Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Maneno 285 ya Prof. Lipumba baada ya kufika Makao Makuu ya CUF jana

0
0

Baada ya Msajili wa Vyama vya Siasa kutangaza kuwa, Prof. Lipumba bado ni mwenyekiti halali wa Chama cha Wananchi (CUF), jana kiongozi huyo aliandamana na wananchi na wananchama wa CUF hadi Makao Makuu ya Chama hicho yaliyopo Buguruni jijini Dar es Salaam.

Akiwa ndani ya ofisi za chama, Prof. Lipumba alipata wasaa wa kuzungumza na waandishi wa habari na alikuwa na haya yakueleza;

"Mimi ni kweli niliandika barua ya kujiuzulu, tarehe 5 Agosti mwaka jana, lakini baada ya uchaguzi wazee walikuja kuoniomba nirejee kwenye nafasi ya uenyekiti kwa sababu hali ya chama haikuwa nzuri kitaifa, alisema Prof. Lipumba

"Tarehe 8 nwezi wa 6 niliandika barua ya kutengua barua yangu ya kujiuzulu na kwa mujibu wa katiba yetu (CUF) kujiuzulu kwako kutakuwa kamili endapo mamlaka iliyokutua/kuchagua itaridhia maamuzi yako, hivyo Mkutano Mkuu haukuwa umekutana kupitisha barua yangu ya kujiuzulu hivyo nilivyoandika barua ya kutengua, nilirudi kuwa Mwenyekiti wa CUF.

"Baada ya mvutano mrefu, tuliandika barua kwenda kwa Msajili wa Vyama, akamuita Katibu Mkuu wa CUF na timu yake, akawaita na walalamikaji, na wazee pamoja na mimi ili aweze kulisuluhisha. 

"Na baada ya yeye kusikiliza, ametoa msimamo wake kuhusu mgogoro wa uongozi wa CUF ambapo amesema mimi bado ni mwenyekiti halali wa CUF hadi sasa", alisema  Prof. Lipumba

Katika msimamo uliotolewa na msajili wa vyama akielezea kwanini Prof. Lipumba ni mwenyekiti halali wa CUF alisema kuwa ni kwa sababu Mkutano Mkuu haujaipitisha barua yake ya kujiuzulu wala haujakataa barua yake ya kurejea kazini, lakini alichoambiwa ni kuwa asienze kazi Juni 10 kama alivyokuwa ameeleza kwenye barua yake.

Aidha, Prof. Lipumba alihitimisha kwa kusema kuwa Kamati iliyoteuliwa kuongoza chama ni batili kwa sababu hata kikao kilichowateua ni batili na hivyo kamati hiyo isijaribu kuongoza chama hicho kwani yeye ndiye mwenyekiti wa CUF.

Rais Magufuli afanya uteuzi wa Naibu Katibu Mkuu TAMISEMI

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili ya Septemba 25

Joti TV Episode 20 Pesa za Babu

0
0
Babu tayari ashakupa mchongo wa milioni 200 alafu anakata kamba..Utafanyaje?

Mwalimu Nyerere Aenziwe Kwa Vitendo – NEC

0
0
Na. Aron Msigwa – NEC.
Viongozi wa vyama vya Siasa wametakiwa kuiga kwa vitendo uzalendo na moyo wa kujitoa  aliokuwa nao Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere enzi za uhai wake  ili kuliwezesha Taifa kupiga hatua kimaendeleo.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Bw. Kailima Ramadhani  mara baada  kutembelea Kaburi na Makumbusho ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere eneo la Mwitongo wilayani Butiama.

Amesema kuwa kumbukumbu za Baba wa Taifa zilizohifadhiwa vizuri katika makumbusho hiyo zina mambo mengi ya kujifunza ambayo wanasiasa wanatakiwa kuyafanya kwa  vitendo hasa  uzalendo kwa nchi, uvumilivu, upendo  na moyo wa kujitoa kwa dhati kuwatumikia wananchi.

“Kupitia kumbukumbu hizi sisi watumishi wa Tume tumejifunza ukomavu wa demokrasia aliokuwa nao Mwalimu Nyerere akiwa ndani na nje ya Bara la Afrika,  wengi wanadhani Demokrasia ni wakati wa uchaguzi tu, kumbe demokrasia ni pamoja na kuheshimu watu wengine” Amesema Kailima.

Ameeleza kuwa maisha aliyoishi Baba wa Taifa ni mfano wa kuigwa na viongozi na watanzania wote hasa pale alipojitofautisha na viongozi wengi wa Bara la Afrika alipoepuka tamaa ya madaraka na mali kwa  manufaa ya taifa.

“Sote ni mashahidi kupitia kumbukumbu zake tumeona mahali alipokuwa anaishi mwalimu kabla hajajengewa nyumba na Jeshi  kama Rais mstaafu wengi walitegemea asingeishi katika  eneo lile, kumbukumbu hii nzuri aliyoiacha inatufundisha watanzania kuwa mwalimu aliitanguliza Tanzania mbele kuliko maslahi yake binafsi” Amesisitiza.

Bw. Kailima amebainisha kuwa  NEC itaendelea  kumuemzi Baba wa Taifa kwa yale aliyoyafanya na kuyasimamia kwa manufaa ya taifa huku akitoa wito kwa  viongozi wa vyama vya Siasa wawe na kiasi na waridhike na vile walivyonavyo.

“Suala la kuridhika na kuwa na kiasi linapaswa kuzingatiwa, wanasiasa  wanapaswa kuwaheshimu wananchi wanaowachagua kupitia chaguzi mbalimbali,  matokeo yanapotoka kama ni sahihi basi wanasiasa wakubaliane na maamuzi yao”  Ameainisha Kailima.

Kwa upande wake Mhifadhi wa Makumbusho ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Bw. Jacob Thomas amesema kuwa  watanzania wanayo mengi ya kujifunza kupitia vitu alivyoviacha Baba wa Taifa ambavyo vimehifadhiwa katika Makumbusho hiyo.

Amesema kuwa maisha ya uadilifu aliyoishi enzi za uhai wake na mchango wake katika kuiletea maendeleo Tanzania na Bara la Afrika vinapaswa kuenziwa kwa nguvu zote na viongozi wa Tanzania.

“Ninyi mliopata nafasi ya kuitembelea makumbusho hii mmejifunza vitu vingi kumhusu Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kwamba alikuwa ni mtu wa namna gani kwa viwango vya Afrika na dunia kutokana na kumbukumbu ya uadilifu aliyoiacha ndani na nje ya mipaka ya Tanzania”
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Kailima Ramadhani akiwasili nyumbani kwa familia ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Butiama Musoma akiwa ameambatana na watumishi wa NEC  na baadhi ya wajumbe wa mkutano wa ALAT kutoka maeneo mbalimbali  kuzuru kaburi la Baba wa Taifa, Mwitongo wilayani Butiama. Tume ya Taifa ya Uchaguzi iko mkoani Mara kutoa elimu ya mpiga kura kwa wananchi.
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Kailima Ramadhani (Kushoto) akisalimiana na Msemaji Mkuu na kiongozi wa familia ya Baba wa Taifa Chifu Japhet Wanzagi (kulia) mara baada ya kuwasili eneo la Mwitongo wilayani Butiama. Wa Pili kutoka Kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Butiama Bi. Annarose Nyamubi.

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Kailima Ramadhani akiwasha mshumaa kwenye kaburi la Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere eneo la Mwitongo, Butiama. Wengine wanaoonekana na baadhi ya wajumbe wa mkutano wa ALAT na watumishi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).

Mwongoza wageni na Mhifadhi wa Makumbusho ya Mwalimu Nyerere Butiama, Jacob Thomas akitoa maelezo kuhusu picha za kumbukumbu za Baba wa Taifa kwa Mkurugenzi wa NEC Bw. Kailima Ramadhani na watumishi wa NEC walioitembelea makumbusho hiyo eneo la Mwitongo, Butiama –Musoma.

Rais Magufuli Ashiriki Ibada Ya Jumapili Kuadhimisha Siku Ya Bwana Ya 19 Baada Ya Pentekoste Kanisa La Mtakatifu Albano Jijini Dar Es Salaam Sept 25,2016

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, leo asubuhi tarehe 25 Septemba, 2016 ameungana na Waumini wa Kanisa la Anglikana la Mtakatifu Albano lililopo Posta Jijini Dar es Salaam kusali ibada ya Jumapili ya kuadhimisha Siku ya Bwana ya 19 baada ya Pentekoste.

