Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya Septemba 27


Waziri Mkuu Majaliwa atoa wiki moja kwa Afisa Elimu kutafuta walimu wa kidato cha tano na sita

$
0
0

WAZIRI MKUUkuu  Mhe. Kassim Majaliwa ametoa wiki moja kwa Afisa Elimu Mkoa wa Pwani, Yussuph Kipengele kupeleka walimu wa kufundisha masomo ya kidato cha tano na sita katika shule za sekondari za Mkongo na Utete wilayani Rufiji. 
 
Ametoa agizo hilo  Jumatatu, Septemba 26, 2016  wakati akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Jumba la Maendeleo wilayani Rufiji.  baada ya Mbunge wa Rufiji, Muhammed Mchengelwa kumwambia kuwa wilaya hiyo inakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa walimu wa kidato cha tano na sita licha ya kuwa na shule. 
 
"Hatuwezi kuwa na shule ambazo hazina walimu, nasikia hapa anayefundisha ni Mkuu wa shule na mwalimu mmoja tu, wakati kule Kibaha kuna walimu walmerundikana ,sasa fanya realocation tarehe 4,Oktoba uniletee taarifa walimu wamefika Rufiji.",alisema Waziri Mkuu. 
 
Akizungumzia suala la upungufu wa watumishi wa umma kwenye sekta mbalimbali, Waziri Mkuu alisema baada ya kazi ya uhakiki watumishi hewa itakapokamilika, serikali itaangalia kwenye maeneo yenye upungufu na hivyo kutangaza ajira. 
 
 "Hivi sasa serikali inakamilisha masuala ya uhakiki wa watumishi, tukimakamilisha na kujua idadi ya watumishi na maeneo yenye upungufu tutaanza tena kuajiri, tulisitisha kupisha kwanza kazi hii,alisema Waziri Majaliwa. 
 
Kuhusu migogoro ya wakulima na wafugaji Waziri, Mkuu alisema watendaji wa halmashauri na vijiji wanapaswa kutenga maeneo ya wafugaji na wakulima na kutaka mifugo isiongezwe kwenye maeneo ambayo hayajaruhusiwa. 
 
 Alisema wenyeviti wa vijiji wanapaswa kusimamia utekelezaji wake katika mpango wa matumizi bora ya ardhi na kwamba atakayeruhusu idadi kubwa ya mifugo kuingia kijijini zaidi ya ile iliyokubalika atawajibishwa ikiwemo kufukuzwa kazi na hatua nyingine za kisheria. 
 
 "Hatuwezi kuendelea kuwa na watumishi wasio na nidhamu, wale wote watakaoingia mifugo zaidi ya uwezo wa kijiji wafukuzwe kazi na kuchukuliwa hatua, lakini pia wafugaji ni marufuko kuingiza mifugo kwenye mazao ya wakulima"alisema Waziri Mkuu. 
 
 Kuhusu ujenzi wa barabara ya lami kwenda makao makuu ya wilaya ya Rufiji, Utete, Waziri Mkuu aliahidi kuchukua ombi hilo na kusema bajeti ijayo litatengewa fedha kuwa ajili ya kufanya maandalizi ya upembuzi kuona gharama yake kabla ya kutangaza zabuni ya ujenzi. 
 
 Kuhusu utengenezaji wa madawati, Waziri Mkuu alisema ifikapo Oktoba 30, mwaka huu kila wilaya nchini inapaswa iwe imekamilisha utengenezaji wa madawati hayo kwenye shule nchini. 
 
 Aidha, alisema ipo miradi mingi inayoendeshwa kwa maslahi binafsi ukiwemo mradi wa Bonde la Rufiji(RUBADA), ambao wamebaini kuna ubabaishaji mkubwa, hivyo wamepeleka timu ya wataalamu kuhakiki ili wale wabadhirifu wachukuliwe hatua. 

IMETOLEWA NA:

OFISI YA WAZIRI MKUU,

JUMATATU, SEPTEMBA 26, 2016

Watoto 2,570 waripotiwa kulawitiwa kwa kipindi cha miezi saba

$
0
0

Vitendo vya ukatilitili wa kijinsia kwa watoto vimeendelea kuongezeka kwa kasi nchini katika kipindi cha mwezi Januari hadi Julai mwaka huu ambapo zaidi ya watoto 2,570 wa kike na kiume wamelawitiwa na kubakwa.

Akizungumza katika sherehe za maadhimisho ya miaka 21 ya Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) yaliyofanyika jana katika Makao makuu ya watoto yaliyopo Kurasini jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC Helen Kijo-Bisimba alisema idadi hiyo ni kubwa ukilinganisha na ya mwaka jana.

Hata hivyo, Mama Bisimba alisema kwa mujibu wa Msemaji wa Jeshi la Polisi, takwimu hizo zinaweza kuwa ndogo kutokana na kesi nyingi za ubakaji na ulawiti kwa watoto kutoripotiwa polisi kwa sababu ya mila na desturi za maeneo mengi nchini.

“Ripoti ya Jeshi la Polisi kupitia dawati la jinsia kati ya Januari na Machi 2016 inaonyesha matukio ya watoto kubakwa na kulawitiwa yakiendelea kuongezeka kutoka 180 hadi 1765 hayo ni matukio yaliyotolewa taarifa katika vituo mbalimbali vya polisi nchi nzima ukilinganisha na matukio 1585 mwaka 2015. Hata hivyo waliohusika na matukio hayo wameonekana wakirandaranda bila kuchukuliwa hatua za kisheria, ” alisema.

Alisema ripoti hiyo inaonyesha kuwa kesi 1,203 zipo katika hatua ya upelelezi, 822 zipo mahakamani na watuhumiwa 234 wamekwisha hukumiwa.

“Pia utafiti uliofanywa na Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto kwa kushirikiana na Tanzania kitengo cha ustawi wa jamii unaonyesha kati ya watoto 10 wa kike 4 wamebakwa, na kati ya watoto 10 wa kiume 3 wamelawitiwa zaidi ya mara tatu. Utafiti huo unaonyesha kwa ujumla kuwa watoto wa kike na wa kiume 6 walifanyiwa ukatili huo na watu ndani ya familia,” alisema.

Bisimba alisema asilimia 49 ya ukatili hufanyika nyumbani, 23 hufanyika njiani wakati wa kwenda shule au kurudi, na asilimia 15 hufanyika shuleni. Pia ripoti hiyo ya UNICEF inaonyeaha kuwepo kwa matukio ya watoto kulawitiana na kubakana wenyewe kwa wenyewe kutokana na kuvizoea vitendo hivyo.

LHRC imeitaka serikali kupitia Wizara ya Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto pamoja na Wizara ya Katiba na Sheria kuifanyia marekebisho sheria ya mtoto na kutilia mkazo malezi bora kwa watoto ikiwemo kuweka kipengele kitakachotoa adhabu kali kwa familia itakayoshindwa kutoa malezi bora kwa mtoto.

LHRC inayoshughulika na utetezi wa sheria na haki za binadamu ilianzishwa Septemba 26, 1995.

'Panya Road' Waibuka Upya Na Kutesa Wananchi Moshi Baa Jijini Dar Es Salaam

$
0
0

Na Dotto Mwaibale

KUNDI la uhalifu la watoto wenye umri kuanzia miaka 18 hadi 25 maarufu kama panya road linatishia usalama wa wananchi na mali zao maeneo ya Moshi Baa na vitongoji vingine katika Manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaam.

Kufuatia kukithiri kwa vitendo hivyo katika kipindi kisichopungua wiki mbili tayari watoto watatu walikuwa wakidaiwa kuhusika na kundi hilo wameuawa na wananchi wenye hasira kali.

