Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Sakata la Oparesheni UKUTA: Viongozi wa Dini Waendelea Kusubiri Maombi Yao Kujibiwa na Rais Magufuli

$
0
0
Viongozi wa dini nchini waliopanga kumwona Rais John Magufuli kwa mazungumzo kuhusu hali ya siasa nchini wanaendelea kusubiri maombi yao kujibiwa licha ya kupita zaidi ya siku 90 sasa. 

Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Askofu Frederick Shoo  jana alisema: “Siwezi kusema Rais amekataa kuonana nasi, hapana. Labda ni kwa lile tulilokuwa tuende kumuona nalo (Ukuta) lakini kwa mazungumzo mengine milango ya Rais iko wazi,” alisema. 

Wazo la viongozi wa dini za Kikristo na Kiislamu kutaka kuonana na Rais lilibuniwa Agosti ili kuzuia maafa ambayo yangejitokeza baada ya Chadema kutangaza kufanya maandamano waliyoyapa jina la Ukuta, Septemba Mosi. 

Hata hivyo, Dk Shoo alielekeza atafutwe Katibu wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT), Mchungaji Dk Leonard Mtaita kwa maelezo zaidi akisema ni mmoja wa wanaoratibu suala hilo. 

Dk Mtaita alipotafutwa kwa mara ya kwanza Septemba azungumzie kama barua waliyopeleka kwa Rais imejibiwa alisema tetemeko la ardhi lililotokea mkoani Kagera na kusababisha maafa makubwa litachelewesha mpango wao wa kukutana na Rais. 

Hata hivyo alipotafutwa tena jana, Dk Mtaita aliomba atafutwe mwenyekiti mwenza wa kikao kilichoibuka na wazo hilo ambaye ni Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhadi Mussa Salim. 

“Tumewaachia wenzetu walioko Dar es Salaam, Sheikh Salim ndiye mwenyekiti mwenza na yeye yuko Dar na ndiye alijitolea kufanya mawasiliano na Mheshimiwa Rais,” alisema Dk Mtaita. 

Sheikh Salim alipotafutwa ili aeleze alipofikia kufanikisha kuonana na Rais alijibu kwa kifupi tu: “Sisi tuko katika kusubiri. Barua tulishatuma kwa Mheshimiwa Rais. Tunasubiri tu”. 

Msemaji wa Serikali, Hassan Abass alipoulizwa alitaka atafutwe Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Gerson Msigwa kwa kuwa ndiye msemaji wa Rais. 

“Mtafute Msigwa maana yeye yupo karibu na Mheshimiwa (Rais Magufuli) na anajua ratiba zote,” alieleza. 

Alipotafutwa, Msigwa aliwataka viongozi hao kuendelea kusubiri kwa kuwa kila kitu kina utaratibu wake na pia inategemea ratiba ya Rais. 

“Kama wameandika, wasubiri watajibiwa,” alisema Msigwa.

Viongozi wa Chadema wanaposoma Katiba na Sheria ya Vyama vya Siasa wanaona wana haki ya kufanya mikutano ya ndani na hadhara na maandamano mradi tu Jeshi la Polisi litaarifiwe siku na mahali pa shughuli hiyo. 

Rais Magufuli alipiga marufuku siasa za ushindani hadi mwaka 2020 jambo ambalo Chadema waliamua kujitokeza kupinga kwa maandamano. 

Mbali ya Rais Magufuli, Jeshi la Polisi lilitangaza kuwa ni marufuku kufanya mikutano na maandamano. 

Hali hiyo iliyotishia kuwepo makabiliano yenye maafa ndiyo iliyowaibua viongozi wa dini ambao walichukua hatua kwanza kuwasihi viongozi wa Chadema na pili kuwataka wasubiri mrejesho.

Jinsi Punyeto Inavyo Sababisha Ukosefu Na Upungufu Wa Nguvu za Kiume

$
0
0

Ukosefu  na/ama  upungufu  wa  nguvu  za  kiume, ni  tatizo  linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume  duniani.  Zipo  sababu  nyingi  zinazo  sababisha  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume.  

Miongoni  mwa  sababu  hizo  ni  pamoja  na  maradhi  kisukari, presha,shinikizo  la  damu, moyo, figo, matatizo  kwenye  mishipa  ya  ubongo  &  mishipa  ya  uti  wa mgongo, matatizo  kwenye  mishipa itumikayo  kusafrisha damu  mwilini, maradhi  ya  ngiri,  pamoja  na   upigaji  punyeto  kwa  muda  mrefu.

Katika  makala  yetu  ya  leo, tutaangalia  namna   suala  la  upigaji  punyeto linavyo  athiri  nguvu  za  kiume.

Kabla  hatujaangalia  namna  suala la upigaji  punyeto linavyo  maliza  nguvu  za  kiume, ni  vyema  tukafahamu  kwanza  kuhusu  SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME.

Kufahamu   kuhusu   SAYANSI  YA  MFUMO  WA  NGUVU  ZA  KIUME  tafadhali  tembelea :

Ukisoma  vizuri  kuhusu  mfumo  wa  nguvu  za  kiume, utagundua  kuwa   Suala  la  nguvu  za  kiume  ni  suala  la  kimfumo.  Ili  mwanaume  awe na nguvu  za  kiume, aendelee  kuwa  na  nguvu  za  kiume na  azilinde  nguvu  zake za  kiume, ni  lazima  ogani  zote zinazo  husika  na  mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ziwe  na  afya  njema  na  ziwe  na  ushirikiano   thabiti  na  wenye  afya.

Vile  vile , utagundua  kuwa , mambo  makuu  muhimu  katika   mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ni  kama  ifuatavyo:

i.Mishipa  imara  ya  ubongo  na  yenye  afya  njema

ii. Mishipa  imara  ya  uti  wa  mgongo  (  spinal  cords )

iii.Mishipa  imara  itumikayo  kusafirisha  damu  mwilini  (  Blood Vessels )

iv. Mfumo  imara  wa  usafirishaji  damu  mwilini

v. Mishipa  ya  uume  iliyo  imara  na  yenye  afya  njema

vi. Uhusiano  imara  na  wenye  afya  kati  ya  mishipa  ya  fahamu  iliyopo  katika  ubongo, mishipa  ya  kwenye  uti  wa  mgongo  pamoja  na  misuli & mishipa  ya  kwenye  uume.

Hivyo  basi, ili  mwanaume  aweze  kuwa  na  nguvu  imara  za  kiume, na  aendelee  kuwa  na  nguvu  hizo ni  lazima  mambo  yote  muhimu  katika  mfumo  wa  nguvu za  kiume  yawe  imara  pasi na  hitilafu  yoyote.

Hitilafu  yoyote  katika  mambo  hayo, itasababisha  ukosefu na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume  kwa  mwanaume  huyo.  Pale inapotokea    hitilafu  ama  mapungufu  katika  ogani  zaidi  ya  moja  kati  ya  zilizo  tajwa hapo  juu, basi  tatizo  kwa  muhusika  huwa  kubwa  mara  dufu.

