Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu Ya Octoba 24


Makamba asikitishwa na upungufu wa maji katika Ziwa Rukwa....Atoa maagizo kwa wakurugenzi

$
0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe.January Makamba ameendelea na ziara ya kikazi katika Mkoa wa Rukwa. Katika ziara yake Waziri Makamba ameshuhudia uharibifumkubwa wa mazingira hususan pembezoni mwa ziwa Rukwa.

Waziri Makamba amewaambiwa wakazi wa Kijiji cha Nankanga kwamba mwaka 2000 kina cha maji katika ziwa Rukwa kilikuwa ni mita sita, na kwa mwaka 2016 chanzo hicho kimepungua hadi kufikia mita tatu.

“Tafiti zinaonyesha kuwa kupungua kwa kina hicho pamoja na mambo mengine kunasababishwa na kilimo cha milimani na kandokando ya ziwa, na ulishajiwa mifugo katika Vyanzo vya maji,” Makamba alibainisha.

Katika ziara yake baada ya kushuhudia uharibifu mkubwa kiasi hicho, Waziri Makamba ameazimia kulitangaza eneo la Ziwa Rukwa kama eneo mahsusi kwa mazingira na kanuni za matumizi ya maeneo hayo zitaandaliwa ilikunusuru Ziwa Rukwa.

Pia, wakurugenzi wote wa Halmashauri za Mkoa wa Rukwa wameagizwa kutenga pesa zitokanazo na tozo mbalimbali ili waweze kugharamia uwekaji wa alama maalumu ‘beacons’ ili kuainisha eneo tengefu na kuagiza kuwazoezi hili lifanyike haraka.

Aidha, Mhe. Makamba amesisitiza juu ya upandaji wa miti na ameonyesha masikitiko yake kwa Mkoa wa Rukwa kuwa na upungufu wa miti ya asili na ile ya kupanda kwa kiwango kikubwa. “nimetembea zaidi ya kilomita 200 sijaona miti iliyopandwa,” Makamba aliongezea.

Wakazi wa Mkoa wa Rukwa wamefahamishwa na kusisitizwa kuwa kuanzia mwakani itakuwa lazima kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari kuripoti na miti na kutakiwa kuitunza mpaka pale watakapomaliza shule. Waziri Makamba ameahidi kuleta wataalamu na kutoa orodha ya miche inayostawi katika kila kijiiji ili kurahisisha uoteshaji wa miti.

Katika hatua nyingine, Waziri Makamba amekutana na viongozi mbalimbali wa dini na wazee wa Mkoa wa Rukwa na kuwataka kuunda Kamati ya Amani,na kuahidi kugharamia Mkutano wa kwanza wa kuundwa kwa baraza hilo nakusisitiza agenda ya mazingira iwepo.

Mkoani Rukwa Waziri Makamba ametembelea mwalo wa ziwa Rukwa na kuzungumza na wananchi wa maeneo hayo na Mkutano wa Hadhara katika

Na Lulu Mussa, Sumbawanga

Sare za CCM zamshusha cheo Mwalimu Mkuu

$
0
0

Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Kasamwa ya mkoani Geita, Dennis Otieno anadaiwa kushushwa cheo kutokana na kuzuia wanafunzi kuvaa sare za CCM kwenye mahafali ya kidato cha nne.

Pia, taarifa hizo zinasema mkuu huyo wa shule alipinga kitendo cha baadhi ya walimu kuchangisha fedha wazazi wa watoto ambao ni wanachama wa Klabu ya Magufuli ili kufanya sherehe hilo kutokana na agizo la Rais la kufuta michango yote mashuleni.

Otieno, ambaye alikataa kuzungumzia suala hilo, anadaiwa kushushwa cheo kutokana na shinikizo la makada wa chama hicho tawala, hasa mwenyekiti wa CCM mkoani Geita, Joseph Kasheku, maarufu kwa jina la Msukuma, ambaye amethibitisha kushushwa cheo kwa mtumishi huyo wa umma.

Kwa mujibu wa taarifa hizo zilizosambazwa kwenye mitandao ya kijamii zinasema Otieno aligombana na mwalimu ambaye ni mlezi wa Klabu ya Magufuli kutokana na kuandaa mahafali hayo.

CCM Wamdhibiti Maalim Seif Zanzibar....SMZ Yapiga Marufuku Siasa Nyumba za Ibada

$
0
0
Serikali  ya Mapinduzi Zanzibar, imepiga marufuku wanasiasa kutumia nyumba za ibada kwa shughuli za kisiasa Visiwani Zanzibar.

Msimamo huo wa Serikali umekuja siku chache tangu Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, kutumia kila siku za Ijumaa kufikisha ujumbe katika msikiti atakaoswali.

Akitoa tamko la Serikali jana, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Mohammed Aboud Mohammed alisema Serikali inawaagiza wakuu wa mikoa yote ya Zanzibar kusimamia utekelezaji wa agizo hilo katika mikoa yao.

“Kwa taarifa hii Serikali inawaagiza wakuu wa mikoa kupitia kamati zao za ulinzi na usalama kusimamia utekelezaji wa agizo hili katika mikoa yao,” alisema Waziri Aboud.

Alisema Serikali imewaagiza wakuu hao wa mikoa kuchukua hatua za kisheria kwa mtu yeyote atakayekiuka agizo hilo.

Waziri Aboud alisema kwamba viongozi wa dini na kamati zao katika nyumba za ibada watakaoruhusu  wanasiasa kuendesha shughuli za kisiasa watawajibika kwa mujibu wa sheria za nchi.

Alisema kwamba hivi karibuni katika baadhi ya maeneo ya Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja katika Misikiti ya Mbuyuni, Kihibnani na Kwabiziredi kumetokea tabia  kwa baadhi ya viongozi wa kisiasa kupita na kutoa hotuba za kisiasa katika misikiti hiyo.

Waziri huyo alisema kwamba shughuli za vyama vya siasa zinaendeshwa chini ya sheria N0 5 ya mwaka 1992 ambayo imeeleza wazi mipaka na shughuli za kisiasa ziendeshwe chini ya sheria hiyo.

“Vitendo vinavyofanywa na viongozi hao  wa kisiasa wanaotumia nyumba za ibada kama majukwaa ya kisiasa  wanakwenda kinyume na dhamira ya katiba na sheria za nchi ikiwemo sheria ya vyama vya siasa namba 5 ya mwaka 1992” Alisisitiza Waziri Aboud.

Waziri Aboud alisema kwamba shughuli zote za  dini ya kiislamu Zanzibar zinasimamiwa kupitia sheria namba 9 ya mwaka 2001, namba 2 ya mwaka 2007 na namba 3 ya mwaka 1985 zinazoongoza Taasisi mahsusi kama vile Ofisi ya Mufti, Ofisi ya Mahakama ya Kadhi na Kamisheni ya Wakfu na Mali ya Amana.

