Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Rais Magufuli Amteua Diwani Athuman kuwa RAS Kagera, pia ameteua Wenyeviti wa Bodi katika taasisi za serikali akiwemo Jaji Warioba.

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 18 Novemba, 2016 amemteua aliyekuwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) Bw. Diwani Athuman kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera.Uteuzi wa Bw. Diwani Athuman unaanza mara moja.

Wakati huo huo, Rais Magufuli amefanya uteuzi wa Wenyeviti wa Bodi katika taasisi tano za Serikali kama ifuatavyo.

Kwanza, Rais Magufuli amemteua Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jaji Joseph Sinde Warioba kuwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA)

Uteuzi huu umeanza tarehe 16 Novemba, 2016.

Pili, Rais Magufuli amemteua Dkt. Jones A. Kilimbe kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) na amemteua Bw. Sylvester M. Mabumba kuwa Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).

Uteuzi huu umeanza tarehe 17 Novemba, 2016

Tatu, Rais Magufuli amemteua Prof. Patrick Makungu kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Uhandisi na Usanifu Mitambo (TEMDO).

Uteuzi huu umeanza tarehe 16 Novemba, 2016.

Nne, Rais Magufuli amemteua Bw. Martin Madekwe kuwa mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Fidia ya Ardhi.

Uteuzi huu umeanza tarehe 17 Novemba, 2016.

Tano, Rais Magufuli amemteua Prof. Raphael Tihelwa Chibunda kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Wakurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Viuatilifu vya Kitropiki Tanzania (TPRI)

Uteuzi huu umeanza tarehe 17 Novemba, 2016.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

18 Novemba, 2016

Kamanda Sirro: Makonda ni Mwenyekiti wangu, Kama ana wasiwasi Atajua atachukua hatua gani dhidi yetu

$
0
0
Kamanda wa Polisi mkoa wa Dar es salaam Simon Sirro, amesema kama Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda, ana wasiwasi na Jeshi la Polisi katika operesheni ya kutokomeza matumizi ya Shisha, achukue hatua zaidi kwa sababu yeye ni kiongozi wao na ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na Usalama Mkoani Dar es salaam.

Akiongea kupitia kipindi cha Sun Rise cha Times Fm leo asubuhi, Sirro amedai wao kama jeshi la Polisi wanafanya kazi kwa mujibu wa Sheria na Operesheni ya kutokomeza Shisha jijini inaendelea kama kawaida kilicho baki ni Mwanasheria mkuu wa Serikali kuandaa mashtaka kwa Watuhumiwa.

“Watu wamekamatwa ni wengi, kimsingi kazi inafanyika, sasa huo ni wasi wasi kama wasi wasi basi unabaki kuwa wasi wasi, kikubwa niseme tunafanya kazi kwa mujibu wa sheria na kanuni, yeye ni mwenyekiti wangu wa kamati ya ulinzi na usalama kwa hiyo ninaamini kama ana wasiwasi na chombo chake najua atakuja kutuita na kutuambia nini cha kufanya.

“Lakini kama ana wasi wasi Zaidi yeye ni kiongozi wetu atajua atachukua hatua gani dhidi ya sisi, kwa hiyo namuachia mkuu wangu wa kazi yeye ndio atajua nini cha kufanya”

Akitolea ufafanuzi kama alipatiwa taarifa juu ya watu 10 waliotaka kumpa ‘Mlungula’ Mkuu wa Mkoa ili kumziba ‘Mdomo’ kukemea matumizi ya kilevi cha Shisha, Kamanda Siro alisema hawezi kulisemea lolote swala hilo na amemtaka Mtangazaji wa Sun Rise Stanslaus Lambat amuulize Mh Makonda taarifa aliipeleka wapi na si yeye.

RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 91 & 92(Riwaya inawafaa kuanzia miaka 18 na kuendelea )

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA

ILIPOISHIA
Madam Mery akanitazama kwa muda, huku akikoaa cha kuzungumza, taratibu nikaanza kukichomoa kisu changu kilichopo kwenye soksi ya mguu wa kushoto, kwa ajili ya kuikata shingo ya madam Mery aliye, nifanyia ukatili mkubwa, akishirikiana na washenzi wezake John na Victoria.

ENDELEA
   Shamsa akanishika mkono, ulio kua ukichomoa kisu kutoka katika soksi. Akanikonyeza huku akinionyesha camera ya ulinzi, iliyopo kwenye moja ya kona ya ukuta wa ofisi hii. Nikakirudisha kisu nilipo kitoa. Nikabaki nikimtazama madam Mery kwa macho makali, yaliyo jaa hasira.

"Eddy ninatambua kwamba una hasira na mimi"
Madam Mery alizumgumza na kukaa kimya huku, akiyakwepesha macho yake kutazamana na macho yangu.
"Sikupenda kufanya kile walicho kufanyia John na nwenzake. Roho yangu iliniuma sana pale nilipo sikia kwamba umekufa."
Madam Mery alizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwake. Shamsa akasimama na kupiga hatau hadi mlangoni.
"Eddy nipo nje ninakusubiri"
Nikamuitikia Shamsa kwa kutingisha kichwa kumuashiria kwamba nimekubali yeye kutoka nje ya ofisi. Madam Mery akatoa kitamba kwenye pochi yake na kujifuta machozi yaliyo tapakaa usoni mwake.

