Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Serikali Yakubali Kurejesha Posho ya Sh. 8500 kwa Siku kwa Wanafunzi wa Vyuo Vikuu Nchini

0
0
Bodi ya Mikopo kwa Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetuliza hasira za wanafunzi wa vyuo vikuu kwa kurejesha posho ya chakula na malazi ya Sh8,500 kwa kila mmoja na kwamba tofauti baina yao itakuwa viwango vya ada.

Ufafanuzi huu uliotolewa jana usiku na Waziri wa Elimu, Sayansi , Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi Profesa Joyce Ndalichako wakati akizungumza katika mahojiano maalimu na kituo cha runinga cha Taifa -TBC utakuwa faraja kwa wanafunzi ambao chini ya Serikali ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Daruso) walipanga kushinikiza walipwe posho ya Sh8,500 kwa siku kama ilivyokuwa awali. 
 
Hatua ya wanafunzi kujenga umoja ili kushinikiza haki katika posho ilitokana na baadhi yao kuingiziwa kati ya Sh40,000 na 70,000 badala ya Sh 510,000, hali ambayo ilizua sintofahamu. 

Ndalichako alisema tofauti ya malipo itakuwa katika ada na siyo posho, “Vigezo vya mikopo vimebadilika, kila mwanafunzi atapata fedha tofauti lakini tumefanya marekebisho kwenye posho ya chakula ambayo kila mwanafunzi atalipwa Sh8,500 kama awali.” 

Kwa mujibu wa utaratibu wa Bodi hiyo, malipo hayo ya chakula na malazi hutolewa kila baada ya miezi miwili. 

Mapema jana, Daruso iliwataka wanafunzi wa chuo hicho kutotia saini fomu za fedha za mikopo yao mpaka itakapowapa ruhusa ya kufanya hivyo. 

Rais wa Daruso, Erasmi Leon alisema hayo jana wakati akizungumza na wanafunzi wenzake kuhusu kusudio la kwenda HESLB kwa ajili ya kutafuta haki yao ya msingi. 

“Ninachowasihi tuwe pamoja. Tuwe wamoja na twende pamoja. Tutakwenda wawakilishi kutafuta nafasi kwa amani waweze kusikia tuna hoja gani lakini tukinyimwa hii nafasi tutaenda kuitafuta tukiwa wengi,” alisema na kuongeza:

 “Tuwe watulivu kwa sasa tutakapowahitaji muda na wakati wowote kwa lolote tushirikiane ili twende pamoja tumalize pamoja tuhakikishe tunapata Sh8,500 kwa kila mwanafunzi kwa chakula na malazi,” alisema. 

Kuhusu suala hilo, uongozi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) ulisema wajibu wake ni kupokea na kusambaza majina na taarifa kutoka Bodi kwa wanafunzi. 

Akitoa ufafanuzi kwa wanafunzi waliofika ofisini kwake kujua hatima yao na waliopata mikopo kuchukua fomu za kutia saini, Ofisa Mikopo wa UDSM, Lugano Mwakyusa alisema wenye jukumu la kujua walio na sifa ya kupata mikopo ni Bodi ya Mikopo. 

“Tunaendelea kupokea majina kutoka bodi. Tayari hapa kuna majina 949 yameshatoka, wengine tuzidi kusubiri na wale mwaka wa pili na tatu ambao walikuwa na mitihani ya marudio taarifa zao zitapelekwa bodi,” Mwakyusa aliwaambia wanafunzi waliokuwa wamejaa ofisini kwake.

 Kulikuwa na hali ya sintofahamu chuoni hapo jana baada ya wanafunzi wengi wa mwaka wa kwanza kuonekana wakiwa wameshika bahasha za kaki zilizokuwa na fomu za usajili wanazotakiwa kujaza huku wakihangaika kutokana na kutojua kiasi cha mkopo. 

Juzi, Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, AbdulRazaq Badru alieleza kwamba ingawa wanafunzi 88,000 waliomba mikopo kutoka HESLB, uwezo wa bodi hiyo ni kutoa kwa wanafunzi 21,500 pekee sawa na asilimia 24 na waliokuwa wameshapatiwa walikuwa 11,000 sawa na asilimia 12. 

Takwimu hizi zinaonyesha zaidi ya robo tatu ya wanafunzi wanaohitaji mikopo watakosa kutokana na uwezo mdogo wa kifedha.

Fahamu Jinsi Ya Kutibu Magonjwa Zaidi Ya 20 Kwa Kutumia Tiba Asilia

0
0

Mti  wa  ukwaju. Majani yake hutumika  katika  tiba  ya  kuongeza  maziwa  kwa  mama  anaye nyonyesha.
Tiba   Ya   Miguu   Kuwaka  Moto
:
1.   Chukua  majani  ya  mti  wa  Mvumbasi, unguza  pamoja  na majani ya  mti  wa  mnungunungu, halafu changanya na  mafuta  ya  taa  lita  moja. Matumizi:  Utakuwa unatumia  kujichua kwenye  miguu  kutwa  mara  tatu  kwa  muda  wa  siku  thelathini. Utapata  nafuu  kubwa  sana.
Tunda  la  topetope;Mizizi ya  mtopetope hutumika  katika  tiba  ya  kuondoa  uvimbe  kwenye  kizazi.
2.     TIBA   YA  KIKOHOZI: Tafuna  majani  ya  mti wa mbaazi. Mbali  na  kutibu  kikohozi, mti  wa mbaazi, unatibu  magonjwa mengine  mengi.  Mfano, mizizi ya  mti wa  mmbaazi, husaidia  kutibu  chango la  kiume  na  kusafisha kibofu cha  mkojo.
 
3.   KUVIMBA  KWA  TEZI LA  SHINGO:  Kama una  sumbuliwa  na  tatizo  la  tezi kuvimba, chukua  unga  wa  Kamun Nyeusi, kisha  changanya  na sega  la  nyuki, halafu  tumia  kukanda kwenye  tezi, kila  siku  kwa  muda wa mwezi  mmoja. Utapata mafanikio  makubwa  sana.
 
4.   TIBA  YA MAUMIVU  YA  MGONGO, MIGUU, NYONGA NA  KIFUA  KUPASUA:
Kama una  sumbuliwa  na  maumivu  ya  mgongo, miguu, nyonga  na  kifua  kupasuka, fuata  maelekezo  yafuatayo:
Chukua mafuta  ya  nyonyo robo lita, mafuta ya   Kamun Nyeusi kiasi cha robo lita pamoja  na  mafuta ya  karafuu robo  lita , changanya  pamoja  halafu  uwe  unatumia  kujichua  sehemu yenye  maumivu, kutwa  mara tatu  kwa siku  thelathini. Utapata  nafuu  kubwa sana.
 
5.   TIBA  YA  KWIKWI : Kama unasumbuliwa  na  kwikwi, fuata  maelekezo  yafuatayo : Chukua  majani ya  mwembe  mkavu, pekecha  kisha  mpe  mgonjwa  atumie  kuvuta  kama  sigara  halafu awe  anameza moshi.  Tatizo  la  kwikwi  litaisha. 
 
6.    Tatizo  La  Kukojoa  Kitandani ;  Kama  una  tatizo  la  kukojoa  kitandani, tumia mizizi ya  mbaazi  kwa  kuchemsha, na  kunywa  maji  yake  kutwa mara  mbili  kwa  siku, kwa muda wa siku  kumi  na  nne.

7.    Tatizo  la  uvimbe  kwenye  kizazi :  Kama  una  tatizo  la  uvimbe  kwenye  kizazi, chukua  mizizi  ya  mtopetope,  tumia kwa  kuchemsha  na kisha  kunywa  maji  yake, mara  tatu  kutwa  kwa siku  thelathini.
 
8.     Vidonda  vya  koo : Kama una  tatizo  la  vidonda  vya  koo, chukua maji  ya  uvuguvugu kiasi  cha nusu  lita, kisha  kamulia  ndimu  tatu fresh, halafu  tumia  kusukutulia. Utafanya  hivyo  mpaka, utakapo  pata  nafuu.
 
9.   Malaria sugu :  Kama  una  malaria sugu, chukua  maji  ya  dafu  moja, weka  kwenye chombo  kisafi, kisha  kamulia  ndimu  saba, halafu  tumia  kunywa. Fanya  hivyo  mara  mbili  kwa  siku, asubuhi  na  jioni  kwa  siku  tatu hadi  saba. Hakika  utapata  matokeo  mazuri  sana.
 
10.         Tiba  ya  tatizo  la kutoa harufu  mbaya  kinywani, sehemu  za  siri, kikwapa  na  jasho lenye  harufu  mbaya :   Chukua  maji  yaliyo  lowekewa  mchele  kiasi  cha  lita  moja, kisha  tumia  kunawia  sehemu  husika  na  kusukutulia  mdomo. Utafanya  hivyo mara  tatu  kwa  siku  hadi  utakapo  ridhika  na  matokeo  unayo  yahitaji.
 
