Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Kesi ya Akina Zombe: Mrakibu wa Polisi (SP) Bageni Apinga Hukumu ya Kunyongwa Hadi Kufa

$
0
0


Aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi Wilaya ya Kinondoni, Mrakibu wa Polisi (SP),Christopher Bageni amewasilisha maombi Mahakama ya Rufaa ya Tanzania kupinga adhabu ya kunyongwa hadi kufa.

SP Bageni alihukumiwa adhabu hiyo baada ya mahakama hiyo kujiridhisha kwamba aliwaua kwa kukusudia wafanyabiashara wanne wa madini kutoka Mahenge mkoani Morogoro na dereva teksi mkazi wa Manzese, Dar es Salaam,  katika Msitu wa Pande.

Bageni kupitia Wakili wake, Gaudioz Ishengoma,  aliwasilisha maombi hayo mwishoni mwa wiki yaliyoambatana na hati ya kiapo iliyoapwa na wakili huyo.

Muwasilisha maombi anaomba mahakama hiyo kuifanyia marejeo hukumu dhidi yake iliyotolewa Septemba 13 na kusomwa  Septemba 16 mwaka huu na Msajili wa Mahakama hiyo, John Kahyoza.

Akitoa sababu kuomba marejeo, anadai  alinyimwa haki sawa ya kusikilizwa wakati wa kutathmini ushahidi ulioko kwenye kumbukumbu za mahakama kwa kuegemea kwenye ushahidi wa upande wa mashtaka.

Alidai katika kuchanganua ushahidi ambao uamuzi wa mahakama uliegemea, mahakama ilishughulika na ushahidi wa msingi (Exam in Chief) wa upande wa mashtaka na iliangalia kwa juu juu tu ushahidi wa utetezi hususan wa Bageni au haikuutazama kabisa.

“Kuna kukinzana kwa haki kwa maana ya kwamba mtoa maombi alinyimwa haki sawa ya kusikilizwa, kwa mahakama kuchagua na kuegemea   upande wa mashtaka pekee na kushindwa kuzingatia ushahidi wa upande wa utetezi, hasa wa mtoa maombi.

“Uamuzi wa mahakama umetolewa katika msingi wa makosa ya dhahiri kwenye kumbukumbu za mahakama, hivyo kusababisha upotoshaji wa haki, kushindwa kuzingatia mwongozo wa kanuni katika asili, thamani na matumizi ya ushahidi wa kuungwa mkono,” ilisema sehemu ya maombi hayo.

Alidai kuwa kwa kushindwa kuchanganua na kutathmini  ushahidi kwa umakini kwenye kumbukumbu, mahakama ilishindwa kuainisha ushahidi wa mjibu rufaa wa nne (Bageni)  kimazingira kama ilivyo ni dhahiri unakosa thamani ya kuhitaji ushahidi wa kuunga mkono na hivyo si salama kuegemea katika kumtia hatiani.

“Kwa kushindwa kuona na kuzingatia ushahidi uliokusudiwa kuwa na ushahidi wa kuunga mkono, siyo ushahidi huru na hauna mashiko kuthibitishwa (PW27) na haupo (PW36).

“Kwa kushindwa kufanya uchambuzi wa ushahidi kwenye kumbukumbu kwa umakini wenye manufaa, vinginevyo mahakama ilipaswa kuona wajibu wa kuthibitisha shtaka kwenye jinai haukufikiwa,”anasema Wakili Ishengoma.

Anadai mahakama katika kuamua, kama ilivyofanya katika uhalisia wake, kuhusu ushiriki wa mtoa maombi katika eneo la tukio la uhalifu, ilishindwa kubaini katika ujumla wake ushahidi wa upande wa mashtaka ambao haukuweza kuthibitisha mashtaka bila kuacha shaka.

Ishengoma alidai mahakama haikuuchukulia ushahidi kwenye kumbukumbu katika ujumla wake hivyo kutengua uamuzi wa kuachiwa huru kwa mtoa maombi na kumtia hatiani na kuhukumiwa adhabu ya kifo kwa kusimamia ushahidi ambao haupo na uvumi pamoja na ushahidi wa mashaka makubwa.

Alidai kutokana na hukumu ya mahakama, haikuwa bayana ni kwa ushahidi wa nani ulithibisha mtoa maombi Bageni alimwezesha au kumsaidia nani katika mauaji ya marehemu hao.

Katika hati ya kiapo iliyoapwa na Wakili Ishengoma, Bageni anadai yeye na wengine wanane ambao hawako katika maombi hayo walishtakiwa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kwa makosa ya mauaji ya watu wanne katika Kesi ya jinai namba 26 ya mwaka 2006.

Bageni alikuwa mshtakiwa wa pili na katika hukumu iliyotolewa na Jaji Salum Massati, amnayo  wote waliachiwa huru, lakini Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) hakuridhishwa na uamuzi huo hivyo alikata rufaa namba 358 ya mwaka 2013.

Kabla ya usikilizwaji wa rufaa hiyo, DPP aliwaondolea rufaa wajibu rufaa watano na kubaki wajibu rufani wanne ambao waliachiwa huru pia Septemba 16, mwaka huu.

Walioachiwa huru ni aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Dar es Salaam (RCO) Kamishna Msaidizi wa Polisi Abdallah Zombe na maofisa wengine wawili baada ya mahakama kuona hakuna ushahidi wa wazi ama mazingira kuwatia hatiani.

Katika kesi ya msingi, Bageni alidaiwa kuwaua kwa kukusudia wafanyabiashara Sabinus Chigumbi, maarufu Jongo na ndugu yake, Ephrahim Chigumbi, Mathias Lunkombe na Juma Ndugu, aliyekuwa dereva wa teksi wa Manzese , Januari 14, mwaka 2006, katika Msitu wa Pande, Mbezi Luis, Dar es Salaam.

Kidato cha Pili Waanza Mitihani leo

$
0
0
Wanafunzi wa kidato cha pili nchini wameanza kufanya mitihani yao ya upimaji leo katika shule za sekondari 4,669 zilizopo Tanzania Bara.

Jumla ya wanafunzi 435,221 wamesajiliwa kufanya mitihani hiyo wakiwamo 67 wasioona na 306 wenye uoni hafifu.

Mbali na mitihani hiyo, Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa (Necta), Dk Charles Msonde amesema mtihani wa Taifa wa darasa la nne utafanyika Novemba 23 na 24, mwaka huu.

"Mitihani hii inafanyika katikati ya mafunzo ili kubaini changamoto zilizopo na kutafuta namna ya kuboresha mafunzo hayo," amesema Dk Msonde.                      

Wakati huo huo, Dk Msonde amefafanua kuwa mafunzo ya ualimu wa shule ya msingi ngazi ya stashahada yamefutwa lakini wanafunzi waliopo vyuoni watamalizia masomo yao kwa muda uliobaki.

Dk Msonde amesema mafunzo hayo ya walimu yataendelea kwa utaratibu wa zamani ambao ulikuwa ngazi ya cheti.

Amesema usimamizi wa mitihani hiyo itakuwa chini ya Necta kama ilivyokuwa zamani badala ya Nacte.

"Wanafunzi walio vyuoni wataendelea na mafunzo hayo, isipokuwa kuanzia mwaka huu hatutadahili kwa ngazi ya diploma, tutadahili ngazi ya cheti kama ilivyokuwa zamani," amesema Dk Msonde. 

