Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Majaliwa awavaa waajiri wanaonyanyasa wafanyakazi, atoa kauli kuhusu viongozi wanaowaweka rumande watumishi.

$
0
0
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Serikali haitawavumilia waajiri ambao hawatoi mikataba ya ajira kwa wafanyakazi wao na amewaonya waache tabia hiyo mara moja.

Ametoa agizo hilo jana (Jumatano, Novemba 23, 2016) wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Sita wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) katika ukumbi wa Mwalimu Julius K. Nyerere ulioko Chuo cha Mipango, nje kidogo ya mji wa Dodoma.

Akijibu hoja ya waajiri kutokutoa mikataba ya ajira kwa wafanyakazi ambayo iliibuliwa kwenye risala yao, Waziri Mkuu alisema kifungu cha 14 cha Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini Na. 6 ya mwaka 2004  kinaelekeza aina mbalimbali za mikataba inayotakiwa kutumika kuajiri wafanyakazi. 

“Kisheria mwajiri anao wajibu wa kuhakikisha kila mtumishi wake ana mkataba wa kazi kwa maandishi,” alisisitiza.

Akijibu hoja kuhusu wafanyakazi kuwekwa ndani kiholela, kunyanyaswa, kushushwa vyeo na kusimamishwa kazi na wanasiasa, Waziri Mkuu alisema Serikali chini ya uongozi wa Dkt. John Pombe Magufuli itaendelea kuzingatia utawala wa sheria na kanuni za utawala bora ili kuhakikisha kuwa haki za wafanyakazi zinalindwa ipasavyo.

”Kimsingi watumishi wanasimamiwa na mamlaka za kinidhamu na sheria mbalimbali ambazo hazina budi kuangaliwa kwa pamoja kabla ya kuchukua hatua. Ninawaagiza viongozi wenzagu wa kisiasa na walioko katika wizara na taasisi zote za Serikali, mikoani, wilayani, kwenye idara za Serikali na Halmashauri wazingatie utawala wa sheria wakati wa kushughulikia masuala mbalimbali yanayohusu wajibu na haki za wafanyakazi,” alisema huku akishangiliwa.

Akijibu hoja kuhusu suala la watumishi kutopandishwa vyeo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala Bora), Bibi Angella Kairuki alisema kwa kipindi cha miaka mitano jumla ya watumishi 343,689 walipandishwa vyeo ikiwa ni kuanzia mwaka 2011 hadi 2016. Hata hivyo, alisema wanakabiliwa na changamoto ya watumishi wengine kutokidhi vigezo.

“Kuna baadhi ya watumishi hawakidhi vigezo vya maendeleo na masharti vya muundo wa masharti ya utumishi wa umma. Tumetoa maelekezo kuwa wale waliokosa vigezo na wamekaa muda mrefu bila kupandishwa vyeo, wapewe mafunzo na bajeti zitengwe ili waweze kutimiza vigezo vya muundo wa utumishi wa umma,” alisema.

Sauti ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akizungumza



Mwanafunzi Apigwa Risasi na Polisi Dar.......Askari Wawili Watiwa Mbaroni

$
0
0
Mwanafunzi wa kidato cha kwanza wa Shule ya Sekondari Gerezani, Shakil Sures amelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) baada ya kujeruhiwa kwa risasi na polisi kwenye mazingira ya kutatanisha. 

Tukio hilo lililotokea Jumatatu eneo la Fire, Upanga licha ya watu kusikia milio ya risasi, kushuhudia polisi wakipita na kumuona kijana huyo akiwa tayari kajeruhiwa, lakini hakuna mwenye maelezo sahihi kuhusu nini kilitokea hadi askari hao wakachukua hatua hiyo. 

Baadhi ya waliokuwapo eneo la tukio siku hiyo walidai kuwaona askari waliokuwa eneo hilo wakirusha risasi, bila kujua walikuwa wakipambana na nani. 

Mmoja wa mashuhuda, Athumani Simba alidai walidhani ni majibizano ya risasi kati ya askari na majambazi, baada ya kuona gari la polisi likipita eneo hilo. 

“Niliwaona askari wawili wakielekea eneo la Fire huku wakipiga risasi, ghafla nilimuona mwanafunzi akilia huku akiwa ameshika mguu wake akiomba msaada,” alisema Simba. 

Ofisa Uhusiano wa MNH, Aminiel Aligaesha alisema mwanafunzi huyo alifikishwa hospitalini hapo jioni ya Jumatatu na kwamba jeraha lake linaendelea vizuri. 

“Tumempokea mwanafunzi Shakil juzi jioni na kidonda chake kimesafishwa na kinaendelea vizuri,” alisema Aligaesha. 

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Hamduni Salum alisema upelelezi kuhusu tukio hilo unaendelea. Hata hivyo, hakueleza mazingira ya tukio lenyewe yalivyokuwa. 

“Tunawashikilia askari polisi wawili waliokuwa zamu siku hiyo ya tukio, upelelezi unaendelea ili kuangalia kwa nini walitumia nguvu kubwa kiasi hicho,” alisema Kamanda Salum.

RC Makonda Aamuru Mwenyekiti wa Mtuu Akamtwe na Kuwekwa Rumande Hadi Upelelezi Utapokamilika

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda jana  aliliagiza jeshi la polisi kumkamata mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Gongolamboto, Bakari Shingo baada ya kutuhumiwa kukusanya mapato kwa kutumia risiti anazozichapisha mwenyewe kinyume na Halmashauri inavyoagiza pamoja na kutoitisha mikutano ya hadhara kwa muda mrefu na kushirikina na wahalifu.
 
Hatua hiyo ilikuja baada ya wananchi kulalamika kwa kumtuhumu mwenyekiti huyo kukaa muda mrefu bila kusoma mapato ya mtaa huo pamoja na kughushi stakabadhii za mapato.

Lawama hizo zilimpelekea Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda ambaye alikuwa  kwenye ziara yake katika wilaya ya Ilala Pugu Kajiungeni, kumuagiza Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Ilala, Salum Hamduni kumsweka rumande Mweyekiti huyo mpaka upelelezi utakapo kamilika.