11.          Kwa wakina  mama; Jinsi yakuzuia uchungu wamimba,maumivu yakiuno, maumivu wakati wahedhi, na damu itokayo bila mpangilio wasiku maalumu,Chukua majani ya mbigili yatwange halafu changanya navijiko vitatu  vikubwa  vya unga wa mti unaitwa msonobali kisha  tumia kunywa glasi 1 yenye  ujazo  wa  milimita  mia  mbili  na  hamsini,  kutwa  mara  tatu hadi  hali yako  itakapokua nzuri
 
12.         Tiba  Ya Vidonda  Vya  Tumbo,Kisukari  pamoja   na  Typhoid:
Chukua mizizi ya mti wa  msongati pamoja na majani ya mkalatusi  vitwange kwa pamoja  kisha  chemsha  kwenye  maji  lita moja,  halafu tumia  kunywa glasi moja ya  robo  lita, mara  tatu kwa  siku  kwa  siku  thelathini. 
 
13.         Tiba  Ya  Tatizo  La  Kukosa  Hamu  Ya  Tendo La  Ndoa  Kwa  Wanawake :   Kama  wewe  ni  mwanamke  unaye  sumbuliwa  na  tatizo  la  kukosa  hamu ya  tendo  la  ndoa,  unaweza  kutibu  tatizo  lako  kwa  kutumia  vyakula  mbalimbali  kama  ifuatavyo :
i.                   JUISI  YA  MIWA :  Tumia  kunywa  nusu lita  hadi  lita  moja  ya  juisi  ya  miwa, mara  tatu  kwa  siku asubuhi, mchana  na  jioni  kwa  siku  thelathini. Utapata  matokeo  mazuri. Mbali  na  kuwasaidia  akina  mama  wenye  tatizo  la  kukosa  hamu  ya  tendo  la  ndoa, juisi  ya  miwa  ina  faida  nyingine  nyingi  kitabibu. Moja kati  ya  faida  kubwa  za  juisi  ya  miwa, ni  uwezo  wake  mkubwa  wa  kusafisha  figo. Hivyo  hata  wanaume  wanashauriwa  kutumia  juisi  ya  miwa  au  miwa  kwa  wingi,kwa  sababu  inasaidia  kusafisha  figo, na  figo  ni  moja  kati  ya  ogani  muhimu  sana  katika  mfumo  wa  nguvu za  kiume.
ii.              MBEGU ZA FENESI : Chukua  mbegu za  fenesi  kiasi  cha  robo kilo,  kisha  chemsha  na  maji lita  mbili, halafu  tumia  kula  pamoja  na  supu yake. Utafanya  hivyo  mara  tatu  kwa  siku kwa  muda  wa  siku  thelathini. Hakika  utapata  matokeo  mazuri  sana.  Unaweza  pia  kuzisaga  na  kutumia  unga  wake, kwa  kuchemsha  na kunywa, kwa  kufuata  utaratibu  huo  hapo  juu.
iii.           KOROSHO : Tumia  kula  korosho  pakti  moja  yenye  ujazo wa  robo  kilo, mara  tatu kwa  siku, asubuhi, mchana  na  jioni  kwa  siku  thelathini. Yaani  asubuhi, tumia  robo kilo, mchana  robo  kilo  na  jioni  robo  kilo kwa siku  thelathini. Utapata  matokeo  mazuri.
iv.            MIHOGO  MIBICHI :  Tumia  kutafuna  walau  vipande  vitatu  vya  mihogo  mibichi  kwa  siku, kwa muda  wa  siku  thelathini. Yaani  asubuhi  utumie  kipande  kimoja  kikubwa,mchana kipande  kimoja  kikubwa  na  usiku, utumie  kipande  kimoja  kikubwa.
 
14.         TIBA  ASILIA  YA  TATIZO  KIFUA KISICHO PONA  KWA  WATOTO  WADOGO WALIO KUNYWA UCHAFU WAKATI WA KUZALIWA, PUMU, KIFUA KISICHO PONA KWA WATU WAZIMA,KICHOMI,KUWASHWA MWILI NA KUPALIWA WAKATI UMELALA USINGIZINI
Tiba  Yake, chukua majani  ya  mpera kiasi  cha kama  viganja  vinne, yaponde  pamoja  na magome  ya  muembe kiasi  cha viganja  vinne, na  tunda  la  koma manga, twanga  vyote  kwa  pamoja  ( Yani majani  ya  mpera, magome  ya  muembe na tunda  moja  la  komamanga ).
Ukisha  maliza  kutwanga, changanya  na  maji  lita mbili  halafu  chemsha  pamoja na lita  moja  ya  asali mbichi  ya  nyuki  wadogo. 
 
Chemsha  hadi  itokote, halafu  ipua  dawa  yako.
 
 Matumizi : Kwa  mtoto  mdogo mwenye  umri wa  kati ya  mwaka  mmoja na  miaka  mitano, tumia  kumpa  kijiko kimoja  kikubwa  mara  mbili kwa  siku, asubuhi  na  jioni n  kwa  siku  saba.
 
Na kwa  mtu mzima, tumia  kunywa  vijiko  vikubwa   viwili  mara  mbili  kwa siku  asubuhi na  jioni, kwa siku  ishirini  na  moja

15.         KUJITIBU  TATIZO LA  MTOTO  WA  JICHO :  Kujitibu  mtoto  wa  jicho, tumia  kunyunyizia  jichoni  matone mawili ya  utomvu  wa toto la  ndizi. Fanya  hivyo  mara  tatu  kwa  siku, asubuhi, mchana  na  jioni kwa  siku  thelathini. Utapata  matokeo mazuri.
 
Mbali  na  kutibu  tatizo  la mtoto  wa  jicho, toto la ndizi, likichanganywa  kitaalamu  na  wine  ya  mnazi ( Palm wine ) au mnazi,  husaidia  kutibu  tatizo  la  kidole  tumbo  au  appendix.
 
16.         TIBA  ASILIA  YA  KUPUNGUZA  GESI TUMBONI
Kuondoa  gesi tumboni, kwa  kutumia  tiba  asilia, chukua juisi ya kitunguu maji kiasi cha glasi moja yenye  ujazo  wa  milimita  mia  mbili  na  hamsini,kisha changanya  na asali mbichi kijiko kimoja  koroga  halafu tumia  kunywa .
Utafanya hivyo  mara tatu kwa siku kwa  muda  wa  siku  kumi  na  nne.
 
AU  chukua  kipande  kimoja  cha  tangawizi,kiponde ponde  kisha  chemsha  kwenye nusu lita ya  maji pamoja  na  kijiko  kimoja kikubwa  cha  asali  mbichi  ya  nyuki wadogo, halafu  tumia kunywa  kutwa  mara  mbili  kwa  siku  ishirini na  moja.
 
AU ; Chukua asali  mbichi  ya  nyuki  wadogo  kiasi  cha  robo  lita,  changanya  na vijiko  vitatu  vikubwa  vya  unga  wa  Kamun nyeusi,kisha chemsha  pamoja  kwenye  maji  lita  moja.Halafu tumia kula  vijiko  vikubwa  vitatu  kutwa  mara  tatu kwa  siku  ishirini  na  moja.
 
17.         TIBA  YA  PUMU :  Chukua magadi vijiko vikubwa  vitatu, saga  upate  unga wake, kisha  changanya  na samli ya  n’gombe   vijiko 21  vikubwa na  asali  vijiko 30 vikubwa. Matumizi : Tumia  kula  vijiko  vikubwa  vitatu  asubuhi, vitatu  jioni na  vitatu  usiku kwa  muda  wa  siku  thelathini.  Utapata  nafuu  kubwa  sana.
 
18.         TIBA  ASILIA  YA  KIHARUSI  NA  KIFAFA :
Chukua mizizi  mitatu  ya  mti  wa  ukwaju, mizizi  mitatu  ya  mti  wa  mkungu, mizizi  mitatu  ya mpapai, pamoja  na  mizizi  mitatu  ya mti  wa  ufwambo.  Iponde  ponde  yote  kisha  chemsha  kwa  pamoja  kwenye  maji  ya  lita tatu  hadi  yachemke. Tumia  kumpa  mgonjwa  glasi  moja, kutwa  mara  tatu kwa  siku  thelathini. Mgonjwa  wako  atapata  nafuu  kubwa  sana.
 
19.         TIBA   ASILIA YA FANGASI ZA   KWENYE DAMU, UKURUTU, UPELE, MCHAFUKO WA DAMU, PAMOJA  NA KUWASHWA  KWA MWILI.
Chemsha  robo  kilo  ya  majani  ya  mti  wa  mdimu kwenye  maji kiasi cha  lita  mbili. Maji yakisha   tokota, ipua  chuja, halafu  tumia  kunywa  glasi mbili  asubuhi, mbili  mchana, mbili  jioni. Utafanya  hivyo  kwa  muda  wa  siku thelathini.  Hakika  utapata  nafuu  kubwa  sana.
 
