MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA
"John rafiki yangu, Sheila mke wangu, niwakate kate, kate vipande vigogo vidogo kama nyana. Au mufe kwa bomu hili, litakalo wachangua vipande vidogo vidogo"
Sheila badala ya kujibu, akaangua kilio likubwa kilichonifanya nimtandike ngumi nzito ya shavu, hadi taya ikapinda, huku meno baadhi yakianguka chini.
ENDELEA
"Ahaaaaa fu**"
John alijikuta akitukana kwa kitendo nilicho mfanyia mke wake. Sheila akaendelea kuangua kilio cha majuto sana.
"Nipe kisu"
Pretty akanipatia kisu chenye makali, John akabaki akiwa amenitumbulia mimacho, huku hakiema kwa woga. Nikamkita John kisu cha kwenye paja, la mguu wake wa kulia.
"Mamaaaa.."
John alilia kwa uchungu, ulio changanyika na maumivu makali.
"Ahaa kuna kitu nahitaji ukifanye kabla haujakufa"
Nilizungumza huku, nikikizungusha kusu kilicho zama kwenye paja lake, John akazidi kutoa mlio wa machozi.
"Kuna mali zangu, ulizo zichukua wewe na ulivyo mjinga ukaamua kumdhulumu Madam Merry. Sasa nazihitaji zote zirudi kwangu"
"Na....ru..disha"
"Sawa kama utazirudisha"
"E...ddy tusa...mehe"
Sheila alizungumza kwa sauti iliyo legea, kutokana na ukosefu wa meno yake mdomoni na kuvunjika kwa taya yake.
"Tena wewe usizungunze. Ni mwanamke gani usiye na huruma katika maisha yangu. Ulipanga kuniua mimi ili muchukue mali za mama yangu. Kwa bahati mbaya ukamuua Fredy. Mtu niliye fanana naye. Leo hii unasema kwamba niwasamehe"
Nilizungumza kwa hasira huku nikimtazama Sheila jinsi anavyo vuja damu.
"Nimezaliwa na roho ya kiatili, na sijawahi kumsamehe mtu abaye kwenda kinyume na mimi."
Nikachukua mkasi mkubwa kiasi. Nikashika kidole kimoja cha John na kukichomeka katikati ya mkasi.
"Ngoja ngoja usinikate nikuambie ukweli"
John alizungumza huku akiendelea kulia hadi makamasi yakaanza kumwagika puani mwake.
"Mali zote nilizo zichukua, kuma mtu ndio mmiliki kabisa na mimi ndio nilikua ninamsimamia"
"Nani?"
"Mzee Godwin na.....na yupo Oman, ndipo yalipo makazi yake"
Ikawa ni taarifa nyingine mpya kwani mzee Godwini ninavyo fahamu mimi amefungwa. Ila gereza alilo fungu ndio sikulifahamu.
"Mmmm kwahiyo, hajafumgwa yeye?"
"Haa....hajafumgwa na mtu aliye kua akishirikiana naye ni madam Mery"
Nikakaa kimya huku nikimtazama John usoni mwake. Sikuhitaji kumuonea huruma John hata kidogo. Nikakikata kidole chake kwa kutumia mkasi na lukitenganisha na vidole vinne vilivyo bakia kwenye mkono wake.
"Nahitaji namba za akaunti zako zote za benki"
"Ehee tena ngoja nichukue laptop"
Pretty alizungumza huku akitoka kwenye chumba tulichopo. Ptetty akarudi akiwa na laptop yake.
"Tunaweza kuzihamisha hizo popote pale kwenye akaunti ya benki"
Pretty alizungumza huku akiminya minya batani za laptop yake.
"Kwanza una akaunti ngapi?"
"Eheeee?"
"Hujanisikia eheee"
Nikachukua koleo, nikalichomeka kwenye sikio la John, la upande wa kushoto na kuanza kulibana taratibu.
"Nakuambia hiviiii, una akaunti ngapi za benki"
Nilizungumza kwa sauti ya kumnong'oneza John
"Tano tano"
John alijibu kwa sauti ya juu.
"Kumbe unanisikia vuzuri. Ila una ihakika ni tano?"
Nilizungumza huku nikiminya zaidi sikio lake
"Zipo saba, nyimgine ni....ni ni...."
"Ni..ni ni sizihitaji kuzisikia, una akaunti ngapi?"
"Kumi"
Nikajikuta nikicheka kwa maana kili ninavyo zidi kulibana sikio lake ndivyo kila alivyo zidisha kutaja idadi ya akaunti zake za benki.
"Tutajie namba ya akaunti na beki"
John akataja namba ya kwanza, huku akimwagikwa na machozi.
"Ni ya benki gani?"
Pretty alimuuliza, huku akiendea kuminya batani za laptop yake.
"Co-operative"
"Ya London?"
"Ndio"
"Yes Eddy, imesoma, tunaomba namba ya siri"
John akataja, Pretty akaiingiza na kusubiria kwa muda kidogo.
"Ohoo My God, Eddy njoo uone"
Nikaliachi sikio la John na kwenda alipo Pretty. Akanionyesha kiasi cha pesa kilichopo kwenye akaunti hiyo. Ambacho dola za limarekani bilioni kumi.