Alisema  kupitia katiba na sheria , uhuru wa mtu kuabudu dini anayoitaka umetolewa bila kuingiliwa na itikadi za vyama vya siasa kama inavyobainishwa  na katiba zote mbili ibara ya 19 ambazo zinaeleza umuhimu wa uhuru wa mtu kuamini dini aitakayo kwa misingi ya kukuza usalama na amani katika jamii.

Jinsi ya Kuandaa na Kutayarisha Dawa Lishe ya Kunenepesha,Kurutubisha na Kuongeza Mwili

$
0
0

Dawa-lishe  ya  kuongeza, kurutubisha  na  kunenepesha  mwili, ni  dawa  maalumu  kwa  watu  wenye  uzito  wa  chini  (  Under weight ) ambao  wanataka  kuongeza  mwili  na  uzito.


Dawa  hii  huwasaidia  watu  ambao  miili  yao  imedhoofu  kutokana  na  sababu  mbalimbali  kama  vile  kuugua  magonjwa  na  maradhi  mbalimbali.

Na  kwa  wale  watu  wembamba  ambao  wanataka  kuongeza  miili  yao, dawa  hii  huwasaidia  vizuri  sana.

FAHAMU  JINSI NA  NAMNA  YA  KUANDAA NA  KUTAYARISHA   DAWA-LISHE  MAALUMU   YA  KUONGEZA, KURUTUBISHA  NA  KUNENEPESHA  MWILI.

MAHITAJI   YA  DAWA –LISHE

i.           Dawa –lishe vijiko  viwili vikubwa.

ii.         Asali  ya  tende  vijiko  vitano  vikubwa.

iii.       Tangawizi  ya  unga  vijiko  vikubwa  viwili

iv.       Unga  wa ufuta

v.         Maziwa  fresh nusu  lita

vi.       Maji  ya  moto  kiasi  cha  milimita  mia  mbili  na  hamsini  ( 250 mills  )


MATAYARISHO
i. Chukua  vijiko  vinne  vyenye  dawa  lishe  yako  kisha  chemsha  na  nusu  lita  ya  maji  hadi  mchanganyiko  wako  utokote  halafu  ipua, chuja , makapi  weka  pembeni  kisha  hifadhi  juisi  yako.

ii.Tayarisha  uji kwa  kutumia  unga  wa  ufuta  na maziwa  fresh

iii.Chukua  vijiko  viwili  vikubwa  vya tangawizi  ya  unga  kisha  changanya  kwenye  kikombe  cha  maji  ya  moto  chenye  ujazo  wa  milimita  mia  mbili  hamsini  (  250  mills )

MATUMIZI:
i. Tumia  kunywa  nusu  lita  ya  dawa –lishe  yako  kisha

ii.Tumia kula  vijiko  vinne  vikubwa  vya  asali  ya  tende

iii.Kisha tumia  kunywa  vikombe  vinne  vya  uji  wa  ufuta  ulio changanywa  na  maziwa  fresh

iv.Halafu  kunywa  glasi  moja  ya  moto  iliyo  changanywa  na  vijiko  viwili  vikubwa vya tangawizi  ya  unga.

UTAFANYA  HIVYO  MARA  MBILI  KWA  SIKU  KWA  MUDA  WA  SIKU  THELATHINI  MFULULIZO.

Baada  ya  siku  thelathini, utaangalia  na  kujitathmini  kiasi  ulicho  ongezeka. Kama  utataka  kuendelea  kuongezeka  zaidi, utaendelea  kutumia  dozi  hii  hadi hapo utakapo fikia kiwango  utakacho  rizika  nacho.

BEI  YA  DAWA-LISHE : Bei  ya  Dawa-Lishe  ni  SHILINGI  ELFU  HAMSINI  TU (TSHS.50,000/=)

JINSI  YA  KUIPATA  DAWA  LISHE:
Dawa  hii  inapatikana  katiuka  duka  la dawa  asilia  la  NEEMA  HERBALIST  &  NUTRITIONAL  FOODS  CLINIC  lililopo  jijini  DAR  ES  SALAAN  katika  eneo  la  TABATA  MAKOKA  karibu  na  SHULE  YA  SEKONDARI  YA  MT. ANNUARITE.

Unaweza  kufika  moja  kwa  moja  katika  ofisi  zetu  AU  unaweza  kuletewa  mahali popote  ulipo  jijini  Dar   Es  salaam.

Kwa  wakaazi  wa  ZANZIBAR  watatumiwa dawa  kwa  njia  ya  usafiri  wa  boti  na  kwa  wateja  wetu  wa  ughaibuni watatumiwa  dawa  kwa  njia  ya  POSTA  au  DHL.

Kwa  mawasiliano  zaidi  wasiliana  nasi  kwa  simu

0766  53  83   84

Vile  vile  tunayo  dawa  ya  asili  iitwayo  JIKO  ambayo  inatibu  na  kuponyesha  kabisa  TATIZO  LA  UKOSEFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.

Kufahamu  kuhusu  SAYANSI  YA  NGUVU  ZA  KIUME  pamoja  na  jinsi  dwa  ya  JIKO  inavyo  fanya  kazi  tafadhali  tembelea:

Lipumba aitaka Chadema Kutoingilia Mgogoro CUF......Aifananisha Opareshi UKUTA na Biskuti

$
0
0
Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba,  amewataka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kutoingilia mgogoro uliopo ndani ya chama hicho kwa sababu hauwahusu.

Kauli hiyo aliitoa jana jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na wanachama wa chama hicho katika kikao cha ndani, kilichofanyika Wilaya ya Kinondoni ambapo alisema Chadema kushindwa kutekeleza Operesheni Ukuta ni dhahiri chama hicho kimeshindwa kutekeleza kile wanachoahidi kwa Watanzania.

Alisema mpaka sasa kumekua na vikao mbalimbali vinavyofanywa na viongozi wa Chadema kwa ajili ya kuivuruga CUF, jambo ambalo alisema haliwekezani.

“Chadema wanajitahidi kutuvuruga kwa kutuma waasi wa chama hiki, lakini naomba niwaambie hawawezi, CUF ni ngangari hata serikali inajua na  wanachokifanya ni kupoteza muda bure.

“Unajenga Ukuta wa biskuti, ukiumwagia juisi unamong’onyoka, Ukuta gani huo, huu muziki wa CUF ni ngangari hawauwezi,” alisema Lipumba.

Alisema katika kipindi hiki ambacho wana kesi mahakamani, wanachama wa chama hicho wataendelea na shughuli za kukijenga chama hicho pamoja na kuwasisitiza  kuwa na msimamo wa kutetea chama na katiba yake, jambo ambalo linaweza kuwasaidia kufikia malengo waliyokusudia ya kushika dola kafika Uchaguzi wa mwaka 2020.

Alisema kutokana na hali hiyo, rasilimali za chama hicho zinasimamiwa kwa umakini chini ya walinzi wa chama hicho, Blue Guard ambao Katibu Mkuu wa chama hicho, Maalim Seif Sharif Hamad alisema ni wavamizi hawatambui.

