Mwandishi: EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA
“Wewe hulali?”
Rahab aliuliza kwa sauti ya unyonge, huku akimtazama Raisi Praygod kwa macho yaliyo jaa usingizi, hadi akajikuta akirembua.
“Nataka nikaoge”
Rais Praygod akapiga hatua moja, ila Rahab akamshika mkono na kumvuta kwa nguvu na kuangukia kitandani. Rahab kwa haraka akausogeza karibu mdomo wake kwa Raisi Praygod na wakaanza kunyonyana, huku wakionekana kuwa katika hisia kali. Raisi Praygod akalivua gauni lake na kulitupa pembeni. Akalishika la Rahab na akamvua, wote wakabakiwa kama walivyo zaliwa.
ENDELEA
Hapakuwa na mtu aliye weza kumuonea mwenzake aibu zaidi ya wote kushiriki tendo la ndoa ipasavyo. Rahab akazidi kujituma kitandani kumpa muheshimiwa Raisi mambo matamu ambayo hata Raisi Praygod, hakuwahi kuyapata kutoka kwa mwanamke wa aina yoyote tangu azaliwe. Hata marehemu mke wake, hakuweza kufikia hata aslimia kumi kwa mambo ambayo Rahab anamfanyia juu ya kitanda. Wote wakajikuta wamesahau kwamba wanapita katika kipindi kigumu cha matatizo.
“Rahab”
Raisi Praygod alimuita Rahab, aliye mkalia juu ya kiuno chake akizidi kukatika kadri ya uwezo wake.
“Mmmmmm”
Rahab aliita huku akiwa amebana pumzi zake, huku jasho kwa mbali likimwagika na nywele zake ndefu zikiwa zimekaa shaghala baghala.
“Nataka nikuoe”
“Kweli?”
“Ndio nahitaji uwe mke wangu, wa ndoa”
Rahab kuambia wahivyo hakujibu kwa sauti, ila akajibu kwa vitendo, vilivyo mfanya Raisi kusahau matatizo yote na kuzidi kuchanganyuikiwa kwa penzi hilo la binti mdogo mwenye mwili mwembamba, fulani, ila si shuuhuli ya kupambana pekee yake na maadui, ila hata shughuli ya kitandani anaiweza kwa asilimia mia moja. Hadi wanafikia kileleni wote kwa pamoja wakajikuta wakicheka huku wakiamini kwamba walicho peana kilistahili kwa wao kuweza kukipata kwa wakati huo.
“Nakupenda sana Rahab”
Raisi Praygod alizungumza huku akihema mithili ya mwana riadha wa mwisho kwenye mbio ndefu, aliyekua na kibarua kirefu cha kuwakimbiza wezake wanao kwenda kwa mbio ndefu sana.
“Nakupenda pia Praygod”
Kwa mara ya kwanza Rahab kufungua kinywa chake na kuliita jina la Raisi, kwani siku zote alizoea kumuita muheshimiwa Raisi. Taratibu Rahab akajilaza kifuani mwa Raisi Praygod, huku taratibu akiupa kazi mkono wake wa kushoto kuchezea nywele nyini lizizopo kifuani mwa raisi Praygod.
“Twende tukaoge”
Raisi Praygod alizungumza, na taratibu wote wakashuka kitandania, wakaingia bafuni na kila mmoja akawa na kazi ya kumuogesha mwenzake kwa kila kona ya mwili. Ukawa ndio mwanzo mpya wa mahusiano kati ya Raisi Praygod na Rahab, kila mmoja aliweza kuufungua moyo kwa mwenzake na kuamini upendo wao umeendana kwa asilimia kubwa sana.
***
Kila jinsi walivyo zidi kuogelea ndivyo jisi walivyo zidi kwenda mbele, huku mara kwa mara wakiwa wanajitokeza kwenye usawa wa bahari kutazama ni wapi wanapo elekea. Ikawachukua muda mrefu sana kuweza kufika pembezoni mwa fukwe za bahari, katika eneo ambalo limetulia sana. Wote wakaivua mitungi ya gesi ambayo walikuwa wameivaa migongoni mwao. Kila mmoja alijihisi njaa kubwa kwenye tumbo lake, kwani waliweza kudumu ndani ya maji takribani masaa nane, wakiwa wanatoroka kutoka sehemu mmoja kwenda nyinine
“Ahaaa kudadadeki, kweli ng’ombe wa masikini hazai”
Halima alizungumza kwa sauti kubwa huku akijilaza kwenye mchanga mweupe ulio kua pembezoni mwa bahari hii kubwa. Hakuna aliye mjibu zaidi ya wezake kuendelea kutazama kila eneo la fukwe hizi zinazo pendeza kuvutia sana.
“Jamani inakuaje?”
Anna aliuliza kwa sauti ya unyonge, dhairi akionekana kuchoka sana.