JINSI  PUNYETO  INAVYO  SABABISHA  TATIZO  LA  UKOSEFU &  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.
Mwanaume   anapopatwa na  wazo  la  kufanya  tendo  la  ndoa, ubongo  hutoa  ishara  kwenye  mishipa  ya  uti  wa  mgongo  ambayo  nayo  husafirisha  taarifa  hadi  kwenye  mishipa &  misuli  ya  uume.

Mishipa  ya  uume inapopokea  taarifa  hiyo, hutanuka. Na  mishipa  ya  uume  inapotanuka, hufanya  mambo  mawili  muhimu  sana :

i.Husababisha  mishipa  ya  ateri  kupanuka  na  hivyo  kuruhusu  damu  kuingia kwa  kasi  sana   ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  hivyo  kuufanya  uume  usimame  na  kuwa  imara  bara bara.

ii. Huibinya na  kuiziba  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kuzuia  kunyonya  ama  kufyonza  damu  iliyo  ingia  ndani  ya  mishipa ya  uume.  (  KAZI  KUBWA  YA  MISHIPA  YA  VENA  ILIYO  KARIBU NA  MISHIPA  YA  UUME  NI KUHAKIKISHA  HAKUNA  DAMU NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME. HIVYO  BASI  DAMU  INAPOINGIA  NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME, MISHIPA  YA  VENA  HU “SENSE” JAMBO  HILO  KWA  HARAKA  NA HIVYO  KUIFYONZA  DAMU  HIYO  KUTOKA KWENYE MISHIPA  YA UUME  YA  KUITOA  NJE YA MISHIPA  YA  UUME.  NA  DAMU INAPOKOSEKANA  NDANI  YA  MISHIPA  YA  UUME, HUUFANYA  UUME  KUSINYAA  NA  KULEGEA )

Mtu  anayepiga  punyeto  husababisha  mambo  yafuatayo  katika  mwili  wake :

1. Huuwa  nguvu  ya  mishipa  & misuli ya  uume ambayo  ndio  inayo husika  na  kusimama  kwa  uume

2. Mishipa  ya   uume  inapo  sinyaa  na  kukosa  nguvu  yake  ya  asili, husababisha  mambo  yafuatayo :

i.Huondoa  uwezo  wa  mishipa  &  misuli  ya  uume  kutanuka, na  hii  ndio  sababu  inayo  wafanya  waathirika  wa  punyeto  kutumia  nguvu  nyingi  sana  katika  kuufanya  uume  usimame.

ii.Huondoa  uwezo  wa  mishipa &  misuli  ya  uume  kuibana  na  kuiziba  mishipa  ya  vena, na  hii ndio  sababu  inayo  fanya  waathirika  wa  punyeto  kufika  kileleni  haraka  sana, kwani damu  inayo  ingia  kwenye misuli  ya  uume   hufyonzwa  ndani ya  muda  mfupi sana. 
 
 Hii  hutokea  kwa  sababu  mishipa na  misuli  ya  uume inakuwa  imelegea,na  mishipa  ya  vena inakuwa  imepwaya, hivyo  msuguano wowote ule  hufanya  mishipa  ya  vena  kufunguka  na  kufyonza  damu  kutoka  kwenye mishipa  ya  uume  na hivyo  kuufanya  uume  kusinyaa  ndani ya dakika ama sekunde  chache sana.

3. Vile  vile  punyeto  hufanya  uume  kusinyaa na  kurudi ndani  na  kuufanya  uonekane kama  uume  wa  motto mdogo.

Kwa  ufupi  punyeto  husababisha  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  sababu  kuu  zifuatazo :

i.Kwanza   hudhoofisha  na  kuharibu  mishipa  ya  uume,  ambayo  ndio  hufanya  uume kusimama.

ii.Pili  hudhoofisha  utendaji  kazi  wa  mishipa  ya  ateri, ambayo  ndio  hutumika  kama  njia  ya  kusafirisha  damu kupeleka kwenye  misuli  ya  uume  na  ivyo  kuufanya  uume  usimame

iii. Tatu, punyeto  hupelekea  kuvuja  kwa  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kusababisha  damu  kufyonzwa  kwa  haraka  sana  kila  iingiapo ndani  ya  misuli ya  uume  na  matokeo  yake  ni  uume   kusimama  kwa  muda  mfupi  sana  wakati wa  tendo  la  ndoa.

iv. Punyeto  huathiri  mtiririko  wa  damu  kwenda  kwenye  mishipa  ya  uume, kwa  sababu  hudhoofisha  misuli &  mishipa  ya  uume  pamoja  na mishipa ya  ateri  ambayo  ndio  hutumika  katika  kusafirisha  damu kwenda  kwenye  uume

DALILI  ZA  MTU  ALIYE  ATHIRIWA  NA  PUNYETO
Dalili  kuu  za  mtu  aliye athiriwa  na  punyeto  ni  kama  ifuatavyo:

i.           Uume  kusinyaa  na  kuwa  kama  wa  mtoto
ii.         Uume kurudi  ndani
iii.       Uume  kusimama  ukiwa  legelege
iv.       Kufika  kileleni  haraka  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

TIBA   YA   NGUVU  ZA  KIUME  KWA MTU  ALIYE  ATHIRIKA  NA  PUNYETO.
Dawa   asilia  ya  nguvu  za  kiume iitwayo JIKO  ni tiba  bora  na  ya  uhakika  kabisa  kwa  mtu  aliye  athiriwa   na  punyeto.  Dawa  hii, pamoja  na  mambo  mengine  mengi, husaidia  kufanya  mambio  yafuatayo  katika  mwili  wa  mwanaume  aliye  athiriwa  na  punyeto :

i.Kuimarisha  mishipa  & misuli  ya  uume  ulio  legea na  hivyo  kuurejeshea  uwezo wake wa  asili

ii. Hutibu   tatizo  la  uume  kurudi  ndani

iii.Humaliza  tatizo  la  kusimama  kwa  uume  ukiwa  legelege

iv.Hutibu  na  kuponya  kabisa  tatizo  la  kufika  kieleleni  haraka.

BEI  YA  DAWA  :  Dawa  hii  inapatikana  kwa  gharama  ya  SHILINGI  ELFU  THEMANINI  TU (Tsh. 80,000/=)

MAHALI  INAPOPATIKANA :  Dawa  hii  inapatikana  katika  duka  la  dawa  asilia  liitwalo  NEEMA  HERBALIST  &  NUTRITIONAL  FOODS  CLINIC  lililopo  jijini  DAR  ES  SALAAM  katika  eneo  la  UBUNGO   nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA   karibu  na SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING.