Akizungumza na Waumini wa Kanisa hilo baada ya kumalizika kwa Ibada, Rais Magufuli aliyeongozana na Mkewe Mama Janeth Magufuli amewashukuru Viongozi na Waumini wa Kanisa la Anglikana na Madhehebu mengine ya Dini hapa nchini kwa kuendelea kuliombea Taifa na kudumisha amani na utulivu.

Dkt. Magufuli amesisitiza kuwa Viongozi wa Dini wanafanya kazi kubwa na muhimu katika Taifa na kwamba Watanzania wote bila kujali dini zao, itikadi za kisiasa, makundi na kanda zao wana wajibu wa kuungana na Viongozi hao ili nia hiyo njema iendelee kufanikiwa.

“Ninawashukuru kwa sababu mnaendelea kuliombea Taifa hili, ninawashukuru kwa sababu siku zote mmekuwa mkipiga magoti na kumtanguliza Mungu mbele, ninawashukuru kwa sababu mnaendelea kuombea amani ya nchi yetu na upendo udumu ndani yetu sisi sote.

“Makanisa yote, Madhehebu yote, Dini zote, Vyama vyote, upendo tukiujenga ndio tutaiendeleza vizuri Tanzania yetu” Amesema Rais Magufuli.

Kwa upande wake Padre Jackson Sostenes aliyeongoza Ibada hiyo amemshukuru Rais Magufuli kwa kuungana na waumini wa Kanisa hilo katika Ibada ya Jumapili na ameahidi kuwa Viongozi na Waumini wa Kanisa hilo wataendelea kumuombea na kuliombea Taifa.

Katika Ibada hiyo Rais Magufuli ametoa Shilingi Milioni 1 kuchangia vikundi vya kwaya vya kanisa hilo.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
25 Septemba, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na baadhi ya waumini wa kanisa la Anglikana la Mtakatifu Albano jijini Dar es salaam baada ya  Ibada ya Jumapili kuadhimisha siku ya Bwana ya 19 baada ya Pentekoste asubuhi ya leo Septemba 25, 2016.
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akisalimia waumini wa  kanisa la Anglikana la Mtakatifu Albano jijini Dar es salaam baada ya  Ibada ya Jumapili kuadhimisha siku ya Bwana ya 19 baada ya Pentekoste asubuhi ya leo Septemba 25, 2016.
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akisalimiana na Padri Thomas Godda na Padri Johnson Godda katika  kanisa la Anglikana la Mtakatifu Albano jijini Dar es salaam baada ya  Ibada ya Jumapili kuadhimisha siku ya Bwana ya 19 baada ya Pentekoste asubuhi ya leo Septemba 25, 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiteta jambo na  Padri Mstaafu Gideon Gweja katika  kanisa la Anglikana la Mtakatifu Albano jijini Dar es salaam baada ya  Ibada ya Jumapili kuadhimisha siku ya Bwana ya 19 baada ya Pentekoste asubuhi ya leo Septemba 25, 2016

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatatu ya Septemba 26

Jela maisha kwa kuchoma moto makanisa Bukoba

0
0

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Bukoba mkoani Kagera imewahukumu kifungo cha maisha watu watatu kwa makosa ya kula njama na kuchoma makanisa mbalimbali mkoani hapa.

Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Emmanuel Manyere alisema licha ya hukumu hiyo, bado watu hao watatu wanakabiliwa na kesi ya kukata makoromeo na mauaji ya watu 16 ambayo inaendelea katika Mahakama Kuu, Kanda ya Bukoba.

Manyere alisema watu hao watatu ambao ni Allyu Dauda, Rashid Mzee na Ngesela Keya walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi, mbele ya Hakimu Mkazi wa Bukoba, Victor Biambo.

Alisema washtakiwa hao kwa pamoja wamekutwa na hatia ya kula njama na kuchoma makanisa 16 ya madhehebu mbalimbali mkoani hapa.

Hakimu Bigambo alisema Mahakama imeridhishwa na ushahidi kutoka upande wa walalamikaji na kutoa adhabu ya kifungo cha miaka saba jela kwa wote watatu kwa kosa la kula njama na kifungo cha maisha kwa kosa la kuchoma makanisa.

Wakati huo huo, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kagera Augustino Ollomi aliipongeza Mahakama kwa kutenda haki katika kesi hiyo pamoja na kuwataka wananchi waendelee kutoa ushirikiano kwa polisi ili kukomesha vitendo kama hivyo.

Licha ya hukumu katika kesi hiyo namba 67, bado watu hao watatu wanakabiliwa na kesi ya mauaji ya watu 20 katika maeneo mbalimbali mkoani humo inayoendelea katika Mahakama Kuu, Kanda ya Bukoba.

Mgogoro CUF Wachukua Sura Mpya

0
0
Kamati ya Uongozi ya Chama cha Wananchi (CUF), imeitisha kikao cha Baraza Kuu la Uongozi Taifa, ili kumhoji mwenyekiti aliyerudishwa madarakani, Profesa Ibrahim Lipumba.

Wakati wajumbe wa baraza hilo wakijiandaa kukutana kesho visiwani Zanzibar kutekeleza mpango huo, jana kutwa nzima, Profesa Lipumba alikuwa na kikao kizito na walinzi wa chama hicho (Blue Guard) makao makuu ya chama hicho Buguruni, Dar es Salaam.

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari jana na Naibu Katibu Mkuu wa CUF (Zanzibar), Nassor Ahmed Mazrui ilisema baraza hilo, linamtaka Profesa Lipumba afike mbele ya kikao hicho ili  ajieleze na kujitetea kwanini asichukuliwe hatua za kinidhamu kutokana na kitendo chake cha kuvamia ofisi za makao makuu na kusababisha uharibifu wa mali.

“Kamati haijakubaliana na maoni na ushauri uliotolewa na Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi juu ya Lipumba. Ilikutana jana (juzi)  kwa kikao cha dharura ofisi za Makao Makuu, Zanzibar na kujadili taarifa ya msajili,” ilisema taarifa hiyo.

Taarifa hiyo, ilisema  kamati pia ilijadili  kitendo cha uvamizi wa ofisi za Buguruni, kilichofanywa na Profesa Lipumba akiwa na kundi  la vijana ambao si wanachama wa CUF.

Alisema baada ya kikao kupitia maoni ya msajili, kamati iliamua kukataa na kupinga kwa hoja thabiti ushauri na maoni aliyoyapendekeza na badala yake inaendelea kusimamia maamuzi ya Mkutano Mkuu Maalumu  Taifa uliofanyika Agosti 21, mwaka huu.

“Katika mkutano ule, wajumbe walikubali Lipumba kujiuzulu kama mwenyekiti wa chama na katika kikao cha Baraza Kuu la Uongozi Taifa cha Agosti 28, mwaka huu, waliridhia kuwasimamisha uanachama Lipumba, Magdalena Sakaya, Maftaha Nachuma, Abdul Kambaya, Masoudi Mhina, Thomas Malima, Ashura Mustafa, Kapasha H. Kapasha, Musa Haji Kombo, Habibu Mnyaa, Haroub Shamis na kumfukuza uanachama Shashu Lugeye,” alisema.

Taarifa hiyo, ilisema Katiba ya CUF  haina kifungu chochote kinachompa mamlaka Msajili wa Vyama vya Siasa kupokea rufaa kuhusiana na uamuzi wa vikao vya chama na kubatilisha uamuzi wa vikao halali.

“Kutokana na kitendo cha kuvamia ofisi za Buguruni na kusababisha uharibifu wa mali za chama, kamati kwa mujibu wa ibara ya 85(5) na ibara ya 108 ya Katiba ya CUF ya mwaka 1992 Toleo la mwaka 2014 imeitisha kikao cha Baraza Kuu la Uongozi Taifa Septemba 27, mwaka huu saa nne asubuhi ofisi za Zanzibar.

“Kwa mujibu wa Ibara ya 12 (6), (7) na (16) ya Katiba ya CUF ya mwaka 1992 , toleo la mwaka 2014, Kamati imeandaa ajenda ya kumfikisha Lipumba mbele ya Baraza Kuu na atatakiwa kujieleza na kujitetea kwa nini baraza lisimchukulie hatua za kinidhamu kwa matendo yake aliyoyafanya jana (juzi),” alisema.