Akitoa ushahidi kuhusu sakata hilo Mkazi wa Gongo la Mboto na Mjumbe wa Serikali ya Mtaa Pili Seif alieleza kuwa hiyo imekuwa ni tabia ya mwenyekiti huyo kwa muda mrefu na taarifa zimefikishwa kwenye mamlaka husika ikiwemo kwa Mkuu wa Wilaya Sophia Mjema, Mkurugenzi Msongela Nitu na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

Waziri Nape Nnauye Alitembelea Kundi la Wasafi Classic Linaloongozwa na Diamond Platinumz

$
0
0
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mheshimiwa Nape Nnauye ametembelea ofisi za Kundi la musiki wa kizazi kipya la Wasafi.

Pamoja na mambo mengine uongozi wa kundi hilo umemuomba waziri huyo kushughulikia changamoto mbalimbali zinazowakabili ikiwa ni pamoja na kupunjwa mapato yatokanayo na miito ya simu (Caller tunes), wizi wa kazi za wasanii, kupata eneo (Ukumbi wa Kisasa) kwa ajili ya kufanyia maonesho makubwa ya musiki, wasanii kupata elimu juu ya kulipa kodi kwa kazi zao na kuongeza kiwango cha uwiyano kwa nyimbo za kitanzania zinazopigwa redioni dhidi ya nyimbo za kigeni.

Kwa upande wake Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye  amehaidi kuzifanyia kazi changamoto hizo na kuifanya tasnia ya muziki kuwa ajira kubwa kwa vijana wengi kwa kuongeza vipato vyao na pato la taifa kwa ujumla.

“Nimewaahidi kuzifanyia kazi changamoto hizi mapema iwezekanavyo ili kuongeza kipato kwa wasanii hapa nchini,” amesema Mheshimiwa Nnauye.

Wasafi Classic ni kundi la Muziki wa kizazi kipya(Bongo Flavour) Tanzania linalomilikiwa na Msanii Naseeb Abdul (Diamond Platinumz) na mpaka sasa lina wasanii wapatao 16 na linaongozwa na mameneja Babu Tale, Said Fella na Sallam SK.

Wataalam wa afya kuanza kusajiliwa na kupewa leseni

$
0
0
Wataalamu mbalimbali wa sekta ya afya, sasa wataanza kusajiliwa na kupewa leseni zitakazowatambulisha na zitakuwa na masharti maalumu.

Hayo yamesema na Mganga Mkuu wa Serikali, Profesa Muhammad Kambi  jana Jumatano  jijini Dar es salaam, wakati akifungua mkutano wa mwaka wa Chama cha Wafiziotherapia (APTA).

Alisema serikali imeanza mchakato wa kuipitia upya Sheria ya Madaktari wa Tanganyika, ambayo itaongezwa sharti hilo pamoja na kuundwa kwa bodi maalumu itakayosimamia maadili ya watumishi hao.

“Lakini hivi sasa kuna taaluma nyingi ndani ya hii fani, kwa mfano ninyi wataalamu wa fiziotherapia. Mpo lakini sheria haiwatambui, kwa maana hiyo inakuwa vigumu hata kuwafuatilia. Ndiyo msingi wa kuipitia upya sheria hii,” alisema.

“Katika sheria mpya itakayoboreshwa, kila mtumishi atatakiwa kukata leseni. Kila mtumishi atatakiwa kujiendeleza kielimu, kuongeza ujuzi ili aendane na wakati uliopo kwa sababu mambo yanabadilika, kile ulichosoma jana unahitaji kujifunza zaidi,” alisema.

Aidha Kambi alisema tayari maboresho ya sheria hiyo yameshawasilishwa katika Kamati ya Baraza la Mawaziri ya Katiba na Sheria na imeshapitiwa.

Rais Magufuli Ataja Sababu za Kuitumbua Bodi ya Wakurugenzi TRA

$
0
0
RAIS John Magufuli amefichua siri ya hatua yake ya kuitumbua Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Amesema alilazimika kuchukua hatua hiyo baada ya bodi hiyo kuidhinisha Sh bilioni 26 kupelekwa kuwekwa kwenye akaunti maalumu( Fixed Account)  katika benki kadhaa za biashara.

Bodi hiyo ilitoa idhini ya kupelekwa fedha hizo katika benki hizo wakati kuna agizo la Rais la kupiga marufuku kwa taasisi za umma, mashirika ya umma, idara za serikali, wakala na wizara kuweka fedha zao katika benki za kibiashara.

Fedha hizo zinatakiwa zifunguliwe akaunti katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Jumapili iliyopita asubuhi, Ikulu ilitangaza kwamba Dk Magufuli ameivunja Bodi ya Wakurugenzi ya TRA, na saa chache akateua Naibu Kamishna Mkuu mpya. 

Ikulu bila kueleza sababu, ilisema kwamba Rais Magufuli ametengua uteuzi wa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TRA, Bernard Mchomvu na kuivunja bodi nzima.

Aidha, pamoja na kuivunja bodi hiyo alimteua Charles Kichere kuwa Naibu Kamishna Mkuu wa TRA, kuziba nafasi iliyokuwa wazi kwa mwaka mmoja baada ya Dk Magufuli kutengua uteuzi wa aliyekuwa akishikilia wadhifa huo Lusekelo Mwaseba.

“Uteuzi wa Mwenyekiti mwingine wa Bodi ya Wakurugenzi wa TRA na Bodi ya Mamlaka hiyo utatangazwa baadaye,” ilieleza taarifa ya Ikulu iliyotolewa Jumapili asubuhi sana.

Akihutubia jana katika Mahafali ya 31 ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) kwenye Makao Makuu ya chuo hicho, Bungo wilayani Kibaha katika mkoa wa Pwani, Dk Magufuli alisema aliitumbua bodi hiyo kutokana na kukiuka taratibu.

Alieleza kuwa kitendo chao cha kuidhinisha fedha hizo kuwekwa kwenye benki tofauti, ni tofauti na maelekezo kwani huo ndio ulikuwa mchezo unaofanywa na taasisi na mashirika mbalimbali.

“Sasa sifahamu kama Chuo Kikuu Huria na nyinyi mmekuwa mkiweka fedha za maendeleo katika Fixed Deposit Account, (akaunti maalumu) lakini huo ndio umekuwa ni mchezo, juzi hapa tumekuta fedha kiasi cha Shilingi bilioni 26 zilizokuwa zimetolewa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa ajili ya matumizi ya TRA, zikapelekwa kwenye benki tatu kama Fixed Deposit Account na Bodi ya TRA ikapitisha, ndio maana nilipozipata hizo taarifa, fedha nikachukua na Bodi kwa heri.