"Eheeee, John mwanangu, kumbe wewe nintajiri hivi. Ukiambiwa utakufa na kuziacha hizi"
Nilizumgumza huku nikimcheka John, ambaye uhai wake upo mikononi mwangu. Nikamtajia Ptetty namba za akaunti yangu ambayo nahitaji wazihamishe pesa hiyo.
"Ohoo wanataja alama ya dole gumba la John ili waweze kudhibitisha kuzihamisha kwenda kwenye akaunti yako"
"Wanataka la upande gani, hilo dolr gumba?"
"Kulia"
Nikachukua mkasi wangu na kumfwata John alipo.
"Nina kazi na kidole chako"
"Eddy kikatie chini chini kidogo ili kifiti hapa"
Pretty aliniambia, John akanitumbulia mimacho akihisi kwamba sinto fanya hilo swala. Nikalikamata dole gumba la kulia na kulikata kwa nguvu. Sheila akatoa ukelele, kama yeye ndio aliye katwa.
"Kinacho kuliza na wewe? Nahisi hili tukio si geni kwako, kwani Derick yule malaya wako naye alikufa kama huyu"
Nikakichukua kidole cha John na kwenda sehemu alipo kaa, Pretty.
"Kisuuze kwanza bwana, si unaona kimejaa damu"
Nikakisuuza vizuri kidole cha John kwa kutumia maji, nikampa Pretty akakiweka kwenye kifaa kingine, alicho chomeka waya wake kwenye laptop. Mwanga mwekundu ukapita kwenye kidole cha John,
"Hapo kinafanyaje?"
"Nina kiscan. Yes kimesoma"
Pretty akanionyesha, kidole kimefanana na alama ya dole gumba iliyopo kwenye benki hiyo.
"Sasa pesa hapa tunaweza kuihamisha"
Pretty akaanza kufanya, kazi ya kuhamisha pesa hiyo kwenye akaunti yangu.
"Asilimia zinakwenda taratibu?"
"Kwa nini?"
"Pesa nyingii hii"
Kama robo saa, pesa, yote ikawa imekamilika luhamishiwa kwenye akaunti yangu. John akaendelea kututajia akaunti zote anazo zimiliki na zote zina pesa nyinhi tu. Pesa nyingine nilimpa ruhusa, Pretty akazihamishia kwenye akauti yake.
Hadi inafika majira ya saa kumi jioni, tukawa tumelikamilisha zoezi zima la kumfilisi John kwenye maakaunti yake ya benki.
"Vifo vyenu nahitaji viwe vya taratibu mno"
Nilizungumza huku nikinywa juisi, aliyo nipa Pretty, hii ni baada ya kukaa kwa muda mrefu pasipo kula chocho.
"Eddy nisamehe kaka, kwani haya yote niliyafanya kwa tamaa"
"Ahaaa tamaaa?"
"Pretty ile video ya mauaji ya Victoria iweke mtandaoni, kila mtu ajionee ukatili wa huyu mjinga"
"Sawa bosi"
Pretty akamuonyesha John, ile vodeo jinsi alivyo muua Voctoria, John akabaki akitokwa na machozi mengi. Sheila naye akabaki akikodoa mimacho, hata kuzungumza alishindwa kutokana na taya kuvunjika.
"Una jengine la kuzungumza?"
John akatingisja kichwa kwamba hana la kuzungumza. Nikachomoa bastola, kiunoni mwangu. Nikaifunga kiwambo cha kuzuia sauti.
"Yupi awe wa kwanza kufa?"
Hakuna aliye nijibu zaidi ya woye kukaa kimya. Nikampiga John risasi za miguu, kwenye magoti, kisha nikachukua kishoka kidogo cha kukatia nyama. Nikakata viganja vyake vya mikono yote miwili.
Yote niliyo yafanya Pretty na Sheila waliyashuhudia kwa macho yao mawili. John alilia kwa uchungu mkubwa huku akiniomba nisimuue ila sikumpatia msamaha wa aina yoyote. Nikamgeukia Sheila na kumtazama kwa macho yaloyo jaa chuki na hasira kali.
"Ed.."
Sheila aliniita, kabla hajamaliza kuliita jina langu, nikampiga risasi tano za kifuani mwake, nikachukua bomu, lakutega. Nikaliweka mbele ya John huku nikiwa nimelitega dakika tano lilipuke.
"Kifo hichi ndicho unacho stahili John"
Nikamaliza kumpiga John risasi za miguu yake yote, hadi nilipo hakilisja hatoweza kusimama wala kulishika bomu hilo, kwani hana tena viganja vya mikono.
Tukatoka na Pretty hadi nje, Pretty akachukua gari lake jengine na tukaliacha gari tulilo kuja nalo, kuepuka kukamatwa na polisi. Tukaondoka eneo la nyumbani, hatukufika mbali sana nyumba nzima ikalipuka huku John na mwili wa Sheila vikiwa ndani.
"Eddy inabidi ukatubu kwa Mungu wako"
Pretty alizungumza huku akiendelea kuendesha gari kwa kasi. Tukaingia kwenye barabara ile tuliyo pita jana, iliyo nyooka. Tukaingia mjini majira ya saa mbili usiku, ambapo tukaelekea moja kwa moja hotelini.
Nikafika chumbani kwangu na kuchukua kila kilicho changu, nikarudisha funguo kwa wahusika
Nikatoka nje na kumkuta Ptetty akinisubiri ili anisindikize uwanja wa ndege. Nikaingia ndani ya gari na tukaondoka eneo la hotelini.