Kwa  wateja  wasio  weza  kufika  ofisini  kwetu. Watafikishiwa  dawa  mahali  popote  walipo  jijini  DAR  ES  SALAAM.

Kwa   wateja  waliopo  mikoani  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  MABASI

Kwa  wateja  waliopo   Zanzibar  wata fikishiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa boti.

Na  kwa  wateja  waliopo  UGHAIBUNI  watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  ama  DHL.

MAWASILIANO :  WASILIANA  NASI   KWA  SIMU  NAMBA  0766  53  83  84.

Kwa  taarifa  zaidi  kuhusu  huduma  zetu, tutembelee kila  siku  kwenye  blogu  yetu :

Nape Amtembelea Na Kumjulia Hali Mkuu Wa Mkoa Wa Tanga.

$
0
0
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akimjulia hali Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Martin Shigela aliyelazwa katika wodi ya Sewahaji Hospitali ya Muhimbili Jijini Dar es Salaam.

Kwa taarifa zilizopo hali ya Mhe. Shigela inaendelea vizuri.

Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini WHUSM

Makamu wa Rais Asema Serikali Itaendelea Kushirikiana na Wadau Mbalimbali Kuhakikisha Rasilimali ya Gesi Inakuza Uchumi wa Taifa

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amesema kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali katika kuhakikisha rasilimali ya gesi na mafuta inakuwa ni chachu ya kukuza uchumi wa taifa na wa wananchi kwa ujumla.
 
Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan amesema hayo jana 22-Nov-2016 Jijini Dar es Salaam wakati akifungua mkutano wa mwaka wa kujadili masuala ya gesi na mafuta barani Afrika ulioandaliwa na Kampuni ya Getenergy ya Uingereza.
 
Katika hotuba yake, Makamu wa Rais aliwahakikishia washiriki wa mkutano huo kuwa Tanzania imeweka mazingira mazuri ya uwekezaji kwenye sekta ya mafuta na gesi na itakuwa bega kwa bega na wadau wanaotaka kuwekeza katika sekta hiyo ili kuhakikisha uwekezaji utakaofanyika unakuwa na manufaa kwa pande zote mbili.
 
Alisisitiza kuwa kwa sasa Serikali ya Tanzania inaendelea na mkakati  kabambe wa kusomesha wataalamu wa fani ya mafuta na gesi ndani na nje ya nchi ili kuhakikisha taifa linajitosheleza kwa wataalamu hao ambao watakuwa na uwezo na ujuzi wa kufanya kazi kwa viwango vinavyotakiwa katika sekta za gesi na mafuta.
 
Makamu wa Rais alisema Tanzania imegundua kiasi kikubwa na gesi na ana imani kubwa kuwa mafuta nayo yanapatikana hivyo ni muhimu kwa mataifa ya Afrika  kujipanga kuwa na wataalamu wake wazalendo wa kutosha watakaoshikiri katika uchumi wa gesi na mafuta kwa kuajiriwa kwenye makampuni yanajihusisha na utafiti na
uchimbaji wa gesi na mafuta.
 
Asema anaimani kubwa kuwa rasilimali ya gesi na mafuta zitakazogundulika na kuchimbwa barani Afrika zitasaidia kwa kiasi kikubwa ukuaji wa uchumi wa mataifa hayo, uchumi ambao utasaidia  kuimarisha utoaji wa huduma bora za kijamii kwa wananchi katika nchi husika.
 
Mkutano huo wa siku Mbili wa Kimataifa umekutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya gesi na mafuta kutoka ndani na nje ya nchi ambao wanajadili kwa kina na kubadilishana uzoefu kuhusu njia bora za uwekezaji katika sekta hiyo barani Afrika.
 
Kwa upande wake,Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo alisisitiza kwa Serikali itaendelea kusomesha wataalamu wake ndani na nje ya nchi ili kujitosheleza kwa wataalamu wa sekta hiyo.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatano ya Novemba 23

RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 93 & 94(Riwaya inawafaa kuanzia miaka 18 na kuendelea )

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA

ILIPOISHIA
Taratibu Phidaya akasimama, akanisogelea huku machozi yakimwagika. Nikataka kumkumbatia, ila akanizuia, nisifanye hivyo.
"Phida.."
Kofi zito kutoka kwa Phidaya likatua shavuni mwangu, lililo mfanya Shamsa kustuka. Phidaya akaachia msunyo mkali na kumshika mkono Jack.
"Junio tuondoke"
Phidaya alizumgumza kwa hasira, na kuanza kuondoka na mwanaye, wakijichanganya katikati ya watu walio kusanyika hapa.

ENDELEA
   Sikuhofia kukatiza katikati ya watu, kuwafwata Phidaya na mwanagu Junio. Furaha moyoni nwangu ikawa imezaliwa upya kuiona familia yangu. Iliyo nigharimu maisha yangu katika kuitafuta hadi leo kuitia machoni kwa mara ya pili, ukiachilia siku ya kwanza Junio alivyo zaliwa mbele ya macho ya watu wengi akiwemo Shatani John na Victoria.
"Phidaya, Phidaya"
Nilimuita Phidaya niliye mkaribia, kumfiki. Akasimama na kunitazama kwa macho makali sana, yaliyo jaa hasira huku machozi yakimwagika taratibu.
"Unakwenda wapi mke wangu, kumbuka nimehangaika kwa ajili yako, nimejitolea maisha yangu kwa ajili yako na mwanangu. Kwa nini unanikasiriki, kosa langu ni nini haswa?"
Nilizungu huku machozi yakianza kunitiririka.
"Nimekua muuaji kwa ajili yako, nimefanya kila niwezalo kufanya kwa ajili yako, ila umaona yote hayana dhamani si ndio?"

"Eddy nyamaza. Nilikuomba usioe, ila kwa nini ulioa. Umeniacha nahangaika, naishi maisha ya kitumwa na mwanangu. Tumekua watu wa kubadilisha majina kwa ajili yako. T...."
"Phidaya mimi sijaoa mwanamke yoyote, nilijitoa kufa na kupona kuwakomboa nyinyi mukiwa kwenye maroli kwenda kuuzwa nchi za nje. Nimefanya kosa?"
"Eddy acha uongo, haukuwa wewe, uliye tuokoa, Umemuoa mwanamke aliye nidhalilisha na kuniita mimi malaya, mimi?"
"Phidaya, achana na hayo maneno. Njoo tukamlee Junio. Twende tukaishi kwa amani na upendo. Unatambua ni mazingira gani ulimzaa Junio, huku na mimi nikiwa kwenye tabu gani."
"Junio sio mwanao, ni mwanangu peke yangu. Junio twende zetu"
Phidaya alizungumza huku akimshika mkono Junio, na kumvuta waondoke ila Junio akagoma kwenda popote.