Katika taarifa hiyo, Mazrui alisema ibara hizo zinaeleza juu ya kulinda heshima ya chama kwa kuwa na tabia njema, kutekeleza masharti ya Katiba, kutii kanuni za sheria na sheria ndogondogo za serikali iliyoundwa kihalali na.

Katika hatua nyingine, Profesa Lipumba jana kutwa nzima alikuwa na kikao na walinzi wa chama hicho, (Blue Guard).

Pamoja na mambo mengine, kikao hicho kilikuwa  na ajenda mbili ikiwamo ya kuimarisha ulinzi katika ofisi zote za chama na kujadili mali za chama ambazo ni pamoja na magari saba na kompyuta zilizoibwa wakati wa vurugu.

Tamko la Kambaya
Pamoja na hali hiyo jana Naibu Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mahusiano ya Umma, Abdul Kambaya, alitoa tamko la kuwataka wanachama wa CUF kuwa watulivu kwa ajili ya kukijenga chama hicho.

Alisema pamoja na hali hiyo CUF ni taasisi na sio eneo la mtu fulani kwani tamko la Naibu Katibu Mkuu CUF Zanzibar, Nassor Hamed Mazrui la kuukataa ushauri wa Msajili wa Vyama vya Siasa uliotolewa kwa mujibu wa Sheria ya Vyama vya Siasa ya mwaka 2002 ni la upotoshaji.

“Kwa mujibu wa Sheria ya Vyama vya Siasa ya mwaka 2002, sehemu ya 20, tamko la msajili ni uamuzi na si tu ushauri kama wanavyotaka kupotosha. Uamuzi huu ni mzito kwa kiwango ambacho hata mahakama inaweza tu kuurejea lakini si kuufuta (rejea ibara ya 20(2).

“Ieleweke kwamba hii si mara kwanza msajili kufanya maamuzi kama haya. Mtakumbuka kwamba aliyekuwa Mwenyekiti wetu Ndugu James Mapalala alienda kwa msajili baada ya kufukuzwa.

“Lakini msajili alitoa uamuzi kwamba maamuzi yale yalikuwa sahihi Kwa kuwa yalifuata katiba yetu ya CUF. Sasa iweje hawa wenzetu leo waseme kwamba ule ni ushauri tu?,” alisema na kuhoji Kambaya ambaye ni mmoja wa wanachama waliosimamishwa na kikao cha Baraza Kuu la Uongozi.

Alisema kilichofanyika Vuga Zanzibar ni uasi wa hali ya juu, hivyo watakaa kama chama kutafakari hatua za kuchukua baada ya kuzuia uasi na kile alichodai mapinduzi haramu kwa chama hicho.

“Sasa kazi yetu ni kujenga chama. Wenzetu walioendesha uasi wana hiari ya kujirudi ili tuungane kufanya kazi ya ujenzi wa chama na kuhudumia wananchi katika maeneo mbalimbali ambapo chama kimepewa ridhaa ya kuongoza."

IPTL, PAP waungana na Tanesco kupinga kuilipa Standard Chartered

0
0

Sakata  la Kampuni ya Kufua Umeme ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL), kugeuziwa kibao kwa kutakiwa kurejesha zaidi ya Dola za Marekani milioni 100 ambazo ni zaidi ya Sh bilioni 216.2 kwa Shirika la Umeme nchini (Tanesco), limezidi kuchukua sura mpya baada uongozi wa kampuni hiyo kuibuka.

Kuibuka kwa viongozi hao kumekuja siku chache baada ya Wakili wa Tanesco, kueleza hatua watakazochukua kuhusu uamuzi huo baadaya Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Kibiashara (ICSID), uliotolewa Septemba 12 mwaka huu unaoitaka Tanesco kuilipa Standard Chartered ya Hong Kong (SCB-HK) Dola za Marekani milioni 148.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Kaimu Mwenyekiti ambaye pia ni Mwanasheria wa Kampuni  wa IPTL,  Joseph Makandege alisema hawatambui madai ya Benki ya Standard Chartered ya Hong Kong (SCB-HK) kama mdai na wala hawana haki kwa mujibu wa sheria.

Kutokana na hali hiyo alisema inaungana na Shirika la Umeme nchini (Tanesco) kukata rufaa katika Mahakama ya ICSID kwani hukumu iliyotolewa ina mapungufu mengi ya kisheria.

Licha ya uamuzi huo Makandege alisema IPTL haikulipwa kwa kutumia viwango vya zamani bali walilipwa kutokana na umeme waliouuza kwa Tanesco na si vinginevyo.

Alisema watu wasifanye makosa kuilipa benki hiyo kwani inachotaka kufanya ni kitendo cha utapeli kwa msukumo wa kampuni za mabeberu.

“Benki ya Standard Chartered ya Hong Kong hawastahili kulipwa fedha na Watanzania kwani hawastahili kwa mujibu wa sheria nasi kama IPTL/PAP hatuwatambui na hawana haki ya kutuzungumzia. Na ndiyo maana wameamua kukimbia mahakama zetu za ndani na kukimbilia nje, hawa wana msukumo wa mabeberu wenye nia ovu.

“Kwa uamuzi huu wenye utata uliotolewa na ICSID ni wazi Standard Chartered walikuwa na nia ovu, ninasema hivyo kwa sababu tangu Septemba 5, mwaka 2013 suala hili liliamuriwa vizuri chini ya Jaji Utamwa (John) na IPTL ikashinda kesi na kutwaa uongozi.

“Na hili si la kwanza kwani Aprili 3, 2014  tulifungua shauri namba 60 chini ya Jaji Dk. Fauz Twalib la kuitaka Mahakama itamke kwamba  benki ya Standard Chartered Hong Kong si wadeni wetu, tena awali waliibuka na hoja kwamba hawasikilizwi na Mahakama zetu za ndani kwa wakati  ambapo shauri hilo lilipangiwa kusikilizwa mfululizo.

“Lakini pia dai letu lingine tuliomba Mahakama Kuu itupe nafuu ya Standard kutulipa gharama kama fidia ya Dola za Marekani bilioni 3.240 ambapo hata tuzo waliopewa na ICSID eti wanataka walipwe Dola za Marekani milioni 148 na kama wakitulipa fedha zetu hata madai yao yaingia humo nabado kuna fedha nyingine inabidi watupatiwe sisi,” alisema Makandege

Wakili huyo ambaye alikuwa akizungumza kwa niaba ya mmiliki wa IPTL/PAP, Harbindar Singh Sethi mwenye makazi yake hapa nchini na Afrika Kusini, alisema licha ya mahakama kutoa uamuzi wataendelea kusimamia uamuzi huo wa kutomtambua mtu anayeitwa Martha Renju wala Benki ya Standard Chartered ya Hong Kong.

“Sisi msimamo wetu kama IPTL/PAP tunasema hadharani kwamba hatuitambua Benki ya Standard Chartered ambao hawa kila wakati wamekuwa wakikimbia mahakama zetu za ndani na kukimbilia nje na hata hukumu hii ya tuzo ina viashiria vya mabeberu.

“Tuzo husika waliyopewa ni dhahiri Standard Chartered ni batili kwa mujibu wa sheria. Wao ni kina nani hadi wakafungie kesi kwa niaba yetu. Hii ni kesi ya ngedere imepelekwa kwa nyani,” alisema

Kutolewa fedha za Escrow
Akizungumzia mchakato wa kutolewa fedha katika akaunti ya Tegeta Escrow, Makandege alisema mchakato wa kutolewa kwa fedha hizo ulikuwa wa kihalali kwa mujibu wa sheria za nchi.

Alisema Julai 5, mwaka 2006, Serikali na IPTL waliingia mkataba wa Escrow ambao ulipelekea kutolewa kwa fedha hizo kwenye akaunti hiyo iliyokuwa imefunguliwa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) bila kuwahusisha Benki ya Standard Chartered.

“Oktoba 8, 2010 IPTL na Tanesco kwa kuzingatia kipengele cha 10 cha mkataba huo ambayo kinaeleza kuwa endapo kuna mgogoro baina ya pande hizo mbili wahusika watakutana na kujadiliana  na hatua ya kuafikiana itahesabika kuisha kwa mgogoro.