20.         TIBA   ASILIA  YA  MARADHI YA FANGASI ZA MIGUU NA KUNUKA MIGUU.
Twanga  majani ya  mwarobaini  robo  kilo,  chemsha  na  maji lita  tano, kisha weka  kwenye  beseni  halafu  loweka  miguu  yako ndani  ya  beseni  kwa  muda  wa  lisaa  limoja. Utafanya  hivyo  kutwa  mara  mbili kwa muda  siku  kumi  na  nne. Utapata  matokeo  mazuri sana.
 
AU  chukua majivu kiasi  cha  robo kilo,changanya  na robo  lita ya  juisi  ya  ndimu, kisha  nyunyizia  kwenye  miguu, na ukae kwa  lisaa  limoja. Utafanya  hivyo  mara mbili  kwa siku  kwa  siku  thelathini. Japo inauma  lakini  ni tiba nzuri  sana.

21. KUONGEZA  MAZIWA  KWA  MAMA  ANAENYONYESHA : Chukua  majani  ya  mti  wa  ukwaju, kiasi  cha nusu kilo, kisha  chemsha  na  maji  lita tano.  Tumia  kunywa glasi  tatu  asubuhi, tatu mchana, tatu  jioni kwa  muda  wa  siku saba.  Hakika  utapata  matokeo  mazuri  sana. Utakuwa  unafanya  hivyo  kila  mara  utakapo  hitaji kuongeza  maziwa. 
 
MAKALA  HAYA  YAMELETWA  KWENU  KWA  HISANI YA  NEEMA  HERBALIST & NUTRITIONAL  FOODS  CLINIC. DUKA  LA  KUUZA  DAWA  MBALIMBALI  ZA  ASILI.
 
 TUNAPATIKANA  UBUNGO  JIJINI  DAR  ES  SALAAM, JIRANI  NA  SHULE  YA  MSINGI,UBUNGO  NATIONA  HOUSING NYUMA  YA  JENGO  LA  UBUNGO  PLAZA.
 
KWA MAHITAJI  YAKO  YA DAWA  MBALIMBALI  ZA ASILI  ZINAZO  TIBU  MAGONJWA  NA  MATATIZO  MBALIMBALI  YA  KIAFYA, WASILIANA  NASI  KWA  SIMU  NAMBA 0766 53 83 84.
 
NA  KWA  TAARIFA  ZAIDI  KUHUSU HUDUMA  ZETU, TEMBELEA  KILA  SIKU KATIKA  BLOGU YETU.

Rais Magufuli Aweka Jiwe La Msingi Mradi Wa Hosteli Za Wanafunzi Katika Chuo Kikuu Cha Dar Es Salaam

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 21 Oktoba, 2016 ameweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa mabweni 20 ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 3,840 ikiwa ni utekelezaji wa ahadi aliyoitoa Mwezi Juni mwaka huu wakati wa sherehe za uzinduzi wa ujenzi wa maktaba ya kisasa ya chuo hicho.

Wakati Rais Magufuli akiweka jiwe la msingi la mradi huo, tayari ujenzi umefikia asilimia 75 ambapo majengo 20 yaliyounganishwa kimuundo yamefikia ghorofa ya nne na ujenzi huo unaofanywa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) unatarajiwa kukamilika ifikapo tarehe 30 Desemba, 2016.

Akizungumza kabla ya kuweka jiwe la msingi Rais Magufuli aliyeambatana na Mkewe Mama Janeth Magufuli ameipongeza TBA na wadau wote wanaoshiriki katika ujenzi huo zikiwemo Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa hatua kubwa ya ujenzi iliyofikiwa tangu ujenzi uanze tarehe 01 Julai, 2016 na amebainisha kuwa kwa kutumia TBA mradi huo utatumia kiasi kidogo cha fedha.

"Nawapongeza sana TBA kwa kazi nzuri mliyoifanya mpaka sasa, mradi huu utatumia Shilingi Bilioni 10 tu, Wakandarasi kutoka nje walitaka kujenga mabweni haya ya wanafunzi kwa Shilingi Bilioni 100, sasa mtaona wenyewe tumeokoa Shilingi ngapi" amesema Rais Magufuli.

Aidha, Rais Magufuli ameahidi kuwa, kwa kuwa majengo hayo yanauwezo wa kubeba ghorofa sita, Serikali itafanya utaratibu wa kutumia moja ya likizo za wanafunzi kuongeza ghorofa nyingine mbili ili kuwawezesha wanafunzi wengi zaidi kupata nafasi.

Kuhusu mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu Dkt. Magufuli amesema Serikali imetenga Shilingi Bilioni 483 kwa mwaka huu ambapo wanafunzi takribani 93,000 wanaoendelea na masomo na wanafunzi takribani 25,000 watakaoanza masomo watapatiwa mikopo lakini ameweka bayana kuwa mikopo hiyo itatolewa kwa wanafunzi ambao wanatoka kwenye familia masikini.

Rais Magufuli ameiagiza Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kurekebisha dosari zilizopo katika mfumo wa utoaji wa mikopo ikiwa ni pamoja na upangaji mbaya wa wanafunzi katika vyuo, kutoa mikopo kwa upendeleo, kutozingatia sifa za mkopaji, kutoa mikopo hewa na kufungua vyuo kabla ya mikopo ya wanafunzi kutolewa na pia amewaonya wanafunzi kujiepusha na vitendo visivyofaa wakati Serikali inarekebisha dosari hizo.

"Na ndio maana wakati mwingine na wabaya wanapitia humo humo, mara fanye hivi fanyeni vile, wakati wanajua kuwa mkifanya yasiyofaa Serikali itawafukuza tu ili mkafanyie mambo yenu huko.

"Kwa sababu huwezi kuwa unahangaika kutafuta fedha za kuwapa mikopo, wakati huo huo unahitaji kujenga reli, wakati huo huo unahitaji kujenga barabara, wakati huo huo unahitaji kulipa mishahara, wakati huo huo unahitaji kutoa elimu bure, wakati huo huo Karagwe kuna njaa, wakati huo huo watu wanahitaji dawa hospitali, halafu watu wengine wanataka kukuendesha kana kwamba hela unayokusanya ni kwa ajili yao tu, ni lazima tuelewane na mimi ninataka kuwaeleza kwa dhati lazima twende katika njia iliyonyooka, ni bora uwe Rais usiye maarufu lakini utimize uliyoyaahidi, asitokee mtu wa kukuendesha, ninajua mmenielewa" amesisitiza Dkt. Magufuli.

Dkt. Magufuli ameiagiza Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB) kujipanga vizuri kukusanya marejesho ya mikopo kwa wote waliokopeshwa na bodi hiyo ambapo mpaka sasa bodi inadai takribani Shilingi Trilioni 2.6.

Awali akitoa taarifa ya mradi huo, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Prof. Rwekaza Mukandala amesema wakati ujenzi huo ukiendelea chuo kimetenga Shilingi Bilioni 4.5 kutoka kwenye mapato yake kwa ajili ya kununua samani ikiwa ni pamoja na vitanda vya wanafunzi na pia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia itashughulikia ujenzi wa uzio, jiko na bwalo la chakula.

Hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi la mradi wa ujenzi wa mabweni ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi, Wabunge, Makatibu Wakuu na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Bw. Paul Makonda.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

21 Oktoba, 2016

Rais Magufuli aagiza HESLB kuongeza kasi ya ukusanyaji wa madeni.

0
0
Na Beatrice Lyimo-MAELEZO
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. John Magufuli ameagiza Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu kutumia Sheria zilizopo kuongeza kasi ya ukusanyaji wa madeni kwa wahitimu walionufaika na mikopo.

Rais Magufuli ametoa agizo hilo leo jijini Dar es salaam wakati akiweka jiwe la msingi la mradi wa ujenzi wa hosteli za wanachuo katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam unajengwa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA)  kwa gharama ya shilingi bilioni 10.

Amesema kuwa Serikali inadai takribani shilingi trilioni 2.6 kwa wahitimu walionufaika na mikopo ya Elimu ya juu.

“Serikali inawadai wahitimu walionufaika na mikopo ya Elimu ya juu takribani shilingi trillion 2.6 ambazo wanatakiwa kuzirudisha ili ziweze kutolewa kama mikopo kwa wanafunzi wapya na waliopo vyuoni” alifafanua Dkt Magufuli.

Aidha Dkt. Magufuli ameitaka Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi kusimamia ipasavyo suala la utoaji wa mikopo kwa wanafunzi kwa kuzingatia vigezo vilivyopo kwani lengo la mikopo hiyo inawalenga watoto maskini.

Alisema kuwa kumekuwa na baadhi ya malalamiko ya kuwa  Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu inafanya zoezi la ugawaji wa mikopo hiyo kwa upendeleo hivyo kuzitaka uongozi wa Wizara kushughulikia suala hilo.