"Mama uliniambia mtu, akiniuliza baba yangu ni nani, nimuambie simjui. Ila Eddy ni baba yangu, mara ngapi ulikua ukimpigis simu. Anamapenzi ya dhati na sisi. Mama nimechoka kuishi maisha haya ya ukimbizi. Mpe baba nafadi yake, aonyeshe ni jinsi gani anavyo tupenda."
Japo Junio kiumri ni mdogo, ila maneno aliyo yazungumza huku akilia yakanifanya mwili wangu kusisimka. Phidaya akamtizama Junio kwa macho ya mshangao, kisha akanitazama na mimi.
Nikafungua vifungo vya shati langu, nikakivua na kumpa Shamsa anishikie.
"Majeraha yote haya, nikwaajili ya kuiokoa familia yangu. Mwili wangu haukua na dhamani juu ya kuziokoa nafsi zenu. Msikilize anacho sema mwanao. Anahitaji malezi yetu sote. Tafadhali mke wangu, rudi mikononi mwangu au unataka mwanangu aendelee kuishi maisha haya ya shida. Tazama jinsi sura yake ilivyo umuka kwa kupigemwa na wezake. Je unataka awe hivi kila siku?"

Nilizungumza kwa uchungu, huku nikipiga magoti chini, sikujali ni idadi ngapi ya wagu walio tuzunguka wakitushangaa. Junio akamshika mkono mama yake.
"Mama, unanifundisha niwe mpatanishaji kwa walio gombana. Mshike baba mkono anakupenda"
Phidaya aliendelea kulia kwa uchungu, sura yake yote ikabadilika na kuwa na uwekundu fulani, kutokana na kulia kwa uchungu sana.
"Nakuomba mama, patana na baba anakuhitaji bado"
Maneno ya Junio yakamlainisha Phidaya. Taratibu Phidaya akarudi sehemu niliyo piga magoti, na yeye akapiga magoti chini, huku akilia. Kwa nguvu akanikumbatia. Nikamvuta Junio wangu, naye nikamkumbatia huku sote machozi ya furaha yakitumwagika. Watu walio tuzunguka wakaanza kupiga makofi, yafuraha. Shamsa akabaki akinikonyeza huku akitabasamu.
"Nakupenda mume wangu"
"Nawapenda wote"
Tukaendelea kukumbatiana kwa furaha.
"Eddy muda"

Shamsa alininong'oneza baada ya kuona tunakumbatiana sana. Tukanyanyuka, nikambeba Junio wangu ambaye kwa sasa anatarajia kufikisha umri wa miaka mitano.
"Nitakufanyia sherehe kubwa siku ya kuzaliwa kwako"
Nilimuambua Junio, huku tukielekea kwenye ofisi kukamilisha taratibu zote za kuwachukua Phidaya na mwanangu, na kuwa mikononi mwangu.
"Kweli baba"
"Ndio unataka ifanyikie wapi?"
"Mama kule kwa kina yule mchezaji uliye ninunulia mpira wenye jina lake ni wapi?"
"Brazil"
"Ndio, dady nataka huko huko na mimi nikawe mchezaji mpira"
"Usijali mwanangu, unaweza kucheza mpira?"
"Ndio baba nataka niwe kama Ronaldo"
"Sawa mwanangu utakuwa, tena kabla sijasahau, huyu ni Shamsa, mdogo wangu. Kwa sasa atakuwa dada yake Junio"
"Kweli dady?"
"Yeah"
Nikambusu Junio kwenye paji la uso, jambo lililo zidisha furaha kati yetu sote wanne.

               ***
   Kitendo cha ndege kutua kwenye uwanja wa ndege nchini Brazil, likawa ni jambo la kumshukuru Mungu, sote tukafungua mikanda ya siti zetu tulizo kalia, ikiashiria kwamba safari yetu immefika mwisho. Tukatoa mabegi yetu ya nguo, katika sehemu tulipo yaweka. Tukatoka ndani ya ndege kama abiria wengine. Tukafika eneo la kukaguliwa, tukafanikiwa kupita pasipo kusumbuliwa, juu ya hati zetu za kusafiria. Tulizo zikata nchini Kenya tukisaidiwa na rafiki wa Smith, aliye tukutanisha naye kipindi tunatoka Tanzania mimi na Manka, ambaye hadi sasa sijui yupo wapi.

   Kwa msaada wa ramani tuliyo pewa na rafiki wa Smith, juu ya miji yote mikuu nchini Brazili, ikatusaidia kutufikisha kwenye hoteli tuliyo kusudua kufikia tangu tukiwa nchini Kenya. Hoteli hii inapatikana pembezoni mwa fukwe za bahari zijulikanazo kwa jina la 'Copar Carban'.x
Sehemu tuliyo chukua kwa ajili ya makazi ya wiki mbili, ina vyumba vitatu, seble, kubwa pamoja na xjiko kubwa. Kila chumba kimejimudu kwa huduma zote muhimu kama choo na bafu.
"Eddy hapa umelipia bei gani?"
Phidaya alizungumza huku akikagua kagua chumba chetu cha kulala, chenye hadhi ya nyota tano.
"Kwa siku ni dola elfu sabini"
"Mmmmm kwa chumba hiki au?"
"Kwa sehemu yote, hii"
"Kweli una pesa ya kuchezea, hii ni birthday ya mwanao mambo ni haya, Je siku ya ndoa yetu itakuaje"
"Ndio ujiulize sasa, nataka kuihakikishia dunia nzima kwamba ninakupenda mke wangu"
Phidaya akanikimbilia, nilipo simama. Akanirukia na kuning'inia kifuani kwangu. Huku miguu yake akiipitisha kiunoni mwangu na kuikutanisha nyuma.

"Wewe ni mwanaume jasiri, i wish wanaume wote wangekua kama wewe. Ninaamini furaha ingepatikana katika ndoa nyingi."
"Ni wachache wenye moyo kama wangu. Ila kikubwa nimekupata wewe na mwanangu, ninaamini furaha itarudi upya"
Phidaya hakusita kuusogeza mdomo wake, karibu na mdomo wangu. Akanitazama kwa muda, kisha kwa haraka akaanza kuunyonya mdomo wangu. Kutokana na nguvu nilizo nazo, sikuweza kutetereka, kwani fujo anazo zifanya Phidaya mdomoni mwangu, huku nikiwa nimembeba, mtu unaweza kuanguka chini.

  Nikamlaza kitandani, huku akiendelea kuninyonya lipsi zangu, mikono yangu nikaishusha kifuani mwake, na kuanza kuzichezea chuchu zake. Kwa raha anazo zipata Phidaya, akajikuta akifumba macho yake. Nikazidi kuutadhimini uzuri wa Phidaya. Hapa ndipo nilipo jilaumu, kwa nini nilikua na magubegube, Sheila na Madam Mery. Kwa kupitia kioo kikubwa, kilichopo kwenye kitanda chetu. Nikamuona Junio akiwa amesimama mlangoni huku akiwa ameshika mpira alio nunuliwa na mama yake. Mdomo wake akiwa ameulegeza akishangaa tunacho kifanya.