Wadaiwa Sugu Bodi ya Mikopo wapewa siku 30

$
0
0

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Mkurugenzi Mtendaji wa bodi hiyo Abdul-Razaq Badru amesema kuwa hadi sasa kuna jumla ya wadaiwa sugu 142,470 wenye mikopo ya shilingi 239,353,750,170.27 iliyokwishaiva hawajajitokeza wala kuanza kulipa mikopo yao.

Akitolea ufafanuzi wa maana ya neo "Wadaiwa Sugu", Badru amesema kuwa ni wanufaika waliokopeshwa, muda wa matarajio ukapita bila kuwasilisha taarifa zao na kulipa madeni ya mikopo waliyokopeshwa tangu mwaka wa masomo 1994/1995.

Kuhusu hatua zinazochukuliwa na bodi hiyo, Badru amesema mbali na kutoa siku 30, bodi hiyo inakamilisha taratibu za kuwafikisha mahakamani kwa kuvunja sheria ya bodi ya mikopo kifungu cha 19A(1).

Hatua nyingine ni pamoja na kuyawasilisha majina hayo katika taasisi za mikopo, kuwasiliana na wadhamini wao pamoja na kuyatangaza hadharani majina ya wadaiwa sugu wote ili waajiri, wadhamini na wadau wengine wayajue na kutoa taarifa katika bodi hiyo.

Kuhusu takwimu za mikopo iliyotolewa, amesema tangu 1994/95 hadi 2015/16 jumla ya shilingi 2,595,932,575.56 zimekopeshwa kwa jumla ya wanufaika 379,179.

Amesema kati ya mikopo yote iliyokopeshwa, mikopo iliyoiva ni shilingi 1,425,708,285,046.48 kwa wanufaika 238,430 ambao tayari wamemaliza kipindi chao cha matazamio.

Badru amesema kuwa jumla ya wanufaika wa mikopo 93,500 wamebainika na kupelekewa ankara za madeni yao, ambapo kati yao wanufaika 81,055 wanaendelea kulipa.

RIWAYA: She is My Wife- Sehemu ya 39 & 40

$
0
0
Mwandishi: EDDAZARIA G.MSULWA

ILIPOISHIA
Bwana Rusev aliendelea kutoa maelezo ya Hotel atakayo fikizia bwana Paul Henry Jr, akaonyesha kila sehemu ambayo bwana Paul Hery Jr atapita akiwa na watu wake wanao mlinda. Hadi mwisho wa maelekezo yake, wote wakawa wamemuelewa vizuri bwana Rusev.
“Agnes hii ni kazi yako ya kwanza na sinto hitaji ukosee, ninakuamini sana”
“Usijali mkuu nipo kwa ajili yako”      
“NITAHITAJI UMUUE KIONGOZI HUYU IWE TISHIO KWA NCHI HII NA DUNIA NZIMA”
“SAWA MKUU”
Agnes alijibu huku akiinamisha kichwa chake chini kama ishara ya kumuheshimu bwana Rusev, kisha bwana Rusev akachuku moja ya chini yenye alama ya X na kumvisha Agnes shingoni, akampa Baraka kwa ajili ya kuitekeleza kazi hiyo hatari sana kwa maisha yake.
                                                                                 
ENDELEA
Agnes akaanza kazi moja ya kulenga shabaha kwa masafa ya mbali pasipo kutumia lensi inayo saidia kuweza kuvuta vitu karibu, kila anacho kilenga kwa kutumia bunduki yake aina ya AS50 Sniper rifle, yenye uzito wa kila zaidi ya kumi na tano ikiwa na risasi zilizo jaa, akahakikisha anakipata vizuri huku akiwa ameishika mkononi mwake, jambo ambalo lilizidi kuwashangaza wengi kwani, hii ni bunduki ambayo mara nyingi mtu huwa anaiweka chini na kuisimamisha kupitia vimiguu viwili vya chuma, ili kuweza kulenga shaba.

“Waooooo”
Fetty alimpigia makofi Agens, baada ya kumkuta akiwa analenga vitu vya mbali kwa bunduki hiyo. Agnes baada ya kumuona Fetty akaacha zoezi lake ambalo analo kifanya
“Mwanangu kweli unatisha, hii ngoma ni nzito”
Fetty alizungumza huku akiinyanyua bundiki aliyo ishika Agnes
“Inahitaji mazoea kuweza kuitumia la sivyo unaweza ukafa, kwa maana ninapiga hadi nasikia mapigo ya moyo yanacheza kama kitenesi”

“Hahahaa, sas mtu wangu si uiweke chini ndio upige?”
“Ahaaa chini najiona kama nakosa shabaha vile”
“Ok tuachanane na hayo, vipi maandalizi yako ya kwenda kwenye hiyo mission?”
“Ndio kama hivi unavyo niona nazidi kujikaza, kwa maana nikicheza vibaya nakufa au nakamatwa na nisinge penda kukamatwa na wamarekani, ni bora nijipige risasi nife hapo hapo”
Maneno ya Agens yakamfanya Fetty kukaa kimya huku akimtazama Agnes usoni mwake, jinsi anavyo mwagikwa na jasho jingi.
 
  ***
Kila mmoja ndani ya maabara akaka kimya huku akimtazama Rahab, jinsi anavyo mchunguza mtu mmoja baada ya mwengine. Rahab akaachia tabasamu pana kisha akapiga hatua na kuingia ndani kabisa ya maabara huku nyuma yake akiingia mume wake pamoja na bosi wa bwana Frednando

“Jamani asanteni kwa ushirikiano wenu kwa kuweza kunihudumi hadi nimekuwa sawa”
Rahab alizungumza kwa furaha kubwa, ikamlazimu Frednando kuweza kuitafsiri kwa kispain. Madaktari walitabasamu kwa uwoga ila mioyoni mwao kila mmoja alikuwa akiliwazia lake kuhusiana na mbwa aliye fufuka dakika chache zilizo pita. Rahabu pasipo kuambiwa na mtu yoyote akaingia kwenye chumba alicho fungiwa mbwa huyo na kumchuku.

“Jamani mbwa huyu nimependa, anaitwa nani?”
Rahab akawauliza madaktari walio baki na mshangao mkubwa, kwa kingeraza ila mmoja wao akajikaza na kuzungumza kwa sauti ya utaraitibu.
“Anaitwa Charity”
“Waoo nitamchukua nimempenda sana”
Hakuana aliye kuwa na ubishi kuhusiana na kuchukuliwa kwa mbwa huyo, waliye mfanyia majaribio, ila kila daktari akabaki kimya. Hapakuwa na daktari aliye weza kuzungumza kwa kile walicho weza kukiona.

Wakarudi katika jumba la Frednando ambapo ikawalazimu kuwasiliana na ubalozi wa Tanzania uliopo nchini Mexco. Balozi baada ya kupokea simu ya raisi Praygod Makuya, ikamlazimu kuongozana na baadhi ya askari wa jeshi la Tanzania hadi kwenye jumba la Frednando, baada ya kufika wakapokelewa vizuri kama ilivyo kuwa kwa raisi wao.
“Yaani raisi siamini kama upo hai?”
Bi Joyce Maagi alizungumza huku akimtazama raisi Praygod machoni mwake.