Mbali na hayo Rais Magufuli amewataka wanufaika wa mikopo hiyo kutimia mikopo hilo kwa malengo mazuri katika kujinufaisha na masuala ya Elimu.

Naye Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi Prof. Joyce Ndalichako  alisema kuwa mradi wa ujenzi wa hosteli hizo utasaidia kuwahudumia wanafunzi 3,840 ambapo unatarajiwa kuisha mwishoni mwa mwezi Desemba 2016.

Katika hatua hiyo Prof. Ndalichako alisema kuwa wanafunzi waliodahuiliwa kwa mwaka huu wapo 58,000 hivyo suala la wanafunzi 66,000 kukosa mikopo hiyo ni upotoshaji unaofanya na baadhi wa watu.

Mradi wa Ujenzi wa Hosteli za wanachuo katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wenye majengo 20 kila jengo gorofa nne zenye vyumba 12 unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa Desemba mwaka huu.

Alichosema Rais Magufuli kuhusu mikopo ya wanafunzi wa Vyuo Vikuu

0
0
Rais wa Tanzania Dkt. John Magufuli amesema Serikali imetenga Shilingi Bilioni 483 kwa mwaka huu kwa ajili ya mikopo ya elimu ya juu ambapo wanafunzi zaidi ya 118,000 watanufaika.

Akizungumza katika uwekaji wa jiwe la msingi la hostel za Chuo Kikuu cha Dar es Salaam leo, Rais Magufuli amesema miongoni mwa hao watakaonufaika, wanafunzi 93,000 ni wanaoendelea na masomo na wanafunzi takribani 25,000 ni watakaoanza masomo mwaka huu huku akiweka bayana kuwa mikopo hiyo itatolewa kwa wanafunzi ambao wanatoka kwenye familia masikini.

Rais Magufuli ameiagiza Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kurekebisha dosari zilizopo katika mfumo wa utoaji wa mikopo ikiwa ni pamoja na upangaji mbaya wa wanafunzi katika vyuo, kutoa mikopo kwa upendeleo, kutozingatia sifa za mkopaji, kutoa mikopo hewa na kufungua vyuo kabla ya mikopo ya wanafunzi kutolewa na pia amewaonya wanafunzi kujiepusha na vitendo visivyofaa wakati Serikali inarekebisha dosari hizo.

"Na ndio maana wakati mwingine na wabaya wanapitia humo humo, mara fanye hivi fanyeni vile, wakati wanajua kuwa mkifanya yasiyofaa Serikali itawafukuza tu ili mkafanyie mambo yenu huko.

"Kwa sababu huwezi kuwa unahangaika kutafuta fedha za kuwapa mikopo, wakati huo huo unahitaji kujenga reli, wakati huo huo unahitaji kujenga barabara, wakati huo huo unahitaji kulipa mishahara, wakati huo huo unahitaji kutoa elimu bure, wakati huo huo Karagwe kuna njaa, wakati huo huo watu wanahitaji dawa hospitali, halafu watu wengine wanataka kukuendesha kana kwamba hela unayokusanya ni kwa ajili yao tu, ni lazima tuelewane na mimi ninataka kuwaeleza kwa dhati lazima twende katika njia iliyonyooka, ni bora uwe Rais usiye maarufu lakini utimize uliyoyaahidi, asitokee mtu wa kukuendesha, ninajua mmenielewa" amesisitiza Dkt. Magufuli.

Dkt. Magufuli ameiagiza Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB) kujipanga vizuri kukusanya marejesho ya mikopo kwa wote waliokopeshwa na bodi hiyo ambapo mpaka sasa bodi inadai takribani Shilingi Trilioni 2.6.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumamosi ya Octoba 22

Jipatie Dawa Asili ya Kuondoa Michirizi, Kuondoa C hunusi, Kuongeza Unene toka Natural Beauty Product

0
0

NATURAL BEAUTY PRODUCT Ni kampuni inayosifika kwa kutoa bidhaa original  zenye matokeo mazuri na ya haraka zaidi bila kemiko wala madhara  yoyote.  tunazo za:-👇👇👇👇
1. Kutengeneza shepu hipsi na makalio kwa:- (a) Vidonge maalum @ 150,000/= (b) Dawa ya kunywa au kupaka @  120,000/=
2. Kupunguza au kuongeza maziwa @ 90,000/=
3. Kushepu miguu kuwa (Chupa ya bia)@ 100,000/=
4. Kubana uke na kuongeza hamu ya tendo la ndoa kwa mwanamke @ 100,000/=
5. Kuondoa mipasuko au (Michirizi) @ 90,000/=
6. Kuwa softi na mweupe mwili mzima kwa:- (a)mafuta @ 90,000/= (b) Vidonge @ 150,000/=
7. Kuongeza unene wa mwili mzima @ 120,000
8. kupunguza tumbo na manyama uzembe kwa:- (a) Mkanda original wa MICRO COMPUTER @ 150,000/= (b) Mkanda wa kawaida au dawa ya kupaka @ 120,000/= (c)  Dawa ya kunywa @ 100,000/=
9. Kuondoa chunusi na madoa sugu @ 90,000/=
10. Kulefusha nywele na kuzuia kukatika ovyo @ 90,000/=
11. Kuondoa mvi milele na zisiludi tena @ 100,000/=
12. Kuongeza uume na nguvu za kiume kwa:- (a) Gel ya kupaka @ 100,000/=  (b)  Vidonge maalum @ 120,000/= (c)  Mashine original ya HANDSOME UP @ 170,000/=
13. Kuondoa vinyweleo @ 80,000/=
14. kuotesha nywele kwenye kipara @ 100,000/=
15. Kuondoa makovu sehemu yoyote @ 90,000/=
N.K Kwa mawasiliano  piga simu namba 065 9618585 au 0759029968. Popote ulipo utapata huduma zetu pia bidhaa  zetu zote zinagarantii na risiti ili kuhakikisha mafanikio yako karibu sana.
   Follow follow follow
      👇👇👇
@Natural2162
@Natural2162
@Natural2162
@Natural2162
        Kwa wateta wa mikoani tunasafilisha kwa njia ya MABASI nchi za nje tunasafilisha kwa njia ya DHL mzigo unaupata bila tatizo lolote.

Taarifa kutoka Ikulu: Rais Magufuli afanya uteuzi wa Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA)

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, amemteua Prof. Ninatubu Mbora Lema kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA).

Taarifa iliyotolewa leo tarehe 22 Oktoba, 2016 na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa uteuzi huu umeanza tarehe 20 Oktoba, 2016.

Prof. Ninatubu Mbora Lema anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Mhandisi Lambert Ndiwaita aliyefariki dunia tarehe 20 Agosti, 2015.

Prof. Ninatubu Mbora Lema ni Profesa Mshiriki Usimamizi wa Ujenzi, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Associate Professor of Construction Management – University of Dar es Salaam).

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

22 Oktoba, 2016

RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 75 & 76 (Riwaya inawafaa kuanzia miaka 18 na kuendelea )

0
0
MWANDISHI : EDDAZARIA

ILIPOISHIA
Macho yangu yakakutana na macho ya Lutfia, aliye pembeni ya mwili wa baba yake, aliye fariki dunia. Nikatembea kwa haraka hadi ulipo mwili wa chifu, kabla sijaugusa, nikastukia, Lutfia akinisukuma kwa nguvu na, nikaanguka chini
"Eddy, hupaswi kuugusa mwili wa baba yangu. Haya yote wewe ndio chanzo. Umekisababishia kijiji changu matatizo...."

"Lutfia ila si mimi niliye waua hawa wote"
"Wewe, ni chanzo Eddy, nakuanzi sasa hivi ninakuomba uondoke kijijini kwangu, la sivyo utakwenda kuungana na kifo cha hawa wote walio tangulia mbele za haki"
Lutfia alizungumza kwa msisitizo, huku machozi yakimwagika, ñà kifua chake kikipanda na kushuka kwa kasi akionekana kujawa na jazba kubwa dhidi yangu.

ENDELEA SASA
"Lu....."
"Eddy nimesema ondoka"
Lutfia alizungumza kwa kupaza sauti, hadi wanakijiji wote wakatutizama sisi, natambua hawajui lugha tunayo izungumza ila, matendo yanaashiria kwamba Lutfia hataki kuniona mbele ya macho yake. Nikamtazama Chifu, huku machozi yakinilenga lenga. Midomo ya Lutfia, inatetemeka kwa kufura kwa hasira, uzuri wake alio kua nao umetoweka kabisa.

Taratibu nikauweka chini upanga wangu, kisha nikasimama na kutazamana na Lutfia aliye nitumbulia mimacho kiasi cha kunifanya nimuogope. Kila mwana kijiji ninaye mtazama sura yake imetawaliwa na majonzi mengi, wamama wengine wakiwa wanalia kwa uchungu huku wakigara gara kwenye vumbi, wakionyesha ni jinsi gàni, walivyo umizwa na tukio zima lililo tokea muda mchache ulio pita.