“Ninamshangaa Maalim Seif sasa hivi anaibuka na kusema hawatambui walinzi wa chama Blue Guard ambao miaka yote walikua wanamlinda pamoja na rasilimali za chama, lakini hayo yamekwisha nitazidi kumwomba aje tujenge chama hata kama kesi inaendelea mahakamani,” alisema.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano anayemunga mkono Profesa Lipumba, Abdallah Kambaya alisema kupoteza nafasi ya umeya na naibu wake katika Manispaa ya Kinondoni ni matokeo ya mgogoro wa CUF na kutokuwepo ushirikiano ndani ya Ukawa.

“Maalim Seif anaunga mkono Ukawa, mbona wanachama wa Ukawa wameshindwa kutusaidia ili kupata meya na naibu wake kwenye uchaguzi wa leo? (jana),” alihoji.

Serikali kuwabana wanafunzi wanaopewa mikopo kwa kipaumbele

$
0
0
Serikali ipo katika mkakati wa kuwabana wanafunzi wanaopewa mikopo katika fani za kipaumbele, kutumikia katika utumishi wa umma nchini kwa muda fulani ili kuhakikisha dhamira ya serikali ya inatimia.

Fani hizo ni sayansi za tiba na afya, ualimu wa sayansi na hisabati, uhandisi wa viwanda, kilimo, mifugo, mafuta, gesi asilia, sayansi asilia, mabadiliko ya tabia nchi, sayansi za ardhi, usanifu majengo na miundombinu.

Serikali inachukua uamuzi huo, baada ya kubaini kuwapo wanafunzi wanaosomea fani hizo ili kupata mikopo, lakini baada ya kumaliza hukimbilia kufanya kazi nyingine au nje ya nchi na hivyo kuendelea kuwepo upungufu wa wataalamu waliowakusudia kubaki.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na mafunzo ya ufundi, Stella Manyanya aliyasema hayo hivi karibuni, alipozungumzia utoaji wa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu. Alieleza kuwa serikali inafikiria kuwe na utaratibu kwa wanaonufaika na mikopo ya kipaumbele kuingia makubaliano na serikali.

Alisema suala hilo halitakuwa jipya kwani hapo nyuma walikuwa wakibanwa kuwa lazima kufanya kazi angalau kwa miaka mitano serikalini na baadaye ni ruhusa kwenda popote, lakini kwa sasa hawawezi kuwabana wote, lakini lazima kufanya hivyo kwa hao wa kipaumbele.

Aidha Manyanya alizungumzia ulipaji mikopo hiyo na kudai wanaboresha sheria ya kukusanya madeni kwa kushirikiana na waajiri.

“Serikali itakusanya madeni hata kwa wakopaji ambao wamejiajiri kwa sababu wengi wakimaliza masomo hawafikirii kulipa,” alisema.”Sasa lazima walipe, wakopaji watambue fedha hizo ni mikopo na lazima kulipa.”

Alisema kwa wakopaji watakaoajiriwa, wizara inataka mkopo huo kuwa wa kwanza kukatwa kabla ya mingine ili kuepuka kuingiliana na sheria za kazi, zinazotaka mkopaji kuachiwa fedha fulani katika mshahara wake.

Jipatie Android Application Kwa Ajili ya Blog au Website Yako Kwa Bei Poa

$
0
0

Unataka biashara yako, blog yako au website yako iwafikie watu wengi zaidi  na kwa haraka?

Kama jibu  ni  Ndiyo, basi hujachelewa...Tuna tengeneza Android Apps ambazo  zinakuwa na muonekano sawia na blog au website yako. 

Baada ya kutenenezwa, Application itawekwa playstore ambapo mtu yeyote mwenye smart phone ataweza kuipata biashara yako au blog yako kupitia Play Store

Kwa mawasiliano, piga: 0656897493



Mbowe aikumbuka Oparesheni UKUTA.....Asema Serikali inaendeshwa kwa hila

$
0
0

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe amesema Demokrasia, Katiba na Sheria haziheshimiwi na kwamba  Jeshi la Polisi limekuwa wakala wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na kilichofanywa kwenye uchaguzi wa umeya wa Manispaa ya Kinondoni kinawapa sababu ya kurejea operesheni yao wanayoiita Umoja wa Kupambana na Udikteta Tanzania (UKUTA).

Mbowe amesema hayo Oktoba 23, 2016 alipofika eneo ulipofanyika uchaguzo wa Meya Kinondoni ambapo madiwani wa Ukawa walisusia uchaguzi huo na kudai kwamba Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Aron Kagurumjuli, ameshirikiana na CCM kuhujumu zoezi hilo, hivyo wametangaza kwenda mahakamani kupinga uchaguzi huo baada ya CCM kuendelea na uchaguzi huo na kutangaza mshindi.

Njama zinazodaiwa kufanywa na mkurugenzi huyo ni kugawanya madiwani kinyume na kanuni kwa kuhamisha madiwani wa upinzani kwenda Halmashauri ya Ubungo na kuwahamishia Kinondoni madiwani wa CCM kutoka halmashauri nyingine.

Mbowe amesema Serikali inaendeshwa kwa hila kwani licha ya uchaguzi kufanyika siku ambayo si ya kazi,  Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, alikataa barua iliyoandikwa na madiwani Jumamosi Oktoba 22 kuzuia uchaguzi huo kwa kudai kuwa si siku ya kazi.

Aliendelea kwa kumlaumu Rais Dk. John Magufuli kwamba ameanzisha utamaduni wa kuuwa demokrasia na kwamba analiletea taifa madhara makubwa.

Kwa upande wake Mbunge wa Kawe, Halima Mdee (Chadema),  amesema wametoka kwenye uchaguzi huo baada ya baadhi ya madiwani wao kuzuiwa kuingia kwenye kikao hicho.

Mdee alisema kuwa  CCM wameingiza madiwani ambao si wajumbe halali wa kikao hicho kwasabau wanatoka katika halmashauri zingine.

“Humo ndani yumo Profesa Joyce Ndalichako ambaye ni Mbunge wa Kuteuliwa na alisajiliwa kama mkazi wa Ilala na alipiga kura za umeya Ilala hivyo mnaweza kuona uhuni unaofanywa.

“Lakini yumo pia Tulia Akson (Dk. Tulia Akson, Mbunge wa Kuteuliwa na Naibu Spika) ambaye si mkazi wa Kinondoni yeye amesajiliwa kama mkazi wa Ubungo,” alisema Mdee.

Amesema kwa mujibu wa kanuni Halmashauri moja haiwezi kuwa na wabunge wa kuteuliwa zaidi ya watatu na kueleza kuwa katika kikao hicho wamo wabunge wanne wa kuteuliwa.

Hivyo, kutokana na hali hiyo Mdee amesema watakwenda mahakama ili kupata tafsiri za kisheria za suala hilo kupata haki.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya Octoba 25

Serikali Yakanusha Taarifa Iliyosambaa Katika Mitandao Ya Kijamii Kuwa Itaanza Kutoa Ajira

$
0
0

1.Ipo taarifa inayosambaa katika mitandao ya kijamii ikimnukuu Waziri wa Nchi -Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb), kuwa Serikali itaanza kutoa ajira, kupandisha Vyeo na kulipa Stahiki mbalimbali za Watumishi wa Umma mwezi Februari, 2017. Chanzo cha habari hiyo ni mtandao wa Jamii Forum kupitia mjadala ulioanzishwa na nkanga chief(JF-Expert Member) na baadaye kusambazwa katika mitandao mingine.