Akizungumza na mwandishi wa habari hii Dar es Salaa jana   mkazi wa eneo la Moshi Baa Relini aliyejitambulisha kwa jina la Mwarami Abubakar alisema hali sio shwari katika eneo kufuatia matukio ya kila siku ya kuvamiwa wananchi kujeruhiwa na kuporwa mali zao na kundi hilo.

"Tayari vijana wawili wiki iliyopita wamechomwa moto na wananchi wenye hasira huku mwingine akipigwa juzi hadi kutolewa utumbo na kufariki papo hapo," alisema Abubakar.

Mkazi mwingine wa eneo la Kwa Mkolemba Khamisi Fadhil alisema kundi hilo limekuwa likifanya vitendo hivyo mchana kweupe na wanatembea kuanzia vijana nane hadi 10 wakiwa na silaha za jadi kama nondo, visu na mapanga na mtu yeyote wanayekutana naye ni lazima wampige na kumpora.

Wenye maduka wanalazimika kufunga kuanzia saa moja jioni kuhofia kundi hilo ambalo huvunja milango ya nyumba na kufanya uporaji" alisema Fadhil.

Fadhil alisema maeneo ambayo vijana hao wameshamiri ni Moshi Baa Relini, Kwa Mkolemba, Diwani na Bomba mbili.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Ilala, Kamishna Msaidizi (ACP), Salum Hamdan alisema polisi imejipanga vilivyokukabiliana na vitendo hivyo katika mkoa wake.

"Kwanza napenda kukuambia kwamba hakuna kundi linalojiita panya road wote tunawahesabu ni wahalifu kama walivyo wahalifu wengine na hivi ninavyongea na wewe tupo katika siku ya sita ya operesheni ya kukakamta watu wanaojihusisha na uhalifu wa ujambazi wakiwemo wanaouza pombe haramu ya gongo," alisema Kamanda Hamdan.

Aliongeza kuwa katika mkoa wake hivi karibuni utakuwa shwari baada ya askari wake kusambaratisha watu hao wanaofanya vitendo hivyo.

Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com-simu namba 0712-727062

Matukio Zaidi Ya Picha Wakati Rais Dkt. Magufuli Alipotembelea Bandari Ya Dar Es Salaam Jana

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akitembelea bandari ya Dar es salaam  Septemba 26, 2016 akiwa ameongozana na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, Katibu Mkuu Uchukuzi i Dkt Leonard Chamriho na uongozi wa Bandari
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akitembelea bandari ya Dar es salaam   Septemba 26, 2016 akiwa ameongozana na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, Katibu Mkuu Uchukuzi i Dkt Leonard Chamriho na uongozi wa Bandari
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akitembelea bandari ya Dar es salaam  Septemba 26, 2016 akiwa ameongozana na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, Katibu Mkuu Uchukuzi  Dkt Leonard Chamriho na uongozi wa Bandari
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipungia wafanyakazi waliokuwa wakimshangilia wakati akitembelea bandari ya Dar es salaam  Septemba 26, 2016 akiwa ameongozana na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, Katibu Mkuu Uchukuzi i Dkt Leonard Chamriho na uongozi wa Bandari
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akitembelea bandari ya Dar es salaam Septemba 26, 2016 akiwa ameongozana na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, Katibu Mkuu Uchukuzi i Dkt Leonard Chamriho na uongozi wa Bandari
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akitembelea bandari ya Dar es salaam Septemba 26, 2016 akiwa ameongozana na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, Katibu Mkuu Uchukuzi i Dkt Leonard Chamriho na uongozi wa Bandari
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipata maelezo kutoka kwa  Meneja wa Kitengo cha Kontena wa  Kampuni ya Ushushaji Shehena ya makasha  Bandarini ya Tanzania International Container Terminal (TICTS)  Bw. Donald Talawa  alipotembelea bandari ya Dar es salaam  Septemba 26, 2016 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akitoa maelekezo kwa  Meneja wa Kitengo cha Kontena wa  Kampuni ya Ushushaji Shehena ya makasha  Bandarini ya Tanzania International Container Terminal (TICTS)  Bw. Donald Talawa  alipotembelea bandari ya Dar es salaam  Septemba 26, 2016 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akitoa mapendekezo  kwa  Kampuni ya Ushushaji Shehena ya makasha  Bandarini ya Tanzania International Container Terminal (TICTS)
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipata maelezo kutoka kwa  Meneja wa Kitengo cha Kontena wa  Kampuni ya Ushushaji Shehena ya makasha  Bandarini ya Tanzania International Container Terminal (TICTS)  Bw. Donald Talawa  alipotembelea bandari ya Dar es salaam  Septemba 26, 2016 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipata maelezo kutoka kwa Mhandisi Mary Mhayaya kuhusu  uthibiti wa kiwango cha mafuta yanayoingia nchini  kutoka kwenye meli (Oil Flow Meter) katika bandari ya Dar es salaam  Septemba 26, 2016 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipata maelezo kutoka kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa kuhusu zoezi la  uthibiti wa kiwango cha mafuta yanayoingia nchini  kutoka kwenye meli (Oil Flow Meter) katika bandari ya Dar es salaam Septemba 26, 2016 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipata maelezo kutoka kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa kuhusu zoezi la  uthibiti wa kiwango cha mafuta yanayoingia nchini  kutoka kwenye meli (Oil Flow Meter) katika bandari ya Dar es salaam  Septemba 26, 2016 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akikagua sehemu ya kupimia kiwango cha mafuta yanayoingia nchini  kutoka kwenye meli (Flow Meter) katika bandari ya Dar es salaam  Septemba 26, 2016 
tpa18
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akikagua sehemu ya kupimia kiwango cha mafuta yanayoingia nchini  kutoka kwenye meli (Flow Meter) katika bandari ya Dar es salaam  Septemba 26, 2016 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akitoa maelekezo  kuangalia sehemu ya kupimia kiwango cha mafuta yanayoingia nchini  kutoka kwenye meli (Flow Meter) katika bandari ya Dar es salaam  Septemba 26, 2016 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiongozwa na Mhandisi Mary Mhayaya kuhusu akikagua mtambo wa  uthibiti wa kiwango cha mafuta yanayoingia nchini  kutoka kwenye meli (Oil Flow Meter) katika bandari ya Dar es salaam  Septemba 26, 2016 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipata maelezo kutoka kwa Mhandisi Mary Mhayaya kuhusu  chumba cha mitambo ya  uthibiti wa kiwango cha mafuta yanayoingia nchini  kutoka kwenye meli (Oil Flow Meter) katika bandari ya Dar es salaam  Septemba 26, 2016 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipata maelezo ya chumba cha ukaguzi wa mizigo (scanner) inayoingia nchini  katika bandari ya Dar es salaam  Septemba 26, 2016 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipata maelezo ya chumba cha ukaguzi wa mizigo (scanner) inayoingia nchini  katika bandari ya Dar es salaam  Septemba 26, 2016 
 Wafanyakazi wa bandari ya Dar es salaam wakimlaki kwa furaha  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli alipofika kuongea nao baada ya kutembelea bandari ya Dar es salaam  Septemba 26, 2016 
 Mwenyekiti wa Wafanyakazi wa Bandarini Bw.  Mashaka Karume akieleza baadhi ya changamoto wanazokabiliana nazo mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli alipotembelea bandari ya Dar es salaam  Septemba 26, 2016
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiongea na wafanyakazi wa bandari baada ya kutembelea bandari ya Dar es salaam  Septemba 26, 2016
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiongea na wafanyakazi wa bandari baada ya kutembelea bandari ya Dar es salaam  Septemba 26, 2016
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiongea na wafanyakazi wa bandari baada ya kutembelea bandari ya Dar es salaam  Septemba 26, 2016
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiongea na wafanyakazi wa bandari baada ya kutembelea bandari ya Dar es salaam  Septemba 26, 2016 
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiongea na wafanyakazi wa bandari baada ya kutembelea bandari ya Dar es salaam Septemba 26, 2016 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiongea na wafanyakazi wa bandari baada ya kutembelea bandari ya Dar es salaam  Septemba 26, 2016 
 Wafanyakazi wa bandari ya Dar es salaam wakimsikiliza   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli alipofika kuongea nao baada ya kutembelea bandari ya Dar es salaam  Septemba 26, 2016 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiaga baada ya kuongea na wafanyakazi wa bandari baada ya kutembelea bandari ya Dar es salaam  Septemba 26, 2016
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiwaaga  wafanyakazi wa bandari baada ya kutembelea bandari ya Dar es salaam  Septemba 26, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiwapungia mkono kuwaaga  na wafanyakazi wa bandari baada ya kutembelea bandari ya Dar es salaam  Septemba 26, 2016

Picha za Rais Magufuli Akimuapisha Naibu Katibu Mkuu Wa Ofisi Ya Tamisemi Dkt. Zainabu Chaula.