Sikumuangali mtu yoyote usoni zaidi ya kugeuka na kuanza kutembea kwa mwendo wa haraka, ulio changanyika na hasira kali. Nikafika kwenye kijumba changu, nikachukua kibuyu changu, ninacho hifadhia maji ya kunywa, nikachukua na kisu changu cha akiba, na kutoka nje ya kibanda changu. Nikautizama mji jinsi unavyo teketea kwa moto, hasira dhidi ya John ikazi kunipanda. Nikaanzà kutokomea msituni, nikijaribu kutafuta njia ya kutokea kwenye kijiji hiki, kutokana na hasira pamoja na uchungu ulio nitawala moyoni mwangu, nikajikuta nikitembea hadi kuna pambazuka, pasipo kuchoka.

  Nikafika kwenye moja ya mlima mrefu, ulio zingirwa na miti mingi, kwa mbali nikaanza kusikia mngurumo wa gari, likipita eneo la karibu na mlima huu, kwa haraka nikashuka, nikiufwatisha mgurumo huo ni wapi unapo tokea. Kwabahati nzuri nikaiona barabara ya lami, iliyo chongwa kwenye mlima huu. Matunaini ya kufika ninapo pahitaji yakaanza kunijia moyoni mwangu.

Nikasimama, katikati ya barabara. Sikuona aibu kwa jinsi nilivyo vaa nusu uchi, huku sehemu zangu za siri, zikiwa nimezifunika na ngozi ya chui. Mlio wa gari sikuusikia tena, kwani ninahisi lilisha pita, kabla ya mimi kuifikia barabara. Nikaendemea kuzunguka zunguka maeneo ya barabara, nikijaribu kusubiria kama ninaweza kupata usafiri.

Gafla gari moja ndogo, likapita kwa kasi pasipo kufanikiwa kulipungia mkono, ila halikufika mbali sana, likasimama. Dereva wa gari hilo akaanza kulirudisha nyuma kwa kasi, hadi sehemu nilipo simama. Kioo cha upande wa dereva kikashuka, nikamuona mvulana mmija wa kizungu, àkiwa na mchumba wake, wakabaki wakinishangaa kwa jinsi nilivyo vaa.
Binti wa kizungu akatoa kamera yake, aina ya digital, na kuanza kunipiga picha, huku akiwa amesimama upande wa lili wa gari, nikaanza kuwafwata taratibu

"Casey get in the car"(Casey ingia ndani ya gari)
Mvulana huyu, alizungumza kwa haraka baada ya mimi kilikaribia gari lao, kabla hajafanya chochote, nikawahi kuingiza mkono kupitia upenyo wa kioo alicho kifungua. Nikachomoa funguo ya gari lao, nakulifanya lizime. Jamaa akashuka, huku akiwa amekasirika, akajaribu kunirukia, ila nikamuwahi kumtuliza kwa ngumi ya shingo iliyo muangusha chini na kuzimia hapo hapo.

Msichana akajaribu, kukimbia ila nikamuwahi na kumdaka, nikambeba begani na kumrudisha ndani ya gari. Nikachomoa kisu changu na kumuwekea kooni mwake huku kidole changu kimoja kikimpa ishara ya kukaa kimya la sivyo nitamkata kichwa. Nikaufunga mlango wake, ña kuzunguka upande wa pili, sehemu alipo anguka mpenzi wake. Kwa haraka nikamvua nguo mpenzi wake, na kuzivaa mimi japo hazinitoshi sana ila nikazilazimisha kukaa mwilini mwangu.

Nikachukua soksi za jamaa, na kumkandamiza nazo mdomoni, kisha nikamnyanua na kufungua, uoande wa pili wa gari. Kwa bahati nzuri nikakuta kamba, kwa haraka nikamfunga miguuni na mikononi. Kisha nikamuwena vizuri nyuma ya gari, hii yenye viandishi vidogo vilivyo andikwa Verosa, kisha nikafunga, nikarudi alipo mpenzi wake.
Nikamkuta akihangaika na simu yake, akijaribu kupiga namba anazo zijua yeye, kwa bahati mbaya, maeneo tuliyopo hakuna mawasiliano.

Nikampokonya simu yake na kuiweka mfukoni mwangu
"Ukijaribu kufanya ujinga wowote, nitakuu"
Nilizungumza kwa sauti ya ukali nikitumia lugha ya kingereza, jambo lililo mfanya binti huyo kushangaa, kwani nahisi alijua kwamba mimi ni mtu misiye jua lugha yoyote zaidi ya lugha ya jamii niliyo tokea
Nikawasha gari na kuondoka, huku mara kwa mara niki muamrisha binti huyu kunielekeza barabara ya kufika kwenye mji wowote. Mwendo wa karibia masaa tisa, tukafika kwenye moja ya mji wenye nyumba, nyingi sana zilizo tengenezwa kwa mbao
"Hapa ni wapi?"
"Soweto"

Casey alinijibu kwa kifupi huku, akiwa amenuna, kwani hajafurahishwa na uwepo wangu mimi, ndani ya gari hili. Nikasimamisha gari nje ya baa moja, iliyo tulia sana,
"Mbona umesimamisha gari?"
"Nahisi njaa, nahitaji kula, nipatie pesa"
Casey akanitazama kwa woga, taratibu akaingiza mkono wake kwenye, mfuko wa suruali aliyo ivaa, akatoa noti moja ya dola mia na kunikabidhi, nikafungua mlango, kabla sijashuka, nikamgeukia Casey.
"Shuka ndani ya gari, tuongozane"
Casey hakuwa na kipingamizi zaidi yakushuka kwenye gari, tukaingia ndani ya baa hii kwa bahati nzuri tukakuta, sehemu wanauza chakula

"Wewe unaitwa nani?"
Casey aliniuliza kwa sauti ya chini, huku tukiendelea kukisubiria chakula tulicho kiagiza
"Eddy"
"Una jina kama la mchumba wangu"
"Yupi, huyo niliye mfungia kwenye buti ya gari?"
"Hapana, huyo ni kaka yangu, mpenzi wangu yupo hospitali"
"Anaumwa na nini?"
"Alishambuliwa na majambazi, wiki moja iliyo pita"
"Ohoo pole saña, ila hali yake inaendeleaje?"
"Sio nzuri, kwani yupo chini ya uangalizi wa madaktari, kwani alipigwa risasi nne za kifua, alipokua anapeleka pesa benki"

Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Ernest Mangu aongoza matembezi ya pamoja ya maofisa na askari wa vyeo mbalimbali

0
0
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Ernest Mangu (watatu kulia) akiwaongoza maofisa na askari wa vyeo mbalimbali wa Jeshi la Polisi kufanya mazoezi ya viungo mara baada ya kumaliza matembezi ya pamoja ya kuimarisha afya na kujenga ushirikiano mahala pakazi katika mkoa wa kipolisi wa Kindondoni mapema leo asubuhi. (Picha zote na Demetrius Njimbwi – Jeshi la Polisi)

Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Ernest Mangu (wapili kushoto) akiwaongoza maofisa na askari wa vyeo mbalimbali wa jeshi la Polisi wakati wa matembezi ya pamoja ya kuimarisha afya na kujenga ushirikiano mahala pakazi katika mkoa wa kipolisi kinondoni mapema leo asubuhi. Kushoto kwake  ni kamanda wa Polisi mkoa wa Kinondoni Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Suzan Kaganda.
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Ernest Mangu, akiwaongoza maofisa na askari wa vyeo mbalimbali wa Jeshi la Polisi katika matembezi ya pamoja ambayo yalianzia katika kituo kikuu cha Polisi Oysterbay na kupita maeneo ya kwa Msasani kwa Mwalimu Nyerere na baadae kuingia barabara ya Ali Hassan Mwinyi jijini Dar es salaam mapema leo asubuhi.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili ya Octoba 23

Makamu Wa Rais Mhe. Samia Awataka Wanawake Kuwafichua Wapenda Rushwa Wanaokwamisha Harakati Zao Za Kujikomboa Kiuchumi

0
0
MAKAMU wa Rais, Samia Suluhu Hassan ameelezea kukerwa na vitendo vya rushwa na kuwataka wanawake wajasiriamali kufichua kila aina ya rushwa wanazoombwa na wenye mamlaka katika sekta ya biashara nchini.

Alisema hayo jana wakati akifungua kongamano la wajasiriamali wanawake lililoandaliwa na Mtandao wa Sauti ya Wajasiriamali Wanawake Tanzania (VOWET) na kuhudhuriwa na wanawake zaidi ya 500.

Alisema iwapo wanawake wakiwafichua waombaji wa rushwa wanaokwamisha harakati zao za kusonga mbele kibiashara, itaiwezesha serikali kuondoa kero hiyo.

Samia alisema baadhi ya wanawake wanaombwa rushwa za ngono na nyinginezo na hukaa kimya bila ya kulifikisha suala lao hilo kwa mamlaka husika ili wasaidiwe na kwamba kukaa kimya kumechangia kuendelea kuwepo kwa kero hiyo.