“Hata ripoti mbalimbali ikiwemo ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) hakuna sehemu yoyote inayoeleza kuwa zile fedha ni za umma. Hata ICSID imetoa hukumu na kusema si fedha za Serikali lakini wanakiri zilitolewa kihalali ingawa hawakupewa Standard na kama kungelikuwa na mgogoro fedha zile singetolewa,” alisema

Kunyang’anywa mitambo
Alipoulizwa kuwa hatua ya suala hili kugubikwa na utata na utekelezaji wa maazimio manane ya Bunge la 10 likiwemo la wao kunyang’anywa mtambo, Makandege alisema wanajua kuna watu hivi sasa wanahaingika wakitaka kuona suala hilo linafanyika.

Pamoja na hali hiyo alisema kuwa mitambo bado ni mali yao kwa mujibu wa sheria na hakuna hatua itakayowafanya wafanikiwe watu hao ambao hakuwataja.

“Tunajua kuna watu hivi sasa wanataka kuona suala hili likitekelezwa ikiwemo IPTL kunyang’anywa mtambo, ninawaambia hakuna jambo kama hilo, nasi kila wakati tumekuwa wazi ikiwemo kulaani maazimio ya Bunge ambayo ni wazi yalikuwa na lengo la kukimbiza wawekezaji wazawa. Suala hili hata Rais mstaafu (Jakaya Kikwete) aliliweka wazi kwa nini lianze sasa baada ya mjadala wake kufungwa,” alisema.

TIC yahamasisha wadau kuwekeza Dodoma

0
0
Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kimefungua milango ya uwekezaji wa nchi mbalimbali kuja kuwekeza Nchini hasa makao makuu ya Nchi, Dodoma.

 Hayo yamebainishwa na Mtendaji Mkuu wa (TIC), Clifford Tandari  juu ya fursa za uwekezaji zilizopo Mkoani Dodoma, wakati wa Mkutano Mkuu wa Uwekezaji wa Dunia kanda ya Afrika uliofanyika Mjini Kigali nchini Rwanda hivi karibuni. 

Mkutano huo uliandaliwa na COMESA kwa kushirikiana na Serikali ya Rwanda.
Rais Paul Kagame wa Rwanda na Rais Yoweri Museveni wa Uganda, wakipatiwa maelezo na Mtendaji Mkuu wa Kituo Cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Clifford Tandari, juu ya fursa za uwekezaji zilizopo Mkoani Dodoma, wakati wa Mkutano Mkuu wa Uwekezaji wa Dunia kanda ya Afrika uliofanyika Mjini Kigali nchini Rwanda hivi karibuni.
Rais Paul Kagame wa Rwanda na Rais Yoweri Museveni wa Uganda, wakimsikiliza kwa makini Mtendaji Mkuu wa Kituo Cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Clifford Tandari, alipokuwa akiwaelezea juu ya fursa mbalimbali za uwekezaji zilizopo Mkoani Dodoma, wakati wa Mkutano Mkuu wa Uwekezaji wa Dunia kanda ya Afrika uliofanyika Mjini Kigali nchini Rwanda hivi karibuni.

Muhongo awapa kibano wakandarasi wazembe

0
0

Serikali imesema  haitawapa kazi wakarandasi nane waliokuwa waliokuwa wakitekeleza miradi ya Wakala wa Umeme Vijijini (REA), kutokana na kuonesha udhaifu na kushindwa kufikia malengo yaliyokusudiwa.

Kauli hiyo imetolewa juzi na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, alipokuwa akizungumza  na wafanyakazi wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) mkoani Kagera.

Profesa Muhongo alisema Serikali haiweze kuendelea kufanya kazi na wakandarasi wazembe  wasiofikia malengo kwa kuwa wanakwamisha juhudi za Rais Dk. John Magufuli za kutaka kuwaondolea matatizo wananchi walioteseka kwa miaka mingi.

Bila kuwataja wakandarasi na kampunin zao, Profesa Muhongo alisema, tayari Serikali imefanya upembuzi wa wakandarasi waliotimiza wajibu wao wakati wa utekelezaji wa REA awamu ya pili na kubaini wakandarasi nane hawakufikia malengo yaliyokusudiwa.

“Tunayo majina ya wakandarasi nane ambao kazi zao hazikuturidhisha,  walishindwa kufikia malengo yaliyokuwa yamewekwa na hivyo hatutathubutu kuwapa kazi tena katika REA awamu ya tatu, tukiendelea kufanya kazi na watu wa aina hii Serikali haitafikia lengo lake la kuwaondolea wananchi changamoto za kukosa nishati hii ambayo ni muhimu katika uchumi wa wakazi wa vijiji.

“Kama Serikali tuwahakikishie wananchi kwamba vijiji vyote nchini vitakuwa vimepata huduma ya umeme katika kipindi cha miaka mitano kupitia Mradi wa Umeme Vijijini Awamu ya Tatu (REA III), kwani tayari zimetengwa Sh trilioni moja kwa ajili ya shughuli hiyo,  fedha nyingi kuliko zilizowahi kutengwa,”
alisema.

Profesa Muhongo alisema  utekelezaji wa  REA awamu ya tatu utakuwa na kasi kubwa  na Serikali itahakikisha  unakamilika kwa wakati kama ilivyokusudiwa huku akiwatahadharisha wakandarasi watakaopewa mradi huo kufanya kazi kwa bidii.

Katika hatua nyingine, Profesa Muhongo aliwaasa wafanyakazi hao wa Tanesco kujiepusha na vitendo vya rushwa  au kutengeneza mazingira  yanayoweza kusababisha ufanisi wa kazi kutokuwapo.

Hata hivyo katika kuonyesha dhamira hiyo ya kuepuka rushwa, wafanyakazi hao walikula kiapo mbele ya Profesa Muhongo  na kuahidi kwamba hawatajihusisha na vitendo vya rushwa.

RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 55 & 56 (Riwaya inawafaa kuanzia miaka 18 na kuendelea )

0
0
Mtunzi : EDDAZARIA G.MSULWA

ILIOISHIA....
 “Sali sala yako ya mwisho?”
Dorecy alizungumza huku sura yake ikiwa imejaa jasho jingi, na mikonjo iliyonifanya niamini huu ni mwisho wa maisha yangu mimi Eddy Godwin

ENDELEA....
“Dorecy umechanganyikiwa?”
Nilimuuliza Dorecy anayeonekana kumaanisha kile kitu anacho kizungumza, hakunijibu kitu cha aina yoyote zaidi ya kuendelea kunielekezea bastola yake kwenye sura yangu
“Eddy usimuamini kila unaye muona utaumia sawa?”

Dorecy alizungumza na gafla nikastukia akinipiga na kitako cha bastola kwenye kichwa changu, giza lililo andamana na maruwe ruwe kitanitawala taratibu katika macho changu na kwa mbali nikausikia mlango ukifunguliwa, baada ya muda kidogo sikujua ni kitu gani kinacho endelea 

Nikahisi nikiguswa mgongoni, taratibu nikayafumbua macho yangu na kukutana na viatu vya mwanaume vikiwa vimesimama kando yangu, nikakinyanyua kichwa changu  taratibu huku nikiwa ninamaumivu makali, nikakutana na sura ya mwanaume ambaye amevalia sare za wahudumu wa hoteli hii

“Kaka, habari yako”
Jamaa alinisalimia, huku akinitazama usoni mwangu.Sikumjibu cha kwanza kutazama ni kuangalia sehemu nilipo weka begi langu lenye madini ndani, sikuliona na kujikuta nikikurupuka na kusimama, nikaingia bafuni na kukuta kweupe hakuna mtu

“Kaka vipi?”
“Ku..kunaa dada hiv...i mrefu ume...muona wapi?”
“Yule uliye ingia naye jana usiku?”
“Jana, usiku? Eheee huyo huyo”
Niliungumza huku nikipiga hatua kuelekea kwenye dirisha, nikatamani kuanguka chini na kupoteza fahamu, kwani mwanga mkali wa jua nilio ukuta nje ya dirisha umenichanganya kiasi kwamba nimekosa la kuzungumza

“Yule mbona aliondoka usiku ule ule?”
“Shitii”
“Kwani, hamujuani?”
“Ehee”
“Hamujuani?”
Hata sikujua nimjibu vipi, muhudumu huyu aliye simama mbele yangu, nikajichunguza na kugundua kuna damu zilizo mwagika kwenye shati langu la kiaskari nililo livaa.
“Unamichirizi ya damu puani kaka”

Muhudumu alinionyesha, nikasimama kwenye kioo kilichopo kwenye hichi chumba na kujikuta ni kweli nilitokwa na damu za puani, ambayo kwa sasa imekauka.Muhudumu akanipatia  taulo na nikaanza kujifuta
“Alafu, kuna askari walinionyesha picha yako mida ya asubuhi, na kuniuliza kama wewe upo kwenye hii hoteli nikwaambia kwamba uliondoka jana usiku”
Mapigo ya moyo yakaanza kunienda mbio, huku wasiwasi mwingi ukianza kunitawala

“Waliondoka?’
“Ndio waliondoka, ila sijajua kama watarudi tena au la”
“Asante ndugu yangu”
Nikatizama chini, na sikuona bastola zangu nikatambua ni lazima Dorecy atakuwa ameondoka nazo zote,
“Kaka kwani wewe ni askari kweli?”
Jamaa aliniuliza, nikamtazama kuanzia juu hadi chini, kwani maneno ya Dorecy aliyo niambia nisimuamini mtu yakaanza kunirejea kichwani mwangu
“Kwani vipi?”
“Nimeuliza hivyo kwa nia nzuri tu?”
“Nia gani?”