 “Hata kwa sasa hivi Waziri (wa Elimu Profesa Joyce Ndalichako) upo hapa, Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) ambayo ilianzishwa kwa sababu maalumu, inachangiwa fedha wakati kuna fedha zao wameziweka kwenye Fixed Deposit Account, Waziri hiyo ni message sent and Delivered,” alisisitiza Rais Magufuli.

Alisema kumekuwa na mchezo wa wakuu wa taasisi mbalimbali kuchukua fedha na kuziwekwa kwenye akaunti maalumu ambako serikali inakwenda kukopa kwa gharama kubwa.

“Kwa sasa huu ndio mchezo ambao unachezwa na kuisababishia serikali kukosa fedha jambo ambalo serikali haiko tayari kuona matumizi mabaya ya fedha zake,” alieleza Dk Magufuli ambaye anafahamika kwa kusisitiza kubana matumizi ya serikali na kukerwa na ukiukwaji wa taratibu za uendeshaji wa serikali.

Alisema mchezo huu umekuwa ukiipa serikali gharama kubwa kwa sababu ya kukopa fedha kwenye benki kwa gharama kubwa na kupotosha upatikanaji wa mapato.

“Naomba mtuombee tuendelee kutumbua kwani nchi ilifika mahali pabaya ambapo wanaweza kuitisha vikao hata Ulaya na kutokana na tumbua hii mapato yameongezeka kutoka trilioni 1.2 na kufikia 1.8 ambapo uchumi umeimarika,” alieleza Dk Magufuli.

Alisema uchumi umeimarika na unatakiwa ukue kwa asilimia 7.2, lakini hadi robo ya mwaka huu umekua kwa asilimia 7.9 na kuwa moja ya nchi ambazo uchumi wake unakua kwa kasi, ambazo kati ya nchi tano imekuwa ya pili baada ya Ivory Coast.

Aidha, alisema thamani ya fedha imepanda na kwamba wanaopotosha juu ya fedha ni wale waliokuwa wanapiga dili ambao kwa sasa hawana nafasi. Jumla ya wahitimu 4,027 walihitimu na kutunukiwa shahada mbalimbali na Mkuu wa Chuo Kikuu Huria Tanzania, Waziri Mkuu mstaafu Mizengo Pinda.

VIDEO: Rais Magufuli akieleza sababu ya kuvunja Bodi ya Mamlaka ya Mapato TRA

$
0
0
RAIS John Magufuli amefichua siri ya hatua yake ya kuitumbua Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Amesema alilazimika kuchukua hatua hiyo baada ya bodi hiyo kuidhinisha Sh bilioni 26 kupelekwa kuwekwa kwenye akaunti maalumu( Fixed Account)  katika benki kadhaa za biashara.

==> Msikilize hapo chini

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa Ya Novemba 25


Kampeni ya kumng’oa Trump yashika kasi

$
0
0

Ndoto za Donald Trump aliyechaguliwa hivi karibuni kuwa Rais wa 45 wa Marekani huenda zikayeyuka baada ya wajumbe sita wa Democratic watakaopiga kura za majimbo kuanzisha kampeni maalumu ya kuwashawishi wajumbe wengine kutomwidhinisha Rais huyo mteule.

Wajumbe hao ambao majina yao yalitangazwa jana wanaamini kuwa iwapo watafanikiwa kuwashawishi wenzao wengine 37 kutoka Chama cha Republican basi watakuwa wamefanikiwa kumzuia bilionea huyo kuingia ikulu.

Desemba 19 wajumbe 538 kutoka majimboni watakutana kupiga kura ya kisheria kumthibitisha Rais mteule anayetarajiwa kuapishwa Januari 20. Kura hizo zitahesabiwa mbele ya Bunge la Congress Januari 6.

Hatua ya wajumbe hao wa Democratic kuanzisha kampeni hiyo imekuja siku chache baada ya makundi ya kiharakati kuanza kukusanya saini nchi nzima ili kuwashinikiza wajumbe hao kutompitisha rais huyo ambaye tayari ameanza kutangaza vipaumbe vyake.

Mmoja wa wajumbe hao aliyetambulika kwa jina la Michael Baca anayewakilisha Colorado amekuwa akizunguka huku na kule kuwashawishi wajumbe wenzake kuepuka kumuunga mkono Trump wakati wa upigaji wa kura.

Mjumbe mwingine ambaye hakupenda jina lake kutajwa alisema kutokana na mvutano unaoendelea kujitokeza sasa kunaweza kuzusha hoja zitakazolazimisha kuangaliwa upya kwa mfumo unaotumika sasa kupitia kura za majimbo kumchagua rais.

Ingawa bado haijajulikana ni wajumbe wangapi wanaendelea kuwa waaminifu kwa kambi ya Trump lakini mchambuzi wa masuala ya siasa, Profesa George Edwards III amesema kama kutatokea wajumbe nane au 10 wakaamua kutomuunga mkono rais huyo mtarajiwa basi kunaweza kubadilisha ndoto za kiongozi huyo kuingia ikulu Januari 20 mwakani.

Tayari wafuasi hao wameitisha kampeni ya kuomba Wamarekani kuwaunga mkono mtandaoni kupitia tovuti ya www.change.org wa kuwashawishi wachaguaji hao kumchagua Clinton badala ya kumthibitisha Trump kwa kuwa hafai kuwa rais wa taifa hilo.

Ujumbe huo unaeleza kuwa iwapo watachagua kama ambavyo majimbo yamepiga kura katika uchaguzi huu, Trump atashinda.

“Hata hivyo, wanaweza kumpigia Hillary Clinton wakiamua,” inasomeka sehemu ya kampeni hiyo yenye kichwa cha habari; “Kura ya uamuzi: Mfanye Hillary Clinton kuwa rais Desemba 19”.

“Hata katika majimbo ambayo wajumbe hawatakiwi kufanya hivyo, wakiamua kura zao zitahesabika, wanaweza wakafanya uamuzi kidogo ambao tutaamini wafuasi wa Clinton watavutiwa nao.”

Mtandao huo unaeleza kuwa Clinton alishinda kura ya wengi hivyo anafaa kuwa rais kwa kuwa Trump alishinda majimbo yenye kura nyingi za majimbo basi mwenendo ukaonyesha bayana kuwa atashinda kura za uamuzi.