“Nahisi hapa kwenye fukwe kunaweza kua na nyumba tutembeeni tembeeni, tunaweza kupata msaada”
Samson aliwashauri wezake
“Lakini jamani, hembu kuweni makini. Hapa tulipo fika sote hatupajui. Isije ikawa fukwe ya jeshi ikala kwetu ohooo”
Halima alizungumza huku akijigeuza geuza kwenye mchanga
“Sasa Halima wewe unataka tuendelee kukaa hapa si ndio?”
“Hapana sijasema hivyo Fetty, ila ninacho sema mimi, tuwe makini tusiwe vihere here. Kama pesa tumezikosa, lile lidude nalo limechukuliwa. Yote kwa tamaa zetu”
“Halima huu muda sio wa kulaumiana bwana”
Agnes alizungumza kwa hasira kali.
“Hata kama, jamani lakini hua siku zote nikizungumzaga ukweli, munaniona mimi fala. Sasa huyo Samson tuliye msaidia naye katuileta huku, nilipo kua ninamkatalia tusiwe pamoja naye mimi nilijua tuu haya yatatokea. Haya baba Samson tuambie tunaelekea wapi?”
“Maneno ya Halima, yakamkera kila mtu ambaye, alionekana kuchoka sana kwa shuhuli nzima waliyo ifanya ya kujioko kutoka kwenye jeshi la nchi ya Russia
Wakaanza kutembea kwa umakin, huku wakitazama kila eneoa la fukwe hii. Kigiza kilisha anza kuchukua nafasi yake huku kila mmoja akaizidi kunyong’onyewa kwa kuchoka sana. Hawakukata tamaa zaidi ya kwenda mbele kubahatisha kama wanaweza kupata sehemu ya kujistiri. Hadi inagonga mishale ya saa mbili usiku hapakuwa na mtu aliye baatika kuona nyumba ama uwepo wa watu katika eneo hilo
“Jamani tupumzikeni bwana na kama kuendelea tutaendelea kutembea tukiwa na nguvu”
Halima alizungumza huku akiwa amesimama, wezake wote wakamgeukia na kumkodolea mimacho. Kila mtu akakubaliana na wazo la Halima, wakatafuta moya ya jiwe kubwa lililo toboka na kuweka kijichumba kidogo, wote wakaingia na kukaa humo. Mwanga wa mbalamwezi uliweza kuwaonyesha ndani ya jiwe hilo kubwa, hapakuwa na kitu chochote kinacho weza kuwadhuru.
Baridi kali kwao ndio ikawa ni changamoto kubwa sana iliyo weza kuwatesa miili yao, isitoshe nguo walizo zivaa zilizo tengenezwa kwa material ya mpira hazikuweza kabisa kuizuia baridi hiyo kuendelea kuwapiga kwenye miili yao.
“Mmmm hili puku ni balaaa”
Agnes alizungumza huku akijikunyata, taratibu Samson akatoka ndani ya jiwe na kusimama nje, akatizama kila kona ya fukwe hakuona mtu yoyote, akazunguka nyuma ya jiwe na kujisaidia haja ndogo ambayo ilikuwa imememkamata kwa kipindi kirefu sana. Akiwa katikati ya kujisaidia haja ndogo kwa mbali akaweza kuona mwanga wa taa ukitokea kwenye moja ya nyumba iliyo mbali kidogo toka hapo walipo, kwa haraka akamaliza haja yake na kuzunguka walipo wezake
“Jamani kuna kitu nimekiona tokeni haraka”
Fetty na wezake wakatoka kwa haraka, Samson akawaonyesha mwanga wa taa hiyo . Kwa haraka bila hata ya kujiuliza wakanza kukimbia kuelekea kwenye nyumba hiyo. Kila walivyo zidi kwenda ndivyo walivyo zidi kuiona mandhari ya nyumba hiyo, ambayo ni kubwa kiasi na yagorofa. Wakafanikiwa kufika kwenye uwanja wa jumba hilo linalo onekana ni jumba la kifahari, ila nje hapakua na taa ya aina yoyote, zaidi ya taa inayo waka kwenye chumba hicho kimoja.
“Jamani, tuweni makini naona tunaenda tu”
Halima alizungumza, kwa kujiamini. Wote wakasimama kutazama mazingira ya jumba hili lililo zungukwa na miti mingi ya minazi. Kwa mbali wakasikia mngurumo wa gari ukiwa unakaribia kufika kwenye jumba hili, kwa haraka wakatafuta sehemu ya kujificha ambayo iliwawezesha kuona mlango mkubwa wa kuingilia ndani ya jumba hilo.
Gari moja ya kifahari aina ya Jaguar, ikasimama nje ya jumba hili. Wakashuka watu wawili walio valia suti huku mikononi mwao wakishika bunduki aina ya Short gun. Mmoja akazunguka upande wa pili wa gari ambapo akaufungua mlango wa gari hiyo. Wote wakamshuhudia bwana Rusev akishuka kwenye gari hilo la kifahari huku akionekana kutazama kila upande wa jumba hilo.