 Nikamuona naye Shamsa, akisimama nyuma ya Junio, wote walikua na safari ya kuingia chumbani kwetu. Shamsa akamfumba macho Junio, aliyeganda akishangaa kama mshumaa wa pasaka. Shamsa akamyanyua Junio taratibu huku akiwa amemfumba macho. Akanikonyeza, na mimi nikamuonyesha ishara ya dole gumba kwa kutumia mkono wa kulia huku mkono wa kushoto akiendelea kuchezea chuchu za Phidaya. Shamsa akatabasamu, taratibu akaurudishia mlango wetu, huku mkono alio mziba macho Junio akiutumia kuufungia mlango, na kumpa fursa Junio kushangaa vya mwisho mwisho.
"Eddy ni nini hicho?"
Phidaya aliniuliza huku akiyafumbua macho, yake kutazama kila kona ya chumba.
"Kitu gani?"
"Kilicho gusa mlango"
"Hakuna kitu bby"
Phidaya akapotezea, na kuendelea na zoezi la kuunyonya mdomo wangu. Huku kila ma}ra akihakikisha ananigusa kila kona ya mwili wangu. Tukavuana nguo tulizo zuvaa, na kubaki kama tulivyo zaliwa.

Jeshi La Polisi Laanza Uchunguzi Dhidi ya Mteja wa NMB Alivyofuatiliwa baada Ya Kutoka Benk na Kuporwa Milioni 15

$
0
0

Jeshi la Polisi linafanya uchunguzi namna mtu mmoja alivyofuatiliwa na watu wasiojulikana alipotoka benki kuchukua fedha hadi wakampora mfuko uliokuwa na kiasi cha Sh15 milioni muda mfupi baada ya kufika nyumbani kwake. 

Naibu Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Ilala, Ernest Matiku alisema wana taarifa za tukio la wizi huo uliofanyika Ijumaa iliyopita baada ya mteja huyo  kutoka Benki ya NMB Tabata na wanalifanyia kazi kubaini wahalifu hao. 

Tukio hilo ni moja ya matukio ambayo katika siku za karibuni watu mbalimbali wamekuwa wakiporwa fedha na watu wenye silaha, ikiwa ni muda mfupi baada ya kutoka benki, hali ambayo inajenga wasiwasi juu ya sehemu ambazo majambazi hao hupata taarifa za watu wanaokwenda benki kuchukua fedha. 

Hofu miongoni mwa wateja imezidi kutokana na tukio lililotokea Ijumaa ya wiki iliyopita ambapo majambazi wakiwa na pikipiki mbili walimfuatilia mteja aliyetoka kuchukua fedha benki kiasi cha Sh15 milioni na kumpora mbele ya nyumba yake. 

Akisimulia tukio hilo mwathiri- ka wa wizi huo, alisema alichukua fedha kwenye tawi la NMB Tabata kisha akapanda daladala akaenda kushuka kituo cha Tabata Bima. 

Alisema alipokuwa anaelekea nyumbani kwake hakuwa na shaka, lakini alipokaribia alihisi kuna mtu anamfuata ingawa hakumuona, hivyo aliingia kwenye baa iliyokuwa njiani na kutokea upande wa pili kwa kutumia uchochoro uliokuwapo. 

Alisema baada ya kutokea upande wa pili aliangaza kushoto na kulia hakuona mtu kisha aliamua kuongoza hadi nyumbani kwake. 

“Nilipofika hapo nje kwenye mwembe (umbali wa mita tatu kuingia ndani ya nyumba yake), nikakuta watu wanne wakiwa na pikipiki mbili wamesimama mbele yangu,” alisimulia akiwa nyumbani kwake muda mfupi baada ya kuruhusiwa Hospitali ya Muhimbili alikokuwa anapatiwa matibabu. 

“Wakanitaka niwape fedha ambazo zilikuwa kwenye mfuko nimezishika mkononi. Kabla sijakaa vizuri wakapiga risasi hewani, kutahamaki wakanipiga juu ya goti la mguu wa kulia ikaniparaza, lakini nilikuwa bado nimeng’ang’ania ule mfuko wenye fedha,” alisema. 

Aliendelea kueleza kuwa baada ya kuona hana mpango wa kutoa fedha, wakampiga risasi mguu huo huo chini ya goti ikapasua mfupa mkubwa na kutokea upande wa pili na kumnyang’anya mfuko wa fedha. 

“Hakuna mtu aliyekuwa anafahamu suala hilo zaidi ya mimi mwenyewe,” alisema huku akiugulia maumivu.

Mwathirika wa UKIMWI Aliyewanajisi Watoto 100 Ahukumiwa Kifungo cha Miaka Miwil

$
0
0
Siku chache baada ya kuripotiwa taarifa za kukamatwa kwa mwanaume mmoja kutoka Malawi ambaye inadaiwa alikuwa akiwanajisi watoto wadogo wanaotajwa kufika 100 kwa maelezo kwamba anawasafisha na kufanya tambiko la kimila, Hatimaye amehukumiwa kwenda jela miaka miwili.

Hukumu hiyo imeonesha kutotenda haki kwa watoto hao kutokana na uchache wa miaka aliyofungwa mwanaume huyo. Tayari mashirika ya kutetea haki za binadamu na asasi za kupambana na maambukizi ya virusi vya HIV nchini Malawi zimekosoa hukumu hiyo

Michael Chipeta, wakili na mwanaharakati wa kutetea haki za binadamu nchini humo amekosoa hukumu hiyo na kusema kuwa kulikuwa na mapungufu mengi katika mchakato mzima wa kesi na hukumu dhidi ya mwathirika huyo wa virusi vya HIV, anayejulikana kama Eric Aniva mwenye umri wa miaka 45.

Eric Aniva alikiri kwamba amefanya ngono na wasichana wadogo kwa kulipwa fedha ambazo ni dola nne mpaka saba za Marekani kwa kuondoa usichana wa (kubikiri) kila mtoto mmoja, kwa imani kuwa ubikira ni mkosi na kwamba kitendo hicho kinawasafisha watoto hao pamoja na jamii hiyo.

Malawi ni katika nchi zenye maambukizi makubwa ya virusi vya Ukimwi duniani.

Rais Magufuli afanya mazungumzo na Rais Mstaafu Mwinyi

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe 23 Novemba, 2016 amekutana na kufanya Mazungumzo na Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Alhaji Dkt. Ali Hassan Mwinyi, Ikulu Jijini Dar es Salaam.


Baada ya mazungumzo hayo, Alhaji Dkt. Ali Hassan Mwinyi amesema lengo la kukutana na Rais Magufuli na kufanya nae mazungumzo kwa mara ya kwanza ni kumpongeza kwa kutimiza mwaka mmoja tangu aingie madarakani na pia kumpongeza kwa kazi kubwa aliyoifanya katika kipindi kifupi cha uongozi wake.