“Kwa maana picha ya sura yako, sio mara yangu ya kwanza kuiona kwenye mach yangu”
“Ulisha wahi kuiona wapi?”
“Wewe si ndio, Eddy?”
Sikustushwa sana kwa maana ninatambua kwamba ninatafutwa karibia nchi nzima ya Tanzania kwa tukio la kumuu Derick
“Mimi sio Eddy?”
“Sawa”

Nikatoka nje ya chumba, nikatizama kwenye kordo zote na kuona hakuna dalili ya kuwa na mtu, nikaanza kutembea kwa hatua za haraka kuelekea kwenye ngazi za kushuka chini, nikaanza kushuka kwenye ngazi ya kwanza, nikaisikia miguu ya watu wakikimbia na kunilazimu kuchungulia chini, nikaona kundi la askari wapatao sita wakipandisha ngazi kwa haraka huku wanne wakiwa na bastola na nyuma yao wakiwa wameongozana na mzee mwenye kitambi kwa haraka nikatambua ni meneja wa hii hoteli.Nikarudi juu haraka na kukutana na muhudumu niliyekuwa chumbani
“Tupandishe huku juu”

Aliniambia huku akitangulia kupandisha ngazi za kuelekea ghorofa ya juu, tukapandisha ghorofa ya juu na kutokea kwenye moja ya mlango wenye ngazi za chuma zilizo elekea chini.Tukaanza kushuka kwa haraka
“Huku ni nyuma ya holet”
Aliniambia, tukashuka hadi chini, tukakuta kijimlango kidogo, kilichopo kwenye ukuta na tuapita na kutokea kwenye hoteli nyingine niliyokuta kibao kikubwa kilicho andikwa ‘Macarios Hotel’

“Tupite huku”
Tukakatiza kwenye reli, na kushika barabara ya kuelekea magharibi kwetu na kutukea kwenye barabara moja inayopitisha magari mengi
“Hapa kunaitwa kwaminchi”
“Sawa”
Tukaendelea kukatiza mitaa, na kufika kwenye mtaa mmoja ulio na nyumba nyingi zilizo banana sana

“Hapa ni mwamboni”
“Kupo kama mbagala”
“Kwa nini?”
“Nyumba zake jinsi zilivyo”
“Karibu ndani”
Tukaingia kwenye nyumba iliyo chakaa kiasi fulani, akanikaribisha ndani kwake, ambapo kuna kitanda na kistuli kimoja, pamoja na nguo baadhi
“Karibu kaka”
“Asante”

Nikakaa kwenye kiti na yeye akaketi kwenye kitanda chake
“Kwa jina mimi ninaitwa Mbasa, ni mwenyeji wa bara, mkoa wa Shinyanga huko”
“Ahaaaa, kwanza ninashukuru kukufahamu, pili ninashukuru kwa kunisaidia”
“Kusaidiana ni jamba la kawaida, hususani kwa vijana kama sisi ambao tunatakiwa kuwa bega kwa bega katika kuhakikisha tunafikia kwenye malengo yetu”
“Nikuulize kitu Mbasa?”
“Uliza tuu”

Unawezaje kumsaidia mtu usiye mjua?”
“Kaka Eddy, mimi ninakujua na nimekuwa nikifwatilia habari zako kwenye magazeti jinsi unavyo tafutwa na jeshi la polisi kwa mauaji ya bwana Derick”
Nikamtazama jamaa vizuri, nikajitazama na mimi vizuri nikajisemea kimoyo moyo hata akitaka kuanzisha ugomvi, ninamudu tena sana
“Isitoshe, nilivutiwa sana na wewe”

“Kwa nini?”
“Umri wako na matukio yako uliyo yafanya ni tofauti”
“Sawa, ila ninakuomba usimuambie mtu juu ya uwepo wangu hapa kwako”
“Si wezi kwa maana ninahitaji tusaidiane”
“Tusaidiane?”
“Ndio, shida uliyo kuwa nayo wewe kidogo inaendana na yakwangu?”
“Shida gani”

“Nilizaliwa kwenye familia ya maisha bora, baba alikuwa anamiliki migodi ya madini, alikuwa ni tajiri sana.Ila niliaziliwa peke yangu kwa bahati mbaya mama yangu alifariki kwa ajali ya gari, nilikuwa darasa la sita”

“Baba alilazimika kumuona mwanamke mwengine, ambaye alikuwa ni binti mdogo kiasi na alijaliwa uzuri halisi kutoka kwa Mungu, kutokana na kazi nyingi za baba tangu, alitumia muda mwingi sana kuwa mbali na mama mdogo, ikafikia kipindi nikawa na mahusiano na mama mdogo”

“Badi mama mdogo alipata ujauzito wangu na mbaya zaidi niliwahi kubalehe haraka sana, ule ujauzito tuliulea katika mzingira ya kificho na ninacho mshukuru MUNGU, baba alisafiri kikazi kwenye Ujerumani na alikaa mwaka na nusu so ile ishu hakuijua”
“Mwanangu alizidi kukua pasipo baba kujua hilo, hadi anatimiza miaka mitatu, kama unavyo jua dunia haina siri baba yangu akaja kuligundua lile swala la mimi kuzaa na mama mdogo”

“Huwezi kuamini, kuna siku baba alituomba twende naye shambani, hatukuwa na kipingamizi kutokana tulikuwa hatujui kinacho endelea”
“Ngoja kwanza hapo mtoto wenu mulikuwa mumemuweka wapi?”
“Mtoto, tulimpeleka kwa dada yake yule mama mdogo, pesa za matumizi mimi ndio nilikuwa ninazipeleka pasipo baba kuelewa mchezo”

“Sasa tuifika shambani, tukiwa na mama mdogo, pamoja na baba.Tulikuta watu wake ambao mara chache huwa ninawaona ona, huwezi amini nilimkuta mwangu akiwa ametundikwa juu ya mti huku ngozi yake ikiwa imechunwa kama mbuzi aliye chunwa ngozi”

“Baba, yangu alitugeukia hapo hapo na kuanza kumshambulia mama mdogo kwa ngumi na mateke, huwezi ukaamini nilimshuhudia mama mdogo akichemshwa katika pipa lenye mafuta ya kula, huku akiwa hai, cha kumshukuru MUNGU, niliweza kufanikiwa kukimbia ila niligwa risasi za ya paja na kuanzia hapo sikuweza kumuona baba tena kwenye maisha yangu”

“Ila nilikuja kugundua kwamba baba pia alihusika na ajali ya mama”
“Kisa kilikuwa ni nini?”
“Hadi leo sijajua kisa kilikuwa ni nini hadi baba akaamua kumuua mama”
Nilimsikiliza Mbasa vizuri sana, kidogo yeye ana nafuu sana katika simu lizi ya maisha yake ya nyuma

“Baba yako anaitwa nani?”
“Godwin?”
Nikastuka, na kumtazama vizuri
“Mbona unastuka kaka Eddy?”
“Anaitwa Godwin, yupoje poje?”
“Mrefu kiasi, ni maji ya kunde kidogo, anamwili ulio jazia kidogo na pia anakovu kwenye mkono wake wa kulia, mama aliniambia baba alipataga ajali akiwa kijana”

Sifa ambazo Mbasa alinielezea zifanana na sifa za Mzee Godwin ambaye hapo mwanzo niliamini ni baba yangu ila ukweli ni kwamba ni baba yangu mkuwa, ila kitu kinacho nichanganya ni Mzee Godwin ninaye mjua mimi ni Mwanajeshi

Msajili: Sikumrudishia Lipumba uenyekiti CUF, Kajirudisha Mwenyewe Kinyemela

0
0
Wakati  wanasiasa na wasomi wakimnyooshea kidole Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi (pichani) kwa uamuzi wake wa kumtambua aliyekuwa Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba, mwenyewe ameibuka na kusema kuwa hatua yake hiyo haikulenga kumrudishia msomi huyo nafasi yake ya uenyekiti.