$
0
0
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Dkt. Zainabu Chaula kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa TAMISEMI Ikulu jijini Dar es Salaam.

Rais Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Dkt. Zainabu Chaula mara baada ya kumuapisha kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa TAMISEMI Ikulu jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU

Waziri Mhagama atoa siku saba kwa wadaiwa wa NSSF

$
0
0
Waziri wa nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu, Bunge, Vijana na Watu Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama ametoa siku saba kwa taasisi za serikali, wizara, kampuni na watu binafsi kuhakikisha wanalipa madeni wanayodaiwa na Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF).

Waziri Mhagama pia ameziagiza bodi za wadhamini za mifuko mingine ya hifadhi ya jamii, kuhakikisha zinawashinikiza wadeni wao kulipa madeni yote wanayodaiwa ili kuiwezesha mifuko hiyo kujiendesha kwa ufanisi zaidi.

Ametoa tamko hilo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam, alipotembelea miradi ya nyumba za NSSF iliyopo wilayani Kigamboni mkoani Dar es Salaam.

Amemtaka Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Erick Shitindi kuhakikisha uongozi wa mifuko unampatia ripoti ya hatua zilizochukuliwa dhidi ya wahusika wote walioshindwa kulipa madeni yao kwa mifuko yao.

“Ninafahamu fika kuna mikataba ambayo ilisainiwa na pande zote mbili kabla ya kutolewa kwa hiyo mikopo na makubaliano mengine hivyo naomba basi mikataba hiyo itumike kufanikisha agizo hili,’’ alisema.

Pia alimuagiza Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa NSSF, Profesa Samwel Wangwe kuhakikisha anampatia ripoti muafaka ya utekelezaji wa agizo hilo.

“Kwa niaba ya serikali, ninataka kuona kwamba wadaiwa wote wa mifuko hii bila kujali nafasi zao kiuchumi au kisiasa wanalipa madeni wanayodaiwa…hii lazima ijumuishe kampuni, wawekezaji na taasisi za serikali,’’ alisisitiza.

Awali, Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Profesa Godius Kahyarara alisema licha ya mfuko wake kufanikisha utekelezaji wa miradi mbalimbali ikiwemo majengo, bado wateja wake wengi hawajalipa madeni wanayodaiwa na mfuko huo ikiwemo watu binafsi, taasisi za serikali na binafsi wakiwemo pia wale walionunua nyumba za shirika hilo.

Alisema shirika hilo, bado linadai Sh bilioni 20 kutoka kwa wapangaji wake, deni linalohusisha pia dola za Marekani milioni 1.2.

Alifafanua kuwa kiasi kingine cha Sh bilioni 86, kinadaiwa kama adhabu kutoka kwa waajiri walioshindwa kukamilisha makato ya wafanyakazi wao.

Madeni mengine ni pamoja na deni la Sh milioni 42 na dola za Marekani milioni 35.9 zilizotolewa kama mikopo kwa sekta binafsi mbalimbali huku mkopo mwingine wa Sh bilioni 38 ulitolewa kupitia Saccs na bado hazijarejeshwa.

“Hata hivyo, tumeanza kuchukua hatua mahsusi kulingana na matakwa ya sheria kuhakikisha kwamba madeni yote yanalipwa,’’ alibainisha Profesa Kahyarara.
Waziri nchi ofisi ya waziri mkuu sera, uratibu, bunge ,vijana na watu wenye ulemavu  Mhe. Jenister Mhagama akiwa ameambatana na uongozi wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) alipotembelea miradi ya nyumba za NSSF iliyopo wilayani Kigamboni mwishoni mwa wiki.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa NSSF Prof Samwel Wangwe. (kushoto) akizungumza mbele ya Waziri nchi ofisi ya waziri mkuu sera, uratibu, bunge ,vijana na watu wenye ulemavu  Mhe. Jenister Mhagama wakati waziri huyo alipotembelea miradi ya nyumba za NSSF iliyopo wilayani Kigamboni mwishoni mwa wiki. Wengine ni pamoja na Mkurugenzi mkuu wa NSSF, Profesa Godius Kahyarara (kulia).
Mkurugenzi mkuu wa NSSF, Profesa Godius Kahyarara (kulia) akizungumza mbele ya Waziri nchi ofisi ya waziri mkuu sera, uratibu, bunge ,vijana na watu wenye ulemavu Mhe.  Jenister Mhagama wakati waziri huyo alipotembelea miradi ya nyumba za NSSF iliyopo wilayani Kigamboni mwishoni mwa wiki. Wengine ni pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa NSSF Prof Samwel Wangwe (kushoto).

Masauni Azindua Wiki Ya Nenda Kwa Usalama Barabarani, Kitaifa Mjini Geita....Aagiza Matuta barabara kuu Yaondolewe

$
0
0

Serikali imeagiza Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), kuondoa matuta kwenye barabara kuu, ambayo yametajwa kuwa chanzo cha ajali.

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni, ametoa agizo hilo jana wakati wa ufunguzi wa Wiki ya Usalama Barabarani katika Viwanja vya Kalangalala mkoani Geita.

Alisema matuta yaliyoko kwenye barabara kuu, yamekuwa moja ya vyanzo vya ajali nyingi nchini na kusisitiza kuwa hali ya ajali iliyopo ni vyema suala la usalama barabarani kuwa ajenda ya kitaifa.

Pia alivitaka vvyombo vya usalama, kuwachukulia hatua kali na stahiki wale wote wanavunja sheria za Usalama Barabarani bila kumuogopa au kumuonea mtu yeyote.

Alisema ajali za barabarani zimekuwa ni tatizo kubwa na kuwa takwimu za miaka mitatu kuanzia Januari 2013 hadi Desemba 2015, zinaonesha kuwa ajali zilizotolewa taarifa ni 46,536 ambazo zimeua watu 11,230.

Masauni alisema kuwa kundi linaloongoza kwa kuathirika na ajali hizo ni abiria ambapo watu 3,444 wamekufa, wakifuatiwa na watembea kwa miguu 3,328.

Alisema wapanda baiskeli wanashika nafasi ya tatu kwa watu 2,493 kupoteza maisha, huku madereva waliokufa ni 813 na wasukuma mikokoteni zaidi ya 400 wamepoteza maisha.

“Takwimu za miezi sita tangu Januari mpaka Agosti mwaka huu, ajali 6,971 zimetokea na kusababisha vifo 2,217 na kati ya hivyo 1,809 ni vile vilivyotokana na pikipiki. Hali ya ajali sio nzuri na ni vyema suala la usalama barabarani likawa ajenda ya kitaifa,” alisema.

