na wanahabari utaendelea kwa ndugu yangu Humphrey Polepole, ni mtu mwenye weledi mpana" amesema Nape

Nape pia amekiri kuwa chama hicho kimemsaidia zaidi kwenye maisha yake kuliko yeye alivyokisaidia wakati akiitumikia nafasi hiyo.

"Nakiri mbele yenu kuwa chama kimenisaidia zaidi kuliko mimi nilivyokisaidia Chama, nashukuru Mungu kuwa nimemaliza kazi hii salama, nilipata wosia wa Mzee Kinana kuwa nishukuru nikimaliza salama"

Wasichana 13 walioingia nchini kinyemela wanaswa Wakifanya UKAHABA

$
0
0
Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Dar es Salaam imewakamata wasichana 13 kutoka nchi za Nebal na India wenye umri kati ya miaka 18 na 26 ambao wameletwa nchini kinyume cha sheria na kuendesha biashara ya ukahaba katika jijini humo.

Akiongea na waandishi wa habari leo mara baada ya kufanya oparesheni ya kufunga madanguro yote na kuwasaka raia wa kigeni wanaoishi nchini kinyume cha Sheria, Kamishna wa Uhamiaji Kanda ya Dar es Salaam John Msumule amesema mbali na raia hao wa kigeni pia wamewamakata raia wa Kitanzania mbao wanashirikiana na wahamiaji hao.

Amemtaja Bwana Mohamed Shabani Magamba ambaye anatengeneza vibali vya kugushi ambapo pia amekutwa na pastpoti  4 za raia wa nchi za Nigeria, Botswana, Somalia na Uingereza.

Bwana Msumule ameitaja Wilaya ya Kinondoni kuwa inaongoza kwa kuwa na Madanguro ikifuatiwa na Temeke ambapo kwa sasa wanajipanga kuyaondoa kwa muda wa siku 10 madanguro hayo pamoja na kuendesha oparesheni kubwa katika Mitaa ya Msimbazi, Lumumba na Uhuru katika soko la Kariakoo na maeneo ya Mtoni Mtongani na Sabasaba ambako wamekwisha yafanyia uchunguzi wa kina.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images

<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>
<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596344.js" async> </script>