Katika uchaguzi uliofanyika Novemba 8 mwaka huu, Wamarekani waliwachagua wagombea wa urais kwa kura ya wengi na kuchagua wapigakura watakaomchagua rais mteule mwezi mmoja ujao.

Clinton aliongoza kura za wengi kwa zaidi ya kura 200,000 lakini Trump aliibuka mshindi kutokana na kushinda majimbo yenye kura nyingi za majimbo.

Ili Rais ashinde kinyang’anyiro hicho, anatakiwa kushinda kura 270 kati ya kura 538 zilizopo kutoka majimboni.

Kwa kutumia mfumo wa mshindi wa jimbo anashinda pia kura za uamuzi. Hadi sasa Trump ana kura 306 wakati mpinzani wake, Clinton akiondoka na kura 232. Ni mara chache kwa Marekani mshindi wa urais kuzidiwa katika kura za wengi.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Fordham, Christina Greer alisema kati ya wajumbe 538 watakaopiga kura mwaka huu, 100 ni maseneta ambao ni wawili kila jimbo, wajumbe watatu kutoka makao makuu ya nchi, Washington D.C, na wabunge 435.

“Majimbo yote kasoro mawili ya Maine na Nebraska mgombea mwenye kura nyingi kwenye jimbo basi ndiye mshindi pia wa kura za wajumbe.

“Hii ina maana matokeo yakitoka tu mwenye kura nyingi huwa ni mshindi licha ya kura kusubiri kura za uamuzi Desemba 19,” Dk Dreer.

Hata hivyo, matumaini ya wafuasi hao wa Clinton huenda yasizae matunda kwa kuwa sheria za majimbo mengi likiwamo la Minnesota Marekani zinakataza uwepo wa “wajumbe wasiowaaminifu” na baadhi yanatoza faini kati ya Dola 500 (Sh1 milioni) za Marekani hadi 1,000 (zaidi ya Sh2 milioni).

Faini hiyo ni matokeo ya uamuzi wa Mahakama juu ya nchi hiyo iliamua mwaka 1952 wapigakura hao wawe wanakula viapo mapema wakati wa mkutano mkuu wa chama juu ya nani watamchagua, mtandao wa Factcheck.org unaochapisha habari za siasa, umeeleza.

Ripoti ya uchunguzi wa mali za BAKWATA yakabidhiwa

$
0
0
Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakari Zuber  jana amekabidhiwa ripoti ya awali iliyoandaliwa na tume ambayo ameiunda  kwa ajili ya kufanya uchunguzi  na kuzibainisha  mali zote za  Baraza kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA).

Akizungumza wakati wa kumkabidhi ripoti hiyo, Mwenyekiti wa tume hiyo Sheikh Abubakari Khalid Hajj alisema kuwa  ripoti hiyo imefanyika kwa muda wa miezi mitatu licha ya kukumbwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ufinyu wa muda.

Aidha aliwambia wanahabari kuwa uchunguzi huo umehusisha ufuatiliaji wa mali za Bakwata katika Mkoa wa Dar es salaam pekee,ikiwemo majengo,viwanja, pamoja na kupitia mikataba mbalimbali ili  kujiridhisha kama imefuata taratibu za kisheria.

Akizungumza mbele ya wanahabari mara baadi ya kupokea ripoti hiyo Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakari Zuber alisema kuwa ataipitia ripoti hiyo  ili kujua yale yaliyobainishwa na tume yake, na kuahidi kuyafanyia kazi mapema iwezekanavyo.

Hata hivyo Mufti huyo ameiongezea muda wa miezi mitatu tume hiyo ambayo ina jumla ya  wajumbe wanane kwa ajili ya kukamilisha kuandaa ripoti ya mkoa wa Dar es salaam kabla ya kuhamia mikoa mingine kwani zoezi hilo litafanyika nchi nzima.

Rais Magufuli amualika Rais wa Zambia kwa ziara ya siku 3

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga, amesema Rais Edgar Lungu wa Zambia anatarajiwa kufanya ziara rasmi ya siku tatu nchini kuanzia Novemba 27 kwa mwaliko wa Rais Dkt. John Pombe Magufuli.

Dkt. Mahiga amesema wakati wa ziara hiyo, Rais Lungu atasaini mikataba mbalimbali ya ushirikiano kati ya Zambia na Tanzania.

Miongoni mwa mikataba hiyo ni pamoja na ushirikiano wa masuala ya anga, ulinzi na usalama, ushirikiano katika masuala ya uhamiaji, na kuweka utaratibu wa kubadilishana wafungwa.

Akiwa nchini Rais Lungu pia atatembelea Bandari ya Dar es Salaam, reli ya Tazara, na bomba la mafuta la Tazama.

Kwa upande wake Mkurugenzi idara ya Afrika Balozi Samweli Shelukindo amesema utekelezaji wa mikataba hiyo utaleta maendeleo baina ya nchi hizi mbili.

Shilingi bilioni 3 zatafunwa kununulia mafuta katika 'magari hewa' .

$
0
0
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Posta Tanzania Luteni Kanali Mstaafu Dkt. Haroun Kondo (Kushoto)
  **
Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Posta Tanzania imeuagiza uongozi wa shirika hilo kuwatambua na kuwafikisha mbele ya vyombo vya sheria, wafanyakazi wake waliolisababishia shirika hilo hasara kupitia mikataba ya kilaghai pamoja na utendaji mbovu

Mwenyekiti wa Bodi hiyo Luteni Kanali Mstaafu Dkt. Haroun Kondo, ametoa agizo hilo jana wakati akitoa taarifa kuhusu utiaji saini ya makubaliano ya kiutendaji kati ya bodi ya wakurugenzi na uongozi juu wa shirika hilo kuhusu jinsi wanavyopaswa kuliendesha shirika hilo kwa faida.

Kwa mujibu wa Dkt. Kondo, ubadhirifu ndani ya shirika hilo umevuka mipaka na kamwe hauwezi kuvumilika ambapo alitaja baadhi ya mianya ya wizi kuwa ni katika uendeshaji na usimamizi wa rasilimali za shirika.

Alitolea mfano jinsi shilingi bilioni tatu zilivyotafunwa na wajanja wachache kwa kisingizio cha malipo ya mafuta kwa magari ambayo taarifa zake zinaonesha kuwa hayatembei kutokana na kuwa katika matengenezo kwa muda mrefu.