Alhaji Dkt. Ali Hassan Mwinyi ameyataja baadhi ya maeneo ambayo Rais Magufuli ameyafanya kwa mafanikio makubwa kuwa ni mapambano dhidi ya rushwa na amebainisha kuwa hatua zilizochukuliwa katika kipindi cha mwaka mmoja zimedhihirisha kasi kubwa ya kukabiliana na tatizo hilo ikilinganishwa na wakati uliopita.

“Rushwa ilikuwepo tangu enzi ya Hayati Mwalimu Nyerere, aliipondaponda kabisa lakini hakuimaliza, na sote tuliosalia ni hivyo hivyo, kila mmoja amefanya kwa kiasi chake, lakini Rais Magufuli kwa mwaka mmoja ameleta Sunami, nafurahi sana” amesema Alhaji Mwinyi.

Eneo jingine ni kuimarisha utendaji kazi Serikalini ambapo Alhaji Dkt. Ali Hassan Mwinyi amesema hatua zilizochukuliwa na Serikali ya Rais Magufuli zimeongeza kasi zaidi na ametoa wito kwa Viongozi na Wananchi kuunga mkono juhudi hizo.

“Tuliobaki tumsaidie, tumsaidie kwa kumuombea Dua, tumsaidie kurekebisha kwa kusema ukweli pale ambapo watu wanapotosha, tuseme sio hivyo, ilivyo ni kadhaa kadhaa kadhaa, tusiwaache watu wakapata nafasi ya kuongea uongo, kila mtu anaweza kuwa anasema kutokana na nia yake na lengo lake, lakini hakuna asiyejua kuwa kazi aliyoifanya mwenzetu ni nzuri nzuri nzuri ya ajabu” amesisitiza Rais Mstaafu Mwinyi.

Wakati huo huo, Rais Magufuli amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Vangimembe Lukuvi, Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

23 Novemba, 2016

Bodi ya Mikopo yawaponza wanafunzi 1,132 wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (Saut) cha Mwanza

$
0
0
Wanafunzi 1,132 wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (Saut), cha Mwanza hawatapewa matokeo yao ya kuhitimu shahada wala kushiriki katika mahafali baada ya Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) kutolipa ada zao za mwaka huu wa masomo.

Kwa mujibu wa orodha ya wanafunzi iliyobandikwa katika ubao wa matangazo chuoni hapo, ni wanafunzi 933 tu watakaoshiriki katika mahafali yaliyopangwa kufanyika Desemba 16 na 17. 

Tangazo hilo lililosainiwa na Makamu wa Mkuu wa Chuo (Taaluma), Dk Negussie Andre limewataka wanafunzi kuhakiki majina yao kwenye orodha na kuwasilisha malalamiko au hoja zao kabla au ifikapo Jumapili ijayo.

Kuhusu madai hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, Abdul Razaq Badru alisema hawezi kuyazungumzia kwa sababu kila chuo kina mamlaka yake.

Alisema Bodi hiyo ipo kwa miaka 10 na kwamba bila shaka kuna taasisi zinazoidai na zinalipwa kulingana na makubaliano na mipango iliyopo akisema kila wakati kuna malipo yanayoendelea katika vyuo mbalimbali.

Hata hivyo, alisema hana takwimu sahihi kama na chuo hicho kimeanza kulipwa. 

“Tunafanya malipo kulingana na mipango iliyopo, kama kuna changamoto katika vyuo tunavyolipa au vinavyotudai huwa tunajadili kwa pamoja na kupata majibu, kwa hilo lililotokea Saut sisi kama Serikali hatuwezi kukemea wala kupongeza kwa sababu ni mamlaka ya chuo,” alisema Badru.

Akizungumza kwa simu jana jioni, Ofisa Mikopo wa Saut, Wilfred Medard alisema uamuzi huo umechukuliwa kutokana na malimbikizo ya ada ya wanafunzi wanaolipiwa na bodi hiyo.

“Siwezi kutaja ghafla ni kiasi gani tunachodai, lakini kwa hakika ni zaidi ya Sh500 milioni,” alisema Medard.

Alisema si rahisi kujua iwapo wanafunzi hao wote watashiriki mahafali kwa sababu bado kuna fursa ya bodi kulipa madeni hayo na kuwapa nafasi ya kushiriki mahafali na wenzao wanaojilipia au wanaolipiwa na kampuni, taasisi na mashirika mbalimbali.

Ingawa tangazo hilo limetoa hadi Jumapili ijayo kwa wahitimu ambao majina yao hayapo kwenye orodha kuhakiki na kuwasilisha taarifa zao, Medard alisema bado kuna fursa ya wahusika kukamilisha taratibu hadi Desemba 2 ambayo ni siku ya mwisho ya maandalizi ya mahafali.

Rais wa Serikali ya Wanafunzi Saut (Sautso), Emmanuel Ayo alisema wanafunzi wanaunga mkono uamuzi wa chuo kuishinikiza Serikali kulipa madeni hayo ili kukiwezesha kujiendesha.

“Hiki ni chuo binafsi kinachojiendesha kupitia ada za wanafunzi. Kutolipa ada ni kukwamisha shughuli na masomo na sisi hatuko tayari kuona tunakosa masomo kwa sababu tu Serikali haitimizi wajibu wake wa kuwalipia wanafunzi inaowadhamini,” alisema Ayo.

Alisema iwapo muda uliotolewa na chuo kuhakiki utapita bila ya kulipwa kwa ada hizo, Sautso imepanga kuonana na Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako kuwasilisha kilio chao.

“Waziri asipotusaidia, tutakwenda hadi Ikulu kumwona Rais John Magufuli ambaye pengine wasaidizi wake hawampi taarifa sahihi kuhusu kinachoendelea Bodi ya Mikopo,” alisema Ayo.

Kiongozi huyo ambaye ni mwanafunzi wa mwaka wa tatu wa shahada ya ualimu, alijitolea mfano kuwa ada yake ya muhula wa pili mwaka jana haijalipwa hadi sasa na bodi hiyo.

Prof. Mbarawa Kumuwakilisha Rais Magufuli Mkutano Wa Usafirishaji Duniani

$
0
0
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa atamuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika mkutano wa kimataifa wa Usafirishaji Duniani utakaofanyika katika mji wa Ashgabat nchini Turkemistan kuanzia tarehe 26-27 Novemba, 2016.

Ajenda kuu ya mkutano huo ulioitishwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ambao utashirikisha viongozi mbalimbali utajadili kwa kina maeneo muhimu ya ushirikiano wa kimataifa kwenye Sekta ya Usafirishaji kwa maendeleo endelevu Duniani.

Aidha katika mkutano huo Waziri Prof. Mbarawa atapata fursa ya kukutana na wawekezaji mbalimbali Duniani waliobobea katika sekta ya usafirishaji na kuwashawishi kuwekeza hapa nchini.