'Huyu mnafki kweli"
Nilijiseme kimoyo moyo huku nikimtazama madam Mery usoni mwake.
"Eddy moyo wangu ulikosa amani, nilijaribu kutafuta japo kaburi lako, nije nipige magoti nikuombe msamaha"
"Ila sikuweza kufanikiwa katika hilo, ila nilikuka kupta amani pale nilipo kuon kwenye tangazo la magari, ndipo nilipo tambua kwamba upo hai"

Madam Mery alizumgumza huku alinyanyuka kwenye kiti chake na kuja nilipo. Akapiga magoti chini, na kuushikilia mguu wangu wa kulia, huku aliendelea kulia kwa uchungu.
"Eddy ninakupenda sana, ndio maana nilikupa nafasi ya kuishi tena duniani"

"Nakuomba unisamehe, ninakuomba unipe nafasi ya msamaha wako, ili niweze kuishi kwa amaani"
Suti ya uchungu, na yamajozi ya Madam Mery ikaanza kuilainisha hasira yangu, iliyo ganda kama barafu. Nikamnyanyua na tukasimama, akanikumbatia kwa nguvu huku akiendelea kutoa kilio cha kujutia makosa aliyo yafanya. Japo hasira bado inanisukuma niweze kumfanyia madam Mery jambo la ukatili, ila nikazidi kujitahidi kuweza kuepukana na kufanya tukio lolote baya.
"Eddy nisamehee'
Madam Mery aliendelea kuzungumza huku akilia kwa uchungu.

"Ni...mekusamehe"
Nilijitahidi kukifungua kinywa changu, kujibu nilicho mjibu Madam Mery, japo muda sote kinatetemeka kwa hasira kali. Taratibu Madam Mery akaniachia, na kunitazama machoni mwangu. Tukabaki tukiwa tumetazamana kama dakika tatu, hisia kali ya mapenzi iliyo pelekea kuyakumbuka matukio kadhaa ya nyumà dhidi ya penzi letu, na madam Mery. Zikanifanya mwili mzima kusisimka, taratibu ñikaupelekà mdomo wangu, ulipo mdomo wa Madam Mery ila akaukwepesha usikutane na mdomo wangu.
"Eddy sio sasa"
Madam Mery akanichia na kurudi, kilipo kiti chake, nikabaki nikiwa nimemtazama kwa mAcho yaliyo jaa matamanio mengi.

"Umetuletea pesa nini?"
"Eheee!"
Nilibaki nikiwa nimemshangaa Madam Mery, huku hisia za mapezi, zikiupelekea mwili wangu kuishiwa kabisa na nguvu. Taratibu nikakaa kwenye kiti changu.
"Eddy sio kwa sasa, hiyo kamera hapo juu ukutani inarekodi kila kitu kinacho endelea humu ndani."b
Madam Mery alizungumza huku, akinionyeshea kamera iliyopo ukutani.
"Ni pesa ulizo beba?"
"Eheeee"
"Una akaunti ya benki hii?"
"Ndio"
"Hembu nitajie"
Nikamtaji madam Mery namba ya akaunti yangu, akaiingiza kwenye computer iliyopo hàpa mezani mwake. Baada ya muda akanigeuzia kioo cha çumputer hii, aina ya 'DELL'. Nikaona taarifa za benki yangu, ikiwemo picha na jina langu kamili.

"Ila inaonyesha kwa Tawi la Tanzania umefungiwa, kwa nini?"
"Ahaaa ni mama, ndio alinifungia"
"Sawa, ngoja nimpigie simu muasibu"
Akampigia simu muasibu wake kwa kupitia simu ya mezani. Tukiwa tunamsubiri muàsibu madam Mery akanipatia kokadi chenye namba ya simu yake.
"Mimi nitakwenda kwenye kikao, kama utaondoka pasipo kuonana na mimi basi utanipigia kuniambia ni wapi ulipo"
"Sawa"
Akaingia jamaa mrefu, mweusi kiasi aliye valia suti, nikatoka naye ofisini na kwenda kwenye chumba chenye mashine za kuhifadhia pesa.

Zoezi la kuzihesabu pesa likaanza, halikuchukua muda sana tukawa tumepata kiwango cha pesa ambacho ni dola za kimarekani milioni saba. Sawa na bilioni kadhaa kwa pesa ya tanzani. Nikatoa dola laki moja na nyingine zilio salia zikaingizwa kwenye akaunti yangu.
"Eddy hatuwezi kwenda kwenye kambi ya wakimbizi muda umesha pita"
Shamsa alizungumza huku tukitoka kwenye mlango wa benki.
"Kwani ni saa ngapi sasa hivi?"
"Saa tisa mchana na muda wa kuingia pale, ni kuanzia saa nne asubuhi hadi saa nanechana"

Steven Wassira Chali....Ester Bulaya Ashinda Kesi ya Kupinga Ushindi Wake

$
0
0

Hatimaye Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza leo imetoa uamuzi wa kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa Ubunge uliompa ushindi Mbunge wa Bunda Mjini, Esther Bulaya (Chadema) dhidi ya Spephen Wassira (CCM).
 
Kesi hiyo ya kupinga matokeo ya uchaguzi ilifunguliwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, lakini ilikuwa inasikilizwa mjini Musoma, Mkoani Mara.

Mahakama hiyo imeeleza kutoridhishwa na ushahidi wa kupinga matokeo hayo uliowasilishwa na upande wa walalamikaji, hivyo imemthibitisha Bulaya kuwa mbunge halali wa jimbo hilo.