“Nipo hai, nasikia nchini watu wapo kwenye maombolezo ya kifo change?”
“Ndio muheshimiwa hapa mwenyewe nilikuwa nimebakisha siku mbili niende kwenye msiba wako”
“ Ok ila sinto hitaji muweze kuzungumza kitu chochote kuhusiana na kuniona kwangu, nitahitaji kurudi siku ya mazishi yangu ninaamini nitakuwa Tanzania”
“Ila kikubwa ninacho hitaji wewe kukifanya nitengenezee mazingira katika uwanja wa ndege kwani nitakuja na private airplane(Ndege binafsi), wajulishe baadhi ya watu watakao nipokea kisiri mimi na mke wangu pasipo watu wengine kuweza kutambua lolote”

“Sawa muheshimiwa ila kuna swala la mke, si tayari amesha fariki au kuna mwengine”
“Yupo”
Raisi Praygod akamngong’oneza mmoja wa wahudumu Frednando na kumuagiza akamuite Rahab, naye akafanya hivyo. Baada ya muda Rahab akafika sebleni, akiwa amevalia gauni jeupe na refu lililo mpendeza sana. Bi Joyce Maagi akusita kumshangaa Rahab, kwani picha yake ipo kwenye moja ya watu wali angamia na ndege ya raisi.

“Huyu binti naye pia amepona?”
“Ndio amepona, ni mmoja wa watu walio weza kuyapigania maisha yangu hadi hapa nilipo”
“Ahaa”
Bi Joyce Maagi akanyanyuka na kwenda kusalimiana na mke wa rais, kwa heshima zote. Wakaendelea na mazungumzo ya kawaida. Siku iliyo fwatia Bi Joyce Maagi akaondoka akiwa na masafara wake kuelekea nchini Tanzania, kitu cha kwanza baada ya kutua katika uwanja wa mwalimu Jk Nyerere, akafanya maagizo yote aliyo agizwa na Raisi Praygod Makuya, japo baadhi ya watu walishangaa kusikia kwamba Raisi Praygod yu hai.

Maandalizi ya safari ya kurudi Tanzania, yakawekwa tayari na Frednando, akahakikisha kwamba kila kitu kipo salama na hakuna jambo baya ambalo litamdhuru raisi Praygod Makuya pamoja na mke wake. Ikawa ni siku nyingine ya huzuni kwa marafiki wawili Praygod na Frednando, kila mmoja Alisha mzoea mwenzake kwa kipindi kifupi walicho ishi, ila hapakuwa na jinsi yoyote yakufanya. Iliwalazimu kuweza kutengana tena na kila mmoja aweze kuendelea na majukumu yake anyo yafahamu.

“Shem siku une ikuli Tanzania”
Rahab alizungumza kwa furaha baada ya kuwaona Praygod na Frednando wakiwa wanalengwa lengwa na machozi ya uchungu
“Usijali Shem, nitakuja siku naamini nikija mutakuwa mumepata kijana mdogo”
“Hahaaa Mungu ni mwema, ombeni Mungu niwazalie kijana wa kiume ili aja kuwa raisi kama baba yake”
“Kwa nini usituzalie wa kike ili awe raisi labda wa kwanza, mwanamke kwa miaka hiyo ijayo?”
“Sawa Mungu ni mwema anaweza kutuwezesha katika hilo”
“Haya jamani niwatakie safari nje, ndege imesha washwa, hiyo mutaitumia katika matumizi yenu binafsi”

Rais Dkt. Magufuli Akutana Na Kufanya Mazungumzo Na Rais Mstaafu Wa Afrika Kusini Thabo Mbeki Ikulu

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumanne ya Novemba 15

Madini ya Bilioni 3 Yakamatwa Yakitoroshwa

$
0
0

Siku chache baada ya Rais John Magufuli kusema kuna utoroshaji mkubwa wa madini kupitia viwanja vya ndege vilivyopo migodini, Wakala wa Ukaguzi wa Madini Tanzania (TMAA) umekamata madini yenye thamani ya Sh3,353,421,381.4 yakitoroshwa katika viwanja vikubwa vya ndege na katika matukio 25 tofauti.

Ofisa Mtendaji Mkuu wa TMAA, Mhandisi Dominic Rwekaza ameeleza hayo katika ripoti ya ukaguzi iliyofanywa na wakala huo mwaka 2015 akisema: “Katika kufuatilia usafirishaji wa madini nje ya nchi katika viwanja vikubwa tulikamata madini yanayotoroshwa yenye thamani ya Dola za Marekani 1,512,186.61 na mengine ya Sh34,670,794 katika matukio 25 tofauti.” 

Akizungumza na wahariri wa vyombo vya habari nchini hivi karibuni jijini, Rais Magufuli alisema pamoja na kwamba Tanzania ina utajiri mkubwa wa madini, kumekuwa na utoroshwaji wa madini kwa ndege zinazoruka kutoka kwenye baadhi ya migodi.

“Tuna dhahabu ambazo zinachimbwa, lakini utakuta watu wanasafirisha makontena ya mchanga unapelekwa kwenda kusafishwa na sisi ndiyo tunasindikiza na wananchi mpo mnashangilia,” alisema Rais Magufuli.

“Kwa sababu kule wanakwenda ku-separate (kutenganisha). Kwa nini tusijenge separation plant hapa tukatengeneza ajira hapa kwa Watanzania,” alihoji. 

Viwanja vya ndege migodini 
Hata hivyo, wakala huo umesema suala la migodi mikubwa kuwa na viwanja vya ndege kwa ajili ya kusafirishia madini haliepukiki kwa sababu za kiusalama.

Akifafanua ripoti ya ukaguzi wa madini ya mwaka 2015, Msemaji wa TMAA, Isambe Shiwa alisema licha ya kudhibiti utoroshwaji huo viwanja vya ndege vinatumika kusafirishia madini kutoka migodini moja kwa moja kwa sababu za kiusalama.

“Katika maeneo yote ya madini, kuna mawakala wa ukaguzi wa madini, wanashuhudia uzalishaji wa madini, hasa kwa dhahabu wana chukua mikuo (mche wa dhahabu) yake na kuileta kwenye maabara zetu ili ipimwe kujua kiasi cha dhahabu na fedha kisha wanakokotoa mrabaha kulingana na madini husika,” alisema.

“Ili kujua faida ya madini katika mgodi husika, huwa tunafanya ukaguzi yakinifu na kukokotoa kodi zinazotakiwa hasa kodi ya shirika. Kama kuna utata kwenye taarifa za mgodi kuhusu ununuzi wa vifaa na mitambo, tunakagua na kuweka wazi gharama zake kisha tunapeleka TRA kiasi kinachotakiwa kulipwa.”

“Kwa mfano ukiangalia bei ya madini ya dhahabu, kwa wastani gramu moja huuzwa Sh100,000, hivyo kilo moja huuzwa Sh1 bilioni.Ule mkuo mmoja una kilo 20 hadi 25. Unaweza kuviweka vile vipande kwenye mkoba ila ni vizito kubeba. Ukishazalisha hadi mikuo 20 ya dhahabu unabeba mabilioni ya fedha, utasafirishaje kwa gari?

“Kuna wakati pale mgodi wa Geita (GGM) kulikuwa na ndege iliyobeba dhahabu, kumbe tayari watu walishatoa taarifa nje kwa watu waliojitayarisha na silaha za kivita, wakaitungua ilipokuwa ikiruka. Bahati nzuri rubani aliimudu na kufanikiwa kuirudisha uwanjani.”

Alisema kutokana na matukio hayo, sasa wanasafirisha madini kwa helikopta ambayo ikichukua mzigo hupaa kwenda juu zaidi kisha kwenda Dar es Salaam ambako hukaguliwa tena kabla ya kwenda nje ya nchi.