Alisisitiza kutolewa elimu ya watumiaji wote kuhusu matumizi sahihi ya barabara, wamiliki na madereva kuacha kuendesha vyombo chakavu na kufanyika kwa ukaguzi wa mara kwa mara.

“Shirika la Viwango Tanzania (TBS) pia linatakiwa kuendelea kufanya ukaguzi wa matairi, bodi na vipuri vya mabasi,” alisema.

Aidha, Masauni aliwataka watumiaji wote wa barabara, kufuata sheria na kanuni za barabarani, kuacha kushabikia mwendo kasi, kuvuka kwenye vivuko vya watembea kwa miguu na waendesha baiskeli na mikokoteni kuacha kuendesha barabarani na watoto kuvuka barabara wakiwa chini ya uangalizi.

Naibu Waziri wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, Edwin Ngonyani, alisema kutokana na kukithiri kwa ajali, Baraza lilikuja na mikakati ya miezi sita ya kupunguza ajali hususan zinazotokana na makosa ya kibinadamu.

Alisema makosa ya kibinadamu yamekuwa yakichangia ajali kwa asilimia 80 na kufuatiwa na mwendokasi ambao unachangia kwa asilimia 12, mazingira ya barabara yanachangia kwa asilimia 6 na asilimia 2 zinatokana na sababu nyingine.

“Tumekuja na mikakati ambayo inatekelezwa kwa miezi sita, lengo kuu ni kuondoa makosa ya kibinadamu yanayochangia ajali, na Februari mwakani tutatathmini mafanikio ya mikakati hiyo,” alisema.

Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani katika Jeshi la Polisi, Mohammed Mpinga, ambaye pia ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, alisema katika Wiki ya maadhimisho hayo watoa elimu ya matumizi sahihi ya barabara, na kutoa elimu kwa waendesha pikipiki 300 na walimu 100, na pia watakagua vyombo vya moto na kupima afya za madereva kwa kutumia zahanati mwendo.
Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, ambaye pia ni Katibu wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, Naibu Kamishna, Mohamed Mpinga akizungumza katika maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani inayofanyika Kitaifa katika Viwabya vya CCM Kalangalala mjini Geita. Maadhimisho hayo yalizinduliwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, Mhandisi Hamad Masauni (kulia).
Mgeni rasmi Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, Mhandisi Hamad Masauni (kulia), akimsikiliza Askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani kutoka Makao Makuu, Koplo Faustina Ndunguru wakati alipokuwa anatoa maelezo jinsi magari mbalimbali yanavyovunja sheria za barabarani. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Mgeni rasmi Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, Mhandisi Hamad Masauni (kushoto) akimpa zawadi ya Kombe la Ushindi wa kwanza Mwanafunzi wa Shule ya Msingi Bunge jijini Dar es Salaam, Veronica Innocent, ambaye alishinda nafasi ya kwanza katika uchorani wa picha zinazoonyesha usalama barabarani ambayo zilipambanishwa katika shule za Mkoa wa Dar es Salaam na Geita.
Washiriki wa maonesho (waendesha bodaboda) wakiwa katika maandamano ya kuadhimisha Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani iliyozinduliwa katika Viwanja vya CCM Kalangalala, mjini Geita jana. Kauli mbiu ya Maadhimisho ya mwaka huu ni “Hatutaki ajali tunataka kuishi salama”.

Majina Ya Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga Chuo Kikuu Tumaini Makumira University 2016/2017

$
0
0

List Of Students Admitted By Tcu To Join Tuma For Academic Year 2016/2017 (1st Selection)

Kupata Majina  << BOFYA  HAPA>>

Majina ya Waliochaguliwa Kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es salaam Degree-2016/2017

$
0
0

The following applicants have been selected to join various undergraduate degree programmes for the 2016/2017 academic year. 

The selected applicants should report at the Mwl. J.K. Nyerere Mlimani Campus on Saturday 8th October 2016 for the orientation week which will start on Monday 10th October 2016. 

Applicants selected for admission into Dar es Salaam University College of Education (DUCE) and Mkwawa University College of Education (MUCE) should report directly to the college's campuses in Chang'ombe and Iringa respectively on the same dates. 

Joining instructions and admission letters should be collected at the University campuses where one is admitted. Joining instructions and other important information can also be downloaded from the University website.

Prof. Lipumba Augomea mkutano wa Baraza Kuu la Uongozi CUF

$
0
0

Mgogoro  ndani ya Chama cha Wananchi (CUF) bado unafukuta ambapo jana Prof. Ibrahim Lipumba, aligomea mkutano wa Baraza Kuu la Uongozi la chama hicho ulioitishwa leo visiwani Zanzibar

Alisema, taarifa zilizotolewa kwa vyombo vya habari kuhusu kufanyika kwa mkutano huo hazitambui kwa kuwa, mamlaka zinazohusika kuitisha kikao hicho hazijakidhi matakwa.

Akizungumza na waandishi wa habari katika Ofisi Kuu ya chama hicho Buguruni jijini Dar es Salaam kupitia taarifa iliyoandaliwa na Magdalena Sakaya, Naibu Katibu Mkuu Bara aliyesimamishwa na chama hicho alisema, matakwa ya katiba hayakuzingatiwa.

“Wajibu wa Kamati ya Utendaji ya Taifa utakuwa kuandaa.. agenda za Baraza Kuu la Uongozi la Taifa na kutayarisha na kuhifadhi mihtusari ya vikao vyote vya Mkutano Mkuu wa Taifa, Baraza Kuu la Uongozi la Taifa na vya kamati ya utendaji ya taifa yenyewe na kuwasilisha taarifa ya yatokanayo kutokana na utekelezaji wa maamuzi ya kikao kilichohusika kilichopita,” Prof. Lipumba amenukuu katiba ya chama hicho ibara ya 85(5).

Prof. Lipumba alisema, Maalim Seif Shariff Hamad, Katibu Mkuu wa chama hicho yupo nje ya nchi na kwamba, kutokana na Katiba ya CUF,Naibu Katibu Mkuu atakayemfuata Katibu Mkuu kwa madaraka ni yule aliyetoka upande tofauti wa Jamhuri ya Muungano na upande anaotoka Katibu Mkuu

Kwa upande wake Magdalena Sakaya, Naibu Katibu Mkuu Bara aliyesimamishwa alisema;

"Mimi sijaitisha wala sina taarifa ya kikao cha kamati  ya utendaji kilichofanyika Zanzibar, kwa taarifa nilizonazo hakuna wajumbe wa kamati ya utendaji kutoka Bara waliokua Zanzibar wakati wa kikao hicho. Nachukua nafasi kuwajulisha wajumbe wote wa baraza kuu kuwa hakuna kikao chochote cha baraza kuu kilichoandaliwa na kamati ya utendaji ya Taifa ambayo kikatiba mimi ndiye mwenyekiti wake wakati katibu mkuu hayupo.

“Mimi ndiye mwenye mamlaka ya Katibu Mkuu kwa sababu Naibu Katibu Mkuu wa CUF Tanzania Bara kikatiba ndiye msimamizi namba moja wa Katibu Mkuu” .

Alisema, Katiba ya CUF ya mwaka 1992 Toleo la 2014 kifungu cha 95 (3) kinaeleza “Naibu Katibu Mkuu atakayemfuata Katibu Mkuu kwa madaraka ni yule aliyetoka upande tofauti wa Jamhuri ya Muungano na upande anaotoka Katibu Mkuu,” na kwamba, Katibu Mkuu anatoka Zanzibar na yeye anatoka Bara.

Hata hivyo Prof. alisisitiza kuwa, Sakaya hana taarifa ya kikao hicho cha kamati tendaji kilichofanyika Zanzibar.

Pamoja na kuwepo kwa sintofahamu kutokana na uamuzi wa Jaji Mutungi kumtambua Prof. Lipumba kuwa mwenyekiti halali wa chama hicho, (Lipumba) amepongeza kurejeshwa kwake.