Kesi ya kupinga matokeo hayo ilifunguliwa na wananchi wanne ambao ni wafuasi wa Wassira ambaye alikuwa mbunge wa jimbo hilo kabla ya kuondolewa kupitia uchaguzi mkuu uliofanyika mwaka jana.

Katika kesi ya msingi, walalamikaji ambao ni wakaazi wa Bunda walidai kuwa uchaguzi haukuwa huru na haki kwakuwa uligubikwa na vitendo vya rushwa, mgombea wanaemuunga mkono kunyimwa fursa ya kuhakiki matokeo pamoja na kuongezeka kwa idadi ya vituo vya kupigia kura visivyo halali.

Katika kesi hiyo, Bulaya alitetewa na mwanasheria wa Chadema, Tundu Lissu.


Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumamosi ya Novemba 19

Majibu ya Jeshi la Polisi Makao Makuu kuhusu tuhuma za Rushwa dhidi ya Kamanda Sirro

$
0
0
Jeshi la polisi nchini limesema litafanya uchunguzi wa tuhuma za rushwa dhidi ya Kamishna wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamanda Simon Sirro na baadhi ya makamanda wa mikoa akiwemo kamanda wa mkoa wa Kinondoni Susan Kaganda.

Kauli hiyo imetolewa jana na Kaimu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, CP Robert Boaz katika makao makuu ya Polisi jijini Dar es Salaam.

Kauli hiyo ya CP Boaz kwa niaba ya jeshi la polisi imetolewa baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda hivi karibuni kuwatuhumu makamanda hao kuwa wanasita kuwachukulia hatua watumiaji na wauzaji wa kilevi cha shisha kwa madai kuwa huenda wakawa wamepokea rushwa kutoka kwa wanaojishughulisha na biashara hiyo.

Makonda alitoa tuhuma hizo licha ya yeye ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama katika kanda hiyo kutoa maagizo wahusika kuchukuliwa hatua.

CP Boaz alisema, kuhusu tuhuma ya rushwa suala hilo lina taasisi zake zinazohusika, na kwamba jeshi hilo limepokea tuhuma hizo dhidi ya askari wao kwa hiyo watazichunguza kubaini ukweli.

Waziri Mkuu akagua ujenzi wa nyumba za Magomeni Kota....Ataka Ukamilishwe Kwa Wakati

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka watalaamu wa ujenzi wa mradi wa nyumba za makazi Magomeni watumie utaalamu wao vizuri na wakamilishe kwa wakati.

Ametoa agizo hilo jana mchana (Ijumaa, Novemba 18, 2016) wakati alipokagua ujenzi wa nyumba hizo zinazojengwa na wataalamu kutoka Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) eneo la Magomeni Kota jijini Dar es Salaam.
 
Waziri Mkuu amewataka wataalamu hao waendelee kufanya kazi hiyo kwa kufuata misingi ya weledi wa taalauma yao kwani Serikali inawaamini.

“Muhimu mjue kwamba mmepewa dhamana hii kubwa ya kukamilisha ujenzi huu ili wananchi waliokuwa wanaishi hapa waweze kurudi katika makazi yao,” alisema.
 
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Ushauri wa TBA, Mhandisi Edwin Nnunduma alisema awamu ya kwanza ya ujenzi huo itahusisha majengo matano ya makazi.

“Kati ya majengo haya matano, manne yatakuwa na ghorofa nane na moja litakuwa na ghorofa tisa, ambapo wakazi zaidi ya 600 waliokuwa wanaishi eneo hili tangu zamani watakabidhiwa,” alisema.
 
Mhandisi Nnunduma alisema majengo hayo yanajengwa kwa teknolojia ambayo imezingatia uwezo wa wakazi wake ambapo ina majiko yanayoweza kutumia kuni na mkaa.
 
Alisema mradi huo ambao unajengwa kwa awamu tofauti utahusisha ujenzi wa nyumba za makazi, maduka makubwa na ya kisasa pamoja na ofisi.
 
Mhandisi huyo alisema awamu ya kwanza iliyoanza Oktoba Mosi, mwaka huu inahusisha ujenzi wa nyumba za makazi ya wananchi waliokuwa wanaishi katika eneo hilo ambayo inatarajiwa kukamilika Oktoba, mwakani.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mshauri wa Wakala ya Majengo Tanzania (TBA), Edwin Nnuduma kuhusu Mradi wa Ujenzi wa Nyumba, Magomeni Kota jijini Dar es salaam wakati alipotembelea mradi huo Novemba 18, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mshauri wa Wakala ya Majengo Tanzania (TBA), Edwin Nnuduma kuhusu Mradi wa Ujenzi wa Nyumba, Magomeni Kota jijini Dar es salaam wakati alipotembelea mradi huo Novemba 18, 2016. Wapili kulia ni Mkuu wa wilaya ya Kinondoni, Ally Happy.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza wakati alipokagua Mradi wa Ujenzi wa Nyumba, Magomeni Kota jijini Dar es salaam Novemba 18, 2016. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Happy. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na wajenzi wakati alipotembelea Mradi wa Ujenzi wa Nyumba, Magomeni Kota jijini Dar es salaam kukagua mendeleo ya mradi huo Novemba 18, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na wajenzi wakati alipotembelea Mradi wa Ujenzi wa Nyumba, Magomeni Kota jijini Dar es salaam kukagua mendeleo ya mradi huo Novemba 18, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na wajenzi wakati alipotembelea Mradi wa Ujenzi wa Nyumba, Magomeni Kota jijini Dar es salaam kukagua mendeleo ya mradi huo Novemba 18, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na wajenzi wakati alipotembelea Mradi wa Ujenzi wa Nyumba, Magomeni Kota jijini Dar es salaam kukagua mendeleo ya mradi huo Novemba 18, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 
IMETOLEWA NA: 
OFISI YA WAZIRI MKUU, 