“Kutokana na ukaguzi unaofanyika, naweza kusema hakuna madini wala mchanga unaosafirishwa kwa wizi kwenye migodi yote.Kwanza hii migodi inamilikiwa na wana hisa walioko ndani na nje ya nchi. Wao nao wanataka kupata taarifa za ukaguzi wetu ili wajue wanalipa kodi kiasi gani na wanapata nini,” alisema.

Akizungumzia sababu za madini ya tanzanite kuuzwa zaidi na Kenya, Afrika Kusini na India, Shiwa alisema ni kutokana na Sheria ya Madini ambayo hukata mrabaha wa asilimia tano ya madini hayo wakati sheria ya nchi hizo haina, hivyo kuvutia zaidi wasafirisha madini kupitia nchi hiyo.

“Baada ya kugundua udhaifu huo, kamishna wetu wa madini na ofisa mtendaji wetu mkuu walikwenda Kenya kuzungumza nao ili nao waweke mrabaha huo na kweli waliweka. Hivyo kwa miaka minne iliyopita madini hayo yamepungua sana Kenya,” alisema.

Alisema wamechukua pia hatua ya kuongeza thamani ya madini hayo kwa kuyakata baada ya kujenga viwanda mkoani Arusha hivyo kupunguza usafirishaji wa madini ghafi kupitia Kenya, Afrika Kusini na India.

DPP amwondolea mashtaka mbunge wa Sumve Mhe Richard Ndassa

$
0
0
Hatimaye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam imemwachia huru Mbunge wa Sumve (CCM),  Richard Ndassa (56) baada ya upande wa Jamhuri kuomba kumuondolea kesi  kushawishi na kuomba  rushwa ya Sh.milioni 30.
 
Ndassa alikuwa anakabiliwa na shtaka la kushawishi na kuomba rushwa kutoka  kwa Mkurugenzi wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), Felichesmi Mramba.
 
Mwendesha Mashtaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dennis Lekayo jana aliwasilisha maombi ya kumwondolea Ndassa mashtaka mbele ya Hakimu Mkazi Victoria Nongwa.

Lekayo alidai kuwa Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini (DPP), ameona hana nia ya kuendelea na mashtaka yaliyopo mahakamani dhidi ya mshtakiwa chini ya kifungu cha 98 (a) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA).
 
Aidha kwa mujibu wa kifungu hicho kinampa mamlaka DPP ya kumwondolea mashtaka mtuhumiwa kabla ya kusikiliza ushahidi lakini anaweza kukamatwa na kushtakiwa upya.
 
Hakimu Nongwa alisema kwa kuwa upande wa Jamhuri umeomba kumwondolea mshtakiwa mashtaka na kwamba hawana nia ya kuendelea na kesi hiyo, mahakama yake imekubali ombi hilo.
 
"Mahakama hii inamwachia mshtakiwa chini ya kifungu cha 98 (a) kama upande wa Jamhuri ulivyowasilisha maombi yao dhidi ya mshtakiwa" alisema Hakimu Nongwa.
 
Mapema mwaka huu,  Mbunge huyo ambaye pia ni mjumbe wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji  ya Umma, alifikishwa mahakamani hapo na kusomewa shtaka la kushawishi na kuomba rushwa ya Sh. milioni 30.
 
Katika kesi ya msingi, Lekayo alidai kuwa Machi 13, mwaka huu, jijini Dar es Salaam,  Ndassa aliomba rushwa Sh.milioni 30 kutoka kwa Mramba.
 
Ilidaiwa kuwa aliomba rushwa ili awashawishi wajumbe wenzake wa kamati hiyo  watowe mapendekezo mazuri  katika mahesabu ya fedha ya Tanesco kwa mwaka wa fedha 2015/2016.
 
Katika shitaka la pili, mwakilishi huyo wa wananchi siku ya tukio la kwanza pia aliomba rushwa ya huduma ya umeme kwa kumshawishi Mramba atowe huduma hiyo kwa ndugu wa mbunge huyo Matanga Mbushi,Richard Ndassa na rafiki wa ndugu yake Lameck Mahewa.
 
Mbunge huyo alikana mashitaka yake na alikuwa nje kwa dhamana.


TB Joshua avunja ukimya kuhusu utabiri wake kuwa Clinton angeshinda Urais

$
0
0

Siku kadhaa baada ya utabiri wa TB Joshua kuwa Hillary Clinton angeshinda urais wa Marekani kuwa tofauti, hatimaye mhubiri huyo maarufu wa Nigeria ametoa ufafanuzi kuhusu kilichotokea.

Awali, TB Joshua aliwaambia waumini wake kuwa aliona ndotoni kuwa Rais wa Marekani atakayechaguliwa atakuwa mwanamke na kwamba atakumbwa na changamoto nyingi ikiwemo jaribio la kutaka kumuondoa madarakani kwa kura za kutokuwa na imani naye.

Mhubiri huyo ametumia ukurasa wake wa Facebook na Twitter kuutetea utabiri wake akidai kuwa Clinton alishinda kupitia kura za jumla, kwa kupata kura nyingi zaidi ya Donald Trump.

“Tumeona matokeo ya uchaguzi wa Marekani. Kwa kusoma, utagundua kuwa [utabiri]ule ulikuwa kuhusu kura za jumla (popular votes), kura za wamarekani wengi,” unasomeka ujumbe wa TB Joshua.

“Katika hali hii, tunahitaji roho ya kinabii kutambua au kujua unabii. Viwango vyetu ni tofauti. Hatuko kwenye viwango sawa. Tunaweza kuwa na makanisa makubwa, kengele kubwa, na shughuli zote ambazo ni nzuri kwa viwango vya kibidamu lakini uwezo wa binadamu una kikomo,” aliongeza.

Alitumia pia Biblia Takatifu kuupa nguvu utetezi wake, akitaja maandiko ya 1 Wakorinto 1: 25, “Maana kinachoonekana kuwa ni upumbavu wa Mungu, kina busara zaidi kuliko hekima ya binadamu; na kinachoonekana kuwa ni udhaifu wa Mungu, kina nguvu zaidi kuliko nguvu za binadamu.”

Clinton alishinda kwa kupata kura nyingi zaidi za Wamarekani (popular votes) lakini alishindwa katika kura za majimbo muhimu (electoral votes). Mgombea wa Republican ambaye tafiti nyingi hazikumpa nafasi, alishinda uchaguzi huo na kuishangaza dunia.

Trump anatarajiwa kuapishwa rasmi kuwa Rais wa Marekani, Januari mwakani.

Mfanyakazi wa ndani Amliza Bosi Wake Vitu vya Milioni 85

$
0
0
Mfanyakazi wa ndani wa Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki, Angella Kizigha, Miraji Mkanga (41) amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni, Dar es Salaam kwa madai ya kumwibia mwajiri wake vitu ikiwemo bastola yenye risasi 23, simu, mikufu na bangili za dhahabu, vyote vikiwa na thamani ya zaidi ya Sh milioni 85.

Akisomewa mashitaka hayo na Karani Dayz Makalala mbele ya Hakimu Joyce Mushi, ilidaiwa kuwa mshitakiwa Mkanga alitenda kosa hilo Oktoba 2, mwaka huu maeneo ya Kijitonyama wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Makakala alidai mtuhumiwa huyo aliiba Dola za Marekani 3,500 zenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 7.5, bangili za dhahabu gramu 300 zenye thamani ya Sh milioni 36, hereni gramu 450 zenye thamani ya Sh milioni 42, doti 30 za vitenge zenye thamani ya Sh milioni 1.5 na shuka 10 zenye thamani ya Sh 700,000.