Amewahakikishia wanawake hao kuwa serikali itakuwa ikiwapa kipaumbele kwenye malipo ya fedha za zabuni ili waweze kusonga mbele zaidi na kuongeza kuwa wapo wanawake ambao wamekuwa wakijikita zaidi kwenye biashara, lakini wanakumbwa na changamoto mbalimbali ikiwamo hiyo ya kucheleweshewa fedha zao.

Akizungumzia kuwaunganisha wanawake na masoko, alisema ofisi yake inashughulikia kutengeneza mtandao utakaotangaza kazi zote za wajasiriamali wanawake kirahisi zaidi.

Alisema wapo wajasiriamali wa nje ya nchi, lakini wakitaka kufahamu fursa za biashara zinazofanywa na wanawake wanashindwa kupata taarifa zao na kuwahakikishia kuwa ofisi yake inalitatua tatizo hilo.

Rais wa Vowet, Maida Waziri katika hotuba yake alimueleza Makamu wa Rais kuwa malipo ya kodi kwa makadirio ya nyuma yanakwamisha maendeleo ya wanawake nchini.

Alimuomba Makamu wa Rais kuwasaidia kufutwa kwa mfumo huo kwa kuwa licha ya kuwaathiri wajasiriamali kiujumla ila wanawake wanaathirika zaidi kwa kuwa wanalipa fedha ambazo hawana taarifa nazo.

Majambazi Mengine Yauawa Katika Mapambano Makali Mkuranga

0
0

Jeshi la Polisi Mkoa wa Temeke limeua watu wanne wanaodhaniwa kuwa ni majambazi katika wilaya ya Mkuranga mkoa wa Pwani.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi Temeke, Gilles Muroto alisema tukio hilo ni la Oktoba 21 baada ya polisi kupata taarifa za kuwepo kwa kundi la watu wanaodhaniwa ni majambazi.

Alisema baada ya taarifa, kikosi kazi cha Polisi cha Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, kilifanya ufuatiliaji na kubaini nyumba ambayo haijakamilika imezungushiwa uzio na muda wote mlango wa uzio huo ulikuwa umefungwa.

Aliongeza kuwa uchunguzi wa kina, ulifanyika na kubaini kuwa kweli kundi hilo, lipo ndani ya nyumba hiyo na kwamba muda mwingi mlango wa uzio, hufungwa na kuongeza kuwa majira ya saa tano askari wa kikosi kazi cha mkoa huo na mkoa wa Pwani, kilizingira nyumba hiyo.

“Baada ya kujipanga mlango wa uzio huo uligongwa na kutoa amri ya kuwataka walioko ndani ya nyumba hiyo wafungue mlango na kujisalimisha, lakini tulishangaa baada ya amri hiyo ghafla milio ya risasi ilianza kutoka ndani ya nyumba hiyo,” alisema Muroto.

Aliongeza kuwa baada ya milio hiyo, askari ambao walikuwa makini na wakiwa wamezingira nyumba hiyo wakiwa wamejipanga katika miundo ya mapigano, walianza mashambulizi kujibu mashambulio hayo.

Alisema majibizano yaliendelea na watu hao waliokuwa wanashambulia kutoka ndani, walivunja uzio na watu wanaokadiriwa kuwa zaidi ya watano walitoka huku wakiwa wanashambulia.

Muroto alisema askari waliendelea kupambana nao na kufanikiwa kuwajeruhi baadhi yao, na wengine walifanikiwa kutoroka na silaha zao.

“Mashambulizi kutoka ndani yalitulia na askari waliingia ndani ya uzio, kwa kuwa yalikuwa mapambano ya nguvu walikuta majambazi watatu wanaokadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 25 na 30 wakiwa wamejeruhiwa kwa risasi na hali zao zilikuwa mbaya na tuliwapeleka Hospitali ya Taifa Muhimbili lakini walibainika kuwa tayari wameshakufa na miili yao imehifadhiwa hapo ikisubiri kutambuliwa,” alisema.

Alisema baada ya kufanya upekuzi, polisi walikuta silaha moja aina ya short gun pump action yenye MV.51516 R na namba ya usajili TZ car 99987 na risasi tano ndani ya magazini yake.

Risasi nyingine sita za short gun zilikutwa ndani ya mfuko wa plastiki pamoja na risasi nane za pistol.

Aidha alisema katika tukio hili, ilibainika kuwa kuna askari mmoja alijeruhiwa bega lake la kushoto na lilikuwa jeraha kubwa la risasi, hivyo alipelekwa katika Hospitali ya Muhimbili ambako amelazwa na anaendelea kupata matibabu akisubiri kufanyiwa upasuaji.

Muroto alisema ufuatiliaji wa majambazi, walitoroka eneo la mapambano uliendelea kwa kushirikiana na wananchi wa kijiji cha Mtambani, ambapo majira ya saa tatu asubuhi jambazi mmoja alipatikana akiwa mahututi na juhudi za kumfikisha hospitali zilifanyika. Hata hivyo, alikufa akiwa njiani.

”Tunawashukuru wananchi wote wema kwa ushirikiano mkubwa waliouonesha kwa Jeshi la Polisi, kwa kuliunga mkono katika kufichua wahalifu na kupambana na wahalifu, nitoe tahadhari kuwa mkoa huu ukifanya tukio ujue utashughulikiwa kabla hujakamilisha na ukifanikiwa kukamilisha azma yako haitachukua muda utakamatwa,” alisisitiza.

Bodi ya Mikopo Ya Elimu Ya Juu Zanzibar Yasitisha Kutoa Mikopo Kwa Wanafunzi Vyuo Vikuu

0
0
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Ali Mohamed Shein ameiagiza Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu Zanzibar kupitia Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, kusimamisha utoaji wa mikopo ya elimu ya juu, hadi hapo serikali itakapojiridhisha na utaratibu mzima wa utoaji wa mikopo hiyo.

“Hatutatoa mikopo mwaka huu mpaka hapo tutakapokamilisha kazi ambayo tumeanza kuifanya ya kupitia upya utaratibu wa utoaji mikopo hiyo ili kuhakikisha inatolewa kulingana na mahitaji ya sasa ya nchi na kwa wanaostahili,” alisema Dk Shein.

Akizungumza katika hafla ya utoaji zawadi kwa wanafunzi waliofaulu daraja la kwanza katika mitihani ya Taifa ya Kidato cha Nne mwaka 2015 na Kidato cha Sita mwaka 2016, Dk Shein alisema kuwa katika utaratibu wa sasa wapo waliodanganya kupata mikopo na ambao wamekopeshwa lakini wamekuwa wagumu kurejesha mikopo hiyo.

Katika hafla hiyo, ambayo ilihudhuriwa pia na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Issa Haji Usii Gavu, jumla ya wanafunzi 119 waliomaliza kidato cha nne na wengine 50 waliomaliza kidato cha sita, walipewa zawadi kwa kupata daraja la kwanza katika mitihani yao ya taifa.

“Wako waliokejeli matokeo yenu, lakini ukweli ni huo mko 50 wa kidato cha tano mliopata daraja la kwanza na wengine 119 mliofaulu daraja la kwanza mtihani wa kidato cha nne,” alieleza Dk Shein na kuhoji msingi wa kukebehi matokeo hayo.

Aliongeza kuwa ufaulu wa wanafunzi hao, ni sifa kwa Zanzibar na anaamini kwa hatua zinazochukuliwa na serikali kuimarisha miundombinu ya elimu pamoja rasilimali watu kiwango cha ufaulu kitazidi kuongezeka.

“Mnapofanya mitihani sote tunakuwa na wasiwasi, nyinyi wenyewe, walimu, wazazi na sisi serikali kwa kuwa tunaelewa kuwa matokeo yoyote yale ni yetu sote kama ni mazuri ni furaha yetu sote na kama si mazuri ni huzuni yetu sote,” Dk Shein aliwaambia wanafunzi hao.

Dk Shein aliwataka wanafunzi hao kujivunia fursa waliyoipata na kuitumia vyema kujiimarisha kielimu, kwa kuwa haikuwa rahisi kabla ya Mapinduzi ya mwaka 1964 kuona vijana kutoka familia masikini wanapata fursa za kuingia sekondari kwa makundi.

“Mmepata bahati kubwa serikali yenu imeweka mazingira mazuri ya kupata elimu na haya ni matokeo ya utekelezaji wa ahadi ya Chama cha Afro-Shirazi na Rais wa Kwanza wa Zanzibar, Sheikh Abeid Amaan Karume ya kutoa elimu bure itakaposhika madaraka,” Dk Shein alieleza.

Katika hatua nyingine, Dk Shein ametoa wito kwa walimu wakuu kuhakikisha kuwa wanasimamia vizuri walimu katika shule zao pamoja na kuwahimiza wakaguzi wa shule kutimiza wajibu wao ipasavyo.