Muhimbili yafanya upasuaji Mkubwa wa kihistoria wa Kuhamisha Misuli

$
0
0
Madaktari wa Hospitali ya Taifa Muhimbili jana kwa mara ya kwanza wamefanya upasuaji kwa kutumia darubini (microvascular surgery) wa kuhamisha misuli na mishipa ya damu kutoka kwenye mguu kwenda sehemu nyingine chini ya mguu (free gracilis muscle transfer).

Upasuaji huu wa aina yake na ambao mara nyingi huchukua muda wa saa sita hadi saba una lengo la kujenga uwezo kwa watalaamu wa ndani ili waendelee kutoa huduma za ubingwa wa hali ya juu kwa Watanzania wengi zaidi na vilevile kupunguza kasi ya kupeleka wagonjwa nje.

Mkuu wa Idara ya Upasuaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) ambaye pia ameshiriki upasuaji huo Dk Ibrahim Mkoma alisema upasuaji huo unagharimu kiasi cha dola 40,000 za Marekani nchini Australia ikiwa ni gharama ya upasuaji tu.

Lengo kubwa la ushirikiano wa upasuaji huu ni wataalamu kutoka Australia kuwaachia taaluma ya upasuaji huo madaktari MNH ili iweze kuendelea kufanya upasuaji huo mbeleni.

Aidha Dk Mkoma alisema kuwa kuanzia mwakani kutakuwa na utaratibu ambao utaanzishwa Chuo Kikuu cha Tiba Muhimbili, wa taaluma maalumu ya kusomea upasuaji wa aina hiyo ili kuweza kupata wataalamu zaidi kutoka nchini. Alisema hakuna chuo chochote Tanzania kinachotoa taaluma hiyo ya plastic surgery kwa sasa.

Dk Mkoma alisema MNH inajivunia kushirikiana na madaktari bingwa kutoka Australia akiwapo Daktari bingwa James Savundra ambaye ni Rais wa Madaktari Bingwa wa upasuaji kutoka timu ya upasuaji nchini Australia.

Daktari bingwa wa upasuaji kutoka Australia, Dk James Savundra alisema upasuaji huo ni moja ya upasuaji ambao umekuwa ukifanyika kwa gharama kubwa.

Makonda azidi kuwabana wenyeviti wa Mitaa.......Amburuza mwingine rumande

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda jana  aliliagiza jeshi la polisi kumkamata mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Zavala kata ya Buyuni Ilala, Chiku Said baada ya kutuhumiwa kuuza viwanja vya watu pamoja na serikali kinyume na sheria.

Hatua hiyo imekuja baada ya wananchi kulalamika kwa kumtuhumu mwenyekiti huyo kuuza viwanja vya serikali kinyume na sheria bila kuwahusisha wajumbe wenzake hali ambayo imesababisha mgogoro mkubwa wa ardhi katika eneo hilo

Hatua hiyo ilimfanya mkuu wa mkoa  kumtaka Afisa Ardhi wa Manispaa ya Ilala, Paul Mbembela kuthibitishwa kuuzwa kwa eneo hilo kinyume na sheria.

“Mkuu wa mkoa, ni kweli tulikuwa na eneo Block J lakini limeuzwa,” alisema afisa huyo “Nataka kuwaambia kitu wenyeviti wa mtaa hawaruhusiwi kuuza eneo katika mtaa. Mimi ningewataka wenyekiti kufuata taratibu za kisheria zilizowekwa ili kuepuka kutokea kwa hayo mambo,”

Baada ya kauli hiyo Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam,  Makonda akaliagiza jeshi la polisi kumkamata mwenyekiti huyo kwa ajili ya uchunguzi zaidi

Wafuasi wa CUF Watwangana Ngumi Mahakamani

$
0
0
Wafuasi  wa Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba na Katibu Mkuu wa Chama hicho,  Maalim Seif Sharif Hamad jana waligeuka sinema ya bure baada ya kutwangana makonde hadharani katika Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam.

Ugomvi huo ulioibua mapambano ya ngumi ulitokea jana baada ya wafuasi wa Maalim Seif waliokuwa mahakamani hapo kumzuia Profesa Lipumba kuingia kusikiliza kesi inayomkabili iliyofunguliwa na Baraza la Wadhamini wa Chama hicho.

Profesa Lipumba alifika mahakamani hapo saa mbili asubuhi, ikiwa ni mara yake ya kwanza tangu kesi hiyo dhidi yake kufunguliwa ikidai kuwa yeye si mwanachama halali wa CUF.

Baada ya kesi za Jaji Sakiet Kihio kuitwa na mtoa matangazo wa Mahakama kwa kuelekeza kuwa kesi za Jaji huyo zinasikilizwa chemba watu wote waliinuka na kuelekea katika chumba hicho wakiwamo mawakili wa pande zote.

Walipofika kwenye mlango wa chumba cha Mahakama, wafuasi wa Maalim Seif walisimama mlangoni kumzuia Profesa Lipumba kwa madai kuwa wanaotakiwa ni mawakili tu na si watu wengine, ndipo wafuasi wa Mwenyekiti huyo walipoingilia kati na kuwashushia kipigo watu hao.

Hatua hiyo ilishuhudia mabadilishno ya  makonde na kusababisha watu wawili upande wa Maalim Seif  kuumia, na kusababisha Jaji Kihio kutoa amri kuwa waingie mawakili na walalamikiwa ndipo Lipumba naye akaingia.

Kesi iliendelea kusikilizwa, huku askari wakiimarisha ulinzi wa chumba hicho, kwa sababu wakati wafuasi hao wanapigana wao hawakuwapo. Jaji Kihio aliahirisha kesi hiyo hadi Desemba 6 zitakaposikilizwa sababu za Bodi hiyo kumtaka ajitoe kusikiliza kesi hiyo.

Baada ya kesi hiyo kuahirishwa, Profesa Lipumba alitolewa na wafuasi wake akiwa chini ya ulinzi mkali kwa kuhakikisha kuwa hakuna mtu atakayemgusa na alipofika nje, alipokewa na wafuasi wengine wakiwa na mabango yenye ujumbe dhidi ya Maalim Seif.

Bango moja liliandikwa: ‘Maalim Seif kama ulikaa na CCM umeshindwaje kukaa na Mwenyekiti wako Lipumba mkayamaliza’, lingine: ‘Maalim Seif tulijua CCM ndiyo kiboko yako, kumbe Lipumba ndiye mwamba wako’, huku wakiendelea kuimba wimbo wa chama hicho.