2.Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora inapenda kuwafahamisha Watumishi wa Umma na Umma kwa ujumla kuwa, taarifa hiyo haina ukweli wowote na ina lengo la kuupotosha

Umma. Hivyo watumishi wa umma na wananchi kwa ujumla wanaombwa kuipuuza taarifa hiyo na kuendelea na majukumu yao kama kawaida.


3.Serikali inasisitiza kuwa, suala la Ajira mpya na upandishaji Vyeo litafanyika kwa kuzingatia Bajeti ya Serikali ya Mwaka wa Fedha 2016/17. Malipo ya stahili za watumishi wa umma yatafanywa na Serikali kwa kuzingatia, Sheria, Kanuni na Taratibu zilizopo.

4.Ikumbukwe, Serikali ina utaratibu maalum wa kutoa taarifa kwa Umma, hivyo Serikali itatoa taarifa rasmi kwa Umma kupitia mamlaka husika.

5.Serikali kupitia taarifa hii inawaasa wananchi kuacha tabia ya kusambaza habari za uongo au zisizothibitishwa dhidi yake. Serikali haitasita kuwachukulia hatua za kisheria wale wote watakaobainika kuzusha na kusambaza habari za upotoshaji kuhusu shughuli za Serikali. 

Imetolewa na:

Morocco na Tanzania zasaini mikataba 21 ya ushirikiano Ikulu jijini Dar

$
0
0
Mfalme  Mohammed VI wa Morocco amekubali maombi ya Rais John Magufuli ya kujenga uwanja wa mpira mjini Dodoma ambao utakuwa mkubwa kuliko ule wa Taifa jijini Dar es Salaam sambamba na kujenga msikiti mkubwa jijini humo. 

Rais Magufuli aliyasema hayo Ikulu Dar es Salaam jana wakati akitoa shukrani baada ya kukutana na kiongozi huyo, aliyeambatana na wajumbe 150 ambao pamoja na mambo mengine, nchi hizo mbili zilisaini Mikataba ya Makubaliano (MoU) 21.

Akitoa taarifa fupi ya mazungumzo baina yao, Rais Magufuli alisema Mfalme Mohammed VI amekubali kujenga msikiti mkubwa jijini Dar es Salaam sambamba na kujenga uwanja wa mpira mjini Dodoma wenye thamani ya Dola za Marekani milioni 80 (zaidi ya Sh bilioni 160).

“Katika mazungumzo yetu, nimshukuru Mfalme Mohammed wa Morocco amekubali ombi langu la kujenga msikiti mkubwa hapa Dar es Salaam, na amekubali kwenye mji mkuu Dodoma, atajenga uwanja wa mpira utakaokuwa mkubwa kuliko wa Dar, na thamani yake ni zaidi ya Dola milioni 80,” alieleza Dk Magufuli.

Uwanja wa Taifa umejengwa na Wachina kwa gharama ya Sh bilioni 60 na una uwezo wa kuchukua watu 60,000 waliokaa. Dodoma ambayo ni Makao Makuu ya nchi na Serikali ya Awamu ya Tano imepanga yote kuhamia huko ifikapo mwaka 2020, inao Uwanja wa Jamhuri ambao unamilikiwa na CCM na unachukua watu 8,000.

Mbali na hayo, katika kuimarisha uhusiano baina ya nchi hizo mbili kwenye nyanja ya usalama na ulinzi, Mfalme huyo amekubali kuanzisha programu ya kubadilishana mafunzo baina ya askari wa Tanzania na Morocco na kwa kuanza wiki ijayo askari 150 wa Tanzania watakwenda mafunzoni nchini Morocco.

Katika ziara ya siku tatu ya kikazi ya Mfalme Mohammed VI aliyewasili nchini juzi, akiwa na ujumbe wa wafanyabiashara pamoja na viongozi wengine, wamefanikiwa kufanya makubaliano ya mikataba 21 katika nyanja mbalimbali zikiwamo za kilimo, gesi, madini na na usafiri wa anga.

Mikataba hiyo ni pamoja na Makubaliano ya Jumla katika Ushirikiano wa Uchumi, Sayansi, Ufundi na Utamaduni baina ya Serikali ya Morocco na Tanzania yaliyosainiwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dk Augustine Mahiga na Waziri wa wizara hiyo wa Morocco, Salahddine Mezouar.

Mwingine ni ule wa kuanzishwa kwa Jukwaa la Mashauriano ya kisiasa baina ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na wizara hiyo nchini Morocco, mkataba wa ushirikiano kwenye sekta ya gesi, nishati, madini na sayansi ya miamba, mkataba wa ushirikiano wa usafiri wa anga, mkataba wa ushirikiano kwenye mradi wa mtangamano wa kuwasaidia wakulima wadogo nchini.

Pia mkataba wa makubaliano kwenye sekta ya uvuvi, mkataba wa makubaliano baina na MASEN-Morocco na Wizara ya Nishati na Madini kwa ajili ya maendeleo ya nishati mbadala, mkataba wa ushirikiano baina ya Shirika la Mbolea la Morocco (OCP) na Shirika la Mbolea la Tanzania katika kuendeleza soko la mbolea na kilimo nchini.

Pia mkataba baina ya Bodi ya Utalii Tanzania na Kamisheni ya Utalii Zanzibar na Ofisi ya Utalii ya Taifa nchini Morocco, Mkataba wa Kundi la Utoaji Mikopo la Morocco na Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania, Mkataba baina ya Shirika la Bima la Taifa (NIC) na Shirika la Bima la Morocco.

Mingine ni Mkataba wa Maeneo Maalumu ya Uwekezaji (EPZA) na Kundi la SNTL la Morocco katika ubia wa uendelezaji na utangazaji wa viwanda, mkataba wa usafirishiaji kwenye reli kupitia Kampuni Hodhi ya Rasilimali za Reli Tanzania (RACO) kwa ajili ya ubia kuendeleza reli ya Mtwara-Mchuchuma/Liganga.

Aidha, mkataba mwingine ni ule wa kuanzishwa kwa Baraza la Biashara baina ya Shirikisho la Wafanyabiashara wa Morocco (CGEM) na Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Mkataba wa Mkopo baina ya Benki ya Afrika (BOA) na Hospitali ya CCBRT na mkataba wa mkopo wa BOA na Kampuni ya gesi ya Lake.

Mkataba wa Mkopo wa BOA na Kampuni ya Superstar Forwarders, Mkataba wa Ushirikiano baina ya Kampuni ya OLAM Tanzania na Benki ya Attijariwafa, mkataba wa ubia baina ya Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB)na Benki ya Centrale Populaire ya Morocco, mkataba wa Kitaalamu baina ya Shirikisho la Bima la Morocco na kampuni za bima Tanzania.