Prof. Lipumba, mwenyekiti wa chama hicho aliyesimamishwa na CUF mwezi uliopita, alirejea kwenye nafasi hiyo kwa kauli ya Jaji Mutungu, Msajili wa Vyama vya Siasa nchini. 

Prof. Lipumba alieleza kushangazwa na hatua ya Jaji Mutungi kukosolewa na baadhi ya wanasheria na majaji mashuhuri kuwa, hakuna sheria inayompa furasa jaji huyo kuchukua hatua aliyoichukua.

List Ya Vyuo Vilivyotoa Selection Ya Majina Ya Wanafunzi Waliochaguliwa Vyuo Vikuu Mbalimbali 2016/2017

$
0
0

Kuona Majina Ya Wanafunzi Waliochaguliwa Chuo Kikuu 2016/2017,
 
==>Chuo  Kikuu Cha Mwalimu Nyerere  <<bonyeza Hapa>> 

==>Chuo  Kikuu Cha  Udsm,duce Na Muce   <<bonyeza Hapa>> 

==>Chuo  Kikuu Cha  Tumaini Makumira    <<Bonyeza Hapa>>   

==>Chuo  Kikuu Cha Udom  <<bonyeza Hapa>>

 ==>Chuo  Kikuu Cha Ifm <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Kikuu Marian << Bonyeza Hapa>>

 ==>Chuo Kikuu Cbe        << Bonyeza Hapa>>

==>Tumaini-mbeya     << Bonyeza Hapa>>& <<hapa>>

 ==>Chuo Kikuu Mum         << Bonyeza Hapa>>

==>Chuo Mum(Diploma) <<Bonyeza Hapa>>

 ==>Chuo- Stella Maris  << Bonyeza Hapa>>

 ==>Chuo- Kampala-kiu  << Bonyeza Hapa>>

Rais Magufuli Apokea Msaada Wa Tsh.milioni 545 Kutoka Serikali Ya India Kwa Ajili Ya Waathirika Wa Tetemeko La Ardhi Lililotokea Mkoani Kagera

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe 27 Septemba, 2016 amepokea msaada wa Shilingi Milioni 545 kutoka kwa Waziri Mkuu wa India Mhe. Narendra Modi kwa ajili ya kusaidia wananchi wa Mkoa wa Kagera waliopatwa na maafa ya tetemeko la ardhi lililotokea tarehe 10 Septemba, 2016.

Hundi ya fedha hizo imekabidhiwa leo Ikulu Jijini Dar es Salaam na Balozi wa India hapa nchini Mhe. Sandeep Arya na baadaye Rais Magufuli akaikabidhi kwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa.

Katika barua yake kwa Rais Magufuli iliyosomwa na Balozi Sandeep Arya, Waziri Mkuu wa India Mhe. Narendra Modi amesema Serikali na Wananchi wa India wamepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kutokea kwa maafa hayo yaliyosababisha vifo vya watu na uharibifu wa mali.

"Tunaziombea amani na uvumilivu familia zote zilizopatwa na madhara na pia tunapenda kuwahakikishia kuwa tupo pamoja na marafiki zetu Serikali ya Tanzania katika kipindi hiki kigumu" amesema Waziri Mkuu Modi.

Kwa Upande wake Rais Magufuli amemshukuru Waziri Mkuu wa India Mhe. Narendra Modi na Serikali yake kwa kutoa mchango huo na kutuma salamu za rambirambi, na amesema Serikali yake imeguswa na moyo wa upendo waliounesha.

"Mhe. Balozi Sandeep Arya naomba unifikishie shukrani zangu za dhati kwa Waziri Mkuu Mhe. Narendra Modi, mwambie kwa niaba ya Serikali yangu tunamshukuru sana kwa kutoa msaada huu muhimu kwa ajili ya Watanzania wenzetu waliopatwa na maafa kule Kagera.

"Mwambie ameonesha moyo wa upendo na ushirikiano kwetu na tumefarijika kwamba marafiki zetu mmeguswa kwa namna ya kipekee na tatizo lililoipata nchi yetu" amesema Rais Magufuli.

Wakati huo huo, Rais Magufuli ametengua uteuzi wa Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera Bw. Amantius Msole na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba Bw. Steven Makonda baada ya kubaini kuwa wamefungua akaunti nyingine ya benki kwa kutumia jina linalofanana na akaunti rasmi ya kuchangia maafa iitwayo "Kamati Maafa Kagera" kwa lengo la kujipatia fedha.

Taarifa iliyotolewa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa muda mfupi baada ya kupokea hundi ya msaada kutoka kwa Waziri Mkuu wa India imeeleza kuwa pamoja na kutengua uteuzi huo Rais Magufuli ameagiza vyombo vya dola vichukue hatua dhidi ya wote waliohusika katika njama za kufungua akaunti hiyo.

Aidha, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa amemsimamisha kazi Mhasibu Mkuu wa Mkoa wa Kagera Bw. Simbaufoo Swai kutokana na kuhusika katika njama hizo.

Hata hivyo Mhe. Kassim Majaliwa ametoa wito kwa wananchi na taasisi mbalimbali kuendelea kuchangia misaada kwa ajili ya walioathirika kwa kutumia akaunti rasmi ya "Kamati Maafa Kagera" ambayo imetangazwa na Serikali.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

27 Septemba, 2016
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akimshukuru Balozi wa India hapa nchini Sandeep Arya mara baada ya kupokea mfano wa hundi yenye thamani ya Shilingi za Kitanzania milioni 545 Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akijadiliana jambo kwa furaha na Balozi wa India hapa nchini Sandeep Arya mara baada ya kupokea mfano wa hundi yenye thamani ya Shilingi za Kitanzania milioni 545 Ikulu jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na kulia ni Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje Balozi Dkt. Aziz Mlima. .

Waziri Mkuu: Tutapitia Upya Sababu Za Kuanzishwa Kwa Rubada

$
0
0

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali itapitia upya sababu za kuanzishwa kwa Mamlaka ya Bonde la Mto Rufiji (RUBADA) kufuatia mamlaka hiyo kuendeshwa kwa ubabaishaji.

Hatua hiyo imekuja baada ya mamlaka hiyo kushindwa kusimamia uendelezaji wa bonde hilo na kusababisha malalamiko kutoka kwa wananchi.

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo jana (Jumatatu, Septemba 26, 2016) wakati akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Ikwiriri mkoani Pwani.

Alisema baada ya mapitio hayo shughuli za mamlaka hiyo zitahamishiwa kwenye mamlaka nyingine za serikali kwani RUBADA  imeshindwa kufanyakazi hiyo kwa muda mrefu.

“RUBADA wamepewa ardhi lakini wameshindwa kuiendeleza, tutafanya upya mapitio ya kuanzishwa kwake,” alisema.
 
Akizungumzia kuhusu Kampuni ya Agro Forestry Plantation inayotaka kujenga kiwanda cha sukari wiyani Rufiji aliitaka kampuni hiyo kuhakikisha asilimia 60 ya watumishi watakaowaajiri wawe ni vijana wa wilaya hiyo.

Katika hatua nyingine Waziri Mkuu alimuagiza Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Willium Lukuvi, kwenda wilayani Rufiji kutatua mgogoro wa mpaka kati ya Wilaya ya Mkuranga na Ikwiriri.

Waziri Mkuu amelitoa agizo hilo baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wananchi wa Ikwiriri kuhusu kutotatuliwa kwa mgogoro huo uliodumu kwa muda mrefu.

Naye Mkurugenzi wa halshauri ya wilaya hiyo, Rashidi Salum alimweleza Waziri Mkuu kuwa, mgogoro huo umeshatatuliwa kwa ngazi ya wilaya  hivyo hatua iliyosalia ni kwa uWaziri wa Ardhi kufika na ramani ili kutoa uamuzi.