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

Serikali yafunguka kuhusu fao la kujitoa

$
0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi Ajira na Vijana) Bibi Jenista Mhagama amesema serikali itakaa na wadau ili kuangalia namna ya kulimaliza sakata la fao la kujitoa katika mifuko ya hifadhi ya jamii.

Waziri Mhagama ametoa kauli hiyo jana  katika mkutano wa sita wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) mjini Dodoma uliofunguliwa leo na Waziri Mkuu Mjini Dodoma, ambapo katika risala yake, TUCTA ilihoji kuhusu  marekebisho ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii na ucheleweshwaji wa malipo ya pensheni.

Mhagama alisema kuwa baada ya uongozi wa TUCTA kukamilika, itabidi wakutane na kukaa pamoja kuainisha sera inataka nini na hali ya uchumi ya sasa ikoje huku wakiangalia dhana nzima ya hifadhi ya jamii nayo inataka nini.

“Kuna haja ya kuangalia sera inataka nini, tunapaswa tuangalie mabadiliko ya kiuchumi katika nchi yetu na kutazama dhana nzima ya hifadhi ya jamii kwenye maisha yetu ya uzeeni. Tukikaa pamoja, yaani, mwajiri, mfanyakazi na Serikali, tutapata njia ya kisheria ya kuweza kulifunga jambo hili ili lisiendelee kuwa kero kwa wafanyakazi wetu,” alisema.

Msikilize hapa waziri Mhagama akifunguka.

Siku ya Maulid kuadhimishwa kwa usafi, kupanda miti na kuchangia damu

$
0
0
Waislamu wote nchini wametakiwa kuadhimisha Siku ya Maulid kwa kufanya usafi, kupanda miti na kuchangia damu.

Aidha, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika Siku ya Maulid ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (S.A.W).

Hata hivyo, ugeni rasmi wa Waziri Mkuu Majaliwa unategemea ratiba yake.

Hayo yalisemwa jana Dar es Salaam na Mufti wa Tanzania, Shehe Abubakar Zubeir wakati akizungumzia Siku ya Maulid ambayo alisema kwa mwaka huu, Maulid itasomwa usiku wa Desemba 11, na kitaifa itafanyika Kata ya Shelui wilayani Iramba Mkoa wa Singida na mapumziko yatakuwa siku inayofuata yaani Desemba 12.

Mufti Zubeir alisema Waislamu wanatakiwa kutumia siku hiyo kuonesha matendo mema na yenye kumpendeza Mwenyezi Mungu pamoja na kuisaidia jamii kufanya usafi kwenye mitaa yao na kuchangia damu ili kusaidia wenye uhitaji huo.

Alisema anatakiwa kiongozi kufanya matendo hayo wanapoifurahia siku ya kuzaliwa Mtume Muhammad (S.A.W) ambaye amesema uislamu ni usafi, basi jisafisheni wenyewe.

“Mimi na familia yangu tutafurahia siku hiyo kwa kufanya usafi mtaani kwetu Mikocheni na kuchangia utoaji damu ili kusaidia watu wenye uhitaji,” alieleza Mufti Zubeir na kuwataka Waislamu kutokujiingiza kwenye makundi ya ugaidi kwani Uislamu sio ugaidi na kuwasihi waachane na hizo tabia.

Tanzania yapiga hatua katika kulinda na kutetea haki za binadamu, Makamu wa Rais afunguka Arusha.

$
0
0
Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan, amesema, Serikali ya Tanzania imepiga hatua kubwa katika kulinda na kutetea haki za binadamu kwa kuzingatia maazimio mbalimbali ya ndani ya nchi na ya kimataifa ikiwemo haki ya kuishi.

Mh. Samia ametoa kauli hiyo jana jijini Arusha kwa niaba ya Rais Dk John Pombe Magufuli wakati anafungua mkutano wa mazungumzo wa masuala ya demokrasia na haki za binadamu ya Mahakama ya Afrika ya Watu na Haki za binadamu.

Alisema Tanzania ni mfano wa kuigwa barani Afrika kwa kuzingatia na kutekeleza ipasavyo mikataba mbalimbali ya kimataifa inayolenga kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma bora na za msingi ikiwemo huduma ya afya na elimu bila kubaguliwa kutokana na ulemavu,jinsia,rangi au dini.

Alisisitiza kuwa Serikali itaendelea kutekeleza na kuzingatia matamko mbalimbali ya Dunia yanayolenga kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za kijamii ikiwemo haki ya kuishi.

Kwa upande wake, Rais wa Mahakama ya Afrika ya Watu na Haki za Binadamu Justice Sylvain Ore alisema kuwa mkutano huo ni muhimu kwani unalenga kujadili na kuweka mikakati inayolenga kuhakikisha nchi za Afrika zinazingatia na kulinda haki za bindamu hasa haki za wanawake kwa kiwango kikubwa.

Mkutano huo wa Mahakama ya Afrika ya Watu na Haki za Binadamu ambao unafanyika Jijini Arusha umehudhuriwa na wajumbe kutoka mataifa mbalimbali ya Afrika wakiwemo wajumbe kutoka Umoja wa Afrika AU na lengo la mkutano huo ni kutajadili masuala ya demokrasia na haki za binadamu katika nchi za Afrika.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya Novemba 24


RC Makonda apiga marufuku wauza mbogamboga na samaki

$
0
0
Mkuu  wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, amepiga marufuku wauzaji holela wa samaki na mboga mitaani badala yake wapeleke katika masoko maalumu.

Aidha ameliagiza jeshi la polisi na halmashauri zote mkoani humu kuwakamata wafanyabiashara watakaokiuka agizo hilo.

Makonda alitoa kauli hiyo jana, wakati alipotembelea Soko la Kimataifa la Samaki la Feri na kuzungumza na wafanyabiashara wa soko hilo, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku mbili katika Wilaya ya Ilala.

Wafanyabiashara hao walieleza kuwa, moja ya changamoto zinazowakabili ni pamoja na kuzagaa kwa wafanyabiashara huria wa samaki hususani katika vituo vya mabasi ya daladala na pembezoni mwa barabara mkoani humo.

Walidai kuwa, hali hiyo inahatarisha uhai wa soko hilo kwani watu wengi hawafiki kununua samaki katika soko hilo, badala yake huishia kununua katika vituo vya mabasi na mitaani.

Mfanyabiashara Said Ally alimueleza mkuu huyo wa mkoa kuwa, masoko huria ya mitaani yanaendelea kushamiri huku viongozi wa halmashauri na wananchi wakikaa kimya.

“Mkuu wa mkoa tusaidie sasa hivi kila kona kuna wauza samaki hasa katika vituo vya mabasi jambo linalosababisha feri tunakosa wateja wanaishia mtaani, soko litakufa kwa sababu watu hawaji tena tofauti na awali,” alisema Ngasa.