Polisi yaongeza muda wa zoezi la uhakiki wa silaha za kiraia kwa nchi nzima

$
0
0
Jeshi la Polisi limeongeza muda wa huruma kwa wamiliki wa silaha walioshindwa kuhakiki silaha zao katika zoezi la uhakiki wa silaha za kiraia Tanzania Bara lililoanza Machi 22 na kumalizika Juni 30, 2016.

Kaimu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai CP Robert Boaz, amesema licha ya Jeshi la Polisi kuongeza muda wa uhakiki hadi mwezi Oktoba mwaka huu, bado wamiliki wengi hawakujitokeza kuhakiki silaha zao.

“Katika kipindi cha kuanzia tarehe 22 Machi, 2016 hadi Juni 30 serikali ilianza kufanya zoezi la uhakiki wa silaha zote za kiraia hapa Tanzania Bara, kutokana na sababu mbalimbali tuliongeza muda lakini bado baadhi ya watu hawakujitokeza,” amesema.

Amesema baada ya zoezi la awali kukamilika, tathmini inaonyesha kuwa asilimia 59.18 ya silaha zote zilizosajiliwa ndizo zilizohakikiwa na kwamba asilimia 40.82 hazijahakikiwa.

CP Boaz amesema polisi imeongeza muda wa mwezi mmoja ili wasio hakiki silaha zao wahakiki, na kwamba muda huo ni wa mwisho hautaongezwa tena.

“Tunatoa tena muda wa huruma tunawataka wamiliki wajitoekeze vituoni kuhakiki silaha zao ndani ya mwezi mmoja kuanzia Novemba 21 hadi Disemba 20, 2016. Huu ni muda wa mwisho na utakapomalizika tutachukua hatua kali.

Amezitaja baadhi ya hatua zitakazochukuliwa ikiwa ni pamoja na kufuta leseni za umiliki kwa silaha zote zisizohakikiwa, kuwatangaza wamiliki wote wa silaha kwenye vyombo vya habari walioshindwa kuhakiki pamoja na kuwafikisha katika vyombo vya sheria.

Ametoa wito kwa wanaomiliki silaha kinyume cha sheria kuzisalimisha silaha zao katika vituo vya polisi au ofisi za serikali za mitaa na kwamba atakae tumia kipindi hiki hawatachukuliwa hatua za kisheria.

Maalim Seif kufuta nyayo za Lipumba Mikoa ya Kusini

$
0
0
Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad anatarajiwa kuzuru mikoa ya Kusini mwa Tanzania katika kipindi ambacho bado kuna sintofahamu kuhusu nafasi ya Uenyekiti wa chama hicho.

Mwanasiasa huyo ambaye ataongozana na Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya chama hicho, Julius Mtatiro pamoja na Wajumbe wa Baraza Kuu watazuru Mtwara na Lindi ikiwa ni miezi michache baada ya Mwenyekiti wa chama hicho anayetambuliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama Vya Siasa, Profesa Ibrahim Lipumba kuzuru eneo hilo la kusini.

Akizungumzia ziara hiyo, Naibu Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Uhusiano wa Umma wa chama hicho, Mbarala Maharagande alisema kuwa lengo la ziara hiyo ni kukagua shughuli za chama na kupokea maoni ya pamoja ya namna ya kuboresha utendaji wa chama hicho kwa ngazi za chini.

Maalim Seif anatua katika eneo hilo wakati ambapo kukiwa na mvutano baada ya baraza la madiwani kufanya jaribio lililoshindikana la kumng’oa Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara Mikindani, Geofrey Mwanchisye.

Jaribio hilo liligonga mwamba baada ya Mwanasheria wa Halmashauri hiyo, Sifaeli Kulanga kueleza kuwa hoja zao hazina msingi kwani tuhuma zao kuhusika na matumizi mabaya ya fedha za umma yanakinzana na ripoti ya kamati maalum iliyoundwa na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara.

Kesi kuhusu Uenyekiti wa chama hicho inaendelea Mahakamani ambapo Baraza Kuu la chama hicho linapinga barua ya Msajili inayomtambua Lipumba kama Mwenyekiti wa chama hicho wakati ambapo Baraza hilo lilikuwa limetangaza kumfuta uanachama.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili ya Novemba 20

Rais Magufuli amjulia hali Mkuu wa Mkoa wa Tanga aliyelazwa Hospitali ya Taifa Muhimbili

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John PombeMagufuli, jana tarehe 19 Novemba, 2016 amemtembelea na kumjulia hali Mkuu wa Mkoa wa Tanga Bw. Martin Shigella ambaye amelazwa katika wodi ya Sewahaji iliyopo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam.

Bw. Martin Shigella alifikishwa hospitalini hapo tangu Jumatano iliyopita kwa ajili ya kupata matibabu.