Pia mkataba wa ushirikiano baina ya kampuni ya kuchanganya chai ya Morocco na Kampuni ya Afri Tea and Coffee ya Tanzania.

Akizungumzia MoU kwenye usafiri wa anga, Rais Magufuli alisema wamekubaliana nchi hizo mbili kuanzisha safari za ndege za moja kwa moja kutoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam kwenda Rabat, mji mkuu wa nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika.

“Na sisi tumeanzisha shirika letu kidodokidogo linasuasua, lakini tutakuwa na ushirikiano mzuri na Shirika la Ndege la Morocco, na makubaliano haya yote ni mwelekeo nzuri wa kuijenga Tanzania na kuwa na uchumi unaokua kwa asilimia 7.2,” alisema Rais Magufuli.

Rais Magufuli alisema Morocco imepiga hatua kubwa kwenye utalii na kwamba mwaka 2015 ilipokea watalii milioni 10.5 na mwakani wanategemea kupokea watalii zaidi ya milioni 14 na kwamba Tanzania imeshaini makubaliano kwenye sekta hiyo kwa lengo la kuendeleza hifadhi za nchi na kuutangaza utalii.

Aidha, alisema makubaliano yote hayo yamelenga kuijenga Tanzania kuwa nchi ya uchumi wa kati wa viwanda na kwamba hilo linawezekana kwa kuwa hata sasa hali ya uchumi wa nchi ni nzuri kwa kuwa unakua kwa asilimia 7.2; na taarifa za uchumi zinaonesha kwenye robo ya pili ya mwaka uchumi umekua kwa asilimia 7.9.

“Tuko kwa ajili ya kuujenga uchumi na niwakaribisheni wageni wetu kutoka Morocco, niwahakikishieni kuwa mko salama na karibuni kuwekeza kwa faida ya nchi hizo mbili ambazo uhusiano wake ulianza tangu enzi za Iban Batutu wa Morocco aliyetembelea Kilwa miaka mingi iliyopita,” alieleza Rais Magufuli.

Vigogo Bandari Kizimbani kwa Rushwa ya Bilioni 8

$
0
0
Vigogo  watatu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) akiwemo aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa mamlaka hiyo, Ephraim Mgawe (62) wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam wakikabiliwa na mashitaka ya kujihusisha na rushwa ya Sh bilioni nane.

Mbali na Mgawe, vigogo wengine katika kesi hiyo ni Mkurugenzi wa zamani wa Uhandisi wa TPA, Bakari Kilo (59) na aliyekuwa Meneja wa Mazingira wa TPA, Theophil Kimaro (54) pamoja na Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa Kampuni ya DB Shapriya, Kishor Shapriya (60).

Washtakiwa hao walifikishwa mahakamani jana na kusomewa mashtaka mawili na Wakili wa Serikali, Mutalemwa Kishenyi mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba. 

Wakili Kishenyi alidai katika tarehe tofauti kati ya mwaka 2009 na 2012, Mgawe, Kilo na Kimaro kwa kutumia nafasi zao, waliomba rushwa ya Dola za Marekani milioni nne ikiwa ni zaidi ya Sh bilioni nane.

Inadaiwa waliomba rushwa hiyo kutoka kwa Shapriya ili kumuwezesha ashinde zabuni iliyokuwa ikishindaniwa yenye namba AE/0116/2008-2009/10/59 kwa ajili ya ujenzi wa bomba la TPA katika RAS ya Mjimwema.

Aidha, inadaiwa katika tarehe tofauti kati mwaka 2008 na 2009 akiwa kama Mkurugenzi wa DB Shapriya alitoa rushwa ya Dola za Marekani milioni nne kwa vigogo hao, kwa ajili ya kuiwezesha kampuni yake ishinde zabuni. Baada ya kusomewa mashtaka hayo, washtakiwa walikana kuhusika na kutenda makosa hayo.

Wakili Kishenyi alisema upelelezi wa kesi bado unaendelea, pia hawana pingamizi la dhamana endapo washtakiwa watatimiza masharti ya dhamana yatakayotolewa na mahakama.

Vigogo hao waliachiwa kwa dhamana baada ya kutimiza masharti ya dhamana yaliyowataka kuwa na wadhamini wawili waaminifu watakaosaini hati ya dhamana ya Sh milioni 500 kwa kila mmoja.

Mawakili Wambana Ester Bulaya Mahakamani....Vielelezo Idadi ya Wapiga Kura Vyatofautiana

$
0
0
Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini (Chadema), Ester Bulaya jana alikaliwa kooni na mawakili wa wadai katika kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi 2015 wakimtaka kutoa ufafanuzi wa idadi ya wapigakura waliojiandikisha kwenye daftari la wapiga kura.

Katika uchaguzi mkuu wa ubunge Jimbo la Bunda Oktoba 25, 2015, Bulaya alimbwaga mgombea wa CCM na mwanasiasa mkongwe, Stephen Wasira lakini wapigakura wanne walifungua kesi katika Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza kupinga matokeo. Ester alikuwa mbunge wa viti maalumu CCM, lakini alihamia Chadema na kumshinda mkongwe Wasira.

Katika kesi hiyo ambayo vikao vyake vinafanyika mjini Musoma na ikiwa ni siku yake ya kwanza kutetea ubunge wake, Bulaya alibanwa na mawakili wa walalamikaji wanaopinga ushindi wake baada ya idadi ya wapiga kura iliyoandikwa kwenye kiapo chake kuwa tofauti na iliyoandikwa na msimamizi wa uchaguzi kwenye fomu namba 24B ya matokeo ya uchaguzi.

Bulaya alidai idadi ya wapiga kura walioandikishwa katika fomu ya matokeo namba 24B aliyopewa ilikuwa 69,369 lakini imetofautiana na aliyokuwa nayo msimamizi wa uchaguzi ambayo kuna jumla ya wapiga kura 69,460 baada ya kujumlisha kura zote.

Wakili wa upande wa mleta maombi, Hajra Mungula alitaka kujua kutoka kwa mbunge huyo idadi ipi sahihi kati ya ile aliyoandikiwa na msimamizi wa uchaguzi kwa mkono baada ya kuikataa ile ya kwanza na kutangaza idadi ya wapigakura wa wilaya nzima ya Bunda ambao ni 164,794 au ile iliyotangazwa na msimamizi huyo.

Mbunge huyo alidai kuwa wakati msimamizi anabadilisha idadi hiyo hakuona takwimu sahihi wakati anaandika kwa kuwa alikuwa amekaa mbali kidogo ila aliamini kilichokuwa kinaandikwa na msimamizi huyo ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo, Lucy Msofe

Wakili huyo alitaka kujua ilikuwaje hadi akaijua idadi hiyo ya wapiga kura wa wilaya nzima waliojiandikisha ambao ni 164,794 wakati hajui idadi ya wapigakura katika majimbo mengine ya wilaya hiyo? Mbunge huyo alijibu kuwa yeye aliifahamu idadi hiyo baada ya kupitia daftari la wapiga kura kabla ya uchaguzi kuanza.