Mbali na hayo wafanyabiashara hao waliomba kuboreshwa kwa miundombinu ya soko hilo ambayo imechakaa licha ya soko kuwa la kimtaifa.

Kutokana na malalamiko hayo, Makonda alipiga marufuku biashara ya samaki na mboga mitaani na kumuagiza Kamanda wa Operesheni, Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lucas Mkondya kuwashughulikia wafanyabiashara wote watakao kiuka agizo hilo kuanzia sasa.

“Ni marufuku kufanya biashara ya samaki na mboga katika maeneo ambayo sio rasmi wafanyabiashara wapeleke katika maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya kufanyia biashara hizo,” alisema Makonda.

Mikoa Mitano inayoongoza kwa Ndoa za utotoni Tanzania

$
0
0
Tanzania imetajwa kuwa ni moja kati ya nchi zenye viwango vya juu vya matukio ya ndoa za utotoni. Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) katika utafiti uliochapishwa mnamo Januari, 2016 uliitaja kuwa ni nchi ya tatu barani Afrika kwa matukio ya ndoa na mimba za utotoni kwa 28%.

Kutokana na shirika la Idadi ya Watu Duniani (UNFPA), kwa wastani watoto wakike wawili kati ya watano huolewa kabla ya kufikisha umri wa miaka 18. Pia takwimu za utafiti wa Idadi ya watu na Afya Tanzania (TDHS, 2010) 37% ya watoto wa kike Tanzania huolewa kabla ya kufikisha miaka 18.

Takwimu za shirika la Watoto Duniani (UNICEF 2012) lilitaja mikoa inayoongoza kwa ndoa za utotoni huku mkoa wa Shinyanga ukiongoza kwa 59%, ukifuatiwa na Tabora 58%, Mara 55%, Dodoma 51%, Lindi 48%.

Mikoa mingine inayofatia ni pamoja na Mbeya 45%, Morogoro 42%, Singida 42%, Rukwa 40%, Ruvuma 39%, Mwanza 37%, Kagera 36%, Mtwara 35%, Manyara 34%, Pwani 33%, Tanga 29%, Arusha 27%, Kilimanjaro 27%, Kigoma 26%, Dar es Salaam 19% na Iringa 8%.

Sababu kuu zinazochangia kukua kwa tatizo hili ni pamoja Mila na desturi potofu, Sheria na sera kinzani, Mifumo dhaifu ya uongozi katika ngazi ya kata, vijiji, Mitaa na vitongoji.

Mikoa inayoongoza kwa maambukizi ya virusi vya ukimwi nchini Tanzania

$
0
0
Mikoa ya Tabora, Katavi na Rukwa imetajwa kuwa ni miongoni  mwa mikoa  10 inayoongoza kwa maambukizi  ya virusi vya ukimwi.

Hiyo ni  kwa mujibu wa takwimu za mwaka 2011/2012 za Taasisi ya Mkapa.

Taarifa hiyo  ilitolewa na Meneja Mradi wa TB na Ukimwi kutoka Taasisi ya Mkapa, Dkt. Happenes  Wilbroad     katika mafunzo ya siku moja  ya viongozi wa dini  yaliyofanyika   Nzega.

Alisema  mkoa unaoongoza kwa maambukizi ya VVU kati ya mikoa hiyo mitatu ni  Rukwa wenyeasilimia  6.2 ukifuatiwa na Katavi asilimia  5.2 na Tabora asilimia 5.1.

Dk. Wilbroad alisema Taasisi ya Mkapa  imeanza kuendesha  mafunzo ya kuhakikisha wananchi wanatambua na kuepuka maambukizi mapya.

Alisema    jitiahada mbalimbali za kudhibiti maambukizi  hayo zinapaswa kufanyika  kunusuru maisha ya  wakazi wa maeneo hayo.

Alitaja sababu zinazochangia   maambukizi kuwa ni pamoja na ndoa za utotoni, tohara za jadi na baadhi ya wananchi kutozingatia elimu ya Ukimwi   na kukithiri  imani potofu za ushirikina.

Mawakili wa Lema wakata rufaa kudai dhamana.....Rufaa hiyo Itasikilizwa Jumatatu

$
0
0
Hatimaye  rufaa ya Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema iliyokatwa na mawakili wake itasikilizwa Jumatatu ijayo.

Rufaa hiyo itasikilizwa na Jaji Fatma Masengi ya kuomba mbunge huyo kupewa dhamana baada ya mawakili wanaomtetea jana kusajili maombi ya rufaa namba 112/113 ya mwaka 2016 Mahakama Kuu Kanda ya Arusha, ili kudai haki ya dhamana ya Lema aliyonyimwa kutokana na makosa ya kisheria yaliyofanywa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha.

Rufaa hiyo imepokewa Mahakama Kuu Kanda ya Arusha na kupangwa kwa Jaji Masengi ambaye ndiye atakayeamua hatma ya Lema kuwa nje kwa dhamana au la.

Mawakili wa Lema  ambao ni Sheck Mfinanga na Peter Kibatala jana walisema tayari wamesajili rufaa yao Mahakama Kuu na wanasubiri siku hiyo ili isikilizwe.

Mfinanga alisema wameamua kufungua maombi ya rufaa kwa ajili ya kujua ni kwa nini Lema amekosa dhamana ambayo awali Hakimu Desdery Kamugisha alisema ipo wazi.

Wakenya watamani Rais Magufuli awe Rais wao angalau kwa mwaka mmoja.

$
0
0
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini Kenya (COTU), Bw. Francis Atwoli amesema anaikubalia kasi ya Rais Magufuli katika kupambana na rushwa.

Pia amewataka Watanzania wamuunge mkono badala ya kulalamikia kasi kwani wao wanatamani mwakani aende kugombea kwao katika uchaguzi mkuu ujao.

Ametoa kauli hiyo jana katika Mkutano Mkuu wa Sita wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) katika ukumbi wa Mwalimu Julius K. Nyerere ulioko Chuo cha Mipango, nje kidogo ya mji wa Dodoma, uliofunguliwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa

“Ninawasihi wanaTUCTA suala la rushwa msilipe nafasi. Mpambane nayo kwa sababu kule kwetu imeota mizizi. Muungeni mkono Rais Magufuli, badala ya kulalamika kuwa kasi yake ni kubwa mno. Mnasema eti ana spidi sana, mkiona taabu mtuazime japo kwa mwaka mmoja ili aje atunyooshee mambo kule kwetu,” alisema huku akishangiliwa.

Aliwataka wahimize uhusiano uliopo baina ya vyama vya wafanyakazi, waajiri na Serikali iliyopo madarakani na kuwataka wadumishe umoja miongoni mwa viongozi na wanachama mara baada ya kumalizika kwa uchaguzi.

Msikilize hapa:-
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images