Ndege Ya Pili Ya Bombardier Q-400 Yawasili Jijini Dar Es Salaam Leo, Rais Magufuli Kuzizindua Ndege Kesho

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli kesho anatarajiwa kuzindua ndege mbili mpya aina ya Bombardier Q 400 zilizonunuliwa na Serikali hivi karibuni.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Uchukuzi) Dkt. Leornard Chamuriho amesema maandalizi yote kwa ajili ya uzinduzi wa ndege hizo yamekamilika na uzinduzi huo utafanyika katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Kesho kuanzia saa mbili asubuhi.

“Tunawaomba wanahabari na wananchi kujitokeza kwa wingi katika uzinduzi huo ili waone utekelezaji wa ahadi wa Serikali katika mkakati wa kuhuisha usafiri wa Anga hapa nchini”, amesema Dkt. Chamuriho.

Ndege hizo aina ya Bombardier Q 400 zenye uwezo wa kubeba abiria 76 kila moja  zimetengenezwa nchini Canada na zitahudumia soko la ndani ndani na nchi za jirani zitakapoanza kazi.
Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.
Katibu Mkuu Uchukuzi, Dkt. Leonard Chamriho akiwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa ATCL Mhandisi Ladislaus Matindi pamoja na maafisa wengine wakiwa katika Ndege ya pili ya Bombadier Q400 iliyonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Taifa (ATCL) mara ilipotua katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Septemba 27, 2017 ikitokea Canada ilikotengenezwa.
Katibu Mkuu Uchukuzi, Dkt. Leonard Chamriho na viongozi wengine wakielekea kwenye Ndege ya pili ya Bombadier Q400 iliyonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Taifa (ATCL) ilipowasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Septemba 27, 2017 ikitokea Canada ilikotengenezwa. Sherehe za uzinduzi rasmi wa ndege hizo umepangwa kuganyika kesho Jumatano Septemba

Baraza Kuu la Uongozi CUF lamfuta uanachama Profesa Lipumba

$
0
0
Baraza Kuu la Uongozi la Chama cha Wananchi (CUF) Taifa lililokutana Zanzibar leo limemfukuza uanachama Mwenyekiti wa chama hicho Taifa, Prof. Ibrahim Lipumba.

Taarifa kutoka katika mkutano chama hicho unaeleza kuwa, wajumbe wote waliohudhuria wamepiga kura ya kuridhia kufukuzwa uanachama kwa Prof. Lipumba.

Hatua hii imekuja ikiwa ni siku chache tangu Prof. Lipumba kurejea na kusema kuwa yeye ni mwenyekiti halali wa chama hicho kufuatia maamuzi yaliyotolewa na Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Mutungi.

Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la CUF limefikia uamuzi huo kwa mujibu wa Katiba ya Chama, Ibara ya 10 (1)(c).

Majina Ya Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga Chuo Kikuu Iringa(University Of Iringa) 2016/2017