Aidha, mfanyakazi huyo wa ndani anatuhumiwa kuiba bastola moja iliyotengenezwa Jamhuri ya Czech yenye namba No B 283994 na risasi 23 thamani ya Sh milioni mbili, simu mbili za Samsung zenye thamani ya Sh 500,000 na nguo tofauti zenye thamani ya Sh 750,000 mali ya mbunge huyo ambaye ni kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Mshitakiwa alikana shitaka hilo wakati huo dhamana yake ipo wazi, akitakiwa kuwa na wadhamini wawili kutoka katika taasisi inayotambulika na kusaini hati ya dhamana ya Sh milioni tano kila mmoja.

Kesi hiyo inatarajiwa kutajwa tena Novemba 28, mwaka huu, na mshitakiwa alirudishwa rumande kutokana na wadhamini wake kutofika huku upelelezi ukiendelea.

Mahakama ya Mafisadi yaendelea kupiga kazi....Yatupilia Mbali Pingamizi la DPP Dhidi ya Watanzania na Mchina Mmoja

$
0
0

Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi maarufu kama Mahakama ya Ufisadi imetupilia mbali pingamizi lililowekwa na Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kuhusu mamlaka iliyonayo katika kutoa dhamana kwa washtakiwa wa makosa ya rushwa.

Uamuzi huo ulitolewa jana na Jaji Mfawidhi wa mahakama hiyo Rehema Mkuye aliyesikiliza pingamizi la DPP dhidi ya maombi ya dhamana yaliyowasilishwa na washtakiwa wawili wa kesi ya Uhujumu Uchumi, wanaokabiliwa na kesi hiyo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu. Washtakiwa hao ni Mtanzania, Jeremiah Madar Kerenge (40) pamoja na Fu Chang Feng (50), raia wa China, na Ally Damji Raza (34) raia wa India, ambao wanadaiwa kukutwa na nyavu haramu za kuvulia samaki zenye thamani ya jumla ya Sh22, 978,750,000.

Kerenge na Raza waliwasilisha maombi ya dhamana katika Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, lakini DPP aliweka pingamizi akidai maombi hayo yamefunguliwa kwenye mahakama isiyo sahihi. 

Wakati wa usikilizwaji wa pingamizi hilo Novemba 3, DPP kupitia kwa Wakili wa Serikali Mkuu (PSA) Vitalis Timon alifafanua kuwa sheria inataka maombi hayo yafunguliwe Mahakama Kuu na siyo katika Mahakama ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi.

Hata hivyo, katika uamuzi wake jana, mahakama hiyo ilitupilia mbali pingamizi hilo la DPP na ikasema kuwa ina uwezo na kwamba mahakamani hapo ndipo mahali sahihi pa kufungua maombi ya dhamana kwa washtakiwa wote wa kesi za rushwa na uhujumu uchumi.

Kuhusu kifungu cha 29 (4) (d) cha Sheria ya Makosa ya Uhujumu Uchumi kinachoonyesha kuwa Mahakama Kuu ya kawaida ndio yenye mamlaka ya kutoa dhamana kwa washtakiwa wa rushwa au uhujumu uchumi, Jaji Mkuye alisema kuwa kuna makosa.

Alifafanua kuwa kinachoonekana katika kifungu hicho ni usahaulifu tu wa Bunge na kwamba nacho kilipaswa kufanyiwa marekebisho, kitamke kuwa maombi ya dhamana katika kesi ya rushwa na uhujumu uchumi, lazima yafunguliwe katika Divesheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi.

Alisema kuwa kwa kuwa divisheni hiyo ina ofisi katika kila Kanda ya Mahakama Kuu, ambako pia tayari kuna majaji maalumu walioteuliwa kushughulikia kesi na maombi ya dhamana ya kesi za rushwa na uhujumu uchumi, hivyo hakuna hofu yoyote ya mlundikano wa wananchi kusubiria maombi yao.

Wakati wa usikilizwaji wa pingamizi hilo Novemba 3, Wakili Vitalis alidai kuwa mahakama hiyo inakuwa na uwezo wa kutoa dhamana pale tu ambapo kesi ya msingi inakuwa tayari imeshafunguliwa kwenye mahakama hiyo.

Hata hivyo, wakili wa washtakiwa hao, Roman Lamwai alipinga hoja hizo akidai kuwa mahakama hiyo ndio mahali sahihi kwa mujibu wa tafsri ya Sheria ya Uhujumu Uchumi kama ilivyofanyiwa marekebisho.

Alisisitiza kuwa hata ukubwa wa kiwango cha pesa katika hati ya mashtaka kwenye kesi hiyo ni lazima maombi hayo yafunguliwe katika mahakama hiyo ambavyo ndio yenye jukumu la kusikiliza na kuamua kesi za Rushwa na Uhujumu Uchumi.

Baada ya Mahakama kutupilia mbali pingamizi hilo, iliendelea kusikiliza maombi ya dhamana ambapo Wakili Lamwai aliieleza mahakama kuwa mashtaka yanayowakabili washtakiwa hao yanadhaminika na kwamba wote wako tayari kutekeleza masharti ya dhamana.
 
Lamwai alidai kuwa mtoa maombi wa kwanza (Kerenge) ana mke ambaye ni mjamzito hivyo anahitaji kuwa naye karibu kumhudumia. 

Kuhusu mtoa maombi wa pili (Raza), alidai kuwa mashtaka mawili yote yanayomkabili hayaangukii kwenye sheria ya Uhujumu uchumi, lakini kwa kuwa yameambatanishwa kwenye kesi ya uhujumu uchumi basi dhamana yake ilikuwa vigumu katika mahakama ya chini.

Aliongeza kuwa yeye ni mfanyabiashara anayefanya biashara zake Dar es Salaam ambako pia ndiko aliko na makazi yake ya kudumu hivyo hawezi kuruka dhamana.

Akijibu hoja za maombi hayo, Wakili Timon alidai kuwa baada ya pingamizi lao kutupiliwa mbali, hawana pingamizi kuhusu dhamana, kwa kuwa mashtaka yanayowakabili yanadhaminika na pia dhamana ni haki yao.

Hata hivyo aliikumbusha mahakama kuwa wakati wa kutoa dhamana izingatie kifungu cha 36 (5) cha Sheria ya Uhujumu Uchumi kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2016.

Kwamba kwa mujibu wa kifungu hicho, watoa maombi wanalazimika kuwasilisha mahakamani pesa taslimu au hati ya mali yenye thamani sawa na nusu ya pesa inayotajwa kwenye hati ya mashtaka, kwa utaratibu wa kanuni ya kugawana au kuchangia wote kiwango hicho cha pesa.

Baada ya kusikiliza hoja za kila upande, Jaji Mkuye aliahirisha shauri hilo hadi kesho atakapotoa uamuzi wa dhamana kwa washtakiwa hao. 

Katika kesi ya msingi namba 45 ya mwaka 2016, inayosikilizwa na Hakimu Mkazi Mkuu, Godfrey Mwambapa wa Mahakama ya Kisutu, inadaiwa walikutwa na nyavu ambazo zimepigwa marufuku kutumika wala kuhifadhiwa nchini zenye thamani ya jumla ya Sh22, 978,750,000.