Jaji Mutungi  jana alisema kuwa alichofanya ni kukishauri chama hicho kuhusu mgogoro uliokuwa ukikisonga na Lipumba aliamua kutumia ushauri huo kurudi mwenyewe kwenye nafasi yake hiyo kinyemela.

Kauli hiyo ya Jaji Mutungi imekuja siku mbili tangu alipotoa waraka unaoelezwa kumtambua Profesa Lipumba kama kiongozi halali wa CUF licha ya kuandika barua ya kujiuzulu Agosti 6, mwaka jana akipinga vyama vinavyounda Ukawa kumpa fursa Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa kugombea urais.

“Isome barua yangu…, mimi nimeamua watu waijadili umenielewa? Ni vizuri wanavyoijadili, ila nilitarajia waijadili kwa tija sio kwa hasira,” alisema Jaji Mutungi.

Alipoulizwa kuhusu polisi kumsaidia Profesa Lipumba kuingia katika makao makuu ya CUF kwa mtutu alisema: “Hizo ni taratibu ambazo (polisi) wanatumia kwa kuzingatia sheria nyingine za nchi.”

Juni mwaka huu, Profesa Lipumba alimwandikia barua Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad kutengua barua yake ya kujiuzulu na kutaka arejee kwenye kiti chake, uamuzi uliozusha mtafaruku huku Mkutano Mkuu wa chama hicho ulioketi Agosti 21 ukiridhia kujiuzulu kwake licha ya kuwa ulivunjika.

“Barua yangu inajieleza sina haja ya kuichambua. Nimekujibu baada ya kuona mjadala huo (katika mitandao) nilitegemea (waliomtukana) wawashauri CUF cha kufanya badala ya kuanza kunitukana,” alisema Jaji Mutungi.

“Sasa huko mahakamani wanakotaka kwenda kama mahakama ikiamua kama Mutungi alivyoshauri huko nako watatukana pia?” alihoji.

Wanasiasa na wasomi 
Mwenyekiti wa Chama cha Kijamii (CCK), Constatine Akitanda alisema alichofanya msajili ni kupandikiza zogo ndani ya CUF jambo ambalo linasikitisha.

Akitanda alisema ndani ya CUF kuna bundi ambaye alikuwa anasumbua watu ila msajili ameongezea mgogoro huo na kuwa alichokifanya si sawa kwa mujibu wa mamlaka yake.

“Unajua hii nchi inachezewa sana hivi mtu anajiuzulu mwenyewe halafu anaamua kurejea mwenyewe bila kufuata taratibu ni aibu, lakini nadhani kuna mkono wa mtu,’ alisema.

Mwenyekiti wa Chama cha ACT-Wazalendo, Anna Mghwira alisema anachokiona ndani ya CUF ni uwepo wa biashara haramu ambayo inaweza kuua chama hicho.

Alisema ni wakati mwafaka kwa wafanyabiashara haramu hao wakajulikana katika pande zote kwani ni aibu kuvumilia kasoro hizo zitawale vyama vya siasa.

Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Tanzania Labour (TLP), Dominata Rwechungura alisema migogoro ndani ya vyama vya siasa ipo, hivyo ni jukumu la CUF kutatua ili kurejesha amani na upendo kati yao.

Mwenyekiti wa Chama cha United People Democratic Party (UPDP), Fahimu Dovutwa alisema kinachotokea ni msiba unaoacha pengo ndani ya CUF na vyama vya siasa nchini.

Dovutwa alisema pia pengo la mwasisi wa CUF, marehemu Shaban Mloo linaonekana na kuwataka wazee wa chama hicho kukaa ili kukinusuru chama. 

“Huu ni msiba katika siasa za Tanzania, naomba CUF watafute wazee wao ili waweze kusuluhisha hali hiyo kwa maslahi ya chama chao kwani pengo la Mloo linaonekana,” alisema.

Katibu wa Habari na Uenezi wa NCCR Mageuzi, David Kafulila alisema mgogoro wa CUF unaweza kutolewa uamuzi na mahakama pekee kwa kuwa msajili hana mamlaka ya kufanya alichokifanya. Kafulila alisema msajili anapaswa kushauri kwa mujibu wa Sheria ya Vyama vya Siasa na si kama alivyoelekeza kwani anaongeza mgogoro zaidi.

Mwenyekiti wa ADC, Hamad Rashid alishauri CUF kutumia vikao kumaliza tofauti zao, huku akibainisha kuwa ndani ya chama hicho kuna viashiria vya udikteta na usultani.

Mbunge wa Tandahimba CUF, Katani Katani alisema kwa sasa wamethibitisha jinsi Lipumba anavyotumika kwani pamoja na Jeshi la Polisi kukataza maandamano, wafuasi wa Lipumba waliandamana bila kuzuiwa.

Alisema haiwezekani chama kikaendeshwa kwa ajenda za watu wachache ambao wanatumikia matumbo yao na makundi yao na si chama.

Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Kitivo cha Sheria, Dk. Onesmo Kyauke alisema msajili anakosea na kuwataka CUF wakimbilie mahakamani kupata haki.

Credit: Jamboleo

NMB yaendelea kutoa elimu kupitia mkutano mkuu wa ALAT mjini Musoma

0
0
BENKI ya NMB imeendelea kutoa elimu kwa viongozi wa Halmashauri, Manispaa, Majiji na wananchi wa kada mbalimbali juu ya huduma za kibenki ambazo wamekuwa wakizitoa kupitia mkutano mkuu wa 32 wa Jumuiya ya Tawala na Serikali za Mitaa (ALAT) unaofanyika kitaifa mjini Musoma mkoani Mara ambapo wajumbe zaidi ya 500 wanahudhuria mkutano huo.
Kwenye picha Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, George Simbachawene akisalimiana na meneja wa NMB tawi la Musoma, Sebastian Kayanga alipokuwa anaingia kwenye ukumbi wa Mikutano wa Mwembeni Complex kwa ajili ya ufunguzi rasmi wa Mkutano wa mwaka wa ALAT Taifa. NMB imedhamini mkutano wa ALAT Taifa kwa shilingi Milioni 206 ikiwa ni gharama za mkutano na zawadi kwa ajili ya Meya bora wa Mwaka. Pichani kulia ni Kaimu Meneja wa NMB Kanda ya ziwa, Amos Mubusi.

Kupitia mkutano huo NMB imeelezea jinsi ilivyounganisha mfumo wake wa kibenki na mfumo wa serikali za mitaa (LGRCIS) kufanikisha ukusanyaji mapato ya kwa wakati na bila kupotea na kuandaa vituo vya makusanyo ya fedha kusaidia serikali katika makusano.

Akitoa mada kwenye mkutano huo ulioingia siku ya 2 hii leo,Afisa Mkaguzi Mkuu wa ndani wa (NMB) Augustino Mbogella,amesema licha ya kusaidia serikali katika suala zima la ukusanyaji wa mapato, benki hiyo pia imesaidia miradi ya maendeleo ya jamii ikilenga zaidi katika utoaji wa misaada katika sekta ya elimu  na afya.

Mbogella amesema mwaka 2015 pekee zaidi ya shule 140 za msingi na sekondari zilipata zaidi ya madawati 7,000 kwa Tanzania nzima katika mpango wa kuendelea kutatua tatizo la madawati mpaka kufikia septemba 2016 tayari wametumia zaidi ya milioni 900. 

“Upande wa afya tumetoa vifaa mbalimbali kwenye hospitali 50 za serikali pamoja na vituo vya afya ambapo kiasi cha fedha takribani shilingi milioni 200 zilitumika” alimalizia Augustino Mbogella.