Dk Shein alisema;“kumekuwepo na tatizo la usimamizi maskulini, hivyo serikali itatengeneza utaratibu wa kuwapatia motisha walimu wakuu na wakaguzi watakaofanya vizuri kwa kuwa ni dhahiri kuwa walimu wakuu wakisimamia vyema skuli zao na wakaguzi wakaifanya kazi yao ya ukaguzi kwa umakini tutapata matokeo mazuri zaidi.”

Katika salamu zake hizo kwa wanafunzi hao, ambao walisindikizwa na uongozi wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, pamoja na walimu wakuu wa baadhi ya shule, Dk Shein aliwataka walimu kuongeza ari ya kufundisha na kwamba ni heshima na furaha ya mwalimu kuona mwanafunzi wake anapata matokeo mazuri.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimkabidhi zawadi Mwanafunzi Mahira Baraka Hamadi wa kidato cha sita Skuli ya Biashara Mombasa Wilaya ya Magharibi Unguja akiwa ni mwanafuzi aliyefanya vizuri katika Mtihani wa Taifa Mei mwaka 2016,hafla iliyofanyika jana Ikulu Mjini Unguja.

Mkuu wa Wilaya Awasweka Rumande Madiwani wa CCM akiwatuhumu kuharibu ofisi ya kijiji

0
0
Zikiwa ni takribani wiki mbili tangu Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Mkoa wa Arusha, Alexander Mnyeti kuwaweka ndani madiwani wanne wa Chadema kwa madai ya kumkwamisha kutekeleza kazi zake, Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro mkoani Manyara, Zephania Chaula naye amewasweka mahabusu madiwani wawili wa CCM. 

Chaula amewaweka ndani madiwani hao akiwamo wa Kata ya Emboreet, Christopher Ole Kuya na wa Viti Maalumu, Diana Kuluo kwa madai ya kuvunja ofisi ya Kijiji cha Emboreet na kushinikiza wananchi kuandamana ili kumpinga mwenyekiti wa kijiji hicho. 

Chaula alitoa amri ya kukamatwa kwa madiwani hao baada ya kuona wanaongoza kuharibu usalama kwenye eneo hilo.

Alisema madiwani hao waliwaongoza baadhi ya wanakijiji kuvunja ofisi ili kumshinikiza mwenyekiti wa kijiji hicho, John Olendikoni kujiuzulu na kusababisha waandamane kumpinga. 

Mkuu huyo wa wilaya alisema alichukua hatua hiyo baada ya vyombo vya ulinzi na usalama kumpa taarifa kuwa madiwani hao wanaongoza harakati za kumng’oa madarakani mwenyekiti wa kijiji bila kufuata taratibu na sheria. 

“Sitakubali kuona kiongozi yeyote hata kama ni kupitia CCM anafanya makosa, kisha nikamuacha kwani suala la kumtaka mwenyekiti wa kijiji ajiuzulu lina taratibu zake siyo kumwambia atoke kwenye kiti,” alisema Chaula. 

Alisema, awali aliwaeleza wahusika kuvuta subira juu ya suala hilo na kufuata taratibu kupitia vikao, ili kubaini tatizo lililopo kwa madai kwamba siasa na Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020 vimeingizwa kwenye suala hilo. 

“Nimeshawaagiza watengeneze mlango na vyombo vyote vilivyoharibika kwenye ofisi hiyo walipovunja na nimewapa taarifa kuwa nitawachukulia hatua wananchi wakiandamana tena,” alisema mkuu huyo wa wilaya. 

Alisema amewaambia madiwani hao mchakato na taratibu za kumtoa mwenyekiti wa kijiji zinaanzia halmashauri ya kijiji, mkutano mkuu wa kijiji, taarifa kwa mkuu wa wilaya na mkuu wa mkoa.

 “Tunafanya kazi kwa utaratibu siyo shinikizo na nimewapa angalizo wawe viongozi wa kuwapo kwa amani katika eneo hilo na yakizuka mengine nitawaweka ndani tena kisha mahakamani,” alisema. 

Akizungumza baada ya kuachiwa kwenye Kituo cha Polisi Orkesumet, Ole Kuya alisema hawakuwashinikiza wananchi kuandamana ili kumkataa mwenyekiti na kuvunja ofisi ya kijiji. 

“Sisi hatuhusiki kwenye kuongoza harakati hizo, ila ni wananchi wenyewe wameamua kupambana kwa ajili ya kudai haki zao baada ya kuona uongozi wa kijiji unafanya mambo ambayo hawaridhiki nayo,” alisema Ole Kuya. 

Kifungu cha 15(1) cha Sheria ya Tawala za Mikoa ya mwaka 1997 kinawapa mamlaka mkuu wa mikoa na wilaya kumuweka ndani mtu kwa saa 48 pale anapobaini mhusika ametenda kosa.

Waziri Mwijage awataka wenye malori kuyaegesha Maana Hakuna Mizigo Bandarini

0
0


Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage jana alitofautiana na wamiliki wa malori aliposema upungufu wa mizigo ni tatizo la muda duniani, wakati wafanyabiashara hao wamesema ni vigumu kuwarejesha wenye mizigo waliokuwa wakitumia Bandari ya Dar es Salam ambao wamehamia bandari za Mombasa na Beira.

Waziri Mwijage alisema hayo wakati akifungua mkutano mkuu wa Chama cha Wamiliki wa Malori (Tatoa), alipowaeleza hali ya kupungua mizigo inaweza kuchukua mwaka na zaidi na kuwataka wafanyabiashara hao kuwa wavumilivu katika kipindi hiki.

Waziri Mwijage aliwataka wamiliki hao wa vyombo vya usafirishaji kusitisha huduma hiyo kwa sasa hadi hali itakapotengemaa.

“Ushauri wangu kwenu ni kusimamisha malori yenu na kuyatunza vizuri kwa sababu mizigo haipo hivi sasa, hali ikirejea muendelee kufanya biashara,” alisema. Alisema kukosekana kwa mizigo ni anguko dogo la uchumi wa dunia ambalo baadaye litaimarika.

“Niwasihi msiangalie sana muda, inaweza kuchukua mwaka mmoja au zaidi kidogo ya hapo ili kurudia hali ya zamani, lakini msikate tamaa,” alisema Mwijage.

Waziri Mwijage alisema kushuka kwa bei ya madini kwenye soko la dunia kumesababisha nchi kama Zambia na Congo DRC kupunguza mizigo inayopitia kwenye Bandari ya Dar es Salaam.

 Alisema baadhi ya migodi ya nchi hizo imesitisha uzalishaji na kusababisha mizigo ya kusafirisha ipungue kwa kiasi kikubwa. Waziri pia alisema mazao ya biashara yameshuka bei kwenye soko la dunia na hivyo kupunguza uzalishaji na kuleta athari katika sekta ya usafirishaji.

Lakini Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya NMC Tracking, Natal Charles alisema itachukua muda mrefu kuwarejesha watumiaji wa Bandari ya Dar es Salaam kwa sababu waliondoka kwasababu ya ushindani wa kibiashara uliopo kwenye bandari nyingine.

“Kukosekana kwa mizigo kwenye Bandari ya Dar es Salaam ni changamoto kwetu wenye malori kwa sababu wapo waliokopa benki ili kuyanunua magari hayo na sasa wako katika hatari ya kufilisika,” alisema.

Alisema pia wako baadhi ya wamiliki wa malori ambao wameshafilisika kutokana na kukosa mizigo.

Kwa mujibu wa vyombo mbalimbali vya habari vya nje, moja ya sababu inayohusishwa na kuathirika kwa usafirishaji wa mizigo duniani ni kufilisika kwa kampuni kubwa ya meli ya Korea Kusini inayoitwa Hanjin, ambayo inashika nafasi ya saba katika biashara hiyo duniani.

Kufilisika kwa kampuni hiyo kumesababisha meli za kampuni hiyo kunyimwa kibali cha kushusha au kupakia mizigo kutokana na kutokuwa na uhakika wa kufikishwa inakoelekea, limeandika gazeti la The Guardian la Uingereza.

Katika hotuba yake ya ufunguzi, Waziri Mwijage aliwashauri wamiliki wa malori kuangalia aina nyingine ya uwekezaji, kama kujenga viwanda.

“Wekezeni katika viwanda vidogo, vya kati na vikubwa kulingana na uwezo na fursa ya kila mmoja wenu,” alisema.

Alisema anawafahamu baadhi ya wanachama wa Tatoa ambao wameanzisha viwanda vya maziwa, maji, kutengeneza mabomba na kusaga mahindi ili kupata unga.

“Mwekezaji makini hawezi kung’ang’ania biashara ya aina moja kwani inapoleta hasara anaachana nayo na kuendelea na ile inayomletea faida,” alisema.

Hata hivyo, Mwijage aliwataka Tatoa kupeleka mapendekezo yao serikalini ya namna ya kuboresha sekta ya usafirishaji huku wakitoa mifano halisi ya namna ya kuiboresha sekta hiyo.