Alidai alifahamu idadi hiyo kwa kuwa aliwahi kuwa diwani na alishakuwa kiongozi kabla ya kuwa mbunge na kusema kuwa taarifa za idadi ya wapiga kura kwa kawaida siyo siri.

Mbunge huyo alieleza kuwa tofauti ya idadi ya wapiga kura 69,460 na 69,469 haikuwa sawa lakini pia haikuathiri matokeo ya uchaguzi katika jimbo hilo wala kuathiri idadi yoyote ya wapiga kura kwa kuwa tofauti hiyo ni ndogo sana.

Alipohojiwa na wakili wa mleta maombi wa tatu Constantine Mutalemwa, “Ni nani aliyeziingiza takwimu hizo zinazopishana kwenye fomu namba 24B ya matokeo ya uchaguzi, Mbunge huyo alijibu kuwa aliyeingiza takwimu hizo kwenye fomu namba 24B ni msimamizi wa uchaguzi.

Mawakili wa upande wa Serikali ni Angela Lushagala na Michael Haule; Bulaya anatetewa na Tundu Lissu huku upande wa waleta maombi watatu mawakili ni Yasini Membe, Hajra Mwingula na Constantine Mutalemwa.

Kesi hiyo inaendelea kusikilizwa katika mahakama hiyo chini ya Jaji Noel Chocha.


RIWAYA: She is My Wife- Sehemu ya 29 & 30

$
0
0
MWANDISHI : EDDAZARIA

ILIPOISHIA
Mtu huyo wa ajaba akaendelelea kutazama tazama kila kona ya sable hii, akapiha hatua mbili mbele na kuzama ndani kabisa ya sable hii, na kuwapa mgongo Rahab na Raisi Praygod walio simama nyuma yake. Akaendelea kuvuta vuta pumzi, iliyo muashiria kwamba humu ndani kuna binadamu waklio hai, akalikoki bunduli lake aina ya gobore na kulishika vizuri huku kidole chake kimoja akiwa amekizamisha kwenye traiga, kwa haraka  akageuka nyuma na kuwaona Rahab na Raisi Praygod wakiwa nyuma yake wanamtazama

ENDELEA
Kwa haraka Rahab akaruka hewani na kuipiga teke bunduki ya mtu huyu mwenye muonekano wa ajabu sana, bunduki yake ikaanguka chini na kumpa nafasi nzuri Raisi Praygod kumrukia mtu huyo kwa kutumia bega lake lililo tua begani kwa mtu huyo na wote wawili wakaanguka chini.

 Rahab kwa haraka akaiokota bunduki ya mtu huto na kwakutymia kitako cha bunduki hiyo aina ya gobore akampiga nayo kichwani zaidi ya mara kumi mtu huyo, na kupelekea kichwa cha mtu huyo kupasuka kwa na kuvuja damu yenye rangi nyeusi ti.
“Mtu gani huyu….?”
Rahabu aliuliza huku akihema kwa nguvu akionekana kuchanganyikiwa kwa kumuona mtu wa aina hii ambaye tangu azaliwe hajawahi kumuona.

“Tuondike hakuna haja ya kuendelea kukaa hapa”
Raisi Pragod alizungumza huku akichungulia mlangoni kutazama kama wale watu wengine wa kutisha wamesha ingia ndani walipo kua wakiingiza mizoga ya watu walio waua. Wakatoka nje wakiwa katika tahadhari kubwa huku Rahab aklwa ameishika bunduki ya mtu huyo.

Wakafanikiwa kutoka nje pasipo kuonekana na watu hao ambao wapo ndani ya kijumba chao wakiendelea kuwakata kata vipande marehemu walio wachukua na kuwafanya ndio chakula chao cha usiku. Wakaanza kutokomea porini huku wakimuomba Mungu waweze kutoka kwenye msitu huu ambao bado haujawapa matumaini ya kuweza kuziokoa nafsi zao zilizo kwenye matatizo makubwa

Hasili ya watu hawa wa kutisha wanajulikana kama Mazombi, walio anza kujitokeza mwaka 1819 katika bara la ulaya. Inasemekana watu hawa ni wale walio weza kupoteza maisha kwa sumu zenye kemikali kubwa na waliweza kurudi katika ulimwengu huu wakiwa katika hali hiyo ya kutisha na kuweza kuwafanya wanadamu halisi kama ndio vitoweo vyao vya kila siku.

Rahab na Raisi Praygod wakaendelea kukata mbuga pasipo kuchoka, japo wanatamani kuweza kupata japo dakika waweze kupumzika, ila kila walipo kumbuka maiti za watu walio waona wakishushwa na mazombi hayo hawakutamani kamwe kuweza kusimama.

Hali ya majonzi ikawatawala mazombi walio mshuhudia mwenzoa aliye pasuliwa kichwa na kusababisha ubongo wote kumwagika nje. Hawakua na hamu hata ya kuendelea kupata vitoweo walivyo kuja navyo na ziadi kila mmoja akachukua silaha yake na kuingia msituni kufwatilia watu hao walio sababisha mauaji ya mmoja wao. Kutokana na kuufahamu vizuri msitu wao, wakajigawa kwenye makundi ya mazombi wawili wawili na kupelekea kuwa na vikundi vinne. Kila mmoaja akajiapiza kuweza kufanya mauaji ya kikatili kwa watu walio sababisha mauji ya mpendwa wao
                                                                                                    ***
Samson na wezake wakafanikiwa kufika katika kiswa cha Kunashir nchini Russia, kwa bahati nzuri wakafanikiwa kupokelewa na mkuu wa kikiso kilicho asi nchi ya Russia bwana Rusev, Wakapelekwa moja moja kwa moja kwenye jengo lenye ofisi za kikundi hichi kinacho endelea kufanya mapinduzi kwenye nchi yake ikiitaka serikali kuweza kuunda serikali mbili, ili wao  wajipatie mamlaka ya kuweza kutengeneza silaha hatari za nyuklia.

Kila mmoja akakabidhiwa kinywaji alicho kihitaji yeye, ili kuweza kujipozwa kwa uchovu mwingi wa safari yao ndani ya maji, tangu pale walipo kamtwa na jeshi la polisi nchini Tanzania. Fetty na wezake hawakuwa na uwezo wa kuielewa lugha ya kirusi, ambayo Samson yeye aliweza kuizungumza vizuri pasipo matatizo ya aina yoyote. Alicho kua akikifanya Samson ni kuwatafsiria kila kitu ambacho alicho kua akikizungumza na bwana Rusev.