Wakati huo, viongozi na wananchi wameombwa kutembelea banda la NMB ili kuweza kupata elimu zaidi likiwemo pia suala la ufunguaji wa akaunti mbambali kwenye benki hiyo ambazo zina manufaa makubwa.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI) George Simbachawene,akisaini kitabu cha wageni kwenye banda la NMB kwenye maonyesho ya ALAT.

Zitto Kabwe: Serikali ya CCM ionyeshe kuwa inawajali Wananchi wake Kuliko inavyowapenda Mafisadi wa PAP.

0
0
NCHI HAINA DAWA MAHOSPITALINI, SERIKALI NA PAP WANAHAHA KUFUJA MABILIONI YA WATANZANIA

Gazeti la The Citizen limeandika Juu ya Suala la Ukosefu wa Madawa Katika Hospitali zote Nchini. Hii ni Habari Mbaya na Kuogopesha Kwa Watanzania Wote.

Sababu Kubwa ya Kukosekana Kwa Madawa kwenye Mahospitali nchi Nzima ni Serikali kukosa Fedha. Serikali imeipa Bohari Kuu ya Dawa nchini (MSD) 32% Tu ya Fedha ambazo ilipaswa kutoa Kwa MSD. Serikali ilipaswa kutoa Shilingi Bilioni 62.5 Kwa MSD Katika Kipindi cha Mwezi Julai mpaka Septemba 30. Lakini mpaka Leo imeipa MSD Kiasi Cha Bilioni 20 tu.

Uchunguzi Umeonyesha mpaka Septemba 16 MSD walikuwa na Tembe za Vidonge vya Paracetamol 170,000 Tu Katika Bohari Yao ya Mbeya. Huku Nchi Hospitali zikiwa hazina Kabisa Tembe Hizo. Hali ikiwa Ni Hivyo Hivyo Hivyo Katika Dawa za Ukimwi (ARVs), Vifaa Tiba kwaajili ya Mama Na Mtoto, Dawa za kipindupindu nk.

Katika Wakati ambao imegundulika tumelipa Kampuni ya Kitapeli ya PAP kwenye Sakata la Escrow zaidi ya Dola Milioni 245 Sawa Na Shilingi Bilioni 530 - Kiasi hiki Cha Fedha Ni zaidi ya Mara Mbili ya Bajeti ya Shilingi Bilioni 251 ya MSD Kwa Mwaka. Na tukilipa Bilioni 320 tunazodaiwa Baada ya Hukumu ya ICSID tutakuwa tumelipa zaidi ya Mara Tatu ya Bajeti ya MSD Kwa Mwaka.

Serikali ya CCM ionyeshe kuwa inawajali Wananchi wake Kuliko inavyowapenda Mafisadi wa PAP.

Zitto Kabwe Ruyagwa
Septemba 26, 2016

RIWAYA: She is My Wife- Sehemu ya 15 & 16

0
0

MUANDISHI : EDDAZARIA G.MSULWA

ILIPOISHIA
“Fanya fasta basi”
Samson akatoka nje huku akiishika shika pua yake iliyo jaa maumivu ya kupigwa ngumi na Rahab, Samson akaingiza baiskeli ya kwanza na kutoka nje akiwa ameishika baiskeli ya pili akitaka kuingia ndani, gafla breki za gari aina ya Defender yenye askari wa kikosi cha F.F.U wapatao sita wakashuka kwenye gari kwa haraka huku wakiwa na bunduki na kunza kumfwata Samson sehemu alipo simama

ENDELEA
“Unafanya nini hapo?”
Askari mmoja alizungumza kwa sauti ya ukali na kumfanya Samson kuanza kutetemeka mwili mzima
“Husikii au?” askari aliendelea kuzungumza kwa sauti ya ukali

“Ni..ninaingiza baiskeli zangu ndani”
“Wewe kama nani?”
“Mimi, ni mmiliki wa hapa, mchana nilikimbia kutokana na tukio la majambazi”
Mazungumzo, yote yanavyo endelea nje Rahab anayasikiliza kwa umakini wa hali ya juu, huku bastola yake ikiwa mkononi mwake
“Mkuu tukague ndani”
Ombi  la askari huyu mwenye alama ya ‘V’ kwenye bega moja, likamfanya Samson kubaki akiwa anaduwaa, ila akajikaza asiuonyeshe mstuko wake kwani hakujua kitatokea nini baada ya askari hao kuingia ndani ya duka lake na kumkuta Rahab
“Kuna vurugu, maeneo ya Sinza kwa Remy, OVER”
Ilisikika sauti kupitia redio ya upepo aliyo ishika mkuu wao na kusababisha, kuto kulijibu ombi la asakri wake
“Tunakuja Over”

Alijibu, huku akiiwatazama askari wake na wote kwa pamoja wakarudi kwa haraka kwenye gari lao na kuondoka kwa kasi kubwa.Sammso akashusha pumzi nyingi, kwa haraka akaanza kuingiza baiskeli zake zote
“Tuondoke, tayari nimesha maliza”
Samson alimuambi Rahab na wote wakatoka nje kwa umakini, huku wakichunguza kila eneo la nje.Samson akapanda kwenye baiskeli yake
“Panda twende”
Rahab akaitazama baiskeli ya Samson kwa umakini,
“Siwezi kukivunja kiti chake”
“Wewe panda twende kwani kikivunjika tutajua mbele ya safari, isije hawa jamaa wakarudi na kunikuta tupo pamoja hapa sijui itakuwaje”
“Mmmm!!”

Rahab akapanda kwenye baiskeli na taratibu Samson akaanza kubadilisha gia moja baada ya nyingine zilizopo kwenye baiskeli yake kutoka gia laini kuelekea gia ngumu, na jinsi anavyozidi kuendesha baiskeli ndivyo mwendo wa baiskeli yake inavyozidi kuongezeka.Ndani ya dakika kumi wakawa wamefika nyumbani kwa Samson, wakaingia ndani kisiri pasipo mtu yoyote kuwaona

Ukimya ukatawala kati yao, na hakuna mtu aliye msemesha mwenzake kwa wakati huu, alicho kifanya Rahab, akavua viatu vyake na kupanda kitandani na kumfanya Samson kuendela kusimama akimtazama Rahab jinsi alivo jilaza chali akitazama paa la chumba chake

“Panda ulale”
Rahab alizungumza huku akimtazama Samson usoni
“Ahaa, mimi nitalala hapa chini”
“Wewe vipi, kinacho kuogopesha wewe ni nini?”
“Siogopi”
“Sasa kinacho kubabaisha ni nini, hebu acha ufala panda kitandani kwako ulale, ila onyo lala usiniguse mwili wangu”
“Mmmmm”
“Guna, tu”
“Ndio maana ninakuambia kwamba nitalala hapa chini”
“Sijawai kuona dume zima likiwa linaogopa kulala na mwanamke kitanda kimoja”

Samson akamtazama Rahab kwa umakini kisha akapanda juu ya kitanda na kuchukua mito miwili na kutengeneza mpaka kati yao ambao hakuna mtu ambeye angeweza kumgusa mwengine, Samson taratibu akajikuta akiaanza kutawaliwa na hisia za mapenzi juu ya Rahab ambaye anaonekana kawa si mtu wa masihara hata kidogo.Samson akauingiza mkono wake mmoja chini ya mto, na taratibu akanza kuupeleka katika eneo alilo lala Rahab.Akafanikiwa kuufikisha mkono wake alipo lala Rahab, akamminya kwenye maeneo ya mbavu , ila Rahab akatulia kimya na kujifanya kama amelala, Samson akarudia tena kumminya Rahab eneo la mbavu na Rahab hakuonyesha mtikisiko wowote

“Kitu kimelinki”
Samson alizungumza kimoyo moyo, huku usoni mwake akiachia tabasamu pana lililojaa uchu mkali wa mapenzi, akajigeuza na kujilaza kiubavu, taratibu mkono wake mmoja ukaanza kupandisha hadi kwenye chuchu ya Rahab, hata kabla Samson hajaukandamiza mkono wake vizuri kwenye chuchu ya Rahab, gafla macho yake yakakutana yakitazamana na jicho la bastola, aliyoishika Rahab kwa umakini

Baada ya kuzushiwa kifo, Bilionea Dangote ameyaandika haya.

0
0
Bilionea namba moja barani Afrika, Aliko Dangote amekanusha uvumi unaosambaa kwenye mitandao ya kijamii kuwa amefariki dunia akiwa nchini Ujerumani.