Lipumba alipoingia kwenye gari alishusha kioo na kusalimu wafuasi wake kwa kuwapungia mikono, huku wengine wakisukuma gari lake kabla ya kuondoka eneo la Mahakama.

Hata hivyo, Profesa Lipumba hakutaka kuzungumza chochote, akitumia muda wake mwingi kutabasamu na kupunga mkono. Wakati hayo yote yakifanyika, nje ya Mahakama askari walikuwa tayari wametenga makundi hayo mawili, lakini bila kufanya hivyo, watu hao wangeendelea kupigana.

Wakili wa Bodi hiyo, Juma Nassoro akiwa nje ya Mahakama, alimkariri Jaji akisema Desemba 6 kesi hiyo ataisikilizia kwenye Mahakama ya Wazi, kwa sababu alikuwa hajui kama watu ni wengi, kwa hiyo hataifanyia tena chemba.

Pia alisema Profesa Lipumba, Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju na wafuasi 11 wamewasilisha pingamizi mahakamani hapo, kuwa wateja wake walifungua kesi hiyo bila idhini ya Mahakama na pia Maalim Seif alibariki kufunguliwa kwa kesi hiyo bila idhini ya Bodi.

Baadaye mawakili wa CUF, Nassor na Hashimu Mziray waliwasilisha ombi la kumtaka Jaji Kihiyo ajitoe kusikiliza shauri hilo kwenye Mahakama hiyo, na sababu za kumkataa zitaelezwa Desemba 6 saa saba mchana wakati kesi hiyo itakapokuja kusikilizwa.

Walalamikaji hao wanaomba Mahakama itengue barua ya Msajili ya kumtambua Profesa Lipumba kuwa mwanachama hai wa CUF.  Wakili Mziray alisema walifungua kesi hiyo kwa hati ya dharura kutokana na mambo yalivyo sasa ndani ya chama hicho, kwa sababu hawajui hata ofisi zingine zinaendeshwaje.

Alisema katika maombi hayo, wanaiomba Mahakama mambo matatu, ambayo ndiyo yanasababisha kufukuta kwa mgogoro, kwa hiyo wanaomba yatenguliwe ili shughuli za kisiasa ziendelee.

Alisema mambo hayo ni pamoja na Mahakama kutengua barua ya Msajili ya Septemba 23 ambayo ilitengua uamuzi wa CUF wa kumfukuza uanachama Profesa Lipumba na kumhalalisha kuwa mwanachama hai wa chama kama Mwenyekiti.

Serikali kufuta utitiri wa kodi kwenye viwanda

$
0
0
Makamu wa Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amesema serikali inajipanga kuondoa utitiri wa kodi mbalimbali zinatozwa kwenye viwanda kama hatua ya kuviwezesha viwanda vingi nchini  kuongeza uzalishaji na kutoa ajira nyingi kwa watanzania.

Samia ametoa kauli hiyo jana Jijini Arusha baada ya kutembelea kiwanda cha kutengeneza mafuta ya kupikia cha Mount Meru Millers ili kujua changamoto zinazokikabili kiwanda hicho ili Serikali iweze kuzifanyia kazi katika kuleta unafuu kwenye uzalishaji wa mafuta ya kupikia nchini.

Alisema mlolongo wa kodi zinazotozwa kwa wamiliki wa viwanda hazina uratibu mzuri hivyo mkakati ya Serikali wa awamu ya Tano inataka kuweka utaratibu mzuri wa ulipaji wa kodi hizo ikiwemo kuondoa kodi ambazo ni kero kwenye viwanda.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya Mount Meru Millers Atul Mittal alisema kama Serikali itafuta au kuondoa utitiri wa kodi wanazotozwa kwenye viwanda hivyo watakuwa na uwezo wa kuongeza maradufu uzalishaji na kutoa ajira nyingi kwa Watanzania.

Alisema kwa sasa Kampuni hiyo inafanya kazi kwenye nchi 10 barani Afrika na kwa Tanzania pekee imeajiri wafanyakazi zaidi ya 1000 ambao wanafanyakazi katika maeneo mbalimbali nchini.

AUDIO: Askari polisi 6 wa Kikosi cha Usalama Barabarani Watumbuliwa Kwa Utovu wa Nidhamu

$
0
0
Askari  polisi sita wa Kikosi cha Usalama Barabarani, wameondolewa baada ya kukiuka taratibu za kazi.

Akizungumza na waandishi wa habari  jana, Kamishana Msaidizi Mwandamizi wa Polisi ambaye pia ni Mkuu wa Operesheni, Kitengo cha Usalama Barabarani Tanzania, Fortunatus Musilimu, alisema askari hao watapangiwa kazi nyingine.

Kwa mujibu wa Kamishna Musilimu, askari hao kutoka katika mikoa mbalimbali nchini, waliondolewa wakati wa ukaguzi wa utendaji wa kazi kwa askari wa kikosi hicho.

“Ukaguzi huo ulifanyika nchi nzima katika barabara kuu kufuatia mpango mkakati wa kupunguza ajali za barabarani nchini,” alisema kiongozi huyo wa polisi.

Aliwataja askari hao kuwa ni D 9363 Sajenti Richard aliyekuwa wilayani Misungwi, Mkoa wa Mwanza, G 9958 PC, Edward, aliyekuwa eneo la Lilambo mkoani Ruvuma, H 8234 PC Mungwe, aliyekuwa eneo la Tanesco Jimboni, wilayani Mbinga, Mkoa wa Ruvuma na WP 3058 Koplo Mariam, aliyekuwa eneo la Igurusi, Mbeya.

“Askari hao walikutwa wakiwa hawakuvaa namba za Jeshi la Polisi kama utambulisho wao kazini, kitendo ambacho ni utovu wa nidhamu na kutozingatia maadili ya kijeshi.

“Yaani kitendo cha kutovaa namba kiliashiria askari hao walikuwa wababaishaji, walikuwa wakificha maovu, hawakuwa wawazi katika utendaji kazi wao na pia waliashiria kujihusisha na vitendo vya rushwa.

“Mbali na hao, askari wengine waliochukuliwa hatua ni D 9603, Sajenti Samwel na G 8264, PC Dickson, waliokutwa eneo la Hanihani, wilayani Igunga, Mkoa wa Tabora.