Makamu wa Rais Samia Suluhu Aokoa Milioni 33 Kwa Kupanda ndege ya ATCL kwenda Mwanza

$
0
0
Katika  kuendelea kujenga dhana ya kubana matumizi ya fedha za serikali, Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan amesafiri kwa ndege ya abiria ya Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL) kutoka Dar es Salaam kwenda Mwanza na kuokoa zaidi ya Sh milioni 33.

Kabla ya kuanza safari hiyo jana kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) jijini Dar es Salaam, Makamu wa Rais akizungumza na waandishi wa habari, alisema kwa kupanda ndege hiyo ameokoa fedha za serikali na kodi za wananchi.

Alisema ameona ashirikiane na Watanzania kuonesha uzalendo kwa kutumia huduma ambazo zinatolewa na serikali na kuwataka Watanzania wote kutumia ndege hizo.

“Ningepanda ndege ya kukodi ningetumia shilingi milioni 40 kwa safari hii, lakini nikaona hapana nikaamua mimi pamoja na msafara wangu tutumie ndege hii ya Shirika la Ndege Tanzania ambapo tumetumia Shilingi milioni 7.6 pekee,” alisema Makamu wa Rais aliyeambatana na watu 16 katika safari hiyo.

Makamu wa Rais ambaye alipanda ndege hiyo pamoja na abiria wengine wa kawaida, aliwataka viongozi wengine pia kufuata mfano huo kusafiri kwa kutumia ndege za shirika hilo.

Alisema ameona kwenye televisheni watu wakitoa maoni yao juu ya kampuni hiyo ya ndege kuwa ni nzuri kwa sasa na yeye akaamua kusafiri na ndege hiyo.

“Niliona kwenye televisheni watu wakitoa maoni mazuri tu juu ya shirika hili na mimi nikaona nitumie nafasi hiyo,” alifafanua Makamu wa Rais.

Hivi karibuni, serikali imenunua ndege mbili aina ya Bombardier Q400 na kuzikabidhiwa kwa ATCL na zimeanza kufanya kazi katika mikoa mbalimbali nchini huku zikiwa na gharama nafuu, lakini pia zikiwa na gharama nafuu ya uendeshaji.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa ambaye alikuwepo uwanjani akimsindikiza Makamu wa Rais, alisema Watanzania waelewe kwa sasa kampuni hiyo iko kwa ajili ya kufanya biashara.

Alimpongeza Makamu wa Rais kwa kuonesha ushirikiano mkubwa na pia uzalendo kwa kusafiri na ndege ya ATCL, kwani angeweza kutumia ndege nyingine yoyote.

“Leo hii kwa kutumia ndege ya Tanzania yeye pamoja na wasaidizi wake ni jambo jema sana alilolifanya na pia ni jambo la kizalendo tunampongeza sana, kwani angeweza kutumia ndege nyingine yoyote anayoitaka,” alisema Profesa Mbarawa.

Alisema ndege za ATCL gharama zake ni nafuu na pia huduma zao zimeboreshwa zaidi, na kwamba ifikapo mwaka 2018 serikali itanunua ndege nyingine moja na pia mwaka 2019 inatarajia kununua ndege nyingine.

Mkurugenzi Mkuu wa ATCL, Ladislaus Matindi alisema kampuni hiyo inaboresha huduma zake ambako kwa sasa wanaboresha huduma za mtandaoni kwa ajili ya watu kushika nafasi ya safari na hata kulipia kupitia mitandao ya simu.

Wanachama 17 Chadema Waliokuwa Wakipanga Maandamano ya UKUTA Wafutiwa Kesi Mahakamani

$
0
0

Mahakama ya Wilaya ya Maswa mkoani Simiyu imewaachia huru viongozi na wanachama 17 wa Chadema walikokuwa wakikabiliwa na mashitaka ya kujaribu kushawishi kutenda kosa Agosti 25 katika ofisi ya wilaya ya chama hicho Mnadani mjini hapa.

Wanachama waliachwa jana na Hakimu Tumaini Marwa aliyekuwa akisikiliza kesi hiyo baada ya upande wa mashitaka chini ya Mwendesha Mashitaka wa Polisi, Nassib Swedy kushindwa kukamilisha upelelezi wa kesi hiyo huku wakitoa sababu mbalimbali.

Swedy alidai kuwa  washitakiwa hao wakiwa kwenye ofisi yao siku hiyo saa 7 mchana walipanga kufanya maandamano na mikutano ya Ukuta, ambayo ingehatarisha amani na utulivu wilayani humo na Taifa kwa ujumla.

Hata hivyo, washitakiwa hao ambao awali walifikishwa mahakamani hapo Agosti 26 chini ya ulinzi mkali wa Polisi, walikana mashitaka na kunyimwa dhamana, walidhaminiwa Septemba 2 baada ya kukamilisha masharti ya dhamana ya kuwa na mdhamini mmoja wa kuaminika ambaye alisaini bondi ya Sh milioni tano.

Akitoa uamuzi huo jana, Hakimu Marwa alitupilia mbali maombi ya upande wa mashitaka yaliyokuwa yakiomba ahirisho la kesi hiyo kwa mara nyingine ukidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika.

Alisema amri ya mwisho aliyoitoa ilikuwa ahirisho la Novemba 4 hivyo upande wa mashitaka umeshindwa kutekeleza amri ya Mahakama na kwa maana hiyo, anawaacha huru washitakiwa wote chini ya kifungu cha sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai kifungu cha 225 (5) sura ya 20.

“Kifungu hiki kilichowaacha huru washitakiwa hakizuii Polisi kuwafikisha mahakamani tena washitakiwa kwa kosa hilo, iwapo watakuwa wamekamilisha uchunguzi juu ya shauri linalowakabili,” alisema Hakimu Marwa.

Hata hivyo, wakati uamuzi unatolewa wakili wa washitakiwa hao, Martine Sabini aliyekuwa akiwakilisha washitakiwa wote hakuwapo mahakamani, lakini alikuwa ameshawasilisha ombi mbele ya Mahakama hiyo kuomba waachiwe huru kwa sababu ya upande wa mashitaka kushindwa kukamilisha upepelezi kwa muda mwafaka.

Walioachiwa huru ni pamoja na  Mwenyekiti wa Chadema wa Wilaya ya Maswa, Peter Shiyo (39), Katibu wa Chadema wa Wilaya, Flora Msuka (31), Katibu wa Bawacha wa Wilaya, Elias Matondo (37) na  Katibu Mwenezi wa Maswa Mashariki, Waziri Peter (46).

Wengine ni  Bundala Baya (30), Edward Makoye (63), Sylvester Ngwege (60), Frank Makaranga (31), Selemani Kombe (39) na Mapambano Jackson (37).

Pia Nkuba  Magwila (40), Ndebile Paul (27), Edgar Ngasa (32), Lucas Nkuba (39), Laurent Mahembo (36) na Mwajuma Said (40).

Baada ya kuachwa, Shiyo aliishukuru Mahakama kwa kutenda haki akilitaka Jeshi la Polisi kuacha kunyanyasa viongozi wa vyama vya upinzani kwa kufanya kazi kwa hisia na matokeo yake, wanaitia aibu Serikali kwa kushindwa kesi mahakamani.