Akimpa pole wodini humo Rais Magufuli alisema “Nakupa pole sana Ndg. Martin Shigella kwa maradhi yaliyokupata, nakuombea kwa Mwenyezi Mungu upone haraka na urejee katika kituo chako cha kazi ili uendelee na majukumu ya ujenzi wa Taifa”

Hali ya Bw. Martin Shigella inaendelea vizuri.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

Rais Magufuli afanya uteuzi wa wenyeviti wengine watatu

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, amefanya uteuzi wa wenyeviti wawili wa bodi za mashirika ya hifadhi za jamii na mmoja wa chuo.

Taarifa iliyotolewa jana na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi iliwataja walioteuliwa kuwa ni kama ifuatavyo;

Kwanza, Rais Magufuli amemteua Mhandisi Alhaji Mussa Iyombe kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF).

Mhandisi Alhaji Mussa Iyombe ni Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Pili, Rais Magufuli amemteua Prof. Faustine Karani Bee kuwa Mwenyekiti wa Mfuko wa Pensheni wa Serikali za Mitaa (LAPF)

Prof. Faustine Karani Bee ni Makamu Mkuu wa Chuo cha Ushirika Moshi.

Tatu, Rais Magufuli amemteua Prof. Tadeo Andrew Satta kuwa Mkuu wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM).

Kabla ya uteuzi huu Prof. Tadeo Andrew Satta alikuwa akikaimu nafasi hiyo.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

Waziri Mkuu Atoa Siku 18 Umeme Ukamilike Mlandizi

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametoa siku 18 kwa Mkandarasi wa umeme kwenye kiwanda cha Kiluwa Steel Group awe amemaliza kazi ya kuweka ume mkubwa ili kiwanda hicho kianze kazi.

Ametoa agizo hilo jana (Jumamosi, Novemba 19, 2016) wakati akizungumza na wananchi na viongozi mbalimbali wa Serikali na wa Mkoa wa Pwani waliofika kiwandani hapo eneo la Mlandizi wakati akikagua utekelezaji wa maagizo aliyoyatoa Julai 12, mwaka huu alipozuru kiwanda kwa mara ya kwanza.

“Nilipokuwa hapa mara ya kwanza niliagiza itengenezwe njia ya reli kutoka njia panda ya reli ya kati, lakini pia niliagiwa uwekwe umeme wa msongo mkubwa ili kiwanda kiweze kuanza uzalishaji mapema mwakani. Nimefarijika kukuta maagizo haya yametekelezwa kwa kiasi kikubwa isipokuwa hili la umeme,” alisema.

“Mkandarasi ameomba siku 14, nimempa hadi tarehe 7 Desemba ahakikishe umeme unafanya kazi kwa kiwango kinachotakiwa. Sasa hivi wameanza test lakini muda ili transforma iweze kuhimili mzigo mkubwa… hili ni suala la kitaalamu kwa hiyo tuwape muda.”

Waziri Mkuu pia alisema amefarijika kusikia kwa orodha ya watu wanaodai fidia sababu ya kuoisha njia ya reli ijengwe, imeshawasilishwa kwa Mkuu wa Mkoa na mwenye kiwanda yuko tayari kuwalipa maa taratibu zitakapokamilika.

Mapema, akiwasilisha taarifa fupi, Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Eng. Evarist Ndikilo alisema haelewi ni kwa nini mkandarasi huyo anazidi kuomba siku 14 ili kukamilisha wakati aliahidi kuwa 14 za awali zingetosha kukamilisha kazi hiyo.

Kuhusu fidia kwa wananchi na Halmashauri ya Wilaya hiyo, Mkuu huyo wa Mkoa alisema wananchi waliopisha njia wanadai fidia ya sh. milioni 95.76 na Halmashauri inadai sh. milioni 307.26 na kwamba jumla yote inafikia sh. milioni 403.

Alipopewa nafasi na Mkuu wa Mkoa huo ajieleze mbele ya Waziri Mkuu, Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Dekan Group Ltd, Eng. Desderius Luhaga ambaye amepewa kazi ya kuweka umeme na transforma Mlandizi alisema anahitaji apewe siku 14 ili aweze kukamilisha kazi hiyo.

“Kazi kubwa ya umeme tumeshaifanya na hii ni ya umeme wa msongo wa kilovoti 132, na tumeanza kutest umeme katika baadhi ya mitambo hapa kiwandani, lakini tunahitaji siku karibu tano ili transforma ipoe tangu tulipoifunga ndipo iweze kupokea mzigo mkubwa. Kisha tutaanza kuunganisha katika maeneo mengine madogo madogo humu ndani,” alisema.

Katika hatua nyingine, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Reli Tanzania (TRL), Bw. Masanja Kadogosa  alisema shirika hilo limetumia sh. milioni 863 kukamilisha ujenzi wa reli ya km.5 kutoka njia panda hadi kwenye kiwanda hicho ambapo kati ya hizo km.1.5 zimo ndani ya kiwanda.

Alisema hadi sasa wameshaweka njia nne za reli, moja ikiwa ni mahsusi kwa ajili ya kubeba makaa ya mawe. 

“Tulilazimika pia kujenga culvert katika eneo moja kwa sababu pailikuwa na shimo kubwa. Tumetumia fedha kidogo kwa sababu tumetumia mafundi wetu badala ya wakandarasi,” aliongeza.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Kiluwa Steel Group, Bw. Mohammed Kiluwa alimweleza Waziri Mkuu kuwa anatarajia kuanza uzalishaji Januari, mwakani na kwamba ataajiri wafanyakazi wapatao 200.