Taarifa hizo zinaeleza kuwa bilionea huyo amefariki akiwa nchini Ujerumani baada ya kuugua kwa muda mfupi. Aidha, taarifa hizo zinaeleza kuwa familia ya bilionea huyo imethibitisha kifo cha ndugu yao huyo na kusema kuwa ni pigo kubwa kwa Afrika.

Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Dangote ameandika hivi “I am hale, hearty and alive. Please disregard malicious report saying otherwise. Thank you.” , akimaanisha kuwa yeye ni mzima wa afya na kuwataka watu kupuuzia taarifa zinazoeleza kivingine.”

Akimaanisha “Mimi ni mzima na buheri wa afya. Tafadhali puuzeni taarifa zote zinazosema vinginevyo. Asanteni.”

Aliko Dangote ni raia wa Nigeria, ndiye mwenye utajiri mkubwa zaidi barani Afrika. Dangote anamiliki kampuni kubwa ya Dangote Group inayofanya kazi katika nchi mbalimbali za Afrika ikiwa ni pamoja na Nigeria, Benin, Ethiopia, Senegal, Cameroon, Ghana, Afrika Kusini,  Togo, Tanzania na Zambia.
Muda mfupi baada ya kuzuka kwa taarifa hizo, Aliko Dangote alikanusha taarifa hizo kupitia mtandao wa Twitter kwa kupost kuwa yuko Afrika kusini na yuko salama kabisa.

Rais Magufuli afanya ziara bandarini, azungumzia vyeti bandia na kutoa maagizo

0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 26 Septemba, 2016 ametembelea Bandari ya Dar es Salaam na kuzungumza na wafanyakazi wa bandari hiyo ambapo pamoja na mambo mengine ametoa miezi miwili kwa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) kununua mashine nne za kukagulia mizigo bandarini (Scanning Mashine).

Rais Magufuli ametoa agizo hilo baada ya kubaini kuwa kati ya mashine nne za ukaguzi wa mizigo zilizopo, ni mashine mbili tu ndizo zinafanya kazi na hazina uwezo wa kukagua mizigo yote inayotoka na kuingia nchini kupitia bandari hiyo hali inayosababisha kutokuwepo kwa udhibiti wa uhakika wa udanganyifu.

“Kwa hiyo nawaagiza TPA, na Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi Prof. Mbarawa na Mamlaka ya Mapato mpo hapa hakikiseni mnanunua mashine za kukagulia mizigo nne ndani ya miezi miwili, na ikifika miezi mitano muwe mmenunua mashine sita, ni lazima mizigo yote ikaguliwe kwa mashine” Amesema Rais Magufuli

Dkt. Magufuli ameiagiza (TPA) kwa kushirikiana na Wizara husika kuanza mazungumzo na kampuni ya kimataifa ya kuhudumia shehena ya makasha bandarini (TICTS) ambayo inapakia na kupakua mizigo katika gati namba nane hadi kumi na moja ili kurekebisha mkataba ambao Kampuni hiyo imeingia na Serikali kwa lengo la kuhakikisha nchi inapata manufaa yanayostahili.

Rais Magufuli aliyetembelea eneo la mita za kupimia mafuta yanayopakuliwa melini (Flow Meters) na kubaini kuwa mita hizo hazifanyi kazi, ameiagiza TPA kuharakisha mchakato wa kununua mita mpya na kuzifunga katika eneo hilo ili kudhibiti ukusanyaji wa mapato ya kodi ya mafuta.

Aidha, Dkt. Magufuli ameitaka TPA kujipanga kujenga bandari kavu (ICD) katika eneo la Ruvu Mkoani Pwani  ili kuachana na bandari kavu zilizoanzishwa na watu binafsi hapa Jijini Dar es Salaam na ambazo zimekuwa zikitumika kukwepa kodi.

Akizungumza na Wafanyakazi mara baada ya kumaliza kutembelea bandari, Rais Magufuli amewatoa shaka wafanyakazi hao na wafanyakazi wengine Serikalini, kuwa zoezi la kuhakiki vyeti linaloendelea nchi nzima halina lengo la kuwafukuza kazi wafanyakazi bali linafanywa kwa lengo la kukabiliana na tatizo kubwa la wafanyakazi hewa ambao wamefikia 17,500 na pia kuondoa tatizo la wafanyakazi wanaotumia vyeti vya kufoji.

Katika ziara hiyo Rais Magufuli ameongozana na Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa Mnyaa.

Katika hatua nyingine, Rais Dkt. John Pombe Magufuli amemuapisha Dkt. Zainab Abdi Seraphin Chaula kuwa Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Dkt. Zainab Abdi Seraphin Chaula amejaza nafasi iliyoachwa wazi na Dkt. Deodatus Mtesiwa ambaye amestaafu.

Kabla ya kuteuliwa katika nafasi hiyo Dkt. Zainab Abdi Seraphin Chaula alikuwa Mganga Mfawidhi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

26 Septemba, 2016

Waziri Mkuu Majaliwa Awasimamisha Kazi Maofisa Misitu Wanne, Apiga ‘stop’ Uvunaji Magogo Rufiji

0
0

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewasimamisha kazi Maofisa Misitu wanne na kusimamisha shughuli za uvunaji wa mazao ya misitu wilayani Rufiji kwa muda usiojulikana baada ya kutoridhishwa na usimamizi wake.

Maofisa waliosimamishwa kazi ni pamoja na Mkuu wa Idara ya Ardhi, Maliasili na Mazingira Dk. Paul Ligonja, Ofisa Misitu wilaya Gaudens Tarimo, Ofisa Misitu Yonas Nyambuya na Ofisa wa Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) wa wilaya Seleman Bulenga.

Waziri Mkuu amefanya uamuzi huo leo (Jumatatu, Septemba 26, 2016) wakati akizungumza na watumishi wa wilaya ya Rufiji kwenye ukumbi wa halmashauri kabla ya kuzungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara kwenye viwanya jumba la maendeleo wilayani Rufiji.

Aidha, Waziri Mkuu amemuagiza Mkuu wa Wilaya hiyo, Juma Njwayo kukusanya magogo yoye yaliyoko msituni na kuyapiga mnada na kuitaka  wizara ya Maliasili na Utalii kwenda wilayani Rufiji kufanya uchunguzi wa leseni za uvunaji walizozitoa kwa wilaya hiyo.

Waziri Mkuu amebainisha kwamba wilaya ya Rufiji ni moja kati ya wilaya inayoongoza kwa uvunaji wa mazao ya misitu bila ya kufuata taratibu licha ya kuwa na maofisa misitu.

“Hakuna mafanikio katika sekta ya misitu kwenye wilaya hii ya Rufiji. Nasimamisha shughuli zote za uvunaji wa mazao ya misitu pamoja na watendaji wake kwa sababu hatuwezi kuacha watu wanakata magogo bila ya kufuata taratibu,”

“Haiwezekani Rufiji iwe shamba la bibi, nimesimamisha uvunaji wa magogo hata kwa wenye leseni hadi tuzichunguze zimetoka wapi. Hatuwezi kuruhusu maofisa wanashiriki vitendo vya hujuma kwa kuvuna misitu Rufiji na kugonga mihuli ya Kilwa kisha fedha wanatia mifukoni,” amesema.

Wakati huo huo Waziri Mkuu amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya hiyo Rashid Salum kufuatilia maagizo aliyoyatoa kuhusu kizuizi cha Ikwiriri kwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe alipokutana na watumishi wa wizara hiyo.

Julai 18 mwaka huu Waziri Mkuu alikutana na watumishi wa wizara hiyo jijini Dar es Salaam  na kusisitiza kwamba hakuna sababu ya Serikali kuendelea kuwa na watumishi wasiokuwa na uaminifu, uadilifu na uwajibikaji.

Waziri Mkuu aliitaka wizara hiyo kupunguza idadi ya vizuizi vya ukaguzi wa mazao ya misitu kwenye  barababara  mbalimbali baada ya kukosa tija, alitoa mfano wa barabara ya kwenda mikoa ya kusini  kuanzia Dar es Salaam yenye vizuizi visivyopungua sita na kila kizuizi kinatumika kwa ajili ya kukagua mazao ya misitu na maliasili inayotoka kuvunwa.

Awali mbunge wa Rufiji Mohammed Mchengelwa alilalamikia vitendo vya dharau vinavyofanywa na watumishi wa sekta mbalimbali katika wilaya hiyo jambo linalosababisha wananchi kukosa imani na Serikali yao.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images