“Hawa walikutwa katika mazingira yanayoonyesha walikuwa wakijihusisha na vitendo vya waziwazi  vya kudai rushwa kutoka kwa wenye magari yaliyokuwa na makosa,” alisema Kamishna Musilimu.

Kutokana na hali hiyo, aliwataka askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani kufanya kazi kwa uadilifu ili wasichukuliwe hatua.

==>Msikilize hapa Kamanda Muslimu akifafanua sababu za uamuzi huo:- 

RIWAYA: She is My Wife- Sehemu ya 45 & 46

$
0
0
Mwandishi: EDDAZARIA G.MSULWA

ILIPOISHIA  
Majibu ya mlinzi huyo mwenye roho ya kikatili sana, yakaustua moyo wa makamu wa raisi kwani ameamini kwamba taarifa hiyo si nzuri kwa upande wake.
“Raisi Praygod Makuya anaelekea hospitalini kuonana na Samson”
“WHAT………!!!”  
Makamu wa raisi alijikuta akiishiwa na nguvu, akajibwaga kwenye sofa lililopo karibu yake akibaki amemtumbulia mimacho mlinzi wake huyo.
                                                                                    
ENDELEA  
Makamu wa raisi akakaa kimya kwa muda akifikiria ni kitu gani anaweza kukifanya, gafla akasimama huku akitabasamu
“Bimgo”
Alizungumza huku akimuomba mlizi wake simu. Akaminya baadhi ya namba kisha  akaiweka simu yake sikioni, baada ya dakika kadhaa ikapokelewa na sauti nzito ya kiume.
“Yaa ni mimi”

Makamu wa raisi alizungumza, na kumfanya mtu aliye ipokea simu hiyo kuweza kujua anazungumza na nani.
“Kuna mgonjwa hapo hospitalini kwako, somebody Samsoni. Ninahitajia umuondoe kwenye ramani ya dunia”
“Sawa nimekuelewa muheshimiwa, uishi daiama”
“Asante”
Makamu wa raisi akakata simu huku akiwa katika tabasamu pana. Ulinzi kwenye hii hoteli yake aliyo ijenga kwa usiri mkubwa pasipo serikali ya Tanzania kuweza kuifahamu, uliendelea kuimarika kila kona huku vijana wake wanao muunga mkono wakiwa makini sana kuhakikisha kwamba hakuna mtu anaye weza kufahamu kwamba kiongozi huyo anaye tafutwa na serikali ya Tanzania yupo kwenye hoteli hii kubwa ya kitalii.
                                                                                              ***
Tayari mawasiliano yalisha fanywa kwenye hospitali ya Muhimbili, ili chumba alicho lazwa Samson kifanyiwe ulinzi wa hali ya juu. Askari wenye bunduki nzito walisha weka ulinzi eneo zima la hospitali wakihakikisha kwamba anapofika Raisi Praygod Makuya, kila jambo linakuwa kwenye mstari na hakuna tatizo la kijinga litakalo kwenda kujitokeza.

Hali ya Samson, kidogo inaleta matumaini kwa madaktari, hii ni baada ya kutolewa risasi mwlinini mwake, ambazo kwa bahati nzuri hazikuweza kuleta madhara makubwa sana kwenye mwili wake.
“Nahitaji kumcheki mgonjwa”
Daktari mkuu wa kitengo cha upasuaji aliwaambia askari wawili walio simamam mlangoni mwa chumba alichopo Samson. Mmoja wa askari akachukua kitambulisho kinacho ning’inia kwenye kifua cha daktari huyo na kulisoma jina lake, ili kudhibitisha kwamba kweli ni daktari wa hospitali hiyo, alipo jiridhisha akamruhusu daktari huyo kuingia ndani ya chumba hicho.

Dokta Maliki, akasimama pembeni ya kitanda alicho lalala Samson, anaye hemea kwa mashine maalumu za kupumulia.
“Nilazima umfe mwanaharamu wewe”
Dokta Maliki alizungumza huku akivaa gloves zake nyeupe kwenye viganja vyake, ili kutoweza kuacha alama za vidole pale atakapo fanya mauaji yale alio agizwa na Makamu wa raisi. Alipo hakikisha gloves zake zipo vizuri, akachomoa mashine iliyo wekwa kwenye kinywa cha Samson, akasababisha Samson kuanza kujitingisha tingisha taratibu, akijaribu kuipigania roho yake na umauti kwani hewa iliyokuwa inaingia kwenye mapafu yake imekatishwa.
                                                                                             ***
“Endesheni haraka”
Rahab alizungumza huku akihangaika hangaika kwenye siti aliyo kalia hadi Raisi Praygod akamshangaa kwani ni kama mtu anaye hitaji kuweza kuliwahi jambo fulani.
“Kwani vipi mke wangu?”
“Kuna tatizo fanyeni haraka”
“Wapi…!!?”

“Dereva ongeza kasi tafadhali”
“Madam sote tunakwenda kwenye mwendo mmoja nikiongeza kasi mimi naweza kusababisha ajali”
Dereva anaye waendesha alizungumza kwa ukanini wa hali ya juu kwani ndivyo sheria ya kazi yake inavyo zingatia, kwenye msafara kama huo wote huwa wanaendesha katika mwendo kasi unao fanana.
“Lakini tunakaribia kufika mke wangu”
Raisi Praygod alimtoa wasiwasi Rahab, aliye yafumba macho yake kwa haraka, kama mtu anaye jaribu kuvuta hisia ya jambo fulani. Kila alipo jaribu kuvuta hisia dhidi ya jambo linalo kwenda kumtokea Samson, akashindwa kuona ni nini kinacho kwenda kutokea.

“Pleaseeeee”
Rahab alizungumza kwa sauti ya juu huku akizidi kuyafumba macho yake kwa nguvu, hadi damu za puani zikaanza kumchuruzika taratibu, Raisi Praygod akajaribu kumshika mkono mke wake kutazama ni nini kinacho msumbua, ila akajikuta mkono wake ukisogezwa kwa nguvu na mke wake huyo hadi akabaki ameduwaa.
Rahab, akashuhudia jinsi shingo ya Samson inavyo kandamizwa kwa nguvu na mtu aliye valia mavazi meupe, baada ya muda kidogo Samson akatulia kimya, ikiashiria tayari amesha yapoteza maisha yake. Rahab akayafumbua macho yake huku akishusha pumzi taratibu, machozi ya uchungu yakaanza kumwagika usoni mwake.