“Tunataraji kuanza uzalishaji Janruari, mwakani na uzalishaji utakuwa tani 2,000 kwa siku. Ila tumekubaliana na wawekezaji wenzangu tuweke pia viwanda vingine vitatu kwa sababu kutakuwa na umeme wa kutosha.”

“Tunatarajia kufungua viwanda vine vya kutengeneza gypsum powder, pikipiki, nguzo na vifaa vya kufungia nyaya za umeme mkubwa pamoja na tissue. Tuna eneo lingine Mkuranga lakini kule hakuna umeme, kwa hiyo tumepanga kuweka hivyo viwanda hapa kwa sababu tuna eneo la kutosha.”

Hata hivyo, Bw. Kiluwa alitumia fursa hiyo kumweleza Waziri Mkuu kwamba wanapata taabu ya makaa ya mawe kwa sababu wanaletewa makaa yenye ukubwa wa milimita 10 hadi 15 badala ya milimita 35 – 40 ambazo wanahitaji kwa ajili ya kiwanda chao.

“Tukiagiza tani 30, tunachambua mawe ya saizi inayotufaa na kujikuta tunabakia na tani saba tu. Kiasi kilichobakia ni vumbi tupu,” alisema.

Waziri Mkuu alimwagiza Naibu Katibu Mkuu wa Viwanda na Biashara, Eng. John Malongo awasiliane na Wizara ya Nishati na Madini ili afuatilie ni kwa nini watengenezaji wa makaa ya mawe hawafuati vipimo halisi vinavyotolewa na wawekezaji.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Atembelea Kiwanda Cha Chuma Na Kiwanda Cha Kuunganisha Magari Na Trekta Mkoani Pwani

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameliegiza Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha lifanye maamuzi ya kupima ardhi haraka na kutenga maeneo kwa ajili makazi na viwanda ili kujiandaa na uwekezaji mkubwa.

Ametoa agizo hilo jana mchana (Jumamosi, Novemba 19, 2016) wakati akizungumza na wananchi na viongozi mbalimbali wa Serikali na wa Mkoa wa Pwani mara baada ya kukagua kiwanda cha kutengeneza magari ya zimamoto na matrekta cha Equator SUMA JKT Limited kilichopo Ruvu JKT, wilayani Kibaha mkoani Pwani. 

“Jiji la Dar es Salaam limejaa, na Kibaha mjini pia hawana ardhi ya kutosha kwa kimbilio pekee hivi sasa ni Kibaha Vijijini. Baraza la Madiwani fanyeni maamuzi, pimeni ardhi na mtenge maeneo ya makazi, viwanda na taasisi za elimu ili mkipata wawekezaji iwe rahisi kuwapa maeneo,” alisema.

Waziri Mkuu alisema ujenzi wa kiwanda hicho utakuwa mkombozi kwa taasisi nyingi na halmashauri nyingi nchini kwani zilikuwa zinashindwa kumudu bei ya kununua magari ya zimamoto. 

“Baadhi ya Halmashauri nyingi zilikuwa zinanunua gari moja kwa sh. milioni 500 na hiki ni kiasi kikubwa mno kwa hiyo kiwanda hiki kitakuwa mkombozi kwa taasisi nyingi na halmashauri zetu,” alisema.

Alisema maeneo mengi nchini yanahitaji magari ya zimamoto lakini yalikuwa yanashndwa kumudu bei za magari hayo. 

Aliyataja maeneo hayo kuwa ni viwanja vya ndege, bandari, taasisi zilizo chini ya TAMISEMI kama vile shule za sekondari za bweni, Majiji, miji mikuu, Manispaa na Halmashauri za Wilaya.

Alisema ameguswa kukuta kiwanda hicho pia kina uwezo wa kutengeneza matreka na zana za kilimo (farm implements) kwani asilimia kubwa ya Watanzania ni wakulima na wanategemea jembe la mkono.

 “Kupitia kiwanda hiki, matrekta mengi yataunganishwa na nina imani bei itakuwa ya chini ili wananchi waweze kumudu.”

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Equator SUMA JKT Ltd, Eng. Robert Mangazini alimweleza Waziri Mkuu kwamba asilimia 80 ya ujenzi wa kiwanda hicho imekamilika na kwamba hivi sasa wako kwenhye hatua ya kufunga mitambo. Hata hivyo, alisema wanaisubiri iwasili kutoka India.

Alisema kiwanda hicho kikikamilika kitaweza kuunganisha matrekta 3,000 kwa mwaka na magari ya zimamoto 100 na kubainisha kuwa faida za kuunganisha magari hayo hapa nchini ni kuwa na uwezo wa kuzalisha vipuri ndani ya nchi.

“Tukiweza kuzalisha vipuri hapa nchini kwa asilimia 60, umiliki wa magari haya na matrekta utakuwa ni wa Tanzania na siyo wa kampuni za nje tena. Pia tutakuwa tumefaulu kuhamisha teknolojia kwa vijana wetu,” alisema.

Alisema hadi sasa vijana 60 wamekwishapatiwa mafunzo na wako tayari kuanza kazi mara uzalishaji utakapoanza Machi, 2017.

Kuhusu teknolojia ya utengenezaji wa magari ya zimamoto, Eng. Mangazini alisema kiwanda hicho ni cha pili kujengwa barani Afrika cha kwanza kikiwa huko Bassa, Afrika Kusini.