$
0
0



Bachelor of Arts in Journalism
S/NSurnameFirstNameSecondNameSex
1AWESOAMINAAF
2MSUYASTEPHANOPM
3HAYUMAEMMANUELATANASM
4ABDALLAHKHATAMISM
5MASANJAJOHNM
6CHRISANTVENANCEM
7SAMKNICOLAUSNICOMEDM
8AMANIMASOUDM
9PASTORYMARCOBUNDALAM
10NYONIGODFREYEM
Bachelor of Laws
1BAKARIMTANARASHIDM
2KAYOMBOMICHAELM
3MBWIGAPIUSM
4MNAKUWILSONM
5MOLLELMATHEWJM
6MUTAKIFELIXWM
7NYALUSIHEKIMAM
8TUNZOGRACEF
Bachelor of Arts in Cultural Anthropology & Tourism
1CHIUNAMAGANGEJM
2EDWARDOLARIVKM
3JUMAJUMASELEMANIM
4KIMAMBOANGELAANDREWF
5KITALEANTHONYM
6MAKONGOELLYMAJURAM
7MASSAMBEATRICEISARIAF
8MKANGAFERDINANDYJOHNM
9MTAKYAWARUBENIPAULOM
Bachelor of Counselling
1AYOELINAMINM
Bachelor of Education (Mathematics)
1DJUMAMARIAMUBUSHIRIF
2JACKSONONESMOM
3JOHNFORTUNATUSM
4MASELEJUMAM
5MOSHAFRANCISPM
6SAJISIASASM
7TAMILWAIHILDAJEREMIAF
Bachelor of Arts in Community Development
1BYABATOWINFRIDADF
2GAJIJIMEHANSIJM
3GAMBAFRANKBISEKOM
4JUSTINEELIFRIDAEUSTADF
5KASSIMNUSURAAF
6KATITIGIVENOSWARDM
7KIWANGOGLORYOLVARISF
8LEONARDRICHARDREGINALDM
9LICHEULAMARYJOHNF
10LUCASHEZRONKALAMUM
11MAHAGULACATHERINECAMARAF
12MASANAGULILOGLADNESSSAMWELF
13MASATIPETERJOFREYAM
14MIRAJIABUBAKARSAIDM
15MLAYGLADNESSDF
16MSANGWACECILIAF
17MWAMLENGAJEREMIAHJAMESM
18MWINUKADAINESYONAF
19MZIRAYHABIBANUHUF
20NAMAZUNGOMARYFF
21REUBENISAYAM
22SANGAJERRYSM
23URASSAGODFREYJACOBM
Bachelor of Business Administration
1MASILUGEAZEM
Bachelor in Divinity
1YAROJACKLINEJF
Bachelor of Science in Information Technology
1ATHUMANIBAKARIM
2FELLICIANBENJAMINM
3GERALDROBERTM
4KABIKAMASOUDSALUMM
5KADAMAEMMANUELM
6KALAGHEPIERREGETTYSPM
7KAONDOYUSUPHM
8KIMWERIMAGRETHTF
9LUGAZOSAUMUHAMISIF
10MBALAJOSEPHRICHARDM
11MERINOFABIANOM
12MGUGUHAMISIMNYAMPINDAM
13MSANGIAMINAF
14MWANITEGALEAHDANIELF
15MWASIGODFREYPM
16PAULFRANKM
17PETROTHERESIAKF
18SILAYOIRENENF
19SUBURYAJAMESM
Bachelor of Accounting and Finance
1TEMUCATHERINEMICHAELF
Bachelor of Science in Economics & Finance
1MEKLAUDGLORYMAKUNDIF
2MHONGOLEABEIDBM
3NSHUSHIALEXRESPICHM
4PETERMARGARETAAF
5RWEYEMAMUJESCALAWRENCEF
Bachelor of Education (Arts)
1ABRAHAMMATILDAF
2AGGREYABRAHAMM
3ALLYSAIDIM
4ANNEYMARIAGF
5ANNEYSAMSONPETERM
6ASSAHISAYAM
7BARNABANATALIAF
8BAYYOPAULODEEMAYM
9BULONGOFURAHADF
10BUNG'ERAROBERTBM
11BUZUKABADEHEBF
12CHAVALAFABIANOM
13CHRISANTWINCHESLAUSRM
14DANIELDEVOTHAF
15DANIELMUSAM
16DEUSMAIGEM
17DONARDNDEBILEFM
18ELIAHLILIANF
19ELIAKIMUNAOMIDF
20EMMANUELEDWARDSHABANIM
21EMMANUELALFREDM
22EMMANUELMICHAELM
23EZEKIELRAFAELM
24FUMBOLUPAKISYOGF
25FUNJIKERAYMONDOSMONDM
26GANGALAPETROM
27GAUDENCEAUGUSTINEM
28HALAMBASAYM
29HAMADICHARLESHAMISIM
30HAMZAZUBEDAOMARYF
31HASSANIHAMISIM
32HUBERTAUGUSTINOM
33JEREMIAOMITOM
34JIMSONJONATHANM
35JOHNKULWAGM
36JOSHUAJENIFERALEXF
37JUMAFURAHAMIRAJIF
38JUMAJUMAMM
39JUSTINEEMMANUELM
40KADUMARUBENADRIANM
41KAJEMBEJAMILLAHSAIDF
42KAMBONAMAUDIASF
43KANDONGAJOSHUAAM
44KASEKWAABELSM
45KAVAYAAGNETALINUSF
46KETUTATEYANOISF
47KIDASIYOBULUTENGAMASOM
48KIIZAVENITHAF
49KIJANGALIGHTNESSPETERF
50KILANGAIGNASKM
51KIMAMBOGEOFREYM
52KIMWELAGEROGASIANAF
53KIRUATWAKYONDOAM
54KISANGAJOSEPHINEG.F
55KITASHUKURULAUDENM
56KOMANYAJERRYM
57KOMBALUCYLUTGELF
58KOMBABAHATIJOHNM
59LEOCHRISTINAHENRICKF
60LUGUMBAERICKMESAUSM
61LUHANGABETHMESIAF
62LUKINISHAFLORAYUSTOF
63LUXUMEDAREBECADF
64LYOGELAROZAREVOCATUSYF
65MABUTULETICIADF
66MAHENGEGODFREYNICKSONM
67MANENTOATHUMANIZAKARIAM
68MANONIFARAJIODILOM
69MAPUNDAAGNESADAMF
70MARCOEUNICEF
71MARCODEOGRATHIASM
72MARTINEEDWARDM
73MARWAZACHARIAMM
74MASABOLEONARDLENATUSM
75MASHIMBAZAKAYOM
76MASUDIHABIBAHUSSEINF
77MATONDONSULWAM
78MBAGOJULIUSJASTICEM
79MBEGALOBARAKARM
80MBWILOKELVINFM
81MDENDEMIUFUNUOPETERM
82MGALEENITHAF
83MGANGAREHEMASAIDF
84MGATASAMWELDONATUSM
85MGAZASHABANIOM
86MGONJAMONICAMOSESF
87MHAGAMAHILARYATHANASM
88MICHAELTHOMASM
89MKILIMAMUMINIHAMISIM
90MKINIMILTONMM
91MLIGOEMILEERNESTF
92MMBAGAAMINANUHUF
93MMBANDOTUMAINISTEVENM
94MNGOMAELIZABETHYONAF
95MNYANYAJENIFERGF
96MOHAMEDIBAKARIBURUHANIM
97MOTTOHAPPYAF
98MPINDAEDSONM
99MSAFIRINURUMF
100MTEMIDAUDIEMMANUELM
101MTUMBELAYOHANAMICHAELM
102MUHSINIADAMISSAM
103MUSTAFASALUMUM
104MUYEMBATHOMASM
105MWAGENICATHERINEF
106MWAMBIPILEORDENKM
107MWAMSOJOATUPAKISYEALLYF
108MWANANSASEYUSTINOMELKIORM
109MWANDAGOAGGREYJULIUSM
110MWAPINGAHONGERADAMIANF
111MWASHALULAJOSHUAUM
112MWIKOLAGETRUDAGAUDENSIF
113NDALIHAZESARAHF
114NDOGAATHUMANMASUDM
115NDULUTEPALYUSIGILBERTM
116NDUNGURUREMIGIUSHYAZINTM
117NGUKUEVERERNESTIF
118NJILESIDAM
119NKULIYEVIOLETHSYLVANUSF
120NKYAELIFASINELSONM
121OBADIAFRANKM
122OMARIAMIRIALLYM
123PENDAELMAWAZOZEPHANIAM
124PETERMARIAF
125PHILEMONBERTHAF
126PHILIDOLINEALICEF
127RAJABURAJABUSAIDIM
128RASHIDASHANTIAF
129RASHIDEMMANUELM
130RENATUSREUBENPHABIANM
131SABBIVENERANDAF
132SAIDIFADHILIM
133SAIDIABEDIM
134SAMSONMARIAMF
135SAMWELLAMECKGABRIELM
136SAMWELKULWAM
137SANGAFRIDAALEXF
138SANJOLILIANF
139SIJAONASUNDAYM
140SIMKOKOSALOMESIMONF
141TAWAHHEMEDHAJJM
142TETEIMANIAM
143TOIMALEKENIM
144TUNGALAZALEONARDMM
145VEDASTOAVETHF
146WATSONINNOMM
147WAZIRISWAUMUAF
148WAZOELFADHILIABRAHAMUM
149WILSONELIWAZAF
150YOHANAMECKTRIDAWANKILOF
Bachelor of Business in Marketing Management
1KIOLOGWEANGELEZEKIELF
2KITOMARYLIGHTNESSIF
3NCHIMBIJOYCESF
Bachelor of Human Resource Management
1MAKUNGAVALENTINEEM
2MAULIDABDULKADRIRM
3WILLIAMSTEPHANOM

Majina Ya Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga Chuo Kikuu Bugando(Cuhas) 2016/2017

$
0
0

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatano ya Septemba 28

Taarifa Rasmi ya Baraza Kuu la Uongozi la CUF lililokutana Zanzibar jana Kumjadili Profesa Lipumba na Msajili wa Vyama

$
0
0
MAAZIMIO NA MAAMUZI YA BARAZA KUU LA UONGOZI LA TAIFA LILILOKUTANA KWENYE MAKAO MAKUU YA CHAMA, MJINI ZANZIBAR
TAREHE 27 SEPTEMBA, 2016

Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la The Civic United Front (CUF – Chama Cha Wananchi) limekutana leo, Jumanne, tarehe 27 Septemba, 2016 katika kikao cha dharura kilichofanyika Makao Makuu ya Chama, mjini Zanzibar na ambacho kiliitishwa na Kamati ya Utendaji ya Taifa kwa mujibu wa Katiba ya Chama ya 1992 (Toleo la 2014), Ibara ya 80 (1). Wajumbe 43 kati ya wajumbe 53 wa Baraza Kuu la Uongozi la Taifa walihudhuria kikao hicho.

Agenda tatu zilizotayarishwa na kuwasilishwa na Kamati ya Utendaji ya Taifa zilijadiliwa na kufanyiwa maamuzi ambazo ni:

1. Kujadili barua ya Msajili wa Vyama vya Siasa ya tarehe 23/09/2016;

2. Kupokea na kujadili mashtaka dhidi ya Prof. Ibrahim Lipumba kutokana na hujuma alizozifanya tarehe 24/09/2016 Afisi Kuu ya Chama, Buguruni, Dar es Salaam;

3. Kumjadili na Kumhoji Prof. Ibrahim Lipumba mbele ya kikao na kumchukulia hatua za kinidhamu.

Baada ya mjadala wa kina wa agenda hizo, Baraza Kuu la Uongozi la Taifa limefikia maazimio na maamuzi yafuatayo:

KUHUSU BARUA YA MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA YA TAREHE 23/09/2016:

1. Baraza Kuu limeukataa ushauri, msimamo na mwongozo wa Msajili wa Vyama vya Siasa alioutoa kupitia barua yake ya tarehe 23/09/2016 kwa sababu Sheria ya Vyama vya Siasa (Political Parties Act, No. 5 of 1992) – Sura ya 258 haimpi mamlaka wala uwezo wowote kutoa ushauri, msimamo au mwongozo kwa vyama vya siasa kuhusiana na maamuzi ya vikao vya Chama na kwa kulitambua hilo ndiyo maana katika matamko yake yote aliyoyatoa, Msajili huyo ameshindwa kutaja kifungu gani cha sheria hiyo kinampa uwezo huo.