“Mke wangu unatatizo gani?”
Raisi Praygod aliuliza huku akiwa na wasiwasi mkubwa, Rahab akatingisha kichwa akidai hakuna tatizo ambalo limejitokeza. Rahab akajifuta damu zilizo kuwa zikimwagika, huku akiamini kwamba safari wanayo iendea haina umuhimu tena kwao. Kwani mtu wanaye mfwata tayaria amesha uawa kinyama, na mtu amabaye hakuiona sura yake.
                                                                                                  ***
Dokta Maliki, alipo hakikisha kwamba tayari amesha muua Samson kwa kuiminya shingo yake, akarudishia kila kitu alicho kitoa kwenye mwili wa Samson, ikiwemo mashine inayo msaidia kuhema. Baada ya mashine hiyo kurudishiwa kwenye mdomo wa Samson, ikaaonyesha mstari  mwekundu ulio nyooka, ukiashiria kwamba mtu huyo tayari amesha poteza maisha. Dokta Maliki akatoka ndani ya chumba hicho.
“Hakikisheni hakuna anaye ingia humu ndani, mgonjwa anahitaji kupumizika”

Aliwaambia askari hao ambao hakuna aliye kuwa akifahamu ni kitu gani kinacho endelea, Dokta Maliki akaanza kutembea kwenye kordo ndefu kuelekea nje, na muda huu hakuhitaji kukaa tena hospitalini kwani tayari anatambua ni kitu gani alicho kifanya na endapo atajulikana kama yeye ni muuaji, basi adhabu kali itaambatana naye.
Akiwa katika eneo la maegesho ya magari, gari kadhaa zinazo ashiria zimembeba kiongozi mkubwa zikasimama, ikamlazimu kuangalia ni kiongozi gani ambaye anashuka. Mlango wa gari moja ukafunguliwa akashuka binti mmoja pamoja na jaama ambaye ni mara yake ya kwanza kuiona sura yake

“Huyu ni nani?”
Alijuliza, huku akiendelea kumtazama jamaa huyo anaye wekewa ulinzi mkubwa kama kiongozi wa nchi. Macho ya dokta Maliki yakagongana na macho ya Rahab, aliye mtazama kwa muda huku akionekana kama msichana huyo anamtambua Dokta Maliki. Raisi Praygod baada ya kumuona mke wake anamshanga sana dkatari aliye simama kwenye moja ya gari huku akiwa na funguo mkononi, ikambidi amshike mke wake mkono.

“Baby twende ndani”
Rahab akaondoka na Raisi Praygod ambaye sura yake halisi imefunikwa na sura bandia ambayo hakuitaji sura yake iweze kuonekana na mtu wa iana yoyote zaidi ya walinzi wake wanao fahamu kwamba ni yeye. Dokta Maliki akiingia ndani ya gari lake na kuondoka katika eneo la hospitali ya Muhimbili huku moyoni mwake akiwa na furaha ya kuweza kukeleza kazi ya kiongozi wake anaye mtumikia.

 

Mchungaji Anthony Lusekelo (Mzee wa Upako) akamatwa na Polisi.....Anadaiwa Kumfanyia Fujo Jirani Yake Huku Akiwa Amelewa

$
0
0

Mchungaji  Kiongozi wa Kanisa la Maombezi (GRC) la Dar es Salaam, Anthony Lusekelo, maarufu Mzee wa Upako, amekamatwa na polisi akituhumiwa kumfanyia fujo na kutishia kumuua jirani yake.

Tukio hilo lilitokea juzi maeneo ya Kawe wilayani Kinondoni, Dar es Salaam, kuanzia saa 11 asubuhi hadi saa tatu alipochukuliwa na polisi wa Kituo cha Kawe.

Wakati wa tukio hilo, Mchungaji Lusekelo alikuwa ameegesha gari lake barabarani kiasi cha kusababisha usumbufu na foleni ya magari mengine.

Chanzo cha tukio hilo kinadaiwa ni kulipiza kisasi kwa jirani zake hao wanaoishi katika nyumba namba KAW/MZN/1348, ambao alidai wamekuwa wakimkebehi kuwa hafai kuwa mchungaji kwa sababu ya ulevi.

Licha ya baadhi ya watu kumsihi aondoke eneo hilo kutokana na hadhi yake, mchungaji huyo alikaidi, huku akiendelea kuongea kwa sauti iliyofanana na mtu mwenye kilevi.

Baadhi ya maneno yaliyosikika kwenye video iliyorekodiwa eneo la tukio  hayaandikiki  kwa kuwa si ya kawaida.

“Mjinga wewe, mimi ni zaidi ya askari na wewe ni mgambo, na si mgambo wewe ni raia tu.

“Umenitukana sana wewe mpaka leo nimeamua kuloana na mvua, usitoe gari hapo mshenzi sana wewe, na nikikuona mahali popote…, mshenzi kabisa, muangalie sana huyo,” alisikika Mchungaji Lusekelo akiongea kwa sauti.

Baada ya kuongea maneno hayo, ilisikika sauti ya mwanamke kutoka ndani ya uzio wa nyumba hiyo ikimjibu mchungaji huyo:“Huwezi, aniangalie kitu gani.”

Hata hivyo, hata watu mbalimbali walipomsihi aache kutoa lugha hizo za kejeli na aondoe gari lake lililokuwa limesababisha foleni, alikataa akisema hataliondoa hadi atakapokuja Kamanda wa Polisi, Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna Simon Sirro.

Baada ya purukushani hizo, polisi kutoka katika Kituo cha Kawe walifika eneo hilo saa tatu asubuhi, wakamchukua mchungaji huyo na kumpeleka kituoni.

Inadaiwa baada ya kufikishwa kituoni hapo, mchungaji huyo alipimwa kiwango cha ulevi na kukutwa 131, ambacho kinaelezwa kuwa ni kikubwa – ulevi wa kupindukia.

Ilipofika saa tano asubuhi, mchungaji huyo alihamishiwa Kituo Kikuu cha Polisi (Central), ambako huko nako inadaiwa alipimwa kilevi na kuonekana kushuka hadi kufikia 121.

Alipotafutwa Kamishna Sirro ili kuzungumzia sakata la mchungaji huyo, alisema atalizungumzia leo katika mkutano wake na waandishi wa habari.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya Leo Novemba 26

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images