Mapema, akisoma risala mbele ya Waziri Mkuu, mwakilishi wa Equator SUMA JKT Ltd. Kapteni Farijala Mkojera alisema kiwanda hicho kinamilikiwa kwa pamoja na kampuni ya Equator Automech Ltd ambao wana hisa asimilia 70 na SUMA JKT inamiliki asilimia 30 ya hisa za kiwanda hicho.

Akizungumzia ujenzi wa kiwanda hicho, alisema hadi sasa wamekwishatumia sh. bilioni 1.5 na kwamba hadi ujenzi utakapokamilika, wanatajia kuwa wametumia sh. bilioni mbili. “Ujenzi ukikamilika, tunatarajia kuajiri wafanyakazi 200 katika fani mbalimbali,” alisema.

Alisema wakianza uzalishaji, mbali ya magari ya zimamoto na matrekta, wataweza pia kuunganisha mabasi na zana za kilimo kama vile combine harvesters. 

“Tutakuwa tumefanikiwa kuhamisha teknolojia kutoka Russia (magari za zimamoto) na India na Poland (matrekta). Tuna uhakika wa soko hapa nchini katika Jumuiaya za EAC na SADC,” alisema.

Waziri Mkuu amerejea Dodoma mchana huu.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU

Wapambe wa Wasira Kukata Rufaa tena Kupinga Ushindi wa Bulaya

$
0
0
Baada ya Mahakama Kuu, Kanda ya Mwanza kutupilia mbali maombi ya wananchi wanne wa kutaka itengue ushindi wa Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini Ester Bulaya (Chadema), walalamikaji hao wamesema watakata rufaa katika Mahakama ya Rufaa kwa kile walichosema kuwa Mahakama hiyo haikutenda haki katika kutoa maamuzi hayo.

Novemba 18, mwaka huu, Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza iliyokuwa inasikiliza kesi hiyo namba moja ya mwaka huu, katika Mahakama ya Mkoa wa Mara mjini Musoma, chini ya Jaji Noel Chocha, ilitupilia mbali kesi hiyo na kumthibitisha Bulaya kuwa ni Mbunge halali wa jimbo hilo.

Wananchi hao wanne walikuwa wamefungua kesi hiyo wakipinga ushindi wa Bulaya dhidi ya Stephen Wasira kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), katika uchaguzi mkuu uliofanyika mwaka jana.

Baada ya hukumu hiyo kutolewa waandishi wa habari walimhoji mmoja wa walalamikaji Janes Ezekiel, ambaye alisema kuwa watakaa na wenzake waone namna ya kukata rufaa.

Hata hivyo baadaye mlalamikaji mwingine Ascetic Malagila alimwambia mwandishi wa habari hii kuwa tayari wamekubaliana na wenzake pamoja na mwanasheria wao kuwa watakata rufaa katika Mahakama ya Rufaa kupinga hukumu hiyo, kwa kile alichoeleza kuwa wameshindwa kwa sababu ya uonevu na kwamba watatafuta haki yao katika Mahakama ya Rufaa.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Wasira alidai kuwa tayari walalamikaji hao pamoja na wakili wao Constantine Mutalemwa, wamekutana na kukubaliana kukata rufaa katika Mahakama ya Rufaa kutafuta haki.

Kabla ya hukumu hiyo kutolewa Jaji Chocha, alirejea baadhi ya vifungu vya sheria pamoja na hoja mbalimbali zilizotolewa na waleta maombi (walalamikaji) na wajibu maombi wa kwanza, wa pili na watatu.

Jaji Chocha alisema kuwa kutokana na kupitia vifungu vyote vya sheria pamoja na ushahidi uliotolewa na waleta maombi katika Mahakama hiyo, ni kwamba ushahidi wao haujajitosheleza katika hatua ya kutengua ubunge wa jimbo hilo.

Alisema kuwa iwapo ataamua kufuta matokeo hayo atawasababishia wananchi wa jimbo hilo ambalo ni miongoni mwa jimbo lenye watu masikini sana kukosa haki yao.

Alisema kuwa madhara ya kurudia uchaguzi ni makubwa sana, sanjari na gharama za uendeshaji wa uchaguzi mpya, ambao utaligharimu taifa na wananchi kwa ujumla kwa sababu gharama za uchaguzi ni sehemu ya kodi ya kila mwananchi.

Akirejea mwenendo mzima wa kesi hiyo tangu ilipofunguliwa katika Mahakama hiyo, Jaji huyo alikiri kutokea kwa kasoro kadhaa katika kipindi cha uchaguzi hadi kutangaza matokeo na kusema kuwa ni kawaida ya uchaguzi wowote kuwa na kasoro ndogondogo na kuongeza kuwa hata nchi zilizoendelea kasoro huwa hazikosekani.

Alisema kuwa katika kesi hiyo kasoro nyingi zilizojitokeza zimeonekana mara baada ya matokeo kutangazwa, lakini katika mchakato mzima wa upigaji kura hakuna kasoro zilizobainishwa, ambazo zingeweza kuonekana kwenye fomu yoyote ya malalamiko anayokuwa nayo msimamizi wa uchaguzi, ambazo zingeonesha kuwa uchaguzi haukuwa wa huru na haki. Alibainisha kuwa si kila kasoro inayojitokeza kwenye uchaguzi inaweza kuathiri matokeo ya uchaguzi.