2. Baraza Kuu limesikitishwa sana na kitendo cha Jaji Francis Mutungi kujishushia hadhi, kujifedhehesha na kujivunjia heshima mbele ya macho ya jamii ndani na nje ya nchi, yeye na Ofisi anayoiongoza kwa kuvunja sheria na kudharau maamuzi ya Mahakama Kuu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia UAMUZI wa tarehe 9/5/2005 wa Jaji T.B. Mihayo katika kesi ya Emmanuel Nyenyemela na Magnus Msambila v/s Registrar of Political Parties & Others (Civil Case No. 6 of 2003) ambapo Jaji Mihayo aliamua kwamba:

“… I do not see anywhere in the Political Parties Act where the Registrar has power to bless or condemn meetings of political parties or decisions that they make.”

Tafsiri yake ikiwa ni kwamba, “… Sioni popote katika Sheria ya Vyama vya Siasa ambapo Msajili ana madaraka ya kubariki au kupinga vikao vya vyama vya siasa ay maamuzi ambayo vikao hivyo vinafanya.”

3. Baraza Kuu limemuagiza Katibu Mkuu wa Chama kumjibu kwa maandishi na kwa kina Msajili wa Vyama vya Siasa na kumueleza maamuzi ya Baraza hilo ambalo kikatiba ndilo lenye madaraka ya kusimamia uendeshaji wa Chama kwamba halitambui ushauri, msimamo na mwongozo huo na limeutupilia mbali kwa kukosa kwake mantiki, hoja na pia kukosa nguvu za kisheria.

4. Baraza Kuu linamtanabahisha Msajili wa Vyama vya Siasa kwamba atabeba dhamana kwa yote yaliyofanywa na yatakayofanywa na Prof. Ibrahim Lipumba na kikundi chake cha wahuni ambacho kilivamia Ofisi Kuu ya CUF, Buguruni, Dar es Salaam tarehe 24 Septemba, 2016 na kupiga watu na kufanya uharibifu wa mali kutokana na tamko lake hilo ambalo halina msingi wa kisheria.

KUHUSU MASHTAKA DHIDI YA PROF. IBRAHIM LIPUMBA KUTOKANA NA HUJUMA ALIZOZIFANYA TAREHE 24/09/2016 AFISI KUU YA CHAMA, BUGURUNI, DAR ES SALAAM:

1. Baraza Kuu limepokea mashtaka dhidi ya Prof. Ibrahim Lipumba yaliyoandaliwa na Kamati ya Utendaji ya Taifa ambayo kwa mujibu wa Katiba ya Chama, Ibara ya 108 (1) ndiyo yenye mamlaka ya kusimamia nidhamu ya Chama katika ngazi ya Taifa na kuyawasilisha mapendekezo yake mbele ya Baraza Kuu la Uongozi la Taifa.

2. Baraza Kuu limeridhika kwamba Kamati ya Utendaji ya Taifa imefuata masharti yote ya Katiba ya Chama ya 1992 (Toleo la 2014) katika kuanda mashtaka hayo kutokana na mtuhumiwa, Prof. Ibrahim Lipumba, kuvunja Katiba ya Chama, Ibara ya 12 inayohusu ‘Wajibu wa Mwanachama” hasa Ibara ndogo za 12 (6), 12(7) na 12(16).

KUHUSU KUMJADILI NA KUMHOJI PROF. IBRAHIM LIPUMBA MBELE YA KIKAO NA KUMCHUKULIA HATUA ZA KINIDHAMU:

1. Baraza Kuu la Uongozi la Taifa limeridhika kwamba Kamati ya Utendaji ya Taifa ilimfikishia mtuhumiwa, Prof. Ibrahim Lipumba, barua ya wito (Kumb. Nam. CUFHQ/OKM/WM/2016/Vol.1/49 ya tarehe 24/09/2016) ambayo pia ilikuwa na maelezo ya tuhuma na kumtaka afike mbele ya kikao cha Baraza Kuu la Uongozi la Taifa kilichofanyika leo, tarehe 27 Septemba, 2016, mjini Zanzibar kuja kujieleza na kujitetea kwa nini asichukuliwe hatua za kinidhamu kwa mujibu wa Katiba ya Chama kwa kuvunja masharti yanayohusu “Wajibu wa Mwanachama” Ibara ya 12(6), 12(7) na 12(16).

2. Baraza Kuu limesikitishwa na dharau iliyooneshwa na Prof. Ibrahim Lipumba dhidi ya kikao hiki ambacho ni chombo cha juu chenye mamlaka ya kusimamia uongozi wa Chama pamoja na kupelekewa wito wa kumtaka afike mbele yake. Kitendo hicho cha dharau kinaonesha tu jinsi gani heshima na uaminifu wa Prof. Ibrahim Lipumba kwa Chama ulivyoshuka.

3. Baraza Kuu limeridhika kwamba kwa kuwa Prof. Ibrahim Lipumba akiwa mtuhumiwa alichagua mwenyewe kudharau wito wa kufika kujieleza na kujitetea ambayo ni haki yake kama mwanachama kwa mujibu wa Ibara ya 11(6) ya Katiba ya Chama, halikuwa na sababu ya kutoendelea kumjadili na kuchukua hatua dhidi yake.

4. Baraza Kuu limeridhika na mashtaka dhidi ya Prof. Ibrahim Lipumba kwamba kwa kitendo chake cha kuongoza na kusimamia kikundi cha wahuni kuvamia Ofisi Kuu ya Chama, Buguruni, Dar es Salaam, siku ya Jumamosi, tarehe 24 Septemba, 2016 na watu hao aliowaongoza na kuwasimamia kupiga walinzi waliokuwepo, kuvunja na kuharibu mali za Chama na hivyo kuharibu heshima na taswira ya Chama mbele ya jamii ndani na nje kwamba amtenda makosa kinyume na “Wajibu wa Mwanachama” kama ilivyoelezwa kwenye Ibara ya 12(6), 12(7) na 12(16) za Katiba ya Chama.

5. Baada ya kuridhika na mashtaka hayo, Baraza Kuu la Uongozi la Taifa limeamua kwa kutumia uwezo wake kwa mujibu wa Ibara ya 10 (1) (c) na kwa kura zote 43 za wajumbe wake waliohudhuria kumfukuza uanachama Prof. Ibrahim Lipumba, kuanzia tarehe ya leo, Jumanne, tarehe 27 Septemba, 2016.

6. Kwa maamuzi haya, Baraza Kuu linaweka bayana kwa wanachama wa CUF, Watanzania na mamlaka zote nchini kwamba kuanzia tarehe ya leo, Prof. Ibrahim Lipumba hana haki ya kujihusisha kwa namna yoyote ile na shughuli zozote za Chama.

MWISHO:

Baraza Kuu la Uongozi la Taifa linawapa pole wanachama wa CUF walioathirika kutokana hatua ya Msajili kuingilia mambo ya Chama kinyume na uwezo alio nao na pia kwa matendo ya kihuni yaliyofanywa na Prof. Ibrahim Lipumba na kikundi chake kuvamia Ofisi Kuu ya Chama. Wakati huo huo, Baraza Kuu linawapongeza wanachama wote kwa kusimama imara kukilinda Chama chao na linawahakikishia litasimamia wajibu wake wa kikatiba kukiongoza na kukilinda Chama hiki dhidi ya njama za maadui wa ndani na nje.

HAKI SAWA KWA WOTE

BARAZA KUU LA UONGOZI LA TAIFA
THE CIVIC UNITED FRONT (CUF – Chama Cha Wananchi)

27 Septemba, 2016
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images