“Jamaa anauliza eti, tunaweza kujiunga na kundi lake?”
“Mmmm……!!” Anna aliguna
“Hatuwezi sisi tupo hapa kwa ajili ya biashara”
Samson akamjibu bwana Rusev kitu alicho kizungumza Fetty anaye onekana kuto kubaliana na swala zima la wao kujiunga na kundi la bwana Rusev
“Je anauliza tunahitaji kiasi gani cha pesa ili tuweze kumkabidhi hii manohari?”
“Sasa hapo ndio umenena la maana” Halima alizungumza huku akitabasamu
“Anatulipa kwa dola au shilingi?” Agnes aliulza
“Hembu na wewe acha ushamba wako, huku shilingi aitolee wapi?” Fetty alimkosoa mwenzake
“Haya yaishe kiongozi Fetty”
“Muambia sisi tunataka dola milioni mia zinatutosha”
Samson akamgeukia bwana Rusev na kumueleza kiasi walicho kitaja wezake na bwana Rusev hakuwa na hiyana zaidi ya kukubali kuwalipa kiasi hicho.


Serikali kuziba pengo la wahadhiri waandamizi

$
0
0
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Serikali itaendelea kutafuta fedha za mafunzo kwa ajili ya wahadhiri wa vyuo vikuu nchini ili kuziba pengo la wahadhiri waandamizi lililopo hivi sasa

Waziri Mkuu  pia amevitaka vyuo hivyo viweke utaratibu wa kuachiana nafasi ama kurithishana kazi (succession plan).

Amesema yeye binafsi anatambua upungufu uliopo umesababishwa na masharti ya ajira za mkataba kwa wahadhiri waandamizi kuwa miaka 65 na maprofesa kuwa miaka 70.

Ametoa kauli hiyo leo (Jumanne, Oktoba 25, 2016) wakati akifunga kilele cha maadhimisho ya miaka 55 ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam yaliyoanza jana kwenye ukumbi wa Nkrumah. Kampasi ya Mwalimu J. K. Nyerere, jijini Dar es Salaam.

“Ninatambua kuwa katika vyuo vya umma kuna upungufu mkubwa wa wahadhiri waandamizi na maprofesa na hivyo kuathiri hali ya utoaji wa taaluma kwa fani za ‘Post-Graduates’. Ninajua kuwa pamoja na sababu nyingine, hali hii inachangiwa pia na masharti ya ajira za mikataba kwa wahadhiri waandamizi kuwa miaka 65 na maprofesa kuwa miaka 70.,” amesema.

Akizungumzia kuhusu maslahi ya watumishi wa vyuo hivyo, kikiwemo Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Waziri Mkuu amesema Serikali ya awamu ya tano imedhamiria kuhakikisha inaondoa malimbikizo ya madai kwa watumishi wote wa umma na hivi sasa inakamilisha uhakiki wa taarifa za kiutumishi kwa watumishi wa umma ili kubaini watumishi hewa.

“Hadi kufikia tarehe 20 Oktoba, 2016 zoezi linaloendelea hivi sasa, limesaidia kuwabaini watumishi wa umma hewa wapatao 16,500. Baada ya zoezi hilo, tutarudia uhakiki wa madeni yote yaliyowasilishwa Serikalini na kisha tutalipa madeni ya watumishi wote,” amesema.

Akifafanua kuhusu mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu, Waziri Mkuu amesema Serikali inaendelea kufanya uhakiki wa taarifa za waombaji wa mikopo. Ametoa wito kwa wanufaika na waombaji wote wa mikopo wahakikishe kuwa wanatoa taarifa zilizo sahihi na za uhakika.

Hata hivyo, Waziri Mkuu amesema Serikali ilikwishaongeza bajeti ya mikopo ya elimu ya juu kutoka sh. bilioni 340 mwaka 2015/2016 hadi sh. bilioni 483 kwa mwaka 2016/2017.

Mapema, akielezea utendaji kazi wa chuo hicho katika miaka yote 55, Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Prof. Rwekaza Mukandala amesema chuo hicho kinakabliwa na changamoto ya uhaba wa wanataaluma waandamizi wa fani mbalimbali.

“Chimbuko la changamoto hii ni kusitishwa kwa ajira katika taasisi za umma kwenye miaka ya 1990. Kutoajiriwa kwa wanataaluma chipukizi kwa miaka mingi, kulivuruga utaratibu wa miaka mingi wa kurithishana uzoefu baina ya wanataaluma wanaostaafu na wale ambao wangelichukua nafasi zao,” amesema.

“Hali hii iko kwenye vyuo vikongwe ambako mamia ya wanataaluma wazoefu wanastaafu kwa wakati mmoja na wengi wa wanataaluma walioajiriwa hivi karibuni bado wako masomoni au wangali chipukizi katika taaluma zao na hivyo hawana uwezo wa kutosha kubeba majukumu ya kufundisha katika ngazi za digrii za umahiri na uzamivu,” amesema.

Wakati huohuo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Leonard Akwilapo alisema wizara hiyo imetenga kiasi cha sh. bilioni 9 kwa ajili ya kufanya ukarabati wa miundombinu kwenye chuo hicho zikiwemo maabara.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya Octoba 26

Tanzania Yapata Mkopo Wenye Masharti Nafuu Wa Zaidi Ya Shilingi Bilioni 300 Kutoka Benki Ya Maendeleo Ya Afrika (Afdb) Na Serikali Ya Korea

$
0
0
Benny Mwaipaja, WFM, Seoul, Korea
TANZANIA, Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) na Korea ya Kusini zimetiliana saini makubaliano ya pamoja kutekeleza mradi wa ujenzi wa njia ya umeme gridi ya Kaskazini Magharibi inayoanzia mkoani Mbeya, Nyakanazi hadi Kigoma, yenye msongo wa kV 400 mbapo Serikali ya Korea imeahidi kutoa Dola za Marekani milioni 50 sawa na zaidi ya shilingi Bilioni 100.18, kwa ajili ya kugharamia mradi huo.
 
Hali kadhalika, Tanzania na Benki ya Exim ya Korea, zimesaini  Mkataba wa mkopo wenye masharti nafuu wa Dola za marekani milioni 90.092 sawa na zaidi ya shilingi Bilioni 194 za Tanzania, kwa ajili ya mradi wa Upanuzi wa Miundombinu ya mfumo wa maji taka Jijini Dar es salaam.
 
Kwa upande wa Tanzania, Makubaliano pamoja na Mkataba vimesainiwa na Mhe. Dkt. Philip Mpango (MB) Waziri wa Fedha na Mipango kwa niaba ya Serikali, Oktoba 25, 2016 Jijini Seoul nchini Korea Kusini huku upande wa AfDB, aliye saini ni Rais wa Benki hiyo Adesina Akinwumi, na kwa upande wa Benki ya Exim, mkataba huo umesainiwa na Mwenyekiti ambaye pia ni Rais wa Benki hiyo Lee Duk-Hoon.
 
Akizungumza mara baada ya kutia saini makubaliano na mkataba huo, Dkt. Mpango amesema makubaliano na mkataba vilivyosainiwa vina manufaa makubwa kwa wananchi wa Tanzania.
 
“Wananchi wa Upande ule waanze kufurahia kwamba maendeleo yanakuja na hasa tunaposema maendeleo ya viwanda ambavyo ni lazima vitumie umeme, na kwamba mradi huu unatarajia kupelekwa hadi Mbeya” Amesisitiza Dkt. Mpango.
 