Hata hivyo alisema kuwa pia msimamizi wa uchaguzi huo Lucy Msoffe alifanya uzembe mkubwa sana wakati alipofika katika hatua ya kuandika idadi ya wapiga kura na kwamba alipaswa kuwa makini kwa kutokuandika takwimu kimakosa.

Akizungumza nje ya Mahakama hiyo wakili wa mjibu maombi Paul Kipeja, alisema maamuzi yaliyotolewa na Mahakama hiyo waliyatarajia tangu mwanzo wa kesi hiyo kwa sababu hakukuwa na hoja zozote za msingi za waleta maombi.

Kuhusu gharama walizotumia katika kesi hiyo wakili Kipeja alisema kuwa watakaa pamoja na wakili Tundu Lissu, ili waweze kurudishiwa gharama zao zote walizotumia kuendeshea kesi hiyo.

Rais Magufuli atengua uteuzi wa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TRA

Bashe adai Lowassa alionewa CCM, aeleza uhusiano wao kwa sasa

$
0
0


Mbunge wa Nzega, Hussein Bashe (CCM) amesema kuwa anaamini waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa aliondolewa kwa kuonewa katika mchakato wa kugombea urais ndani ya CCM.

Bashe amesema kuwa kitendo hicho alichokiita cha kiuonevu ni changamoto kubwa ndani ya CCM na kwamba wengi wameonewa katika michakato ya kuwania nafasi mbalimbali.

“Yaliyomkuta Lowassa yamewakuta wengi ndani ya CCM, hivyo jambo hilo sio geni,” Bashe anakaririwa na Mwananchi. “Wapo waliobaki na wapo walioamua kuhama chama kwa sababu ni binadamu. CCM ina historia hiyo, hii ndiyo changamoto yake kubwa,” aliongeza.

Mbunge huyo alifafanua kuwa kwakuwa Lowassa alituhumiwa kwa mengi ndani ya chama hicho, alipaswa kuitwa na kuelezwa tuhuma zake na sababu za kuondolewa jina lake ili umma ufahamu.

Alisema kuwa katika chama hicho, kashfa nyingi hufanywa kwa sababu maalum na hubuniwa kwa ajili ya kufikia lengo fulani dhidi ya mtu au kikundi cha watu.

Alisema kuwa mbali na sakata la Richmond lililopelekea Lowassa kujiuzulu nafasi ya uwaziri mkuu, masakata ya Lugumi na Tegeta Escrow ni sehemu yale yaliyobuniwa kwa lengo maalum.

“Tazama wanavyofunika sakata la Lugumi. Usiende mbali angalia sakata la Escrow. Tumeadhibu waliopata fedha kutoka benki ya Mkombozi, vipi wa Stanbic? Wizi mwingine uliofanywa nchi hii una uhusiano kati ya Serikali na vikundi vya watu wenye uhusiano na Serikali,” Bashe aliliambia Mwananchi.

Akizungumzia uhusiano wake na Lowassa ambaye alikuwa anamuunga mkono wakati wa mchakato wa kugombea urais kupitia CCM, Bashe alisema hivi sasa hawana uhusiano tena wa urafiki wa kisiasa.

Alisema kuwa alimshauri sana Lowassa kutohama CCM, avumilie, lakini hakufanikiwa kumshawishi, hivyo waliagana.

“Lowassa ni mzee wangu. Ni mtu ambaye namheshimu na nitaendelea kufanya hivyo, ingawa kwa sasa hatuna uhusiano wa kisiasa,” alisema.

Lowassa alihama CCM baada ya jina lake kukatwa katika mchakato wa kuwania urais, alihamia Chadema na kupewa nafasi ya kugombea urais katika uchaguzi unaotajwa kuwa na ushindani mkali zaidi tangu kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatatu ya Novemba 21

Rais Magufuli ateua Naibu Kamishna Mkuu wa TRA

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, jana tarehe 20 Novemba, 2016 amemteua Bw. Charles E. Kichere kuwa Naibu Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Bw. Charles E. Kichere anajaza nafasi ya Naibu Kamishna Mkuu wa TRA iliyokuwa wazi kwa zaidi ya mwaka mmoja.

Uteuzi huu umeanza mara moja.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

Bibi amlisha kinyesi mjukuu wake Jijini Mwanza

$
0
0

Mtu mmoja aliyejulikana kwa jina la Amina Hamisi (56) mkazi wa mtaa wa mahina kata ya Butimba Jijini Mwanza, anashikiliwa na polisi baada ya kumlazimisha mjukuu wake aliyejulikana kwa jina la Rehema Sadiki mwenye umri wa miaka 7 kula kinyesi.

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza Kamishina Msaidizi wa Polisi Augustino Senga amedai kuwa tukio hilo limetokea Novemba 11, mwaka huu ambapo mtoto huyo alikwenda chooni kujisaidia na kushindwa kumwagia maji ili kuondoa kinyesi chake ndipo bibi yake ili kumuadhibu alimuamuru kula kinyesi hicho kitendo ambacho mtoto huyo alikitekeleza.

Baada ya tukio hilo kutokea raia wema walitoa taarifa polisi ambao walifika eneo la tukio na kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo.

Kamanda Senga ametoa wito kwa wakazi wa jiii la Mwanza kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi ili kudhibiti vitendo vya kikatili hasa kwa watoto wadogo na kuongeza kuwa ukatili ni kosa kisheria hivyo wananchi waache kufanya vitendo hivyo na watakao bainika sheria itachukua mkondo wake.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images