 “Wizara yangu ndiyo yenye dhamana ya kuboresha wepesi wa kufanya biashara. “Nileteeni masuala yote yanayowakwamisha nami nitayawasilisha kwenye mamlaka husika,” alisema waziri huyo.

Alisema kama malori ya mizigo hayasafiri, biashara ya vipuri itashuka na matumizi ya mafuta yatashuka na hivyo kuziathiri sekta nyingi.

Alisema malori yamekuwa yakisaidia kuongeza mapato ya Serikali na kutunisha mfuko wa barabara.

 Awali, Mwenyekiti wa Tatoa, Elias Lukumay alisema wamiliki wa malori wanakabiliwa na tatizo la ukosefu wa maeneo ya kuegesha malori wakati yakisubiri kupakia mizigo katika Bandari ya Dar es Salaam.

Alisema mara kwa mara wanapoegesha kwenye maeneo ya barabara jirani na bandari hiyo wamekuwa wakikamatwa na kutozwa faini.

Mfalme wa Morocco Kupokewa kwa ‘Mabango’ Leo Hapa Nchini

0
0
Wakati Mfalme wa Morocco, Mohamed VI akitarajiwa kuwasili leo nchini kwa ziara ya kikazi, huenda akapokewa kwa mabango baada ya vijana wanaounda kamati ya mshikamano wa Tanzania na Sahara Magharibi (TASSC) kujipanga kufanya hivyo kushinikiza nchi hiyo kuacha kuitawala kwa mabavu Sahara Magharibi. 

Vijana hao wamefikia uamuzi huo kutokana na kile walichodai kusikitishwa kwao na kitendo cha Morocco kuendelea kuitawala kwa mabavu nchi ya Sahara Magharibi na kupuuza wito wa Umoja wa Mataifa (UN) unaoitaka kuipa uhuru nchi hiyo. 

Hata hivyo, Serikali ya Tanzania kupitia msemaji wake, Hassan Abass imesema ujio huo ni muhimu kwa uhusiano wa kidiplomasia na uchumi. 

“Serikali ilishaeleza msimamo wake, kuna uhusiano wa aina nyingi, ujio huu ni muhimu kwa uhusiano wa kidemokrasia na uchumi kama hisia zitawatuma kufanya hivyo, wanapaswa kufuata sheria,” alisema Abass.

 Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Mratibu wa TASSC, Alphonce Lusako alisema jitihada mbalimbali zimekuwa zikifanyika ili Morocco iiache huru Sahara Magharibi lakini watawala wa nchi hiyo wamekuwa wagumu kuruhusu hilo. 

Lusako alieleza kuwa TASSC inafahamu fika kwamba Mfalme Mohamed VI amekuwa akifanya ziara katika mataifa mbalimbali akijaribu kutafuta kuungwa mkono ili Morocco iendelee kuitawala Sahara Magharibi. 

Alisema Tanzania ikiwa miongoni mwa nchi zinazoitambua Sahara Magharibi inapaswa kumuonyesha wazi Mfalme Mohamed VI kuwa haiungi mkono utawala wa kimabavu.

 “Tunamtaka Mfalme wa Morocco kuacha mara moja vitendo vya kibeberu vya kuikalia Sahara Magharibi sambamba na kuwaachia huru wafungwa wa kisiasa na wanaharakati wanaoshikiliwa magerezani katika maeneo yanayokaliwa kimabavu. 

"Ni aibu kwa nchi moja ya Kiafrika kuitawala nchi nyingine: Tunaunga mkono msimamo wa Tanzania wa kuendelea kuitambua na kuiunga mkono Sahara Magharibi kwenye vyombo vya kimataifa na tunasisitiza isiyumbishwe katika msimamo huo, ” alisema.

 Katibu wa TASSC, Jasper Hassan alisema tangu kamati hiyo ianzishwe mwaka jana imekuwa ikifanya harakati mbalimbali ikiwamo mihadhara ya wazi inayolenga kuisukuma Morocco kuacha kuitawala Sahara Magharibi.

 “Jitihada zilianza muda mrefu ila mwaka jana ndiyo vijana tukaona tuingilie kati tukiwa kama Waafrika, tunapinga kila aina ya unyonyaji tunataka Sahara Magharibi iwe huru,” alisema Hassan. 

Juzi, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alisema ziara ya kiongozi huyo itakuwa na manufaa kwa nchi, kwani akiwa na mwenyeji wake, Rais John Magufuli watasaini makubaliano 11 ya ushirikiano katika sekta za kilimo, gesi, mafuta, Reli ya Liganga na Mchuchuma na sekta ya utalii.

Madiwani CUF Watwangana Ngumi Hadharani ....Polisi Waingilia Kati

0
0

Polisi mjini Tanga jana walilazimika kuingilia na kuzima vurugu zilizotokea katika ofisi za Chama cha Wananchi (CUF), Wilaya ya Tanga zilizotokana na madiwani kugawanyika katika makundi mawili. 

Makundi hayo ya madiwani yaligawanyika kuhusu uamuzi wa wenzao waliohudhuria kikao cha baraza la madiwani wa jiji hilo Oktoba 12.

Vurugu zilianza baada ya Mwenyekiti wa CUF wilayani humo, Rashid Jumbe ambaye pia ni diwani wa Mwanzage aliyegombea nafasi ya umeya kuamuru madiwani waliohudhuria baraza hilo watoke nje ili wajumbe waanze kumjadili mmoja mmoja.

Baada ya amri hiyo kundi la madiwani 12 waliotolewa nje kusubiri kuhojiwa waliamua kuingia kwa nguvu kutaka kumtoa Jumbe wakidai anasababisha makundi ndani ya chama hicho. 

Vurugu ziliendelea kwenye mlango wa kuingilia, jambo lililosababisha wanachama waliokuwa nje kuingilia kati, huku wakirushiana ngumi.

Baadaye magari matatu ya polisi yaliwasili katika ofisi hizo na kuwatawanya wanachama waliokuwa wamejaa, jambo lililomsaidia Jumbe kufanikiwa kutoka.

 Akizungumza baada ya vurugu hizo, Jumbe alisema kikao hicho kilikuwa na ajenda ya kuwahoji na kisha kuwajadili madiwani waliohudhuria baraza hilo kinyume na msimamo wa CUF.

Katibu wa CUF wa wilaya hiyo, Thobias Haule ambaye pia ni diwani wa Mnyanjani alisema madiwani waliohudhuria kikao cha baraza hawakwenda kinyume na chama kwa sababu waliamua kuwawakilisha wananchi waliowachagua, badala ya kuendeleza mgomo ambao hauwasaidii.

“Tukubali kwamba kwa kipindi cha mwaka mmoja tulichokaa bila kushiriki vikao vya baraza kuna mambo mengi ya maendeleo ya wananchi ambayo hayakufanyika, tumeamua kuhudhuria kwa masilahi mapana ya wananchi,” alisema Haule.

Mbunge wa Tanga Mjini, Mussa Mbarouk aliwataka wanachama wao kuwa wavumilivu kwa viongozi wako imara na hawatakubali kuyumbishwa.

 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Benedict Wakulyamba alisema Jumbe alifikishwa Kituo cha Polisi Chumbageni kuhojiwa kuhusu sakata hilo. Halmashauri ya Jiji la Tanga ina jumla ya madiwani 36; CUF inao 20 na CCM wako 16.

Mfalme Mohammed Vi Wa Morocco Awasili Jijini Dar Jioni Hii, Apokelewa Na Mwenyeji Wake Rais Dkt Magufuli

Ndalichako, Mahiga Wawavuruga Chadema..... CCM wajichagulia Meya bila mpinzani

0
0
Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) leo kimeususia uchaguzi wa Meya na Naibu Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, hali iliyopelekea wajumbe wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kufanya uchaguzi peke yao na kuwapigia kura wagombea wao bila upinzani.

CCM wamemchagua Benjamin Sitta kuwa Meya wa Manispaa hiyo kwa kura zote 18 za wajumbe wa chama hicho. George Manyama amepata Baraka za wajumbe hao wa chama tawala kuwa Naibu Meya wa Manispaa hiyo.

Chadema waliususia uchaguzi huo kwa madai kuwa CCM wamechakachua kwa kuwaleta Profesa Joyce Ndalichako (Waziri wa Elimu) na Balozi Agustine Mahiga (Waziri wa Mambo ya Nje) kupiga kura katika Manispaa hiyo ili hali waliapa na kusajiliwa katika Halmashauri ya Manispaa ya Ilala. Hivyo, sio wajumbe halali wa Kinondoni na hawakupaswa kupiga kura.

Wajumbe wa Chadema wanadai kuwa uchaguzi uliofanywa na CCM peke yao sio halali kwani pamoja na mambo mengine akidi ambayo ni 2/3 ya wajumbe waliopaswa kufanya uchaguzi huo kuwa halali haikutimia.

Chadema imepanga kupinga uchaguzi huo mahakamani.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images