Dkt. Mpango, amesema kuwa mradi huo una umuhimu mkubwa pia kwa kuwa serikali imedhamiria kuufungua ukanda wa Magharibi mwa Tanzania, kwa upande wa viwanda vya aina mbalimbali.
 
Kwa upande wake, Naibu Mkurugenzi Mtendaji (Uwekezaji) wa Shirika la Ugavi wa Umeme nchini Tanzania-TANESCO, Decklan Mhaiki, amesema mradi wa umeme wa Nyakanazi hadi Kigoma utakuwa na urefu wa kilometa 280 na utakapo kamilika utaondoa changamoto ya shirika hilo kuzalisha umeme unatumika katika ukanda huo wa Magharibi hususan Kigoma, kwa kutumia majenereta ambayo uendeshaji wake ni ghali na umeme wake si wa uhakika.
 
“Kuleta laini kama hii, kwanza itapunguza gharama kubwa, na umeme wa ziada utakao zalishwa tunaweza kuuza nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia Congo, upande wa pili wa Ziwa Tanganyika, lakini kikubwa ni kuwahakikishia wananchi wa mkoa wa Kigoma kuwa na umeme wa uhakika” ameongeza Bw. Mhaiki.
 
Akizungumzia mkataba wa ujenzi wa miundombinu ya maji taka Jijini Dar es salaam, Dkt. Philip Mpango, amebainisha kuwa mradi huo unatarajia kuwa na tija kwakuwa utatatua changamoto ya majitaka kutuama mitaani hasa wakati wa mvua na kusababisha magonjwa ya mlipuko kikiwemo kipindupindu.
 
Akifafanua kuhusu mradi huo, Mchumi ambaye pia ni  Afisa anayeshughulika na utafutaji wa Fedha za Nje kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Melckzedek Mbise, amesema kuwa mradi wa maji wa Ruvu  unatarajia kuongeza wingi wa maji Jijini Dar es salaam, utakaosababisha uzalishaji wa maji taka pia kuongezeka, hivyo mradi huo wa kuondoa maji taka umekuja  wakati muafaka.
 
“Mradi huu umekuja wakati muhimu na mkopo una masharti nafuu sana” Amesisitiza Bw. Mbise.
 
Naye Afisa Mkuu wa utafutaji rasilimali kutoka Wizara ya Fedha na Mipango Zanzibar, Sabra Issa Machano, amesema kuwa  kati ya nchi 54 za Kiafrika zinazohudhuria mkutano wa Tano wa Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Korea na Afrika, Mjini Seoul Korea, ni nchi nne tu zilizopewa mkopo na ufadhili ambazo ni Kenya, Uganda na Ethiopia, huku Tanzania ikipewa kiasi kikubwa zaidi cha fedha jambo linaloonesha kuwa Tanzania inakubalika Kimataifa.

Rais Magufuli Ateuliwa kuwania tuzo ya Forbes kwa watu maarufu barani Afrika

$
0
0
Rais wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli ameingia katika listi ya watu ambao wametajwa kuwania tuzo ya Person Of The Year 2016 ambayo hutolewa na Jarida la Forbes Africa.

Rais Magufuli ameingia katika kinyang’anyio hicho, akiwania tuzo hiyo pamoja na Mwanzilishi wa Capitec Bank, Michiel le Roux, Thuli Madonsela, Ameenah Gurib na watu wa Rwanda.

Kama Rais Magufuli atafanikiwa kushinda tuzo hiyo, basi Tanzania itakuwa imepata tuzo hiyo kwa mara ya pili mfululizo kwani mwaka jana 2015, mshindi wa tuzo hiyo alikuwa Mkurugenzi Mtendaji na Rais wa Makampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania Limited (MeTL Group), Mohammed Dewji.

Utaratibu wa jinsi ya kupiga kura kwa mwaka huu ni kutumia tovuti ya http://poy2016.com/ ambapo baada ya kuingia hapo, unaweza kugusa jina la mtu ambaye unapendekeza ashinde tuzo na hapo kura itakuwa imehesabiwa.

Umeya Kinondoni: CHADEMA Wafungua Kesi Mahakamani, Wadai Uchaguzi Haukuwa Halali

$
0
0
Viongozi  wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) wamekimbilia mahakamani kupinga matokeo ya uchaguzi wa umeya na naibu meya wa Manispaa ya Kinondoni katika Jiji la Dar es Salaam uliompa ushindi Diwani wa Msasani, Benjamin Sitta wa CCM kuwa Meya.

Ukawa kupitia kwa Wakili wao, John Mallya wamewasilisha kesi hiyo jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam kupinga matokeo ya uchaguzi uliofanyika Oktoba 23 mwaka huu, kwa kuwa ulikuwa batili na ulikiuka taratibu za kisheria.

Mallya alisema kesi hiyo ambayo walalamikaji ni aliyekuwa Naibu Meya wa Manispaa hiyo, Jumanne Mbunju na aliyekuwa mgombea wa umeya, Diwani wa Kata ya Kinondoni, Mustafa Muro, imepokelewa lakini haijafunguliwa.
 
Mbali na Sitta, walalamikiwa wengine katika kesi hiyo ni Naibu Meya, Manyama Mangaru, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, Aron Kagurumjuli na Ofisa Tawala wa Halmashauri hiyo.

Akizungumza baada ya kesi hiyo kupokelewa, Wakili Mallya alisema wamefungua kesi hiyo kupinga kile wanachoita uchaguzi ambao CCM walikaa wenyewe na kupigiana kura.

Alisema: “Katika kesi hiyo tunaiomba Mahakama itengue uamuzi uliomchagua meya huyo, iamuru manispaa iitishe uchaguzi wa umeya mara moja pia imuamuru Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa na wasimamizi wa uchaguzi wafuate taratibu za kisheria.”

Katibu wa Chadema mkoa wa Dar es Salaam, Henry Kileo alisema wamefika mahakamani kutafuta haki kwa sababu wanaamini wamenyang’anywa haki yao.

Alisema kilichosababisha uchaguzi wa Ubungo kuahirishwa ni kukiukwa kwa taratibu hivyo Mkurugenzi na Ofisa Tawala wa Ubungo walipoona taratibu zimekiukwa Kinondoni, waliamua kuahirisha uchaguzi.

“Kilichofanyika siku ile ilikuwa ni kuchagua Mwenyekiti wa CCM, lakini siyo uchaguzi wa kumchagua meya wa Kinondoni kwa sababu hata kisheria, uchaguzi unatakiwa kuwa robo tatu ya wajumbe ambao walitakiwa kuwa 23, lakini walikuwa 18, ndiyo maana hata matokeo yalikuwa kura 18,” alisema.

Alidai madiwani wao walinyimwa fursa ya kuingia manispaa na kuwasilisha malalamiko yao hivyo hawamtambui Meya wa Kinondoni na kwa sasa hakuna Meya wa Manispaa hiyo.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images