JIKO: Tiba Yenye Nguvu Za Ajabu Katika Kutibu Tatizo la Upungufu wa Nguvu za Kiume

$
0
0
Tiba  hii  inaitwa  JIKO. Kila mwanaume  anae  itumia, INAMPONYESHA  KABISA  tatizo  la  UKOSEFU  na  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.   Imethibitishwa  na  MKEMIA  MKUU  WA  SERIKALI  YA TANZANIA  

Kufahamu   jinsi  tiba  hii  inavyo  fanya  kazi, bofya  link  hii  hapa  chini :


Kwa  mahitaji  yako  ya  tiba  hii, wasiliana  na   duka  la  NEEMA  HERBALIST & NUTRITIONAL  FOODS  CLINIC   kwa  simu  namba   0766   53 83 84.

Tunapatikana  UBUNGO  jijini  DAR  ES  SALAAM, jirani  na  SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING  nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA.

·Kwa wateja  waliopo  DAR  ES  SALAAM, wasio  na  nafasi  ya  kufika  ofisini  kwetu, watapelekewa  dawa  mahali  walipo  ( HOME  & OFFICE  DELIVERY ).

·Kwa  wateja  waliopo  mikoani, watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  mabasi  mbalimbali.

·Kwa  wateja  waliopo  Zanzibar, watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa  boti.

·Kwa  wateja  wa  Mombasa, watatumiwa  dawa  kwa  basi  la  TAHMEED  COACH.

·Kwa  wateja  wa  NAIROBI  watatumiwa  dawa  kwa  basi  la  DAR EXPRESS.

·Na  kwa  wateja  wa  UGHAIBUNI  ( DIASPORA), watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  au  DHL.

· Kwa  taarifa  zaidi  kuhusu  huduma  zetu, tembelea  kila  siku  blogu  yetu :

Maombi ya dhamana ya Godbless Lema kuwasilishwa leo Baada ya Jana Kushindikana

$
0
0
Mawakili wa Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema ambaye yupo mahabusu katika Gereza kuu la Kisongo, jana walishindwa kukamilisha taratibu za kisheria za kuwasilisha maombi ya dhamana Mahakama Kuu .

Wakili wa Lema, John Mallya jana alisema watawasilisha maombi hayo leo wakati wa kusikilizwa kesi nyingine za mteja wao. “Bado kuna taratibu zinaendelea na tunatarajia kesho (leo) tutazikamilisha,” alisema Mallya. 

Katibu wa Mbunge Lema, Innocent Kisayegi, alisema baadhi ya mawakili wa Lema walikuwa na kikao cha kisheria kujipanga kwa kesi ya leo huku wakisubiri timu nyingine ya mawakili kutoka makao makuu ya Chadema jijini Dar es Salaam. 

“Muda huu leo (jana) mawakili wanaendelea na kikao na tuna imani leo watakuwa tayari kwa utetezi wa Lema,” alisema. 

Mawakili wa Lema ambao jana walikutana ni James Lyatuu, Sheck Mfinanga na Charles Aidieli na wanatarajia kuungana na mawakili wengine akiwamo Mallya. 

Hata hivyo, Kisayegi aliwataka wakazi wa Arusha wajitokeze mahakamani kusikiliza kesi inayomkabili mbunge huyo na mkewe. 

Lema anakabiliwa na mashtaka ya kutoa kauli za uchochezi dhidi ya Rais John Magufuli ambayo yanatajwa kusababisha kukosa dhamana kutokana na rufani ya dhamana yake kuwekewa pingamizi na wanasheria wa Serikali. 

Lema na mke wake, pia wanakabiliwa na kesi ya kutuma ujumbe wa uchochezi dhidi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo na shitaka jingine la kuhamasisha maandamano ya Ukuta Agosti.

Wanafunzi wakumbwa na ugonjwa wa kuanguka

$
0
0
Wanafunzi wa kike 12 wanaosoma Shule ya Msingi Nditi, Wilaya ya Nachingwea, mkoani Lindi, wamekumbwa na ugonjwa wa kuanguka ghafla na wengine kupoteza fahamu, walipokuwa wakicheza katika viwanja vya shule hiyo.

Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Amon Livigha, alikiri kutokea tukio hilo katikati ya wiki iliyopita, saa mbili asubuhi.

Alisema baada ya tukio hilo, baadhi ya wazazi walifika shuleni hapo na kuwachukua watoto wao na kwenda nao nyumbani.

“Nilipata taarifa ya kuanguka kwa wanafunzi hao nikiwa darasani nafundisha, hivyo kutokana na uzito wa tatizo, nililazimika kukatisha masomo na kwenda kuwahudumia watoto hao.

“Wakati tukiendelea kufanya utaratibu wa kuwakimbiza wanafunzi hao kituo cha afya kupatiwa huduma, baadhi ya wazazi walikataa watoto wao wasipelekwe hospitali na kuondoka nao,” alisema.

Mwalimu Livigha alisema kutokana na tukio hilo, kamati ya shule, wazazi na uongozi wa Serikali ya kijiji na kata hiyo wamekutana kujadili suala hilo.

Mtendaji wa kata hiyo, Juma Mng’anga, alikiri kutokea tukio hilo na kueleza kuwa tayari wameshatoa taarifa makao makuu ya wilaya, Nachingwea.

RAS Dar Theresia Mmbando aieleza mahakama alivyovamiwa, kupigwa, kushikwa matiti na kujeruhiwa akisimamia uchaguzi wa Meya Dar

$
0
0
Katibu Tawala Mkoa (RAS) wa Dar es Salaam, Theresia Mmbando ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jinsi alivyovamiwa, kupigwa kwenzi, kushikwa matiti, hadi zipu ya sketi yake kung’oka na kujeruhiwa wakati akisimamia uchaguzi wa meya na naibu wake wa Jiji la Dar es Salaam uliopaswa kufanyika Februari 27. 

Pia, alidai kugongwa kichwani na kupokonywa faili lililokuwa na ajenda ya uchaguzi. 

“Walinifuata mezani nilipokuwa wakitaka niendelee na uchaguzi, Mbunge wa Kawe, Halima Mdee alilivuta faili lililokuwa na mwongozo wa uchaguzi na katika tukio hilo niliwafahamu walionivamia kwa majina na wengine kwa sura,” alidai Mmbando. 

Akiongozwa na Wakili wa Serikali, Flontina Sumawe kutoa ushahidi mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi, Mmbando alidai kuwa Februari 27 alipewa jukumu la kusimamia uchaguzi huo ambao ulipaswa kufanyika nyakati za saa nne asubuhi katika Ukumbi wa Karimjee. 

“Nikiwa Katibu Tawala Mkoa wa Dar es Salaam nilikuwa ni mwenyekiti wa uchaguzi huo, wajumbe wote walifika, Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Salehe Yohana ambaye alikuwa Katibu alifungua uchaguzi huo kwa sababu kolamu ya wajumbe ilikuwa inajitosheleza,” alidai Mmbando. 

Alidai kikao kilifunguliwa, lakini katibu aliahirisha uchaguzi kwa sababu alipokea zuio la Mahakama la kuendelea na akawaarifu wajumbe. 

Mmbando aliendelea kudai kuwa baada ya kuahirishwa, wajumbe wa CCM walitoka nje, lakini wa vyama vingine wakiwamo Ukawa, walimvamia wakimtaka aendelee. 

Alidai watu wengine aliowatambua siku hiyo ni Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea ambaye alimuambia kuwa yeye ni kibaraka wa CCM, Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara aliyekuwa akimsisitiza hakuna kuondoka bila kuendesha kikao. 

Akiendelea kutoa ushahidi mahakamani hapo, Mmbando alidai Diwani wa Kimanga, Manase Mjema (56) alimuona akiwatuliza wenzake na kuwataka wamuachie.

Mmbando alidai aliokolewa na polisi na wafanyakazi wa jiji kupitia mlango wa nyuma. Hakimu Shaidi aliahirisha kesi hiyo hadi Desemba 8, atakapoendelea kusikiliza ushahidi.

Bodi ya Mikopo(HESLB) Yatangaza majina ya wadaiwa sugu kuanzia mwaka 1994 hadi 2014....Bofya Hapa Kuyaona

$
0
0
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu inatangaza orodha ya majina ya Wadaiwa Sugu ambao wamehitimu katika Vyuo mbalimbali vya Elimu ya Juu kuanzia mwaka wa masomo 1994/1995. 

Wasugu hao wanapewa siku 30 kulipa madeni yao ndani ya muda huo kabla hatua za kisheria hazijachukuliwa na wahusika kulazimika kulipia gharama za kuwasaka na kuendesha kesi.

Kwa mawasiliano zaidi piga 0763 459 165 au 0767 513 208 au tembelea ofisi zetu za Makao Makuu, Dar es salaam au ofisi zetu za kanda zilizopo Dodoma, Zanzibar, Mwanza na Arusha.

Kuona orodha hiyo bofya viunganishi vifuatavyo:









RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 89 & 90(Riwaya inawafaa kuanzia miaka 18 na kuendelea )

$
0
0

MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA

ILIPOISHIA
Mapigo ya moyo yakaanza kuniendaa mbio. Nikaanza kufwata michuruziko ya damu iliyo elekea chumbani mwa amina kabla sijufikia mlango wa chumbani kwake, kitu kizito kikangia kupitia dirishani. Kikaanza kutoa moshi mkali ulioa anza kunipalia, nikagundua ni bomu la machozi, lililo ambanata nailio ya risasi iliyoanza kusikika ikitokea nje.

ENDELEA
  Ikanilazimu kulala chini haraka haraka, risasi zikazidi kumiminika zikipigwa kupitia maditishani, ambayo ni yaviol na tayari yamesha vunjika vibaya mno. Kitu kilicho nichanganya sikujua risasi hizo zinatokea upande gai, na mbaya sijajua watu hawa nj waaina gani, na wanamalengo ganjni kwangu.

Nikatamba haraka na kuyachukua masanduku ya pesa nikaufungua mlango wa chumba cha Amina, nukayasukumia ndani, na mi nikaingia nikiwa ninatambaa, japo moshi huu, mkali uliendelea kunipalia na kuyafanya macho yangu kumwagikwa na machozi mengi. Nikamkuta polisi akiwa ameuawa ndani ya chumba cha Amina, huku risasi kadhaa, zikiwa zimekichangua kichwa chake vibaya. Nikafunga mlango kwa ndani, nikaatafuta maji ya kunawa usoni, ila sikuyapata.

Nikavua shati langu nililo livaa, nikalikojolea na kulitotesha vizuri kwa maji mengi. Nikajifunika usoni, kidogi hali ya kumwagikwa kwa machozi ikapungua. Risasi zikaendelea kurindima, nikawa ninajiuliza watu hawa huwenda wakawa ni wendawazimu, kutokana risasi zao wanazimalizia katika kuzifyatua pasipo malengo, isitoshe ukuta waa nyumba hi, kidogo ni imara sana, na risasi kupenya si rahisi sana.

   Nikatafuta kila koa ya chumba kama kuna kitu cha kuweza kunisaidia kuepukana katika adha hii ya kuingia mikononi mwa watu amwa watu ambao hadi sasa hivi sijajua kama ni poliai au laa. Katika kuyembea tembea ndani ya chumba cha Amina, nikahisi mlio fulani kutokea chuni ya kapeti lililo tandazwa chumba kizima.

Nilalifunua kwa haraka na kukuta, mfuniko wa chuma, ulio fungwa kwa kufuli. Nikaanza kutafuta jinsi ya kuufungua mfuniko huu, kwakutumia ncha ya sanduku moja wapo, ñikafanikiwa kulivuñja kufuli. Nikalifungua, nikakuta ngazi ya kushuka chini, kwa haraka nikashuka japo kuna giza totoro, ila nikajiamini. Kufika chini ya ngazi, nikahisi kuna kitu, kinanigusa kichwani, nikaupeleka mkoni wanguna kushika, nikakuta kijikamba, katika kukivuta chini, taa karibia nne, zilizopo ndani ya chumba hichi zikawaka.

Bunduki nyingi za kila aina nikaziona zikiwa zimepangiliwa vizuri kwenye kuta za handaki hili, nikapnda juu haraka, nikayasukumia ndani masanduku ya pesa, nikajibanza kwenye moja ya kuta, yenye dirisha, nikachungulia nje. Nikaona watu wakikatiza katiza kwenye miti mingi ya hii, nyumba. Mikononi mwao wakiwa na silaha. Kitendo cha wao kukimbia kimbia kwenye miti hii, ni kubadilishana nafasi za kufyatua risasi. Kitu kilicho nifanya nigundue hawa si polisi, hii nikutokana na vilemba vyao walivyo jifunga, pamoja na mavazi yasiyo na sare maalumu.

"Jamaa wamekuja hadi huku"
Nilijisemea, mwenyewe huku nikiendelea kuwatazama jinsi wanavyo fyatua risasi zinazo piga kwenye kuta ya nyumba hii.
'Wameanza mimi, nitamaliza'
Nilizungumza, huku nikishuka kwenye ngazi za kuingia kwenye handaki. Nikanza kufungua makabati manne yaliyopo humu ndani, nikayakuta yakiwa na bunduki pamoja na silaha kadhaa, nikakuta kisanduku cha kuhifadhia, vitu vya huduma ya kwanza.

 Nikafungua na kuchukua clip bandeji, nikajifunga sejemu nilizo pata majeraha ya kukatwa na visu. Nilipo hakilisha nipo salama, nikachukua bunduki, aina ya SMG, nikachukua na magazine kumi, zilizo jaa risasi.Nikachukua shati langu, nililo lilowanisha kwa mikojo, nikajifunga kichwani. Nikapanda juu, nikakuta hali ikiwa imetulia. Nikaanza kusikia minong'ono ikitokea sebleni, iloashiria jamaa, wamesha ingia ndani. Nikajibanza pembeni ya ukuta wenye mlango, taratibu nikakifungua kitasa, Na kuuvuta mlango taratibu, nikauachia, nikañza kusikia hatua za mtu akija chumbabi.

Nikashañgàà, kunuona mtoto mdogi wa kike mwenye umri chini ya miaka kumi na tato, akiwa ameshika bunduki huku akimshangaa, polisi aliye lala chini.
"Amefia huku"
Alizungumza pasipo kuniona nyuma ya mlango, nilipo simama. Akaiweka bunduki yake chini na kuanza umpapasa askari huyu, nikasogea pembeni kidogo, ili asinione, kwa bahati mbaya nikagusa kikopo chenye poda kilichokua juu ya 'dreasing table'
na kikaanguka chini na kumfanya binti huyo kugeuka haraka, tukakutana macho kwa macho.

Taarifa Rasmi Ya Maafa ya Tetemeko la Kagera Kutoka Ofisi Ya Waziri Mkuu

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live


Latest Images